Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104709 articles
Browse latest View live

Takukuru Yamchukua Kaburu Mahakamani Ili Kumuhoji

$
0
0
Takukuru Yamchukua Kaburu Mahakamani Ili Kumuhoji
Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) imemchukua Makamu wa Rais wa klabu ya Simba, Godfrey Nyange ‘Kaburu’ anayekabiliwa na kesi ya utakatishaji fedha wa USD 300,000 katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kwa ajili ya kumuhoji.

Mbali ya Kaburu, mshtakiwa mwingine ni Rais wa Klabu hiyo, Evans Aveva ambaye hakufika mahakamani hapo.

Mwendesha Mashtaka wa TAKUKURU, Leornad Swai amemueleza Hakimu Mkazi Mkuu, Victoria Nongwa kwamba kesi hiyo haikupangwa leo isipokuwa wamemtoa Kaburu gerezani kwa kibali ili akahojiwe.

Baada ya kueleza hayo, Hakimu Nongwa alimkabidhi Kaburu kwa Wakili Swai huku akimtaka amrudishe leo kama alivyoomba, ambapo aliahirisha kesi hiyo hadi tarehe iliyopangwa January 25,2018.

Aveva na makamu wake, Geofrey wanakabiliwa na mashtaka matano ya kughushi, kuwasilisha nyaraka ya uongo na kutakatisha fedha USD 300,000.

Washtakiwa hao wanadaiwa kuwa walikula njama ya kughushi fomu ya maombi ya kuhamisha fedha ya Machi 15, 2016 wakionesha Klabu ya Simba inalipa mkopo wa USD 300,000 kwa Evans Aveva wakati si kweli.

Afya ya Tundu Lissu Yaendelea Kuimarika

$
0
0
Afya ya Tundu Lissu Yaendelea Kuimarika
Afya ya Mbunge wa Singida Mashariki (Chadema), Tundu Lissu, ambaye anaendelea na matibabu nchini Ubelgiji, inazidi kuimarika na sasa anaweza kufanya mambo mengi mwenyewe ikiwamo kwenda kuoga na kutembea kwa kutumia magongo.

Lissu ambaye pia ni Rais wa Chama cha Mawakili wa Tanganyika (TLS), alipelekwa Ubelgiji Januari 7, mwaka huu, akitokea Hospitali ya Nairobi nchini Kenya alipokuwa akipatiwa matibabu tangu Septemba 7, mwaka jana.

Mbunge huyo aliumia vibaya baada ya kushambuliwa kwa risasi 32 na watu wasiojulikana nyumbani kwake mjini Dodoma Septemba 7, mwaka jana, tano kati ya hizo zikimpata katika maeneo mbalimbali ya mwili.

Vinceti Mghwai, ambaye ni mdogo wa Lissu, alisema  jana kuwa Lissu ameanza kutembea mwenyewe kwa kutumia magongo na kujipatia huduma mbalimbali ikiwemo kwenda kuoga bila msaada wa mtu mwingine.

"Tunamshukuru Mungu sana, Lissu anaendelea vizuri... tangu ameanza kupatiwa matibabu na mazoezi ya viungo tunaona mabadiliko makubwa mno," alisema na kueleza zaidi:

"Maendeleo ni makubwa sana, kuna vitu alikuwa hawezi kuvifanya lakini sasa anaweza kuvifanya mwenyewe kama kuoga. Siku za nyuma alikuwa akipelekwa maliwatoni lakini sasa hivi anatembea na magongo mwenyewe kwa kukanyagia mguu chini.

"Anakula mwenyewe.Tunaamini atatengamaa mapema zaidi, (na) haya kwetu ni maendeleo makubwa."

Mghwai alisema Lissu anapata muda mwingi wa kupumzika na huenda hiyo ndiyo ikawa sababu kubwa ya yeye kuendelea kupona haraka kutokana na kupatiwa matibabu na bila usumbufu wowote.

Alisema Lissu anapata matibabu katika mazingira tulivu tofauti na alipokuwa Hospitali ya Nairobi ambako alikuwa akisumbuliwa na makundi ya watu waliokuwa wakienda kumjulia hali.

"Kwa sasa ana muda wa kutosha kufanyiwa matibabu ya mazoezi, madaktari wanamfanyia mazoezi muda wote kwa sababu hakuna watu wanaokwenda kumuona na ndiyo sababu anaendelea kupona haraka," alisema Mghwai.

"Ubelgiji muda wote yuko na madaktari akipatiwa matibabu hasa mazoezi ya viungo... huku ni kazi kazi tu. Na madaktari waliahidi kufanya kazi.

"Kule Nairobi wakati mwingine alikuwa akiwaambia madaktari wamuache pale anaposikia maumivu wakati wa mazoezi lakini sasa hakuna kitu kama hicho na wamemwambia avumilie apone."

Kuhusu risasi iliyobakia kwenye nyonga, Mghwai alisema madaktari wa Ubelgiji hawataitoa na wataiacha kwa sababu walishaeleza kuwa haiwezi kuwa na madhara kwake kiafya.

