Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104785 articles
Browse latest View live

Katibu Mkuu wa CUF, Maalim Seif ammwagia sifa Rais Dkt Magufuli

$
0
0
Katibu Mkuu wa Chama cha Wananchi (CUF), Maalim Seif Sharif Hamad, amempongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. John Magufuli, kwa kuiongoza nchi vizuri kwa mwaka uliopita wa 2017.

Seif ametoa pongezi hizo katika salamu zake za mwisho wa mwaka ambapo alisema kwamba, kwa mwaka 2017, Rais Magufuli ameweza kuiongoza nchi vizuri kwa kudhibiti rushwa pamoja na ubadhirifu wa mali za umma.

Akitolea ufafanuzi suala la makinikia, Seif alisema kuwa, Rais Magufuli ameweza kupigania rasilimali za nchi hasa madini ili kuhakikisha wananchi wote wanafaidika, hatua ambayo amefanikiwa kwa kiasi kikubwa.

Kiongozi huyo wa upinzani alisema, licha ya kuwa rushwa bado haijaisha, lakini juhudi zilizofanywa haziwezi kubezwa kwani imepungua ikilinganishwa na kipindi cha serikali ya awamu ya nne.

Pia, aliwataka wanasiasa kutokuona shida kusifia mazuri ambayo yamefanywa na serikali wakati wakifanya tathmini ya mwaka 2017. Seif alieleza namna serikali ilivyowafikisha mahakamani vigogo wa rushwa, kurejesha nidhamu ya fedha lakini pia kuokoa fedha zilizokuwa zikipotea kwa kuwalipa watumishi hewa.

Mbali na hayo, Seif pia alizungumzia changamoto za mwaka 2017 na kusema kuwa, uhuru wa kufanya siasa nchini umebanwa kufuatia kuzuiwa kwa mikutano ya kisiasa pamoja na maandamano.

Lakini akielezea suala la Zanzibar, alisema, ubaguzi katika visiwa hivyo bado ni changamoto kubwa kwani hata ajira zinatolewa kwa kufuata mrengo wa kisiasa badala ya utaalamu wa mtu.

Amber Lulu: Kukaa utupu kumepitwa na wakati

$
0
0
MUUZA nyago ambaye pia ni msanii wa Bongo Fleva, Lulu Augen ‘Amber Lulu’ amefunguka kuwa, kipindi cha kukaa utupu ili mtu apate umaarufu kumepitwa na wakati.

Amber aliliambia Ijumaa Wikienda kuwa, hata yeye alikuwa akifanya kosa la kuacha mwili wake wazi, lakini sasa akili yake imepanuka na hataki kusikia mambo hayo.

“Kuachia wazi sehemu kubwa ya mwili kwa sasa ni ushamba na vitu hivyo vimepitwa na wakati. Hata mimi ninajilaumu sana,” alisema Amber Lulu ambaye awali alikuwa miongoni mwa mastaa waliojiachia utupu na kutupia picha mitandaoni.

Ufupi wa Maisha Wamfanya Mwigizaji Johari Kuokoka

$
0
0
MWIGIZAJI ‘mhenga’ Bongo, Blandina Chagula ‘Johari’ amedai kubadili mfumo wa maisha yake na kuahidi kuokoka ili kujiweka karibu na Mungu, ikiwa ni pamoja na kuachana na maisha ya ajabu kama matumizi ya pombe.

Johari aliliambia Ijumaa Wikienda kuwa, amebaini maisha ni mafupi duniani hivyo ni vyema kujisafishia njia na kumrudia Mungu ambaye ndiye mwokozi wa maisha ya wanadamu.

“Ninaachana kabisa na mambo ya kidunia, sitaki tena pombe wala kujihusisha na maisha mengine yenye kumchukiza Mungu, nimefanya mambo mengi yasiyokuwa mazuri. Kama binadamu, ninajipanga kuwa mpya na ninasema kabisa kwamba nimeokoka,” alisema Johari.

Wananchi wana hali ngumu ya maisha – Mhe. Freeman Mbowe

$
0
0
Mwenyekiti wa CHADEMA Taifa, Mhe. Freeman Mbowe amesema kuwa maisha ya Watanzania yamekuwa magumu kuliko katika kipindi chochote katika historia ya Tanzania.

 Mhe. Mbowe amesema hayo leo jumapili Desemba 31, 2017 jijini Dar es Salaam wakati akizungumza na Waandishi wa Habari.

“Sio siri maisha ya wananchi yamekaza, mimi nimezunguuka nchi hii mikoa mingi, Wananchi wana hali ngumu ya maisha kuliko kipindi chochote katika historia ya nchi yetu,“amesema Mhe. Mbowe huku akifafanua kauli ya kupigwa marufuku kwa matumizi ya neno la vyuma vimekaza.

“Bwana mkubwa hataki neno hili kutumika anasema neno Vyuma vimekaza hataki litumike, Bwana mkubwa yeye vyuma vyake havijakaza kwa sababu halipi umeme, halipii nyumba ya kulala kwa sababu anafanyiwa kila kitu na serikali kwa kodi zetu.“amesema Mhe. Freeman Mbowe.

