Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104702 articles
Browse latest View live

Wema Sepetu Akana Penzi la Mahombi Asema ni Shemeji Tu

$
0
0
Wema Sepetu Akana Penzi la Mahombi Asema ni Shemeji Tu
STAA mwenye nyota kali Bongo, Wema Sepetu amefungukia madai ya kubanjuka kimapenzi na mwanamuziki mwenye asili ya Congo, Mohombi Nzasi Moupondo na kusema kuwa ni shemeji yake na si vinginevyo.

Akizungumza na Risasi Jumamosi Wema alisema kuwa, watu waache kutabiri vitu bila kujua ukweli wenyewe, kwani alipiga picha na mwanamuziki huyo kama shemeji yake kwa rafiki yake.

“Hivi kwa nini watu ni wepesi wa kuongea mambo? Mohombi ni shemeji yangu, kama watu wanataka kumjua mpenzi wangu watamjua hivi karibuni tu, kwani nimejipanga kumuanika ‘soon’ hivyo waache kuotea,” alisema Wema.

Aika na Nahreel Waachia Sura ya Mtoto Wao

$
0
0
 Aika na Nahreel Waachia Sura ya Mtoto Wao
Baada ya Familia ya Noel Mkono maarufu kama Aika na Nahreel kubahatika kupata mtoto mwishoni mwa mwaka jana hawakuwahi kupost picha yoyote ya mtoto wao inayoonesha sura yake mpaka siku ya leo January 12, 2018 ambapo kupitia ukurasa wa Instagram wa Nahreel na Navykenzo wameweka picha ya mtoto wao na kuonesha Sura yake.

Mtoto wa Aika na Nahreel ambaye amepewa jina la Gold ameonekana kwenye picha akiwa amevaa cheni ya Gold kama lilivyo jina lake..




Hiki Hapa Alichokisema Manara Juu ya Mziki wa Aslay

$
0
0
Hiki Hapa Alichokisema Manara Juu ya Mziki wa Aslay
Msemaji wa club ya Simba Haji Manara ni mshabiki mkubwa wa muziki wa Bongofleva na mara nyingi utakuta akitoa maoni yake mbalimbali akizungumzia muziki wa bongofleva na wasanii wenyewe.

Leo January 12 2018 ameandika na kuonyesha kuwa yeye ni miongoni mwa watu wanaoamini kuwa muimbaji wa Bongofleva Aslay hapewi heshima anayostahili lakini ana uwezo mkubwa na anacho kipaji na ameandika kupitia instagram account yake.



“Sijawahi kuwa na mashaka juu ya uwezo wako,najua nchi inawataja sana wengine,bt nnapokusikiliza naona hujapewa heshma unayostahili…you are a Real Super Duper Star @aslayisihaka 👏👏“>>>Manara

Baada ya Kuonyesha Mjengo wa Tv, Radio Sasa Diamond Aweka Picha ya Mnara wa Radio ya WCB

$
0
0
Baada ya Kuonyesha Mnara wa Tv, Radio Sasa Diamond Aweka Picha ya Mnara wa Radio ya WCB
Baada ya kutuonesha mjengo mpya ambapo ndio zitakuwa ofisi za radio ya Wasafi FM na Wasafi Tv  sasa CEO wa WCB Diamond Platnumz  leo January 12, 2018 amepost picha inayomuonesha yuko na Harmonize huku nyuma yao kukiwa na mnara mrefu ambao inawezekana ukawa ndiyo mnara wa radio tuliyo ahidiwa..

Diamond amepost picha hiyo na kuandika Caption iliyosomeka…“What a Busy Day #Mnarani…. InshaAllah Mwenyez Mungu atujaalie sisi Pamoja nawe Mwaka 2018 Uwe Mwaka Mwema na Wamafanikio…Tuseme “Ameen”🙏 Cc @harmonize_tz” – Diamond

Mama Aliyeingizwa Mkenge na Mchungaji Nyumba Yake Yapigwa Mnada

$
0
0
Mama Aliyeingizwa Mkenge na Mchungaji Nyumba Yake Yapigwa Mnada
Mama mmoja ambaye ni mkazi wa Kunduchi Beach jijini Dar es salaam Mtaa wa Kondo Ijumaa hii amejikuta katika wakati mgumu baada ya nyumba yake iliyopo mtaa huo plot No.239 Block B, kupigwa mnada ‘kimagumashi’ na kampuni ya udalali inayojitambulisha kwa jina la Nkaya Company Limited yenye makazi yake Namanga Kinondoni jijini Dar es salaam.


Akiongea na waandishi wa habari mama huyo aliyejitambulisha kwa jina la Zainabu J Kaswaka muda mfupi baada ya mnada huo, alisema tayari nyumba hiyo ilikuwa na zuio la mahakama mpaka pale kesi ya msingi itakapozungumza juu ya nyumba hiyo na deni analodaiwa mama huyo na benki moja kubwa nchini.

