Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104789 articles
Browse latest View live

Mwanachama Mwingine wa Upinzani Ajitoa Ndani ya Chama

$
0
0
Mwanachama Mwingine wa Upinzani Ajitoa Uwanachama
Mwanachama wa NCCR- Mageuzi, Dk George Kahangwa ametangaza kujiondoa ndani ya chama hicho.



Dk. Kahangwa amesema kuwa haoni dalili yoyote ya mwanga katika chumba cha giza nene linaloighubika NCCR- Mageuzi.

“Mniwie radhi kuwataarifu hili. Sioni dalili yoyote ya mwanga katika chumba cha giza nene linaloigubika NCCR- Mageuzi. Hivyo, hiari ileile niliyoitumia kujiunga, sasa naitumia kukaa pembeni,” ameandia Dk. Kahangwa katika ukurasaw wake wa Facebook.

Katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2015, Dk Kahangwa alipendekezwa na NCCR-Mageuzi kuwania urais ndani ya vyama vinavyounda Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa) ili kupitishwa kupeperusha bendera ya umoja huo.

Hata hivyo, Mkuu wa Oganaizesheni na Utawala wa NCCR-Mageuzi, Florian Mbeo amethibitisha kwa gazeti la Mwananchi kujiondoa kwa Dk Kahangwa.

“Ni kweli amejivua uanachama, alikieleza chama kuhusu suala hilo na hata leo asubuhi nimezungumza naye. Uamuzi aliochukua ni wa kawaida tunauheshimu,” amesema Mbeo.

Mahakama Yaamuru Mtoto Kumlipa Mama Yake Gharama za Malezi

$
0
0
Mahakama yaamuru mtoto kumlipa mama yake gharama za malezi
Mahakama ya juu zaidi nchini Taiwan imemuru kuwa mwanamume mmoja amlipe mamake karibu $1m (£710,000)kugharamia malezi na masomo ya kuwa daktari wa meno.



Wazazi nchini humo wamekuwa wakiwashtaki watoto wao ili kupata usaidizi wa kifedha lakini kesi hii nitofauti kwa sababu inahusisha mkataba wa maandishi uliofikiwa kati ya mzazi na mwanawe

Uamuzi wa mahakama ya juu zaidi nchini humo uliezea kwamba mama yake anakabiliwa na deni la dola elfu mia sita alilopata akiwalea na kuwasomesha watoto wake wawili tangu kutengana na mumewe.

Alikuwa na wasiwasi kwamba wanawe huenda hawatatimiza wajibu wa kumlinda siku za baadaye, ndiposa akaandikisha mkataba na wanawe wa jinsi watakavyomlipa pesa alizotumia kuwaelimisha na kuwatunza.

Kwa mujibu wa mkataba huo ulioletwa mbele ya mahakama, wanawe wawili, punde tu wanavyohitimu kama madakatari wa meno, walifaa kulipa mama yao asilimia 60 ya mapato yao kila mwezi.

Mwanawe wa pili ana kliniki yake ya meno, na alimuuliza amlipe kulingana na mkataba wao.

Mwanawe naye amesema kwamba wakati alipoingia mkataba huo, alikuwa na miaka ishirini tu, na ni ukiukaji wa haki zake kama binadamu na si halali.

Mahakama ya Juu zaidi ilishikilia msimamo kwamba sheria ya mizozo ya kiraia inakubali mtu kufanya mkataba na kuna kiwango fulani kinachoruhusiwa wakati wa malipo.

Mahakama hiyo pia imesema kwamba makubaliano hayo kati ya mzazi na watoto haitaathiri maisha ya wanawe mwanamke huyo, watamudu, na pia mkataba haujakiuka haki yake kwani alikuwa ametimiza umri wa mtu mzima

Mahakama imeamua kwamba mwanawe ambaye ni dakatari wa meno tangu mwaka wa 2003, atimize matakwa ya mkataba wake na mama yake kwa kumlipa deni ambalo limefika kwa dola milioni moja za Marekani

Katika nchi hiyo ya Taiwan, wazazi wakongwe wana mazoea ya kuwashtaki watoto wao wanapokuwa watu wazima na nia ya kupata msaada.

Walimu ‘Watemwa’ kwa Utoro, Wanafunzi Washindwa Kumaliza kwa Mimba

$
0
0
Walimu ‘Watemwa’ kwa Utoro, Wanafunzi Washindwa Kumaliza kwa Mimba
Walimu tisa wa shule za msingi wilayani Bahi wamefukuzwa kazi kutokana na utoro huku wanafunzi sita wakishindwa kumaliza elimu ya msingi kutokana na mimba.

Ofisa elimu na taaluma wilayani humo, Issa Nchila ametoa taarifa hiyo leo Jumatano kwenye kikao cha wadau wa elimu waliokutana kujadili changamoto zinazosababisha wilaya hiyo kuendelea kushuka kielimu.

Nchila amesema walimu hao walikuwa miongoni mwa walimu 11 waliokuwa wameshtakiwa kwa makosa mbalimbali ya utoro na nidhamu kazini.