Maneno ya Wastara kwa Sajuki ‘nitakuwa na wewe kokote niendapo’

$
0
0
Muigizaji wa Filamu nchini Tanzania, Wastara ameupokea mwaka mpya wa 2018 kwa kumkumbuka aliyekuwa mumewe Marehemu Juma Kilowoko Sajuki .


Wastara amesema kila mwaka tarehe kama ya leo (Januari 1) huwa anaitumia kuangalia picha za Sajuki ili kujipa faraja na kitendo hicho kwa sasa kimekuwa kama desturi huku akiahidi kuwa kamwe hatoacha kufanya hivyo.

“Kama kuposti picha zako kila mwanzo wa mwaka huwa kunaniletea shida na matatizo katika maisha yangu Basi wacha tu yanikute niko tayari kuyapokea lakin hakuna wa kusitisha zoezi hili katika maisha yote mpaka nakufa,“ameandika Wastara kwenye ukurasa wake wa Instagram.

Wastara amedai kuwa anajua kitendo cha kufanya hivyo kinawaumiza baadhi ya watu lakini yeye anaamini kuwa ni faraja kwake na anafanya hivyo ili kuwa pamoja na marehemu kiroho.

“Nitakuwa na wewe kokote niendapo japo kiroho inanitosha na kujiona tupo pamoja kwa siku chache ukinipa ile furaha uliyoondokana nayo Mungu akupe kauli thabiti akuondosheee adhabu na mchanga mzito kaburini kwako”ameandika Wastara.

Marehemu Juma Kilowoko Sajuki alifariki Januari 2, 2013 katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili baada ya kuugua kwa muda mrefu.

Video: Wema Sepetu Bila Matukio yasiyo yakawaida sio Wema – Kadinda

$
0
0
Aliyekuwa meneja wa malkia wa filamu, Wema Sepetu, Martin Kadinda amefunguka kwa kusema kuwa matukio mengi ambayo anayafanya Wema Sepetu sio kutafuta kiki kama baadhi ya watu wanavyofikiria bali ndio maisha yake. VIDEO:

Habari Njema: Tunatibu Busha, Korodani Kuvimba,Ngiri, Miguu Kufa Ganzi Pamoja na Matatizo ya Nguvu za Kiume

$
0
0
Ni dawa ya nguvu za kiume inayorefusha na kunenepesha uume saizi uipendayo (Inch 1-7) kwa muda wa siku 6 tu.Dozi hii itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa muda wa dakika 30, utarudia tendo la ndoa zaidi ya mara 4 bila hamu kuisha bila kujali umri na garantee ni miaka 60 baada ya kutibu tatizo.

Pia tunatibu Busha bila kufanyiwa Oparesheni, korodani moja kuvimba, ngiri, tumbo kujaa gesi na kuunguruma, kutopata choo vizuri, miguu kuwaka moto na kufa ganzi, chango la wanawake, kisukari na kutokwa na kinyama sehemu ya haja kubwa.

MIHAYO:
Inarudisha mke, mchumba, hawara na atakutimizia kila kitu unachotaka kutoka kwake ndani ya  saa 2 tu hata kama yupo mbali. atarudi na kumfunga asiwe na mwingine zaidi yako.

Umefukuzwa kazini? unataka kupandishwa cheo? Umepoteza pesa zako kwenye biashara bila kujua umepandikizwa chuma ulete? Njoo urudishe pesa zako. Unauza mali yako haiendi? Wasiliana na mtaalam Challo kwa; 0714006521

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumanne ya January 2

$
0
0

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumanne ya January 2

Polepole: Lema 2020 utalisikia hewani tu jimbo la Arusha Mjini

$
0
0
Katibu wa Itikadi na Uenezi  wa  Chama Cha Mapinduzi CCM, Humphrey Polepole amemtahadharisha Mbunge wa Arusha Mjini Godbless Lema kwakumwambia kuwa  kipindi hiki ni cha mwisho kuongoza Jimbo hilo la Arusha Mjini.

Hayo yamekuja mara baada ya Mbunge huyo kupitia kurasa zake za twitter kujibizana huku Lema akionyesha kumhoji Polepole kama familia yake huwa inamuelewa kweli anachokizungumza.

“Term ya mwisho Arusha, tunataka Mbunge wa Masuala na si wa Matukio, hata mkichezesha draft ili uende Hai, haitawezekana maana hata “fly to…” maji yako shingoni, na ukiamua kurudia kazi yako ya zamani. anko Siro is very serious,”ameandika Polepole

PICHA 3: Baraka Da Prince Alivyomtembelea Tundu Lissu Hospitali

$
0
0
Mwishoni wa mwaka 2017 Mbunge wa Singida Mashariki kupitia tiketi ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA Tundu Lissu aliripotiwa kupigwa risasi na watu wasiojulikana akiwa nyumbani kwake Dodoma.

