Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104762 articles
Browse latest View live

Dk. Shein Atunuku Nishani Zilizotukuka 43 kwa Viongozi na Watumishi wa Umma

$
0
0
Dk. Shein Atunuku Nishani Zilizotukuka 43 kwa Viongozi na Watumishi wa Umma
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dkt. Ali Mohammed Shein ametunuku nishani zilizotukuka 43 kwa viongozi na watumishi wa umma ikiwa ni maadhimisho ya miaka 54 ya Mapinduzi matukufu ya Zanzibar.

Dkt. Shein ametoa nishani hizo kwa mutu ambae aliasisi,alishiriki na kutukuza pamoja na kuyaenzi Mapinduzi ya Zanzibar yaliyotokea mwaka 1964.

Pamoja na hayo Dk. Shein amewataka wananchi wa Zanzibar kuendelea kudumisha amani na utulivu uliopo ili kuwa chachu ya kuendelea kuwa kivutio kikubwa kwa uwekezaji miradi mikubwa ya maendeleo visiwani .

Katika maadhimisho hayo mbali ya nishani hizo serikali ya Zanzibar huzindua miradi mbalimbali ya maendeleo ikiwa ni ishara ya ukombozi wa fikra na maendeleo ya kiuchumi ya taifa hilo.

Bodaboda Wala Kiapo Mbele ya Waziri cha Kuwalinda Wanafunzi wa Kike

$
0
0
Bodaboda Wala Kiapo Mbele ya Waziri cha Kuwalinda Wanafunzi wa Kike
Madereva Bodaboda wa wa Manispaa ya Mpanda Mkoa wa Katavi wamekula kiapo cha uaminifu cha kuwalinda watoto wa kike dhidi ya vitendo vya ngono na mimba za utotoni zinazo sababisha kukatisha haki yao ya kuendelezwa.



Kiapo hicho kimeongoza na Naibu Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Dkt. Faustine Ndugulile(Mb) ikiwa ni mwendelezo wa utekelezaji wa Kampeni ya “Mimi ni Msichana Najitambua Elimu Ndio Mpango mzima” iliyozinduliwa tarehe 11 Oktoba, 2017 kwa lengo la kuhamasisha wananchi kupambana na kuzuia matukio ya mimba za utotoni katika jamii zetu.

Dkt.Ndugulile amesema kuwa ili kufanikisha kutokomeza mimba za utotoni hatuna budi kuweka ushirikiano baina ya wazazi, walezi, jamii, Serikali na wadau wengine ili kuwaepusha watoto wa kike kupata vishawishi vya mahusiano ya kingono katika umri mdogo na hatimaye kupata mimba za utotoni.

Ameongeza kuwa lengo la Kampeni ya “Mimi ni Msichana Najitambua Elimu ndio Mpango Mzima” imelenga kuunganisha nguvu za pamoja za wanajamii wakiwemo madreva wa Bodaboda kushirikiana na Serikali kuzuia na kutokomeza matukio ya mimba za utotoni katika ngazi ya jamii na shuleni.

“Niseme kampeni hii itasaidia kwa asilimia kubwa kuunganisha nguvu zetu kama wananchi na sisi Serikali katika kutokomeza vitendo hivi viovu”alisisitiza Mhe. Dkt. Ndugulile.

Aidha Dkt. Ndugulile amewaasa madereva hao kuondokana na tamaa za kujihususha na mahusiano na kingono na watoto wadogo bali wao kuwa walinzi wao katika kutokomeza suala mimba kwa watoto wetu.

Amewataka kufichua vitendo vyovyote vyenye ushawishi wa mahusiano yanayosababisha mimba kwa watoto wa kike ili Sheria iweze kuchukua mkondo wake.

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Mpanda Mhe. Lilian Matinga amesema kuwa wataendelea kushirikiana na wadau mbalimbali kwa kuweka mikakati ya kupambana na wanaume na vijana wakware wanaotumia fursa zao kuwa na mahusiano maovu na watoto wa kike katika Wilaya ya Mpanda Mkoa wa Katavi ambao ndio unaoongoza kitaifa kwa kuwa na asilimia 45.

Mmoja wa dereva Boda boda wa Wilaya ya Mpanda Bw. Juma Salum kwa wakati tofauti wameishukuru Serikali kwa kuandaa Kampeni hiyo itakayowajengea uelewa wananchi kusaidiana katika kuwalinda watoto wa kike kwa kuweka miundo mbinu salama ya kusomea na kujifunzia ili kupunguza kiwango cha mimba za utotoni kwa silimia 50 ifikapo mwak 2021/22.

