Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104744 articles
Browse latest View live

Mgombea Ubunge Kupitia CHADEMA Awatahadharisha CCM

$
0
0
Mgombea Ubunge Kupitia CHADEMA Awatahadharisha CCM
Mgombea ubunge wa jimbo la Kinondoni kupitia tiketi ya CHADEMA, Salum Mwalimu amekitahadharisha Chama cha Mapinduzi kuwa uchaguzi mdogo wa ubunge katika majimbo mawili CHADEMA haitakuwa na muda wa kulialia badala yake watapambana kwa kila aina kupata haki stahiki.


Mwalimu ambaye pia ni Naibu Katibu Mkuu wa CHADEMA Zanzibar amedai kuwa katika uchaguzi huo yupo mbele katika kutetea maslahi ya wananchi wa Kinondoni hivyo atapigania haki kwa kila aina.

“Kama ni nidhamu ya siasa waliyoikataa hapa watairudisha, na wasipokubali kuirudisha Kinondoni maana yake ustaarabu katika siasa tunaamini utakuwa umeshamalizika, hatutakuwa wakulia safari hii kama ikibidi tutasababisha wale waliokuwa wanatufanya sisi tunalialia hao ndio walie. Nimedhamiria kuitafuta haki ya watu wa Kinondoni, nimejitoa katika kusimamia haki ya watu Kinondoni sitoyumba.“amesema Mwalimu mbele ya Waandishi wa Habari wikiendi iliyopita mapema baada ya kurudisha fomu yake ya kugombea ubunge.

Kwa upande mwingine Mwalimu aliwasilisha pingamizi kwa mgombea ubunge kwenye jimbo hilo kwa tiketi ya CCM, Ndg Maulid Mtulia kwa kutoa hoja tano ikiwemo ya kutorudisha mrejesho wa gharama za uchaguzi mkuu wa mwaka 2015, wakati akigombea ubunge akiwa CUF.

Wakati hayo yakiendelea jijini Dar es salaam, kule mkoani Kilimanjaro katika jimbo la Siha kampeni zimeanza ambapo CCM kupitia kwa mgombea wao Dkt. Gabriel Mollel wanachuana vikali na Elvis Mosi wa CHADEMA.

Uchaguzi wa majimbo mawili ya Kinondoni na Siha umekuja baada ya waliokuwa wabunge wa majimbo hayo kuhamia CCM na uchaguzi huo mdogo unatarajiwa kufanyika mnamo tarehe 17 Februari mwaka huu.


Wanaume Tata Wamtolea Udenda Idris

$
0
0
Wanaume Tata Wamtolea Udenda Idris
WANAUME tata wameonekana kumtolea udenda Mshindi wa Shindano la Big Brother ‘Hot Shot’ 2014, Idris Sultan baada ya kuposti picha yake kwenye mtandao wake wa kijamii wa Instagram akiwa amevaa nguo ya ndani tu, huku wanaume tata hao wakiweka miguno kwenye picha hiyo.

Kitendo cha wanaume tata hao kuguna kulizua mjadala mkubwa, jambo ambalo Idris aliona ni cha kawaida na kudai kuwa yupo kazini na kama kuna watu wengine nao wapo kazini kumwangalia maungo yake, basi imekula kwao.

“Jamani mimi niko kazini. Kama kuna mtu anajadili na maungo yangu, atakuwa naye yupo kazini na anajisumbua tu,” alisema.

‘ Nabii Tito’: Amtaka wema sepetu

$
0
0
‘ Nabii Tito’: Wafadhili Wangu ni Walevi
Mkazi mmoja wa Dodoma anayejitangaza kama nabii, Tito Machija amesema watu wasimuona kuwa hana akili kutokana na mahubiri yake ambayo yanatofautiana kwa kiasi kikubwa na imani za waumini wa dini nyingine, hasa Wakristo.

Machija, ambaye anajulikana kama ‘Nabii Tito’ anahamasisha kuoa mke zaidi ya mmoja, ikiwa ni pamoja na kutembea na wafanyakazi wa ndani; anatumia pombe kunasa waumini na anadai hataki nyimbo za injili kwenye ‘ibada’ zake, ambazo nyingi hufanyikia baa.

‘Nabii’ huyo anaonekana kwenye mitandao ya kijamii akiwa amevalia kanzu nyeupe yenye misalaba miwili, chupa ya bia na kitabu kitakatifu aina ya Biblia.

