Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104689 articles
Browse latest View live

“Nimekaa Ndani Wiki 3, Nimeona Waliosema Nina Ukimwi” – Steve Nyerere

$
0
0
January 19, 2018 Muigizaji maarufu wa Bongomovie Steve Nyerere amezungumza baada ya kuugua kwa wiki tatu Steve ameeleza kuwa alichokuwa anaumwa kuwa ni miguu na siyo VVU kama ilivyokuwa inasemwa kwenye mitandao japo hashangai watu kumsema.

Steve amesema hakuna mtu wake wa karibu aliyezusha suala la ugonjwa wake bali ni mitandao tu ndo imevujisha, alipoulizwa kama Wema Sepetu alikuwa miongoni mwa watu walioenda kumtembelea alijibu kuwa Utu haulazimishwi na kumuona mgonjwa hakulazimishwi pia.

Bonyeza PLAY hapa chini kusikiliza FULL STORY



Faiza Kazungumza “Siongei na Sugu ila Sifurahii Akipata Matatizo”

$
0
0
Baada ya Mbunge wa Mbeya Mjini Joseph Mbilinyi maarufu kama Sugu kushikiliwa na Jeshi la Polisi na kufikishwa Mahakamani kwa kosa la uchochezi, Mzazi mwenzake Faiza Ally amezungumza na kusema haongei na Sugu lakini akipata matatizo hawezi kufurahia.

Kuhusu suala la mtoto wao Faiza Ally amesema kwamba Sugu anampenda mwanae na amemlipia ada japo amuhudumii kwenye vitu vingine na hiyo haisababishi yeye kutokuguswa na matatizo ambayo anayapata kutokana ni baba wa mtoto wake.

Bonyeza PLAY hapa chini kusikiliza FULL STORY..

VIDEO: Mtatiro Afunguka CHADEMA Kusimamisha Wagombea

$
0
0
Mwenyekiti wa kamati ya uongozi wa Chama cha CUF Julius Mtatiro amesema kuwa kitendo cha CHADEMA kusimamisha wagombea katika uchaguzi mdogo wa marudio majimbo mawili ya Kinondoni na Siha sio kitendo kibaya, Msimamo wa UKAWA ulikua ni kugomea uchaguzi mdogo wa January 11.


TAZAMA FULL VIDEO HAPA CHINI........ 

Miujiza ya Sharifu Seif Mohamed..JE Umeachwa na Mme/Mke au Mpenzi, Umesongwa na Mitihani ya Maisha..Piga Simu Upate Muujiza Wako

$
0
0
SHARIFU SEIF MOHAMED ANAWASHUKURU WALE WOTE WANAOENDELEA KUPIGA SIMU, WENYE MATATIZO NA WALE WANAOTOA  SHUKRANI NA SHUHUDA JINSI TIBA ZAKE ZINAVYO WASAIDIA,

(Rudisha mahusiano yako ndani ya masaa 72 tu)

SHARIFU MOHAMED Ni  mtaalam na mnajimu maarufu wa nyota na kubashiri mambo yanayo watesa binadamu duniani kote na kupata ufumbuzi, Anatumia kitabu cha QUR'AN, Dawa za Asili, Dawa za Kiarabu na majini kwa kumtuliza mke/mme, mchumba au mpenzi ndani ya masaa 72 tu, na kutatua matatizo yote ya kimaisha,

Je Umeachwa na UMPENDAE awe Mme/Mke na bado unampenda? Je Umekimbiwa na Mmeo/ Mkeo n anaishi na mtu mwingine? Je Umejaribu sehemu nyingi bila mafanikio? Mpigie simu SHARIFU SEIF sasa hivi ujionee Muujiza wa Papo kwa Papo, Anauwezo wa hali ya juu wa kusambaratisha mahusiano yao na kumrejesha kwako haraka sana na Kumfanya Atimize Ahadi zote Ndani ya Muda Mfupi Endapo Utafwata Atakacho Kuelekeza

ANAZO DAWA ZA MAPENZI, NGUVU ZA KIUME, CHANGO NGIRI MAJI NA N.K, ZINDIKO LA NYUMBA NA BIASHARA, PETE ZA BAHATI, HUMALIZA KABISA TATIZO LA NGUVU ZA KIUME NA KUREFUSHA UUME KWA SAIZI UNAYOTAKA, HUZUIA CHUMA ULETE KWENYE BIASHARA, HURUDISHA MALI ZILIZOPOTEA, MAGONJWA SUGU, MIGUU KUWAKA MOTO AU KUFA GANZI, HUTIBU BUSHA BILA KUPASUA, ANAO UWEZO WA KUMRUDISHA ALIE MBALI AU ALIECHUKULIWA MSUKULE, KUPANDISHA NYOTA NA KUSHINDA BAHATI NA SIBU, KASAFISHA NYOTA NA KUKUPA MVUTO WA AJABU, KUTOA NUKSI NA VIFUNGO MBALIMBALI,  MAFANIKIO YA MAISHA NA UTAJIRI BILA MASHARI, NA MENGINE MENGI YA SIRI,

Je UMAHANGAIKA KUPATA MTOTO BILA MAFANIKIO? WASILIANA NA MTAALAMU HUYU KWANI YEYE HUFAULU PALE WOTE WALIPOSHINDWA, PIA UMALIZA KAZI ZILIZO SHINDIKANA NA WATAALAM WENGINE NDANI YA MASAA 24 TU,

(NA ANATIBU KWA NJIA YA SIMU UKIWA NCHI YOYOTE AU MKOA WOWOTE ENDAPO UTAFWATA MAELEKEZO YAKE)

Kwa ushauri na mawasiliano  zaidi Piga SIMU No:

Mobile +255 654-836970
WhatsApp +255 756-033670

Kocha Simba Sc Amtolea ‘Povu’ Mavugo

$
0
0
Kocha Simba Sc Amtolea ‘Povu’ Mavugo
KOCHA Msaidizi wa Simba, Masoud Djuma amesema kuwa ushindi ambao timu yake iliyoupata jana Alhamisi katika mchezo dhidi ya Singida United ulichangiwa kwa kiasi kikubwa na mabadiliko ya wachezaji wake huku akimtolea ‘povu’ straika wale Laudit Mavugo.

