Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104712 articles
Browse latest View live

Salum Mwalim Ajiweka Mguu Sawa Kupambana Vikali na CCM Ubunge Kinondoni

$
0
0

Mgombea Ubunge kwa tiketi ya CHADEMA katika Jimbo la Kinondoni, Salum Mwalim Juma amerudisha fomu ya kugombea Ubunge Jimbo hilo

Fomu ya Mgombea huyo ambaye pia ni Naibu Katibu Mkuu wa CHADEMA kwa Upande wa Zanzibar imepokelewa na Msimamizi Msaidizi wa Uchaguzi wa Jimbo la Kinondoni Bi. Latipha Ramadhani Almas

Jimbo la Kinondoni lilitangazwa kuwa wazi na Tume ya Uchaguzi (NEC) baada ya aliyekuwa Mbunge wake kupitia chama cha CUF, Maulid Mtulia kujiuzulu na kuhamia CCM

Salum Mwalimu pamoja na Wagombea wa Vyama vingine watachuana na aliyekuwa Mbunge wa Jimbo hilo ambaye ameipitishwa na CCM kugombea tena nafasi hiyo

Jack Wolper Ageuka Kuwa Kungwi Kwa Mabinti

$
0
0
Msanii wa filamu bongo ambaye sasa amegeukia ujasiriamli, Jackline Wolper, amewapa somo mabinti na kuwafunda juu ya kujishughulisha ili kujipatia kipato chao, na hatimaye waweze kuheshimika.

Akizungumza kwenye Friday Night Live ya East Africa Television, Jackline Wolper amesema ni wakati sasa mabinti kuacha kutegemea pesa wanazopewa na wanaume, na badala yake wajishughulishe ili kutengeneza pesa yako mwenyewe. “Wadogo zangu wa kike 2018 mi ntaendelea kuwatia hasira, na kuendelea kuwaambia kwamba hela ya mwanaume sio ya kwako, ukishachukua hela ya mwanaume fanya kitu chako, iwe hela yako, usikubali kunyanyasika, kwa hela ya mtu, kwa hiyo wadogo zangu nitaendelea kuwaisipire ili mfanye kazi ili utambe na hela yako, usitambe kwa hela ya kuhongwa”, amesema Wolper.

Hivi sasa Wolper anamiliki biashara yake ya mavazi ambayo ana buni na kushona mwenyewe, ambayo aliwahi kusikika akisema inamuingizia pesa nyingi ingawa watu wengi wakimdharau kwa kumuita 'fundi cherehani'.

Lazaro Mambosasa Akamea Trafiki Wanao Onea Wenye Vyombo vya Moto Baada ya Kuwakamata

$
0
0

Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Lazaro Mambosasa atoa maelezo ya wa jinsi Askari wa Usalama Barabarani(Trafiki), wanavyotakiwa kutekeleza majukumu yao.

Kamanda Mambosasa ameeleza kuwa Trafiki wamekuwa na tabia ya kusimamisha gari, kuomba leseni na kukagua kama dereva au mmliki wa gari ana vitu kama stika ya bima, taa, magurudumu, mtungi wa gesi ya kuzimia moto na viakisi mwanga(Reflector).

Akafafanua kuwa Askari akisimamisha gari ni lazima akueleza sababu za kukusimamisha. Pia ni lazima aeleze anataka kukagua nini katika gari lako

Akaongeza kuwa Trafiki wanatakiwa kutumia busara kumtoza faini Dereva ambaye gari lake lina matatizo ya taa kwa kuwa huenda hatumii gari hilo nyakati za usiku.

Ufafanuzi huu umekuja wakati ambapo watumiaji wa vyombo vya moto wamekuwa wakilalamikia vitendo wanavyoviita vya kionezi kutoka kwa Askari wa Usalama Barabarani pamoja na kutozwa faini kubwa kwa makosa madogo

Binti mwenye uvimbe begani afariki dunia....Waziri Ummy Amlilia

$
0
0

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu amesema amesikitishwa na kifo cha msichana Marim Sandalu (17) aliyekuwa na uvimbe begani.


Mariam ambaye ni mkazi wa Masasi mkoani Mtwara, amefariki dunia leo alfajiri akipatiwa matibabu katika Taasisi ya Saratani ya Ocean Road (ORCI).

 

Binti huyo ambaye alitakiwa kufanyiwa upasuaji Muhimbili mwaka mmoja uliopita wakati huo uvimbe ukiwa bado mdogo, alitoweka baada ya kwenda katika tiba za asili kabla ya kurejea hospitalini hapo Januari 3 mwaka huu, baadaye kuhamishiwa katika taasisi hiyo.


Waziri Ummy amesema inasikitisha kwani msaada wa Watanzania haukuweza kuokoa maisha yake.


“Tutaongeza jitihada zaidi kuwaelimisha wananchi juu ya umuhimu wa kuwahi hospitalini kufanyiwa uchunguzi na kuzingatia maelekezo ya madaktari wanayopewa ikiwamo kuanza matibabu mara moja na si kwenda kukaa nyumbani na mgonjwa,” amesema Waziri Ummy ambaye hivi karibuni alimtembelea Mariam hospitalini kumjulia hali.

