Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104432 articles
Browse latest View live

Hizi Hapa Sababu ya Chirwa Kukosa Penalti

0
0
Hizi Hapa Sababu ya Chirwa Kukosa Penalti
Shujaa aliyetarajiwa kuleta heshima kwa Yanga kuipeleka fainali ya Kombe la Mapinduzi, Obrey Chirwa amepeleka kilio makutano ya Mtaa wa Twiga na Jangwani, Dar es Salaam.

Chirwa amegeuka shubiri kwa mashabiki wa Yanga baada ya kukosa penalti ya mwisho dhidi ya URA ya Uganda, katika mchezo wa nusu fainali uliochezwa jana kwenye Uwanja wa Amaan mjini hapa.

Mshambuliaji huyo aliwasili visiwani hapa jana asubuhi kutoka Dar es Salaam baada ya kutokuwemo katika kikosi muda mrefu.

Mchezaji huyo alikosa penalti ya tano iliyoamua ushindi wa mabao 5-4 baada ya URA kupata penalti zote tano baada ya timu hizo kutoka suluhu dakika 90.

Sababu za kukosa penalti

Pamoja na kucheza kwa dakika 37, mshambuliaji huyo kipenzi cha Yanga, hakupaswa kucheza jana kwa kuwa hakuwa fiti kimchezo kwasababu muda mrefu alikuwa kwao Zambia kumuuguza mama yake huku kukiwa na moja ya picha alizoweka katika mitandao ya kijamii akiwa analima mahindi shambani.

Baadhi ya mashabiki waliamini kuwa angekuwa mtazamaji, lakini kocha msaidizi wa timu hiyo, Shadrack Nsajigwa hakutaka kuingia ndani jana zaidi ya kusema ni uamuzi wa timu.

Mbali na kucheza, Chirwa hakutakiwa hata kukaa benchi la wachezaji wa akiba kwa kuwa kisaikolojia hakuwa mchezoni na hakustahili hata kupewa penalti kwani hata wakati anakwenda kupiga, hakuwa mwenye kujiamini ikilinganishwa na Papy Tshishimbi, Gadiel Michael, Hassan Kessy na Rafael Daud waliofunga penalti zao.

Penalti za URA zilifungwa na Mbowa Patrick, Kibumba Enoch, Shafiq Kagimu, Jimmy Kulaba na Brian Majwega.

Kauli za Watafiti

Watafiti wa soka nchini Norway wanasema kukosa na kufunga penalti kupo na kwamba mpiga penalti ana asilimia 92 ya kufunga kama ni penalti ya kawaida mchezoni, lakini kama penalti inataka ufunge matokeo yawe sare au kuipa timu ushindi (penalti ya kuamua) mpigaji ana asilimia 60 za kufunga.

Mchambuzi wa masuala ya soka, Pprofesa Geir Jordet wa Chuo cha Sayansi ya Michezo Norway kilichopo mjini Oslo anasema katika penalti tano tano, asilimia za kupata pia hupungua kwa wanaopiga kwani penalti ya kwanza kupata ni asilimia 86.6, penalti ya pili asilimia 81.7 na asilimia 79.3 kwa panalti ya tatu na kuendelea.

“Hii inahusisha zaidi suala la kisaikolojia,” anasema profesa Jordet.

Mtafiti mwingine, Rich Masters wa Taasisi ya Human Performance nchini Hong Kong, Masters, anasema kuwa wakati mwingine mpiga penalti anakosa kwa kuwa na hofu kama atapata ama la na mwisho wa siku anakosa.

Naye Mchambuzi wa vitabu, Mark Wilson nchini Uingereza anasema wakati mchezaji anakwenda kupiga penalti anawaza mengi: “Umetajwa kupiga penalti, unatoka katikati ya uwanja na mawazo, unachukua mpira, unauweka kwenye eneo lake la penalti, unarudi nyuma tayari kupiga, sasa hapo unawaza; hili ndilo tumaini la timu yangu, kila mmoja ananiangalia, sijui nitapata au nitakosa na mwisho wa siku anakosa.

Pambano lilivyokuwa

Yanga ilianza mchezo ikiwa imefanya mabadiliko ya wachezaji wanne waliocheza dhidi ya Singida United ulimalizika kwa timu hizo kutoka sare ya bao 1-1.

Lwandamina aliitazama mechi hiyo akiwa jukwaani akiendelea kuwaamini wasaidizi Shadrack Nsajigwa na Noel Mwandila tangu kuanza kwa mashindano hayo.

Yanga iliwapumzisha Edward Makka, Gadiel Michael, Yohana Nkomola na Rafael Daud na nafasi zao kujazwa na Papy Tshishimbi, Juma Mahadhi,Haji Mwinyi na Said Juma ‘Makapu.

Tofauti na Yanga, URA ilifanya mabadiliko mawili katika kikosi chao kilichocheza na Simba jana iliwaanzisha Ssemda Charles na Bokota Labama wakichukua nafasi za Peter Lwasa na Sseruyide Moses.

Hata hivyo, muda mrefu wa mchezo mpira ulichezwa eneo la katikati kwa kila timu kuonekana kuwa na hofu ya kutoruhusu bao la mapema.

URA ilijaribu mara kadhaa kupeleka mashambulizi langoni mwa Yanga, lakini ustadi wa mabeki wa timu hiyo uliisaidia kutowapa mwanya Waganda hao kupata bao.

Moja ya shambulizi ilitokea dakika ya 10 ambapo kipa Youthe Rostand alilazimika kufanya kazi ya ziada kuokoa mkwaju wa faulo wa Brian Majwega ambao ulipatikana baada ya Haji Mwinyi kufanya madhambi.

Yanga ilijaribu kuamka na kuanza kushambulia kwa zamu na URA lakini safu yake ya ushambuliaji ilionekana kukosa uelewano na kuwapa mwanya mabeki wa wapinzani wao kucheza kwa uhuru mkubwa.

Nusura Nkomola aipatie Yanga bao la ushindi dakika moja baadaye baada ya kupiga shuti kali nje ya eneo la hatari la URA.Taharuki ilitokea dakika ya 81 baada ya Lwassa kuunganisha kwa kichwa mpira uliopita nyavu za nje ambazo zilikuwa zimechanika na kuingia ndani ya bao la Yanga lakini mwamuzi alikataa bao hilo jambo lililosababisha azongwe na wachezaji wa URA.

