Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104785 articles
Browse latest View live

Hiki Hapa Alichokisema Mama Samia Wakati wa Uzinduzi za Vijana Zanzibar

$
0
0
Hiki Hapa Alichokisema Mama Samia Wakati wa Uzinduzi za Vijana Zanzibar
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan amesema kuwa jamii haina budi kutambua kuwa vijana wana fursa kubwa katika kuleta maendeleo ya nchi .

Makamu wa Rais aliyasema hayo wakati wa Uzinduzi wa Baraza la Vijana Zanzibar uliofanyika kwenye ukumbi wa Baraza la Wawakilishi wa Zamani Kikwajuni.

Makamu wa Rais alisema kuwa Baraza la Vijana Zanzibar ni Chombo au jukwaa litakalowavusha vijana kufikia maendeleo wanayohitaji kiuchumi, kijamii, kisiasa na kufuatana na kasi ya maendeleo ya sayansi na teknolojia Duniani.

“Ni imani yangu kuwa Baraza hili litakuza mioyo yenu ili muweze kujituma, kujiendeleza na kuwa mstari wa mbele katika kuunga mkono serikali yenu pamoja na kutetea na kuyalinda Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar na kuenzi fikra za Muasisi wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, Marehemu Mzee Abeid Amani Karume (Mungu amrehemu)”

Makamu wa Rais aliendelea kusema kuwa Uzinduzi wa Baraza la Vijana Zanzibar ni mwendelezo wa mawazo ya Wana Mapinduzi ya kutaka kuweka hali za wananchi kuwa sawa (Bora), na kujenga Taifa lenye Vijana Imara.

Makamu wa Rais alisisitiza kuwa ni matarajio yake kuwa Baraza la Vijana Zanzibar litaendeshwa kwa misingi ya demokrasia na sheria, kanuni na miongozo ya taasisi itakavyoelekeza.

Baraza hilo linalotokana na Sera ya Maendeleo ya Vijana ya Mwaka 2005, sera hii ndio iliyopelekea kupitishwa kwa sheria nambari 16/2016 iliyoanzisha Baraza hilo, hatua ya utekelezaji wa Mkataba wa Vijana Afrika 2006 ambapo Jamhuri ya Muungano imeridhia.

Makamu wa Rais aliwataka Vijana kuwa mstari wa mbele katika kutunza amani ya nchi, kutoa ushauri pale wakiwa na mawazo mbadala, kutengeneza mtandao na kuitumia mitandao kwa manufaa ya kuwaleta pamoja na kukemea vitendo vyote vya udhalilishwaji wa watoto na wanawake.

Aidha Makamu wa Rais aliwataka vijana hao kuwa wamoja na kujenga hali ya kujitegemea na badala kuwa tegemezi, watetezi wan chi, kuibua mawazo mapya ya maendeleo na washiriki kwa kupaza sauti katika mambo yanayowahusu.

Baada ya Yanga Kutolewa Kombe la Mapinduzi Warudi Dar Vichwa Chini

$
0
0
Baada ya Yanga Kutolewa Kombe la Mapinduzi Warudi Dar Vichwa Chini
BAADA ya jana Klabu ya Yanga kuondoshwa kwenye Michuano ya Mapinduzi Cup na Klabu ya URA ya Uganda katika nusu fainali ya kwanza, wachezaji na viongozi wa klabu hiyo wamewasili Dar es Salaam leo kutoka Mjinni Unguja visiwani Zanzibar  huku wakiwa na sura za huzuni.

 Yanga abayo jana ilicheza chezo wa Nusu Fainali na URA huku ikiondolewa kwa njia ya mikwaju ya penati 5-4, baada ya nyota wao raia wa Zambia, Obrey Chirwa kukosa penati ya mwisho na kuwafanya waungane na wapinzani wao Simba SC, ambao nao waliondolewa juzi Jumatatu na Azam FC, baada ya kuchapwa bao 1-0.







Kiyombo Amechaguliwa Kuwa Mchezaji Bora wa Mwezi Desemba

$
0
0
Kiyombo Amechaguliwa Kuwa Mchezaji Bora wa Mwezi Desemba
Mshambuliaji wa Mbao FC ya Mwanza, Habibu Kiyombo amechaguliwa Mchezaji Bora wa mwezi Disemba wa Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) msimu wa 2017/2018.



Kiyombo ameibuka mchezaji bora baada ya kuwashinda wachezaji wenzake wawili alioingia nao fainali kutokana na tathmini iliyofanywa na kikao cha Kamati ya Tuzo wiki hii.

