Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104417 articles
Browse latest View live

Babu Seya Wako Wapi na Papii Kocha?

0
0
Toka Babu Seya na Mtoto wake watoke jela Watu tulitegemea tutasikia wakifanya mengi na pengine kuimba au kufanya matamasha na appearance nyingi ili kukata kiu ya mashabiki zao ambao wamewamiss muda mrefu lakini kinyume chake ..Babu Seya na Mwanamwe toka Watoke wamekuwa kimya na kujichimbia kabisa...Je wameamua kuacha mziki au wanaandaa mabomu mapya?

Lema Afunguka Kutoa Utabiri wa Majibu ya Kakobe Kwa TRA

0
0
Msanii wa muziki wa bongo fleva Juma Jux ambaye sasa anafanya vyema na wimbo wake 'Utaniua' amefunguka na kumpa neno mpenzi wake Vanessa Mdee kuwa katika mwaka 2017 amepambana sana na kufanya kazi kubwa mno katika maisha yake.

Jux na Vanessa kwa sasa wapo pamoja nchini Kenya ambapo leo Vanessa Mdee anategemea kufanya show Kenya na huuu ndiyo ujumbe wa mpenzi wake Jux kwake

"Umepambana sana mwaka huu baby. 'Am so proud of what you have done' pumzika leo (jana) Kesho (leo) tukaweke historia nyingine" aliandika Jux

Maimartha Amfungukia Hamisa Mobeto

0
0
MTANGAZAJI maarufu Bongo, Maimartha Jesse ameibuka na kusema ataendelea kumfunda mwanamitindo Hamisa Mobeto ingawa amemjibu vibaya, kwani alichoamua ni kumshauri kwani anaona anakoelekea siko.

Akiongea na Risasi Jumamosi, Maimartha alisema kuwa alimshauri Hamisa kuwa makini kwani kuwa mgeni rasmi kwenye tamasha la Gal Power lililofanyika Uganda hivi karibuni halikuwa na hadhi yake na ilionekana yupo kwenye kushindana na Zarinah Hassan ambaye hamuwezi.

“Kiukweli niliamua kumshauri na nitaendelea kumshauri ingawa alinijibu vibaya, lakini naamini ujumbe umemfikia na anatakiwa ajirekebishe na lile tamasha halikuwa na hadhi yake,” alisema Maimartha.

Hata hivyo, Maimartha alisema ataendelea kuwapa Kitchen Party mastaa mbalimbali ambao wanaonekana kwenda kinyume na wanavyotakiwa kuwa na anaomba watu mbalimbali wanaokerwa na tabia zao wapige kelele za kupinga ili zisiendelee.

Manchester United yapata matokeo mabovu

0
0
Klabu ya Manchester United bado imeendelea kupata matokeo mabovu kwenye Ligi Kuu soka England baada ya jana kulazimishwa sare ya bila kufungana dhidi ya klabu ya Southampton.

Kwa matokeo hayo Manchester United ambayo ilikuwa nafasi ya pili kwa muda mrefu kwenye msimamo wa EPL imeshuka hadi nafasi ya tatu baada ya Chelsea jana kupata ushindi mnono.

Wakati hayo yakitokea Manchester United imepata janga lingine kubwa zaidi kwa kuumia mchezaji wao tegemezi, Paul Pogba jana kwenye mchezo huo.

Pia kupitia mtandao wa klabu hiyo umethibitisha kuwa mshambuliaji wao Zlatan Ibrahimović kuwa atakuwa nje ya uwanja kwa mwezi mmoja kuanzia jana.

Matokeo hayo yanaifanya Manchester United kupata sare tatu mfululizo kwenye EPL na kupoteza mechi moja ya kombe la EFL.

Matokeo mengine ya ya mechi za jana za EPL ni kama ifuatavyo

Freeman Mbowe Adai Kama Serikali Inaona Upinzani ni Hasara Basi Waufute

0
0

Mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Mbowe amesema kama serikali na CCM wanaamini upinzani ni hasara kwa nchi wana wingi wa kutosha katika bunge, wapitishe sheria wavifute.

