Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104432 articles
Browse latest View live

Msaada Please, Mpenzi Wangu Ananing'ata Tukiwa Sita kwa Sita Mpaka Natoka Damu

0
0
Wakuu nifanyeje juu ya sweetie wangu huyu. I really love and Am dying for her ila hili tatizo nahisi ipo siku nitachoka
Tatizo ninapomdinya nashtukia ghafla kaning'ata,nimebadili style,nikapiga doggy kajipinda hadi kang'ata paja , yaaani huku shingoni nimejaa alama alama , wengine wanasemaga ni love bite ila hii yangu imezidi kipimo , sometimes mpaka damu zinanitoka na kuuguza kidonda..

Wakuu what should I do

Kina Kaka Acheni Ujinga, Hakuna Mwanamke Asiyetaka Kuhongwa! Shauri Lako

0
0
Wakaka acheni ujinga, ukitaka dem wa peke yako basi jua kugharamia. Nakwambia wanawake asilimia kubwa hukumbuka fadhila za mtu anayemgharamikia kuliko wanaume wa ai lavii yuu maneno.

Usidanganyike hakuna mwanamke asiyependa kuhongwa, kuna wanawake natural hawawezi kuomba,ila anakua anataka ujiongeze, sasa kama wewe ni wale ambao akikwambia "baby kifurushi kimekata" unajibu "basi mumy pls ukiweka nicheki" umekwishaaaa!!!

Anakueleza shida zake unasema "mpenz vumilia nakuombea upate kazi" kaka umeishaaa kabisaaaa aiseeee!!! Huna chako!!!
Ujue ulivyokata simu umefatiwa na bonge la msonyoooo ka sio tusi la nguoni basi la mwilini. Yani wewe kama ni wale wa baby mwezi huu mambo yangu hayako sawa, nakuapia unagongewa weeeeeeeeee . . . . mpaka ujute!!

Unamuona dem wako kasuka, kapendeza na hana kazi, we umekazana tu "beibi umependeza" . . . . . . Yaani wee boya ujue!! Mume mwenzio kaweka nguvu, so anapokua anatoa calendar za kukuona tulizana, service inakua kwa anayehudumia.
Hakuna dem wa siku hizi anayetaka kuambiwa nakupenda jumapili mpaka jumapili we mhonge tu uone heshima.
____________
Ujumbe wa Leo:
Old friends pass away, new friends appear. It is just like the days. An old day passes, a new day arrives. The important thing is to make it meaningful: a meaningful friend - or a meaningful day.

Upatikanaji wa Ngono Kirahisi Uwafanya Vijana Wengi Kuchelewa Kuoa hasa Mijini

0
0
Kuna sababu nyingi zimetolewa kwa vijana kushindwa Kuoa na Kuolewa, nyingi kati ya hizo ni za kiuchumi na kujifanya wanajipanga kimaisha.

Ukweli ni kwamba watu wengi hawaingii kwenye Ndoa kwa sababu wanapata kirahisi tendo lenyewe la Ndoa.

Msingi wa Ndoa sio tendo la Ndoa pekee, kunafaida nyingi katika Ndoa hilo liko wazi kabisa.
Lakini ukwel ni kwamba tendo hili la ndoa lina msukumo wa pekee na ushawishi mkubwa katika kuanzisha mahusiano ya ndoa.

Maeneo ambayo vija upenda kupunguzia mahitaji yao ya Ndoa ni kwenye Madanguro, Bar, Massage parlour, makaburini.

Ukweli kungekuwa na Tamaduni au Sheria kali zinazodhibiti matendo ya Ndoa holela ndoa zingekua nyingi.

Mchezo Mchafu Siha, Kinondoni...Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumatano ya January 24

0
0


Mchezo Mchafu Siha, Kinondoni...Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumatano ya January 24

Polisi Waeleza Sababu za Kumkamata Nabii Titto

0
0
Jeshi la Polisi mkoani Dodoma, linamshikilia Onesmo Machibya maarufu Nabii Tito mwenye miaka 44 ambaye ni mkazi wa kijiji cha Ng’ong’ona Manispaa ya Dodoma, kwa kosa la kueneza chuki ya kidini dhidi ya watu wengine.