Simba ilipata ushindi wa mabao 4-0 katika mchezo wa Ligi kuu Bara kwenye Uwanja wa Taifa dhidi ya wababe hao wa Singida ambapo mabao yake yalifungwa na Shiza Kichuya, Asante Kwasi na Emmanuel Okwi aliyefunga mawili. Akizungumza mara baada ya mchezo huo, Djuma alisema nafasi ya Okwi kucheza ilitakiwa ichukuliwe na Mavugo lakini kwa kuwa

Mavugo hakuonyesha kiwango kizuri mazoezini ilimbidi afanye mabadiliko hayo. “Okwi amefanya mazoezi na sisi siku mbili tu kama mnavyojua hakuwepo kambini, nilipanga kumtumia Mavugo lakini nimemwambia kuwa hakuonyesha uwezo mzuri, ndiyo maana nikaamua kumpa nafasi Okwi na kweli ameitumia vizuri. “Nimeshamueleza Mavugo kuwa yeye ni ndugu yangu lakini katika hili suala la kazi anatakiwa kuonyesha uwezo na kufanya kweli, siwezi kumpa nafasi kama haonyeshi uwezo,” alisema kocha huyo.

KUHUSU KOCHA MPYA

Kuhusu kocha mpya wa Simba, Pierre Lechantre raia wa Ufaransa aliyekuwepo jukwaani akifuatilia mchezo huo, Djuma alisema yeye hana tatizo na ujio wa kocha huyo, anamkaribisha na yupo tayari ku- fanya naye kazi. “Nipo tayari wala sina tatizo, namkaribisha na tutakuwa pamoja, kuhusu mfumo na maendeleo mengine nitampatia ripoti kisha yeye ndiye atakayeamua juu ya kutumia au la,” alisema. Upande wa Kocha wa Singida United, Hans van Pluijm alisema matokeo ya mchezo huo yametokana na walinzi wake kufanya makosa na Simba wakayatumia vizuri.

Kajala Aumizwa na Penzi la kujificha

$
0
0
Kajala Aumizwa na Penzi la kujificha
STAA wa filamu za Kibongo, Kajala Masanja amefunguka kuwa hivi sasa anaumizwa na mapenzi ya kufichaficha kwa sababu ya kulinda heshima yake kwa mtoto wake wa kike, Paula kwa kuwa sasa amekuwa msichana mkubwa.

Akizungumza na Risasi Jumamosi, Kajala alisema amekuwa kwenye wakati mgumu sana wa kuwa na uhusiano wa kificho lengo likiwa ni kutomharibu mwanaye huyo ambaye ana uelewa mkubwa na anatambua kila kitu.

“Sipendi Paula anijue kiundani kuhusiana na mahusiano kwa sababu kwa umri aliofikia na darasa alilopo (Kidato cha nne) kama sitakuwa na usiri ataelewa kila kitu, sio Kajala yule tena wa zamani wa kuweka mpenzi wazi ingawa inaniumiza kwani sikuzoea, na mapenzi ya siri yanaumiza asikwambie mtu,” alisema Kajala.

Chuchu Hans Anena Kuhusu Kuachana na Ray

$
0
0
Chuchu Hans Anena Kuhusu Kuachana na Ray
MSANII wa filamu za Kibongo, Chuchu Hans ameibuka na kusema kuwa tetesi zilizozagaa akidaiwa kuachana na mzazi mwenziye Vincent Kigosi ‘Ray’ na kwamba ndiyo sababu ya kubadili jina lake kwenye ukurasa wake wa Instagram siyo za kweli.

Awali kwenye ukurasa wa Insta Chuchu alikuwa akijiita Chuchu Hans the Great na sasa anajiita Chuhans Kichuna, jambo lililowafanya wengi waamini safari ya mapenzi yao imefika mwisho.

Akizungumza na Risasi Jumamosi, Chuchu alisema kuwa yeye ameamua tu kubadili jina na wala hajaachana na Ray na kama wapo wanaosubiri penzi livunjike, watasubiri sana.

“Waniache jamani kila siku nimeachana na Ray… nimeachana na Ray…, nina sababu zangu za kubadilisha jina, haina maana kwamba tumeachana, hata hivyo sitaki kuongelea sana suala hilo kama tumeachana au la, majibu mtayapata subirini tu,”alisema Chuchu.

Wazungu Washindwa Kumuondoa Ndemla Simba

$
0
0
Wazungu Washindwa Kumuondoa Ndemla Simba
KIUNGO wa Simba, Said Ndemla, sasa anajiandaa kusaini mkataba mpya wa kuendelea kuwepo Msimbazi huku ikielezwa lile dili la kwenda kucheza Ulaya limeyeyuka.

