Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104780 articles
Browse latest View live

Mwanamke Ambwambia Mumewe Anatamani Wanaume Wengine

$
0
0

 ANITA CASSIDY (40) mwanamke ambaye amekuwa katika ndoa kwa miaka ipatayo kumi, alimwambia mumewe aitwaye Marc (46) kwamba anaona maisha na ndoa ya mume na mke yamemchosha na alitaka kuwa na wenza wengine wa kufanya nao mapenzi.

Katika mazungumzo ya wawili hao ambao ni raia wa Italia, mumewe alikubali kwamba wote wawili kila mmoja angekuwa na wapenzi wengine.    Lakini, je, katika ndoa moja panawezekana kuwa na watu zaidi ya wawili?
Anita Cassidy (katikati) akiwa na mpenzi wake wa kiume Andrea (kushoto) na mumewe Marc (kulia) wakichangia penzi la watu watatu.

 “Mwaka mmoja uliopita niliweka kila kitu bayana kwenye mtandao wa Facebook kwa picha niliyokuwa na mume wangu na watoto wetu wawili.  Marafiki zangu wakaanza kuniuliza kwamba mwanamme mwingine aliyekuwa katika picha alikuwa nani.  Niliwaambia alikuwa Andrea – mpenzi wangu wa kiume.


… Watatu hao wakiwa pamoja kando ya bahari wakipunga upepo.

“Nafahamu wengi watashangaa kwani walijua Marc ndiye mume wangu halisi.   Lakini ukweli ni kwamnba nilikaa naye jikoni mwaka mmoja tukafanya mjadala  mgumu wa aina yake miaka mitatu iliyopita kuhusu maisha yetu.  Nilimwambia Marc kwamba yeye peke yake alikuwa hatoshi kumaliza hamu yangu ya mapenzi.

“Baada ya kukubaliana naye, nilianza kutafuta mpenzi mwingine kwenye mitandao na tukagunduana mimi na Andrea ambaye tulianza kukutana na hatimaye kufanya naye mapenzi.

“Nilikuwa na umri wa miaka 28 nilipokutana na Marc, hivyo wazo la kufanya mapenzi na mtu mmoja kwa miaka zaidi ya 40 ambayo ingefuata, lilinivuruga akili.  Ni kweli nilikuwa nampenda Marc lakini kimapenzi nilijiona kama nilikuwa peke yangu.  Matokeo yake nilimtambulisha Andrea kwa Marc akawa anakuja nyumbani na tunafurahi naye wote.

 “Muda si muda, Marc naye akawa na uhusiano wa wazi na wanawake wengine, akawa anaondoka kwenda kufurahi nao kwengine.  Mwanzoni nilijisikia vibaya kwani alikuwa amenionyesha wanawake hao.  Hata hivyo, sikuwa na la kufanya.

 “Sikutaka kuwaambia watoto wangu kilichokuwa kinatokea, kwani umri wao ulikuwa mdogo mno na wasingenielewa.  Tuliendelea hivyo kwa furaha hadi ikafikia mimi na Marc tukatengana na kila mtu akawa analala chumba chake kwenye nyumba ileile.  Hivi sasa tunasubiri kutengana kabisa ili niondoke na watoto.
“Tangu tutengane miezi 18 iliyopita, bado nampenda Marc na atakuwa nembo muhimu katika maisha yangu.. Ni vyema kuwa na maisha ya wazi, kuliko maisha ya kudanganyana kwa siri….”


 Wakifurahi bila ya chuki wala uchungu.

Naye Andrea anasema kabla ya kukutana na Anita alikuwa na mpenzi mwingine ambaye aliachana naye baada ya mwanamke huyo kukataa kuwa na uhuru wa kufanya mapenzi na watu wengine nje ya wao wawili.

 Hivyo,  alikazania kwa Anita ambaye walipendana na kushirikiana kila kitu likiwemo penzi kabla ya kukutanishwa na mumewe mwaka mmoja baadaye.  Mumewe alikubali kila kitu na watoto wakajua baba yao alikuwa Marc na Andrea alikuwa ‘boifrendi’ wa mama yao…



Hivi sasa Anita na Andrea wanasubiri kuendeleza penzi mara Marc na Anita watakapoachana rasmi.

WALUSANGA NDAKI/MITANDAO/MASHIRIKA

Tangaza Biashara Yako Hapa Uweze Kupata Wateja wa Haraka

$
0
0

Mtu wangu wa nguvu unaweza Tangaza Biashara yako hapa nasi uweze kuwafikia watu wengi zaidi kwa mara moja kupitia blog ya Udaku Special..

Piga simu 0714604974 

Sababu 5 Zinazosababisha Uume Kuwa Mdogo (Kibamia)...Soma Hapa Kidume Ufahamu

$
0
0
Mapenzi
Kundi kubwa la wanaume ambao wanashindwa kufurahia tendo la ndoa kutokana na kuwa na uume mdogo kupita kawaida...
Wanaume walio na tatizo hili wengi wao huwa hawana confidence ya kuingia katika mahusiano na wasichana ama wanawake wanao fahamiana nao kutokana na kuogopa " siri" zao kujulikana hususani pale uhusiano wao unapofika mwisho..Ikitokea mwanaume akiwa katika uhusiano na mwanamke "mcharuko" ( asiye mstaarabu ) mwanamke huyo anaweza kuanza kumvua nguo hadharani kwa kumtangazia kwa watu kuwa na uume mdogo . " Mwanaume utakuwa wewe!" na lugha za namna hiyo hutawala midomoni mwa wanawake hawo....


