Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104709 articles
Browse latest View live

Picha: Neymar Atembea na Mkanda wa tiba Kiunoni akiwa na Mpenzi Wake

$
0
0
Hali ya Jeraha la mshambuliaji wa Barcelona Neymar kufuatia kugongwa kwa nyuma wakati wa fainali ya kombe la dunia na kupelekea kufanyiwa upasuaji wa mgongo sasa anaendelea vizuri ambapo amenza kula bata taratibu kwa kutoka na mpenzi wake Bruna Marquezine fukweni nchini Hispania.

Wapenzi hao wamekuwa wakivinjari fukweni Formantera ambapo Neymar amekamilikisha siku za kuendelea kutembea na kitu kilichokuwa kinampa msaada wa mgongo (yaani Back-Support).

Neymar hakucheza michezo miwili ya mwisho ya timu yake ya taifa katika michuano ya kombe la dunia kufuatia kupata kuumia vibaya mgongoni katika mchezo wa robo fainali dhidi ya Colombia.


Jokate Ajipanga Kujitambulisha Rasmi kama Mwanamuziki Kupitia Kampuni Yake

$
0
0
Ndoto ya kufanya muziki kwa asilimia 100 haijayeyuka, bado ipo kichwani mwa Jokate Mwegelo.
Baada ya kushirikiana na Lucci kwenye Kaka Dada, mrembo huyo amedai kuwa mpango uliopo ni yeye kujitambulisha rasmi kama mwanamuziki kupitia kampuni yake.

“Sasa hivi nataka nijiintroduce kama mimi as a music artist,” Jokate alikiambia kipindi cha Mambo Mseto cha Radio Citizen ya Kenya ambako alienda kikazi.

“Kwahiyo niwe na single zangu mwenyewe ambazo nazifanyia kazi kupitia kampuni yangu mwenyewe, that’s the way forward.

Kisa cha Beyonce na Jay Z kususia harusi ya Kimye chabainika

$
0
0
Kitendo cha Beyonce na Jay Z kutohudhuria harusi ya Kanye West na Kim Kardashian kiliwashtua wengi kutokana na ukaribu wao.

Na sasa ripoti mpya zinadai kuwa Beyonce na Jay Z waliamua kuitosa harusi hiyo kwakuwa Queen Bey hakutaka kufunikwa na bibi harusi, Kim. Chanzo cha karibu kimeiambia safu ya Page Six ya gazeti la New York Post kuwa wanandao hao waliichukulia harusi ya Kimye kuwa si ya hadhi yao.

“Beyoncé hakutaka kuruhusu Kardashian amemzidi umaarufu. Na Jay hakutaka uwepo Kanye na Kim – anadhani ni mbaya kwa biashara. Nadhani Jay amepoteza heshima Kanye hapo.”

Aibu Kubwa Uhamiaji: Uchakachuaji wa matokeo ya usaili wa nafasi za koplo na konstebo

$
0
0
Matokeo ya Usaili wa nafasi za Konstebo wa Uhamiaji yaliyotolewa katika magazeti ya tarehe 23 Julai, 2014 yameonesha kuwa katika Idara hiyo watanzania wengine mbali ya watoto au ndugu wa wafanyakazi wa Idara hiyo hawawezi kupata ajiya ndani ya Idara hiyo ya Serikali. Majina ya wengi walioitwa kazini ni watoto au ndugu wa wafanyakazi wa idara hiyo.

Abdulhaq Amin Mandemla – Mtoto wa afisa Uhamiaji Amin Mandemla
Alphonce Kishe – Mtoto wa Afisa Uhamiaji Aleluya Kishe
Asha Burhani Idd – Ndugu ya Afisa Uhamiaji Tatu Burhani Idd
Beatrice Temba – Ndugu wa Afisa Uhamiaji Joseph Kasike
Geofrey Justine Mhagama – Ndugu ya Afisa Uhamiaji Rose Mhagama
Iginga Daniel Mgendi – Mtoto wa Afisa Uhamiaji Daniel Mgendi
Issack Michael Makwinya – mtoto wa aliyekuwa Afisa Uhamiaji Makwinya
John Alfred Mungulu – mtoto wa Afisa Uhamiaji Alfred Mungulu
Joseph A. Milambo - mtoto wa Karani wa Uhamiaji Milambo
Michael J. Choma – mtoto wa Afisa Uhamiaji John Choma
Shimba H Zakayo – mtoto wa Afisa Uhamiaji Zakayo Mchele
Upendo E. Mgonja - mtoto wa Afisa Uhamiaji Mgonja
Vaileth A. Kidesu – mtoto wa Afisa Uhamiaji Adam Kidesu
Elizabeth Edward – Ndugu wa Afisa Uhamiaji Edward Martin
Ester Mahirane – Ndugu wa Afisa Uhamiaji Mahirane
Basil Lucian John – Ndugu wa Afisa Uhamiaji Dismas Lucian
Frank E Kajura- Ndugu wa Afisa Uhamiaji Kajura
Jacob P. Ulungi – Ndugu wa Afisa Uhamiaji Magnus Ulungi
Janeth John Milinga – Ndugu wa aliyekuwa Afisa Uhamiaji Milinga
Janeth R Lukuwi – Ndugu wa Afisa Uhamiaji Eliza Lukuwi
Joseph N. Yondani – Mtoto wa Afisa Uhamiaji Mary Yondani
Leila khatib Irovya - Mtoto wa Afisa Uhamiaji Abbas Irovya
Lucian F. Mlula – ndugu wa Afisa Uhamiaji Dismas Mlula
Neema Kasian Lukosi- Ndugu wa Afisa Uhamiaji Zubeda Abbas
Pendo D. Gambadu – ndugu wa Afisa Uhamiaji Gambadu
Paschalia E. Mwenda – ndugu wa Martin Edward mwenda
Theresia Ernest Kalunde – Mtoto wa Ernest Kalunde
Veronica G Vitalis – Mtoto wa aliyekuwa Afisa Uhamiaji Vitalis Mlay
Victor G. Mlay- Mtoto wa aliyekuwa Afisa Uhamiaji Vitalis Mlay
Catherine J. Mapunda- mtoto wa Afisa Lucy Mapunda