BREAKING: Whatsapp Imeacha Kufanya Kazi kwa Mataifa Mbalimbali Duniani

$
0
0
Mtu wangu wa nguvu nikusogezee taarifa kuhusiana na Mtandao wa Whatsapp leo December 31, 2017 umekuwa chini kwa mamilioni ya watumiaji ulimwenguni kote, na kusababisha hofu kwa kwa watumiaj hasa kwenye kipindi hiki wakati watu wa nguvu wakiwa wanasubiri Mwaka Mpya.

Watumiaji nchini Uingereza , Barbados, India, Japan, Panama, Afrika Kusini, Hispania, na Qatar wamesema hawakuweza kuungana na programu hiyo kwa kutuma meseji au kupokea wala kuweka Status.

Programu hiyo maarufu ya ujumbe ilitoa tangazo mapema wiki hii na kuelezea kuwa inatazamia kuwa mahiri kwenye mfumo wa iOS na Android kitu ambacho watalaam wanasema kinaweza kuwa kimechangia usumbufu huo unaojitokeza sasa.

“Tunapotarajia  miaka saba ijayo, tunataka kuzingatia jitihada zetu kwenye ambazo simu idadi kubwa ya watu hutumia,” kampuni hiyo imesema katika  majarida mbalimbali.

Mapema kampuni ya Tech imetangaza kuwa kifaa chochote cha BlackBerry kinaendesha BlackBer

“Kitufe cha Nyuklia Kipo Mezani Kwangu, Marekani isithubutu”- Rais Korea Kaskazini

$
0
0
Korea Kaskazini Kim Jong-Un amelihutubia Taifa lake January 1, 2018 katika sherehe za mwaka mpyahotuba ambayo imerushwa LIVE na vituo mbalimbali vya television nchi humo.

Kim Jong-Un amesema kuwa ana kitufe cha kubonyeza cha silaha za nyuklia kipo kwenye meza yake wakati wowote anaweza kukitumia, hivyo Marekani isithubutu kuanza vita.

“Marekani inaweza kufikiwa na silaha za nyuklia za Korea Kaskazini, kweli na wala sio vitisho.” – Kim Jong-un

Mbali na hilo, pia Kim ametoa wito kwa Korea Kusini kwamba anawakaribisha kwenye mazungumzo.

Taifa la Korea Kaskazini limewekewa vikwazo zaidi mwaka uliopita 2017 kutokana na mipango yake ya silaha za nyuklia na majaribio ya mara kwa mara ya silaha hizo.

Soma Nafasi za Ajira Zilizotangazwa Leo Jumanne

Miujiza ya Sharifu Seif Mohamed..JE Umeachwa na Mme/Mke au Mpenzi, Umesongwa na Mitihani ya Maisha..Piga Simu Upate Muujiza Wako

$
0
0

SHARIFU SEIF MOHAMED ANAWASHUKURU WALE WOTE WANAOENDELEA KUPIGA SIMU, WENYE MATATIZO NA WALE WANAOTOA  SHUKRANI NA SHUHUDA JINSI TIBA ZAKE ZINAVYO WASAIDIA,

(Rudisha mahusiano yako ndani ya masaa 72 tu)

SHARIFU MOHAMED Ni  mtaalam na mnajimu maarufu wa nyota na kubashiri mambo yanayo watesa binadamu duniani kote na kupata ufumbuzi, Anatumia kitabu cha QUR'AN, Dawa za Asili, Dawa za Kiarabu na majini kwa kumtuliza mke/mme, mchumba au mpenzi ndani ya masaa 72 tu, na kutatua matatizo yote ya kimaisha,

Je Umeachwa na UMPENDAE awe Mme/Mke na bado unampenda? Je Umekimbiwa na Mmeo/ Mkeo n anaishi na mtu mwingine? Je Umejaribu sehemu nyingi bila mafanikio? Mpigie simu SHARIFU SEIF sasa hivi ujionee Muujiza wa Papo kwa Papo, Anauwezo wa hali ya juu wa kusambaratisha mahusiano yao na kumrejesha kwako haraka sana na Kumfanya Atimize Ahadi zote Ndani ya Muda Mfupi Endapo Utafwata Atakacho Kuelekeza

ANAZO DAWA ZA MAPENZI, NGUVU ZA KIUME, CHANGO NGIRI MAJI NA N.K, ZINDIKO LA NYUMBA NA BIASHARA, PETE ZA BAHATI, HUMALIZA KABISA TATIZO LA NGUVU ZA KIUME NA KUREFUSHA UUME KWA SAIZI UNAYOTAKA, HUZUIA CHUMA ULETE KWENYE BIASHARA, HURUDISHA MALI ZILIZOPOTEA, MAGONJWA SUGU, MIGUU KUWAKA MOTO AU KUFA GANZI, HUTIBU BUSHA BILA KUPASUA, ANAO UWEZO WA KUMRUDISHA ALIE MBALI AU ALIECHUKULIWA MSUKULE, KUPANDISHA NYOTA NA KUSHINDA BAHATI NA SIBU, KASAFISHA NYOTA NA KUKUPA MVUTO WA AJABU, KUTOA NUKSI NA VIFUNGO MBALIMBALI,  MAFANIKIO YA MAISHA NA UTAJIRI BILA MASHARI, NA MENGINE MENGI YA SIRI,

