Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104747 articles
Browse latest View live

Yanga Kuwakosa Kuukosa Mchezo wa Kesho Dhidi ya Azam FC

$
0
0
Yanga Kuwakosa  Kuukosa Mchezo wa Kesho Dhidi ya Azam FC
Wachezaji saba wa Mabingwa watetezi wa Ligi Kuu Tanzania Bara, Yanga wataukosa mchezo wa kesho unaotarajiwa kuchezwa dhidi ya Azam FC katika dimba la Azam Complex kutokana na sababu mbalimbali walizokuwa nazo.


Hayo yamebainishwa leo na Afisa Habari wa klabu hiyo Dismas Ten na kuwataja wachezaji kuwa ni Yohana Mkomola, Thaban Kamusoko, Amisi Tambwe, Abdallah Shaibu, Donald Ngoma pamoja na Patongonyani ambao wote hawa ni majeruhi huku Pius Buswita akiwa anatumikia adhabu ya kadi tatu za njano alizozipata katika michuano ya Ligi Kuu Tanzania Bara.

"Kuelekea mchezo wa kesho dhidi ya Azam FC ni wachezaji saba pekee ndio watakaokosa mchezo huo kama nilivyosema lakini kila kitu kimekamilika. Tunaiheshimu sana Azam kwani wamekuwa na msimu mzuri wanapata matokeo ndani na nje ya uwanja wao wa nyumbani ila ata sisi Yanga SC tupo vizuri na tunatarajia kupata matokeo kwenye mchezo wa kesho", alisema Dismas Ten.

Azam FC kesho itakuwa inamkaribisha Yanga SC katika dimba lao la nyumbani ambapo mchezo huo utachezwa majira ya 10:00 alasiri kwa saa za Afrika Mashariki na Kati.

Simba Yajipanga Kuimaliza Majimaji

$
0
0
Simba Yajipanga Kuimaliza Majimaji
Kocha Msaidizi wa Simba, Masoud Djuma, amesema kikosi chao kipo fiti kuivaa Majimaji katika mchezo wa Ligi Kuu Bara utakaochezwa Jumapili Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Mchezo huo utakuwa wa kwanza kwa Kocha Mkuu mpya wa Simba, Mfaransa Pierre Lechantre aliyeanza kukinoa kikosi hicho juzi.

Akizungumzia mchezo huo, Djuma ambaye ni raia wa Burundi, alisema wanauchukulia mchezo huo kwa uzito kwa sababu hawana mashindani mengine makubwa wanayoshiriki zaidi ya ligi kwa michuano ya ndani.

“Mategemeo yetu ni kupata ushindi ili tumalize mzunguko wa kwanza tukiwa tumejiimarisha zaidi kileleni,” alisema.

Kwa sasa Simba inaendelea kuongoza ligi ikiwa na pointi 32, mbili zaidi ya zile za Azam FC iliyo nafasi ya pili na saba mbele ya Yanga iliyo nafasi ya tatu.

Masoud pia ameuzungumzia ujio wa bosi wake mpya huyo akisema anaamini utaongeza kasi waliyonayo sasa huku akiahidi kumpa ushirikiano wa kutosha.

“Nilikuwa naye siku yake ya kwanza mazoezini (juzi). Kilichotokea ni utambulisho kwa wachezaji wote wa kikosi cha Simba pamoja na kutizama utimamu wa wachezaji,” alisema Masoud.

Miongoni mwa wachezaji waliokuwepo kwenye utambulisho huo uliofanyika Uwanja wa Bandari ni pamoja na majeruhi Haruna Niyonzima, Salim Mbonde na Said Mohammed ‘Nduda’.

Kamanda Muslim Kushuhudia Mtanange wa Azam na Yanga Kesho

$
0
0
Kamanda Muslim Kushuhudia Mtanange wa Azam na Yanga  Kesho
Klabu ya soka ya Azam FC imemtangaza Kamanda wa Polisi Kikosi cha Usalama Barabarani Fortunatus Muslim, kuwa ndiye mgeni rasmi kwenye mchezo wake wa kesho dhidi ya Yanga.