Akizungumza na waandishi wa habari Kamanda wa Polisi mkoa wa Dodoma Gilles Muroto, amesema Nabii Tito amekamatwa baada ya kurekodi vipande vifupi vya video na picha vyenye maudhui ya kukashifu dini nyingine, na kuleta chuki dhidi ya watu wengine na kurusha mitandao ya kijamii, kinyume na kifungu cha sheria namba 129 cha kanuni ya adhabu sura ya 16 na marekebisho yake ya 2002.

Aidha, kamanda Muroto amesema mtuhumiwa huyo amesambaza vipeperushi mbalimbali katika maeneo ya starehe akitangaza imani ya kidini inayokiuka maadili ya nchi na kufanya hadharini vitendo visivyofaa, akitumia kitabu kitakatifu cha Biblia.

Nabii huyo amekamatwa akiwa na majoho (kanzu) yakiwa na misalaba miwili, vipeperushi 80, Biblia moja ambayo anatangazia imani inayokwenda kinyume na maadili mema ya taifa.

Nabii Tito kwenye mahubiri yake amekuwa akiwahamasisha watu kutumia vilevi, kufanya maasi, kuoa wanwake zaidi ya mmoja akiwemo msaidizi wa kazi, kitendo ambacho ni kinyume naa maagizo ya kitabu hicho kitakatifu na imani anayoihubiri

Walichokibaini Polisi Baada ya Kumhoji ‘Nabii’ Tito

0
0
JESHI la Polisi mkoani Dodoma,  baada ya kumkamata na kumfanyia mahojiano Onesmo Machija (44) anayejiita ‘nabii’ Tito, kutokana na mahubiri ya kidini anayoyafanya, limesema mtu huyo ana  matatizo ya akili.

Akizungumza na wanahabari mjini Dodoma leo, Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Dodoma, Gillesi Muroto, amesema mnamo Juni 23, 2014, mtu huyo aliwahi kulazwa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili kwa ajili ya matibabu ya akili chini ya daktari aliyejulikana kwa jina moja la William ambapo aliporuhusiwa alitakiwa kurejea hospitalini hapo Julai 9 mwaka huohuo lakini hakurejea.

Kamanda Muroto aliendelea kusema kwamba baada ya hapo, Machija ambaye kanisa lake halijasajiliwa popote,  aliibukia mkoani Dodoma katika kijiji cha Nong’ona kilicho karibu na Chuo Kikuu cha Dodoma (Udom) akifanya  mahubiri ya kidini yaliyodaiwa kuwa hayakuwa na maadili ya kidini.

Kwa msingi huo, alisema jeshi la polisi limempeleka Hospitali ya Rufaa ya Mirembe iliyoko mkoani Dodoma  kwa ajili ya kumpima tena matatizo hayo ya akili na baada ya majibu kutolewa,  Dkt. Dixon Philipo aliyemshughulikia alithibitisha kwamba bado ana matatizo hayo.

Pamoja na hayo, Muroto alisema jeshi la polisi mkoani humo  bado linaendelea kumshikilia kutokana na matendo yake aliyoyafanya ili kufanya uchunguzi zaidi.

Mapingamizi yatupiliwa Mbali Kinondoni....Mtulia na Mwalimu Rasmi Ulingoni

0
0
Msimamizi wa uchaguzi wa jimbo la Kinondoni ambaye pia mkurugenzi wa manispaa hiyo, Aron Kagurumjuli ameyatupilia mbali mapingamizi matatu yaliyowasilishwa na wagombea wa vyama vya Chadema, CCM na CUF.

Mapingamizi hayo ni kwa mgombea wa CUF, Rajab Juma kumwekea mgombea wa Chadema, Salumu Mwalimu, wakati Mwalimu yeye alimwekea Maulid Mtulia wa CCM na mgombea huyo wa chama tawala alimwekea mgombea wa SAU, Johnson Mwangosi.

Baada ya jana ofisi ya msimamizi wa uchaguzi kutoa barua ya utetezi kwa wagombea waliowekewa mapingamizi leo Jumanne imetoa majibu ya kuyatupilia mbali mapingamizi hayo.

