Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104747 articles
Browse latest View live

HUDDAH MONROE AMCHANA LIVE VERA SIDIKA KWA KUSEMA ANAMILIKI NYUMBA NIGERIA..VERA AMJIBU

$
0
0
Well, yo'all know them for flaunting their cash, or shaking their booties while showing off what they've got...the Bootylicious Vera Sidika and Socialite Queen Huddah Monroe, the two ladies who rule the socialite industry in Kenya. As it seems, Vera Sidika of late has been claiming to own a mansion in Abuja, Nigeria a  fact that has not gone down well with other socialites, Huddah Monroe in particular.
In response to Vera Sidika's self professed glory, Huddah Monroe attacked Vera on her Instagram account mocking her that she claims to have a big mansion in "ABUJA" yet she doesn't even own a Kitched in Kenya....oh sorry..not a Kitchen, but a small house, at least. Check it out
Lets wait for Vera's response...lets just hope its gonna be big.
And just like we said...Vera Sidika has replied to Huddah Monroe, calling her a Jealous Bitch

BREAKING NEWS:WATU 200 WALIOKUWA WAKISAFIRI KWA NDEGE YA ETHIOPIAN AIRLINE WANUSURIKA KUFA BAADA YA KUTUA DHARURA KWENYE UWANJA WA NDEGE WA ARUSHA

$
0
0
Watu 200 waliokuwa wakisafiri kwa ndege ya Ethiopian Airline wanusurika kufa baada ya ndege kupitiliza hadi nje ya uwanja mdogo wa ndege wa Arusha baada ya kutua kwa dharura.

 Watu 200 waliokuwa wakisafiri kwa ndege ya Ethiopian Airline wanusurika kufa baada ya ndege kupitiliza hadi nje ya uwanja mdogo wa ndege wa Arusha baada ya kutua kwa dharura.

UFISADI MPYAAA WA MWENYEKITI WA TAIFA CHADEMA NA MBUNGE WA HAI, FREEMAN MBOWE WAANIKWA

$
0
0

Imeandikwa na 
Habibu Mchange
0762178678:
-------
 Juzi niliandika kuhusu unafiki wa MBOWE kuwahadaa Watanzania ya kwamba yeye hanunuliki, nilitoa ushuhuda wa MBOWE kupokea million 100 kutoka kwa ROSTAM AZIZ aliyekuwa mwanamkakati muhimu wa ushindi wa Urais kwa mgombea wa CCM mwaka 2005 Mheshimiwa JAKAYA KIKWETE, ambapo pesa hizo zilipokelewa mwezi oktoba 2005 na kumfikia mbowe kupitia kwa mke wake ndugu LILIAN MTEI MBOWE, na kumfikia MBOWE ambaye kipindi hicho alikuwa anagombea URAIS kupitia CHADEMA,

hapa mbowe sio tu kwamba alinunuliwa, alihongwa ama kutumiwa kuwadhoofisha wapinzani waliokuwa na nguvu kipindi hicho, bali pia alidhihirisha namna gani yeye ni mpinzani mtiifu kwa CCM (alikubali kutumika) na ni MNAFIKI ALIYETUKUKA.

Leo tarehe 18.12.2013, Magazeti kadhaa yameripoti juu ya muendelezo wa unafiki wa MBOWE na vibaraka wake.

Magazeti yameandika pamoja na mambo mengine, kwa ufupi kabisa hivi ifuatavyo.

• Amemshinikiza mbunge wa viti maalum ndugu JOYCE MUKYA kukatisha ziara ya kikazi za kibunge alipopangiwa na kumlazimisha wakakutane nyumbani kwake DUBAI, inawezekana ni kwenda kumlea motto wao FREELADY MBOWE, ama vinginevyo, lakini huu ni uthibitisho wa UNAFIKI wa MBOWE mbele ya WATANZANIA, kushiriki kutumia kodi za watanzania kwa matumizi binafsi tena ya KIMAPENZI na mwanamke aliyemteua kuwa mbunge bila ya kuwa na uwezo wa kukidhi vigezo vya uteuzi wa UBUNGE ndani ya chama. Kwa sasa JOYCE MUKYA ni mbunge, Hawara na mama wa motto mmoja aitwaye FREELADY MBOWE, Aliyejifungulia NEW YORK NCHINI MAREKANI kwa kutumia kodi za Watanzania.


• MFUASI WAKE ASIYEJIELEWA – JOSHUA NASSARY, wiki chache zilizopita mbunge huyu wa UPEPO WA CHAMA alishiriki kumtuhumu ndugu Zitto Kabwe Kuwa anasafiri nchi nyingi ili apate posho za safari, afadhali aliyemtuhumu kuwa anasafiri, lakini yeye ameumbuliwa kuwa AMESHIRIKI KUCHUKUA pesa za UMMA WA WATANZANIA, kisha kutokwenda kushiriki ziara ya kimafunzo kwa maslahi ya nchi. Million 8 alizopewa nassary si pesa nyingi kusema anaweza kutia hasara sana, lakini ni pesa zinazoweka rehani ule upambanaji anaojitambulisha nao mbele ya jamii, ni pesa zinazoweka hatiani uwajibikaji anaojitamba nao, ni pesa zinazomdhihirisha kwamba yeye ni mwizi wa mali ya umma kama walivyo wezi wengine.

UNAFIKI WA AWALI WA MBOWE NA WAFUASI WAKE.

• Walijitangaza hadharani kuwa Hawapokei na wanapinga posho, LAKINI MPAKA SASA WANARAMBA POSHO KAMA KAWAIDA, na pindi inapotokea imecheleweshwa kulipwa wanasimama kidete kuidai, mwanachadema pekee asiyepokea posho ni ZITTO KABWE.

• MBOWE, kwa mbwe mbwe kubwa alilirudisha gari la kiongozi wa upinzani, kwa nderemo, vigeregere, matarumbeta waandishi wa habari na vifijo, kuwa kutumia gari la KUB ni kuwakosea Watanzania, kuwadharirisha na kuzitumia vibaya rasilimali za Taifa letu, hapa mbowe akajidai ni mzalendo, tuliokuwa tunamfahamu tulicheka tukamuacha kama ataweza kuhimili alichokisema.