Naibu Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Dkt. Faustine Ndugulile (Mb) alikuwa na ziara ya siku mbili mkoani Katavi kuhamasisha wananchi kupambana na kuzuia mimba za utotoni kupitia “Kampeni ya Mimi ni Msichana Najitambua Elimu Ndio Mpango mzima”.

Trump Akataa Kufungua Ubalozi Mpya wa Marekani Uingereza

$
0
0
Trump akataa kufungua ubalozi mpya wa Marekani Uingereza
Rais Donald Trump wa Marekani amefutilia mbali mpango wa kuzuru nchini Uingereza mnamo mwezi Februari ambapo alikuwa ametarajiwa kufungua ubalozi mpya wa taifa hilo uliogharimu takriban dola bilioni moja.

Katika ujumbe wake kwa Twitter, rais huyo wa Marekani alisema yeye sio shabiki wa ubalozi huo mpya ambao unahamia kutoka Mayfair kuelekea mjini London akidai kuwa ulikuwa ''mpango mbaya''.

''Jumba la zamani la ubalozi huo liliuzwa kwa fedha chache na utawala wa rais Obama'', aliongezea.

Downing Street ilikataa kutoa tamko kuhusu hatua hiyo ya rais Trump.

Muhariri wa BBC kaskazini mwa Marekani Jon Sopel alisema kuwa kuna uwezekano wa maandamano katika barabara za mji wa London iwapo angezuru.

Hatua hiyo ya ubalozi wa Marekani ilithibitishwa mnamo mwezi Oktoba 2008 wakati rais George W Bush alipokuwa mamlakani.

Hatahivyo rais Trump aliulaumu utawala wa aliyekuwa rais wa taifa hilo Barrack Obama kwa kuuza eneo zuri la ubalozi huo kwa ''fedha chache''.

Alisema kuwa jengo hilo jipya katika eneo la Vauxhall, kusini mwa London lilikuwa katika eneo baya, akiongezea.''Walitaka mimi nilifungue rasmi-Hapana!''

Kamati Kuu Chadema Kukutana Kesho Katika Kikao cha Dharura

$
0
0

Kamati Kuu Chadema Kukutana Kesho Katika Kikao cha Dharura
Kamati Kuu ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kesho inakutana katika kikao cha ‘dharura’ jijini Dar es Salaam.

Akizungumza na Mwananchi leo Ijumaa Januari 12, 2018, Naibu Katibu Mkuu wa Chadema-Zanzibar, Salum Mwalimu amesema lengo la kikao hicho ni kufanya tathmini ya hali ya kisiasa nchini.

Mwananchi lilipotaka kujua kama lengo la kikao hicho ni kujadili ziara ya waziri mkuu wa zamani, Edward Lowassa kwenda Ikulu, Mwalimu amesema kikao hicho si cha dharura kwani kilipangwa kufanyika Desemba mwaka jana lakini kiliahirishwa kutokana na sikukuu za mwisho wa mwaka.

Amesema ajenda za kikao hicho zilipangwa kabla Lowassa ambaye ni Mjumbe wa Kamati Kuu ya Chadema hajaenda Ikulu hivyo hakika uhusiano na ziara hiyo ila huenda jambo hilo likajitokeza.

“Suala hilo halipo kwenye ajenda ila linaweza kujitokeza na likijitokeza litazungumziwa lisipojitokeza basi,” amesema Mwalimu na kuongeza;

“Hata hivyo kwa upande wake inaweza kuwa fursa nzuri kuielezea Kamati Kuu na viongozi wenzake nini kilitokea.”



Mrema Atinga Polisi Kuhusu Suala la Kuzushiwa Kifo

$
0
0
Mrema Atinga Polisi Kuhusu Suala la Kuzushiwa Kifo
Mwenyekiti wa TLP, Augustine Mrema leo Ijumaa ametoa taarifa za kuzushiwa kifo katika Kituo cha Polisi cha Oysterbay wilayani Kinondoni ili wahusika waweze kuchukuliwa hatua za kisheria.

Juzi katika mitandao ya kijamii zilisambaa taarifa za kufariki kwa mwanasiasa huyo lakini muda mfupi baadaye Mrema alikanusha akisema ni mzima wa afya njema.

Akizungumza na Mwananchi leo Ijumaa, Mrema amesema yupo Oysterbay kutoa taarifa ili suala hilo lichunguzwe na Jeshi la Polisi ili wamnase aliyesambaza taarifa hizo.

“Nipo Oysterbay Polisi namalizia taratibu za kuandikisha kesi hii, nikimaliza nitakujulisha kwa kina kuhusu suala hili,” amesema.