Mgombea Ubunge CHADEMA Jimbo la Siha Naye Kajiapiza Kuichapa CCM

$
0
0

Mgombea ubunge wa Jimbo la Siha, kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) Elvis Mosi, amesema atashinda ubunge wa jimbo hilo mapema asubuhi kutokana na mgombea aliyepitishwa na Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dk. Godwin Mollel, kutokuwa na nguvu ya kushinda kwani amekosa sifa za kuwa kiongozi kwa madai kuwa ni mtu mwenye tamaa na asiyekuwa na msimamo.

Mgombea huyo amesema chama chake kimemuamini na kumpitisha baada ya kumpima na kuona anao uwezo wa kukabiliana na Dk. Mollel na kwamba ushindi wake utapatikana asubuhi.

“Mgombea wa CCM hawezi kamwe kushindana na mimi yaani ni ardhi na mbingu na sifa ya kumshinda tunayo, kwanza ni mtu aliye na tamaa na asiyekuwa na msimamo wananchi hawawezi kumchagua mtu wa namna hiyo kwani walimuamini lakini amewasaliti,” amesema.

Kutana na Mtabibu Mwenye KUBRI kutoka kwa ALLAH issa simba said Mtabibu wa Nyota za Binadamu na Dawa za Asili

$
0
0

Kutana na Mtabibu Mwenye KUBRI kutoka kwa ALLAH issa simba said Mtabibu wa Nyota za Binadamu na Dawa za Asili ya Africa Mwenye UWEZO Kubaini tatizo lako Pindi tu Utakapo Fanya Mawasilino Kupitia Wasaa Husika..JE UNASUMBULIWA NA Mapenzi? (Umeachwa na Umpendae,Awe Mume,Mke na Bado unampenda?Na Umejaribu Sehemu nyingi Bila Mafanikio?Wasilina na Maalim Hussein Ujione muujiza wa Papo kwa Papo.. anauwezo WA KURUDISHA MAHUSIANO NA KUIMARISHA NDOA YAKO NDANI YA SAA 12 TU. Umekimbiwa na Mumeo,mkeo au Mpenzi na anaishi na mtu mwingine? Muone akutatulie Anauwezo wa Hali ya Juu wa Kusambalatisha Mahusiano yao Endapo utafata Atakacho kuelekeza.
Atamfanya Atimize Ahadi zote kwa Muda Mfupi.

Issa simba said Anatumia Jina la Muhusika au Picha Kumaliza Tatizo lako..
Anatibu kwa Kutumia Vitabu vya QUR-AN Dawa za Asili za Africa,Dawa za Kiarabu na Majini.Anatafsiri Ndoto. Kushinda BAHATI NASIBU, KUSAFISHA NYOTA. Mvuto wa Mwili na BIASHARA, Kinga ya Mwili,ZINDIKO za Nyumba.MIGUU Kufa GANZI.Kufungua KIZAZI kwa wale walio fungwa kwa njia za KISHIRIKINA. Anakupa Jini la Mali kwa yule anaehitaji Utajiri BILA MASHARTI. Nguvu za KIUME, Humaliza Kesi zilishindika ndani ya siku 14 tu..na mengi zaidi

Wasiliana nasi +255 622588038au 0679119679 au +255 764318107

NB: TIBA KWA DINI ZOTE NA IMANI ZOTE.

Zitto Kabwe aweka wazi uwekezaji mzito Kigoma

$
0
0

Mbunge wa Kigoma Mjini (ACT- Wazalendo),  Zitto Kabwe amesema amepatikana mwekezaji wa kujenga maduka makubwa la biashara (malls) mkoani humo kama yale ya  Mlimani City ya jijini Dar es Salaam.

 

Akihutubia mkutano wa hadhara katika viwanja vya Community Center, Mwanga jana Januari 20, 2018,  Zitto amesema haiwezekani mkoa wa Kigoma ukaendelea kubaki nyuma kimaendeleo.

 

Zitto ambaye pia ni Kiongozi wa ACT- Wazalendo amesema inapofika jioni mji wa Kigoma unakuwa kimya jambo alilodai kuwa haliwezi kuleta mabadiliko na kukuza mzunguko wa fedha.


 “Tumepata mwekezaji wa kujenga mall kubwa kama ya Mlimani City ili ikifika usiku kuwe kumechangamka. Hatuwezi kuendelea kuwa mkoa au mji wa mwisho,”  amesema Zitto na kuongeza,


“Haina maana sisi watoto wenu kusomeshwa na kuuacha mji huu ukaendelea kuwa hivi. Tunahangaika, mtuache tufanye kazi na mwaka 2020 mtaniuliza kupitia kile nilichoahidi na mtaninyonga kwa nilichowaahidi.”


Kuhusu mapato ya halmashauri ya Kigoma Ujiji, Zitto amesema kitendo cha Serikali kuu kuchukua vyanzo vya mapato vilivyokuwa vikiiingizia mapato halmashauri hiyo na kutekeleza mipango yake,  imewalazimu kuongeza kodi kwa wafanyabishara.


“Tukiwaumiza kidogo katika kodi tuvumiliane na mimi sitawaangusha lakini huwezi kwenda peponi bila kufa, kwa hiyo lazima tuumie kidogo na nitakuwa kiongozi mwongo nikija hapa na kusema kila kitu mtapata ni uongo,” amesema Zitto na kuongeza,


“Sisi hatuna wa kutubeba. Lazima tupambane wenyewe na tutiane moyo. Hakuna jambo baya tunapopambana kuleta maendeleo lakini wengine wanaturudisha nyuma, haipendezi, tutiane moyo jamani.”

