Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104709 articles
Browse latest View live

Habari Njema: Tunatibu Busha, Korodani Kuvimba,Ngiri, Miguu Kufa Ganzi Pamoja na Matatizo ya Nguvu za Kiume

$
0
0
Ni Dawa ya nguvu za kiume inayorefusha na kunenepesha uume saizi uipendayo (Inch 1-7) kwa muda wa siku 6 tu.Dozi hii itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa muda wa dakika 30, utarudia tendo la ndoa zaidi ya mara 4 bila hamu kuisha bila kujali umri na garantee ni miaka 60 baada ya kutibu tatizo.

Pia tunatibu Busha bila kufanyiwa Oparesheni, korodani moja kuvimba, ngiri, tumbo kujaa gesi na kuunguruma, kutopata choo vizuri, miguu kuwaka moto na kufa ganzi, chango la wanawake, kisukari na kutokwa na kinyama sehemu ya haja kubwa.

MIHAYO:
Inarudisha mke, mchumba, hawara na atakutimizia kila kitu unachotaka kutoka kwake ndani ya  saa 2 tu hata kama yupo mbali. atarudi na kumfunga asiwe na mwingine zaidi yako.

Umefukuzwa kazini? unataka kupandishwa cheo? Umepoteza pesa zako kwenye biashara bila kujua umepandikizwa chuma ulete? Njoo urudishe pesa zako. Unauza mali yako haiendi?

Faiza Ally Afunguka 'Alama ya Kwanza ya Mwanamke Mjinga Ndani ya Ndoa'

$
0
0
Alama ya kwanza ya mwanamke. Mjinga Ndani ya Ndoa

1. Kuficha manyanyaso na kuvumilia uovu ikiwemo kupigwa
2. Kuzaraulika
3. Kuhisi kutokua na mume ni aibu
4. Na kulea mwanaume

Ukiona unapata hayo yote kwenye ndoa na bado upo unahitaji kansela ya kujijua . Na mapenzi hayana maumivu ukiona unaumia kila siku ujue hamna kitu hapo mnaishi tu
Na kikubwa cha kuzingatia sisi wanawake tunao uwezo wa kuishi na mwanaume kwa kuwavumilia lkn wanaume kama hakupendi hata ukimvumilia haitasaidia yeye kukupenda kamwe! Utaishi kwa maumivu mpaka mwisho wa maisha yako! Kuvumilia uovu sio mapenzi ni ujinga .....kuishi bila ndoa sio aibu . Mwanaume mmbaya kwenye maisha yako hatabadili toka katafute wengine hata 100 wa 101 atakua mwema ....JAMBO BEAUTIFUL WOMAN

Katika Safari Yangu, Nilichokiona Maeneo ya Pwani Kinasikitisha..Ni Umaskini na Uvivu wa Kutisha

$
0
0
Wadau,

Katika mizunguko yangu ya kikazi kuna kitu nilikuwa nakiangalia hasa katika maeneo mbalimbali ya nchi yetu.

Huu ni msimu wa kilimo, wakati nikiwa kwenye gari kuanzia kanda ya ziwa hadi Morogoro nimeona kuna pilikapilika nyingi za kilimo. Yaani kuanzia kanda ya Ziwa inaonekana green ya mahindi na mazao mengine.

Lakini maajabu ni kwamba wakati nikitokea Dar es salaam kuelekea Arusha, kuanzia Mlandizi karibu mto Ruvu hadi Segera, kila nikitizama kwenye vijiji vya pembeni nimekuwa nikiona green ya mapori tu.

Ukweli nimejiuliza sana, kwanini naona green ya mapori badala ya Mazao wakati huu ni msimu wa kilimo, au eneo hili ni hifadhi ya taifa? Nikajiuliza, hawa watu hawalimi, lakini pia hawafugi, je wanaishije?.

Lakini maajabu mengine ni kwamba eneo lote hili hasa Chalinze hadi Segera, nyumba asilimia kubwa ni za fito na tope (Mbavu za mbwa tunaita), yaani unakuta nyumba mbavu za mbwa iko katikati ya kijani cha pori lakini hakuna mazao wala maandalizi kwa ajili ya kilimo licha ya kwamba ni msimu wa mvua. Vijiji hivi vina umasikini wa kutupa, utajua kwa kutizama mbavu za mbwa zilizopo.

Ndugu zangu, vijana wenzangu mnaoishi maeneo hayo, mnarudisha taifa nyuma, kwanini hamtaki kutumia ukaribu wenu na Dar es salaam mkauza mazao mkabadilisha hali zenu za maisha? Kwanini wakulima wa Songea wanufaike na uuzaji wa mahindi Dar na nyie msitumie fursa ya ukaribu huo? Kwa tabia hii nina uhakika kila mwaka huwa mnaletewa mahindi ya njaa kutoka serikalini.