Ibrahim Ajibu Aiangukia Yanga Kutokana na Matokeo Mabaya

$
0
0
Ibrahim Ajibu Aiangukia Yanga Kutokana na Matokeo Mabaya
BAADA ya kipigo cha penalti 5-4 dhidi ya URA, juzi mshambuliaji wa Yanga, Ibrahim Ajibu Migomba ameom­ba radhi kwa mashabiki wa timu hiyo kuto­kana na ma­tokeo ma­baya.

Yanga ilion­dolewa kwenye michuano ya Kombe la Map­induzi katika hatua ya nusu fainali na URA ya Uganda kutinga fainali dhidi ya Azam FC.

Msham­buliaji huyo alisema hawakupenda kupata matokeo ya aina ile lakini ilitokea vile kwa sababu mpira una matokeo matatu.

“Naomba mashabiki wetu wa Yanga wa­tusamehe kwa matokeo mabaya hakuna timu ambayo inapenda kupoteza zaidi mtupe sapoti ,”al­isema Ajibu.

Hata hivyo katika mchezo huo wachezaji ambao wali­piga penalti ni Papy Tshishim­bi, Hassan Kessy, Gadiel Michael, Daud Raphael na Obrey Chirwa ambaye alikosa.

Mvua Yaleta Maafa Yaua Watoto Wawili Chato

$
0
0

Mvua Yaleta Maafa Yaua Watoto Wawili Chato
Mvua kubwa iliyonyesha katika kijiji cha Mwekako kata ya Kasenga wilayani Chato mkoani Geita imesababisha vifo vya watoto wawili na kuharibu mali.

Diwani wa Kata ya Kasenga, Damian Vilarie amethibitisha kutokea kwa vifo hivyo na kusema mvua imesababisha uharibufu wa miundombinu ya barabara.

Amesema mvua hiyo iliyonyesha kwa saa tatu jana Alhamisi Januari 11 ilisababisha mafuriko yaliyowasomba watoto wawili wa mzee Kurwa waliotoka soko la Igalula kununua bidhaa za nyumbani.

Amesema watoto hao mmoja anakadiriwa kuwa na miaka 13 na mdogo miaka mawili.


Dalali wa Nyumba ya Diamond: “Diamond Anamiliki Nyumba 29 Hii Ndiyo Nyumba ya Gharama Sana”

$
0
0
Dalali wa Nyumba ya Diamond: “Diamond Anamiliki Nyumba 29 Hii Ndiyo Nyumba ya Gharama Sana”
Dalali Skoba ambaye amemtafutia Diamond Platnumz mjengo ambao amenunua amezungumza na kusema kuwa Diamond anamiliki nyumba 29 na kati ya nyumba hizo hii ndiyo nyumba yenye gharama kubwa zaidi aliyoitaja kuwa ni Billion moja na kusema kwamba swala la nyumba ni kitu cha kawaida kwa Diamond kumiliki.

Dalali huyo amesema kuwa hakuna staa mwingine aliowahi kumuuzia nyumba ya gharama kama hiyo kwani mastaa wengi anawauzia viwanja na nyumba za kupangisha lakini siyo za kununua na anaamini huwenda Dimaond akawa anashikilia record hiyo kwa wasanii..



Miujiza ya Sharifu Seif Mohamed..JE Umeachwa na Mme/Mke au Mpenzi, Umesongwa na Mitihani ya Maisha..Piga Simu Upate Muujiza Wako

$
0
0
SHARIFU SEIF MOHAMED ANAWASHUKURU WALE WOTE WANAOENDELEA KUPIGA SIMU, WENYE MATATIZO NA WALE WANAOTOA  SHUKRANI NA SHUHUDA JINSI TIBA ZAKE ZINAVYO WASAIDIA,

(Rudisha mahusiano yako ndani ya masaa 72 tu)

SHARIFU MOHAMED Ni  mtaalam na mnajimu maarufu wa nyota na kubashiri mambo yanayo watesa binadamu duniani kote na kupata ufumbuzi, Anatumia kitabu cha QUR'AN, Dawa za Asili, Dawa za Kiarabu na majini kwa kumtuliza mke/mme, mchumba au mpenzi ndani ya masaa 72 tu, na kutatua matatizo yote ya kimaisha,

Je Umeachwa na UMPENDAE awe Mme/Mke na bado unampenda? Je Umekimbiwa na Mmeo/ Mkeo n anaishi na mtu mwingine? Je Umejaribu sehemu nyingi bila mafanikio? Mpigie simu SHARIFU SEIF sasa hivi ujionee Muujiza wa Papo kwa Papo, Anauwezo wa hali ya juu wa kusambaratisha mahusiano yao na kumrejesha kwako haraka sana na Kumfanya Atimize Ahadi zote Ndani ya Muda Mfupi Endapo Utafwata Atakacho Kuelekeza

