Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104689 articles
Browse latest View live

Nisha Afunguka Kuhusu Kuzaa

$
0
0
Nisha Afunguka Kuhusu Kuzaa
MWIGIZAJI wa Filamu za Kibongo, Salma Jabu ‘Nisha’, amefunguka kuwa kwa sasa hana mpango wa kuzaa tena kwa sababu ya kumpa malezi bora mwanaye aliyenaye.

Full Shangwe ilizungumza na Nisha ambaye alikuwa kwenye harakati za kumpeleka mtoto wake wa kike shuleni na kusema;

“Sijafikiria kuzaa mtoto mwingine kwa sasa, acha kwanza mwanangu nimpe malezi bora, kwa sasa namuandaa ili arudi shuleni kupambana,”alisema Nisha.

Baada ya Simba Kula Kichapo Haji Manara Ajitetea Hivi “Shida Yangu Mimi ni Msemaji na Shabiki wa Hii Timu”

$
0
0
Baada ya Simba Kula Kichapo Haji Manara Ajitetea “Shida Yangu Mimi ni Msemaji na Shabiki wa Hii Timu”
January 8 2018 wekundu wa Msimbazi Simba walirejea uwanjani kuwania nafasi yao ya kufuzu kucheza nusu fainali ya michuano ya Mapinduzi Cup 2018 kwa kucheza dhidi ya URA ya Uganda katika mchezo wao wa mwisho wa Kundi A.

Simba walikuwa wanahitaji ushindi katika mchezo huo ili kuitoa URA ya Uganda ambao wao walikuwa wanahitaji sare pekee ili wafuzu tofauti na Simba ambao walikuwa ni lazima washinde ili kama watataka kusonga mbele.

Bahati haikuwa ya Simba na dakika ya 48 URA wakapata goli la ushindi kupitia kwa Kalama Debossi na kuufanya mchezo umalizike kwa Simba kupoteza kwa goli 1-0 na kuyaaga mashindano hayo, baada ya game afisa habari wa Simba Haji Manara alitumia ukurasa wake wa instagram kuwaandikia wanasimba ujumbe huu.



“Kila sentesi niliyoandika nimefuta, hakuna neno linalotosha kuelezea hisia zangu kwa kilichotokea leo Amaan Stadium..nayajua maumivu ya wanasimba….shida yangu mimi ni msemaji kisha shabiki wa hii timu..najua sana pain yenu…but lazma maisha yasonge mbele…🙏🙏”>>>Manara

Polepole Atangaza Siku Ambayo CCM Itampokea Kiongozi Mkubwa wa Upinzani Toka DSM

$
0
0
Polepole Atangaza Siku Ambayo CCM Itampokea Kiongozi Mkubwa wa Upinzani Toka DSM
Katibu wa Itikadi na Uenezi wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Humphrey Polepole ku-tweet kuwa muda wowote watamchomoa kiongozi mkubwa upinzani toka DSM. Leo January 8, 2018 ameitangaza siku ya kesho kuwa ndo siku watampokea kiongozi huyo.

Namnukuu Polepole >>> “Kesho Tar 9/1 saa 3:30 Asubuhi kutakuwa na shughuli ya kumpokea Kiongozi Mkubwa wa Upinzani ambaye ameomba kujiunga na CCM na atapokelewa na Mzee Mangula Makamu wa Mwenyekiti wa CCM Bara.”


Humphrey Polepole
@hpolepole
TAARIFA KWA WANAHABARI

Kesho Tar 9/1 saa 3:30 Asubuhi kutakuwa na shughuli ya kumpokea Kiongozi Mkubwa wa Upinzani ambaye ameomba kujiunga na CCM na atapokelewa na Mzee Mangula Makamu wa Mwenyekiti wa CCM Bara.

Ukumbi wa Checkpoint Pugu.

IDARA YA ITIKADI NA UENEZI
OND LUMUMBA


Kutana na Mtabibu Wanyota Duniani Kote Maalim Fadhili Rashid Kutoka COMORO Kwa Sasa Yupo Tanzania

$
0
0

KUTANA NA MTABIBIBU WANYOTA DUNIANIKOTE MAALIM FADHILI RASHIDI KUTOKA COMORO KWA SASA YUPO TANZANIA NI BINGWA WAKUTIBU MARADHI SUGU KAMA VILE MIGUU KUUMA NA KUWAKA MOTO PRESHA KISUKARI VIDONDA VYA TUMBO PUMU