Nashauri, itungwe sheria ya kulazimisha watu kufanya kazi. Pia wabunge wa maeneo haya, hasa Ridhiwani na wengine, tafadhali hamasisha watu wako kufanya kazi.

By Nkobe

Jibu la Mr. Blue Kuhusu Beef na Diamond, Mpango wa kolabo

$
0
0
Msanii wa muziki Bongo, Mr. Blue amefunguka kuhusu kuwa na beef na Diamond na mipango ya kolabo.

Rapper huyo ambaye kwa sasa anatamba na ngoma ‘Mbwa Koko’ ameiambia FNL ya EATV kuwa kolabo na Diamond alishafanya mara mbili ila kama kuna uwezekano wanaweza kufanya tena ila kudhihirisha watu kuwa hawana beef kama inavyokuwa ikienezwa.

“Ni mtu nishashirikiana naye sio kitu cha kushangaza labda kusema haiwezekani lakini unajua siku zote mnapokuwa wasanii wakubwa kila mtu anakuwa yupo bize kwa upande wake lakini ikifanyika kolabo ya kati yangu na Diamond ni kitu kizuri kwa sababu tutaonyesha raia hatuna tatizo,” amesema Mr. Blue.

“Na kweli sina tatizo na Diamond, ni mdogo wangu namuheshimu, naheshimu hustle zake na amekuwa kama mfano kwa watu, hayo mambo mengine watu wasiyachukulie sana serious,” amesisitiza.

Diamond ameshawahi kumshirikisha Mr. Blue katika ngoma yake inayokwenda kwa jina la kiss to the Lady, pia wote walishirikishwa na Marehemu Ngwea katika ngoma ‘BBM’.

Kutana na Mtabibu Mwenye KUBRI kutoka kwa ALLAH issa simba said Mtabibu wa Nyota za Binadamu na Dawa za Asili

$
0
0
Kutana na Mtabibu Mwenye KUBRI kutoka kwa ALLAH issa simba said Mtabibu wa Nyota za Binadamu na Dawa za Asili ya Africa Mwenye UWEZO Kubaini tatizo lako Pindi tu Utakapo Fanya Mawasilino Kupitia Wasaa Husika..JE UNASUMBULIWA NA Mapenzi? (Umeachwa na Umpendae,Awe Mume,Mke na Bado unampenda?Na Umejaribu Sehemu nyingi Bila Mafanikio?Wasilina na Maalim Hussein Ujione muujiza wa Papo kwa Papo.. anauwezo WA KURUDISHA MAHUSIANO NA KUIMARISHA NDOA YAKO NDANI YA SAA 12 TU. Umekimbiwa na Mumeo,mkeo au Mpenzi na anaishi na mtu mwingine? Muone akutatulie Anauwezo wa Hali ya Juu wa Kusambalatisha Mahusiano yao Endapo utafata Atakacho kuelekeza.
Atamfanya Atimize Ahadi zote kwa Muda Mfupi.

Issa simba said Anatumia Jina la Muhusika au Picha Kumaliza Tatizo lako..
Anatibu kwa Kutumia Vitabu vya QUR-AN Dawa za Asili za Africa,Dawa za Kiarabu na Majini.Anatafsiri Ndoto. Kushinda BAHATI NASIBU, KUSAFISHA NYOTA. Mvuto wa Mwili na BIASHARA, Kinga ya Mwili,ZINDIKO za Nyumba.MIGUU Kufa GANZI.Kufungua KIZAZI kwa wale walio fungwa kwa njia za KISHIRIKINA. Anakupa Jini la Mali kwa yule anaehitaji Utajiri BILA MASHARTI. Nguvu za KIUME, Humaliza Kesi zilishindika ndani ya siku 14 tu..na mengi zaidi

Wasiliana nasi +255 622588038au 0679119679 au +255 764318107

Mkurugenzi Mtwara Apinga

$
0
0
Mkurugenzi Mtwara Apinga
Mkurugenzi wa manispaa ya Mtwara Mikindani Bi. Beatrice Dominic Kwai, amekanusha taarifa za kuchangia elimu, wafanyakazi wa manispaa hiyo.


Akizungumza na mwandishi wa www.eatv.tv, Mkurugenzi huyo amesema yeye binafsi hajatoa taarifa yoyote kuomba wananchi wala wafanyakazi wa manispaa hiyo kuchangia elimu, kwani kufanya hivyo ni kukiuka agizo la Rais la kutaka elimu itolewe bure.