“Tumeyatupilia mbali mapingamizi yao kwa sababu hayana mashiko, kilichobaki ni wagombea kwenda uwanjani wakapambane,” amesema msimamizi huyo.

Habari Njema: Tunatibu Busha, Korodani Kuvimba,Ngiri, Miguu Kufa Ganzi Pamoja na Matatizo ya Nguvu za Kium

0
0
Ni Dawa ya nguvu za kiume inayorefusha na kunenepesha uume saizi uipendayo (Inch 1-7) kwa muda wa siku 6 tu.Dozi hii itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa muda wa dakika 30, utarudia tendo la ndoa zaidi ya mara 4 bila hamu kuisha bila kujali umri na garantee ni miaka 60 baada ya kutibu tatizo.

Pia tunatibu Busha bila kufanyiwa Oparesheni, korodani moja kuvimba, ngiri, tumbo kujaa gesi na kuunguruma, kutopata choo vizuri, miguu kuwaka moto na kufa ganzi, chango la wanawake, kisukari na kutokwa na kinyama sehemu ya haja kubwa.

MIHAYO:
Inarudisha mke, mchumba, hawara na atakutimizia kila kitu unachotaka kutoka kwake ndani ya  saa 2 tu hata kama yupo mbali. atarudi na kumfunga asiwe na mwingine zaidi yako.

Umefukuzwa kazini? unataka kupandishwa cheo? Umepoteza pesa zako kwenye biashara bila kujua umepandikizwa chuma ulete? Njoo urudishe pesa zako. Unauza mali yako haiendi?


Wasiliana na mtaalam Challo kwa; 0714006521

Kama Una Roho Ndogo Ukiisoma Hii Barua ya Dogo Aslay Lazima Chozi lidondoke

0
0

"Jina langu ni Aslay Isihack, jina hili alinipa Mama yangu mwenyewe Bi. Mozza kutokana na maisha niliyopita ya Muziki wengi wananifahamu kwa jina la Aslay.

Barua kwa Mama yangu kipenzi pamoja na mashabiki zangu.

Hellow Mama najua unanisikia mwanao tangu uondoke life its so complicated kuliko nilivyodhania, kila kitu kwangu tabu nakosa sana ushauri wako natamani kuongea nawe japo hata siku moja lakini nafahamu kwa mapenzi ya Mola haiwezekani nakuombea kila la heri huko ulipo.

Japo kwasasa nimepata kibinti pacha wako, jina lake nimemuita Mozza I wish ungemuona mmefanana sana. Kuna kitu Mama nataka kukugusia juu ya ndoto yangu bado sana natamani kuwa msanii mkubwa kama Kaka zangu na Dada zangu walionitangulia kwenye Muziki. Ndoto niliyokuwa nakusimulia kila wakati tukila Chakula cha jioni.

Mama Kila kukicha Wananirushia mawe nisifike niendapo. Mawe yote Mama nimeyaokota najengea barabara nifike niendapo, hakuna wakunifuta mimi machozi yangu nalia kilio cha mtu mzima maumivu ndani kwa ndani.

Juzi nilitamani nikupigie simu nikuambie yanayonisibu mwanao, Namba yako haipatikani labda umeweka call busy unaniombea dua njema. Nimuambie nani yanayonisibu ndani ya Moyo wangu juu ya Mziki wangu na maisha yangu?

Mashabiki wangu ndiyo wananipa Ujasiri wa kupambana na kukomaa hivo hivo. Sikufaidika na kile nilichokifanya kwa zaidi ya miaka 15
Hata mimi ukiniuliza ilikuwaje nakosa cha kukujibu Mama nataka tukae kikao cha dharura, tuone ilikuwaje.

I feel inferior, najihisi mnyonge, Nawaza nitaanzia wapi?. I just feel hopless and more hopeless day by day. I dont know. Kila ninaposhika panageuka mwiba mchungu kwangu.
Natamani kujua kama unafahamu nanyanyaswa kisa Muziki wangu .

Kiukweli Mama siwezi kulalamika sanaa maana hata wakati napokuwa mpweke mashabiki zangu huniliwaza kwa kusapoti kazi zangu wamekuwa ndiyo faraja kwangu.

