Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104431 articles
Browse latest View live

Serikali Kumshughurikia Nabii Tito

0
0
Serikali Kumshughurikia Nabii Tito
Mkurugenzi wa Idara ya Huduma za Sheria wa Wizara ya Mambo ya Ndani, Marlin Komba amesema hamtambui mtu anayejiita nabii Tito na kwamba hajasajili kanisa lake katika ofisi ya msajili wa taasisi za dini.

Komba amesema Serikali imeona vitendo anavyovifanya ‘nabii’ huyo kupitia mitandao ya kijamii na imeanza kuchukua hatua.

“Ninachoweza kusema ni kwamba hakuna mtu anayezuiwa kuongea hapa nchini, mwache aongee anavyoweza ila Serikali imeshaona anachokifanya na yanayoendelea mitandaoni hatua zinachukuliwa dhidi yake,” amesema Komba.

Kauli hii imekuja kufuatia kusambaa kwa video mbalimbali zikimuonyesha ‘nabii’ huyo akitoa mafundisho yake huku akinywa vilevi pamoja na kufanya matendo ambayo ni kinyume cha maadili ya dini, jambo ambalo limeonekana kuwakera wadau wengi wa dini.

Kwa upande wao viongozi mbalimbali wa dini wameonyeshwa kukerwa na kulaani vitendo anavyovifanya mtu
huyo anayejiita ‘nabii’ na kusisitiza kuwa hakuna dini inayoruhusu hayo.

Askofu Msaidizi wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Dayosisi ya Mashariki na Pwani, Mchungaji Chediel Lwiza amesema kuwa, kutokana na vitendo anavyofanya, mtu huyo hapaswi kujiita mtumishi wa Mungu.

“Huyo hawezi kuwa mtumishi wa Mungu na wala hafanyi huduma ya kanisa. Ni vyema watu kama hawa wafuatiliwe na hatua za kisheria zichukuliwe dhidi yao. Natumaini Wizara ya Mambo ya Ndani ambayo ndani yake ina ofisi ya msajili wa taasisi za dini itafanya kazi yake,” amesema Mchungaji Lwiza.

Naye Msemaji wa Jumuiya na Taasisi za Kiislamu nchini, Rajab Katimba amesisitiza Serikali na viongozi wa dini kuingilia kati suala hilo na kueleza kuwa, hakuna kitabu chochote cha dini kinachohamasisha ulevi na ukosefu wa maadili.

“Hilo suala linakwenda tofauti na dini na mila na desturi zetu pia. Dini zinatakiwa kuleta amani na kuhamasisha watu waheshimiane si kuzungumza mambo yanayokiuka maadili yetu. Naona ipo haja ya viongozi wa dini na Serikali kuingilia suala hili na waende mbali zaidi kwa kuongea naye huenda hafahamu anachokifanya,” amesema Rajab Katimba.

DC Matatani kwa Kupiga Kampeni

0
0
DC Matatani kwa Kupiga Kampeni
Kitendo cha Mkuu wa Wilaya ya Siha, Onesmo Buswelu kupanda jukwaani kumnadi mgombea wa CCM katika Jimbo la Siha, Dk Godwin Mollel kimechafua hali ya hewa baada ya kupingwa na vyama vya siasa huku Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) ikisema hakufanya jambo sahihi.

Mkurugenzi wa Uchaguzi wa NEC, Ramadhani Kailima ameliambia Mwananchi jana kuwa ili Buswelu aweze kuchukuliwa hatua, wenye jukumu la kumshtaki ni vyama vinavyopinga jambo alilolifanya.

Alisema vyama hivyo vinatakiwa kumshtaki katika kamati ya maadili inayoundwa na wajumbe wa vyama vinavyoshiriki uchaguzi katika jimbo husika na kwamba jambo hilo linapaswa kufanyika ndani ya saa 72, tangu apande jukwaani.

Wakati DC huyo akiibua kizazaa hicho, CCM imeendelea kumnadi Dk Mollel huku katika Jimbo la Kinondoni, wagombea ubunge wa CCM, Chadema na Sau wakiwekewa pingamizi.

Uchaguzi wa Siha na Kinondoni utafanyika Februari 17 na unavishirikisha vyama 12, huku ukitajwa kuwa ni mpambano mkali baina ya CCM na Chadema inayoungwa mkono na vyama vitano vya Ukawa ambavyo ni NLD, NCCR-Mageuzi, CUF upande wa Maalim Seif Sharif Hamad na Chaumma iliyojiunga hivi karibuni.

Uchaguzi huo unafanyika baada ya waliokuwa wabunge; Mollel (Siha- Chadema) na Maulid Mtulia (Kinondoni-CUF) kujivua uanachama wa vyama hivyo kwa maelezo kuwa wanamuunga mkono Rais John Magufuli na baadaye kujiunga CCM.

Chama hicho tawala kimewapitisha wawili hao kutetea majimbo hayo, huku Chadema ikimsimamisha naibu katibu mkuu (Zanzibar), Salum Mwalimu (Kinondoni) na Elvis Mosi (Siha).

Buswelu ‘alivyochafua hewa’

Juzi katika uzinduzi wa kampeni za Dk Mollel katika viwanja vya KKKT Karansi Jimbo la Siha, Buswelu alisema Serikali haijaribiwi hivyo ni vyema kila mmoja akahakikisha anadumisha amani na kufanya siasa za kistaarabu katika kipindi chote cha kampeni.

Alisema Dk Mollel ameleta heshima kwa wananchi wa Siha huku akiwataka wananchi wote kumuunga mkono na kuhakikisha anapata ushindi wa kishindo.

NEC ilivyomruka Buswelu

Akizungumza na Mwananchi, Kailima alikiri kitendo alichokifanya mkuu huyo wa wilaya kuwa hakikubaliki na kwamba ni kinyume cha kanuni za maadili, lakini haiwezi kumchukulia hatua.

“Wakuu wa mikoa na wilaya hawaruhusiwi kwenda katika kampeni na akifanya hivyo anakuwa amekiuka maadili ya uchaguzi,” alisema na kuongeza,

“Na kama amekiuka vyama vinavyoshiriki uchaguzi vinapaswa kuwasilisha malalamiko katika Kamati ya Maadili ndani ya saa 72.”

