Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104762 articles
Browse latest View live

Taarifa ya serikali kuhusu kuzimwa kwa 'chaneli' za bure kwenye ving'amuzi

$
0
0
 Kufuatia uwepo wa malalamiko ya mara kwa mara kutoka kwa wananchi kuhusu kukosa huduma ya runinga za bure pindi vifurushi katika visimbusi (ving’amuzi) vyao vinapomalizika, serikali imetolea ufafanuzi suala hilo kwa kueleza namna mfumo wa utendaji unavyotakiwa kufanya kazi.

Akijibu maswali ya watumiaji mbalimbali wa mtandao wa Twitter kuhusu urushwaji wa runinga za bure, Msemaji Mkuu wa Serikali, Dkt. Abbas alisema, kwa mujibu wa sheria iliyopo sasa, vituo vyote vya runinga ambavyo vimepewa leseni ya FTA (Free to Air) vinapaswa kuonekana hata baada ya kifurushi kwenye kisimbusi kwisha.

Dkt. Abbas alisema kwamba, hadi sasa kuna vituo 16 vya runinga vya ndani ya nchi vilivyopewa leseni hizo, vikiwemo vituo vya ITV, Clouds TV na Channel 10.

Aidha, alifafanua kuwa, ili mtumiaji aweze kutazama hata baada ya kufurushi chake cha malipo kwisha, kituo cha runinga (mfano ITV) kinapaswa kuwalipa warushaji wa masafa (mfano Azam) ili ITV iweze kuonekana kwa wananchi hata ambao hawajalipia visimbusi vyao.

“… mfumo uko hivi: ili wewe uone bure hizo channeli kuna mzalishaji wa vipindi ambaye ni kituo cha TV na msafirisha masafa mfano StarMedia. Ili wewe uone bure kuna gharama huyo wa kwanza anatakiwa kulipia kwa wa pili. Asipolipia akakatiwa huduma hautaona. Kwa sasa ndio mfumo.”

Pia, Dkt. Abbas alitahadharisha kuwa, endapo kituo cha runinga hakutawalipa wasafirishaji wa masafa, watakatiwa huduma na hivyo kuwafanya wananchi washindwe kuweza kutazama runinga bure.

Kuhusu TBC kuonekana katika visimbusi vyote hata bila malipo, msemaji alifafanua kuwa, kila kisimbusi kinatakiwa kuweka TBC kupitia sera ya ‘must carry’ ambayo inaiwezesha kuonekana kwa wananchi bila malipo yoyote.

“Unapata TBC mda wote kwa sababu TBC anahadhi inayoitwa “must carry” ambaye mrusha masafa yeyote Tz lazima aioneshe TBC. Kama hupati channeli zingine za FTA muulize mtoa huduma wako. Majibu atakayokupa nijulishe na unipe jina la mtoa huduma wako,” aliandika Dkt. Abbas.

Alisema kuwa, kwa sasa serikali haina mfumo wa kuwaadhibu wamiliki wa vituo vya runinga wenye leseni za FTA lakini hawawalipi warusha masafa ili wananchi waweze kuona runinga hizo bure, badala yake, warusha matangazo hayo wanatawakati huduma kama hawajalipwa.

“…kwa kanuni iliyoanza Machi mwaka huu, mtoa huduma za TV asipolipa kwa msafirisha masafa anaweza kukatiwa huduma.”

Kuhusu Dstv na Azam kukata matangazo ya runinga za ndani baada ya kifurushi kwisha, Dkt Abbas alisema suala hilo lipo Baraza la Ushindani hivyo wananchi wasubirie majibu, na kwamba asingependa kulizungumzia kwa sasa.

Nec Yathibitisha Mgombea wa CHADEMA Kujitoa kwa Nyalandu

$
0
0

Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) imethibitisha kumtoa kwenye kinyang’anyiro cha ubunge Singida Kaskazini mgombea kwa tiketi ya Chadema, David Djumbe.

Mgombea huyo ameondolewa kwenye orodha baada ya kutimiza masharti ya kujitoa katika uchaguzi kwa mujibu wa sheria.

Mkurugenzi wa Uchaguzi wa NEC, Ramadhan Kailima alisema jana kuwa Djumbe alifuata maelekezo kwa mujibu wa sheria ya uchaguzi.

“Kama Sheria inavyosema Kifungu cha 49(1)(2) cha Sheria ya Taifa ya Uchaguzi, Sura 343 mgombea anaweza kujitoa kwa kuandika barua na kuisaini yeye mwenyewe pamoja na ahadi ya kiapo cha sheria alichoapa mbele ya hakimu.

“Tume haimkubalii wala haimkatalii sababu ni hiari yake. Amewasilisha taarifa hizo na Tume imemfuta katika orodha ya wagombea,” alisema Kailima alipoulizwa jana kuhusu hatima ya mgombea huyo.

Desemba 20, Djumbe aliwasilisha nyaraka za kujitoa katika uchaguzi huo uliopangwa kufanyika Januari 13 mwakani akieleza kuwa jina lake lilipelekwa kimakosa.

