Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104785 articles
Browse latest View live

Chagga Barbie Aposti Video ya Makalio yake, Yaangalie Hapa Anavyoyatingisha

$
0
0
Siku hizi Kiki zinatafutwa kwa Nguvu Jamani ..She shares this video on her INSTAGRAM PAGE!!!!...See that Massive ASSET she has!!!

Msikilize Kamanda wa Polisi Kinondoni Akitoa Ufafanuzi Tukilo la Kutupwa Vingo vya Binadamu Bunju

$
0
0
Mfuatiliaji wa mitandao ya kijamii kuanzia usiku wa July 21 kulisambaa taarifa na picha zinazoonyesha viungo mbalimbali vya binadamu ambavyo vilitupwa katika daraja la Mpiji.
Kamanda wa Polisi mkoa wa kipolisi Kinondoni ameongea na Power Breakfast ya Clouds Fm na kusema>>’Kweli tumekwenda tumevikuta viungo mbalimbali vya binadamu kama mikono,miguu,vichwa na viungo vingine’
‘Lakini vipo ndani ya mifuko ya sulphet na iko mifuko kama 80 hivi lakini tumechukua viungo hivyo na kuvipeleka hospital ya Muhimbili kwanza kuhifadhi na kwa ajili ya uchunguzi Mpaka sasa hakuna mtu aliyekamatwa’
Bonyeza play kumsikiliza kamanda wa polisi mkoa wa kipolisi kinondoni Kamilius Wambura

Mwanamke: Usafi wa 'Maakuli' Muhimu, Kitu Kinanuka Kama Panya Kafia Humo...!

$
0
0
Nimekuwa na mpenzi wangu takribani mwaka mmoja sasa na mapenzi yetu yamekuwa mazuri bila ugomvi wa mara kwa mara.

Tatizo la mpenzi wangu ni kutoa harufu kali na tutoa utoko mweupe wakati tukiwa faragha.Nimevumilia kwa muda wote huo nami nimejitahidi sana kutafta dawa lakini tatizo naona haliishi.

Japo nampenda sana lakini hali ile inasababisha nikose hamu ya tendo la ndoa na kusababisha niishie round moja na hilo round moja najitahidi kumweka katika style ambayo hata harufu ikitoka sitoweza kuiskia moja kwa moja.

Mpenzi wangu huyo ni mzuri,ana shape nzuri kwakweli Mungu kamjalia lakini kama wasemavyo watu wazima kuwa Mungu hakupi vyote basi yule ndo kapata huo ugonjwa.

Mara ya kwanza wakati nasex nae ile wakati tunafanya romance sasa nikawa nimepeleka mkono sehemu ya papuchi bt nilikuwa bado sijamvua skin jeans lakin harufu iliweza kupita kwenye chupi,tyte na mpaka skin jeans na kufikia mkono wangu....aibu gani mwanamke kuwa na harufu hiyo.

Kwakweli nilijitahid kuvumilia harufu hiyo na utoko lakini naona nimeshindwa maana hata tokea nimekuwa nae mtoto wa kiume sikuwahi kuzama chumvini kwa kuhofia kupata fangasi.

Nahisi nakuwa simfikishi kileleni maana nakosa hata ujasiri wa kumwandaa kutokana na harufu hiyo.

Tatizo jingine huyo mpenzi akinyoa nywele sehemu za siri kama kwapa na papuchi anatokwa na mapele,kwakweli nakuwa nakosa amani.

Naomba ushauri wa namna ya kumaliza hili tatizo au dokta mzuri wa wanawake ili niweze kumsaidia huyu dada huko mbeleni asije kuhadhirika.

Asanteni sana.

Man City waingilia mazungumzo ya Chelsea na Drogba

$
0
0
Mabingwa wa soka nchini Uingereza Man City, wameingia kati mazungumzo ya mshambuliaji kutoka nchini Ivory Coast, Didier Drogba ambaye kutwa nzima ya jana alikuwa anapewa nafasi kubwa ya kurejea kwenye klabu ya Chelsea ya jijini London.

Man City, wameingilia kati mazungumzo kati ya pande hizo mbili kutokana na hitaji lao kwa sasa la kuziba nafasi ya mshambuliaji wao kutoka nchini Hispania Alvaro Negredo, ambaye atakuwa nje ya uwanja kwa muda wa miezi miwili hadi mitatu kutokana na jeraha la mguu linalomkabili.

Mabingwa hao wa soka nchini Uingereza, wanaamini Didier Drogba ambaye ni mchezaji huru baada ya kumaliza mkataba wake na klabu ya Galatasaray ya nchini Uturuki, atafaa kuziba pengo lililopo kwenye kikosi chao.

Hata hivyo bado jibu kamili la nani atafanikiwa kumsajili Didier Drogba lipo moyoni mwa mshambuliaji huyo mwemnye umri wa miaka 36.