Ndemla ambaye mkataba wake wa sasa na Simba unamalizika Aprili, mwaka huu, mwishoni mwa mwaka jana alikwenda Sweden kufanya majaribio kwenye timu ya AFC Eskelistuna na kufuzu.



Hata hivyo, licha ya kufuzu majaribio hayo, Ndemla ameshindwa kujiunga na timu hiyo.

Taarifa kutoka ndani ya Simba zinasema kuwa, uongozi umeridhishwa na kiwango cha Ndemla, hivyo wameona bora waendelee kuwa naye ili kukiongezea nguvu kikosi katika mechi za Kombe la Shirikisho Afrika.



“Mkataba wake unaelekea ukingoni lakini wakati wowote anaweza kuongezewa kwa sababu uongozi unaridhishwa na kiwango chake ukizingatia kwamba tuna michuano ya kimataifa.

“Hii inamaanisha kuwa, huu si wakati wa kuacha wachezaji kama yeye,” kilisema chanzo hicho.



Alipotafutwa meneja wa mchezaji huyo, Jamal Kisongo kuzungumzia mustakabali wa Ndemla, alisema: “Lile dili lake kule Sweden tumewaachia Simba waamue kwani bado ni mchezaji wao, vyovyote watakavyosema ni sawa hakuna shida.”



Wakati hayo yakijiri, Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili ya Simba, Zacharia Hans Poppe amemuahidi kiungo huyo kumpatia gari kutokana na kiwango chake bora alichokionyesha msimu huu

Okwi Ampagawisha Kocha Mpya wa Simba

$
0
0
Okwi Ampagawisha Kocha Mpya wa Simba
KIKOSI cha Simba,  Alhamisi kilijitanua kileleni mwa msimamo wa Ligi Kuu Bara baada ya kuibuka na ushindi wa mabao 4-0 dhidi ya Singida United katika mchezo wa Ligi Kuu Bara uliopigwa kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.



Katika mchezo huo ambao Simba ilikuwa ikihitaji zaidi matokeo ya ushindi ili ijihakikishie nafasi yake ya kukaa kileleni, ilifanikiwa kupata bao la mapema dakika ya tatu lililofungwa na Shiza Kichuya. Beki wa kati wa timu hiyo,

Asante Kwasi, aliongeza bao la pili dakika ya 24 baada ya kukwepa mtego wa kuotea aliowekewa na mabeki wa Singida United.

Mara baada ya Kwasi kufunga bao hilo, kocha mpya wa Simba, Pierre Lechantre raia wa Ufaransa, alinyanyuka kwenye kiti chake akiwa jukwaani na kuanza kushangilia pamoja na ofisa habari wa timu hiyo, Haji Manara huku akiwapungia mkono mashabiki wa timu hiyo.



Dakika ya 65 wakati Emmanuel Okwi wa Simba anajiandaa kuingia kuchukua nafasi Mzamiru Yasin, mashabiki wa timu hiyo walikuwa wakimshangilia kwa nguvu jambo ambalo lilimhamasisha straika huyo na kuipatia Simba bao la tatu dakika ya 75.



Okwi aliongeza bao la nne dakika ya 82 ambapo kwa mara nyingine, Mfaransa, Lechantre aliinuka kwenye kiti na kushangilia kwa nguvu. Katika mchezo huo, Simba ilifanya mabadiliko ya wachezaji wawili ambapo ilianza kumtoa Mwinyi Kazimoto dakika ya 22 na nafasi yake kuchukuliwa na Said Ndemla kabla ya dakika ya 65 kutoka Mzamiru na kuingia Okwi.



Kwa upande wa Singida United, dakika ya 59 ilimtoa Kiggy Makasi na nafasi yake kuchukuliwa na Salum Chuku. Kwa matokeo hayo, Simba inaendelea kukaa kileleni mwa msimamo wa ligi hiyo ikiwa na pointi 29 ikifuatiwa na Azam yenye pointi 27. Mtibwa Sugar ni ya tatu ina pointi 24, Singida inakamata nafasi ya nne na pointi 23, huku Yanga ikiwa ya tano na pointi 22.

''Hakuna kama Ronaldinho labda Messi''

$
0
0
'Hakuna kama Ronaldinho labda Messi''
Kocha wa Manchester City Pep Guardiola ametoa heshima ya kumuaga nyota wa zamani wa Barcelona na Brazil Ronaldino Gaucho ambaye amestaafu soka kwa kusema hakuna kama yeye labda Messi.


Guardiola ambaye alimuuza Ronaldinho kutoka Barcelona kwenda AC Milan mwaka 2008, amesema wakati Ronaldinho anacheza Barcelona alikuwa mchezaji bora kuwahi kutokea hadi Lionel Messi alipochukua nafasi yake.

"Alikuwa mchezaji mwenye kipaji cha ajabu nafikiri hadi Messi alipokuja kuiteka dunia lakini kiukweli sikuwahi kuona kiwango cha namna ile katika siku za nyuma, hivyo namtakia mapumziko mema na kila la kheri katika majukumu mengine atakayoyaanza'', Guardiola amewaambia wanahabari.

Guardiola pia ameongeza kuwa mafanikio aliyoyapata akiwa Barcelona ilikuwa ni mwendelezo wa kile walichokianzisha Ronaldinho na Rais wa kipindi hicho wa Barcelona Joan Laporta kutokana na ukweli kwamba kabla ya Ronaldinho timu haikuwa kwenye kiwango kizuri.