Amesema pia viongozi wa dini wana uhuru wa kutoa mawazo yao na wana wajibu wa kusema, wakiona serikali au vyama vya upinzani vinakosea

Habari Njema: Tunatibu Busha, Korodani Kuvimba,Ngiri, Miguu Kufa Ganzi Pamoja na Matatizo ya Nguvu za Kiume

0
0
Ni dawa ya nguvu za kiume inayorefusha na kunenepesha uume saizi uipendayo (Inch 1-7) kwa muda wa siku 6 tu.Dozi hii itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa muda wa dakika 30, utarudia tendo la ndoa zaidi ya mara 4 bila hamu kuisha bila kujali umri na garantee ni miaka 60 baada ya kutibu tatizo.

Pia tunatibu Busha bila kufanyiwa Oparesheni, korodani moja kuvimba, ngiri, tumbo kujaa gesi na kuunguruma, kutopata choo vizuri, miguu kuwaka moto na kufa ganzi, chango la wanawake, kisukari na kutokwa na kinyama sehemu ya haja kubwa.

MIHAYO:
Inarudisha mke, mchumba, hawara na atakutimizia kila kitu unachotaka kutoka kwake ndani ya  saa 2 tu hata kama yupo mbali. atarudi na kumfunga asiwe na mwingine zaidi yako.

Umefukuzwa kazini? unataka kupandishwa cheo? Umepoteza pesa zako kwenye biashara bila kujua umepandikizwa chuma ulete? Njoo urudishe pesa zako. Unauza mali yako haiendi? Wasiliana na mtaalam Challo kwa; 0714006521

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumatatu ya January 1 , 2018.....Ni Mwaka Mpya !....

0
0


Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumatatu ya January 1 , 2018.....Ni Mwaka Mpya !....

Tundu Lissu kupelekwa Ulaya kwa matibabu Januari 6

0
0
Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo, Freeman Mbowe ameeleza kuwa hali ya Mbunge Tundu Lissu anayepatiwa matibabu katika Hospitali ya Nairobi nchini Kenya, imeimarika na hivi karibuni atahamishiwa katika hospitali nyingine kwa ajili ya mazoezi ya viungo.

“Tiba zote ameshamaliza kinachoendelea sasa ni mazoezi,” amesema Freeman Mbowe.

Mbowe amesema hayo leo, Disemba 31, 2017 wakati akizungumza na waandishi wa habari na kueleza kuwa tarehe 6 Januari, 208 Tundu Lissu atasafirishwa kupelekwa katika nchi moja ya Ulaya ambayo hakuitaja kwa kile kilichotajwa kuwa ni kwa sababu za kiusalama.

“Kwa sasa siwezi kuitaja nchi anakokwenda kwa ajili ya usalama,” amesema Mbowe.

Amesema gharama zilizotumika hadi sasa kumuuguza ni dola 300,000 za Marekani sawa na zaidi ya Sh 600 milioni.

Ikiwa ni siku zaidi ya 100, tokea Mbunge Tundu Lissu aliposhambuliwa kwa risasi eneo la nyumbani kwake, Area D, Dododma, majira ya saa 7 mchana, akiwa anatokea kazini, kwa sasa hali yake imeimarika ambapo picha za mwisho kutumwa kwenye mitandao mbalimbali ya kijamii, zilimuonyesha akiwa amekaa mwenyewe juu ya kitanda cha Hospitali.

Kigwangalla:Tukimpeleka Askofu Kakobe Mahakamani Atatushinda

0
0
Waziri wa Maliasili na Utalii Dkt. Hamisi Kigwangalla amesema kuwa ukimpeleka mahakamani Askofu Zacharia Kakobe atashinda kwasababu watu wanasema inawezekana anasumbuliwa na ugonjwa wa akili.

Kigwangalla ameyasema hayo leo kupitia ukurasa wake wa mtandao wa Twitter ambapo ameeleza kuwa ugonjwa unaotajwa kuwa huenda unamsumbua Kakobe dalili zake ni kujisifia.

Kigwangalla amefafanua aina ya ugonjwa huo wa akili ambao inawezekana unamsumbua Askofu Kakobe kuwa ni 'Bipolar Disorder: Currently Mania’. Pia amesisitiza kuwa hata ukimpeleka mahakamani anaweza akashinda kwa kigezo hicho.

