Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104709 articles
Browse latest View live

Azamu Yawaahidi Ushindi Mashabiki Wake

$
0
0
Nahodha wa Klabu Bingwa ya Afrika Mashariki na Kati Azam FC, Himid Mao ‘Ninja’, amewahakikishia mashabiki wa timu hiyo kuwa wataendelea kulinda heshima ya Uwanja wa Azam Complex kwa kuhakikisha wanaifunga Yanga SC na kuzoa pointi zote tatu.



Azam FC itakuwa kwenye vita kali ya kuwania kilele cha Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara (VPL) leo siku ya Jumamosi majira ya saa 10.00 jioni pale watakapowakaribisha Wanajangwani hao, ambapo ushindi wowote utaifanya kufikisha jumla ya pointi 33  na kuongoza ligi kwa pointi moja dhidi ya Simba, ambao watakuwa na mchezo mmoja mkononi.

Akizungumza hapo jana na wandishi wa habari kuelekea mchezo huo, Mao amesema anaamini ya kuwa yeye pamoja na wachezaji wenzake watakaopata nafasi ya kucheza basi wataiwakilisha vema timu hiyo na kupata matokeo.

“Sisi kama Azam FC daima tunapocheza mechi za hapa nyumbani huwa hatuna presha japo tunajua nini tunatakiwa tukifanye, kwa hiyo mechi ya nyumbani mtu anakuja nyumbani kwetu tunamkaribisha lakini anatakiwa ajue haitakuwa rahisi,” amesema Mao.

Huo ni mchezo wa kwanza kihistoria kwa Azam FC na Yanga kupigwa katika uwanja huo, baada ya msimu huu Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) kuridhia mechi zote zinazoihusu timu hiyo watakapokuwa nyumbani dhidi ya Simba na Yanga zipigwe ndani ya viunga hivyo vya Azam Complex, badala ya utaratibu wa awali zote zikipangwa kufanyika Uwanja wa Taifa au Uhuru.

Kocha Msaidizi wa Azam FC, Idd Nassor Cheche, naye hakuwa mbali kukielezea kiufundi kikosi chake, akidai vijana wake wako kwenye hali nzuri na anachoamini ni ushindi katika mchezo huku akikiri kuiheshimu Yanga kutokana na ukongwe wao.

“Vijana wako vizuri na wako katika maandalizi mazuri na kiafya, kiakili wako vizuri na wanataka kuwahakikishia mashabiki wao kesho kuwa wanatimiza ile adhma yao katika kulinda heshima ya uwanja wetu wa Azam Complex kwamba hatuhitaji kufungwa hapa na kesho vijana wako sawa na watafanya lile tulilolipanga nao,” alisema.

Azam FC itaingia kwenye mtanange huo ikiwa na kumbukumbu ya kutoka kuifunga Tanzania Prisons mabao 2-0 katika mchezo wake wa mwisho wa ligi uliofanyika Uwanja wa Sokoine, mjini Mbeya, huku Yanga yenyewe ikiifunga Ruvu Shooting bao 1-0.

Mabingwa hao mara mbili mfululizo wa Kombe la Mapinduzi mwaka jana na mwaka huu, watanufaika na urejeo wa mshambuliaji wake anayetoka kwenye majeruhi Mbaraka Yusuph huku beki Daniel Amoah, akiwa kwenye hatua za mwisho za kuanza kuonekana tena dimbani baada ya kupona majeraha yake ya goti.

Kihistoria timu hizo zimekutana mara 18 kwenye mechi za ligi, Azam FC ikiwa imeshinda mara tano na Yanga ikiibuka kidedea mara sita huku ikishuhudiwa mechi saba wakitoka sare, ambapo katika mchezo wa mwisho Yanga ilishinda bao 1-0 lililofungwa na Obrey Chirwa.

Hadi sasa Azam FC ikiwa inahitimisha raundi ya kwanza ya ligi leo kwa mechi ya 15, imefanikiwa kushinda mechi nane na kutoka sare mara sita huku ikiwa haijapoteza mechi hata moja na ikiwa ndio timu pekee iliyofungwa mabao machache baada ya kuruhusu nyavu zake kutikiswa mara nne na ikifunga 15.

Majuto Aweka Wazi Ugonjwa Ambao Unamsumbua

$
0
0
Mchekeshaji maarufu Bongo, Amri Athumani alimaarufu kama 'Mzee Majuto' amefunguka na kuweka wazi ugonjwa ambao unamsumbua kwa sasa kuwa ni tezi dume na kudai kuwa atafurahi sana endapo atafanyiwa upasuaji na kuondolewa maradhi hayo.


Mzee Majuto ambaye kwa sasa yupo jijini Dar es Salaam na tayari ameanza hatua za awali kuhakikisha kuwa anafanyiwa upasuaji kuondolewa tezi dume amesema kuwa kutokana na umri wake hashangazwi yeye kupata ugonjwa huo na kudai ni ugonjwa tu kama yalivyo magonjwa mengine.

"Tayari nimeshafanyiwa vipimo kadhaa toka nilipofikishwa Muhimbili hapa saizi nasubiri siku ya Jumanne niende kuonana na daktari ambaye anashughulika zaidi na tezi dume ili aweze kusoma vipimo hivyo vizuri na kuona jinsi gani naweza kufanyiwa upasuaji. Huu ni ugonjwa wa kawaida na wapo watu wengi wameshaupata hata wengine nyinyi mnawajua sema mimi sitaki kuwataja tu hapa" alisema Mzee Majuto

Aidha Mzee Majuto ameshauri watu wengine ambao wana ugonjwa huo wa tezi dume kuhakikisha wanafanyiwa upasuaji mapema kabla ya njia za mkojo kuziba kwani ikifika hatua hiyo watapata shida sana.

