Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104785 articles
Browse latest View live

Zitto Kabwe Azuiliwa Kufanya Mkutano na Polisi

$
0
0
Zitto Kabwe Azuiliwa na Polisi
Jeshi la Polisi Kigoma limemzuia Mbunge wa Kigoma Mjini Zitto Kabwe kufanya mkutano wa hadhara katika Uwanja wa Uwanja wa Mwanga Community Center, mkoani Kigoma ambao ulipaswa kufanyika leo Januari 16, 2018.


Taarifa iliyotolewa na OCD inasema kuwa kiongozi huyo hakufuata utaratibu wa kutoa taarifa ndani ya masaa 48 kabla ya kufanyika kwa mkutano huo jambo ambalo Mbunge Zitto Kabwe amelilamikia na kusema kuwa amezuiwa kufanya Mkutano kinyume na sheria ya Bunge ya mwaka 1988.

"Mimi sitaki kuwapa polisi sifa ya kupambana nasi. Tumeahirisha mkutano mpaka siku ya jumamosi Lakini tumewaandikia barua rasmi kuwa sheria waliyonukuu sio sheria halali na haihusiani na mikutano ya Mbunge kwenye jimbo lake la Uchaguzi. Sheria wanayopaswa kunukuu ni sheria namba 3 ya mwaka 1988 kifungu cha 4(1)". Alisema Zitto Kabwe

Kufuatia jambo hilo Zitto Kabwe amedai kuwa atamwandikia barua rasmi Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Job Ndugai kuhusu suala hilo ili kutengeneza mazingira kwa siku za usoni lisije kumtokea Mbunge mwingine yoyote.


Man Fongo Akili Hatokuja Kutoa Ngoma Kubwa Kama Hakunaga Ushemeji

$
0
0
Man Fongo Akili Hatokuja Kutoa Ngoma Kubwa Kama Hakunaga Ushemeji
Msanii wa muziki wa Singeli Bongo, Man Fongo amesema katika maisha yake ya muziki hatokuja kutoa ngoma kubwa kama Hainaga Ushemeji.

Muimbaji huyo ambaye anatamba na ngoma yake mpya ‘Lau Nafasi’ ameiambia E-Newz ya EATV kuwa ngoma hiyo ndio ilifungua milango kwa muziki wa singeli hivyo ni vigumu kuishusha.

“Ile Hainaga Ushemeji ni official kutambulisha muziki wa singeli na kuwaelekeza watu kuna muziki unaitwa kisingeli na sitaokuja kutoa ngoma kubwa kama hainaga ushemeji,” amesema Man Fongo.

Ameongeza kuwa kwa sasa wasanii wengine wanapata fedha nyingi kutokana na ngoma hiyo hiyo ku-hit kitu ambacho sasa kushika milioni mbili hadi tatu ni jambo la kawaida.

Picha: Hivi Ndivyo Itakavyokuwa Kituo cha Mabasi Dodoma

$
0
0
Picha: Hivi Ndivyo Itakavyokuwa Kituo cha Mabasi Dodoma
SERIKALI ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Wizara ya Ujenzi imejipanga kuanza utekelezaji wa mradi wa ujenzi wa kituo kipya na cha kisasa cha mabasiyaendayo mikoani katika Makao Makuu ya Nchiu, Mjini Dodomna.

Kituo hicho ambacho kinajengwa nje kidogo ya mji, kitakuwa na manufaa makubwa katika kudhibiti msongamano wa magari unaochangiwa na kukua kwa haraka kwa mji.

Aidha, mradi wa Ujenzi wa kituo hicho unatarajiwa kuanza hivi karibuni.

TFF Yawapeleka Viongozi Wanne Kamati ya Maadili

$
0
0
TFF Yawapeleka Viongozi Wanne Kamati ya Maadili
Shirikisho la soka Tanzania TFF leo Jumanne ya January 16 2018 limetangaza kuwapeleka katika kamati ya maadili viongozi wanne, hiyo inatokana na viongozi hao kubainika kugushi na udanganyifu.

Msaidizi wa Zamani wa Mugabe: Nilihofia Mugabe Angeuawa Kama Gaddafi

$
0
0
Msaidizi wa Zamani wa Mugabe: Nilihofia Mugabe Angeuawa Kama Gaddafi
Msemaji wa rais wa zamani wa Zimbabwe Robert Mugabe amesema alikuwa na wasiwasi kwamba raia nchini humo "wangemburura na kumuua" kiongozi huyo kama ilivyotokea nchini Libya.