Guardiola ambaye timu yake ya Manchester City leo itakuwa nyumbani kucheza na Newcastle United amemaliza kwa kusema kuwa anamshukuru Ronaldinho aliondoka vizuri na hana tatizo naye.

Soma Nafasi za Ajira Zilizotangazwa Leo Jumamosi

ENGINE: ''Wolper ni Mwanamke Jasiri''

$
0
0
ENGINE: ''Wolper ni Mwanamke Jasiri''

Msanii wa muziki wa kizazi kipya Engine ambaye hivi karibuni kulikuwa na tetesi za kumng'oa Jackline Wolper na kumuweka ndani, ameweka wazi sababu za kuamua kumtumia msanii huyo kwenye kazi yake.


Akizungumza kwenye Friday Night Live Engine amesema Wolper ni miongoni mwa wanawake wachache Tanzania wanaojitambua, na ndio sababu iliyomfanya asifikirie mara mbili kumfuata.

“Wolper ni mwanamke jasiri, mwanamke anayejitambua , anajituma yuko fit kila idara, na ndio maana nikamfuata”, amesema Engine.

Msanii huyo ambaye ameachia kazi yake mpya, amewaomba watanzania kufuatilia kazi zake kwani alishafanya kazi nyingi siku za nyuma lakini hazikuwahi kufanya vizuri.

"Sitozikwa na wasanii Pekee"- Wastara

$
0
0
"Sitozikwa na wasanii Pekee"- Wastara
Msanii wa filamu nchini Wastara Juma amesema hatokuja kumladhimisha mtu yeyote katika tasnia ya 'bongo movie' kuwa yeye hana pesa ya kujitibia ugonjwa wake unaomsumbua kwa madai hata siku ikitokea akifa hawezi kuzikwa na hao pekee yao.

Wastara ametoa kauli hiyo kwenye kipindi cha 'FRIDAY NIGHT LIVE' (FNL) kinachorushwa na EATV tinga namba moja kwa vijana, baaada ya kuwepo kwa baadhi ya watu kutomuamini kwa kile kinachomsumbua huku wengine wakidiriki hata kujaribu kumwambia anatafuta kiki kupitia tatizo hilo linalomsumbua la mguu wake.

"Yani hapa mtu anaweza akaniumiza kwa maneno au vitendo kwa sababu yeye anaamini kwa mawazo yake na kichwa chake kwamba, mimi nimekaa kitandani siumwi au pengine nimejiona nimepotea katika ulimwengu hivyo natafuta kiki yaani nijifunue nguo niupige picha mguu wangu uliyochanika kisha niuweke kwenye gazeti ama kwenye runinga (Tv) ?", alihoji Wastara.

Hata hivyo Wastara amesema hawezi kubadilisha fikra za watu wanavyofikilia kwa kuwa hayo ndiyo maisha yao ya kutoamini jambo lolote lile.

"Na kama kuna wasanii ambao wanaamini mimi siumwi siwezi kumladhimisha hata siku moja na ambaye atasema hatokuja kumtembelea Wastara kwa sababu haumwi au hana shida pesa, mimi siwezi kumfanya aniamini kwamba sina pesa. Sitoweza kufanya hicho kitu kwa sababu maelezo ninayoyaeleza katika runinga ndiyo yaleyale hayotokuja kubadilika. Kwa hiyo ninachoongea hapa ni ukweli hautokuja kubadilika miaka yote hata nikifa", alisisitiza Wastara.

Pamoja na hayo Wastara aliendelea kwa kusema "wapo watu wa kweli wanaoamini na wengine wasioamini ambao huwezi kuwafanya waniamini. Watanzania wanaoniamini mimi wanatosha kwa sababu mwisho wa siku sitokuja kujizika mwenyewe au kuzikwa na wasanii pekee yake", alisema Wastara.

Waziri Mkuu Aagiza Kiongozi Huyu Akamatwe

$
0
0
Waziri Mkuu Aagiza Kiongozi Huyu Akamatwe
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa ameamuru Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) mkoa wa Mara kumkamata na kumuhoji Mkurugenzi Mtendani wa Mamlaka ya Maji Musoma (MUWASA) Mhandisi Gantala Said.


Agizo la Waziri Mkuu limekuja kufuatia tuhuma za ubadhirifu wa fedha za mradi wa maji Wilayani Bunda mkoani Mara zinazomkabili Mkuregenzi huyo. Waziri Mkuu yupo Mkoani humo kwa ziara ya kikazi.

Mhandisi Gantala Said ameshindwa kueleza sababu zilizosababisha mradi wa maji mjini Bunda kutokamilika pamoja na Serikali kutoa fedha nyingi kwaajili ya kutekeleza Kampeni ya Rais Dkt. John Magufuli ya kumtua mama ndoo kichwani.

Majaliwa amesema Mkurugenzi huyo amekuwa akimlipa mkandarasi fedha kabla ya kufanya kazi ambapo hadi sasa tayari mkandarasi wa mradi huo ameshalipwa zaidi ya Sh. bilioni saba na mradi haujakamilika huku wananchi wakiendelea kutumia maji ambayo siyo salama.

Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Mara Bw. Adam Malima ameagiza kufungwa kwa ofisi za MUWASA na kuwataka wafanyakazi wa mamlaka hiyo kutoruhusiwa kuingia ofisini hadi hapo uchungi utakapokamilika.