MAALIM FADHILI RASHIDI ANAJUWA UMEHANGAIKA SANA LAKINI HUJAFANIKIWA MUONE HARAKA AKUSAIDIE ANADAWA ZA KI COMRO DAWAZAKE HABAHATISHI MUONE HARAKA AKUSAIDIE TEZI NAUVIMBE TUMBONI ANAUWEZO WAKURUDISHA MTUALIE POTEA KIMAZINGIRA (MSUKURE) KUMFANYA MKE MUME MPENZI ASIKUSALITI DAWA YA (LIMBWATA) KUMTAWALA MPENZI WAKO UNAVYOTAKA KUMUONA MBAYA WAKO LIVE KWASABABI MALUM ANATOA PETE YA BAHATI INAYO ENDANA NA NYOTA YAKO ITAKAYO KULETEA MALI BILA YA MASHARITI NAKUMILIKI MALI ZAMAJINI DAWA YAKUONGEZA UUME ZAIZI UIPENDAYO DAWA YA NGUVU ZAKIUME PIA ANAYO DAWA YAKUONGEZA HIPS SHEPU KUWA NAUMBO BOMBA KAMA UMEIBIWA AMA KUDHULUMIWA UTARUDISHIWA MALIYAKO NDANI YA MASAA (24) ANAFUNGA KESI NAKUPATA HAKIYAKO DAWA YA MVUTO WABIASHARA KUUZA MALIYAKO KWAHARAKA KUZUIYA CHUMAULETE KUSAFISHA NYOTA NAKUTOWA MIKOSI NA KUPANDISHWA CHEO KAZINI KARIBUNI WOTE TIBA NIKWADINI ZOTE UTAPATA HUDUMA POPOTE ULIPO DUNIANI

CALLING +255719362806/

WHATSAPP CALLING +255785786436/

BREAKING NEWS: Hassanal wa Chedema Ajivua Uanachama na Kujiunga CCM

$
0
0

Mjumbe wa Kamati kuu ya Chadema na Bodi ya wadhamini ambaye pia ni mshauri wa Mameya Dar es salaam Muslim Hassanal amejivua Uanachama wa Chadema na kujiunga na CCM.

Hii Hapa Siri ya Lissu Kwenda na Dereva Wake Ubelgiji

$
0
0
Hii Hapa Siri ya Lissu Kwenda na Dereva Wake Ubelgiji
SIRI tatu za dereva wa Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu (Chadema), Simon Bakari (pichani) kwenda Ubelgiji na bosi wake zimevuja.

Mbunge mmoja ndani ya chama hicho aliyeomba jina lake lisiandikwe gazetini kwa kuwa siyo msemaji wa chama wala familia, alisema kamati maalum inayoratibu matibabu ya Lissu iliyokutana jijini Nairobi, Kenya iliona ni vema Simon aongozane na bosi wake pamoja na mkewe mbunge huyo, Alicia kwa kuwa ndiye aliyefanya kazi kubwa ya kumuuguza akiwa Nairobi akisaidiana na Mkuu wa Idara ya Uenezi, Hemedi Ali.

“Pamoja na ukweli kwamba dereva Simon alikuwa ana matatizo ya kisaikolojia baada ya kushambuliwa na watu wasiojulikana akiwa na Lissu mkoani Dodoma

Septemba 7, mwaka jana, alijitahidi kutoa huduma zisizo za kitabibu pamoja na Hemedi (Mkuu wa Idara ya Habari na Uenezi, Chadema) Nairobi ndiyo maana kamati maalum ya kuratibu tiba ya mbunge huyo ikaona ni vema naye aongozane na bosi wake kwani bado anahitaji msaidizi,” alisema mbunge huyo.



USALAMA WA DEREVA

Akifafanua zaidi, alisema Simon kwenda Ulaya kutasaidia pia kuwa salama zaidi kama alivyokuwa Nairobi kwa sababu huko Ubelgiji, Chadema imewasiliana na serikali ya huko ili nako akapewe ulinzi mkali kwa sababu waliomshambulia hadi sasa chama chao hakijapata taarifa kama wamekamatwa au la.

Mbunge huyo alisema sababu ya tatu iliyomfanya dereva huyo kwenda na Lissu Ulaya ni uaminifu wake kwa bosi wake huyo.

“Unajua Simon kwa kiasi kikubwa alichangia kuokoa maisha ya Lissu kwa sababu mbalimbali ambazo zinaeleweka kabla na baada ya mashambulizi ya kutisha ya kama vita ya upande mmoja, Lissu mwenyewe ameshaeleza jinsi kijana huyo alivyo mwaminifu kwake kwani ameishi naye tangu akiwa mtoto,” alisema mbunge huyo.



Aliongeza kuwa sababu ya nne ni kwamba Ubelgiji atakutana na wataalam wengine wa saikolojia, hivyo atapata tiba kwa sababu tukio alilolishuhudia Septemba 7, mwaka jana Area D Dodoma lilikuwa siyo la kawaida.



LISSU ATATIBIWA HOSPITALI GANI?

Mbunge huyo alipoulizwa Lissu atapelekwa hospitali gani au mji gani alijibu: “Kwa sasa ni mapema mno kutaja hospitali isipokuwa atakapokuwa huko atapata ulinzi binafsi na pia tumezungumza na serikali ya nchi hiyo kwa ajili ya ulinzi zaidi.”