Baada ya mchezo huo, nahodha wa URA, Allan Munaaba alisema kilichowapa mafanikio hadi wakaweza kucheza fainali ni nidhamu.   



Wagonjwa wa Muhimbili Wahamishwa kwa Basi Kwenda Hospitali ya Mlonganzila

0
0
Wagonjwa wa Muhimbili Wahamishwa kwa Basi Kwenda Hospitali ya Mlonganzila
Wagonjwa 40 jana Jumatano Januari 10, 2018 wametumia usafiri wa basi kuhamishwa  kutoka Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) kwenda Hospitali ya Taaluma na Tiba ya Mloganzila, iliyopo nje kidogo ya Jiji la Dar es Salaam.

Safari ya wagonjwa hao ilianza saa 9 alasiri baada ya kutolewa katika wodi zao kwa msaada wa wauguzi na madaktari kwa kutumia baiskeli za wagonjwa, kupandishwa katika basi hilo aina ya Coaster.

Mwananchi ilishuhudia baadhi yao wakishindwa kutumia baiskeli hizo, kulazimika kutolewa wodini wakiwa katika vitanda.

Walipoingizwa katika magari hayo, baadhi walishindwa kuketi, kuamua kulala katika viti vya vyuma vya basi.

Hata hivyo, utaratibu huo wa kuwahamisha, MNH ilihakikisha kila mgonjwa anakuwa na ndugu mmoja ambaye aliambatana naye katika safari hiyo.

Mmoja wa ndugu wa wagonjwa hao, Jenifer Kimaro amelalamikia utaratibu huo kwa madai kuwa wagonjwa hawawezi kuwa salama kutokana na umbali kutoka Muhimbili hadi Mloganzila.

"Nafikiri wangetumia gari la wagonjwa ingekuwa salama zaidi, huu usafiri waliotumia si sawa,” amesema.

Alipoulizwa sababu za kutumia basi badala ya magari ya wagonjwa, Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano kwa Umma MNH, Aminiel Eligaesha amesema wamelazimika kufanya hivyo kutokana na wingi wa wagonjwa.

"Wagonjwa ni wengi wanaotakiwa kuhama na hatuwezi kutumia magari ya wagonjwa kwa wote 40 na leo pia tunatarajia kuhamisha wengine 40. Tunaowahamisha si wagonjwa mahututi,” amesema.

Kuhusu kutotumika kwa magari ya wagonjwa amesema magari hayo yana uwezo wa kubeba mgonjwa mmoja tu tofauti na basi linaloweza kubeba idadi kubwa zaidi.

"Tulizungumza nao kwamba wale wagonjwa wenye uwezo wa kukaa wapande kwenye basi na wasioweza kukaa tunawahamisha kwa kutumia magari maalum ya kubebea wagonjwa. Mabasi yanayobeba wagonjwa huongozwa na gari mbili za kubebea wagonjwa ili kutotumia muda mrefu njiani,” amesema.

Jana Serikali ilihamisha rasmi idara ya magonjwa ya ndani kutoka MNH  kwenda Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili kampasi ya Mloganzila (MAMC).

Uteketezaji huo umekuja mwezi mmoja baada ya Rais John Magufuli kuzindua hospitali hiyo na kutoa maagizo kuwa baadhi ya wagonjwa waliolazwa katika jengo la Mwaisela wahamishiwe MAMC ili kupunguza msongamano uliopo katika jengo hilo.

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu amesema wagonjwa watakaohama ni pamoja na wale waliopo katika wodi namba 3,4,5,6,7 na 8 zilizopo kwenye jengo la Mwaisela, na haitahusisha wale walio mahututi na wenye sababu maalum.


Ole Sendeka Amvaa Mange Kimambi Sakata la Kuvuja kwa Audio Inayosemekana ni Yake

0
0
Ole Sendeka Amvaa Mange Kimambi Sakata la Kuvuja kwa Audio Inayosemekana ni Yake
Mkuu wa Mkoa wa Njombe, Christopher Ole Sendeka amefunguka na kumvaa mwanaharakati Mange Kimambi na kusema kuwa dada huyo anamchafua na kutaka kumgombanisha na viongozi wa nchi kwa kusambaza sauti ambayo si yake.


Ole Sendeka amesema hayo alipokuwa kwenye Mkutano wa hadhara wa CCM katika kampeni za kumnadi mgombea wa Ubunge wa jimbo la Longido Arusha kwa chama hicho na kusema hiyo sauti ambayo inasambazwa na huyo dada kuonesha kuwa anamzungumzia Rais John Pombe Magufuli vibaya pamoja na Bunge si sauti yake bali imetengenezwa na watu wa upinzani kwa lengo la kumchafua na kumchonganisha.

"Akutukanaye hakuchagulii tusi, kupitia mitandao ya kijamii wameendelea kutengeneza na kusambaza 'clip' za kutafuta namna ya kunifarakanisha mimi na viongozi wa Serikali nataka niwaambieni ambazo mmeziona kwenye mitandao zinasambazwa na watu wa upinzani pamoja na sijui Mange Kimambi sijui kitu gani kile, ninaomba mzipuuze kwa kiwango kinachostahili maana zote ni uzushi mtupu" alisisitiza Ole Sendeka.

Katika moja ya sauti ambayo ilikuwa inasambaa ikidaiwa kuwa ni ya Mkuu wa Mkoa huyo wa Njombe ilikuwa inasema kuwa Bunge sasa limeshikwa na kushindwa kufanya kazi yake jambo ambalo limempeleka Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Job Ndugai kuiagiza Kamati ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge kujadili na kuchunguza kauli ya Mhe. Christopher Ole Sendeka inayodaiwa kudhalilisha Bunge.

Abiria Waliokuwa Wakigombea Siti Wakamatwa na Polisi

0
0
Abiria Waliokuwa Wakigombea Siti Wakamatwa na Polisi
Jeshi la Polisi mjini Hong Kong, nchini China limewashikilia abiria watatu waliokuwa wanazozana na kuvutana nywele kwenye treni la abiria wakigombania siti.