Hii ni sampuli tu yaani nimeorodhesha moja ya tatu tu kwani zaidi ya asilimia tisini ni watoto na ndugu wa Maafisa Uhamiaji.
Nadhani ingekuwa vyema wasingekuwa wanatangaza nafasi hizi bali wawe wanagawiana ndani kwa ndani.
Alamsiki.

Wanawake Watumia MikorogoI na Wavulana Wavaa Milegezo Kutimuliwa Mashuleni

$
0
0
Shule ya Sekondari Mwadui iliyopo wilayani Kishapu mkoani Shinyanga, imetangaza kufukuza wanafunzi wote wanaotumia vipodozi, wanaovaa sketi fupi, milegezo na wanaotumia simu za mkononi shuleni.

Mwalimu Mkuu wa shule hiyo inayomilikiwa na Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Dayosisi ya Kusini Mashariki ya Ziwa Victoria, Mchungaji Yohana Nzelu, alisema hayo jana katika kikao cha Bodi ya Shule na Wazazi.

Mwalimu Nzelu alisema moja ya chachu ya mafanikio ya wanafunzi shuleni, ni nidhamu ya kutosha na maadili mema na kuongeza kuwa Bodi hiyo ilikaa na kujadili namna ya kuongeza ufaulu kwa wanafunzi wake na kuweka mikakati, ikiwemo hatua hizo.

Akisoma taarifa kwa wazazi na walezi wa wanafunzi walio katika shule hiyo, Mwalimu Nzelu alisema hatua hizo zinalenga kuzuia wanafunzi kujiingiza katika makundi mabaya na kuboresha taaluma.

‘’Shule hii katika matokeo ya Mtihani wa Taifa wa Kidato cha Nne mwaka 2012, wanafunzi 61 waliopata daraja la kwanza mpaka la tatu na mwanafunzi mmoja alichaguliwa kwenda kidato cha tano.

‘’Mwaka jana (2013) wanafunzi 76 walifanya mtihani wa kidato cha nne, waliopata daraja la kwanza mpaka la tatu 33, waliochaguliwa na Serikali kujiunga kidato cha tano wanafunzi 24, na waliokwenda shule binafsi walikuwa saba.

 “Tumepiga hatua hivyo mikakati iliyopo ni kusisitiza maadili na kuondoa changamoto zilizokuwepo za wanafunzi kukosa nidhamu,“ alieleza Mwalimu Nzelu.

Akizungumza kwenye kikao hicho, Askofu Mkuu wa KKKT  Dayosisi hiyo, Emmanuel Makala, ambaye ndiye msimamizi wa shule hiyo, alisema suala hilo si la kupuuzwa na hawatakuwa na msamaha kwa mwanafuzi atakayekiuka sheria hizo huku akitoa mwito kwa wazazi na walezi kushirikiana kwa pamoja.

Askofu Makala alisema wazazi na walezi wakishirikiana ipasavyo na walimu kwa kufuatilia taarifa za watoto wao shuleni, itasaidia kwa kiwango kikubwa kuongeza taaluma ya wanafunzi na kupata ufaulu mzuri.

Madai ya undugu kwenye ajira: Uhamiaji wasitisha kupisha uchunguzi

$
0
0
Kimenuka uhamiaji Baada ya Maafisa kuajiri ndugu zao , Ajiri zimesitishwa Kupisha Uchunguzi ..Soma hapa Chini:


Mke wa Kingwendu Abakwa.

$
0
0
MKE  wa  Kingwendu  ambaye  ni  muigizaji  maarufu  wa  filamu  za  vichekesho  nchini  amefanyiwa  kitendo  kibaya  cha  ubakaji  na  mwanaume  aliyefahamika  kama  Upunguvuku  katika  pagala  moja  huko  Mbagala  Kingugi  kwa  Kisauti.

Mke  wa  Kingwendu  anayejulikana  zaidi  kwa  jina  la  mama  Maua, alikutwa  na  masahibu  hayo  Alhamisi  iliyopita  baada  ya  kuvamiwa  na  Upunguvuku  anayedaiwa  kuwa  alikuwa  amelewa  na  kuingizwa  kwenye  jumba  ambalo halijasha  kujengwa  lililopo  maeneo  ya  Kwa  Dunga    ambapo  wapita  njia  waliwafuma  na  kuanzisha  mtiti.....

Shuhuda  wa  tukio  hilo  ambaye  hakutaka  jina  lake  liandikwe  amesema  kuwa, wakati  tukio  hilo  linatokea, Kingwendu  mwenyewe  alikuwa  safarini  na  hivyo  majirani  zake  ndio  waliomuokoa  mkewe.

Hata  hivyo  baadhi  ya  majirani  walioongea  na  mwandishi  wamedai  kuwa  wawili  hao ( Upunguvuku  na  mama  Maua)  ni  wapenzi  wa  siku  nyingi  na  wamekuwa  wakionekana  mara  kadhaa  wakienda  kunywa  pombe  za  kienyeji.