Mkanganyiko ndani ya Chadema ndiyo uliosababisha jina la Djumbe kupelekwa NEC na kupitishwa kuwa mgombea ubunge Singida Kaskazini.

Wakati Chadema ngazi ya Taifa ikisema haitashiriki katika uchaguzi huo mpaka NEC itakapokutana na wadau kujadili changamoto zilizojitokeza katika uchaguzi wa udiwani katika kata 43, uongozi wa chama hicho mkoani Singida ulipeleka Tume jina la Djumbe kuwa mgombea.

Mwenyekiti wa Chadema Mkoa wa Singida, Shaban Limu alisema Djumbe aliteuliwa kugombea na kamati ya utendaji ya wilaya.

Alisema wakati anateuliwa uongozi wilaya na mkoa ulikuwa haujawasiliana na makao makuu kujua msimamo juu ya uchaguzi huo.

Jimbo la Singida Kaskazini liko wazi baada ya aliyekuwa mbunge kwa tiketi ya CCM, Lazaro Nyalandu kujivua uanachama wa chama hicho hivyo kupoteza nyadhifa zote ukiwamo ubunge. Alijiunga na Chadema.

Uchaguzi pia unafanyika katika majimbo ya Longido ambako matokeo ya uchaguzi wa ubunge ya mwaka 2015 yalibatilishwa na Mahakama; na Songea Mjini ambako aliyekuwa mbunge kwa tiketi ya CCM, Leonidas Gama alifariki dunia.

Wanaovaa Nusu Uchi Kuanza Kushughulikiwa

$
0
0

Waziri wa Habari, Utamaduni, sanaa na Michezo, Dkt Harrison Mwakyembe amesema wizara imeanza kutekeleza agizo la Rais Magufuli juu ya baadhi ya wasanii ambao wanadaiwa kuwa chanzo cha kuporomoka kwa maadili ya kitanzania.

Waziri Mwakyembe ametoa taarifa hiyo alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari na kusema kwamba kitendo cha Rasi Magufuli kusema suala hilo, kimewapa nguvu ya kuzidi kupambana na wasanii, ambapo hapo awali walikuwa wakiwagusa huwajia juu na kulalamika.

"Pale tunapoona kuna ukiukwaji, tufumbe macho tusijali malalamiko yanavyokuja kutolewa, maana ukiwagusa wasanii walikuwa wanakuja juu sana, lakini tunashukuru mkuu wa nchi kulisemea hilo, basi na sisi tumeongezewa nguvu basi hatutaachia suala hilo kuendelea kuharibu vizazi vyetu", amesema Waziri Mwakyembe.

Hivi karibuni Rais Magufuli alizitaka mamlaka husika kuwachukulia hatua wasanii wanaovaa nusu utupu kwenye kazi zao za sanaa ambazo zingine huonyeshwa kwenye television, ambazo amedai hazina maadili na zinadhalilisha utamaduni wetu na kuharibu kizazi kijacho.

CCM Yamjia Juu Askofu Kakobe, Wadai Amekosa Hekima...VIDEO

$
0
0

Chama cha Mapinduzi (CCM) kimesema Askofu Zakaria Kakobe wa Kanisa la FGBF lililopo Mwenge jijini Dar es Salaam amekosa hekima na busara kwa kugeuza madhabahu ya kanisa kuwa jukwaa la kisiasa na kuanza kukashifu viongozi wa serikali akiwemo Rais Dkt John Pombe Magufuli.

Hayo yamesemwa na Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi Mkoa wa Dar es Salaam, Frank Kamugisha alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari ikiwa ni siku moja baada ya Aksofu Kakobe kukosoa namna serikali inavyotenda mambo yake, akisisitiza kwamba Tanzania si nchi ya chama kimoja kama ambavyo viongozi wanataka kuigeuza na hivyo kuwataka viongozi wa serikali waanze kutubu.

Kamugisha amesema kuwa, wao kama viongozi wa CCM hawaweza wakakaa kimya wanapoona chama kinachafuliwa na viongozi wake ambao wanafanya kazi kwa niaba ya watanzania wakikashifiwa.

Aidha, alisema kuwa, siasa ni kwa ajili ya wanasiasa, na kama kiongozi wa dini ana jambo lolote analotaka kuzungumzia, kuna busara za kutumia na sio kutumia kanisa kusema hayo.

==>Msikilize Kamugisha hapa chini akizungumza,

Marekani Yawawekea Vikwazo Wataalamu wa Makombora Korea Kaskazini

$
0
0

Marekani imewawekea vikwazo maafisa wawili wa Korea Kaskazini ambao inasema kuwa wamechangia kuundwa makombora ya nchi hiyo.

Wizara ya fedha nchini Marekani iliwataja Kim Jong-sik na Ri Pyong-chol na kusema kuwa wote walikuwa viongozi wakuu katika mpango wa makombora ya masafa marefu wa Korea Kaskazini.

Baraza la ulianzi la Umoja wa Mataifa liliiwekea vikwazo vipya Korea Kaskazini siku ya Ijumaa kujibu majaribio yake ya makombora ya masafa marefu. Korea Kaskazini ilisema kwa hatua hiyo ni kama ya vita.

