Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104417 articles
Browse latest View live

Shilole Atoa ya Moyoni..Hata Malaya Huwa Wanaolewa

0
0
MSANII wa muziki wa mduara, Zuwena Mohammed maarufu kwa jina la Shilole ametoa kauli ngumu wakati wa sherehe yake iliyofanyika usiku wa kuamkia jana Jumatatu, akisema watu wengi walikuwa wakidhani kwamba hamaanishi kuhusu kufunga ndoa na mpenzi wake Uchebe na kuwataka sasa waamini uamuzi wake huo.

“Namshukuru Mungu nimepata mume anayeijua dini, amenifichia aibu yangu. Watu wasidhani kila jambo ni utani, mimi nilikuwa namaanisha. Sasa waelewe kwamba hata ‘kicheche’ huwa anaolewa, wasichukulie maisha yangu niliyokuwa ninaishi, kwa sasa nimepata mume na ninampenda sana,” alisema Shilole.

VIDEO:


Miujiza ya Sharifu Seif Mohamed..JE Umeachwa na Mme/Mke au Mpenzi, Umesongwa na Mitihani ya Maisha..Piga Simu Upate Muujiza Wako

0
0
SHARIFU SEIF MOHAMED ANAWASHUKURU WALE WOTE WANAOENDELEA KUPIGA SIMU, WENYE MATATIZO NA WALE WANAOTOA  SHUKRANI NA SHUHUDA JINSI TIBA ZAKE ZINAVYO WASAIDIA,

(Rudisha mahusiano yako ndani ya masaa 72 tu)

SHARIFU MOHAMED Ni  mtaalam na mnajimu maarufu wa nyota na kubashiri mambo yanayo watesa binadamu duniani kote na kupata ufumbuzi, Anatumia kitabu cha QUR'AN, Dawa za Asili, Dawa za Kiarabu na majini kwa kumtuliza mke/mme, mchumba au mpenzi ndani ya masaa 72 tu, na kutatua matatizo yote ya kimaisha,

Je Umeachwa na UMPENDAE awe Mme/Mke na bado unampenda? Je Umekimbiwa na Mmeo/ Mkeo n anaishi na mtu mwingine? Je Umejaribu sehemu nyingi bila mafanikio? Mpigie simu SHARIFU SEIF sasa hivi ujionee Muujiza wa Papo kwa Papo, Anauwezo wa hali ya juu wa kusambaratisha mahusiano yao na kumrejesha kwako haraka sana na Kumfanya Atimize Ahadi zote Ndani ya Muda Mfupi Endapo Utafwata Atakacho Kuelekeza

ANAZO DAWA ZA MAPENZI, NGUVU ZA KIUME, CHANGO NGIRI MAJI NA N.K, ZINDIKO LA NYUMBA NA BIASHARA, PETE ZA BAHATI, HUMALIZA KABISA TATIZO LA NGUVU ZA KIUME NA KUREFUSHA UUME KWA SAIZI UNAYOTAKA, HUZUIA CHUMA ULETE KWENYE BIASHARA, HURUDISHA MALI ZILIZOPOTEA, MAGONJWA SUGU, MIGUU KUWAKA MOTO AU KUFA GANZI, HUTIBU BUSHA BILA KUPASUA, ANAO UWEZO WA KUMRUDISHA ALIE MBALI AU ALIECHUKULIWA MSUKULE, KUPANDISHA NYOTA NA KUSHINDA BAHATI NA SIBU, KASAFISHA NYOTA NA KUKUPA MVUTO WA AJABU, KUTOA NUKSI NA VIFUNGO MBALIMBALI,  MAFANIKIO YA MAISHA NA UTAJIRI BILA MASHARI, NA MENGINE MENGI YA SIRI,

Je UMAHANGAIKA KUPATA MTOTO BILA MAFANIKIO? WASILIANA NA MTAALAMU HUYU KWANI YEYE HUFAULU PALE WOTE WALIPOSHINDWA, PIA UMALIZA KAZI ZILIZO SHINDIKANA NA WATAALAM WENGINE NDANI YA MASAA 24 TU,

