Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104709 articles
Browse latest View live

Maskini Wastara! Tazama Mguu Wake Ulivyoharibika, Anaomba Msaada (VIDEO)

$
0
0
AMA kweli hujafa, hujaumbika! Ndivyo unavyoweza kusema endapo utaisoma simulizi ya hali ya sasa ya msanii wa filamu Bongo, Wastara Juma anayesumbuliwa na mguu wake wa kulia aliokatwa baada ya kupata ajali, Risasi limeongea naye na kutoa simulizi ya kukutoa machozi.

Akiongea kwa masikitiko, Wastara ambaye alikuwa akilia kila wakati anapoongelea maumivu anayoyapata, alifikia hatua ya kuonesha mguu wake wenye jeraha kwa mara ya kwanza, kitendo kilichowafanya waandishi na baadhi ya watu waliokuwa karibu naye kutokwa na machozi.

Wastara alisema kuwa, amefikia hatua ya kuuonesha mguu wake huo na maumivu anayopata kutokana na baadhi ya watu kutomuamini pale anapoelezea wakati mgumu anaopitia.


“Jamani ninavyoumwa hivi kiuweli natamani nisingekuwa staa kwa sababu inafikia wakati natamani hata niingie barabarani kuomba, hii ni katika kuonesha ni jinsi gani nataka kwenda kupata matibabu ya mguu huu unaoniuma kila sekunde na dakika. Wapo watu ambao hawanielewi kabisa na sidhani kama watanielewa,” alisema Wastara.
Wastara aliendelea kusema kuwa amelazimika kuomba msaada kutoka kwa watu si kwa kutaka ila ni kwa sababu ameshafanya kazi za kila aina ili atumie jasho lake katika kujitibu lakini amejikuta akiambulia patupu huku watu wengine wakimkimbia.

KAZI ALIZOZIFANYA AKAAMBULIA PATUPU
Wastara alieleza kazi alizozifanya ambazo zimempotezea pesa na mpaka leo anaumia kuwa ni pamoja na mkataba aliosaini na Wachina wa kuwatangazia simu zao za KZG ambao walimkimbia bila kumlipa pesa zake kiasi cha shilingi milioni 80 na anaiomba serikali iingilie kati suala lake.

“Sipendi kuomba kabisa kwani uwezo wa kutafuta kama nikiwa na mguu naweza lakini dah… sijui nianzie wapi lakini hili suala la kudhulumiwa na watu linaniumiza sana (analia…) Wachina na Kampuni yao ya Simu ya KZG wamenikimbia nikiwa nawadai milioni 80, tukio la pili Msumbiji nimepoteza mzigo wa milioni 19 kwenye vurugu za kufukuzwa Watanzania ambapo nilikuwa nafanya biashara zangu nikijikusanyia pesa za kurudi hospitalini.

“Tukio la tatu nimeenda nchini Sweden kufanya filamu, nimerudi mikono mitupu kwani kule sikulipwa kama nilivyotarajia, mwezi wa 4 nimedai pesa yangu Steps, tumeishia mahakamani bila kulipwa nilivyokuwa natarajia, badala yake nikaahidiwa kulipwa milioni mojamoja ambayo haiwezi kunisaidia kwani nahitaji pesa ndefu kwa ajili ya kujitibu.

“Tokea hapo chochote ninachofanya kinachohusu pesa lazima tuishie polisi au mahakamani, silipwi vile tunavyokubaliana na baya zaidi ninaofanya nao kazi hawajui kuwa tangu nimerudi nchini toka Sweden nahaha kutafuta pesa ya matibabu, silali kwa maumivu makali ya mgongo na ninazimia kila muda.
“Hii imetokana na kuchelewa kurudi hospitalini kufanya tiba ya mgongo na kubadilisha ‘Soberly Skoner’ inayowekwa kwenye mguu kama tiba kuu ya kurudisha mgongo wangu ukae sawa,” anaeleza Wastara na kusisitiza kuwa, endapo hatapata matibabu ya haraka, anaweza kuondoka duniani.

SABABU YA MAUMIVU
Wastara ameeleza sababu ya maumivu ya mguu kuwa ni kuvimba na kuchanika kila mara kutokana na mguu wa bandia anaouvaa kupitwa na wakati huku mwingine ambao una afadhali ukisababisha mishipa ya mgongo kuhama.
“Hii hali inanikosesha raha, kwa kusimulia tu huwezi kunielewa msomaji lakini navimba na kuchanika, mara kwa mara mgongo unauma kitu ambacho sasa kinaniathiri kiakili kwani maumivu ni makali na natumia dawa za maumivu kila mara yanapotokea,” alisema Wastara.

AWAANGUKIA JPM, MAMA SAMIA NA MAKONDA
Wastara amemuomba Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, John Magufuli kuliingilia kati suala lake la Wachina wenye Kiwanda cha KZG ambao ‘wamemzima’ pesa hizo alizozitaja ili alipwe na aweze kupata matibabu kuokoa uhai wake.
Mbali na rais, amemtaka Mkuu wa Mkoa wa Dar, Paul Makonda ambaye muda mwingi amekuwa karibu na wananchi wake hasa wanapokuwa kwenye matatizo kulifuatilia suala lake na Wachina hao ili alipwe haki zake.
Pia msanii huyo alimuomba Makamu wa Rais, Mama Samia Suluhu kuangalia jinsi anavyoweza kumsaidia katika matibabu yake kwani hata mwanzo wa tatizo lake aliwahi kuwa naye karibu.
“Nimeamua kuwaandikia hata barua viongozi hao watatu wa nchi, huenda barua zangu hazijawafikia lakini kiukweli peke yangu bila mkono wao mimi siwezi, nahitaji pesa nyingi ambazo si familia wala mimi mwenyewe tunaoweza kuzipata kwa ajili ya matibabu yangu,” alisema Wastara.

AOMBA MSAADA KWA WATANZANIA
Mbali na kuomba msaada kwa viongozi hao, staa huyo ambaye maisha yake kwa sasa yanasikitisha amewaomba Watanzania wenye moyo wa huruma wamsaidie ili aweze kwenda kwenye matibabu kwani anajiona anakufa hivihivi.
“Watanzania wenzangu, naomba mnisaidie ninakufa najiona, mficha uchi siku zote hazai. Leo nimeona niweke ustaa pembeni, nimeamua kufunua mguu wangu mnielewe ni maumivu gani nayapata. Mimi nimejaribu kila aina ya biashara ambayo ni halali lakini nimeshindwa kupata pesa za kurudi kwenye matibabu, kwa yeyote aliyeguswa naomba anipigie simu kwa namba yangu hiyo hapo chini,” alisema Wastara.

ANAHITAJI MIL 37
Ili awe sawa, Wastara anahitaji milioni 37 kwa ajili ya kutengenezewa mguu ambao ndiyo dawa ya mgongo pia. Mguu huo pamoja na siku atakazokaa hospitali ndiyo gharama inayohitajika kwani atafikia kwenye Hospitali ya Sifael iliyopo India.