Umemuona yule Model wa Video ya Ice Cream Alivyobadilika Baada ya Kupata Matibabu ya Dawa za Kulevya

$
0
0
Doreen video model wa Ice cream by Noorah alijikuta kwenye hali mbaya baada ya kuathirika na dawa za kulevya lakini Ray C akiwa na foundation yake walimchukua na kumpeleka kupata matibabu.
Hivi sasa Ray C ame post picha ya Doreen na kuonyesha jinsi alivyobadirika baada ya kupata matibabu. Hapo chini ni picha kabla hajapata matibabu na ya juu ni Doreen mpya. Caption ya chini aliandika Ray C baada ya kupost muonekano mpya wa Doreen


Wahusika Waliotupa Vipande vya Miili ya Binadamu Bunju Wajulikana

$
0
0
Habari zimethibitisha kwamba masalia ya viungo vya binadamu vilivyotupwa maeneo ya Bunju yametoka chuo cha udaktari IMTU kilichopo Mbezi baada ya wanafunzikumaliza kutumia kwa mazoezi. Viungo hivi vilitupwa baada ya mukosa pesa za kuteketeza kwenye tanuri maalum. 

Wanane Mbaroni Sakata la Vipande vya Miili ya Binadamu iliyotupwa Bunju

$
0
0
Watu wanane wanashikiliwa na polisi wakiwemo Madaktari kwa tuhuma za kuhusika kwenye tukio l a kutupwa kwa mabaki ya miili ya binadamu jana jioni nje kidogo ya jiji la Dsm
Huku likiendelea na uchunguzi kuhusu tukio hilo,Kamanda wa polisi kanda maalum ya Dar es Salaam Suleiman Kova ametangaza kuundwa kwa jopo la upelelezi kuchunguza tukio hilo, ili kubaini taratibu gani zilikiukwa na kujua aina ya mashtaka itakayowakabili.

Uchunguzi wa awali umebainisha kuwa miili hiyo ilikua katika Taasisi ya mafunzo ya udaktari IMTU kabla ya kukutwa imetupwa eneo la Bunju.
Taasisi hiyo imekiri kwamba mabaki ya miili ilikua katika taasisi hiyo lakini haijatoa maelezo kuhusu kutupwa kwa miili hiyo.
Kamanda Kova amewatoa wasiwasi watanzania kuwa hakuna mauaji yoyote ya kimbari yaliyotokea sehemu yeyote nchini hivyo polisi iachiwe ifanye kazi yake kisha itatoa taarifa hapo baadae.

Aunt Ezekiel: Filamu Hazilipi Kabisa, Sapoti ya Waume au Wapenzi Ndio Inasaidia Kutuweka Mjini

$
0
0
STAA wa filamu za Bongo, Aunt Ezekiel, amesema mafanikio ya wasanii wengi wa kike hayatokani na mauzo ya kazi hiyo bali sapoti ya waume au wapenzi wao kwa kuwa soko la filamu limeharibika.

“Filamu kwa Tanzania hakuna soko, walau wanaume, si wanawake, huwezi kunilinganisha mimi na Ray… Mimi kama si kuwa mwanamke, sidhani kama leo hii bado ningekuwepo katika filamu, kwa sababu kwa kiasi kikubwa nategemea sapoti ya wadau wangu, si mauzo ya filamu,” alisema.

Aunt alisema tatizo jingine katika soko la filamu nchini, ni wasanii kutopendana hali ambayo inashusha tasnia kila kukicha. Kwamba wangekuwa na mshikamano, wangeweza kufanya kitu cha kuwasaidia katika kuiboresha.

“Umoja ndiyo kila kitu hata kama tutakuwa hatuna hela, lakini tukikaa watu wengi kujadili kitu fulani, tutajua tufanye nini, hata kimawazo tu tutaendelea,” alisema.

Tazama Picha za Lunch Party ya Kajala Kwa Ajili ya Birthday yake ilivyokuwa Jana Mchana

$
0
0



Tazama picha za lunch ya mwanadada Kajala ilivyokuwa leo kwenye birthday yake.

Baby Madaha:Shilole anatafuta kiki kupitia jina langu, kwanza si hadhi yangu. Siwezi kujibishana na msanii wa Vigodoro

$
0
0
Stori: Gladness Mallya

MTIFUANO mzito umeibuka kati ya mastaa wa Bongo, Zuwena Mohamed ‘Shilole’ na Baby Madaha baada ya kurushiana vijembe.

Awali katika gazeti la Amani toleo la wiki iliyopita, Baby Madaha alinukuliwa akisema kuwa Mwezi wa Ramadhani unambana kiuchumi, kwa vile kumbi nyingi za starehe zimefungwa, hivyo anakosa shoo.

Akizungumza na Risasi Mchanganyiko, Shilole alisema anamshangaa Madaha kwa kukosa hofu ya Mungu, huku akimchana kuwa, haweki akiba, anaishi maisha ya kutegemea shoo ndiyo maana anaulalamikia mwezi huu.

Madaha alivyoelezwa kuhusu maoni ya Shilole, alikuja juu na kutema cheche: “Shilole anatafuta kiki kupitia jina langu, kwanza si hadhi yangu. Siwezi kujibishana na msanii anayetegemea shoo za kwenye vigodoro, akatafute pa kutokea.”