“Naomba msaada wa serikali kwenye hili sakata, hii kampuni ya udalali imekuja kuuza nyumba yangu wakati kuna zuio la mahakama, mwaka jana wakati wanataka kuuza nyumba yangu nilienda mahakamani na nikapewa zuio mpaka kesi ya msingi isikilizwe, nashangaa hawa wamekuja bila kutoa taarifa yoyote, hata kwa mwenyekiti hawakufika, wamekuja na mtu wao ambaye wanadai ni mnunuzi, wameuza nyumba yangu kwa milioni 200 wakati wao wanadai bilioni 1.6 kitu ambacho hakiwezekani,” alisema mama huyo.

Naye mwenyekiti wa mtaa huyo, Hamis Haule amesema ni kweli amesikia kuna kampuni ya udalali ya Nkaya ilifika mtaani kwake na kupiga mnada nyumba ya mama huyo bila taarifa yake.

“Hata mimi nimesikia hiyo habari na kwa kifupi siutambui huo mnada kwa sababu hawajanishirikisha, mimi nilitakiwa kuwepo katika mnada, na hii barua ambayo inadaiwa imesainiwa na mimi siitambui hata kidogo, hao watu wamefoji muhuri wangu pamoja na saini lakini hawajapita kwangu kabisa,” alisema Haule.

Baada ya sakata hilo, Bongo5 ilimtafuta Mkurugenzi wa kampuni ya udalali inayojitambulisha kwa jina la Nkaya Company Limited, Hassan Magogo na kuzungumza naye kuhusu sakata hilo.

“Ndugu mwandishi sisi tunafanya kazi kwa kufuata taratibu na sheria, sisi tumepewa kazi na KCB na tumeifanya kama tulivyoambiwa, ni kweli hiyo nyumba niliwa na zuio la mahakama lakini lilishapita, na kabla ya huu mnada tumetangaza kwenye gazeti kwamba kutakuwa na mnada wa nyumba baada ya siku 21, na leo ni siku ya mnada tumefanya mnada na nyumba imeuzwa. Lakini pia hawajaambiwa wahame leo, notisi waliyopewa ni ya siku 30, ndani ya kipindi hicho wanaweza kufanya chochote kama wanaona wameonewa na baada ya hapo watahamishwa,” alisema Mkurugenzi Magogo.

Airtel Yamjibu Waziri wa Fedha Sakata la Ubinafsishaji wa TTCL

$
0
0
Airtel Yamjibu Waziri wa Fedha Sakata la Ubinafsishaji wa TTCL
Kampuni ya Bharti Airtel inayomiliki kampuni ya Airtel Tanzania, imeeleza kusikitishwa kwake na taarifa ya kamati iliyoundwa kuchunguza umiliki wake iliyotolewa na Waziri wa Fedha na Mipango, Dk Philip Mpango juzi.

Taarifa ya Bharti iliyotolewa jana imeeleza kuwa uwekezaji wake ulifuata na kuzingatia sheria na taratibu zote za nchi kabla ya baraka za Serikali ya Tanzania.

Juzi, Waziri Mpango aliwasilisha kwa Rais John Magufuli taarifa ya kamati iliyoundwa kuchunguza umiliki wa kampuni ya simu ya Airtel na kueleza jinsi sheria na taratibu zilivyokiukwa katika ubinafsishaji wake.

Kutokana na ukiukwaji huo, Dk Mpango alisema Serikali inayomiliki asilimia 40 ya hisa za kampuni ya Airtel imeamua kufanya mazungumzo na kampuni ya Airtel inayomiliki asilimia 60 ya hisa ili nchi iweze kupata haki yake.

“Lakini niwaambie Watanzania yale ambayo tumeyaona ni machafu sana, ni mambo ya hovyo kabisa, nchi yetu kwa kifupi tuliingizwa mkenge, ni fedha nyingi zimepotea kwa hiyo sisi katika majadiliano haya lengo letu litakuwa ni kuhakikisha Watanzania wanapata haki yao” alisema. Waziri Mpango aliunda kamati hiyo ikiwa ni utekelezaji wa agizo la Rais Magufuli la Desemba 20 mwaka jana wakati akiweka jiwe la msingi katika jengo la Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) mjini Dodoma.

Lakini katika taarifa yake ya jana, Bharti imeonyesha mlolongo wa miamala na matukio kadhaa wakati wa ubinafsishaji ikidai kuwa hiyo inaweza ikaonyesha uwazi uliokuwapo.

Mchakato huo ni ule wa kuanzia kutafutwa kwa mwekezaji ndani ya TTCL kwa ajili huduma za simu za mkononi mwaka 2001 hadi uuzwaji wa Zain kwenda Airtel.

Taarifa hiyo inaeleza kuwa katika kila hatua, Serikali ilikuwa ikishirikishwa na kulikuwa na uwazi mkubwa na matakwa yote ya kisheria yalikuwa yakifuatwa.

“Miamala yote ilikuwa ikifanyika chini ya usimamizi wa bodi ya wanahisa wa MSI, wawakilishi wa Benki ya Dunia, Serikali ya Uingereza, Marekani, Uholanzi na Ujerumani. Makundi hayo ya watu yalishirikishwa ili kuhakikisha maadili na misingi ya utawala bora katika kampuni,” inaeleza taarifa hiyo.