Amesema walimu wawili kati ya hao, walishushwa vyeo ikiwemo kupunguziwa mishahara yao.

Ofisa huyo amekiri hali mbaya kwa matokeo ya elimu huku wilaya ikiwa imeshika nafasi ya tano katika halmashauri 8 za Mkoa wa Dodoma.

"Bado tutaendelea kuwachukulia hatua kali kwa kushirikiana na TSD ili kukomesha vitendo hivyo kwani ni moja ya mambo yanayotukwamisha na kufanya watoto wetu wafanye vibaya," amesema Nchila.

Amesema bado wilaya inakabiliwa na mdondoko mkubwa wa elimu kwani wanafunzi walioandikishwa darasa la kwanza walikuwa  4,564 lakini waliofanya mtihani wa darasa la saba ni wanafunzi 3,005 huku watoto 1559 wakiishia njiani.

Mkuu wa Wilaya ya Bahi, Elizabeth Kitundu amesema wilaya hiyo ina tatizo la mimba kwa shule za msingi na sekondari ambalo watalikomesha.

Kitundu amewaambia wadau wa elimu kuwa mimba zinamkera wakati wote anaposikia watoto wanashindwa kumaliza elimu zao huku wadau wakishindwa kutoa ushirikiano wa kuwabaini wahusika.




Mbunge Ataka Chips Kuanza Kusafirishwa

$
0
0
Mbunge Ataka Chips Kuanza Kusafirishwa
Mbunge wa Njombe Mjini, amewataka wajasiriamali wadogo mkoani Njombe kuwekeza kwenye viwanda vidogo vidogo na kuanza kusafirisha viazi ambavyo tayari vimecharagwa chips ili kuepuka kulaliwa na wafanyabiashara wanaolazimisha kufunga lumbesa za viazi.


Edward Mwalongo amesema hayo akiwa anaongea na baadhi ya wajasiriamali mkoani humo ambao wameanzisha kiwanda kidogo cha kumenya viazi na kucharanga chips na kudai kuwa wana Njombe wanapaswa kuvitumia viazi kama malighafi yao ambayo inaweza kuwaletea viwanda vingi vidogo vidogo.

"Viazi ni sehemu ya malighafi ambavyo tungeweza kuvitumia kama hivi na huo ndiyo mwanzo tuitumie malighafi ya viazi ili kusudi tuanzishe viwanda vidogo vidogo vingi kadri inavyowezekana, kwa sababu kila kiazi kinachotoka Njombe kikisafirishwa hakipelekwi kwa ajili ya mbegu bali kinakwenda kuliwa na kama kinakwenda kuliwa kinaliwa kama chips au kinakwenda kumenywa lakini sehemu kubwa inajulikana vinakwenda kuliwa kama chips sasa tufike mahala wana Njombe badala ya kulalamika na Lumbesa tuanze kusafirisha chips zilizomenywa kwa kuweka kwenye ubaridi na ziwafikie walaji" alisisitiza

Mbunge huyo wa Njombe Mjini aliwakabidhi mashine ya kukatia viazi wanawake wajasiriamali ambao wameunda kikundi chao na kuanza kufanya kazi hiyo ya kukata chips na kuziuza kwenye mahoteli, migahawa na wapishi wa chips mkoani humo.



Miujiza ya Sharifu Seif Mohamed..JE Umeachwa na Mme/Mke au Mpenzi, Umesongwa na Mitihani ya Maisha..Piga Simu Upate Muujiza Wako

$
0
0
SHARIFU SEIF MOHAMED ANAWASHUKURU WALE WOTE WANAOENDELEA KUPIGA SIMU, WENYE MATATIZO NA WALE WANAOTOA  SHUKRANI NA SHUHUDA JINSI TIBA ZAKE ZINAVYO WASAIDIA,

(Rudisha mahusiano yako ndani ya masaa 72 tu)

SHARIFU MOHAMED Ni  mtaalam na mnajimu maarufu wa nyota na kubashiri mambo yanayo watesa binadamu duniani kote na kupata ufumbuzi, Anatumia kitabu cha QUR'AN, Dawa za Asili, Dawa za Kiarabu na majini kwa kumtuliza mke/mme, mchumba au mpenzi ndani ya masaa 72 tu, na kutatua matatizo yote ya kimaisha,

Je Umeachwa na UMPENDAE awe Mme/Mke na bado unampenda? Je Umekimbiwa na Mmeo/ Mkeo n anaishi na mtu mwingine? Je Umejaribu sehemu nyingi bila mafanikio? Mpigie simu SHARIFU SEIF sasa hivi ujionee Muujiza wa Papo kwa Papo, Anauwezo wa hali ya juu wa kusambaratisha mahusiano yao na kumrejesha kwako haraka sana na Kumfanya Atimize Ahadi zote Ndani ya Muda Mfupi Endapo Utafwata Atakacho Kuelekeza