Alisisitiza, “Jambo hili tume hatuingii popote na vyama hivyo vya siasa vinalijua hili. Wanatakiwa kumpeleka kamati ya maadili ambayo wajumbe wake wanatoka katika vyama vinavyoshiriki uchaguzi, lakini iwe ndani ya saa 72 tangu kitendo hicho kilipotokea na wao watachukua hatua.”

Alivitaka vyama vya siasa kutokimbilia kulalamika bila kuchukua hatua kwani kama kuna uvunjifu wa maadili, kamati ina mamlaka ya kuwasilisha hilo katika ngazi nyingine ya kisheria kama polisi au kwa DPP (mkurugenzi wa mashtaka).

Kailima alibainisha kuwa NEC katika barua zao hawakuwazuia wakuu wa wilaya na mikoa kushiriki kampeni, bali waliwakumbusha kutojihusisha na kampeni kwani ni kinyume cha kanuni za maadili.

Vyama vyacharuka

Mkurugenzi wa itikadi, mawasiliano na mambo ya nje wa Chadema, John Mrema alisema, “Kama kweli NEC inasema iliwaandikia barua basi ituonyeshe hizo barua, lakini ichukue hatua kwa mkuu huyo wa wilaya ambaye amekiuka agizo hilo walilolitoa.”

Alisema waliposusia kushiriki uchaguzi wa Januari 13, moja ya sababu ni watendaji wa Serikali kuingilia chaguzi na endapo NEC haitachukua hatua wataeleza watakachokifanya kukomesha tabia hiyo.

“Sheria ya utumishi wa umma inazuia watumishi wa umma kujihusisha na siasa, huyu DC kavunja hiyo sheria na kama kuna usawa katika hili basi mamlaka zimchukulie hatua, anatumia nyenzo za Serikali katika mambo ya siasa, NEC ichukue hatua,” alisisitiza.

Mkurugenzi wa Habari wa CUF upande wa Profesa Ibrahim Lipumba, Abdul Kambaya alisema tatizo la wakuu wa mikoa na wilaya ni kubwa.

Alisema viongozi hao wamekuwa wakichangia uchaguzi kutokuwa huru na haki na kwamba jambo hilo linachangiwa na NEC kutokuwa na nguvu ya kuwashughulikia watendaji wa Serikali.

“NEC ina changamoto ya kusimamia uchaguzi na ina watendaji wachache ukilinganisha na wakurugenzi wanaosimamia uchaguzi na kutangaza matokeo. Kama akihakikishiwa ulinzi anamtangaza asiye mshindi na hii ni changamoto kubwa sana kwa tume yetu,” alisema Kambaya.

Kampeni Siha

Jana, katika kampeni za uchaguzi Siha zilizofanyika viwanja vya Ngarenairobi, katibu wa itikadi na uenezi wa CCM, Humphrey Polepole alimpigia debe Dk Mollel akitaka wananchi wamchague ili akashirikiane kwa karibu na Serikali kutatua changamoto mbalimbali zinazowakabili.

Alizitaja baadhi ya changamoto hizo kuwa ni migogoro ya ardhi, miundombinu mibovu ya barabara, ukosefu wa kituo cha afya na ukosefu wa ajira.

“Mkitupa Dk Mollel, lazima turudi hapa kushughulikia tatizo la ardhi ambalo limewafanya kuishi kwa msongamano wakati mmezungukwa na maheka ya ardhi,” alisema Polepole na kuongeza,

“CCM hatubebi mizigo ya misumari, tunapokea watu ambao ni vichwa na wanaweza kushirikiana na Serikali kuwaletea wananchi maendeleo.”

Kwa upande wake, Dk Mollel aliwaambia wananchi wa Ngarenairobi kuwa anatambua mchango wao wa mwaka 2015, hivyo wamrudishe ulingoni ili akatatue changamoto zinazowakabili ambazo alishindwa kuzitatua akiwa upinzani.

Kinondoni pingamizi kibao

Katika Jimbo la Kinodnoni, wagombea watatu wa Chadema, CCM na Sau waliwekeana pingamizi.

Msimamizi msaidizi wa jimbo hilo, Latifa Almas aliwataja wagombea hao kuwa ni Mtulia, Mwalimu na Johnson Mwangosi (Sau).

Almas alisema pingamizi la kwanza ni lile la Mwalimu alilomuwekea Mtulia, la pili ni la Mtulia kumwekea Mwangosi na la mwisho ni la mgombea wa CUF, Rajab Salum Juma kumuwekea Mwalimu.

Almasi alisema wagombea hao wote wameshapewa taarifa za pingamizi hizo, tayari wameshachukua fomu za kutakiwa kujieleza wanazotakiwa kuzijaza na kuzirejesha haraka iwezekanavyo.

Alisema iwapo waliowasilisha mapingamizi hao hawataridhika, wanaweza kukata rufaa NEC.

Wakili wa Mwalimu, Fredirick Kihwelo alisema pingamizi dhidi ya mgombea wa CCM ni kutofanya mrejesho wa gharama za Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2015.

Alisema nyingine ni Mtulia kushindwa kukidhi matakwa ya kisheria kwa kutojaza kwa usahihi fomu zake, kwa madai kuwa zimepigwa muhuri wa katibu wa CCM badala ya muhuri wa chama hicho tawala.

Alisema hoja ya mwisho ni Mtulia kujaza fomu akieleza kuwa anajishughulisha na kilimo cha mbogamboga, jambo ambalo Kihwelo amesema si kweli.

Hata hivyo, Mtulia alizijibu hoja hizo akisema ”Hili jambo jepesi sana na nimeandika ninachokijua na hakuna pingamizi hapo.”

Katika pingamizi la Mwalimu dhidi ya mgombea wa Sau, amesema Mwangosi amekosea kujaza fomu kwa maelezo kuwa jina lake linasomeka Mwangosi Johnson Joel badala Joel Johnson Mwangosi kama alivyoandika katika fomu ya kiapo.

Diamond Azidi Kupeperusha Bendera Akutana na Wasanii wa Rwanda

0
0
Diamond Akutana na Wasanii wa Rwanda
Kutokea Bongoflevani Diamond Platnumz mwishoni mwa weekend hii alikuwa nchini Rwanda ambapo alienda kwenye mambo yake binafsi ikiwa ni pamoja na kutangaza bidhaa zake za Diamond Karanga na Chibu Perfume kisha kupata nafasi ya kukutana na wasanii wa nchi hiyo..