Imemuomba Waziri Mpango kuipatia matokeo ya kamati hiyo kuhusiana na ubinafsishaji wake ili kama kuna hoja zozote iweze kuzijibu kwa hoja kutokana na kumbukumbu za kampuni.



Serikali ya Botswana Yamshutumu Trump kwa Kutusi Nchi za Afrika

$
0
0
Serikali ya Botswana Yamshutumu Trump kwa Kutusi Nchi za Afrika
Serikali ya Botswana imemshutumu Rais wa Marekani kwa kusema mataifa ya Afrika ni "machafu" na kusema tamko lake rais huyo ni la kukosa kuwajibika, la kukera na "ubaguzi wa rangi".

Bw Trump alisema hayo alipokuwa akizungumzia sera ya uhamiaji ya Marekani, ambapo alisema anafikiti watu kutoka Haiti, El Salvador na nchi za Afrika hawafai kuruhusiwa kuingia kama wahamiaji Marekani.

Botswana imesema kupitia taarifa kwamba imemwita balozi wa Marekani nchini humo kufafanua iwapo Marekani inachukulia taifa hilo la kusini mwa Afrika kama "taifa chafu" na taifa la mabwege.

Taarifa hiyo ya Botswana imesema tamko la Trump ni la kukosea heshima taifa ambalo lina urafiki wa kufana na uhusiano wa kibalozi.

Botswana imeitaka jumuiya ya kiuchumi ya nchi za kusini mwa Afrika Sadc pamoja na Umoja wa Afrika kushutumu tamko hilo la Trump.

Bw Trump kwenye Twitter hata hivyo amejitetea na kusema hakutumia maneno hayo, lakini akasema aliyoyasema yalikuwa na "lugha kali".

Msemaji wa Umoja wa Mataifa amesema tamko hilo la Trump ni la kushangaza, la aibu na la ubaguzi wa rangi.

Rupert Colville amesema: "Iwapo yatathibitishwa, matamshi haya ni ya kushangaza na ya aibu sana kutoka wka rais wa Marekani, nasikitika kwamba hakuna maneno mengine ya kueleza hili ila kusema kwamba ni ubaguzi wa rangi.

Bw Colville amezungumzia hotuba ya Trump wakati wa kampeni 2016 ambapo alisema wahamiaji kutoka Mexico ni wahalifu na wabakaji.

Na pia, amerejelea tamko lake akijibu maandamano ya waandamanaji watetezi wa ubabe wa Wazungu mwaka jana yaliyokumbwa na vurugu Charlottesville, Virginia walipokabiliana na waandamanaji waliokuwa wanawapinga.

Trump wakati huo alisema "pande zote" zilifaa kulaumiwa.

Afisa huyo wa UN amesema tamko hilo la Trump linaenda "kinyume na maadili ambayo ulimwengu umekuwa ukiazimia kufikia" tangu mwisho wa Vita Vikuu vya Pili vya Dunia, na kufungua "mlango wa kuonyesha ukatili zaidi wa binadamu".


Waandamanaji wanaopinga chuki ya rais Donald Trump dhidi ya wahamiaji
Image caption
Waandamanaji wanaopinga chuki ya rais Donald Trump dhidi ya wahamiaji
Alisema: ''Kwa nini tunawaruhusu watu hawa kutoka mataifa 'machafu'"?

Tamko hilo lilidaiwa kuwalenga watu kutoka Afrika, Haiti na El Salvador.

Picha tano za kusisimua mkutano wa Trump na Obama
Trump akataa Air Force One mpya
Ikulu ya Whitehouse haikukana tamko hilo ambalo lilithibitishwa na vyombo vyengine vya habari.

''Wanasiasa fulani wa Washington hupendelea kupigania mataifa ya kigeni, lakini rais Trump atawapigania raia wa M arekani pekee,taarifa iliotoka katika msemaji wa Ikulu Raj Sha ilisema.

Iliendelea: „Kama mataifa mengine ambayo yana wahamiaji wanaofaa kuwa nchini humo, rais Trump anapigania suluhu ya kudumu inazofanya taifa hilo kuwa thabiti kwa kuwakaribisha wale ambao wana mchango katika jamii ,hukuza uchumi wetu na kuingiliana na raia wa taifa letu.

„Kamwe hatakubali mkakati wa muda mfupi ulio hafifu na hatari ambao unahatarisha maisha ya raia wa Marekani, mbali na kutowaruhusu wahamiaji wanaotaka maisha mazuri Marekani ijapokuwa kupitia njia halali."

Matamshi hayo ya rais Trump yanajiri huku wabunge kutika vyama vyote wakimtembelea kupendekeza mpango wa wahamaiji usiopendelea upande wowote.

Seneta wa Democrat Richard Durbin alikuwa akizungumza kuhusu vibali vya muda wa kuishi vinavyotolewa kwa raia wanaotoka katika mataifa yaliokumbwa na majanga, vita ama milipuko ya magonjwa, vilisema vyombi vya habari.

Kulingana gazeti la Washington Post , bwana Trump aliwaambia wabunge kwamba Marekani badala yake inachukua wahamiaji kutoka Norway, ambayo waziri wake mkuu alimtembelea rais Trump siku ya Jumatano.