ANAZO DAWA ZA MAPENZI, NGUVU ZA KIUME, CHANGO NGIRI MAJI NA N.K, ZINDIKO LA NYUMBA NA BIASHARA, PETE ZA BAHATI, HUMALIZA KABISA TATIZO LA NGUVU ZA KIUME NA KUREFUSHA UUME KWA SAIZI UNAYOTAKA, HUZUIA CHUMA ULETE KWENYE BIASHARA, HURUDISHA MALI ZILIZOPOTEA, MAGONJWA SUGU, MIGUU KUWAKA MOTO AU KUFA GANZI, HUTIBU BUSHA BILA KUPASUA, ANAO UWEZO WA KUMRUDISHA ALIE MBALI AU ALIECHUKULIWA MSUKULE, KUPANDISHA NYOTA NA KUSHINDA BAHATI NA SIBU, KASAFISHA NYOTA NA KUKUPA MVUTO WA AJABU, KUTOA NUKSI NA VIFUNGO MBALIMBALI,  MAFANIKIO YA MAISHA NA UTAJIRI BILA MASHARI, NA MENGINE MENGI YA SIRI,

Je UMAHANGAIKA KUPATA MTOTO BILA MAFANIKIO? WASILIANA NA MTAALAMU HUYU KWANI YEYE HUFAULU PALE WOTE WALIPOSHINDWA, PIA UMALIZA KAZI ZILIZO SHINDIKANA NA WATAALAM WENGINE NDANI YA MASAA 24 TU,

(NA ANATIBU KWA NJIA YA SIMU UKIWA NCHI YOYOTE AU MKOA WOWOTE ENDAPO UTAFWATA MAELEKEZO YAKE)

Kwa ushauri na mawasiliano  zaidi Piga SIMU No:

Mobile +255 654-836970
WhatsApp +255 756-033670

Hivi Kwanini Single Mothers Wengi Wao ni Dhaifu kwa Wanaume Waliozaa Nao?

$
0
0
Kuna rafiki yangu mmoja hivi nilisoma naye chuo, huyu jamaa katika mwaka wake wa pili tangu aanze kazi alikutana na mfanyakazi mwenzie ambaye ni mtaalamu wa madawa ya binadamu (Pharmacist)

Wakaanza mahusiano ya mapenzi,lakini kiuhalisia jamaa yeye alikuwa naye kwa kujifurahisha tu kwa kuwa tayarialikuwa na mchumba wake lakini alikuwa anafanya kazi mkoa mwingine, akaamua amchukue huyu mfamasia kwa ajili ya kucheza rafu za hapa na pale na kuondoa upweke usio wa lazima.

Lakini kumbe mdada wa watu kajiongeza na hatimaye akamtegea jamaa siku zile za hatari, jamaa akiwa hana habari na mpango wa bibiye hatimaye akamtandika ujauzito, jamaa akaja juu kwamba kwanini ameshika ujauzito bila makubaliano? Akamwambia achoropoe,bibiye akagoma.

Basi jamaa kwa hasira akampiga kibuti demu,mahusiano yakafa lakini baadaye akasema wtashirikiana kumlea mtoto ila mapenzi yafe, mdada akasema haina shida.

Kwa hiyo kila mara wanatembeleana kwa ajili ya mtoto ila mambo ya mapenzi hakuna.

Sasa imepita miaka kama miwili hivi kajitokeza mshikaji mwingine anataka kuchukua mzigo jumla (kuoa), sasa katika process za utoaji barua, eti bibiye anampigia simu baba wa mtoto kuwa anataka kuolewa hivyo ampe ruhusa ya kuolewa ahahahahahhahahahah; jamaa akamwambia we olewa,unaniomba ruhusa kama nani wakati mi na wewe tulishaachana?

Kwa kufupisha stori, kiufupi pamoja na mchakato wa ndoa kuendelea lakini binti anaonesha matendo ya kidhaifu mno kwa mzazi mwenzie kiasi kwamba hata jamaa akiamua kuomba mzigo anaweza kupewa bila masharti; hali hii imefanya kutokea mgogoro mkubwa kati ya mume mtarajiwa na binti,mgogoro unaotokana na wivu wa mapenzi unaochagizwa na tabia ya binti kuwa dhaifu mno kwa mzazi mwenzie.

Kwa mujibu wa rafiki yangu anakiri kiukweli wakikutana na bibiye kwa ajili ya kumjulia hali mtoto, bibiye anakilegeza mno,yani anajiweka kiromantic na hayuko seriously sana kama mtu ambaye kweli anatarajiwa kuolewa.

Sasa, mimi naomba kuwauliza , Hivi ni sababu ipi haswa inayopelekea mabinti wengi kuwa dhaifu kwa wanaume waliozaa nao kiasi cha kuwapa wakati mgumu waoaji?

Hivi haiwezekani mkizaa mkaachana moja kwa moja bila kuwa na shauku ya kukumbushia mapenzi?