"Kule Ubelgiji kazi kubwa ni kumfanyisha mazoezi ili sasa aweze kurejea katika hali yake na ndicho ambacho wanaendelea nacho na kwa kweli tumeanza kuona maendeleo makubwa."

Kuhusu gharama za matibabu, Mghwai alisema, zaidi ya Sh. milioni 100 zinatumika kila mwezi kwa ajili ya kumtibu na kwamba hadi sasa Bunge halijatoa fedha na familia inafuatilia lakini wamekuwa wakizungushwa huku na kule.

Alisema fedha zinazotumika kwa ajili ya matibabu yake ni zile zilizochangwa na wadau mbalimbali na wamekuwa wakifanya harambee kadhaa za kuchangia.

"Gharama ni kubwa sana kwa mwezi analipia zaidi ya milioni 100 katika hospitali hiyo na kama atakaa miezi miwili tutatumia zaidi ya milioni 200 na hizi ni fedha za matibabu pekee," alisema Mghwai.

Alieleza zaidi kuwa fedha zilizochangwa hazitoshi kumtibu Lissu na kwamba kwa sasa wadau wamesitisha kutoa michango baada ya tetesi kuwa serikali inagharamia matibabu yake.

Alisema familia inaendelea na juhudi za kuchangisha fedha zaidi ili kukamilisha matibabu yake.

"Tunaamini hakuna kitakachoharibika kwa sababu tumeshaweza kumponya tunaamini atakuwa mzima."

Alisema gharama kamili za matibabu na fedha zilizopatikana kwa ajili ya matibabu ya Lissu zinaweza kuzungumzwa katika vikao vya makubaliano na si yeye peke yake kuzungumzia.

Lissu ambaye Januari 6 alizungumza na waandishi wa habari akiwa nje ya Hospitali ya Nairobi, ikiwa ni siku moja kabla ya kusafiri kuelekea nchini Ubelgiji, alieleza kuwa alishambuliwa kwa risasi zaidi ya 20 na 16 zilimjeruhi maeneo mbalimbali ya miguu, mikononi na kwenye nyonga.

Lissu alisema kutokana na shambulio hilo alifanyiwa operesheni 17 zilizofanikisha kuondoa risasi saba zilizoingia mwilini huku risasi moja ikisalia.

Wataalam wa afya walimshauri kuiacha risasi hiyo iliyopo kwenye nyonga wakisema kuwa inaweza kuleta madhara zaidi kama watajaribu kuitoa.

Vanessa Mdee Kuinufaisha Familia ya Mubaraka Mwishehe

$
0
0
Vanessa Mdee Kuinufaisha Familia ya Mubaraka Mwishehe
Msanii wa muziki anayefanya vizuri kwa wanawake Bongo, Vanessa Mdee amebainisha ngoma ya ‘Pumzi ya Mwisho’ kuwa ni moja ya ngoma anayoikubali katika albamu yake ya Monday Money ambayo ina kionjo cha ngoma ya marehemu Mubaraka Mwishehe iitwayo ‘Jogoo la Shamba’
Vanessa amebaisha  kuwa kabla ya kutoa ngoma hiyo ya ‘Pumzi ya Mwisho’ aliyowashirikisha marapper wakali Joh Makini na Cassper Nyovest alifika nyumbani kwa marehemu Mubaraka Mwishehe na kuonana na familia yake ili aombe idhini ya kutumia kionja katika ngoma ya nguli huyo wa muziki wa dance pia kuona familia hiyo itanufaika vipi na mauzo ya ngoma hiyo.

“Pumzi ya mwisho ni wimbo ninao upenda sana kwenye ulbum yangu ya #MondayMondays. Ni moja kati ya nyimbo zangu bora kwenye album. Sababu kubwa ya Mimi kuchagua beat ya huu mwimbo ni kionjo kimoja kutoka kwenye wimbo wa hayati MBARAKA MWINSHEHE #Legend kabla ya album kutoka nikaona ni vema kuwaona familia ya MBARAKA kwanza ili nipate idhini ya kuendelea na kazi hiyo na kuona watanufaika vipi kama familia kupitika huo wimbo. Nashukuru walinipokea vizuri sana na walitoa idhini yao kwa mikono miwili kabisa.,” ameandika Vanessa katika mtandao wake wa kijamii wa Instagram.

Akaongeza “Nusu ya mauzo ya wimbo huu kwenye mitandao ya kidigitali yataenda kwenye familia ya Mzee Mwinshehe siku zote. Nisingeweza kukamilisha kazi hii bila mkono wa @s2kizzy producer, Sauti ya @CassperNvoyest kutoka #SouthAfricana Mwamba @johmakini asanteni sana. Kuna mengi tuliongea kuhusu mzee ya kusikitisha na kufurahisha pia unaweza kuona video yote ukiwa na #VeeMoneyApp inapatikana kwenye store zote #PlayStore na #AppStoreAsanteni sana #MoneyMondays#PumziYaMwisho.

Mahakamani: Rugemalila Hana Saratani na Puto la Sethi Limeisha Muda Wake.