(NA ANATIBU KWA NJIA YA SIMU UKIWA NCHI YOYOTE AU MKOA WOWOTE ENDAPO UTAFWATA MAELEKEZO YAKE)

Kwa ushauri na mawasiliano  zaidi Piga SIMU No:

Mobile +255 654-836970
WhatsApp +255 756-033670

Maskini Johari! Apata Pigo Afiwa na Mama Yake

0
0
Maskini Johari!  Apata Pigo Afiwa na Mama Yake
Muigizaji wa sinema za Kibongo, Blandina Chagula ‘Johari’ amepata pigo kwa kuondokewa na mama yake mzazi. Mungu ailaze roho ya mama Johari mahala pema peponi, Amina.

Habari Kuwajia baadae.

Amba Lulu nAfukunguka Pona Yake kwa Waziri Shonza

0
0
Amba Lulu nAfukunguka Pona Yake kwa Waziri Shonza
Amber Lulu amedai kuwa rungu la kuitwa na Naibu Waziri wa Habari, Sanaa utamaduni na Michezo, Mh. Juliana Shonza ni kutokana na kuwa watu walishamtoa kwenye kundi la wakaa utupu mitandaoni na kumuweka kwenye kundi la wasanii.


Kupitia 5Selekt ya EATV  Amber Lulu amesema kwamba baada ya kuingia kwenye muziki aliamua kufuta picha zote ambazo hazikuwa zikimtambulisha kama msanii.

"Mimi nimeshatoka kwenye lile kundi. Sikutajwa kwasababu watu wameshanitoa  kabisa kwenye Amber yule na wanamjua huyu wa sasa ambaye anaimba. Hata kwenye mitandao yangu ya kijamii ukipitia hutakutana na picha za miaka ile" Amber Lulu.

Amber Lulu aliingia rasmi kwenye sanaa ya muziki mwishoni mwa 2016,  akiachana na sanaa ya upendezeshaji wa nyimbo za wasanii 'Video Vixen'.

Hivi karibuni Msanii wa karibu na Amber Lulu aliitwa na Naibu Waziri Shonza kwenda ofisini kwake kutokana na kuvunja maadili kwa kupiga picha za utupu  na kuziweka katika mitandao yake ya kijamii.

Mahabusu Wanaotuhumiwa na Kesi za Ugaidi Wazua Tafrani Wavua Nguo Mahakamani

0
0

Mahabusu Wanaotuhumiwa na Kesi za Ugaidi Wazua Tafrani Wavua Nguo Mahakamani
Baadhi ya mahabusu wanaokabiliwa na tuhuma za ugaidi, jana walizua tafrani katika viwanja vya Mahakama ya Hakimu Mkazi jijini hapa baada ya kuvua nguo wakipinga kuchelewa kukamilika kwa upelelezi wa kesi zao.

Waliovua nguo ni kati ya watuhumiwa 61 wanaokabiliwa na tuhuma hizo za ugaidi na ambao wako katika Gereza la Kisongo.

Kabla ya kushuka kutoka kwenye karandinga baada ya kufika mahakamani hapo saa 3:30 asubuhi, baadhi yao walivua nguo na kusababisha utaratibu wa kuwapeleka chumba cha mahabusu kabla ya mahakamani kuingia dosari.

Askari Magereza walilazimika kuimarisha ulinzi mahakamani hapo huku wakiendelea na jitihada za kuwataka wavae nguo zao lakini waligoma na hivyo kulazimika kuwapeleka chumba hicho wakiwa hawajavaa chochote.

Baada ya kuwafikisha mahabusu na kuwaacha huko, askari hao waliwachukua watuhumiwa ambao hawakuwa wamevua nguo na kuwapeleka mahakamani kusikiliza shauri lao.

Pamoja na kufanya kituko hicho kupinga kucheleweshwa kwa upelelezi, hakimu mkazi wa mahakama hiyo, Patricia Kisinda aliahirisha kesi hiyo hadi Januari 30 kutokana na upelelezi kutokamilika.