By likandambwasada

UKAWA wanyakua nafasi ya Unaibu Meya wa Jiji la Dar es Salaam

$
0
0
Mgombea wa Ukawa, Mussa Kafana (CUF) ameshinda uchaguzi wa Naibu Meya jiji la Dar es Salaam akiwa kwenye machela.

UKAWA wajumbe 11

CCM. 11

Jumla ya kura. 22

CCM. Kura. 10
CUF. 12

NOTE:
CCM yaipigia kura UKAWA Naibu Meya


Meya wa Ubungo (Wakala wa UKAWA) Akipambana na Madiwani wa ccm Waliotaka Kumpora Kura, Wakati wa Uchaguzi wa Naibu Meya Dar es salaam. Hii Ilitokea Baada kura Kuhesabiwa na Kukuta UKAWA Wana Kura 12 na ccm 10.

Pata Dawa Bora ya Nguvu za Kiume na Maumbile Madogo

$
0
0
MHULI: Ni dawa ya nguvu za kiume inayorefusha na kunenepesha uume saizi uipendayo (Inch 1-7) kwa muda wa siku 6 tu.Dozi hii itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa muda wa dakika 30, utarudia tendo la ndoa zaidi ya mara 4 bila hamu kuisha bila kujali umri na garantee ni miaka 60 baada ya kutibu tatizo.

Pia tunatibu Busha bila kufanyiwa Oparesheni, korodani moja kuvimba, ngiri, tumbo kujaa gesi na kuunguruma, kutopata choo vizuri, miguu kuwaka moto na kufa ganzi, chango la wanawake, kisukari na kutokwa na kinyama sehemu ya haja kubwa.


Inarudisha mke, mchumba, hawara na atakutimizia kila kitu unachotaka kutoka kwake ndani ya  saa 2 tu hata kama yupo mbali. atarudi na kumfunga asiwe na mwingine zaidi yako.

Umefukuzwa kazini? unataka kupandishwa cheo? Umepoteza pesa zako kwenye biashara bila kujua umepandikizwa chuma ulete? Njoo urudishe pesa zako. Unauza mali yako haiendi?

Wasiliana na Nasi kwa Namba; 0783140065 

Kimenuka Tena..Madiwani Wawili Chadema Wajiunga CCM

$
0
0
Madiwani wawili wa Chadema katika Halmashauri ya Manispaa ya Iringa wamejiuzulu nyadhifa zao na kuhamia CCM.

Wakati diwani wa Ruaha, Tandesy Sanga akitangaza uamuzi huo leo Jumatano Januari 3,2018 jijini Dar es Salaam; mwenzake wa Kwakilosa, Joseph Ryata ametangaza uamuzi huo mjini Iringa.
Katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2015 Chadema ilishinda ubunge wa Iringa Mjini na kupata madiwani katika kata 14 kati ya 18, hivyo kuongoza Halmashauri ya Manispaa ya Iringa kwa mara ya kwanza tangu kuanza kwa mfumo wa vyama vingi vya siasa nchini mwaka 1992.

Ryata aliyewahi kuwa naibu meya wa manispaa hiyo ametangaza uamuzi huo leo alipozungumza na waandishi wa habari, na kuonyesha barua aliyoiwasilisha kwa meya na mkurugenzi mtendaji wa halmashauri Desemba 22,2017.

Chadema imeshapoteza madiwani sita akiwemo wa kata ya Kitwiru, Baraka Kimata aliyejiuzulu na kujiunga CCM ambako alishinda tena katika uchaguzi mdogo uliofanyika Novemba 26,2017.
Madiwani wengine waliojiuzulu na kujiunga na CCM ni aliyekuwa wa kata ya Kihesa, Edger Mgimwa; wa viti maalumu Leah Mleleu na Husna Daudi.

Ryata akitangaza kujiuzulu amedai hajaridhishwa na uendeshaji wa Chadema na wa baraza la madiwani la Halmashauri y Manispaa ya Iringa.
Akiwa ameambatana na Mgimwa alidai amekwepa vitendo vya uongozi wa kidikteta ndani ya Chadema.

Jijini Dar es Salaam, Sanga amesema uamuzi wake wa kujiuzulu unatokana na kuunga mkono jitihada za maendeleo za Rais John Magufuli.

"Huwezi kumsifia Rais wala utendaji wake ukiwa nje ya chama chake, binafsi nimeshaonywa kwenye vikao hata kutishiwa kuvuliwa uanachama kwa sababu hiyo," amesema.
Sanga amesema ilikuwa vigumu kwake kuhudhuria ziara za viongozi wa Serikali kwa kuonekana msaliti hata kama nia yake ilikuwa ya kiuongozi.

"Kwa hiyo bila kutumwa, kushinikizwa wala kununuliwa na yeyote kama inavyodaiwa na baadhi ya watu najiunga na chama kilicho taasisi, si cha mtu mmoja," amesema.
Sanga amesema jingine lililomsukuma kuhama ni tabia ya baadhi ya viongozi kuwa na nguvu kuliko chama chenyewe tofauti na fikra zake wakati alipojiunga Chadema.