Mahakama Yaridhia Madaktari Kutoka Nje Waje Kesi ya IPTL

$
0
0
Mahakama Yaridhia Madaktari Kutoka Nje Waje Kesi ya IPTL
Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu imeruhusu madaktari kutoka Afrika Kusini na India kuja nchini kushuhudia matibabu ya washtakiwa wawili katika kesi inayohusu fedha za escrow.

Kesi hiyo inamkabili Seth Harbinder Singh, ambaye ni mwenyekiti wa kampuni ya Pan African Power Solutions (PAP) inayomiliki IPTL, na James Rugemalira, mkurugenzi wa VIP Engineering iliyokuwa ikimiliki asilimia 30 ya kampuni hiyo ya kufua umeme.

Wawili hao ni wagonjwa na wamekuwa wakiomba kwenda kutibiwa nje au madaktari wao waje nchini wakati wakitibiwa.

Jana, hakimu mkazi mkuu wa Mahakama ya Kisutu, Thomas Simba alikubaliana na maombi ya wawili hao baada ya Wakili Alex Balomi, anayemwakilisha Sethi, kudai kuwa wamethibitisha kuwa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH) haina uwezo wa kumfanyia upasuaji mteja wake.

Alisema MNH haiwezi kuondoa au kuweka puto lililo tumboni kwa mteja wake, hivyo kuomba  madaktari wake wa Afrika Kusini kuja nchini.

“Tumepokea maoni kutoka kwa hao madaktari wa Afrika Kusini kuwa ni lazima wawepo wakati wa upasuaji wa Sethi,” alisema wakili huyo wa utetezi.

Maombi kama hayo yalitolewa na Respicious Didas anayemwakilisha Rugemarila, aliyeiambia mahakama kuwa suala la afya ya washtakiwa ni muhimu sana na ugonjwa wa mteja wake ni bayana; kwamba ana uvimbe unaoonekana.

“Licha ya ugonjwa wa mteja wangu kuwa wazi, bado upande wa mashtaka haujachukua hatua yoyote kuhusu uvimbe huo,” alieleza Wakili Didas.

Alidai kuwa Rugemalira aliwahi kuugua saratani na kufanyiwa upasuaji mwaka 2008 na kwamba ugunduzi huo pamoja na matibabu yote, vilifanyika nchini India.

Didas alieleza kuwa matibabu na vipimo vilivyokuwa vinafanyika hapa nchini vilikuwa na matatizo na ndio maana aliamua kuanzisha kituo cha saratani nchini kwa ajili kutibu wananchi wasio na uwezo wa kwenda kutibiwa nje ya nchi, ili waweze kupata matibabu katika kituo chake.

Wakili huyo alisema anaamini mteja wake akitibiwa India ambako kuna vifaa na hivyo kuwa na uwezo wa kugundua tatizo la uvimbe alionao.

“Suala la afya ya mteja wangu linapaswa kupewa kipaumbele na ugunduzi wa ugonjwa wake ufanyike kwa kutumia madaktari wa India,” alisema.

Kutokana na maelezo ya mawakili wa utetezi, Hakimu Simba alisema mahakama inashukuru kwa kuona kuwa amri ya kutaka washtakiwa wakatibiwe iliyoitoa Januari 5, imetekelezwa.

Hakimu Simba alisema kutokana na hali hiyo, Mahakama imeona madaktari kutoka Afrika Kusini wa mshtakiwa wa kwanza, wawepo na utaratibu huohuo utumike kwa mshtakiwa wa pili.

“Magereza wawasiliane na madaktari wa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili ili madaktari ya India wawepo wakati wa upasuaji,” alisema Hakimu Simba.

Awali upande wa mashtaka ulidai kuwa Rugemalira hana saratani na pia puto la Sethi limeisha muda wake.

Mwendesha mashitaka wa Takukuru, Leonard Swai alisema  hayo wakati akitoa taarifa baada ya kwenda gerezani kama alivyotakiwa na mahakama.

Swai alisema washitakiwa hao wameomba kuwa wakati wanapofanyiwa uchunguzi wa afya, madaktari wao kutoka nje ya nchi wawepo.

“Sethi ambaye ni mshtakiwa wa kwanza katika kesi hii, anaishi na puto tumboni tangu Desemba mwaka jana na limeisha muda wake,” alisema.

“Daktari wa Muhimbili walimfanyia uchunguzi na kubaini kuwa puto hilo linatakiwa kuondolewa na mshtakiwa alishirikishwa katika hatua hiyo akaomba daktari wake kutoka Afrika Kusini awepo wakati wa kufanyiwa upasuaji na kuomba muda wa kuwasiliana na daktari huyo.”

Hata hivyo, Swai alisema madaktari wa hapa nchini wapo tayari kuondoa puto hilo kama afya ya mshtakiwa itaendelea kuathirika au kuwa mbaya.

Pia alisema Rugemalira  anatibiwa na magereza pamoja na daktari anayeitwa Fred ambaye anachukua vipimo na kupeleka hospitalini kwake Sanitas na kurudisha majibu magereza.

Alidai katika majibu hayo yanaonyesha kuwa hana saratani kama alivyodai na kwamba Serikali inafuatilia afya zao kwa kuwa hakuna jambo linaloweza kuhatarisha maisha yao.

Hakimu Simba aliahirisha kesi hiyo hadi Februari 2.


Wafanyabiashara Waijia Juu Serikali

$
0
0
Wafanyabiashara Waijia Juu Serikali
Wafanyabiashara nchini wameiomba Serikali kuacha kufanyakazi kwa kukurupuka ikiwamo kuwaadhibu kwa makosa ya wengine badala yake iwe kitu kimoja na sekta binafsi ambayo ina mchango mkubwa kwa Taifa.