Mwaka jana Mzee Majuto alifanyiwa upasuaji akiwa mjini Tanga alipokuwa akisumbuliwa na ugonjwa wa 'Hernia' lakini mwaka huu ameamua kuja Muhimbili jijini Dar es Salaam kufanyiwa upasuaji wa Tezi dume kutokana na ushauri wa madaktari baada ya kugundua kuwa ana tatizo la moyo.

Masaa Machache kabla ya Mchezo wa Azam, Yanga TFF Yambadirisha Mwamuzi

$
0
0
Masaa Machache kabla ya Mchezo wa Azam, Yanga TFF Yambadirisha Mwamuzi
Bado saa chache kabla ya mchezo wa Azam FC dhidi ya Yanga uchezwe katika uwanja wa Azam Complex Mbanda Chamazi lakini kabla ya kuanza kwa mchezo huo shirikisho la soka Tanzania TFF limetangaza mabadiliko madogo katika upande wa muamuzi msaidizi.

Rais Kabila: Uchaguzi wa DR Congo kufanyika Disemba

$
0
0
Rais Kabila: Uchaguzi wa DR Congo kufanyika Disemba
Rais Joseph Kabila amepinga ukosoaji unaotekelezwa na jamii ya kimataifa kuhusu kucheleweshwa kwa uchaguzi katika jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo.

Katika mkutano na wanahabari kuadhimisha miaka 17 madarakani, aliahidi kwamba uchaguzi huo utafanyika mwisho wa mwaka huu.

Kulingana na mwandishi wa BBC Alex Duval Smith mkutano huo na vyombo vya habari mjini Kinshasa ulikuwa wa kwanza katika kipindi cha miaka mitano.Na ulichukua saa tatu.

Aliikosoa Monusco akisema ujumbe huo wa Umoja wa Mataifa hauko nchini DRC ili kuendesha shughuli za taifa hilo.

Kabila: Sitowania urais tena
Maandamano ya kumtaka Kabila aondoke madarakani yashuhudiwa Kinshasa
Kabila kuwa madarakani hadi mwaka ujao
Katika shutuma dhidi ya muungano wa Ulaya na Marekani, ambao wamekosoa makabiliano dhidi ya waandamanaji, alisema: DRC sio koloni .Taifa hili lazima liheshimiwe.

Alionekana akilikumbusha kanisa katoliki akisema kuwa maandamano yanayofanywa na wakristo dhidi ya serikali yake yanafaa kuruhusiwa lakini waandalizi ni lazima washtakiwe.

Serikali hiyo hivi majuzi ilitangaza kwamba uchaguzi utafanyika tarehe 23 Disemba, ikiwa ni miaka miwili baada ya kukamilika kwa muda wa utawala wa rais huyo

Kampuni ya Mugabe Yakabiliwa na Mashtaka ya Unyakuzi wa Ardhi

$
0
0
Kampuni ya Mugabe Yakabiliwa na Mashtaka ya Unyakuzi wa Ardhi
Kampuni moja ya rais wa zamani wa Zimbabwe Robert Mugabe inatakiwa kuondoka katika kipade kimoja cha ardhi kinachomilikiwa na shule moja la sivyo ishtakiwe.

Kampuni hiyo kwa Jina Gushungu Holdings inadaiwa kunyakuwa kipande hicho cha ardhi chenye ukubwa wa hekari 23 katika eneo moja la makaazi ya mji wa Harare.

Kanisa la Reform linasema kuwa ardhi hiyo inamilikiwa na kundi la shule zake la Eaglesvale.

Wakili wa shule hiyo Rodney Makausi aliambia BBC kwamba mwaka 2016 serikali ilichukua ardhi hiyo kwa nguvu.

Serikali baadaye ikaondoa madai yake baada ya swala hilo kuwasilishwa mahakamani.


Lakini mwenyekiti wa bodi ya shule hiyo Enos Chomutiri anasema kuwa mahindi yalipandwa katika shamba hilo mwaka uliopita na bango kubwa la shule hiyo likaondolewa.

Mawakili wametaka kampuni hiyo kuondoka katika shamba hilo mwisho wa mwezi huu ama ishtakiwe.

Sio mara ya kwanza familia ya Mugabe imetuhumiwa kuchukua mali kwa nguvu.

Awali, familia hiyo imekuwa na mgogoro na wakulima masikini kuhusu ardhi moja inayodaiwa kuwa na utajiri wa dhahabu ,pia familia hiyo imetuhumiwa kwa kunyakua shamba moja linalalozalisha ndimu zinazouzwa nje ya taifa katika eneo hilo hilo.

Kwa nini Wanaume Wengi Wanaupungufu Wa nguvu Za Kiume Na Maumbile Madogo?

$
0
0
Asilimia 45 ya wanaume wapo tofauti na wengine kwa kuwatimizia vyema wake au wapenzi Wao na kuwasababishia kutoka nje ya ndoa zao.


NINI CHANZO CHA HAYO?Kupiga punyeto,Ngiri,Vidonda vya tumbo,Magonjwa ya moyo,Presha,Kisukari,Korodani moja kuvimba,Msongo wa mwazo,Kufanyiwa tohara ukiwa mtu mzima n.k.DOKTA MANYANDA sasa kapata tiba sahihi ya tatizo la NGUVU ZA KIUME.


MUHAMA:Hii hutibu na kuponyesha kabisa tatizo la nguvu za kiume,utakuwa na uwezo wa kurudia tendo zaidi ya mara tatu bila kuchoka na itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa mda wa dakika 15-20.DAWA hii imechanganywa miti 12.Hata wazee wenye umri mkubwa wanapona kabisa.OKO NDOA YAKO SASA.