Je UMAHANGAIKA KUPATA MTOTO BILA MAFANIKIO? WASILIANA NA MTAALAMU HUYU KWANI YEYE HUFAULU PALE WOTE WALIPOSHINDWA, PIA UMALIZA KAZI ZILIZO SHINDIKANA NA WATAALAM WENGINE NDANI YA MASAA 24 TU,

(NA ANATIBU KWA NJIA YA SIMU UKIWA NCHI YOYOTE AU MKOA WOWOTE ENDAPO UTAFWATA MAELEKEZO YAKE)

Kwa ushauri na mawasiliano  zaidi Piga SIMU No:

Mobile +255 654-836970
WhatsApp +255 756-033670 

Uchangudoa wa Zari Waibua Kimbembe

$
0
0
MAMBO ni moto! Ndivyo unavyoweza kusema baada ya mfanyabiashara maarufu Afrika Mashariki, Zarinah Hassan ‘Zari The Boss Lady’ kukiri kuwa yeye ni changudoa mzee, kauli yake imeibua kimbembe.

KUPITIA SNAPCHAT
Kupitia mtandao wake wa kijamii wa Snapchat, mwishoni mwa wiki iliyopita, Zari alitupia ujumbe akionesha kuwa yeye ni changudoa mzee, lakini mwenye mafanikio akimjibu hasimu wake, mwanamitindo Hamisa Mobeto bila kumtaja. “Bora mimi changudoa mzee niliye na mafanikio na bado ananipenda kuliko kijana wa miaka 20+, mama uliyeachwa mara mbili na tuzo juu,” alisema Zari kupitia Snapchat. Kwa muda mrefu, Zari amekuwa kwenye tifu la aina yake baada ya Mobeto kuzaa na bwana wake, msanii wa Bongo Fleva miezi michache iliyopita.

KIBEMBE KILIVYOIBUKA
Kitendo cha Zari kutoa kauli hiyo, kimbembe kiliibuka mtandaoni mara baada ya ukurasa wa Instagram wa Global Publisher, kutupia habari hiyo ambapo wafausi wa mtandao huo walianza kurushiana maneno makali huku kila mmoja akitoa msimamo wake.

AUNGWA MKONO, AKOSOLEWA
Kuna ambao waliunga mkono kauli hiyo kwa kile walichosema kwamba aliandika kwa maana ya kumkejeli Mobeto, lakini si kwamba ni kweli yeye ni changudoa, lakini wengine walicharuka na kusema kweli yeye ni changudoa. “Jamani Zari siyo changudoa acheni kumshambulia kwa matusi. Yule amesema vile kama kumkejeli Mobeto ambaye aliingia kwenye anga zake, watu wengine sijui mkoje, mmekalia ujingaujinga tu,” alichangia shabiki mmoja mtandaoni akimkingia kifua Zari.
Baada ya shabiki huyo kumtetea Zari, wengine waliibuka na kumshambulia mama huyo wa watoto watano kwa kile walichosema kwamba kweli mrembo huyo wa Uganda ni changudoa aliyejivisha ‘ngozi’ ya ustarabu. “Acheni mambo ya kipuuzi…hivi mnafikiri Zari ana hela kama inavyodaiwa? Yule ni changuduoa tu kama walivyo machangu wengine na kama yeye mwenyewe alivyosema. Sema kinachompa hadhi yeye anajiuza kwa staha tofauti na wenzake wanaojipanga barabarani.

UTAJIRI WAKE WAHUSISHWA
“Kule Sauz (Afrika Kusini) mnavyoona anaishi kwenye majumba ya kifahari, anavyoonekana ana magari mapya kila siku mnafikiri yale ni jasho lake? Uchangudoa tu ule ndiyo unaompa utajiri wote alionao, yule msanii anajiona amepata kumbe amepatikana,” alisema shabiki huyo.
Mvutano huo ambao hadi tunakwenda mitamboni ulikuwa ukiendelea kwenye ukurasa huo wa Global Publishers unaaongoza kwa kutembelewa na watu wengi ndani na nje ya Bongo, ulisababisha watu kurushiana matusi ya nguoni huku wengine wakienda mbali kwa kutaka kutafutana uso kwa uso, nje ya mtandao huo wa Instagram ili wapeane ngumi kavukavu.

MWENYEWE AANIKA UKWELI
Baada ya kauli hiyo kuibua kimbembe, Zari amekuwa amewatolea uvivu kwa kuonesha namna ambavyo ni mchapakazi kupitia ofisi zake mbalimbali zinazomuingizia kipato halali tofauti na watu wanavyofikiri na kuweka mawazo yao kwenye mitandao ya kijamii.
Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Zari amekuwa akionesha picha za maduka yake ya nguo yaliyopo Afrika Kusini kwa kusindikiza na meseji mbalimbali zinazoashiria kwamba yeye si mtu wa mchezomchezo linapokuja suala la uwajibikaji. Ameonesha kwamba anatenga muda wake kwa kuwa bize na kazi, lakini pia anatenga muda wake kwa ajili ya kufurahia maisha kwa maana ya kuponda starehe katika viunga mbalimbali pande za Sauz na nyumbani kwao, Uganda.