“Nawashangaa wanaoniona mimi sina akili, niko timamu kabisa na ninaelewa ninachokifanya,” alisema alipozungumza na MCL Digital.

“Narudia tena kusisitiza kuwa walevi ndio watakaoingia ‘mbinguni’ na mafundisho ninayoyatoa ni sahihi,”

Tito amekuwa akionekana kwenye mitandao ya kijamii, hususani kwenye video fupifupi za Instagram, akiwa amevalia mavazi kama ya kichungaji na kucheza muziki huku akinywa bia na akiwa ameshika biblia.

‘Nabii’ huyo, mwenye wake watano na watoto 12, amedai kuwa kwa sasa hitaji lake kubwa ni kumuoa mwigizaji Wema Sepetu ili aungane naye katika huduma zake.

“Wema ni msichana mzuri wa sura na umbo nataka nimuoe awe sehemu ya kanisa langu na nina imani watu wengi wataongezeka kwenye ibada ili kuja kumuona yeye na wake zangu hawana tatizo na hilo hata mmoja wao ananisaidia kumshawishi ili tuungane naye,” alisema Tito.

Tito anakiri kuwa ‘kanisa’ lake halijasajiliwa ila anadai kwamba anapata ufadhili kutoka kwa walevi mbalimbali.

Tito amedai  kuwa ‘kanisa’ lake lipo karibu na Chuo Kikuu cha Dodoma na mara nyingi ibada zake huwa anazifanya kwenye baa na ana wafuasi  wengi kiasi cha kutojua  idadi yao.

Amesema kabla ya ibada kufanyika kwenye baa husika, huanza kwa kupeleka vipeperushi kwa mmiliki ili kuwapa taarifa waumini wake siku hasa ya ibada kufanyika katika baa hiyo.

“Siku ya ibada ikifika naenda pale nikiwa na bia zangu za (anaitaja aina ya bia) ambazo nimeshaziombea. Zina ‘upako’. Kila anayetaka kuingia kwenye ibada analipa kiingilio cha Sh12,500. Ukilipa pesa hiyo unapata bia zako tano ndiyo huduma inaendelea usipotoa unafukuzwa,” alisema.

Tito anajinasibu kuwa ana waumini wengi ambao hujitokeza kusikiliza mafundisho yake ambayo kwa kiasi kikubwa yanahamasisha ulevi na mapenzi kwa wasichana wa kazi wa majumbani.

Amesema kwenye huduma zake nyimbo za injili hazina nafasi kwa kuwa huwaburudisha waumini wake kwa nyimbo za kisasa.

“Mtu akishaweza safari zake kichwani ukimuwekea bongofleva anacheza na kufurahi huku ibada inaendelea,” alisema.

Nabii huyo amedai kuwa hakuna anachokizungumza kutoka kichwani mwake bali anasimamia mistari ya vitabu vitakatifu.

 “Wapo wengi wanaopinga huduma zangu ila nawaambia sijakurupuka nafanya kitu ambacho kipo na wala sioni kama ninakosea,” alisema.

Kwanini ‘ibada’ kwenye baa

Tito amedai kuwa anaingia makubaliano na wenye baa kwa kuwa ndiyo sehemu ambayo walevi hukutana na kwake ni mahali sahihi pa kutoa huduma.

“Pale nakwenda na bia zangu kadhaa kwa ajili ya waumini watakaoingia kwenye ‘ibada’. Zikiisha naondoka zangu, nawaacha wanaendelea kununua za baa hapo ndipo mwenye baa anaponufaika,” alisema.

Watu wengi wamekuwa wakilaumu mafundisho ya Tito kuwa yanapotosha na wameiomba Serikali kuchukua hatua.

Johari Ana Kidonda Kisichopona

$
0
0
MWIGIZAJI wa kitambo Bongo, Blandina Chagula ‘Johari’ amefunguka kuwa tangu ampoteze mama yake mzazi, Asha Chagula aliyefariki dunia wiki iliyopita, amepata kidonda kikubwa ambacho hakiwezi kupona katika maisha yake yote.


Huku akiwa na majonzi, Johari aliliambia Ijumaa Wikienda kuwa, mama yake huyo alikuwa ni nguzo muhimu katika maisha yake kwani alikuwa ndiye mshauri wake mkubwa.

 “Mama yangu alikuwa ni mtu muhimu sana katika maisha yangu na amenipa kidonda kikubwa sana katika maisha yangu ambacho hakiwezi kupona milele, ninaumia mno na sijui nitawezeje bila mama yangu,” alisema Johari.