Nandy Acharuka Kimasai Baada ya Taarifa Kusambaa Kuwa Anatoka na Ruge Mutahaba

$
0
0
January 3, 2018 kumekuwepo na post kwenye mitandao ya kijamii kuhusu msanii Nandy kudaiwa kutoka kimapenzi na Mkurugenzi wa Vipindi na Uzalishaji wa Clouds Media Group, Ruge Mutahaba, Nandy ameamua kuandika kwenye ukurasa wake wa Istagram kuhusu tuhuma hizo.

Nandy Kupitia ukurasa wake wa Isntagram ameandika kuwa. “Mtu akifanya mziki wake kwa amani bila drama kuna watu wanakuwa hawatosheki kabisa. hivi mimi ni kichaa mpaka kujiachia kama uyo msambaza habari anavyo sambaza!”

“Kwani suala la watu kusema na toka na boss wangu nalijua leo au nigeni kwangu sana mpaka nijiachie kwenda naye ma camp sijui ma club kama mnavosema???” – Nandy

“Embu tuwe na utu please kwa hiyo me nimekuwa wakuja kiasi kwamba mshamba kiasi nikashindwa kujificha na mashungi juu basi kama ni hivyo  tumeshindwa kupishana kusafiri atangulie ndo nifuate,”– Nandy

“Kwani sijui hata kama ingekuwa ni kwa nia nzuri  msingesema mnazani mambo ni marahisi kiasi hicho tupeane heshima kuna watu wengine hatutaki drama za kitoto msi force mambo..” – Nandy

CCM, Ukawa Wazidunda Umeya Dar...Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Alhamisi ya January 4

$
0
0


CCM, Ukawa Wazidunda Umeya Dar...Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Alhamisi ya January 4

CHADEMA Iringa yapata pigo tena.....Madiwani Wawili Watimkia CCM

$
0
0
Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) mkoani Iringa kimepata pigo baada ya madiwani wake wawili kutangaza kujiuzulu nafasi zao na kujiunga na Chama Cha Mapinduzi (CCM)

Wakiongea na waandishi wa habari aliyekuwa diwani wa Ruaha, Tandesy Sanga ambaye ametangaza uamuzi wa kujiuzulu jana  Jumatano Januari 3, 2018 jijini Dar es Salaam na mwenzake wa Kwakilosa, Joseph Ryata ambaye yeye aliandika barua ya kujiuzulu toka Disemba 2017 na kusema kuwa wamefanya maamuzi hayo kutokana na mgongano wa maslahi ndani ya CHADEMA.

Joseph Ryata amedai kuwa wao uamuzi wao wa kwenda Chama Cha Mapinduzi upo tofauti na wale wengine ambao wanadaiwa kununuliwa na baadhi ya viongozi wa CCM

"Mnamo Disemba 22, 2017 nilifanya maamuzi mwenyewe wala sikushinikizwa na mtu niliamua kujiuzulu nafasi ya udiwani wa Kata ya Kwakilosa na nilifanya hivyo kwa sababu za msingi zifuatazo sikuwa na ushirikiano mzuri na wenzangu.

"Kumekuwa na wimbo la madiwani kuhama lakini niwahakikishie kwamba kuhama kwangu mimi hakuendani na hilo wimbo ambalo linazungumzwa kwamba madiwani wananunuliwa wanahama bali kuhama kwangu mimi ni migongano, kutokuelewana, na kule kutofuata mifumo ya kichama ya uendeshaji mzima wa baraza la halmashauri ya Iringa Mjini" alisema  Ryata

Mbali na hilo Ryata amesema kuwa uchaguzi wa kumpata Naibu Meya wa Manispa ya Iringa Mjini haukufuata utaratibu na kudai kuwa ulitumika ubabe na mabavu kuendesha zoezi hilo ambalo kila baada ya mwaka linapaswa kufanyika illi kuwapata viongozi wapya wa baraza.

Mpaka sasa Manispaa ya Iringa Mjini imepoteza madiwani wa Kata sita ambao wote baada ya kujiuzulu walijiunga na Chama Cha Mapinduzi (CCM)

Bond Ateswa na Ujambazi, Penzi la Wastara 2017

$
0
0
MENEJA na aliyekuwa mpenzi wa msanii wa Bongo Muvi, Wastara Juma, Bond Suleiman amefunguka kuwa mwaka 2017 ulikuwa ni mchungu sana kwake, baada ya kuhusishwa na tukio la ujambazi na ishu ya kuachana na Wastara.

Akizungumza na Za Motomoto, Bond alisema kuwa kwenye uhusiano aliumia sana kumuacha Wastara hasa baada ya kumuona ni kama anataka mafanikio ya haraka wakati yeye uchumi ulikuwa umeyumba.