Akiongea leo mbele ya waandishi wa habari msemaji wa klabu hiyo Jaffary Idd amemtaja Kamanda Muslim kuwa mgeni rasmi katika mchezo huo ambao utawashuhudia mabingwa watetezi Yanga wakicheza kwa mara ya kwanza dhidi ya Azam kwenye uwanja wa Azam Complex.

Aidha Jaffary pia amesema pamoja na kuandika barua ya kuomba kubadilishwa kwa mwamuzi aliyepangwa kuchezesha mchezo huo Israel Nkongo, lakini hadi sasa bado wanamtambua kama mwamuzi kwani hawajapata taarifa yoyote ya kukubaliwa au kukataliwa kwa ombi lao.

Bado tunamtambua Israel Nkongo kama mwamuzi wa mchezo wetu wa kesho lakini tunamuomba atende haki'', amesema Jafarry.

Kwa upande wake kocha msaidizi wa mabingwa hao wa mapinduzi Idd Cheche, amesema wanaiheshimu klabu ya Yanga lakini wamejiandaa kuhakikisha wanawapa raha na ladha ya soka mashabiki wa soka watakaojitokeza sambamba na kusaka alama tatu muhimu.

Dawa Bora za Nguvu za Kiume na Kukosa Hamu ya Tendo la Ndoa

$
0
0

DAWA BORA ZA NGUVU ZA KIUME NA KUKOSA HAMU YA TENDO LA NDOA baada ya utafiti wa muda mrefu juu ya matatinzo ya upungufu wa nguvu za kiume na ukosaji wa hamu ya tendo la ndoa ama kushindwa kurundia tendo kwa haraka Sasa inakuletea suluhisho juu ya matatizo haya kwa kutumia dawa za full power ni dawa asili yenye vidonge inayotibu tatizo la upungufu au ukosefu wa nguvu za kiume dawa hii inamchanganyiko wa kutosha kuzalisha vichocheo vingi vya hernone za gestro gen zikiwemo vitamin b6 na b1 vitamin e pamoja na madini aina ya zinc vitakufanya kuwa na nguvu na mzunguko mzuri wa damu na kuongeza hamu na uwezo wakufanya tendo la ndoa zaidi hatua nne au zaidi na kuchelewa kufika kileleni zaidi ya dakika 20/30 ZAT 50 inarundisha maumbile ya uume yaani kurefusha na kunenepesha nchi 3/7 na upana cm 3/4 standard.kiafya haijalishi umri wako hata kwa wazeeukitumia.maumbile yatabaki kuwa hivyo siku zote pia anatibu matatizo mengine kama presha kisukari ngiri chango la tumbo kujaa gesi kutopata choo vizuri minguu kuwaka moto matatizo ya uzazi bawasili na magonjwa ya zinaa kama kisonono na kaswende tunapatikana daresalaam na mikao wasiliana nasi dr oshinda no 0755505099/0714126118 karibuni kwa hunduma bora

Taasisi ya Aga Khan Yazindua Kituo cha Afya Wilaya ya Ilala

$
0
0
Taasisi ya Aga Khan Yazindua Kituo cha Afya Wilaya ya Ilala
Taasisi ya Huduma za Afya Aga Khan Tanzania imezindua  kituo kingine cha afya wilayani Ilala cha Aga Khan Polyclinic.

Akizungumza leo Januari 26, mwaka 2018 katika ufunguzi wa kituo hicho, Mkurugenzi Mtendaji Mkuu wa taasisi hiyo Kanda ya Afrika Mashariki,  Sulaiman Shahabuddin amesema kitakuwa alama kuu ya ukuaji wa uboreshaji wa huduma za afya katika mkoa huo..
"Hiki ni kituo chetu cha tisa katika mkoa wa Dar es Salaam na cha 16 nchini, kituo hiki kitaleta tija ya huduma bora za afya kwa wananchi wa Ilala hasa katika eneo la Ukonga na Gongo la Mboto,” amesema.