$
0
0
Mahakamani: Rugemalila Hana Saratani na Puto la Sethi Limeisha Muda Wake.
Upande wa Mashtaka katika kesi ya uhujumu uchumi, utakatishaji fedha  na kuisababisha Serikali hasara, inayomkabili Mmiliki wa Kampuni ya Kufua Umeme ya IPTL, Habinder Sethi na mfanyabiashara, James Rugemalira, umedai kuwa mshtakiwa Rugemalila hana saratani na puto la Sethi limeisha muda wake.

Mwendesha Mashitaka wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), Leonard Swai ameeleza  hay oleo Ijumaa mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Thomas Simba wakati akitoa taarifa baada ya kwenda gerezani kama alivyotakiwa na Mahakama.

Swai meeleza mbele ya Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, kuwa yeye alikwenda magereza kufuatilia hali za washitakiwa hao kama Mahakama ilivyoagiza.

Swai amesema washitakiwa hao wameomba magereza kuwa wakati wanapofanyiwa uchunguzi kiafya madaktari wao kutoka nje ya nchi wawepo.

"Sethi ambaye ni mshtakiwa wa kwanza katika kesi hii, yeye anayeishi na puto tumboni tangu Desemba mwaka jana na limeisha muda wake na kwamba daktari wa Hospitali ya Taifa Muhimbili walimfanyia uchunguzi na kubaini kuwa puto hilo linatakiwa kuondolewa na mshtakiwa alishirikishwa katika hatua hiyo akaomba daktari wake kutoka Afrika Kusini awepo wakati wa kufanyiwa upasuaji na kuomba muda wa kuwasiliana na daktari huyo," ameeleza Swai.

Hata hivyo, Swai ameeleza kuwa madaktari wa hapa nchini wapo tayari kuondoa puto hilo kama afya ya mshtakiwa itaendelea kuathirika au kuwa mbaya.

Ameeleza kuwa kwa upande wa mshitakiwa wa pili (Rugemalira) yeye  anatibiwa na magereza pamoja na daktari wake anayeitwa Fred ambaye anachukua vipimo na kupeleka hospitalini kwake Sanitas na kurudisha majibu magereza.

Amedai katika majibu hayo yanaonyesha kuwa hana saratani kama alivyodai na kwamba Serikali inafuatilia afya zao kwani hakuna jambo nyeti litakaloweza kuhatarisha maisha yao.

Baada ya maelezo ya upande  wa mashtaka, washtakiwa hao waliomba madaktari wao kutoka India na Afrika Kusini kuwepo wakati wakifanyiwa uchunguzi wa kiafya.

Awali, wakili wa Sethi,  Alex Balomi  alidai kuwa wamethibitisha kuwa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili haina uwezo wa kumfanyia upasuaji wa ama kuondoa au kuweka hilo puto kwa mteja wake hivyo kitu muhimu ni  madaktari wa Afrika Kusini kuwepo nchini na hili ni suala la kutilia mkazo.

"Sisi tumepokea maoni kutoka kwa hao madaktari wa Afrika Kusini  kuwa ni lazima wawepo wakati wa upasuaji wa Sethi," amesema wakili wa utetezi, Balomi.

Kwa upande wake, wakili wa Rugemarila, Respicious Didas ameeleza kuwa suala la afya ya washtakiwa ni muhimu sana na ugonjwa wa mteja wake upo wazi kwamba ana uvimbe unaoonekana.

"Licha ya ugonjwa wa mteja wangu kuwa wazi, bado upande wa mashtaka haujachukua hatua yoyote kuhusiana na uvimbe huo," ameeleza wakili Didas.

Amedai kuwa Rugemalira aliwahi kuugua saratani na kufanyiwa upasuaji mwaka 2008 na kwamba ugunduzi huo pamoja na matibabu yote, vilifanyika nchini India.

Didas alieleza kuwa matibabu na vipimo vikivyokuwa vinafanyika hapa nchini vilikuwa vina shida na ndio maana aliamua kuanzisha kituo cha saratani hapa kwa ajili kutibu wananchi wasio na uwezo wa kwenda kutibiwa nje ya nchi, wanaweza kupata matibabu katika kituo chake.

Wakili huyo alieleza kuwa anaamini kuwa mteja wake akitibiwa nchini India kulipo na vifaa vya kutosha wanaweza kugundua tatizo la uvimbe aliokuwa nao.

"Suala la afya ya mteja wangu linapaswa kupewa kipaumbele na ugunduzi wa ugonjwa wake ufanyike kwa kutumia madaktari wa India.”

Kutokana na maelezo ya mawakili wa utetezi, Hakimu Simba alisema Mahakama inashukuru kwa kuona kuwa amri iliyotoa Januari 5, mwaka huu ya washtakiwa hao wakatibiwe imetekelezwa.

Hakimu Simba alisema kutokana na hali hiyo, Mahakama imenukuu na imeona mshtakiwa wa kwanza wakati wa upasuaji, madaktari wake wa Afrika Kusini wawepo na utaratibu huo huo utumike kwa mshtakiwa wa pili.

"Magereza wawasiliane na madaktari wa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili ili madaktari ya India wawepo wakati wa upasuaji," amesema Hakimu Simba.