Wito huo ulitolewa jana na makamu mwenyekiti wa Mfuko wa Sekta Binafsi Tanzania (TPSF), Salum Shamte kwenye mkutano baina yao na Serikali ulifanyika katika ukumbi wa Hazina mjini hapa na kuhudhuriwa na wabunge na baadhi ya mawaziri.

Shamte alisema katika baadhi ya maeneo, Serikali imekuwa ikifanya mambo kwa kukurupuka na kujikuta ikiwaumiza wafanyabiashara ikiwamo masuala ya kodi.

Makamu mwenyekiti huyo alisema sekta binafsi inaumizwa kwa kiasi kikubwa na uamuzi wa kukurupuka hasa wa kuwaadhibu watu wasiohusika kwa kosa la mtu mmoja.

“Wakati mwingine watu wanaumizwa sana kwa ajili ya maamuzi haya, kodi na kufunga biashara za watu ilhali kosa linakuwa la mtu mmoja. Kwa nini hamuondoi kasoro hiyo?” alihoji Shamte wazo ambalo liliungwa mkono na mkurugenzi mtendaji wake, Godfrey Simbeye.

Akijibu hoja hiyo, waziri wa fedha na mipango, Dk Philip Mpango alikiri kuwapo kwa uamuzi wa kushtukiza serikalini na kusema wakati mwingine inalazimika kufanya hivyo.

Dk Mpango alisema wakati mwingine kuna madhara kwa watu kukurupuka na kufanya vitu visivyokuwepo na kusema ndani ya Serikali, kuna baadhi ya watumishi wasiokuwa waaminifu ambao wanafanya vitu ama kwa kukurupuka au kutokujua.

“Nakiri kweli ndani ya Serikali kuna watu ambao wanafanya mambo ya ovyo na kuisababishia Serikali hasara kubwa, lakini kuna wakati tunafanya hivyo kwa sababu inabidi tufanye hivyo kwa masilahi ya nchi,” alisema Dk Mpango.

Hata hivyo, aliwatupia lawama baadhi ya wafanyabiashara akisema wamekuwa na tabia ya kukwepa kodi jambo ambalo ni kinyume na Serikali.

Mama Uwoya Amjia Dogo Janja juu ni Baada ya Kupachika Mimba

$
0
0
Mama Uwoya Amjia Dogo Janja juu ni Baada ya Kupachika Mimba
Staa wa sinema za Kibongo, Irene Pancras Uwoya, Naima Uwoya akiongea jambo na anayedaiwa kuwa mume wake, Abdulaziz Chende ‘Dogo Janja.


Mwisho wa mjadala! Wakati mwanaye akidaiwa kupewa mjamzito, mama mzazi wa staa wa sinema za Kibongo, Irene Pancras Uwoya, Naima Uwoya amefunga mjadala baada ya kutoa ya moyoni kuhusu ndoa ya binti yake huyo na msanii wa Bongo Fleva, Abdulaziz Chende ‘Dogo Janja’, maelezo yaliyotafsiriwa kuwa ni kumtapika jamaa huyo.



Awali, kabla ya mama Uwoya kuzungumza na Ijumaa, kwenye mitandao ya kijamii kulienea picha na vipande vya video vikimuonesha Dogo Janja na Irene Uwoya wakiwa wanafunga ndoa huku wakipongezwa na wasanii wenzao.

Mbali na kupongezwa huko, Dogo Janja pia amekuwa akitamba waziwazi mara kadhaa kwamba anafurahia kumpata mweza wa maisha yake na Uwoya kwake ni mke bora.


Drama hizo zimeendelea kwa muda mrefu huku Dogo Janja akisisitiza kila mara kwamba Uwoya ni mkewe na hata meneja wake, msanii Hamad Ally ‘Madee’ naye amekuwa akipigilia msumari kuwa wasanii hao ni mke na mume, lakini Uwoya mwenyewe amekuwa akikanusha ishu hiyo.



Katika mahojiano na Ijumaa, mara kadhaa Uwoya alifunguka kwamba, picha na vipande hivyo vya video ni vya filamu yake mpya.

DOGO JANJA AZIDI KUSISITIZA

Kwa upande wake Dogo Janja amekuwa akibanwa kwa nyakati tofauti na kuzidi kung’ang’ania kwamba, Uwoya ni mkewe suala ambalo liliifanya timu ya gazeti hili kuingia kazini ili kubaini kama kweli wawili hao wanaishi pamoja au la.

Wakati timu hiyo ikiwa kazini, Uwoya alipatwa na majanga ya kufiwa na mumewe aliyezaa naye mtoto mmoja wa kiume, Hamad Ndikumana ‘Katauti’ kisha kusafiri kwenda nchini Rwanda kwa ajili ya mazishi.

Baada ya Uwoya kurejea Bongo, madai ya yeye kuoana na Dogo Janja yalizidi kuenea na nyepesinyepesi za sasa ni kwamba mwanadada huyo amenasa ujauzito wa Dogo Janja ambaye ni maarufu kwa jina la Janjaro.



Mbali na nyepesi hizo, hivi karibuni wawili hao walionekana kwenye harusi ya mwanamuziki na mwigizaji, Zuwena Mohamed ‘Shilole’ ambapo walitambulishwa kama mke na mume kwenye, jambo ambalo lilizidi kuzua gumzo kwa baadhi ya watu ambao bado wapo njiapanda juu ya suala hilo.