"Sina taarifa na hilo, ninachojua mifuko ya elimu ipo kisheria na wa kwangu tunajiandaa kuuzindua, kwakuwa sina document yoyote niliyosaini inayohusiana na michango, na mimi ninatambua maagizo ya Mheshimiwa Rais, siwezi kuchagisha michango ambayo ipo kinyume na utaratibu na sijamuagiza mtu yeyote achangishe", amesema Beatrice Kwai.

Hivi karibuni kumekuwa na taarifa kuwa wananchi wa Manispaa hiyo pamoja na wanafunzi wametakiwa kuchangia elimu kiasi cha shilingi elfu 5 kila mmoja, jambo ambalo lipo kinyume na agizo la Mheshimiwa Rais Magufuli.

Serikali Yaisisitiza klabu ya Simba

$
0
0
Serikali Yaisisitiza klabu ya Simba
Serikali imeiagiza Klabu ya Simba kuzingatia sheria na kanuni zinazosimamia suala la uwekezaji kwa Klabu zilizoanzishwa na wanachama ambapo inawataka kuchukua 51% na mwekezaji  49%.


Msisitizo huo umetolewa na Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Dkt. Harrison Mwakyembe alipokutana na uongozi wa Klabu ya Simba na kuzungumza nao kufuatia kutoa asilimia 50% kwa mwekezaji wa klabu hiyo Bw. Mohamed Dewji waliyemtanganza hivi karibuni ambapo ni kinyume na sheria.

“Kanuni zinazosimamia masuala ya udhamini kwa vilabu zilifanyiwa marekebisho Novemba  2017 ambapo ilioneka ni vyema klabu za michezo zilizoanzishwa na wanachama wanapopata mwekezaji basi achukue 49% na wanachama wapewe 51% lengo ikiwa ni mwanachama aweze kunufaika vizuri,”  amesema Dkt. Mwakyembe.

Kwa Upande wa Kaimu Rais wa Klabu ya Simba Bw. Salim Abdallah ameishukuru serikali kwa kuwafungulia milango pale watakapo kuwa na tatizo au watakapo hitaji ushauri na kuahidi kuzingatia maagizo ya Waziri pamoja na matakwa ya sheria hiyo ya uwekezaji kwa vilabu.

Disemba 3, 2017 klabu ya Simba kupitia mkutano wake mkuu uliofanyika jijini Dar es salaam ilimtangaza Mfanyabiashara Mohamed Dewji kama mshindi wa zabuni ya kuwekeza ndani ya klabu hiyo kwa dau la shilingi bilioni 20.

"Hii ni Dunia Nyingine"- Papii Kocha

$
0
0
"Hii ni Dunia Nyingine"- Papii Kocha
Mtoto wa msanii nguli wa muziki wa dance, Papii Kocha amefunguka na kudai maisha ya uraiani ni sawa na dunia nyingine kwani mtu akiwa anatumikia adhabu ya kifungo gerezani, huwa vitu vingi vizuri anashindwa kufanya ama hata kushiriki kabisa.

Papii ameeleza hayo pindi alipokuwa kwenye matayarisho ya ujio wake mpya katika muziki akiwa pamoja na Baba yake Nguza Viking maarufu kama Babu Seya ambapo wawili hao walitoka jela kwa msamaha wa Rais Dkt. John Magufuli katika maadhimisho ya miaka 56 ya Uhuru yaliyofanyikia katika uwanja wa Jamhuri Mkoani Dodoma mwaka huu.

"Miaka 14 siyo mchezo, mambo kama haya si unayaona mwenyewe, niliya-miss, nime-miss vitu vingi, picha za ukweli, mambo haya kule tulipotoka hamna. Lazima uelewe hii ni dunia nyingine", alisema Papii Kocha.

Pamoja na hayo, Papii ametoa ahadi kwa mashabiki na wapenzi wa 'dance' kwa kuwapa kitu kilichokuwa bora zaidi tofauti na zile walizokuwa wamezifanya kipindi cha awali.

"Tumejipanga vizuri na kazi zinazokuja zitakuwa nzuri zaidi ya zile tulizofanya mwanzo,” amesisitiza Papii.

Sugu Afikishwa Mahakamani Leo

$
0
0
Sugu Afikishwa Mahakamani Leo
Mbunge wa Mbeya Mjini (Chadema), Joseph Mbilinyi ‘Sugu’  amefikishwa mahakama ya Hakimu Mkazi Mbeya leo Januari 22, 2018 kusikiliza kesi inayomkabili  ya kutumia lugha ya fedheha dhidi ya Rais John Magufuli.

Sugu pamoja  Katibu wa Chadema Kanda ya Nyanda za Juu Kusini, Emmanuel Masonga walifikishwa mahakamani hapo Januari 19, 2018 lakini  mahakama ilizuia dhamana zao na kuwarejesha rumande hadi leo.