Kigali: Watu Wajazana Kumuona Diamond Platnumz

$
0
0
Nyamirambo - Kigali, Watu kutoka huku na kule walifurika siku ya Jumamosi Januari 20, 208 kumuona mubashara msanii wa kitanzania Diamond Platnumz.

Msanii huyo alikwenda sehemu inaitwa Tapis Rouge iliyoko tarafani Nyamirambo, wilayani Nyarugenge mjini Kigali, ili kuwasalimu mashabiki wake ambao walikuwa wamejitokeza kwa wingi.

Wakati wakitaraji kumuona akiwatumbuizia nyimbo zake, Diamond kwa muda wa dakika kama 20 alizokuwa sehemu hiyo hakuimba wimbo wowote bali alipita katikati ya umati wa watu akiwapungia mikono kama mfalme na baadaye kuwasambazia karanga zake za Diamond Karanga bwerere.

Diamond aliwasili mjini Kigali siku ya Ijumaa Januari 19, 2019, kwa ajili ya kuwatembelea watoto wenye ulemavu wa macho waishio tarafani Gatsata wilayani Gasabo mjini Kigali katika kituo cha Jordan Foundation, ambao aliahidi kugharamia matibabu yao kwa muda wa mwaka mmoja.

Baada ya kuwatembelea watoto hao alikutana na waandishi wa habari kwa mahojiano ambapo alipata kuzindua Diamond Karanga na Chibu Parfume na kuweka bayana mipango yake mingine ya kuanzisha Wasafi FM na Wasafi TV mwaka huu, na hata kuzindua albamu yake nyingine yenye jumla ya nyimbo zisizopungua 18, kwa mujibu wa maelezo yake.

Amesema anataka hata kufungua tawi la lebo yake ya WCB nchini Rwanda, akisema anaamini Rwanda kuna vipaji vingi lakini wasanii hawapati studio zenye uwezo mkubwa wa kuwainua kumuziki.

Amesema pia kuwa anataka kuwa na makazi Rwanda, na kesho yake alipelekwa sehemu tofauti ambazo kuna nyumba nzuri ili azikague na achague anayoona inamfaa. Kaisifia Rwanda kwa usalama na usafi na kusema ameona ana kila sababu ya kuwa na makazi Kigali.

Hizi hapa chini ni picha za jinsi watu walivyofurika Nyamirambo kumuona ambapo wengine walilazimika kusimama juu ya pikipiki zao ili waweze kumuona.

Pata Dawa Bora ya Nguvu za Kiume na Maumbile Madogo ya Kiume ( Super Shafti)

$
0
0

DAWA BORA YA NGUVU ZA KIUME NA MAUMBILE MADOGO YA KIUME ( SUPER SHAFITI) NI DAWA YENYE UWEZO MKUBWA WAKUTIBU UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME


 (SUPER SHAFITI ni dawa ya asili yenye uwezo mkubwa wa kuogeza nguvu za kiume maradufu
(1) itakufanya uwe na nguvu za ajabu ukiwa unafanya ntedo la ndoa
(2) inaogeza hamu ya kurudia ntedo la ndoa zaidi ya mara tatu bila kuchoka
( 3) itakufanya uchelewe kufika kileleni dani ya dk 30
( 4)  itaimalisha milija ya uume iliyo legea au kusinyaa
(5) lnarefusha na kunenepesha uume saizi utakavyo kuazia ichi 1-8 unene sm 2-4
 (6) itakupa nguvu za kusimamiasha uume wako barabara kama_ msumari wakati wa ntedo la ndoa
(7) inasaidia kusafisha mishipa. ya kwenye uume na hivyo kusaidia Katika kuongeza kasi ya msukumo wa damu kwenye mishipa ya uume
(8) usaidia kuurudisha nje uume ulioingia ndani
(9) inasaidia kuogeza manii nyingi ambazo vina viini vya uzazi
(10)usaidia kutibu madhara ya punyeto ,matumizi makali ya  madawa ya kizugu mirungi bangi na sigara
                                                                          KWA NINI BAADHI YA WANAUME WENGI WANA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME NA KUWA NA MAUMBILE MADOGO YA KIUME NINI CHANZO CHAKE?