• MBOWE, kwa aibu kubwa, akajirudishia gari la KIONGOZI WA UPINZANI, hapa akatafuna matapishi yake mwenyewe, ila safari hii alifanya kimya kimya.

• Kwa masikitiko makubwa hivi sasa mbowe anashirikiana na watuhumiwa wengine wanaomiliki mali nyingi nje ya nchi ikiwemo uswiz na kwengineko. 

• Mbowe anamiliki NYUMBA TATU, Pesa na mali nyinginezo nje ya nchi, anamiliki NYUMBA – AFRIKA YA KUSINI , DUBAI NA MAREKANI. Ameshaitwa kuhojiwa namna alivyoweza kuzipata NYUMBA HIZO ama kama kuna biashara anafanya zaidi ya UMILIKI WA DANGURO LA BILLCANAS.

• Mbowe anawatetea watoto wa kimasikini wa Kitanzania, ili hali watoto wake wote sio Watanzania kwa Kuzaliwa, Mpaka sasa anajitamba kwenye vikao vya chama kuwa mtoto wake mmoja amezaliwa NEW YORK (Huyu ni mmarekani wa kuzaliwa), Mtoto wake Mwingine amezaliwa LONDONI huyu ni Muingereza kwa kuzaliwa , na motto wake wa sasa hivi aliyemzaa na JOYCE MUKYA amezaliwa NEW YORK (Huyu naye pia ni mmarekani wa kuzaliwa). Uzalendo wa MBOWE uko wapi mpaka sasa?.

UNAFIKI ZAIDI

Naomba nishirikiane nanyi kujiuliza maswali machache, UKO WAPI UZALENDO WA MBOWE?, 
Kuna Tofauti gani kati ya mali za Mbowe nje ya Nchi na Vijisenti vya Andrew Chenge?. Mbona hawa wote ni wamiliki wa mabilioni nje ya nchi?.

Uzalendo wa Mbowe unatokana na nini kwa Watanzania, kwanini Watanzania Tumpende Mbowe ambaye hatupendi?, hapendi shule zetu, Hapendi Hospitali zetu, hapendi ardhi yetu ndio maana anamiliki majumba nchi za nje.

Kwanini tusiamini mbowe anashiriki kutuchafua kama Taifa hasa vijana akijua kabisa watoto wake yeye sio Watanzania. Ina maana mbowe hapendi watoto zake waje kuwa viongozi wa Taifa hili kama ilivyo kwake?, kama la, kwanini amewanyang’anya haki ya wao kuwa watanzania wa kuzaliwa?.

Nimeamua kujitoa Muhanga kuwaelewesha masikini wenzangu, walalahoi wenzangu na wanyonge wenzangu, Mbowe sio mtetezi wetu, mbowe ni mfanyabiashara ambaye mtaji wake ni umasikini wetu, anatutumia sisi masikini na walalahoi kama mtaji wake wa kisiasa, anatutumia bila ya sisi kujijua, mbowe ni Tapeli wa kisiasa.

HISTORIA INAMPINGA

Mimi ni mkuumini wa Historia ya ukombozi, ninafahamu dunia nzima namna nchi zilizohitaji ukombozi namna zilivyopata ukombozi na namna ya viongozi wao waliowakomboa walivyojitokeza kwenye jamii.

Mbowe ndio mfanyabiashara pekee anayejiita mtetezi wa masikini duniani, tangu nimewahi kuifahamu historia ya ukombozi,

Hakujawahi kutokea Duniani labda ahera, Masikini wakatetewa na Tajiri, Haijawahi na Jaitawahi kutokea Mfanya biashara yoyote akapanga kupata hasarfa eti kwa maslahi ya Umma, wafanya biashara wote wanawaza faida, hata mbowe anawaza faida na sasa anatafuta faida kwa gharama yoyote.

Tunamsifia Mandela leo, Mandela hakuwa mfanyabiashara, Mandela hakuwa tajiri, Mandela alichangiwa na masikini wenzake kuikomboa Arika ya Kusini, Mandela hakuwahi Kuikopesha ANC pesa ili iwaondoe Makaburuu, Mandela alifanana na jamii aliyotaka kuikomboa na Mandela alifanikiwa kuikomboa.

Wote tunamsifia Nyerere Hapa Tanzania, Nyerere Hakuwa Mfanyabiashara, mwalimu Hakuwa Tajiri, mwalimu Hakuwahi kuikopesha TANU ili kumuondoa MKOLONI, nyerere alichangiwa na masikini wenzake, aliombewa na walalhoi wenzake na alilindwa na mafukara wenzake.

Mkifano ni mingi, hivyo hivyo kwa Samora Machel, Kwame Nkuruma, Milton Obote, Robert Mugabe, Kamuzu Banda, Dkt Martin Lutherking, Mahatma Gandh, Mao Zedong, AmilicaCabra na wengineo wote, KAMWE KUNGURU WASIOFANANA HAWAWEZI KURUKA PAMOJA.
Nitaendelea kuwafundisha mengi ninayoyajua kuhusu MBOWE NA CHADEMA kwa kadri itakavyowezekana.

Itoshe tu kusema kwa sasa kwamba Taifa letu kweli linahitaji mabadiliko makubwa ya kiutawala, linahitaji mabadiliko makubwa sana ya kisera kimfumo na kimuundo, na ni kweli kabisa CCM imeshindwa kuendana na Kasi hii ya uhitaji wa mabadiliko, lakini Bahati mbaya sana watu sahihi wa kufanya Mabadiliko bado hawaonekani, bado Hawapo, Bado wanafanyabiashara ya kisiasa.

TAHADHARI.
Nimekuwa nikipokea meseji za vitisho kupitia simu, email na facebook, kuwa nitauawa kama wangwe, ninasema hivi, nipo tayari kwa yote na mwenye uhakika wa kufanya hivyo asipate shida, anipigie simu kwa namba yangu 0762178678 NITAMFUATA ALIPO ATIMIZE LENGO LAKE.