Kwa mwezi Disemba ambao timu 12 kati ya 16 zinazoshiriki ligi hiyo kila moja ilicheza mechi moja, Kiyombo aliisaidia timu yake kufunga mabao mawili katika mchezo dhidi ya Yanga ambao Mbao ilishinda mabao 2-0.



Kutokana na matokeo hayo, Mbao ilipanda kutoka nafasi ya nane hadi ya saba katika msimamo wa ligi, huku Kiyombo akifikisha mabao saba ya kufunga kwake msimu huu, akiwa nyuma ya Emmanuel Okwi wa Simba anayeongoza akiwa na mabao nane.

Kiyombo aliwashinda mshambuliaji wa Simba, John Bocco aliyefunga mabao mawili katika ushindi wa 2-0 wa Simba dhidi ya Ndanda na beki Bruce Kangwa aliyeisaidia Azam katika ushindi wa mabao 3-0 dhidi ya Stand United.

Katika mchezo huo wa Azam, beki huyo alifunga bao moja na kutoa pasi ya usaidizi wa bao lingine. Wachezaji wote hao hakuna aliyepata kadi.

Kutokana na ushindi huo, Kiyombo atazawadiwa tuzo, kisimbusi cha Azam na fedha taslimu sh. 1,000,000 (milioni moja) kutoka kwa wadhamini wakuu wa Ligi hiyo, Kampuni ya Vodacom.

Wachezaji wengine ambao tayari wametwaa tuzo ya mwezi kwa msimu huu ni Emmanuel Okwi (Agosti), Shafiq Batambuze (Septemba), Obrey Chirwa (Oktoba) na Mudathir Yahya( Novemba).

Je Una Upungufu wa Nguvu za Kiume, Hamu ya Tendo la Ndoa au Maumbile Madogo ya Uume?

$
0
0

JE, UNA UPUNGUVU WA NGUVU ZA KIUME, HAMU YA TENDO LA NDOA AU MAUMBILE MADOGO YA UUME?
SOMA HAPA👇👇.
Tatizo la upungufu wa nguvu za kiume au ukosefu wa hamu ya tendo la ndoa limezidi kuongezeka kwa kasi duniani kote na limekuwa chanzo kikubwa cha ndoa nyingi na mahusiano kukosa uaminifu kutokana na wengi kutoka nje ya ndoa ili kupata mtu atakayemtosheleza na kumfikisha kileleni. Pia udogo wa maumbile ni tatizo kubwa na limekuwa likiwakosesha wanaume wengi uwezo wa kujiamini katika tendo na kusababisha tendo hilo kutokufanyika kwa usahihi. Hili pia huchangia kwa kiasi kikubwa wanawake wengi kwenda nje ya ndoa ( MAHUSIANO) kutafuta mbadala wake.
BAADHI YA DALILI ZA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME NI KAMA:-
☆Kukosa hamu ya tendo la ndoa
☆Uume kusimama kwa ulegevu
☆Kuwahi kufika kileleni
☆Uume kusinyaa katikati ya tendo
☆Kushindwa kurudia tendo kwa wakati
☆Kuchoka sana baada ya round ya kwanza na hata kukinai kabisa.

Kwa kutumia mimea na matunda bila kemikali 🍇🍍🍓🌿🍉🍒🍎🍑 @markson_beauty_pr Tunakuletea suluhisho la matatizo hayo hata kwa wenye "KISUKARI NA PRESSURE" kwa:-
1.HANDSOME UP ORIGINAL:- kifaa chenye uwezo wa 99% kuongeza uume kwa size uipendayo na kuimarisha misuli ya uume iliyolegea @250,000/=
2.SHARK POWER ni gely ya kupaka inayoongeza uume kwa wastani wa inch 5.5 hadi 6 @150,000/=
3.VigRX CREAM:- ni gely iliyoboreshwa mahususi kwa ajili ya kuongeza maumbile kwa wastani wa inch 6.5 hadi 8 na kuimarisha misuli ya uume iliyolegea @200,000/=
4.Vidonge maalum kwa ajili ya kuongeza nguvu na hamu ya tendo la ndoa hata kwa wenye kisukari @150,000/=
5.Spray ya kuchelewesha kufika kileleni na kuweza kurudia tendo ×3. @150,000/=
BIDHAA HIZI HAZINA MADHARA KIAFYA NA ZIMETHIBITISHWA
NA SHIRIKA LA AFYA DUNIANI (WHO).
KWA BIDHAA HIZI NA NYINGINE NYINGI TEMBELEA UKURASA WETU WA INSTAGRAM :-
@markson_beauty_pr
@markson_beauty_pr
@markson_beauty_pr
WEB:www.markbeauty.org
Wasiliana nasi Popote
ulipo duniani kwa (+255)
0767447444 na
0714335378
UTAPATA HUDUMA
NB:Matokeo ni uhakika na garantii na hakikisha unapata risiti yenye muhuri halisi wa MARKSON CO pamoja na garantii ili kukuhakikishia kufanikiwa kwako.