ANAZO DAWA ZA MAPENZI, NGUVU ZA KIUME, CHANGO NGIRI MAJI NA N.K, ZINDIKO LA NYUMBA NA BIASHARA, PETE ZA BAHATI, HUMALIZA KABISA TATIZO LA NGUVU ZA KIUME NA KUREFUSHA UUME KWA SAIZI UNAYOTAKA, HUZUIA CHUMA ULETE KWENYE BIASHARA, HURUDISHA MALI ZILIZOPOTEA, MAGONJWA SUGU, MIGUU KUWAKA MOTO AU KUFA GANZI, HUTIBU BUSHA BILA KUPASUA, ANAO UWEZO WA KUMRUDISHA ALIE MBALI AU ALIECHUKULIWA MSUKULE, KUPANDISHA NYOTA NA KUSHINDA BAHATI NA SIBU, KASAFISHA NYOTA NA KUKUPA MVUTO WA AJABU, KUTOA NUKSI NA VIFUNGO MBALIMBALI,  MAFANIKIO YA MAISHA NA UTAJIRI BILA MASHARI, NA MENGINE MENGI YA SIRI,

Je UMAHANGAIKA KUPATA MTOTO BILA MAFANIKIO? WASILIANA NA MTAALAMU HUYU KWANI YEYE HUFAULU PALE WOTE WALIPOSHINDWA, PIA UMALIZA KAZI ZILIZO SHINDIKANA NA WATAALAM WENGINE NDANI YA MASAA 24 TU,

(NA ANATIBU KWA NJIA YA SIMU UKIWA NCHI YOYOTE AU MKOA WOWOTE ENDAPO UTAFWATA MAELEKEZO YAKE)

Kwa ushauri na mawasiliano  zaidi Piga SIMU No:

Mobile +255 654-836970
WhatsApp +255 756-033670

Nani Anafaa Kupeperusha Bendera ya Chadema 2020?

$
0
0
LOWASSA ALIWASALITI WENZAKE.

Na Thadei Ole Mushi.

Maana halisi ya chama cha siasa ni kikundi cha watu wenye nia moja na Lengo moja la kushika madaraka ya nchi.

Hii maana imekuwapo karne na karne na ndio msingi na lengo kuu la kuundwa kwa vyama vya siasa.

Hakuna chama cha Siasa duniani ambacho kiliundwa na hakitambui lengo hili kama lengo la msingi

LOWASSA HAFAI TENA KUWA MGOMBEA URAIS KUPITIA UPINZANI.

Huu ni ukweli ulio uchi kuwa kwa kitendo cha Lowassa kujitokeza hadharani na kusifia serikali ya awamu ya Tano moja kwa moja inamvua sifa ya kupeperusha bendera ya Chadema kwenye uchaguzi mkuu

Kitendo alichokifanya hakina Tofauti na wabunge au madiwani walioamua kujivua nafasi zao na kujiunga ccm kwa kisingizio cha kuunga mkono juhudi za Rais Magufuli.



Lowassa amesema kuwa Rais kafanya mazuri sana katika uongozi wake moja kwa moja kaunga Mkono juhudi za Rais Magufuli sasa huyu unamtofautishaje na Dr Molel? Au kina Mtulia?

Lowassa atapata wapi tena ujasiri wa Kusimama jukwaani na kusema achaguliwe huku yote yaliyofanywa amekubaliana nayo? Litakuwa ni kosa la Kiufundi kweli kama chadema itamchagua tena Lowassa kuwa mgombea Urais 2020.

Huu ni usaliti katika dhana ya maana ya chama cha Siasa kama nilivyoielezea hapo mwanzo.

NINI KINAWEZA KUFANYIKA.
Kwa sasa Chadema inatakiwa ianze kuoiga mahesabu mapya ya nani anauzika kwa wananchi. Kwa upande wao wafikirie majina haya mawili.

1. Fredrick Sumaye.

2. Tundu lisu.

SUMAYE.
Huyu anafaa kwa sifa moja tu kubwa kwamba aliwahi kushika nafasi kubwa ya kiuongoz nchini lakini hakuwahi kuwa mwanasiasa mkubwa.

Kuna tofauti kati ya kuwa mwanasiasa mkubwa na Kiongozi mkubwa. Hii ina maana kuwa Sumaye alidondokewa na bahati ya kupitishwa kuwa waziri mkuu na sio kwamba alikuwa na ushawishi kwa jamii kuipata nafasi hiyo aliyodumu nayo kwa miaka 10.