Diamond amepost picha kwenye ukurasa wake wa instagram akiwa na wasanii wa Rwanda wakipata Dinner na kushare experience kuhusu muziki…>>>”Last night during my Dinner with my Fellow Artists from #Rwanda! It was a great evening, sharing experiences and ideas….Time to put our East African / African industry on the global map! Let’s do it, fam….✊” – Diamond Platnumz


Alichokisema Haji Manara Baada ya Kusikia Juma Nyoso Kampiga Shabiki

0
0
Alichokisema Haji Manara Baada ya Kusikia Juma Nyoso Kampiga Shabiki
Jumatatu ya January 22 2018 beki wa Kagera Sugar Juma Nyosso amejikuta akiingia matatizoni baada ya kujikuta akikamatwa na Polisi kwa madai ya kumpiga shabiki na kuzimia baada ya mchezo wao dhidi ya Simba uliyomalizika kwa Simba kupata ushindi wa magoli 2-0.

Afisa habari wa Simba Haji Manara ni miongoni mwa watanzania waliojitokeza kuangalia mchezo huo na baada ya kusikia Nyosso kampiga shabiki akaandika hivikupiti instagram account yake.


Wanawake Kuandamana Kuhusu Madai ya Ubakaji Katika Hospitali Kenya

0
0
Wanawake Kuandamana Kuhusu Madai ya Ubakaji Katika Hospitali Kenya
Kundi la wanawake nchini Kenya limeandaa maanadamano hii leo ya kuishinikiza serikali kuchukua hatua kuhusiana na madai kuwa akina mama waliojifungua wamekuwa wakidhulumiwa kingono katika Hospitali kuu ya Taifa, Kenyatta National Hospital.

Maandamano hayo yanatarajiwa kufanyika wakati ambapo pia usomwaji wa ripoti ya uchunguzi uliyoagizwa na waziri wa afya nchini humo utakuwa ukifanyika.

Waziri wa afya nchini Kenya Dkt Cleopha Mailu aliagiza uchunguzi kufanywa katika hospitali ya kitaifa ya Kenyatta baada ya wanawake waliojifungua kudai kwamba wanadhalilishwa kingono.

Taarifa zilizoenezwa kwenye mitandao siku ya Ijumaa zinadai kina mama waliojifungua wamekuwa wanashambuliwa na baadhi ya wafanyikazi wakati wakienda kwenye chumba cha watoto wachanga kuwanyonyesha watoto wao.

Wanawake 100 hujifungua kila siku hospitali ya Kenyatta
Wanaotuhumiwa ni wahudumu katika vyumba vya maiti, wanaonyooshewa kidole pia kwa kutumia maiti kuwashutua akina mama waliojifungua katika hospitali hiyo.

Kundi hilo la wanawake linaloandamana leo katika mji mkuu, linasema dhamira yao kuu kumiminika barabarani ni kutaka mabadiliko yafanyike, na kwamba usalama wa wanawake ni jambo linalopaswa kutiliwa umuhimu.

Hospitali ya taifa ya Kenyatta, Nairobi huwahudumia kina mama takriban 100 wanaojifungua kila siku.

'Limekuwa likiendelea kwa muda usiojulikana, na ni lazima liishe'.
Mildred Atty, Moja ya waandalizi wa maandamano
Watoto waliozaliwa huwekwa chumbani ghorofa ya kwanza nao wanawake kwenye wodi za kujifungulia kwenye ghorofa ya chini.

Maswali sasa yameanza kuulizwa kuhusu muundo na mpangilio wa vyumba katika hospitali hiyo ambao huwalazimu kina mama waliojifungua kupanda ngazi au lifti kwenda kuwanyonyesha watoto wao, ikizingatiwa kwamba baadhi hujifungua kupitia upasuaji.

Mashahidi Wanne Wammaliza Scorpion Hadi Kuhukumiwa Miaka Saba Jela

0
0
Mashahidi Wanne Wammaliza Scorpion Hadi Kuhukumiwa Miaka Saba Jela
Hakimu Mkazi wa Mahakama ya Ilala, Flora Haule amemuhukumu Salum Njwete, maarufu kwa jina la Scopion, kwenda jela kwa miaka saba na kulipa haraka fidia ya Sh30 milioni baada ya kuridhika na maelezo ya mashahidi wanne uliodhihirisha kuwa mshtakiwa alimjeruhi Said Mrisho kwa kumtoboa macho yote.

Hata hivyo, Hakimu Haule amesema ushahidi wa upande wa mashtaka umeshindwa kuthibitisha kuwa mshtakiwa alifanya kosa la unyang’anyi kwa kutumia silaha.

Lakini Mrisho amesema hajaridhika na hukumu hiyo, akisema haiendani na kosa alilotenda mshtakiwa kwa kuwa amemuacha akiwa kipofu na tegemezi.

“Sijajua utaratibu wa kulipwa hizo hela. Kwanza Sh30 millioni ni hela ndogo sana,” alisema Mrisho baada ya hukumu hiyo.

“Nitaomba kuonana na Rais (John Magufuli) kwa kuwa sina uwezo wa kufanya shughuli yoyote. Hata watoto wangu nimewahamisha shule kutokana na kukosa ada.”

Kutokana na tukio hilo kuripotiwa na vyombo vya habari, Mrisho alipata misaada kutoka kwa watu walioguswa, ikiwa ni pamoja na pikipiki za magurudumu matatu kwa ajili ya kufanyia biashara.

Scorpion anadaiwa kutenda kosa hilo Septemba 6, 2016 saa 4:00 usiku, maeneo ya Buguruni. Anadaiwa kumchoma Mrisho sehemu mbalimbali za mwili ikiwamo machoni, tumboni na mabegani akitumia kitu chenye ncha kali.

Pia anatuhumiwa kuiba vitu vyenye thamani ya zaidi ya Sh300,000.