MAPAMBANO YA DEMOKRASIA

Kwa upande wake, Mkuu wa Kitengo cha Uenezi wa Chadema, Hemedi Ali katika maelezo yake alikiri kumhudumia Lissu akiwa Nairobi wakati wa matibabu kwa miezi minne aliyolazwa na kufafanua kuwa hatua aliyofikia ni ya kushukuru kwa sababu alimpokea huku mwili wake ukiwa na shaka.

Alisema alikuwa akimhudumia Lissu huku akiwa katika darasa la kupata moyo wa ujasiri katika mapambano ya demokrasia.



“Nimempokea Lissu mwili wake ukiwa na mashaka lakini kupitia yeye nimeona miujiza ya Mungu, kipindi chote cha miezi minne nimejifunza ujasiri mkubwa katika mapambano ya haki na demokrasia,” alisema Ali.

Lissu aliondoka nchini Kenya Januari 6, mwaka huu siku ya Jumamosi iliyopita kwenda Ubelgiji kwa matibabu zaidi ambapo inaaminika atafanyiwa matibabu ya viungo na pia kutolewa risasi moja iliyobaki kwenye nyonga yake.

Itakumbukwa kuwa akiwa Hospitali ya Dodoma alitolewa risasi nane na Hospitali ya Nairobi alitolewa risasi saba na alifanyiwa operesheni 17.
Chanzo: Global Publishers

Wolper Aandika Hivi Baada ya Waziri Kuwaita na Kuwafungia Wasanii Wanaokiuka Maadili

$
0
0
Wolper Aandika Hivi Baada ya Waziri Kuwaita na Kuwafungia Wasanii Wanaokiuka Maadili
Baada ya kuona Naibu Waziri wa Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo Juliana Shonza kuwataka wasanii ambao wamekuwa wakikaa nusu utupu katika mitandao ya kijamii na kwenye music videos zao kuwa wanahitajika kuripoti BASATA wakiwemo wasanii Gigy Money, na Sanchi.

Baada ya Pretty Kind kutangazwa kufungiwa miezi sita katika kazi yake ya sanaa  muigizaji Jacquline Wolper kupitia katika ukurasa wake wa instagram alipost picha ya wanawake wamevaa mabaibui na kuandika caption inayosema “Akuna namna dadekiiii mambo ya miezi 6 sitakiii” na baada ya muda mfupi kuifuta caption hiyo

Watu Waliojichubua na Wenye Michirizi Wanyimwa Ajira

$
0
0
Watu Waliojichubua na Wenye Michirizi Wanyimwa Ajira
Kitengo cha Uhamiaji kimewaondoa watu waliotuma maombi ya kazi wakati wa zoezi la kukusanya wafanyakazi wapya kwa sababu ya kubadilisha rangi ya miili yao maarufu kama kujichubua na wenye michirizi mwilini nchini Ghana.

Msemaji wa kitengo cha Uhamiaji amesema kuwa wamewaondoa kwa sababu wanaweza kupata majeraha na kutokwa na damu wakati wakiwa kwenye mafunzo.

Baadhi ya raia Waghana wamepinga hatua hiyo na kusema ni ubaguzi, huku baadhi wakikasirishwa zaidi na waliondolewa kwa vigezo cha kuwa na michirizi mwilini.

Baadhi watu wamesifia hatua ya kuwaondoa waliobadili rangi zao za mwili. Walioondolewa wengine ni wenye michoro mwilini (tattoo) na wenye rasta.

Waliotuma maombi ya ajira wanapitia vipimo vya mwili na afya kama sehemu ya zoezi la kuwachuja wenye vigezo. Watu 84,000 walituma maombi ya kazi hiyo, huku wanaohitajika wakiwa ni 500 pekee.

Wasichana Wang,aa Ufaulu Kidato cha Pili, Darasa la Saba

$
0
0
Wasichana Wang,aa Ufaulu Kidato cha Pili, Darasa la Saba
Katibu Mtendaji Baraza la Mitihani Tanzania (NECTA),Dk Charles Msonde ametangaza matokeo ya upimaji wa kitaifa kwa wanafunzi wa kidato cha pili na darasa la nne huku wasichana wakiongoza (waking’ara).


Akizungumzia matokeo ya kidato cha pili,Dk Msonde alisema wanafunzi 433,453 ambao ni asilimia 89.32 wamepata ujuzi na maarifa ya kuwawezesha kuendelea na Kidato cha Tatu. Kati ya hayo wasichana ni 224,736 ambao ni asilimia 88.55 na wavulana ni 208,717 ambao ni asilimia 90.17.

