Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104709 articles
Browse latest View live

Rais Magufuli Amtaka Jaji Mkuu Kuwachukulia Hatua Majaji Wanaenda Ughaibuni Kula Bata

$
0
0
Rais Magufuli Amtaka Jaji Mkuu Kuwachukulia Hatua Majaji Wanaenda Ughaibuni Kula Bata
Rais John Magufuli amemtaka Jaji Mkuu wa Tanzania, Profesa Ibrahim Juma kuwachunguza majaji wote ambao wamekuwa wakisafiri wakati wa likizo zao kwenda ughaibuni ‘kula bata.’

Pia, Rais Magufuli amesikitishwa na Waziri wa Katiba na Sheria, Profesa Palamagamba Kabudi na Mwanasheria Mkuu wa Serikali, George Masaju akisema kwa miezi tisa wameshindwa kuandaa kanuni za msaada wa kisheria na kuagiza zikamilike mwezi huu.

Akizungumza jana jijini Dar es Salaam katika maadhimisho ya Siku ya Sheria, Rais Magufuli alisema kuna watumishi wachache wasiokuwa waadilifu ambao wanachafua vyombo vya kutoa haki na “Sitaki kuona hili likiendelea kwa wale wasiokuwa na uadilifu.”

Kuhusu majaji hao, Rais Magufuli alisema kumekuwapo na baadhi yao ambao kila wanapopata likizo wanasafiri kwenda nje ya nchi kwa siku 28 na yeye ndiye anayetoa vibali huku anayegharamikia usafiri na kuishi hoteli nzuri akiwa hajulikani.

Alisema aliwahi kumuuliza Jaji Mkuu Profesa Ibrahim Juma kuhusu majaji hao wanaokwenda huko kwamba ni nani anayegharamia huku akidokeza kuwa anazo taarifa nyingi.

“Jaji Mkuu, hili ni swali najiuliza sana, wanapokwenda na familia zao wanaishi hoteli nzuri, mishahara ya majaji naijua kama wa kwangu tu, Jaji Mkuu kupitia Tume ya Utumishi wa Mahakama ambayo wewe ni mwenyekiti chunguza vibali vyao, kwa nini iwe kina fulani fulani tu,” alihoji Rais Magufuli.

Rais alipongeza Profesa Juma kwa kuwachukulia hatua watumishi 112 wa Idara ya Mahakama ambao awali, jaji mkuu alieleza kwamba baadhi yao walifukuzwa kazi na wengine kustaafishwa akisema uamuzi huo unajenga taswira nzuri ya chombo cha utoaji haki.

Hata hivyo, alisema licha ya pongezi alizozitoa, usimamizi wa sheria na utoaji wa haki bado una changamoto kwani wapo watumishi wachache wasio waadilifu ambao vitendo vyao vinachafua mhimili huo.

“Wapo wachache, wachache, nasema wachache wanaochafua taswira yetu ambao wanatoa hukumu zinazopendelea watu, kuchelewesha hukumu, kuchelewa kuandika hukumu na kati yao ni hao 112 tulioelezwa na Jaji Mkuu waliofukizwa au kustaafishwa,” alisema Rais Magufuli na kuongeza,

“27 walistaafishwa kwa masilahi ya wananchi na walikuwa mahakimu na wote walipopelekwa mahakamani walishinda, yaani kesi ya ngedere unaipeleka kwa nyani unategemea nini? Mahakimu 14 walifukuzwa kazi, 67 watumishi wa kawaida nao walifukuzwa kazi.”

Kuhusu hilo, Jaji Mkuu Profesa Juma alisema kati mwaka 2016/17, Tume ya Utumishi wa Mahakama ilisikiliza malalamiko ya kimaadili 143 na kati ya waliofukuzwa au kustafishwa ni 112 na 17 walirudishwa kazini.

“Hatutamwonea mtumishi lakini hatutamvumilia mtu anayetupaka matope sisi kama Mahakama,” alisema Jaji Mkuu.

Akizungumza kwa msisitizo, Rais Magufuli alisema “Wito wangu kwa vyombo vingine IGP (Inspekta Jenerali wa Polisi- Saimon Sirro) yupo hapa, Mkuu wa Magereza, Takukuru na vyombo vingine vinavyotoa haki muige mfano wa Profesa Juma.