Siku hiyo hakimu mkazi mfawidhi wa mahakama hiyo, Michael Mteite alitoa uamuzi wa kuwarejesha rumande, kwamba kesi hiyo inatakiwa isikilizwe mfululizo kwa muda mfupi na washtakiwa wakiwa wanafika mahakamani hapo wakitokea mahabusu.

“Mahakama hii inataka kusikiliza kesi hii kwa muda mfupi sana, ndani ya wiki moja kuanzia Jumatatu ijayo (leo)  iwe imeamuriwa, hivyo washtakiwa wataendelea kuwekwa mahabusu,” amesema Mteite.



Sugu na Masonga wameshtakiwa kwa kosa la kutumia lugha ya fedheha dhidi ya Rais John Magufuli ambayo waliyatoa katika mkutano wa hadhara walioufanya Desemba30 mwaka jana wakiwa viwanja vya Shule ya Msingi Mwenge jijini Mbeya

Majaliwa Afungua Makucha Yake Butiama

$
0
0
Majaliwa Afungua Makucha Yake Butiama
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa ameiagiza Takukuru imkamate na kumhoji meneja wa mkoa wa Wakala wa Majengo Tanzania (TBA), Peter Salim baada ya kushindwa kutekeleza ujenzi wa mradi wa ofisi za Halmashauri ya Wilaya ya Butiama.

Taarifa iliyotolewa jana na Ofisi ya Waziri Mkuu imesema mtendaji huyo mkuu wa Serikali alisema licha ya Serikali kutoa Sh600 milioni Aprili mwaka jana kwa ajili ya kuanza ujenzi wa ofisi hizo, hadi sasa hakuna kilichofanyika.

Hata hivyo, meneja huyo katika alisema maelezo yake alieleza kuwa hadi kukamilika ujenzi wa ofisi hiyo utagharimu Sh3 bilioni na kwamba kati ya fedha zilizotolewa na Serikali, Sh400 milioni zimetumika kujengea msingi, kauli ambayo ilipingwa na mkuu wa wilaya hiyo, Anna-Rose Nyamubi.

“Waziri Mkuu si kweli kwamba kuna kazi inayoendelea, bali kilichopo pale ni mashimo ambayo hayajulikani ni ya nini. Pia, kuna jengo moja lilijengwa kwa mabati kama stoo hakuna mafundi wanaoendelea na kazi,” alisema Nyamubi.

Majaliwa alisema Serikali ipo katika mchakato wa kuboresha mazingira ya wafanyakazi, ikiwamo ujenzi wa ofisi za watumishi na kwamba haitamvumilia mtu yeyote atayekwamisha juhudi hizo.

Katika hatua nyingine, Waziri Mkuu amemuagiza kaimu katibu tawala wa Mara, Raphael Nyanda kutuma timu ya wakaguzi kufanya ukaguzi maalumu katika ofisi ya mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Butiama.

Alisema halmashauri hiyo imekuwa na tabia ya kutumia fedha za miradi ya maendeleo kwa shughuli nyingine.

Alikuwa akizungumza na watumishi na madiwani wa Butiama katika ukumbi wa Chuo Kikuu cha Kilimo cha Mwalimu Nyerere.

Pia, Waziri Mkuu aliagiza kuchunguzwa kwa Solomon Ngiliule, ambaye ni mkurugenzi wa halmashauri hiyo, Masanja Sabuni (mweka hazina) na Robert Makendo (ofisa ununuzi).

TPSF Nayo Yataka Marekebisho Umakini Muswada wa Ardhi

$
0
0
TPSF Nayo Yataka Marekebisho Umakini Muswada wa Ardhi
Taasisi ya Sekta Binafsi Tanzania (TPSF) imeiomba Serikali kuondoa mabadiliko ya Sheria ya Ardhi yaliyomo katika Muswada wa Marekebisho ya Sheria Mbalimbali ili kuepuka madhara ya kiuchumi yanayoweza kusababishwa na mabadiliko hayo iwapo yatapitishwa.

Katika kuhimiza hilo, TPSF imemuandikia barua Waziri wa Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Lukuvi ikimtaka kuwashirikisha wadau kabla ya muswada huo kujadiliwa na Kamati ya Bunge.

Msimamo wa TPSF unafanana na wa Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS) ambacho kimesema iwapo marekebisho hayo yatapitishwa na sheria kuanza kutumika, yataathiri mfumo wa rehani nchini.

Mjumbe wa Kamati ya Katiba na sheria ya TLS, John Seka alisema kwa muda mrefu wananchi wengi wamekuwa wakitumia mashamba kama rehani kwenye taasisi za fedha.

