Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104775 articles
Browse latest View live

Kutana na Mtabibu Wanyota Duniani Kote Maalim Fadhili Rashid Kutoka COMORO Kwa Sasa Yupo Tanzania

$
0
0
KUTANA NA MTABIBIBU WANYOTA DUNIANIKOTE MAALIM FADHILI RASHIDI KUTOKA COMORO KWA SASA YUPO TANZANIA NI BINGWA WAKUTIBU MARADHI SUGU KAMA VILE MIGUU KUUMA NA KUWAKA MOTO PRESHA KISUKARI VIDONDA VYA TUMBO PUMU

MAALIM FADHILI RASHIDI ANAJUWA UMEHANGAIKA SANA LAKINI HUJAFANIKIWA MUONE HARAKA AKUSAIDIE ANADAWA ZA KI COMRO DAWAZAKE HABAHATISHI MUONE HARAKA AKUSAIDIE TEZI NAUVIMBE TUMBONI ANAUWEZO WAKURUDISHA MTUALIE POTEA KIMAZINGIRA (MSUKURE) KUMFANYA MKE MUME MPENZI ASIKUSALITI DAWA YA (LIMBWATA) KUMTAWALA MPENZI WAKO UNAVYOTAKA KUMUONA MBAYA WAKO LIVE KWASABABI MALUM ANATOA PETE YA BAHATI INAYO ENDANA NA NYOTA YAKO ITAKAYO KULETEA MALI BILA YA MASHARITI NAKUMILIKI MALI ZAMAJINI DAWA YAKUONGEZA UUME ZAIZI UIPENDAYO DAWA YA NGUVU ZAKIUME PIA ANAYO DAWA YAKUONGEZA HIPS SHEPU KUWA NAUMBO BOMBA KAMA UMEIBIWA AMA KUDHULUMIWA UTARUDISHIWA MALIYAKO NDANI YA MASAA (24) ANAFUNGA KESI NAKUPATA HAKIYAKO DAWA YA MVUTO
WABIASHARA KUUZA MALIYAKO KWAHARAKA KUZUIYA CHUMAULETE KUSAFISHA NYOTA NAKUTOWA MIKOSI NA KUPANDISHWA CHEO KAZINI KARIBUNI WOTE TIBA NIKWADINI ZOTE UTAPATA HUDUMA POPOTE ULIPO DUNIANI

CALLING +255719362806/ 

WHATSAPP CALLING +255785786436/

Huu ni Mwaka wa Mtoto Kwenye Ndoa Yangu na Tushaanza Kumtafuta- Shamsa Ford

$
0
0
Huu ni Mwaka wa Mtoto Kwenye Ndoa Yangu na Tushaanza Kumtafuta- Shamsa Ford
HUKU ndoa yake na mfanyabiashara Rashidi Said ‘Chid Mapenzi’ ikiwa na mwaka mmoja na miezi minne bila kupata mtoto, staa wa filamu za Kibongo, Shamsa Ford ameibuka na kufunguka kuwa mwaka huu wa 2018 ndiyo wa kupata mtoto.

Akichonga na Za Motomoto News, Shamsa alisema kama alivyowaahidi mashabiki wake tangu mwaka uliopita kwamba mwaka huu ndiyo atapata mtoto hivyo yupo kwenye harakati za kumtafuta na anaamini kwa uwezo wa Mungu atampata.

“Huu ndiyo mwaka wa mtoto na tayari mimi na mume wangu tumeshaanza kumtafuta, kikubwa tunamuomba Mungu atupatie kwani kwa akili na nguvu za kibinadamu hatuwezi na mtoto ni zawadi kutoka kwa Mungu,” alisema Shamsa.

Tasnia ya Habari Yapata Pigo Mwandishi Mwingine Afariki Dunia

$
0
0
Tasnia ya Habari Yapata Pigo  Mwandishi Mwingine Afariki Dunia
TANZIA: Aliye kuwa mtangazaji maarufu wa Radio Free Africa, Zubery Msabaha amefariki dunia usiku wa kuamkia leo. Shughuli za mazishi inatarajiwa kufanyika leo huko Mabatini jijini Mwanza

Azam Kibaluani Leo Yawatoa Hofu Mashabiki Wake

$
0
0
Azam Kibaruani Leo Yawatoa Hofu Mashabiki Wake
Ikiwa leo ndio nusu fainali ya michuano ya Kombe la Mapinduzi inayoendelea visiwani Zanzibar, kocha msaidizi wa Azam FC Idd Cheche amesema mashabiki waondoe hofu kwani watatetea ubingwa wao.