MGUU KUKATWA
Endapo atakosa pesa hiyo, inatakiwa akatwe mguu wake tena jambo ambalo hayuko tayari nalo huku akieleza kuwa hataweza kuendesha maisha yake kwa kutembelea magongo mawili.
Kumsikia Wastara akiongea kwa masikitiko fungua mtandao wa You Tube kisha andika neno Global TV ONLINE halafu bofya kwenye alama nyekundu yenye maandishi SUBSCRIBE, utaona habari yote ya Wastara.

NENO LA MHARIRI
Wastara anahitaji msaada wako, yeyote anayeweza kumsaidia awasiliane naye kwa namba yake 0768666113.

VIDEO:

GPL

Nafasi za Ajira Zilizotangazwa Leo

Miujiza ya Sharifu Seif Mohamed..JE Umeachwa na Mme/Mke au Mpenzi, Umesongwa na Mitihani ya Maisha..Piga Simu Upate Muujiza Wako

$
0
0
SHARIFU SEIF MOHAMED ANAWASHUKURU WALE WOTE WANAOENDELEA KUPIGA SIMU, WENYE MATATIZO NA WALE WANAOTOA  SHUKRANI NA SHUHUDA JINSI TIBA ZAKE ZINAVYO WASAIDIA,

(Rudisha mahusiano yako ndani ya masaa 72 tu)

SHARIFU MOHAMED Ni  mtaalam na mnajimu maarufu wa nyota na kubashiri mambo yanayo watesa binadamu duniani kote na kupata ufumbuzi, Anatumia kitabu cha QUR'AN, Dawa za Asili, Dawa za Kiarabu na majini kwa kumtuliza mke/mme, mchumba au mpenzi ndani ya masaa 72 tu, na kutatua matatizo yote ya kimaisha,

Je Umeachwa na UMPENDAE awe Mme/Mke na bado unampenda? Je Umekimbiwa na Mmeo/ Mkeo n anaishi na mtu mwingine? Je Umejaribu sehemu nyingi bila mafanikio? Mpigie simu SHARIFU SEIF sasa hivi ujionee Muujiza wa Papo kwa Papo, Anauwezo wa hali ya juu wa kusambaratisha mahusiano yao na kumrejesha kwako haraka sana na Kumfanya Atimize Ahadi zote Ndani ya Muda Mfupi Endapo Utafwata Atakacho Kuelekeza

ANAZO DAWA ZA MAPENZI, NGUVU ZA KIUME, CHANGO NGIRI MAJI NA N.K, ZINDIKO LA NYUMBA NA BIASHARA, PETE ZA BAHATI, HUMALIZA KABISA TATIZO LA NGUVU ZA KIUME NA KUREFUSHA UUME KWA SAIZI UNAYOTAKA, HUZUIA CHUMA ULETE KWENYE BIASHARA, HURUDISHA MALI ZILIZOPOTEA, MAGONJWA SUGU, MIGUU KUWAKA MOTO AU KUFA GANZI, HUTIBU BUSHA BILA KUPASUA, ANAO UWEZO WA KUMRUDISHA ALIE MBALI AU ALIECHUKULIWA MSUKULE, KUPANDISHA NYOTA NA KUSHINDA BAHATI NA SIBU, KASAFISHA NYOTA NA KUKUPA MVUTO WA AJABU, KUTOA NUKSI NA VIFUNGO MBALIMBALI,  MAFANIKIO YA MAISHA NA UTAJIRI BILA MASHARI, NA MENGINE MENGI YA SIRI,

Je UMAHANGAIKA KUPATA MTOTO BILA MAFANIKIO? WASILIANA NA MTAALAMU HUYU KWANI YEYE HUFAULU PALE WOTE WALIPOSHINDWA, PIA UMALIZA KAZI ZILIZO SHINDIKANA NA WATAALAM WENGINE NDANI YA MASAA 24 TU,

(NA ANATIBU KWA NJIA YA SIMU UKIWA NCHI YOYOTE AU MKOA WOWOTE ENDAPO UTAFWATA MAELEKEZO YAKE)

Kwa ushauri na mawasiliano  zaidi Piga SIMU No:

Mobile +255 654-836970
WhatsApp +255 756-033670

Brown Amshangaa Jack Wolper Kutangaza Ndoa na Mwanaume Mwingine Mwezi Mmoja tu Baada ya Kuachana

$
0
0

Kijana Brown ambaye alikuwa kwenye mahusiano na Jackline Wolper amesema mpaka sasa wana mwezi mmoja tangu wawili hao waachane, lakini tayari Jackline Wolper ameshapata mwenzi na ametangaza ndoa.

Mchungaji Peter Msigwa adai kuna njama za Kumwangamiza

$
0
0

Mbunge wa Jimbo la Iringa Mjini Chadema  Mchungaji Peter Msigwa amesema mbinu inayotumika  kuwashawishi na kuwanunua madiwani wa Chama hicho imelenga kupunguza nguvu zake katika kuikosoa Serikali.


Amesema taarifa hizo amepewa na viongozi wa CCM ambao wamemthibitishia  kuwa hawana shida nao.


"CCM hawana shida na madiwani, wanachama wanashida na wale wakosoaji wakubwa wa Serikali Kuu"amesema Msigwa


Msigwa amewataja wabunge wengine wa upinzani aliodai watapitia kipindi hicho kuwa ni Mbunge wa Jimbo la Hai  Freeman Mbowe, Mbunge wa Jimbo la Singida Mashariki Tundu Lisu, Mbunge wa Jimbo la Mbeya Joseph Mbilinyi, Mbunge wa Kawe Halima Mdee na Mbunge wa Arusha Mjini Godbles Lema.

Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) Yazijibu hoja za UKAWA

$
0
0

Tume  ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) imejibu hoja mbili kati ya 14 zilizowasilishwa kwake na Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa) huku ikisisitiza kuwa hoja zingine 12 hazimo ndani ya mamlaka yake.


Hata hivyo, Mwenyekiti wa Ukawa, Freeman Mbowe amesema tume kwa kutoa kauli hiyo, inakwepa wajibu wake na kuwa sehemu ya serikali.


Katika mkutano wake na vyama vya siasa jijini Dar es Salaam jana uliohudhuriwa na vyama 17 kati ya 19, Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa na Jeshi la Polisi, NEC ilisema imeamua kuuitisha kwa lengo la kupeana taarifa na kujadiliana mambo mbalimbali na uchaguzi mdogo katika majimbo matatu na madiwani katika kata sita Tanzania Bara.


Majibu ya hoja za Ukawa yalitolewa baada ya mchangiaji wa mada, Katibu Mkuu wa NCCR-Mageuzi, Juju Danda, kuhoji juu ya barua hiyo huku akiituhumu tume kunyamaza na kutoitisha mkutano wa wadau kabla ya kufanyika kwa uchaguzi mdogo.


"Ukawa tuliomba kukutana na wadau wote pamoja na tume kabla ya uchaguzi, lakini sasa mmetuita, mmeshapanga tarehe ya uchaguzi," Danda alisema.


"Wasimamizi wa uchaguzi ni makada, tunakwenda kushindana kwenye uchaguzi wa nini wakati mshindi anajulikana?” Danda alihoji.