Alisema wamewasilisha maoni yao Kamati ya Bunge ya Katiba na Sheria inaouchambua muswada huo unaomtaka mmiliki wa shamba ambalo halijaendelezwa au kuendelezwa kidogo, kutumia fedha anayokopa kuliendeleza zaidi.

Jana, mkurugenzi mtendaji wa TPSF, Godfrey Simbeye alisema muswada huo unapaswa kuondolewa kabisa bungeni kwani endapo kosa lolote litafanyika, madhara yake ni makubwa kwenye uchumi.

“Inawezekana Serikali ina lengo zuri, lakini hatukushirikishwa. Uwekezaji utakufa nchini kwa sababu wengi hukopa ili kuendeleza biashara walizonazo jambo linalozuiwa kwa sasa,” alisema Simbeye.

Kwa hali hiyo, alisema sekta ya kwanza kuanguka itakuwa ya benki na taasisi za fedha ambazo zitakosa wateja.

TPSF imeipongeza Serikali kwa juhudi za kuboresha mazingira ya biashara hasa kwa kurahisisha upatikanaji wa ardhi kwa ajili ya kuwekeza, lakini imetoa angalizo kwa marekebisho yanayopendekezwa.

TPSF imepokea malalamiko kutoka kwa wanachama, benki na taasisi za fedha, wamiliki wa viwanda pamoja na wakulima kuhusu mabadiliko yanayopendekezwa, inasema barua hiyo.

Miongoni mwa hoja zilitolewa na taasisi hiyo ni kutoshirikishwa kwa wadau katika utungaji wa mabadiliko hayo ili wawasilishe maoni yao.

Imesema kwa namna muswada huo ulivyoandaliwa, Serikali inaweza isipate mafanikio inayoyatarajia na mapendekezo ya vifungu hivyo vitatu yanaweza kuwa na athari kwa uchumi wa nchi.

“Kwa barua hii, tunaiomba wizara yako iuondoe mara moja muswada huo kabla haujajadiliwa na Kamati ya Bunge au Bunge lenyewe mpaka wadau, ikiwamo TPSF watakaposhirikishwa,” inasema barua hiyo.

Muswada huo unapendekeza kufanya marekebisho katika sheria tano ambazo ni Sura ya 25 ya Sheria ya Ufilisi, Sura ya 439 ya Sheria ya Bajeti, Sura ya 113 ya Sheria ya Ardhi na Sura ya 238 ya Sheria ya Utumishi wa Umma ili kuondoa mapungufu mbalimbali yaliyomo katika utekelezaji wa sheria hizo.

Marekebisho ya Sheria ya Ardhi ambayo TPSF inapendekeza maoni yao yazingatiwe, inabadili masharti yaliyopo kwenye Kifungu cha 45 kwa kuongeza adhabu ya ukiukwaji wa masharti kwa mtu anayeweka dhamana ya miliki ya ardhi.

Kwenye sheria inayofanyiwa marekebisho, vifungu vya 120A, 120 B na 120 C vimeongezwa kuwezesha fedha zinazopatikana kutokana na mkopo uliotolewa kwa dhamana ya miliki ya ardhi Tanzania zitumike kuendeleza sehemu ya ardhi iliyowekwa rehani kwa miliki zote ambazo hazijaendelezwa.

Marekebisho hayo yanawataka wote wawili; mkopaji na mkopeshaji, kuwasilisha taarifa kwa kamishna wa ardhi. Licha ya hilo, yanataka fedha itakayopatikana iwekezwe Tanzania.

Aidha, muswada unataka benki na taasisi zote za fedha zinazotoa mkopo husika; ndani na nje ya nchi kuwasilisha tamko kwa kamishna wa ardhi kwamba fedha hizo zitawekezwa Tanzania.

Maana yake, mkopo wa fedha zozote zitakazokopwa kwa dhamana ya ardhi ya Tanzania kisha zikawekezwa nje, utakuwa batili.

Waziri Lukuvi amewataka wadau wenye maoni kuhusu marekebisho yanayopendekezwa kwenye muswada huo kuyawasilisha kwenye kamati husika ya Bunge.

“Huo ndio utaratibu. Kama kuna malalamiko yoyote, ni vizuri yawahishwe wakati huu vikao vinapoendelea, yatachambuliwa,” alisema.

Mimi Ndio Msanii wa Kwanza Kupanda Ndege Kwenda Mwanza – Dully Sykes

$
0
0
Mimi Ndio Msanii wa Kwanza Kupanda Ndege Kwenda Mwanza – Dully Sykes
Msanii wa muziki Bongo, Dully Sykes amesema baadhi ya watu wamekuwa wakihofia kumpa nafasi anayostahili katika muziki kwa madai kuwa huwa hapandi ndege wakati yeye ndiye msanii wa kwanza Bongo kupanda ndege na kwenda kufanya show mkoani Mwanza mwaka 2000.