MANGUNGU MIX: Ndio tiba tosha kwa sasa ambayo hurefusha na kunenepesha uume saizi uipendayo inch 1-8 na unene sentimita 1-5,dawa hii ipo ya kupaka na kunywa na haina madhara yoyote kwa mtumiaji.


NITOFAUTI NA ULIZO WAHI KUZITUMIA.Pia tuna dawa za kupatanisha mke,mme,mpenzi au bosi wako kwa mda mfupi sana,Uzazi,Kusafisha nyota,


Je unamali yako unauza hupati wateja?

Wasiliana nami 0716-263605


DOKTA MANYANDA ANAPATIKANA KASULU KIGOMA,Kwa wale wa mikoani huduma hii utaipata popote pale

Nikki Ajibu Tuhuma za Joshua Nassari Kuhusu Wasanii Kutompigania Sugu Akiwa Mahabusu

$
0
0
Msanii kutoka kampuni ya Weusi, Nikki wa Pili amemjibu Mbunge wa Arumeru Mashariki Joshua Nassari kwamba si kweli kuwa wameamua kumtumikia 'kafiri' ila kimsingi wao hawana ufahamu wa kuongelea masuala ambayo bado yanaendelea Kimahakama.


Nikki amebainisha hayo wakati alipokuwa akifanya mahojiano na mwandishi wa habari hii baada ya Mbunge huyo kutoa lawama zake kwa wasanii katika ukurasa wake wa twitter asubuhi ya leo kutokana na kuwaona wapo kimya katika kesi inayomkabili Mbunge wa Mbeya Joseph Mbilinyi 'Sugu' ya kutoa maneno yenye kuleta chuki kati ya serikali na wananchi wakati alipokuwa katika mkutano wake wa hadhra ambao ulifanyika Disemba 31, 2017 jijini Mbeya.

Huu hapa chini ndio ujumbe wenyewe wa Mhe. Joshua Nassari
"Wasanii hawana umoja, chama chao hakina nguvu kwa hiyo hata kunapotokea jambo wasanii walitolee sauti kwa pamoja kuna hakuna 'platform' ya kushikilia jambo hilo na kujikuta kila msanii yupo peke yake, na kupaza sauti kila mtu peke yake wasanii wengi wanaogopa hilo", alisema Nikki wa Pili.

Pamoja na hayo, Nikki wa Pili aliendelea kwa kusema si jambo la kweli kama watu wanavyodhania kuwa tasnia ya muziki imemtenga Sugu ila tatizo lipo katika namna ya uwasilishaji wa jambo hilo.

"Hapana hatuwezi kumtenga Mhe. Sugu ila kuna jambo moja naweza kusema kwamba hili suala bado lipo kimahakama na tumeona wenyewe wamewaweka Wanasheria, kwa hiyo sisi wasanii bado hatuna ufahamu wa kujua jambo likiwa Mahakamani unaweza kulisema kwa upande gani kwa maana mara nyingi huwa tunaambiwa tusiingilie kazi za Mahakama", alisisitiza Nikki wa Pili.

Kitaalamu Haya ndio Madhara ya Kuchora TATTOO

$
0
0
Tattoo ni utamaduni ambao asili yake ni kutoka mabara ya Ulaya, Amerika na Asia lakini kwa sasa hata hapa Tanzania umekuaja kwa kasi hasa kwa vijana.

Leo January 27, 2018 nakusogezea Daktari Bingwa kutoka Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) Dr. Heri Tungaraza ambaye ametufafanulia madhara yanayoweza kutokea kutokana na kuchora Tattoo.

VIDEO:


Pata Dawa Bora ya Nguvu za Kiume na Maumbile Madogo ya Kiume ( Super Shafti)

$
0
0

DAWA BORA YA NGUVU ZA KIUME NA MAUMBILE MADOGO YA KIUME ( SUPER SHAFITI) NI DAWA YENYE UWEZO MKUBWA WAKUTIBU UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME


 (SUPER SHAFITI ni dawa ya asili yenye uwezo mkubwa wa kuogeza nguvu za kiume maradufu
(1) itakufanya uwe na nguvu za ajabu ukiwa unafanya ntedo la ndoa
(2) inaogeza hamu ya kurudia ntedo la ndoa zaidi ya mara tatu bila kuchoka
( 3) itakufanya uchelewe kufika kileleni dani ya dk 30
( 4)  itaimalisha milija ya uume iliyo legea au kusinyaa
(5) lnarefusha na kunenepesha uume saizi utakavyo kuazia ichi 1-8 unene sm 2-4
 (6) itakupa nguvu za kusimamiasha uume wako barabara kama_ msumari wakati wa ntedo la ndoa
(7) inasaidia kusafisha mishipa. ya kwenye uume na hivyo kusaidia Katika kuongeza kasi ya msukumo wa damu kwenye mishipa ya uume
(8) usaidia kuurudisha nje uume ulioingia ndani
(9) inasaidia kuogeza manii nyingi ambazo vina viini vya uzazi
(10)usaidia kutibu madhara ya punyeto ,matumizi makali ya  madawa ya kizugu mirungi bangi na sigara

KWA NINI BAADHI YA WANAUME WENGI WANA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME NA KUWA NA MAUMBILE MADOGO YA KIUME NINI CHANZO CHAKE?