 

Amesema lengo ni kuubadili mji wa Kigoma kwa kuwa umekuwa nyuma kwa muda mrefu.

Miujiza ya Sharifu Seif Mohamed..JE Umeachwa na Mme/Mke au Mpenzi, Umesongwa na Mitihani ya Maisha..Piga Simu Upate Muujiza Wako

$
0
0
SHARIFU SEIF MOHAMED ANAWASHUKURU WALE WOTE WANAOENDELEA KUPIGA SIMU, WENYE MATATIZO NA WALE WANAOTOA  SHUKRANI NA SHUHUDA JINSI TIBA ZAKE ZINAVYO WASAIDIA,

(Rudisha mahusiano yako ndani ya masaa 72 tu)

SHARIFU MOHAMED Ni  mtaalam na mnajimu maarufu wa nyota na kubashiri mambo yanayo watesa binadamu duniani kote na kupata ufumbuzi, Anatumia kitabu cha QUR'AN, Dawa za Asili, Dawa za Kiarabu na majini kwa kumtuliza mke/mme, mchumba au mpenzi ndani ya masaa 72 tu, na kutatua matatizo yote ya kimaisha,

Je Umeachwa na UMPENDAE awe Mme/Mke na bado unampenda? Je Umekimbiwa na Mmeo/ Mkeo n anaishi na mtu mwingine? Je Umejaribu sehemu nyingi bila mafanikio? Mpigie simu SHARIFU SEIF sasa hivi ujionee Muujiza wa Papo kwa Papo, Anauwezo wa hali ya juu wa kusambaratisha mahusiano yao na kumrejesha kwako haraka sana na Kumfanya Atimize Ahadi zote Ndani ya Muda Mfupi Endapo Utafwata Atakacho Kuelekeza

ANAZO DAWA ZA MAPENZI, NGUVU ZA KIUME, CHANGO NGIRI MAJI NA N.K, ZINDIKO LA NYUMBA NA BIASHARA, PETE ZA BAHATI, HUMALIZA KABISA TATIZO LA NGUVU ZA KIUME NA KUREFUSHA UUME KWA SAIZI UNAYOTAKA, HUZUIA CHUMA ULETE KWENYE BIASHARA, HURUDISHA MALI ZILIZOPOTEA, MAGONJWA SUGU, MIGUU KUWAKA MOTO AU KUFA GANZI, HUTIBU BUSHA BILA KUPASUA, ANAO UWEZO WA KUMRUDISHA ALIE MBALI AU ALIECHUKULIWA MSUKULE, KUPANDISHA NYOTA NA KUSHINDA BAHATI NA SIBU, KASAFISHA NYOTA NA KUKUPA MVUTO WA AJABU, KUTOA NUKSI NA VIFUNGO MBALIMBALI,  MAFANIKIO YA MAISHA NA UTAJIRI BILA MASHARI, NA MENGINE MENGI YA SIRI,

Je UMAHANGAIKA KUPATA MTOTO BILA MAFANIKIO? WASILIANA NA MTAALAMU HUYU KWANI YEYE HUFAULU PALE WOTE WALIPOSHINDWA, PIA UMALIZA KAZI ZILIZO SHINDIKANA NA WATAALAM WENGINE NDANI YA MASAA 24 TU,

(NA ANATIBU KWA NJIA YA SIMU UKIWA NCHI YOYOTE AU MKOA WOWOTE ENDAPO UTAFWATA MAELEKEZO YAKE)

Kwa ushauri na mawasiliano  zaidi Piga SIMU No:

Mobile +255 654-836970
WhatsApp +255 756-033670 

Kamanda wa Trafiki Aunga Mkono Kauli ya Mambosasa ya Trafiki Kutosumbua Madereva Kwa Matatizo Madogo Madogo

$
0
0
Kamanda wa Kikosi cha Polisi wa Usalama Barabarani nchini, Fortunatus Muslim ameunga mkono kauli ya kamanda wa jeshi hilo Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Lazaro Mambosasa kuhusu utendaji kazi wa trafiki.

Haukuishia kuunga mkono tu, Kamanda Muslim amesema askari wa usalama barabarani wanatakiwa kuangalia makosa hatarishi yanayoweza kusababisha kutokea kwa ajali na kuachana na yale yasiyokuwa ya msingi.

Juzi, Kamanda Mambosasa aliwataka askari hususan wa usalama barabarani kutumia busara katika utendaji kazi wao ili kuondoa malalamiko ya uonevu na kuwakandamiza raia na kusisitiza kuwa Jeshi la Polisi lipo kwa ajili ya kulinda raia na mali zao na kusimamia sheria.

Akizungumza na Mwananchi jana, Kamanda Muslim alisema askari wote wa kikosi hicho wanaelekezwa kuzingatia makosa hatarishi kwa kuwa kazi kubwa ya kikosi hicho ni kuhakikisha sheria za barabarani zinazingatiwa ili kupunguza ajali zinazogharimu maisha ya watu.

Alisema kuna makosa ambayo hayana athari kulingana na mazingira husika hivyo askari hawana sababu ya kuyapa kipaumbele.