Mganga Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Dk Grace Magembe amesema, “Naelewa tafsiri nyingine kubwa ya uwekezaji mnaofanya mbali na kuongeza  nafasi kuchagia ukuaji wa kasi wa huduma bora, salama na nafuu za afya kwa Watanzania pia mnafungua  milango ya ajira.”
Kituo hicho kitatoa huduma za afya ya mama na mtoto, kliniki za watoto na kinamama, ultrasound, X Ray na vipimo vya awali vya moyo.

Nelly Atetewa na Mpenziwe Kuhusu Kesi ya Ubakaji

$
0
0
Nelly Atetewa na Mpenziwe Kuhusu Kesi ya Ubakaji
Msanii wa muziki nchini Marekani Nelly, huwenda akapona katika sakata linalomkabili la kumfanyia unyanyasaji wa kingono binti mmoja wakatiwa tour yake mwaka 2017.

Mpenzi wa msanii huyo Shantel Jackson, ameeleza kuwa mwanadada anayedai kubakwa na rapper huyo sio kweli kwani hata yeye alikuwepo katika eneo la tukio hilo ila alikuwa chumba cha kubadilishia nguo.

“Ni kweli mimi na Nelly tulikoseana ila hawezi kufanya tendo la ubakaji,” ameeleza mrembo huyo.

Monique Greene  ndiyo  mrembo anayedai kufanyiwa ubakaji na rapper huyo katika gari  la Tamasha maeno ya Washington, na sasa wanawake wengine wawili wameibuka na kudai kufanyiwa kitendo kama hicho na msanii huyo.

Maelezo ya mpenzi wa Nelly, Shantel Jackson:

“Kama Odinga Ataapishwa Itadhihirisha Kuwa Afrika ni Tundu la Choo”- Mutua

$
0
0
“Kama Odinga Ataapishwa Itadhihirisha Kuwa Afrika ni Tundu la Choo”- Mutua
Wakati wananchi wa Kenya wakisubiria kwa hamu tukio la kuapishwa kwa Kiongozi wa Umoja wa Vyama vya Upinzani nchini humo (NASA) Raila Odinga, Gavana wa Kaunti ya Machakos Dkt. Alfred Mutua amesema kuwa kama tukio hilo litafanikiwa kufanyika basi ni dhahiri kuwa bara la Afrika ni tundu la choo.


Dkt. Mutua amesema kuwa Kenya itakuwa nchi ya kwanza duniani kuapisha marais wawili katika awamu moja.

“Kama hili la kuapishwa kwa kiongozi wa NASA litafanikiwa basi utakuwa mfano mzuri utakaodhihirisha kuwa bara letu ni mfano wa Tundu la Choo. Mtu utawezaje kuapishwa wakati huo huo kuna kiongozi mwingine ameshaapishwa na Jaji Mkuu? hii ni aibu kwa bara letu,“ameandika Dkt. Mutua kwenye ukurasa wake wa Twitter.

Neno ‘Tundu la Choo’ limewa maarufu zaidi duniani baada ya Rais Donald Trump wiki mbili zilizopita kutamka nchi za Afrika na Haiti ni mfano wa ‘Tundu la Choo’.

Kiongozi huyo wa upinzani nchini Kenya anatarajiwa kuapishwa Januari 30, 2018 na kuwa Rais wa watu wengi kama anavyojiita.

Wagombea Kinondoni na Siha Wanasubiria Kuapishwa Tu na Kuingia Bungeni - Polepole

$
0
0
Wagombea  Kinondoni na Siha Wanasubiria Kuapishwa Tu na Kuingia Bungeni - Polepole
Katibu wa Itikadi na Uenezi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Humphrey Polepole amefunguka na kusema kuwa wagombea wa Ubunge kupitia chama chake katika uchaguzi wa marudio katika majimbo ya Kinondoni na Siha wanasubiri kuapishwa tu na kuingia bungeni.