Ningefurahi kuona “IGP anatoa majina ya polisi wanaochelewesha upelelezi. Unakuta mtu ameshikwa na dawa za kulevya unaambiwa upelelezi bado, Magereza watu wanaoingiza simu au dawa za kulevya gerezani na DPP (Mkurugenzi wa Mashtaka) ambaye hata hivyo, hana uwezo wa kuhamisha watumishi na ndio maana wengine wanaletwa kwangu.”

Rais Magufuli alisema hayo yamesababisha baadhi ya kesi kushindwa na kudokeza kuwa ameshajua wapi tatizo lilipo na kwamba atachukua hatua haraka.

“Majaji mnisamehe. Sitalalamika tena, nishajifunza, najua wapi tunakosea, mwaka jana nililalamika, mwaka huu sitalalamika, najua jinsi ya kufanya na wala mwezi huu hautaisha,” alisema Rais Magufuli.

Profesa Kabudi, AG Masaju

Rais Magufuli akijibu ombi la Jaji Mkuu Profesa Juma la mkwamo wa utekelezaji wa Mahakama inayohama kutokana na kanuni kutokukamilika, alisema inasikitisha wale anaowateua wanashindwa kutekeleza wajibu wao ipasavyo licha ya kulipwa mishahara.

“Bunge limepitisha, mimi nimesaini lakini Waziri wa Katiba na Sheria tena Profesa (Kabudi), tatizo huyu mtani wangu, lakini mimi ndivyo nilivyo kusema hadharani, Mwanasheria Mkuu (Masaju), Naibu Mwanasheria Mkuu (Gerson Mdeme) wote wapo, wanakula mishahara, magari ya kiyoyozi wanayo lakini miezi tisa wameshindwa kuandaa kanuni,” alisema Rais Magufuli.

“Wakati mwingine na mimi najitathimini nawachaguaje chaguaje hawa. Nataka mwezi huu kanuni ziwe zimekamilika kwani wakati mwingine majaji na Mahakama wanalalamikiwa bure kuchelewesha haki kwa makosa ambayo sio ya kwao.”

Profesa Juma alisema Mahakam inayotembea (katika gari) imeshindwa kuanza kazi kutokana na kutukuwapo kwa kanuni hivyo kuiomba Wizara ya Katiba na Sheria kuzifanyia kazi ili huduma hiyo ianze kutolewa.

Kuhusu vitendo vya rushwa, Rais alisema vipo na “Nina taarifa nyingi kwelikweli, rushwa haifichiki na Jaji Mkuu hao majaji wanaokwenda Ulaya fuatilia vibali vyao.”

Matumizi ya Tehama

Awali, Profesa Juma alisema umuhimu wa Mahakama lazima upewe kipaumbele na kwa kutumia Siku ya Sheria, watafakari walipotoka, walipo na wanapokwenda hasa matumizi ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (Tehama).

Alisema Mahakama imejiwekea malengo ya kuongeza kasi, uwazi na uadilifu na hawataki kusikia shauri la mtu halijulikani lilipo, kesi yake ni lini na nani atalisikiliza akisisitiza Tehama inakuja kuweka uwazi zaidi na kuondoa unjanjaunjanja.

“Wananchi wa Tanzania, watarajie huduma bora za uendeshaji wa kesi, uwazi na huona hukumu kwani Tehama itarahisisha yote haya na sisi majaji, mahakimu na watendaji wa Mahakama tubadili fikra zetu na kuijua Tehama kwani karne hii inahitaji kwenda na wakati,” alisema Profesa Juma.

Alisema utaratibu unafanyika ili kukamilisha mfumo wa menejimenti za kesi ambao utatumika kulipa ada na uendeshaji wa kesi kwa masafa ya mbali.

Jaji Mkuu alizungumzia upungufu wa majaji akisema kwa sasa wapo 62 pekee ambao kwa mwaka kila mmoja anakuwa na majalada 535 badala ya 225 jambo ambalo linawasababishia mzigo mzito.

“Huu ni mzigo mkubwa sana na uko nje ya makubaliano kwamba kila jaji amalize majalada 225 lakini kwa idadi hii ni mzigo mkubwa sana,” alisema Profesa Juma

Alisema mpaka sasa ni mikoa 14 kati 26 pekee yenye Mahakama Kuu na kusema malengo ni kuwa na Mahakama Kuu katika mikoa 22 ifikapo mwaka 2020.