''Kuhangaika na mtu kama KAKOBE  ni kupoteza muda bure. Kuna watu wanasema inawezekana akawa na ugonjwa wa akili ‘Bipolar Disorder: Currently Mania’ ambao katika dalili zake ni ‘delusions of grandeur’ . Akipelekwa mahakamani anaweza kutetewa kwa kigezo hiki na akashinda!'' ameandika Kigwangalla.

Nape Nnauye Aponda Hamahama ya Wanasiasa

0
0
Mbunge wa Mtama (CCM), Nape Nnauye amehoji sababu za vyama vya siasa kuhangaika kupokea wanachama wa vyama vingine, badala ya kushughulika na Watanzania wasio na vyama.

Akizungumza leo Jumapili Desemba 31,2017 katika mahojiano na kituo cha televisheni cha Azam, Nape amesema siku zote amekuwa na msimamo tofauti na wanachama wanaovihama vyama vyao kwa maelezo kuwa unawajenga wanaohama, si vyama.

"Kama tunataka kujenga vyama viwe vya kitaasisi ni lazima kuhamahama lisiwe suala la kawaida. Yaani mtu mpaka anahama watu waseme kweli huyu alistahili kuhama," amesema Nape.

Amesema, "Watanzania wapo zaidi ya 50 milioni, wenye uwezo wa kujiunga na vyama kikatiba wanaweza kuwa zaidi ya 30 milioni, waliopo kwenye vyama wanaweza wasifike 10 milioni. Kwa nini tunakwenda kuhangaika na wanachama wa vyama vingine badala ya kushughulika na Watanzania wasio na vyama. Tushughulike kuwashawishi hawa."

Katika kipindi hicho, mwenyekiti wa kamati ya uongozi ya Chama cha Wananchi (CUF), Julius Mtatiro na mwanahabari mkongwe, Dk Gideon Shoo waliungana na Nape kukosoa vitendo vya wanachama kuvihama vyama vyao.

Kwa mtazamo wao, hamahama ya wanasiasa ni miongoni mwa kasoro zilizojitokeza mwaka 2017.

PPF wazungumzia kukamatwa kwa mfanyakazi wao na mirungi

0
0
Mfuko wa Pensheni wa PPF umesema mfanyakazi wake, Anitha Oswald, wa ofisi ndogo ya Moshi aliyekamatwa wiki hii akiwa na madawa ya kulevya aina ya mirungi huko Moshi, Kilimanjaro, alikuwa kwenye likizo ya dharura na kwamba alikamatwa akiwa kwenye gari lake binafsi na nje ya eneo la kazi.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na PPF vyombo vya habari na Meneja Uhusiano  leo, shirika hilo limesema tuhuma hizo zinamkabili mfanyakazi huyo yeye binafsi na si PPF.  Vilevile limelaani vitendo vya aina hiyo na linaunga mkono juhudi za serikali za kupiga vita madawa hayo.

Shirika pia limemchukulia hatua mfanyakazi huyo kwa kuzingatia sera za wafanyakazi wake.

Miujiza ya Sharifu Seif Mohamed..JE Umeachwa na Mme/Mke au Mpenzi, Umesongwa na Mitihani ya Maisha..Piga Simu Upate Muujiza Wako

0
0
SHARIFU SEIF MOHAMED ANAWASHUKURU WALE WOTE WANAOENDELEA KUPIGA SIMU, WENYE MATATIZO NA WALE WANAOTOA  SHUKRANI NA SHUHUDA JINSI TIBA ZAKE ZINAVYO WASAIDIA,

(Rudisha mahusiano yako ndani ya masaa 72 tu)

SHARIFU MOHAMED Ni  mtaalam na mnajimu maarufu wa nyota na kubashiri mambo yanayo watesa binadamu duniani kote na kupata ufumbuzi, Anatumia kitabu cha QUR'AN, Dawa za Asili, Dawa za Kiarabu na majini kwa kumtuliza mke/mme, mchumba au mpenzi ndani ya masaa 72 tu, na kutatua matatizo yote ya kimaisha,