Wanawake hao watatu wamekamatwa na polisi baada ya video yao kuvuja mtandaoni ikiwaonesha mmoja wao akivutwa nywele na kupigwa ngumi.

Polisi mjini Hongo Kong wamesema tukio hilo limetokea jana jumatano majira ya 12:00 asubuhi kwenye treni iliyokuwa inatoka Mei Foo kwenda Tuen Mun .

Kwa mujibu wa mtandao wa HK01.com wa nchini ambao ndiyo ulikuwa wa kwanza kusambaza video hiyo umeripoti kuwa tayari polisi wameshawatambua kwa majina watu hao kuwa ni Lau (54), Zhang (49) na msichana He mwenye miaka 24 wote walikamatwa katika kituo cha treni cha Tsuen Wan masaa machavhe baada ya tukio hilo.

Hata hivyo Polisi wamesema wanawashikilia kwa kosa la uvunjivu wa amani kwenye usafiri wa umma na wote afya zao zipo sawa isipokuwa Bi. Lau (54) aliyekuwa anavutwa nywele ndiye aliyepelekwa hospitali kwa matibabu.

Matatizo ya Figo Yamtesa Aveva Ashindwa Kufika Mahakamani

0
0
Matatizo ya Figo Yamtesa Aveva Ashindwa Kufika Mahakamani
klabu ya Simba, Evans Aveva anayekabiliwa na kesi ya utakatishaji fedha wa USD 300,000 ameshindwa kufika katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kwa sababu ana matatizo ya figo.

Mwendesha Mashtaka Mwandamizi wa TAKUKURU, Leonard Swai amemueleza Hakimu Mkazi Mwandamizi, Victoria Nongwa kuwa kesi imekuja kwa ajili ya kutajwa, upelelezi haujakamilika lakini amepewa taarifa kuwa Aveva anaumwa.

Mbali ya Aveva mshtakiwa mwingine katika kesi iyo ni Geofrey Nyange maarufu kama Kaburu.

Swai ameeleza kuwa amepewa taarifa kutoka Magereza kuwa Aveva hakufika mahakamani kwa sababu ana matatizo ya figo.

Baada ya kueleza hayo, Hakimu Nongwa alikubaliana na maombi ya kutaka kumuhoji Kaburu, ambapo aliahirisha kesi hiyo hadi January 25, 2018.

Kiwanja Kinauzwa Kwa Bei Poa Kabisa....

0
0

Kiwanja cha Kujenga Nyumba Kinauzwa , Kina Size ya 20 Kwa 20 Mita, Kipo Eneo la Mapinga Karibu na Bunju B
Shilingi Mil 8.5
Piga simu 0714604974 Kwa Mawasiliano zaidi

Kutana na Mtabibu Mwenye KUBRI kutoka kwa ALLAH issa simba said Mtabibu wa Nyota za Binadamu na Dawa za Asili

0
0
Kutana na Mtabibu Mwenye KUBRI kutoka kwa ALLAH issa simba said Mtabibu wa Nyota za Binadamu na Dawa za Asili ya Africa Mwenye UWEZO Kubaini tatizo lako Pindi tu Utakapo Fanya Mawasilino Kupitia Wasaa Husika..JE UNASUMBULIWA NA Mapenzi? (Umeachwa na Umpendae,Awe Mume,Mke na Bado unampenda?Na Umejaribu Sehemu nyingi Bila Mafanikio?Wasilina na Maalim Hussein Ujione muujiza wa Papo kwa Papo.. anauwezo WA KURUDISHA MAHUSIANO NA KUIMARISHA NDOA YAKO NDANI YA SAA 12 TU. Umekimbiwa na Mumeo,mkeo au Mpenzi na anaishi na mtu mwingine? Muone akutatulie Anauwezo wa Hali ya Juu wa Kusambalatisha Mahusiano yao Endapo utafata Atakacho kuelekeza.
Atamfanya Atimize Ahadi zote kwa Muda Mfupi.

Issa simba said Anatumia Jina la Muhusika au Picha Kumaliza Tatizo lako..
Anatibu kwa Kutumia Vitabu vya QUR-AN Dawa za Asili za Africa,Dawa za Kiarabu na Majini.Anatafsiri Ndoto. Kushinda BAHATI NASIBU, KUSAFISHA NYOTA. Mvuto wa Mwili na BIASHARA, Kinga ya Mwili,ZINDIKO za Nyumba.MIGUU Kufa GANZI.Kufungua KIZAZI kwa wale walio fungwa kwa njia za KISHIRIKINA. Anakupa Jini la Mali kwa yule anaehitaji Utajiri BILA MASHARTI. Nguvu za KIUME, Humaliza Kesi zilishindika ndani ya siku 14 tu..na mengi zaidi

Wasiliana nasi +255 622588038au 0679119679 au +255 764318107

NB: TIBA KWA DINI ZOTE NA IMANI ZOTE...

Kikwete na Viongozi Mbalimbali Wamfariji Mzee Kikunge Kufuatia Kifo cha Mkewe

0
0
Kikwete na Viongozi Mbalimbali Wamfariji Mzee Kikunge Kufuatia Kifo cha Mkewe
Rais Mstaafu, Dkt. Jakaya Kikwete na baadhi ya viongozi wamefika nyumbani kwa Mzee Kingunge Ngomale Mwiru, nyumbani kwake Victoria, jijini Dar es salaam kumfariji baada ya kufiwa na mke wake Peras Ngombale hivi karibuni  na anatarajiwa kuzikwa leo jioni kwenye makaburi ya Kinondoni.

Jeneza lenye mwili wa Marehemu Mama Peras Ngombale Mwiru, Mke wa Mmoja waasisi wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Mzee Kingunge Ngomale Mwiru ukiwasili nyumbani tayari kwa ibada maalum ya maombolezo, iliyofanyika jioni ya jana. Marehemu Mama Peras Ngombale Mwiru anatarajiwa kuzikwa leo jioni kwenye makaburi ya Kinondoni, jijini Dar es salaam.

Rais Mstaafu, Dkt. Jakaya Kikwete akisalimiana na Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Freeman Mbowe wakati walipokutana kwenye Msiba wa Mama Peras Ngombale Mwiru, Mke wa Mmoja waasisi wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Mzee Kingunge Ngomale Mwiru, nyumbani kwake Victoria, jijini Dar es salaam jana.