Hata hivyo, Hakimu Simba aliahirisha kesi hiyo hadi Februari 2, mwaka huu itakapotajwa.

Waziri wa Maji Avunja Bodi za Wakurugenzi Majisafi na Usafi wa Mazingira

$
0
0
Waziri wa Maji Avunja Bodi za Wakurugenzi Majisafi na Usafi wa Mazingira
Taarifa zilizotufikia  ni kwamba Waziri wa Maji na Umwagiliaji Mhandisi Isack Aloyce Kamwelwe amezivunja Bodi za Wakurugenzi za Majisafi na Usafi wa Mazingira za mikoa miwili.

Bodi hizo ni za Jiji la Arusha yaani AUWSA na ile ya mkoani Musoma ya MUWASA na kwa mujibu wa taarifa hiyo iliyotolewa na Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Profesa Kitila Mkumbo, Waziri Kamwelwe amevunja bodi hizo baada ya kutoridhishwa na utendaji wake.

Kikosi cha Simba Chatua Kagera

$
0
0
Kikosi cha Simba Chatua Kagera
Mapema asubuhi ya leo kikosi cha klabu ya soka ya Simba kimetua mkoani Kagera kwa ajili ya kucheza mechi yao ya ligi kuu Tanzania Bara na Kagera Sugar.

Simba waliondoka alfajiri kwa ndege huku ikiwa na wachezaji wake muhimu ambao jana waliiangamiza Singida United kwa mabao 4-0.

Simba ambao wanaongoza ligi hiyo inatarajiwa kucheza na Kagera Sugar Jumatatu ya wiki ijayo ya January 22 katika uwanja wa Kaitaba.

Bushoke Awapa Ushauli Huu Babu Seya na Papii Kocha

$
0
0
Bushoke Awapa Ushauli Huu Babu Seya na Papii Kocha
Msanii Bushoke amefunguka na kuwashauri wasanii Nguza Viking maarufu kama Babu Seya na mwanaye Jonson Nguza (Papii Kocha) na kusema kuwa kwa sasa wanatakiwa kukitumia kipindi hichi vizuri ili kuweza kufanikiwa na kupiga hatua zaidi katika muziki.


Bushoke amesema hayo alipokuwa kwenye kipindi cha Planet bongo ya East Africa Radio kwenye Heshima ya Bongo fleva na kudai kuwa anaamini watu hao saizi wamechelewa kutokana na kukaa muda mrefu jela lakini kwa nafasi walionayo sasa wanaweza kufanya mambo makubwa kama wataitumia vizuri.

"Nawaombea watulie, watumie hii nafasi waliyopata sasa vizuri, naweza kusema wamechelewa lakini pia hawajachelewa kutokana na nafasi waliyonayo sasa najua watafanya makubwa sana" alisema Bushoke

Mbali na hilo Bushoke amesema toka wasanii hao wametoka jela na kurudi mtaani wamekuwa wakikutana na kufanya mazungumzo mara kwa mara lakini bado hawajakaa na kuzungumza juu ya wao kufanya kazi pamoja.

Vigogo wa Six Telecoms Waendelea Kusota Rumande

$
0
0
Vigogo wa Six Telecoms Waendelea Kusota Rumande
Kesi ya uhujumu uchumi inayowakabili vigogo wanne wa Kampuni ya Mawasiliano ya Six Telecoms,akiwemo Wakili Dk Ringo Tenga, imeahirishwa baada ya upande wa mashtaka kudai kuwa upepezi bado haujakamilika.
Vigogo wa kampuni ya Six Telecoms, mfanyabiashara Peter Noni (kushoto) na Wakili maarufu Dk. Ringo Tenga wakiwa katika chumba cha Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Dar es Salaam.

Mbali na Dk Tenga, washitakiwa wengine katika kesi hiyo ni mfanyabiashara Peter Noni, Mhandisi na Mkurugenzi Mkuu wa Kampuni hiyo, Hafidhi Shamte, Mkuu wa Fedha wa kampuni hiyo, Noel Odeny Chacha na kampuni  yenyewe ambayo ni Six Telecoms Limited.

Washtakiwa hao wanakabiliwa na mashtaka hayo, katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu

Wakili wa Serikali, Leonard Challo ameeleza mbele ya Hakimu Mkazi Mwandamizi, Victoria
Nongwa kuwa kesi hiyo imekuja kwa ajili ya kutajwa na kwamba upelelezi bado unaendelea.

Hakimu Nongwa ameahirisha kesi hiyo hadi Januari 26, mwaka huu kwa ajili ya kutajwa.

Simba Yasainishana Mkataba na Kocha Wao Mpya Leo

$
0
0
Simba Yasainishana Mkataba na Kocha Wao Mpya Leo
Klabu ya Soka ya Simba ya jijini Dar es Salaam, leo mchana imemtambulisha rasmi kocha wao mpya Raia wa Ufaransa, Pierre Lichantre, ili kuanza kuinoa Klabu hiyo baada ya kuachana na aliyekuwa kocha wao, Mkameruni Joseph Omog.