Irene Pancras Uwoya akiwa katika pozi.

IJUMAA KAZINI TENA

Kwa mara nyingine Ijumaa liliingia kazini ili kukubaini kama ni kweli wawili hao wameoana na wanaishi pamoja.

NYUMBANI KWA MAMA UWOYA

Gazeti hili liliweka ‘patroo’ nyumbani kwa mama Uwoya, Mbezi-Jogoo jijini Dar, lengo hasa likiwa ni kuzungumza na mzazi wa mrembo huyo ili kubainisha ukweli, maana kama ni Uwoya na Dogo Janja, wote wamekwishazungumza, lakini maelezo yao yanatofautiana.

Baada ya kutinga nyumbani hapo mama huyo hakuwepo badala yake gazeti hili lilikutana na dada wa kazi ambaye ndiye aliyebainisha kwamba mama mwenye nyumba hakuwepo.

IJUMAA LAMVUTIA WAYA MAMA UWOYA

Juhudi za kumtafuta mama huyo ziliendelea kwa Ijumaa kumvutia waya ambapo alipopokea simu na kuelezwa kila kitu kisha kutakiwa kusema anachokifahamu juu ya ndoa ya mwanaye huyo alikuwa na haya ya kusema:

“Ngojeni niwaambie, hakuna ndoa ambayo wazazi hawashirikishwi. Ndoa yoyote lazima wazazi wahusishwe na kushiriki.

“Ninachofahamu Irene ni mjane, mumewe ambaye sisi tunamfahamu ndiye huyo ambaye amekwishafariki dunia.

“Ninachojua mimi suala la kuoa au kuolewa, lazima wazazi wanashirikishwa kuanzia mwanzo hadi mwisho, kama tulivyoshiriki kwa mkwe wetu (Ndikumana).

AFUNGA MJADALA

“Irene ni mtu mzima, siwezi kumshikilia kwa chochote na hayo niseme tu kwamba ameamua kuyafanya mwenyewe.

“Kama yeye mwenyewe hajatupa taarifa kama kuna kitu kinaendelea, hatuwezi kumfuata na hatujui kama alishawahi kupewa talaka.

“Kwanza sisi wazazi wake siyo watu wa kwenda kwenye media (vyombo vya habari) na kusema hiki na hiki. Kama ingekuwa ni ndoa, mngeiona, mbona ndoa yake ile ya kwanza ya halali mliishuhudia kila kitu na mlituona? Hii ya sasa hatuitambui.

“Tunachojua mwanetu ni mjane. Kama ana ndoa, anaijua yeye, sisi hatuamini na wala hatumtambui huyo mtu anayeitwa Dogo Janja. Labda wanaigiza.”

TULIKOTOKA

Uwoya ambaye anafahamika kuwa ni mke wa ndoa wa Ndikumana kwani hajawahi kupewa talaka, aliwahi kudaiwa kuingia kwenye mapenzi na wanaume kadhaa kabla ya sasa kugandana na Dogo Janja.

Tukio la FastJet kugonga Lazua Sintofahamu Mwanza

$
0
0
Tukio la FastJet kugonga Lazua Sintofahamu Mwanza

Hali ya sintofahamu imetanda baada ya mtu mmoja, ambaye jina lake halijajulikana, kugongwa na ndege ya FastJet iliyokuwa ikiondoka mjini Mwanza Jumatano usiku.

Uongozi wa Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwanza jana haukuwa tayari kuzungumzia suala hilo, isipokuwa kampuni ya FastJet ambayo taarifa yake ya jana ilisema ndege yake inaendelea na shughuli zake, huku Mamlaka ya Anga ikilaumu kutokuwepo kwa uzio kuzunguka uwanja huo.

Mtu huyo aligongwa saa 3:00 usiku, kwa mujibu wa FastJet.

Ukweli kwamba mtu huyo alikuwa katika njia ambayo ndege hutumia wakati wa kupaa au kutua bila ya kizuizi chochote, unatia shaka kuhusu usalama wa vyombo hivyo vya usafiri wa anga ambavyo hubeba idadi kubwa ya wasafiri.

Mwandishi wetu wa Mwanza, ambaye hakufanikiwa kupata taarifa zaidi za tukio hilo kutoka kwa wahusika, alisema mazingira ya uwanja huo yanaweka uwezekano wa kuwepo kwa ajali kama hizo.

“Kwa watu wanaoenda au kutoka Kayenze na Igombe, wanaweza kukatisha uwanja wa ndege licha ya barabara kufungwa,” alisema mwandishi huyo wa Mwananchi, Peter Saramba.

“Zamani barabara ilikuwa inakatisha uwanjani, lakini ikafungwa. Kwa sasa barabara ya magari imechepushwa kuelekea ziwani (Victoria), lakini wanaotembea kwa mguu wanaweza kukatisha uwanjani kwa kuwa hakuna uzio.

“Mwenyeji anaweza kukatisha, ila kwa huyo mtu kupita muda huo wa usiku uwanjani, haileti picha halisi ya nini kilitokea na alikuwa anatokea wapi.”

Uwanja wa Mwanza ni moja ya viwanja vikubwa nchini, vikipokea ndege za ndani na nje na unapakana na makazi, kambi ya jeshi na Ziwa Victoria. Kwa sasa Serikali inataka kuupanua.

Katika taarifa yake, FastJet imesema ndege hiyo haikupata madhara na tayari inaendelea na shughuli zake

Msemaji wa FastJet, Lucy Mbogoro alisema ndege hiyo imeruhusiwa kuendelea na safari tangu juzi asubuhi baada ya uchunguzi uliofanywa na mamlaka husika.