Waziri Mkuu Mstaafu, Jaji Joseph Warioba akimfariji Mzee Kingunge Ngomale Mwiru kwa kufiwa na Mkewe, Mama Peras Ngombale Mwiru, alipofika Nyumbani kwale Victoria, jijini Dar.





Bunduki Zatumiwa Kuunda Hedifoni za Simu

0
0
Bunduki Zatumiwa Kuunda Hedifoni za Simu
Kampuni ya Yevo Labs kutoka Sweden imeanza kuunda hedifoni (kisaa cha kutumiwa kwenye simu au kompyuta kusikilizia) ambazo zinaundwa kwa kutumia vyuma kutoka kwa silaha haramu.

Kifaa cha kutia chaji kwenye hedifoni hizo, pamoja na sehemu muhimu ya hedifoni hizo, vimeundwa kwa chuma ambayo imepewa jina Humanium.

Matukio 10 makuu mwongo mmoja wa iPhone
Imeundwa na kundi linalojiita Humanium Metal Initiative, lenye makao yake Sweden, na inatumiwa na kampuni kadha za kutengeneza bidhaa za eneo la Scandinavia.

Mchanganuzi mmoja amesema wazo hilo ni zuri sana na litafanya wanaotumia hedifoni hizo kuonekana wa kipekee, kwani zinapendeza.

Afisa mkuu mtendaji wa Yevo Andreas Vural amekiri kwamba bei yake ya $499 (£370) ni ya juu mno, lakini amesema asilimia 50 ya pesa hizo zitatumwa kwa shirika ambalo hutengeneza na kuuza chuma hiyo.

"Ndicho kitu cha thamani zaidi duniani unachoweza kupata kwa sababu huwezi kukadiria thamani ya uhai wa binadamu," amesema.

Hedifoni hizo ni miongoni mwa vifaa na teknolojia mpya ambazo zimekuwa kwenye maonesho ya teknolojia ya kila mwaka yanayoendelea Nevada.

Bw Vural amesema ilichukua miaka miwili kujua jinsi ya kutumia chuma hiyo kwenye hedifoni.

Shehena ya kwanza ya Humanium ilitoka kwa bunduki haramu zilizotwaliwa na serikali Amerika Kusini.

Hedifoni hizo zinatumia teknolojia ya NFMI (inayotumia nguvu za sumaku) badala ya nyaya, na pia zinatumia teknolojia ya Bluetooth.

Mtoto wa Rais Mstaafu Atumbuliwa

0
0
Mtoto wa Rais Mstaafu Atumbuliwa
Rais wa Angola  João Lourenço, amemfukuza kazi mtoto wa rais wa zamani wa nchi hiyo José Eduardo dos Santos ambaye alikuwa Mkuu wa mfuko wa utajiri wa taifa hilo.


Rais  Lourenço alikaririwa akisema kwamba ameamua kumbadilisha José Filomeno dos Santos kufuatia tume ya ndani ya uchunguzi juu ya utawala wa mfuko huo huku kukiwa na taarifa kwamba dola bilioni 5 kutoka katika mfuko huo zimetumika katika hali tete tangu mwaka 2011 mfuko huo ulipoanzishwa.

Awali Novemba 15, Rais huyo alimfukuza kazi binti mkubwa wa rais huo wa zamani, Bi Isabel dos Santos kama mkuu wa kampuni ya mafuta ya serikali ya nchi ya Sonangol.

Aidha Rais huyo amemteuwa Waziri wa Zamani wa Fedha kuwa mwenyekiti wa bodi  ya mfuko huo (FSDEA) Carlos Alberto Lopes.

Mfuko huo umekuwa ukitajwa sana kufuatia tuhuma zilizovujishwa na gazeti la Paradise kwamba ulilipa fedha nyingi mamilioni ya dola ikiwa na malipo ya ada kwa mfanyabiashara ambaye anafanya kazi kwa karibu na José Filomeno.

DPP Awapa Maagizo Takukuru Kuhusu Jarada la Kesi ya Malinzi

0
0
DPP Awapa Maagizo Takukuru Kuhusu Jarada la Kesi ya Malinzi
Mkurugenzi wa Mashtaka nchini (DPP) amewarejeshea TAKUKURU jalada la kesi ya utakatishaji wa fedha inayomkabili aliyekuwa rais wa (TFF), Jamal Malinzi na wenzake ili warekebishe vitu vichache vya kiuchunguzi.

Mbali ya Malinzi, wengine ni Katibu wa TFF, Mwesigwa Selestine na Mhasibu wa shirikisho hilo, Msiande Mwanga.

Hayo yameelezwa na Wakili wa TAKUKURU, Leornad Swai mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Wilbard Mashauri, wakati shauri hilo lilipoitishwa kwa ajili ya kutajwa.

Swai amedai jalada la kesi hiyo limesharudi TAKUKURU likitokea kwa DPP, hivyo wamepewa maelekezo ya kukamilisha baadhi ya uchunguzi.

Baada kueleza hayo, wakili wa Utetezi Nehemia Nkonko aliomba upelelezi wa shauri hilo ukamilike kwa haraka kwa sababu washtakiwa wapo ndani.

Hakimu Mashauri ameahirisha kesi hiyo hadi January 25, 2018 kwa ajili ya kutajwa.

Ushangiliaji Huu wa Neymar Umekuwa Gumzo Mitandaoni

0
0
Ushangiliaji Huu wa Neymar Wawa Gumzo Mitandaoni
Neymar amekuwa akiangazwa zaidi toka alipojiunga na matajiri wa Ufaransa klabu ya PSG kwa dau nono la paundi milioni 200 na kwa sasa amekuwa gumzo katika mitandao ya kijamii baada ya kuonyesha staili yake mpya ushangiliaji.

Baada ya kushinda bao lake hilo kwanjia ya mkwaju wa penati akaweka kiatu chake chenye chata la Nike katika paji la uso wake kitendo ambacho kimetawala katika vichwa vya habari huku watu wengi wakitumiana picha hiyo.

Katika mchezo huo Neymar, Kylian Mbappe na Angel Di Maria wote wametupia mara mbili na kuifanya Paris Saint-Germain kutoka na ushindi wa mabao 6-1 dhidi ya Rennes katika michuano ya French Cup siku ya Jumapili.