Kwangu Daima NYEUPE NI NYEUPE na NJANO NI NJANO.
Mimi
Habibu Mchange
0762178678
mchangehabibu@yahoo.com

TAZAMA PICHA JINSI ILIVYOKUWA NDANI YA PANTONI BAADA YA KIVUKO KUPOTEZA MWELEKEO MCHANA WA LEO

$
0
0


Ilikuwa ni mida ya saa nane mchana ambapo Pantoni kubwa ya Mv. Magogoni ikiwa imesheheni abiria ikiwavusha kutokea Posta kuelekea Kigamboni , ilipatwa na wakati mgumu baada ya kushindwa kutia nanga ili iweze kusimama na abiria waweze kushuka..
Tukio hilo ambalo chanzo chake kimetokana na Injini za Pantoni hilo kushindwa kufanya kazi  haikuweza kutia nanga kwa muda wote huo.. na ambapo kulikuwa na upepo mkali sana ambao ulisababisha  Pantoni hiyo kukosa muelekeo na kuanza kuambaa ambaa mpaka maeneo ya Chuo Kikuu cha Mwalimu Nyerere kisha kusukumwa zaidi hadi eneo la bandari ya Zanzibar.
Hata hivyo baada ya hali kuzidikuwa si nzuri walilazimika kuita meli ndogo za uokoaji ambapo meli ya kwanza haikuweza kuvuta pantoni hiyo na kulazimika kuongeza meli nyingine ili iweze kuongeza nguvu pamoja na boti za Jeshi la polisi ambazo zote zilifika na kwa ushirikiano mkubwa ziliweza kufanikiwa zoezi hilo la kuirudisha pantoni hiyo katika eneo lake husika. 
Na abiria ambao walinusurika kuweza kushuka na kuendelea na shughuli zao za kawaida..

KENYA YAFIKIA PABAYA MACHANGU DOA WAANDAMANA KUDAI HAKI ZAO

$
0
0
Makahaba mjini Nairobi Kenya waliungana na wenzao duniani kuadhimisha siku ya kimataifa ya kupinga unyanyasaji dhidi yao.
Waliandamana Jumanne kulalamikia kile wanachosema ni unyanyasaji wanaofanyiwa na polisi pamoja na askari wa baraza la jiji wakati wakiendesha biashara zao.

Walikusanyika katikati ya mji na kuelekea katika ofisi za baraza la jiji kuwasilisha malalamiko yao wakisema kuwa wamechoka kuhangaishwa na polisi na wanataka ulinzi.
Mwanaharakati wa maswala ya biashara ya ngono, John Mathenge aliyekuwa miongoni mwa waandamanaji, alisema kuwa wengi wao wameuawa na kunyanyaswa hata na wateja wao pamoja na maafisa wa usalama.

Siku hii ya kimataifa, huadhimishwa kila mwaka tarehe 17.
Biashara ya ngono imeharamishwa nchini Kenya lakini baadhi ya watetezi wa makahaba wanasema kuwa katiba haijaeleza bayana ikiwa mtu atakayekamatwa akijihusisha na biashara hiyo achukuliwe hatua gani za kisheria.
Mathenge alielezea kuwa lazima watu wakome kuwabagua wanaofanya biashara ya ngono, kwani ni kazi kama kazi nyingine tu.
Wengi walilalamika kuwa jamii imepuuza watu wanaofanya biashara ya ngono wala haiwatetei wakati wanaponyanyaswa au kuuawa .
Ripoyi iliyotolewa mwaka jana kuhusu makahaba mjini Nairobi ilisema kuwa wanahangaiswa sana na askari wa baraza la jiji na kuwa wengi wao huachiliwa tu pindi wanapotoa rushwa.

HIVI NDIVYO JINSI NDEGE YA ETHIOPIA AIRLINE ILIVYOCHIMBA UWANJA WA NDEGE ARUSHA BAADA YA KUTUA GHAFLA

$
0
0
Watu 200 waliokuwa wakisafiri kwa ndege ya Ethiopian Airline wanusurika kufa baada ya ndege kupitiliza hadi nje ya uwanja mdogo wa ndege wa Arusha baada ya kutua kwa dharura.

Ndege aina ya Boeing 767 inayosadikiwa kuwa ni ya Shirika la Ndege la Ethiopia imetua kwa dharura majira ya saa tisa alasiri katika kiwanja cha kurushia ndege ndogo cha Arusha badala ya kiwanja cha ndege cha Kimataifa cha Kilimanjaro,

NILIKOSA ULAJI WA KUFANYA FILAMU YA ULAYA KWASABABU YA CHARGER YA SIMU-BIGGIE

$
0
0
Mwigizaji mwenye muonekano wa kipekee katika tasnia ya filamu Bongo Lumole Matovolwa ‘Biggie’ anasema kuwa alikosa kwenda kuigiza filamu Ulaya kwa sababu ya kwenda kurekodi filamu mbali na ukosefu wa ratiba nzuri katika filamu za Tanzania umfanya kuchelewa alipofanya usaili kwa ajili kwenda kushiriki katika filamu ya Afrika iliyotakiwa kuanza kurekodiwa nchini Ujerumani alisafiri nje ya mjini na kutopatikana katika simu.

“Iliniuma sana baada ya kurudi na kukuta ujumbe ambao nilikuwa nimepewa maelekezo kwa ajili ya kumuona mhusika kusafiri na kuungana na wasanii wa nchi mbalimbali kwa ajili ya utengenezaji wa filamu na mimi muonekano wangu wa kipekee uliwavutia sana wazungu,”anasema.

Biggie anasema pamoja na kukosa nafasi hiyo kwa kuchelewa kuwasiliana na wahusika alijisikia vibaya lakini kwa sababu lengo lake ni kuwa msanii wa kipekee katika tasnia ya filamu kwa ukanda wa Afrika Mashariki na kati amekuwa makini sana anapopata nafasi kwa ajili ya kuigiza, ndio akiwa kama mhusika mkuu katika filamu ya Mdundiko ameweza kufanya makubwa na filamu hiyo kuibuka na ushindi nje ya nchi.