ni kutokana na magonjwa megi kuongezeka yakiwemo kisukari presha ya kupanda na kushuka upigaji wa punyeto wa mda mrefu magonjwa ya moyo ngiri ya kuviba korondani vidonda vya tumbo
Msongo wa mawazo  tumbo kuuguruma kujaa ngesi kutopata choo vinzuri maumivu ya mgongo kiuno na tumiaji wa madawa makali ya kizungu ya kuongeza nguvu za kiume kuzaliwa na chango linaloshabulia neva za ukuwaji wa uume utumiaji wa mirungi bangi sigara na nk  tunapenda kuwatangazia wasomaji, wa makala zetu kuwa tunazo dawa nzuri za asili ambazo hazina mazala na zinazotibu na kuponyesha matatizo ya upungufu wa nguvu za kiume na maumbile ya kiume

NA TUNATIBU MAGONJWA YOTE SUGU KAMA KISUKARI PRESHA AINA YOTE UGONJWA WA MOYO SITRUKO KWIKWI KICHOMI MINGUU KUFA NGAZI ASIMA NK MZEE ISAYA ANAPATIKANA MAGOMENI MIKUMI KARIBU NA KANISA  TUMAINI HEBRAST CLINI NDIYO JIBU NA SULULISHO YA MATATIZO YOTE

PIGA simu 0745495181 au 0682644040

Kwa watu wa mikoa huduma utatumiwa na watu wa nje ya nchi utazipata dsm kama huna nafasi ya kufika ofisini kwetu utaletewa popote ulipo

Bodi ya Ligi Yaipiga Faini Jumla Milioni Moja Mbeya City

$
0
0
Bodi ya Ligi Yaipiga Faini Jumla Milioni Moja Mbeya City
Kamati ya Utendaji ya Shirikisho la mpira wa miguu Tanzania kupitia Mkurugenzi wa Ligi Boniface Wambura imetangaza kuipiga faini ya jumla ya shilingi milioni moja klabu ya Mbeya City kwa makosa mawili tofauti.


Wambura amebainisha hayo wakati alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari leo Jijini Dar es Salaam na kusema timu hiyo ilitenda kosa la kutumia mlango usio rasmi kuingilia uwanjani katika mechi iliyofanyika Januari 1,2018 Jijini Mbeya ambapo kitendo hicho ni kosa kwa mujibu wa kanuni za ligi kuu na kutozwa laki 5 kama adhabu yao.

Aidha, Wambura alisema Kamati iliiagiza Sekretarieti ya Bodi ya Ligi kutoa waraka kwa wamiliki wa viwanja kuhakikisha timu zote zinaingia uwanjani kwa kutumia milango rasmi nasio vinginevyo.

Mbali na hilo, Wambura amesema Klabu hiyo pia imepigwa faini ya laki 5 kutokana na mashabiki wake kuingia uwanjani na kumzonga mwamuzi kwa madai alikataa kutoa 'penalti' kwa timu hiyo.

Kwa upande mwingine, Kamati ya Utendaji ya Shirikisho la mpira wa miguu Tanzania kupitia Mkurugenzi wa Ligi Boniface Wambura imetangaza kumfungia kocha wa timu hiyo Ramadhani Mwazurimo mechi mbili na kupigwa faini ya laki 5 kutokana na kutoa lugha ya kashfa katika mechi ya Tanzania Prisons dhidi ya Mbeya City iliyochezwa Januari 14, 2018 kwenye uwanja wa Kumbukumbu ya Sokoine jijini Mbeya.

Watumishi 58 Wakufukuzwa Kazi Ruvuma

$
0
0
Watumishi 58 Wakufukuzwa Kazi Ruvuma
Halmashauri ya mji wa Mbinga mkoani Ruvuma imewafukuza kazi watumishi wake 58 kwa makosa mbalimbali ikiwemo kughushi vyeti vya kidato cha nne na wengine kwa kuisababishia hasara halmashauri hiyo.


Uamuzi huo umetangazwa na Mwenyekiti wa halmashauri ya mji wa Mbinga Mheshimiwa Egno Kipwere ambapo watumishi waliofukuzwa kazi ni wa kada mbalimbali wakiwemo walimu na Maofisa Watendaji pamoja na Afisa Misitu wa halmashauri hiyo Bw. David Hyera.

Auawa Kikatili Baada ya Kutekwa na Mume Wake

$
0
0
Binti wa miaka 24 mwenye mtoto mmoja ambaye ni raia wa Kenya, ameuawa kikatili baada ya kutekwa na mume wake ambaye alikuwa na rafiki yake kisha kumwambia rafiki yake huyo ambake binti huyo na baada ya mateso hayo kwa kushirikiana wakamwagia tindikali.

Lucy Ndungu aliwekewa dawa za kulevya na mumewe na ndipo alipoweza kumteka akiwa na rafiki yake, na baada ya kumbaka na kummwagia tindikali waliutupa mwili wake kando ya barabara.

Familia ya marehemu imeeleza kuwa ilimkuta Lucy anamajeraha ya kuungua kwa 75% ya mwili mzima huku hali yake ikiwa mbaya sana na hivyo akawahishwa katika Hospitali ya Taifa Kenyatta kupatiwa matibabu lakini hata hivyo akiwa kwenye matibabu hayo alifariki dunia.

Inaelezwa sababu ya mume huyo kufanya hivyo ni kwamba, walikuwa kwenye ugomvi na Lucy akaamua kuachana naye na kuondoka nyumba waliokuwa wanaishi pamoja na kukataa kurudiana na mumewe huyo jambo ambalo linadaiwa kumkasirisha mwanaume huyo.

VIDEO: Full Video CCM Wakizindua Kampeni Kinondoni

$
0
0
Chama cha Mapinduzi CCM kimezindua kampeni zake za Ubunge wa jimbo la Kinondoni huku Waziri wa Mambo ya Ndani, Mwigulu Nchemba pamoja na Waziri wa zamani wa Maji, Steven Wassira wakimnadi mgombea wa Chama hicho, Maulid Mtulia.