Seneta Lindsey Graham, ambaye ni mwanachama wa chama cha Republian kutoka Carolina Kusini pia alikuwa katika mkutano huo lakini hakuweza kuzungumzia kuhusu matusi hayo yaliotolewa na rais Trum.

Gazeti la The New York Times liliripoti miaka mitatu iliopita kwamba bwana Trump alisema kuwa raia wa Haiti wote wana ''ukimwi'' wakati wa mkutano wa mwezi Juni kuhusu wahamiaji.

Na kufuatia matamshi hayo rais Trump hakusazwa katika mitandao ya kijamii.

Elijah Cummings, mbunge wa Democrat katika eneo la Maryland alichapisha ujumbe katika mtandao wa twitter akisema: Nayashutumu matamshi hayo yasiosameheka na yanayoshusha hadhi ya afisi ya rais.

Mbunge mwengine mweusi kutoka chama cha Democrat. Cedric Richmond, alisema matamshi ya bwana Trump ni dhihirisho tosha kwamba sera yake ya kuliimarisha taifa la Marekani ni sawa na kulifanya taifa la Marekani kuwa la watu weupe pekee.

Mia Love, raia wa chama cha Republican katika eneo la Utah ambaye pia ni mbunge wa pekee mwenye mizizi ya Haiti nchini Marekani amemtaka rais Trump kuomba msamaha kwa maneno hayo yalio na chuki na yenye kugawanya watu.

Muungano unaopigania haki za watu weusi NAACP ulimshutumu rais Trump kwa kuzidi kuegemea katika ubaguzi wa rangi.

Lakini Ikulu ya Whitehouse imepuuzilia mbalia shutuma hizo zinazomkabili rais.

Afisa mmoja wa Trump alinukuliwa na chombo cha habari cha CNN akisema: Ijapokuwa hili litawakasirisha watu wa Washington, wafanyikazi wanadhani kwamba matamshi hayo yanatokana na mizizi yake, sawa na matamshi yake dhidi ya wachezaji wa NFL waliopiga goti wakati wa kuimbwa kwa wimbo wa taifa.

Msemaji wa ubalozi wa El Salvador mjini Washington alikataa kuzungumzia kuhusu matamshi hayo.

Tunda Afichwa na Penzi la Mbunge Apangiwa Apartment

$
0
0
Tunda Afichwa na Penzi la Mbunge Apangiwa Apartment
BAADA ya Dishi Bovu kunasa ubuyu kwamba mwanadada, Tunda Sebastian kuwa anatoka na mbunge mmoja hivi anayemiliki hoteli ya kifahari jijini Dar na kumpangishia ‘apartment’ maeneo ya Tegeta, liliamua kutega antena zake ili kuweza kunasa kinachoendelea baina ya Tunda na mbunge huyo ambaye anawekwa kwenye mabano kwa kipindi hiki!



Dishi Bovu kwa kuanza liliwachokonoa watu wa karibu wa mwanadada huyo ili waweze kuunguza picha ambapo baada ya kumpata shoga yake mmoja mzurimzuri ambaye huonekana na Tunda mara kwa mara kwenye sherehe za kiburudani (hakupenda tummulike tochi) hivi ndivyo alivyofunguka; Shoga Mtu: Aaah! Kwani Tunda hata akiwa na mbunge au waziri kuna tatizo gani? Dishi Bovu: Tunataka tu ututhibitishie, hata sisi tunajua hakuna tatizo!


Shoga Mtu: Sasa niwathibitishie vipi? Niwatumie picha wakiwa faragha?

Dishi Bovu: Kama inawezekana, tena hapo utakuwa umesafisha picha haswaa! Shoga Mtu: Haa haaa! Siwezi kufanya huo ujinga ingawa ninafahamu kwamba ni kweli Tunda yupo na mbunge, ila mtafuteni mwenyewe, si namba yake mnayo. (Twiiii…shoga huyo aliminya kitufe chekundu cha simu yake, ikakatika.)

Dishi Bovu huyoo sambamba na Tunda Baada ya Dishi Bovu kuchonga na Shoga Mtu halikupenda kuacha ‘network’ ikisachi mchelemchele, liliamua kumtafuta Tunda ili aweze kufunguka ukweli wa madai hayo.

Dishi Bovu: Tundaa… Tunda: Nambie!



Dishi Bovu: Hongera mamaa!



Tunda: Kwa lipi? Kwanza naongea na nani mwenzangu?

Dishi Bovu: Ahaaa Tundaaaa!

Dishi Bovu hapa! Tunda: Shida yako?

Dishi Bovu: Nakuona unawakimbiza wenzio mjini!

Tunda: Kina nani?

Dishi Bovu: Mastaa wenzako! Tena huyo mbunge ambaye mna-share shuka eti amekupangishia apartment Tegeta siyo?

Tunda: Simjui bhana huyo mtu unayemzungumzia. (Twiii…naye alikata simu. Ingawa alipigiwa mara kadhaa hakuweza kupokea kabisa.)


