Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104414 articles
Browse latest View live

Shilole Atumbukiwa Nyongo na Gauni Alilonunua Mtandaoni ....Ataka Kulichoma Moto

0
0
Shilole Atumbukiwa Nyongo na Gauni Alilonunua Mtandaoni ....Ataka Kulichoma Moto
Mwanamuziki wa wa miondoko ya Mduara, Zuwena Mohamed ‘Shilole’ amesema gauni alilovaa kwenye uzinduzi wa kumtambulisha mwanamuziki Maromboso ‘Mbosso’ uliofanyika katika Ukumbi wa Hyatt hivi karibuni, limemtia aibu kiasi cha kutaka kulichoma moto.

Akizungumza na Star Mix, Shilole alisema kuwa, aliagiza gauni lile mtandaoni lakini hakujua kuwa lingemtia aibu vile kwa maana lilimkosesha kabisa raha kwenye sherehe hiyo na kujutia hela ambayo aliitoa.

“Jamani katika kitu ambacho kimenitia aibu kwenye gauni nililovaa siku ile sitosahau yaani mpaka sasa nataka nilichome moto kabisa nisiwe naliona,” alisema Shilole.

Picha: Mamia Wakusanyika Usiku Nyumbani kwa Radio Kwaajili ya Kuomboleza

0
0
Picha: Mamia Wakusanyika Usiku  Nyumbani kwa Radio Kwaajili ya Kuomboleza
Usiku wa jana watu kibao wamehudhuria nyumbani kwa Moses Ssekibogo maarufu kama Mowzey Radio, kuomboleza msiba wa msanii huyo ambapo shughuli hizo zinafanyika nyumbani kwake Makindye mjini Kampala.

Radio alifariki Alhamisi hii katika Hospitali Kuu ya Kampala baada ya kulazwa kwa siku 10 baada ya kudaiwa kushambuliwa kwenye bar moja huko Entebbe.


Marekani Yamshutumu Odinga kwa 'Kujiapisha' Kenya

0
0
Marekani Yamshutumu Odinga kwa 'Kujiapisha' Kenya
Serikali ya Marekani imesema imesikitishwa na hatua ya kiongozi wa upinznai nchini Kenya Raila Odinga ya kujiapisha Jumanne wiki hii.

Marekani pia imeishutumu serikali kwa kufungia vituo vinne vya habari nchini humo ambavyo viliadhibiwa baada ya kupeperusha moja kwa moja hafla hiyo ya upinzani.

Kupitia taarifa, wizara ya mambo ya nje ya Marekani imesema taifa hilo linaamini mizozo yoyote ile inafaa kutatuliwa kwa njia zifaazo kisheria.

"Tunakataa vitendo vyovyote ambavyo vinahujumu Katiba ya Kenya na utawala wa sheria. Uhuru Kenya alichaguliwa kuwa Rais wa Jamhuri ya Kenya mnamo Oktoba 26, 2017 katika uchaguzi ambao uliidhinishwa na Mahakama ya Juu," taarifa hiyo iliyotumwa na msemaji wa wizara hiyo Hearther Nauerth imesema.

Bw Odinga alisusia uchaguzi huo wa marudio na amesema hamtambui Rais Kenyatta kama rais halali wa taifa hilo.

Jumanne, alikula kiapo kuwa Rais wa Wananchi katika hafla iliyohudhuriwa na maelfu ya wafuasi wake uwanja wa Uhuru Park, Nairobi.

Mgombea mwenza wake Kalonzo Musyoka, ambaye ni makamu wa rais wa zamani, hakuhudhuria sherehe hiyo ingawa walikuwa wameahidi kuapishwa wote wawili kwa pamoja.

Wafuasi wa Bw Odinga wakisherehekea Kisumu baada yake kula kiapo Uhuru Park, Nairobi
Image caption
Wafuasi wa Bw Odinga wakisherehekea Kisumu baada yake kula kiapo Uhuru Park, Nairobi
Bw Musyoka baadaye alisema alipokonywa walinzi wake na hivyo kuzuiwa kuondoka nyumbani kwake kwenda kuhudhuria sherehe hiyo.

Jumatano, mbunge wa upinzani Tom Joseph Kajwang' anayewakilisha eneo bunge la Ruaraka, Nairobi alikamatwa na akashtakiwa kwa makosa ya kuhudhuria mkutano haramu na kushiriki katika kulishwa kiapo kwa Bw Odinga kwa njia ya kudai kumfunga Bw Odinga "kutekeleza kosa la jinai la uhaini".

Bw Kajwang', ambaye ni wakili, alikuwa amevalia sare za uwakili na kwa pamoja na mshauri wa zamani wa Bw Odinga, Miguna Miguna, walikuwa karibu na Bw Odinga alipokuwa anakula kiapo.

Marekani imesema imesikitishwa sana na vitendo vya serikali kwa "kufunga, kutisha na kuminya vyombo vya habari".

"Uhuru wa kujieleza, ikiwa ni pamoja na kwa wanahabari, ni muhimu sana kwa demokrasia, na umelindwa kwenye Katiba ya Kenya," taarifa ya Marekani imesema.

"Tunaihimiza serikali na Wakenya wote kuheshimu uhuru wa kujieleza na kutii agizo la mahakama na kuvifungulia vituo hivyo vya televisheni."