Mara baada ya kuahirisha shauri hilo watuhumiwa hao walirudishwa ndani ya chumba cha mahabusu ambako walikaa humo kwa muda na wenzao waliokuwa wamevua nguo kabla ya kupandishwa  kwenye  karandiga kurejea Kisongo.

Mbali na kutuhumiwa kujihusisha na vitendo vya kigaidi, baadhi yao wanatuhumiwa kutoa msaada wa fedha kufadhili mpango huo.

Watuhumiwa 13 wanadaiwa kufanya mauaji na kujaribu kuua. Wanatuhumiwa kuwa mwaka 2014 waliwaua Judith Mushi, Ramadhan Juma, Fahad Jamal na Amir Daffa katika Uwanja wa Soweto, Arusha.

Wengine 10  wanatuhumiwa kukusanya zana, yakiwamo mabomu na kuzisambaza kati ya Julai 22 na 23, 2015 kwa lengo la kufanya ugaidi.

Wanne wanatuhumiwa kummwagia tindikali Mustapha Kiago kati ya Julai 2009 na Julai 2013 katika eneo la Msikiti Mkuu wa Arusha na kumsababishia majeraha.

Washtakiwa wengine wanne wanatuhumiwa kutupa bomu la kienyeji nyumbani kwa Sheikh Abdulkarim Njonjo kati ya Oktoba Mosi na 25, 2012 na kumsababishia majereha mwilini. Wengine watatu katika kesi hiyo wanatuhumiwa kushawishi vijana kujiunga na kikundi cha ugaidi cha Al-Shabaab, vitendo wanavyodaiwa kuvifanya kati ya Machi 8 na Julai 14, 2014.


Watu Walijua ni Utani Sasa Waelewe Hata Kicheche Anaolewa- Shilole

0
0
Watu Walijua ni Utani Sasa Waelewe Hata Kicheche Anaolewa- Shilole
MSANII wa muziki wa mduara, Zuwena Mohammed maarufu kwa jina la Shilole ametoa kauli ngumu wakati wa sherehe yake iliyofanyika usiku wa kuamkia jana Jumatatu, akisema watu wengi walikuwa wakidhani kwamba hamaanishi kuhusu kufunga ndoa na mpenzi wake Uchebe na kuwataka sasa waamini uamuzi wake huo.

“Namshukuru Mungu nimepata mume anayeijua dini, amenifichia aibu yangu. Watu wasidhani kila jambo ni utani, mimi nilikuwa namaanisha. Sasa waelewe kwamba hata ‘kicheche’ huwa anaolewa, wasichukulie maisha yangu niliyokuwa ninaishi, kwa sasa nimepata mume na ninampenda sana,” alisema Shilole.

Jeshi la Polisi Lamkamata Mtuhumiwa Aliyeua Mkewe na Kichanga kwa Jembe

0
0
Jeshi la Polisi Lamkamata Mtuhumiwa Aliyeua Mkewe na Kichanga kwa Jembe
JESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limemtia mbaroni Ami Lukule, anayedaiwa kuwaua mke na mtoto wake kichanga cha umri wa miezi minane na mdogo wake wa kike, katika eneo la Matosa Darajani, Goba wilaya ya Kinodnini jijini Dar es Salaam wiki chache zilizopita.

Akizungumza na wanahabari leo Januari 16, 2017 jijini Dar es Salaam, Kamanda wa Polisi Kanda Maalumya Dar, Lazaro Mambosasa amemsema mtuhumiwa huyo alikamatwa hivi karibuni mkoani Iringa.

“Mtuhumiwa huyo tayari tumeshamkamata na baada ya kumhoji alikiri kufanya tukio hilo na kusema chanzo alikuwa mtoto. Amedai mkewe huyo alimtilia mashaka kwa kuingia kwenye mahusiano na mwanammme mwingine, anadai mke huyo alimzalia mtoto nje ya ndoa, hivyo akaamua kumnyonga mtoto na kufanya mauaji mengine mliyoyasikia,” alisema Mambosasa.