Azam FC ndio mabingwa watetezi wa kombe hilo na wametinga nusu fainali wakitokea kundi B kwa kushika nafasi ya pili nyuma ya URA ya Uganda.

''Kuhusu kutetea ubingwa wetu mashabiki wasitie shaka, tumekuja kwa dhamira moja tu na tuko pamoja tumeungana kupambana kuhakikisha tunatetea ubingwa wetu'', amesema Cheche.

Azam FC itakuwa kibaruani dhidi ya Singida United ambayo nayo imetinga nusu fainali kwa kuongoza kundi A. Mchezo huo utachezwa majira ya saa 2:00 usiku.

Kuhusu mchezo wa leo kocha Cheche amesema wamejiandaa vizuri kuhakikisha wanashinda huku akikiri kuwa hatua ya nusu fainali itakuwa ngumu tofauti na ilivyokuwa hatua ya makundi.

Msimu huu Azam FC na Singida United zimekutana mara moja kwenye mchezo wa ligi kuu soka Tanzania bara ambao ulipigwa kwenye uwanja wa Jamhuri mjini Dodoma ambapo timu hizo zilitoka sare.

Hii Hapa Taarifa za Polisi Kuhusu Tukio la Kulipuka Boma la Gesi Buguruni

$
0
0
Hii Hapa Taarifa za Polisi Kuhusu Tukio la Kulipuka Boma la Gesi Buguruni
Jeshi la Polisi Kanda Maalum jijini Dar es salaam limetoa tathmini yake baada ya tukio la kulipuka bomba la gesi kutokea Mtwara, kwenye eneo la Buguruni.


Akizungumza na mwandishi wa www.eatv.tv Kamanda wa Polisi Kanda Maalum jijini Dar es salaam Benedict Kitalika, amesema mpaka sasa hakuna taarifa ya kifo cha mtu yeyote wala majeruhi, isipokuwa baadhi ya vibanda vya wafanya biashara kwenye eneo hilo ndio vimeteketea kwa moto.

"Kifo hakuna wala  kujeruhiwa mtu hakuna, isipokuwa mabandamabanda ya wafanya biashara ndio vimeungua si unajua wale huwa wanajenga kando ya barabara, na tumekuja kugundua kwamba Dawasco wenyewe walimpa mtu contractor lakini chini ya usimamizi wao wenyewe, sasa sijui kwa nini hawakumpa ramani, lakini mpaka sasa kuko shwari na wataalam wanaendelea kuunganisha", amesema Kamanda Kitalika.

Hapo jana majira ya saa 1 usiku moto mkubwa uliwaka katika eneo la Buguruni kwa Mnyamani, baada ya mafundi wa dawasco kupasua bomba la gesi kutoka Mtwara na kuleta taharuki kubwa kwa wakazi wa eneo hilo.

Nape Atangaza Kufia CCM

$
0
0
Nape Atangaza Kufia CCM
MBUNGE wa Mtama, Nape Nnauye (CCM), amesema kuwa hana mpango wa kuhamia chama chochote cha upinzani na ataendelea kubaki ndani ya CCM. Alisema hawezi kufanya uamuzi wa kuhamia katika vyama vya upinzani , huku akidai magari ya upinzani kwa sasa yanazidi kuzama na haijulikani yataibuka lini.
Kauli hiyo aliitoa mjini Songea wakati akimnadi mgombea Ubunge wa Songea kupitia CCM, DK. Damas Ndumbaro katika mkutano wa kampeni uliofanyika kata ya Bombambili mjini hapa. Nape ambaye pia aliwahi kuwa katibu Mwnezi wa CCM, alisema kama kuna watu walidhani atakihama chama tawala CCM na kujiunga na upinzani wasahau.
Alisema matatizo ya chama humalizwa ndani ya chama na si kukihama kama walivyofanya wanachama wengine
waliokimbia ndani ya CCM.
“Naikubali serikali ya Awamu ya Tano inayoongozwa na Jemedari, DK. John Magufuli, Makamu wa Rais Samia Suluhu Hassan na Waziri Mkuu, Kassimu Majaliwa. Ni serikali yenye viongozi imara na mimi naapa kufia CCM na sivinginevyo.