Mahakama ilikuwa imeamuru vituo hivyo vya Citizen, Inooro, NTV na KTN vifunguliwe Alhamisi lakini kufikia Ijumaa asubuhi, agizo hilo lilikuwa bado halijatekelezwa.

Ingawa Marekani imewasifu polisi na vikosi vya usalama kwa jinsi walivyosimamia hafla hiyo ya kuapishwa kwa Bw Odinga Jumanne, wamesema visa vya kukamatwa na kushtakiwa kwa washukiwa vinafaa kutekelezwa kwa kufuata sheria kikamilifu.

Marekani imewahimiza viongozi wa kisiasa Kenya kufanya mazungumzo kwa lengo la kuimarisha uwiano na utangamano na kutatua matatizo ya muda mrefu nchini humo.

Hatari Tupu! Huu Hapa Uamuzi Alioufanya Zari kwa Diamond

0
0
Hatari Tupu! Huu Hapa Uamuzi Alioufanya Zari kwa Diamond
Saa chache zimepita toka msanii Diamond Platnumz kudaiwa kutoka kimapenzi na wasichana wengine tofauti na mama watoto wake Zari the bosslady.

Inasemekana kuwa Diamond Platnumz hupeleka wasichana tofautitofauti nyumbani kwake Madale, kutokana na tetesi zilizokuwa zikiendelea kwenye mitandao ya kijamii ikaonekana Zari kukasirishwa na tabia hiyo.

Hivyo kupitia instagram account ya Zari ameonekana kumu’unfollow baba watoto wake Diamond Platnumz, kitu hiki kimeleta maswali mengi kwa baadhi ya mashabiki na wengi kuhusisha ukaribu uliotokea kati ya Wema Sepetu na Diamond siku ya uzinduzi wa kutambulisha rasmi Marombosso WCB.

Zari amwambia Mama Diamond “Tuhame Guest House tumwachie mwanao”

Vanessa Mdee Afunguka Kuhusu Wimbo wake Alioufanya na Marehemu Radio

0
0
Vanessa Mdee Afunguka Kuhusu Wimbo wake Alioufanya na Marehemu Radio
Mwimbaji Staa wa Bongofleva Vanessa Mdee ambaye kwa sasa yupo nchini Nigeria katika ziara yake ya kimuziki kwaajili ya kutambulisha albam yake ya Money Mondays amemzungumzia marehemu Radio ambaye hivi karibuni alipost picha wakiwa pamoja kumbe ilikuwa ni ishu ya wimbo walioufanya.

Vanessa amesema kuwa walikuwa kwenye mipango ya kushoot video ya wimbo huo na walikuwa wanamawasiliano mpaka alipopata ajali.

Pia ameeleza jinsi alivyopokea taarifa za msiba kwa mshtuko kwani mara ya mwisho aliwasiliana na Weasel kupitia simu ya Radio kipindi akiwa amelazwa na alipanga kwenda kumuona kipindi akirudi kutoka Lagos Nigeria lakini ndipo ikatokea amefariki..

Serikali Yawapa Onyo Wanaojidunga Sindano Kuongeza Maumbile

0
0
Serikali Yawapa Onyo Wanaojidunga Sindano Kuongeza Maumbile
SERIKALI imeonya kuwa dawa za kuongeza maumbile zina madhara makubwa katika mwili wa binadamu, ikiwamo kusababisha saratani hivyo kuwaasa wananchi kukubaliana na uumbaji wa Mungu.

Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya jamii, Jinsia, Wazee na Watoto,  Dk. Faustine Ndugulile, alisema hayo jana mjini hapa, alipokuwa akijibu swali la nyongeza la Mbunge wa Viti Maalum (Chadema), Suzan Lyimo.

Katika swali lake, Lyimo alihoji athari za kiafya kwa wanaoongeza maumbile kwa kujichoma sindano au kutumia dawa na serikali inatoa tamko gani kuhusu hilo.

"Kumekuwapo na matumizi ya dawa au sindano za kuongeza makalio na matiti, nataka kujua kuna athari yoyote kiafya na kama ndiyo serikali inatoa tamko gani?" alihoji.

Akijibu swali hilo, Dk. Ndugulile alisema sindano, vipodozi na dawa zingine zinazotumika kuongeza maumbile, zina madhara makubwa kwenye mwili ikiwamo kusababisha saratani.

“Mwenyezi Mungu alituumba kila mtu kwa aina yake, kwa rangi yake na maumbile yake. Nyongeza  hizi kitaalam zina madhara kama vilivyo vipodozi haramu.

“Ngozi ina matumizi yake Mwenyezi Mungu hakuiweka pale kwa makosa. Inatusaidia kujikinga na mionzi, kujikinga na magonjwa na matumizi ya vipodozi yanaleta madhara katika ngozi. Pia  yanasababisha mtu kupata saratani,” alisema Dk. Ndugulile.

Aliongeza kuwa: “Kauli yangu kwa wananchi waache kutumia vipodozi hivi na dawa hizi. Mwenyezi Mungu alituumba na makusudio yake tuendelee kwa maumbile na rangi zetu,”.

Katika swali la msingi, Mbunge wa Shaurimoyo, Mattar Ally  Salum (CCM), alihoji serikali ina mpango gani madhubuti wa kuzuia uingizwaji wa vipodozi visivyokuwa na viwango.

"Je, serikali inaweza kutumia fedha kiasi gani kuzuia bidhaa hizo kuingia  nchini? Je, adhabu gani inatolewa kwa yeyote anayekamatwa akiingiza nchini vipodozi visivyofaa kwa matumizi?" alihoji.