Wakati wa wiki ya mwisho madarakani, Bw Mugabe alikuwa amewekwa kwenye kizuizi kwake nyumbani baada ya jeshi kuchukua udhibiti wa serikali.

Baadaye aliondolewa kikamilifu kutoka madarakani.

"Nilianza kufikiria picha sawa na za Muammar Gaddafi," George Charamba, ambaye ni msemaji wa zamani wa Bw Mugabe amesema.

Alikuwa anazungumza na tovuti ya kibinafsi nchini Zimbabwe ya Daily News.

Huku akikumbuka siku za mwisho za utawala wa Mugabe wa miaka 37, Charamba anasema kiongozi huyo wa miaka 93 alitaka kuondoka madarakani "kwa masharti yake" na kwamba alikuwa ametahadharishwa kuhusu hatari iliyokuwepo baada ya jeshi kuchukua udhibiti wa nchi na maandamano kuzuka.

Mugabe alipokuwa anazuiliwa katika makao yake ya kifahari ya Blue Roof mazungumzo kuhusu mustakabali wake yalikuwa yanafanyika kati ya majenerali, makasisi wa kanisa Katoliki, wasaidizi wake wa kisiasa na wajumbe kutoka Afrika Kusini.

Bw Charamba anasema maafisa wa jeshi waliwafahamisha kwamba maelfu ya waandamanaji waliokuwa wanamtaka Mugabe angejiuzulu, kulikuwa na uwezekano, wangetaka kumfikia Mugabe binafsi.

"Ingewezekana kwa sababu wanajeshi hao walitwambia 'hatuwezi kuwafyatulia risasi raia ambao wanaandamana dhidi ya rais na kummwaga damu," Charamba amenukuliwa na tovuti ya Daily News.

Kiongozi wa zamani wa Libya Muammar Gaddafi alikamatwa na kisha kuuawa mwaka 2011 baada ya maandamano na maasi ambayo yalifikisha kikomo utawala wake wa miongo minne.

Vijana 1,000 Washtakiwa kwa Kusambaza Picha na Video za Ngono

$
0
0
Vijana 1,000 Washtakiwa kwa Kusambaza Picha na Video za Ngono
Zaidi ya vijana 1,000 wameshtakiwa na polisi Denmark kwa kusambaza picha na video za ngono.

Wameshitakiwa kwa kutumia mtandao wa jamii wa Facebook Messenger kusambaza vipande vya video vilivyoonesha vijana wawili wenye miaka 15 wakifanya mapenzi.

Polisi wamesema kwa sababu vijana hao walikuwa wenye umri chini ya miaka 18, mashtaka yawaweza ongezeka hadi kosa la kusambaza picha zisizo ma maadili ya watoto.

Kampuni ya Facebook iiliwataarifu mamlaka wa Marekani ambao wakawatoa taarifa kwa polisi Denmark.

Kama wakipatikana na hatia ya kusambaza picha zisizo na maadili kwa watoto, watawekwa kwenye orodha ya wadhalilishaji ya watoto kingono kwa miaka 10.

Vijana elfu moja na nne wanamashtaka nchi nzima ikiwa ni baada ya kusambaza picha na video kwa kutumia app hiyo ya kutuma ujumbe mwishoni wa mwaka jana.

Baadhi ya watuhumiwa wenye umri juu ya miaka 18 waliitwa katika vituo vya polisi kuhojiwa.

Watuhumiwa chini ya miaka 18 wapatikana kupitia wazazi wao.

Mkuu wa polisi wa Denmark amesema mashitaka hayo yanakuja kama onyo kwa vijana kuthubutu kutuma video za ngono.

Yeyote atakayepatwa na hatia na mashtaka hayo anaweza kupata kifungo cha siku 20.

Kumekuwa na wito kwa serikali ya Denmark kuchukua hatua zaidi kuzuia picha za ngono ili kulipa kisasi.

Polisi Dar Wakamata Silaha za Moto Zilizotumika Katika Matukio ya Uhalifu

$
0
0
Polisi Dar Wakamata Silaha za Moto Zilizotumika Katika Matukio ya Uhalifu
JESHI la Polisi kanda Maalumya Dar es Salaam limekamata silaha mbalimbali zikiwemo bunduki, bastola na vifaa vingine vya kufanyia matukio ya uhalifu pamoja na watuhumiwa mbalimbali wa makosa ya uhalifu ambao walikuwa wakijiandaa kutekeleleza matukio hayo.