Muimbaji huyo amesema kwenye muziki wake alitakiwa awe mbali sana kama Wanigeria na kama watu wa Afrika wangesikia muziki wake angewakilisha vizuri Tanzania.

“Lakini watu wanakuwa wananihofia sana, wananiogopa wanajua wakijaribu sijui kitatokea kitu gani,” Dully Sykes ameiambia Choice Fm.

“Wanasema wewe hupandi ndege, mimi napanda kwenye maendeleo nisipande ndege kwa ajili gani?, nafikiri mimi ndio msanii wa kwanza kupanda ndege na kwenda kufanya show Mwanza, kuna wengine walipanda ndege miaka hiyo lakini mimi nilipanda kwenda kufanya kazi,” amesisitiza.

Ameongeza kuwa kipindi hicho wasanii wote walikuwa wanakwenda Mwanza kwa mabasi.

BREAKING NEWS: Scorpion Ahukumiwa Kwenda Jela

$
0
0
BREAKING NEWS: Scorpion Ahukumiwa Kwenda Jela
MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Wilaya ya Ilala jijini Dar es Salaam imemhukumu mwalimu wa sanaa ya kujihami, ‘Martial Arts’ na msanii wa filamu za kibongo, Salum Njwete maarufu Scorpion miaka 7 jela kwa kosa la kumjeruhi na kumtoboa macho kinyozi, Said Mrisho, pia mahakama imemtaka kulipa faini ya TSH. Milioni 30 kwa ajili ya fidia kwa majeruhi huyo.

Kwa upande wake, mlalamikaji katika kesi hiyo ambaye ni majeruhi, Said Mrisho amelia mahakamani hapo akidai adhabu aliyopewa Scorpion haitoshi ikilinganishwa na kosa alilotenda huku akieleza kuwa atakwenda kwa Rais Dkt. John Magufuli kumueleza masikitiko yake.

 Njwete anlikuwa akikabiliwa na mashtaka mawili ambayo ni  unyang’anyi wa kutumia silaha na kumjeruhi Said Mrisho kwa kumchoma kisu sehemu mbalimbali za mwili zikiwemo, tumboni na mabegani na kisha kumtoboa macho kitendo anachodaiwa kutenda Septemba 6, mwaka jana  katika eneo  la Buguruni Sheli, jijini Dar es Salaam. Pia, anadaiwa kumwibia mali yenye thamani ya Sh 476,000/-.

Hatimaye Sanchez Avaa Jezi ya MAN U kwa Mara ya Kwanza

$
0
0
Hatimaye Sanchez Avaa Jezi ya MAN U kwa Mara ya Kwanza
MSHAMBULIAJI Alexis Sanchez raia wa Chile ameonekana akiwa katika uzi wa Manchester United namba 7 saa chache baada ya usajili wake kukamilika akitokea Arsenal.
SNyota huyo anatarajia kutangazwa rasmi ndani ya saa 24 rasmi akiwa mchezaji wa Manchester United. Katika picha ya uficho, Sanchez anaonekana akipiga picha hiyo akiwa ndani ya Uwanja wa Manchester United, Old Trafford ambapo inaelezwa amepelekwa OT kwa ajili ya kupiga picha maalum.
Raia huyo wa Chile kutoka Arsenal, anatarajia kuwa akilipwa pauni 600,000 kwa wiki zitakazomfanya kuwa mchezaji anayelipwa zaidi ndani ya klabu hiyo. Mgawanyo wa fedha hizo uko mshahara pauni 350,000, haki za picha pauni 100,000 na bonas itakuwa pauni 144,000.

Ronaldo Apasuliwa Uso, Madrid Ikishinda 7-1

$
0
0
Ronaldo Apasuliwa Uso, Madrid Ikishinda 7-1
LICHA ya ushindi wa bao 7-1 dhidi ya Derpotivo la Coruna walioupata Real Madrid katika La Liga, mshambuliaji wake, wa Kimataifa Raia wa Ureno, Cristiano Ronaldo alikutana na dhoruba baada ya kuumia kwa kupasuka usoni.
Ronaldo aliumia kwa kuchanipa sehemu ya usoni baada ya kugongwa wakati akijaribu kufunga.

Alikuwa ameruka kichwa kwa lengo la kufunga lakini akagongana na mchezaji wa Derpotivo. Hata hivyo, Ronaldo alipata huduma nzuri na kilichovutia zaidi ni yeye kutumia simu ya daktari kuangalia kama alikuwa ameumia au la.