ni kutokana na magonjwa megi kuongezeka yakiwemo kisukari presha ya kupanda na kushuka upigaji wa punyeto wa mda mrefu magonjwa ya moyo ngiri ya kuviba korondani vidonda vya tumbo
Msongo wa mawazo  tumbo kuuguruma kujaa ngesi kutopata choo vinzuri maumivu ya mgongo kiuno na tumiaji wa madawa makali ya kizungu ya kuongeza nguvu za kiume kuzaliwa na chango linaloshabulia neva za ukuwaji wa uume utumiaji wa mirungi bangi sigara na nk  tunapenda kuwatangazia wasomaji, wa makala zetu kuwa tunazo dawa nzuri za asili ambazo hazina mazala na zinazotibu na kuponyesha matatizo ya upungufu wa nguvu za kiume na maumbile ya kiume

NA TUNATIBU MAGONJWA YOTE SUGU KAMA KISUKARI PRESHA AINA YOTE UGONJWA WA MOYO SITRUKO KWIKWI KICHOMI MINGUU KUFA NGAZI ASIMA NK MZEE ISAYA ANAPATIKANA MAGOMENI MIKUMI KARIBU NA KANISA  TUMAINI HEBRAST CLINI NDIYO JIBU NA SULULISHO YA MATATIZO YOTE

PIGA simu 0745495181 au 0682644040

Kwa watu wa mikoa huduma utatumiwa na watu wa nje ya nchi utazipata dsm kama huna nafasi ya kufika ofisini kwetu utaletewa popote ulipo

Mama Uwoya Amkana Dogo Janja, Asema Haitambui Ndoa yao na Mwanae ni Jjane

$
0
0
Mama mzazi wa muigizaji wa filamu hapa nchini, Irene Uwoya amefunguka na kueleza kuwa hamtambui mume wa sasa wa mwanaye, Dogo Janja na anachokijua yeye ni kuwa mume wa ndoa wa mwanaye amefariki mwaka jana.

Mama Uwoya ameongeza kuwa anachokifahamu yeye mpaka sasa mwanaye ni mjane, kwani aliyekuwa mume wake, Ndikumana amefariki dunia, na kabla ya hapo walikuwa wana ugomvi tu ila hawakuwahi kuachana.

Mama huyo aliendelea kueleza kuwa mwanaye, Irene uwoya, alifunga ndoa ya kanisani na aliyekuwa muewe, marehemu Ndikumana, ambaye walijaliwa kupata mtoto mmoja wa kiume na walikuwa hawajaachana lakini walikuwa katika mgogoro ambao walishindwa kuutatua mpaka mwanasoka huyo alipopatwa na umauti.

“Ngoja nikwambie hakuna ndoa ambayo wazazi hawashirikishwi, ndoa yoyote lazima wazazi wajue na washiriki. Ninachojua kuwa irene ni mjane, mumewe ambae sisi tunamjua ndo huyo ameshafariki. Ninachojua mimi ni kuwa swala la ndoa lazima watu wazazi washirikishwe kuanzia mwanzo hadi mwisho,” alisema mama Uwoya.

Hata hivyo mama huyo anasema kwa kuwa kama Irene ni mtu mzima, basi anajua kitu anachofanya, hivyo hawawezi kumzuia na kumkataza. Lakini kitu cha kujua ni kwamba wazazi hawakuwahi kuapata taarifa kuwa mtoto wao alipewa talaka na mwanaume aliyefunga nae ndoa; na kwa sababu wao sio watu wa kufatilia vyombo vya habari hawakutaka kufatilia maswala ya media, ila walitaka kusikia kutoka kwa mtoto wao.

“Tunachojua mwanetu ni mjane, kama ana ndoa anaijua yeye. Lakini sisi hatuitambui na wala hatuaamini. Wala hatumjui huyo mtu anaitwa Dogo Janja labda wanaigiza,” alisema mama Uwoya.

Mimi ndio Msanii wa Kwanza Kupanda Ndege Kwenda Mwanza – Dully Sykes

$
0
0
Msanii wa muziki Bongo, Dully Sykes amesema baadhi ya watu wamekuwa wakihofia kumpa nafasi anayostahili katika muziki kwa madai kuwa huwa hapandi ndege wakati yeye ndiye msanii wa kwanza Bongo kupanda ndege na kwenda kufanya show mkoani Mwanza mwaka 2000.

Muimbaji huyo amesema kwenye muziki wake alitakiwa awe mbali sana kama Wanigeria na kama watu wa Afrika wangesikia muziki wake angewakilisha vizuri Tanzania.