Wavuta Bangi na Watumia Unga Waiwinda Roho ya RAY C

$
0
0
Wiki  za  hivi  karibuni  mwanamuziki  wa  bongo  fleva  ambaye  pia  ni  mwanaharakati  wa  kupinga  matumizi  ya  dawa  za  kulevya  Rehema  Chamila  ‘Ray C’   amepatwa  na  misukosuko  mingi  ambayo  haikuwa    mbali  sana  na  mahusiano  na  dawa  za  kulevya….
Ni  wiki  mbili  zilizopita  tangu  mwanadada  huyo  achezee  kichapo  toka  kwa  mwanamuziki  wa  bongo  fleva  Rashid  Makwilo  maarufu  kama  Chid  Benz  akimtuhumu  kumpotosha  mkewe….
Ikumbukwe  kuwa  kabla  ya  tukio  hilo  la  Chid, Ray  C alikwaruzana  na  Legend  wa  bongo  fleva  TID  baada  ya  kuposti  kwenye  mtandao  wake  ujumbe  wa  kumuomba  waongee….
TID  alimuijia  juu  mrembo  huyo  kwa  matusi  kibao  na  kumtaka  akae  mbali  nae  na  asimfuatefuate….
Ni  hivi  karibuni  Ray  C  ameanza  harakati za  kuokoa  wasanii  na  watu  ambao  wanahisiwa  kutumia  madawa  ya  kulevya, hali  ambayo  imemfanya  ajijengee  maadaui  wengi  kwenye  jamii  ya  watumiaji  wa  madawa  ya  kulevya  ambao  wameapa    kumsambaratisha….

“Ray  C anajisumbua  bure  tu, anashindana  na  sisi, sisi  kama  anaona  tumepotea  atuache,kwanini  asihangaike  na  mabwana  zake  kwanza?  huyu  demu  vipi?,”   alisikika  teja  mmoja  maarufu  kwa  jina  la Lima  wa  Tandika.

Lima  aliyekuwa  akipewa  sapoti  na  wenzake  waliokuwa  pembeni  yake  aliendelea  kufunguka  kuwa  Ray  C asiendelee  kuumiza  kichwa  kudili  nao, kama  yeye  ni  mwanaharakati  wa  kweli  basi  adili  na  wanaowafikishia  hayo  madawa….
“Mi  nashangaa  kumuona  akihangaika  na  sisi  wakati  kuna  watu  ambao  anapaswa  adili  nao. Awatafute  wale  kama kweli  yeye  ni  shujaa,” aliongeza  kijana  mmoja  aliyeonekana  kuzidiwa  na  kilevi.
Kijana  huyo  alimuonya  mwanadada  huyo  asiwafuatilie, lasivyo  atahatarisha  maisha  yake  kwani  wakubwa  wakijua  watakasirika  sana  na  wanaweza  kumfanyia  chochote.
“Mngemshauri  tu  aachane  na  sisi, wakubwa  wetu  wakijua  ni  kesi  kubwa  mno, sijui  kama  anaweza  kupambana  nao,” aliongeza  kijana  huyo.
 Teja  huyo  alienda  mbali  zaidi  na  kudai  kuwa  alichofanyiwa  na  TID  na  Chid  Benz  ni trela  tu, akitaka  picha  kamili  aendelee  kuwafuatilia.

Wema Sepetu: Ugonjwa wa Ngozi Umeniharibu

$
0
0
MISS Tanzania 2006/07 Wema Sepetu amesema ugonjwa wa ngozi ulioshambulia sehemu ya shavu lake la kushoto umeharibu urembo wake na kumfanya ashindwe kutoka.
Akizungumza kwa huzuni, Wema alisema hakutegemea kama tatizo hilo lingekuwa kubwa, kwani lilianza kama kipele kidogo ambacho baadaye sehemu kubwa ilivimba na kuharibu mwonekano wake.

“Ulianza muwasho, kikawa kipele kisha kikageuka kama kishilingi.
Nilipokwenda hospitali nilipewa dawa ya crime ya kupaka, mimi nikachua eneo lililoathirika, kumbe ndiyo nikawa nasababisha matatizo, kukavimba zaidi kama unavyoona,” alisema Wema ambaye alikataa kupigwa picha.

Kumbe Utamu wa Mwanamke Unaweza Kusababisha Kifo Ndani ya 6x6

$
0
0
AFARIKI DUNIA KWA KUZIDIWA UTAMU WA MAPENZI.


Kijana mmoja nchini Malawi Fletcher Jere (26) amefariki dunia kutokana na kuzidiwa utamu wakati akifanya ngono na kahaba mmoja mjini Blantyre.



Gazeti la Daily Times nchini Malawi limeripoti kuwa kijana huyo alinunua kahaba huyo maeneo ya Ndirabe katikati ya jiji la Blantyre.



Afisa wa Polisi mjini Blantyre Bi.Edina Ligowe amesema Jerre alikufa kutokana na kuwa na hisia za juu sana pamoja na kuhisi utamu uliopitiliza wakati akifanya ngono na kahaba huyo (sexual excitement and sweetness).



Aidha Afisa huyo amesema kuwa kahaba huyo hatafunguliwa mashtaka yoyote kwa sababu hakuna kosa alilofanya kwa yeye kuwa mtamu kupitiliza.



"She committed no crime by being too sweet to the man" Ilisema ripoti ya Polisi nchini Malawi.