Polepole amesema hayo alipokuwa akihojiwa na moja ya kituo cha habari na kusema kuwa kwa jinsi ambavyo wana CCM wamefanya kazi nzuri sana Kinondoni na Siha kuhakikisha wanawanadi na kuwauza wagombea wao hivyo wana uhakika wa kushinda uchaguzi huo kwa kishindo.

"Kwa utafiti tunaofanya na kazi nzuri tuliyofanya tunasubiri kutangazwa washindi katika majimbo yote mawili pale Kinondoni na Siha" alisisikika Polepole akisema

Mbali na hilo Polepole amekanusha chama hicho kuwa na mvurugano wa wenyewe kwa wenyewe kufuatia kusimamisha wagombea katika majimbo hayo ambao hawana muda mrefu katika chama hicho wakitokea upinzani na kusema kwa CCM kila mwanachama ana haki sawa na wanachama wengine.

Chama Cha Mapinduzi kimemsimamisha Maulid Mtulia kugombea Ubunge kwa jimbo la Kinondoni wakati katika jimbo la Siha kimemsimamisha Dk Godwin Mollel ambao wote walikuwa ni wabunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kutokea vyama vya upinzani, lakini walijivua uanachama kwenye vyama vyao na kujiunga na CCM.

Donald Trump Ampa Salamu Kagame Kuzifikisha kwa Viongozi wa Afrika

$
0
0
Donald Trump Ampa Salamu Kagame Kuzifikisha kwa Viongozi wa Afrika
Rais wa Marekani Donald Trump amemuomba Rais wa Rwanda Paul Kagame ambaye kwa sasa ndiye mwenyekiti wa Umoja wa Afrika (AU) kufikisha salamu zake kwa viongozi wengine wa mataifa wanachama wa AU.

Viongozi hao wawili wamekutana mjini Davos, Uswizi pambizoni mwa mkutano wa viongozi na watu mashuhuri kuhusu uchumi na biashara duniani.

Mkutano huo wa Kagame na Trump umetokea wiki chache baada ya kiongozi huyo wa Marekani kuyaeleza mataifa ya Afrika kama "machafu" au mataifa ya "mabwege".

Hatua hiyo ilimfanya kushutumiwa vikali na viongozi wa AU na baadhi ya viongozi wa nchi za Afrika kama vile Botswana na Ghana.

Bw Trump amekanusha kwamba alitumia neno hilo kuyaelezea mataifa ya Afrika.

Hata hivyo alikiri kwamba alitumia maneno makali akiyaeleza mataifa ya Afrika, Haiti na El Salvador alipokuwa anazungumzia wahamiaji wanaoingia Marekani.

Lakini katika mkutano wake na Kagame pambizoni mwa Mkutano wa Uchumi wa Dunia mjini Davos, Trump hajaonyesha dalili zozote za majuto kuhusu tamko lake la awali kuhusu Afrika.

Bw Trump ameeleza mkutano wake wa leo na Kagame kama "wa kufana sana", na kueleza nchi hizo mbili kama washirika wa kibiashara ambao wanajivunia "uhusiano mzuri sana."

Ameongeza: "Ningependa kukupongeza, Bw Rais, unapochukua majukumu ya kuwa kiongozi mpya wa Umoja wa Afrika, ni heshima kubwa … najua unaenda kuhudhuria mkutano wa kwanza karibuni. Tafadhali, fikisha salamu zangu."

Rais Kagame alisema wameshauriana kuhusu ushirikiano wa nchi hizo mbili, ikiwa ni pamoja na usaidizi wa Marekani kwa Rwanda katika "operesheni zake kote duniani", pamoja na masuala ya kiuchumi, biashara, uwekezaji na idadi ya watalii wa Marekani wanaozuru Rwanda, ambayo inaongezeka.

Mkutano wa viongozi wa nchi wanachama wa AU utafanyika Jumapili na Jumatatu.

Wastara Afunguka Baada ya Rais Magufuli Kumchangia Milioni 15

$
0
0
Msanii wa filamu nchini Wastara Juma amefunguka na kudai hakutegemea kama Rais Magufuli angeweza kulipa kipaumbele tatizo lake alilokuwa kwa sasa huku akimshukuru kwa kuweza kumsaidia suala hilo.