Je Umeachwa na UMPENDAE awe Mme/Mke na bado unampenda? Je Umekimbiwa na Mmeo/ Mkeo n anaishi na mtu mwingine? Je Umejaribu sehemu nyingi bila mafanikio? Mpigie simu SHARIFU SEIF sasa hivi ujionee Muujiza wa Papo kwa Papo, Anauwezo wa hali ya juu wa kusambaratisha mahusiano yao na kumrejesha kwako haraka sana na Kumfanya Atimize Ahadi zote Ndani ya Muda Mfupi Endapo Utafwata Atakacho Kuelekeza

ANAZO DAWA ZA MAPENZI, NGUVU ZA KIUME, CHANGO NGIRI MAJI NA N.K, ZINDIKO LA NYUMBA NA BIASHARA, PETE ZA BAHATI, HUMALIZA KABISA TATIZO LA NGUVU ZA KIUME NA KUREFUSHA UUME KWA SAIZI UNAYOTAKA, HUZUIA CHUMA ULETE KWENYE BIASHARA, HURUDISHA MALI ZILIZOPOTEA, MAGONJWA SUGU, MIGUU KUWAKA MOTO AU KUFA GANZI, HUTIBU BUSHA BILA KUPASUA, ANAO UWEZO WA KUMRUDISHA ALIE MBALI AU ALIECHUKULIWA MSUKULE, KUPANDISHA NYOTA NA KUSHINDA BAHATI NA SIBU, KASAFISHA NYOTA NA KUKUPA MVUTO WA AJABU, KUTOA NUKSI NA VIFUNGO MBALIMBALI,  MAFANIKIO YA MAISHA NA UTAJIRI BILA MASHARI, NA MENGINE MENGI YA SIRI,

Je UMAHANGAIKA KUPATA MTOTO BILA MAFANIKIO? WASILIANA NA MTAALAMU HUYU KWANI YEYE HUFAULU PALE WOTE WALIPOSHINDWA, PIA UMALIZA KAZI ZILIZO SHINDIKANA NA WATAALAM WENGINE NDANI YA MASAA 24 TU,

(NA ANATIBU KWA NJIA YA SIMU UKIWA NCHI YOYOTE AU MKOA WOWOTE ENDAPO UTAFWATA MAELEKEZO YAKE)

Kwa ushauri na mawasiliano  zaidi Piga SIMU No:

Mobile +255 654-836970
WhatsApp +255 756-033670

Lipumba Ataka Mjadala wa Kitaifa Kuhusu Uchumi

0
0
Mtaalamu wa Uchumi, Profesa Ibrahim Lipumba amesema kuna haja ya kuwa na mjadala wa kitaifa kuhusu uchumi na mustakabali wa Taifa.

Profesa Lipumba ameyasema hayo jana Jumapili Desemba 31,2017 wakati wa mahojiano na kituo cha televisheni cha Azam kujadili hali ya uchumi kwa mwaka 2017.

Alisema kuna haja ya kujadili sera za kiuchumi, namna ya kujenga uchumi unaoongeza ajira kwa wananchi na kutafuta suluhisho la matatizo yanayowakabili Watanzania.

“Tuitishe mjadala wa kitaifa tuje kujadili, tutazame upya sera za kiuchumi, namna ya kujenga uchumi unaoongeza ajira utakaoleta manufaa kwa wananchi wote. Tujadili kimsingi na tutoke na sera ambazo tunaweza kuishauri Serikali nini cha kufanya,” alisema Profesa Lipumba.

Katika mjadala huo, Profesa Lipumba alisema Serikali haiwezi kufanikisha mapinduzi ya viwanda kama haijafanikisha ya kilimo kwa sababu ukuaji wa kilimo ndiyo ukuaji wa sekta nyingine za kiuchumi.

Alisema robo tatu ya Watanzania wanategemea kilimo lakini ukuaji wa sekta hiyo ni mdogo kutokana na Serikali kukiacha nyuma kilimo na kukumbatia sekta nyingine.

Profesa Lipumba alisema kuna changamoto kubwa kwenye kilimo ambazo zinatokana na ukweli kwamba, Serikali haijawekeza vya kutosha kwenye utafiti wa kilimo, mafunzo kwa wakulima na usambazaji wa pembejeo.

“Tujifunze kwa nchi za Asia kama vile China, India na Malaysia, wao wamewekeza kwa wakulima wadogowadogo,” alisema Profesa Lipumba.