Tiba na Kinga ya Ukimwi Vyanukia

$
0
0
Watafiti katika Chuo Kikuu cha Sayansi na Tiba cha Temple, Marekani wamegundua dawa ya kuangamiza Virusi Vya Ukimwi (VVU) ambayo ni ya uhakika zaidi ukilinganisha na zilizowahi kupatikana katika tafiti za awali duniani.

Dawa yao inaweza kutumika kwa tiba ya wanaoishi na VVU na kinga kwa wale ambao bado hawajaambukizwa.

Mmoja wa watafiti hao, Dk Kamel Khalili aliwaambia waandishi wa habari juzi mjini Philadelphia, Marekani kuwa tofauti na utafiti mwingine, wao wamegundua namna ya kukiondoa kirusi kilichoingia kwenye kinasaba (DNA) ndani ya CD4 na kukitoa nje na hatimaye kukiua.

Alisema dawa hiyo inafanya kazi hiyo bila kuathiri seli za mwili wa binadamu.

Dk Khalili alisema ugunduzi wao ni wa hali ya juu zaidi kwa sababu teknolojia ya kutengeneza dawa hiyo ni tofauti na nyingine zilizokwisha kugunduliwa ambazo hazina uwezo wa kupenya ndani ya seli za binadamu, bali kuathiri tu VVU vilivyopo nje yake, ndani ya mfumo wa damu.

“Dawa yetu inakivuta kirusi nje ya seli (CD4) bila kuiathiri seli yenyewe na kukiua. Hivyo dawa hii itatumika kwa muda fulani na kuua virusi vyote mwilini na hakuna haja ya kuitumia wakati wote kama ilivyo dawa ya kufubaza VVU (ARV).”

ARV huangamiza VVU vilivyopo kwenye damu na kuendelea kuviacha hai vile ambavyo tayari vimeingia ndani ya CD4, hivyo kufanya virusi kuzuka upya pindi mwathirika anapoacha kutumia dawa.

Mmoja wa wataalamu katika Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu Kituo cha Mbeya (NIMR-MMRC), Clifford Majani ameuelezea utafiti huo kama mwanga mpya katika teknolojia ya kukabili VVU.

“Kama imepatikana teknolojia ya kukiondoa kirusi ndani ya seli ni hatua nzuri ya kukabili VVU. Hili lilionekana kuwa gumu mwanzoni,” alisema Majani.

Alisema imekuwa vigumu kuua kirusi kikiwa ndani ya seli na hata baadhi ya wanasayansi wamejaribu kutengeneza dawa itakayotambua seli zilizoathirika ili ziuawe lakini hilo likawa gumu.

“Inaweza ikapatikana dawa ya namna hiyo (inayoua seli zilizoathirika) lakini ikawa inaathiri vitu vingine ndani ya mwili. Hilo halikubaliki. Kikubwa katika ugunduzi huo ni dawa kuweza kukifuata kirusi kinakojificha na kukiondoa, jambo ambalo dawa nyingi zimeshindwa zikiwamo ARV,” alisema.

Hata hivyo, Majani alisema changamoto ambayo inaweza kujitokeza katika majaribio ya dawa hiyo ni usalama wakati wa matumizi.

Siri Utupaji Viungo vya Maiti Yabainika

$
0
0
Wakati ikibainika kuwa viungo vya miili ya binadamu vilivyookotwa juzi katika Bonde la Mto Mpiji nje kidogo ya Jiji la Dar es Salaam vilitoka katika Chuo Kikuu cha Kimataifa cha Tiba na Teknolojia (IMTU), jana Jeshi la Polisi liliwatia nguvuni watumishi wanane wa chuo hicho kuhusiana na sakata hilo.

Kukamatwa kwa watumishi hao kumeelezwa na Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Suleiman Kova kuwa ni baada ya uchunguzi wa awali kubaini kuwa viungo hivyo kwa mara ya mwisho vilikuwa katika maabara ya IMTU.

Alisema tukio hilo lilitokea juzi jioni eneo la Bonde la Mbweni Mpiji ambako iligundulika mifuko ya plastiki 85 yenye mabaki ya viungo vya binadamu.

Kutokana na tukio hilo, Polisi imeunda jopo la wapelelezi saba likiongozwa na Mkuu wa Upelelezi Kanda Maalumu, Jafari Mohamed kusaidiana na daktari wa jeshi hilo kufanya uchunguzi wa miili hiyo.

“Katika uchunguzi wetu tulibaini kuwa hivyo viungo vya binadamu vilitolewa katika Chuo cha IMTU na kusindikizwa na mfanyakazi wa ngazi ya juu kwa ajili ya  kutupwa eneo la Bonde la Mbweni Mpiji,” alisema Kova.

Alisema mifuko hiyo ilikuwa myeusi ikiwa na viungo vya aina mbalimbali vikiwamo vichwa, miguu, mikono, moyo, mapafu, vifua na mifupa ya aina mbalimbali.

“Viungo hivyo havikuwa na harufu wala uvundo wa aina yoyote na vilionekana vimekaushwa na kukakamaa,” alisema.

Alisema katika eneo hilo walikuta vifaa vinavyotumika hospitali kama glovu, nguo maalumu (apron) 20 na karatasi mbili zenye maswali ya kujibu.

Kova alisema viungo hivyo vilichukuliwa na kupelekwa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH).