Huyu Ndiye Binadamu Mwenye Nywele Nyingi Zaidi Duniani

$
0
0

Kutoka katika Mtandao wa World Ranking ambapo umemtaja Yu Zhenhuan wa China  kuwa ndiye mwanaume mwenye nywele nyingi zaidi duniani.

Mwili wa Yu Zhenhuan umefunikwa na nywele nyingi tofauti na binadamu wengine hali iliyosababishwa na yeye kuwa na ugonjwa unaofahamika Hypertrichosis.

Sasa anataka kuondoa sehemu muhimu ya nywele kutoka kwenye mwili wake. Lakini nywele zote zitahitajika kuteketezwa kwa laser na utaratibu huu utamsababishia maumivu makali sana katika mwili wake.

Yu Zhenhuan amekuwa kwa muda mrefu anaishi na mkewe ambaye amekuwa akimsaidia kupata njia ya kumwezesha kupunguza nywele katika mwili wake huo.

Mwanamke Amuuza Mwanawe wa Siku Tatu Siku ya Mwaka Mpya

$
0
0

ITUI, KENYA: Mwanamke aliyejulikana kama Sarahi Kwamboka amepandishwa kizimbani kujibu tuhuma za kumuuza mwanae wa siku 3 siku ya mwaka mpya kwa dau la Shilingi 10,000 za Kenya.
-
Mtuhumiwa huyo ambaye ni Mama wa Watoto 3 alipandishwa kizimbani pamoja na anayedaiwa kumnunua mtoto huyo, Bi. Bernadette Musanya.
-
Korti ilielezwa kuwa Mtuhumiwa huyo wa kwanza alijifungua mtoto wa kike aitwaye Fridah Mutheu katika kituo cha afya cha Kanyangi siku ya Desemba 29, 2017 huko Kitui na siku 3 baadaye yaani siku ya mwaka mpya ndipo alimuuza kwa Bi. Musanya.
-
Wawili hao walikubali mashtaka ambapo mama huyo alidai amefanya hayo kutokana na umasikini unaomkabili na aliona atashindwa kumlea mtoto huyo pamoja na watoto wake wengine wawili.

Habari Njema: Tunatibu Busha, Korodani Kuvimba,Ngiri, Miguu Kufa Ganzi Pamoja na Matatizo ya Nguvu za Kiume

$
0
0

Ni Dawa ya nguvu za kiume inayorefusha na kunenepesha uume saizi uipendayo (Inch 1-7) kwa muda wa siku 6 tu.Dozi hii itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa muda wa dakika 30, utarudia tendo la ndoa zaidi ya mara 4 bila hamu kuisha bila kujali umri na garantee ni miaka 60 baada ya kutibu tatizo.

Pia tunatibu Busha bila kufanyiwa Oparesheni, korodani moja kuvimba, ngiri, tumbo kujaa gesi na kuunguruma, kutopata choo vizuri, miguu kuwaka moto na kufa ganzi, chango la wanawake, kisukari na kutokwa na kinyama sehemu ya haja kubwa.

MIHAYO:
Inarudisha mke, mchumba, hawara na atakutimizia kila kitu unachotaka kutoka kwake ndani ya  saa 2 tu hata kama yupo mbali. atarudi na kumfunga asiwe na mwingine zaidi yako.

Umefukuzwa kazini? unataka kupandishwa cheo? Umepoteza pesa zako kwenye biashara bila kujua umepandikizwa chuma ulete? Njoo urudishe pesa zako. Unauza mali yako haiendi?

Wasiliana na mtaalam Challo kwa; 0714006521

Serikali Yakiri Kuingizwa Mkenge Ubinafsishaji TTCL, Dr Mpango Akabidhi Ripoti ya Uchunguzi Kwa Rais Magufuli

$
0
0

Waziri wa Fedha na Mipango Dkt. Philip Isdor Mpango jana tarehe 11 Januari, 2018 amewasilisha taarifa ya kamati aliyoiunda kuchunguza umiliki wa kampuni ya simu Airtel kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli aliyeagiza kufanyika kwa uchunguzi huo tarehe 20 Desemba, 2017.