Akizungumza na wanahabari ofisini kwake leo, Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar, Lazaro Mambosasaamesema jeshi hilo limekamata silaha aina ya AK 47 na watuhumiwa wawili nyumbani kwa mzee Said Omary (62) baada ya kupata taarifa kuwa kuna wahalifu wanataka kufanya tukio la wizi wa kutumia silaha.

Aidha Polisi imewakamata watuhumiwa 2 wa wizi wa magari ambao baada ya kufanyiwa upekuzi walikutwa na radio call, kadi 10 za benki mbalimbali, leseni za udereva, master keys 15 ambapo baada ya kuhojiwa walikiri kutekeleza matukio mbalimbali ua uhalifu huku wakionesha magari mawili na pikipiki moja vinavyodhaniwa kuwa ni vya wizi.

Bill Nass Amuwezesha Uchebe Ili Kupambana na Nuh Mziwanda

$
0
0
Bill Nass Amuwezesha Uchebe Ili Kupambana na Nuh Mziwanda
Msanii wa Bongo Fleva anayefanya vizuri katika game kwa sasa, Billnass amemtaka mume wa msanii Shilole, Uchebe kupambana pale inapobidi ndiyo maana ameamua kumzawadia vifaa vya mazoezi ili hata kupambana na Nuh Mziwanda pale ambapo inabidi.


Billnass ametoa kauli hiiyo wakati alipokuwa akiahidi zawadi kwa maharusi hao (Shilole na Uchebe) kwenye ukumbi uliofanyika Mikocheni, Jijini Dar es salaam usiku wa kuamkia jana Jumatatu.

Msanii huyo amesema kwamba licha ya kuwa maharusi hao wamezawadiwa na kupewa ahadi mbalimbali yeye anafahamu mume wa msanii huyo anapenda sana michezo ya ngumi hivyo atampatia benchi la 'gym', punching bag na vifaa vinginevyo.

"Najua Mwanangu  Ashraf (Uchebe) anapenda nini, anapenda michezo ya ngumi. Kwa kulitambua hilo mimi namzawadia mwanangu vifaa vya mazoezi ili aweze kufanya fitness. Ufanye mazoezi ya kupambana hata na kina Mziwanda, sisi watoto wakiume bana tunatakiwa kujilinda pale ambapo inabidi," Billnass.

Shilole na Uchebe walifanya sherehe ya harusi yao juzi Jumapili ambapo ilihudhuriwa na wasanii kibao na wengi wakitoa ahadi ya zawadi mbalimbali ikiwepo elimu na nyinginezo nyingi.

Pata Tiba ya Tatizo la Nguvu Za Kiume, Inasaidia Kukufanya Urudie Mara 5 na Kuchelewa Kwa Dakika 20

$
0
0

TATIZO LA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME NA MAUMBILE MADOGO LINATIBIKA.Baada ya utafiti wa mda mrefu juu ya matatizo ya upungufu wa nguvu za kiume na ukosaji wa hamu ya tendo la ndoa ama kushindwa kurudia tendo kwa haraka DR Magise imekuletea tiba ya matatizo hayo kwa kutumia dawa za:


FULL POWER: Ni dawa asili ya vidonge inayotibu tatizo la upungufu au ukosefu wa nguvu za kiume,dawa hii inamchanganyiko wakutosha wenyekuzalisha vichocheo vingi vya Hemone za Gestrogen vikiwemo vitamin B6&B1,vitamini E,pamoja na madini aina ya zinc vitakufanya kuwa na nguvu na mzunguko mzuri wa damu na kuongeza hamu na uwezo wa kufanya tendo la ndoa zaidi ya hatua nne au zaidi,na kuchelewa kufika kileleni zaidi dakka 20-30.


NYAMVA: Inarutubisha maumbile ya uume yani kurefusha na kunenepesha nchi 4-7 upana cm3-4 standard kiafya haijalishi umri wako hata kwa wazee ukiitumia maumbile yako yatabaki kuwa hivyo siku zote,Pia tunatibu Presha,kisukari siku7,ngiri,chango la tumbo tumbo kujaa gesi,kutopata choo vizuri

 TUPO TZ DAR ES SALAAM   MBAGALA RANGI TATU.HUDUMA HII UTALETEWA POPOTE ULIPO .WASILIANA NAMI 0783741788/ 0715741788 -DR MAGISE

Hemed Naye ni Chawa Wangu- Gerry wa Rhymes

$
0
0
Hemed Naye ni Chawa Wangu- Gerrybwa Rhymes
Msanii wa mziki na filamu Gelly wa Rhymes amejibu fununu zisemazo yeye ni chawa wa Hemed na hana mchongo mwengine wa maana mjini kwa kusema yeye na Hemed ni zaidi ya ndugu.