HASARA YA SUMAYE.
Sumaye kama alivyo Lowassa ni mtu mwenye makando kando mengi. Kama ilivyo kwa viongozi wengi hasa kujilimbikizia Mali.
Sumaye naye amekuwa akitajwa tajwa kama ataanza kujiandaa kwa ajili ya kushika form ya urais basi CCM wanajua pa kugusa ili atulie. Na wakipagusa sana anaweza akahamia kabisa CCM kulinda asife maskini. Huu ndio ukweli wenyewe......
Hawa kina Lowassa wanalinda tu mali zao kwa sasa hawana ubavu tena wa kuzungumza lugha ya kuiondoa ccm madarakan.

LISU.

Huyu pamoja na kuwa ni msomi mzuri, ni mwanaharakati na ni mpinzani haswa haswa. Kwa sifa hizo anatosha sana kupeperusha bendera za Chadema Kwa sasa.

Huyu hakuwahi kushika nafasi kubwa za kiuongozi ila ni mwanasiasa mkubwa sana kwenye ukanda huu wa Africa Mashariki.. angelikuwa CCM huyu ni dhahiri angeliteuliwa kushika nafasi kubwa kabisa za Kiuongozi.

Narudia kama tunataka kuona kampeni zenye mvuto 2020 Lisu ndio chaguo pekee la Chadema. Wakimsimamisha huyu atatusumbua sana CCM.

HASARA YA LISU.
Kipingamizi kikubwa cha Lisu kwa sasa ni Afya yake. Lisu anatakiwa kwa sasa apiganie zaidi Afya yake kuliko kitu kingine kile.
Kipingamizi cha pili cha lisu hana agenda ya msingi ya Kiuchumi ya kumpeleka Ikulu zaidi ya kuwa mkosoaji mkubwa. Lisu anapaswa sasa kuanza kuonyesha Plan B zake katika maswala ya kitaifa yaani kama jambo limefeli yeye kama yeye angelifanyaje.
Naamini na ndivyo ilivyo kiongozi mzuri ni yule mwenye maono yake juu ya mambo flan yaani mawazo yake binafsi na sio ya kuandikiwa (Ilani) na ndio maana hata Rais wetu kuna saa anaweka ilani Pembeni na kunyoosha kwa namna anavyoamini yeye.

Lisu anatakiwa sasa atuonyeshe nje ya Ukosoaji wake nini plan na Dira yake kwa taifa hili.


By Ole Mushi/JF

0712702602


Mume wa Shilole Uchebe Aendelea Kuaibisha Wanaume wa Dar....Atoa Mpya na Kuonyesha Kuwa Analelewa na Shilole

$
0
0
Wanaume wa Dar Mnalalamika watu wanawaonea oneni sasa nini hiki!? Kweli kidume anamwambia mkewe ahustle kwa bidii ili wasije kosa hela!? You hoes ain't loyal kabisa!

Oneni akili za wanaume wa Dar!

Hashimu Rungwe Naye Ataka Kutinga Ikulu ili Kumpa Rais ya Moyoni

$
0
0
Mwenyekiti Chama cha Chaumma, Hashim Rungwe amesema anatamani kwenda Ikulu kuonana na Rais John Magufuli ili kumweleza mambo ambayo yatawezesha kusaidia kuleta mabadiliko katika utawala wake.

Akizungumza na Mwananchi leo Ijumaa Januari 12, 2018, Rungwe amesema kila mtu anatamani kuonana na Rais Magufuli lakini nafasi hiyo imekuwa haipatikani.

Rungwe anatoa kauli hiyo ikiwa imepita siku tatu tangu waziri mkuu wa zamani, Edward Lowassa alipofanya ziara Ikulu na kuzungumza na Rais Magufuli.

“Hata mimi nataka kuonana na Rais, nimekuwa natamani sana lakini hatupati nafasi hiyo, nikikutana naye tutazungumza mambo mengi, ambayo yatamsaidia yeye mwenyewe katika uongozi wake,” amesema Rungwe na kuongeza;

“Sisi upinzani tulikuwa tunasema hatutaki mafisadi, hatutaki wabidhirifu au tunapiga kelele dawa hakuna hospitalini kwa hiyo anapopeleka dawa hospitalini ni sisi tumesaidia, kwa hiyo kuongoza ni kusikiliza watu wanasema nini wakati mwingine.”

Mwananchi lilipotaka kujua hasa ni kitu gani ambacho anataka kumweleza Rais Magufuli, Rungwe amesema “hiyo ni siri yangu, lakini tumekuwa tikitafuta nafasi hiyo lakini wapi, lakini naona Lowassa kaenda na wamezungumza.”

Chanzo: Mwananchi

Je Una Upungufu wa Nguvu za Kiume, Hamu ya Tendo la Ndoa au Maumbile Madogo ya Uume?

$
0
0
JE, UNA UPUNGUVU WA NGUVU ZA KIUME, HAMU YA TENDO LA NDOA AU MAUMBILE MADOGO YA UUME?