Kwa upande wa kidato cha pili, wasichana wameshika nafasi zote 10 bora kutoka kwenye shule tatu za Feza Girls, Canossa na Precious Blood. Kwa darasa la nne, wasichana wameshika nafasi nane za juu na wavulana wakishika nafasi ya tisa na 10. Katika matokeo ya mwaka 2016, wasichana walikuwa wanane na wawili wavulana, na mwaka 2015 wavulana walikuwa watano na wasichana watano.

Aidha, Msonde alisema wanafunzi 51.807 ambao ni asilimia 10.68 wamefeli kwa kushindwa kupata alama za kuwawezesha kuendelea na kidato cha tatu. Mwaka 2016 wanafunzi 372,228 (asilimia 9.02) waliendelea na kidato cha tatu huku wanafunzi huku asilimia 8.98 ambao ni wanafunzi 36,737 walifeli.

“Somo ambalo wanafunzi wamefaulu zaidi ni Kiswahili kwa asilimia 91.92 na lile la ufaulu wa chini ni Hisabati yenye asilimia 32,” alisema. Akizitaja shule 10 zilizofanya vizuri kuwa ni Kemebos (Kagera), Canossa (Dar), St. Francis Girls (Mbeya), Marian Boys (Pwani), Kilimanjaro Islamic na Precious Blood (Arusha), St Augustine-Tagaste (Dar), Don Bosco Seminary (Iringa), Marian Girls (Pwani na Anwarite Girls (Kilimanjaro).

Yanga Yapewa Kibali cha Kufanya Mikutano

$
0
0
Yanga  Yapewa Kibali cha Kufanya Mikutano
Klabu ya Yanga imepata kibali cha kufanya mikutano yake ya viongozi wa matawi ambayo hapo awali ilizuiliwa kufanyika na Jeshi la Polisi.

Wizara ya mambo ya ndani imeipatia Yanga kibali maalum cha kufanya mkutano wao siku na tarehe watakayopanga kufanyika.

Wizara imeitaka klabu hiyo kutumia fursa hiyo vema na kushirikiana na Jeshi la Polisi katika kuhakikisha hakuna uvunjifu wa amani utakao jitokeza katika vikao vyao.

Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Awasimamisha Kazi Mwenyekiti wa Kijiji na Wajumbe wa Serikali

$
0
0
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Awasimamisha Kazi Mwenyekiti wa Kijiji na Wajumbe wa Serikali
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe.Anthony Mtaka amemsimamisha kazi kwa muda wa mwezi mmoja Mwenyekiti wa Kijiji cha Lamadi Wilayani Busega Mhe.Nzala Hezron pamoja na Wajumbe wa Serikali ya Kijiji hicho, ili kupisha uchunguzi kufuatia tuhuma mbalimbali zinazowakabili.

Uamuzi huo umekuja kufuatia malalamiko yaliyotolewa na wananchi wa Lamadi dhidi ya Mwenyeiti huyo kwa Mkuu Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe.Anthony Mtaka katika Mkutano wa hadhara uliofanyika jana Lamadi, kuhusu tuhuma mbalimbali ikiwemo matumizi mabaya ya fedha za michango ya wananchi katika Ujenzi wa Shule ya Sekondari Lukungu pamoja na kutosoma mapato na matumizi ya fedha za michango mbalimbali ya wananchi.

“Ili tuweze kutenda haki ya uchunguzi na ukaguzi tumeona ni busara Mwenyekiti asiwe Ofisini na wajumbe wanaounda Serikali ya Kijiji wasiwe ofisini ili uchunguzi na ukaguzi wa akaunti uweze kufanyika kwa haki” alisema Mtaka.

Mtaka amesema Mkaguzi wa Ndani kutoka katika Ofisi yake atakayeshirikiana na Mkaguzi wa ndani wa Wilaya ya Busega kufanya ukaguzi katika Akaunti ya Shule kujua namna fedha zilizochangwa na wananchi na zilizotolewa na Halmashauri zilivyofanya kazi ya Ujenzi wa Vyumba vya madarasa na matundu ya vyoo katika Shule ya Sekondari Lukungu.

Ameongeza kuwa kutokana na malalamilo ya baadhi ya wadau pamoja na wananchi uchunguzi na ukaguzi huo pia utahusisha pia Akaunti ya Kijiji cha Lamadi kwa kuwa Kijiji hicho kina hali nzuri kimapato na kimekuwa kikichangiwa na wadau mbalimbali wa maendeleo, hivyo ni vema ikabainishwa wadau wanaokichangia, wanachangia kitu gani na namna michango hiyo inavyotumika.

Aidha, Mtaka amesema ukaguzi huo pia utafanywa kwenye kamati iliyohusika katika upimaji viwanja katika Mji Mdogo wa Lamadi kwa sababu nayo imekuwa ikilalamikiwa na baadhi ya wananchi kuwa haikuwatendea haki.