“Naungana kabisa na Mambosasa ila mimi nisitumie neno busara labda niseme askari wakamate makosa hatarishi, mnamkamata vipi dereva kwa kosa la taa mchana au wiper mbovu wakati wa jua kali? Hayo yote hayawezi kusababisha ajali kwa nyakati hizo. Hapo ndipo linapokuja suala na mazingira, wiper zinatakiwa kufanya kazi kipindi cha mvua.”

Kuhusu askari wa usalama barabarani kumsimamisha dereva na kuanza kutafuta kosa, Kamanda Muslim alisema ni muhimu kwa madereva kuzingatia sheria si muda wote wanasimamishwa kwa sababu ya makosa.

“Tatizo ni kwamba madereva wenyewe wameshajenga mtazamo hasi, sio kila wakati askari anapokusimamisha lazima uwe na kosa inawezekana anataka kukupa tahadhari huko unakoelekea sio kuzuri hivyo uongeze umakini.

“Ninachosisitiza madereva wafuate sheria, waache kulalamika. Wakizingatia sheria sidhani kama hao askari watakuwa wanawasimamisha ovyo kama wanavyodai,” alisema Kamanda Muslim.

Pia aliungana na Mambosasa kuwataka madereva wasikubali kutoa fedha kwa askari bila kupata risiti zinazotokana na mashine au fomu namba 101 ya polisi inayofahamika kama ‘notification’.

Kadhalika alisema askari wa pikipiki maarufu kama tigo wataendelea kufanya kazi yao ya kuzuia uhalifu unaohusisha makosa ya jinai na usalama barabarani na kusisitiza kuwa hawana mamlaka ya kutoza faini.

Ukusanyaji wa mapato

Kamanda Muslim alionyesha kukerwa na watu wanaohusisha tozo zinazotokana na makosa ya barabarani na ukusanyaji wa mapato.

Alisema kazi ya kukusanya mapato inafanywa na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) tofauti na tozo zinazokusanywa na kikosi hicho kutokana na uvunjifu wa sheria barabarani.

“Nashangaa wanaosema tunakusanya mapato kwani Jeshi la Polisi lina biashara gani? Sisi tunatoza tozo zinazotokana na makosa ya barabarani na lengo letu ni kuzuia ajali na kuhakikisha usalama unakuwa wa kutosha katika barabara zetu.

“Tozo hizo zipo kwa mujibu wa sheria na anayepaswa kulipa ni yule aliyevunja sheria na inasimama badala ya kifungo kwa hiyo watu wanapaswa kutambua askari wa usalama barabarani hawakusanyi mapato.”

Hali ya usalama barabarani

Kamanda hiyo alisema hali ya usalama barabarani nchini imeimarika na ajali zinaendelea kupungua kwa kiasi kikubwa.

Alisema hiyo inatokana na askari wa kikosi hicho kuimarisha ukaguzi na usimamizi wa sheria.

“Nikitolea mfano wa leo (jana) yaani ndani ya saa 24, nchi nzima kuna ajali tatu pekee. Hii ni hatua kubwa na siku nyingine hakuna ajali kabisa hayo ni matokeo ya usimamizi wa sheria kazi inayofanywa vizuri kabisa na askari wa kikosi cha usalama barabarani.

“Usimamizi wa sheria umeongezwa maradufu kwenye maeneo ya kuvukia watembea kwa miguu, nimesisitiza lazima dereva asimame aangalie pande zote ndipo apite hata kama hakuna mtu anayevuka. Kwa magari yanayosafiri ukaguzi unafanyika kabla hayajatoka vituoni na madereva tunawapima ulevi, huko njiani askari nao wanajipanga vizuri.”

Kamanda Muslim alisema jitihada zote hizo zinafanyika kuhakikisha ajali zinapungua au kutokomezwa kabisa.

Alisema, “Hatuwezi kuvumilia watu wapoteze maisha sababu ya madereva wazembe, hatutafungua ‘tuition’ barabarani ya kutoa elimu. Kama unataka elimu acha gari lako nyumbani ukija nalo barabarani na ukavunja sheria neno ni moja tu “kamata” na watalipa faini na wale ambao watakuwa wagumu zaidi kuelewa neno lao ni “funga” hawa tutawafungia leseni zao.”

Kimenuka..Kamati ya Bunge Yashtushwa na Bei Nyumba za NSSF

$
0
0
Wajumbe wa Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC) wameshtushwa na bei ya kuuza nyumba za mradi wa Shirika la Hifadhi ya Jamii (NSSF) zilizoko eneo la Dege Kigamboni jijini Dar es Salaam wakisema haziendani ya hadhi na hali ya wananchi walio wengi.

Kwa mujibu wa Mkurugenzi wa NSSF, Profesa Godius Kahyarara, bei za nyumba za Dege ni kati ya Dola za Marekani 110,000 (Sh220 milioni) hadi Dola 250,000 (Sh500 milioni) kulingana na aina ya nyumba.

Wakizungumza jana baada ya kutembelea miradi ya NSSF jijini Dar es Salaam, wabunge hao walitilia shaka uuzwaji wa nyumba hizo huku shirika hilo likikiri kutozitangaza mapema kwa wateja.

Mwenyekiti wa PAC, Naghenjwa Kaboyoka alisema nyumba za mradi wa Dege hazina hadhi ya kuuzwa bei hiyo.