Akijibu swali hilo, Dk. Ndugulile alisema Mamlaka ya Chakula na Dawa (TFDA) imekuwa ikichukua hatua mbalimbali kudhibiti uingizwaji na utumiaji wa vipodozi hivyo.

Alisema mpaka sasa TFDA imesajili vipodozi 3,179 ambavyo ndivyo vinavyoruhusiwa kuingizwa na kutumika nchini.

Aidha, Dk. Ngugulile alisema  katika mwaka wa fedha wa 2016/17 maeneo 3,648 yalikaguliwa na kati ya hayo,  120 yalikutwa na vipodozi ambavyo havina viwango vinavyofaa kwa matumizi ya binadamu na wahusika walichukuliwa hatua za kisheria.

Pia alisema tani 407.82 za vipodozi vilivyopigwa marufuku vyenye thamani  ya Sh.  bilioni 1.36 ziliteketezwa na TFDA na kesi 52 zilifunguliwa mahakamani baada ya upelelezi kukamilika.

Kichuya Awapa raha Mashabiki wa Simba

0
0
Kichuya Awapa raha Mashabiki wa Simba
MAMBO anayoyafanya winga wa vinara wa ligi kuu, Simba, Shiza Kichuya, kwenye mazoezi ya timu hiyo yanayofanyika kwenye uwanja Chuo cha Bandari yamewakosha mashabiki wa timu hiyo.

Kichuya amekuwa akijituma kwenye mazoezi hayo na kuepelekea kupigiwa makofi kila anapogusa mpira na mamia ya mashabiki wanaohudhuria mazoezi hayo.

Mara baada ya kumalizika kwa mazoezi ya jana, kundi la watoto pamoja na watu wazima walimvamia Kichuya na kutaka kumbeba kumpeleka kwenye basi la timu hiyo.

Akizungumza na Nipashe, Kichuya, alisema kuwa mapenzi anayoonyeshwa na mashabiki hao yanamfanya kujituma zaidi ili asiwaangushe.

“Kwangu hii ni hamasa kubwa, hii itanifanya nijitume zaidi mazoezini ili kwenye mechi niisaidie timu yangu ipate ushindi,”alisema Kichuya.

Alisema, anajipanga kuhakikisha Simba inapata ushindi kwenye mchezo wao wa Jumapili dhidi ya Ruvu Shooting utakaochezwa kwenye uwanja wa Taifa.

Katika mzunguko wa kwanza timu hizo zilipokutana kwenye uwanja wa Uhuru, Simba waliibuka na ushindi mnono wa mabao 7-0.

Wizkid Aguswa na Kifo cha Radio Aandika Ujumbe Huu

0
0
Wizkid Aguswa na Kifo cha Radio Aandika Ujumbe Huu
Wizkid ameonyesha kugusa sana na kifo cha msanii wa Uganda ambaye amedumu kwenye tasnia ya muziki kwa zaidi ya miaka 10, Moses Ssekibogo maarufu kama Mowzey Radio ambaye amefariki jana (Alhamisi).

Wizkid ameonyesha hisia zake za kuumizwa na msiba huo, kutokana na ujumbe ambao ameuandika kupitia mtandao wake wa Instagram ukiwa unaosomeka, “Rest in paradise my brother Radio! 💔…Speechless… Love u forever star! ❤️ !! Nothing can ever be the same! 💔! Superstar lives forever…🖤🖤🖤.”

Radio alilazwa katika Hospital Kuu ya Uganda akipatiwa matibabu tangu January 23 mwaka huu ambapo hali yake ilidaiwa kuwa mbaya kufuatia majereha aliyoyapata kutokana na ugomvi uliotokea klabu huko mjini Entebbe.

Kwanini Baadhi ya Wanaume Wana Maumbile Madogo?

0
0
Matatizo haya yame kuwa yakiwaathiri watu wengi sana kisaikolijia hasa baada ya kujiona tofauti sana na wenzao kwa kawaida mwanaume ana takiwa awe na uume kuanzia inch(6_8)vinginevyo mtu huyo atakuwa na matatizo.

Zipo sababu nyingi zinazo sababisha tatizo hilo baadhi ni upungufu wa vichocheo (Hormones za Getrogen) Ambazo mwanaume akisha balehe vichocheo hivi huchochea ukuaji wa uume, chango husababisha NEVA ambayo huathiri misuri ya uume. Ngiri ambayo Huleta maumivu ya tumbo kuunguruma na kujaa guess, korodani moja kuvimba, kutopata choo vizuri , miguu kufa ganzi, maumivu ya kiuno,upigaji wa punyeto sababu hizi na nyingine hufanya uume kulegea na kusinyaa na kuwa mfupi na mwembaba na mara kwa mara hipelekea kupunguka kwa nguvu za kiume na ham ya tendo la ndoa hukosekana na kuisha kabisa

NSUMBU:__Ni dawa dawa inayo zalisha hormones za Gestrogen na kufanya uume kukua na kuongezeka mara dufu.