TAZAMA FULL VIDEO HAPA CHINI...USISAHAU KUSUBSCRIBE

VIDEO: Makonda Aangua Kilio

$
0
0
Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Paul Makonda  leo ametembelea na kutoa pole  kwa Familia ya Wastaafu ya Bwana Edward Bejumula na Bi. Stella Bejumula walioteseka kwa Miaka Sita bila Makazi baada ya kudhulumiwa Nyumba yao ambapo ameahidi kulivalia njuga suala hilo kuhakikisha haki inatendeka bila kuvunja sheria.

 TAZAMA FULL VIDEO HAPA CHINI .....USISAHAU KUSUBSCRIBE 

Kauli ya Jaji Mkuu Yaamsha Upya hoja ya Mgawanyo wa Madaraka

$
0
0
Kauli ya hivi karibuni Jaji Mkuu wa Tanzania, Profesa Ibrahim Juma kuwa viongozi wa Serikali na wanasiasa wasiingilie Mahakama na kudharau amri za mhimili huo, imeamsha upya hoja la mgawanyo wa madaraka baina ya mihimili mitatu ya dola ambayo imekuwa mjadala kwa muda mrefu.

Mjadala kuhusu mgawanyo huo wa Serikali, Bunge na Mahakama umekuwapo nchini kwa muda mrefu hasa wakati wa mchakato wa mabadiliko ya Katiba kuwa inaonekana Serikali ama inaizidi nguvu au inaingilia shughuli za mihimili mingine, licha ya kwamba yote hiyo inatakiwa kuonekana sawa.

Hata hivyo, baadhi ya watu huamini kwamba mhimili wa Serikali ambao unaongoza dolo ndio wenye nguvu kwa kuwa unasimamia mapato na matumizi ya mihimili mingine.

Hata Rais John Magufuli alipozungumza na wahariri wa vyombo vya habari kuhusu suala hilo Novemba 2016, alisema, “Mihimili hiyo (Bunge, Serikali na Mahakama) inaweza ikalingana, lakini inawezekana kuna mhimili ambao umechimbiwa zaidi kwenda chini.”

Akisisitiza jibu lake, Rais alizungumzia jinsi alivyokwenda kwenye shughuli ya mahakama na akaombwa fedha na uongozi wa mhimili huo kwa ajili ya uendeshaji wa shughuli zake kwa kutambua kuwa, Rais ndiye mwenye uwezo wa kuwapatia fedha hizo.

Ndani ya mjadala huo, pia yamekuwapo madai miongoni mwa wananchi kupitia maoni yao wakati wa mchakato wa Katiba, wanasiasa, wanaharakati kuwa Serikali imekuwa inaingilia shughuli na mihimili mingine – Bunge na Mahakama, jambo ambalo linaathiri uhuru wake.

Pengine ni kutokana na madai hayo au mengine, ndipo Jaji Mkuu anaibuka na ujumbe mahususi kuhusu maandalizi ya maadhimisho ya Wiki ya Sheria kwa Serikali;

“Nawasihi viongozi wote wa Serikali wenye mamlaka za kikatiba na kisheria, wabaki ndani ya maeneo yao ya kikatiba na wajiepushe na kuingilia maeneo yaliyo ndani ya haki, hadhi na mamlaka ya Kikatiba ya Mahakama.”

Akaongeza kwamba kuanzia sasa (Mahakama) watakuwa wakali kwa mtu atakayeingia katika anga zao, huku akiwataka mahakimu na majaji kuchukua hatua kwa watu wanaodharau amri zao, kwa mujibu wa Katiba ya Tanzania, mamlaka ya utoaji haki ni ya Mahakama pekee.

Hata hivyo, akijibu kwa nini aliamua kutoa kauli hiyo, Jaji Mkuu anasema ni kutokana na taarifa za vyombo vya habari ambavyo vimekuwa vikiripoti matukio hayo ya amri za Mahakama kuvunjwa.

Hakuishia hapo, Jaji Mkuu akawataka mahakimu ambao kwa bahati mbaya amri zao zinavunjwa na wanaonekana hawachukui hatua waanze kufanya hivyo kama Bunge linavyofanya, kwamba ukiingia katika anga zake, utaitwa mbele ya kamati, utaulizwa maswali na hatua zinachukuliwa.

Jaji Mkuu anasema Mahakama ina nguvu kama hiyo na si Jaji Mkuu mwenye nguvu hiyo pekee bali kwenye kila Mahakama; mahakama za mwanzo, mahakama za wilaya na mahakama za hakimu mkazi na asitokee mtu akajivika kofia ya kimahakama, atachukuliwa hatua.

Jaji Juma anasema kwa mujibu wa Katiba, sheria ndio inayotakiwa ipewe nguvu na si masuala ya kisiasa kwa kuwa nguvu ya Serikali ni sheria na si mtu.

“Sheria ikikupa nguvu unaitumia, ikikupa mamlaka unayatumia. Siasa haikupi nguvu, sheria ndio inakupa nguvu na tujaribu tubaki ndani ya sheria na ndani ya Katiba hakutakuwa na mvurugano. Vilevile tunawataka wale ambao wamepewa mamlaka yao, wabaki huko waliko na tukifanya hivyo hatutakuwa na migongano yoyote,” anahitimisha.