SOMA HAPA 
Tatizo la upungufu wa nguvu za kiume au ukosefu wa hamu ya tendo la ndoa limezidi kuongezeka kwa kasi duniani kote na limekuwa chanzo kikubwa cha ndoa nyingi na mahusiano kukosa uaminifu kutokana na wengi kutoka nje ya ndoa ili kupata mtu atakayemtosheleza na kumfikisha kileleni. Pia udogo wa maumbile ni tatizo kubwa na limekuwa likiwakosesha wanaume wengi uwezo wa kujiamini katika tendo na kusababisha tendo hilo kutokufanyika kwa usahihi. Hili pia huchangia kwa kiasi kikubwa wanawake wengi kwenda nje ya ndoa ( MAHUSIANO) kutafuta mbadala wake.
BAADHI YA DALILI ZA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME NI KAMA:-
☆Kukosa hamu ya tendo la ndoa
☆Uume kusimama kwa ulegevu
☆Kuwahi kufika kileleni
☆Uume kusinyaa katikati ya tendo
☆Kushindwa kurudia tendo kwa wakati
☆Kuchoka sana baada ya round ya kwanza na hata kukinai kabisa.

Kwa kutumia mimea na matunda bila kemikali   @markson_beauty_pr Tunakuletea suluhisho la matatizo hayo hata kwa wenye "KISUKARI NA PRESSURE" kwa:-

1.HANDSOME UP ORIGINAL:- kifaa chenye uwezo wa 99% kuongeza uume kwa size uipendayo na kuimarisha misuli ya uume iliyolegea @250,000/=
2.SHARK POWER ni gely ya kupaka inayoongeza uume kwa wastani wa inch 5.5 hadi 6 @150,000/=
3.VigRX CREAM:- ni gely iliyoboreshwa mahususi kwa ajili ya kuongeza maumbile kwa wastani wa inch 6.5 hadi 8 na kuimarisha misuli ya uume iliyolegea @200,000/=
4.Vidonge maalum kwa ajili ya kuongeza nguvu na hamu ya tendo la ndoa hata kwa wenye kisukari @150,000/=
5.Spray ya kuchelewesha kufika kileleni na kuweza kurudia tendo ×3. @150,000/=
BIDHAA HIZI HAZINA MADHARA KIAFYA NA ZIMETHIBITISHWA
NA SHIRIKA LA AFYA DUNIANI (WHO).
KWA BIDHAA HIZI NA NYINGINE NYINGI TEMBELEA UKURASA WETU WA INSTAGRAM :-
@markson_beauty_pr

WEB:www.markbeauty.org
Wasiliana nasi Popote
ulipo duniani kwa
(+255)0767447444 na
0714335378

UTAPATA HUDUMA
NB:Matokeo ni uhakika na garantii na hakikisha unapata risiti yenye muhuri halisi wa MARKSON CO pamoja na garantii ili kukuhakikishia kufanikiwa kwako.

Edward Lowassa Ana Hekima Sana, Hapa Nimemuelewa Vizuri

$
0
0
Huenda hujawahi kumsikiliza Mheshimiwa Edward Lowassa akielezea issue yake ya Richmond. Hebu msikilize hapa vizuri naamini utamuelewa vizuri na utakuwa huna swali la nyongeza.

VIDEO:

Nandy na Ruby Wamaliza Bifu lao?

$
0
0
KUTOKANA na madai ya hapa na pale kwamba wasanii wa Bongo Fleva, Faustina Charles ‘Nandy’ na msanii mwenzake, Hellen George ‘Ruby’ wana bifu zito, hatimaye bifu hilo linadaiwa kuzimwa baada ya Ruby kuonekana akiimba nyimbo za Nandy.

Siku chache zilizopita, Ruby alionekana akiwa kwenye ‘interview’ ya kituo kimoja cha redio akiimba Wimbo wa Kivuruge ya Nandy, kisha baada ya muda Nandy akaposti kwenye ukurasa wake wa Instagram na kumsifu kwa uimbaji wake, jambo lililozua gumzo na kudhihirisha kuwa sasa hakuna tofauti baina yao.

Kutokana na ishu hiyo, Ruby alipotafutwa simu yake haikuwa hewani, kwa upande wake Nandy alisema; “Nimefurahi mno Ruby kuimba wimbo wangu, anajua, ujue sisi hatujawahi kuwa na bifu hayo yanazushwa na mashabiki, tarajieni kuona makubwa huko mbeleni, sababu tunafanya kazi sehemu moja hata tukiamua kufanya kolabo kama mashabiki wanavyotushauri ni sekunde tu, ila suala hilo siwezi kuliongelea sana kwa sasa

Wasichana Wanaopata Hedhi Wapigwa Marufuku Kuvuka Mto

$
0
0
Wasichana Wanaopata Hedhi Wapigwa Marufuku Kuvuka Mto
Wasichana katika eneo moja nchini Ghana wamepigwa marufuku kuvuka mto mmoja wanapopata hedhi, na pia kuuvuka mto huo Jumanne.