“Ukiangalia nyumba zenyewe zina ‘poor quality’ (kiwango cha chini), hata ukiangalia ‘design’ yake sio nzuri. Vyumba ni vidogo, hivi kweli mtu atashawishika kutoa Sh200 milioni kununua nyumba hiyo?” alihoji Kaboyoka.

Hoja hiyo, iliungwa mkono na Mbunge wa Magomeni Zanzibar, Jamal Kassim akisema hazikujengwa kwa kuwalenga watu wa kipato cha chini.

“Hizi nyumba hazikujengwa kwa ajili ya watu wa kipato cha chini, bali wenye kipato cha juu hasa wageni. Hata hivyo, kwa kuwa wameshawekeza fedha lazima mradi ukamilike na nyumba ziuzwe,” alisema.

Mbunge wa Viti Maalumu Dodoma, Felister Bura alihoji upatikanaji wa wateja ikiwa watumishi wa umma wanaotegemewa wengi wao wanahamia Dodoma ambako ndiko makao makuu ya nchi.

Akijibu hoja na maswali ya wabunge, Profesa Kahyarara alisema nyumba hizo za Dege zitauzwa kati ya Dola 110,000 hadi Dola 125,000 kwa moja na Dola 195,000 hadi Dola 250,000 kwa nyumba aina ya villa.

Alisema mteja atatakiwa kulipa kwa muda wa miaka sita.

Mbali na mradi wa Dege, NSSF pia iliwaonyesha wajumbe hao wa PAC mradi wa Dungu, ambao Profesa Kahyarara alisema una nyumba 439 na umegharimu jumla ya Sh89.5 bilioni.

“Mradi wa nyumba hizo utakamilika Juni mwaka huu na mpaka sasa tumeshatumia Sh50 bilioni,” alisema Profesa Kahyarara.

Kuhusu mradi wa Toangoma wenye nyumba 161, mkurugenzi huyo alisema umetumia gharama ya Sh61 bilioni.

Hata hivyo, Profesa Kahyarara alikiri kutozitangaza nyumba hizo mapema jambo lililozua maswali kwa wabunge kuhusu uhakika wa kuziuza.

Mbali na bei hizo, pia imeelezwa kuwa mvutano wa hisa kati ya NSSF na kampuni ya Azimio ni chanzo mojawapo cha kucheleweshwa kwa mradi wa nyumba zaidi ya 7,000.

Profesa Kahyayara aliiambia kamati hiyo kuwa mradi huo umeshatekelezwa katika awamu mbili na nyumba 3,750 zimeshakamilika kati ya 7,160 za mradi mzima.

Kwa mujibu wa mkataba huo, kampuni ya Azimio iliyotoa ardhi ya hekta 300 inamiliki hisa asilimia 55 huku NSSF iliyowekeza zaidi ya Dola 500 ikimiliki hisa asilimia 45.

Alisema mradi huo ulitarajiwa kukamilika mwisho wa mwaka huu lakini haitawezekana kutokana na dosari za mkataba. Baadhi ya wajumbe wa PAC walihoji sababu ya mkurugenzi wa kampuni ya Azimio kutoonekana kila anapotafutwa.

Mbunge wa Viti Maalumu Mkoa wa Kilimanjaro, Shaly Raymond alisema kuchelewa kwa mradi huo kutapandisha gharama kutoka Dola 544 milioni hadi 700 na kuhoji nani atakayelipa, huku pia akihoji sababu za mwekezaji wa Azimio kutokuwapo katika ziara hiyo.

“Angalia hiyo meza kuu, mwekezaji hayupo, wewe mkurugenzi umekuja peke yako, wenzako wako wapi?” alihoji Shaly.

Mbunge Bura alisema kama Azimio hawataki kuonyesha ushirikiano, atafutwe mwekezaji mwingine. “Tulipozungumza na mwekezaji huyu alikubali kupunguza hisa zake kwa sababu amewekeza kidogo. Kama anasumbua, NSSF waangalie namna ya kupata mwekezaji mwingine.”

Akijibu hoja za wabunge, Profesa Kahyarara alikiri kucheleweshwa kwa mradi huku akisema bado wanajadiliana na kampuni ya Azimio.

Alimtetea mwekezaji huyo akisema amekuwa na safari nyingi nje ya nchi na kwamba atakuwepo kwenye kikao cha Januari 26 na mambo yote yatajadiliwa na kutolewa uamuzi.

Faiza Ally Amfungukia Diamond 'Diamond Bado ni Kijana Mdogo Anahitaji Kuenjoy na Watoto Wenzake na sio Wanawake Wazima'

$
0
0
Muigizaji wa Filamu nchini Tanzania, Faiza Ally amempa ushauri msanii wa muziki wa Bongo Fleva Diamond Platnumz kuwa kwa sasa ni muda wake wa kula ujana na kuizunguuka dunia na sio muda wa kujipa majukumu mazito ile hali umri wake bado mdogo.

Faiza Ally amesema Diamond bado hajamaliza hata robo ya dunia hivyo ingawaje ana jina kubwa barani Afrika hivyo angefanya kwanza vitu kama hivyo kuizunguuka dunia ikibidi ajiweke kando na mambo ya mahusiano.