Kocha Pierre Lechantre ametambulishwa leo katika ukumbi wa mikutano wa hotel ya Movenpick jijini Dar es salaam, tukio lililoendana na kusainishana mikataba. Kocha huyo amekuja pamoja na kocha wa viungo Amin Mohamed Habib.Kocha Lechantre amewahi fundisha timu ya taifa ya Cameroon iliyochukua ubingwa wa Afrika.

Klabu ya soka ya Simba ipo mjini Bukoba kujiandaa na mchezo dhidi ya Kagera Sugar Jumatatu. Lechantre ataanza kazi mara moja timu itakaporejea Jumanne baada ya mchezo huo.

Msemaji wa Simba, Haji Manara pia amewashukuru mashabiki wa Simba kwa sapoti ambayo wameionyesha na kuwahkikishia ushindi mpaka watakapochukua ushindi wa ligi kuu. Hii ni mara ya kwanza kwa kocha Mfaransa kufundisha vilabu vya Tanzania.

Lechntre amesema; “Nitajitahidi kufanya kazi na kocha Djuma, kuipigania timu kuipeleka mbele katika mashindano ya Afrika. Nipo hapa kuipigania timu na kumfanya kila mtu awe na furaha katika klabu”

Katika mkutano huo Simba iliwatangaza viongozi walioteuliwa kuongoza kamati ya maadili itakayoongozwa na Mwenyekiti, Suleiman Kova aliyekua mkuu wa Polisi, Robert Selasela, Suleiman Ali aliyekua katibu wa zoezi la kuibadilsha simba kuwa kampuni pamoja na Steven Ali.

Familia Yarudisha Mwili wa Marehemu Mahali Alipopigwa Hadi Kuuawa

$
0
0
Familia Yarudisha Mwili wa Marehemu Mahali Alipopigwa Hadi Kuuawa
Familia ya marehemu kijana David Wokabi ambaye alikuwa akifanya kazi benki nchini Kenya, imerudisha mwili wa marehemu huyo mahali ambapo alipigwa na watu waliosababisha kifo chake, ili kudai haki na fidia.

Msemaji wa familia amesema David alikuwa na majukumu yake, kwa hivyo kifo chake kimewapa wakati mgumu wa kuhudumia familia yake.

“Tumeleta huu mwili hapa kwa sababu damu yake ilimwagwa hapa, kama wanataka kumla wamle lakini sisi familia tuna watoto wawili na mke wa marehemu, Alikuwa na majukumu yake, kwa hiyo tunaiomba serikali itende haki kwa sbabau kuna watoto wa miaka miwili na mitatu, ambao hatujui nani atawahudumia”, amesema Msemaji huyo ambaye jina lake halikutajwa kwa mara moja.

Davidi alipigwa na walinzi watano wa benki hiyo kwa kosa la kukojoa kwenye parking ya magari, alifariki siku saba zilizopita, akiwa hospitali kwenye chumba cha wagonjwa mahututi alipokuwa akiuguza majeraha aliyoyapata kwa kipigo.

Camera za ulinzi za CCTV zimeonyesha walinzi hao wakimtoa David Wakobi kwenye gari lake alipokuwa akianza kutoka sehemu ya parking na kumvuta nje, na kisha kuanza kumshushia kipigo kilichomuacha na hali mbaya kiafya.

Tayari jeshi la Polisi limewakamata watu wawili kufuatia tukio hilo, huku wengine watatu wakikimbilia kusikojulikana huku wakiendelea na msako wa kuwakamata.

Hatimaye Chadema Kushiriki Uchaguzi Mdogo wa Wabunge Kinondoni, Siha

$
0
0
Hatimaye Chadema Kushiriki  Uchaguzi Mdogo wa Wabunge Kinondoni, Siha
CHAMA Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kimeridhia na kurejea kushiriki wa uchaguzi mdogo wa wabunge katika majimbo ya Kinondoni na Siha baada ya kutangaza kuwa hawatashairiki uchaguzi huo mpaka pale mapendekezo yao yatakaposikilizwa.

Uamuzi huo wa kushiriki uchaguzi umetangazwa le0 Januari 19, 2017 na Mkurugenzi wa Itikadi, Mawasiliano na Mambo ya Nje, John Mrema kupitia taarifa yake kwa umma.



CHAMA CHA DEMOKRASIA NA MAENDELEO (CHADEMA)

TAARIFA KWA UMMA, KUHUSU UCHAGUZI MDOGO WA KINONDONI NA SIHA.

Kamati Kuu ya Chama imemaliza Vikao vyake Leo tarehe 19 Januari, 2018 na imefanya uamuzi wa kushiriki kwenye uchaguzi mdogo kwenye majimbo ya Kinondoni na Siha unaotarajiwa kufanyika tarehe 19 Februari, 2018.

Baada ya uamuzi huu kufanyika , Kamati Kuu imewateua wagombea wa Majimbo hayo kama ifuatavyo;

1. Jimbo la Kinondoni ameteuliwa Mhe. Salum Mwalim Juma

2. Jimbo la Siha ameteuliwa Bwana Elvis Christopher Mosi

Wagombea wote wameshachukua fomu za uteuzi kutoka kwa wasimamizi wa uchaguzi kwenye majimbo husika na watazirejesha kesho Jumamosi tarehe 20 Januari 2018 , kwa ajili ya uteuzi.