Baada ya hoja hiyo, Mwenyekiti wa NEC, Jaji Semistocles Kaijage, alitoa barua ya Ukawa na kueleza kubainisha kuwa iliwafikia Desemba 14 na waliijibu siku nne baadaye na kurejesha majibu kwa aliyeiandika.


"Mwandishi wa barua ndiye alijibiwa, fuatilia kwenye vyama vyenu, aliyeandika alipata jibu na alijulishwa kwa maandishi, alitakiwa kufika leo kwenye kikao ili yaliyomo kwenye barua yaweze kujadiliwa, lakini hajafika,” alisema Jaji Kaijage.


Mwenyekiti wa NEC huyo alijibu hoja moja baada ya nyingine zilizowasilishwa kwao na Ukawa kupitia barua hiyo akibainisha kuwa hoja yao ya kwanza na ya pili ndiyo ziko ndani ya mamlaka ya tume, akianza na hoja ya kutolewa nje kwa mawakala wa uchaguzi na kuzuiwa kwa mikutano ya siasa nchini.


“Niwasihi sana viongozi wa vyama vya siasa, makosa yoyote yanayokiuka taratibu za kisheria, za kiuchaguzi, taratibu muhimu zinazomnyima mgombea haki ya kugombea na kupitishwa yafuate mkondo. Sheria na taratibu zetu hazijaacha ombwe, foramu imewekwa ya kuwasilisha tatizo hilo, hakuna sababu yoyote ya msingi kwa wakala kutolewa nje,” alisema na kueleza zaidi:


“Wakala anapotolewa maana yake uchaguzi haujaenda vizuri, na sheria imeweka utaratibu wa wapi malalamiko yapelekwe ili ufumbuzi upatikane."


Mwenyekiti wa NEC huyo alisema kama kuna wakala alitolewa nje, uchunguzi ufanyike na hatua zichukuliwe kwa mujibu wa sheria za nchi, maadili, taratibu na kanuni.


Jaji Kaijage alisema hoja ya pili ni madai ya Ukawa kuwa matokeo halisi hayatangazwi akifafanua kuwa kifungu cha 81 cha Sheria ya Uchaguzi na kifungu 82 cha Uchaguzi wa Serikali za Mitaa, vinaeleza anayetangazwa kuwa mshindi ni ambaye amepata kura nyingi halali zaidi ya mwingine.


“Lalamiko la msingi kuwa matokeo halisi kutotangazwa, pengine ambaye siyo mshindi ndiye katangazwa, hili ni kosa kubwa sana. Sheria ya Uchaguzi na Sheria ya Serikali za Mitaa imeweka wazi kwamba malalamiko yenye ushahidi wa msingi ya kukiuka sheria na taratibu, ana haki ya kwenda mbele ya vyombo vya sheria kulalamika na ikithibitika uchaguzi unatenguliwa,” alisema na kuongeza:


“Laiti kama haya na mengine yangewasilishwa katika mamlaka za kisheria na kanuni yangekuwa yamepata majibu. Kusita au kukataa kwa sababu nyingine ndiyo kunaleta malalamiko. Tulishasema malalamiko yote yaliyopo humu (barua) hakuna ambalo haliwezi kushughulikiwa chini ya sheria za nchi."


Kuhusu kupigwa marufuku kwa mikutano ya vyama vya siasa, Jaji Kaijage alisema majukumu ya NEC yako kwenye katiba na sheria, hivyo ni suala ambalo haliko kwenye mamlaka ya tume na wanabaki kuwa wasikilizaji pekee.


Alisema hoja ya tatu ya Ukawa ni kuwapo kwa mauaji nchini ambayo alikiri kuwa ni tatizo na ni kosa kubwa la jinai, lakini akasisitiza kuwa halipo ndani ya majukumu ya NEC.


“Tume kuitisha kikao cha kujadiliana kuhusu mauaji tunaweza kushtakiwa kwa kuparamia mamlaka na madaraka ambayo tume haina," Jaji Kaijage alieleza.


Alibainisha kuwa hoja ya nne ya Ukawa ni madai ya kuminywa kwa vyombo vya habari, akieleza kuwa suala hilo pia lipo nje ya mamlaka yao na kwamba linaweza kuwaingiza kwenye matatizo.


"Uchaguzi hauwezi kutenguliwa na huwezi kuitisha kikao kujadili mambo ambayo tume haina mamlaka nayo," alisema.


Aliitaja hoja ya tano kuwa ni vituo kuvamiwa wakati wa kuhesabu kura akifafanua kuwa vifungu na maelekezo yametolewa vizuri kabla ya kuanza upigaji wa kura na wakati wa kufunga kituo kuna fomu maalum inajazwa kama kuna malalamiko yoyote yanaainishwa.


Alisema kama tatizo lilijitokeza, kanuni na taratibu zinaweka wajibu kwa msimamizi wa kituo kutoa ufafanuzi, kama hakutoa inakuwa ndiyo msingi wa kupeleka kwenye mamlaka za kisheria.


Jaji Kaijage alisema hoja zingine za Ukawa ni kutaka kuwa na tume huru, katiba mpya, mikutano ya hadhara, maandamano na kutofanya kazi za kisiasa.


"Sisi kama Tume tunafuata Katiba, sheria zilizopo, kanuni, suala la kikatiba tunajiuliza hivi tume inayo mamlaka ya kufanya marekebisho ya sheria au kuhitisha mkutano wenye lengo la kuweka sawa katiba inayolalamikiwa," Jaji Kaijage alisema na kuongeza:


"Tume inaweza ikatoa ufumbuzi juu ya kuruhusiwa au kutoruhusiwa kwa mikutano ya hadhara?


"Kuhusu katiba mpya, sisi tunaweza tukatoa maoni kama watu wengine mbele ya chombo kilichokabidhiwa jukumu la kufanya marekebisho ya katiba au sheria."


Alisema lawama kwa tume ni zinapaswa kuwa kushindwa kutekeleza mamlaka yake, kanuni na sheria zinazoongoza uchaguzi.


“Tume iko makini kuhakikisha inafuata taratibu zote za kisheria, kanuni na kimaadili. Tume itakuwa ya mwisho kukiuka sheria, taratibu na katiba ya nchi,” alisema.


Katika mkutano huo, baadhi ya wajumbe waliitaka tume kutokukwepa majukumu yake kwa kuwa ndiyo chombo mama na kwamba siyo dhambi kuishauri serikali pale wanapoona wana nafasi ya kufanya hivyo.


“Mtu anafika kituoni na mapanga anakata watu, ukilalamika unaambiwa ni suala la polisi. Tume haichukui hatua, unatuambie tukaelimishe wananchi, lakini wanajua wamezuiliwa kufanya mikutano, kazi yao ilikuwa ni kuelimisha jamii,” alisema mmoja wa wajumbe waliohudhuria mkutano huo.


Katika mkutano huo, Mkurugenzi wa NEC, Kailima Ramadhani, aliwasilisha taarifa ya maandalizi ya uchaguzi mdogo katika majimbo ya Longido, Singida Kaskazini na Songea mjini na kata sita, akibainisha kuwa Chadema na NCCR- Mageuzi wamesusa.