ANA VYUO SAUZ
Kama hiyo haitoshi, kupitia mahojiano yake ambayo yapo kwenye mtandao wa Kijamii wa You Tube, Zari alifunguka kuwa anavyo vyuo vya urembo na masuala ya ulinzi. Pamoja na hayo, amekuwa amekuwa akizungumzia mafanikio mbalimbali anayoyapata kupitia matamasha yake makubwa hususan lile la Zari All White Party ambalo linampa mkwanja mrefu kila mwaka.
STORI: Erick Evarist, Dar IJUMAA WIKIENDA

Ikulu Yafunguka Kutoapishwa Kwa Dr Willibrod Slaa Baada ya Kuteuliwa Kuwa Balozi

$
0
0
WAKATI zikiwa zimetimia siku 40 baada ya kuteuliwa kuwa balozi, Dk. Willibrod Slaa (pichani), hajaapishwa na kuzua minong’ono hatimaye Ikulu imefunguka na kuweka kila kitu wazi.
Itakumbukwa kuwa Rais Dk. John Magufuli alitangaza uteuzi wa Dk. Slaa kushika nafasi ya ubalozi Novemba 23, mwaka jana, lakini tangu wakati huo hajaapishwa.

Rais Magufuli amekuwa na utamaduni wa kuteua viongozi na baada ya siku chache wanaapishwa, lakini kwa Dk. Slaa imechukua muda mrefu na kuibua sintofahamu.
“Hili ni jambo ambalo siyo la kawaida, tumezoea mtu akiteuliwa kushika wadhifa fulani na rais baada ya siku chache, tunaona au kusikia kuwa ameapishwa, lakini kwa Dk Slaa ni zaidi ya mwezi sasa, kuna sababu zimetolewa? Tujulisheni,” ni moja kati ya simu nyingi za wasomaji wetu waliopiga chumba cha habari kutaka ufafanuzi.

Kutokana na hali hiyo, Uwazi liliwasiliana na Kurugenzi ya Mawasiliano Ikulu ili kujua kwa nini imechukua muda mrefu kumuapisha Dk. Slaa.
Mkurugenzi wa Mawasiliano Ikulu, Gerson Msigwa, aliliambia gazeti kwa njia ya simu kuwa, si Dk. Slaa peke yake ambaye hajaapishwa.

“Utaratibu ukikamilika ataapishwa. Na sio yeye peke yake ambaye hajaapishwa,” alisema kwa kifupi Msigwa bila kuingia kwa undani zaidi kuhusu suala hilo.
Siku chache baada ya kutangazwa kushika nafasi hiyo, Dk. Slaa alikaririwa akisema anashukuru Mungu kwa kuteuliwa na rais.

Dk. Slaa kwa sasa yupo Canada na alitimkia nchini humo baada ya kutangaza kujiuzulu nafasi ya ukatibu mkuu Chadema.
Aliondoka Chadema baada ya kuwepo sintofahamu kati ya viongozi wa chama hicho, baada ya kumpokea waziri mkuu wa zamani, Edward Lowassa aliyehama CCM.
Lowassa ndiye alipewa baraka za kupeperusha bendera ya urais kupitia Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa) iliyoshirikisha vyama vya Chadema, CUF, NCCR na NLD katika Uchaguzi Mkuu wa 2015.

Pamoja na kupewa ridhaa hiyo, alishindwa kufurukuta na hatimaye Dk. Magufuli kuibuka kidedea kwa nafasi ya urais kupitia CCM.
Itakumbukwa kuwa jina la Dk. Slaa lilianza kufahamika nchini kwa kasi kubwa wakati akiwa mbunge wa Jimbo la Karatu kupitia Chadema.

Kufahamika huko kulitokana na kusimama kidete kupiga vita rushwa kiasi kwamba alitetemesha baadhi ya viongozi waliokuwa madarakani kwani aliwataja.

Uhodari wake katika vita hiyo unaelezwa kuwa ndiyo uliomfanya Rais Magufuli kuguswa naye kiutendaji na kumteua kushika nafasi hiyo.
Dk. Slaa ana historia ndefu ya uongozi kwani aliwahi kuwa Katibu Mkuu wa Baraza la Maaskofu Tanzania (TEC) alipokuwa padre kabla ya kuingia kwenye siasa.

Baraza hilo ni chombo cha juu katika masuala mbalimbali ya usimamizi wa mambo ya Kanisa Katoliki nchini.
Katika andiko la Profesa Kitila Mkumbo ambaye kwa sasa ni Katibu Mkuu Wizara ya Maji na Umwagiliaji ni kwamba, Dk. Slaa alijitoa rasmi kwenye upadri mwaka 1991.
Kwa mujibu wa andiko hilo, Dk. Slaa aliacha nafasi hiyo kwa kufuata taratibu kamili za Kanisa Katoliki na aliacha mwenyewe bila kushinikizwa, kufukuzwa au kupewa onyo.