“Mimi ndiye niliyemuacha Wastara na kuamua kuondoka zangu na kwenda kufanya maisha yangu mengine kwa sababu niliona kama namkosesha amani na pia alitaka mafanikio ya haraka wakati uchumi wangu uliyumba. Pia ishu ya kuhusishwa kwenye ujambazi ilinitesa sana kwani nilikaa selo siku ishirini ila nashukuru polisi waliujua ukweli nikawa huru,”alisema Bond.
Stori na Jacqueline Oisso

GPL

Hamisa Mobeto Usipo Invest Muda Huu, Utafeli...

$
0
0
Ninamshukuru sana Mwenyezi Mungu kwa kunipa afya njema na kuuona mwaka mpya 2018. Kuna ndugu, jamaa na marafiki wengi ambao walitamani kuuona mwaka mpya lakini Mungu aliwapenda zaidi. Wengine wako vitandani hospitalini, lakini mimi na wewe tumeweza kusherehekea Krismasi na Mwaka Mpya kwa shangwe.

Leo kwenye Barua Nzito, ninapenda kumkumbusha dada yangu kipenzi ambaye ni Mwanamitindo wa Bongo, Hamisa Mobeto. Dada yangu, nafasi uliyonayo kwenye jamii ni kubwa. Ni nafasi ambayo imekufanya utambulike ndani na nje ya mipaka ya Tanzania kwa kazi na figisufigisu zako za kila siku.

Kupitia shughuli zako za kila siku, umeweza kupata dili mbalimbali ambazo kama ukizitumia vizuri zinaweza kukufanya ukatoboa mazima kwa kuwa na maisha f’lani hivi mazuri.
Ikiwa tumeuanza mwaka mpya 2018, ninapenda kukuasa dada yangu Mobeto, inawezekana hatujuani ana kwa ana kwa sababu sikumbuki kama nimeshawahi kufanya kazi kwa ukaribu zaidi na wewe. Lakini najaribu kukufikishia barua yangu kwa sababu ya mapenzi mema kwako na kwa kukutakia heri ya mwaka mpya.

Mobeto, ninakukubali kwa maana ya kazi yako ya u-modo lakini pia kwa jinsi unavyojua kupangilia mavazi yako, hujawahi kuharibu.
Leo ninajaribu kukukumbusha kuwa, mwaka jana ulitengeneza sana vichwa vya habari mbalimbali kutokana na mishe zako za kila siku.

Ninachoamini mimi kwa mwaka jana ulitengeneza mtandao mkubwa ndani na nje ya nchi. Kama kweli mtandao wako utautumia vizuri basi una nafasi kubwa ya kutoboa kwa kwenda levo za kimataifa.

Kitendo chako cha kupata shavu la kupata shoo nchini Uganda inamaanisha kuwa unakubalika bila kujali upinzani na figisu za aina yoyote iliyokuwepo kwenye shoo hiyo.

Nakumbuka Novemba 4, mwaka jana ulikuwa ni mmoja wa wanamitindo wa Kitanzania ukiwakilisha na Afrika Mashariki uliyechanguliwa kwenye Tuzo ya Starqt Awards zinazohusisha biashara, mitindo, burudani na ukachaguliwa katika vipengele vya ‘People Choice Awards’ na ‘Super Mum’ ila amefanikiwa kuibuka kidedea katika kipengele kimoja tu. Tuzo ambazo zilitolewa katika Ukumbi wa Bedford View City Hall, mjini Johannesburg Afrika Kusini.
Umekuwa na sarakasi za hapa na pale kwenye maisha yako lakini kama ukizitumia vizuri basi zinaweza kukusaidia kufika sehemu nzuri.

Kama msanii kuna wakati unakuwa uko kwenye ‘peak’ kila mitandao inakusema wewe, vyombo vya habari mbalimbali navyo vinaandika habari zako. Huo ndiyo muda muafaka wa wewe kufanya biashara kama ukishindwa kuutumia vyema muda huo ambao uko juu basi utakuwa umefeli.
Wapo wasanii wengi ambao walipata nafasi kama ya kwako lakini pengine kwa kuwa na akili ya ziada, hawakuwa na washauri wazuri au sikupata nafasi ya kuwakumbusha kwenye barua yangu. Wakajikuta wametumia vibaya pesa, rasilimali na muda wao pasipo kunufaika na ustaa wao.
Mobeto kwa kila unachofanya lazima ujue kuwa wewe ni mama wa watoto wawili ambao unatakiwa kuwalea katika mazingira na maadili mzuri hasa ya Kitanzania.

Fanya jambo kwa kuangalia pia je, ni alama au athari zipi unaweza kuziacha kwa wanao baada ya maisha yako ya u-modo.

Mwisho kabisa, napenda niwatakie kila la heri wasomaji wa Barua Nzito kwa mwaka huu 2018. Mungu akusimamie na akupe wepesi katika kila jambo jema unalolifanya katika maisha yako ya kila siku.

Download Application ya MCHAMBUZI Kwenye Simu yako Kusoma Habari za Siasa Kila Baada ya Lisaa Limoja

$
0
0
Maswala ya Siasa na Matamko ya kila siku ya Wanasiasa Hakikisha Umedownload App ya Mchambuzi Kwenye simu yako

Kama we ni Mpenzi wa Habari za Siasa Usipitwe na Hii Application ya Mchambuzi..... 