“Nasikia maneno maneno kutoka kwa baadhi ya watu wakisema Nape anataka kuhamia upinzani jambo ambalo siyo la kweli kuanzia leo watu hao waondokane na mawazo hayo,” alisema Nape.

Hussen Machozi Amshukuru Alikiba kwa Kumpa Shavu

$
0
0
Hussen Machozi Amshukuru Alikiba kwa Kumpa Shavu
Msanii Hussein Machozi ambaye sasa anafanya vyema na wimbo wake 'Sweet Melody' amefunguka na kusema kuwa kitendo ambacho amefanya msanii Alikiba kumpa 'support' katika kazi yake hiyo kimempa nguvu zaidi na kuona na yeye ni mtu muhimu.


Hussein Machozi amesema hayo wakati akiongea na mwandishi wa EATV.TV na kusema anaamini Alikiba amesikiliza na kuiona kazi yake mpya na kuikubali ndiyo maana ameamua kumpa support.


Joh Makini Afunguka Uhusiano Wake wa Kimapenzi na Mimi Mars

$
0
0
Joh Makini Afunguka Uhusiano Wake wa Kimapenzi na Mimi Mars
Mwamba wa Kaskazini anayesumbua masikio ya wapenda burudani na ngoma ya 'Mipaka' Joh Makini amepangua tetesi za kujihusisha kimapenzi na mwanamuziki Mimi Mars ambaye pia ni mdogo wake msanii Vanesa Mdee.


Joh Makini amepangua tetesi hizo kwenye Friday Night Live ya EATV ambapo amesema kwamba tetesi hizo hazina ukweli wowote na kwamba yeye anamchukulia Mimi Mars kama mdogo wake kupitia heshima aliyojenga kwa wasanii hao ambao pia wanatokea kanda ya Kaskazini.

"A Big No. Mimi Mars ni kama mdogo wangu wa kike. Sisi ni familia moja aisee. Ni nani huyo ambaye anasambaza? alijibu Joh Makini kwa mtindo wa kuuliza.

Mbali na hayo Joh Makini amegoma kuweka wazi kuhusu mahusiano yanayodaiwa kuwa ni ya mdogo wake Nikki wa Pili na mpenzi wake Joan kwa madai kuwa hafahamu chochote.

Hata hivyo kumbukumbu zinaonyesha Joh Makini ni moja kati ya wasanii wachache hapa Bongo ambao amefanikiwa kuficha mahusiano yake kwa kipindi kirefu ambacho amesimama kwenye muziki.

Mrema Kudai Mabilioni ya Hela kwa Aliyemzushia Kifo

$
0
0
Mrema Kudai Mabilioni ya Hela kwa Aliyemzushia Kifo
Mwenyekti wa Bodi ya Parole nchini Mheshimiwa Agustino Lyatonga Mrema, amesema anaenda kufungua kesi ya madai ya mabilioni ya shilingi kwa watu waliomzushia taarifa za kifo hapo jana.


Akizungumza kwenye kipindi cha East Africa Breakfast kinachorushwa na East Africa Radio, Mrema amesema watu hao wamemletea tatizo kubwa sana la kushtua familia yake na watu wake wa karibu, hivyo anaelekea TCRA ili aweze kusaidiwa kuwabaini, na kuwapeleka polisi kuwafungulia kesi.

"Walivyotangaza jana Mrema amefariki kwanza nasikitika sana, kumtangazia mtu amekufa ni kweli nilihangaika jana, mke wangu alihangaika sana, watoto wangu, marafiki zangu wapenzi wangu walikuwa wanalia kwenye simu kufuatilia hizo habari kumbe ni uzushi, ni uongo habari za kijinga kabisa, nikitoka hapa sasa hivi naenda TCRA", amesema Mrema

Mrema ameendelea kwa kusema .."Nitakuwa kiongozi wa kwanza katika nchi hii kuchukua hatua kali, wanipe fidia inayostahili kwa kuniletea ujinga, nataka kujua huyu mtu aliyeanzisha huu uvumi na kuweka kwenye mitandao kwa ajili ya kunifedhehesha na kuniabisha, bilioni 20 wanilipe kwa usumbufu kwa aibu niliyopata jana".