“Diamond kijana mdogo sana anahitaji kuhave funny na watoto wenzie na sisi wadada wazima lazima taungalie watu wa kutoka nao, Go baba have a funny enjoy the world ndio useto down,“ameandika Faiza Ally kwenye ukurasa wake wa Instagram na kumshauri kuwa ikibidi ajiweke mbali na mahusiano.

“Jiachie uwe huru ikibidi usiwe na mahusiano, bado hujaiona dunia hata robo wewe ni star hela ipo there is alot to see nasema with clean heart no hate kwa Zari au kwa yeyote.“ameandika Faiza.

Ushauri huo umekuja ikiwa ni wiki sasa imepita tangu kuenee tetesi kuwa Diamond Platnumz yupo kwenye mahusiano na msichana maarufu kwenye mitandao ya kijamii anayejulikana kwa jina la Tunda.

Breaking News: ACT Wazalendo Wametangaza Kujitoa Kwenye Marudio ya Uchaguzi

$
0
0
Chama cha ACT Wazalendo kupitia kwa Naibu Katibu Mkuu wake Bara Msafiri Mtemelwa kimetangaza kutoshiriki Uchaguzi mdogo wa marudio katika Majimbo ya Kinondoni na Siha.

 Mtemelwa alisema wamefikia hatua hiyo baada ya kuona mazingira ya Uchaguzi ambayo waliyalalamikia kwa Tume ya Uchaguzi hayajafanyiwa marekebisho.

Mrembo Johari Afunguka Siri ya Kifo cha Mama yake..'Nimepambana Jamani'

$
0
0
MREMBO wa filamu za Kibongo, Blandina Chagula ‘Johari’ ameanika siri ya kifo cha mama yake kwa kueleza namna ambavyo alipigana kutetea kifo cha mama yake mzazi.

Johari alipata pigo hilo usiku wa kuamkia Jumatano iliyopita katika Hospitali ya Hindu Mandali, jijini Dar es Salaam baada ya mama yake kulazwa kwa ugonjwa wa kisukari kwa saa chache tangu afikishwe hospitalini hapo.

Kabla ya kupatwa na umauti huo, Johari alikuwa akiishi na mama yake mzazi, maeneo ya Gereji, Mabibo jijini Dar ambapo kwa zaidi ya miaka mitatu, msanii huyo alihangaika kutetea uhai wa mama yake, kwa nyakati tofauti.

Katika kipindi chote hicho, Johari alikuwa mzito sana kuelezea mateso aliyokuwa anayapitia mama yake, zaidi alikuwa akiwaelezea watu wake wa karibu sana. Akizungumza na Risasi Jumamosi, akiwa kwenye nyumba ya familia, Mburahati jijini Dar, Johari alisema kifo cha mama yake kimekuwa pigo kubwa kwake na kueleza namna alivyopambana kumpigania.

“Nimehangaika jamani. Nilikuwa silali, mchana na usiku nilikuwa nikipambana kuhakikisha naokoa maisha ya mama yangu. “Unajua alikuwa kuna wakati anakuwa na hali nzuri, kuna wakati ndio hivyo kikipanda, hali inakuwa mbaya sana. Kwa miaka zaidi ya mitatu nimekuwa nikipambana na afya ya mama yangu,” alisema Johari huku akilengwalengwa machozi.

Akizungumza kuhusu ratiba ya mazishi Jumatano iliyopita, muigizaji Salum Mchoma ‘Chiki’, ambaye alichaguliwa kuwa msemaji wa familia, alisema siku ya Alhamisi (juzi), mwili wa mama yake Johari ungefikishwa nyumbani hapo kisha ungepelekwa Msikitini wa Mbukusi, Mburahati baadaye kuzikwa katika Makaburi ya Kisutu jijini Dar. Msiba huo ulihudhuriwa na waigizaji wengi akiwemo, Vincent Kigosi ‘Ray’, Ndambangwe Misayo ‘Thea’, Sabrina Rupia ‘Cathy’, Nuru Nassor ‘Nora’ na wengine wengi.

'Chupi' Matatani Lindi

$
0
0
'Chupi' Matatani Lindi
Mfanyabiashara wa duka kata ya Chamazi, wilaya ya Temeke, Dar es Salaam, Mateso Chupi (39) amefikishwa mahakama ya wilaya ya Lindi, akikabiliwa na shitaka la kukutwa na vipande sita vya meno ya Tembo vyenye thamani ya Tsh,67,365,000 visivyo halali.


Chupi amefikishwa kwa Hakimu wa Mahakama ya wilaya hiyo, Mussa Ngaru, Januari 19 mwaka huu, na kusomewa shitaka linalomkabiri na mwanasheria wa serikali, Abdurahamani Mohamedi.

Mshitakiwa Chupi inadaiwa kukamatwa na vipande hivyo vya Meno,eneo la kituo cha kuuzia Mafuta mjini Liwale Septemba 27/2008,na kufanikiwa kuwatoroka askari na kwenda kuishi nchi Jirani ya Msumbiji.

Mshatakiwa amekamatwa nchini Msumbiji Januari 16 mwaka huu,na askari Polisi waliokuwa wakimsaka kwa udi na ubani kwa muda mrefu.

Akisomewa Shitaka linalomkabiri mbele ya Hakimu Ngaru, mwanasheria wa Serikali Abdurahamani Mohamedi alidai mshitakiwa alikamatwa na askari Polisi akiwa na vipande hivyo sita,Septemba 27/2008,akiwa tayari kuvisafirisha kuelekea kutafuta soko.