Aidha, Kamanda Mambosasa amesema kwa sasa wanafanya taratibu za kumsafirisha mtuhumiwa huyo kutoka Iringa hadi Dar ili kufikishwa mahakamani.

Ronaldinho Gaucho Atangaza Kustaafu Kucheza Soka

0
0
Ronaldinho Gaucho Atangaza Kustaafu Kucheza Soka
Mchezaji wa soka wa kimataifa wa Brazil Ronaldinho Gaucho leo ametangaza rasmi kustaa kucheza soka la ushindani baada ya kudumu katika soka la ushindani kwa zaidi ya miaka 15, Ronaldinho amefikia maamuzi hayo baada ya kucheza soka kwa muda mrefu na sasa anaamini inatosha.

Ronaldinho hadi anatangaza kustaafu kucheza soka akiwa na umri wa miaka 37, amecheza vilabu zaidi ya saba toka aanze kucheza soka vikiwemo vilabu vya Paris Saint Germain ya Ufaransa, FC Barcelona na AC Milan.

Kama hufahamu Ronaldinho alizaliwa mwaka March 21 1980 Porto Alegre kwao Brazil na alinza kucheza soka katika timu ya vijana ya Gremio 1987, jina lake halisi ni Ronaldo lakini aliitwa Ronaldinho kutokana na kuwa na umbo dogo kuliko wote katika timu ya vijana aliyokuwa anacheza wakati huo akiwa na umri wa miaka 8.

Ronaldinho alianza kuingia kwenye headlines za vyombo vya habari akiwa na umri wa miaka 13, hiyo ni baada ya kufanikiwa kuipatia ushindi timu yake wa magoli 23-0 lakini magoli yote 23 alifunga yeye, hivyo nyota yake ya kuja kuwa staa wengi wanaamini walianza kuiona mapema.

Wasichana Waliotekwa na Boko Haram Wagoma Kurudi Nyumbani

0
0
Wasichana Waliotekwa na Boko Haram Wagoma Kurudi Nyumbani
Kundi la wanamgambo wa Kiislamu la Boko Haram limerusha mkanda wa video mpya unaoonyesha wanafunzi kumi na nne wasichana waliotekwa katika mji wa Chibok, Kaskazini mwa Nigeria, mwezi April 2014.

Mmoja kati ya wasichana hao ameongea kwa niaba ya wenzake namnukuu “Sisi ni wasichana wa chibok, kwa uwezo wa Mungu, hatutorudi, tunawasikitikia wasichana wenzetu ambao waliamua kurudi nyumbani. Mungu aliwabariki na kuwaleta kwa Khalifa (sehemu takatifu) lakini badala yake, waliamua kurudi katika uovu “

Huu ni mkanda wa kwanza wa video unaowaonesha wasichana wa Chibok ukiachilia mbali uliotoka mwezi May 2017, ulioonyesha msichana mmoja akisema yeye ni miongoni mwa wanafunzi 219 waliotekwa katika mji wa Chibok, alionekana ameshika bunduki na yeye pia alikataa kurudi nyumbani.

Hakuna kitu kinachoonyesha muda au mahali video hiyo iliporekodiwa, wala kuonyesha kuwa wasichana hao wamelazimishwa kufanya hivyo.

Msichana huyo pia amewaambia wazazi wake: “mnapaswa kutubu, moto wa Jahannamu ni makazi yenu ikiwa hamtotubu, kwa sababu Allah ametuumba ili tumuabudu”.

Pia amemshukuru kiongozi wa kundi la Boko Haram, “baba yetu Abubakar Shekau, ambaye alitutoa huko, tunaishi katika faraja , Abubakar Shekau ni kiongozi wetu”.

Shekau ambaye alidaiwa mara kadhaa kuwa amefariki, pia ameonekana kwenye video hiyo, akirusha risasi kwa ktumia bunduki kubwa ya kivita kabla ya kuongea ambapo aliongea kwa dakika 13.