Bonyeza HAPA Kudownload kwenye Simu yako


Chin Bees Afunguka Kuhusu Skendo ya Picha za Utupu na Mwanamke

$
0
0
Chin Bees Afunguk Kuhusu  Skendo ya  Picha za Utupu na Mwanamke
Msanii wa Bongo Fleva anayefanya vizuri kwenye mitindo ya Trap, Chin Bees baada ya kupata skendo kwenye mitandao ya kijamii kwa kusambaa picha akiwa mtupu na mwanamke chumbani, hatimaye amekiri picha hizo zilisambazwa na watu wasiomtakia mema, kwani alikuwa amepoteza simu yake.

Chin Bees ameiambia  eNEWZ kwamba picha iliyosambaa mitandaoni kweli ilikuwepo kwenye simu yake na huyo mwanamke aliwahi kuwa mpenzi wake lakini hakufanya kusudi kuziweka mitandaoni kama jinsi ambavyo watu walivyoanza kumshtumu na kumwambia anatafuta kiki.

"Hiyo picha iloyosambaa kwanza sijajua ni nani aliyeisambaza kiukweli ila sio mimi na huyo dada sipo nae tena kwenye mahusiano, na hayupo hata Tanzania. Lakini ninachofahamu nilipoteza simu yangu muda kidogo nilikuwa kwenye bata  moja hivi. Mimi nimefanya kazi zangu za muziki mpaka leo sijatumia kiki sasa kwanini ijekuwa leo" Chin Bees.

Pamoja na hayo Chin Bees amesema kwamba baada ya kutumiwa picha hizo alilazimika kumtafuta mwanamke huyo na kumuuliza kuhusu kusambaza picha hizo lakini pia alikanusha.

Hii ni skendo ya kwanza kwa Chin Bees kuanikwa mitandaoni kwa kusambaa picha zake za utupu akiwa na mwanamke tangu kuanza safari yake ya muziki.

‘Sanchi’ na Mama Yake Mzazi Wamezua Gumzo la Aina Yake Mtandaoni

$
0
0
‘Sanchi’ na Mama Yake Mzazi Wamezua Gumzo la Aina Yake Mtandaoni
Modo maarufu Bongo, Jane Rimoy ‘Sanchi’ na mama yake mzazi wamezua gumzo la aina yake mtandaoni baada kuanika picha zao mbalimbali. Gumzo hilo lilianza mwishoni mwa wiki iliyopita baada ya Sanchi kuweka picha mbalimbali akiwa na mama yake na watu wakaanza kuzijadili.



“Mh! Kwa kweli mama naye kaumbika, kumbe Sanchi kafuata kwa mama kila kitu, hebu angalia shepu, angalia mambo yetu ni hatarii,” aliandika mchangiaji mmoja mtandaoni. Kama hiyo haitoshi, wapo wengine waliomponda Sanchi kwa kitendo cha kumuweka mama yake mtandaoni ilhali anatambua fika siku zote yeye ni mtu wa picha chafu katika ukurasa wake wa Instagram. “Anamdhalilisha mama wa watu.



Yeye hakutakiwa kabisa kumposti mama yake maana watu wengi walikuwa wanajaribu kuhoji kwa binti mwenye wazazi iweje kila siku aposti picha za utupu?” alihoji mdau mtandaoni. Picha hizo zilisambazwa haraka sana mitandaoni ambapo wafausi wa mitandao mbalimbali waliibua mijadala mbalimbali huku wengine wakimsifu na kumponda. Kuhusu kuibua mjadala, Sanchi alipozungumza na mwanahabari wetu hivi karibuni, alisema hajali watu wanasema nini kuhusu yeye na mama yake na kwamba atakuwa akiposti picha kulingana na anavyojisikia.

Sherehe ya Kuchumbiwa Wolper Balaa..... Muoaji Afanya Kufuru ya Aina Yake

$
0
0
Sherehe ya Kuchumbiwa Wolper  Balaa..... Muoaji Afanya Kufuru ya Aina Yake
SHEREHE ya kuchumbiwa kwa Staa wa sinema za Kibongo na Malkia wa Mavazi, Jacqueline Wolper imezua gumzo la aina yake baada ya muoaji kufanya kufuru ya aina yake, Amani linaripoti habari hii kwa mara ya kwanza (exclusive).

Sherehe hiyo iliyohusisha msafara mkubwa wa magari kutoka jijini Dar, ilifanyika Moshi, wikiendi iliyopita nyumbani kwa bibi yake kijijini Moshi.

Ili kutazama picha zote za tukio zima la kuchumbiwa kwa Wolper na mpenzi wake, Sadiki Athanasy Sanga ‘Engine’, ingia kwenye Application yetu ya Global Publishers sehemu ya magazeti.

Kama Huja-download fanya hivyo sasa, install kwa kupitia hizi Link uzitazame picha zote za kuchumbiwa kwa Wolper.