Baada ya kuwasilisha taarifa hiyo, Dkt. Mpango amesema Serikali imejiridhisha kuwa ubinafsishaji wa Shirika la Simu Tanzania (TTCL) kwenda Celtel, baadaye kuhamishiwa Zain na sasa Airtel ulifanyika kwa ukiukwaji mkubwa wa sheria, kanuni na taratibu.


Kufuatia ukiukwaji huo Dkt. Mpango amesema Serikali inayomiliki asilimia 40 ya hisa za kampuni ya Airtel imeamua kufanya mazungumzo na kampuni ya Airtel inayomiliki asilimia 60 ya hisa ili nchi iweze kupata haki yake.


“Lakini niwaambie Watanzania yale ambayo tumeyaona ni machafu sana, ni mambo ya hovyo kabisa, nchi yetu kwa kifupi tuliingizwa mkenge, ni fedha nyingi zimepotea kwa hiyo sisi katika majadiliano haya lengo letu litakuwa ni kuhakikisha Watanzania wanapata haki yao” amesema Dkt. Mpango.


Wakati huo huo, Mhe. Rais Magufuli amepokea taarifa ya utekelezaji wa maagizo aliyoyatoa tarehe 25 Novemba, 2017 wakati wa ufunguzi wa Hospitali ya Taaluma na Tiba ya Chuo Kikuu cha Tiba na Sayansi Shirikishi  (Mloganzila) kutoka kwa Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu.


Baadhi ya maagizo hayo ni kupunguza baadhi ya idara na madaktari katika hospitali ya Taifa Muhimbili na kuhamishia Mloganzila na hospitali za mikoa kuhamishwa kutoka Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) kwenda Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto.


Mhe. Ummy Mwalimu amewasilisha taarifa hiyo akiwa ameongozana na  viongozi wakuu wa Hospitali ya Taifa Muhimbili, Taasisi ya Mifupa (MOI), Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKHI), Chuo Kikuu cha Tiba na Sayansi Shirikishi (MUHAS).


Katika hatua nyingine, Waziri wa Katiba na Sheria Prof. Palamagamba Kabudi amekamilisha kanuni za sheria ya madini namba 7 ya mwaka 2017 na kuwasilisha vitabu vya kanuni hizo kwa Katibu Mkuu Kiongozi Balozi John Kijazi.


Akiwa na Naibu Mawaziri wa Madini Mhe. Stanslaus Haroon Nyongo na Mhe. Doto Mashaka Biteko, Prof. Kabudi amesema kanuni hizo zimekamilika siku moja kabla ya tarehe ya mwisho iliyotolewa na Mhe. Rais Magufuli na kubainisha kuwa sasa sheria inaweza kuanza kutumika.


Kwa upande wao Naibu Mawaziri wa Madini wamewataka Watanzania na wadau wote wa sekta ya madini kushirikiana na Serikali kutekeleza sheria hiyo na wamempongeza Mhe. Rais Magufuli kwa kutoa msukumo wa kukamilishwa kwa kanuni hizo.

Wanaomba Rushwa ya Ngono Kukiona cha Moto

$
0
0

Naibu Waziri wa Fedha na Mipango Dk Ashatu Kijaji amesema wizara yake imeanza kuchukua hatua kali za kisheria kwa watumishi wa taasisi za elimu ya juu wanaotumia wadhifa wao kuomba rushwa ya  ngono  kwa wanafunzi na kisha kuwapa alama za juu za ufaulu tofauti na uwezo wao kitaaluma.

Dakta kijaji anatoa angalizo hilo jijini Arusha alipokua akizungumza watumishi na wajumbe wa Baraza la wafanyakazi wa chuo cha Uhasibu cha Arusha.

Akizungumza kwa niaba ya watumishi hao makamu Mwenyekiti wa Baraza la wafanyakazi Juma Kaniki akaahidi kuhakikisha maadili yanasimamiwa huku akitumia fursa hiyo kuiomba serikali kuongeza idadi ya watumishi.

Mkuu wa wilaya ya Arusha Gabriel Daqaro aliyeambatana na Naibu Waziri akawakumbusha wajumbe wa Baraza la wafanyakazi kuepuka kuwa chanzo cha migogoro ndani ya taasisi.