Mbowe Afunguka:

Akizungumza jana, Mbowe alisema katika mambo yanayohusu uchaguzi na maisha ya watu, hakutakiwi kuangalia kama lipo ndani ya mamlaka au la, bali kinachotakiwa ni kushauriana.


“Kuna mambo kadhaa wanajadiliana, jambo linahusu idara nyingine na kuishauri ni mambo ya kawaida katika uongozi, NEC kama mhusika mkuu wa uchaguzi, watendaji wengine wa idara za serikali wanapofanya mambo yaliyo kinyume ni wajibu wao kukemea,” alisema.


Mbowe alisema polisi wanapoumiza wafuasi wa chama fulani katika uchaguzi ni ngumu kusema NEC haihusiki na wanaohusika ni polisi pekee. Alisema wajibu wao ni kuhakikisha uchaguzi unakuwa huru na haki kwa njia zote za amani na haki.


“Jambo lolote linapoibuliwa halijadiliwi kwenye mkutano wa waandishi wa habari, bali wadau wakiwa na kikao cha ndani. Tuliwaandikia tukutane na NEC, polisi, usalama wa taifa na Msajili wa Vyama vya Siasa,” alisema.


Mbowe ambaye pia ni Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni, alidai uchaguzi mdogo uliopita ulikuwa na kasoro mbalimbali zinazolalamikiwa na wadau, lakini inashangaza tume kusema haikuona tatizo.


Kiongozi huyo wa Ukawa pia alidai kikao kilichofanyika jana kilipangwa kufanyika mapema zaidi lakini kikaahirishwa na kwamba Chadema hawakupata barua ya tarehe mpya ya kikao.


“Tulikuwa Nairobi, Kenya kwa ajili ya kumsafirisha Tundu Lissu. Kikao kiliitwa mwezi uliopita, kikahairishwa japo hawakueleza agenda za kikao. Taarifa za uwapo wa mkutano mimi (Mwenyekiti), Makamu Mwenyekiti na Katibu Mkuu hatuna taarifa,” alisema na kuongeza:


“Tuna wajibu wa kuhakikisha nchi inakuwa na uchaguzi wa haki amani, kila mmoja aone faida ya vyama vya siasa na siyo hasara.


“Tatizo lililopo, tume inajiona wao ni serikali, wanatuangalia kama watu wa kupambana nao, kukinzana na hoja na siyo watu wa kushirikiana kutafuta suluhisho. Ndiyo maana kila tukilalamika wanajenga ‘defence’ (kujilinda), wameegemea upande wa serikali.


“Ni bahati mbaya sana iliyopo nchini kwamba vyombo vyetu vya kusimamia mambo ya kuleta umoja katika taifa wanaanza kuwa sehemu ya vyama, wanashiriki upande mmoja na kukandamiza haki ya upande wa pili na wanadanganya umma kuwa haki inatolewa kumbe haitolewi."


Awali wakati wa mkutano Mwakilishi wa ACT-Wazalendo, Msafiri Mtemelwa, alisema Chadema hakikufika kushiriki kwa kuwa imekuwa kawaida kuzungumza lakini mambo hayashughulikiwi.


“Jeshi la Polisi linatumika vibaya, magari ya polisi maana yake wapinzani wasijitokeze watakamatwa, kwanini polisi wanaenda na magari yenye bendera nyekundu, mavazi ya kutisha wananchi?" Alihoji.


Aliitaka tume kuacha kuwatumia wakurugenzi wa halmashauri kusimamia uchaguzi na wakuu wa wilaya na mikoa kuacha kufanya siasa.


“Unakuta RC na DC ambao ni wenyeviti wa kamati za ulinzi na usalama wanafanya kampeni za CCM. Ndiyo maana tunasema wapeni ushindi CCM waendelee kutawala, hakuna haja ya kufanyika uchaguzi,” alisema Mtemelwa.


Katibu Mkuu wa Sau, Jonson Mwangosi na Lulu Kimwaga wa Tadea, waliiomba tume kusaidia vyama visisivyo na uwakilishi bungeni vipate ruzuku ili viweze kushindana kwenye chaguzi mbalimbali.


“Uchaguzi wa sasa ni sawa na kumpa nyama kibogoyo ashindane na mwenye meno," alisema Kimwaga.


Mwezi uliopita Ukawa kupitia kwa Mbowe ulitangaza kususa kushiriki uchaguzi mdogo wa majimbo matatu na kata sita uliopangwa kufanyika Jumamosi ukitaka uitishwe kwanza mkutano wa NEC na wadau wa uchaguzi kujadili na kuzitafutia ufumbuzi changamoto zilizojitokeza katika uchaguzi mdogo wa madiwani wa kata 43 Tanzania Bara uliofanyika Novemba 26.

Msanii aliyesambaza picha za uchi aomba radhi baada kufungiwa

$
0
0

Msanii filamu na video vixen, Suzan Michael maarufu kama Pretty Kind amefunguka na kuomba radhi kwa Serikali na Watanzania kwa ujumla kutokana na vitendo vyake vya kupiga na kuweka picha mitandaoni za nusu uchi.


Akiongea jana na waandishi wa habari muda mfupi baada ya kufungiwa na serikali kujihusisha kufanya kazi zozote za sanaa kwa miezi sita, Pretty Kind alisema kuwa amejifunza na kugundua kuwa alikuwa anafanya makosa hivyo sasa hataweza kurudi tena kufanya mambo hayo.


“Naomba niombe radhi kwa Watanzania wote kwa hiki nilichokifanya natambua nimefanya kosa naomba msamaha aweze kunisamehe, pia naomba msamaha kwa mashabiki zangu kwa hiki kilichotokea nimejifunza hivyo nitakuwa Pretty Kind mwingine mpya na kufanya yale yanayotakiwa katika jamii” alisema


Pretty Kind amefungiwa kujihusisha na sanaa kwa takribani miezi sita baada ya kuposti picha katika mtandao wake wa Instagram ikimuonyesha akiwa nusu utupu jambo ambalo ni kinyume na maadili ya Kitanzania na kwenda kinyume na maagizo ya Rais John Pombe Magufuli ambayo aliyatoa hivi karibuni kuwataka wasanii wa kike kuvaa kwa staha.

Ukikutwa wamesimama na wanafunzi wa kike, viboko 12

$
0
0

Wakati uongozi wa kata ya Nyehunge wilayani Sengerema ukipitisha sheria ya kuwacharaza viboko 12 au faini ya Sh10,000 wanaume watakaokutwa wamesimama na wanafunzi wa kike, Wilaya ya Tandahimba imekamata wanafunzi watano waliopata ujauzito mwaka jana.

Sheria hiyo ndogo imepitishwa juzi kwenye kikao cha maendeleo ya kata (WODC) baada ya tatizo la wanafunzi kukatisha masomo kutokana na kupata uja uzito kuzidi kuwa sugu.