Filamu ya Mdundiko ilishinda tuzo ya hadithi bora ya asili katika tamasha kubwa la Silicon Valley African Film Festival (SVAFF 2013) sinema ya Mdundiko ilinyakua tuzo ya (Achievement Narrative in Feature Film) iliyotolewa katika jumba la sinema la San Antonio Circle Mountain View, katika Chuo cha Muziki na Sanaa California, Marekani.

FASTJET RESISTS PRECISION'S $32M BAILOUT

$
0
0
Dar es Salaam.The battle to control Tanzania’s skies has taken a new twist after Fastjet, a low-cost airline which entered the market with a bang, strongly opposed Precision Air’s(PW) decision to seek a bailout amounting to $32 million (Sh51.2 billion) from the government.

Fastjet has termed the move as unfair, saying if the bailout is granted, it would adversely affect competition in the aviation industry in Tanzania.

But it is not clear why Fastjet sees the move as unfair while when the low-cost airline announced its lowest fare of $20 per one-way ticket, neither Precision Air nor Air Tanzania complained about the move.

In what points to a looming business war between the two airlines, Fastjet chief commercial officer Richard Bodin says that bailing out PW using taxpayers’ money would create an unfair playing field among operators who are competing in the market. He says if Precision Air is bailed out, similar assistance should be extended to both Air Tanzania and Fastjet if the government wants to a create competitive and fair aviation industry.


WABUNGE WAUMBUANA HADHARANI BUNGENI

$
0
0
Dodoma. Wabunge jana waliumbuana kuhusu matumizi mabaya ya fedha za umma huku Kiongozi wa Kambi ya Upinzani, Freeman Mbowe akituhumiwa kuagiza kubadilishwa kwa tiketi ya ndege ya Mbunge wa Viti Maalumu (Chadema), Joyce Mukya ili afupishe ziara yake ya kikazi huko Marekani na kwenda Uarabuni kwa shughuli binafsi.

Mbali ya Mbowe, Mbunge wa Mbozi Mashariki, Godfrey Zambi (CCM) anadaiwa kuchukua posho ya Kamati ya Hesabu za Bunge (PAC), kwa safari ya kwenda Dubai na wenzake lakini badala yake akaenda Mbeya kwenye ziara za chama chake.

Malumbano hayo yaliibuka jana baada ya Mbunge wa Iramba Magharibi, Mwigulu Nchemba (CCM), kuomba mwongozo wa Spika akitaka kufahamu kauli ya ofisi yake kwa Mbowe kutumia nafasi yake kumrudisha mbunge ambaye ameshatumia fedha za Serikali.

Alidai kwamba Mbowe aliagiza Mukya aanze safari Desemba Mosi, mwaka huu kutoka New York, Marekani ili aende Dubai, Falme za Kiarabu (UAE) kabla ya kwenda Dar es Salaam, Desemba 3, mwaka huu.

Alipoulizwa kuhusu tuhuma hizo jana, Mbowe alisema hawezi kuzungumza chochote kwa kuwa hakuwapo bungeni akisema alikuwa Dar es Salaam kwenye kikao.... “Siwezi kusema lolote mpaka nipate hansard (kumbukumbu rasmi ya Bunge) na kutoka kwa wabunge wangu walioko Dodoma kujua nini kimesemwa.”

Akiomba mwongozo Nchemba ambaye pia ni Naibu Katibu Mkuu wa CCM alisema: “Jambo hili limechukua taswira kama ni Bunge lote linafanya mambo haya na limevunja heshima ya Bunge. Jambo hili linatuvunjia heshima hata watu ambao tuna maadili ya uongozi na tunaliheshimu taifa letu...

“Pamoja na kuwa jambo hilo lilikuwa la binafsi, lakini kuna ujumbe tumeupata kuwa Kiongozi wa Kambi ya Upinzani amemzuia mbunge wake kusafiri na magazeti yakaandika kwamba wana mahusiano. Mimi sipendi kwenda kwenye uhusiano, nataka kwenye taswira ya Bunge na Taifa.”

Alisema Bunge linapopanga safari za wabunge linazingatia wa chama tawala na wapinzani ili kuweka uwakilishi.

Nchemba alisema Mbowe ambaye pia ni Mwenyekiti wa Chadema, aliandika ujumbe mfupi wa simu kwa mtumishi mmoja wa Bunge akitaka kubadilishwa kwa tiketi ya ndege ya mbunge.

Aliusoma ujumbe huo: “Rejea mazungumzo yetu bwana Kabunju kuhusu mheshimiwa Joyce Mukya ambaye yupo safarini. Nitashukuru kama utambadilishia booking (safari) yake ili aweze kurudi, aondoke New York tarehe moja Desemba na kurejea Dubai baadaye ataunganisha kurejea Dar es Salaam by Mbowe kiongozi wa kambi ya upinzani bungeni nakala kwa Joyce Mukya.” Kabunju S. Kabunju ni Ofisa wa Bunge anayeshughulikia masuala ya usafiri.

Nchemba alisema: “Ameshakatiwa tiketi, ameziba nafasi ya kwenda kuliwakilisha taifa kule, anamwita arudi Dubai na ni mbunge viti maalumu. Je, hili lina taswira gani kwa taifa na kiti chako kinatoa kauli gani kwa watu ambao wanakwenda kutumia fedha za Serikali kwa mambo binafsi, Dubai?” alisema.

Pia alitaka kufahamu Bunge linachukua hatua gani stahiki kwa mbunge anapoingilia kazi za kiti na pia watumishi wanapoingiliwa na kubadilisha yale waliyotumwa kwa ajili ya Serikali.

Tuhuma za Zambi

Mbunge wa Mbozi Magharibi (Chadema), David Silinde alisema Nchemba anaegemea zaidi wabunge wa upinzani wakati wapo wa CCM waliochukua posho.

“Mheshimiwa Mwenyekiti, yaliyosemwa na magazeti na mwombaji wa mwisho (Nchemba), alipokuwa anatoa mwongozo amejaribu kuainisha wabunge wa upande mmoja wa upinzani,” alisema.