Jumla ya wasichana 276 walikamatwa mwezi April 2014 katika shule yao ya sekondari huko Chibok, katika jimbo la Borno, na kusababisha manung’uniko kwa watu wa mataifa mbalimbali

Soma Nafasi za Ajira Zilizotangazwa Leo

Baba Awapa Adhabu ya Ajabu Watoto Wake.

0
0

Mwanamume mmoja ametoroka nchini Burundi baada ya kuwapa adhabu ya kikatili watoto wake wawili ambao inadaiwa aliwapata wakiiba mahindi kwenye shamba lake.

Mwanaume huyo aliwazika ardhini wanawe wawili hadi sehemu ya vifua kabla ya kuwachapa viboko.

Walibahatika kuokolewa na mpita njia ambaye alikuwa jirani yao .

Kulingana na taarifa ya mwandishi wa BBC Prime Ndikumagenge kutoka Bujumbura.

Tukio hilo la ajabu lilitokea katika kijiji cha Bubanza, mkoa wa kaskazini magharibi mwa mji mkuu Bujumbura Jumapili jioni.

Taarifa zinasema watoto hao wenye umri kati ya miaka 8 na 10 walikamatwa wakiwa wanaiba katika shamba la mahindi.

Mmiliki wa shamba hilo aliamua kuchimba mashimo mawili na kumzika kila mmoja wao hadi usawa wa vifua vyao na kuanza kuwatandika viboko.

Wakazi wa eneo hilo wanasema kuwa hawajui ni nini kingetokea kwa watoto hao kama jirani yao asingepita.

Mwanaume huyo kisha alitoroka na watoto hao wakaokolewa.

Polisi wanasema bado wanamsaka mwanaume huyo kwa ajili ya kumfikisha mbele ya sheria.

Si mara ya kwanza kwa tukio la aina hii la kikatili dhidi ya watoto kufanyika nchini Burundi.

Watoto wawili walikatwa mikono yao ya kushoto katika jimbo la kati la Gitega mwezi Novemba mwaka jana baada ya kupatikana wakiiba mahindi



Chanzo: BBC Swahili

Hii Hapa Kauli ya Jokate kuhusu kugombea CCM

0
0

Mjasiriamali na Mwanamitindo maarufu Bongo, Jokate Mwegelo amesema hana mpango wa kugombea nafasi yoyote ya uongozi ndani ya Chama cha Mapinduzi (CCM).

Jokate ameiambia Clouds Fm kuwa anachofanya sasa hivi ndani ya chama hicho ni kuhamasisha ili kiweze kuwasaidia wananchi wa Kitanzania kwa ueledi na kwa usahihi.

“Tunajitolea kwa ajili ya chama naamini kuwa chama ndio serikali, kwa hiyo mimi nasaidia tu, naishia hapo, ni mapenzi wangu kwa vijana,” amesema.

Kuhusu kugombea nafasi yoyote ya uongozi ndani CCM, alijibu, “Sijui, haipo kwenye plan, haipo kwenye ramani yangu,”.


Moni Amfungukia Roma

0
0


Msanii wa muziki wa Hip Hop, Moni Centrozone amedai kwamba Roma Mkatoliki hana mchango wowote katika maisha yake ya muziki kama watu wanavyofikiria.

Rapa huyo kutoka Dodoma, amesema kwamba hawezi kumzungumzia Roma kwa jinsi yoyote kwenye sanaa yake na hata kolabo watu wanayofikiria kuwa ilimpa msaada wa kumtambulisha wanakosea kwani haijam[patia lolote zaidi ya dhahama.

Majibu hayo ya ku-‘panick’ yaliyotolewa na Moni yallikuja baada ya kuulizwa na mtangazaji wa kipindi hicho kama yeye na Country Boy wameamua kuanzisha muungano waliouita (MoCo) ili kushindana na muungano wa ROSTAM unaoundwa na Roma na Stamina na kudai yeye hashindani na watu hao bali yupo kwenye muziki kwa ajili ya kushindana na wasanii.