Ofisa mtendaji wa Kata ya Nyehunge, Mabula Enock alisema sheria hiyo itasaidia kudhibiti vitendo vya wanaume wanaoshawishi wasichana kufanya nao mapenzi na baadaye kuwapa ujauzito unaokatisha ndoto zao.

“Tumelazimika kupitisha sheria hiyo ili kuungana na mkuu wa wilaya yetu, Emmanuel Kipole aliyeagiza wanaume watakaokutwa wamesimama na wanafunzi wacharazwe viboko au kutozwa faini ya Sh10, 000 ama vyote kwa pamoja,” alisema Enock.

Agizo la mkuu huyo wa wilaya alilitoa Oktoba mwaka 2017 wakati akikaribisha wanafunzi 81 kujiunga na masomo ya kidato cha tano katika Shule ya Sekondari ya Nyehunge.

Mkazi wa kata hiyo, Mussa Kazimili alisema sheria hiyo ndogo itasaidia kupunguza tatizo hilo na kuwataka wananchi na wazazi kusaidia kubaini wanaume watakogundulika kufanya vitendo hivyo.

Diwani wa kata hiyo, Charles Mbogo alisema kitendo cha kukatiza masomo si cha kuungwa mkono, hivyo adhabu inapaswa kuongezwa na kuitaka jamii kuachana na suala hilo.

Kwa mujibu wa takwimu zilizotolewa na ofisa elimu ya sekondari wa Buchosa, Benjamini Siperato halmashauri hiyo ina jumla ya wanafunzi 1,136 katika shule 20 za sekondari 20 na mwaka 2016/17 wanafunzi 18 wa kike walipata ujauzito, hivyo jamii inapaswa kuacha tabia ya kuwarubuni watoto wa kike.

Wakati huohuo, serikali wilayani Tandahimba imewakamata wanafunzi watano waliopata ujauzito kwa lengo la kutaka habari kuhusu wanaume waliowapa ujauzito na kukatiza masomo yao.

Katibu tawala wa wilaya hiyo, Mohamed Azizi, ambaye alikuwa akizungumza kwa niaba ya mkuu wa wilaya ya Tandahimba, Sebastian Waryuba, alisema wanafunzi ha walikamatwa na watoto wao, lakini wahusika hawajakamatwa.

“Tumefanikiwa kuwakamata wazazi na wanafunzi watano wakiwa wamejifungua. Kati yao, mmoja aliacha shule akiwa kidato cha nne,” alisema.

“Wengine watatu wa kidato cha pili. Baada ya kuzungumza nao wamesema hawapati huduma zozote kutoka kwa wahusika ambao wamewapa ujauzito. Hali hiyo ni wazi kuwa inawapa shida wazazi.”

Alisema wazazi wamekuwa wakilaumiwa kwa kushindwa kutekeleza majukumu yao ipasavyo ili kuhakikisha watoto wao wanamaliza elimu ya sekondari bila kupata ujauzito.

“Inasikitisha. Mmoja ameacha shule akiwa kidato cha nne mwaka jana, alibakiza siku chache tu aweze kumaliza masomo yake. Hili liwe somo kwa wazazi na wanafunzi wengine.

Kauli ya Kingunge yawaibua Wapinzani

$
0
0

Viongozi wa vyama vya upinzani wamesema kauli ya mwanasiasa mkongwe nchini, Kingunge Ngombale Mwiru kwamba CCM ni chama chake, ni maoni yake binafsi na hayaondoi ukweli kuwa ameshiriki kukijenga chama hicho tawala.

Akizungumza na Rais John Magufuli aliyemtembelea hospitalini juzi, Kingunge alisema: “CCM ni chama changu, nimetoka tu, nimeachana. Lakini nimefanya kazi zote. Nimejipinda mimi kwelikweli. Kwa hiyo hakiwezi kuwa kinyume changu hata kidogo.”

Kauli hiyo ilitafsiriwa na Rais Magufuli kuwa Kingunge bado ni CCM moyoni, lakini wapinzani waliohojiwa na Mwananchi wana maoni yao.

“Hiyo huwa haibadiliki. Ukiasisi chama na ukiachana nacho, utaendelea kuwa muasisi wake,” alisema mwenyekiti wa Kamati ya Uongozi ya CUF, Julius Mtatiro ambaye pia sema kauli ya mwanasiasa huyo mkongwe pia ililenga kumkumbusha Rais kwamba pamoja na yote yaliyotokea, Kingunge ataendelea kuwa muasisi wa CCM.

“Nadhani hicho ndicho alichokilenga Kingunge. Ni kama alikuwa anamkumbusha Rais,” alisema Mtatiro.

Kingunge aliyetengaza kuhama CCM Oktoba 4, 2015 alitoa kauli hiyo juzi akiwa kitandani Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) ambako anatibiwa majeraha ya kung’atwa na mbwa takribani siku sita zilizopita.

Katika maelezo yake, Mtatiro alisema Kingunge ana haki ya kutoa maoni na kwamba huo ndio ukweli.

“Tangu kuanzishwa kwa TANU wao ndiyo waliokipigania na kuunda CCM na ndiyo wazee ambao wamekifikisha kile chama kilipo leo. Waliopo sasa wamekikuta na kuendeleza walipoishia wao,” alisema Mtatiro.

“Kauli yake inamaanisha kuwa hata akipata matatizo, wana-CCM hawataweza kumkimbia pamoja na kwamba alijitoa.”

Alisema japokuwa mwanasiasa huyo hakuwahi kusema amejiunga na chama gani, aliondoka CCM vizuri na aliweka wazi sababu za kukikimbia chama hicho.

Naye katibu mkuu wa NLD, Tozi Matwange alisema kauli ya Kingunge haumaanishi kuwa anaweza kurejea.

Alisema kauli ya mwanasiasa huyo inaonyesha dhahiri kwamba CCM ni chama chake kwani alishiriki kukiasisi, kukisimamia.

“Ametoka huko na hatabadilika,” alisema.

Katibu mkuu wa NCCR– Mageuzi, Danda Juju alisema Kingunge amefanya kazi kubwa akiwa ndani ya CCM katika kipindi chote cha maisha yake, hivyo kauli hiyo anatafsiri kuwa kumbukumbu zake bado zipo katika chama hicho japokuwa amekiacha.

Wakati huohuo, mtoto wa mwanasiasa huyo, Kinje Mwiru ameliambia gazeti hili kuwa juzi mchana walimpa taarifa Kingunge kuhusu kifo cha mkewe, Pares na jana akaridhia azikwe Alhamisi.

Pares alifariki dunia Januari 4 saa 8:00 mchana akiwa wodi ya Sewahaji alikokuwa amelazwa, tangu Oktoba 3 mwaka jana.

“Mzee ametupa mwongozo wa nini cha kufanya. Mazishi yatafanyika Alhamisi katika makaburi ya Kinondoni,” alisema.

“Mpaka sasa ratiba bado haijapangwa na leo jioni (jana) familia itakutana na kutakuwa na kikao pale nyumbani,” alisema.