Ndiyo wananifanya niwe jasiri wa kuwatengenezea Muziki mzuri kila kukicha. Sometimes nikiwaza mwanangu ataishije, na familia nitaitunza vipi, bila Muziki?

Natumaini utanijibu basi hata ndotoni Mama kama barua yangu utaipokea.

Nimekukumbuka sana mwanao
Aslay.
Nakupenda Mama."

Jini Kbura Aibuka na Kuanika Siri ya Kunawiri

0
0
Jini Kbura Aibuka na Kuanika Siri ya Kunawiri
BAADA ya mwaka jana kuugua na kwenda kupumzika kwao Mwanza na sasa kuonekana kuwa na hali nzuri, msanii wa filamu za Kibongo, Miriam Jolwa ‘Jini Kabula’ ameibuka na kuanika siri ya kunawiri kwake.

Akipiga stori na Za Motomoto News, Jini Kabula alisema kunawiri kwake kunatokana na kupumzika kwa miezi mitatu bila mikikimikiki huku akila vinono nyumbani kwa kaka yake alikoenda kwa mapumziko na hivi karibuni ana mpango wa kurejea tena Dar kwa ajili ya kufanya biashara ili kujiendeshea maisha na siyo sanaa tena kwa sasa.

“Jamani kunawiri kwangu ni kwamba ninakula vinono kwa kaka yangu huku Mwanza, sina stress maisha yanaenda tu vizuri, nimeshapumzika miezi mitatu kama daktari alivyoshauri na ninajiandaa kurudi kwa ajili ya mishe nyingine za kimaisha,” alisema Jini Kabula.

Vanessa Mdee Apewa Tuzo Maalum ya 'Nyota wa Mchezo'

0
0
Vanessa Mdee Apewa Tuzo Maalum ya 'Nyota wa Mchezo'
Vanessa Mdee amekuwa msanii wa kwanza Tanzania kupokea Plaque ya ‘Nyota Wa Mchezo’ baada ya kutajwa kwenye vipengele vya  #BestFemaleAct #BestPerformer #BestLiveAct #EmergingArtistOfTheYear.
Plaque hiyo inatolewa na kipindi cha The Playlist cha Times FM na mtangazaji Omary Tambwe aka Lil Ommy kwa kutambua mchango na mafanikio ya msanii na kazi nzuri aliyozofanya.

Wakiwa katika picha ya pamoja na wafanyakazi wa Times FM.

Kwa mujibu wa Lil Ommy, lengo la Plaque hiyo ni kuwapa nguvu na kusherehekea mafanikio ya kazi za msanii na sanaa kwa ujumla Tanzania.
“Wazo la kumtambua na kumtunuku ‘Nyota wa Mchezo’ lilianza Disemba mwaka jana tarehe 18 ambapo nilitumia twitter kutaja wasanii wengi kama ‘Nyota wa Mchezo’ kuwatambua waliofanya vizuri kwenye sanaa ya muziki wa kizazi kipya,” amesema Lil Ommy.


“Vanessa alikuwa ni miongoni mwa mtu wa kwanza kuandika tweet yake na wazo lilianzia baada ya kumfikiria yeye na kuona kazi nzuri alizofanya na baadae nikaendeleza orodha ya watu wengi kwa hashtag ya #BongoFleva2017 #NyotawaMchezo na kutaja nafasi zao (vipengele) ambavyo wamefanya vizuri,” ameongeza.

Vee Money na tuzo yake.

Mtangazaji huyo ameeleza kuwa aliangalia impact (matokeo/athari) ya msanii, impact ya kazi zake, popularity (umaarufu), kujulikana, airplays (kazi yake kuchezwa kwenye Radio na TV), Views (watazamani kwenye YouTube), anavyozungumziwa kwenye mitandao ya kijamii, ubora wa kazi, ukuaji wa msanii, ukomavu wa msanii na kuwataja kama NYOTA WA MCHEZO.