Kwa upande mwengine Mheshimiwa Mrema amesema kitendo hiko kilimsaidia kujua ni watu gani wanampenda kweli na kina nani hawampendi, kutokana na reaction zao baada ya taarifa feki za kifo chake.

Taharuki Yazuka Mtwara Wakesha Wakinywa Uji kwa Kutekeleza Agizo la Mtoto Aliyezaliwa na Kuongea Papo Hapo

$
0
0
Taharuki Yazuka Mtwala Wakesha Wakinywa Uji kwa  Kutekeleza Agizo la Mtoto Aliyezaliwa na  Kuongea
Katika hali isiyo ya kawaida, baadhi ya wakazi wa maeneo mbalimbali mkoani Mtwara na maeneo mengine ya mikoa ya jirani wamejikuta wakikesha nje ya nyumba zao usiku wa kuamkia leo Januari 10, 2018, wakipika na kunywa uji utokanao na unga wa muhogo.

Wakazi hao wamedai kuwa wanatekeleza agizo la mtoto mdogo aliyezaliwa katika kijiji cha Mchichira kilicho kati ya nchi ya Msumbiji na mkoa wa Mtwara na kisha papo hapo kuanza kuzungumza.

Imedaiwa kuwa mtoto huyo alisema kuwa mvua ya maajabu yenye sumu itanyesha katika maeneo hayo na ili kujikinga nayo, watu wanapaswa kunywa uji huo kwa Imani kuwa uji huo utazuia kabisa mvua hiyo ya ajabu.

Licha ya kuwepo kwa taarifa za kutatanisha kuhusu ukweli wa jambo hilo, watu waliendelea kuamshana usiku wa manane kunywa uji  huo.

Hukumu ya Scopion Yakwama Kusomwa Mahakamani

$
0
0
Hukumu ya Scopion Yakwama Kusomwa Mahakamani
Hukumu ya mwalimu wa sanaa ya kujihami ‘Martia Arts’  Salum Njwete maarufu kama Scorpion ya kumjeruhi na kumtoboa macho Kinyozi Said Mrisho leo ilishindwa kusomwa katika Makahama ya Wilaya ya Ilala jijini Dar kufuatia hakimu aliyekuwa anasikiliza kesi hiyo, Frola Haule, kusema bado hajakamilisha kuiandaa.


Majeruhi Said Mrisho aliyetobolewa macho (katikati) akiongozwa na ndugu zake kuondoka makamani hapo baada ya kesi hiyo kuahirishwa.

Hakimu huyo ameiharisha kesi hiyo mpaka Januari 22 mwaka huu ambapo amesema ndiyo atatoa hukumu hiyo.  Kufuatian hali hiyo Scopion amerudishwa rumande mpaka tarehe hiyo.


Kibatala, Msando Wapigana Vikumbo Kesi ya Wema .....Kibatala Ajitoa Msando Achukua Nafasi

$
0
0
Kibatala, Msando Wapigana Vikumbo Kesi ya Wema
Wakili Msomi Peter Kibatalaaliyekuwa akisimamia kesi ya Wema Sepetu ameandika barua ya kujitoa kuwa wakili wa wema. Kufuatia kujitoa kwa Kibatala kwenye kesi hiyo Alberto Msando ambaye amejiunga na CCM hivi karibuni naye ameandika barua ya kuwa wakili mpya wa wema sepetu .

Katika kesi hiyo iliyokuwa inaendelea katika Mahakama hiyo. Mahakama imepokea barua mbili kutoka Wakili wa Malkia huyo, Peter Kibatala barua ya kujitoa kuwa Wakili wa Wema na nyingine kutoka kwa Wakili Alberto Msando ya kuwa Wakili mpya wa Wema sepetu.

Wema anakabiliwa na kesi ya kukutwa na misoko ya bangi nyumbani kwake.
Kesi hiyo imeahairishwa mpaka february 8, mwaka huu.