Matokeo yake sasa wanaume walio na tatizo hili huamua kutokuwa na uhusiano wa kimapenzi na wanawake wanao fahamiana nao, na badala yake huamua kuanzisha tabia ya kuwa wanajamiiana na wanawake wanaouza miili yao amakujihusisha na upigaji punyeto n.k.

NINI CHANZO CHA UUME KUWA MDOGO.

1. Kupiga Punyeto kwa muda mrefu..
Hali hii husababisha kusinyaa kwa uume na hatimaye uume kurudi ndani.
2. Kuugua chango la uzazi.
3. Magonjwa ya utotoni.
4. Kutahiriwa mapema
5. Kurithi kutoka kwa wazazi :

Wanaume wengine wana maumbile madogo kwa sababu wamerithi maumbilehayo kutoka kwa wazazi wao.

Pata Dawa Bora ya Nguvu za Kiume na Maumbile Madogo ya Kiume ( Super Shafti)

$
0
0
DAWA BORA YA NGUVU ZA KIUME NA MAUMBILE MADOGO YA KIUME ( SUPER SHAFITI) NI DAWA YENYE UWEZO MKUBWA WAKUTIBU UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME


 (SUPER SHAFITI ni dawa ya asili yenye uwezo mkubwa wa kuogeza nguvu za kiume maradufu
(1) itakufanya uwe na nguvu za ajabu ukiwa unafanya ntedo la ndoa
(2) inaogeza hamu ya kurudia ntedo la ndoa zaidi ya mara tatu bila kuchoka
( 3) itakufanya uchelewe kufika kileleni dani ya dk 30
( 4)  itaimalisha milija ya uume iliyo legea au kusinyaa
(5) lnarefusha na kunenepesha uume saizi utakavyo kuazia ichi 1-8 unene sm 2-4
 (6) itakupa nguvu za kusimamiasha uume wako barabara kama_ msumari wakati wa ntedo la ndoa
(7) inasaidia kusafisha mishipa. ya kwenye uume na hivyo kusaidia Katika kuongeza kasi ya msukumo wa damu kwenye mishipa ya uume
(8) usaidia kuurudisha nje uume ulioingia ndani
(9) inasaidia kuogeza manii nyingi ambazo vina viini vya uzazi
(10)usaidia kutibu madhara ya punyeto ,matumizi makali ya  madawa ya kizugu mirungi bangi na sigara

KWA NINI BAADHI YA WANAUME WENGI WANA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME NA KUWA NA MAUMBILE MADOGO YA KIUME NINI CHANZO CHAKE?

ni kutokana na magonjwa megi kuongezeka yakiwemo kisukari presha ya kupanda na kushuka upigaji wa punyeto wa mda mrefu magonjwa ya moyo ngiri ya kuviba korondani vidonda vya tumbo
Msongo wa mawazo  tumbo kuuguruma kujaa ngesi kutopata choo vinzuri maumivu ya mgongo kiuno na tumiaji wa madawa makali ya kizungu ya kuongeza nguvu za kiume kuzaliwa na chango linaloshabulia neva za ukuwaji wa uume utumiaji wa mirungi bangi sigara na nk  tunapenda kuwatangazia wasomaji, wa makala zetu kuwa tunazo dawa nzuri za asili ambazo hazina mazala na zinazotibu na kuponyesha matatizo ya upungufu wa nguvu za kiume na maumbile ya kiume

NA TUNATIBU MAGONJWA YOTE SUGU KAMA KISUKARI PRESHA AINA YOTE UGONJWA WA MOYO SITRUKO KWIKWI KICHOMI MINGUU KUFA NGAZI ASIMA NK MZEE ISAYA ANAPATIKANA MAGOMENI MIKUMI KARIBU NA KANISA  TUMAINI HEBRAST CLINI NDIYO JIBU NA SULULISHO YA MATATIZO YOTE

PIGA simu 0745495181 au 0682644040

Kwa watu wa mikoa huduma utatumiwa na watu wa nje ya nchi utazipata dsm kama huna nafasi ya kufika ofisini kwetu utaletewa popote ulipo

Juma Nyoso Aachiwa Kwa Dhamana

$
0
0
Juma Nyoso Aachiwa Kwa Dhamana
Swala la beki wa klabu ya Kagera Sugar, Juma Said Nyoso kumshambulia shabiki anaesadikika kuwa wa timu ya Simba, Shabani Hussein hadi kuzimia katika mchezo wao wa wiki hii uliyofanyika uwanja wa Kaitaba mjini Bukoba bado halijakwisha licha ya Jeshi la Polisi kumuachia kwa dhamana mchezaji huyo.