NZAGI :--Ni dawa bora ya kurudisha nguvu za kiume na kukupa hamu ya kurudia tendo la ndoa mara dufu utakuwa na uwezo wa kufanya tendo la ndoa zaidi ya mara nne
(4)bila hamu kuisha (kuchoka) dawa hii ni tiba kamili kwa matatizo hayo. Dawa hii pia itakufanya uchelewe kufika kileleni zaidi ya dk(15_30)kwa tendo moja la ndoa dawa hizi hazina madhara yoyote kwa mtumiaji kuanzia miaka(18_90)wana ruhusiwa kuzitumia Pia tunatibu KISUKARI, PRESHA, PUMU, MALARIA SUGU, MIMBA KUHARIBIKA(Chango)

POWER :__Ni dawa ya mitishamba inaongeza hips, (makalio), miguu, ina punguza maziwa (chuchu). Ina toa harufu mbaya sehem za siri Nk.

Pia anazo dawa za mvuto wa mapenzi,biashara, kurudishwa kazini, kumuita aliye mbali kwa mda mfupi tu

OSTADH JUMA ANAPATIKANA MBANGALA ZAKHIEM SIMU: 0769-597778 au 0784-002216 au 0627457957 Wote mnakaribishwa

Rais Magufuli Amlilia Kingunge "Ametuachia Somo la Kupigania Maslahi ya Nchi"

0
0
Rais Magufuli Apokea kwa Huzuni Kifo cha Kingunge "Ametuachia Somo la Kupigania Maslahi ya Nchi"
February 2, 2018 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli amepokea kwa huzuni na masikitiko taarifa za kifo cha mmoja wa waasisi wa Taifa na mwanasiasa mkongwe nchini Mzee Kingunge Ngombale Mwiru kilichotokea saa 10:30 alfajiri katika Hospitali ya Taifa Muhimbili Jijini Dar es Salaam.

Mzee Kingunge Ngombale Mwiru alikuwa akipatiwa matibabu hospitalini hapo baada ya kushambuliwa na mbwa wake nyumbani kwake December 22, 2017.

Rais Magufuli amesema Taifa limempoteza mtu muhimu ambaye alitoa mchango mkubwa katika juhudi za kupigania uhuru na baada ya kupata uhuru akiwa mtumishi mtiifu wa Chama cha TANU na baadaye Chama Cha Mapinduzi (CCM), na katika nyadhifa mbalimbali za uongozi ndani ya Serikali.

“Mzee Kingunge Ngombale Mwiru ametoa mchango mkubwa sana, sisi kama Taifa hatuwezi kusahau na tutayaenzi mema yote aliyoyafanya wakati wa utumishi wake uliotukuka, ametuachia somo la kupigania maslahi ya nchi wakati wote, kuwa wazalendo wa kweli, kudumisha amani na mshikamano, kuchapa kazi kwa juhudi na maarifa na kuwa na nidhamu”-Rais Magufuli.

Pia Rais Magufuli amewapa pole wanafamilia wote, wanachama wa CCM, ndugu, jamaa, marafiki na wote walioguswa na msiba huu, na amewaombea kuwa na moyo wa subira, uvumilivu na ustahimilivu katika kipindi hiki cha majonzi.

Uongozi Waifungia Baa Aliyekuwepo ‘Mowzey Radio' na Kujeruhiwa

0
0
Uongozi Waifungia Baa Aliyekuwepo ‘Mowzey Radio' na Kujeruhiwa Yafungwa
Uongozi wa Jiji la Entebbe nchini Uganda umeifunga  Baa  ya De ambayo mwanamuziki Moses Ssekibogo maarufu kwa jina ‘Mowzey Radio’ alikuwapo na kujeruhiwa wiki mbili zilizopita.

Mwanamuziki huyo alifariki dunia jana katika Hospitali ya Case alipokuwa akipatiwa matibabu.

Gazeti la Daily Monitor nchini humo limeripoti kuwa agizo la kufungwa kwa baa hiyo limetoka kwa Meya wa Jiji, Paul Kayanjana.

 Mbali na kuchukua hatua hiyo, Meya Kayanjana ameagiza apelekewe vibali vyote  vya baa  hiyo  ikiwamo leseni na  kuwekwa  makufuli  katika milango yote.

Hata hivyo, ameonya kuwa endapo mmiliki wa baa hiyo atakaidi amri  hiyo ya kutoendelea na uendeshaji atatozwa faini ya Sh1milioni  za Uganda ambazo atapaswa kuzilipia kupitia Benki  ya Stanbic, Tawi la Entebbe.

Katika hatua nyingine, watu wameonekana kuzidi kumiminika katika ukumbi wa  Taifa wa maonyesho ambako wananchi watauaga mwili kabla ya maziko yatakayofanyika kesho saa 10 jioni Kaga, Barabara ya Entebbe.

Mwanamuziki Radio aliyewahi kutamba na kundi la Goodlyfe alilazwa katika Hospitali ya Case baada ya kushambuliwa katika ugomvi uliotokea wiki mbili zilizopita katika Baa ya De.



Ugomvi huo unaodaiwa kuwa kati yake na mlinzi wa baa hiyo, ulimsababishia apasuke fuvu na kulazwa katika chumba cha wagonjwa mahututi kwa wiki mbili.

Chama cha ACT- Wazalendo Watoa Taarifa Kufuatia Kifo cha Kingunge

0
0
Chama cha ACT- Wazalendo Watoa Taarifa Kufuatia Kifo cha Kingunge
Chama cha cha ACT – Wazalendo kimeeleza kuwa kimepokea kwa masikitiko makubwa taarifa ya kifo cha Mwanasiasa Mkongwe hapa nchini Mzee Kingunge Ngombale Mwiru kilichotokea usiku wa kuamkia leo katika hopsitali ya Taifa Muhimbili.