“Lakini watu wanakuwa wananihofia sana, wananiogopa wanajua wakijaribu sijui kitatokea kitu gani,” Dully Sykes ameiambia Choice Fm.

“Wanasema wewe hupandi ndege, mimi napanda kwenye maendeleo nisipande ndege kwa ajili gani?, nafikiri mimi ndio msanii wa kwanza kupanda ndege na kwenda kufanya show Mwanza, kuna wengine walipanda ndege miaka hiyo lakini mimi nilipanda kwenda kufanya kazi,” amesisitiza.

Ameongeza kuwa kipindi hicho wasanii wote walikuwa wanakwenda Mwanza kwa mabasi.


Mpiga Picha Raqey Aachia Waraka kwa Wapiga Picha ‘Naona Aibu Kuitwa Mpiga Picha’

$
0
0
Mpiga picha maarufu nchini Tanzania, Raqey Allaraqya kutoka I View Studios amefunguka kwa kudai kwamba kuna wapiga picha kutoka mtaani wameivamia tasnia hiyo.


Raqey ameanda taarifa hii…

I was thinking of where to start writing this note; i think things are way out of hands, it seems like no one is there to talk about it. people are afraid because of some stupid people in the industry who sit aside and talk some shit about others just because they are intimidated.

Im not here to talk about stupid childish argument you have with each other im here to talk about how photography is being depreciated.

Who is to blame for this???guess what……. it is you!!!!! Wacha tuu niandike kiswahili hakuna kupamba hapa im so pissed.

Yaani photography umeharibika to a point hata unaona aibu kuitwa mpiga picha, when i started after i graduated i was afraid to call myself a photographer i felt like i had to work hard and present my work more before i call myself mpiga picha.

Sasa siku hizi auntie akitoka tuu dubai akileta camera basi nishakuwa mpiga picha. Ndugu zangu niliongea hili muda mrefu sana mkaniona mjinga blah blah wengine wakajifananisha na mimi and being on top of the game.

Well look at the industry now i found some stupid people at some places fucking taking picture being treated like dumbs and loosers i felt so bad as one of us being treated like shit;

Tumefika mahali tunarudi kule kwa photo me kesho na sisi tutaweka picha chini baada ya events tuuze 500 each photo kwa ajili tuu ya njaa za kijinga na wivu.

PHOTOGRAPHY IS AN ART not selling some senene damn it. Akili za kimaandazi kabisa clients take you as stupid cheap group of people who ignite flashlights and eat their food at the events.

Being reasonable cost wise is an OK factor thats the heart of competition who does not know that??
But instead of being a photographer you are becoming are ASS KISSER well you are nothing but an ASSHOLE.

Ikiwa unajidhalilisha to a point unaenda kwenye harusi kushoot halafu unaonekana like a piss of shit hell no ndugu zangu mmefika mbali mno.

Na hii ndio sababu mnakuwa treated so cheap to a point you have no VALUE any more; at the end mnagombana wenyewe kwa wenyewe na kulalamika pembeni.

Client can can choose who ever they want to work with at any cost that they can afford. Perhaps budget utakuta ni shilingi 3.500.000 kwa ujinga wenu mnadhalilishana kugombea kazi kutoka 3.500.000 mpaka 600.000 sasa mnaishije wapiga picha 3 kwa 600.000? Mwisho wa yote majungu ugomvi utasikia jamaa pesa yote anachukua yeye sisi anatulipa buku 40 tuu.

i made a lot of effort kwenye industry from commercial photography, studio photography, wedding photography/videography, bongo movie, bongo flava etc.

I took the initiative to move the industry to where you all found it ,where you make money and call each other wapiga picha.
It is the time to fix this shit.

Do not miss quote me mtu yoyote anaweza kununua camera na kupiga picha ila sio kila mtu ni mpiga picha. Wengine tubaki tuu ku like na ku comment kwenye social media.

Hate me or love me i dont give a shit this industry need someone to straighten things up; if it is not you then it is me. . . Haya kaeni kwenye magroup sasa mpige domo.

Van Persie Arejea Timu Yake Iliyomkuza Feyenoord

$
0
0
Van Persie Arejea Timu Yake Iliyomkuza Feyenoord
Mchezaji wa zamani wa timu ya taifa ya Uholanzi Robin Van Persie amerejea katika timu yake ya zamani iliyomkuza ya Feyenoord na kusaini mkataba wenyethamani ya paundi milioni 1.5 kwa mwaka akitokea Fenerbahce kwa uhamisho huru.