Akipiga story kupitia eNEWZ ya East Africa Television Gelly amesema yeye na Hemed wamepita hatua za urafiki na sasa wapo kama ndugu kwa kuwa wamepitia mambo mengi sana na wamekuwa wakisaidiana mambo mengi sana kiasi kwamba kwa sasa wanaishi kama mtu na kaka ake.

''Watu wanaosema mimi ni Chawa wa Hemed basi wafahamu kwamba hata Hemed ni chawa wangu kwasababu sisi tunashirikiana kwa mambo mengi'', amefunguka Gerry. Gelly pia amefunguka kuwa yeye na Hemed Phd wana mpango wa kuanzisha 'Lebel' yao ambayo itakuwa na wasanii na pia itasimamia mziki wao.

Gelly amemalizia kwa kusema kwamba nyimbo yake mpya inayokuja anampango wa kuwachana 'Vibenten' wote ambao wanaishi mjini kwa kuwategemea wanawake wawaletee hela ambazo wanahongwa na wanaume wengine. Amesema wengine ni watu maarufu na atawaja kwa majina.

Kutana na Mtabibu Wanyota Duniani Kote Maalim Fadhili Rashid Kutoka COMORO Kwa Sasa Yupo Tanzania

$
0
0
KUTANA NA MTABIBIBU WANYOTA DUNIANIKOTE MAALIM FADHILI RASHIDI KUTOKA COMORO KWA SASA YUPO TANZANIA NI BINGWA WAKUTIBU MARADHI SUGU KAMA VILE MIGUU KUUMA NA KUWAKA MOTO PRESHA KISUKARI VIDONDA VYA TUMBO PUMU

MAALIM FADHILI RASHIDI ANAJUWA UMEHANGAIKA SANA LAKINI HUJAFANIKIWA MUONE HARAKA AKUSAIDIE ANADAWA ZA KI COMRO DAWAZAKE HABAHATISHI MUONE HARAKA AKUSAIDIE TEZI NAUVIMBE TUMBONI ANAUWEZO WAKURUDISHA MTUALIE POTEA KIMAZINGIRA (MSUKURE) KUMFANYA MKE MUME MPENZI ASIKUSALITI DAWA YA (LIMBWATA) KUMTAWALA MPENZI WAKO UNAVYOTAKA KUMUONA MBAYA WAKO LIVE KWASABABI MALUM ANATOA PETE YA BAHATI INAYO ENDANA NA NYOTA YAKO ITAKAYO KULETEA MALI BILA YA MASHARITI NAKUMILIKI MALI ZAMAJINI DAWA YAKUONGEZA UUME ZAIZI UIPENDAYO DAWA YA NGUVU ZAKIUME PIA ANAYO DAWA YAKUONGEZA HIPS SHEPU KUWA NAUMBO BOMBA KAMA UMEIBIWA AMA KUDHULUMIWA UTARUDISHIWA MALIYAKO NDANI YA MASAA (24) ANAFUNGA KESI NAKUPATA HAKIYAKO DAWA YA MVUTO
WABIASHARA KUUZA MALIYAKO KWAHARAKA KUZUIYA CHUMAULETE KUSAFISHA NYOTA NAKUTOWA MIKOSI NA KUPANDISHWA CHEO KAZINI KARIBUNI WOTE TIBA NIKWADINI ZOTE UTAPATA HUDUMA POPOTE ULIPO DUNIANI

CALLING +255719362806/

WHATSAPP CALLING +255785786436/

Nkamia Akomalia Kuongeza Muda wa Urais "Rais Hataki Kubadili Ila Wananchi Tunataka"

$
0
0
Nkamia Akomalia Kuongeza Muda wa Urais "Rais Hataki Kubadili Ila Wananchi Tunataka"
Ikiwa ni wiki chache toka Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli kusema kwamba hapendezwi na mjadala unaoendelea juu ya kuongeza muda wa urais kutoka miaka 5 hadi 7, Jumatatu hii Mbunge wa jimbo la Mchemba kutoka Chama cha Mapinduzi (CCM), Juma Nkamia, amesema yeye haoni kama ni tatizo kama rais akiamua kuongeza muda wa uongozi kutoka miaka 5 hadi 7.