Katika taarifa iliyotolewa leo na Chama hicho imeeleza kuwa Mzee Kingunge atakumbukwa kwa mchango wake kwenye mapambano ya kupigania uhuru wa Tanganyika.

Aidha Chama cha ACT Wazalendo wanatoa pole kwa familia ya Mzee Kingunge kwa kupata misiba miwili ndani ya kipindi kifupi Mzee Kingunge aliyefariki usiku wa kuamkia Februari 2, 2018 na Mkewe Mama Peras Kingunge aliyefariki Januari 4, 2018

Meli ya Uvuvi Kutoka Malaysia Yakamatwa na Mapezi ya Papa

0
0
Meli ya Uvuvi Kutoka Malaysia Yakamatwa na Mapezi ya Papa
Meli ya uvuvi kutoka Malaysia imekamatwa mjini hapa baada ya kukutwa na mapezi ya samaki aina ya papa na kutozwa faini ya Sh770 milioni.

Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Luhaga Mpina alisema jana kwamba meli hiyo inayomilikiwa na kampuni ya Buah Naga ilikamatwa Januari 26.

Alisema samaki hao ambao wamekatwa hawakuwa na miili yake kinyume cha kanuni ya 66 ya Mamlaka ya Uvuvi wa Bahari Kuu, pamoja na kifungu cha 18 (2) cha Sheria ya Mamlaka ya Uvuvi wa Bahari Kuu ya mwaka 1998 na marekebisho yake ya mwaka 2007.

“Serikali hii mtakaguliwa na kupekuliwa kuliko wakati wowote hivyo ni vizuri mkatii sheria za nchi kwa mujibu wa leseni zenu,: alisema huku kapteni wa meli hiyo, Han Ming Chuan raia wa Taiwan akimsikiliza.

Mpina alisema meli zimekuwa zikitumika pia kufadhili biashara nyingine haramu ikiwamo, usafirishaji haramu wa binadamu, dawa za kulevya na silaha na pia kutorosha nyara za Serikali.

Alisema kitendo cha wamiliki wa meli hiyo kuwakata samaki hao mapezi na kisha kutupa miili yao baharini kimeleta athari kubwa kwa taifa kwani samaki hao wangeweza kutumika kwa matumizi mengine ya binadamu na kuchochea uchumi wa nchi.

Mbali ya faini hiyo, Mpina aliagiza samaki wasioruhusiwa wataifishwe na kugawiwa kwa wananchi wa maeneo jirani ya Manispaa ya Mtwara na kuonya kuwa siku nyingine Serikali ikikamata meli iliyofanya makosa ya aina hiyo itataifishwa kwa mujibu wa sheria.

Kamishna wa Oparesheni wa Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya, Luteni Kanali Frederick Milanzi alisema meli hiyo baada ya kukaguliwa imekutwa na kilo 90 za mapezi hayo na bastola yenye risasi 10 ambayo inaendelea kushikiliwa katika ofisi ya mkuu wa upelelezi wa makosa ya jinai Mkoa wa Mtwara hadi hati za umiliki zitakapowasilishwa.

Kaimu Mkurugenzi wa Mamlaka ya Usimamizi wa Bahari Kuu, Hosea Mbilinyi alisema hatua zinazochukuliwa zimelenga kudhibiti uvuvi haramu na utoroshaji wa samaki na mazao yake nje ya nchi na kwamba ni endelevu.

Wakili wa Serikali, Wankyo Simon alisema makosa hayo adhabu yake ni kubwa na kwamba wanapaswa kulipa faini hiyo vinginevyo hatua kali zaidi zitachukuliwa dhidi yao ikiwa na pamoja na kapteni kufikishwa Mahakamani.

Mowzey Radio Aleta Simanzi kwa Wasanii wa Afrika Mashariki

0
0
Mowzey Radio Aleta Simanzi kwa Wasanii wa Afrika Mashariki
Simanzi ilitawala jana katika mitandao ya kijamii Afrika Mashariki baada ya kuenea kwa taarifa ya kifo cha mwanamuziki wa Uganda, Moses Sekibooga maarufu Mowzey Radio aliyefariki dunia baada ya kuugua kwa takribani wiki mbili.

Radio aliyewahi kutamba na kundi la Goodlyfe alilazwa katika Hospitali ya Case baada ya kushambuliwa katika ugomvi uliotokea wiki mbili zilizopita katika baa ya De.

Ugomvi huo ulimsababishia apasuke fuvu na kulazwa katika chumba cha wagonjwa mahututi.

Wasanii mbalimbali nchi za Afrika Mashariki, wamemlilia msanii huyo akiwamo Lady Jay Dee, Profesa Jay, Diamond Platnumz, Vannesa Mdee, Nameless, MwanaFA, Jose Chameleone na Juacali.

Rais wa Uganda, Yowere Museven ni miongoni mwa watu waliotumia mtandao wa Twitter kueleza namna alivyoguswa na msiba wa mwanamuziki akisema nchi hiyo imepoteza nguvu kazi.

Wiki iliyopita Rais Museven alitoa Sh30 milioni za Uganda ili kugharamia matibabu ya mwanamuziki huyo aliyeshiriki katika Kampeni za Urais mwaka 2015.