Kauli hiyo ya inaungwa mkono na Ibara ya 107 A (1) ya Katiba ya Tanzania inayosema: “Mamlaka ya utoaji haki katika Jamhuri ya Muungano itakuwa mikononi mwa Mahakama ya Tanzania na Mahakama ya Zanzibar, na kwa hiyo hakuna chombo cha Serikali wala cha Bunge au Baraza la Wawakilishi la Zanzibar kitakachokuwa na kauli ya mwisho katika utoaji haki.”

Mjadala mtandaoni

Muda mfupi baada ya maelezo hayo, Mbunge wa Arusha Mjini (Chadema), Godbless Lema aliandika kwenye ukurasa wake wa Twitter, “Mh Jaji Mkuu kauli kuhusu wanasiasa na watendaji wa Serikali kutokuingilia Mahakama ni kauli muhimu kwa wakati huu, lakini Mahakama ambayo ni imara katika haki inawezaje kukubali kuingiliwa? Mahakama inapaswa kujitazama zaidi. Mahakama ikiyumba Taifa linayumba.”

Si Lema tu aliyezungumzia hilo, wananchi wengine mbalimbali walitoa maoni yao kuhusu kauli hiyo kupitia ukurasa wa Facebook wa Mwananchi, Twitter na Instagram, huku wengine wakienda mbali zaidi kwa kumtaka Jaji Mkuu kuwaeleza maneno hayo wafuasi wa CCM, wakidai kwamba wapinzani hawana jeuri ya kuingilia Mahakama.

Kwa jinsi mjadala ulivyokwenda ni wazi kuwa Jaji Mkuu Profesa Juma ameona kuna kitu ambacho pia wananchi wanakiona hakiendi sawa na kuamua kufikisha ujumbe wake kwa njia hiyo.

Wachambuzi wa masuala ya siasa wanatafsiri kauli ya Jaji Mkuu kama “kuchoshwa kwa mhimili huo kuingiliwa na hivyo ameamua kufikisha ujumbe kwa wenye tabia hizo ili waache mara moja.

Hatua ya Jaji Juma bila shaka ni ya kupongezwa kwani si tu imeonyesha kwamba mahakama imezinduka na kutambua wajibu na nguvu zake na hivyo inafungua pazia la demokrasia na mgawanyo wa madaraka baina ya mihimili hii mitatu ya dola.

Hatua hiyo ikizingatiwa na kutekelezwa itasaidia kuifanya mahakama iaminike na kiwe chombo pekee kimbilio kwa kila mtu kwa ajili ya utoaji haki.

Ingawa Jaji Mkuu hakutoa mifano ya matukio ya kuingilia uhuru wa mahakama, mifano ipo mingi, mfano wameshuhudiwa baadhi ya watendaji wa Serikali wakiamuru ubomoaji wa nyumba ambazo inadaiwa zimejengwa katika hifadhi ya barabara, zikiwamo zilizokuwa na amri ya mahakama ya kuzuia zisibomolewe.

Mbali na mahakama, hivi karibuni Mbunge wa Kigoma Mjini (ACT-Wazalendo), Zitto Kabwe aliwakaririwa akisema hata Bunge limekuwa likifanya kazi kwa kuingiliwa na Serikali.

“Maneno na vitendo vya Rais vinaashiria kuwa Bunge halina uhuru wake na mimi kama mbunge nina wajibu wa kuonyesha kutopendezwa kwangu,” alisema Zitto kupitia mtandao wa Twitter na kuongeza kuwa “Ni dalili ya wazi ya kufifisha sauti ya Bunge na kupandisha sauti ya Serikali.

Moja ya matukio ambayo mbunge huyo alitaja kama kuingilia mhimili huo ni kuzuia matangazo ya moja kwa moja ya Bunge kwa kigezo cha gharama, huku hata vituo binafsi ambavyo vilipanga kurusha Bunge moja kwa moja bila malipo vikizuiwa.

Akijadili suala la uhuru wa mahakama na kauli ya Jaji Mkuu, Mratibu wa Kitaifa wa Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binadamu (THRDC), Onesmo Olengurumwa anasema kwa muda mrefu wanasiasa na watetezi wa haki wamekuwa wakipigia kelele suala hilo lakini halikuonekana kufanyiwa kazi, hivyo hatua ya Jaji Mkuu italeta matumaini yalikuwa yametoweka.

Anasema katika suala la utoaji haki, Mahakama inapaswa kusimama kwa miguu yake isishurutishwe na isiingiliwe; majaji wazingatie sheria wakati wa kutoa hukumu.

Haiingii akilini kwamba mahakama inatoa amri fulani, lakini watendaji walioko chini ya Serikali wakapuuza na wakaendelea na shughuli zao kana kwamba hakuna amri yoyote,” anasisitiza.

“Jaji Mkuu yuko sahihi kama kweli anamaanisha. Kwa muda mrefu tumeshuhudia viongozi mbalimbali wakiwamo wakuu wa wilaya wakijitokeza kuingilia mhimili huo na kusababisha ama kupingana au kuwagawa na matokeo yake wanashurutishana na kutishana hadharani.”

Onesmo anasema hata kama Mahakama imekosea, kuna utaratibu wa kisheria wa kufuata ili kuipinga na si kama hali ilivyo sasa.

Anasema kuwa jambo hilo la kuingiliwa Mahakama likiachiwa liendelee litasababisha athari kuu tatu kwa jamii na kuzitaja kuwa ni pamoja na kuvunja Katiba.

Mosi, anasema mahakama ni chombo cha kutoa haki na endapo haitakuwa huru, ni wazi kuwa Katiba itakuwa inavunjwa na mwananchi atakosa haki zake za msingi.

Pili, anasema tatizo jingine ni kutengeneza Taifa lisilo fuata utawala wa kisheria na kwamba watu wataamua wanavyotaka wao, jambo ambalo litakuwa si zuri kwa mustakabali wa nchi.