“Suala hili tayari limetolewa ufafanuzi na TAA ambao ndio wasimamizi wetu,” alisema.

“Hatuwezi kulizungumzia zaidi ya kuwaomba wateja wetu kutokuwa na wasiwasi kwa sababu ndege yetu haikupata madhara yoyote na inaendelea na safari tangu jana (juzi), baada ya kufanyiwa uchunguzi.”

Kaimu mkurugenzi mkuu wa Mamlaka ya Anga (TAA), Richard Mayongela alisema kukosekana kwa uzio kunaweza kuwa chanzo cha mtu huyo kukatiza.

Alisema kabla ya ndege hiyo kuruka, taratibu zote za kiusalama zilifanyika.

“Vyombo vya ulinzi na usalama vinachunguza tukio hilo kwa kina na tutatoa taarifa kamili uchunguzi utakapokamilika,” alisema.

Hata hivyo, Mayongela anataja uwanja huo kukosa uzio kuwa inaweza kuwa miongoni mwa sababu za mtu huyo kukatisha katikati ya njia ya kuruka na kutua ndege.

“Uwanja wetu wa Mwanza hauna uzio; hii inaweza kuwa chanzo cha mtu huyo kuingia katika njia ya kurukia na kutua ndege,” alisema Mayongela akitoa pole kwa familia, ndugu na jamaa wa marehemu

Ili kukabiliana na matukio ya aina hiyo alisema wataimarisha mifumo ya usalama kwenye viwanja vya ndege nchini ikiwemo kuweka uzio kudhibiti watu na vitu visivyotakiwa kuwepo maeneo ya viwanja vya ndege.

Akiwa ziarani mkoani Mwanza Oktoba 30 mwaka jana, Rais John Magufuli aliahidi kuwa Serikali ingetoa zaidi ya Sh9 bilioni kukamilisha ujenzi na upanuzi wa uwanja huo kwa kiwango cha kimataifa kama moja ya mikakati ya kuboresha miundombinu ya usafirishaji kwa jiji la Mwanza ambalo ni kitovu cha biashara kwa nchi za Ukanda wa maziwa Makuu

Katika Muziki Ushirikina Upo – Man Fongo

$
0
0
Katika Muziki Ushirikina Upo – Man Fongo
Msanii wa muziki wa Singeli, Man Fongo amefunguka tetesi za kufanyiwa ushirikina katika muziki wake ili asifanye vizuri.

Muimbaji huyo ameiambia Times Fm kuwa hawezi kujua hilo moja kwa moja kwa sababu yeye ndiye msanii mkubwa kuliko wote katika muziki huo ila ushirikina ni kitu ambacho kipo katika muziki.

“Katika muziki mambo ya ushirikina yapo lakini huwezi ukamshawishi mtu ukasema mtu fulani hamna ila vitu vinatokea, hivyo ushirikina upo,” amesema.

Ameongeza kuwa licha ya hayo yote hakuna anayeweza kushusha nyota yake kimuziki kwa sasa. Man Fongo kwa sasa anafanya vizuri na ngoma yake mpya ‘La Nafasi

Kutana na Mtabibu Mwenye KUBRI kutoka kwa ALLAH issa simba said Mtabibu wa Nyota za Binadamu na Dawa za Asili

$
0
0
Kutana na Mtabibu Mwenye KUBRI kutoka kwa ALLAH issa simba said Mtabibu wa Nyota za Binadamu na Dawa za Asili ya Africa Mwenye UWEZO Kubaini tatizo lako Pindi tu Utakapo Fanya Mawasilino Kupitia Wasaa Husika..JE UNASUMBULIWA NA Mapenzi? (Umeachwa na Umpendae,Awe Mume,Mke na Bado unampenda?Na Umejaribu Sehemu nyingi Bila Mafanikio?Wasilina na Maalim Hussein Ujione muujiza wa Papo kwa Papo.. anauwezo WA KURUDISHA MAHUSIANO NA KUIMARISHA NDOA YAKO NDANI YA SAA 12 TU. Umekimbiwa na Mumeo,mkeo au Mpenzi na anaishi na mtu mwingine? Muone akutatulie Anauwezo wa Hali ya Juu wa Kusambalatisha Mahusiano yao Endapo utafata Atakacho kuelekeza.
Atamfanya Atimize Ahadi zote kwa Muda Mfupi.

Issa simba said Anatumia Jina la Muhusika au Picha Kumaliza Tatizo lako..
Anatibu kwa Kutumia Vitabu vya QUR-AN Dawa za Asili za Africa,Dawa za Kiarabu na Majini.Anatafsiri Ndoto. Kushinda BAHATI NASIBU, KUSAFISHA NYOTA. Mvuto wa Mwili na BIASHARA, Kinga ya Mwili,ZINDIKO za Nyumba.MIGUU Kufa GANZI.Kufungua KIZAZI kwa wale walio fungwa kwa njia za KISHIRIKINA. Anakupa Jini la Mali kwa yule anaehitaji Utajiri BILA MASHARTI. Nguvu za KIUME, Humaliza Kesi zilishindika ndani ya siku 14 tu..na mengi zaidi

Wasiliana nasi +255 622588038au 0679119679 au +255 764318107

NB: TIBA KWA DINI ZOTE NA IMANI ZOTE...
Viewing all 104689 articles
Browse latest View live


Latest Images