"Huyu  Upunguvuku  ni  fundi  Mwashi, tunamfahamu  vizuri  kuwa  ni  hawara  wa  mama  Maua, mara  kadhaa  huwa  tunawaona  wakinywa  pombe  za  kienyeji  pamoja, sema  tu  leo  wamefumwa  wakijivinjari  ndo  mwanamke  anamsingizia  eti  kambaka," alisema  shuhuda  mmoja.

Juhudi  za  kumpata  Kingwendu  kuongelea  mkasa  huo  hazikuzaaa  matunda  kutokana  na  simu  yake  kutopatikana  kila  akipigiwa.

Wema Afunguka Kuhusu Ushindi wa Tuzo Alizopata Diamond

$
0
0
Shemeji Wema Sepetu afunguka Baada ya Diamond Kushinda Tuzo za Afrima


Utafiti: Kufanya kazi zaidi ya saa nane kwa siku ofisini kunavyoweza 'kukuua'

$
0
0

Je, wewe ni mchapakazi sana, wa kwanza kufika ofisini na kuwa busy na pia wa mwisho kutoka ukikabiliana majukumu yanayozidi saa za kawaida za kazi? Hongera kwa uchapakazi lakini utafiti huu unaweza kukufanya ubadili ratiba yako.

Tafiti nyingi zilizofanywa zimekuwa zikionesha madhara makubwa kwa watu wanaofanya kazi ofisini kwa muda mrefu zaidi, utafiti uliofanywa mwishoni mwa mwaka 2012 na kuchapishwa kwenye American Jounal of Epidemiology na kutolewa na mtandao wa Forbes, unaonesha kuwa mkusanyiko wa msongo wa mawazo (stress), shinikizo la damu (pressure), kutokuwa na hamu ya kula mlo kamili kunaweza kuwa kati ya sababu zaidi ya elfu moja zinaweza kusababisha matatizo makubwa ya afya.

Utafiti huo umebeba pia matokeo ya tafiti mbalimbali zilizofanywa katika miaka 50 iliyopita na kuonesha kuwa kufanya kazi kwa muda mrefu zaidi ofisini kunaweza kusababisha uwezekano wa kuugua magojwa ya moyo kwa asilimia kati ya 40 na 80 ukilinganisha na mtu anaefanya kazi chini ya saa tisa kwa siku.

Tabia hii inaelezwa kusababisha pia tatizo la kumbukumbu hasa unapokuwa na umri mkubwa, hupunguza nafasi ya ubunifu wa hali ya juu na hupunguza uwezo wa kufanya maamuzi haraka kwa siku za usoni.

Dr. Marianna Virtanen na timu yake ya wafanya utafiti walikusanya data kutoka kwenye vyanzo vya tafiti 12 zilizowahi kufanyika tangu mwaka 1958, na walieleza kuwa watafiti wengi waligundua kuwa watu wanaofanya kazi muda mrefu zaidi kwa siku (zaidi ya saa nane) walikuwa katika hatari zaidi ya kuugua magonjwa ya moyo.

Katika utafiti wake, Dr Mariana aliwafanyia majaribio watu zaidi ya 22,000 kutoka Uingereza, Marekani, Japan, Sweden, Finland, Denmark na Netherlands.

Alisisitiza kuwa moja kati ya tatizo kubwa zaidi kwa wengi ni msongo wa mawazo wa muda mrefu, pia kukosa muda mzuri wa kufanya mazoezi ya viungo na zaidi wengi huwa hawana tabia ya kula vizuri kwa muda.

Inabidi ujiulize kama unafanya kazi muda mrefu, angalia pia matokeo ya harakaharaka yanayotokana na tabia hiyo. Utagundua afya yako huwa inakuwa hatarini ingawa unaingiza pesa nyingi au unakamilisha majumu kwa ubora uliotukuka.

Eid Mubarak!

Kituko kingine alichofanya Balotelli uwanjani hiki hapa

$
0
0
Baada ya kukaa kimya kwa muda mfupi, staa wa soka asiyeisha vituko Mario Balotelli amerudi tena kwenye ‘headlines’ za vyombo vya habari ulimwenguni.
Balotelli ambaye kwa sasa yupo nchini Marekani akijiandaa na msimu mpya kwa pamoja na wachezaji wenzie wa klabu ya AC Milan, jana wakiwa kwenye mechi ya pre season dhidi ya Manchester City, Balotelli akafanya kituko kingine kilichowaacha watu midomo wazi.
Wakati mchezo ukiwa unaendelea mashabiki wawili wa AC Milan waliingia uwanjani na kwenda moja kwa moja kumvamia Mario Balotelli, huku walinzi wakiwa wanawakimbiza kwa nyuma, mashabiki hao wawili walitoa simu na kumuomba Balotelli kupiga nae picha

Balotelli alionyesha kufurahishwa na hilo suala na kutoa ushirikiano kwa mashabiki hao kwa kupozi nao na kupiga ‘selfie’ – kitendo ambacho kiliibua shangwe za kutosha kutoka mashabiki wengine waliojazana kwenye uwanja wa Pittsburgh.
Mchezo huo uliisha kwa Manchester City kuifunga AC Milan 5-1.

Habari Kuhusu Hamisa Mabeto Kuvalishwa Pete ya Uchumba Tarehe 2 Aug Excape1

$
0
0
Wanasema kimya kingi kina mshondo baada ya kudaiwa, hapo mwanzo ilidaiwa kua  Hamisa Mobeto alikua akichepuka na Bwana Almas aka Dangote aka Diamond au Chibu kama mwenyewe anavyopenda kujiita. Lakini baada ikaja kujulikana kua yalikua ni maneno ya wabongo.