Kutana na Mtabibu Mwenye KUBRI kutoka kwa ALLAH issa simba said Mtabibu wa Nyota za Binadamu na Dawa za Asili

$
0
0

Kutana na Mtabibu Mwenye KUBRI kutoka kwa ALLAH issa simba said Mtabibu wa Nyota za Binadamu na Dawa za Asili ya Africa Mwenye UWEZO Kubaini tatizo lako Pindi tu Utakapo Fanya Mawasilino Kupitia Wasaa Husika..JE UNASUMBULIWA NA Mapenzi? (Umeachwa na Umpendae,Awe Mume,Mke na Bado unampenda?Na Umejaribu Sehemu nyingi Bila Mafanikio?Wasilina na Maalim Hussein Ujione muujiza wa Papo kwa Papo.. anauwezo WA KURUDISHA MAHUSIANO NA KUIMARISHA NDOA YAKO NDANI YA SAA 12 TU. Umekimbiwa na Mumeo,mkeo au Mpenzi na anaishi na mtu mwingine? Muone akutatulie Anauwezo wa Hali ya Juu wa Kusambalatisha Mahusiano yao Endapo utafata Atakacho kuelekeza.
Atamfanya Atimize Ahadi zote kwa Muda Mfupi.

Issa simba said Anatumia Jina la Muhusika au Picha Kumaliza Tatizo lako..
Anatibu kwa Kutumia Vitabu vya QUR-AN Dawa za Asili za Africa,Dawa za Kiarabu na Majini.Anatafsiri Ndoto. Kushinda BAHATI NASIBU, KUSAFISHA NYOTA. Mvuto wa Mwili na BIASHARA, Kinga ya Mwili,ZINDIKO za Nyumba.MIGUU Kufa GANZI.Kufungua KIZAZI kwa wale walio fungwa kwa njia za KISHIRIKINA. Anakupa Jini la Mali kwa yule anaehitaji Utajiri BILA MASHARTI. Nguvu za KIUME, Humaliza Kesi zilishindika ndani ya siku 14 tu..na mengi zaidi

Wasiliana nasi +255 622588038au 0679119679 au +255 764318107

NB: TIBA KWA DINI ZOTE NA IMANI ZOTE... 

Quick Rocka Akanusha Kutoka Kimapenzi na Msanii Alice

$
0
0
Quick Rocka Akanusha Kutoka Kimapenzi na Msanii Alice
Msanii Quick Rocka amekanusha tetesi zilizokuwa zikiendelea mitandaoni kuwa yupo kwenye uhusiano mzito wa kimapenzi na Muigizaji Alice Kella.


Rocka amekanusha tetesi hizo wakati akizungumza na eNEWZ ya EATV na kupinga kwamba tetesi ambazo zilianza kusambazwa na msanii Alice kwa kuweka picha mtandaoni na kuandika maneno "mume wangu nampenda sana" ambayo  yalitafsiriwa kuwa ni wapenzi.

Aidha Quick Rocka amesema kwamba  hakuna mahusiano yoyote ya kimapenzi kati yao bali picha ambazo zilisambaa ni sehemu ya kazi zao za filamu.

"Mimi na Alice hatuna mahusiano yoyote yale na zile picha ni series tu ambayo tunaifanya ndio tulikuwa tunafanya photoshoot na hakuna kingine chochote kinachoendelea kati yetu zaidi ya kazi na Alice ni kama mdogo wangu hivyo watu wasichukulie tofauti" Quick

Msanii Quick Rocka kwa sasa  ni moja kati ya wasanii wakongwe na bado wanaendelea kufanya muziki na anafanya vizuri  huku akiwa anasimamia kundi la muziki liitwalo OMG.

Young Killer Afunguka Alivyozinguliwa Kisa Dogo Janja

$
0
0
Young Killer Afunguka Alivyozinguliwa Kisa Dogo Janja
RAPA anayefanya vizuri kwenye gemu la Hip Hop Bongo, Young Killer, amefunguka kuwa, katika harakati zake za muziki amewahi kukosa msaada wa kimuziki kisa akionekana anataka kuingia kwenye fani hiyo kumuiga Dogo Janja ambaye alikuwa ameshatoboa kimuziki.


Akichonga na Showbiz- Xtra, Young Killer alisema kamwe hawezi kusahau alivyobaniwa na watu ambao wangeweza kumfanya atoke kimuziki muda mrefu, lakini alionekana anataka kuingia kwenye fani hiyo kwa kuwa ameona Dogo Janja anafanya vizuri kwenye gemu.