Vikwazo hivyo vipya vya Marekani vitazuia shughuli zozote za wanaume hao wawili zinazofanywa nchini Marekani, na hata kutwaliwa kwa mali zao zilizo  nchini Marekani.

Wanaume hao wawili wanaonekana mara kwa mara wakiwa na kiongozi wa Korea Kaskazini Kim Jong-un wakiwa maeneo ya kuyafanyia majaribio makombora.

Mwaka huu nchi hiyo imefanya majaribio kadha ya makombora tofauti ambayo inasema kuwa yanaweza kufika nchini Marekani.

Mbunge Aliyejiuzulu Awatolea Mapovu CHADEMA....." Waulizeni milioni 360 za Ruzuku walimpa nani?”

$
0
0

Aliyekuwa Mbunge wa Siha kwa tiketi ya CHADEMA, Godwin Molel amewataka wananchi wa Siha kutoogopa akisema ametazama mbali hadi kuhama Chama hicho na kudai kuwa hawatajuta.

Akiwa kwenye Kampeni Longido Mollel amesema amehoji kama CHADEMA hawanunui watu huwa wanapeleka wapi Tsh Milioni 360 za ruzuku wanayopata kama chama kwa mwezi.

Mollel amesema kwamba; "Niwaambie watu wangu wa Siha. Msiogope. Mliponichagua kuwa Mbunge nilitakiwa kulitetea taifa na kuitetea Siha. Cheo ni zaidi ya maslahi ya taifa na Siha. Msiogope nimetazama mbali na nimeona mbali hivyo hamtajuta. Nataka kuwamba Rais aliyoko madarakani analitetea taifa".

Godwin Mollel alijivua ubunge Disemba 14 mwaka huu kwa kusema kwamba; “Nimeona nia ya dhati ya Serikali CCM kutetea rasirimali za Taifa, nikaona niweze kujiuzulu nafasi yangu ya ubunge ili niweze kwenda kujiunga kwa vitendo katika kulinda rasirimali za Taifa letu, aminini watu wangu wa Siha nimeona mbali katika maamuzi haya".

Kutana na Mtabibu Mwenye KUBRI kutoka kwa ALLAH issa simba said Mtabibu wa Nyota za Binadamu na Dawa za Asili ya Africa

$
0
0
Kutana na Mtabibu Mwenye KUBRI kutoka kwa ALLAH issa simba said Mtabibu wa Nyota za Binadamu na Dawa za Asili ya Africa Mwenye UWEZO Kubaini tatizo lako Pindi tu Utakapo Fanya Mawasilino Kupitia Wasaa Husika..JE UNASUMBULIWA NA Mapenzi? (Umeachwa na Umpendae,Awe Mume,Mke na Bado unampenda?Na Umejaribu Sehemu nyingi Bila Mafanikio?Wasilina na Maalim Hussein Ujione muujiza wa Papo kwa Papo.. anauwezo WA KURUDISHA MAHUSIANO NA KUIMARISHA NDOA YAKO NDANI YA SAA 12 TU. Umekimbiwa na Mumeo,mkeo au Mpenzi na anaishi na mtu mwingine? Muone akutatulie Anauwezo wa Hali ya Juu wa Kusambalatisha Mahusiano yao Endapo utafata Atakacho kuelekeza.
Atamfanya Atimize Ahadi zote kwa Muda Mfupi.

Issa simba said Anatumia Jina la Muhusika au Picha Kumaliza Tatizo lako..
Anatibu kwa Kutumia Vitabu vya QUR-AN Dawa za Asili za Africa,Dawa za Kiarabu na Majini.Anatafsiri Ndoto. Kushinda BAHATI NASIBU, KUSAFISHA NYOTA. Mvuto wa Mwili na BIASHARA, Kinga ya Mwili,ZINDIKO za Nyumba.MIGUU Kufa GANZI.Kufungua KIZAZI kwa wale walio fungwa kwa njia za KISHIRIKINA. Anakupa Jini la Mali kwa yule anaehitaji Utajiri BILA MASHARTI. Nguvu za KIUME, Humaliza Kesi zilishindika ndani ya siku 14 tu..na mengi zaidi

+255 622588038au 0679119679 au +255 764318107
NB: TIBA KWA DINI ZOTE NA IMANI ZOTE...

RPC Shanna Atoa Onyo Kali kwa Wafunga Barabara na Kuchoma Matairi Mkesha wa Mwaka Mpya

$
0
0

Kamanda wa polisi mkoani Pwani (ACP) Jonathan Shanna ,ametoa onyo kwa watu wenye tabia ya kufunga barabara kwa kuchoma matairi katika mkesha wa mwaka mpya na kupelekea usumbufu kwa watuamiaji wengine wa barabara kuacha kufanya kitendo hicho .

Amesema atakaejaribu kuchoma moto matairi kwenye mkesha huo,jeshi la polisi mkoani hapo litamchukulia hatua kali ili iwe fundisho kwa wengine.