Kutana na Mtabibu Wanyota Duniani Kote Maalim Fadhili Rashid Kutoka COMORO Kwa Sasa Yupo Tanzania

$
0
0
KUTANA NA MTABIBIBU WANYOTA DUNIANIKOTE MAALIM FADHILI RASHIDI KUTOKA COMORO KWA SASA YUPO TANZANIA NI BINGWA WAKUTIBU MARADHI SUGU KAMA VILE MIGUU KUUMA NA KUWAKA MOTO PRESHA KISUKARI VIDONDA VYA TUMBO PUMU

MAALIM FADHILI RASHIDI ANAJUWA UMEHANGAIKA SANA LAKINI HUJAFANIKIWA MUONE HARAKA AKUSAIDIE ANADAWA ZA KI COMRO DAWAZAKE HABAHATISHI MUONE HARAKA AKUSAIDIE TEZI NAUVIMBE TUMBONI ANAUWEZO WAKURUDISHA MTUALIE POTEA KIMAZINGIRA (MSUKURE) KUMFANYA MKE MUME MPENZI ASIKUSALITI DAWA YA (LIMBWATA) KUMTAWALA MPENZI WAKO UNAVYOTAKA KUMUONA MBAYA WAKO LIVE KWASABABI MALUM ANATOA PETE YA BAHATI INAYO ENDANA NA NYOTA YAKO ITAKAYO KULETEA MALI BILA YA MASHARITI NAKUMILIKI MALI ZAMAJINI DAWA YAKUONGEZA UUME ZAIZI UIPENDAYO DAWA YA NGUVU ZAKIUME PIA ANAYO DAWA YAKUONGEZA HIPS SHEPU KUWA NAUMBO BOMBA KAMA UMEIBIWA AMA KUDHULUMIWA UTARUDISHIWA MALIYAKO NDANI YA MASAA (24) ANAFUNGA KESI NAKUPATA HAKIYAKO DAWA YA MVUTO
WABIASHARA KUUZA MALIYAKO KWAHARAKA KUZUIYA CHUMAULETE KUSAFISHA NYOTA NAKUTOWA MIKOSI NA KUPANDISHWA CHEO KAZINI KARIBUNI WOTE TIBA NIKWADINI ZOTE UTAPATA HUDUMA POPOTE ULIPO DUNIANI

CALLING +255719362806/

WHATSAPP CALLING +255785786436/

VIDEO: Zamaradi Mketema Afunguka kwa Mara ya Kwanza Kuhusu Ndoa yake, Ruge, Clouds na Vingine *Exclusive

$
0
0
Kwenye Chill na Sky, Zamaradi Mketema anafunguka kwa mara ya kwanza kuhusu ndoa yake, uhusiano wake na baba wa watoto wake wawili, Ruge Mutahaba, alivyojisikia baada ya Adam Mchomvu na Soudy Brown kuiponda ndoa yake na mengine

VIDEO:

Picha ya Diamond na Harmonize Kwenye Mnara wa Redio ya WCB

$
0
0
Baada ya kutuonesha mjengo mpya ambapo ndio zitakuwa ofisi za radio ya Wasafi FM na Wasafi Tv  sasa CEO wa WCB Diamond Platnumz  leo January 12, 2018 amepost picha inayomuonesha yuko na Harmonize huku nyuma yao kukiwa na mnara mrefu ambao inawezekana ukawa ndiyo mnara wa radio tuliyo ahidiwa..

Diamond amepost picha hiyo na kuandika Caption iliyosomeka…“What a Busy Day #Mnarani…. InshaAllah Mwenyez Mungu atujaalie sisi Pamoja nawe Mwaka 2018 Uwe Mwaka Mwema na Wamafanikio…Tuseme “Ameen”🙏 Cc @harmonize_tz” – Diamond

VIDEO:


Utani wa Mpoki Kuhusu Studio Mpya za WCB

$
0
0
Mchekeshaji wa kundi la original comedy Mpoki ameamua kufanya utani kuhusiana na headquaters mpya za WCB baada ya kufanya vice versa na kile alichokipost Diamond Platnumz kwa kuonesha nyumba ya udongo katika page yake ya instagram na kusema ni studio za wachafu wakati Diamond alisema ni studio za wasafi.

Mpoki aliandika caption inayosema “tutaonana, hii ndio headquarters ya wachafu fm na tv kama kawa tukutane sehemu ya kuosha magari tutaonana hivi karibuni”

Kwa Nini Wanaume Wengi Wanaupungufu Wa Nguvu Za Kiume Na Maumbile Madogo?

$
0
0
Asilimia 45 ya wanaume wapo tofauti na wengine kwa kuwatimizia vyema wake au wapenzi Wao na kuwasababishia kutoka nje ya ndoa zao.


NINI CHANZO CHA HAYO?Kupiga punyeto,Ngiri,Vidonda vya tumbo,Magonjwa ya moyo,Presha,Kisukari,Korodani moja kuvimba,Msongo wa mwazo,Kufanyiwa tohara ukiwa mtu mzima n.k.DOKTA MANYANDA sasa kapata tiba sahihi ya tatizo la NGUVU ZA KIUME.