"Mh,Hakimu huyu mshitakiwa alikutwa eneo la kituo cha kuuzia Mafuta pale Liwale mjini,akijiandaa kwa safari,lakini kabla ya kuondoka alikamatwa na askari Polisi"Alisema Mohamedi.

Mwanasheria huyo alidai kuwa mshitakiwa ambaye hakutakiwa kujibu wala kukataa amefanya kosa chini ya kifungu cha (70) kifungu kidogo cha (1) na (2) na (3) cha Sheria na (283) na kifungu cha (57) cha Sheria ya Uhifadhi wanyama pori namba 5/2009,ikisomwa pamoja na Sheria ya hujumu uchumi,sura ya 200 marejeo ya 2002.

Hata hivyo mshitakiwa hakutakiwa kusema lolote, kwani Mahakama hiyo kisheria haina uwezo wa kusikiliza kesi za aina hiyo hadi hapo itakapopata kibari kutoka kwa Mkurugenzi wa Mashitaka nchini (DPP).

Mshitakiwa Mateso Chupi amepelekwa rumande ambapo kesi hiyo namba 01/2018,itafikishwa tena katika Mahakama hiyo Januari 31 mwaka huu.

Waziri Dkipa Siku 14 Kiwanda cha Dangote

$
0
0
Waziri Dkipa Siku 14 Kiwanda cha Dangote
Naibu Waziri wa Madini, Doto Biteko ametoa siku 14 kwa uongozi wa kiwanda cha Saruji cha Dangote Mkoa wa Mtwara kuingia mkataba na wachimbaji wadogo wa gypsum.


Biteko ametoa agizo hilo baada ya kutembelea kiwanda hicho na kuzungumza na uongozi ambapo amesema mikataba hiyo inapaswa kuwa na kipengele cha kuwalipa ndani ya siku 30 baada ya kiwanda kukusanya gypsum kutoka kwa wachimbaji hao, lengo likiwa ni kuleta ufanisi na tija katika biashara zao.

Aidha Biteko amesema wachimbaji hao wamekuwa wakilalamikia kucheleweshewa malipo yao baada ya kupeleka kiwandani bidhaa zao hivyo kuagiza jambo hilo limalizike na watu wapate haki zao.


Katika hatua nyingine Biteko amesema Serikali ya awamu ya tano inalenga kuwasaidia wachimbaji wadogo sambamba na wawekezaji ambao wanapaswa kufanya kazi bila kusumbuliwa.

ACT Wazalendo Kutoshiriki Uchaguzi Kinondoni, Siha

$
0
0
ACT Wazalendo Kutoshiriki Uchaguzi Kinondoni, Siha

Chama cha ACT-Wazalendo kimesema hakitashiriki uchaguzi katika majimbo ya Kinondoni na Siha kwa kuwa sababu zilizowafanya wasusie uchaguzi mdogo uliopita,  bado hazijafanyiwa kazi.

Akizungumza na waandishi wa habari leo Januari 21, 2018 Naibu Katibu Mkuu wa chama hicho-Bara, Msafiri Mtemelwa amesema changamoto walizozilalamikia katika uchaguzi wa Januari 13 katika majimbo ya Singida Kaskazini, Songea Mjini na Longido bado hazijafanyiwa kazi.

Amesema bado chama hicho kitaendelea kushinikiza Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) kufanya mageuzi katika mchakato wa uchaguzi.

Amesema malalamiko ya chama hicho kwa NEC ni matumizi ya nguvu ya vyombo vya dola dhidi ya vyama vya upinzani kwa lengo la kukisaidia chama tawala CCM.

Uchaguzi wa Siha na Kinondoni unafanyika baada ya waliokuwa wabunge wa majimbo hayo kuhamia CCM Desemba mwaka jana.

Mashabiki Wawili wa WCB Wafariki Dunia kwa Ajali

$
0
0
Mashabiki Wawili wa WCB Wafariki Dunia kwa Ajali
Mashabiki hao waliopata ajali ya gari maeneo ya Chalinze wakitokea Morogoro kurudi Dar es Salaam, ni Philly Nevvo na mwingine ni Platnumz Mondi kwa majina ambayo walikuwa wanatua Instagram.

Bongo5 bado inafuatilia taarifa zaidi za ajali hiyo lakini rais wa WCB, Diamond Platnumz amesikitisha kutokea kwa ajali hiyo.

“Mbele Yenu Nyuma yetu, Siku zote tutaendela kuwakumbuka na kuthamini Mapenzi na mchango wenu Mkubwa kwa @wcb_wasafi…..Mwenyez Mungu azilaze Roho zenu mahali pema peponi….amen🙏 @philly_nevvo_msafi @,” aliandika Diamond.

Miaka 14 Jela Sio Mchezo, Lazima Tuwamiss Mashabiki – Papii Kocha na Babu Seya

$
0
0
Miaka 14 Jela Sio Mchezo, Lazima Tuwamiss Mashabiki – Papii Kocha na Babu Seya
Muimbaji nguli wa muziki wa dance, Nguza Viking maarufu kama Babu Seya pamoja na mwanae, Papii Kocha wameanza maandalizi ya ujio wao mpya, ikiwa ni takribani miaka 14 tangu waachie kibao kipya.