Wastara ameeleza hayo wakati alipokuwa akipokea pesa ya matibabu iliyotolewa na Rais Magufuli na mke wake Mama Janeth jumla ya milioni 15 ili iweze kumsaidia katika matibabu yake kama waliyovyoongea katika simu hapo awali.

"Kubwa niseme tu nashukuru, kwa sababu sikutegemea kama tatizo langu Mhe. Rais angeweza kulipa kipaumbele. Nashukuru pia naomba mpeleke salamu zangu kwa Mhe kwamba natamani siku moja nisimame ili niweze kuwa naye bega kwa bega katika kazi za kujenga nchi yetu ya Tanzania",alisema Wastara.

Pamoja na hayo Wastara ameendelea kwa kusema "natambua kuna watu wengi wana shida, mimi kama mimi natamani nifanye kazi yangu ili niweze kutoa 'percent' yangu niweze kuwasaidia na nimekuwa nikiomba sana muda mwingi jambo hilo".

Kutana na Mtabibu Mwenye KUBRI kutoka kwa ALLAH issa simba said Mtabibu wa Nyota za Binadamu na Dawa za Asili

$
0
0
Kutana na Mtabibu Mwenye KUBRI kutoka kwa ALLAH issa simba said Mtabibu wa Nyota za Binadamu na Dawa za Asili ya Africa Mwenye UWEZO Kubaini tatizo lako Pindi tu Utakapo Fanya Mawasilino Kupitia Wasaa Husika..JE UNASUMBULIWA NA Mapenzi? (Umeachwa na Umpendae,Awe Mume,Mke na Bado unampenda?Na Umejaribu Sehemu nyingi Bila Mafanikio?Wasilina na Maalim Hussein Ujione muujiza wa Papo kwa Papo.. anauwezo WA KURUDISHA MAHUSIANO NA KUIMARISHA NDOA YAKO NDANI YA SAA 12 TU. Umekimbiwa na Mumeo,mkeo au Mpenzi na anaishi na mtu mwingine? Muone akutatulie Anauwezo wa Hali ya Juu wa Kusambalatisha Mahusiano yao Endapo utafata Atakacho kuelekeza.
Atamfanya Atimize Ahadi zote kwa Muda Mfupi.

Issa simba said Anatumia Jina la Muhusika au Picha Kumaliza Tatizo lako..
Anatibu kwa Kutumia Vitabu vya QUR-AN Dawa za Asili za Africa,Dawa za Kiarabu na Majini.Anatafsiri Ndoto. Kushinda BAHATI NASIBU, KUSAFISHA NYOTA. Mvuto wa Mwili na BIASHARA, Kinga ya Mwili,ZINDIKO za Nyumba.MIGUU Kufa GANZI.Kufungua KIZAZI kwa wale walio fungwa kwa njia za KISHIRIKINA. Anakupa Jini la Mali kwa yule anaehitaji Utajiri BILA MASHARTI. Nguvu za KIUME, Humaliza Kesi zilishindika ndani ya siku 14 tu..na mengi zaidi

Wasiliana nasi  Kwa Numba Hizi +255 622588038 , 0679119679 , +255 764318107, 0656145170, 0762899488 

Jibu la Polisi baada ya kuagizwa na Waziri kuwakamata watuhumiwa ndani ya siku 7

$
0
0
Jeshi la Polisi limesema limepokea agizo la Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk Hamisi Kigwangalla la kuwachukulia hatua watu wanne ndani ya siku saba kwa madai wanashiriki katika mtandao wa ujangili, lakini halifanyi kazi kwa shinikizo.

Msemaji wa Jeshi hilo, Barnabas Mwakalukwa amesema polisi wanafanya kazi kwa kufuata kanuni, taratibu na sheria za Jeshi hilo.