Mbowe Asikitishwa na Kauli ya Lowassa Kuisifia Serikali Asema " Siwezi Kujibishana na Lowassa"

$
0
0
Mbowe Asikitishwa na Kauli ya Lowassa Kuisifia Srikali Asema " Siwezi Kujinishana na Lowassa"
Mwenyekiti wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) amefunguka na kutoa msimamo wa chama chake kuhusu kitendo alichofanya Mjumbe wa Kamati Kuu ya (CHADEMA), Edward Lowassa kwenda Ikulu na kumsifia Rais Magufuli kwa utendaji wake.


Mbowe amesema kuwa kauli mbalimbali alizotoa Lowassa jana si msimamo wa chama chake na kudai kuwa amesikitishwa na kauli za kiongozi huyo kuisifia Serikali ambayo wao wanaona hajatenda hata hayo ambayo amejaribu kuyasifia.

"Siyasemi haya kubishana na kauli alizozitoa Mhe. Lowassa, pengine yeye anazo takwimu zake tofauti ambazo tunazijua kwa sababu amezungumzia kuhusu ajira lakini hakusema kutolewa kwa ajira ngapi? Japo imelinganishwa na ujenzi wa reli ya kati unaweza ukaongeza ajira, Naona kuna tatizo kubwa la ajira katika nchi, na kuna ongezeko kubwa la vijana wengi ambao hawana ajira, tunatambua wanamaliza Shule hawapati ajira, lakini vile vile kuna makampuni yanafungwa, biashara zinafungwa, benki zinaelekea kufungwa nafasi nyingi za ajira zinapotea" alisema Mbowe

Aidha Mbowe aliendelea kusisitiza na kuonesha masikitiko yake kwa kauli ya Lowassa jana  "Nisikitike tu kwamba sisi tuna kilio kikubwa, utakumbuka kwamba tunaendelea kumtibu Mhe. Tundu Lissu ambae alishambuliwa kwa risasi, unashindwa kupata ujasiri wowote, kiongozi wa CHADEMA kweli unamsifia Magufuli, wakati tunauguza watu, msaidizi wangu Ben Sanane amepotea, viongozi wetu wameuawa, wengine wamefungwa, Wabunge wanafukuzwa Bungeni, wakina Ester Bulaya, Halima Mdee kwa mashtaka ambayo ni ya kubambikiza ambayo hayafuati kanuni za Bunge" alisisitiza Mbowe

Mbali na hilo Freeman Mbowe ametoa kauli ambayo huenda ina ashiria kiongozi huyo kutaka kurudi kwenye chama chake cha awali CCM na kuachana na CHADEMA

"Kuhama watu kutoka chama kimoja kwenda chama kingine, haijawa jambo geni kwenye siasa za Tanzania, kazi ya kujenga Upinzani katika Taifa letu sio tukio la siku moja ni mchakato wa muda mrefu, lazima ipitie vipindi mbalimbali ambapo linafanya mchujo wa asili na kubakiza watu wachache ambao watasonga mbele wataleta uhuru wa kweli Maendeleo ya kweli na haki zote za kidemokrasia katika Taifa" alisema Mbowe

Kesi ya ‘Ndama Mtoto wa Ng’ombe’ Yasubiriwa Nyaraka Kutoka Australia

$
0
0
Kesi inayomkabili Shaban Hussein (Ndama mtoto wa Ng’ombe) ya makosa matano imehairishwa mpaka 12/2/2018. Wakati wa kusikiliza kesi hiyo upande wa mshtakiwa umedai unasubiri nyaraka kutoka nchini Australia ziweze kuwasilishwa.



Wakili wa Serikali, Estazia Wilson amemueleza Hakimu Mkazi Mkuu, Victoria Nongwa kuwa wameshapeleka maombi ya nyaraka za kesi hiyo (Foreigner Affairs). Kutokana na hatua hiyo, Wakili wa utetezi Jeremiah Ntobesya aliomba upande wa mashtaka kuharakisha upelelezi.