Mashabiki wafurika hospitali

Polisi walilazimika kuimarisha ulinzi nje ya Hospitali ya Case alipofia mwanamuziki huyo baada ya mashabiki kufurika kila mmoja akitaka kuushuhudia mwili wake.

Ndugu na wanamuziki wengine walifika katika eneo hilo kila mmoja akijaribu kupata nafasi ya kushuhudia mwili wa Radio.

Vilio vililipuka katika eneo hilo baada ya mwanamuziki Weasel aliyekuwa kundi moja na Radio aliyezaliwa Januari 1, 1985, kufika hospitalini hapo. Mashabiki walisikika wakimuuliza kwa simanzi: “Itakuwa vipi Weasel bila Mowzey (Radio)”?

Radio akiwa na Weasel katika kundi la Goodlyfe waliwahi kutamba na nyimbo kama Nakudata, Bread and Butter, Magnetic, Nyambura na Home to Africa.

Wiki iliyopita polisi walimkamata mmiliki wa baa hiyo, George Egesa na rafiki yake Xavier Rukere ili waisaidie polisi kumpata mtuhumiwa anayedaiwa kumpiga mwanamuziki huyo.

Mapenzi Yamtesa Mwanaume Mwenye Maumbile Marefu Duniani "Nimeachika Mara 10 Lakini Sikati Tamaa"

0
0
Mwanaume Mwenye Maumbile Marefu Duniani Ahangaikia Mwanamke wa Kuishi Naye "Nimeachika Mara 10 Lakini Sikati Tamaa"
Wakati kukiwa na kasumba ya wanawake kuwachekwa kama sio kuwadharau wanaume wenye maumbile madogo hapa Afrika, hii ni tofauti kabisa na  Roberto Esquivel Cabrera mwanaume pekee duniani anayekadiriwa kuwa na maumbile marefu zaidi duniani ambaye anahangaika hadi leo kupata mwanamke wa kuishi wa kuishi naye.

Roberto Esquivel Cabrera (54) raia wa Mexico amesema amekuwa akipata tabu kuchagua wanawake kwani amedai kipindi akiwa sekondari miaka 30 iliyopita wanawake wengi walikuwa wanampenda lakini kadri umri ulivyozidi kukua maumbile yake yalikuwa yanaongezeka na kuanza kumnyima raha kwani alianza kukimbiwa na wanawake.

Kwenye mahojiano yake na mtandao wa IFL Science, Cabrera amesema amefanikiwa kupata mtoto mmoja tu kwenye maisha yake na mke wake wa kwanza ambaye naye alimkimbia kutokana na ukubwa wa maumbile yake.

Cabrera amesema mpaka kufikia sasa amefanikiwa kuishi na wanawake 10 lakini wote wamemuacha sababu kubwa ni kukosa furaha ya tendo la ndoa.

“Nilipokuwa kijana wa miaka 20+ nilikuwa najiona mwanaume haswa kwani hata sikuwa naogopa wanawake na nilipendwa kweli lakini kadri muda ulivyozidi kwenda nikawa nahisi maumivu kwenye sehemu zangu za siri kitu ambacho kilianza kuniumiza kisaikolojia nikaanza kuwa mpweke kwani kila mwanamke niliyetaka kwenda naye faragha alinikimbia,“amesema Cabrera.



Cabrera amesema ameenda hospitali mara kadhaa akihitaji dawa za kupunguza maumbile yake lakini alichoshauriwa ni kufanyiwa upasuaji mdogo kiytu ambacho hakuafikiana nacho.

“Kuna watalaamu walikuja baada ya kuandikwa na vyombo vya habari wakitaka kunifanyia upasuaji nilikataa napenda niwe hivi hivi najua, kuachika na wanawake kumi hakunifanyi nikose amani najua Mungu ataniletea mwenzangu mwenye maumbile yanayoendana na yangu bado sikati tamaa,“amefunga Cabrera.

Cabrera amesema hata kama akiona amechelewa kupata mwenza nchini Mexico atasafiri hadi Marekani ambako amesema atapata wanawake wenye maumbile makubwa kwani huwa anawaona kwenye picha chafu (Video za X) na anaamini atapata mke.

“Mimi nimeshakuwa mtu maarufu kutokana na maumbile yangu siwezi kuyapunguza nitaenda Marekani kule kuna wanawake wengi wenye maumbile makubwa huwa nawaona mitandaoni, siwezi kupunguza kamwe,“amesema Cabrera kwenye mahojiano yake na gazeti la The Sun la Uingereza.

Kwa upande mwingine Madaktari wamesema kuwa Cabrera kama angetahiriwa akiwa mdogo huenda asingelipatwa na tatizo hilo kwani linachangiwa na ongezeko la homoni.

Maumbile ya Cabrera yanakadiriwa kuwa na urefu wa nchi 18.9 hadi 20 pale yanapokuwa yamesimama na kumfanya kuwa mwanaume wa kwanza mwenye maumbile marefu zaidi duniani aliyerekodiwa.

Hata hivyo bado Cabrera hajaingizwa kwenye kitabu cha maarufu cha kumbukumbu cha (Guinness World Records). Tazama mahojiano yake hapa chini aliyowahi kufanya kipindi cha nyuma (Video by Barcroft TV).