Wasifu wa Mchora Katuni Masoud Kipanya

$
0
0
Wengi humfahamu kwa jina la Masoud Kipanya, lakini hilo si jina lake halisi, tunaweza kusema hilo ni jina lake la sanaa kwani limetokana na na katuni za Kipanya ambazo huwa anachora.

Jina lake ni i Ali Masoud, jina la Kipanya ni matokeo ya katuni ya Kipanya aliyoibuni zaidi ya miaka 28 iliyopita. Alizaliwa tareha 23 Juni 1972 jijini Dar es salaam.

Kipanya alianza kuchora katuni akiwa darasa la pili, na alianza kwa kuiga tu katuni za ndani na za nje kama ilivyo kawaida kwa yoyote anayeanza kufanya kitu, ila ‘professionally’ alianza rasmi mwaka 1988, huo ndio mwaka ambao katuni yake ya kwanza ilitoka katika gazeti la Heko.

Amewahi kufanya kazi kama mhariri wa katuni kwenye gazeti la Sanifu na mhariri mtendaji wa katuni gazeti la majira, pia katuni zake hutokea gazeti la Mwananchi.

Licha ya kujizolea umaarufu mkubwa katika uchoraji katuni, katika familia yake hakukuwa na mchoraji kabla yangu, isipokuwa baada ya yeye, mdogo wake naye ameshaanza kuja juu katika fani ya katuni. Licha ya kuwa wazazi wake si wachoraji, lakini mfumo wa maisha yao unatosha kabisa kusema nao pia ni wasanii.

Akizungumzia kazi yake ya uchoraji katuni, Kipanya alisema kuwa, changamoto kubwa anayokumbana nayo ni censorship. Kwa wasioelewa, censorship ni ile kitendo ambacho unachora katuni halafu kabla haijachapishwa inapitiwa na kama itaonekana ina madhara kwa mtu ama jamii Fulani, basi itarekebishwa ama isichapishwe kabisa.

Amesema hayo yamemtokea mara nyingi tu katika maisha yake akiwa katika magazeti mbalimbali. Mara nyingi censorship hutokea pale inapoonekana unachora katuni zinazosumbua mioyo ya walengwa hususani wanasiasa wasiopenda kukosolewa.

Alipoulizwa kama amewahi kupata misukosuko kutokana na katuni zake, Masoud alisema, “nakumbuka siku niliyomchora mtu mnene akiwa amemshika kamba iliyomfunga mbwa ambaye ameandikwa ‘polisi’, maana ya katuni hii ukiangalia kwa haraka haraka ni kwamba jeshi la polisi haliko kwa manufaa ya umma bali kwa manufaa ya watu wachache hasa viongozi wa chama tawala.Hiki kilikuwa ni kile kipindi ambacho wapinzani walikuwa wakibughudhiwa na polisi kila walipotaka kufanya mikutano yao ya hadhara.”

“La pili ni wakati ule mbunge mmoja aliyejulikana kwa jina la Tuntemeke Sanga alipokuwa anaumwa, nilichora katuni inayomuonyesha mheshimiwa Sanga akiwa amelazwa huku akiwa ametundikiwa damu, halafu pembeni yuko serikali akiwa amegeukia upande mwingine huku akivuta sigara kana kwamba hajali, bahati mbaya siku iliyofuata Mzee Sanga akafariki, naikumbuka siku hiyo vizuri, aliyekuwa katibu wa bunge wa wakati huo, Mzee Mlawa, alivamia ofisi za gazeti la majira, bahati nzuri, wakati anaingia mimi nikawa natoka, na pengine kutokana na umbo langu, hakuweza kudhani kwamba pengine huyu ndio masoud kipanya. Kilichoendelea kati yake na mhariri wangu kwa kweli sikukifahamu.”

“Alarm inaniamsha saa 11 alfajiri, naoga, navaa na kuelekea studio. Naanza kipindi saa 12 mpaka 3 asubuhi, baada ya hapo napumzisha akili kwa kama nusu saa kwa kupitia magazeti mbalimbali then naanza kufikiria wazo la katuni, wakati mwingine kama sina wazo hunichukua mpaka nusu saa kudevelop wazo la katuni, by saa 4 asubuhi naanza kuchora editorial cartoon. Huwa natumia mpaka masaa mawili kutegemeana na aina ya katuni, baada ya hapo, saa sita mchana namkabidhi dereva (wa taxi, sio wangu jamani) apaleke katuni ofisi za gazeti la mwananchi kwa ajili ya kesho yake. Baada ya hapo nageukia upande wa illustrations, mara nyingi huwa nina kazi za taasisi mbalimbali za ku-Simplify text into cartoons kwa ajili popular versions za machapisho mbalimbali ya ndani na nje ya nchi. By saa 8 mchana huwa nimemaliza, kama kunakuwa na mikutano ofisini naingia, kwa kifupi by saa 10 jioni nakuwa nimemaliza ingawa wakati mwingine humaliza jioni zaidi, baada ya hapo narudi nyumbani kwa ajili ya kubadilisha nguo then naenda mazoezini. Nikitoka mazoezini huwa sitoki tena nyumbani,” alisimulia Kipanya wakati akijibu kuhusu ratiba yake kwa siku.