Pata Tiba ya Tatizo la Nguvu Za Kiume........Inasaidia Kukufanya Urudie Mara 5 na Kuchelewa Kwa Dakika 20

$
0
0
TATIZO LA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME NA MAUMBILE MADOGO LINATIBIKA.Baada ya utafiti wa mda mrefu juu ya matatizo ya upungufu wa nguvu za kiume na ukosaji wa hamu ya tendo la ndoa ama kushindwa kurudia tendo kwa haraka DR Magise imekuletea tiba ya matatizo hayo kwa kutumia dawa za:


FULL POWER: Ni dawa asili ya vidonge inayotibu tatizo la upungufu au ukosefu wa nguvu za kiume,dawa hii inamchanganyiko wakutosha wenyekuzalisha vichocheo vingi vya Hemone za Gestrogen vikiwemo vitamin B6&B1,vitamini E,pamoja na madini aina ya zinc vitakufanya kuwa na nguvu na mzunguko mzuri wa damu na kuongeza hamu na uwezo wa kufanya tendo la ndoa zaidi ya hatua nne au zaidi,na kuchelewa kufika kileleni zaidi dakka 20-30.


NYAMVA: Inarutubisha maumbile ya uume yani kurefusha na kunenepesha nchi 4-7 upana cm3-4 standard kiafya haijalishi umri wako hata kwa wazee ukiitumia maumbile yako yatabaki kuwa hivyo siku zote,Pia tunatibu Presha,kisukari siku7,ngiri,chango la tumbo tumbo kujaa gesi,kutopata choo vizuri

 TUPO TZ DAR ES SALAAM   MBAGALA RANGI TATU.HUDUMA HII UTALETEWA POPOTE ULIPO .WASILIANA NAMI 0783741788/ 0715741788 -DR MAGISE

Magufuli Aanika Madudu Mengine ya Wizara ya Madini

$
0
0
Magufuli Aanika Madudu Mengine ya Wizara ya Madini
RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli ameanika madudu mengine ya Wizara ya Madini akisema kuwa baadhi ya wateule wake katika wizara hiyo wamekuwa wazembe katika kutekeleza maagizo na kutimiza majukumu yao kama watendaji wa serikali.



Magufuli ameyasema hayo leo Jumatatu wakati akimwapisha Mhe. Dotto Mashaka Biteko kuwa Naibu Waziri wa Madini Ikulu jijini Dar es Salaam. Rais ametolea mfano wa sheria mpya ya madini iliyopitishwa bungeni mwezi Julai mwaka jana, ambapo amesema mpaka sasa wizara hiyo haijapitisha kanuni (regulations) ili sheria hiyo iweze kufanya kazi jambo ambalo amesema ni uzembe usiovumilika huku akimwagiza Waziri wa Sheria, Prof. Palamagamba Kabudi kukamilisha kanuni hizo na kuzisaini kufikia Ijumaa ya wiki hii.



“Nakushukuru Mhe spika kwa kutoa ushauri kwa serikali na sisi tumekuwa tukiufuata sana. Wizara ya madini ina changamoto sana na hata sasa ina changamoto na haifanyi kazi vizuri. Spika utakumbuka mwezi wa saba mlifanya marekebisho ya sheria ya madini. Na ilipokuja kwa kwangu siku hiyo hiyo nilisaini na kuipitisha, lakini tangu Julai mpaka sasa regulations (kanuni) hazijasainiwa lakini sheria imepitishwa na bunge, hivyo sisi Watanzania watumishi hatupo serious.



“Nasikitika kusema baadhi ya ninaowateua hawajajua nataka nini. Ndiyo maana nikamteua aliyekuwa kwenye kamati ya madini, labda atatoa changamoto kwa wenzake maana huenda yeye anaelewa zaidi. Na mnada wa Tanzanite hautafanyika tena mpaka regulations zitakaposainiwa. Sasa mpo manaibu wawili na waziri wa sheria yupo hapa nataka regulations hizi zisainiwe kabla ya Ijumaa, tumeibiwa mno, sasa nimesema imetosha,” alisema Rais Magufuli kwa uchungu.

Biteko Aapishwa Ikulu Leo Kuwa Naibu Waziri wa Madini

$
0
0
Biteko Aapishwa Ikulu Leo Kuwa Naibu Waziri wa Madini
Rais Dkt. John Pombe Magufuli ameamuapisha Mhe. Doto Mashaka Biteko kuwa Naibu Waziri wa Madini, Ikulu Jijini Dar es Salaam leo Jumatatu, Januari 8, 2018, asubuhi.


“Kwanza namshukuru Mungu  kwa siku ya leo na namshukuru kwa kuweza kutokea haya yote. Nakushukuru wewe Mheshimiwa rais kwa kuweza kuniteua, sina la kukupa ila kutenda kazi kwa bidii. Mhe. Rais nina bahati kubwa sana na hata wewe umelishuhudia kwenye mikutano mingi sana, umenipa sifa kubwa kwa kuhudumu chini ya mwanamke ambaye ni mchapa kazi sana. Niko tayari kufanya kazi kwa bidii na namuomba Mungu usije jutia uamuzi wako,” alisema Biteko.



Naye Mhe. Spika Ndugai alipota fursa ya kuzungumza akasema;
“Sisi Bunge tumekuwa tukishauri kwa muda sana kwa serikali kuwa wizara ya nishati na madini imekuwa wizara kubwa na nzito sana na nashukuru umeifanyia kazi kwa kuweka wizara mbili za madini na nishati. Tunakushukuru sana mheshimiwa Rais. Mhe. Dotto ni mchapakazi na ana utumishi uliotukuka,” alisema Ndugai.

Lava Lava Ameamua Kuja na Kilio

$
0
0
Lava Lava Ameamua Kuja na Kilio
Ikiwa ni muda mchache tu! toka aachia video ya ngoma yake mpya iitwayo ‘Teja’ Lava Lava ameamua kuachia ngoma nyingine iitwayo ‘Kilio’ audio ya ngoma hiyo imetayarishwa na Laizer wakati video imeongozwa na Zoom Production.

Huyu ni msanii mwingine kutoka WCB kuachia ngoma mfululizo kama ilivyokuwa mwishoni mwa mwaka 2017 ambapo Diamond Platnumz aliachia video mbili ziitwazo’Niache’ na ‘Sikomi’

Kijana Mmoja Afariki Dunia Wakati Akiwa Anaanika Nguo

$
0
0
Kijana Mmoja Afariki Dunia Wakati Akiwa Anaanika Nguo
Kijana mmoja aliyetambulika kwa jina la Rahimu Haruni (30) ambaye anaishi mtaa wa Mwembesongo Manispaa ya Morogoro amefariki dunia leo wakati akianika nguo kwenye waya uliofungwa ndani ya nyumba hiyo baada ya kupigwa shoti ya umeme.


Taarifa zilizothibitishwa zinadai kuwa nyumba hiyo ambayo kijana huyo amepigwa shoto ilikuwa na tatizo la umeme ambalo lilitolewa taarifa kwenye shirika la Umeme TANESCO mkoa wa Morogoro lakini tatizo hilo lilishindwa kutatulia na TANESCO mpaka leo ambapo shoti hiyo imesababisha kifo cha kijana huyo.   