Mkuu wa Mkoa huyo amesema uchunguzi na ukaguzi katika maeneo hayo matatu utaanza tarehe 10/01/2018 na taarifa rasmi ya zoezi hilo itatolewa tarehe 10/02/2018 kwa wananchi kupitia Mkutano wa hadhara, itakapobainika kuwa tuhuma zilizotolewa dhidi ya watu hao ni za kweli Serikali itachukua hatua.

Wakati huo huo Mtaka amemtaka Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Busega kumuondoa Afisa Mtendaji wa Kata ya Lamadi Bw.Furaha Magese Ng’onela na kuhakikisha kuwa ifikapo tarehe 10/01/2018 Kijiji cha Lamadi kinapata Mtendaji wa Kijiji kwa kuwa aliyepo sasa anakaimu na Kata ya Lamadi ipangiwe Afisa Mtendaji mwingine.

Vile vile Mtaka ameahidi kuchangia mifuko 100 ya saruji katika Ujenzi wa Shule ya Sekondari Lukungu ambayo sasa imepewe jina lake(Mtaka Sekondari) na wananchi hao, Mkuu wa Wilaya ya Busega,Mhe.Tano Mwera ameahidi kuchangia mifuko 40 na Mbunge wa Jimbo la Busega, Mhe.Dkt.Raphael Chegeni ameahidi kutoa vifaa vya ujenzi vyenye thamani ya shilingi milioni 10 kufanikisha ujenzi huo.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Kijiji cha Lamadi, Mhe.Nzala Hezron amesema kuhusu suala la ujenzi wa Shule yeye pamoja na Serikali yake ya Kijiji haikushirikishwa kikamilifu na Kamati ya Maendeleo ya Kata(WADC).

Naye Mhe.Chegeni amemhakikishia Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe.Anthony Mtaka kuwa michango ya viongozi, wadau wa mendeleo na wananchi wa Lamadi inayotolewa sasa itatumika kama ilivyokusudiwa na ikiwa kuna atakayebainika kutumia tofauti na utararibu atachukuliwa hatua.

Mkuu wa Wilaya ya Busega, Mhe.Tano mwera ametoa wito kwa wananchi wa Lamadi kuunga mkono juhudi za Serikali kwa kuchangia shilingi 10,000 kwa kaya ili kufikia Februari 15, 2018 vyumba vinne vya madarasa viwe vimekamilika katika Shule ya Sekondari Lukungu(imebadilishiwa jina na wananchi na kuitwa Mtaka Sekondari), ambayo hadi sasa ina madarasa manne na matundu ya vyoo 16 yanayoendelea kukamilishwa ili wanafunzi waanze masomo.

Nao wananchi wa Vijiji vinavyounda Kata ya Lamadi wamesema wamejipanga kuhakikisha vyumba vya madarasa vinajengwa na kukamilika  katika shule hiyo kabla ya Februari 15, 2018 ambapo kila Kitongoji kimejipanga kuanza na ujenzi wa chumba kimoja cha darasa na vitongoji vyenye watu wachache vitaungana viwili kujenga chumba kimoja cha darasa, ambapo kamati za ujenzi zitachaguliwa na wananchi wenyewe.
Chanzo: Michuzi

Mfungwa Aliyedaiwa Kufa Afufuka Akiwa Chumba cha Kuhifadhia Maiti

$
0
0
Mfungwa Aliyedaiwa Kufa Azinduka Akiwa Chumba cha Kuhifadhia Maiti
Mfungwa mmoja kaskazini mwa Uhispania alizinduka na kujipata akiwa kwenye chumba cha kuhifadhia maiti baada ya kuthibitishwa kwamba alikuwa amefariki na madaktari watatu, vyombo vya habari Uhispania vinasema.

Gonzalo Montoya Jiménez alikuwa anazuiliwa katika gereza moja jimbo la Asturias na alizinduka saa chache tu kabla yake kufanyiwa upasuaji wa kubainisha chanzo cha kifo chake.

Mwili wake tayari ulikuwa umechorwa alama tayari kwa upasuaji.

Kwa sasa, amewekwa chini ya uangalizi wa madaktari katika chumba cha wagonjwa mahututi hospitali ya Oviedo.

Mmoja wa jamaa zake ameambia gazeti la La Voz de Asturias kwamba Montoya "alikuwa na alama ya kufanyiwa upasuaji, tayari kupasuliwa".

Inadhaniwa kwamba hicho kilikuwa kisa cha hali iitwayo 'catalepsy' duru katika hospitali hiyo zimeambia runinga ya Telecinco ya Uhispania.

Catalepsy ni hali ambapo ishara muhimu za uhai kwenye mwili wa binadamu hufifia kiasi cha kutoweza kutambulika.

"Kifo" chake kilikuwa kimethibitishwa na madaktari watatu gerezani ambao waliagiza mwili wake upelekwe kwenye ufuo kwa uchunguzi zaidi.