Amesema Januari 22 mwaka huu (jana) alim-surprise Vanessa Mdee baada ya kufanya naye mahojiano maalum wakiichambua albam yake bora kabisa ya kwanza na ‘nzito’ ya Money Mondays, kisha kufanya makabidhiano maalum ya Plaque hiyo kutokana na kazi yake katika ofisi za Times FM, DAR ES SALAAM, Tanzania.
Naye Vee Money alionesha furaha yake kwa plaque hiyo kupitia kwenye akaunti yake ya Instagram, akiitaja Jumatatu kama siku yake nzuri zaidi.
“Asanteni Sana Sana Sana…Leo nimezawadiwa tuzo ya Playlist Nyota wa Mchezo 2017. #BestFemaleAct #BestPerformer #BestLiveAct #EmergingArtistOfTheYear.
“Mondays are my FAVORITES 😍 just received a plaque from @timesfmtz Playlist MVP of the year 2017. Asante Sana @lilommy 😍😘💜 album link in my bio,” Vee ameandika kwenye Instagram.
Lil Ommy ambaye anatajwa kushika nafasi ya kwanza katika  watangazaji watano waliofanya vizuri zaidi mwaka jana, na kutanjwa kama MTANGAZAJI BORA WA KIUME Bongo, amesema lengo lake ni kuhamasisha kiwanda cha burudani Tanzania kutambua kazi za wasanii na kusapoti sanaa kama kiwanda kinachotoa ajira kwa vijana na kuchangia pato la Taifa.

Tanzia: Kocha Mwadui FC, Afariki Dunia

0
0
Kocha Mwadui FC, Afariki Dunia
Kocha msaidizi wa Klabu ya Mwadui Jumanne Ntambi amefariki dunia usiku wa kuamkia leo huko Mkoani Shinyanga, huku chanzo cha kifo chake kikidaiwa ni kutokana na ugonjwa wa shinikizo la damu alilokuwa akisumbuliwa nalo kwa kipindi kirefu.

Hayo yamethibitishwa na Katibu wa Klabu hiyo Ramadhani Kilao wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa 'East Afrika Television' asubuhi ya leo na kusema amepokea taarifa hizo kwa masikitiko makubwa huku akibainisha baadhi ya mambo kuwa ni bado mapema sana kama timu kutoa msimamo wao kuhusiana na kifo hicho cha Ntambi.

"Ni kweli kocha Jumanne Ntambi amefariki dunia kutokana na tatizo la 'presha' lililokuwa likimsumbua takribani wiki  moja mpaka umauti ulipomfika. Mpaka sasa bado tunashikilikiana na familia ya marehemu ili tuweze kujua utaratibu mzima ila kitakachokuwa kimejiri tutaikiweka bayana kwa watu wote", alisema Kilao.

Marehemu Jumanne Ntambi alijiunga na timu ya Mwadui FC mwaka jana (2017) wakati michuano ya Ligi Kuu Tanzania Bara inaanza akiwa ametokea katika timu ya mkoa wa Moshi.

Rais Museveni Ammwagia Sifa Trump “Ninampenda Trump, Anasema Ukweli Mtupu”

0
0
Rais Museveni Ammwagia Sifa Trump “Ninampenda Trump, Anasema Ukweli Mtupu”
Rais wa Uganda Yoweri Museveni amesema anampenda rais wa Marekani Donald Trump katika hotuba yake wakati wa ufunguzi wa bunge la Afrika Mashariki jijini Kampala.

Museveni alisema Marekani ina rais mzuri sana wakati wa ufunguzi wa mkutano huo wa bunge la Afrka mashariki.

''Ninampenda trump kwasababu anasema ukweli mtupu, waafrika wanatakiwa kusuhisha matatizo yao wenyewe, Waafrika ni dhaifu sana'' Museveni.

Pongezi hizo za museven kwa Trump zinakuja saa chache tuu baada ya balozi wa Uganda kwa Marekani Deborah Malac kumkosoa Trump.

''Kauli zake zinachukiza na kukera sana'' amesema Deborah.

Magufuli na Mseven waahidi kuimarisha mshikamano
Maoni hayo ya rais Museveni ni tofauti sana na viongozi wengi wanaochukizwa na kauli za Trump.

Mapema mwezi huu Trump alidaiwa kutoa kauli za kejeli juu ya nchi za Afrika wakati wa mkutano wa kujadili masuala ya wahamiaji.