Baada ya kutoa kifo cha kijana huyo kabla ya mwili wake kuondolewa ndipo mafundi wa TANESCO walipofika na kuzima umeme kwa ajili ya kuanza uchunguzi wa tatizo hilo chini ya ulinzi wa jeshi la polisi kwa kuhofia wananchi kuchukua sheria mkononi dhidi ya mafundi hao wa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO).

Ushoga Huu wa Aunt Ezekiel na Shamsa Ford Waibua Mambo

$
0
0
Ushoga Huu wa Aunt Ezekiel na Shamsa Ford Waibua Mambo
USHOSTI uliochipuka na kukolea hivi karibuni wa mastaa wa sinema za Kibongo, Shamsa Ford na Aunt Ezekiel, umeibua mambo huku wengi wakihoji ulikoanzia kwa sababu haukuwahi kuwepo na kwamba hawaendani.


Wakizungumza na Ijumaa Wikienda kwa nyakati tofauti, mastaa hao walisema kuwa, wanashangazwa na watu wanaohoji urafiki wao huo ulianza lini na wengine wakisema hawapendezani ambapo Shamsa alisema kuwa, wanaoongea hivyo wamekosa vitu vya kufanya.



Kwa upande wa Aunt aliliambia gazeti hili kuwa, wanaojadili urafiki wake na Shamsa hawana jipya kwani alishakuwa na marafiki wangapi hadi waujadili huo wa sasa? “Nimeshakuwa na marafiki wengi sana. Kwa nini wajadili urafiki wangu na Shamsa?” Alihoji Aunt

Rais Magufuli Ameteua Kamishina Mpya wa Madini

$
0
0
Rais Magufuli Amemteua Kamishina Mpya wa Madini  Leo Wakati wa Sherehe za Kumuapisha Biteko
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dr. John Pombe Magufuli ametangaza kumteua Kamishina mpya wa Madini ambaye pia atasimama kama Mtendaji Mkuu wa Tume ya Madini.

President Magufuli ametangaza uamuzi huo katika hafla iliyofanyika Ikulu Jijini DSM ya kumuapisha Dotto Biteko kuwa Naibu Waziri wa Madini. Ambapo amemteua Prof. Shukuruni Elisha Manya kuwa Kamishina wa Madini.

“Nimeambiwa Kamishina wa Madini ni tatizo inawezekana yupo hapa, Nimeamua kumteua Prof. Elisha Manya atakuwa Kamishina wa Madini na ndo atakuwa Mtendaji Mkuu wa Tume ya Madini.”- President Magufuli

“Nimeambiwa Kamishina wa Madini ni tatizo inawezekana yupo hapa, Nimeamua kumteua Prof. Elisha Manya atakuwa Kamishina wa Madini na ndo atakuwa Mtendaji Mkuu wa Kamishina ya Madini.”- President Magufuli

Marekani: Tuko Tayari Kusaidia Uchunguzi wa Shambulio la Tundu Lissu Iwapo Tutaombwa

$
0
0
Marekani Yasema Iko Tayari Kusaidia Uchunguzi wa Shambulio la Tundu  Lissu Pale  Waatakapoombwa
Wakati mbunge wa Singida Mashariki (Chadema), Tundu Lissu akiwa amewasili nchini Ubelgiji kwa matibabu zaidi, ubalozi wa Marekani nchini umesema uko tayari kusaidia uchunguzi dhidi ya shambulio lake iwapo utaombwa.

Mbali na ubalozi huo, Umoja wa Ulaya (AU) nao umesema unategemea kuona maendeleo mazuri kutokana na uchunguzi wa tukio hilo unaoendelea.

Familia ya Lissu na chama chake cha Chadema vimekuwa vikisisitiza haja ya uchunguzi wa shambulio dhidi ya Lissu lililofanywa na watu wasiojulikana mjini Dodoma, ufanywe na taasisi huru na mwishoni mwa wiki mwanasheria huyo wa kujitegemea aliomba jumuiya ya kimataifa iingilie kati.

Hata hivyo, Jeshi la Polisi limekuwa likisema kuwa bado lina uwezo wa kuchunguza tukio hilo.

Pia Waziri wa Mambo ya Ndani, Mwigulu Nchemba alisema uchunguzi ulikamata magari zaidi ya kumi 10 yanayofanana na lililotajwa kuhusika katika tukio hilo, lakini hakuna mtu aliyekamatwa.

Baadaye Oktoba 8, Mkuu wa Jeshi la Polisi (IGP), Simon Sirro alisema mjadala wa tukio hilo umefungwa.

Kwa sasa Lissu, aliyekuwa akitibiwa Hospitali ya Nairobi nchini Kenya ameruhusiwa kutoka na amehamishiwa Ubelgiji kwa matibabu ya awamu ya pili yakayohusisha mazoezi baada ya mifupa yake kuharibiwa na risasi katika shambulio hilo la Septemba 7.

Msemaji wa Jeshi la Polisi, Barnabas Mwakalukwa alisema jana kuwa chombo hicho hakizungumzii suala la Lissu.

Akijibu swali la gazeti lililomtaka kutoa maoni yake kuhusu kutokubaliwa kwa wachunguzi wa kimataifa kusaidia upelelezi dhidi ya shambulizi la Lissu, ofisa ubalozi wa Marekani nchini alisema kwa njia ya barua pepe kuwa itakuwa tayari kutoa ushirikiano wake ikiwa itaombwa na Serikali ya Tanzania.

“Wakati Serikali ya Marekani huko nyuma imekuwa ikitoa ushirikiano katika baadhi ya uchunguzi wa kimataifa, kufikiria uwezekano wa kushiriki, utahitaji kwanza ombi la msaada kutoka Serikali ya Tanzania,” inasema barua pepe kutoka ubalozi wa Marekani.

Barua hiyo pepe inataka mtoaji taarifa hiyo anukuliwe kama ofisa ubalozi wa Marekani jijini Dar es Salaam.

Lissu alishambuliwa wakati akiwa nje ya makazi yake mjini Dodoma, akiwa ndani ya gari lake.

Mbunge huyo aliwaambia waandishi wa habari jijini Nairobi kuwa nyumba hiyo ni moja ya zile za viongozi zilizopo eneo hilo ambazo zinalindwa wakati wote na kwamba eneo la kuingilia kwenye nyumba hizo lina geti ambalo hukaa askari wakati wote, lakini siku hiyo hawakuwepo.

Kama Marekani wataombwa kushiriki uchunguzi huo, haitakuwa mara ya kwanza kuja nchini. Mwaka 2013 Shirika la Uchunguzi la Marekani (FBI) lilichunguza mauaji ya aliyekuwa Paroko wa Parokia ya Mpendae, Padri Evarist Mushi aliyeuawa kwa kupigwa risasi na watu wasiojulikana.

Hata hivyo, mtuhumiwa aliyebainishwa na FBI, Mussa Omar Makame alikuja kuachiwa na Jeshi la Polisi baada ya ushahidi kutotosha kumtia hatiani.