TLS yalia na Mahakama

Makamu wa Rais wa Chama cha Mawakili Tanganyika (TLS), Godwin Ngwilimi mbali na kupongeza jitihada mbalimbali zinazofanywa na Rais Magufuli alitoa wito kwa majaji kuhakikisha wanasimamia haki ipasavyo.

Alisema Mahakama panafaa kuwa mahali palipotukuka kwani ndipo pekee ambako kunapokuwa na migogoro na watu wanapoililia sheria wanakwenda bila kujali aina ya mtu.

“Tusiitumie Mahakama kama majaribio, maabara au jumba la kamari. Majaji msiitumie hata mara moja kwani mnalindwa kisheria na msimamie hilo ili Mahakama isionekane ya ajabu ajabu.”

Awali, Mdeme alisema utoaji haki unahitaji ushirikiano kutoka wa wadau mbalimbali na ofisi ya Mwanasheria Mkuu imekuwa ikifanya hivyo kwa masilahi ya Taifa na wananchi.

Mdeme alisema mfumo wa Tehema utapunguza gharama, urasimu, kuwahisha utoaji wa haki na utawaanika watumishi wasio waaminifu hivyo kuhimiza kila mmoja kujifunza na kuutumia.

Miujiza ya Sharifu Seif Mohamed..JE Umeachwa na Mme/Mke au Mpenzi, Umesongwa na Mitihani ya Maisha..Piga Simu Upate Muujiza Wako

$
0
0

SHARIFU SEIF MOHAMED ANAWASHUKURU WALE WOTE WANAOENDELEA KUPIGA SIMU, WENYE MATATIZO NA WALE WANAOTOA  SHUKRANI NA SHUHUDA JINSI TIBA ZAKE ZINAVYO WASAIDIA,

(Rudisha mahusiano yako ndani ya masaa 72 tu)

SHARIFU MOHAMED Ni  mtaalam na mnajimu maarufu wa nyota na kubashiri mambo yanayo watesa binadamu duniani kote na kupata ufumbuzi, Anatumia kitabu cha QUR'AN, Dawa za Asili, Dawa za Kiarabu na majini kwa kumtuliza mke/mme, mchumba au mpenzi ndani ya masaa 72 tu, na kutatua matatizo yote ya kimaisha,

Je Umeachwa na UMPENDAE awe Mme/Mke na bado unampenda? Je Umekimbiwa na Mmeo/ Mkeo n anaishi na mtu mwingine? Je Umejaribu sehemu nyingi bila mafanikio? Mpigie simu SHARIFU SEIF sasa hivi ujionee Muujiza wa Papo kwa Papo, Anauwezo wa hali ya juu wa kusambaratisha mahusiano yao na kumrejesha kwako haraka sana na Kumfanya Atimize Ahadi zote Ndani ya Muda Mfupi Endapo Utafwata Atakacho Kuelekeza

ANAZO DAWA ZA MAPENZI, NGUVU ZA KIUME, CHANGO NGIRI MAJI NA N.K, ZINDIKO LA NYUMBA NA BIASHARA, PETE ZA BAHATI, HUMALIZA KABISA TATIZO LA NGUVU ZA KIUME NA KUREFUSHA UUME KWA SAIZI UNAYOTAKA, HUZUIA CHUMA ULETE KWENYE BIASHARA, HURUDISHA MALI ZILIZOPOTEA, MAGONJWA SUGU, MIGUU KUWAKA MOTO AU KUFA GANZI, HUTIBU BUSHA BILA KUPASUA, ANAO UWEZO WA KUMRUDISHA ALIE MBALI AU ALIECHUKULIWA MSUKULE, KUPANDISHA NYOTA NA KUSHINDA BAHATI NA SIBU, KASAFISHA NYOTA NA KUKUPA MVUTO WA AJABU, KUTOA NUKSI NA VIFUNGO MBALIMBALI,  MAFANIKIO YA MAISHA NA UTAJIRI BILA MASHARI, NA MENGINE MENGI YA SIRI,

Je UMAHANGAIKA KUPATA MTOTO BILA MAFANIKIO? WASILIANA NA MTAALAMU HUYU KWANI YEYE HUFAULU PALE WOTE WALIPOSHINDWA, PIA UMALIZA KAZI ZILIZO SHINDIKANA NA WATAALAM WENGINE NDANI YA MASAA 24 TU,