Ushahidi uliomtia hatiani

Hakimu Haule alisema ushahidi uliotolewa na shahidi wa saba na wa nane katika kesi hiyo, umeonyesha kuwa Njwete alikuwa mlinzi katika eneo la wafanyabiashara wa Buguruni na alikuwa na jukumu la kuhakikisha vibaka wanapungua eneo hilo.

Haule alisema shahidi wa kwanza ambaye ni Mrisho ameonyesha jeraha la macho alilolipata.

Pia, alisema wakati tukio hilo linatokea, jina la Njwete lilikuwa likitajwa na baadhi ya wafanyabiashara, jambo linalofanya ushahidi huo kutotia shaka.

Alisema matokeo ya uchunguzi uliofanywa na shahidi wa nne na wa tano ambao wote ni madaktari kutoka Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH) umethibitisha kuwa Mrisho alichomwa na kitu chenye ncha kali machoni na kusababisha asiweze kuona tena.

Lakini hakukubaliana na hoja ya uporaji wa kutumia silaha.

“Nimepitia hoja zote za upande wa mashtaka wameshindwa kuthibitisha kosa la unyang’anyi wa kutumia silaha. Mahakama imeona nia ya mtuhumiwa ilikuwa kupambana na vibaka,” alisema Haule.

Baada ya Hakimu Haule kutoa maelezo hayo, wakili wa Serikali, Frank Tawali aliomba mahakama itoe adhabu stahiki kwa kuwa Mrisho amekuwa tegemezi, pia Taifa limepoteza nguvu kazi kwa kuwa amekuwa kipofu.

Lakini wakili wa utetezi, Hussein Hitu aliiomba mahakama kumpunguzia mteja wake adhabu kwa sababu ameshakaa ndani kwa muda mrefu na ana familia inayomtegemea.

Haule alitoa hukumu hiyo kutumikia kifungo cha miaka saba jela na kulipa fidia ya Sh30 milioni itakayotakiwa kulipwa haraka.

Awali, Oktoba 19, 2017 Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP) aliomba kutoendelea na kesi hiyo kutokana na mapungufu kwenye mashtaka, lakini akafungua upya kesi hiyo baada ya kurekebisha mashtaka ya awali.

Kesi hiyo ilirudi mahakamani Novemba 30, 2017 wakati mshtakiwa aliposomewa mashtaka upya.

“Miaka 14 si Mchezo, Mambo Kama Haya Niliyamiss”-Papii Kocha

0
0
“Miaka 14 si Mchezo, Mambo Kama Haya Niliyamiss”-Papii Kocha
 Muimbaji wa muziki wa Dance hapa Bongo, Nguza Viking maarufu kama Babu Seya na mwanae, Papii Kocha good news ni kwamba wameanza maandalizi ya ujio wao mpya, ikiwa ni takriban miaka 14 tangu waachie kibao kipya.

Babu Seya na Papii Kocha walipewa msamaha na President JPM  kwenye maadhimisho ya miaka 56 ya Uhuru. Serikali imeonesha nia ya kuwasaidia waimbaji hao kurejea tena kwenye muziki.

Naibu Waziri wa Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo, Juliana Shonza aliwakutanisha na uongozi wa Wanene Studios waliokubali kuchukua jukumu la kuwarudisha tena kwenye muziki. Tayari wameanza kuingia studio kuandaa kazi mpya katika studio hizo kubwa katika ukanda wa Afrika Mashariki.

Babu Seya na Papii Kocha wamefanya photoshoot kitu ambacho Papii amekiri kuwa ni kigeni mno kwao kutokana na kuwa gerezani kwa miaka 14 na wametoka katika nyakati ambazo muziki wa Tanzania umepiga hatua kubwa ukilinganisha na zamani.

“Miaka 14 si mchezo, mambo kama haya, niliyamiss, nimemiss vitu vingi, picha za ukweli, mambo haya kule tulipotoka hamna. lazima uelewe hii ni dunia nyingine,” -Papii Kocha

Papii pia amesema kuwa kazi zao mpya zitakuwa kali zaidi ya zile za zamani. “Kwasababu tumejipanga vizuri na kazi zinazokuja zitakuwa nzuri zaidi ya zile tulizofanya mwanzo,” – Papii Kocha

Kiwanja Cha Kujenga Nyumba Kinauzwa Eneo la Mapinga Karibu na Bunju B

0
0
Kiwanja cha Kujenga Nyumba Kinauzwa , Kina Size ya 20 Kwa 20 Mita, Kipo Eneo la Mapinga Karibu na Bunju B, Kipo Karibu na Barabara ya Lami
Shilingi Mil 8. Maongezi yapo Kidogo

Piga simu 0714604974 Kwa Mawasiliano zaidi


Pata Dawa Bora ya Nguvu za Kiume na Maumbile Madogo ya Kiume ( Super Shafti)

0
0
DAWA BORA YA NGUVU ZA KIUME NA MAUMBILE MADOGO YA KIUME ( SUPER SHAFITI) NI DAWA YENYE UWEZO MKUBWA WAKUTIBU UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME


 (SUPER SHAFITI ni dawa ya asili yenye uwezo mkubwa wa kuogeza nguvu za kiume maradufu
(1) itakufanya uwe na nguvu za ajabu ukiwa unafanya ntedo la ndoa
(2) inaogeza hamu ya kurudia ntedo la ndoa zaidi ya mara tatu bila kuchoka
( 3) itakufanya uchelewe kufika kileleni dani ya dk 30
( 4)  itaimalisha milija ya uume iliyo legea au kusinyaa
(5) lnarefusha na kunenepesha uume saizi utakavyo kuazia ichi 1-8 unene sm 2-4
 (6) itakupa nguvu za kusimamiasha uume wako barabara kama_ msumari wakati wa ntedo la ndoa
(7) inasaidia kusafisha mishipa. ya kwenye uume na hivyo kusaidia Katika kuongeza kasi ya msukumo wa damu kwenye mishipa ya uume
(8) usaidia kuurudisha nje uume ulioingia ndani
(9) inasaidia kuogeza manii nyingi ambazo vina viini vya uzazi
(10)usaidia kutibu madhara ya punyeto ,matumizi makali ya  madawa ya kizugu mirungi bangi na sigara

KWA NINI BAADHI YA WANAUME WENGI WANA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME NA KUWA NA MAUMBILE MADOGO YA KIUME NINI CHANZO CHAKE? 