Akizungumza na waandishi wa habari kuhusiana na hali ya kiusalama inavyoendelea hasa katika kipindi hiki cha kuelekea kwenye sikukuu ya mwisho wa mwaka ,kamanda Shanna alisema wanazidi kuimarisha doria katika pande zote za mkoa huo.

Alisema kipindi cha sikukuu ya x-mas hali ilikuwa shwarii hivyo wanaendelea na misako ya miguu kwa kushirikiana na vyombo vingine vya ulinzi na usalama na doria hizo zitakuwa mtaa kwa mtaa na nyumba kwa nyumba ili kuhakikisha watu waishi kwa amani .

Akielezea kuhusiana na hali ya uhalifu katika kipindi cha Januari hadi disemba mwaka huu ndani ya mkoa huo ,kamanda Shanna alisema wamefanikiwa kupunguza idadi ya makosa kwa kiwango kikubwa.

Kamanda huyo alisema,matukio ya makosa ya uvunjaji yamepungua kutoka 771 kipindi kama hicho 2016 na kufikia 233 mwaka huu ikiwa ni tofauti ya matukio 538.

Makosa mengine ni yale ya unyang’anyi wa kutumia silaha ambayo yamepungua kutoka 31 mwaka jana hadi nane kwa mwaka 2017  tofauti makosa 23.

“Unyang’anyi wa kutumia nguvu  yameripotiwa makosa 43 ,kipindi kilichopita ilikuwa 112 tofauti makosa 69,:;na mauaji makosa yaliyoripotiwa januari hadi disemba mwaka huu ni 34 ,mwaka uliopita ilikuwa 126  tofauti ni makosa 92.” alifafanua kamanda Shanna.

Aliwataka wananchi kutoa ushirikiano kwa jeshi hilo mara wanapotilia shaka kundi ama mtu ni mhalifu ,kwani kila mmoja ana wajibu wa kudhibiti vitendo vya uhalifu .

Kamanda Shanna ,alisema Pwani yenye utulivu,amani ,yenye kushikamana inawezekana endapo kila mmoja atatimiza wajibu wake.


Pigo Jingine Tena Kwa CHADEMA Diwani wa Siha Ajiuzulu na Kuhamia CCM

$
0
0

Mwenyekiti wa Chadema Wilaya ya Siha ambaye pia ni diwani wa Gararagua, Zakaria Lukumay amejiuzulu uanachama wa (Chadema) na kujiunga na CCM.

Lukumay ametangaza kujiuzulu siku kadhaa baada ya aliyekuwa mbunge wa Siha (Chadema), Dk Godwin Mollel kujivua ubunge na kujiunga na CCM.

Sawa na Dk Mollel, diwani huyo amesema uamuzi wake unatokana na kumuunga mkono Rais John Magufuli katika kutetea na kulinda rasilimali za Taifa.

Katika barua kwa Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Siha inayoonyesha iliandikwa Desemba 24,2017 Lukumay amesema anajiunga na CCM kwa sababu ndicho chama kinachogusa mahitaji ya Watanzania wote.

Aliyekuwa diwani wa Chadema wa Donyomurwak wilayani Siha,  Lwite Ndossi maarufu Nsonuu Desemba 19,2017 alijivua uanachama wa chama hicho na kujiunga na CCM.

Taarifa iliyotolewa na idara ya itikadi na uenezi ya CCM Desemba 19,2017 ilisema Ndossi alieleza sababu za kujiunga na CCM ni kuwa amejiunga na watu wanaofanya siasa za kufanya kazi za maendeleo na si kulumbana na maneno matupu.


Ali Kiba Awaomba Radhi Mashabiki Wake

$
0
0

Msanii wa muziki Bongo, Alikiba amewaomba radhi mashabiki wake kufuatia kushindwa kufanyika kwa tamasha la Funga Mwaka na King Kiba.

Hapo awali muimbaji huyo alihaidi kufanya hivyo lakini kwa sababu zilizoko nje ya uwezo wake kitu hicho kimeshindikana kufanyika. Kupitia ukurasa wale wa Instagram Alikiba ameandika;

Hello fans, natumaini kila mmoja wenu amekuwa na wakati mzuri katika kipindi hiki cha sikukuu. Ningependa kuchukua nafasi hii kuwaomba radhi kwa kushindwa kuwatimizia ahadi ya kufanya #FungaMwakaNaKingKiba kama ambavyo niliwatangazia mwanzo.

Haikuwa lengo langu ila kuna mambo yamejitokeza yaliyo nje ya uwezo wangu ambayo yamesababisha kutoweza kufanyika kwa tukio letu ambalo pia lingehusisha uzinduzi wa products zangu pamoja na wimbo wangu mpya.

Pia ameongeza kuwa hivi karibuni Mungu akijaalia atawapa taarifa mashabiki wake namna watakavyoufungua Mwaka. Alikiba kwa sasa anafanya vizuri na ngoma ‘Single’ aliyoshirikishwa na Abdu Kiba.