Mwili huo ulipelekwa ufuo wa Taasisi ya Matibabu ya Kisheria katika makao makuu ya jimbo Oviedo.

Jeshi la Polisi Mkoani Dodoma Lathibitisha Chid Benz Kukamatwa na Dawa za Kulevya

$
0
0
Jeshi la Polisi Mkoani Dodoma Yathibitisha Chid Benz Kukamatwa na Dawa za Kulevya
Rapa Rashid Makwiro ‘Chid Benz’ anashikiliwa tena na jeshi la polisi mkoani Dodoma kwa tuhuma za kukutwa na dawa za kulevya na hii inakuwa mara ya tatu kwa msanii huyu kukumbwa na sakata hili.

Akithibitisha taarifa hizo Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Dodoma, SACP, Giless Muroto amesema kwamba ni kweli msanii huyo alikamatwa na taarifa kamili zitatolewa hapo kesho.

Kamanda Muroto amesema “Ni kweli Chidi Benz mnamo tar 30/12/2017, tulimkamata akiwa yeye na mke wake na vijana wawili. Tumemkamata akiwa na dawa za kulevya zidhaniwayo kuwa ni Heroine. jalada lake lipo tayari kwa Mwanasheria wa wa serikali linafanyiwa uchunguzi na muda wowote watapelekwa mahakamani”

Aidha ameongza kuwa watuhumiwa wote bado wako mahabusu.

Faida na Hasara Zampa Kigugumizi Harmorapa

$
0
0
Faida na Hasara Zampa Kigugumizi Harmorapa
Msanii wa muziki anayefanya vyema katika mitandao ya kijamii hasa Instagram, Harmorapa amejikuta akipata kigugumizi kuhusu kuingiza faida au hasara katika menejementi yake Sabuka Music.

Akiongea na Bongo5 msanii huyo anayehit na ngoma kadhaa kama vile ‘Shindu’ na ‘Mr.Kiki’ amedai kuwa yeye hafahamu kama ameingiza hasara au faida alipokuwa Sabuka Music.

“Baada ya Mr. Kiki kuna kazi zinakuja nitandondosha mzigo baada ya mzigo, harafu kwanza sipo katika menejiment mpya nafanya kazi zangu mimi kama mimi” amesema msanii huyo baada ya kuulizwa kama yupo katika manejement mpya.
Harmo akaongeza kuwa ni mpiango ya kazi tu kufanya kazi mwenyewe kwani ni jambo la kawaida ku-move kutoka hapo kwenda sehemu nyingine.

“Mimi nikizungumzia sana hapo kuhusu kama kuna faida ama hakuna faida hapo mimi sijui kiufupi yani. Nisema imeingiza faida hapo ama sijaingiza faida yoyote kipindi ambapo nipo sabuka muziki” Amesisitiza msanii huyo baada ya kuulizwa kuwa kuna tetesi kuwa amaingizia hasara menejimenti yake ya Sabuka.

Kuhusu kuhusika katika sakata la kumfukuzisha msanii mwezake katika menejimenti hiyo Harmo amedai kuwa yeye hakuhusika kumfukuzisha Kiloriti ila alikuwa na mambo yake.

Batuli Aitetea Tasnia ya Filamu, Muziki "Inachafuliwa na Wanaojifanaya Wasanii Kumbe Sio Asilimia Kubwa Wanapost Picha Chafu Mitandaoni"

$
0
0
Batuli Aitetea Tasnia ya Filamu, Muziki "Inachafuliwa na Wanaojifanaya Wasanii Kumbe Sio Asilimia Kubwa Wanapost Picha Chafu Mitandaoni"
Msanii wa filamu, Batuli amefunguka kwa kudai kuwa tasnia ya filamu na muziki inachafuliwa na watu ambao wanajifanya wao ni wasanii kumbe sio.

Muigizaji huyo amesema hayo baada ya Naibu Waziri wa Habari,Juliana Shonza kumtaka Gigy Money kuripoti ofisi kwake kutokana na kupiga picha za nusu uchi huku mwanadada Pretty Kind anayedaiwa kuwa ni msanii wa filamu akifungiwa miezi 6 kujihusisha na kazi za sanaa.

“Asilimia kubwa ya wanaotupia picha chafu kwenye mitandao hawapo kwenye makundi haya mawili muziki na filamu, umaarufu wao wameupata kwa kupiga picha za utupu na kuzitupia kwenye mitandao ya kijamii na watanzania wasio na maadili kuwapokea kwa shangwe #SanaaIpeweHeshimaYake,” alisema Batuti.