“Walidhani naingia kwenye muziki kwa sababu ya kumuiga Dogo Janja, nilibaniwa msaada nikionekana mkurupukaji, nilionekana kama nataka kufanya kwa kuwa nimeona mtoto mwenzangu anafanya, niliumia sana,”alisema Young Killer bila kuwataja watu hao. Killer alisema anashukuru Mungu alikuja kutoka kivingine na mashabiki wakamkubali.

Kuhusu Msanii 'Nini' Jibu Ninalo Moyoni Mwangu- Nay wa Mitego

$
0
0
 Jibu Kuhusu Msanii 'Nini' Ninalo Moyoni Mwangu- Nay wa Mitego
MKALI wa Bongo Fleva, Emmanuel Elibariki ‘Nay wa Mitego’ amefunguka kuwa, baada ya kufanya kazi na mrembo anayekuja kwa kasi kwenye muziki, Nini, maneno yamekuwa hayaishi hivyo wamuache kwani ukweli anao yeye mwenyewe.

Akizungumza na Showbiz-Xtra, Nay alisema kuna baadhi ya mashabiki hata uwaambie nini huwa hawawezi kukuelewa hivyo kwa sasa kila atakayemuuliza kuhusu uhusiano wake na Nini, atakuwa hana jibu zaidi ya kusema ukweli anao moyoni.

“Unajua ukiwaambia watu kwamba ni rafiki tu, hawakuelewi. Ukiwaambia kwamba mnafanya naye tu kazi hawakuelewi basi mimi nafikiri kwa sasa itoshe tu kusema kwamba jibu ninalo moyoni mwangu,” alisema Nay.

Nay na mrembo Nini wamekuwa wakihusishwa kuwa na uhusiano wa kimapenzi hususan baada ya kufanya kazi pamoja katika Wimbo wa Niwe Dawa wa mrembo huyo.

Siwezi Kushuka Kimuziki Kisa Ndoa- Belle 9

$
0
0
Siwezi Kushuka Kimuziki Kisa Ndoa- Belle 9
MWANA-MUZIKI anayetamba na Ngoma ya Mfalme, Abednego Damian ‘Belle 9’ ambaye hivi karibuni aliingia kwenye ndoa ameibuka na kusema hawezi kupotea kimuziki kisa kuoa kama wasanii wengi wanavyokuwa.

Akizungumza na Showbiz-Xtra, Belle 9 alisema, yeye ni msanii anayejiamini kwenye kazi zake hivyo hawezi kutetereka sababu ya ndoa, akashuka kimuziki kama ilivyotokea kwa wasanii wengine.

“Suala la kushuka kimuziki kisa ndoa sikubaliani nalo hata kidogo, hao wanaoshuka wanashuka kwa sababu zao binafsi, sidhani kama sababu ni ndoa, kwanza huyu mwanamke ninaye siku nyingi vipi nifeli baada ya kumuoa,”alisema.

Hashim Rungwe Naye Ataka Kuonana na Rais Ikulu

$
0
0
Hashim Rungwe Naye Ataka Kuonana na Rais Ikulu
 Mwenyekiti Chama cha Chaumma, Hashim Rungwe amesema anatamani kwenda Ikulu kuonana na Rais John Magufuli ili kumweleza mambo ambayo yatawezesha kusaidia kuleta mabadiliko katika utawala wake.

Akizungumza na Mwananchi leo Ijumaa Januari 12, 2018, Rungwe amesema kila mtu anatamani kuonana na Rais Magufuli lakini nafasi hiyo imekuwa haipatikani.

Rungwe anatoa kauli hiyo ikiwa imepita siku tatu tangu waziri mkuu wa zamani, Edward Lowassa alipofanya ziara Ikulu na kuzungumza na Rais Magufuli.

“Hata mimi nataka kuonana na Rais, nimekuwa natamani sana lakini hatupati nafasi hiyo, nikikutana naye tutazungumza mambo mengi, ambayo yatamsaidia yeye mwenyewe katika uongozi wake,” amesema Rungwe na kuongeza;

“Sisi upinzani tulikuwa tunasema hatutaki mafisadi, hatutaki wabidhirifu au tunapiga kelele dawa hakuna hospitalini kwa hiyo anapopeleka dawa hospitalini ni sisi tumesaidia, kwa hiyo kuongoza ni kusikiliza watu wanasema nini wakati mwingine.”