Wawili hao walipewa msamaha na Rais Dkt John Magufuli kwenye maadhimisho ya miaka 56 ya Uhuru. Serikali imeonesha nia ya kuwasaidia waimbaji hao wanaopendwa sana kurejea tena kwenye muziki kwa kishindo.

Naibu Waziri wa Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo, Bi. Juliana Shonza aliwakutanisha na uongozi wa Wanene Studios waliokubali kuchukua jukumu la kuwarudisha tena kwenye muziki. Tayari wameanza kuingia studio kuandaa kazi mpya katika studio hizo kubwa na bora zaidi katika ukanda wa Afrika Mashariki na kati.

Wameanza kwa kufanya photoshoot, kitu ambacho wamekiri kuwa ni kigeni mno kwao kutokana na kuwa gerezani kwa miaka 14 na wametoka katika nyakati ambazo muziki wa Tanzania umepiga hatua kubwa ukilinganisha na zamani.

“Miaka 14 si mchezo, mambo kama haya si unayaona mwenyewe, niliyamiss, nimemiss vitu vingi, picha za ukweli, mambo haya kule tulipotoka hamna. Lazima uelewe hii ni dunia nyingine,” alisema Papii Kocha wakati wa photoshoot.

Kwa kujiamini, Papii amesema kuwa kazi zao mpya zitakuwa kali zaidi ya zile za zamani. “Kwasababu tumejipanga vizuri na kazi zinazokuja zitakuwa nzuri zaidi ya zile tulizofanya mwanzo,” amesisitiza Papii.

Kwenye photoshoot hiyo iliyofanywa na mpiga picha mahiri Eric Luga, Babu Seya na Papii Kocha walivalishwa na mbunifu wa mavazi, Mtani Nyamakababi.

Unaweza kufuatilia kila hatua ya safari yao kuelekea kuachia kazi mpya kwa kulike ukurasa wao rasmi wa Instagram @babanamwana, Facebook: baba na mwana. Pia subscribe kwenye channel yao ya Youtube iitwayo Baba na Mwana kuona video mbalimbali za behind the scenes.

George Weah kukalia kiti cha Urais Liberia leo

$
0
0
George Weah kukalia kiti cha Urais Liberia leo
Rais mteule wa Liberia George Oppong Ousman Weah ambaye pia amewahi kuwa mchezaji bora wa soka wa dunia, anatarajiwa kuapishwa leo kuwa Rais kamili wa nchi hiyo.

Weah ambaye alishinda kiti hicho mwezi uliopita atakuwa Rais wa 25 wa Liberia akichukua mikoba ya Rais Ellen Johnson Sirleaf ambaye amekalia kiti hicho kwa miaka 12.

Tukio hilo ambalo linasubiriwa kwa hamu kubwa na wananchi wa Liberia pamoja wa wadau wa soka duniani, litafanyika katika uwanja wa mpira wa Samuel Kanyon Doe majira ya saa sita mchana kwa saa za Afrika Mashariki.

Hii ni historia fupi ya George Weah.

Raisi Mteule wa Liberia 🇱🇷 ;

Senator: wa bunge la Liberia 2015

African Footballer of the (1989, 94, 95)

UEFA Champions League Top Scorer: 1994 – 15

1995 Ballon d’Or winner, FIFA World Player of the Year: 1995

1996 FIFA Fair Play Award

IFFHS African Player of the Century: 1996

Isha Mashauzi Aibuka na Jipya Kuhusu Taarabu

$
0
0
Isha Mashauzi Aibuka na Jipya Kuhusu Taarabu
Msanii Isha Mashauzi maarufu kama Jike la Simba ameibuka na kusema muziki wa miondoko ya taarabu nchini hauwezi kufa kama baadhi ya watu wanavyodhani, kwa madai wao hawategemei 'kiki' katika kufanya kazi zao kama wanavyofanya wasanii wengine.

Isha amebainisha hayo wakati akitambulisha 'video' yake mpya ya wimbo 'nibembeleze' kwenye kipindi cha 'FRIDAY NIGHT LIVE' (FNL) kinachorushwa na EATV tinga namba moja kwa vijana, baada ya kuwepo minong'ono mingi kwa wapenzi na mashabiki wa nyimbo hizo wakidai huenda muziki huo umekufa, kwa maana hawasikii vijembe vya maneno wanavyopigana wasanii wenyewe kwa wenyewe kama wanavyofanya baadhi ya waimbaji wa muziki wa bongo fleva.

"Taarabu haiwezi kufa, naweza kusema ni muziki mama wa Afrika, Tanzania au hata duniani. Muziki wa taarabu ukipigwa sehemu yeyote kila mtu ataujua fika kwamba hii ni taarabu tofauti na muziki mingine kwa hiyo hauwezi kufa", alisema Isha Mashauzi.

Pamoja na hayo Isha ameendelea kwa kusema "naweza sema tu kwamba labda wanamuziki wa taarabu hawapendi zile kiki ambazo zipo kwa wanamuziki wengine, leo utasikia huyu sijui anatoka na fulani mara yule vile ndiyo mwisho wa siku aachie kazi yake mpya. Hicho kitu kwenye taarabu hamna naweza kutetea hivyo ndiyo maana wanasema hivyo"
Viewing all 104712 articles
Browse latest View live




Latest Images