(NA ANATIBU KWA NJIA YA SIMU UKIWA NCHI YOYOTE AU MKOA WOWOTE ENDAPO UTAFWATA MAELEKEZO YAKE)

Kwa ushauri na mawasiliano  zaidi Piga SIMU No:

Mobile +255 654-836970
WhatsApp +255 756-033670

Video-Baada ya kuifunga Azam “Sikusujudu, nilibusu uwanja”-Gadiel

$
0
0
Januari 27, 2018 Yanga ilikuwa ugenini kucheza dhidi ya Azam FC kwenye uwanja wa Azam Complex uliopo maeneo ya Chamazi nje kidogo ya jiji la Dar. Katika mchezo huo, beki wa kushoto wa yanga Gadiel Michael alikuwa anakutana kwa mara ya kwanza na timu yake ya zamani tangu asajiliwe na Yanga wakati wa dirisha la usajili kabla ya kuanza msimu huu (2017/18)

Gadiel amekulia katika kikosi cha vijana cha Azam kabla ya kupandishwa timu ya wakubwa na baadae kuwa mchezaji muhimu wa kokosi cha kwanza cha Azam, kijana huyo alifunga goli zuri lililoihakikishia Yanga ushindi wa 2-1 sasa gumzo likawa ni aina yake ya ushangiliaji baada ya kuifungia timu yake bao la pili huku akiwa ameifunga timu iliyomlea.

Dauda TV imepiga story na gadiel ambaye ameeleza kila kitu kuhusu alichomaanisha kutokana na style yake ya kushangilia lakini miongoni mwa alivyovisema ni kwamba hakusujudu bali alibusu uwanja, sasa kwanini aliubusu uwanja wa Azam Complex angalia vieo kupata majibu yote.

Pata Dawa Bora ya Nguvu za Kiume na Maumbile Madogo ya Kiume ( Super Shafti)

$
0
0

DAWA BORA YA NGUVU ZA KIUME NA MAUMBILE MADOGO YA KIUME ( SUPER SHAFITI) NI DAWA YENYE UWEZO MKUBWA WAKUTIBU UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME


 (SUPER SHAFITI ni dawa ya asili yenye uwezo mkubwa wa kuogeza nguvu za kiume maradufu
(1) itakufanya uwe na nguvu za ajabu ukiwa unafanya ntedo la ndoa
(2) inaogeza hamu ya kurudia ntedo la ndoa zaidi ya mara tatu bila kuchoka
( 3) itakufanya uchelewe kufika kileleni dani ya dk 30
( 4)  itaimalisha milija ya uume iliyo legea au kusinyaa
(5) lnarefusha na kunenepesha uume saizi utakavyo kuazia ichi 1-8 unene sm 2-4
 (6) itakupa nguvu za kusimamiasha uume wako barabara kama_ msumari wakati wa ntedo la ndoa
(7) inasaidia kusafisha mishipa. ya kwenye uume na hivyo kusaidia Katika kuongeza kasi ya msukumo wa damu kwenye mishipa ya uume
(8) usaidia kuurudisha nje uume ulioingia ndani
(9) inasaidia kuogeza manii nyingi ambazo vina viini vya uzazi
(10)usaidia kutibu madhara ya punyeto ,matumizi makali ya  madawa ya kizugu mirungi bangi na sigara

KWA NINI BAADHI YA WANAUME WENGI WANA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME NA KUWA NA MAUMBILE MADOGO YA KIUME NINI CHANZO CHAKE?

ni kutokana na magonjwa megi kuongezeka yakiwemo kisukari presha ya kupanda na kushuka upigaji wa punyeto wa mda mrefu magonjwa ya moyo ngiri ya kuviba korondani vidonda vya tumbo
Msongo wa mawazo  tumbo kuuguruma kujaa ngesi kutopata choo vinzuri maumivu ya mgongo kiuno na tumiaji wa madawa makali ya kizungu ya kuongeza nguvu za kiume kuzaliwa na chango linaloshabulia neva za ukuwaji wa uume utumiaji wa mirungi bangi sigara na nk  tunapenda kuwatangazia wasomaji, wa makala zetu kuwa tunazo dawa nzuri za asili ambazo hazina mazala na zinazotibu na kuponyesha matatizo ya upungufu wa nguvu za kiume na maumbile ya kiume