Mbunge wa Nzega Mjini, Hussein Bashe aliyeshiriki mjadala huo, alisema mfumo wa elimu wa sasa wa Tanzania unamwandaa mtu kuwa tegemezi badala ya kujitegemea kama ilivyokuwa zamani.

Alisema kuna umuhimu wa kufumuliwa upya kwa mfumo huo tegemezi ili kujenga utakaowafanya vijana wajifunze kujitegemea au ujasiriamali.

Bashe alisema Tanzania ni nchi ya pili Afrika kwa idadi kubwa ya mifugo lakini hakuna dira ya wazi ni wapi pajengwe viwanda.

Akichangia mada ya hali ya uchumi, mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Kimataifa cha Kampala (KIU), Dk Bravious Kahyoza alisema Tanzania haijazalisha ajira za kutosha kwa wananchi kwa sababu ya kusinyaa kwa uchumi.

Alisema Serikali imekuwa ikishindana kukopa na sekta binafsi jambo lililosababisha sekta binafsi kubaki nyuma na kushindwa kuajiri watu wengi kwa sababu ya hali ngumu ya kiuchumi.

lietaka kuwepo uwiano kati ya sera za kifedha na zile za kibajeti ili kuleta matokeo mazuri kwenye uchumi.

“Wataalamu wetu wanapaswa kukaa chini na kuangalia kama tuko kwenye njia sahihi kuelekea mpango wa maendeleo wa miaka mitano na uchumi wa viwanda ifikapo mwaka 2025. Kama hatuko sahihi basi ni vyema tukabadilisha mbinu tunazotumia kufika huko,” alisema.

Kakobe Asema Yuko Tayari Kuchunguzwa Utajiri Wake

0
0
Askofu  mkuu wa kanisa la Full Gospel Bible Fellowship (FGBF) Zakaria Kakobe,  amesema hahofii kuchunguzwa na serikali kuhusiana na ukwasi anaoumiliki na kuongeza kuwa fedha alizonazo ni zaidi ya fedha zinazomilikiwa na serikali nyingi duniani.

Akizungumza wakati wa ibada ya Jumapili kanisani hapo, Askofu Kakobe amesema  hana wasiwasi wa kuchunguzwa utajiri wake na kuongeza kuwa kwa sasa anamiliki pesa nyingi zaidi ya serikali za China na Marekani.

Pia, alitumia fursa hiyo kuwajibu watu wote waliokuwa wakihoji uraia wake.

 " Wanaosema Kakobe amekimbia nchi nawashangaa sana nipo na wala siendi popote, kipindi Fulani walikuja kuchunguza uraia wangu lakini wakaambulia patupu, tutabanana hapa hapa.

" Watu wanasema Niko kimya sana wala sipo kimya tatizo wanataka nizungumze wanayoyataka wao, sasa Mimi sio mtu wa namna hiyo, ukiniona nimesimama katika madhabau Hays basi ujue nina kibali cha Mungu, mtu ukiitwa Mbwa kwani wewe ndio utakua Mbwa? Sasa nashangaa unaogopa nini kuitwa Mbwa wakati wewe sio Mbwa" -Kakobe

Akihubiri wakati wa mkesha wa sikukuu ya Krismasi wiki iliyopita, askofu huyo alisema yeye ni tajiri zaidi ya serikali ya Tanzania.

Katika mahubiri ya leo,  Askofu Kakobe amewaambia waumini wake kuwa utajiri anaomiliki kwa sasa ni zaidi ya serikali nyingi duniani.

Kutana na Mtabibu wa Nyota Duniani Maalim Fadhil Rashid Kutoka Comoro Kwa sasa Yupo Tanzania

0
0

KUTANA NA MTABIBIBU WANYOTA DUNIANIKOTE MAALIM FADHILI RASHIDI KUTOKA COMORO KWA SASA YUPO TANZANIA NI BINGWA WAKUTIBU MARADHI SUGU KAMA VILE MIGUU KUUMA NA KUWAKA MOTO PRESHA KISUKARI VIDONDA VYA TUMBO PUMU