Mwananchi lilipotaka kujua hasa ni kitu gani ambacho anataka kumweleza Rais Magufuli, Rungwe amesema “hiyo ni siri yangu, lakini tumekuwa tikitafuta nafasi hiyo lakini wapi, lakini naona Lowassa kaenda na wamezungumza.”



Chama cha Mawakili (TLS) Kimekusanya Milioni 138 ya Kugharamia Matibabu ya Lissu

$
0
0
Chama cha Mawakili (TLS) Kimekusanya Milioni 138 ya Kugharamia Matibabu ya Lissu
Chama cha Mawakili Tanganyika (TLS) kimesema kimefanikiwa kukusanya Sh138 milioni kugharamia matibabu ya Rais wa Chama hicho, Tundu Lissu aliyelazwa Hospitali ya Chuo Kikuu cha Leuven nchini Ubelgiji.

Taarifa iliyotolewa na Makamu Mwenyekiti wa TLS, Godwin Ngwilimi amesema kiasi hicho wamekipata kutoka kwa watu mbalimbali walijitolea kuchangia wa ndani na nje ya nchi wakiwemo wanachama wa chama hicho.

Kuhusu mchanganuo wa fedha hizo, Ngwilimi amesema kimetumika kulipa gharama za matibabu ya Lissu katika Hospitali ya Nairobi, Leuven na visa kwa watu watatu wakiwa nchini Ubelgiji.

Ngwilimi ametoa shukuran kwa wale wote waliojitokeza kuchangia matibabu ya Lissu ambaye pia ni mbunge wa Singida Mashariki na mwanasheria mkuu wa Chadema.

Lissu aliyeshambuliwa kwa risasi zaidi ya 30 na watu wasiojulikana Septemba 7, 2017 akiwa katika makazi yake mjini Dodoma ambapo alipelekwa Hospitali ya Rufaa ya Dodoma na usiku wa siku hiyo alihamishiwa Hospitali ya Nairobi alikolazwa hadi Januari 6 baada ya kahamishiwa Leaven, Ubelgiji kwa mazoezi ya viungo na saikolojia.


Sitetereki na Majina Ninayopewa Instagram kwani Hayanipunguzii Uhai- Hamissa Mobetto

$
0
0
Sitetereki na Majina Ninayopewa Instagram kwani Hayanipunguzii Uhai- Hamissa Mobetto
Mwanamitindo Hamisa Mobetto amesema hana tatizo na majina aliyopewa Instagram na mashabiki wanaomchukia kwani hayampunguzii uhai wa kuishi zaidi ya kumpa kiki na kuweza kufanya biashara zake na mambo yake yenye maana kwa kiki wanazompa.

Hamisa katika mtandao wa Instagran kuna mashabiki ambao wameunda team na kumpa majina ya maudhi ilimradi kumdhalilisha au kumchukiza.

Majina hayo ni chuchunge, Ruba, Mbu, Laki tano, ambapo watu hao huyatumia kwa kutuma picha ya Hamisa katika akaunti zao na kuandika jina moja kati ya hayo na maelezo yanayomuhusu Hamisa.

Hamisa alipata kupiga stori na MCL Digital ,ambapo amesema anawashangaa sana wanaompa majina ya ajabu ajabu wakitegemea anaweza kuchukia kumbe anayafurahia na kuyapenda na anawashauri wamuongezee majina mengine ili aweze kupata dili zaidi.


Redio, TV ya Diamond Kufunguliwa February Mwaka Huu

$
0
0
Redio, TV ya Diamond Kufunguliwa February Mwaka Huu
Kampuni ya Wasafi Classic (WCB), inayomilikiwa na msanii maarufu wa muziki wa Bongofleva, Naseeb Abdul ‘Diamond’ wanatarajia kufungua televisheni na redio Februari mwaka huu.

Haya yamebainika ikiwa ni saa chache tangu Diamond na viongozi wa kampuni hiyo watupie jumba la kifahari  ambalo linaelezwa  litakuwa ndiyo ndiyo makao makuu ya WCB ambapo mbali ya kuwa na studio za kurekodia muziki pia litakuwa na Redio na TV.

Mwananchi ilimtafuta mmoja wa mameneja wa Diamond, Said Fela  kuweza kujua hasa ni lini TV na redio hizo zitaanza kufanya kazi alisema itaanza rasmi Februari mwaka huu.

Katika mahojiano hayo, Fela amesema hatua waliofikia ni katika harakati za kampuni hiyo kuendelea kujitanua na kutoa fursa kwa vijana wengi zaidi.