Van Persie ameripoti hii leo De Kuip ili kukamilisha uhamisho huo  wa kurejea  Feyenoord tangu ipite miaka 14 toka kuondoka kwake na kujiunga na  Arsenal 2004 akiondoka hapo mwaka 2002.

Miongoni mwa klabu alizopata kuchezea Van Persie  kabla ya kurejea tena katika ligi ya Uholanzi ni the Gunners , Manchester United na Fenerbahce.

Magufuli Apokea Hati za Utambulisho wa Mabalozi 6

$
0
0
Magufuli Apokea Hati za Utambulisho wa Mabalozi 6
Rais Dkt. John Pombe Magufuli amepokea hati za utambulisho kutoka Mabalozi 6 walioteuliwa kuziwakilisha nchi zao hapa nchini.

Hakuna Kitu Kinaitwa UKAWA – Humphrey Polepole

$
0
0
Katibu wa Itikadi na Uenezi wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Humphrey Polepole amesema kuwa hakuna kitu kinaitwa UKAWA kwani mpango huo ulianzishwa na CHADEMA ili kuvitumia vyama vingine kisiasa.

Polepole amesema kuwa kama UKAWA ingelikuwepo hadi leo basi isingetokea baadhi ya majimbo CHADEMA kushindana na CUF ile hali vyama vyote vipo chini ya muavuli wa UKAWA.

“Hakuna kitu kinaitwa UKAWA, hii ilikuwa project ya Chadema ikivitumia vyama vingine, CUF, NCCR na NLD. Kilichobaki ni UKIWA, katika jimbo lililokuwa la CUF leo CDM na CUF wanamenyana,”ameandika Humphrey Polepole kupitia Twitter.

Hata hivyo, kwenye uchaguzi mdogo wa ubunge katika jimbo la Kinondoni CUF kwa upande wa Prof Lipumba imesimamisha mgombea wake huku CHADEMA nao wakisimamisha mgombea wao.

Pata bidhaa za Kayla's zitokanazo na karanga zikiwa zimeandaliwa kwa ustadi mkubwa.

$
0
0

Pata bidhaa za Kayla's zitokanazo na karanga zikiwa zimeandaliwa kwa ustadi mkubwa.

Kuna Kayla's Peanut butter , peanut butter fudge plain na zilizo na chocolate, dark /white chocolate cups, Flourless cakes (zenye chocolates)

Jipatie kwa jumla na reja reja.

Direct calls: +255716898444

Baada ya Kuvurugana na Heri Muziki Mrembo Diva Atangazia Dunia Kuwa Yupo Single

$
0
0

From Diva - "Im single ....baada ya mwaka sasa niko huru ..sina mahusiano na mtu yoyote n not looking .....life huh?
2018 wuddapppp..
JIMBO HURU..
DIVA WA WATANZANIA
P:s make up on fleek "

Mchezaji Juma Nyosa Aingia Matatani Tena Baada ya Kumshushia Kipigo Shabiki Mpaka Kuzirai Leo

$
0
0

KAITABA: Jeshi la Polisi linamshikilia Beki wa Kati wa Klabu ya Kagera Sugar, Juma Nyoso kwa tuhuma za kumpiga shabiki hadi kuzirai

Inadaiwa kuwa Mchezaji huyo alikerwa na maneno(matusi) ya Mashabiki ndipo alichukua uamuzi huo wa kumshambulia mmoja wao

Majeruhi huyo ameondolewa Uwanjani hapo(Kaitaba) kwa gari maalum la kubebea Wagonjwa(Ambulance)

Ikumbukwe kuwa Mchezaji huyo wakati akiichezea Mbeya City aliwahi kuadhibiwa na Shirikisho la Mpira wa Miguu Nchini(TFF) kwa kosa la kumdhalilisha kwa kutumia kidole cha kati Mshambuliaji, John Bocco(aliyekuwa akiichezea Azam FC)

Zijue Faida za Kiafya za Kunywa Maji ya Moto

$
0
0
Kuna tiba nyingi za kitabibu zilizogawanyika katika makundi mbalimbali. Kuna zile za hospitali ambazo ni lazima zinunuliwe, lakini kuna tiba ambazo kwa ushauri wa daktari hata wewe unaweza kuziandaa bila kutumia gharama kubwa. Moja ya tiba hizo ni kunywa maji ya moto.