MAALIM FADHILI RASHIDI ANAJUWA UMEHANGAIKA SANA LAKINI HUJAFANIKIWA MUONE HARAKA AKUSAIDIE ANADAWA ZA KI COMRO DAWAZAKE HABAHATISHI MUONE HARAKA AKUSAIDIE TEZI NAUVIMBE TUMBONI ANAUWEZO WAKURUDISHA MTUALIE POTEA KIMAZINGIRA (MSUKURE) KUMFANYA MKE MUME MPENZI ASIKUSALITI DAWA YA (LIMBWATA) KUMTAWALA MPENZI WAKO UNAVYOTAKA KUMUONA MBAYA WAKO LIVE KWASABABI MALUM ANATOA PETE YA BAHATI INAYO ENDANA NA NYOTA YAKO ITAKAYO KULETEA MALI BILA YA MASHARITI NAKUMILIKI MALI ZAMAJINI DAWA YAKUONGEZA UUME ZAIZI UIPENDAYO DAWA YA NGUVU ZAKIUME PIA ANAYO DAWA YAKUONGEZA HIPS SHEPU KUWA NAUMBO BOMBA KAMA UMEIBIWA AMA KUDHULUMIWA UTARUDISHIWA MALIYAKO NDANI YA MASAA (24) ANAFUNGA KESI NAKUPATA HAKIYAKO DAWA YA MVUTO WABIASHARA KUUZA MALIYAKO KWAHARAKA KUZUIYA CHUMAULETE KUSAFISHA NYOTA NAKUTOWA MIKOSI NA KUPANDISHWA CHEO KAZINI KARIBUNI WOTE TIBA NIKWADINI ZOTE UTAPATA HUDUMA POPOTE ULIPO DUNIANI

CALLING +255719362806/

WHATSAPP CALLING +255785786436

Chadema Yawataka Viongozi Wa Dini Kuendelea Kuikosoa Serikali

0
0
Mwenyekiti wa CHADEMA na Kiongozi Mkuu wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni, Freeman Mbowe amewataka Watanzania kuwa tayari kukosolewa na viongozi wa dini kwani ndio wanaoliombea Taifa liwe na amani katika kipindi chote tangu nchi ilipopata Uhuru.

Mbowe ameyasema hayo jana wakati akizungumza na wahariri wa vyombo vya habari kuhusu hali ya kisiasa kwa mwaka 2017, ambapo alisema kila mtu ana mapungufu katika utendaji wake wa kazi hivyo kila mmoja awe tayari kupokea ushauri kutoka kwa viongozi wa dini.

“Lakini viongozi wetu wa dini wana haki ya kusema, wana wajibu wa kusema, hawa ni watu wanaolea Taifa hili kiroho, huwezi kumshambulia Kakobe kama unamshambulia mtoto mdogo, hawa wana waumini wana followers (wafuasi) na hawa ndio kila siku Rais anasema wamwombee, sasa wanamwombea vipi wakati unawapa masharti?,” alisema Mbowe na kuongeza.

“Sisi wapinzani tunakosolewa, viongozi tuwe na unyenyekevu wa kukubali mawazo tofauti tukisemwa, tusijenge chuki katika jamii, vyama vyetu vyote vinaongozwa na binadamu vinaweza vikakosea, tuwaache viongozi wa dini wafanye kazi yao, tukikosea waseme.”

“Ukisikia Kakobe amezungumza, tafakari kwanza kabla ya kumkabili,”

0
0
Askofu Mkuu wa Kanisa la Full Gospel Bible Fellowship (FGBF), Zachary Kakobe amejibu hoja zinazotolewa dhidi yake, baadhi zikitolewqa na Serikali akisema anapozungumza ni lazima kutafakari kabla ya kumkabili.

Askofu Kakobe alizungumza jana wakati wa ibada katika kanisa la FGBF lililopo Mwenge jijini Dar es Salaam.

“Ukisikia Kakobe amezungumza, tafakari kwanza kabla ya kumkabili,” alisema.

Kauli hiyo aliitoa ikiwa ni siku moja baada ya Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) kutangaza kuanzakufuatilia ulipaji wake wa kodi.

Uamuzi wa TRAulitangazwa juzi na Kamishna Mkuu, Charles Kichere mbele ya waandishi wa habari baada ya hivi karibuni Askofu Kakobe kusikika akisema ana fedha nyingi kuliko Serikali.