Juzi,  Kigwangalla mbali na kutoa agizo hilo, amesema watu hao wanne pia walipanga njama za kumuua mwanaharakati, Wayne Lotter na kwamba polisi wakishindwa kuwakamata atawashtaki kwa Amiri Jeshi Mkuu ambaye ni Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Mwakalukwa amesema jukumu lao ni kukamata wanapopata shitaka la kuwapo kwa kitu kisicho cha kawaida, kuchunguza na kupeleka kwa Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP) kwa ajili ya kukamilisha taratibu nyingine.

“Kazi yetu ni kukamata, kuchunguza na kupeleka kwa  DPP kwa ajili ya taratibu nyingine, hatufanyi kazi kwa matamko ya bungeni,” amesema na kuongeza;

“Alichokisema mheshimiwa Kigwangalla nimekisoma kwenye vyombo vya habari akihusisha na suala la mwanaharakati aliyeuawa, sisi hatufanyi kazi kwa kufuata vyombo vya habari vimeandika nini au limetolewa tamko gani au kuna shinikizo gani, tunafanya kwa kufuata taratibu zilizopo.”

Mbowe, Lowassa na Sumaye Kuamsha Dude leo...Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumamosi ya January 27

$
0
0

Mbowe, Lowassa na Sumaye Kuamsha Dude leo...Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumamosi ya January 27

Taarifa Muhimu kwa Wanafunzi wa vyuo Kutoka Bodi ya Mikopo (HESLB)

$
0
0
Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB) inawataarifu wanafunzi wanaonufaika na mikopo kuwa  wanatakiwa kuendelea kuingiza taarifa zao kwa njia ya mtandao kupitia http://olas.heslb.go.tz  hadi tarehe 31 Januari, 2018.

Wanafunzi wanufaika wanapaswa kufanya yafuatayo:
•    Tembelea mtandao wa http://olas.heslb.go.tz
•  Fungua kiunganishi cha “Click here to start” kwenye maelezo ya mwanzo ya kukaribisha.
•    Weka namba yako ya mtihani ya Kidato cha Nne na mwaka uliofanya mtihani huo, kwa mfano: S0129.0004.2020
•   Weka namba yako ya akaunti ya Benki kama ilivyowasilishwa HESLB au kama inavyoonekana kwenye “signing sheet”
•    Ingiza neno jipya la siri na ulithibitishe.
•   Baada ya kuthibitisha, ukurasa wa kuweka picha yako “passport size photo” utafunguka.
•    Weka picha yako ya rangi katika ukubwa wa 120×150
•    Wanufaika wapya wa mikopo kwa mwaka wa masomo 2017/2018 hawatahusika kwenye zoezi hili kwa vile taarifa zao ziliwasilishwa wakati wa kuomba mikopo.

Imetolewa na:
Kitengo cha Habari, Elimu na Mawasiliano
BODI YA MIKOPO YA WANAFUNZI WA ELIMU YA JUU
Tarehe 26/01/2018

Zitto: Nilipokuwa Mwenyekiti Kamati ya Bunge ya Mashirika ya Umma tulimhoji Tido na Kuthibitisha Hakuwa na kosa

$
0
0
Kupia ukurasa wake wa mtandao wa kijamii wa twitter Mbunge Zitto Kabwe amesema alipokuwa Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Mashirika ya Umma, walimuita Tido Mhando na kumhoji kuhusu tuhuma alizofikishwa nazo kortini leo.


Zitto Kabwe Ruyagwa
We did it. And I am pretty sure there was no wrong doing. We had all the documents scrutinized and it was proven beyond doubt that it went through board and only thing to do was review the contract and improve it





Walithibitisha hakuna kosa alilolifanya, aitaka TAKUKURU isome ripoti zote na kuna uwezekano wakashindwa kesi.



Tweet hiyo hapo juu imekuja ikiwa ni muendelezo baada ya kuandika tweet nyingine ambayo ilikuwa inamjibu mdau mmoja ambaye alisema Tido alitumika kwenye uchaguzi mkuu wa mwaka 2005. Tweet hiyo imesema;

Rick Ross Afuta Picha zote za Diamond Platnumz Kuna nini??