ni kutokana na magonjwa megi kuongezeka yakiwemo kisukari presha ya kupanda na kushuka upigaji wa punyeto wa mda mrefu magonjwa ya moyo ngiri ya kuviba korondani vidonda vya tumbo
Msongo wa mawazo  tumbo kuuguruma kujaa ngesi kutopata choo vinzuri maumivu ya mgongo kiuno na tumiaji wa madawa makali ya kizungu ya kuongeza nguvu za kiume kuzaliwa na chango linaloshabulia neva za ukuwaji wa uume utumiaji wa mirungi bangi sigara na nk  tunapenda kuwatangazia wasomaji, wa makala zetu kuwa tunazo dawa nzuri za asili ambazo hazina mazala na zinazotibu na kuponyesha matatizo ya upungufu wa nguvu za kiume na maumbile ya kiume

NA TUNATIBU MAGONJWA YOTE SUGU KAMA KISUKARI PRESHA AINA YOTE UGONJWA WA MOYO SITRUKO KWIKWI KICHOMI MINGUU KUFA NGAZI ASIMA NK MZEE ISAYA ANAPATIKANA MAGOMENI MIKUMI KARIBU NA KANISA  TUMAINI HEBRAST CLINI NDIYO JIBU NA SULULISHO YA MATATIZO YOTE

PIGA simu 0745495181 au 0682644040

Kwa watu wa mikoa huduma utatumiwa na watu wa nje ya nchi utazipata dsm kama huna nafasi ya kufika ofisini kwetu utaletewa popote ulipo

Fahamu Vitu Ambavyo ‘Sex Dolls’ Wanaweza Kuvifanya

0
0
Midoli ya ngono yaani ‘sex dolls’ bado ni mada kwenye mitandao ya kijamii na imesababisha watu kutoa maoni mbalimbali. Baadhi ya wanaume wametoa maoni yao kwamba midoli hiyo ni bora kuliko wanawake huku baadhi ya wanawake wanasema kwamba midoli hiyo haitodumu kwa mdaa mrefu.

Vitu anavyoweza kuvifanya ni kama;

1. Anatumia betri ambazo zinaweza kuchajiwa kama vile simu za mkononi na laptops.

2. Ameundwa ili kukidhi matakwa ya kimapenzi kama vile mwanadamu anavyofanya.

3. Anaweza kufanya mambo mengi wakati wa kujamiiana, kama vile kuzungumza lugha ya kimapenzi, kutajaa jina lako, kukaa mkao wowote uupendao.

4. Ni mpenzi mzuri na anaweza kukushirikisha kwenye majadiliano kama vile mwanadamu anavyofanya.

5. Anauwezo wa kutuunza vizuri mwili wake.

6. Mdomo wake pia ni kama wa binadamu.

7. Ngozi yake ni laini sana na yenye hisia kama ngozi halisi ya binadamu na kampuni ya ROBOTIX ina mpango wa kuwafanya midoi hao kuwa na unyevu kama ule wa binadamu halisi wakati wa ngono.

8. Unaweza kumfanya aongee lugha yoyote uipendayo

Midoli hiyo ya ngono inapatitakana kwa kiasi cha Dola 2500 na wanaweza kuwekewa shepu, sura na hata rangi ya ngozi unayoipendelea. Kampuni hiyo ya ROBOTIX inauza zaidi ya midoli 600 kila mwaka Marekani pekee.
Bongo5

Mwenye Uume Mdogo Usiwe na Shaka Fuata Ushauri Huu Utakusaidia Kumridhisha Mpenzi

0
0
Je, ni urefu au unene?
Je, urefu wa uume ni suala muhimu kwa mwanamke kuridhika kimapenzi?Hii ni imani potofu ambayo imewafanya wanaume wengi kujiingiza kufanya surgery za gharama kubwa na wengine kupoteza pesa zao kwa ajili ya kutafuta dawa za kienyeji ili kuongeza maumbile kuwa marefu zaidi.

Huko ni kupoteza muda na pesa.
Ingawa urefu wa uume hauna umuhimu kama imani potofu inavyodai bado suala la msingi ni uimara wa misuli ya uume; kwani misuli ya uume ikiwa imara basi mwanaume huwa na uwezo (strength/flexibility) ambayo itaweza kumpa sifa mume kwa mke wake kuliko kushabikia kuwa na jumbo size.


Hii ina maana bila kujali una urefu kiasi gani au ufupi kiasi gani, kama una misuli imara hilo ndilo jambo la msingi kwa mwanaume.


Tuweke suala la hiyo imani potofu pembeni hivi ni kitu gani mwanamke huhitaji physically ili afurahie tendo la ndoa?Suala la muhimu ni kuwa na ufahamu wa anatomy kuhusu mwanamke (uke); ukweli ni kwamba nervesnyingi zipo within inches mbili kutoka mlango wa uke (vaginal opening) na asilimia kubwa ya nerves zipo katika mzunguko wa mlango wa uke.

Hii ina maana mwanaume yeyote mwenye uume wa inches mbili kama anajua namna ya kumfikisha mke kuridhika au kufika kileleni kupitia uke (vaginal climax) basi ataweza kumfikisha mke wake kileleni.

Je, ni unene (thickness) wa uume huweza kumridhisha mwanamke kimapenzi?Ni kweli unene inaweza kuwa ni factor hasa kutokana na uwezo wa mwanamke alionao kukaza misuli ya uke.

Je mwanamke ana umri gani, amekuwa na partners kiasi gani na amezaa watoto wangapi na zaidi amefanya kitu gani kuhakikisha misuli yake (uke) inakuwa imara.

Mfano:Ingawa suala la thickness si tatizo kwa wanawake wa nchi za Asia kama Japan, Singapore au Philippines kwa kuwa suala la kukaza misuli kwa wanawake ni moja ya sanaa.

Wanawake wa huko hucheza michezo ya kuingiza ping pong-ball (mipira mfano wa tennis) sita kwenye uke na kuzirusha futi 15 ili kuingia kwenye ndoo huku kila kimpira kinapotoka kinaendana na popping sound bila kukosa hata kimoja.

Pia huweza kuingia ndizi iliyomenywa kwenye uke huanza kuzikata ndizo (slice) vipande vipande huku vikidondoka.