TRA ilisema uamuzi huo unatokana na kiongozi huyo wa kiroho kutokuwemo katika kumbukumbu za ulipaji kodi za mamlaka hiyo. Mamlaka hiyo ilisema kama utajiri wake unatokana na sadaka pekee litakuwa jambo la kushtua.

Jana, Askofu Kakobe alitumia ibada hiyo kuwajibu TRA na pia alizungumzia mambo mengine mawili; uraia wake na onyo la Serikali la kuwataka viongozi wa dini kutokuzungumzia masuala ya siasa.

“Tangu nilipoitika wito huu miaka 30 iliyopita, sijawahi kufanya biashara yoyote zaidi ya hii na kanisa hili halina mradi wowote wa kiuchumi. Kakobe hana mradi wowote na kama yupo anayejua ajitokeze aseme nitampa zawadi,” alisema Askofu Kakobe.

“Akaunti yetu iko Benki ya NBC na iko chini ya Bodi ya Wadhamini, bodi ambayo imesajiliwa Rita (Wakala wa Usajili, Ufilisi na Udhamini). Kwa hiyo, hao wanaotaka kujua zaidi waende Rita wakaulize wajumbe wa bodi hii ni akina nani na waende NBC kuona vyanzo vyetu vya mapato kama ni tofauti na sadaka.”

Huku akishangiliwa na waumini, alisema tatizo kubwa lililojitokeza nchini ni watu kutafasiri wanavyojua na kujikuta wakipotoka. Alisema hilo ni tatizo watu kutopenda kusoma Biblia kwa undani na kwa upana zaidi.

“Wamemsikia Kakobe anazungumza hapa, anazungumza mambo ya rohoni kuhusu haya ya utajiri. Unaweza kusikia maneno ukatafsiri kivyako kwa sababu haya tunayozungumza hapa ni mambo ya rohoni, wewe unayatafsiri kisiasa,” alisema Kakobe.

“Wanasema wewe una hela kweli kuliko Tanzania sema... ninaweza kuvunja hekalu na kulisimamisha kwa siku tatu. Mtu anajiuliza hekalu gani hili? Hekalu hili ni mwili wake. Maana yake niueni, nisulubisheni, lakini nitakufa na siku ya tatu nitafufuka, hii ndio hekalu, unatafsiri kwa akili.”

Kwa sauti ya juu na yenye msisitizo, Askofu Kakobe alisema: “Kimsingi, mimi si mtu tu tajiri kuliko Serikali, bali ni tajiri kuliko Serikali zote duniani. Kwa hiyo ukisikia Kakobe amezungumza, tafakari kwanza kabla ya kumkabili.”

“Hela yote ya Serikali ya Tanzania au dunia nzima haiwezi kununua tiketi hata moja ya Mbinguni. Mimi ni tajiri kuliko Serikali ya Magufuli (Rais John Magufuli) au Serikali ya Trump (Rais wa Marekani Donald Trump),” alisema.

Alisema nyumba anayoishi iliyopo Kijitonyama karibu na Kituo cha Polisi Mabatini jijini Dar es Salaam aliijenga miaka ya sabini na tangu wakati huo hajawahi kujenga kokote na gari lake ni la kawaida.

Askofu Kakobe alisema maisha yake si ya kifahari kama wasemavyo watu.

Uraia wake
Kuhusu uraia, Askofu Kakobe alisema wazazi wake walikuwa wakiishi Kakonko mkoani Kigoma na baada ya kufariki walizikwa huko, huku uraia wake ukifuatiliwa na ilibainika ni raia halali.

“Baba yangu alikuwa mwalimu kwa kipindi kirefu, amefanya kazi Tanga, Sumbawanga, Usukumani kwa Wanyamwezi, Tabora na Shinyanga. Miongoni mwa watu tuliocheza pamoja katika utoto wetu ni Christopher Chiza, huyu alikuwa waziri,” alisema Kakobe.

“Ukitaja kwa jumla familia yetu, inajulikana miaka mingi. Walikwenda kuchunguza uraia wangu na kujiridhisha pasina shaka na kusema huyu ni Mtanzania. Kuna kipindi watu walikwenda mara tatu kijijini kwangu Kakonko kuchunguza uraia.”