Mtulia Atii Agizo la CCM Aanza Taratibu za Kuomba Kura Kinondoni

$
0
0

Mtulia Atii Agizo la CCM Aanza Taratibu za Kuomba Kura Kinondoni
Aliyekuwa Mbunge wa Kinondoni (CUF), kisha kuhamia CCM, Maulid Mtulia ametii agizo la chama hicho lililomtaka kuripoti leo Jumanne ofisi ya CCM mkoa kwa ajili ya kuchukua maelekezo ya uchaguzi.

Hatua hiyo imekuja baada ya wiki iliyopita CCM kutangaza kuwarudisha kugombea majimbo yao waliokuwa wabunge Maulid Mtulia (Kinondoni-CUF) na Dk Godwin Molell (Siha-Chadema) ambao wamejiunga na chama hicho tawala.

Mtulia alitangaza kujiuzulu nafasi ya ubunge Desemba 2 mwaka jana huku akisema amefikia uamuzi huo bila kushawishiwa na mtu yeyote na amebaini Serikali ya CCM inafanya kazi kubwa ya kutekeleza Ilani na imefanya vizuri katika mambo mengi ambayo upinzani iliahidi kuyatekeleza.

Wakati Dk Molell alijiuzulu Desemba 14 huku akieleza amefikia uamuzi huo akiwa na akili timamu na hakushinikizwa na mtu yeyote.

Akizungumza na gazeti hili Mtulia amesema tayari ameshatekeleza agizo hilo leo, Jumanne Januari 9, 2017 na ameshakabidhiwa maelekezo hayo ya uchaguzi na viongozi husika wa CCM Mkoa wa Dar es Salaam.

“Namshukuru Mungu nimekabidhiwa maelekezo haya ya uchaguzi, ninachosubiri hivi sasa na utaratibu kutoka Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) kuhusu uchaguzi wa jimbo la Kinondoni,” amesema Mtulia.

Hata hivyo, Mtulia hakuwa tayari kueleza ni maelekezo ya aina gani badala yake amesisitiza kuwa anaisubiri NEC kutoa utaratibu wa kampeni.

Uchaguzi wa mdogo wa marudio wa  majimbo ya Kinondoni na Siha unatarajiwa kufanyika  Februari 17 baada ya NEC, kupokea barua kutoka kwa Spika wa Bunge, Job Ndugai ikieleza majimbo hayo yapo wazi.

Katika taarifa yake kwa vyombo vya habari wiki iliyopita, Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Hamphrey Polepole alisema baada ya kutafakari na kutathimni kwa kina Kamati Kuu ya CCM imewateua Mtulia na Dk Molell kugombea tena nafasi hizo.


Kiwanja Cha Kujenga Nyumba Kinauzwa Eneo la Mapinga Karibu na Bunju B

$
0
0

Kiwanja Chenye Ukubwa wa Mita 20 kwa 20 Kinauzwa Mapinga Bagamoyo Jirani na Bunju B, Kipo Karibu na Barabara ya lami ya kwenda Bagamoyo...Kina Ukubwa wa 20 Kwa 20 ...
Bei Sh Mil 8.5

Wasiliana na Namba hii 0714604974

Miujiza ya Sharifu Seif Mohamed..JE Umeachwa na Mme/Mke au Mpenzi, Umesongwa na Mitihani ya Maisha..Piga Simu Upate Muujiza Wako

$
0
0

SHARIFU SEIF MOHAMED ANAWASHUKURU WALE WOTE WANAOENDELEA KUPIGA SIMU, WENYE MATATIZO NA WALE WANAOTOA  SHUKRANI NA SHUHUDA JINSI TIBA ZAKE ZINAVYO WASAIDIA,

(Rudisha mahusiano yako ndani ya masaa 72 tu)

SHARIFU MOHAMED Ni  mtaalam na mnajimu maarufu wa nyota na kubashiri mambo yanayo watesa binadamu duniani kote na kupata ufumbuzi, Anatumia kitabu cha QUR'AN, Dawa za Asili, Dawa za Kiarabu na majini kwa kumtuliza mke/mme, mchumba au mpenzi ndani ya masaa 72 tu, na kutatua matatizo yote ya kimaisha,

Je Umeachwa na UMPENDAE awe Mme/Mke na bado unampenda? Je Umekimbiwa na Mmeo/ Mkeo n anaishi na mtu mwingine? Je Umejaribu sehemu nyingi bila mafanikio? Mpigie simu SHARIFU SEIF sasa hivi ujionee Muujiza wa Papo kwa Papo, Anauwezo wa hali ya juu wa kusambaratisha mahusiano yao na kumrejesha kwako haraka sana na Kumfanya Atimize Ahadi zote Ndani ya Muda Mfupi Endapo Utafwata Atakacho Kuelekeza