Makosa anayokabiliwa Ndama inadaiwa February 20, 2014 Dar es Salaam, alighushi nyaraka za kibali cha kusafirisha madini na sampuli za madini kwa kusudi la kuonesha kuwa kampuni ya Muru Platnum Tanzania Investment Company Limited iliruhusiwa kusafirisha mabox manne ya dhahabu yenye kilogramu 207 yenye thamani ya Dola za Marekani 8,280,000.00 kwenda Australia kwa kampuni ya Trade TJL DTYL Limited wakati akijua si kweli.

March 6, 2014, Dar es Salaam, anadaiwa kughushi kwa kutengeneza hati ya kibali ya Umoja wa Mataifa ofisi ya Dar es Salaam akijaribu kuonesha kilogramu 207 za dhahabu kutoka nchini Congo zinatarajiwa kusafirishwa na kampuni ya Muru Platnum Tanzania Investment Company Limited kwenda Australia kwa kampuni ya Trade TJL DTYL Limited, zimesafirishwa bila jinai yoyote wakati akijua si kweli.

Pata Tiba ya Tatizo la Nguvu Za Kiume........Inasaidia Kukufanya Urudie Mara 5 na Kuchelewa Kwa Dakika 20

$
0
0
TATIZO LA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME NA MAUMBILE MADOGO LINATIBIKA.Baada ya utafiti wa mda mrefu juu ya matatizo ya upungufu wa nguvu za kiume na ukosaji wa hamu ya tendo la ndoa ama kushindwa kurudia tendo kwa haraka DR Magise imekuletea tiba ya matatizo hayo kwa kutumia dawa za:


FULL POWER: Ni dawa asili ya vidonge inayotibu tatizo la upungufu au ukosefu wa nguvu za kiume,dawa hii inamchanganyiko wakutosha wenyekuzalisha vichocheo vingi vya Hemone za Gestrogen vikiwemo vitamin B6&B1,vitamini E,pamoja na madini aina ya zinc vitakufanya kuwa na nguvu na mzunguko mzuri wa damu na kuongeza hamu na uwezo wa kufanya tendo la ndoa zaidi ya hatua nne au zaidi,na kuchelewa kufika kileleni zaidi dakka 20-30.


NYAMVA: Inarutubisha maumbile ya uume yani kurefusha na kunenepesha nchi 4-7 upana cm3-4 standard kiafya haijalishi umri wako hata kwa wazee ukiitumia maumbile yako yatabaki kuwa hivyo siku zote,Pia tunatibu Presha,kisukari siku7,ngiri,chango la tumbo tumbo kujaa gesi,kutopata choo vizuri

 TUPO TZ DAR ES SALAAM   MBAGALA RANGI TATU.HUDUMA HII UTALETEWA POPOTE ULIPO .WASILIANA NAMI 0783741788/ 0715741788 -DR MAGISE

Rage Aibuka na Kuiponda Simba " Haiwezi Kutwaa Ubingwa"

$
0
0
Rage Aibuka na Kuiponda Simba " Haiwezi Kutwaa Ubingwa"
ALIYEWAHI kuwa Mwenyekiti wa Klabu ya Simba, Ismail Aden Rage, ameibuka na kusema kuwa, ndani ya klabu hiyo kuna tatizo na kama hawa­takuwa makini, basi kuna uwezekano hata ubingwa wa Ligi Kuu Bara msimu huu timu hiyo ikauokosa.


Rage ameyasema hayo kufuatia Simba, juzi Jumatatu kuondoshwa kwenye Kombe la Mapinduzi, huku pia ikiwa imeshaondolewa kwenye Kombe la FA.

Aliyewahi kuwa Mwenyekiti wa Klabu ya Simba, Ismail Aden Rage.

Rage amesema licha ya Simba kuwa vinara wa ligi kwa sasa, lakini kama viongozi, wachezaji na benchi la ufundi hawatakuwa na umoja, timu itavurugana zaidi na kushindwa kufikia malengo.

“Ukiangalia Simba ya msimu huu naona kama imerudia makosa ya Yanga waliyowahi kuyafanya huko nyuma, wamesajili wachezaji wengi bila ya kuangalia uhitaji wa timu zaidi ya kuangalia majina tu. Hili ni tatizo.

“Tatizo lingine ninaloliona ndani ya Simba mpaka kusababisha kufanya kwao vibaya ni kutokuwa na umoja baina ya wachezaji, benchi la ufundi na viongozi, wanatakiwa kukaa chini na kumaliza tofauti zao haraka kabla hatari zaidi haijatokea. Kugombana kumepitwa na wakati.