NA TUNATIBU MAGONJWA YOTE SUGU KAMA KISUKARI PRESHA AINA YOTE UGONJWA WA MOYO SITRUKO KWIKWI KICHOMI MINGUU KUFA NGAZI ASIMA NK MZEE ISAYA ANAPATIKANA MAGOMENI MIKUMI KARIBU NA KANISA  TUMAINI HEBRAST CLINI NDIYO JIBU NA SULULISHO YA MATATIZO YOTE

PIGA simu 0745495181 au 0682644040

Kwa watu wa mikoa huduma utatumiwa na watu wa nje ya nchi utazipata dsm kama huna nafasi ya kufika ofisini kwetu utaletewa popote ulipo

Zitto Kabwe Amuwakia Waziri Mpango

$
0
0
Zitto Kabwe Amuwakia Waziri Mpango
Mbunge wa Kigoma Mjini kwa tiketi ya ACT Wazalendo Mhe. Zitto Kabwe amefunguka na kusema kuwa deni la taifa limeweza kuongezeka kwa asilimia 168% ndani ya muda mfupi toka Serikali ya awamu ya tano imeingia madarakani.


Zitto Kabwe amesema hayo Januari 1, 2018 wakati akichangia Bungeni na kudai kuwa kwa mujibu wa Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) Profesa Musa Juma Assad ndani ya kipindi kifupi deni la taifa limeongezeka.

"Ukitizama aliyosema CAG kuhusu deni la taifa inaonyesha kwamba ndani ya kipindi kifupi sana deni la Taifa limeongezeka kwa asilimia 168% lakini baya zaidi deni ambalo linatokana na masharti ya biashara limeongezeka kwa asilimia 17 ndani ya mwaka mmoja, madeni yanayotokana na masharti ya biashara gharama zake ni kubwa sana na inawezekana uwezo wetu wa kuyalipa ukawa na matatizo makubwa sana. Ndani ya taarifa hii ya CAG inaonesha kwamba taarifa ambayo Serikali ilitoa kuhusu deni la Taifa, deni la jumla ya tilioni 3.2 halikuwepo kwenye taarifa ya deni la Taifa, tulitarajia leo tungepata maelezo kwanini tilioni 3.2 hazikuhusisha katika taarifa ya pamoja ya deni la Taifa" alisema Zitto Kabwe

Mbali na hilo Zitto Kabwe alimjia juu Waziri wa Fedha na Mipango Dkt. Philip Mpango na Naibu wake kwa kitendo cha kuwadanganya wananchii juu ya ujenzi wa reli mpya wa kisasa Standard Gauge kwa kusema inajengwa kwa fedha za ndani ili hali Serikali inakopa fedha ili kujenga reli hiyo.

"Serikali imekamilisha majadiliano na taasisi za kifedha kwa lengo la kukopa kiasi cha dollar za Marekani Bilioni 1.5 kwa ajili ya kugharamia ujenzi wa reli ya kati kwa kiwango cha 'standard gauge' kutoka Morogoro hadi Makutopora Serikali inakamilisha utaratibu wa kusaini mkataba. Waziri Mpango ruhusa uliyopewa na Bunge ni kukopa dollar za Marekani Milioni 700 ni wapi ulipata ruhusa ya kwenda kujadiliana kukopa ziada ya 1.5 Bilioni ?

Zitto Kabwe aliendelea kuhoji

"Wabunge wote humu ndani ni mashahidi kila siku tunaambiwa, tunajenga reli ya Standa gauge kwa fedha zetu za ndani lakini leo Serikali inasema tunakopa, Kwanini tunawalaghai wananchi? Kwanini hatuwaelezi wananchi ukweli kwamba hatuna uwezo wa kujenga kwa fedha za ndani lakini tunakopa, kuna ubaya gani maanake kukupa si dhambi, kwanini tunamuacha Rais anasema tunajenga reli kwa fedha zetu za ndani halafu tunakuja Bungeni taarifa za Serikali zinasema kwamba tunakopa mnamuaibisha Rais" alisisitiza Zitto Kabwe 

Kikwete Amlilia Kingunge "Maneno ya Kutosha Kubeba Uzito wa Simanzi Zake"

$
0
0
Kikwete Amlilia Kingunge "Maneno ya Kutosha Kubeba Uzito wa Simanzi Zake"
Rais Mstaafu wa Awamu ya Nne, Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete amesema kuwa hana maneno ya kutosha kubeba uzito wa simanzi zake kwa Mwanasiasa Mkongwe Kingunge Ngombali Mwiru.