Kupitia Mwanaspoti Kaimu Kamanda wa Polisi wa Mkoa huo, Issack Msengi amesema wamemwachia kwadhamana mchezaji Juma Nyoso wakati wakiendelea na upelelezi na ikibainika kuwa ana makosa atafikishwa mahakamani.

Shabiki anaesadikika kuwa wa timu ya Simba, Shabani Hussein ambaye anadaiwa kupigwa na mchezaji Juma Nyoso

“Kuhusu aliyejeruhiwa kwa sasa anaendelea vyema na kesho (leo) tunatarajia kupata ripoti ya kipimo cha Xray alichofanyiwa,” amesema Kamanda Msengi.

Kamanda Issack Msengi ameongeza kuwa wakimuachia Juma Nyoso baada ya kukamilisha taratibu za dhamana na wanaendelea kupeleleza kwa hatua zaidi huku akisema kama itabainika shabiki aliyepigwa alifanya kosa la jinai la kutukana hadharani nayeatafunguliwa kesi juu ya tukio hilo.

Beki huyo wa Kagera Sugar amejikuta akiingia mikononi mwa Jeshi la Polisi hapo juzi baada ya kutuhumiwa kumpiga shabiki na kumzimisha kitendo alichokifanya mara baada ya kumalizika kwa mchezo wao dhidi ya Simba SC uliyomalizika kwa kufungwa mabao 2-0 dhidi ya vinara hao wa ligi kuu soka Tanzania Bara.

Membe na Lowassa Uso kwa Uso Nyumbani kwa Gwajima

$
0
0
 Membe na Lowassa Uso kwa Uso Nyumbani kwa Gwajima
Waziri Mkuu Mstaafu na Mjumbe wa Kamati Kuu ya CHADEMA, Edward Lowassa akiteta na Waziri wa Mambo ya Nje wa zamani, Bernard Membe walipokutana leo katika msiba wa mama mzazi wa Askofu Josephat Gwajima nyumbani kwake Salasala.

Lowassa, Mbunge wa Vunjo, James Mbatia, Mbunge wa Arusha mjini, Godbless Lema na Bernard Membe kwenye msiba wa mama mzazi wa Askofu Gwajima.

WAZIRI Mkuu wa zamani na Mjumbe wa Kamati Kuu ya CHADEMA, Edward Lowassa wamekutana na kuzungumza na Waziri wa Mambo ya Nje wa zamani, Bernard Membe leo katika msiba wa mama mzazi wa Askofu Josephat Gwajima nyumbani kwake Salasala jijini Dar es Salaam.

Mwigulu Apiga Stop Utoaji wa Pasipoti za Makundi.

$
0
0
 Mwigulu Apiga Stop  Utoaji wa Pasipoti  za Makundi.
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Dk Mwigulu Nchemba amesitisha utoaji wa hati za kusafiria za makundi.

Amesema uamuzi huo unatokana na baadhi ya waombaji wa hati hizo kwa ajili ya kwenda kufanya kazi nje ya nchi kufanyishwa shughuli zingine kinyume cha sheria za nchini.

Dk Nchemba amesema Serikali itaandaa utaratibu mzuri kati ya Tanzania na nchi husika wanakokwenda wahusika ili waandaliwe mazingira mazuri na salama ya kufanyia kazi na kujiridhisha na kile wanachokwenda kufanya.

Akizungumza na waandishi wa habari leo Alhamisi Januari 25,2018 Dk Nchemba amesema baadhi ya matendo yanayokiuka sheria za nchi wanayofanyiwa ni kazi zisizo na maadili na kuwekwa rehani kutokana na masuala ya dawa za kulevya.

Dk Nchemba pia ameagiza kampuni zinazoingiza makundi ya watu wanaokuja kufanya kazi nchini kuripoti leo kwa  kamishna wa mipaka na vibali.

Agizo hilo amesema linatokana na baadhi ya kampuni hizo kuwatafutia kazi raia wa kigeni na wanapofika nchini hufanya kazi tofauti ikiwemo biashara ya ngono.

Kigwangalla "Nawajua Vigogo Waliopanga Mauaji ya Wayne Lotter"

$
0
0
Kigwangalla Alitega Jeshi la Polisi Awaagiza Kuwakamata Vigogo Wanne Waliopanga Mauaji ya Wayne Lotter
Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Hamisi Kigwangalla amesema anawajua vigogo wanne waliopanga mauaji ya muhamasishaji wa utalii ‘Wayne Lotter’ mwaka jana na kulitaka jeshi la polisi liwakamate watu hao ingawaje hajawataja hadharani.

Akizungumza na Waandishi wa Habari leo mjini Dodoma, Dkt. Kigwangalla amelitaka jeshi hilo lichukue hatua haraka za kuwakamata vigogo hao la sivyo ataenda moja kwa moja kutoa taarifa kwa Amiri jeshi Mkuu.

“Nawajua watu 4 waliopanga mauaji ya mhamasishaji wa utalii Wayne Lotter, watu hao ni vigogo na wanajulikana,“amesema Dkt. Kigwangalla.