Mtoto wa Kwanza wa Aliyekuwa Rais wa Cuba Fidel Castro Ajiua

0
0
Mtoto wa Kwanza wa Aliyekuwa Rais wa Cuba Amejiua
Taarifa iliyoshika headlines kwenye vyomba vya habari nchini Cuba ni kuhusu Mtoto wa Mwanamapinduzi na aliyekuwa Rais wa Cuba Fidel Castro, Fidel Ángel Castro Díaz-Balart, mwenye umri wa miaka 68 amejiua akiwa mji mkuu wa Havana.

Amekutwa amefariki February 1, 2018 na inadaiwa alikuwa anatatizwa na msongo wa mawazo. Castro Díaz-Balart alifahamika sana kama “Fidelito” na alikuwa mtoto wa kwanza wa rais huyo wa zamani wa Cuba aliyefariki dunia November 2016.

Alikuwa mshauri wa kisayansi wa Baraza la Serikali ya Cuba na alihudumu kama makamu rais wa Chuo cha Sayansi cha Cuba pia alifanya kazi kama Mwanafizikia ya nyuklia.

Gazeti rasmi la Serikali ya Cuba la Granma limeandika hivi>>> “Fidel Castro Diaz-Balart, aliyekuwa ametibiwa na kundi la madaktari kwa miezi kadha kutokana na msongo wa mawazo, alijitoa uhai asubuhi hii,”

Runinga ya taifa imesema amekuwa akipokea matibabu miezi ya karibuni kama mgonjwa wa kutibiwa na kurudi nyumbani, baada yake kulazwa hospitalini kwa muda.

Kamati ya Nidhamu Yamfungia Mwamuzi Kuchezesha Soka

0
0
Kamati ya Nidhamu Yamfungia Mwamuzi Kuchezesha Soka
Shirikisho la soka la Ufaransa (FFF) kupitia kamati ya nidhamu inayosimamia ligi kuu nchini humo Ligue 1 imemfungia miezi sita mwamuzi Tony Chapron kwa kosa la kumpiga mchezaji kisha kumwadhibu kwa kadi.

Sehemu ya taarifa ya FFF imeeleza kuwa, ''Baada ya kumsikiliza Tony Chapron na kusoma ripoti ya kamisaa wa mchezo, kamati imeamua kumfungia kwa muda wa miezi sita, pamoja na wiki tatu ambazo alisimamishwa".

Disemba mwaka jana kwenye mchezo wa Ligue 1 kati ya Nantes dhidi ya PSG Chapron alikwatuliwa kwa bahati mbaya na mchezaji wa Nantes Diego Carlos lakini alilipiza kwa kumkwatua mchezaji huyo kisha kumwonesha kadi ya pili ya njano.

Baada ya mechi Tony Chapron alisimamishwa kabla ya usiku wa kuamkia leo kamati ya nidhamu kutangaza kumfungia miezi sita mwamuzi huyo ambaye amechexzesha mechi zaidi ya 400 za Ligue 1 tangu mwaka 2004.

Kabla ya tukio hilo Chapron mwenye miaka 45 alikuwa ametangaza kuwa huu utakuwa msimu wake wa mwisho kama mwamuzi na alitarajia kustaafu mwishoni mwa msimu wa 2017/18.

Baba Diamond Amjia Juu Mwanaye "Nikifa Mwanangu Asiguse Jeneza Langu"

0
0
Baba Diamond Amjia Juu Mwanaye "Nikifa Mwanangu Asiguse Jeneza Langu"
Kauli hiyo ya mzee Abdul imekuja baada ya Queen Darleen hivi karibuni kufunguka alipokuwa anahojiwa na kituo kimoja kinachorusha matangazo yake kupitia mtandao wa You Tube alipokuwa akimzungumzia mke wa kaka yake, Zarina Hassan ‘Zari The Boss Lady’.


MAHOJIANO YENYEWE

Kwenye mahojiano hayo, Queen alimmwagia sifa Zari kwa kusema ana roho nzuri na ndiye mwanamke pekee aliyekuwa anawahimiza angalau yeye na kaka yake (Diamond) wamthamini baba yao.

“Zari ni wifi mzuri, ana roho nzuri na ndiye mtu pekee aliyekuwa anatushauri tumjali baba (mzee Abdul) japo baba mwenyewe kuumwa kwake amekuwa kama mtoto…

“Kwa kweli kwa sasa siwezi kusema baba yangu ni Abdul, baba yangu mimi ni Nasibu…” alisikika Queen mbeleni katika mazungumzo hayo.

WATU SASA

Baada Queen kusema maneno hayo, watu mbalimbali walioiona ‘intaviu’ hiyo walimjia juu na kusema kuwa, kusema baba yake ni kama mtoto ni tusi kubwa na hakustahili kabisa kusema hivyo.

“Hivi anawezaje kumuita baba yake mtoto, halafu eti leo anamkana kuwa si baba yake, laana anayoitafuta ataipata,” alisema mdau mmoja aliyejitambulisha kwa jina la Mama Caren wa Sinza jijini Dar.

BABA DIAMOND AJIBU

Baada ya baba Diamond kusikia mahojiano hayo, alizungumza na Amani nyumbani kwake, Magomeni- Kagera jijini Dar na kueleza hisia zake juu ya mwanaye huyo.

“Yani nimeumia sana. Amezungumza mazito sana kuhusu mimi, sasa niseme tu, na mimi nikifa hata leo asije kabisa kunizika.