TCRA Yamtosa Mrema Sakata la Kuzushiwa Kifo Yamtaka Kuanzia Polisi

0
0
TCRA Yamtosa Mrema Sakata la Kuzushiwa Kifo Yamtaka Kuanzia Polisi
Baada ya Mwenyekiti wa Bodi ya Parole nchini, Mh. Agustino Lyatonga Mrema kusema anaenda kufungua kesi ya madai ya mabilioni ya shilingi TCRA  kwa watu waliomzushia taarifa za kifo, Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania imemuelekeza kiongozi huyo kuanzia kituo cha polisi kabla ya kufika kwenye ngazi hiyo.

Akizungumza baada ya Mrema kuwasilisha malalamiko yake katika Mamlaka hiyo Naibu Mkurugenzi - Huduma za Bidhaa na Mawasiliano  Bw. Tadayo Joseph amesema kuwa Kabla ya Mrema kufika katika mamlaka hiyo alitakiwa kuanzia ndani ya jeshi la polisi kwani malalamiko hayo yanahusu kosa la jinai.

"Mzee Mrema na wananchi wengine wanaoleta taarifa za malalmiko  tunawapongeza kwa hatua hiyo. Suala ambalo alilileta ni linahusu kosa la jinai. Mamlaka hii na jeshi la polisi zinafanya kazi kwa ukaribu sana. Ameshauriwa kwanza akaripoti huko kisha atapatiwa wapelelezi kabla ya kufika kwenye mamlaka hii,".

Mrema ambaye alizushiwa kifo na watu wasofahamika siku ya Jumanne, aliahidi jana kwenye kipindi cha East Africa Breakfast kwamba  angekwenda  kufungua kesi TCRA na kisha kudai Bilioni 20  kutokana na matatizo pamoja na usumbufu uliosababishwa na mzushaji wa taarifa hizo.

Mbali na hayo  Mheshimiwa Mrema jana alisema  alisema kitendo cha kuzushiwa kifo kilimsaidia kujua ni watu gani wanampenda kweli na kina nani hawampendi, kutokana na reaction zao baada ya taarifa feki za kifo chake.

Kisa Lissu Bavicha Yamvaa Shaka Hamdu wa UVCCM Yasema ni Kichaa

0
0
Bavicha Yamvaa Shaka Hamdu wa UVCCM Yasema ni Kichaa
Katibu Mkuu wa Baraza la Vijana wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (BAVICHA) Julius Mwita amefunguka na kusema kuwa Kaimu Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana Wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Shaka Hamdu Shaka huenda ana matatizo ya akili.


Mwita amesema hayo leo Januari 11, 2018 katika Mkutano na waandishi wa habari wakati akijibu tuhuma alizotoa kiongozi huyo wa UVCCM dhidi ya Tundu Lissu ambapo alisema kuwa Tundu Lissu ni muongo na hapaswi kuaminiwa kwani atafuta tu umaarufu.

Kufuatia kauli hiyo ya Shaka ndipo hapo viongozi wa Baraza la Vijana wa CHADEMA walipoaamua kujitokeza na kuzungumzia juu ya kauli hizo za kijana wa CCM na kusema kuwa "Tumetafakari kauli ya Shaka kwa kina na tumejaribu kufikiri kama Shaka ana akili timamu au ni kichaa? Kwa sababu kama chama chake chenyewe wamekiri pamoja na Serikali hawawezi kuzungumza suala la Lissu kwa sababu ni mgonjwa na yupo hospitali, Shaka anapata wapi ujasiri wa kuja kuzungumza mambo yanayomuhusu Tundu Lissu tena kwa kuzungumza mambo ya uongo na ushahidi usio na tija yoyote na anawadanganya Watanzania kuwa katika nchi hii Lissu siyo wa kwanza kupigwa risasi" alisema Mwita

Aidha kiongozi huyo wa BAVICHA amemtaka Kaimu Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana Wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Shaka Hamdu Shaka alisimame na kusema mpaka sasa Tundu Lissu ametibiwa kwa fedha ya Serikali shilingi ngapi.

"Tulitegemea umoja wa vijana wa chama ambacho kinaendesha Serikali watoke wawaambie Watanzania kwamba tunakitaka chama chetu yaani kiiagize Serikali kutibu mgonjwa ambaye yupo hospitali na ameshambuliwa katika majukumu yake ya Ubunge lakini Shaka anatoka kupotosha kwa maneno ya kejeli na ya kihuni. Lakini tumkumbushe Shaka, Amani Abed Karume hakuuawa kwa sababu za kisiasa na wala hajawahi kuwa mpinzani, wala hajawahi kuwa mkosoaji wa Serikali iliyopo madarakani kwa wakati huo useme kwamba alishambuliwa kwa sababu ya ukosoaji wake bali kulikuwa na sababu zingine tofauti zilizopelekea Karume kushambuliwa"

Siku kadhaa zilizopita Mbunge wa Singida Mashariki Tundu Lissu alifunguka na kuishtumu Serikali ya awamu ya tano kuhusika katika kushambuliwa kwake baada ya kali hiyo Kaimu Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana Wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Shaka Hamdu Shaka naye amlijibu Tundu Lissu na kusema kuwa mwanasiasa huyo ni muongo na anatafuta umaarufu.

Donald Trump Kufanyiwa Uchunguzi Wa Kiafya ....Akataa Kutangazwa Hadharani Matokeo Yake

0
0
Donald Trump Kufanyiwa Uchunguzi Wa Kiafya ....Akataa Kutangazwa Hadharani Matokeo Yake
Donald Trump atafanyiwa uchunguzi wake wa kiafya wa kwanza akiwa rais Ijumaa - ni kipi anakitarajia?

Wakati Trump anatafika katika kituo cha afya cha Walter Reed Medical Center huko Bethesda, Maryland, atakuwa na habari nzuri na mbaya kwa daktari wake.

Hakunywi pombe, na hajawai. Anasema alijifunza kutoka kwa ndugu yake mkubwa Fred ambaye alifariki dunia akiwa na miaka 4.

Pia havuti sigara, "ninawatazama watu wakivuta sigara, alisema mwaka 2015. ni kitu cha kutisha kwangu.