Waziri Kigwangalla amesema ndani ya kipindi cha siku 100, Wizara yake imebaini mitandao 74 ya watu wanaojihusisha na ujangili ikiwa na washiriki 949 ambapo amedai baadhi ya washiriki hao tayari wameshafikisha Mahakamani kujibu tuhuma hizo.

Kuhusu kifo cha Mwanaharakati Wayne Lotter soma zaidi kwa kubonyeza link hii “Mwili wa mwanaharakati wa tembo aliyeuawa kwa risasi kuagwa Dar“.

Hakimu Amekataa Kujitoa Kusikiliza Kesi ya Sugu

$
0
0
Hakimu Amekataa Kujitoa Kusikiliza Kesi ya Sugu
Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Mbeya, Michael Mteite amekataa kujitoa kusikiliza kesi inayomkabili mbunge wa Mbeya Mjini, Joseph Mbilinyi maarufu Sugu na mwenzake.

Sugu na Katibu wa Chadema Kanda ya Nyanda za Juu Kusini, Emmanuel Masonga wanashtakiwa kwa kosa la kutumia lugha ya fedheha dhidi ya Rais John Magufuli wanayodaiwa kuitoa Desemba 30,2017.

Awali, leo Alhamisi Januari 25,2018 Sugu na Masonga waliwasilisha ombi mahakamani wakimkataa hakimu huyo wakitaka ajitoe kusikiliza kesi kwa maelezo kuwa hawana imani naye.

Hakimu Mteite amesema sababu zilizotolewa na akina Sugu hazipo kisheria na hazimfanyi kujitoa.

Baada ya hakimu kukataa kujitoa, mawakili Boniface Mwabukusi, Hekima Mwasipu na Sabina Yongo wanaowawakilisha washtakiwa walitangaza kujitoa katika shauri hilo.


Sugu na Masonga wameiomba Mahakama kuwapatia wiki mbili za kutafuta mawakili wengine.

Hakimu Mteite ameahirisha kesi hadi Februari 2,2018  na ameamuru washtakiwa kurejeshwa rumande.

Je Wafahamu Kuwa Kitunguu ni Tiba ya TB?

$
0
0
Je Wafahamu Kuwa Kitunguu  ni Tiba ya TB?
KUNA aina ya vitunguu vinavyotumika katika mapishi, imegunduliwa ina uwezo wa kutibu kifua kikuu (TB) na zingine za aina mbalimbali, utafiti mpya umebaini.

Watafiti wamebaini pia, vimelea na yaliyomo katika vitunguu hivyo, inaweza kuzalisha antibaiotiki inayomudu usugu huo, ingawaje kunahitajika utafiti zaidi.

Aina hiyo ya TB sugu inatajwa takwimu zake mathlan kwa mwaka 2016 pekee yake, iliathiri jumla ya watu 490,000 nchini Uingereza.

Hadi sasa, utafiti huo unaendelea chini ya uratibu wa Chuo Kikuu cha London, Uingereza ulifuatilia kwa kina matumizi wa vitunguu hivyo katika mapishi mbalimbali.

Utafiti umefanywa kwa mara nne tofauti na matokeo ya ripoti zote tofauti, zinaonyesha matokeo chanya, baadhi yakiwa kwa kiwango cha juu asilimia 99.9.

Maoni hayo ya kitaalamu yanaeleza kwamba, tiba hiyo ya kitunguu inaweza kutumiwa sambamba na ile ya kila siku.

Mshiriki katika utafiti huo, Dk. Sanjib Bhakta, ana lake la kuchangia:"Licha ya juhudi za serikali kuzuia kuenea kwa kifua kikuu, ni takriban wagonjwa wapya milioni 10 walipatikana (duniani) katika mwaka 2016.”

Mwanazuoni mwingine, Profesa Simon Gibbons, anasema: "Mazao ya asili na mimea, ina nafasi yake kubwa kama antinbaiotiki. Mazingira ni mkemia mbunifu.”

Anasema mimea hiyo ya asili inazalisha kemikali dhidi ya vijidudu na mazingira.

Mnamo Oktoba Mosi, Mganga Mkuu wa Serikali ya Uingereza, Profesa Dame Davies, alisisitiza kuwa viongozi mbalimbali duniani kuwa mstari wa mbele kupiga vita usugu wa vijidudu dhidi ya dawa za antibaotiki dhidi yao.

Wataalamu wa tiba wanasema kuwa, dawa hizo zinazotajwa kuwa sugu, zinatumiwa na watu wasiopungua 25,000 barani Ulaya, huku Afrika mataifa na shirika yasiyo ya kiserikali na ndio maana wanahisi ugunduzi huo mpya ni hatua inayojitegemea ya mafanikio.

Cilic Atinga Fainali Baada ya Kumchapa Mpinzani Wake Kyle Edmund

$
0
0
Cilic Atinga Fainali Baada ya Kumchapa Mpinzani Wake Kyle Edmund
Mcheza tenisi kutoka nchini Croatia, Marin Cilic amefanikiwa kutinga katika hatua ya fainali baada ya kumchapa mpinzani wake Kyle Edmund katika hatua ya nusu fainali.