“Haiwezekani leo hii eti wachezaji wanafanyiwa mabadiliko halafu wanaondoka kwenye benchi, huu ni utovu wa nidhamu.

“Nawasihi wote kwa pamoja wakae chini wamalize tofauti zao wafanye kazi kwani wana kikosi kizuri lakini mambo madogomadogo kama hayo ndiyo yanawasumbua,” alisema Rage.

Miujiza ya Sharifu Seif Mohamed..JE Umeachwa na Mme/Mke au Mpenzi, Umesongwa na Mitihani ya Maisha..Piga Simu Upate Muujiza Wako

$
0
0
SHARIFU SEIF MOHAMED ANAWASHUKURU WALE WOTE WANAOENDELEA KUPIGA SIMU, WENYE MATATIZO NA WALE WANAOTOA  SHUKRANI NA SHUHUDA JINSI TIBA ZAKE ZINAVYO WASAIDIA,

(Rudisha mahusiano yako ndani ya masaa 72 tu)

SHARIFU MOHAMED Ni  mtaalam na mnajimu maarufu wa nyota na kubashiri mambo yanayo watesa binadamu duniani kote na kupata ufumbuzi, Anatumia kitabu cha QUR'AN, Dawa za Asili, Dawa za Kiarabu na majini kwa kumtuliza mke/mme, mchumba au mpenzi ndani ya masaa 72 tu, na kutatua matatizo yote ya kimaisha,

Je Umeachwa na UMPENDAE awe Mme/Mke na bado unampenda? Je Umekimbiwa na Mmeo/ Mkeo n anaishi na mtu mwingine? Je Umejaribu sehemu nyingi bila mafanikio? Mpigie simu SHARIFU SEIF sasa hivi ujionee Muujiza wa Papo kwa Papo, Anauwezo wa hali ya juu wa kusambaratisha mahusiano yao na kumrejesha kwako haraka sana na Kumfanya Atimize Ahadi zote Ndani ya Muda Mfupi Endapo Utafwata Atakacho Kuelekeza

ANAZO DAWA ZA MAPENZI, NGUVU ZA KIUME, CHANGO NGIRI MAJI NA N.K, ZINDIKO LA NYUMBA NA BIASHARA, PETE ZA BAHATI, HUMALIZA KABISA TATIZO LA NGUVU ZA KIUME NA KUREFUSHA UUME KWA SAIZI UNAYOTAKA, HUZUIA CHUMA ULETE KWENYE BIASHARA, HURUDISHA MALI ZILIZOPOTEA, MAGONJWA SUGU, MIGUU KUWAKA MOTO AU KUFA GANZI, HUTIBU BUSHA BILA KUPASUA, ANAO UWEZO WA KUMRUDISHA ALIE MBALI AU ALIECHUKULIWA MSUKULE, KUPANDISHA NYOTA NA KUSHINDA BAHATI NA SIBU, KASAFISHA NYOTA NA KUKUPA MVUTO WA AJABU, KUTOA NUKSI NA VIFUNGO MBALIMBALI,  MAFANIKIO YA MAISHA NA UTAJIRI BILA MASHARI, NA MENGINE MENGI YA SIRI,

Je UMAHANGAIKA KUPATA MTOTO BILA MAFANIKIO? WASILIANA NA MTAALAMU HUYU KWANI YEYE HUFAULU PALE WOTE WALIPOSHINDWA, PIA UMALIZA KAZI ZILIZO SHINDIKANA NA WATAALAM WENGINE NDANI YA MASAA 24 TU,

(NA ANATIBU KWA NJIA YA SIMU UKIWA NCHI YOYOTE AU MKOA WOWOTE ENDAPO UTAFWATA MAELEKEZO YAKE)

Kwa ushauri na mawasiliano  zaidi Piga SIMU No:

Mobile +255 654-836970
WhatsApp +255 756-033670

Madiwani Wengine Watatu Wajitoa Chadema na Kujiunga CCM

$
0
0
Madiwani Wengine wa  Chadema Wajiuzulu na Kujiunga CCM
Madiwani watatu wa Chadema, katika halmashauri ya Longido mkoa wa Arusha , wametangaza kujiuzulu na kujiunga na Chama cha Mapinduzi ( CCM).