Akiongea katika mahojiano na kituo cha BBC, Mhe. Nkamia amesema sio rais ambaye anataka suala hilo bali wananchi ndio ambao wanaonekana kuwa na shauku na suala hilo pamoja na kupunguza gharaza za uchuguzi kila baada ya miaka 5.

“Nimemsikiliza Mhe Rais na mwenyekiti wa chama changu amesema yeye asingependa na hafurahishi na hilo jambo,” alisema Nkamia. “Mkubwa akishasema wewe wa chini unatafakari lakini mimi nakubaliana na hoja yake. “Lakini sio yeye anayetaka, mimi kwa mtazamo wangu, kazi anazozifanya na wananchi wanavyosema nikipita katika maeneo mengi naona jinsi anavyokubalika,”

Aliongeza,”Siku zote Rais hawezi kusema mimi nataka kuendelea,wale wanaomwangalia utendaji wake wa kazi na kuona anafaa kupewa muda zaidi. Nisema mimi kwamba sisi wananchi, mimi kama Mbunge kwa mujibu wa kanuni na taratibu za bunge, Mhe Rais kubadilisha miaka 5 kwenda 7 sio jambo baya sana, kwa mujibu wa kanuni za bunge, nitazungumza na Mhe Spika, maelekezo ambayo nitapewa na Mhe Spika ndiyo nitakayoyatekeleza,”

Hivi karibuni Mhe Rais akiwa na Katibu Mwenezi wa CCM, Humphrey PolePole alisema hana mpango wa kuongeza muda wa urais kutoka miaka 5 hadi 7 na pia hapendezwi na mijadala inayoendelea juu ya hilo.

Hii Hapa Kauli ya Zitto Kabwe Baada Kuzuiwa Kufanya Mkutano na Polisi

$
0
0
Hii Hapa Kauli ya Zitto Kabwe Baada Kuzuiwa Kufanya Mkutano  na Polisi
January 16, 2018 Mbunge Kigoma Mjini na Kiongozi wa chama cha ACT wazalendo Zitto Zuber Kabwe ameonesha kutokuridhishwa na uamuzi wa  jeshi la polisi mkoani Kigoma baada ya kuzuia Mkutano wa hadhara wa Mbunge huyo.

Kupitia ukurasa wake wa Facebook Zitto Kabwe ameandika “Jeshi la polisi limezuia Mkutano wangu wa hadhara kama Mbunge wa Kigoma Mjini kinyume na sheria ya Bunge ya mwaka 1988. Sheria ya Haki, Kinga na Madaraka ya Bunge inayolazimisha  Mbunge kufanya mkutano kwenye jimbo lake bila vikwazo”.

“Sitaki kuwapa polisi sifa ya kupambana nasi. Tumeghairisha mkutano mpaka siku ya jumamosi, tumewaandikia barua rasmi kuwa sheria waliyoinukuu sio sheria halali na haihusiani na mikutano ya Mbunge kwenye jimbo lake. Sheria wanayopaswa kunukuu ni sheria namba 3 ya mwaka 1988 kifungu cha 4(1). “- Zitto Kabwe

 “Ofisi yangu  itamwandikia Spika wa Bunge rasmi kuhusu suala hili ili lisifanyike kwa Mbunge mwingine yeyote”. -Zitto Kabwe

Waliotoka Jela kwa Msamaha wa Rais Tutawarudisha Jela – Mambosasa

$
0
0
Waliotoka Jela kwa Msamaha wa Rais Tutawarudisha Jela – Mambosasa
Kamanda wa Polisi Kanda Maalum Jijini Dar es salaam Lazaro Mambosasa, amesema wahalifu waliotoka jela kwa msamaha wa Rais hawatasita kuwarudisha tena jela iwapo wataendelea na tabia za uhalifu.


Kamanda Mambosasa ametoa kauli hiyo leo alipokuwa akizungumza na waandihsi wa habari alipokuwa akiwapa taarifa za uhalifu, na kusema kwamba watu wanaoongoza kwa vitendo vya uhalifu ni wale waliotoka kwa msamaha wa Rais, na kwamba wanatumwa na wenzao walio jela.

Akiendelea kuzungumzia suala hilo Kamanda Mambosasa amesema watu hao wamekuwa wakirudia maeneo walioficha silaha kabla hawajakamata na kufungwa, na kuzichukua kuzitumia kwenye matukio ya uhalifu, huku wakendelea kuwasiliana na wale ambao bado wako gerezani kujua wameweka wapi silaha ili kuzitumia kwenye kazi zao, na kisha kuwapelekea posho.