Cilic amefanikiwa kutinga katika hatua hiyo kwa ushindi wa seti 6-2 7-6 (7-4) 6-2.

Kutokana na ushindi huo, Cilic anaweza kupanda mpaka nafasi ya tatu katika viwango vya ubora wa mchezo huo duniani vitakavyotoka wiki ijayo.

Kwa sasa mchezaji huyo ana subiri kucheza fainali na mshindi wa mchezo kati ya Roger Federer na Hyeon Chung ambao watachuana kesho (Ijumaa).

Mtoto Abakwa na Kuuawa Kikatili na Dereva ‘Boda Boda’

$
0
0
Mtoto Abakwa na Kuuawa Kikatili na Dereva ‘Boda Boda’
Mtoto wa kike mwenye umri wa miaka 14 ambaye pia ni mwanafunzi ameuawa kikatili baada ya kubakwa na muendesha pikipiki akiwa anaenda shule.



Imeelezwa kuwa Mwanafunzi huyo mwenye umri wa miaka 14 alikuwa anasoma darasa la sita katika shule ya Msingi ya Vikonge iliyopo wilayani Tanganyika mkoani Katavi.

Mwili wa marehemu ulikutwa ukiwa na majeraha ya kisu ubavuni mwake na sehemu zake za siri kunyofolewa .

Kamanda wa Polisi mkoa wa Katavi, Damas Nyanda amethibitisha kutokea kwa tukio hilo juzi Jumanne tarehe 23 Januari 2018 saa moja asubuhi umbali wa kilometa moja na nusu kutoka shuleni kwake.

“Asubuhi hiyo ya tukio, marehemu akiwa ameongozana na mdogo wake wa kiume huku wakielekea shuleni walikutana na mwendesha pikipiki maarufu ‘bodaboda’ ambaye alikuwa hawamfahamu na kuwaambia kwamba atawapa lifti. Marehemu alipopanda mwendesha bodaboda alimzuia mdogo wake wa kiume asipande ambapo aliondoka akiendesha pikipiki hiyo kwa kasi isiyo ya kawaida huku kaka wa marehemu akiikimbilia bila mafaniko.“amesema Kamanda Nyanda.

Kamanda Nyanda amesema kuwa mdogo wa marehemu alitembea kwa miguu kuelekea shuleni baada ya kuchoka kuifukuza pikipiki hiyo, ghafla aliiona pikipiki ile iliyombeba dada yake ikiwa imeegeshwa karibu na kichaka kando ya barabara inayoelekea shuleni kwao na akaipita.

“Kaka wa marehemu bila shaka kutokana na umri wake kuwa bado mdogo baada ya kufika shuleni hakushughulika kumtafuta dada yake, aliingia darasani na kuendelea na masomo kama kawaida na baada ya muda wa masomo yaani saa nane na nusu alianza safari ya kurejea nyumbani bila kumtafuta dada yake,” ameeleza Kamanda Nyanda.

Hata hivyo, baada ya mtoto huyo kufika nyumbani wazazi wake walishtuka kumuona akiwa pekee yake ndipo walipomuhoji alikomuacha dada yake ndipo alipowasimulia kila kitu.

“Wazazi wa marehemu baada ya kupata maelezo hayo walipatwa na mashaka hivyo walimtaka mdogo wa marehemu awapeleke kwenye eneo alipoina pikipiki iliyombeba dada yake ikiwa imepakiwa karibu na kichaka. Mtoto huyo aliwaongoza wazazi wake ambao walikuwa wamefutana na majirani zao hadi kwenye eneo la tukio, walishtuka kuona kuwa kuna nyasi zilikuwa zimelala ndipo walipoona mwili wa marehemu ukiwa umechomwa kisu ubavuni huku sehemu zake za siri zikiwa zimenyofolewa,“amesema Kamanda Nyanda.

Hili sio tukio la kwanza kutokea wilayani humo ambapo mwaka jana mwanafunzi wa Shule ya Msingi Kipanga, Wilayani Tanganyika anayekadiriwa kuwa na umri wa miaka 13 alikutwa amebakwa hadi kufa na mwili wake kutelekezwa vichakani.

Jeshi la Polisi mkoani humo linaendelea na msako mkali kuwabaini wahusika wa tukio hilo ili kuwafikisha kwenye vyombo vya sheria.

Mawakili Watatu wa Sugu Wajitoa

$
0
0
Mawakili Watatu wa Sugu Wajitoa
Mawakili wa utetezi katika kesi inayowakabili Mbunge wa Mbeya Joseph Mbilinyi 'Sugu' na Katibu CHADEMA kanda ya Nyasa Emmanuel Masonga wamejiondoa kutokana na kutokuwa na imani na muenendo wa kesi hiyo na kuwataka watafute Mawakili wengine.


Uamuzi huo wa Mawakili hao watatu ambao ni Boniface Mwabukusi, Hekima Mwasipu na Sabina Yongo umetolewa leo (Alhamisi) baada ya Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Mbeya Michael Mteite, kugoma kujitoa katika usikilizaji wa kesi hiyo kama walivyotaka washtakiwa hao hapo awali kwa madai hawana imani nae.