“Asisogelee hata jeneza langu, yeye si amesema baba yake siyo mimi, baba yake ni Diamond basi sawa. Hata mimi simtambui. Nikiumwa, nikifanya chochote simhitaji,” alisema baba Diamond huku akibubujikwa na machozi.

Akizidi kumuelezea zaidi Queen, baba Diamond alisema, anasikitika sana binti huyo kutoa maneno mabaya kwake, wakati ni mtoto ambaye alimlea kabla hajawa maarufu.

“Yani kabla hajawa na hilo jina, alikuwa anakuja hapa, anapika na tunakula pamoja leo hii kweli anasema mimi nina akili za kitoto, kwamba nikiumwa nakuwa sina akili? Lini mimi niliumwa nikawa kama mtoto au sina akili?” alihoji baba Diamond na kuongeza:

“Diamond pamoja na ustaa wake wote hajawahi kuniambia maneno mazito kama hayo, hicho kiburi anakitoa wapi mtoto wa kike?”

AFUKUNYUA MAMBO

Kama hiyo haitoshi, baba Diamond alisema anashangaa Queen kujiona mjanja sasa hivi wakati yeye ndiye aliyekuwa anampa habari za uchonganishi kipindi cha nyuma akidai mama Diamond ndiyo chanzo cha Diamond kugombana na wapenzi wake akiwemo Wema.

“Yule mtoto mbaya sana. Yeye ndiye alikuwa anakuja hapa anasema ooh… sijui mama Diamond ndiye anayemsababishia Diamond agombane na Wema…ooh… sijui mara hivi kumbe mnafiki mkubwa,” alisema mzee huyo na kuongeza:

“Binafsi hata mimi Zari namkubali maana natambua ana moyo wa huruma na akili kuliko huyu Queen.”

HATUA ALIZOCHUKUA

Akizungumzia hatua alizozichukua kuhusu mwanaye huyo, kwanza baba Diamond alisema anamlaani, akifa asimzike lakini pia amechoma moto baadhi ya picha alizokuwa nazo nyumbani kwake.

“Nimezichoma kabisa moto picha zake. Siwezi kuwa na mtoto halafu akanikana hadharani. Acha na mimi nimkane hadharani, hana maana. Asinisaidie kwa chochote, sihitaji msaada wake kwanza,” alisema baba Diamond.

TUJIKUMBUSHE

Mzee Abdul aliwazaa Queen Darleen na Diamond kwa mama tofauti, miaka ya nyuma ambapo kama baba, alihakikisha anawapa huduma muhimu ambapo baadaye aliachana na mama yake Diamond, Sanura Kassim ‘Bi Sandra’ na kuanzisha maisha yake.

Wakati Diamond akiwa tayari na jina kubwa, Queen alikuwa angali hana jina kwenye gemu ya Bongo Fleva lakini baadaye, Diamond ‘alimbusti’ kwa kumpa sapoti ya kumuingiza katika kruu lake la Wasafi Classic Baby (WCB) ndipo nyota ya mrembo huyo ilipozidi kung’aa.
Chanzo: Global Publishers

Marubani Wawili Wapoteza Maisha kwa Ajali ya Ndege Zanzibar

0
0
Marubani wawili wamefariki dunia papo hapo katika ajali ya ndege iliyotokea Uwanja wa Ndege wa kimataifa wa Abeid Amani Karume mjini Zanzibar walipokuwa wakiifanyia majaribio ya kuruka wakati wa matengenezo.

Marubani hao wametajwa kuwa ni injinia Edger Alfred Mcha (26) na Dominic Bomani (64).

Mhandisi Mkuu wa Kampuni ya Tropical Air, David Kisusi amesema ndege hiyo ilianguka na kuungua jana, Alhamisi Februari Mosi saa saba mchana.

Kisusi amesema ndege hiyo 5H-TDF yenye uwezo wa kubeba abiria wanne ni mali ya Chuo cha Taifa cha Usafirishaji (NIT) iliyokuwa Zanzibar kwa matengenezo.

Amesema kwa takriban miezi sita ndege hiyo ilikuwa uwanjani hapo kwa matengenezo.

“Tulikuwa tunaijaribu baada ya matengenezo, iliporuka tu ilianguka na kulipuka, marubani wetu wamefariki dunia,” amesema Kisusi leo Februari 2, 2018.

Daktari bingwa wa uchunguzi katika Hospitali Kuu ya Mnazi Mmoja Zanzibar, Dk Msafiri Marijani amesema vifo vya marubani hao vimesababishwa na kukosa hewa safi wakati wa ajali na kuathiriwa na moto.

Amesema uchunguzi wa miili ya marubani hao uliofanywa jana saa 12:45 jioni.

TRA Yafunguka Kuhusu Kugawa Magari ya Kanisa, Msikiti na NGO's

0
0
TRA Yafunguka Kuhusu Kugawa Magari ya Kanisa, Msikiti na NGO's
Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) imekanusha taarifa iliyokuwa inasambaa katika mitandao ya kijamii kuwa inagawa magari kwa taasisi zinazotoa huduma za kijamii kama Kanisa, Msikiti, NGO na vituo vya watoto yatima pamoja na kutuzia wazee.


Hayo yamebainishwa na Mkurugenzi wa Huduma na Elimu kwa Mlipakodi wa mamlaka hiyo na kuwataka wanaanchi kuipuuza pindi waipatapo au kuiona katika mitandao hiyo.

Kwa habari kamili soma hapa chini..

Viewing all 104414 articles
Browse latest View live




Latest Images