“Taarifa tulizonazo baada ya wahalifu wengine waliochiwa kwa msamaha wa Rais, wachache hawataki kubadili tabia zao, wanakwenda kufichua silaha ambazo walilizika ardhini na sasa wanazifukua kwa ajili ya kuanza kuzitumia. Ninatoa onyo kwa mtu yeyote ambaye amepata msamaha, badala ya kumshukuru Mungu akabadili tabia akaanza kuishi kwa kufuata sheria za nchi, anaenda kufukua silaha mahali alipoficha kwa ajili ya kuendeleza vitendo vya uhalifu, niwaambie hawatabaki salama, tutawarudisha huko walikotoka”, amesema Mambosasa.

Kufuatia tukio hilo Kamanda Mambosasa amewataka watu waliopewa msamaha na Rais na kuwa huru, uacha kabisa matendo maovu, na kuwaomba wananchi kutoa ushirikiano pale wanapohisi kuna mtu anafanya vitendo vya uhalifu.

Waliotoboa Bomba la Mafuta na Kujiunganishia Wafikishwa Mahakamani

$
0
0
Waliotoboa Bomba la Mafuta na Kujiunganishia Wafikishwa Mahakamani
January 16, 2018 Watu saba ambao wanadaiwa kujiunganishia bomba kuu la mafuta ya Dizeli hadi nyumbani kwao  wamefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kwaajili ya kusomewa mashtaka hayo.

Watu hao walikamatwa siku chache za nyuma na Jeshi la Polisi katika maeneo mbalimbali Kigamboni ambapo wote walikuwa wakifanya kazi hiyo ya kunyonya mafuta katika bomba hilo la Tanzania na Zambia (TAZAMA).

Yanga Yasaini Mkataba Mnono wa Mabilioni

$
0
0
Yanga Yasaini Mkataba Mnono wa Mabilioni
Mabingwa wateteziwa ligi kuu Tanzania Bara Yanga, leo wamesaini mkataba wa miaka 3 na kampuni ya utengenezaji wa vifaa vya michezo Macron wenye thamani ya bilioni mbili.


Katika mkataba huo uliosainiwa kwenye makao makuu ya klabu hiyo, Yanga itatoa haki zote za utengenezaji na usambazaji wa jezi zao huku pia nembo ya kampuni ya Macron itaanza kuonekana kwenye jezi za Yanga SC.

Kwa upande wake Katibu mkuu wa Yanga Charles Mkwasa amewaonya wote wanaouza jezi za klabu hiyo bila kuwepo kwa makubaliano na watawachukulia hatua za kisheria kwasababu sasa yupo mwenye haki ya kufanya hivyo. Pia Mkwasa amewakaribisha wawekezaji zaidi ndani ya klabu hiyo.

Naye Mkurugenezi mtendaji wa kampuni hiyo hapa Tanzania Suleiman Karim amewahakikishia wana Yanga kuwa klabu hiyo itapata faida kupitia mauzo ya jezi orijino za klabu.

Kampuni ya Macron inafanya kazi katika nchi zaidi ya 16 duniani zikiwemo England, Italia na Ufaransa. Hivi karibuni kampuni hiyo iliingia mkatata wa miaka 2 na timu ya taifa ya Tanzania (Taifa Stars) wenye thamani ya milion 800.

Habari Njema: Tunatibu Busha, Korodani Kuvimba,Ngiri, Miguu Kufa Ganzi Pamoja na Matatizo ya Nguvu za Kiume

$
0
0

Ni Dawa ya nguvu za kiume inayorefusha na kunenepesha uume saizi uipendayo (Inch 1-7) kwa muda wa siku 6 tu.Dozi hii itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa muda wa dakika 30, utarudia tendo la ndoa zaidi ya mara 4 bila hamu kuisha bila kujali umri na garantee ni miaka 60 baada ya kutibu tatizo.

Pia tunatibu Busha bila kufanyiwa Oparesheni, korodani moja kuvimba, ngiri, tumbo kujaa gesi na kuunguruma, kutopata choo vizuri, miguu kuwaka moto na kufa ganzi, chango la wanawake, kisukari na kutokwa na kinyama sehemu ya haja kubwa.

MIHAYO:
Inarudisha mke, mchumba, hawara na atakutimizia kila kitu unachotaka kutoka kwake ndani ya  saa 2 tu hata kama yupo mbali. atarudi na kumfunga asiwe na mwingine zaidi yako.

Umefukuzwa kazini? unataka kupandishwa cheo? Umepoteza pesa zako kwenye biashara bila kujua umepandikizwa chuma ulete? Njoo urudishe pesa zako. Unauza mali yako haiendi?