Tuzo ya Mbwana Samatta Yafutwa

$
0
0

Kama unaikumbuka tuzo ya mchezaji bora wa ndani wa Afrika ambayo Mbwana Samatta alishinda usiku wa January 7, 2017 haitakuwepo kwa mwaka huu 2017 kwa mara ya kwanza tangu ilipoanza kutolewa mwaka 1992.

Sababu ya msingi ambayo imetolewa na shirikisho la soka barani Afrika ni kwamba, waliopewa jukumu la kuchagua mchezaji bora wa kipengele hicho wote wamekosa sifa na walichaguliwa kimakosa kuwepo katika jopo hilo.

Kwa mujibu wa CAF tuzo hiyo huenda ikarudi endapo watapatikana watu sahihi watakaounda jopo ambalo kazi yake ni kuteua majina ambayo yatawania tuzo hiyo.

Kwa maana hiyo, kwa sasa wachezaji wa ndani watapambanishwa na wachezaji wanaocheza nje ya Afrika kuwania tuzo ya mchezaji bora hadi hapo itakapotangazwa vinginevyo.

Habari Njema: Tunatibu Busha, Korodani Kuvimba,Ngiri, Miguu Kufa Ganzi Pamoja na Matatizo ya Nguvu za Kiume.

$
0
0

Ni dawa ya nguvu za kiume inayorefusha na kunenepesha uume saizi uipendayo (Inch 1-7) kwa muda wa siku 6 tu.Dozi hii itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa muda wa dakika 30, utarudia tendo la ndoa zaidi ya mara 4 bila hamu kuisha bila kujali umri na garantee ni miaka 60 baada ya kutibu tatizo.

Pia tunatibu Busha bila kufanyiwa Oparesheni, korodani moja kuvimba, ngiri, tumbo kujaa gesi na kuunguruma, kutopata choo vizuri, miguu kuwaka moto na kufa ganzi, chango la wanawake, kisukari na kutokwa na kinyama sehemu ya haja kubwa.

MIHAYO:
Inarudisha mke, mchumba, hawara na atakutimizia kila kitu unachotaka kutoka kwake ndani ya  saa 2 tu hata kama yupo mbali. atarudi na kumfunga asiwe na mwingine zaidi yako.

Umefukuzwa kazini? unataka kupandishwa cheo? Umepoteza pesa zako kwenye biashara bila kujua umepandikizwa chuma ulete? Njoo urudishe pesa zako. Unauza mali yako haiendi? Wasiliana na mtaalam Challo kwa; 0714006521

Young Dee Amtolea Mapovu Amber Lulu,...."Hana Hadhi ya Kuwa na Mimi"

$
0
0


MKALI wa ngoma ya KibenTen, David Genzi maarufu kwa jina la Young Dee, amemponda mpenzi wake wa zamani, Amber Lulu kuwa hana hadhi ya kuwa naye kwa sasa.

Akichonga na Risasi Vibes, Young Dee alisema kwa sasa yupo kwenye uhusiano ‘siriaz’ na

“Nimechoka kuulizwa maswali kuhusu kuwa kwenye uhusiano na Amber Lulu, hana hadhi ya kuwa na mimi na ninaomba nisiharibiwe uhusiano wangu na mpenzi wangu ambaye nipo naye kwa sasa,” alisema Young Dee.

Wawili hao wamejikuta katika malumbano kufuatia wiki iliyopita, msichana huyo kusema kuwa ni kumkosea heshima kumfananisha mpenzi wake wa sasa, rapa wa Kenya, Prezoo na kijana huyo wa Dar es Salaam.

Tambwe Ajtamba Kuwapa Ushindi Yanga

$
0
0

Amissi Tambwe

MSHAMBULIAJI wa Yanga, Amissi Tambwe aliyekuwa majeruhi kwa kipindi kirefu ameibuka na kufunguka kuwa amerejea kwenye makali yake.

Tambwe ambaye alikuwa nje kutokana na kusumbuliwa na goti lililomfanya akose mechi 11 za timu hiyo za ligi kwa mara ya kwanza Jumapili iliyopita alionekana uwanjani kwenye mchezo wa timu hiyo wa Kombe la Shirikisho (FA) dhidi ya Reha ambapo alihusika kwa kufunga bao moja katika ushindi wa mabao 2-0.

Mshambuliaji huyo ambaye alipita VItal’O na Simba kabla ya kutua Yanga ameliambia Championi Jumatano, kuwa mara baada ya kuonekana tena uwanja kwa sasa mtihani wa kwanza kwake ni kuhakikisha Yanga inakuwa na matokeo mazuri katika kila mchezo wake pamoja na kufunga mabao mengi tofauti na ilivyokuwa kwenye baadhi ya mechi.

“Nashukuru kwamba nimerejea ndani ya timu baada ya kupita kwa muda mrefu nikiwa nje kutokana na majeraha, na pia jambo la kushukuru ni kuwa nimeingia na kuiwezesha timu kupata matokeo kwenye mechi yetu iliyopita tena nikifunga na bao.

“Jambo ambalo lipo mbele yangu kwa sasa ni kuona kwamba Yanga inafanya vizuri kwenye kila mechi ya michuano tena na mimi nikiwa nafunga mabao, naamini yote hayo yatawezekana kwa sababu ya ushirikiano ambao nimeupata kwa wenzake mara baada ya kurejea tena uwanjani,” alisema mshambuliaji huyo.