Alimtaja Zambi kuwa alichukua fedha ili kwenda Dubai na wenzake lakini badala yake alikwenda Mbeya wakati Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana alipokuwa katika ziara mkoani humo. Zambi pia ni Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Mbeya.

“Tunaomba mwongozo wako namna gani hili suala litachukuliwa hatua na wala siyo kufanya propaganda za kisiasa ndani ya Bunge lako,” alisema Silinde.

Mbunge wa Viti Maalumu (Chadema), Mariam Msabaha alisema kuna mambo mengi yanayofanyika ndani ya Bunge hilo lakini hayasemwi.

“Kuna watu wameandikwa ndani ya magazeti wanaiba vidani licha ya kutosemwa lakini imeonekanika huku. Mambo ya mapenzi ni ya mtu na mtu wake, humu kila mtu ana mpenzi wake,” alisema.

Mwenyekiti wa PAC na Mbunge wa Kigoma Kaskazini (Chadema), Zitto Kabwe alisema: “Kamati ya PAC ambayo inahusika na masuala ya fedha za umma tayari imeshamwomba Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), afanye uchunguzi kuhusiana na safari zote ili jambo hili liweze kufika mwisho.”

Alisema taarifa hiyo itapelekwa kwa Spika na kama atapendezwa italetwa bungeni ili jambo hilo liweze kumalizika.

Akijibu mwongozo huo, Mwenyekiti wa Bunge aliyekuwa akiongoza shughuli za jana asubuhi, Mussa Azzan Zungu alisema: “Nimepokea miongozo yote na kiti kinasema hakina lazima ya kujibu sasa hivi, kitatoa mwongozo baada ya kufikiria na kuyatafakari hapo kitakapopata nafasi.”

Hata hivyo, kabla ya kuahirisha Bunge jana mchana, Zungu alisema suala hilo ni la kiutawala na masuala yote yanayohusu masuala ya fedha yanatawaliwa na sheria na kanuni za fedha.

Sakata hilo liliibuliwa bungeni wiki iliyopita na Mbunge wa Nkasi Kaskazini (CCM), Ally Keissy alipokuwa akichangia taarifa ya Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa (Laac).
-Mwananchi

RAGE AJIVUA LAWAMA SIMBA KUHUSU SUALA LA MCHEZAJI OKWI KWENDA YANGA

$
0
0
Dar es Salaam. Mwenyekiti wa klabu ya Simba, Ismail Aden Rage ameibuka na kusema kuwa lawama za kutokumsajili mshambuliaji wao wa zamani kutoka Uganda, Emmanuel Okwi zielekezwe kwa Kamati ya Usajili na Ufundi wa timu hiyo na wala siyo yeye.

Rage ambaye alikuwa nchini Marekani kwa mwezi mmoja akimuuguza mwanaye, alisisitiza kuwa Okwi alikwishauzwa kwa timu ya Etoile Du Sahel ya Tunisia na wala hakuwa wa Simba tena pamoja na wao kuendelea kudai fedha zao.

Alisema kuwa wakati anakwenda kumuuguza mwanaye, alikuwa amefanikiwa kusajili wachezaji wawili, Awadh Juma na Badru Ali tu, lakini huku nyuma bila ya kupata baraka zake, Kamati ya Usajili ilifanikiwa kumpa mkataba kocha mpya, Zdravko Logarusic kutoka Croatia na kusajili wachezaji watatu, makipa, Yaw Berko, na Ivo Mapunda na mlinzi Mkenya, Donald Musoti.

“Ikumbukwe kuwa Okwi alikuwa anakuja mara kwa mara hapa nchini, lakini kamati hizo hazikuona umuhimu wake, hawakufanya naye mazungumzo kujua nini kinachoendelea kuhusiana na timu yake ya Tunisia na sababu kubwa ya kufanya hivyo ni kutaka kunichafua mimi na kuonekana mbaya na adui kwa klabu ya Simba,” alisema Rage.

Alisema kuwa kilichokuwa kinazungumzwa muda wote ni kunitaka mimi kujiuzulu na kuwaachia madaraka, jambo ambalo haliwezekani kwani lazima wajue kuwa mimi ndiye mkombozi wa Simba.

“Nimefanya mabadiliko makubwa, kuanzia kuongeza kodi ya mapango yetu na klabu kuingiza fedha, kutoka kodi ya Sh200,000 mpaka sasa ya mamilioni, sasa watu wanataka kuona fedha hizo zinapotea na kuwatumia watu ili niondoke, nasema hili halitawezekana na kwa taarifa tu, wale wenye mipango ya kunivamia nyumbani, nimekwisha toa taarifa polisi na hatua kali watachukuliwa wakithubutu kufanya hivyo,” alisema.

Alisema kuwa njama nyingi zimefanyika katika suala la Okwi mpaka kujiunga na Yanga, lakini kwa sasa yeye anasimamia zaidi suala la malipo ya timu ya Etoile na mchakato huo unakwenda vizuri.

 “Hivi leo Mbwana Samatta akijiunga na Yanga au Azam FC, watanilaumu mimi, Okwi hakuwa mchezaji wetu, wana-Simba wajue hilo, kuzungumzia suala la Okwi na kunishutumu mimi ni kunionea tu, walipaswa kujua suala la fedha, nalo nimelizungumza sana na kutoa ufafanuzi, lakini kwa vile lengo lao mimi niondoke, wanaongea maneno mengi ya uzushi juu yangu… mimi ni kiongozi mwenye sifa na kujua mambo ya uongozi, siwezi kukurupuka kujibu suala lolote,” alisema.

Alisema kuwa suala la malipo ya Okwi siyo siri, kwani Kamati ya Utendaji inaelewa kuwa tumefungua kesi Fifa na kulipa Dola 10,000 ili malalamiko yetu yapangiwe jaji na kusikilizwa.

“Kuna barua ililetwa na Fifa kwa njia ya DHL, ilifika klabuni muda mrefu, barua hiyo ilikuwa na majibu ya Fifa na njia gani tufuate ili tuweze kupata haki yetu ya Dola 300,000 za Marekani, makusudi haikutiliwa mkazo, leo (jana) nimefanikiwa kulipa Dola 10,000 kutoka mfukoni mwangu na tunasubiri kusikilizwa kwa madai yetu,” alisema.