Moni ameendelea kusema mtu pekee ambaye anayemkumbuka na hawezi kumsahau katika sanaa yake miaka yake yote ni Marehemu Langa kwa kuwa ndo msanii ambaye aligundua kipaji chake na kumchukua kutoka kijijini kisha kumleta mjini kwa ajili ya kurikodi nyimbo na mapaka leo watu wanamtambua.

“Who is Roma kwenye maisha yangu. Mimi simfahamu na wala hajawahi kuntoa kwenye muziki kama jinsi watu wanavyoodhani. Mimi namjua Langa aliyenichukua uswahilini kwetu na kunileta mjini. Sipendi kutajiwa majina ya watu wasio na umuhimu na mimi” alikiambia kipindi cha Enewz cha EATV.

Mbali na hayo Moni amesema kwamba kundi lao MoCo’ haliwazuii kufanya nyimbo zao binafsi kama ‘solo artist’ na kusema kundi lao limewaunganisha ili kuweza kuleta changamoto kwa wasanii wote ambao wanafanya mziki sawa na wakwao na hawajamlenga kundi wala mtu yeyote.

Mapema mwaka jana Moni alimshirikisha Roma wimbo wake ambao ulimtambulisha zaidi kwenye ‘game’ ya Bongo kisha kumpatia mashabiki kibao na baadae mahusiano yao yakaonekana kuingia dosari pale mwezi Aprili wasanii hao walipotekwa na watu wasiojulikana kisha kuachiwa baada ya siku tatu na baada ya miezi kadhaa Roma akaachia wimbo aliouita ‘Zimbabwe’ ambao ulipata mapokeo makubwa na baadaye Moni kukasirika kwamba kwa nini Roma ameamua kutumia Idea ya kutekwa kwao na kufanya kama tukio hilo lilimtokea yeye binafsi na kumbe liliwapata watu wanne. (Roma, Moni

Kesi ya Agnes Masogange Yakwama

0
0

Upande wa mashtaka katika kesi ya  kutumia dawa za kulevya inayomkabili Agnes Gerald maarufu kama ‘Masogange’ umeiomba Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, kuwaonya  upande wa utetezi kwa kushindwa kutoa ushahidi  wao  kwa mara ya tatu mfululizo.

Hatua hiyo imekuja baada ya wakili wa utetezi, Nehemia Nkoko kudai mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Wilbard Mashauri kuwa wakili mwenzake, Reuben Simwanza ndiye aliyeandaa mashahidi na kwamba ameshindwa kutokea kwa kuwa anaumwa.

Wakili wa Serikali, Constantine Kakula alitaka upande huo uonywe leo Jumatano baada ya shauri hilo kufikishwa mahakamani hapo kwa ajili ya kuendelea na ushahidi.

Kutokana na hali hiyo, Wakili Nkoko amesema atahakikisha anaandaa mashahidi ili itakapotokea wakili mmoja hayupo, mwengine aendelee na shauri.

"Hatuna pingamizi na sababu zilizotolewa na upande wa utetezi lakini tunaomba  Mahakama itambue kuwa ni mara ya tatu kwa upande wa utetezi inaahirishwa kesi hii? Amesema wakili wa Kakula na kuongeza;

"Mawakili wapo wengi lakini wanashindwa kuendelea kutoa ushahidi wao wa upande wa utetezi basi kama hawawezi, waache mshitakiwa aendelee na kesi mwenyewe."

Kutokana na hali hiyo, upande wa mashtaka umeomba ahirisho la mwisho kwa sababu kesi ni ya muda mrefu.

Hakimu Mashauri aliahirisha kesi hiyo hadi Januari 26, mwaka huu  kwa ajili ya kusikilizwa.

Masogange ataanza kujitetea baada ya Mahakama kumkuta na kesi ya kujibu baada ya kusikiliza mashahidi watatu wa upande wa mashitaka.