Buswita Aanza Kuleta Mbwembwe Yanga

$
0
0

Kiungo wa ti,mu ya Yanga Pius Buswita.

BAADA ya kufunga bao lake la pili tangu atue Yanga, kiungo mshambuliaji wa timu hiyo amewaambia mashabiki wa timu hiyo: “Tulieni, mbona mtafurahi sana.” Kauli hiyo, aliitoa wikiendi iliyopita mara baada ya kuifungia timu yake bao la kuongoza akipokea pasi ya Mrundi, Amissi Tambwe wakati Yanga ilipovaana na Reha FC katika mechi ya Kombe la FA iliyochezwa Uwanja wa Uhuru jijini Dar.

Kiungo huyo, hilo ni bao lake la pili kulifunga tangu ametua kuichezea Yanga kwenye msimu huu wa Ligi Kuu Bara akitokea Mbao FC ya Mwanza. Akizungumza na Championi Jumatano, Buswita alisema anafahamu mashabiki wa Yanga wanapenda kumuona akionyesha kiwango cha juu zaidi ya hicho amekionyesha kwa kifupi, hivyo ameomba muda kidogo.

Buswita alisema, ana mfupi tangu ametua kuichezea Yanga, hivyo kikubwa mashabiki wamvumilie huku akiendelea kuwathibitishia ubora wake taratibu kwenye mechi zijazo za ligi kuu na mashindano mengine. “Kikubwa watu wanatakiwa wafahamu kuwa, mimi nimetoka kwenye timu ndogo ya Mbao na nimekuja kwenye timu kubwa ya Yanga yenye presha kubwa ya mashabiki.

“Hivyo, ni lazima nibadilike taratibu kutoka mfumo niliokuwa nautumia nikiwa na Mbao na kuuchukua huu wa Yanga, hivyo siyo kazi ndogo inayohitaji muda kidogo wa mimi kuushika, pia kuzoeana na wenzangu. “Niwaahidi Wanayanga kuwa, mtafurahi na kunielewa wenyewe, kwani ninaamini uwezo wangu wa ndani ya uwanja ikiwemo kufunga na kutengeneza nafasi za kufunga mabao,” alisema.


"Raisi Magufuli Hakunilenga mimi, Nitaendelea Kuvaa Mavazi Niliyozoea" Sanchoka

$
0
0

WAKATI Rais John Pombe Magufuli akiziagiza mamlaka zinazohusika kuhakikisha maadili ya Kitanzania yanalindwa kwa kudhibiti vitendo vya ukiukwaji wake, mrembo Jane Rimoy maarufu kama Sanchoka au Sanchi anaonekana kuwavimbia kichwa Polisi baada ya kuendelea kuposti picha zake akiwa nusu utupu.

Akillihutubia taifa wakati wa sherehe za kumbukumbu ya miaka 56 ya Uhuru wa Tanzania Bara mjini Dodoma Desemba 9 mwaka huu, Rais Magufuli alizitaka mamlaka zinazohusika na makosa ya mitandao, kuwachukulia hatua mara moja watu wanaokiuka maadili, huku akitoa onyo kwa wasanii na watu wengine wanaovaa nusu utupu.

Lakini akiendelea kutupia picha hizo, Sanchi ameliambia Risasi Mchanganyiko kuwa hawezi kubadili aina ya mavazi anayovaa kwa kuwa hayakiuki maadili.

Sanchi alisema ataendelea kuvaa mavazi yake aliyozoea kila siku kwa vile anajua havinji sheria maana ni mazuri na hayana shida.

“Mimi naendelea kuvaa mavazi yangu kwa sababu toka zamani ndiyo navaa hivi na ninajua wazi sio mlengwa wa hiyo kauli ya mkuu, halafu mimi pia ni mwanamitindo, ni lazima nibuni mtindo wangu,” alisema.

Akizungumzia suala hilo, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kinondoni, Jumanne Murilo, alisema jambo hilo bado halijafika mezani kwake, lakini anaamini vijana wake watalifanyia kazi mara moja, kwa kuwa wapo hapo kwa ajili ya kuhakikisha sheria inafuatwa.

“Kazi inafanyika kwa watu wote wanaotumia mitandao vibaya, siyo Sanchi tu bali wasanii wengine pia, tupo hapa kuhakikisha agizo la rais linatekelezwa na hakuna mtu atakayeachwa, hilo ndilo ninaloweza kusema kwa sasa,” alisema Kamanda Murilo.

Daktari Mmoja atoa Huduma kwa Vijiji Saba

$
0
0

Mtwara. Umewahi kujiuliza kwamba inaweza kuwapo zahanati inayotoa huduma kwa vijiji saba? Tena ikiwa na daktari mmoja?

Basi ipo zahanati moja katika kijiji cha Madimba wilayani Mtwara ambayo ina daktari mmoja huku ikitoa huduma kwa vijiji saba ikiwa ni pamoja na kuhudumia wajawazito.