Fikiria sasa likija suala la mapenzi hii inaonesha kwamba hao wanawake wanajua jinsi ya kuridhishana na kwao size does not matter.

Bahati mbaya ni kwamba tamaduni nyingi za Africa, ulaya na Amerika hazina mazoea ya kuwa na mazoezi ya kukaza misuli ya uke au uume.

Hivyo thickness ni muhimu kwa mwanamke ambaye uke wake ni loose na weak pia kama misuli yake hoi.

NB:
Hapa sina maana mwanamke ajihusishe na mchezo huu, it is illegal; najaribu kuelezea uwezo wa misuli ya uke ukifanyiwa mazoezi vitu inaweza kufanya.

Je, inakuwaje kama mwanaume ana uume mkubwa (unene na urefu) zaidi ya wastani ambao wanaume wengi huwa?Tafiti nyingi zinaonesha wanawake wengi hulalamika pale mwanaume anapokuwa na uume mkubwa zaidi ya kawaida na hasa kama hajui namna ya kuutumia.

Wanawake wengi huona ni huge barrier kwa ajili ya ku-enjoy sex kama mke na mume na wakati mwingine mwanamke hujisikia uncomfortable na huishia kukwepa.

Pia wanaume wenyewe ambao wana uume mkubwa tafiti zinaonesha kwamba wengi hujikuta katika huzuni na wanaombolezo kwa sababu partners wao kujisikia maumivu na kuumia na hata imesababisha mahusiano ya kimapenzi kati ya mke na mume kuzolota.

Je, hutokea nini pale mwanaume mwenye jumbo size akakutana na mwanamke mwenye uke uliobana?

Na wanaume ambao ukubwa wa uume (thickness ni zaidi ya kawaida wanapokutana na mwanamke ambaye ana size ndogo ya uke, au hakuwa wet sawasawa au hajazaa mtoto kabisa au bikira suala la sex linakuwa shughuli nzito kuihimili kwani lazima mwanamke akubaliane na pressure na pain za kuta za uke zinapochanwa.

Na pia kama mwanaume ana urefu unaozidi inches 6 ambayo ni average size kwa wanaume basi mwanamke anaweza kujikuta anajuta kwani anaweza kuhisi mwanaume anagonga hadi kwenye kizazi (internal reproductive organs).

Na matokeo yake mwanamke hujikuta anakaribisha magonjwa kama cysts ambayo huhitaji surgery na pia huweza kupata infections ambazo huweza kusababisha kukosa watoto.
Nini kifanyike?Jambo la msingi ni kwa mwanaume kufahamu namna ya kutumia tool yake vizuri, hii ni pamoja na kuwa caring, kufanya maandalizi ya kutosha.

Je, nini faida ya kuwa na uume mkubwa au uume mdogo?Kama mwanamke ana uke ambao ni loose na hawezi kuthibiti mwendo (misuli imelegea) basi tool kubwa kama hiyo huweza kumsaidia kupata feelings za kufurahia mapenzi hapa haijalishi mwanaume ana skills zozote au la.

Na mwanaume ambaye ana uume mdogo kuliko kawaida anaweza kuwa na faida kwa mwanamke ambaye ana uke mdogo (tight).

Hii ina maana mwanaume mwenye uume mkubwa ana match na mwanamke mwenye uke loose na hii combination huwezesha hao wawili kuwa na ridhiko kimapenzi.

Na mwanaume mwenye umbile dogo ana match na mwanamke mwenye uke tight.

Breaking News: Rais Magufuli Amtumbua Mkurugenzi Butiama

0
0
Breaking News: Rais Magufuli Amtumbua Mkurugenzi Butiama
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli leo Januari 23, 2018 ametengua uteuzi wa Mkurugenzi wa halmashauri ya Butiama mkoani Mara Solomoni Ngiliule kuanzia leo kutokana na ubadhirifu wa fedha za Umma.


Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais TAMISEMI, Selemani Jafo ametangaza maamuzi hayo leo zikiwa zimepita siku tatu toka Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa alipotoa maagizo kwa Kaimu Katibu Tawala wa Mkoa wa Mara Bw. Raphael Nyanda kutuma timu ya wakaguzi kwenda kufanya ukaguzi maalumu katika ofisi ya Mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya ya Butiama.

Waziri Mkuu aliagiza kiongozi huyo kuchunguzwa kutokana na matumizi yasiyoeleweka ya fedha za miradi ya maendeleo zinazotolewa na Serikali zikiwemo sh. milioni 12 walizotumia kuandaa profile ya Halmashauri hiyo huku fedha zingine ni pamoja na sh. milioni 70 za elimu maalumu, sh. milioni 288 za mradi wa maji Butiama ambazo zote hazikujulikani zimetumikaje.

Hatimaye Halima Mdee, Bulaya Wamaliza Kifungo Bungeni

0
0
Hatimaye Halima Mdee, Bulaya Wamaliza Kifungo Bungeni
 Kifungo walichokuwa wakitumikia wabunge wa Chadema, Ester Bulaya (Bunda Mjini) na Halima Mdee (Kawe) cha kutokuhudhuria shughuli za Bunge kimemalizika na wamesema wamerejea na kasi ileile.

Wabunge hao waliadhibiwa kwa azimio la Bunge Juni 5 mwaka jana kutohudhuria mikutano mitatu ya Bunge ambayo ni jumla ya siku 47, waliyokosa ukiondoa shughuli zote za mikutano ya kamati za Bunge.

Adhabu hiyo ilikwenda sanjari na kulipwa nusu mshahara na posho kwa kipindi chote walichotumikia adhabu hiyo wakituhumiwa kudharau kiti cha spika.

Mikutano mitatu waliyoikosa ni wa bajeti uliokuwa ukiendelea, wa saba uliofanyika kati ya Septemba 5 hadi 15 na mkutano wa tisa wa Novemba 7 hadi 17.

Makato ya mshahara na posho yamebainishwa katika Kanuni 75 ya Bunge inayosema: “Mbunge aliyesimamishwa kazi atatoka katika Bunge na hataingia tena katika sehemu yoyote ya ukumbi wa Bunge na maeneo ya Bunge kwa muda wote atakapokuwa amesimamishwa na atalipwa nusu mshahara na nusu posho zinazoambatana na mshahara huo.”