Trump alikataa kuwa ametoa kauli hizo za kejeli lakini seneta mmoja aliyehudhuria mkutano huo alisema kuwa Trump alitamka maneno ya kejeli na matusi kwa nchi kama Haiti, elsalvador na nchi za Afrika.

Kwa mujibu wa gazeti la New York times, mwaka jana Trump alisema kuwa watu wote wanaotoka Haiti wana ukimwi, na wananigeria wakiruhusiwa kuingia marekani basi watakataa kurudi Kwao.

Shakira Huenda Akahukumiwa Kutumikia Kifungo Gerezani

0
0
Shakira Huenda Akahukumiwa Kutumikia Kifungo Gerezani
Mwimbaji staa tokea nchini Colombia, Shakira anaweza kufungwa jela kutokana na kosa ambalo limekuwa likiwapeleka mastaa wengi Mahakamani nchini Hispania la kushindwa kulipa kodi.

Mamlaka ya kukusanya kodi nchini Uhispania imemtaka Shakira kupeleka  rekodi ya fedha zake kuanzia 2011-2014 kufuatia habari za Shakira kukwepa kulipa kodi mwaka jana.

Habari hizo ziliandikwa katika magazeti ya Panama na taarifa katika gazeti la “La Vanguardia” la Catalonia, ofisi ya kulipa kodi ya Catalonia imesema kuwa Shakira aliishi Uhispania katika kipindi cha kati ya miaka  2011-2014 na anatakiwa kulipa kodi.

Shakira mwenye umri wa miaka 40 ana watoto wawili na mchezaji mpira maarufu wa Uhispania Gerard Pique.

Buswita Kuukosa Mchezo Dhidi ya Azam

0
0
Buswita Kuukosa Mchezo Dhidi ya Azam
KIUNGO wa Yanga, Pius Buswita atakosa mchezo dhidi ya Azam kutokana na adhabu ya kadi tatu za njano huku Kelvin Yondani akirejea baada ya adhabu yake kumalizika.

Jumamosi ijayo, Azam FC itavaana na Yanga mchezo ambao utapigwa katika Uwanja wa Azam Complex Chamazi jijini Dar es Salaam.

Akizungumza na Championi Juma­tano, Meneja wa Yanga Hafidhi Saleh al­isema Buswita na Andrew Vincent ‘Dante’ watakosekana kutokana na kupata kadi katika michezo tofauti.

“Ni kweli Buswita kwenye mchezo dhidi ya Azam hatakuwepo kutokana na kutumikia adhabu ya kadi tatu za njano ambazo alipata kwenye michezo iliyopita pamoja na beki Andrew Vincent ‘Dante’.

“Lakini pia Yondani amemaliza adhabu yake hivyo atakuwepo uwanjani,” alisema Saleh ambaye anaheshimika miongoni mwa wanachama na viongozi wa Yanga.

Jaji Mstaafu, Robert Kisanga Amefariki Dunia

0
0
Jaji Mstaafu, Robert Kisanga Amefariki Dunia
Jaji mstaafu, Robert Kisanga amefariki dunia katika Hospitali ya Regency Dar. Rais wa Chama cha Majaji Wastaafu, Thomas Mihayo athibitisha

Majimaji Kutinga Dar Leo Kwaajiri ya Mechi Yao na Simba

0
0
Majimaji Kutinga Dar Leo Kwaajiri ya Mechi Yao na Simba
KIKOSI cha Majimaji leo Jumatano kinatarajia kuingia jijini Dar ikiwa ni muda mfupi kabla ya kuvaana na wapinzani wao Simba katika pambano la ligi ambalo litapigwa wikiendi hii kwenye Uwanja wa Taifa.

Majimaji wanaodhaminiwa na Kampuni ya Kubashiri Matokeo ya Sokabet, inatua Dar ikiwa na kikosi kamili kwa ajili ya mchezo huo na Sim­ba ambapo mchezo wao wa mwisho waliilazimisha sare Singida United ya kufungana bao 1-1.

Kocha msaidizi wa timu hiyo iliyo katika nafasi ya 12, Habibu Kondo ame­liambia Championi Jumatano, kuwa wamekuja Dar kuhakikisha wanaendele­za mwendo wa kukusanya pointi kama walivyofanya kwenye michezo yao miwili ya mwisho dhidi ya Azam na Singida United kabla ya kuivaa Simba.