Waumini wakiwa kimya wakimsikiliza, Askofu Kakobe alisema, ‘’ Nimezaliwa Tanzania, wazazi wangu wamezaliwa Tanzania, mimi ni Mtanzania kwa hiyo sitoki hapa, tutabanana hapa hana.”

“Baada ya kuona, yote hayo, mara waende huku, waende huko waulize wazazi wangu ambao wamefariki hivi karibuni na makaburi yapo kijijini na niliwaambia makaburi wayaweke barabarani ili anayechunguza uraia wangu aanzie pale,” alisema.

Alisema, ‘’Kila jambo chini ya mbingu kuna kusudi, kuna kusudi la Mungu mimi kuzaliwa Tanzania, kwa hiyo wanaosema nimetoroka hawanisumbui kichwa.”

Kuhusu taarifa za kutoroka nchini alisema: “Ninapokwenda na kurudi washirika wa hapa wanajua. Kwa mfano safari ya mwisho ilikuwa Agosti (mwaka jana) na tangu hapo sijasafiri. Niko hapa na haya mengine nayasikia nimetoroka, hayanisumbui, ukiitwa majina si yako unasumbukia nini?”

Mauaji ya Watu Wanne Mkesha wa Mwaka Mpya Zanzibar

0
0

ZANZIBAR: Watu wanne akiwemo mzee wa miaka 60 ambaye ni raia wa Ujerumani wameuawa kwenye matukio tofauti wakati wa kusherehekea mkesha wa mwaka mpya visiwani humo.

Mpaka sasa watu wanne wanashikiliwa na Jeshi la Polisi visiwani humo wakihusishwa na mauaji hayo huku uchunguzi ukiendelea

atalii 10 ambao ni Raia wa Marekani Wafariki Dunia Baada ya Ndege Kuanguka na Kulipuka

0
0

COSTA RICA: Watalii 10 ambao ni Raia wa Marekani pamoja na Marubani 2 wa Costa Rica wamefariki dunia baada ya ndege waliyokuwa wakisafiria kuanguka na kulipuka Jumapili ya jana
-
Watano kati yao wamebainika ni ndugu kutokana na majina yao ya mwisho kufanana
-
Watalii hao walikodisha ndege na kutembelea eneo maarufu la kivutio lenye ufukwe na msitu la Guanacaste linalopatikana nchini humo
-
Chanzo cha hitilafu iliyosababisha ajali hiyo bado hakijafahamika

Tundu Lissu: Walionipiga risasi niliwaona lakini siwafahamu

0
0
HALI ya Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu inaendelea kuimarika huku akiendelea na mazoezi ya viungo katika Hospitali ya Nairobi nchini Kenya ambako anapatiwa matibabu ya majeraha aliyoyapata baada ya kushambuliwa kwa risasi nyumbani kwake Area D, mjini Dodoma mnamo Septemba 7, 2017.

Akizungumzakatika mahojiano maalum na Kituo cha Runinga cha Azam TV, Lissu ameeleza namna alivyoshambuliwa huku akisema kuwa watu waliotekeleza tukio hilo la kinyama dhidi yake aliwaona japo hawajui,” alisema Lissu.

Watu walionishambulia kwa risasi niliwaona lakini siwafahamu, nilikuwa nina jitambua mpaka muda nafikishwa Hospitali ya Dodoma, na mtu wa kwanza kumpigia simu alikuwa ni Mwenyekiti wangu wa Chadema, Freeman Mbowe. Dereva wangu ndiye alinisaidia kuwasiliana naye pamoja na watu wengine kuwapa taarifa hizo.

Aidha Lissu amewashukuru madaktari wa Dodoma na wa Hospitali ya Nairobi kwa kufanya jitihada zao kuokosa maisha yake.

“Nisingefika Nairobi bila msaada wa kwanza wa Madaktari wa Dodoma, nilipofika Nairobi Hospital madaktari walifanya kazi kubwa sana kunitibu na kuokoa maisha yangu hadi kufikia hapa nilipo leo.
Madaktari wametoa risasi 16 mwilini mwangu tangu nimefika hapa Hospitali ya Nairobi, risasi moja bado ipo mwilini na risasi zingine 16 zilinikosa siku hiyo ya tukio,” alifafanua Lissu.
Viewing all 104417 articles
Browse latest View live




Latest Images