MUHAMA:Hii hutibu na kuponyesha kabisa tatizo la nguvu za kiume,utakuwa na uwezo wa kurudia tendo zaidi ya mara tatu bila kuchoka na itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa mda wa dakika 15-20.DAWA hii imechanganywa miti 12.Hata wazee wenye umri mkubwa wanapona kabisa.OKO NDOA YAKO SASA.


MANGUNGU MIX: Ndio tiba tosha kwa sasa ambayo hurefusha na kunenepesha uume saizi uipendayo inch 1-8 na unene sentimita 1-5,dawa hii ipo ya kupaka na kunywa na haina madhara yoyote kwa mtumiaji.


NITOFAUTI NA ULIZO WAHI KUZITUMIA.Pia tuna dawa za kupatanisha mke,mme,mpenzi au bosi wako kwa mda mfupi sana,Uzazi,Kusafisha nyota,


Je unamali yako unauza hupati wateja?Wasiliana nami 0716-263605


DOKTA MANYANDA ANAPATIKANA KASULU KIGOMA,Kwa wale wa mikoani huduma hii utaipata popote pale

Mbeya City Yafanya Mabadiriko

$
0
0
Mbeya City Yafanya Mabadiriko
Timu ya Mbeya City inayocheza ligi kuu soka Tanzania bara imefanya mabadiliko madogo kwenye benchi lake la ufundi kuelekea mchezo wake wa ligi dhidi ya Tanzania Prisons.


Taarifa kutoka klabu hiyo imeeleza kuwa mabadiliko hayo yamewagusa kocha msaidizi, Mohammed Kijuso na Meneja wa timu Geoffrey Katepa.

Mohammed Kijuso ambaye aliwahi kuichezea klabu ya Simba anakwenda kuwa kocha mkuu wa timu ya vijana, huku aliyekuwa meneja wa timu Katepa akiachana na timu hiyo baada ya kumaliza mkataba wake.

“Kijuso anakwenda kuwa kocha wa timu ya vijana kazi ambayo aliifanya kwa mafanikio kabla ya kuwa kocha msaidizi sasa tunamrudisha huko, lakini Katepa aliajiriwa kwaajili ya kumsaidia kocha wa zamani Kinnah Phiri kwasababu hakuwa anajua Kiswahili ila kwasasa tuna mwalimu anayejua Kiswahili hivyo hakuna haja ya kumwongeza mkataba'', amesema Mtendaji wa timu hiyo Kimbe.

Kwasasa Mbeya City inayoshika nafasi ya 11 kwenye Ligi Kuu ikiwa na alama 12 baada ya mechi 12, itaendelea kufundishwa na kocha mkuu Ramadhani Nswanzurino akisaidiwa na kocha wa makipa Josiah Stephen.Kesho jioni Mbeya City itakuwa uwanjani kucheza na mahasimu wao wa jiji la Mbeya Tanzania Prison kwenye uwanja wa Sokoine.

Diamond Ashinda Tuzo ya Best Male MVP Nigeria

$
0
0
Diamond Ashinda Tuzo ya Best Male MVP Nigeria
Msanii wa muziki Bongo, Diamond Platnumz ameshinda tuzo kutoka Kituo cha Runinga cha Soundcity.

Muimbaji huyo ameshinda katika kipengele cha Best Male MVP ambapo alikuwa akichuana na wasanii wengine kama Davido, RunTown, Olamide, Wizkid, 2Baba (2face) wote kutoka Nigeria na Sarkodie, Shatta Wale kutoka Ghana pamoja na Navio kutoka Uganda.

Diamond ndio msanii pekee kutoka Tanzania na Afrika mashariki kushinda katika tuzo hizo.

Wasanii wengine wa Tanzania walikuwa wakiwania tuzo hizo ni Vanessa Mdee katika kipengele cha ‘Best Female MVP’ ambapo alichuana na wasanii kama Tiwa Savage, Niniola, Yemi Alade na wengineo.

Aslay naye alikuwa akiwania kwenye kipengele cha ‘Best New MVP’ ambapo alikuwa na wasanii kama Maleekberry, Mayorkun, Diceailes, SmallDoctor wote kutoka Nigeria, Na Nadia Nakai kutoka Afrika Kusini.

Wengine ni Alikiba katika kipengele cha Song of The Year kupitia wimbo wake wa Seduce Me na kundi la Nany Kenzo katika kipengele cha Best Group or Duo.

Lava Lava Afunguka Kuhusu Kufanya Cover ya Ngoma ya Alikiba

$
0
0
Lava Lava Afunguka Kuhusu Kufanya Cover ya Ngoma ya Alikiba
Msanii wa muziki Bongo, Lava Lava amefunguka iwapo anaweza kufanya cover ya ngoma yoyote ya msanii Alikiba.

Muimbaji huyo kutoka label ya WCB ameiambia The Playlist ya Times Fm kwa sasa bado hajafikiria hilo ila Alikiba ni msanii ambaye anajifunza mengi mazuri kutoka kwake.

“Kwa sasa hivi siwezi kusema, unajua mpaka kufanya cover ya msanii inabidi huo wimbo uwe unaufuatilia, unajua kufanya cover ni ku-present kile ambacho amekifanya lakini kukiboresha zaidi,” amesema.