Fela amesema pamoja na kwamba wao ni watu wanaojishughulisha na kazi za burudani, lakini TV yao na redio zitakuwa zinarusha vipindi vya aina zote vikiwemo vya kuelimisha na habari kama vilivyo vituo vingine.

“Kwetu sisi hii tunaona ni hatua nzuri kwa kuwa tunajua tukifungua vituo hivi ndivyo kadri tunavyozidi kuzalisha ajira na tumeamua kutumia wataalam ambao walikuwa kwenye fani hiyo ikiwemo wazee waliostaafu katika Shirika la Utangazaji(TBC) enzi hizo TVT kwa ajili ya kutuongoza kwa kuwa sisi wenyewe hatuwezi,”amesema Fela.

Hata hivyo, alipoulizwa kama wamejenga wenyewe mjengo huo au Fela amesema wamekodisha kama walivyokuwa wamekodisha ile ya Sinza huku sababu za kuhama akieleza ni kutokana na kuongeza huduma na pia sehemu waliyokuwepo kulikuwa na taabu ya maegesho ya magari na kujaa maji hasa mvua zinaponyesha.

Mjengo huo wa wasafi wa ghorofa moja ambao upo maeneo ya Mbezi umeonekana kuwa gumzo leo Alhamisi katika mitandao ya kijamii na watu wengi wamempongeza Diomond na uongozi wake kwa hatua aliofikia.

Mbali na redio, tayari Diamond ameshajiingiza katika biashara nyingine ikiwemo ya manukato yanayoitwa 'Chibu', na 'Diamond karanga'



Mama Aliyejifungua Watoto Watatu Mapacha Awapa Majina ya Viongozi Chadema Mbowe, Lissu na Halima

$
0
0
Mama Aliyejifungua Watoto Watatu Mapacha Awapa Majina ya Mbowe, Lissu na Halima
Mwanamke mmoja Martha Haule mkazi wa  Sumbawanga mkoani Rukwa amejifungua watoto mapacha watatu na kuwapatia majina ya Halima Mdee (wa kike) pamoja na Mbowe(Freeman) na Lissu (Tundu).

Taarifa iliyotolewa na Chadema Kanda ya Nyasa na kuthibitishwa na mwenyekiti wa kanda hiyo, Mchungaji Peter Msigwa imeeleza kuwa watoto hao ambao wana mwezi mmoja wamezaliwa kufuatia mwanamke huyo kupata uchungu ghafla baada ya kusikia Mwenyekiti huyo wa Baraza la Wanawake wa Chadema(Bawacha), Mdee atazuru Sumbawanga na kutembelea kikundi chao cha Wanawake Tunaweza kilichopo katika Kata ya Mafulala.

Mwenyekiti huyo wa Bawacha leo  Alhamisi Januari 11 akiwa katika siku ya pili ya ziara yake yenye lengo la ujenzi na uenezi wa chama ikiwa ni pamoja na kuangalia uhai wa baraza hilo.

Alichoandika Mama wa Mtoto Aliyebaguliwa na Kampuni ya Nguo ya H&M

$
0
0
Alichoandika Mama wa Mtoto Aliyebaguliwa na Kampuni ya Nguo ya H&M
Baada ya ubaguzi wa rangi kufanyika kwa mtoto wa kiume na kampuni ya nguo ya H&M kwa kumvalisha nguo yenye maneno ya kudhalilisha watu weusi yanayosema “Coolest Monkey in the Jungle” yakimaanisha “Mimi ni nyani mtulivu msituni”

Mastaa kadhaa kutokea Marekani walichukizwa na kitendo hicho kilichofanywa na kampuni hiyo ya H&M akiwemo  P.Diddy, T.I huku THE WEEKEND  akitaka kujitoa katika mkataba wa kufanya kazi na H&M baada ya kuona kitendo hicho cha kibaguzi.

Kupitia mtandao wa instagram maneno ya mama mzazi wa mtoto huyo yamewashangaza wengi baada ya mama mzazi wa mtoto huyo kuwataka watu waache kulia muda wote kutokana na ishu hiyo ya mwanae kwamba haina ulazima wa kuiongelea kwenye mitandao ya kijamii.

Baada ya maneno ya mama huyo watu wengi wametafsiri kuwa huenda akawa hampendi mwanae au hajali kwa unyanyasaji aliofanyiwa mwanae, wengi wamehisi kuwa huenda kampuni ya H&M imempa pesa mama huyo ili kujisafisha na kulifanya suala hilo lionekane la kawaida.
Viewing all 104785 articles
Browse latest View live




Latest Images