Aidha, Hakimu Mteite alisema kuwa miongoni mwa sababu za yeye kuendelea na kesi hiyo ni kuwa Mahakama inayojukumu la kutoa dhamana au kutotoa kwa jinsi itakavyoona pia kuhusu ugumu wa kesi hiyo alikua anaamanisha ni kwamba inamvuto huku akidai hataweza kuendesha kesi hiyo kwa kumuogopa mtu kwa maana alikula kiapo.

Hata hivyo Wakili wa Jamhuri Joseph Pande aliiambia Mahakama kwamba Mawakili wa utetezi kujitoa kwenye kesi hiyo ni jambo la kawaida kwa kuwa wana sababu zao mbalimbali ambazo hawawezi kuzizungumza licha ya kuwa awali upande wa utetezi walikubali kuendelea na kesi hiyo.

Pamoja na hayo, Sugu na Masonga waliomba Mahakama kutoa (kuwapa) muda wiki mbili ili waweze kutafuta Mawakili wengine wawasimamie kesi yao hiyo kwa sababu wapo rumande hivyo itawachukua muda mrefu kujipanga na kuwatafuta na endapo itashindikana basi watajitetea wenyewe.

Kutokana na ombi hilo Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahamaka ya Hakimu Mkazi Mbeya Michael Mteite aliwakubalia washtakiwa hao  matakwa yao na kuiharisha kesi hadi Februari 8 mwaka huu ambao itasikilizwa kwa mara nyingine.

Kutana na Mtabibu Mwenye KUBRI kutoka kwa ALLAH issa simba said Mtabibu wa Nyota za Binadamu na Dawa za Asili

$
0
0

Kutana na Mtabibu Mwenye KUBRI kutoka kwa ALLAH issa simba said Mtabibu wa Nyota za Binadamu na Dawa za Asili ya Africa Mwenye UWEZO Kubaini tatizo lako Pindi tu Utakapo Fanya Mawasilino Kupitia Wasaa Husika..JE UNASUMBULIWA NA Mapenzi? (Umeachwa na Umpendae,Awe Mume,Mke na Bado unampenda?Na Umejaribu Sehemu nyingi Bila Mafanikio?Wasilina na Maalim Hussein Ujione muujiza wa Papo kwa Papo.. anauwezo WA KURUDISHA MAHUSIANO NA KUIMARISHA NDOA YAKO NDANI YA SAA 12 TU. Umekimbiwa na Mumeo,mkeo au Mpenzi na anaishi na mtu mwingine? Muone akutatulie Anauwezo wa Hali ya Juu wa Kusambalatisha Mahusiano yao Endapo utafata Atakacho kuelekeza.
Atamfanya Atimize Ahadi zote kwa Muda Mfupi.

Issa simba said Anatumia Jina la Muhusika au Picha Kumaliza Tatizo lako..
Anatibu kwa Kutumia Vitabu vya QUR-AN Dawa za Asili za Africa,Dawa za Kiarabu na Majini.Anatafsiri Ndoto. Kushinda BAHATI NASIBU, KUSAFISHA NYOTA. Mvuto wa Mwili na BIASHARA, Kinga ya Mwili,ZINDIKO za Nyumba.MIGUU Kufa GANZI.Kufungua KIZAZI kwa wale walio fungwa kwa njia za KISHIRIKINA. Anakupa Jini la Mali kwa yule anaehitaji Utajiri BILA MASHARTI. Nguvu za KIUME, Humaliza Kesi zilishindika ndani ya siku 14 tu..na mengi zaidi

Wasiliana nasi  Kwa Numba Hizi +255 622588038 , 0679119679 , +255 764318107, 0656145170, 0762899488

Captain Gardner Ameguswa na Habari za Mchezaji Juma Nyoso

$
0
0
Tukio la juma Nyoso kumpiga shabiki baada ya mchezo wa Kagera Sugar dhidi ya Simba bado limeendelea kuibua mijadala mbalimbali kitaa, wapo ambao wanamlaumu mchezaji huyo kwa tukio hilo lakini kuna upande ambao unataka kujua kwa nini Nyoso alifikia hatua ya kumpiga shabiki kabla adhabu haijatoka.

Mtangazaji wa Clouds FM Gardner G Habash amesema ni vyema kuangalia kwanza nini kilitokea kabla ya Nyoso kumpiga shabiki kabla ya kuanza kumhukumu.

“Hatusemi alichofanya Nyoso ni sawa, lakini tuangalie kitu gani kilimtokea mpaka akafanya lile kosa kwa sababu alipopewa adhabu mara ya kwanza kama tunanakumbuka alikuwa memfanyia vitendo ambavyo si vya kiungwana kwa Bocco, adhabu aliyopewa haikutokna na mazingira ya uwanjkani au ripoti ya mwamuzi adhabu aliyopewa ilitokana na ushahidi wa video na picha ndio TFF wakaifanyia kazi.”