Sakata la Kiria Kudai Kupigwa na Mumewe: Haya Machozi Namlilia Mungu

$
0
0
Sakata la Kiria Kudai Kupigwa na Mumewe: Haya Machozi Namlilia Mungu
MWANAHARAKATI na masuala ya wanawake nchini Tanzania, Joyce Kiria ameweka hadharani kuwa mahusiano yake na mumewe Henry Kileo ambaye amewahi kuwa kiongozi na Mgombea Ubunge ndani ya Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) katika Jimbo la Mwanga, Kilimanjaro kuwa hayapo sawa.



Kiria amesema mahusiano yao hayapo sawa kwani yeye amekuwa ndiye baba na mama wa familia ikiwa ni pamoja na kuihudumia familia nzima na kumhudumia mumewe huyo.



Kupitia ukurasa wake wa Instagram huku akibubujikwa na majozi, Kiria amededai huwa anamshauri mumewe atafute japo kazi itakayowaingizia kipato ili kusaidiana kutunza familia lakini mumewe amekuwa mkali na kumshushia kipigo.


“Sikutegemea kama ipo siku kwa mkono wako ungeunyanyua kunipiga (@kilewo2020mwanga) ukasahau kabisa! ukasahau yooote. Nimeharibu career yangu kupigania ndoto yako kwa kugawa watu wangu kwenye biashara zangu, nimepoteza ndugu jamaa na marafiki, umeniachia nimebeba mzigo wa familia kwa muda wote, Malipo yako ni kunipiga/ kunidhalilisha na kunitoa machozi, umenipiga kwa sababu Mimi ni mnyonge siyo! sina nguvu, kwa sababu ni MWANAMKE Sina nguvu za kupigana na MWANAUME.

“Umeniumiza mwili wangu unauma kila mahali, ukanigongesha kwenye gari, ili iweje? Nia yako ilikuwa ni nini? kuniua??,“ameandika Kiria huku akielezea jinsi alivyompigania mumewe hadi kwenye kampeni za uchaguzi mkuu mwaka 2015 hadi akaingiza deni kubwa na kufungiwa kipindi chake cha Wanawake Live kilichokuwa kinaruka EATV.



“Haya MACHOZI yangu namlilia Mungu wangu aliye juu, yeye ndo ataamua, kama ni mimi niliandamana na watoto, nikakufanyia kampeni na deni kubwa nikaingia mpaka nikafungiwa Kipindi hewami, ninakutunza wewe na Watoto wako kwa miaka yote Mungu yupo. Leo umenipiga (@kilewo2020mwanga)?? Sawa watakusifia hao wanaokusifu ujinga, wanaokuambiaga Mimi sikuheshimu, badala wakwambie ufanye kazi utunze familia, Leo watakuona wewe ni mwanaume kwa kunipiga.“amemaliza Kiria.

Okwi Afumua kikosi Simba

$
0
0
Okwi Afumua kikosi Simba
Okwi Afumua kikosi Simba
UJIO wa mshambuliaji wa Simba, Mganda, Emmanuel Okwi, umemfanya kocha msaidizi wa timu hiyo, Mrundi, Masoud Djuma kufumua kikosi chake cha leo kitakachoivaa Kagera Sugar ili nyota huyo aingie kikosini.


Hiyo, ni baada ya mshambuliaji huyo kurejea nchini na kucheza mechi dhidi ya Singida United akitokea benchi, akichukua nafasi ya James Kotei na kufunga mabao mawili kwenye ushindi wa mabao 4-0.

Simba inatarajiwa kuvaana na Kagera leo katika mechi ya Ligi Kuu Bara itakayochezwa kwenye Uwanja wa Kaitaba huko Kagera.



Akizungumza na Championi Jumatatu, Djuma alisema kuwa amevutiwa na kiwango cha Okwi alichokionyesha huku akicheza kwa maelekezo yake, hivyo upo uwezekano mkubwa wa mshambuliaji huyo kumuondoa mchezaji mmoja katika kikosi cha kwanza ili yeye aingie kikosini.



Djuma alisema, Okwi anafaa kwenye mfumo wake kutokana na aina yake ya uchezaji wa soka la mashambulizi ya kushtukiza ‘counter attack’ wakiwa wanashambulia goli la wapinzani wakati wakiwa na mpira.

Djuma alisema, anafurahia kuona Okwi akijiunga na timu na kuushika haraka mfumo wake wa kushambulia goli la wapinzani wakiutumia mfumo ambao awali ulikuwa unabezwa wa 3-5-2 na kupata matokeo mazuri ya ushindi wa mabao mengi.