NANI KASEMA BONGO FLAVA HAILIPI-BARNABA AVUTA MKOKO MPYAAA

$
0
0
Bado huamini kwamba muziki wa bongo sasa unalipa? Kama umejibu ndiyo nakushauri u-update fikra zako sababu wasanii wa miaka ya sasa wamekuwa wakionesha mafanikio ya aina mbalimbali yanayotokana na kazi ya muziki wanayoifanya.

Barnaba wa THT leo amemwonesha ‘baby wake’ mpya kupitia Instagram, tena akiwa bado hata hajapewa ‘birth certificate’. 

LULU: KAMA SI KANUMBA YANGENIKUTA MAZITO

$
0
0

SURA ya mauzo katika sinema za Kibongo, Elizabeth Michael Kimemeta ‘Lulu’ ametoa ya moyoni kuwa kama siyo kuwekwa nyuma ya nondo za Mahabusu ya Segerea, Dar basi yangemkuta mazito.

Lulu alikaa Gereza la Segerea kwa takribani miezi kumi baada ya kutokea kifo cha aliyekuwa mwandani wake, marehemu Steven Kanumba ‘The Great’ aliyefariki dunia Aprili 7, 2012.
Nyota huyo wa Filamu ya Foolish Age alifunguka mambo ya kushangaza hivi karibuni juu ya tukio hilo kupitia Kipindi cha Take-One, kinachorushwa  na Clouds TV.

TATIZO FOOLISH AGE
Lulu alikuwa akizungumzia filamu yake hiyo ya Foolish Age ambapo alisema sinema hiyo inawasihi wasichana ambao wanapitia kipindi cha balehe ambacho ni hatari sana kwao.
“Kwa kweli kipindi cha foolish age ni cha hatari sana, nilicheza filamu hiyo ili kuwaasa wasichana wenzangu.
“Asikwambie mtu, mimi mwenyewe nilikokuwa nikielekea si kuzuri kabisa.

KAMA SIYO KANUMBA
“Ukweli ni kwamba kama siyo matatizo (kifo cha Kanumba) nikaenda mahabusu sijui ingekuwaje sasa hivi. Kukaa jela kulinisaidia kusitisha kasi ya tabia yangu, nikatoka nikiwa mpya.
“Yangenikuta mazito zaidi maana kipindi kile ilikuwa hatari tupu,” alisema Lulu ambaye ni mrembo wa haja.

Staa huyo aliongeza kuwa kipindi hicho kilikuwa cha hatari na hakitamani kijirudie hata kidogo katika maisha yake.
Alisema kwamba si ajabu inawezekana kipindi hicho ndicho kilisababisha matatizo yote yaliyomkuta. Alisema alikuwa akielekea kubaya.

HATAKI KIJIRUDIE
“Ni kipindi ambacho siwezi kukuhitaji tena katika maisha yangu si kizuri na kinatisha maana kuna wakati nilikuwa sisikii la mtu yeyote hata mama yangu mzazi,” alisema Lulu ambaye baada ya kutoka mahabusu haonekani akirandaranda mjini kama zamani.
Kabla ya utulivu huo alioupata nyuma ya nondo, Lulu alikuwa hakauki kwenye kumbi za usiku za starehe huku akilewa tilalila na kuyaweka maisha yake hatarini endapo angefanyiwa kitu mbaya.

Lulu alihusishwa na kifo cha Kanumba kwa kuwa siku ya tukio alidaiwa kuwa naye eneo la tukio ambapo alikamatwa na baadaye kuachiwa kwa dhamana akisubiri kesi ya kuua bila kukusudia.


SKENDO MPYA
Wakati hayo hayajapoa kumeibuka skendo mpya inayomgusa staa huyo mkubwa Bongo.
Madai mazito yameshushwa na wafuatiliaji wa mambo ya watu kuwa nyuma ya mwanadada huyo anayeng’ara kuna mbunge maarufu anayemiliki jimbo kwa kura za wananchi jijini Dar (tutamtaja baadaye).

ILIKUWA HIVI
Sosi: Hivi ninyi Global siku hizi hamuandiki skendo za mastaa?
Global: Tunaandika sana kwani vipi?
Sosi: Mna habari?
Global: Tunazo nyingi fuatilia magazeti yetu lakini ukitupatia ya kwako tutairusha hewani.
Sosi: Sasa mimi nina habari yangu.

Global: Inakuhusu wewe? Funguka. 
Sosi: Hainihusu mimi. Ni ya ‘Kalulu Kadogo’.
Global: Siku hizi amekua, sema Lulu inatosha. Eeh... hiyo habari ikoje?
Sosi: Kwa taarifa yenu siku hizi anatoka na mbunge (anamtaja). Ndiye kamnunulia lile gari analokatiza nalo mjini na kampangishia bonge la mjengo kule Tegeta (Dar). Fuatilieni kwa watu wake wa karibu, naombeni msinitaje.
Global: Hatuwezi kukutaja ngoja tuzame mzigoni.

Gazeti hili lilifanya uchunguzi wake kwa watu wa karibu wa Lulu na kubaini kuwa ni kweli kwa sasa staa huyo amehama Tabata alikokuwa akiishi na mama yake, Lucresia Karugila na kuhamia kwenye bonge la mjengo Tegeta huku akisukuma gari kali (aina haikujulikana mara moja).
Madai mengine yalisema kwamba  mke wa mbunge huyo alishamtafuta Lulu na kumuonya kuachana na mume wake


LULU AFYATUKA  
Baada ya kujiridhisha kuwepo madai hayo, juzi gazeti hili lilimtafuta Lulu na kumsomea mashitaka yake mwanzo hadi mwisho ambapo alifyatuka:
“Hivi ni nani anayeleta habari zangu Global? Analipwa na nani? Maana kila kukicha unasikia hili, halijapoa unasikia lingine.

“Si kweli kwamba natembea na huyo mbunge. Kwanza sina mazoea naye. Nakumbuka nilimuona mara moja tu sikumbuki ilikuwa kwenye shughuli gani.
“Huyo mkewe mimi simjui anafananaje. Nasema huko ni kuchafuana kusikokuwa na maana.”