Rais Magufuli Akutana na Waziri wa TAMISEMI, Selemani Jafo Na Kupiga Marufuku Michango Yote Shuleni

0
0

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli leo Januari 17, 2018 amepiga marufuku aina yoyote ya michango katika shule za Serikali za msingi na Sekondari na kuwaagiza Mawaziri Jafo na Ndalichako kusimamia hilo.

Magufuli amepiga marufuku hiyo hiyo leo alipokutana na Waziri Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Mhe. Selemani S. Jafo na Waziri wa Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi Profesa Joyce L. Ndalichako Ikulu jijini Dar es salaam na kuwataka mawaziri hao kwenda kusimamia jambo hilo na kuhakikisha hakuna michango yoyote wanafunzi au wazazi wanachangishwa kwenye shule za sekondari.



BRELA yaleta mfumo mpya wa kusajili biashara na Makampuni Tanzania

Maulid Mtulia Achukuwa Form Tayari Kugombea Ubunge Kinondoni

0
0

Dar es Salaam. Aliyekuwa mbunge wa Kinondoni (CUF), kisha kuhamia CCM, Maulid Mtulia leo Januari 17, 2018 amechukua fomu ya kuomba kuteuliwa kuwa mgombea wa jimbo hilo kwa tiketi ya chama tawala.

Amechukua fomu hizo hizo za Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) katika ofisi za manispaa yaKinondoni.

Hatua hiyo imekuja baada ya siku nane zilizopita Mtulia kutii agizo la chama hicho lililomtaka kuripoti ofisi ya CCM mkoa kwa ajili ya kuchukua maelekezo ya uchaguzi.

Hivi karibuni CCM kilitangaza kuwarudisha kugombea majimbo yao waliokuwa wabunge, Mtulia wa Kinondoni na Dk Godwin Mollel (Siha-Chadema) ambao wamejiunga na chama hicho tawala.

Mtulia alipoulizwa nini ambacho anawaeleza wananchi wa Kinondoni, amesema siku ikifika atazungumza mengi.

Uchaguzi mdogo wa marudio wa majimbo ya Kinondoni na Siha unatarajiwa kufanyika Februari 17 baada ya NEC, kupokea barua kutoka kwa Spika wa Bunge Job Ndugai ikieleza majimbo hayo yapo wazi.


Swali la mwandishi wa CCN lamkera Trump

0
0


Rais Donald Trump alichukizwa na maswali ya mwandishi wa kituo cha televisheni cha CNN, Jim Acosta aliyeuliza mara kwa mara kuhusu kauli yake ya kuita mataifa ya Afrika kuwa ni machafu.

Mwishoni mwa hafla ya pamoja na Rais Nursultan Nazarbayev wa Kazakhstan, Trump aliulizwa na Acosta kama alisema katika mkutano wa chama chake kuwa anapendelea zaidi wageni kutoka Norway.

"Nawataka waje kutoka kila sehemu. ...Asante sana," Trump said, wakati maofisa wa Ikulu ya Marekani wakiwataka waandishi kutoka nje.

Baadaye Acosta akamuuliza Trump kama anapendelea wahamiaji kutoka nchi za watu weupe au wa jamii ya kihindi.

"Nje," alijibu Trump, akionyesha kidole sehemu ya kutokea wakati mkutano huo na waandishi ukiisha.

Trump na Acosta walipambana tena mwaka mmoja uliopita baada ya kuchapishwa kwa nyaraka kuhusu uhusiano wa Trump na Russia, huku Trump akisema "nyinyi ni habari za kubuni."


Mwananchi

Kwa Nini Wanaume Wengi Wanaupungufu Wa Nguvu Za Kiume Na Maumbile Madogo?

0
0
Asilimia 45 ya wanaume wapo tofauti na wengine kwa kuwatimizia vyema wake au wapenzi Wao na kuwasababishia kutoka nje ya ndoa zao.


NINI CHANZO CHA HAYO?Kupiga punyeto,Ngiri,Vidonda vya tumbo,Magonjwa ya moyo,Presha,Kisukari,Korodani moja kuvimba,Msongo wa mwazo,Kufanyiwa tohara ukiwa mtu mzima n.k.DOKTA MANYANDA sasa kapata tiba sahihi ya tatizo la NGUVU ZA KIUME.