Mkurugenzi Mtendaji wa halmashauri ya Longido, Jumaa Mhina alithibitisha leo  Januari 10 kujiuzulu kwa madiwani hao, Jacob Silas Mollel Kata ya Elang'atadapash, Elias Mepukori Mbao  Kata ya Kamwaga na  Diyoo Lomayani Laizer Kata ya Olmolog.

Mhina amesema  sababu za kujiuzulu madiwani hao wamezitoa kuwa ni kuunga mkono jitihada za Rais John Magufuli katika vita dhidi ya ufisadi, kuinua uchumi na pia kurejesha nidhamu kazini.

"Tayari tumepokea barua zao na tumezipeleka TAMISEMI kwa ajili ya utaratibu wa kisheria ili kuwezesha kufanyika uchaguzi mdogo baada ya Tume kupata taarifa" Amesema

Aliyekuwa mbunge wa jimbo la Longido, Onesmo ole Nangole pia amethibitisha kuondoka kwa madiwani hao na kueleza chama hicho, kinafuatilia tukio hilo.

Madiwani hao kujiunga na CCM wanafanya mkoa wa Arusha pekee kuwa na jumla ya madiwani 13 wa Chadema ambao wamejiuzulu na kujiunga na CCM tangu kumalizika uchaguzi mkuu mwaka 2015.


Dudu Baya Awachana Basata

$
0
0
Dudu Baya Awachana Basata
Msanii wa muziki wa Bongo Fleva, Dudubaya amesema hajapendezwa na tabia ya Baraza la Sanaa Tanzania la kufungia fungia kazi za Wasanii kwa vigezo vya kukiuka maadili.

Dudubaya amedai BASATA wamekuwa wakifungia kazi za wasanii ambazo tayari zimeshatoka na zimeanza kutumika kitu ambacho kinaonekana kama msukumo kutoka kwa watu.

Dudubaya amesema BASATA wamekuwa wakitoa maamuzi hayo kwa kukurupuka na sio kwa kufuata taratibu kama inavyotakiwa.

Kwa upande mwingine Dudubaya ameweka wazi msimamo wake kuhusu  utawala wa Rais Magufuli, ambapo amesema anapendezwa na maamuzi yake ya kuzuia wasanii wa kike kuvaa nguo za ajabu kwenye video.

Mwanaume Achoma Moto Nyumba Akiua Buibui

$
0
0
Mwanaume Achoma Moto Nyumba Akiua Buibui
Mwanamume mmoja katika mji wa Redding kaskazini mwa California, Marekani anadaiwa kuchoma moto nyumba akijaribu kumuua buibui.

Kisa hicho kilitokea Jumapili kwa mujibu wa vyombo vya habari Marekani.

Mmoja wa walioshuhudia, ambaye alikuwa anaishi katika nyumba hiyo kubwa ya makazi, ameambia gazeti moja California kwamba buibui huyo huenda alichangia kueneza moto huo chumbani, akikimbia akiwa anaungua.

Afisa wa idara ya wazimamoto eneo hilo Gerry Gray ameambia BBC ni kwenye kwamba moto ulizuka katika jumba hilo lakini akasema chanzo cha moto huo bado kinachunguzwa.

"Taarifa kuhusu 'buibui' zilitolewa na raia walioshuhudia, waliokuwa eneo la mkasa, na bila shaka zinatumiwa katika uchunguzi.

Buibui huyo alikuwa aina ya 'wolf spider' ambao ni buibui wakubwa.

Idara ya kuzima moto imeambia gazeti la Redding Record Searchlight kwamba dalili zinaonesha moto huo uliwashwa kwa mwenye.

Mto huo ulishika moto na moto huo, na ingawa wakazi waliweza kuuzima hapo, ulikuwa tayari umeenea maeneo mengine ya jumba hilo.

Maafisa wanasema moto huo ulisababisha uharibifu wa takriban $11,000 (£8,000) na baadhi ya vyumba vya jumba hilo vitahitaji kukarabatiwa kabla ya watu kuishi huko tena.
Viewing all 104775 articles
Browse latest View live




Latest Images