Marufuku hiyo, ambayo inadaiwa kutolewa na miungu wa mto wa eneo hilo imeshutumiwa sana na wanaharakati watetezi wa haki za watoto.

Hii ni kwa sababu wasichana wengi hulazimika kuvuka mto huo kufika shuleni.

Hii ina maana kwamba wasichana wa wilaya ya Denkyira ya Juu Mashariki, katika mkoa wa kati, wanakabiliwa na hatari ya kutopata elimu.

Mataifa mengi Afrika kusini mwa jangwa la Sahara yamekuwa wakikabiliwa na changamoto ya kuhakikisha wanafunzi wa kike wanasalia shuleni wakati wanapopata hedhi.

Shirika la Umoja wa Mataifa kuhusu Sayansi na Elimu, Unesco, linakadiria kwamba asilimia kumi ya wasichana Afrika kusini mwa jangwa la Sahara huwa hawahudhurii masomo shuleni wanapopata hedhi.

Ripoti moja ya Benki ya Dunia inasema wanawake 11.5 milioni nchini Ghana hukosa huduma na vifaa vya usafi.

Balozi wa usafi wakati wa heshi wa Unicef Shamima Muslim Alhassan ameambia BBC Pidgin kwamba amri hiyo kuhusu sehemu ya Mto Ofin inakiuka haki ya wasichana kupata elimu.

"Inaonekana miungu hawa wana nguvu sana, si ni kweli?" alisema.

"Wakati mwingine huwa nafikiri tunafaa kuomba uwajibikaji kiasi kutoka kwa miungu hawa wanaoendelea kuzuia mambo mengi yasifanyike, wawajibishwe kuhusu jinsi wanavyotumia mamlaka haya makubwa ambayo tumewapa."

Waziri wa mkoa wa kati Kwamena Duncan ametoa ishara kwamba atashirikiana na mwenzake wa mkoa wa Ashanti kutafuta suluhu.

Mto wa Ofin ndio mpaka kati ya mikoa ya Ashanti na Kati.

Katika jamii nyingi huwa kuna itikadi nyingi na miiko kuhusu hedhi.

Nchini Madagascar, baadhi ya wanawake hutakiwa kutooga wanapopata hedhi na Nepal wengine hulazimika kulala katika vyumba maalum mbali na familia.

Nguza na Wanaye Watinga Katika Sherehe za Mapinduzi ya Zanzibar

$
0
0
Nguza na Wanaye Watinga Katika Sherehe za Mapinduzi ya Zanzibar
Familia ya mwanamuziki  Nguza Vicking 'Babu Seya' leo Ijumaa imeungana na Wazanzibari kwa ajili ya kusherehekea maadhimisho ya miaka 54 ya Mapinduzi ya Zanzibar.

Maadhimisho hayo yaliyafanyika leo Ijumaa katika Uwanja wa Amaan Zanzibar yakihudhuriwa na viongozi mbalimbali wa kitaifa akiwamo Rais wa Zanzibar, Dk Ali Mohamed Shein.

Tayari Serikali imewatafutia studio ya kurekodi muziki familia familia hiyo baada ya kuonana na Rais John  Magufuli  Ikulu waliopokwenda kutoa shukurani.

Mmoja mtoto wa Babu Seya, Michael Nguza maarufu kama Nabii Nguza aliliambia Mwananchi kuwa lengo la kwenda Zanzibar ni kusherekea maadhimisho ya mapinduzi hayo.

“Tumekuja kusherehekea  sikukuu ya Mapinduzi ya Zanzibar,” amesema Nabii Nguza.

Babu Seya na wanawe Johnson Nguza ‘ Papii Kocha na Nabii Nguza wameanza kuonekana hadharani mfululizo ikiwa ni baada ya kuonana na Rais Magufuli walikokwenda kutoa shukurani baada ya kuachiwa huru Desemba 9 mwaka jana.

Baada ya kuonana na Rais Magufuli siku zilizofuata wakiwa na , Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni,  Sanaa na Michezo, Juliana Shonza walikwenda  katika Studio  za Wanene zilizopo Mwenge  kwa ajili ya mchakato wa kuanza kufanya kazi zao.

Rais wa TFF Ameteuliwa Kufungua Fainali za AFCON 2018

$
0
0
Rais wa TFF Ameteuliwa Kufungua Fainali za AFCON 2018
Pamoja na Tanzania kutolewa na Rwanda kwenye michuano ya kuwania kufuzu fainali za AFCON 2018 kwa wachezaji wa ndani (CHAN), lakini Rais wa TFF ameteuliwa kufungua michuano hiyo.