Kwa mujibu wa wataalamu wa afya, maji moto yanatibu magonjwa mengi ikiwemo figo, kutoa sumu mwilini na kuyeyusha mafuta tumboni. Pia hurahisisha mzunguko wa damu, huondoa sumu kwenye ubongo na kusafisha haja ndogo.

Kunywa maji ya moto kila unapotaka kwenda kufanya kazi ya nguvu au mazoezi iwe kama kinga na inashauriwa kila siku unywe glasi nane ili kutoa taka na kila kisichotakiwa kubaki mwilini, kupitia jasho. Wataalamu wa afya wanasema kuwa ni vyema pia kunywa maji ya moto yenye ndimu au limao kabla ya kifungua kinywa ili kurahisisha mfumo wa mwili kwa siku nzima.

Mwinyimvua Pazi, Mtaalamu wa Chakula na Lishe kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, anasema kuwa maji yanarahisisha uyeyushaji wa chakula na mafuta mwilini, hivyo kutokana na umuhimu huo ni vyema kunywa maji ya moto yatakayofanya kazi haraka na kwa ufanisi mkubwa bila kuchosha figo.

Anaitaja faida nyingine ya kunywa maji ya moto kuwa ni kutoa sumu zilizopo kwenye mishipa ya fahamu na kuisaidia figo kufanya kazi kikamilifu, Fahamu aina za maumivu ya kichwa kwenda kufanya mazoezi, kitu kinachoweza kuzidisha maumivu au maji kucheza wakati wa kukimbia kama mazoezi ya kukimbia.

Lakini yakiwa ya moto ni kama umekunywa chai au kula chakula cha kawaida, tofauti na maji baridi ambayo yanagandisha na kuilazimisha figo kuyeyusha kwanza na kisha kuchuja. Anashauri umuhimu wa kunywa maji moto kabla ya kufanya mazoezi kuwa ni kujiandaa kwa ajili ya kuchuja jasho ambalo litatoa sumu.

Maji yakiwa ya moto yakifika kwenye figo yanaanza kufanya kazi moja kwa moja, kuliko yakiwa ya baridi yanaweza kusumbua kwa kuwa ni lazima yapate joto la mwili kwanza kabla ya kuanza kufanya kazi.

“Ukiachilia kusubiri yachemke, pia ni kumuepusha mtumiaji na hatari ya kuumwa tumbo kutokana na kunywa maji ya baridi bila kuweka kitu tumboni na  Maji Ya Moto Yalivyo Na Faida Mwilini anasema Mwinyimvua. Mwinyimvua anaongeza kuwa maji ya moto ni mazuri hata kwa kupata choo, kwa vile yanarahisisha uyeyushaji na uchambuaji wa kinachotakiwa na kisichotakiwa.

Wanaokunywa ya baridi wana uwezekanao mkubwa wa kupata haja kubwa kwa shida. Vilevile, Mwinyimvua anashauri kuwa ni vyema kunywa maji moto yaliyochemshwa na kuyaacha yapoe na kuwa ya uvuguvugu na kuongeza limao na asali ambapo mbali na kuongeza ladha, asali na limao vina faida kiafya.

Gayl Canfield, Mkurugenzi wa Lishe kutoka katika Kituo cha Biashara cha Pritikin Longevity kwenye Mji wa Miami, Florida nchini Marekani, anasema kuwa kunywa maji ya uvuguvugu au ya moto ni vyema kwa kuwa hufanya kazi moja kwa moja kutokana na hali ya tumbo kuwa na joto muda wote. Canfield anasisitiza, “Maji ni muhimu kwa mwili wako, yakiwa ya moto ni bora zaidi, kwa kuwa yanatoa rangi ya njano ya mkojo na kuufanya uwe msafi na wenye rangi angavu.”

Habari Njema: Tunatibu Busha, Korodani Kuvimba,Ngiri, Miguu Kufa Ganzi Pamoja na Matatizo ya Nguvu za Kiume

$
0
0

Ni Dawa ya nguvu za kiume inayorefusha na kunenepesha uume saizi uipendayo (Inch 1-7) kwa muda wa siku 6 tu.Dozi hii itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa muda wa dakika 30, utarudia tendo la ndoa zaidi ya mara 4 bila hamu kuisha bila kujali umri na garantee ni miaka 60 baada ya kutibu tatizo.

Pia tunatibu Busha bila kufanyiwa Oparesheni, korodani moja kuvimba, ngiri, tumbo kujaa gesi na kuunguruma, kutopata choo vizuri, miguu kuwaka moto na kufa ganzi, chango la wanawake, kisukari na kutokwa na kinyama sehemu ya haja kubwa.