ANAZO DAWA ZA MAPENZI, NGUVU ZA KIUME, CHANGO NGIRI MAJI NA N.K, ZINDIKO LA NYUMBA NA BIASHARA, PETE ZA BAHATI, HUMALIZA KABISA TATIZO LA NGUVU ZA KIUME NA KUREFUSHA UUME KWA SAIZI UNAYOTAKA, HUZUIA CHUMA ULETE KWENYE BIASHARA, HURUDISHA MALI ZILIZOPOTEA, MAGONJWA SUGU, MIGUU KUWAKA MOTO AU KUFA GANZI, HUTIBU BUSHA BILA KUPASUA, ANAO UWEZO WA KUMRUDISHA ALIE MBALI AU ALIECHUKULIWA MSUKULE, KUPANDISHA NYOTA NA KUSHINDA BAHATI NA SIBU, KASAFISHA NYOTA NA KUKUPA MVUTO WA AJABU, KUTOA NUKSI NA VIFUNGO MBALIMBALI,  MAFANIKIO YA MAISHA NA UTAJIRI BILA MASHARI, NA MENGINE MENGI YA SIRI,

Je UMAHANGAIKA KUPATA MTOTO BILA MAFANIKIO? WASILIANA NA MTAALAMU HUYU KWANI YEYE HUFAULU PALE WOTE WALIPOSHINDWA, PIA UMALIZA KAZI ZILIZO SHINDIKANA NA WATAALAM WENGINE NDANI YA MASAA 24 TU,

(NA ANATIBU KWA NJIA YA SIMU UKIWA NCHI YOYOTE AU MKOA WOWOTE ENDAPO UTAFWATA MAELEKEZO YAKE)

Kwa ushauri na mawasiliano  zaidi Piga SIMU No:

Mobile +255 654-836970
WhatsApp +255 756-033670 

Diwani wa Chadema Ataja Sababu ya Wenzake Kujiuzulu

$
0
0

Diwani Kata ya Mivinjeni (Chadema), Frank Nyalusi ametaja sababu za madiwani wanane wa chama hicho kujiuzulu kuwa ni mgogoro uliotokana na uchaguzi wa naibu meya uliofanyika mwishoni mwa mwaka jana.

Katika uchaguzi huo Diwani wa Kata ya Gangilonga, Dadi Igogo alichaguliwa kuwa Naibu Meya wa Manispaa ya Iringa akichukua nafasi iliyoachwa wazi na Joseph Ryata wa Kata ya Kwakilosa ambaye alikuwa amemaliza muda wake.

“Mimi niseme tu kilichosababisha madiwani wote nane kuondoka ndani ya Chadema ni uchaguzi wa naibu meya, katika uchaguzi ule chama kidogo kiliteleza, madiwani tulikaa na kukubaliana kuwa Ryata aendelee na unaibu meya, baada ya kukubaliana watu watatu walifanya mabadiliko na kuondoa jina la Ryata na kuweka la Igogo,” amesema Nyalusi na kuongeza:

“Na hii ni matokeo ya watu kung’ang’ania madaraka chanzo cha kuondolewa kwenye nafasi yangu ya mwenyekiti wa wilaya ilikuwa ni hiyo mimi nilihoji kwa kuwa naibu meya amefanya vizuri aendelee kwa sababu vyama vya upinzani huingiziwa matatizo kipindi cha uchaguzi,” amesema.

Hata hivyo, Nyalusi ambaye amesema yeye hatajiuzulu nafasi yake ya udiwani kwa kuwa wamekaa na kukubaliana kwenye kikao ambacho wamemaliza mgogoro huo na kukubaliana kila mtu sehemu aliyokoea na kwamba dhambi waliyobaki nayo madiwani waliojiuzulu ni kukosa uvumilivu

Mbinu Mpya ya Kiki kwa Wasanii Yatolewa

$
0
0
Mbinu Mpya ya Kiki kwa Wasanii Yatolewa
Mwanamuziki wa bongo fleva aliyetamba na kibao cha 'Na Yule' Ruby amesema zipo njia nyingi za wasanii kupata kiki kuliko kupiga picha za utupu au kudhalilishana na badadala yake wanaweza kutumia njia aliyofanya yeye ya kuutengeneza umbo lake.

Ruby amefunguka hayo wakati akijibu maswali ya kuhusu kuweka picha mtandaoni zilizosababisha utata wa um,bo lake tofauti na alivyozoeleka.

Ruby amesema kwamba kupitia simu msanii anaweza kujiremba kwa jinsi ambavyo ataweza kusababisha mashabiki zake waendelee kumfuatilia na hata kumjadili.

"Zile picha zenye kunionyesha umbo kwanza alinitengenezea shabiki yangu akanitumia kisha mimi nikaona niiweke mtandaoni kama somo kwa wasanii wenzangu. Unaweza kufanya kitu kama ile na ukapata attention uliyokuwa unaitaka. Badala ya kupiga picha za utupu na kwa sasa serikali iko macho siyo vizuri. Napenda tuwe wabunifu" amesema Rubby..
Viewing all 104689 articles
Browse latest View live




Latest Images