Imetolewa Leo tarehe 19 Januari, 2018.

John Mrema – Mkurugenzi wa Itikadi, Mawasiliano na Mambo ya Nje.

Makamu wa Rais Mama Samia Akutana na Bosi wa UN Tanzania

$
0
0
Makamu wa Rais Mama Samia Akutana na Bosi wa UN Tanzania
Makamu wa Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu leo amekutana na Mratibu wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi Mkazi wa UNDP, Alvaro Rodriguez ambaye alimtembelea ofisini kwake.


Makamu wa Rais Mama Samia Suluhu akizungumza na Mratibu wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi Mkazi wa UNDP, Alvaro Rodriguez

Miongoni mwa mambo waliyojadili ni ushirikiano mzuri unaoendelea kati ya mashirika lake na serikali ya Tanzania.

Bushoke Awapa Ushauri Babu Seya na Papii Kocha

$
0
0
Msanii Bushoke amefunguka na kuwashauri wasanii Nguza Viking maarufu kama Babu Seya na mwanaye Jonson Nguza (Papii Kocha) na kusema kuwa kwa sasa wanatakiwa kukitumia kipindi hichi vizuri ili kuweza kufanikiwa na kupiga hatua zaidi katika muziki.

Bushoke amesema hayo alipokuwa kwenye kipindi cha Planet bongo ya East Africa Radio kwenye Heshima ya Bongo fleva na kudai kuwa anaamini watu hao saizi wamechelewa kutokana na kukaa muda mrefu jela lakini kwa nafasi walionayo sasa wanaweza kufanya mambo makubwa kama wataitumia vizuri.

"Nawaombea watulie, watumie hii nafasi waliyopata sasa vizuri, naweza kusema wamechelewa lakini pia hawajachelewa kutokana na nafasi waliyonayo sasa najua watafanya makubwa sana" alisema Bushoke

Mbali na hilo Bushoke amesema toka wasanii hao wametoka jela na kurudi mtaani wamekuwa wakikutana na kufanya mazungumzo mara kwa mara lakini bado hawajakaa na kuzungumza juu ya wao kufanya kazi pamoja.

Bushoke ameiachia video ya wimbo wake mpya unaokwenda kwa jina la 'Goma la ukaye'

Majina ya Walioteuliwa na CHADEMA Kugombea Ubunge Kinondoni na Siha

$
0
0

Kamati Kuu ya Chama imemaliza Vikao vyake Leo tarehe 19 Januari, 2018 na imefanya uamuzi wa kushiriki kwenye uchaguzi mdogo kwenye majimbo ya Kinondoni na Siha unaotarajiwa kufanyika tarehe 19 Februari, 2018.

Baada ya uamuzi huu kufanyika , Kamati Kuu imewateua wagombea wa Majimbo hayo kama ifuatavyo;

1. Jimbo la Kinondoni ameteuliwa Mhe. Salum Mwalim Juma

2. Jimbo la Siha ameteuliwa Bwana Elvis Christopher Mosi

Wagombea wote wameshachukua fomu za uteuzi kutoka kwa wasimamizi wa uchaguzi kwenye majimbo husika na watazirejesha kesho Jumamosi tarehe 20 Januari 2018 , kwa ajili ya uteuzi.

Imetolewa Leo tarehe 19 Januari, 2018.

John Mrema – Mkurugenzi wa Itikadi, Mawasiliano na Mambo ya Nje.

Mwili wa Marehemu Warudishwa Pale Alipouwawa

$
0
0
Familia ya marehemu kijana David Wokabi ambaye alikuwa akifanya kazi benki nchini Kenya, imerudisha mwili wa marehemu huyo mahali ambapo alipigwa na watu waliosababisha kifo chake, ili kudai haki na fidia.

Msemaji wa familia amesema David alikuwa na majukumu yake, kwa hivyo kifo chake kimewapa wakati mgumu wa kuhudumia familia yake.

“Tumeleta huu mwili hapa kwa sababu damu yake ilimwagwa hapa, kama wanataka kumla wamle lakini sisi familia tuna watoto wawili na mke wa marehemu, Alikuwa na majukumu yake, kwa hiyo tunaiomba serikali itende haki kwa sbabau kuna watoto wa miaka miwili na mitatu, ambao hatujui nani atawahudumia”, amesema Msemaji huyo ambaye jina lake halikutajwa kwa mara moja.

Davidi alipigwa na walinzi watano wa benki hiyo kwa kosa la kukojoa kwenye parking ya magari, alifariki siku saba zilizopita, akiwa hospitali kwenye chumba cha wagonjwa mahututi alipokuwa akiuguza majeraha aliyoyapata kwa kipigo.

Camera za ulinzi za CCTV zimeonyesha walinzi hao wakimtoa David Wakobi kwenye gari lake alipokuwa akianza kutoka sehemu ya parking na kumvuta nje, na kisha kuanza kumshushia kipigo kilichomuacha na hali mbaya kiafya.