Shirikisho la Soka Barani Afrika CAF limemteua Rais wa shirikisho la soka nchini TFF Wallace Karia kuwa kamishna wa mechi ya ufunguzi wa fainali za ndani (CHAN) kati ya wenyeji Morocco dhidi ya Mauritania itakayochezwa kesho Januari 13.

Michuano hiyo ambayo inafanyika kwa mara ya tano tangu ianzishwe, inatarajiwa kuanza kesho ikishirikisha nchi 16 na itamalizika Februari 4, 2018 nchini Morocco.

Kabla ya Morocco kupewa uenyeji wa michuano hiyo awali ilikuwa ifanyike nchini Kenya ambapo shirikisho la soka Afrika CAF lilibadilisha kutokana na Kenya kushindwa kumaliza maandalizi ndani ya wakati.

Tanzania iliondolewa na Rwanda kwenye hatua ya kuwania kufuzu baada ya kutoka sare kwenye mchezo wa kwanza uliochezwa CCM Kirumba kabla ya kushinda mchezo wa pili uliopigwa nchini Rwanda.

Mzee Yusuph Ataka Wenye Nyimbo Zake za Taarabu Wazifute

$
0
0
Mzee Yusuph Ataka Wenye Nyimbo Zake za Taarabu Wazifute
Aliyekuwa mwimbaji na Mkurugenzi wa bendi ya Jahazi Modern Taarab, Mzee Yusuf amefunguka na kutilia mkazo na kuwaomba watu hususani wanawake ambao bado wana nyimbo zake za Taarab kwenye simu wazifute ili iwe kheri zaidi kwenye imani yake na dini yake


Mzee Yusuf alisema hayo alipokwenda Babati mkoani Manyara katika harakati ya kuzidi kukutana na watu na kuwaomba wazifute nyimbo zake hizo za Taarab kwa kuwa anaamini zinakwenda kinyume na imani yake.

"Niko Babati kuzidi kuwaomba Waislam wanifanyie 'Ihsaan' ya kuzidi kuniombea dua na kuzifuta nyimbo zangu kwenye simu zao kwa ajili ya dini ya 'Allah' iwe kheri na salama. Wengine nyinyi mpaka sasa simu zenu bado zinabalaa naombeni mzifute kwa ajili ya 'Allah' naona haya simu zikipigwa zikaita hizo nyimbo kwani najisikia vibaya sijui nifanyaje" alisema Mzee Yusuf

Aidha Mzee Yusuf alisema kuwa kwa sasa anaogopa na kuwataka wale ambao wanasema wamemkumbuka kwenye masuala ya uimbaji wa nyimbo za Taarabu waache kumkumbuka kwenye mambo hayo bali wamsaidie kwa kuzifuta nyimbo hizo. Mbali na hilo Mzee amewaomba watu wa vyombo vya habari na kwenye mitandao ya kijamii kufuta kazi zake zote hizo kwa ajili ya hisani ya 'Allah'

Tanesco Yawawashia Taa Nyekundu Wadaiwa Sugu Watoa Siku 4 Kulipa Deni

$
0
0
Tanesco Yawawashia Taa Nyekundu Wadaiwa Sugu
Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO), limetoa siku 4 kwa wateja wao wote wale wadaiwa sugu kuanzia tarehe 12 Januari mwaka huu hadi Januari 15, mwaka huu wawe wamelipa madeni yao.



SHIRIKA LA UMEME TANZANIA (TANESCO) TAARIFA KWA UMMA – WADAIWA SUGU

Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) tunautaarifu Umma na Wateja wetu wote kuwa, tumetoa muda wa siku nne (4) kuanzia Januari 12, 2018 hadi siku ya Jumatatu Januari 15, 2018 kwa wadaiwa sugu wawe wamelipa madeni yao.

Baada ya muda huo kuisha Shirika litasitisha Huduma ya umeme dhidi ya Wateja watakaoshindwa kulipa madeni ikiwa ni pamoja na kuchukua hatua zingine za kisheria.

Ofisi za TANESCO zitakuwa wazi siku ya Jumamosi Saa 3:00 Asubuhi hadi Saa 9:00 Mchana.

Mawasiliano

Kituo cha miito ya simu Makao Makuu +255 222 194 400 na +255 768 985 100

Mitandao ya kijamii

Twitter, www.twitter.com/tanescoyetu,

Facebook https://www.facebook.com/tanescoyetultd/

IMETOLEWA NA: OFISI YA UHUSIANO

TANESCO MAKAO MAKUU
Viewing all 104762 articles
Browse latest View live




Latest Images