“Adhabu aliyopewa ilikuwa kubwa hadi watu wakalalamika, kwa sababu alifungiwa kucheza soka kwa miaka miwili. Adhabu ilikuwa kubwa sana afadhali wangempiga faini au wangemwambia asicheze tena mpira kwa sababu hata ukienda kwenye kanuni za FIFA sijui kama kuna adhabu za kuzuia wachezaji kucheza kwa muda huo.”

“Baada ya adhabu ya TFF kutoka ikatoka video nyingine ambayo ilikuwa ndefu kidogo kuliko ile ya kwanza iliyotumika kama ushahidi kwa TFF, video hiyo ilikuwa ikionesha chanzo kwa nini nyoso alifanya tendo lile, alitendewa jambo kwanza likamuudhi kabla ya yeye kulipiza. Alikosea kulipiza na alistahili kuadhibiwa lakini sijui kama adhabu ile ndiyo ilikuwa inamstahili, ilipotoka video ya pili Bocco anaonekana anampiga mateke Nyoso kwa kumchoza mbona TFF haikutoa adhabu?”

“Kwa nini wakati ule Nyoso alikaa kimya hakulalamika? Mimi niliwahi kumtafuta akiwa ameshatumikia adhabu kwa miezi sita nikamwambia kata rufaa labda utasikilizwa akaniambia klabu yangu imenikataza kusema chochote wao wapo kwenye mchakato wanaendelea na masuala hayo  lakini hadi miaka miwili ikaisha hakuna mtu aliyemtetea.”

“Miaka miwili baadaye linajitokeza tena jambo kama lile na ninaona kutakuwa na ukimya hakutakuwa na mtu wa kumtetea Nyoso hata angalau kutia shaka kwa nini Nyoso alifanya kitendo kile wengine wanasema yule kijana alimtusi lakini kuna ukimya, jambo la kukamatwa na polisi hatuwezi kulaumu kwa sababu wanafanya kazi yao walimkamata kwa kosa la kumpiga mtu au kupigana hadharani ambapo kwa mujibu wa taratibu za nchi ni kosa.”

Hali si shwari Soka la Majirani Zetu Kenya

$
0
0
Hali si hali nchini Kenya, rais wa shirikisho la soka nchini humo Nick Mwendwa amesema kujiondoka kwa baadhi ya wadhamini waliokuwa wakidhamini shirikisho hilo pamoja na michezo ya ligi kuu kumelifanya soka la nchi hiyo kuanza kuyumba na wasiwasi umetanga kwamba huenda ligi ikasuasua lakini huenda timu ya taifa ikatetereka kwa sababu kama ligi haitochezwa kwa ushindani uliokusudiwa moja kwa moja timu ya taifa itaathirika.

Changamoto hiyo imekwenda mbali kidogo kwa sababu wadhamini wakubwa ambao walikuwa wakitoa kiasi kikubwa cha fedha katika soka la Kenya, kuondoka kwao pia kunaweza kufanya soka likadidimia.

Mwandishi wa habari wa gazeti la The Nation David Kalimwa amezungumzia hali ya mchezo wa soka nchini Kenya baada ya kuondokewa na udhamini wa baadhi ya makampuni.

“Hali ya sintofahamu imelikumba soka la Kenya baada ya kuondokewa na wadhamini wakubwa Sport Pesa kujiondoa katika udhamini pamoja na mashirika mbalimbali ikiwamo vilabu vikuu hapa nchini Kenya AFC Leopard na Gor Mahia pamoja na klabu ya daraja la pili Nakuru All Stars na shirikisho la soka la Kenya Football Kenya Federation (FKF) na wasimamizi wa ligi kuu ya Kenya ambao wote walikuwa wananufaika kwa udhamini wa takribani dola milioni sita za Marekani kwa mwaka sawa na shilingi milioni 600 za Kenya.”

“Sport Pesa wamejiondoka kwenye udhamini kwa sababu serikali ya Kenya imeongeza kodi kwa makampuni yote ya betting, kujitoa kwa Sport Pesa kumeleta shida mbalimbali ambapo wasimamizi wengi wa soka hapa nchini wamesema labda hakuta kuwa na maendeleo ya michezo lakini rais wa FKF Nick Mwendwa ambaye alidai wanafanya mazungumzo na serikali kuona kama itaweza kudhamini michezo hiyo ya ligi bada ya Sport Pesa kujiondoa.”

“Kampuni ya Sport Pesa pia ilikuwa ikilipa mshahara wa kocha mkuu wa Kenya pamoja na mkurugenzi wa ufundi wa FKF kwa hiyo kujiondoa kwa Sport Pesa kunaweza kufanya wawili hao kukosa mishahara.”

Moto Wateketeza Numba ya Makazi

$
0
0
Moto Wateketeza Numba ya Makazi
Watu watano wamenusurika kifo baada ya nyumba wanayoishi kuteketea kwa moto.

Tukio hilo limetokea usiku wa kuamkia leo Alhamisi Januari 25,2018 eneo la Mitondooni wilayani Magharibi B, Unguja.

Chanzo cha moto kinaelezwa kuwa ni hitilafu ya umeme ndani ya nyumba waliyokuwa wakiishi.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mjini Magharibi, Hassan Nassir Ali amesema moto ulitokea saa moja usiku.