Dkt Kikwete ameeleza kuwa Mzee Kingunge ni moja ya walezi wake waliomlea kisiasa na wametoka mbali.

“Nimepokea kwa mshtuko mkubwa taarifa za kifo cha Mzee Kingunge Ngombare Mwiru.Sina maneno ya kutosha kubeba uzito wa simanzi zangu.Mzee huyu ni moja ya walezi wangu kisiasa. Tumetoka nae mbali. Natoa pole zangu kwa familia na Watanzania wote. Alale kwa amani,“ ameandika Dkt. Kikwete katika ukurasa wake wa Twitter.

Shilole Amkana Uchebe "Sina Mimba ya Uchebe"

$
0
0
Shilole Amkana Uchebe "Sina Mimba ya Uchebe"
Msanii wa muziki Bongo, Shilole amedai kuwa hana ujauzito wa mumuwe Uchebe kama watu wanavyomdhania baada ya kumuona amenenepa sana hivi karibuni.


Mrembo huyo amesema hayo kupitia kipindi cha Leo Tena na kudai kuwa mume aliyenaye anamfanya anenepe. “Sina Ujauzito, ila watu wananiombea mema, mume niliyenaye ananifanya ninenepe,” amesema Shilole huku akiwa na mumuewe kwenye kipindi hicho.

Akongeza kuwa dada yake alimkataza yeye kuolewa na Uchebe. “Dada alimkataa Uchebe kwa sababu anaonekana hana kipato kikubwa.”

Kwa mujibu wa wapenzi hao wamedai kuwa walikutana kisiwani Zanzibar na huki ndiko mapenzi yao yalipoanzia baada ya Uchebe ambaye ni mumuwe kuamua kueleza hisia zake.

Kifo cha Kingunge Chawagusa Wengi Wasanii Wamlilia

$
0
0
Kifo cha Kingunge Chawagusa Wengi Wasanii Wamlilia
Wasanii wameungana kuomboleza kifo cha mwanasiasa mkongwe, Kingunge Ngombale -Mwiru aliyefariki dunia usiku wa kuamkia leo Februari 2,2018 katika Hospitali ya Taifa Muhimbili.

Kwa takriban mwezi mmoja alikuwa akipatiwa matibabu baada ya kung’atwa na mbwa nyumbani kwake jijini Dar es Salaam.

Mwezi uliopita mkewe, Peras Ngombale-Mwiru alifariki dunia na Kingunge alitolewa kwa muda hospitalini ili kuhudhuria mazishi.

Kutokana na msiba huo, baadhi ya wasanii waliogushwa kwa kutumia kurasa zao katika mtandao wa Instagram wanaomboleza.

Msanii Chege Chigunda ameweka picha ya mwanasiasa huyo na kuandika, “lala salama.”

Jackline Wolper ameandika, “Nitoe pole kwa wafiwa wote na kwa familia ya mzee wetu Kingunge. Najua jinsi gani inauma kumpoteza baba, babu, mlezi na kiongozi pia.”

“Lakini Mungu kampenda zaidi na maumivu yanazidi hasa mama naye tumempoteza siku si nyingi hata arobaini bado na leo hii mzee wetu pia ametuacha. Mungu ana mitihani yake lakini kazi zake pia hazina makosa.”

“Poleni sana Watanzania wote! Mungu alaze roho ya mzee wetu mahala pema peponi...bwana ametoa, bwana ametwaa jina lake lihimidiwe,” ameandika Wolper.

Wasanii wengine walioomboleza ni Lady Jay Dee na Profesa Jay walioandika maneno, “Pumzika kwa Amani.”


Mbunge Ahofia Usalama Wake

$
0
0
Mbunge Ahofia Usalama Wake
Mbunge wa Tabora Mjini (CCM), Emmanuel Mwakasaka ameonyesha hofu kuhusu usalama wa wabunge bungeni kutokana na viti kuwa vibovu.

Ametoa mfano akisema amewahi kuanguka baada ya kukalia kiti kibovu.