Tayari jeshi la Polisi limewakamata watu wawili kufuatia tukio hilo, huku wengine watatu wakikimbilia kusikojulikana huku wakiendelea na msako wa kuwakamata.


Wana CHADEMA Wenzangu, Mara hii Tumesahau ya November 26 na ya Chaguzi za nyuma?

$
0
0
Maswali yangu ni haya:
1.Tume ya Uchaguzi imebadilika?
Kama haijabadilika,tumejipangaje?

2. Wakurugenzi na watendaji wa Kata watakuwa fair safari hii?
Kama hawatakuwa fair,tumejipangaje?

3. Tumejipanga vipi kukabiliana na wale wavaa sare tunaowalalamikia kila kukicha?


4. Tumejipanga vipi kukubaliana na maagizo kutoka juu?


5. Je, mnajua jamaa zetu safari hii watakuja na mbinu gani?

6. Chama chetu kimejipangaje japo inaweza kuwa ni siri yao?

7. Tunaikabili vipi sheria ya mita 200?

8. Tumejipanga na tuko tayari kukusanya na kuchukua ushahidi kwa gharama yoyote ile na katika mazingira yoyote yale?

9. Tuna uhakika Mawakala wetu wote hakuna watakoweza kurubuniwa na vipande 30 vya fedha?

Mwisho:
Kwa kuwa tumekubali kuingia katika kinyang'anyiro hiki,nashauri wabunge wa chama wa mikoa ya Dar-es-Salaam na Kilimanjaro pamoja na wa mikoa ya jirani(kama ikibidi) na hata vingozi wa juu wa chama kama itabidi pia, ndio wawe mawakala kwenye huu uchaguzi.

Wagombea/Mgombea mzuri ni jambo moja na kushinda uchaguzi ni jambo lingine kwa nchi zetu hizi za kiafrika.

Salary Slip

Fahamu jinsi ya kupata Watoto Mapacha

$
0
0
Siku ya leo naomba tujifunze elimu mpya kabisa ya uzazi ambapo mwanamke yeyote anaweza kupata ujauzito wenye watoto mapacha hata kama si asili ya ukoo wake, ambavyo wengi wanavyosema.

Nimetumia neno ‘mwanamke yeyote’ kwa sababu kuna imani ya miaka na miaka kwamba, si kila mwanamke anaweza kupata ujauzito bali itategemea na asili yake.

Imani ya kale kuhusu ujauzito
Baadhi ya mila na desturi, hasa katika nchi za Kiafrika zinaamini kwamba, mwanamke kupata watoto mapacha kunatokana na urithi wa kizazi chake, kuanzia mababu wa upande mmoja kati ya wanandoa hivyo uzao huo hufuata mkondo kwa miaka na miaka.

Wengi wakipata mapacha huulizwa kama kwenye kizazi chake, kuna watoto mapacha. Akitokea mama akasema hakuna, basi huaminika kwamba lazima upande wa mwanaume kuna waliowahi kuzaliwa mapacha hata kama si katika miaka ya karibuni.

Imani hii ni ya kizamani sana, ukweli ni kwamba mwanamke yeyote mwenye sifa ya kushika mimba na kuzaa, anaweza kupata ujauzito na kuzaa mapacha bila kujali asili ya kizazi chake.

Kwa nchi zilizoendelea wanawake wanaweza kuzaa mapacha kwa kupandikiza mayai yaliyopevuka kwa kutegemea na idadi unayoitaka mwenyewe lakini bila kujua wangeweza kuzaa hata bila ya kupandikizwa.

Nina ushahidi kuwa, baadhi ya wanawake huenda kwa waganga wa kienyeji kwa lengo la kupatiwa dawa ya kuwasaidia kuzaa mapacha, jambo ambalo si sahihi na halipo. Sanasana utaliwa pesa zako bure na mapacha usiwapate.

Wanawake wengi wanaoongoza kwa kushika mimba za mapacha ni wale ambao wakati wa kulala wanabadili staili mara kwa mara. Mara nyingi inashauriwa kuwa, mwanamke akishaingia kwenye siku zake za hatari kulingana na mzunguko wake wa hedhi, akutane kimwili na mumewe au mwanaume anayetaka kuzaa naye.

Baada ya tendo la ndoa, mwanaume anashauriwa kulala kwa kujigeuzageuza kitandani. Hapa namaanisha kwamba, akiwa amelala, ajigeuze kuangalia juu, kulalia ubavu wa kulia, kushoto, kulala kifudifudi kwa usiku kucha.

Fanya hivi kwa kurudiarudia siku kadhaa katika kipindi hicho cha hatari, hapo uwezekano wa kushika mimba ya mapacha utakuwa mkubwa sana.

Kwa Nini Wanaume Wengi Wanaupungufu Wa Nguvu Za Kiume Na Maumbile Madogo?

$
0
0
Asilimia 45 ya wanaume wapo tofauti na wengine kwa kuwatimizia vyema wake au wapenzi Wao na kuwasababishia kutoka nje ya ndoa zao.