Habari za kuaminika Bongoclan ilizozipata ni kua kwa sasa Mwanadada Hamisa kazama kabisa kwenye penzi zito la Seth De Jesus Giovan almaarufu kama Bikira wa kisukuma. Mmoja wa mashostito wa wapenzi hao ambaye hakupenda jina lake litajwe alisema kua Hamisa keshatambulishwa nyumbani kwao na Bikira na kilichobaki ni tukio la kuvishana pete ndo lililobakia.

Team yetu iliamua kufatilia kama ni kuna ukweli  kuhusiana na ishu ya kuvishana pete kwa wapenzi hao na kugundua ni kweli kua watavishana pete tarehe 2 ya mwezi wa 8 ndani ya Escape 1 ambako pia ndani ya siku hiyo kutakua na Instagram Party.

Kupitia akaunti yake bikira wa kisukuma alifunguka haya kuhusiana na tukio hilo " Mungu anipe nini mie...Nimeokota Embe Dodo vhini ya Mpera..I cant wait tarehe 2 pale ESCAPE 1.. Asante Mungu kwa kuileta INSTAGRAM maana nisingempata huyu na kudolishia watu hapa... Nakupenda we mtoto kuliko Ng'ombe anavyopenda majani,Nakuhusudu kuliko Mngoni anavyopenda ngono,Nakuthamini kama Mchungaji anavyoithamini Biblia... I cant wait to engage you pale jukwaani mbele ya halaiki maelfu TAREHE 2...Kama Chibu kaweza kwanini mie nishindwe...Niko tayari kuwa bwege juu yako hamisa wangu,Sitakuwa na wivu wala SitakuSPY kama mme wa yule dada nanii yule mtangazaji,Msukuma nimezama kwako @hamisamobeto DONT MISS MY ENGAGEMENT PARTY kwenye INSTAGRAM PARTY TAREHE 2...iam excited..Nikipigwa kibuti ntalia balaa ntafunga akaunti wallah"

Pia inadaiwa kua Hamisa amewaalika mastar mbalimbali ambao watahudhuria tukio hilo wakiwemo Diamond akisindikizwa na Wema,  Adam Mchomvu, William Malecela, Jerry Slaa na wengine kibao huku burudani ikitolewa na Skylight Band.
Kiingili siku hiyo itakua ni elfu 10 tu huku mambo yakianza mapema kuanzia saa1 ya usiku.
Unakaribishwa Kusoma habari za udaku na za siasa kila siku, usikubali kupitwa, like page yetu ya swahilitz katika facebook na pia usisahau kutufollow katika instagra @swahilitz vile vile katika twitter @swahilitz1. unakaribishwa kutoa maoni yako hapo chini.

Picha Tatu za Bahati Bukuku akiwa Hospitalini baada ya kupata Ajali mbaya ya Gari

$
0
0
Nyota wa nyimbo za Injili Bongo, Bahati Lusako Bukuku ameumia mgongo na maeneo kadhaa ya mwili (nusu kifo) kiasi cha kushindwa kukaa, kusimama wala kutembea kufuatia ajali mbaya ya gari iliyotokea kwenye eneo la Ranchi ya Narco wilayani Kongwa, Dodoma saa tisa usiku wa kuamkia Jumamosi.Katika ajali hiyo ambayo Bahati alikuwa akienda Kahama, Shinyanga kwenye mkutano wa Injili, dereva wa gari alilokuwa akisafiria aina ya Toyota Nadia lenye namba za usajili IT 7945, Edison Mwakabungu ‘Eddy’ (31) aliumia sana kwenye vidole vya miguu na hawezi kutembea.

Wengine waliokuwemo kwenye ajali hiyo ni wacheza shoo wa Bahati, Frank Muha (20) na mwenzake ambaye jina lake halikupatikana mara moja.

Alfajiri ya juzi, mwandishi wa habari hizi alimpigia simu Bahati na kuongea naye kuhusu ajali hiyo ambapo huku akisikika kama anayepata tabu kwa maumivu, alisema:

“Ni kweli tumepata ajali, nimeumia mgongoni, dereva ameumia mguu. Namshukuru Mungu. Sijui nini kilitokea, nilishtukia kuona gari kubwa mbele yetu likituvaa, mara nikashtukia tuko porini. Lakini kabla ya safari Dar tulifanya maombi makubwa, najua Mungu ametunusuru na kifo kibaya,” alisema Bahati.

Kumbukumbu zinaonesha kuwa hii si mara ya kwanza kuripotiwa kwa ajali za magari mkoani Dodoma zikiwahusisha watu wa tasnia Injili Bongo.

Aprili, mwaka huu, Mkurugenzi wa Kampuni ya Msama Promotion, Alex Msama alipata ajali mbaya ya gari kwa kugongana na mwendesha bodaboda.Ajali hiyo ilitokea maeneo ya Ipagala Mwisho, kilomita chache kabla ya kufika mjini Dodoma. Msama alikuwa kwenye gari lake aina ya Toyota Mark II GX 100.


Katika ajali hiyo, Msama na mwendesha bodaboda huyo waliumia sehemu mbalimbali za mwili na kukimbizwa Hospitali ya Mkoa wa Dodoma kwa matibabu.
Kabla ajali ya Msama haijapoa, Mei, mwaka huu, Edson Mwasabwite naye alipata ajali kwenye Barabara Kuu ya  Dodoma–Morogoro. Alikuwa akitoka Dodoma kurudi Dar. Alinusurika.