MIHAYO:
Inarudisha mke, mchumba, hawara na atakutimizia kila kitu unachotaka kutoka kwake ndani ya  saa 2 tu hata kama yupo mbali. atarudi na kumfunga asiwe na mwingine zaidi yako.

Umefukuzwa kazini? unataka kupandishwa cheo? Umepoteza pesa zako kwenye biashara bila kujua umepandikizwa chuma ulete? Njoo urudishe pesa zako. Unauza mali yako haiendi?

Dr Mollel 'Nilifanya Jambo la Kitoto Nilipokuwa Chadema, Waliniambia Nitoke Bungeni Magufuli Akiingia"

$
0
0
Aliyekuwa Mbunge wa Jimbo la Siha kwa tiketi ya CHADEMA, Godwin Ole Mollel ambaye alihama chama hicho na kujiunga na CCM amefunguka na kusema alipotoka Bungeni wakati Rais Magufuli anaingia ulikuwa ni uamuzi wa kitoto.


Mollel amesema hayo jana wakati wa uzinduzi wa kampeni za Uchaguzi wa marudio ambao unatarajiwa kufanyika Februari 17, 2018 ambapo Mollel sasa anagombea ubunge wa jimbo la Siha kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM).

"Nilipofika Bungeni nikaambiwa ukimuona Magufuli anaingia Bungeni wewe toka nje, nikabisha kidogo nikaambiwa wewe ambaye ni mbishi kwanza tangulia mbele, kwa sababu mimi nina nidhamu na naheshimu viongozi nikatangulia kikamanda mbele nikatoka nje, nikiumia nikisema nimefanya jambo la kitoto lakini ikafika mahali nikaambiwa hauruhusiwi kuongea na Mbunge wa CCM, wala kumsalimia" alisema Mollel 

Mbali na hilo Mollel anasema baadaye aliambiwa ashone suti ili siku bajeti ikiwa inajadiliwa watoke nje lakini yeye anadai aligoma na kuanzia hapo alianza kuchukiwa ndani ya chama chake hicho alichokihama.

Pia Mollel amedai kuwa anatambua Lowassa atakuja kupiga kampeni za CHADEMA Siha na kusema anatambua kiongozi huyo amepangwa na hawezi kukataa kwa kuwa anaogopa kufukuzwa kwenye chama kwa kuwa tayari yeye ni mzee lakini amesema alishawaeleza ukweli kutoka Ikulu kwamba CCM ndiyo mpango.

Soma Nafasi za Ajira Zilizotangazwa Leo Jumanne

$
0
0

Juma Nyoso Baada ya Kumtwanga Shabiki Kupandishwa Mahakamani

$
0
0
Juma Nyoso Baada ya  Kumtwanga Shabiki Akamatwa na Polisi
Mlinzi wa timu ya Kagera Sugar Juma Said Nyosso anatarajiwa kupandishwa Mahakamani siku yeyote kutoka leo (Jumanne), kutokana na kutenda kosa la jinai wakati akitoka nje ya uwanja.

Hayo yamebainishwa na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kagera, RPC Agustine Ollom na kusema bado wanamshikilia mchezaji huyo wa Kagera na endapo watakapomaliza mahojiano naye wanatarajia kumpeleka Mahamakani kwa ajili ya mashtaka yake.

"Bado mtuhumiwa yuko mahabusu anaendelea kuhojiwa na yule majeruhi yupo hospitali kwa hiyo tunategemea madaktari wakatakavyo kuwa wamepita hii 'round' ya asubuhi watatupa hali yake jinsi anavyoendelea. Juma Nyoso amefanya kosa la jinai hivyo sisi tutampeleka Mahakamani mapema itakavyowezekana na huko ndipo itakapojulikana kama alitenda kosa au laa na mwisho kutolewa adhabu juu yake", alisema RPC Agustine Ollom.

Juma Said Nyosso alikamatwa jioni ya jana (Jumatatu) baada ya mechi kumalizika dhidi ya Simba katika dimba la Kaitaba ambapo wachezaji wa Kagera Sugar walikuwa wanaelekea katika vyumba vya kubadilishia nguo kwa bahati mbaya mmoja ya mashabiki inasemekana alimpulizia vuvu zela Nyosso ndipo naye alipompiga shabiki huyo mpaka kupoteza fahamu.
Viewing all 104744 articles
Browse latest View live




Latest Images