NINI CHANZO CHA HAYO?Kupiga punyeto,Ngiri,Vidonda vya tumbo,Magonjwa ya moyo,Presha,Kisukari,Korodani moja kuvimba,Msongo wa mwazo,Kufanyiwa tohara ukiwa mtu mzima n.k.DOKTA MANYANDA sasa kapata tiba sahihi ya tatizo la NGUVU ZA KIUME.


MUHAMA:Hii hutibu na kuponyesha kabisa tatizo la nguvu za kiume,utakuwa na uwezo wa kurudia tendo zaidi ya mara tatu bila kuchoka na itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa mda wa dakika 15-20.DAWA hii imechanganywa miti 12.Hata wazee wenye umri mkubwa wanapona kabisa.OKO NDOA YAKO SASA.


MANGUNGU MIX: Ndio tiba tosha kwa sasa ambayo hurefusha na kunenepesha uume saizi uipendayo inch 1-8 na unene sentimita 1-5,dawa hii ipo ya kupaka na kunywa na haina madhara yoyote kwa mtumiaji.


NITOFAUTI NA ULIZO WAHI KUZITUMIA.Pia tuna dawa za kupatanisha mke,mme,mpenzi au bosi wako kwa mda mfupi sana,Uzazi,Kusafisha nyota,


Je unamali yako unauza hupati wateja?

Wasiliana nami 0716-263605


DOKTA MANYANDA ANAPATIKANA KASULU KIGOMA,Kwa wale wa mikoani huduma hii utaipata popote pale

JE Wivu Kwa Mpenzi wako Unatokana na nini Hasa Kati ya Haya yafuatayo?

$
0
0
Kadri siku zinavyozidi tu kwenda mbele Kiwango cha Wivu baina ya ama Wapendanao walio pamoja au hata wale waliokuwa Wapenzi na wakaachana ndiyo kinaongezeka tena kwa Kasi sana hadi kusababisha Watu wengi kuamua Kujitoa uhai au kumtoa uhai mlengwa wake au hata kujidhuru kabisa Yeye kama Yeye au kufanya tukio la ajabu ambalo Kibinadamu linastaajabisha na halikutegemewa.

Je katika haya yafuatayo ni vitu gani ndiyo huongeza zaidi Kiwango cha Wivu baina ya Wapendanao au walioachana hadi wanafikia hatua Kali hizo tajwa hapo juu?

  • Kulikumbuka tendo la ndoa la mwenza wake?
  • Kukumbuka hasa yale manjonjo ya Kitandani ya mwenza wake kabla ya kuanza Kutinduana / Kungonoka / Kubaiolojiana?
  • Kukumbuka maumbile ya mwenza wake Mkuyenge / Mbunye hasa Kiutamu na Kimwonekano?
  • Kukumbuka jinsi mwenza wake anavyomjali / alivyokuwa akimjali Kimaisha?
  • Kukumbuka ahadi na mwenza wake hasa katika Mahusiano yao?
  • Kukumbuka jinsi alivyohangaika kumpata, kumgharamikia na kumvumilia?
  • Kuamini kwamba hatoweza tena kumpata mwenza wake kama huyo tena katika maisha yake?

ANGALIZO

Sihitaji jibu la kwamba majibu yote ni sawa / sahihi bali nahitaji jibu moja tu kutoka katika hayo mambo Saba ( 7 ) niliyoyaorodhesha hapo juu. Huenda majibu yenu ya hapa yakasaidia katika kupatikana kwa ufumbuzi wa hili tatizo kubwa la sasa la Wivu na Watu kuchukua hatua Kali na za Hatari juu ya Wenza / Wapenzi wao.

Karibuni sana na mno!

Nawasilisha.

“Jamani Huu Mjadala wa Nguo Fupi… Haiwezekani Watu Watembee na Futi Mitaani” – Tibaijuka

$
0
0
Kumekua na mjadala kwenye mitandao mbalimbali ya kijamii baada ya habari kusambaa kwamba Wanawake wanaovaa nguo fupi na Wanaume wanaovaa milegezo, kunyoa viduku na suruali zilizobana Arusha na Dar es salaam wanakamatwa na Polisi.

Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es salaam Lazaro Mambosasa alikanusha kuhusu Polisi Dar kukamata wanaofanya hivyo kwa kusema alinukuliwa vibaya.

Sasa baada ya kuona mijadala inaendelea kwenye mitandao ya kijamii, Mbunge wa Muleba Kusini Profesa Anna Tibaijuka amejitokeza na kuongea yafuatayo >>> “Yani kuna vitu vingine huwezi kusema Muafrika alikua anavaa nguo ndefu, hapana sio kweli…”

“Mwili wa Mwanamke unaonekana ni kifaa ambacho Mungu amekiweka kwa shughuli maalum ya Uzazi, Ulezi n.k sasa ambae anajiheshimu anajua nini cha kuvaa katika wakati gani, cha msingi ni maadili ya mavazi na pale ulipo“

“Hiki sio kitu ambacho kitasimamiwa huwezi tena kuwa tena na Watu wanatembea na futi mitaani kupima urefu au ufupi wa nguo, jamanijamani tunazo kazi nyingi za kufanya” – Profesa Tibaijuka …… msikilize zaidi hapa chini
Viewing all 104709 articles
Browse latest View live


Latest Images