Jana, kwa nyakati tofauti Bulaya na Mdee walizungumza na gazeti hili juu ya kurejea kwao, huku wakisema hawajutii kwa adhabu hiyo na hawatorudi nyuma au kutetereka katika kusimamia wanachokiamini.

“Nitaendelea kuwa Mdee yuleyule wa siku zote, kama walidhani wakinifungia mwaka nitabadilika. Hapana! Sitaraji kubadilika. Nimetumwa na wananchi wangu kusema ukweli na nitausema, sijaja kumpigia magoti mtu,” alisema.

Mdee ambaye pia ni mwenyekiti wa Baraza la Wanawake wa Chadema (Bawacha), alisema wakati akitumikia adhabu hiyo amepata fursa ya kufanya shughuli kwa karibu za jimboni kwake na zile za Bawacha.

Naye Bulaya alisema: “Nimerudi bungeni tayari na leo (jana) nilihudhuria kamati yangu ya uwekezaji na mitaji.”

Alipoulizwa amejifunza nini kutokana na adhabu hiyo, alisema: “Bulaya wa kukosoa, Bulaya anayesimamia kile anachokiamini pasi na kuvunja sheria na taratibu hajabadilika, nitaendelea kuwakosoa.”

“Hata nilipokuwa natoka CCM kuja Chadema nilijua mambo kama haya ya kukamatana, kufungiana yatakuwapo kwa hiyo nilijipanga na wala hawanitetereshi, nimerudi na sitarudi nyuma,” aliongeza.

Nakwenda Kulia na Kuwa Mwendawazimu- Salumu Mwalimu

0
0
Nakwenda Kulia na Kuwa Mwendawazimu- Salumu Mwalimu
Mgombea Ubunge wa Jimbo la Kinondoni ambaye pia ni Naibu Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Zanzibar Salum Mwalimu amefunguka na kudai yupo tayari kuwa mwendawazimu kwa kuwapigania wananchi wa jimbo hilo akiwa Bungeni.

Salum Mwalim ameeleza hayo ikiwa imepita siku moja tokea Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) kuruhusu kuanza kwa kampeni rasmi za uchaguzi mdogo katika majimbo mawili ambayo ni Kinondoni na Siha.

"Nakwenda Bungeni kulia na kuwa mwendawazimu kwa ajili mahitaji ya watu wa Kinondoni, hakuna wa kunikataza kuongea jambo lolote ambalo litakuwa lina tija kwa watu wangu. Nitahakikisha narudisha heshima ya kinondoni", alisema Salum Mwalim.

Uchaguzi wa Jimbo la Kinondoni unatarajiwa kufanyika mwezi ujao (Februari 17, 2018) ili kuweza kuziba nafasi iliyoachwa wazi na aliyekuwa Mbunge wa Jimbo hilo kwa tiketi ya chama cha wananchi (CUF), Maulid Mtulia aliyejiuzulu kiti na uanachama kwa chama hicho na nafasi zote za uongozi alizokuwa nazo hapo awali.


Ray Vanny Ampeleka Mama Watoto Wake Nyumbani Kwao Mbeya

0
0
Ray Vanny Ampeleka  Mama Watoto Wake Nyumbani Kwao Mbeya
Muiambaji wa WCB, Ray Vanny ambaye ni mzaliwa mkoani Mbeya, weekend hii alionekana akiwa na mama watoto wake nyumbani kwao Mbeya.

Wawili hao wakiwa mkoani humo waliweza kuhudhuria ibada katika kanisa moja ambalo halikutambulika mara moja. Pia waliambata na mtoto wao mdogo aitwaye, Jaydan.

Couple hiyo ni moja kati ya Couple ambazo zinawavutia watu wengi zaidi nchini kwasasa kutokana na kuishi maisha yao bila kuwa na skendo kama za mastaa wengine. Angalia picha zao wakiwa Mbeya.

Peter Msikwa Ashikiliwa na Polisi

0
0
Peter Msikwa Ashikiliwa na Polisi
Mbunge wa Jimbo la Iringa Mjini, Mchungaji Peter Msigwa anashikiliwa na Jeshi la Polisi kwa mahojiano kutokana na matukio ya kiuharifu yanayotokea mjini Iringa.

Mbunge huyo anahojiwa kuhusu kuchomwa nyumba ya Katibu wa UVCCM na kuvunjwa Nyumba ya Diwani aliyehamia CCM akitokea CHADEMA.

Kamanda wa polisi mkoa wa Iringa (RPC) Julius Mjengi ameuthibitisha kushikiliwa kwa Mchungaji Peter Msigwa ambapo ameeleza anahojiwa kuhusu  matukio ya uvunjwaji wa nyumba ya aliyekuwa diwani wa kata ya Mwangata kupitia chadema aliyejiuzulu na kujiunga na CCM pamoja na tukio la kuchomwa moto kwa nyumba aliyokuwa akiishi katibu wa UVCCM Iringa mjini.

Meno ya Viboko 12,467 Kupiga Mnada Serikali

0
0
Meno ya Viboko  12,467 Kupiga Mnada Serikali
Wizara ya Maliasili na Utalii na Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania (Tawa) itafanya mnada wa hadhara wa meno ya viboko vipande 12,467 vyenye uzito wa kilo 3,580.29.

Mnada huo utakaosimamiwa na Wizara ya Fedha na Mipango umepangwa kufanyika Januari 29 kuanzia saa nne asubuhi katika Jengo la Mpingo, Barabara ya Nyerere jijini Dar es Salaam, zilipokuwa ofisi za Wizara ya Maliasili na Utalii (Ivory Room).

Taarifa iliyotolewa na Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Tawa, Dk James Wakibara amesema  mnada huo utawahusisha wafanyabiashara wa Nyara waliopewa leseni ya Nyara Daraja la Kwanza mwaka 2017.

Amesema wafanyabiashara hao wataruhusiwa kukagua meno hayo kati ya tarehe 25 na 26 Januari, 2018 kuanzia saa nne asubuhi hadi saa tisa na nusu jioni kabla ya siku ya mnada huo.

Amesema wanunuzi watakaoshinda mnada huo watatakiwa kulipa asilimia 25 ya malipo yote papo hapo na asilimia 75 itakayosalia itatakiwa kulipwa ndani ya siku kumi na nne zijazo baada ya mnada huo.