Kipanya, ameshiriki maonyesho mbalimbali Tanzania na Afrika Kusini kama mtaalam wa matumizi ya rangi ‘Painter’ na amejishindia tuzo nyingi ikiwa pamoja na tuzo ya kwanza ya katuni Afrika Mashariki.

Mbali na kuchora katuni, Kipanya ni mtangazaji wa kipindi cha Power Breakfast cha Clouds FM, ni mwanamitindo lakini pia ndiye mbunifu wa vipindi vya runinga vya ‘Maisha Plus’ na ‘Inawezekana.’

Fahamu Vyanzo vya Utajiri vya Wachungaji Wengi

$
0
0
 Mchungaji ni kiongozi mwenye jukumu la kuwalinda na kuwaongoza waumini wake, kwa mafundisho mbalimbali ya kiroho. Jina hili siyo geni katika masikio ya wengi.

Wachungaji jukumu lao kubwa ni kuhakikisha kuwa waumini wanapewa mafundisho ya kiroho ya namna ya kuenenda na kuishi kufuata maagizo waliyopewa na Mungu.

Katika makala hii, tunajaribu kuangalia namna ambavyo baadhi ya wachungaji hutumia njia mbali mbali kuhakikisha kuwa wanajiingizia kipato na kujipatia utajiri kupitia kanisa.

Hapa naomba ieleweke kuwa, siyo wachungaji wote wanaotumia mbinu hizi kujipatia utajiri, wapo ambao ni waaminifu na hutumia kwa kasi walichopangiwa. Lakini wapo baadhi ambao utakuta wanaishi maisha ya raha, wanafuja fedha, wanamiliki magari ya thamani, wanaishii katika nyumba za kifahari n.k. hawa ndio tunaowazungumzia hapa.

Katika kuhakikisha kuwa wanapata utajiri kutoka kwa waumini wao, hizi ni baadhi ya mbinu wanazozitumia wachungaji hao ili kujiingizia kipato cha ziada.

Uchapishaji wa vitabu

Wachungaji wengi wamekuwa na kaida ya kuandika vitabu mbalimbali vyenye mafunzo ya aina tofauti tofauti. Uuzwaji wa vitabu hivyo hufanikiwa kwa kiasi kikubwa kutokana na nguvu ya ushawishi waliyo nayo wachungaji. Hata kama kitabu hicho hakijakidhi ubora, alimradi tu kimeandikwa na mchungaji, basi waumini watashawishiwa kukinunua. Na kupitia mauzi ya vitabu hivyo, basi wachungaji hujiongezea kipato jambo ambalo huchangia wao kuwa matajiri.

DVD na CD

Kama wewe ni muumini wa dini ya kikristo, basi utakubaliana na mimi katika hili. Siku hizi katika makanisa mbalimbali kumekuwa na CD na DVD za mafundisho mbalimbali zinazouzwa. Utakuta CD ya mahubiri ya Ibada ya jumapili iliyopita, yanauzwa jumapili hii kwa waumini walewale waliokuwa wamehudhuria ibada hiyo. Kununua CD ya mafundisho ili urudie kuisikiliza mara kwa mara ni jambo jema sana. Lakini tatizo ni pale ambapo waumini wanauziwa CD hizo kwa bei ya faida. Yaani utakuta gharama za maandlizi na ya CD hizo mpaka zikamilike, ni ndogo sana kulinganisha na kiwango wananchotozwa waumini. Hii ni njia ambayo wachungaji wengi huitumia kujipatia kipato, na waumini wengi bado hawajaitambua.

Semina

Semina mbalimbali za mafundisho ya dini zimekuwa zikiandaliwa na wachungaji wengi. Kumekuwa na semina za vijana, semina za watoto, semina za wanandoa, semina za akina mama na nyingine nyingi. TAtizo siyo seina hizi, tatizo ni pale ambapo wewe kama muumini wa kanisa hilo, ili uweze kuhudhuria semina hiyo, basi inakubidi kulipia kiasi fulani cha fedha kama kiingilio.

Semina za aina hii mara nyingi hutangazwa sana na wachungaji hutumia nguvu kubwa kuwashawishi waumini wahudhurie. Sawa, kazi yao ni kuokoa roho nyingi, lakini kwa upande wa pili (kibiashara) wanapohudhuria watu wengi, ndivyo pesa nyingi ya kiingilio itakavyopatikana.

Ushawishi mkubwa kwenye utoaji wa sadaka

Kutoa ni moyo, na kadiri unavyotoa kwa wingi, ndivyo unavyopata baraka. Ni kweli, lakini wachungaji wengi hutumia mwanya huu kuwashawishi waumini wao kutoa zaidi na zaidi. Kumbuka hata maandiko ya Biblia yanasema toa kwa kadiri ya uwezo wako, siyo tu kutoa hata kama huna, na wala usitoe eti kwa sababu mchungaji amesisitiza ufanye hivyo.