“Kesho (leo) Jumatano ndiyo tunatara­jia kufika huko Dar kwa ajili ya kuweka kambi ya muda mfupi kabla ya kucheza na wenyeji wetu Simba, tunawaheshimu wapinzani wetu kama timu kubwa lakini tunataka kufanya vizuri mbele yao.

“Tunajua kwamba mchezo utakuwa mgumu ila tumejipanga vyema kwa ajili ya kupata pointi mbele ya wenzetu hao, tunakuja tukiwa kamili kwa maana ya kikosi chote na siku chache ambazo tutakaa huko zitatufanya kuzoea mazin­gira kabla ya kupambana na wapinzani wetu,” alisema Kondo.

Soma Nafasi za Ajira Zilizotangazwa Siku ya Leo

0
0

Miujiza ya Sharifu Seif Mohamed..JE Umeachwa na Mme/Mke au Mpenzi, Umesongwa na Mitihani ya Maisha..Piga Simu Upate Muujiza Wako

0
0
SHARIFU SEIF MOHAMED ANAWASHUKURU WALE WOTE WANAOENDELEA KUPIGA SIMU, WENYE MATATIZO NA WALE WANAOTOA  SHUKRANI NA SHUHUDA JINSI TIBA ZAKE ZINAVYO WASAIDIA,

(Rudisha mahusiano yako ndani ya masaa 72 tu)

SHARIFU MOHAMED Ni  mtaalam na mnajimu maarufu wa nyota na kubashiri mambo yanayo watesa binadamu duniani kote na kupata ufumbuzi, Anatumia kitabu cha QUR'AN, Dawa za Asili, Dawa za Kiarabu na majini kwa kumtuliza mke/mme, mchumba au mpenzi ndani ya masaa 72 tu, na kutatua matatizo yote ya kimaisha,

Je Umeachwa na UMPENDAE awe Mme/Mke na bado unampenda? Je Umekimbiwa na Mmeo/ Mkeo n anaishi na mtu mwingine? Je Umejaribu sehemu nyingi bila mafanikio? Mpigie simu SHARIFU SEIF sasa hivi ujionee Muujiza wa Papo kwa Papo, Anauwezo wa hali ya juu wa kusambaratisha mahusiano yao na kumrejesha kwako haraka sana na Kumfanya Atimize Ahadi zote Ndani ya Muda Mfupi Endapo Utafwata Atakacho Kuelekeza

ANAZO DAWA ZA MAPENZI, NGUVU ZA KIUME, CHANGO NGIRI MAJI NA N.K, ZINDIKO LA NYUMBA NA BIASHARA, PETE ZA BAHATI, HUMALIZA KABISA TATIZO LA NGUVU ZA KIUME NA KUREFUSHA UUME KWA SAIZI UNAYOTAKA, HUZUIA CHUMA ULETE KWENYE BIASHARA, HURUDISHA MALI ZILIZOPOTEA, MAGONJWA SUGU, MIGUU KUWAKA MOTO AU KUFA GANZI, HUTIBU BUSHA BILA KUPASUA, ANAO UWEZO WA KUMRUDISHA ALIE MBALI AU ALIECHUKULIWA MSUKULE, KUPANDISHA NYOTA NA KUSHINDA BAHATI NA SIBU, KASAFISHA NYOTA NA KUKUPA MVUTO WA AJABU, KUTOA NUKSI NA VIFUNGO MBALIMBALI,  MAFANIKIO YA MAISHA NA UTAJIRI BILA MASHARI, NA MENGINE MENGI YA SIRI,

Je UMAHANGAIKA KUPATA MTOTO BILA MAFANIKIO? WASILIANA NA MTAALAMU HUYU KWANI YEYE HUFAULU PALE WOTE WALIPOSHINDWA, PIA UMALIZA KAZI ZILIZO SHINDIKANA NA WATAALAM WENGINE NDANI YA MASAA 24 TU,

(NA ANATIBU KWA NJIA YA SIMU UKIWA NCHI YOYOTE AU MKOA WOWOTE ENDAPO UTAFWATA MAELEKEZO YAKE)

Kwa ushauri na mawasiliano  zaidi Piga SIMU No:

Mobile +255 654-836970
WhatsApp +255 756-033670  

Simba na Yanga Zalaumiwa Kuongoza Kustaafisha Wachezaji Wakiwa Bado Wanavipaji

0
0

Kiungo wa zamani wa Simba amri Kiemba amefunguka kuwa, idadi kubwa ya wachezaji wa Tanzania wanastaafishwa na vilabu vya Simba na Yanga.