“Jingine, ni kuingia katika migogoro isiyo na tija; itafika wakati wananchi watachoshwa na matendo hayo na kusababisha migogoro mikubwa na matokeo yake hayatakuwa mazuri,” anasisitiza Mratibu huyo wa masuala ya haki za binadamu.

Ni kutokana na umuhimu huo na mjadala mpana katika mchakato wa Katiba ikawekwa ibara ya 169 inazungumzia kwa kina uhuru wa mahakama.

Katiba inayopendekezwa

196 (1) Katika kutekeleza mamlaka ya utoaji haki, Mahakama zote zitaongozwa na masharti ya Katiba hii na hazitaingiliwa ama kwa kudhibitiwa, kushinikizwa au kupewa maelekezo na mtu au chombo chochote.

(2) Nafasi ya madaraka ya Jaji wa Mahakama ya Juu, Mahakama ya Rufani au Mahakama Kuu ya Jamhuri ya Muungano haitafutwa wakati wowote ule ikiwa kuna mtu ambaye kwa wakati huo anashikilia nafasi hiyo.

(3) Mishahara na malipo mengine ya Majaji wa Mahakama ya Juu, Mahakama ya Rufani na Mahakama Kuu ya Jamhuri ya Muungano yatalipwa kutoka katika Mfuko Mkuu wa Hazina.

(4) Mshahara na malipo mengine yanayolipwa kwa Jaji wa Mahakama ya Juu, Mahakama ya Rufani au Mahakama Kuu ya Jamhuri ya Muungano hayatabadilishwa kwa maana ya kumuondolea faida Jaji husika.

(5) Malipo ya mafao ya kustaafu ya Jaji wa Mahakama ya Juu, Mahakama ya Rufani au Mahakamu Kuu ya Jamhuri ya Muungano hayatabadilishwa kwa maana ya kumuondolea faida Jaji husika wakati wote wa uhai wake.

(6) Jaji wa Mahakama ya Juu, Mahakama ya Rufani, Mahakamu Kuu ya Jamhuri ya Muungano au Mahakama Kuu ya Zanzibar hatashtakiwa kwa jambo lolote alilolifanya au kutolifanya kwa nia njema katika   


Yanga SC yavunja rekodi ya Azam FC Chamazi

$
0
0
Mchezo wa ligi kuu soka Tanzania Bara baina ya mabingwa watetezi klabu ya Yanga dhidi ya Azam FC umemalizika katika uwanja wa Azam Complex Chamazi kwa mabingwa hao kushinda jumla ya mabao 2-0.

Kwa ushindi wa Yanga SC unaifanya timu hiyo kuvunja rekodi ya wana lamba lamba Azam FC ya kutokupoteza hata mchezo mmoja toka kuanza kwa ligi kuu soka Tanzania Bara msimu huu wa mwaka 2017/18.

Wafungaji katika mchezo alikuwa Shabani Chilunda wa Azam FC wakati kwa upande wa Yanga SC akiwa Obrey Chirwa na Gadiel Michael.

Kwa matokeo hayo inaifanya mabingwa watetezi Yanga SC kufikisha jumla ya pointi 28 wakiwa nafasi ya tatu, Azam FC ikisalia na alama zake 30 nafasi ya pili huku Simba SC ikiongo katika msimamo wa ligi kwa kuwa na pointi 32 na mchezo mmoja mkononi ambao unatarajiwa kupigwa hapo kesho siku ya Jumapili.

Katika michezo mingine iliyopigwa hii leo timu ya Mbeya City ikiwa nyumbani imekubali kutoka sare ya mabao 0 – 0 dhidi ya Mtibwa Sugar wakati Mwadui FC ikiwa nyumbani imelizimishwa sare ya magoli 2 – 2 na Njombe Mji wakati Kagera Sugar ikitoka suluhu ya bila kufungana dhidi ya Lipuli FC.

Chadema yazidi Kukimbiwa na Madiwani wake

$
0
0
Wimbi la madiwani wa Chadema kujivua uanachama na kujiunga na CCM limezidi kukikumba chama hicho kikuu cha upinzani nchini baada ya leo Januari 27, mwaka 2018 madiwani wake wanne kujiunga na chama tawala, wakiwemo watatu wa Halmashauri ya Wilaya ya Rombo  mkoa wa Kilimanjaro.

Wakati diwani wa Kimara (Chadema), Pachal Manota akitambulishwa katika uzinduzi wa kampeni za ubunge za chama hicho jimbo la Kinondoni zilizofanyika viwanja wa Biafra, wenzake watatu walitambulishwa kwenye mkutano wa kampeni za ubunge jimbo la Siha mkoani Kilimanjaro uliofanyika eneo la Makiwaru.

Madiwani hao ni Juliana Malamsha, Martha Ushaki (wote Viti maalum) na Frank Umega (kata ya Kelamfua).

Wametambulishwa na Naibu Katibu Mkuu wa CCM-Bara, Rodrick Mpogolo wakati akimnadi mgombea ubunge wa chama hicho jimbo la Siha, Dk Godwin Mollel.

Mpogolo amesema viongozi wa upinzani wanajiunga na CCM baada ya kubaini ajenda ya kuwahudumia wananchi, kuwaletea maendeleo ipo katika chama tawala pekee .

"Kuna  wimbi kubwa la viongozi wa upinzani kujiunga na CCM. Hii inatokana na viongozi hao kubaini kuwa ajenda ya huduma na maendeleo iko katika chama hiki pekee. Tupeni Dk Mollel ili tuweze kutekeleza agenda hii muhimu,” amesema Mpogolo.