Alisema jeshi hilo limefungua jalada la uchunguzi ili kujua sheria gani imevunjwa na kwa nini viungo hivyo vilitupwa hapo na kwa nini wasitumie utaratibu mzuri wa kuhifadhi na kwamba endapo kuna makosa ya kisheria, hatua zitachukuliwa na Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP).

Muhimbili wapokea mabaki

Meneja Uhusiano wa MNH, Aminiel Aligaesha alisema jana kuwa hospitali hiyo imepokea vifurushi 40 vyenye mabaki ya miili ya binadamu na kuhifadhiwa wakisubiri maelekezo ya polisi... “Hili ni suala la polisi, ninachoweza kusema ni kweli tumepokea vifurushi hivyo jana (juzi) usiku.”

IMTU yakiri kuhusika

Wakati Kova akisema hayo, uongozi wa IMTU ulikiri kuhusika na mabaki ya miili hiyo yaliyotupwa katika mto huo usiku wa kuamkia Jumapili iliyopita.

Naibu Makamu Mkuu wa chuo hicho, Dk Fariji Mtango alisema jana kwamba anaamini miili hiyo inaweza kuwa ni ile iliyotoka katika chuo hicho, ambayo imekuwa ikifanyiwa mazoezi na wanafunzi kwa kuwa walihitaji kuiteketeza na walishatoa agizo hilo.

Alisema walitoa agizo kwamba mabaki hayo yapelekwe Muhimbili kwa mujibu wa utaratibu wao kwa kuwa hayakuwa na matumizi tena, kwa kuwa ndiyo sehemu yenye uwezo wa kuyateketeza na kutoa jukumu hilo kwa mmoja wa wakufunzi wa chuo hicho ambaye jana alikuwa safarini.

“Sasa zaidi hatujui kilichoendelea lakini tulipoangalia jana (Jumatatu) tulikuta sehemu yalipohifadhiwa imesafishwa, hivyo inawezekana ni sehemu ya vile vilivyoondolewa hapa. Hatukutarajia kwamba vingetupwa katika eneo lisilokuwa sahihi kama ilivyofanyika,” alisema.

Dk Mtango alisema hiyo ilikuwa moja ya hatua za kupisha wakaguzi ambao walitarajiwa kukuta maeneo yote ya kufundishia yakiwa katika hali ya usafi na unadhifu.

“Hawa wakaguzi wanapokuja wanatakiwa waone vitu vyote vikiwa sawa. Hata kama wangeona hayo mabaki ya miili ya binadamu isingekuwa tatizo, bahati nzuri wamekuja jana na wamefanya kazi yao vizuri,” alisema.

Muda mfupi baada ya kutolewa kauli hiyo, viongozi tisa wa chuo hicho na walinzi wawili walikamatwa mnamo saa 7.30 mchana na kupelekwa katika Kituo cha Polisi Oysterbay ambako wanashikiliwa, lakini baadaye Kova alisema waliokamatwa ni wanane.

Jana mchana eneo la chuo cha IMTU lilikuwa chini ya ulinzi mkali wa polisi waliotanda kuanzia getini, mapokezi na kwenye bustani za chuo hicho na wengine waliovalia sare maarufu kama ‘tigo’ ambao walikuwa wakishika doria mbele ya chuo hicho.

Hatua kuchukuliwa

Dk Mtango alisema uongozi wa chuo hicho umeshtushwa na kutupwa kwa mabaki hayo katika utaratibu usiokubalika na utafanya uchunguzi na kuchukua hatua kwa wote waliohusika.

“Tunaanza na huyu ambaye tulimpa hili jukumu. Yeye ndiye aliyetakiwa kusimamia na anaujua wazi utaratibu wetu. Kwa sasa hajafika hapa na hata simu yake haipatikani. Tunaarifiwa kwamba amekwenda Zanzibar,” alisema.

Jinsi ilivyotokea

Juzi jioni, ilitokea taharuki baada ya wananchi kubaini viungo hivyo na taarifa kuanza kusambaa katika mitandao ya kijamii na baadaye vyombo vya habari na hadi jana mjadala kuhusu suala hilo ulikuwa mzito na wananchi wakihoji miili hiyo ni ya watu gani, imetoka wapi na imetupwa na watu gani.

Shuhuda wa tukio hilo, Mariam Nkumba alisema mara ya kwanza aliona mifuko yenye viungo hivyo Jumapili alipokwenda kuponda kokoto katika eneo hilo lakini hakubaini kulikuwa na nini.

Siku hiyo, Nkumba alisema aliondoka katika eneo hilo saa 12 jioni bila kujua nini kilikuwa ndani ya mifuko hiyo na siku iliyofuata (Jumatatu), alikwenda kuchukua mfuko mmoja ili ahifadhie kokoto zake, ndipo aliposhtuka kuona viungo vya binadamu.

“Mifuko ilikuwa mingi kweli, yote ilikuwa imejaa viungo vya binadamu. Mpaka sasa sijala na sina hamu ya kula. Ukiiona ile miili huwezi kula chakula,” alisema.

Mfanyakazi wa Kampuni ya Ujenzi ya Skol iliyopo karibu na eneo hilo, Supery Kaijunga alisema mara alipopata taarifa kutoka kwa Nkumba alianza kutoa taarifa kwa wananchi wengine ili kwa pamoja wajue la kufanya.