Vijiji ambavyo vinapata huduma kwenye zahanati hiyo ni pamoja na Madimba, Namindondi, Mngoji, Mitembe, Mayaya, Mitambo na Mtendachi.

Zahanati hiyo ina daktari mmoja na watumishi wengine watatu akiwamo muuguzi mmoja, mkunga na mama afya.

Hata hivyo, wakati mwandishi wa habari hizi alipofika katika zahanati hiyo alimkuta mtumishi mmoja huku watatu hawakuwapo kutokana na kilichoelezwa kuwa ni majukumu mengine ya kikazi.

Akizungumza na Mwananchi, mjamzito Sharifa Khamis, mkazi wa kijiji cha Mtendachi alisema kuna wakati wanalazimika kushinda njaa kutwa nzima na hurudi nyumbani bila kuhudumiwa kutokana na wingi wa wagonjwa.

“Nimefika hapa tangu asubuhi, huduma ni kama mnavyoona mhudumu yuko mmoja anahudumia huko anarudi kule, akitoka kule anakwenda kule yaani hakuna huduma,” alisema.

“Siku nyingine tunakuja tarehe za kliniki zilishafika anaona watu ni wengi muuguzi anatuambia rudini mje kesho nishaelemewa na ukiangalia ni kweli inabidi tuondoke tu.”

Muuguzi wa zahanati hiyo, Veronica Haule alisema: “(Kwa) idadi tuko wanne, mganga, mkunga, mama afya na mimi muuguzi, lakini daktari sasa ana kitengo kingine cha kifua kikuu na ukoma kwa hiyo kituoni anapatikana mara mbili kwa wiki, mkunga yuko likizo anamaliza leo. Kwa hiyo kwa ndani ya mwezi mzima niko mwenyewe na mama afya hapa anapatikana kwa siku moja ,” alisema Haule.

Mkazi wa kijiji hicho, Athumani Ramadhani alisema zahanati kutokana na uchache wa watumishi wananchi wanalazimika kuwa wapole kwa kila jambo wanaloelezwa hata kama hawakubaliani nalo.

“Zahanati inahudumia vijiji saba na wahudumu hawatoshi mmoja anaweza kufanya kazi kutwa nzima, hata akigoma hatuwezi kumuonya kwa sababu anakuwa na uchovu,” alisema Ramadhani.

Akizungumzia kadhia wanayopata wagonjwa, mwenyekiti wa kijiji cha Madimba, Mohammed Mussa alisema zahanati hiyo inakabiliwa na uhaba wa watumishi kwa muda mrefu na walishachukua hatua lakini hakuna utekelezaji.

“Kama msimamizi wa masuala ya hapa kijijini nilionana na daktari wa hiyo zahanati akasema atafikisha hili suala kwa mganga mkuu wa wilaya zaidi ya hapo sijaona matokeo,” alisema.

Mratibu wa afya halmashauri ya Mtwara Vijijini, Elizabeth Mrope alisema zahanati hiyo inakabiliwa na upungufu wa watumishi badala ya 13 aliodai kuwa wanahitajika wapo wanne.

Sera ya Afya ya 2007 inaelekeza kila kijiji kiwe na zahanati na kata kuwa na kituo cha afya vyenye watumishi wa kutosha. Kwa mujibu wa Sensa ya Watu na Makazi ya mwaka 2012, Kata ya Madimba ilikuwa na wakazi 13,139 na kuna mradi mkubwa wa kuchakata gesi asilia unaoendeshwa na Kiwanda cha Madimba.

Source; Mwananchi

Mkuu wa Mkoa wa Arusha Anena na Wakuu wa Shule

$
0
0

Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Mrisho Gambo amewataka Wakuu wa shule mbalimmbali mkoani humo kuhakikisha fursa zinagawanywa kwa usawa kwa walimu wote na kutaka dhana ya walimu wanaojipendekeza tu kwa mkuu wa shule kuwa wanufaika wa fursa hizo inakufa.

Mrisho Gambo ameyasema hayo alipokuwa akiongea na baadhi ya walimu wa shule ya  Embarway Sekondari iliyopo Arusha na kusema kama walimu Wakuu wakifanya utaratibu mzuri itasaidia walimu hao kunufaika na fursa mbalimbali kwa usawa, jambo ambalo litasaidia kuondoa upendeleo.

"Kumekuwepo na malalamiko sehemu zingine kwenye zoezi kama la leo hili la kusimamia mitihani unakuta kila mwaka wanakwenda walimu wale wale rafiki zake Mkuu wa shule, kama wewe kiwango chako cha kujipendekeza ni kidogo wewe utakuwa unasikia kwa wengine tu maana orodha ya walimu wanaokwenda kwenye usimamizi huwa inapagwa na Mkuu wa Shule, maeneo mengine nasikia wanaangalia sana jinsi kama ni mdada akimpa ushirikiano zaidi Mkuu wa Shule huyo dada hakosi lakini tumekuwa tukisisitiza hiyo kazi ya kusimamia mitihani ni kazi ya kila mwalimu" alisema Gambo