“Nikuhakikishie kuwa, kama Okwi akiendelea kufanya mazoezi kwa muda mrefu na timu na kuushika mfumo wangu huu mpya vizuri zaidi ya hivi sasa, basi nikuhakikishie timu yangu itapata matokeo mazuri katika michezo ijayo ya ligi kuu.

“Ninakwenda kucheza na Kagera, huenda kikosi changu kikawa na mabadiliko kidogo, ni baada ya Okwi kuingia kwenye mfumo wangu vizuri na kuushika, hivyo upo uwezekano wa mchezaji mmoja kumpisha Okwi,” alisema Djuma.

Prezzo kumwaga Amber Lulu

$
0
0
Prezzo kumwaga Amber  Lulu
VIDEO Queen anayekuja juu kwenye Bongo Fleva, Lulu Eugen ‘Amber Lulu’ ameshtuka kusikia mwanamuziki maarufu wa Kenya, Jackson Makini ‘Prezzo’ ambaye ni mpenzi wake kuwa amemmwaga na kumtambulisha mwanamke wake mwingine kwenye siku yake ya kuzaliwa.

 Amber aliliambia Ijumaa Wikienda kuwa, haamini kama mpenzi wake huyo amempiga kibuti na ni kama kweli atakuwa amepata mwanamke mwingine, basi atakuwa amemdhalilisha mno ukizingatia Prezzo alikuwa tayari ni mwanaume ambaye alishamweka moyoni mwake.

 “Hilo la kutambulisha mwanamke mwingine nimelisikia, lakini kama ni kweli amemtambulisha mwanamke mwingine, atakuwa amenikosea kwa sababu yeye alikubali nimtambulishe hadi kwa ndugu zangu na nilishamweka moyoni,” alisema Amber Lulu.

Magogo Yaliyokosa Mmiliki Bandarini Kupigwa Mnada

$
0
0
Magogo Yaliyokosa Mmiliki Bandarini Kupigwa Mnada
Waziri wa Maliasili na Utalii, Dkt. Hamisi Kigwangalla amesema magogo 938 yaliyopo Bandari ya Dar es Salaam yatauzwa wakati wowote kuanzia sasa baada ya kukosa wamiliki wa mzigo huo.


Waziri Kigwangalla aliyeshika kirungu kwenye picha

Maamuzi hayo yamekuja  baada ya Waziri Kigwangalla mwezi uliopita kufanya ziara ya kushitukiza bandarini hapo baada ya kupata taarifa kuwa kuna shehena hiyo ya magogo ambayo umiliki wake ulikuwa na utata.

Mhe. Kigwangalla alieleza kuwa magogo hayo yamekuwa bandarini kwa miaka 10 huku mengine yakiwa kwenye makontena 55 .

Kutokana na utata huo, Kigwangalla alitoa siku 30 kwa wamiliki wa makontena 55 kujitokeza wakiwa na nyaraka zote ili kuthibitisha kama kweli yalivunwa Zambia kama ilivyodaiwa au laah!.

“Kulikuwa na vikao mbalimbali ndani ya serikali kujadili suala hilo, na tumekubaliana kuyauza baada ya wahusika kutojitokeza kuthibitisha umiliki wake,” amesema Waziri Kigwangalla.

Waziri Kingwangalla amesema jukumu la kuyauza magogo hayo wamepewa Mamlaka ya Mapato nchini (TRA) wanaoruhusiwa kisheria kufanya kazi hiyo, ambapo watashirikiana na Wakala wa Huduma za Misitu nchini (TFS).

Tuzo Zangu za Marekani Siwezi Kuzipasua – AT

$
0
0
Tuzo Zangu za Marekani Siwezi Kuzipasua – AT
Msanii wa muziki Bongo, AT amesema hawezi kuzipasua tuzo zake alizoshinda nchini Marekani November mwaka jana, 2017.

Muimbaji huyo katika mahojiano na kipindi cha Leo Tena cha Clouds Fm amesema awali alipanga kupasua tuzo zake za Kilimanjaro Music Award (KTMA) zilizokuwa zikitolewa hapa nchini lakini baadaye akagundua kuwa tuzo hizo ni mali ya Baraza la Sanaa Taifa (BASATA).

“Ni baada ya kuomba msaada ili nisaidiwe kwenda Kongo nikafanye kolabo na Koffi Olomide, wakanizungusha sana, ilikuwa hasira tu, ila hizi tuzo zangu za Marekani siwezi kuzipasua,” amesema AT.

November mwaka jana AT alishinda tuzo mbili katika ‘B&K Music & Video Music Awards’, vipengele alivyoshinda ni International Artist na Best Music Video kupitia wimbo wake ‘Sili Feel’.
Viewing all 104709 articles
Browse latest View live




Latest Images