Baadaye walitoa taarifa polisi ambao walifika saa mbili usiku na kukusanya mabaki yote na kuondoka nayo.

Hata hivyo, Kaijunga alieleza wasiwasi wake kuhusu wingi wa miili hiyo na kuhoji walikuwa watu gani na walitoka maeneo gani.

“Tukio hili siyo la kawaida na halijawahi kutokea huku kwetu. Tunakuwa na wasiwasi sana labda nasi maisha yetu yatachukuliwa kama hawa; polisi wafanye uchunguzi wa kina kubaini ukweli wake,” alisema Kaijunga.

Imeandikwa na Andrew Msechu, Peter Elias na Pamela Chilongola


Kama Ulisikia au Kusoma Udaku Kwamba Mama Diamond na Wema Hawapatani Hii Inakuhusu

$
0
0
Najua kuna stori nyingine huwa zinaandikwa alafu wahusika wakuu wanakuja kuziongelea baadae kwa kushangaa kilichoandikwa ambacho mara nyingi kinakua sio cha kweli.
Stori ya Wema kutopatana na ‘mama mkwe’ yaani Mama mzazi wa Diamond ni miongoni mwa stori ambazo kuna uwezekano umeshawahi kukutana nazo kwenye Magazeti au baadhi ya mitandao, stori ambazo zilianza kuandikwa tu baada ya mastaa hawa kurudi mapenzini.

 Wema anasema ‘Watu wanasikia vitu vingi hata kwenye Magazeti watu wanaandika vitu vingi hususani Waandishi huwa wanatengeneza ili tu kupata habari lakini hatuwezi kusema kila kitu kinachotuhusu sisi kila mtu anajua….. hapana, mbona mimi na mama tunapatana tuuuu’

‘Mbona mami ake wangu mieeeee…. mwenyewe ananiitaga chizi langu, kwa hiyo tuko okey sana, nadhani watu wanamawazo hayo kwa sababu Mama ni mama yake Naseeb na mwisho wa siku Naseeb anakua sometimes hivi sometimes vile yeye kama mama lazima asimame nyuma ya mtoto wake ila mama yuko okey, mama ni mchizi wetu.. kamanda wetu mwenyewe’Msikilize Hapa Wema Akiongea:

Kilichoendelea Kesi ya Mbasha Mahakamani July 23 2014, Kakubali Sentensi Mbili Tu.

$
0
0
KESI ya ubakaji inayomkabili mume wa Flora Mbasha ambae ni mwimbaji maarufu wa nyimbo za injili Tanzania Emmanuel Mbasha (32), ilitajwa tena July 23 2014 katika mahakama ya wilaya ya Ilala ambapo Mbasha amesomewa tena mashataka yake huku akikubali sentensi mbili tu kati ya nne zilizosomwa.
Akisoma hoja hizo mbele ya hakimu Wilbert Luago, mwendesha mashtaka wa serikali Nasoro Katunga alisema May 23 2014 mtuhumiwa alimbaka binti aitwaye  Yerusalemu Boazi (17) ambae ni mdogo wa Flora na kumlazimisha asimwambie mtu yoyote ambapo wakati akitenda kosa hilo mkewe Flora hakuwepo nyumbani.
Katunga aliendelea kufafanua kuwa May 25 2014 Mbasha alirudia tena kitendo cha ubakaji baada ya kumuomba binti huyo amsindikize kumtafuta mke wake ambae hakuwepo nyumbani ambapo walipofika Tabata peke yao, Mbasha alimbaka tena binti.
Hizo sentensi zote mbili za juu Mbasha amezikana Mahakamani kwa kusema sio kweli.
Hata hivyo iliendelea kuelezwa kwamba tukio hilo la ubakaji liliripotiwa katika kituo cha polisi Tabata ambako Boazi alipewa PF3 kwa ajili ya kupata matibabu ambapo uchunguzi uliofanywa ulionyesha ni kweli binti huyo aliingiliwa kimwili.

Katika kesi hiyo ambayo Mbasha anatetewa na wakili Mathew Kakamba, Mbasha alikubali sentensi mbili na kuzikataa mbili zilizobaki kwamba alimbaka binti huyo.
Alichokubali ni kusema ni kweli alimuomba binti huyo amsindikize kumtafuta mke wake ambaye hakuwepo nyumbani na pia alikubali ni kweli Mei 23 2014 mke wake Flora Mbasha hakuwepo nyumbani.
Baada ya kusomewa mashataka hayo na mwendesha mashataka wa serikali, Jaji Luago aliahirisha kesi hiyo hadi August 22 2014 baada ya wakili anayemtetea Mbasha kudai atakuwa na safari kwa siku za karibuni nje ya Mkoa

Pinda: UKAWA Njooni Tuombane Msamaha

$
0
0
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, ‘amewaangukia’ wajumbe wa Bunge Maalumu la Katiba wanaounda Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa) kutoendelea na msimamo wao, badala yake wakutane ili atakayebainika kuteleza na kusababisha mgogoro waombane radhi na kuendelea mchakato wa kupata katiba mpya.