$
0
0
Staa wa muziki kutokea nchini Marekani Rick Ross  January 26,2018 alichukua headlines katika mitandao ya kijamii baada ya kujulikana kafuta picha zote za Diamond Platnumz katika ukurasa wake wa Instagram.

 Rick Ross amewahi kumpost mara mbiliDiamond Platnumz kupitia ukurasa wake wa instagram, post zote zikihusiana na ishu ya ubalozi wa kinywaji cha Belaire mwezi September 2017.

 Maswali yamezidi kuwa mengi kutoka kwa mashabiki baada ya Rick Ross kutofuta picha za kinywaji cha Belaire na kuacha picha yaHuddah Monroe ambaye pia ni balozi wa kinywaji hicho kutokea nchini Kenya lakini post za Diamond pekee ndio amefuta.

Nini kinaendelea kati ya Diamond na Rick Ross? ikumbukwe tu Rick Ross na Diamond Platnumz wameshafanya kazi pamoja katika wimbo wa Waka Waka ambao ulifanyika nchini Marekani.

Makonda Aagiza Utuhumiwa Uvamizi wa Shule Akamatwe

$
0
0
Makonda Aagiza Utuhumiwa Uvamizi wa Shule Akamatwe
Ongeza kichwa
Paul Makonda ameagiza kukamatwa Ajay Chohan anayedaiwa kuvamia eneo la Shule ya Msingi Mapinduzi wilaya ya Kinondoni na kumiliki ardhi kinyume cha utaratibu.
Chohan amekamatwa leo Ijumaa Januari 26,2018 baada ya Makonda kutoa amri kwa mkuu wa polisi wa wilaya hiyo, muda mfupi baada ya kuzindua ujenzi wa ofisi za walimu wa shule hiyo.
Anadaiwa kumiliki kinyume cha utaratibu kiwanja kilichopo katika Kata ya Kigogo, Mtaa wa Mbuyuni.
Hata hivyo, Chohan ameieleza MCL Digital kuwa ana vielelezo vya umiliki wa eneo hilo kutoka serikalini.
Awali, mwalimu mkuu wa shule hiyo, Fina Mauki alimuomba Makonda kutafuta suluhu.
“Tuna tatizo la wananchi kuvamia maeneo ya shule na kujimilikisha kinyume cha utaratibu. Tunakuomba ukemee suala hili kwa kuwa ardhi ya shule iliyopo haitoshelezi mahitaji,” amesema Mauki.
Akijibu ombi hilo, Makonda amesema ujenzi wa ofisi za walimu wa shule za msingi Dar es Salaam utakwenda sambamba na kurudishwa mipaka ya awali ya shule husika.
Ametoa wito kwa wote waliovamia maeneo ya shule kuondoka kabla sheria haijachukua mkondo wake.
“Nimesikia eneo hili kuna mtu anadai ni la kwake, yuko  wapi huyo? Polisi mkamateni mara moja. Jambo hili lianze kuchunguzwa, haiwezekani suala hili la kuvamia maeneo ya shule tukaendelea kulifumbia macho,” amesema.

Amber Lulu Adai Alikataa Zaidi Tsh. Milioni 200 ili Kupiga Picha za Utupu

$
0
0
Amber Lulu adai alikataa zaidi Tsh. Milioni 200 ili kupiga picha za utupu
Msanii wa muziki Bongo, Amber Lulu amedai aliwahi kutaa dili la zaidi ya Tsh. Milioni 200 ambazo zilitolewa ili aweza kupiga picha za utupu.

Muimbaji huyo ambaye anafanya vizuri na ngoma ‘True Love’ ameimbia XXL ya Clouds Fm sababu ya kukataa fedha hizo ni kwamba alikuwa ameshaacha kupiga aina hizo ya picha.

“Ndio nitachukua hiyo hela nitakuwa na kila kitu mwisho wa siku kuna kitu kitamisi, ni hela nyingi sometime unaweza ukatamani lakini naamini nikiwekeza nguvu naweza nikapata hizo hela zaidi ya wanazoniambia,” amesema.