Sakata la viungo vya maiti vilivyotupwa…..Dk Slaa Amtaka Waziri wa Afya AJIUZULU

$
0
0
Katibu Mkuu wa Chadema, Dk Willbrod Slaa amemtaka Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Dk Seif Rashid kujiuzulu kutokana na sakata la utupaji viungo vya binadamu katika Bonde la Mto Mpiji, Dar es Salaam. 

Akizungumza katika hafla ya kuuaga uongozi wa Chama cha Wanafunzi wa Vyuo Vikuu wa Chadema (Chaso) na kufungua Tawi la Chuo Kikuu cha Sayansi ya Afya na Tiba Muhimbili (Muhas) jana, Dk Slaa alisema utupaji wa viungo hivyo ni udhalilishaji mkubwa wa binadamu na kwamba Serikali inatakiwa kuwajibika moja kwa moja.

Inashangaza kuona miguu, mikono, pua vinatupwa dampo na Serikali na viongozi wake bado wamesimama. Halafu unafunga hospitali ili umuathiri nani? Si unawaathiri wanafunzi wa chuo hicho wanaoitumia kujifunza?” alisema na kuongeza:

Nilitarajia waziri angejiuzulu tangu siku ya kwanza baada ya kubainika vile viungo na asingejiuzulu basi Rais Jakaya Kikwete amfukuze kazi.”

Dk Slaa alisema Serikali imelegalega katika udhibiti wa viungo vya binadamu ambavyo hutumiwa na madaktari kujifunzia kwa kukosa sheria madhubuti ya kudhibiti taratibu za matumizi yake.

Niambieni kama kuna sheria ya kuharibu miili ya binadamu hapa nchini na hivyo viungo vinavyoingizwa kutoka nchi za nje vinaongozwa na sheria gani? Huwezi  kuwa na madaktari halafu huna sheria,” alisema Dk Slaa.

Mapema wiki iliyopita viliokotwa viungo vya binadamu katika bonde hilo vikiwa katika mifuko myeusi na baadaye vilibainika kuwa vilitoka katika Chuo Kikuu cha Kimataifa cha Tiba na Teknolojia (IMTU).

Tayari viongozi wanane wa chuo hicho wamekamatwa na Polisi na Serikali imeunda timu ya wataalamu kuchunguza na mwishoni wa wiki iliifungia Hospitali ya IMTU kwa kukosa sifa ya kutoa huduma za matibabu.

Akisoma risala kwa niaba ya uongozi wa Chaso-Muhas unaomaliza muda wake, mwenyekiti mstaafu wa tawi hilo, Elias Mwakapimba alisema wanakabiliwa na changamoto za uhaba wa vifaa vya kusomea, upendeleo wa ajira na kuzuiwa kufanya siasa chuoni.

Pia, wanafunzi hao waliiomba Serikali iongeze bajeti katika sekta ya afya ili iliweze kuzalisha wataalamu wengi na kuwapa motisha ya kufanya kazi kwa ufanisi.

Mwenyekiti wa Chadema Kanda ya Mashariki na Pwani, Profesa Abdallah Safari aliwataka wanafunzi hao kusimamia harakati za mapinduzi ya kisiasa na kuwataka wasiogope vitisho vinavyotolewa na CCM.

Kazi ya wasomi ni kujitoa muhanga ili kuwakomboa wanyonge wengi… lazima msimame imara msiyumbishwe na mabwanyenye wanaotaka kuyumbisha harakati zenu,” alisema Profesa Safari.

Tundu Lissu: Wachungaji, Maaskofu na Masheikh ni Wala Rushwa.

$
0
0
Wakati akichangia katika mdahalo wa ‘Nani anataka kuwazuia Watanzania kupata katiba mpya, jijini Dar es Salaam na kurushwa na kituo cha ITV, Gazeti la Nipashe limemnukuu Mbunge wa Singida Mashariki (Chadema), Tundu Lissu, akisema baadhi ya Maaskofu na Masheik nchini ni viongozi wanaopewa chakula, vinywaji na pesa kama rushwa. 

Lissu alinukuliwa akisema, “Akina Sheikh Jongo (Thabit Norman) na Jongo mwenzake (Hamid Masoud), Askofu Muhagachi (Amos), Askofu Mtetemela (Donald) na Mchungaji Mgimwa wapo 166 wote hawa ni wana CCM na wameteuliwa na Mwenyekiti wa CCM, wanaitwa kwa Waziri Mkuu, kwa mawaziri wanapewa hela, wanapewa chakula, vinywaji maana yake ni wala rushwa …”.

Ukiyasikiliza na kusoma madai ya Tundu Lissu bila kuyachambua kimantiki unaweza ukadhani ni mambo ya kawaida kisiasa lakini kiuhalisia ni madai ambayo yanagusa taasisi na viongozi ambao uongozi wao unagusa misingi ya kiroho kwa wananchi ambayo hukumu yake haifanywi na binadamu bali na Mwenyezi Mungu. Viongozi wa Taasisi za kiroho ni wajumbe wa Mwenyezi Mungu.

Heshima na utu wa taasisi za kidini nchini ambazo zilipeleka viongozi wake kwenye Bunge la Katiba ambao leo wanaodaiwa na Tundu Lissu kuwa ni wala rushwa, lazima ziheshimiwe kwa njia ya kumtaka Tundu Lissu atoe pia ushahidi wa madai yake.