Aliendelea kufafanua kuwa "Kwa Mkuu wa shule anayejitambua anapaswa kutengeneza utaratibu mzuri ili kuwe na mzunguko, kila mwalimu mwenye sifa aweze kushiriki kwenye zoezi hilo, haiwezekani ukaenda kila mwaka, unaweza kwenda mwaka huu mwakani akaenda mwingine, baadaye ikafika tena zamu yako. Kwa sababu walimu hawa hawana kazi ya ziada, ofisi zingine wanalipwa masaa ya ziada lakini walimu hawalipwi, mwalimu hana posho, mwalimu hana safari, mwalimu yeye ni mitihani, sensa na kusimamia uchaguzi basi sasa hizo fursa zinapaswa kuwekewa utaratibu mzuri ili kila mmoja anufaike nazo"

Mbunge Ammwagia Sifa Godwin Gondwe

$
0
0
Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mh. Luhaga Mpina amesifu utendaji kazi wa Mkuu wa Wilaya ya Handeni mkoani Tanga, Godwin Gondwe katika usimamizi wenye weledi wa sheria za mifugo nchini.

Luhaga ametoa sifa hizo kwa Gondwe akiwa kwenye ziara yake wilayani Handeni ambapo amekemea tabia ya baadhi ya watendaji wa Serikali katika Hifadhi za Misitu, Mapori ya Akiba na Serikali za Mitaa kukamata mifugo kiholela na kutoza faini zisizo na misingi ya kisheria.

“Ninamsifu mkuu wa Wilaya ya Handeni Ndugu Godwin Gondwe kwa utendaji wake mzuri na ripoti ya mifugo wilayani kwake ni nzuri lakini watendaji wa Serikali waliofanya hujuma na dhuluma kwa wafugaji hawatabaki salama, tutawafuatilia na kuchukua hatua stahiki kwa mujibu wa sheria” amesema Luhaga.

Waziri Mpina ameongeza kuwa jumla ya kaya milioni 4.49 za  kilimo nchini zinajishughulisha na ufugaji mifugo ya aina mbalimbali. Pia ameweka wazi kuwa kama sekta hiyo isingekuwa inazalisha mazao ya mifugo na Serikali kuamua kuagiza kutoka nje ya nchi basi ingelazimu kutumia kiasi cha sh. Trilioni 17.8.

Kwa upande wake Godwin Gondwe amesema pamoja na pongezi za Waziri Mpina, wao kama serikali ya Wilaya wataendelea kubuni mbinu mbalimbali za kuboresha sekta ya ufugaji ikiwemo uimarishaji wa majosho, malisho na uzuiaji uuzaji nyama kiholela barabarani.

Kutana na Sharifu Juma Mohamedi Mtabiri Wa Nyota Za Binadamu Duniani

$
0
0

KUTANA NA SHARIFU JUMA MOHAMEDI NIMTABIBU WANYOTA ZA BINANADAM DUNIANIKOTE RUDISHA MAHUSIANO NA MPEZIWAKO NDANI YA MASAA (72) TU SHARIFU JUMA MOHAMED ANATIBU MARADHI SUGU KAMA VILE MIGUU KUUMA NA KUWAKAMOTO PRESHA KISUKARI VIDONDA VYATUMBO PUMU NA TEZI NA UVIMBETUMBONI

ANAUWEZO WAKURUDISHA MTUALIE A KIMAZINGIRA (MSUKURE) KUMFANYA MUME MKE MPENZI ASIKUSALITI DAWA YA (LIMBWATA) KUMTAWALAMPENZIWAKO UNAVYOTAKA KUMUONA MBAYAWAKO LIV KWASABABU MAALUM ANATOA PETE YA BAHATI INAYO ENDANA NA NYOTA YAKO ITAKAYO KULETEA PESA BILA YA MASHARITI NA ITAKUONGOZA KATIKA SHUGURI ZAKO NAKUMILIKI PESA ZAMAJINI DAWA YA UZAZI KWAKINAMAMA KUSHIKA UJAUZITO NDANI YASIKU 14 UWELEWA WAMASOMO DARASANI PAMOJA NAKUFAULU MITIHANI DAWA YA NGUVU ZAKIUME NAKUREFUSHA UUME SAIZI UIPENDAYO KAMA UMEIBIWA AMA KUDHULUMIWA UTARUDISHIWA MALIYAKO NDANI YAMASAA(24) ANAFUNGAKESI NAKUPATA HAKIYAKO DAWA YA MVUTO WABIASHARA KUUZA MALI YAKO KWA HARAKA PIA ANAWEKA KINGA KWENYE SHAMBA NYUMBA KIWANJA NA KWENYE VYOMBO VYAUSAFIRI

KUZUIYA CHUMA ULETE KUSAFISHA NYOTA NAKUONDOWA MIKOSI PIA ANA PUNGA MARUHANI ANATOWA MAJINI MACHAFU DAWA YA KUACHAPOMBE NASIGARA UTAPATA HUDUMAHII POPOTE ULIPO DUNIANI


CALLING WHATSAPP+255713679496/
Viewing all 104762 articles
Browse latest View live




Latest Images