Wasiliana na mtaalam Challo kwa; 0714006521

MADHARA ya Upigaji Punyeto, na Namna ya Kuepuka

$
0
0

Watu wengi sana wanataka kufahamu jinsi gani wafanye ili kuachana na kitendo cha upigaji punyeto.

Punyeto ni tendo la mtu la kuamsha hisia za mapenzi au msisimko ambao unampelekea mtu huyu kufikia kilele cha kujimalizia tamaa zake! Bila kufanya tendo halisi, hutumia fikra zake katika picha za zinazoitwa za ngono au picha zozote zinazoweza kulifanikisha tendo hilo, movie n.k.

Kilele cha yote anafikia mahali anajimalzia tamaa zake mwenyewe!. Nimekuwa nikiona baadhi ya watu wanaosema wameelimika wakipingana wao kwa wao katika suala zima la kupiga punyeto! Wako wanaotetea kutokana na elimu yao na wanasema kwa ujasiri mkubwa kwamba “kupiga punyeto ni sehemu ya maisha ya mwanadamu” Ina maana katika maisha ya mwanadamu upigaji punyeto inaelezwa ni kama tendo la lazima mpaka inafikia mahali wanasema ni sehemu ya maisha (Maisha) ya mwanadamu.

Nimekuwa nikipata kesi nyingi sana juu ya madhara yatokanayo na punyeto. Aslimia 60 ya vijana wenye umri kuanzia miaka 15 hadi 30 wameathirika na tatzo hili (chronic masturbation) na inakuwa ngumu kujinasua kutoka kwenye hili janga, kama wewe ni mmoja wapo na ulkuwa ukitafuta kwa mda mrefu ufanye nini ili uachane na tabia ya kupiga punyeto basi fatilia kwa makini makala hii.

MADHARA YA UPIGAJI PUNYETO KWA MWANAUME 
Haya ndio baadhi ya madhara ya kimwili ambayo yanaletekezwa na upigaji punyeto

1. PUNYETO INAUA NGUVU ZA KIUME: 
Upigaji wa punyeto unaweza kusababisha upungufu wa nguvu za kiume, kwani kipindi unapiga punyeto jua ile mishipa inayofanya uume usimame unakuwa unaichua na uume unakuwa umesimama kwa muda mrefu sasa ikitokea ukawa unafanya hivi kila siku ile mishipa inalegea na uume unakuwa unakosa nguvu hata ukisimama haui strong unakuwa kama umelegea.

2. KUWAHI KUMALIZA MAPEMA KATIKA TENDO: 
Mara nyingi mtu aliezoea kupiga punyeto huwahi kumaliza mapema pindi akiwa anafanya tendo la ndoa na wakati mwingine uume hushindwa kusimama kwa mara ya pili na kujikuta anashindwa kurudia tendo ikiwa mwenzake bado hajaridhika na anahitaji kuendelea kufanya tendo hilo.
Athari nyingine ni kama zifuatazo :

3.Uchovu wakati wote / Fatigue. Feeling tired all the time.
4.Maumivu ya nyonga / Lower back pain.
5.Kusinyaa kwa Nywele / Nywele kunyonyoka / Thinning hair / Hair Loss
6.Maumivu ya kende
7.Maumivu ya kiuno

Hayo ni baadhi ya nukuu zangu!
Kuna faida nyingi sana ambazo utazipata endapo utaachana na tabia ya upigaji punyeto na hiyo napenda iwe sababu ya wewe msomaji kuachana hicho kitendo.

Kuacha punyeto ama mtindo flani wa maisha inahitaji utambuzi, uamue na pia uweze kjicontrol wewe mwenyewe, inahitaji nguvu ya ndani yako kushinda vishawishi , zifuatazo ni njia ambazo utaanza kutekeleza ukiwa nyumbani kwako bila gharama yoyote na zitaanza kukupa matunda, lazima uwe mwaminifu kufuata kile ninachoelekeza maaana ni njia ambayo imewasaidia vijana wengi.

1.PATA MDA MWINGI WA KUPUMZIKA 
Baada ya shuguli za kawaida haikisha unapata mda wa kupumzika, lala mapema ili uweze kuipa akili mda wa kuchambua na kutunza taarifa za muhimu na kufuta zile ziszo za muhimu. Hakikisha unalala mapema hapo ndipo utaongeza uwezo wa akili kuweza kupambana na hisia na mawazo mabaya.