Utakumbuka Lala Lava alishafanya cover ya ngoma ya Diamond inayokwenda kwa jina la Utanipenda.

Alipoulizwa ni kitu gani anajifunza kutoka kwa Alikiba alijibu; “vitu vingi sana, Alikiba ni msanii mzuri na anafanya vizuri, kwa hiyo wasanii wote wanaofanya vizuri lazima uchungulie kuona wanafanya vitu gani ili ujifunze,”.

TFF Yatoa Onyo Kali Upangaji Matokeo Ligi Daraja la Kwanza

$
0
0
TFF Yatoa Onyo Kali Upangaji Matokeo Ligi Daraja la Kwanza
Moja kati ya kosa kubwa katika mchezo wa soka ambalo linaweza kugharimu timu, kiongozi, mchezaji au refa ni ishu nzima ya upangaji wa matokeo ya mechi, adhabu za upangaji wa matokeo mara nyingi hutolewa kubwa ili kukomesha tabia hiyo na haishangazi ukisikia mtu kafungiwa maisha.

Jumamosi ya January 13 Tanzania zitachezwa baadhi ya game za Ligi daraja la kwanza ambazo zitaamua ni timu ipi na ipi zitapanda kucheza Ligi Kuu msimu wa 2018/2019, hivyo baada ya Ligi daraja la kwanza kuwahi kutuhumiwa kuwa tabia ya upangaji wa matokeo TFF limetoa onyo.

Kama utakuwa unakumbuka vizuri refa Joseph Lamptey raia wa Ghana ni mmoja kati ya marefa wahanga wa vitendo vya upangaji wa matokeo, March 20 2017 Lamptey alitangazwa kufungiwa maisha na FIFA kujihusisha na soka baada ya kubainika kujihusisha na upangaji wa matokeo wa game ya Afrika Kusini dhidi ya Senegal ya kuwania kufuzu World Cup 2018.

Bunge Bado Halijamuandikia Barua ya Kumuita Ole Sendeka

$
0
0
 Bunge Bado Halijamuandikia Barua ya Kumuita Ole Sendeka
 Bunge bado halijamuandikia barua ya kumuita Mkuu wa Mkoa wa Njombe, Christopher Ole Sendeka ili kujibu tuhuma za kukejeli na kudharau muhimili huo.

Akizungumza na Mwananchi leo Jumamosi, Katibu wa Bunge Stephen Kigaigai amesema kuwa bado hawajamuandikia barua ya kumwita kufika katika kamati hiyo.

"Niko katika kikao lakini ninachofahamu kuwa bado hatujamuandikia," amesema Kigaigai.

Januari 9 mwaka huu Spika wa Bunge, Job Ndugai aliagiza Kamati ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge kumuita na kumhoji Sendeka wakati wa uchunguzi wa kamati hiyo kuhusu tuhuma hizo zilizonukuliwa katika mitandao ya jamii kwa lugha ya Kimasai, Kiswahili na Kingereza.

Spika alisema lengo la kumuita ni kubaini ukweli wa dhamira ua kauli hizo na lutoa mapendekezo kuhusu hatua zinazopaswa kuchukuliwa na Bunge.
Chanzo: Mwananchi


Kamati Kuu ya Chadema Kukutana Leo

$
0
0
Kamati Kuu ya Chadema Kukutana Leo
Chama cha demokrasia na Maendeleo Chadema Leo Jumamosi January 13, kinatakiwa kufanya kikao cha Kamati Kuu ya Chama.

Kikao hicho kimekuja siku tatu tangu mmoja wa wajumbe wake, Edward Lowassa kufanye ziara Ikulu na kuzungumza na Rais John Magufuli kitendo ambacho kilisababisha mvutano ndani ya chama hicho kikuu cha upinzani nchini.

Bila shaka, kikao cha leo kitakachokuwa chini ya uenyekiti wa Freeman Mbowe, mbali na mambo mengine kitataka kujua undani wa mazungumzo ya mjumbe huyo na Rais Magufuli.

Ingawa Naibu Katibu Mkuu wa Chadema-Zanzibar, Salum Mwalimu alisema jana kwamba kikao hicho kimeitishwa kwa lengo la kufanya tathmini ya hali ya kisiasa nchini, baadhi ya wadadisi wa masuala ya kisiasa wamesema suala la kikao cha Lowassa na Rais Ikulu linaweza kuwa na mjadala mpana zaidi katika kikao hicho.

Hata hivyo, Mwalimu alisema ajenda za kikao hicho zilipangwa kabla Waziri Mkuu huyo wa zamani hajaenda Ikulu hivyo hakina uhusiano na ziara hiyo ila huenda jambo hilo likajitokeza.

“Suala hilo halipo kwenye ajenda ila linaweza kujitokeza na likijitokeza litazungumziwa lisipojitokeza basi,” alisema Mwalimu na kuongeza;

“Hata hivyo, kwa upande wake inaweza kuwa fursa nzuri kuielezea Kamati Kuu na viongozi wenzake nini kilitokea.”

Alisisitiza kuwa kikao hicho si cha dharura kwani kilipangwa kufanyika Desemba mwaka jana lakini kiliahirishwa kutokana na sikukuu za mwisho wa mwaka.