Ndio, Kiemba amethibitisha hilo kwakuwa wachezaji wengi hustaafu bila ridhaa yao lakini viongozi au kelele za mashabiki wa timu hizo huchangia kwa kiasi kikubwa wachezaji kuamua kustaafu huku wakiwa bado wanatamani kuendelea kucheza.

Mchezaji kama musa hassani mgosi alitangaza kustaafu soka kisha kupewa umeneja kwenye klabu ya Simba nafasi ambayo hakudumu nayo kwa muda mrefu akatolewa na kupelekwa kuwa kocha wa timu ya vijana lakini baadae akasajiliwa na Dodoma FC ya ligi daraja la kwanza kwa ajili bya kuitumikia kama mchezaji na sasa anacheza.

Inaelezwa NIco Nyagawa pia alistaafishwa Simba lakini hata Yanga kuna wahezaji ambao kwa sababu waliitumikia klabu hiyo kwa muda mrefu baada ya kuondoka mashabiki wanawapigia kelele kwamba ni wazee, Jerry Tegete na Mrisho Ngasa kwa sababu wameshacheza yanga kuondoka kwao kunafanya waonekane ni wazee kwa sababu tumezoea kuona wachezaji wakishacheza vilabu hivyo wengi mwisho wao huwa ni kustaafu.

Unapomzungumzia mchezaji kama Ramadhani Singano ‘Messi’ ni mchezaji aliyecheza timu ya vijana ya Simba pamoja na Mkude, Ndemla, Ajib lakini kwa kuwa yeye ameshatoka kwenye vilabu hivyo usishangae siku utakaposikia akiitwa mzee.

“Kwa sisi wachezaji tunavyojua, mchezaji anakuwa mkubwa akicheza Simba na Yanga. Cheza timu nyingine zote hata kwa misimu 20 lakini ukienda simba na yanga utaonekana bado kijana. Mchezaji anaonekana mzee akishacheza simba au yanga ndiyo maana wachezaji wa timu hizo ndio huwa wanastaafu lakini wale wa timu nyingine hawastaafu.”

“Unajua unapocheza Simba au Yanga watu wanakusikia, wanakuona na kusoma sana habari zako kwa hiyo inafika wakati wanakuchoka lakini ukiwa nje ya simba na yanga husikiki sana hadi timu yako inapokutana na simba au yanga lakini ukiwa mchezaji wa hivyo vilabu viwili hata ukienda mazoezini habari zako zinasikika.”

Kiemba amesema kuna wakati mchezaji anakuwa kwenye kiwango bora sana lakini kuna wakati anapitia kipindi kigumu ambacho kiwango chake kinapokuwa kimeshuka, nyota huyo wa zamani anasema hilo ni jambo la kawaida kwenye soka na halihusiani na mara nyingi halihusiani na umri wa mchezaji.

“Kwa mchezaji kiwango ni kitu cha kupanda na kushuka, inawezekana mashabiki wakakusikia kwa miaka miwili ukiwa katika kiwango cha juu halafu unapofika mwaka wa tatu kiwango kinakuwa kimeshuka hapo ndio unaonekana umezeeka kwa hiyo wanataka uondoke.”

“Mimi najua kwamba kiwango ni kitu cha kupanda na kushuka kwa hiyo kinaposhuka huwa sipati shida kwa sababu najua hiki ni kipindi cha mpito, unaweza ukacheza kwa kiwango cha juu hata kwa miaka mitano lakini itafika wakati unaweza ukashuka hata kwa miezi miwili, sasa wachezaji wengi ikifika wakati kiwango kimeshuka namna ya kurudi kwenye ubora wao ndio inakuwa shida.”
Viewing all 104432 articles
Browse latest View live




Latest Images