2. MATUMIZI YA MBOGAMBOGA NA MATUNDA KWA WINGI
Utafiti wa kisayansi unaonesha kwamba matumizi mazuri ya vyakula vya mbogamboga na matunda Husaidia kuongeza uwezo binafsi wa kujisimamia juu ya tamaa na mihemko mbalimbali, matumizi ya vyakula vilivyosindikwa (junk foods) ni chanzo cha kushindwa kujizuia na hapo safari yako ya kuachana na upigaji punyeto itakwama.

3. FANYA MAZOEZI NA USHUGULISHE MWILI 
Maozezi yanasaidia mwili kutofikiria kufanya mambo machafu sababu mara nyingi unakuwa bize, akili inapokuwa inashugulishwa basi uwezekano wa kuleta fikra mbaya ni mdogo sana

4. ACHA KUANGALIA PICHA ZA NGONO
Tafiti zinasema kwamba vijana wengi wenye umri kuanzia miaka 15 mpaka 30 ndo kundi kubwa lililoathirika kwa kutazama picha za pono, piacha au video za ngono huleta msukumo kwenye akili ili kuweza kujiridhisha na hivo hupelekea watu kupiga punyeto ili kukata ile kiu ya  tamaa zao za mwili.

Shilole Achoshwa na Wanaomdhalilisha Mitandaoni

$
0
0

Msanii wa muziki nchini Tanzania, Zuwena Mohamed 'Shilole' amefunguka na kusema kuwa amechoshwa na mtu ambaye anajiita na kutumia jina la mume wake Uchebe na kumchafua kwenye mitandao ya kijamii kwa kuweka posti za kumdhalilisha mumewe.

Shilole amesema hayo kupitia mtandao wake wa Instgram na kudai kuwa Uchebe feki huyo amekuwa akiharibu muonekane wa mume wake kwa jamii kutokana na jumbe mbalimbali ambazo anaziweka kwenye mtandao huo.

"Plzzz plzzz nimechoka na huyo uchebe feki 'walah' ananiharibia muonekano wa mume wangu maana hana maneno haya lol! Mashabiki wangu naomba muipuuze hii acount! Acount ya mume wangu ni @uchebe1 hana fans wala nini" aliandika Shilole

Mbali na Shilole Mkuu wa Kitengo cha Habari na Mawasiliano cha Klabu ya Simba SC, Haji Manara pia ameonekana kukerwa na jambo hilo na kusema kuwa anashindwa kuelewa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) kwanini inashindwa kuchukua hatua kwa watu ambao wanatumia majina ya watu wengine kwenye mitandao ya kijamii na kuwachafua watu kwa kuwa hata yeye pia amekuwa akifanyiwa mchezo kama huo ambao mume wa Shilole Uchebe anafanyiwa.

Wolper Afunguka Pesa itayogharimu Harusi yake

$
0
0
Mwanadada mwanamitindo na mwigizaji maarufu nchini, jackline Wolper Massawe ametangaza makubwa ujio wa ndoa yake inayotarajiwa kufanyika hivi karibuni mara baada ya kuwa tayari ameshatolewa mahali.

Wolper amedai kuwa ndoa hiyo inatarajia kugharimu kiasi cha shilingi milioni 60 za kitanzania, ikiwa milioni 50 kutumika kwa ajili ya harusi itayofanyika Dar huku milioni 10 kutumika harusi itayofanyika Marekani.

“Milioni kama 50 zitatumika kwenye sherehe ya hapa Bongo na nyingine 10 nje kwa sababu kule Marekani hatutakuwa na watu wengi sana,” alisema Wolper.
Akizungumza hayo pindi alipohojiwa na moja ya chombo cha habari mjini , Wolper amesema kuwa kwenye harusi inayotarajiwa kufanyika Marekani anatarajia kusindikizwa na wasanii wanne akiwepo Anty Ezekiel, huku wengine watatu bado hawajajulikana kwa majina yao.

‘’Wasanii ambao nitaenda nao kwa ajili ya kuhudhuria harusi yangu ni wanne tu, mmoja kati yao ni Aunt Ezekiel kwa sababu huwa ananipa sapoti kwenye biashara zangu hivyo siwezi kumwacha,” alisema Wolper

Wolper amesema kuwa gharama zote za wasanii watao msindikiza zitaakuwa juu yake yaani kuanzia usafiri wa hapa nchini hadi pesa yao ya kujikimu pindi wawapo nchini Marekani.


Dar 24
Viewing all 104785 articles
Browse latest View live




Latest Images