MUHAMA:Hii hutibu na kuponyesha kabisa tatizo la nguvu za kiume,utakuwa na uwezo wa kurudia tendo zaidi ya mara tatu bila kuchoka na itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa mda wa dakika 15-20.DAWA hii imechanganywa miti 12.Hata wazee wenye umri mkubwa wanapona kabisa.OKO NDOA YAKO SASA.


MANGUNGU MIX: Ndio tiba tosha kwa sasa ambayo hurefusha na kunenepesha uume saizi uipendayo inch 1-8 na unene sentimita 1-5,dawa hii ipo ya kupaka na kunywa na haina madhara yoyote kwa mtumiaji.


NITOFAUTI NA ULIZO WAHI KUZITUMIA.Pia tuna dawa za kupatanisha mke,mme,mpenzi au bosi wako kwa mda mfupi sana,Uzazi,Kusafisha nyota,


Je unamali yako unauza hupati wateja?

Wasiliana nami 0716-263605


DOKTA MANYANDA ANAPATIKANA KASULU KIGOMA,Kwa wale wa mikoani huduma hii utaipata popote pale

Yanga Yalalamika Simba inabebwa

0
0
Klabu ya Yanga kupitia kwa Katibu Mkuu wake wamelalamikia kutokuwepo na usawa kwa Simba na yanga katika matumizi ya viwanja vya Uhuru na ule wa Taifa.

Mkwasa amesema, Yanga kesho inatakiwa kucheza kwenye uwanja wa Uhuru mchezo wake wa ligi kuu Tanzania bara dhidi ya Mwadui FC ya Shinyanga wakati Simba wao watatumia uwanja wa taifa siku ya Alhamisi kwenye mechi yao ya ligi kuu dhidi ya Singida United hivyo amesisitiza kuwepo na usawa kati ya vilabu hivyo juu ya matumizi ya viwanja tajwa.

Kuna wakati bodi ya ligi ilitangaza kuwa, Simba na Yanga zitatakiwa kucheza mechi zao kwenye uwanja wa Azam Complex kupisha shughuli za kiserikali siku ambazo timu hizo zingeutumia uwanja wa Uhuru kwa mechi zao, badala yake yanga ilicheza azam complex mchezo wake dhidi Tanzania Prisons lakini mechi ya Simba ikachezwa kwenye uwanja wa Uhuru.

“Tunatambua kwamba uwanja wa Taifa ulikuwa katika matengenezo na haujatumika kwa muda mrefu lakini kwa sasa unaonekana umekamilika, tulijaribu kuomba tuweze kuutumia lakini tumekosa hiyo fursa na tumepata taarifa kwamba kuna baadhi ya mechi zitachezwa poale lakini sisi mechi yetu ya kesho (Jumatano) itachezwa uwanja wa Uhuru.”

“Tulitegemea tungeanza kucheza pale lakini tunakosa hiyo fursa sasa inatupa shida upande wetu tunaonekana kama hatupewi thamani au umuhimu.”

“Nakumbuka mechi yetu na Prisons yanga ilicheza Jumamosi, Simba wakacheza Jumapili lakini sisi tukacheza kwenye uwanja wa Azam Complex  Simba wakacheza uwanja wa Uhuru kwa hiyo sisi tukakosa hiyo fursa, hii ni mara ya pili inakuwa wenzetu wanaanza kucheza na Singida Alhamisi kwenye uwanja wa taifa sisi kesho tumeambiwa tunacheza uwanja wa Uhuru.”

“Sasa angalieni namna gani hakuna usawa katika mambo kama haya, sisi tunaomba kuwepo na usawa kwa sababu hizi timu zote ni za watanzania wazalendo, kama kuna haki basi itolewe kwa sawa kwa vilabu vyote kuliko kubagua kwamba timu hii inatumia uwanja fulani hii inakosa fursa.”
Viewing all 104417 articles
Browse latest View live




Latest Images