Kwa ufupi daktari wake Harold Bornstein, aliandika kuwa Trump alikuwa katika hali nzuri ya afya.

Licha ya afya ya akili ya Tump kutiliwa shaka, vipimo vya leo haviwezi kuhusu hali yake ya kiakili.

Trump ahitaji kutanga hadharani matokeo yake ya kiafya lakini msemaji wake alisema kuwa daktari wa White Hosue Ronny Jackson, atayasoma

Dr Jackson alitoa taarifa ya kurasa mbili baada ya vipimo vya mwisho vya rais Obama mwezi Machi mwaka 2016.

Mkuu wa Genge la Yazuka la Japan Akamatwa Thailand

0
0
Mkuu wa Genge la Yazuka la Japan Akamatwa Thailand
Polisi wamekamata mkuu wa genge la Yazuka la nchini Jopan ambaye amekuwa mafichoni kwa miaka 15 baada ya picha za chale zake (tattoo) kusamba katika mtadao wa Facebook.

Shigeharu Shirai analaumiwa kwa kumuua mshindan wake kwenye genge hilo mwaka 2003.

Picha za mtoro huyo wa umri wa miaka 74 zilichukuliwa na mtu mmoja nchini Thailand ambaye hakufahamu yeye ni nani.

Magenge ya Yazuka yamekuwa miongoni mwa jamii nchini Japan kwa karne kadhaa na wanakadiriwa kuwa na wanachama 60,000.

Licha magenge hayo kutokuwa haramu, asilimia kubwa ya pesa zao hutokana na kucheza kamari, ukahaba, ulanguzi wa madawa ya kulevya na udukuzi wa mitandao.

Wakati picha hizo zilisambaa mitandaoni, zilivutia polisi wa Japan walioombaa akamatwe.

Polisi walimkamata kwenye mji wa Lopduri kaskanizi mwa Bangkok na atasafirishwa kwenda Japan kukabiliana na mashtaka ya mauaji.

Kulingana na polisi nchini Thailand, alikiri kuwa yeye ni mwanachama wa Yazuka lakini hakukiri kuwa alihusika kwenye mauaji ya mwaka 2003. Alitorokea Thailand mwaka 2005.

Kwa Nini Wanaume Wengi Wanaupungufu Wa Nguvu Za Kiume Na Maumbile Madogo?

0
0
Asilimia 45 ya wanaume wapo tofauti na wengine kwa kuwatimizia vyema wake au wapenzi Wao na kuwasababishia kutoka nje ya ndoa zao.


NINI CHANZO CHA HAYO?Kupiga punyeto,Ngiri,Vidonda vya tumbo,Magonjwa ya moyo,Presha,Kisukari,Korodani moja kuvimba,Msongo wa mwazo,Kufanyiwa tohara ukiwa mtu mzima n.k.DOKTA MANYANDA sasa kapata tiba sahihi ya tatizo la NGUVU ZA KIUME.


MUHAMA:Hii hutibu na kuponyesha kabisa tatizo la nguvu za kiume,utakuwa na uwezo wa kurudia tendo zaidi ya mara tatu bila kuchoka na itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa mda wa dakika 15-20.DAWA hii imechanganywa miti 12.Hata wazee wenye umri mkubwa wanapona kabisa.OKO NDOA YAKO SASA.


MANGUNGU MIX: Ndio tiba tosha kwa sasa ambayo hurefusha na kunenepesha uume saizi uipendayo inch 1-8 na unene sentimita 1-5,dawa hii ipo ya kupaka na kunywa na haina madhara yoyote kwa mtumiaji.


NITOFAUTI NA ULIZO WAHI KUZITUMIA.Pia tuna dawa za kupatanisha mke,mme,mpenzi au bosi wako kwa mda mfupi sana,Uzazi,Kusafisha nyota,


Je unamali yako unauza hupati wateja?Wasiliana nami 0716-263605


DOKTA MANYANDA ANAPATIKANA KASULU KIGOMA,Kwa wale wa mikoani huduma hii utaipata popote pale

Anguko la Simba Liliandaliwa, Omog Alikosa Meno, Djuma Haijui Klabu

0
0

Na Baraka Mbolembole

KUMUACHA Method Mwanjale na kumsaini Asante Kwasi katika usajili uliopita wa dirisha dogo ni muendelezo wa usajili mbovu wa ‘Mr. Kazinyingi’ pale Simba SC. Sitaacha kuwaambia ukweli na huu ni ukweli wangu mwingine kuhusu mwelekeo wa klabu hiyo katika miezi hii mitano kabla ya kumalizika kwa msimu.

Mwanzoni mwa msimu niliandika makala na kusema, Azam FC inaweza kushinda ubingwa wa ligi kuu msimu huu ‘ikipenya’ katikati ya mabingwa mara tatu mfululizo na watetezi wa taji Yanga SC na Simba SC ambayo ndiyo klabu iliyofanya usajili wa gharama kubwa zaidi msimu huu. Baada ya mwenendo wa Mtibwa Sugar FC katika game za mwanzo niliipa pia nafasi timu hiyo bingwa mara mbili ya zamani Tanzania Bara ikiwa watatumia vizuri uwanja wao wa Manungu Complex, Turiani, Morogoro.

Yanga niliwapa nafasi kubwa pia ya kushinda ubingwa wa nne mfululizo kutokana na mseto wao mzuri wa wachezaji na aina ya sajili zao zilizopendekezwa na benchi la ufundi.  Simba sikuipa nafasi ya ubingwa na sababu kubwa iliyonifanya niamini timu hiyo haina nafasi ya kushinda ubingwa ni kuendelea kumkumbatia kocha Joseph Omog, ukosefu wa busara na utulivu.

Kufikia raundi ya 12 ya ligi Simba inaongoza kwa tofauti ya magoli dhidi ya Azam FC. Timu zote hazijapoteza mchezo, zimeshinda michezo saba na kutoa sare mara tano kila moja, zikiwa na alama sare 26. Je, unaamini Simba inakwenda kumaliza ukame wa misimu mitano bila taji la VPL?