Uchaguzi Mdogo wa Marudio Kufanyika Majimbo Matatu Mrithi wa Nyalandu Kujulikana Leo

$
0
0
Uchaguzi Mdogo wa Marudio Kufanyika Majimbo Matatu  Mrithi wa Nyalandu Kujulikana Leo
Warithi wa Lazaro Nyalandu, Leonidas Gama na Onesmo Ole Nangole wanatarajiwa kupatikana leo katika uchaguzi mdogo wa marudio wa majimbo matatu.

Majimbo hayo ni Singida Kaskazini (Singida), Songea Mjini (Ruvuma) na Longido (Arusha). Uchaguzi wa majimbo hayo unafanyika kutokana na sababu tofauti ambazo ni kujiuzulu ubunge, kifo na kutenguliwa na Mahakama.

Jimbo la Singida Kaskazini lilikuwa chini ya Nyalandu kwa muda mrefu lakini Oktoba mwaka jana alitangaza kujivua uanachama wa CCM na nyadhifa zake zote akisema haridhishwi na mwenendo wa siasa nchini.

Mbali na hilo, Nyalandu alimwandikia barua Spika wa Bunge, Job Ndugai akimweleza kwamba anajiuzulu wadhifa huo alioutumikia kwa vipindi vinne mfulululizo tangu alipochaguliwa kwa mara ya kwanza mwaka 2000.

Baada ya kuchukua hatua hiyo, Nyalandu ambaye aliwahi kuwa Waziri wa Maliasili na Utalii katika Serikali ya Awamu Nne, alitangaza kuhamia chama kikuu cha upinzani cha Chadema.

Wakati Nyalandu akijiuzulu, Ole Nangole wa Chadema alivuliwa wadhifa wa ubunge wa Longido na Mahakama kutokana na kasoro kadhaa zilizojitokeza kwenye Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2015.

Jimbo la Songea Mjini nalo lilibaki wazi kutokana na kifo cha Gama aliyefariki dunia Novemba mwaka jana baada ya kuugua ghafla.

Tofauti na chaguzi nyingine ndogo zilizotangulia, uchaguzi wa leo hautarajiwi kuwa na ushindani kutokana na baadhi ya vyama vya upinzani vikiongozwa na Chadema kususia kwa sababu ya kasoro zilizojitokeza katika uchaguzi mdogo wa udiwani wa kata 43 uliofanyika Novemba 26 mwaka jana.

Akizungumza na wanahabari Desemba 11 mwaka jana, akiwa ameambatana na viongozi wenzake wa Ukawa, Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe alisema uchaguzi wa kata hizo uligeuka uwanja wa vita badala ya jukwaa la kuchagua viongozi na aliitaka Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), kuahirisha uchaguzi wa majimbo hayo matatu.

Mbowe alitaka majadiliano ya wadau ili kuondoa kasoro hizo hivyo kuwa na uchaguzi ulio huru na haki katika majimbo hayo matatu.

“Hatuwezi kushiriki uchaguzi wakati tumefungwa mikono, hii ni sawa na timu ya mpira kwenda kwenye mashindano bila kufanya mazoezi,” alisema Mbowe katika mkutano huo na wanahabari.

Hata hivyo, matakwa hayo yalitupiliwa mbali na NEC ambayo ilisema taratibu za uchaguzi huo upo kwa mujibu wa sheria na kama upinzani unadhani kuna kasoro ungeweza kwenda mahakamani kupinga.

Wakati Mbowe akieleza hayo, mwezi uliofuata Chama cha ACT-Wazalendo kupitia kwa mwenyekiti wake, Yeremia Maganja kilitangaza pia kususia ili kufikisha ujumbe kwa wadau wa siasa kuwa kuna tatizo hivyo kuwepo jana ya majadaliano.

Vyama vya Chadema, NCCR-Mageuzi, CUF, NLD, Chaumma na ACT-Wazalendo vimetangaza kususia uchaguzi huo, wakati CUF upande wa unaomuunga mkono mwenyekiti wa chama hicho, Profesa Ibrahim Lipumba anayetambuliwa na ofisi ya Msajili ya Vyama vya Siasa, ukitangaza kushiriki uchaguzi huo.

Tayari Katibu wa Uenezi CCM Arusha, Shaaban Mdoe ameshaweka wazi ya kuwa chama hicho kitaibuka kidedea kwa asilimia 96 katika uchaguzi huo baada ya Chadema kuweka mpira kwapani.

Mkurugenzi wa Habari, Uenezi na Mawasiliano kwa Umma, upande wa Profesa Lipumba, Abdul Kambaya aliwataka wananchi wa majimbo na kata zinazorudia uchaguzi kujitokeza kwa wingi leo.

“Ingawa uchaguzi wa kata 43 ulikuwa una dosari kadhaa, lakini tumeona kususia siyo jambo jema.Kesho (leo) wananchi wajitokeza kwa wingi na kupiga kura na CUF itazilinda kwa mujibu wa taratibu,” alisema Kambaya.
Chanzo: Mwananchi

Viewing all 104702 articles
Browse latest View live




Latest Images