Mbali na kauli hiyo ya ubalozi huo, mkuu wa ujumbe wa Umoja wa Ulaya (EU) nchini, Balozi Roeland van de Geer ameliambia gazeti hili kwa njia ya barua pepe kuwa jumuiya hiyo imekuwa ikifanya majadiliano na Serikali kuhusu masuala ya haki za binadamu, siasa na uchumi yanayoibuliwa na kwamba unaamini uchunguzi wa shambulio la Lissu utapiga hatua.

“Umoja wa Ulaya na nchi wanachama wake wana mazungumzo ya mara kwa mara yakiwemo ya kisiasa yaliyowekewa utaratibu rasmi, masuala yanayohusu haki za binadamu pamoja na siasa na kiuchumi kwa pande zote, Tanzania na Ulaya huibuliwa na kujadiliwa,” inasema baruapepe ya Balozi Geer.

“EU na wanachama wake na Tanzania wataendelea na mazungumzo haya ikiwa ni pamoja na matukio ya kisiasa ya hivi karibuni. EU inaamini kuwa kutakuwa na maendeleo katika uchunguzi wa jaribio la maisha ya Lissu.”

Hata hivyo, Wakili maarufu nchini, Dk Onesmo Kyauke alisema suala la kuita vyombo vya kimataifa kuchunguza ni gumu kwa sababu linaingilia mamlaka ya ndani ya nchi.

“Kila nchi ina vyombo vyake vya usalama vinavyoshughulikia uhalifu wa ndani. Nchi inaweza kuomba msaada wa kimataifa kama kuna makosa yaliyovuka mipaka kama ugaidi au kutakatisha fedha, lakini makosa ya ndani inakuwa vigumu, kwa sababu lazima waseme wameshindwa,” alisema Dk Kyauke.

Alisema bado ana imani ya vyombo vya ndani vya usalama, hata kama vimekaa kimya.

Aliongeza kuwa sheria zinaruhusu watu kufanya uchunguzi wao binafsi, lakini pia zinaruhusu mwendesha mashtaka wa Serikali kuuchukua uchunguzi huo kwa manufaa ya Serikali.

“Zipo sheria zinazoruhusu watu kufanya uchunguzi wao binafsi, lakini pia sheria hizo hizo zinampa mamlaka DPP kuchukua suala hilo kwa manufaa ya Serikali.”

Alipoulizwa maoni yake kuhusu suala hilo, Profesa wa sayansi ya siasa wa Chuo Kikuu cha Ruaha mkoani Iringa, Gaudence Mpangala alisema shambulio la Lissu limeshachafua taswira ya Tanzania kimataifa.

“Hili suala lina impact (athari) kubwa kimataifa, siyo la kuchukulia kijuujuu,” alisema.

Profesa Mpangala alipendekeza kuwepo mjadala kujadili demokrasia na uhuru wa maoni.

Alisema ni muhimu kujadili suala hilo kwa kuwa hata wakati wa mfumo wa chama kimoja, muasisi wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere alikubali kukosoa Serikali.

 Chanzo: Mwananchi

Mabasi ya Mikoani Kufanya Safari Zake kwa Saa 24

$
0
0
Mabasi ya Mikoani Kufanya Safari Zake kwa Saa 24
Mamlaka ya Usafiri wa Majini na nchi kavu Tanzania (SUMATRA) imetoa maelezo kwa nini inakusudia kuruhusu mabasi yanayofanya safari zake kwenda mikoani, kufanya safari zake kwa saa 24.


Akizungumza na mwandishi wa www.eatv.tv Mkurugenzi wa Barabara SUMATRA Bwn. Johansen Kahatano, amesema wameona kuna uhitaji mkubwa kwa abiria, na kama njia mojawapo ya kupunguza msongamano wa mabasi barabarani.

"Tupo kwenye maandalizi bado hatujaamua, mambo yakikaa sawa sawa tutakwenda na utaratibu huo wa saa 24, ni mahitaji ya wananchi kwamba watu wangependa wafanye kazi muda wote, na matumizi ya magari yenyewe yanaweza yakaenda yakarudi yakaenda, lakini pia kupunguza msongamano wa mabasi pale Ubungo, unaona jinsi hali inavyokuwa muda wa kutoka, sasa ikiwa masaa 24 yatapeana nafasi, na mwisho wa mwaka mabasi baada ya kwenda kulala mahali, yanaendelea na safari zake", amesema Bw. Kahatano.

Hivi karibuni mamlaka hiyo ilikuwa hairuhusu mabasi kufanya safari zake nyakati za usiku kwa kuhofia usalama na ajali za barabarani, wakisema kwamba madereva huwa wanajisahau wanapokuwa barabarani hasa nyakati za usiku.

Mafuriko Yasababisha Kufungwa kwa Barabara Dar... Magari ya Mwendokasi Yasitisha Huduma ya Usafiri

$
0
0
Mafuriko Yasababisha Kufungwa kwa Barabara aMto Msimbazi... Magaai ya Mwendokasi Yasitisha Huduma ya Usafiri
Kufuatia kujaa maji juu ya daraja la Mto Msimbazi kwenye Barabara ya Morogoro na kusababishwa kufungwa kwa muda kwa barabara hiyo, Kamapuni inayotoa huduma katika mradi wa Mabasi yaendayo haraka jijini Dra es Salaam, UDA Rapid Transit (UDART) inauarifu umma kuwa huduma za mabasi hayo zimesitishwa kwa muda kuanzia saa 3:00 asubuhi ya Januari 08, 2018.

Mara baada ya hali kutengemaa na mamlaka husika kuruhusu barabara hiyo kuendelea kutumika, huduma zitarejea mara moja. Tunaomba radhi kwa usumbufu utakaojitokeza. Deus Bugaywa, Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano UDART.

Meli ya Kubeba Mizigo Inayoteketea Baharini Ipo Katika Hatari ya Kulipuka na Kuzama

$
0
0
Meli ya Kubeba Mizigo Inayoteketea Baharini Ipo Katika Hatari ya Kulipuka na Kuzama
Kuna hofu kubwa ya kutokea janga la kimazingira Kusini mwa bahari ya China wakati meli ya kubeba mafuta inazidi kufuja siki mbili baada ya kugongana na meli nyingine ya mizigo.

Maafisa nchini China wamevyambia vyombo vuya habari kuwa meli hiyo iko kweney hatari ya kulipuka na kuzama.

Wakoaji wanaojaribu kufika eneo hilo wanazuiwa na moshi mkubwa.

Wahuhudumu 30 raia wa Irana na 2 wa Bangladesh bado hawajulikani waliko licha ya jitihada za kimataifa kuwaokoa.

Kiwangi cha uchafuzi wa mazingira bado hakijulikani. Chombo hicho bado kilikuwa kinateketea leo Jumatatu.

Licha ya kuwa na usajili wa Panama meli hiyo inamilikiwa na kampuni ya Iran.

Sanchi ilikuwa imebeba tani 136,000 za mafuta ya Iran wakati iligongana na meli ya mizigo ya China Jumamosi usiku.
Viewing all 104709 articles
Browse latest View live




Latest Images