Kumuacha Omog ambaye tayari alionyesha udhaifu

Sahau kuhusu sajili ‘bab-kubwa’ zilizosimamiwa na mwenyekiti wa kamati ya usajili ya klabu hiyo wakati wa usajili wa dirisha kubwa katikati ya mwaka uliopita. Hadi kesho nitaamini sajili hizo hazikuwa mapendekezo ya kocha Omog na kwa kiongozi anayetaka maendeleo ni lazima atahoji moyoni mwake-huyu kocha vipi? Tunamsajilia wachezaji lakini hasemi chochote.

Omog alikuwa akifanya kazi ‘za waajiri wake’ na si klabu ndiyo maana nilisisitiza mara kadhaa kuendelea kuwa na Mcameroon huyo ni makosa kwa sababu hawezi kuipaisha klabu kwa wachezaji wa kusajiliwa. Omog alipaswa kujiuzulu mwenyewe baada ya kuona anaingiliwa katika kila maamuzi. Alimtaka Yusuph Ndikumana lakini uongozi ukamletea wachezaji wengine watatu tena ambao hakuwahitaji, lakini akakubali kuwapokea.

Omog hakumtaka Haruna Niyonzima kwa sababu aliona timu ikinyanyuka zaidi msimu  huu kwa kuwategemea Mohamed Ibrahim, Said Ndemla, Muzamiru Yassin na Shiza Kichuya ambao waliisaidia klabu kukaribia kutwaa ubingwa msimu uliopita. Lakini kukubali kufanya kazi na wachezaji aliosajiliwa kwa kocha wa kimataifa kama yeye niliamini kunatokana na maslahi binafsi aliyokuwa akipata-kama mshahara na posho.

Nilijua wazi atafukuzwa kwa maana asingeweza kutengeneza timu inayocheza vizuri kutokana na rundo la wachezaji wapya ‘aliosajiliwa.’ Omog alikuwa tayari ametengebneza nusu ya tarajio la timu aitakayo pale Simba na kutokana na kikosi chake kilichopita niliona kocha huyo alikuwa anasumbuliwa na tatizo moja tu-timu kufunga magoli.

Wakati anakuja alikuta tayari kuna wachezaji wamesajiliwa lakini ni wachezaji ambao walimfaa na kama kocha wa kimataifa alipaswa kusimamia usajili na kuhakikisha anapata wafungaji-labda Emmanuel Okwi, Nicholas Gyan, John Bocco lakini kuonyesha hakuwa makini katika kutatua tatizo hilo Laudit Mavugo, Juma Liuzio, wote wamebaki hivyo akalazimika kufanya kazi na washambuliaji saba kwa wakati mmoja jambo ambalo ni aibu kwa kocha mkubwa yeyote.

Kuachwa kwa Mwanjale hayakuwa mapendekezo yake lakini kwa vile hakuwa na ‘meno’ akasifia usajili wa Kwasi ambaye kwa Simba haikuwa na haja naye kutokana na uwepo wa Erasto Nyoni, Yusuph Mlipili, Salim Mbonde,  Mwanjale, Juuko Murshid-ambao ukimtoa Juuko wengine wote walisajiliwa June-Agosti mwaka uliopita.

Kwasi alikuwa pacha wa Ndikumana pale Mbao FC msimu uliopita lakini Omog alimuona Ndikumana kutokana na umakini wa meneja/wakala wa beki huyo raia wa Burundi ‘wapiga’ dili walishindwa kumsaini kwa kigezo kuwa dau lake ni ghali mno-sasa mbona wamemsaini Kwasi kwa pesa zaidi ya aliyotaka Ndikumana? Huku Mghana huyo akiwa mchezaji wa tano kusajiliwa katika beki ya kati ambayo Omog alijua suluhisho ni Ndikumana.

Usajili wa James Kotei haukuwa na mbwembwe nyingi lakini Mghana huyo ni kielelezo tosha kuwa Omog alikuwa na uwezo wa kutazama vizuri wachezaji  na kutengeneza kikosi kama angepewa uhuru wa kufanya hivyo. Ila sikumtaka kwa sababu hakuwahi kuwa imara kama ilivyowahi kuwa kwa makocha wenzake wa kimataifa waliamua kuacha kazi baada ya kuingiliwa katika majukumu yao.

Mzambia Patrick Phiri, Moloto, Papic, Tom Saintifiet, Brandts, Hans van der Pluijm wote hawa wamewahi kuonyesha misimamo yao kwa viongozi wa klabu za Simba na Yanga ambao walidiriki kuwaingilia katika kila majukumu yao ya kujenga  kikosi walichokitaka.

Omog alipaswa kufukuzwa mapema na kisha angepatikana kocha anayestahili kuwaendeleza wachezaji waliosajiliwa ‘ki-holela’ Nilimpenda sana Mganda, Jackson Mayanja-ni kocha ambaye anajua sana kutengeneza kikosi kinachocheza mchezo wa kushambulia na kutawala mechi. Lakini sasa nashangazwa sana kuona Mrundi Masoud Djuma akielekea kupewa majukumu hayo.

Hata kama wanataka kumpima, kwa kweli Simba watajutia zaidi uamuzi wa kumpa majukumu ya ukocha mkuu kocha huyo.

Kwanza anaonekana haijui klabu, hajui tamaduni ya kiuchezaji ya klabu ndiyo maana amekuja na mfumo wa 3-5-2 ambao kwa kweli hauwezi kuleta tija hadi kwa mashabiki ambao wamezoea kuona vikosi vyao vikali vikishambulia mwanzo-mwisho.

Kama Djuma atapewa kukaimu nafasi ya Omog hadi mwishni mwa msimu Simba wanaweza kumaliza nafasi ya nne, tano na pengine ya sita katika ligi hii. Weka hili katika utimamu wako wa akili. Simba waliandaa wenyewe anguko lao kwa kusajili hovyo na kumkumbatia kocha asiye na meno-muoga wa kuhoji.

Jeshi la Polisi Lawashikiria Ofisa Ardhi kwa Tuhuma za Utapeli

0
0
Jeshi la Polisi Lawashikiria Ofisa Ardhi kwa Tuhuma za Utapeli
Jeshi la Polisi mkoani Mwanza linawashikilia watu sita akiwemo Ofisa Ardhi wa Manispaa ya Ilemela, Alex Nyabange (30), kwa tuhuma mbalimbali ikiwemo utapeli wa viwanja, kutengeneza vyeti bandia vya kitaaluma pamoja namba za mlipa kodi za (TIN), za Mamlaka ya Mapato Tanzania(TRA).

Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake leo Alhamisi, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza, Ahmed Msangi amesema watu hao walikamatwa kwa nyakati tofauti kati ya Desemba 30, 2017 na Janauari 9 mwaka huu.

Msangi aliwataja waliokamatwa kwa tuhuma za kuwatapeli watu kwa madai ya kuwauzia viwanja kuwa ni Aloyce Nyabange (30) ambaye ni ofisa Ardhi wa  Manispaa ya Ilemela, Alex Josephat(41) ambaye ni mfanyabishara, Juma Malulu (60) mkazi wa mta wa Ilemela.

Wengini ni Katibu Mhatasi wa kampuni ya Nyambale Civil Works, Getruda Peter (42) mkazi wa Nyegezi na mchora ramani Deodatus Bety (51) mkazi wa Usagara ambao wote walikamatwa Desemba 30, 2017 kwa nyakati tofauti.

“Tulipata taarifa hizi baada ya mtu mmoja ajulikanaye kwa jina la Barnabasi Ibengo (39) mfanyabishara wa Kiseke kuwa ametapeliwa na watu waliosema wana viwanja viwili eneo la Nyasaka na kwamba vinahitaji Sh45 milioni, lakini akawa ametanguliza Sh10 milioni akiamini kuwa ni ukweli kutokana na nyaraka zote walizomuonyesha,” amesema Msangi.

Hata hivyo Msagi amesema mfanyabishara huyo, aligundua kuwa ametapeliwa baada ya kwenda eneo vilipo viwanja hivyo na kuonana na mwenyekiti wa mtaa huo na kuaambiwa hakuna jambo la namna hiyo ndipo alitoa taarifa polisi na kuanza kufuatilia kukamatwa mmoja baada ya mwingine.

Alisema watuhumiwa hao walikutwa na komputa inayotumika kutengenezea nyaraka mbalimbali na baadhi ya nyaraka zinazoonyesha viwanja kwa ajili ya kuuzwa.

Kuhusu vyeti feki Kamanda Msangi amesema walimkamata Evancy Wilson (33) katika mtaa wa Buzuruga Ilemela akiwa na vifaa vya kughushi vyeti vya taaluma mbalimbali.

Amesema tukio hilo lilitokea Janauri 9, mwaka huu saa 11:00 jioni ambapo mtuhumiwa baada ya kukamatwa na kuchunguzwa kwenye kompyuta yake walikuta namba inayofanana na TIN ya TRA na vyeti hivyo vya taaluma vya kughushi.

Amesema walikuta vyeti vya kughushi vya, stashahada, shahada, vyeti, vitambulisho vya mpigakura, nyaraka zinazoonyesha kuwa ni za kuombea mikopo benki, leseni za biashara na flash ambazo zimejazwa vitu hivyo.

“Hili lilitokana na taarifa tulizopata kutoka kwa raia wema kuhusu kuwapo kwa mtu anayetenegeza vitu hivyo ndipo tulianza kufuataili, watuhumiwa wote wapo polisi, upelelezi ukikamilika tutawafakisha mahakamani.

Kenya Airways Yazindua Safari za Moja kwa Moja Hadi Marekani

0
0
Shirika la ndege la Kenya, Kenya Airways, limezindua uuzaji wa tiketi za safari ya kwanza kabisa ya ndege zake za moja kwa moja kutoka Nairobi hadi Marekani.

Kenya Airways Yazindua Safari za Moja kwa Moja Hadi Marekani
Shirika hilo linapanga kufanya safari yake ya kwanza mnamo 28 Oktoba, hatua itakayoifanya Kenya Airways kuwa shirika la kwanza kutoka Afrika Mashariki kuwa na safari za moja kwa moja Marekani.

Ndege za shirika hilo litakuwa zinafasiri moja kwa moja hadi uwanja wa ndege wa JFK, New York.

Meneja Mkurugenzi wa Kenya Airways Sebastian Mikosz akizungumza wakati wa uzinduzi huo amesema safari hizo zitawafaa sana katika mpango wake wa ukuaji.

"Huu ni wakati wa kusisimua sana kwetu. Mpango huu unaingiana vyema na mpango wetu wa kuvutia abiria kutoka kwa mashirika na kampuni mbalimbali pamoja na watalii wa hadhi kufika Kenya na Afrika," amesema.


Safari hiyo itachukua saa 15 kutoka New York hadi Nairobi na saa 14 kutoka Nairobi hadi New York.
Shirika hilo limesema litatumia marubani wanne na wahudumu 12 wa ndege.
Safari yote itatumia tani 85 za mafuta.
Shirika hilo litatumia ndege zake za kisasa aina ya Boeing 787 Dreamliner ambazo huwabeba abiria 234.
Ndege za kwenda Marekani zitaondoka JKIA Nairobi saa 23:25 na kufika JFK kesho yake saa 06:25.
Ndege za kurudi Nairobi zitaondoka New York 12:25 na kutua JKIA saa 10:55 kesho yake.
Masharti
Kwa mujibu wa Bodi ya Utalii Kenya, Kenya hupokea watalii 100,000 kutoka Marekani kila mwaka na safari hizo zinatarajiwa kuifanya nafuu kuzuru Kenya kwa kupunguza muda wa kusafiri na gharama.

Wahudumu wa Kenya Airways wakati wa uzinduzi huo
Kuzinduliwa kwa safari hizo ni matunda ya mashauriano ya muda mrefu kati ya Kenya na serikali ya Marekani.

Kenya ilipewa masharti ya kuimarisha usalama, ikiwa ni pamoja na kuwatenganisha abiria wanaotua na wanaoondoka, kufanya salama njia za safari ya ndege na pia kuweka ua katika uwanja wa ndege wa JKIA.

Kenya ilipewa hadi ya Kiwango cha Kwanza kutoka kwa Shirika la Safari za Ndege la Marekani Februari mwaka jana na kuifungulia njia Kenya Airways kufanya safari za moja kwa moja.


Viewing all 104432 articles
Browse latest View live




Latest Images