Kwa lugha nyingine, Tundu Lissu anadai taasisi za kidini (kiroho) zimejaa wala rushwa!. Really? 

I believe these are extremely serious allegations and needs solid evidence. Madai ya Tundu Lissu hayawezi yakapita bila kupata majibu ya uhakika.

Alex Massawe Anayetafutwa na Polisi Aonyesha Jeuri ya Pesa Alizonazo Huko South Afrika

$
0
0
WAKATI akisakwa kwa udi na uvumba na serikali ya Tanzania ili kuunganishwa katika kesi ya mauaji jijini Dar es Salaam, mfanyabiashara maarufu nchini, Alex Massawe anadaiwa kufanya jeuri ye fedha nchini Afrika Kusini ‘Sauzi’.

Katika video iliyowekwa katika mtandao mmoja wa internet na kurushiwa kwenye gazeti hili juzi, inamuonesha mtu anayedaiwa kuwa ni mfanyabiashara huyo akiwa na afya njema, akiwa na kijana mmoja aliyekuwa akimsifia mzee huyo kwa kumiliki fedha nyingi na gari la kifahari la kutembelea aina ya Toyota Lexus.

Video Hapa:

Kijana huyo aliyejitambulisha kwa jina la Floyd akitamba kuwa jina lake lingine la utani ni ATM Mashine, anasikika akimpamba mfanyabiashara huyo kuwa hana shida na fedha, kwani gari alilokuwa akiliendesha pekee lina thamani ya Dola za Marekani 120,000 (karibu shilingi milioni 200 za Tanzania).

SIKIA MAELEZO YA KIJANA
Huku wakiwa ndani ya gari moja, kijana huyo anasikika akisema: “Hi guys, huyu hapa ni Mr. Alex Massawe, anaendesha gari lenye thamani ya dola 120,000 za Marekani na hapa ana pesa anazokwenda kufanya ‘shopping’ pale Mike Ranger Mall. Ni fedha ndogo sana kwake.

Ni za kununulia nguo na viatu tu,” anasema kijana huyo mdogo huku video ikimuonesha mfanyabiashara huyo aliyewahi kutangazwa kuwa ni bilionea, akitoa burungutu la dola katika mfuko wa koti.

MWONEKANO WAKE
Katika video hiyo, mtu huyo anaonekana  akiwa amevaa suti nyeusi, kofia nyeusi, miwani, pete kwenye vidole vya mkono wa kushoto na akiashiria kujiamini kupita kiasi.

NJIANI KUPONDA RAHA
Aidha, kijana anayemsifia ambaye pia amejitambulisha kwa jina la Half a Billionaire Man, aliendelea kusema kuwa walikuwa njiani kuelekea kuponda raha, hasa kwa vile siku hiyo ilikuwa ni Jumapili.
Mkononi kijana huyo akaonekana ameshika dola alizopewa na mtu huyo na akasema ni 15,000 (kama shilingi milioni 25).

“Hatuna shida na fedha, tunazo na tunatumia bila wasiwasi, tunaendesha magari mazuri kama hili unaloliona, Lexus na Guchi,” aliendelea kutamba kijana huyo huku mtu huyo akiwa anaendesha gari lake kwa utulivu bila kusema neno.

WADAU WASEMA NI DHARAU
Baadhi ya wadau katika maoni yao walisema kama kweli mtu huyo ni Alex Massawe ni dharau kwa mamlaka zinazohusika nchini kwa vile mtu huyo anaonekana hana hofu yoyote huku serikali ya Tanzania ikimsaka na ni vigumu kumkamata  .“Kama kweli inamsaka, mbona anatanua bila wasiwasi wowote ule jamani?” alihoji mdau mmoja.

AMETENGENEZWA?
Baadhi ya watu walitilia shaka kuwa, huenda video hiyo ilitengenezwa lakini Uwazi iliipeleka kwa wataalam wa kompyuta IT ambao walipoiangalia walisema hakuna kilichotengenezwa, ni halisia. Uwazi lilichukua picha za video hiyo na nyingine kwa kuziweka pamoja zikaonesha kushabihiana kwa sehemu kubwa.

RPC KINONDONI AZUNGUMZA NA UWAZI
Baada ya kuinyaka video hiyo, Uwazi lilizungumza na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kinondoni, Camillius Wambura ambaye anasimamia upelelezi wa tukio la mauaji ya mfanyabiashara aliyeuawa katika mkoa wake.

Yeye alisema: “Hilo suala lipo kwa Polisi wa Kimataifa (Interpol), wao wanamfuatilia kwa karibu sana. Atapatikana tu.”

KAMANDA KOVA NAYE
Baada ya hapo, Uwazi likamtafuta Kamanda wa Polisi wa Kanda Maalum ya Dar es Salaam, CP Suleiman Kova ambaye alisema:

“Alex Massawe anaendelea kusakwa, Interpol inamfuatilia kila kukicha. Atanaswa tu.”
Aidha, Kamanda Kova alitaka kujua jinsi inavyopatikana hiyo video ambapo alielekezwa na mwandishi wetu.

DCI AONGEA
Uwazi likamsaka Mkurugenzi wa Makosa ya Jinai Tanzania DCI, Isaya Mngulu na kumuuliza anasemaje kuhusu mtu huyo kudaiwa ni Alex Massawe kutanua Afrika Kusini ambapo alisema:
“Kwanza niko nje ya nchi. Lakini Massawe anafuatiliwa kwa karibu na Polisi wa Kimataifa (Interpol). Kwanza tayari yuko kwenye mazingira mazuri ya kumkamata, tena muda si mrefu.”