Uamuzi wa madiwani wa Chadema kuhamia CCM mpaka sasa umeziweka Halmashauri tano zilizo chini ya vyama vinavyounda Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa) kuwa hatarini kuchukuliwa na CCM.

Halmashauri hizo ni Arusha, Arumeru, Hai, Siha na Iringa ambazo madiwani wake, hasa kutoka Chadema wametimkia CCM kutokana na sababu tofauti, kubwa ikiwa ni kuunga mkono jitihada zinazofanywa na Rais John Magufuli.

Chadema yazindua kampeni zake Kinondoni

$
0
0
Kampeni za Ubunge katika jimbo la Kinondoni kwa Chama cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA zimefunguliwa leo rasmi katika uwanja wa Ali Mapilau ,Mwananyamala na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali wa Chama hicho akiwemo Waziri Mkuu Mstaafu na Mjumbe wa kamati kuu, Edward Lowassa.

Chadema imemsimamisha Niabu Katibu Mkuu wake Zanzibar, Salum Mwalimu kugombea jimbo hilo ambalo lilikuwa likishikiliwa na Maulid Mtulia wa CUF ambaye amejiunga na CCM ambayo imemsimamisha tena kugombea nafasi hiyo.

Akizungumza katika kampeni hizo Mbunge wa Arusha Mjini, Gobless Lema alisema muda wa chama hicho kulia umekwisha na kuwataka wanachama na hasa vijana wa Kinondoni kutembea nyumba kwa nyumba kuhakikisha mgombea wao Salumu Mwalimu anaibuka mshindi.

Nae Mwenyekiti wa Baraza la Vijana la Chadema Taifa BAVICHA, Patrick Ole Sosopi alisema, " Mimi kama Mwenyekiti wa Vijana wajanja zaidi Tanzania nitahakikisha tunabeba lawama hadi Mwalimu anatangazwa mshindi, tunawataka Polisi kutuacha tupambane wenyewe na wasiingilie na wakijaribu kumteka kiongozi wetu yeyote na wao tutawateka,"

Mbunge wa Mikumi, Joseph Haule Profesa Jay licha ya kufanya kampeni hizo kwa kuimba nyimbo zake na wanachama wa chama hicho pia alitumia fursa hiyo kuwaomba wapiga kura wa Kinondoni kuhakikisha hawamchagui Maulid Mtulia kuwa mbunge wao kutokana na usaliti aliowafanyia.

Lowassa Amnadi Salum Mwalimu Kinondoni

$
0
0
Waziri Mkuu Mstaafu na Mjumbe wa Kamati Kuu wa Chama cha Demokrasia na  Maendeleo CHADEMA, Edward Lowassa jioni leo amemnadi Mgombea wa Ubunge wa Kinondoni kupitia chama hicho, Salumu Mwalimu huku akiwataka wakazi wa Kinondoni kuacha kumuongelea mgombea wa CCM, Maulid Mtulia maana amekuwa msaliti kwao.

Lowassa alitumia wakati huo pia kuwashukuru wananchi wa Kinondoni kwa kumpigia kura wakati wa uchaguzi mkuu uliopita, na kuwaomba zile kura walizompigia 2015 basi wazielekeze kwa Mwalimu ambaye anaamini ni msomi mwenye kuweza kuwatetea wakazi wa Kinondoni.

" Msiogope vijana wa Kinondoni wenzetu wamekuwa wajanja wakilinda kura zao sasa na sisi kama ambavyo wazungumzaji wengine wamesema basi tunaomba mlinde kura zetu ikiwezekana tulale katika vituo vya kupigia kura kuhakikisha hatuibiwi.

Nae Waziri Mkuu Mstaafu wa awamu ya tatu, Fredrick Sumaye alisem, " Hakikisheni mnamchagua Mwalimu huyu ndie mtu safi wa kuhakikisha analeta maendeleo katika jimbo lenu,"

Kwa upande wake Mwalimu ambaye pia ni Naibu Katibu Mkuu Zanzibar, alisema " Achaneni na wao wanaosema mimi sio mkazi wa hapa nachoomba ni kura zenu ambazo zitanifanya nikawatetee kuwajengea shule, kuhakikisha ajira kwa vijana,"

Kampeni za chama hicho zitaendelea kesho katika eneo la Kigogo jijiji Dar es Salaam ambapo zitaongozwa na Mwenyekiti wa Chama hicho, Freeman Mbowe.

Alichokisema Mr T Kuhusu Darassa Kuwa Teja wa Madawa

$
0
0
Baada ya kimya cha muda mrefu kwa msanii Darassa ambaye mwaka juzi 2016 alitingisha sana na wimbo wake 'Muziki' kumeibuka tetesi kuwa msanii huyo naye amejiingiza katika matumizi ya dawa za kulevya, jambo ambalo limewashtua wengi.

Kufuatia tetesi hizo mtangazaji wa kipindi cha Bongo fleva Top 20 ya East Africa Radio, Jr Junior alimvutia waya msanii huyo lakini bahati mbaya hakuweza kupokea simu yake jambo ambalo lilimfanya kumpigia simu mtu wake wa karibu ambaye ni producer wake Mr T Touchez ili kufahamu ukweli juu ya tuhuma au tetesi hizo.

Baada ya Mr T Touchez kupigiwa simu alisema yeye hafahamu lolote juu ya jambo hilo na kukiri kuwa kwa sasa hajakutana na msanii huyo muda kidogo, hivyo hafahamu lolote kuhusu hicho kinachoelezwa kutumia dawa za kulevya.
Viewing all 104709 articles
Browse latest View live


Latest Images