Mayasa Makame aliyenusurika katika janga hilo amesema moto ulizuka ghafla walipokuwa wakipika.

Amesema wamepoteza kila kitu kilichokuwamo ndani.

Kuhusu chanzo cha moto imeelezwa huenda ikawa ni hitilafu ya umeme kwenye jokofu.

Mayasa ameiomba Serikali na wananchi kwa jumla kuwasaidia kwa kuwa hawana chochote kwa sasa.

Man City Yakaribia Kunasa Saini ya Beki wa Athletic Bilbao

$
0
0
Man City Yakaribia Kunasa Saini ya Beki wa Athletic Bilbao
Klabu ya Manchester City inakaribia kumsajili beki wa Athletic Bilbao inayoshiriki ligi kuu ya nchini Hispania La Liga, Aymeric Laporte kwa dau la paundi milioni 57.

Meneja wa Man City, Pep Guardiola amevutiwa na kipaji alichonacho beki huyo raia wa Ufaransa mwenye umri wa miaka 23 na hivyo yupo tayari kukabiliana na kipengele cha kumsajili mchezaji huyo.

Dili la kumnasa beki huyo wakati, Laporte linatarajiwa kukamilika kabla ya dirisha la usajili kufungwa siku ya Jumatano.

Endapo City itafanikiwa kukamilisha usajili huo wa paundi milioni 57 itakuwa imevunja rekodi yake baada ya mara ya mwisho kufanya usajili mkubwa ilikuwa ni paundi milioni 55 ilipomnasa Kevin de Bruyne mwaka 2015.

Kiungo huyo wa Ubelgiji, Kevin de Bruyne ambaye amejiunga akitokea Bundesliga katika klabu ya Wolfsburg hivi karibuni ameongeza mkataba wake na City utakao mfanya aendelee kusalia katika timu hiyo mpaka mwaka 2023.

Ambaka Askari Mwenzake Baada ya Kumringishia Uume Mrefu

$
0
0
Ambaka Askari Mwenzake Baada ya Kumringishia Uume Mrefu
ASKARI wa Uingereza aliyewahi kuwa shujaa wa vita nchini Afghanistan, hivi majuzi alimbaka askari mwenzake wa kike baada ya kujigamba kwamba alikuwa na uume mrefu.

Haya yalisema mahakamani ambapo Luteni-Kanali Chris Davies anashitakiwa kwa kumbaka askari ambaye ni mama wa watoto wawili na  umri wa miaka 53 katika tukio linalodaiwa kufanyika huko Kingston, Ontario,  Canada.


Davies anadaiwa kumwambia mwanamke huyo kwamba: “Nina uume wenye urefu wa inchi nane (sentimita 20.3) ambao unaweza kuubomoa ulimwengu wako.”  Jina na utambulisho wa mwanamke huyo vimehifadhiwa.

Mwanamme huyo anadaiwa alimfuata mwanamke huyo hadi hotelini kwake baada ya mwanamkehuyo ‘kubugia’ pombe mbalimbali za kutosha walipokuwa askari hao na wenzao wakinywa vileo.


Davies na mwanamke mwathirika walikuwa sehemu ya kundi la askari waliokuwa wakinywa vileo baada ya gwaride maalum kwenye kambi ya kijeshi ya Fort Frontenac (pichani).

Kwa mujibu wa gazeti la The Sun, Davies alimwuliza mwanamke huyo: “Je, tukajaribu?”  Hii ni baada ya kujigamba kwamba kuhusu uume wake, jambo lililomfanya mwanamke huyo aondoke sehemu hiyo.



Mwanamke huyo aliripoti tukio hilo polisi mjini Kingston, Ontario, nchini Canada ambapo askari hao walikuwa wameungana na wale wa Canada kuadhimisha Mapigano ya Tuta (Ridge) la Vimy katika Vita Kuu ya Kwanza ya Dunia.

Lord Eyes Amefunguka Kuhusu Kuacha Muziki "Nimejaribu Kuacha Muziki Nimeshindwa"

$
0
0
Lord Eyes Amefunguka Kuhusu Kuacha Muziki "Nimejaribu Kuacha Muziki Nimeshindwa"
Msanii wa hip hop Bongo, Lord Eyes amefunguka kuhusu kuacha muziki na kufanya mambo mengine.

Rapper huyo ameiambia Funiko Base ya Radio Five kuwa hana mpango wa kuacha muziki kwa sasa ila ni kitu ambacho amewahi kujaribu.

“Nina albamu mbili halafu hata moja haikwenda sokoni lakini bado narekodi, sichoki kurekodi am keeping recording ndio maana nawahaidi watu Load Eyes hawezi kuacha muziki,” amesema.

“Hata mimi nimejaribu kuacha muziki nimeshindwa kwa sababu muziki ni maisha yangu hata nikitaka kuacha nashindwa kwa sababu watu wananisumbua kuhusu muziki,” amesisitiza.

Loard Eyes kwa sasa anatamba na ngoma ‘Hardcore’ ambayo wamefanya kundi la Nako 2 Nako.
Viewing all 104780 articles
Browse latest View live




Latest Images