MASSAWE AMEFIKAJE HAPA?
Massawe na mfanyabiashara mwenzake, Abubakar Marijani ’Papa Msofe’ na mtu anayejulikana kwa jina la Makongoro Nyerere (si wa hayati Baba wa Taifa, Julius Nyerere) wanadaiwa kuhusika na kifo cha mfanyabiashara Onesphory Kituly mwaka 2012 nyumbani kwake, Magomeni Mapipa jijini Dar.

Papa Msofe na Makongoro wapo Gereza la Keko, Dar kwa kesi hiyo huku Massawe akiwa anaendelea kusakwa aunganishwe na watuhumiwa wenzake hao.
GPL

Afande Mpinga: Kila Traffic Ana Kitabu Cha Faini Mnafundisha Uhasibu Siku Hizi? Hata FFU Nao Wamo

$
0
0
KAMA KUNA SIKU NILIOCHEKA DUNIANI NI LEO AFAND MPINGA
Kwanza shikamoo mkuu na baada ya shikamoo na kaswali changu cha kizushi ambacho ukisoma hata zawadi ya EID uitaji 
kifurahisho tosha

Mh Mpinga sikuhizi za usoni kila traffic amekuwa akishika kitabu ..zamani sikupata kuona hii afande hasa wakati wa mzee wetu wa kichaga tosha..pamoja na wachaga zao lao ni pesa lakini akukuwa na wingi wa vitabu vya faini vinagiwa kama njugu kwa kila traffic kama wakati huu

ingekuwa wakati wa mzee ruksa ningesema mnamalizia ya mwisho mwisho 2015 ..lakini hekima yako sipendi kufika huko
Mh Mpinga hivi vitabu vingi ni feki naomba niongee hili kabla ujasherekea sikukuu..inaatia aibu kuona mtu anakukimbilia kwenye boneti ...kuandika faini ya kosa ambalo ajakwambia alafu anakuja kwako kuanza kuomba rushwa 

ili jambo nimecheka sana sana leo na pengine huyu traffic anajiuliza ni nani mimi kufanya nilichokifanya.....nikiwa naelekea tabata nikakutana na utitiri wa traffic wanasimamisha kila gari kama wanakagua visa namanga

wa mbele yangu aliposimamishwa akaunganisha waala akuitaji kuona sura zao..akaamua kuntoa msala mimi kama kawaida hao naitaga ma furendi....niliposimama jamaa akanipita na kwenda kwenye boneti...akaanza kuandika faini yake ....sikujua anaandika sh ngapi akanifwata bila hata salamu mwanaizaya yule ananiambia unajua kosa lako...nikamwambia nisingesubiri unisimamishe ..umenisimamisha unajua kosa langu akawaanaangalia kwa ndani ...

akanichania karatasi anasema ndio kosa langu ninasemaje..nikaisoma nikamwambia nisemeje si ushaandika ??nilipojibu hili akaiomba karatasi ..kitendo cha kuiomba takataka yake aliishia kuiona plate namba tu mwishoni ...

SWALI LANGU MH MPINGA HAWA TRAAFFIC WANAFUNDISHA UHASIBU AMA??KILA MTU ANA KITABU
AJABU VITABU VYOTE HAVINA COVER NA VIMEKUNJWA KAMA VINASUBIRI MAANDAZI WAFUNGIE//

NASEMA HIVI IPO SIKU UTAAGIIZA MAANDAZI MZAZI WANGU UKUTE KARATASI YA FAINI TENA COPY INAYOTAKIWA KUBAKI KWENU IKIWA IMEFUNGIA MAANDAZI

Ray C Unastahili Pongezi Kwa Kumuokoa Huyu Mrembo kwenye Janga la Madawa ya Kulevya

$
0
0
Mrembo  Doreen  aliyekuwa  video  Queen  wa  wimbo  uliotokea  kutamba  miaka  ya  nyuma  wa  Ice  Cream  ulioimbwa  na  Haji  Nura  ‘Noorah’  akimshirikisha  Suma  Lee  ameanza  kurejea  katika  hali  yake  ya  kaaida  ikiwa  ni  baada  ya  kutopea  katika  matumizi  ya  dawa  za  kulevya…..

Doreen  anakuwa  wa  kwanza  kuionyesha  jamii  juu  ya  taasisi  ya  mwanamuziki  Rehema  Chamila  ‘Ray  C’  ya  Ray  C  Foundation  kuanza  kutimiza  malengo  yake  baada  ya  kufanikisha  mrembo  huyo  kuanza  kutumia  tiba  ya  dawa  za  Methadone  na  afya  yake  kuanza  kurejea  kwenye  hali  yake  ya  kawaida…..

Ray  C  akizungumza  na  mwandishi  wetu  amesema  kuwa  anajisikia  fahari  kuona  afya  ya  Doreen  ikiimarika  kwa  haraka.

“Karudi  katika  hali  yake  ya  kawaida  baada  ya  kuanza  tiba  ya  Methadone……Nafurah  sana  nikiona  matuda  ya  Ray  C  Foundation, nimefurahi  kumuona  akiwa  na  afya  njema,” amesema  Ray  C.

Ray  C  ni  mwanamuziki  wa  kwanza  nchini  kujitoa  mhanga  kuwasaidia  vijana  waliojiingiza  katika  matumizi  ya  dawa  za  kulevya

Walio Tupa Viungo Vya Binadamu Bunju Wapandishwa Kizimbani, Mashataka Yafutwa

$
0
0
Sakata la kutupwa kwa viungo vya binadamu bila kufuata utaratibu jana liligeuka sinema wakati maofisa wanne wa Chuo Kikuu cha Tiba na Teknolojia (IMTU), walipofikishwa mahakamani Dar es Salaam.