“Kila mmoja na afanye kama alivyoazimia moyoni mwake, si kwa kutopenda, wala kwa kulazimishwa, kwa maana Mungu humpenda mtoaji mchangamfu” 2 Wakorinto 9:7

Mishahara mikubwa

Biblia inafundisha kuwa wote wanaotoa huduma za kiroho wanapaswa kulipwa. Na malipo yao hayatoki pengine popote zaidi ya kwenye matoleo na sadaka za waumini.

Wazee wanaowaongoza watu vizuri wanastahili kupata riziki maradufu, hasa wale wanaofanya bidii katika kuhubiri na kufundisha. Maana Maandiko Matakatifu yasema: “Usimfunge ng’ombe kinywa anapopura nafaka.” na tena “Mfanyakazi astahili malipo yake.” 1 Timotheo 5: 17-18

Wapo viongozi wa dini ambao wanatumia sadaka za waumini kujipatia mishahara mikubwa na kuishi maisha ya starehe na ya kitajiri. Hawa wameonywa katika Biblia kuwa wasiwe na tamaa ya fedha bali waifanye kazi ya Mungu kwa kujitolea.

“wazee! Mimi niliye mzee ninalo ombi moja kwenu wazee wenzangu. Mimi mwenyewe nilishuhudia kwa macho yangu mateso ya Kristo na natumaini kuushiriki ule utukufu utakaofunuliwa. Mimi nawaombeni. mlichunge lile kundi la Mungu mlilokabidhiwa, mlitunze si kwa kulazimika, bali kwa hiari kama atakavyo Mungu. Fanyeni kazi hiyo si kwa tamaa ya fedha, bali kwa moyo wenu wote. Msiwatawale kwa mabavu hao waliowekwa chini ya ulinzi wenu, bali muwe mfano kwa hilo kundi.” 1 Petro 5: 1-3

Kutana na Mtabibu Mwenye KUBRI kutoka kwa ALLAH issa simba said Mtabibu wa Nyota za Binadamu na Dawa za Asili

$
0
0

Kutana na Mtabibu Mwenye KUBRI kutoka kwa ALLAH issa simba said Mtabibu wa Nyota za Binadamu na Dawa za Asili ya Africa Mwenye UWEZO Kubaini tatizo lako Pindi tu Utakapo Fanya Mawasilino Kupitia Wasaa Husika..JE UNASUMBULIWA NA Mapenzi? (Umeachwa na Umpendae,Awe Mume,Mke na Bado unampenda?Na Umejaribu Sehemu nyingi Bila Mafanikio?Wasilina na Maalim Hussein Ujione muujiza wa Papo kwa Papo.. anauwezo WA KURUDISHA MAHUSIANO NA KUIMARISHA NDOA YAKO NDANI YA SAA 12 TU. Umekimbiwa na Mumeo,mkeo au Mpenzi na anaishi na mtu mwingine? Muone akutatulie Anauwezo wa Hali ya Juu wa Kusambalatisha Mahusiano yao Endapo utafata Atakacho kuelekeza.
Atamfanya Atimize Ahadi zote kwa Muda Mfupi.
Issa simba said Anatumia Jina la Muhusika au Picha Kumaliza Tatizo lako..
Anatibu kwa Kutumia Vitabu vya QUR-AN Dawa za Asili za Africa,Dawa za Kiarabu na Majini.Anatafsiri Ndoto. Kushinda BAHATI NASIBU, KUSAFISHA NYOTA. Mvuto wa Mwili na BIASHARA, Kinga ya Mwili,ZINDIKO za Nyumba.MIGUU Kufa GANZI.Kufungua KIZAZI kwa wale walio fungwa kwa njia za KISHIRIKINA. Anakupa Jini la Mali kwa yule anaehitaji Utajiri BILA MASHARTI. Nguvu za KIUME, Humaliza Kesi zilishindika ndani ya siku 14 tu..na mengi zaidi +255 622588038au 0679119679 au +255 764318107
NB: TIBA KWA DINI ZOTE NA IMANI ZOTE...

Kamanda Mambosasa Atembelea Kibiti

$
0
0
Kamanda wa kanda maalumu ya Dar es salaam Lazaro Mambosasa leo ametembelea kikosi kazi cha Operesheni maalumu ya kulinda usalama katika mkoa wa kipolisi wa Rufiji hatua hiyo ni moja ya kuwatia moyo vikosi ambavyo vipo kwa ajili ya kuhakikisha wananchi walio eneo la Rufiji,  Kibiti, Mkuranga na Mafia wanaishia kwa hali amani.

Aidha Ziara hiyo ya kamanda Mambosasa ameongozana na wakuu wa mikoa ya kipolisi ya Temeke, Kinondoni na Ilala.

Taarifa zaidi itakujia kupitia hapahapa Muungwana blog kwa kila kinachoendelea
Viewing all 104785 articles
Browse latest View live




Latest Images