Pinda alisema hayo jana wakati akiweka jiwe la msingi katika Chuo cha Ufundi Gonja/Mheza, kilichopo Wilaya ya Same, mkoani Kilimanjaro.

“Wenzetu wanaojiita Ukawa wameamua kususia Bunge Maalumu la Katiba, lakini jitihada zinazoendelea sasa hivi ni kuwasihi warudi bungeni kwa sababu mjadala upo bungeni.
Na mimi nawasihi waje tuzungumze, tuelewane na pale tunapoonekana tuliteleza tuombane msamaha ili tusonge mbele na kupata katiba, ambayo wananchi wanaitarajia,” alisema Pinda.

Alisema hakuna haja ya kubishana katika mambo, ambayo bado waamuzi wa mwisho wa mchakato mzima wa katiba mpya watabaki kuwa ni wananchi, ambao wataamua kwa kupiga kura ya maoni baadaye mwaka huu.

“Uzuri wenyewe ni kwamba, chochote kile tutakachokubaliana pale bungeni si lazima kikakubaliwa na wananchi. Kwa sababu kule mwisho kuna kura ya maoni.
Kwa hiyo, wananchi ndiyo watakaosema hiki ndiyo na hiki sicho…Hakuna haja ya kubishana kwenye kitu, ambacho wananchi watakuwa ndiyo wenye maamuzi ya mwisho,” alisema Pinda.

Kuhusu uchaguzi wa serikali za mitaa unaotarajiwa kufanyika Oktoba, mwaka huu, Pinda alisema serikali itatumia katiba ya sasa katika uchaguzi huo endapo Ukawa wataendelea kushikilia msimamo wao wa kutorudi bungeni au kuafikiana.

Alisema iwapo Ukawa hawatarudi bungeni mwezi ujao, katiba ya sasa (ya mwaka 1977) itaendelea kutumika ingawa italazimika kufanyiwa marekebisho katika maeneo Fulani, ambayo hakuyataja baada ya maridhiano na pande zote.

UKAWA, CCM wakwama
JK akingiwa kifua asikutane na wajumbe
Kinana na timu yake waja na ajenda mpya
Katibu Mkuu wa CCM, KinanaMAZUNGUMZO yanayoendelea kuhusu jinsi ya kunasua mchakato wa katiba mpya kati ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) na wajumbe wanaounda Umoja wa Katiba ya Wananchi (UKAWA), yanaelekea kukwama kwa sababu yameingiliwa na hila, Tanzania Daima Jumatano limebaini.

Kwa mujibu wa vyanzo vyetu vya taarifa, kikao cha mwisho kilivunjika bila muafaka kutokana na CCM kuleta mapendekezo yasiyotekelezeka, kama njia ya kuondoa wajumbe kwenye hoja kuu.

Miongoni mwa mapendekezo mapya yaliyoletwa mezani, ni pamoja na kutaka wajumbe wajadili maeneo mengine ya sheria ambayo CCM haiyataki, na kutaka wajumbe wengine waongezwe katika mjadala huo ili idadi iwe kubwa zaidi.

Hata hivyo, kwa mujibu wa taarifa tulizonazo, wajumbe wa UKAWA walikataa mapendekezo hayo kwa misingi kwamba hoja ya kwanza ingesababisha warudi kwenye hoja nyingine inayohoji jinsi Rais Jakaya Kikwete alivyoteua baadhi ya wajumbe wa kundi la 201, ambao imekuwa inadaiwa kwamba wengi wao ni mawakala wa CCM walioongezwa makusudi ili kukuza idadi kwa ajili ya kuongeza kura katika hatua ya uamuzi.

“Katibu Mkuu wa CCM alipoleta hoja hiyo, wenzetu wakamwonyesha kwamba kupanua maeneo yenye ugomvi ni kufungua Pandora box ambalo CCM tusingelipenda, kwa mfano kuanza kuhoji upya idadi na utaratibu wa kupata wajumbe wa kundi la 201. Hoja hiyo ikafa,” kilisema chanzo chetu kilicho karibu na kiongozi huyo.

“Ndipo alipopendekeza kuwa ingekuwa vema waletwe wajumbe wengine kwenye mazungumzo, ambao ni wajumbe wa Bunge Maalum la Katiba, hoja ikapingwa pia na wajumbe wa UKAWA kwa maelezo hao ni sehemu ya waliosababisha mazungumzo kuvunjika.”

Chanzo chetu kiliongeza: “UKAWA walisema kwamba hao ndio waliokimbiwa bungeni, na kwamba kuwaleta kwenye mjadala kungesababisha mabishano zaidi badala ya kutafuta usuluhishi.

“Mjumbe mmoja alizungumza kwa ukali, kwamba hiyo ni non-starter, kwamba UKAWA wametoka kwa sababu ya wajumbe hao hao, hivyo kuwaleta kwenye mazungumzo haya kungekuwa sawa na kuongeza watu walewale halafu kutarajia matokeo tofauti.”

Kwa mantiki hiyo, mjumbe mmoja aliyeshiriki mjadala huo, huku akikataa kuingia kwa undani, amekiri kwa kusema kwamba “mazungumzo hayaendi kokote.”