VIPI KUHUSU KUPANGISHIWA NYUMBA?
“Ni kweli nimehamia Tegeta lakini sijapangishiwa, nimepanga mwenyewe. Hivi nikifanya jambo lazima iwe kuna mwanaume? Watu waache hizo. Wabadilike.”

VIPI KUHUSU GARI?
“Gari ninalo muda mrefu nimenunua kwa fedha yangu. Halina mkono wa mbunge, ni jasho langu.”
Kabla ya kuwekwa mahabusu, Lulu aliwahi kudaiwa kuhongwa nyumba na mbunge mwenye kitambi kikubwa, ishu hiyo aliikanusha kwa nguvu zote.

Imeandikwa na Imelda Mtema na Musa Mateja.
Gpl

RAY C AANIKA VIGEZO VYA MUMEWE MTARAJIWA

$
0
0
Na Gladness Mallya
STAA wa muziki wa Bongo Fleva, Rehema Chalamila ‘Ray C’ ameibuka na kusema kuwa anahitaji mume anayemzidi umri kwa miaka kumi.

Akizungumza hivi karibuni kwenye kituo kimoja maarufu cha runinga, Ray C alisema anahitaji mwanaume mtu mzima anayemzidi miaka kumi, anayejitambua na asiwe mwanamuziki kwani anaamini akiwa na mtu kama huyo uhusiano wao utakuwa mzuri kuliko ule wa awali uliokuwa wa machungu.

“Ninamtaka mwanaume anayenizidi miaka kumi kwani kwa sasa nina miaka 31 japokuwa kwa sasa nafanya kazi kwanza ili nirudi kwenye levo yangu na nitakuwa juu zaidi ya zamani kwa sababu najitambua japokuwa nina hamu sana ya mtoto lakini yote namwachia Mungu.

“Nashukuru sasa hivi niko vizuri nakumbuka  meneja wangu wa kwanza alinikataza nisiwe na uhusiano na mwanamuziki lakini ndiyo hivyo nikajikuta niko na Lord Eyes ambaye alianza kunichanganyia cha Arusha (bangi) bila mimi kujua na kujikuta ninaharibikiwa lakini nimeshamsamehe na ninamuombea heri katika maisha yake,” alisema Ray C.

Aidha, Ray C alisema anamshukuru Mungu kwa sababu hana mume wala mtoto kwa sababu kwa jinsi alivyokuwa mwanzo angejenga picha mbaya sana kwa mwanaye.

“Wakati nilipokuwa na matatizo nilijifunza mengi kwamba hakuna rafiki wa kweli kwa sababu walinipenda nikiwa mzima lakini nilipokuwa naumwa hakuna hata mmoja aliyenipigia simu kunijulia hali zaidi ya mashabiki zangu tu kwa hiyo nimebadilisha mfumo wa maisha yangu,” alisema Ray C.

Miezi kadhaa iliyopita, mwanamuziki huyo alitangaza kuachana na madawa ya kulevya ambayo alikiri kuwa yalimharibia mwenendo mzima wa maisha yake.

JACK WOLPER NA ZAMARADI NDANI YA BIFU ZITO

$
0
0
Na Shakoor Jongo
STAA wa sinema za Bongo, Jacqueline Wolper amemrushia maneno ya lawama Mtangazaji wa Kipindi cha Take One, Zamaradi Mketema kuwa ni mnafki na adui yake mkubwa katika maisha.

Akizungumza na Amani juzikati, Wolper alisema amegundua kuwa mtangazaji huyo amekuwa akimfuatilia kwa karibu sana maisha yake kwa mtindo wa chanya (negative), akamuomba amuache.

“Nilibadili dini kutoka Ukristo kwenda Uislamu, Zamaradi akanifuatilia, juzijuzi nimerudi kundini (kwenye Ukristo) kwa kusikiliza maneno ya wazazi wangu, akanifuatilia tena.

“Huko nyuma kupitia kipindi chake alikubali nidhalilishwe na waigizaji wenzangu kwa faida yake (hakutaka kufafanua), iliniuma sana. Leo (hivi karibuni)  kaniweka hewani (kwenye redio) bila ya ridhaa yangu. Naomba niseme kuwa naanza kugundua azma yake kwangu ni nini, aniache na maisha yangu,” alilalama Wolper.

Baada ya Wolper kulalamika sana, Amani lilimtafuta Zamaradi kwa njia ya simu ya kiganjani ambapo alisema yeye anawajibika kwa kazi yake hakuna ishu ya kumfuatilia mtu.

“Mimi simfuatilii maisha yake, ni kazi tu. Kama mwandishi wa habari nikipata habari ya mtu natakiwa kubalansi (uwiano) naye,” alisema Zamaradi.
GPL

BABY MADAHA: DIAMOND HANIWEZI, AWATISHIE WATOTO TANDALE

$
0
0
MWIGIZAJI na mwanamuziki Bongo, Baby Joseph Madaha amemchana Nasibu Abdul ‘Diamond’ kwa kumwambia awatishie watoto wa Tandale kwani hana ubavu wa kuchuana naye.

Akizungumza na paparazi wetu, Baby alifunguka kuwa anamshangaa Diamond kujibu kuhusu jinsi alivyomchana wiki kadhaa zilizopita gazetini na kusema yeye hamuwezi kwani alimtangulia kuchomoka kistaa.

“….akiwa bado ana-struggle kupata mkwanja awatishie watoto wenzake wa Tandale, mimi nishazindua brand yangu ya manukato na mikoba ya zawadi, bidhaa ambazo zinaingia sokoni rasmi Desemba 31, awatishe haohao watoto wenzake, mimi siyo saizi yake,” alisema Baby. 

Diamond alipotafutwa, simu yake iliita bila kupokelewa.