Shndika Arejea Dimbani Aanza Mazoezi Rasmi

$
0
0
Shndika Arejea Dimbani Aanza Mazoezi Rasmi
Kiungo wa zamani wa Simba na timu ya taifa ya Tanzania anayechezea klabu ya Mtibwa Sugar kwasasa Henry Joseph Shindika ameanza mazoezi rasmi leo baada ya kuwa nje kwa muda mrefu.


Katibu msaidizi wa Mtibwa Sugar, Abubakar Swabur amethibitisha kuwa Henry ameanza mazoezi baada ya kupona majeraha ya goti yaliyokuwa yanamsumbua kwa muda mrefu hali iliyompelekea kukaa nje ya uwanja kwa muda mrefu.

Swabur amesema mchezaji huyo wa zamani wa Simba SC na Kongsvinger ya Norway, amepona kikamilifu hivyo kufanya idadi ya majeruhi katika kikosi cha Mtibwa kubaki watatu, ambao ni beki Salum Kanoni, kiungo Mohammed Issa ‘Banka’ na mshambuliaji Kelvin Sabato.

“Henry amepona vizuri kabisa na hata hawa majeruhi wengine watatu nao maendeleo yao ni mazuri, ni watu ambao tunawatarajia kurudi wakati wowote,” amesema.

Katibu huyo msaidizi pia ameongeza kuwa mlinzi wa kati wa klabu hiyo Stahimili Mbonde hayupo kwenye kikosi cha Mtibwa kwasasa akiwa na ruhusa maalum ya kushughulikia matatizo ya kifamilia.

Mtibwa Sugar inashika nafasi ya tano kwenye Ligi ikiwa na pointi 21 na inatarajiwa kushuka dimbani Januari 13 kumenyana na wenyeji, Lipuli kwenye uwanja wa Samora mkoani Iringa katika mchezo wa rauandi ya 13 ya VPL.

Haya Hapa Maamuzi ya Diva Baada ya Kula Kichapo Kutoka kwa Mpenzi Wake

$
0
0
Haya Hapa Maamuzi ya Diva Baada ya Kula Kichapo Kutoka kwa Mpenzi Wake
Baada ya kuvuja kwa picha za Mtangazaji wa Clouds FM, Diva ikimuonesha akizozana na mpenzi wake Heri Muziki huku picha nyingine zikimuonesha akivuja damu, mrembo huyo amekiri wazi kuwa ni kweli ugomvi  huo ulitokea na picha ni zake.

Diva amesema tukio hilo lilitokea wiki iliyopita wakiwa maeneo ya Kinondoni na kudai kuwa wakati wakizozana walirekodiwa na mtu aliyekuwa karibu nao na ndiye aliyevujisha picha hizo.

Akieleza chanzo cha vurugu hizo na mpenzi wake amesema lilikuwa ni tukio la wivu ambapo Heri Muziki alikuwa anamtuhumu kumsaliti na baadae kufuta picha zote alizopiga na Diva kwenye ukurasa wake wa Instagram.

“Heri amefuta picha zinazonihusu mimi katika page yake ya Instagram anyway ni maamuzi yake najua hilo limetokea baada ya tukio lililotokea wiki iliyopita, He is grown up he knows nini anafanya. Mimi sijafuta hata picha moja zinazomuhusu yeye kwenye ukurasa wangu i always keep memories,“amesema Diva kwenye mahojiano yake na Bongo5 huku akifafanua skendo ya usaliti

“Mimi sijawahi kumsaliti Heri sijawahi fanya hivyo hata mara moja, i’m very faithful in my life ninapokuwa kwenye mahusiano. He has his own issues going on in his life but that has nothing to do with me, siwezi kumzungumzia kwa mabaya namheshimu sana amekuwa na mimi kwenye kipindi cha shida na raha so haitakuja tokea mimi kukaa na kumzungumzia kwa mabaya, then maisha yangu ya mapenzi nataka yawe private.“amesema Diva.

Soma na hii – Diva awakutanisha Mwana FA, Heri Muziki na Mr. Paul kwenye album yake ya ‘Ala za roho’

Hata hivyo, Diva baada ya tukio ametoa msimamo wake juu ya mapenzi yake na Heri Muziki kwa sasa ambapo amesema kuwa kukoseana ni vitu vya kawaida.

“In my life or relationship kukoseana kupo. Beyonce na Jay Z watu walihisi wale walikuwa perfect couple but dunia ilishuhudia, so that normal i keep the positive life coz mwisho wa siku Heri he’s a father of my child. He is a good guy and i hope watu wataheshimu maisha ya watu hasa ya kimapenzi.“amesema Diva na kuwaomba radhi mashabiki wake na wafanyakazi wenzake wa Clouds FM.

“Sorry for my disapointment waliyoipata mashabiki wangu, wafanyakazi wenzangu na ndugu jamaa na marafiki baada ya picha hizo kusambaa, sh*t happens and life goes on.“amemaliza Diva.
Viewing all 104789 articles
Browse latest View live




Latest Images