Maofisa hao ambao ni maprofesa na wahadhiri wa chuo hicho walifikishwa katika Mahakama ya Wilaya ya Kinondoni wakikabiliwa na mashtaka mawili likiwamo la kushindwa kufukia viroba 83 vya miili ya binadamu.

Baada ya mashtaka hayo kusomwa na taratibu za dhamana kukamilika huku mmoja wao akishindwa kutimiza masharti, watuhumiwa hao walirejeshwa kizimbani na kufutiwa mashtaka hayo kwa amri ya Mkurugenzi wa Mashtaka (DDP) aliyewasilisha hati ya kutokuwa na nia ya kuendelea na mashtaka hayo.

Hata hivyo, furaha waliyoipata washtakiwa hao, Venkat Subbaiah (57), Appm Shankar Rao (64), Prabhakar  Rai (69) na Dinesh Kumar (27) ilikuwa ya muda tu, kwani polisi waliokuwapo mahakamani hapo waliwakamata tena na kuondoka nao.

Mashtaka yafutwa

Wakati washtakiwa hao wakikamilisha taratibu za dhamana wakiwa ndani ya mahakama hiyo, Wakili wa Serikali, Salum Ahmed aliingia na kuiomba mahakama kuifuta kesi hiyo chini ya Kifungu cha 91 (1) cha Mwenendo wa Mashauri ya Jinai (CPA) kwa kuwa Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP) hana nia ya kuendeleza mashtaka dhidi yao.

Kifungu hicho cha sheria kinampa mamlaka DPP kuifuta kesi mahakamani wakati wowote pale anapoona hana nia ya kuendeleza mashtaka dhidi ya mtu yoyote.

Baada ya kuwasilishwa kwa ombi hilo, Hakimu Rusemwa aliwaachia huru washtakiwa hao bila masharti yoyote.

Wakamatwa tena

Muda mfupi baada ya washtakiwa hao kuwa huru, walianza kutoka mahakamani kwa furaha lakini kumbe furaha yenyewe ilikuwa inaishia mlangoni mwa mahakama hiyo tu kwani walikutana na polisi waliowakamata tena na kuwaweka chini ya ulinzi.

Wakati washtakiwa hao wakiwa chini ya ulinzi, Wakili wao, Gaudiosus Ishengoma alieleza kusikitishwa na kitendo hicho, akidai DPP aliwafutia mashtaka wateja wake na kuwaachia huru ili awafungulie mashtaka mengine ambayo hayana dhamana.

Mwanamke Akinivulia tu Mgegedo Wangu Hausimamishi!!! Kuna Mwanamke Kanifunga Kichawi?

$
0
0
Mie Nikipata Mwanmke yeyote hata awe mzuri kivipi akinivulia tu mgegedo hulala palepale na haisimami tena! tatizo hili limekuwa likitokea mara kwa mara kiasi kwamba nahisi nimechezewa! au ni tatizo la kisaikolojia? na nifanyeje ili liishe? Maana napata Aibu sana na kuonekana si Mwanaume Rijali nimeanza kusikia Maneno mtaani kuwa mimi ni Bwabwa...Naomba Ushauri

Diamond Platnumz Awaomba mashabiki "KUMPOKEA" Airport.

$
0
0
Msanii wa kizazi kipya, Diamond platnums, amewaomba mashabiki wake kumpokea Airport usiku wa saa nne kesho jumatano kwenye viwanja vya julius k nyerere, akitokea nchini marekani alipoenda kwenye ugawaji wa tuzo za afrimma ambapo msanii huyo alishinda kipengele cha msanii bora africa mashariki.

"Baba ubaya na wewe sasa umetuchoka mashabiki wako, sasa sisi tukae macho hadi saa nne za usiku mpaka uje , sasa ukishakuja ndo nini labda? Yani tukupokee usiku halafu wewe na hao vibaraka wako mpande prado mrudi sinza , aya na sisi wakina abdala msogoti tunarudije kwetu usiku wote huo? Au utatukodishia mabasi ya kuturudisha om? Maana umetuita, Unapenda sifa mwenyewe kiama hadi unaita watu wakupokee? mmh ila utawapata maana kuna mashabiki wako wakikuona had wanajikojolea, mimi unitolee upuuzi wako apa.

Ndio tunajua unataka ufurahi na mashabiki wako, kwani unashindwa kuandaa special event pale leaders na mashabiki wakaja kukupongeza apo tena pakubwa tu, unasumbua watu tena bila aibu eti wakupokee saa nne usiku au ndo unataka kuvunja rekodi airport? Mnataka tu kuwasababishia watoto wa watu matatizo wabakwe uko na kuibiwa ndo ufurahi, mwenyew huyo unarud kwako na usafiri wako unawaacha wenzio wakihangaika na usafir au utawalipa? Apo utataka watu wakusindikize kwa miguu toka airport hadi kwako, wewe unapigwa na Ac wenzio wanapiga mguu, na utawapata wapo wengi tu ma jobless watakuja kukupokea".

Na bora umewaambia mapema maana kuna watu watatoka morogoro,kimbiji na mikoa yote watakuja kukupokea airport, maana kuna watu wana ndoto japo tu wakuone super star wao, sasa ndo uandae na guest wenzio walale maana si unapenda sifa ulipe na gharama , aya nadhani ujumbe wameupata.
Viewing all 104709 articles
Browse latest View live




Latest Images