DR SLAA TUKISHIKA DOLA TUTARUHUSU UTENGENEZAJI WA POMBE YA GONGO KISHERIA

$
0
0
Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kimetoa mpya baada ya kueleza kuwa kitakapofanikiwa kushika dola kitaruhu Shirika la Viwanda Vidogo Vidogo (SIDO) kutengeneza mitambo ya kutengenezea pombe aina ya gongo. Katibu Mkuu wa Chadema, Dk.Willbroad Slaa, akizungumza na wananchi wa Jimbo la Kasulu Vijijini alisema kama gongo itatengenezwa kwa mitambo maalum itaondoa mianya ya rushwa kwa polisi ambao wamekuwa wakiwakamata wanaotengeneza kwa kificho na kuwafanya vitega uchumi vyao.

"Gongo sasa hivi ni haramu sababu inatengenezwa kwa kificho katika mazingira machafu, tukishika dola tutataka SIDO itengeneze mitambo ya kutengeneza gongo ili iwe katika hali ya usafi," alisema.

Mitambo hiyo itakayotengenezwa na SIDO itakapouzwa itaiingizia mapato serikali pia wauzaji wa gongo watafanya biashara hiyo kwa amani tofauti na sasa ambapo wanaifanya kwa kificho na wakikamatwa fedha zote wananufaika polisi.

Dk. Slaa alisema hata suala la kukamata watu wanaotengeneza silaha linapaswa kuangaliwa upya kwani wanaokamatwa wakifanya kazi hiyo wangekuwa wanashikiliwa kwa muda na baadaye wanapelekwa katika kiwanda cha serikali cha kutengenezea silaha ili watuhumiwa hao wapeleke ujuzi huo huko badala ya kuwafunga jela.

Dk. Slaa alisema matatizo yote yanatokana na wasomi kutofikiri namna ya kuisogea nchi mbele kimaendeleo.

"Nchi hii imelala, imechoka sababu waliopewa madaraka wamelala, wamejisahau hawatambui kuwa wamepewa nafasi hizo ili kuwatumikia wananchi," alisema.

KWA WANAUME TU-UNAPENDA MWANAMKE GANI KATI YA HAWA HAPA CHINI?

$
0
0
Embu niambieni bandugu mnapendelea mwanamke wa aina gani kati ya hawa unapotongoza?

1) Yule ambaye anakukatalia na kujibu kashfa na matusi huku akifoka unapomtongoza?
2) Msumbufu na umempata baada ya kumfuatilia kwa muda mrefu bila kukata tamaa?
3) Kigeugeu mara ndio au nimebadili mawazo au mpaka uje kwa wazazi?
4) Anakubali lakini No sex mpaka tuoane?
5) Maharage ya Mbeya Ukigusa tu yupo tayari kwa lolote iwe kufanywa kimada wa pembeni, kuchezewa au kuolewa.

Mimi binafsi napendelea sana No 2. Unajua mwanamke akinipa tabu sana siku ya kuja kumpata ntamthamini zaidi na ndio atakuwa mwepesi kwa mimi kutangaza ndoa kwake. 
Wa aina hii ananipa matumaini ndani ya moyo kwamba anayejaribu kumchukua kwangu naye itabidi apitie tabu niliyopitia mimi.
By Maskni Wa Akili

SAMWELI ETOO AAMBULIA MATUSI YA NGUONI KUTOKA KWA MASHABIKI WA CHELSEA BAADA YA KUPOST TWEET HII

$
0
0


Mashabiki wa Chelsea wanamrushia matusi pamoja na maneno ya kebehi striker Samuel Eto’0 baada ya kupost picha ambayo sio kawaida kwa mchezaji ku-tweet pale timu yake inapokua imepata matokeo mabaya uwanjani.
Picha yenyewe ni hii hapa chini inaonyesha matokeo ya Chelsea dhidi ya Sunderland then Samuel Eto’o aka-tweet kwa followers wake zaidi ya laki moja na nusu kitu ambacho baadhi yao wamekichukulia vibaya kwamba kwa nini timu ifungwe alafu apost?
etoo
Hizi ni baadhi ya tweets kutoka kwa mashabiki ambapo tweet nyingine zina maneno mazito kutoka kwa mashabiki hawa ambao wamemjibu Samuel.e1
e2
e3
e4

HIZI NDIO HABARI NJEMA KUHUSU TOZO YA KODI KWA LINE ZA SIMU KUTOKA KWA JANUARY MAKAMBA

$
0
0
Habari za kodi kwa laini za simu ilichukua vichwa vya habari kwa wakati wake hadi pale mheshimiwa Rais alivyotoa agizo kwa wahusika kulishughulikia hili suala.
Naibu Waziri mwenye dhamana ya mawasiliano,sayansi na teknolojia “January Makamba” ametoa habari mpya na nzuri  kuhusu kodi hii.
Kupita ukurasa wake wa facebook alipost “Mheshimiwa Rais ametia sahihi Hati ya Dharura (Certificate of Emergency) kufanyika marekebisho kwa Muswada wa Fedha wa mwaka 2013 kuondoa tozo ya kodi kwa laini za simu (SimCard Tax). Asante Mheshimiwa Rais.”.

MWIGAMBA:BAADA YA ZITTO KUONDOLEWA ANAEFUATA NI DR SLAA

$
0
0
Aliyekuwa mwenyekiti wa chadema mkoa wa Arusha Samson Mwigamba amesema kuwa mpango unaofuata kwa sasa ni kumuondoa Dr slaa ndani ya chadema.
amesema baada ya zitto kuondolewa ndani ya chama mtu atayefuata katika kushughulikiwa ni Dr Slaa ambaye kwa sasa amekuwa amekuwa akifanya shughuli za chama kwa kupelekwa pelekwa bila yeye mwenyewe kujua.

Mwigamba amesema kuwa upo mkakati kabambe unaendeshwa na baadhi ya watu kwa kushirikiana na watu walio nje ya chama ili kukimaliza chama kabla ya kufika kwenye uchaguzi mkuu 2015.
Amesema kuwa Mwenyekiti wao Freeman Mbowe ambaye yupo karibu sana na mbunge wa Arusha mjini Godbless Lema ndio vinara wa mkakati wa kukiangamiza chama, huku John mnyika na Tundu Lissu wakijiweka mbele bila kujua hatima yao.
Rai
Viewing all 104747 articles
Browse latest View live




Latest Images