Hata hivyo, baada ya Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana na timu yake kukataliwa mapendekezo yao mawili kwa sababu hizo, wajumbe wa UKAWA walitoa pendekezo jipya, ambalo kwa ujumbe wa CCM lilionekana kuwa zito na gumu zaidi.

“Walipomaliza kupangua mapendekezo yetu, ndipo nao wakapendekeza kwamba badala ya watu walewale, sasa ni vema waitwe marais wawili – Jakaya Kikwete wa Muungano na Dk. Ali Mohamed Shein wa Zanzibar, ambao ndio viongozi wa mihimili ya dola,” alisema mtoa habari huyo na kuongeza:

“Nani akubali? Hapo katibu mkuu (Kinana) na timu yake waliruka kama wameona joka kubwa, kwa sababu tunajua rais akikutana na wapinzani anaweza kuwasikiliza. Imeshatokea huko nyuma, na hatutaki itokee sasa, maana rais akishakubali hoja zao, kama chama tutalazimika kufuata ushauri atakaotoa, nao watakuwa wameshinda.”

Hoja ya UKAWA kutaka kujadiliana na marais wawili ililenga kumpa fursa Rais Kikwete kurejesha nyuma msimamo wake kuhusu rasimu ya pili ya katiba, maana siku alipozindua Bunge la Katiba, aliweka msimamo ambao ndio umekuwa ukifuatwa na wajumbe wote wenye maslahi na CCM.

Mara kadhaa, baadhi ya watu mashuhuri na taasisi zimesema kwamba kama Rais Kikwete asingeleta msimamo wa chama chake bungeni, ingejadiliwa rasimu ya tume, na UKAWA wasingetoka.

Miongoni mwa watu maarufu waliokiri kwamba rais alikosea ni pamoja na Msajili ya Vyama vya Siasa mstaafu, John Tendwa, ambaye alikiri kwamba rais aliteleza.

Jumuiya ya Wakristo Tanzania (CCT) ilitoa waraka wake kusisitiza hoja hiyo, kwamba kauli ya rais ndiyo ilivuruga mchakato, na kwamba ili Bunge liendelee kwa amani inabidi wajumbe wote wajielekeze kwenye rasimu ya pili ya katiba iliyowasilishwa na Mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Jaji Joseph Warioba.

Mara kadhaa, viongozi wa UKAWA wametamka wazi kwamba iwapo mjadala wa Bunge hilo hautajikita katika rasimu hiyo, hawatarejea bungeni.

Serikali imekuwa inafanya jitihada za chini chini, na za wazi kuhakikisha wajumbe wa UKAWA wanarudi bungeni, lakini wao wanadai kwamba hawawezi kurudi kujadili rasimu ya CCM badala ya rasimu ya wananchi iliyowasilishwa na Jaji Warioba.

Wadada: Wanaume Warefu Wanajisikia na Wana Dharau Sana Kwenye Swala la Mahusiano

$
0
0
Kuna mdada mmoja aliniambia kuwa aliwahi kutoka kimapenzi na wanaume watatu kwa nyakati tofauti-tofauti. Mdada huyo ameniambia kuwa wanaume warefu wanakera, kwani wanajiona sana na kujisikia, pia wana dharau na hawapendi mazungumzo mengi kama watu wafupi walivyo.

Nimejaribu kuuliza kwa wa baadhi ya wadada wanasema kuwa wanaume warefu ni wazuri nje ila tabia zao sio, wengi wanawaona watu walio wafupi kama takataka. nimeona nililete kwenu Tujadili Kama Kuna Ukweli wowote wa Jambo Hili.

Kifo Cha Mke wa Askari Aliyefia Chumbani Kwa Dereva wa Bodaboda Utata

$
0
0
Wingu zito limegubika kifo cha mke wa askari polisi wa wilayani Mwanga, Kilimanjaro aliyefia chumbani kwa dereva wa bodaboda. Uchunguzi wa awali wa polisi unadai kuwa mwanamke huyo alilala chumbani huko usiku mzima wa kuamkia Jumapili, siku ambayo maiti yake iligunduliwa saa 12 jioni.

Uchunguzi huo pia unadai kuwa mtuhumiwa ndiye aliyempigia simu shangazi ya mwanamke huyo na kumuita nyumbani kwake kwa dharura.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kilimanjaro, Robert Boaz alisema jana kuwa baada ya shangazi kufika, alishuku jambo baada ya kuona mtuhumiwa anaweweseka bila kumweleza alichomwitia.

“Akiwa amesimama nje ya chumba cha huyo bodaboda ambaye alionekana kama mlevi hivi, aliona kwa ndani kukiwa na mwanamke aliyekuwa amelala sakafuni,” alisema na kuongeza kuwa shangazi huyo aliamua kusukuma mlango ndipo alipomkuta mtoto wa kaka yake akiwa amelala sakafuni.

“Shangazi aliita majirani na katika hekaheka hiyo polisi waliitwa na kukuta mwanamke huyo akiwa amekufa na ndani ya chumba kulikuwa kumezagaa paketi za pombe,” alisema.

Mtuhumiwa anashikiliwa na polisi wilayani Mwanga huku taarifa ya chanzo cha kifo hicho zikisubiri uchunguzi wa mwili wa marehemu.
Viewing all 104785 articles
Browse latest View live




Latest Images