“Sikuwachukulia hivyo kwa sababu nilikuwa tayari katika situation ya kuondoka katika hiyo hali, ilikuwa dola laki moja,” amesisitiza

Hivi karibuni serikali kupitia Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo ilimuita msanii wa Bongo Fleva Gigy Money na Mwanamitindo Sanchoka kwa mahojiano maalumu kuhusu kazi zao ambazo zinaonekana zipo kinyume na maadili hususani kwenye mavazi wanayovaa

MAN U Yaichapa YEOVIL 4-0

$
0
0
MAN U Yaichapa YEOVIL 4-0
KLABU ya Soka ya Manchester United imeenedeleza ushindi kwa michezo mitatu mfurulizo tangu itoke mapumzikoni, Dubai ambpo usiku wa kuamkia leo imeitwanga timu ya Yeovil bao 4-0 katika michuano ya Kombe la Shirikisho (FA Cup).

Katika game hiyo mchezaji mpya wa Man U aliyesajiliwa hivi majuzi akitokea Arsenal, Alex Sanchez ikiwa ni mechi yake ya kwanza alionyesha uwezo mkubwa huku akiisaidia timu yake hiyo kuibuka na ushindi mnono katika Mji wa Yeovil.

Wenyeji Yeovil walianza vizuri lakini walifanya makosa yaliyopelekea kuadhibiwa na klabu hiyo tajiri zaidi duniani kwa sasa.

Wafungaji ni; Rashford 40, Ander Herrera 61, Lingard 90, Lukaku 90+3.

Donald Trump Amekutana na Kufanya Mazungumzo na Rais wa Rwanda Paul Kagame

$
0
0
RAIS wa Marekani, Donald Trump amekutana na kufanya mazungumzo na Rais wa Rwanda Paul Kagame ambaye ni Mwenyekiti wa Umoja wa Afrika (AU) na kumuomba afikishe salamu zake za upenzo kwa viongozi wengine wa mataifa wanachama wa AU.

Viongozi hao wawili wamekutana mjini Davos, Uswizi baada ya Mkutano wa Viongozi na Watu Mashuhuri Kuhusu Uchumi na Biashara Duniani.

Mkutano huo wa Kagame na Trump umekuja wiki chache baada ya kiongozi huyo wa Marekani kutoa kauli iliyotafsiliwa kama ni kuyakashifu mataifa ya Afrika.


Hatua hiyo ilimfanya kushutumiwa vikali na viongozi wa AU na baadhi ya viongozi wa nchi za Afrika kama vile Botswana na Ghana ambapo amekanusha kwamba alitumia neno hilo kuyakashifu mataifa ya Afrika huku akikiri kutumia maneno makali akiyaeleza mataifa ya Afrika, Haiti na El Salvador alipokuwa anazungumzia wahamiaji wanaoingia Marekani.

Wakati wa mkutano wake na Kagame,  Trump hajaonyesha dalili zozote za majuto kuhusu tamko lake la awali kuhusu Afrika huku akisifia kuwa mkutano wao huo ulikuwa “wa kufana sana”, na kueleza nchi hizo mbili kama washirika wa kibiashara ambao wanajivunia “uhusiano mzuri sana.”


“Ningependa kukupongeza, Bw Rais, unapochukua majukumu ya kuwa kiongozi mpya wa Umoja wa Afrika, ni heshima kubwa … najua unaenda kuhudhuria mkutano wa kwanza karibuni. Tafadhali, fikisha salamu zangu.”

Rais Kagame alisema wameshauriana kuhusu ushirikiano wa nchi hizo mbili, ikiwa ni pamoja na usaidizi wa Marekani kwa Rwanda katika operesheni zake kote duniani, pamoja na masuala ya kiuchumi, biashara, uwekezaji na idadi ya watalii wa Marekani wanaozuru Rwanda, ambayo inaongezeka. Mkutano wa viongozi wa nchi wanachama wa AU utafanyika kesho Jumapili na Jumatatu.
Viewing all 104747 articles
Browse latest View live




Latest Images