“Mtu yeyote atakayekuwa ametamka bei ya juu, kisha akashindwa kulipa asilimia 25 ya bei aliyotamka, atachukuliwa kuwa ni mwenye kutaka kuvuruga mnada na hivyo hatua kali za kisheria zitachukuliwa dhidi yake,” ameonya mkurugenzi huyo.

Amesema meno hayo yatauzwa kwa wastani wa uzito wa nusu kilo bila kugawanywa au kuchambuliwa wakati wa mnada na wanunuzi wataruhusiwa kuondoa bidhaa kwenye eneo la mnada baada ya kulipia ada na kodi husika kikamilifu na kupewa hati ya kumiliki nyara hizo.

Tanzia: Mwanamuziki Mkongwe Afrika Kusini Hugh Masekela Afariki Dunia Baada ya Kuugua Saratani ya Tezi Dume

0
0
Tanzia: Mwanamuziki Hugh Masekela Afariki Dunia Baada ya Kuugua Saratani ya Tezi Dume
Hugh Masekela, mwanamuziki maarufu wa mtindo wa jazz kutoka Afrika Kusini aliyechangia juhudi za kukabiliana na utawala wa ubaguzi wa rangi nchini humo, amefariki dunia akiwa na miaka 78.

Familia ya mwanamuziki huyo mcheza tarumbeta, kupitia taarifa, imesema Masekela amefariki akiwa mjini Johannesburg baada ya kuugua saratani ya tezi dume kwa muda mrefu.

Masekela alipata umaarufu mkubwa kutokana na mtindo wake wa kipekee wa Afro-Jazz na vibao vilivyokuwa maarufu kama vile Soweto Blues.

Wimbo huo alioutoa 1977 ulihusika sana katika harakati za kupambana na utawala wa ubaguzi wa rangi nchini humo.

Amekuwa akitambuliwa na wengi kama "baba wa Jazz nchini Afrika Kusini.
Alisaidia kutumbuiza wakati wa ufunguzi wa michuano ya Kombe la Dunia 2010 Afrika Kusini na mwanamuziki mwenzake Femi Kuti

Wafanyakazi Walipwa Mshahara wa Matofali Badala ya Pesa Taslimu

0
0
Wafanyakazi Walipwa Mshahara wa Matofali Badala ya Pesa Taslimu
Wafanyakazi katika kiwanda cha matofali kusini mashariki mwa China wanaokidai kiwanda hicho mishahara yao yenye thamani ya $14,050, wamelipwa matofali, inaripotiwa.

Kwa mujibu wa shirika la habari Xinhua, takriban wafanyakazi 30 wa kiwanda hicho huko Nanchang, katika jimbo la Jiangxi , walikubali kulipwa matofali 290,000 badala ya mshahara wanaodai.

Gazeti la Jiangxi Daily linaripoti kuwa wafanyakazi hao , wote wakiwa ni wahamiaji , wametoka katika eneo la milima la jimbo la Yunnan kuini magharibi, na hawakuwa na namna ili kuishi kwa "kutumia mishumaa na kuwasha kuni moto ili kupunguza baridi ".

China kujenga kiwanda cha vifaa vya mawasiliano Tanzania
Nyoka 'watoroka' katika shamba China
Baada ya chama chao cha wafanyakazi kuingilia kati na kwa usadizi wa mahakama, wafanyakazi hao walikubali kupokea matofali hayo kutoka wamiliki wa kiwanda badala ya mshahara wao ambao hawajalipwa.

Xinhua linasema kuwa waajiri wao, ambaye hakutajwa jina katika vyombo vya habari, bado anajaribu kutafakari namna ya kuwalipa, tofuati iliosalia ya Yuan 10,000 wanaodai wafanyakazi hao.



Kijiji ambacho wanaume wengi ni makapera China
Taarifa hii imezusha mjadala mkubwa katika mitandao ya kijamii China, huku wengi wakielezea wasiwasi wao kuhusu ni kwanini mara kwa mara wafanyakazi wa vijijini wahamiaji ndio hulipwa kidogo kidogo?

Wengine wametania wakisema hali imekuwa mbaya kiasi cha matofali kuonekana kuwana thamani sawana fedha.

Je wewe ungekubali kulipwa mshahara wako kwa bidhaa nyingine yoyote kando na pesa taslimu?

Kijana Mmoja Akamatwa na Polisi kwa Kosa la Kuiba Majeneza

0
0
Kijana Mmoja Akamatwa na Polisi kwa Kosa la Kuiba Majeneza
Kijana mmoja aliyetambulika kwa jina moja la Boniface mkazi wa Mwananyamala kwa Msisiri anashikiliwa na jeshi la Polisi Mkoa wa Kinondoni kwa kuiba masanduku ya kuzikia (majeneza) mawili na kuyaficha nyuma ya choo cha mkazi mwengine wa mtaa huo.


Akithibitisha kutokea kwa tukio hilo Kamanda wa Polisi mkoa wa Kinondoni Jumanne Muliro, amesema tukio hilo limetokea kati ya ofisi mbili za kuuza masanduku hayo ambapo moja ndiyo iliyoibiwa majeneza hayo, ambayo moja ni la mtu mzima na moja likiwa la mtoto mdogo

“Kuna work shop mbili ambazo zinajishusisha na kutengeneza masanduku, zipo kwenye sehemu moja, asubuhi mtu kaingia kwenye work shop yake akakuta masanduku mawili hayapo akaanza kufuatilia, baada ya muda akajua yapo kwenye workshop nyingine, kwa hiyo kilichofanyika ni ufuatiliaji na askari wakafanikiwa kuyapata, ni suala ambalo linachunguzwa kujua kama wanadaiana au ni wizi umefanyika, ndipo sheria ifuate”, amesema Kamanda Muliro.

Mmiliki wa masanduku hayo Bi. Judith Carlos amesema masanduku hayo aligundua yapo kwa jirani yake baada ya kumuahidi mtu atampa elfu 50 iwapo atamsaidia kujua nani kayachukua, na ndipo baadaye akaambiwa mahali yalipo.
Viewing all 104431 articles
Browse latest View live




Latest Images