Mwakasaka ametoa kauli hiyo bungeni leo Februari 2,2018 baada ya kuomba mwongozo wa Spika.

Amesema viti wanavyokalia vingi ni vibovu, vimefumuka na baadhi kung’oka hivyo kuwa hatari kwa wabunge kwa kuwa vinaweza kuwategua nyonga.



"Hivi ninavyoongea pale nyuma anapokaa mheshimiwa Obama (Albert- Mbunge Manyovu-CCM) hakuna kiti, nimebinuka nacho mimi. Isingekuwa mazoezi kisogo changu kingekuwaje? Pale kiti kipo chini nimeanguka nacho mimi,” amesema.

Amesema, "Naomba mwongozo wako hivi viti vinafanyiwa matengenezo wakati gani? Hasa kwa kuangalia usalama wa wabunge kwa kuwa wengine ni watu wazima wakiteguka nyonga itakuwaje?”

Akijibu, Mwenyekiti wa Bunge, Andrew Chenge amesema mwongozo huo umepokewa na wataona ni nini cha kufanya kulingana na hali ya fedha.

Afya ya Rugemalila, Sethi Yazidi Kuwa na Mashaka

$
0
0
Afya ya Rugemalila, Sethi Yazidi Kuwa na Mashaka
February 2, 2018 Upande wa utetezi umeieleza Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kuwa afya ya mmiliki wa IPTL, Harbinder Singh Sethi na mfanyabiashara James Rugemarila zinaendelea kuwa za mashaka.

Hayo yameelezwa na Wakili wa utetezi, Respicius Didas baada ya Mwendesha Mashtaka wa TAKUKURU, Leornad Swai kumueleza Hakimu Mkazi Mkuu, Huruma Shaidi kuwa upelelezi wa kesi hiyo haujakamilika.

Wakili Didas amedai kuwa wakati afya za washtakiwa zikiendelea kuwa za mashaka wanauomba upande wa mashtaka ukamilishe upelelezi ambapo Wakili Swai alijibu kuwa ni kweli upelelezi unachukua muda mrefu ila upo katika hatua za mwisho na kinachochelewesha ni upelelezi mwingine kuwa nje ya nchi.

Hata hivyo, Rugemarila aliieleza Mahakama kuwa hajawahi kupelekwa Hospital ya Taifa Muhimbili kwa ajili ya matibabu, pia anahisi ana saratani kutokana na uvimbe alionao mwilini mwake.

Baada ya kueleza hayo, Hakimu Shaidi amesema mahakama hiyo haina mamlaka ya kutoa amri wakatibiwe nje ya nchi na alishatoa amri kwamba watibiwe Muhimbili na kama inahitajika wakatibiwe nje ya nchi serikali ndio itasimamia. Aliahirisha kesi hadi February 16,2018.

Patrobas Katambi Aibuka na Kufunguka Udhaifu wa Vyama vya Upinzani

$
0
0
 Patrobas Katambi Aibuka na Kufunguka Udhaifu wa Vyama vya Upinzani
Aliyewahi kuwa Mwenyekiti wa Baraza la vijana la Chama cha Demookrasia na Maendeleo-CHADEMA ambaye hivi karibuni alikihama chama hicho na kuhamia CCM Patrobas Katambi amejitokeza kwa mara ya kwanza na kueleza udhaifu mkubwa wa kiuongozi uliopo ndani ya vyama vya siasa hapa nchini.

Akizungumza na waandishi wa habari Jijini Dar es salaam Patrobas amesema, vyama vingi vya siasa vya upinzani vimekuwa mali ya wenyeviti wa vyama hivyo na kueleza kuwa haviwezi kusonga mbele kutokana na mwenendo wa vyama hivyo.

Katambi amesema kuwa vyama vya siasa vya upinzani, vimekuwa vikifuja fedha za ruzuku na mara zote vimekuwa vikipata hati chafu katika matumizi yao ya ruzuku na fedha nyingine za chama.

Mwanasiasa huyo machachari amesema, alimua kutoka-CHADEMA kutokana na kupotea kwa ajenda na hoja za msingi na kusema kuwa wote waliobakia katika vyama vya upinzani wananufaika na mfumo uliopo.

Utata Nafasi ya Lionel Mess, Coutinho

$
0
0
Lionel Nafasi ya Mess Yazua Utata
Kocha wa Barcelona Ernesto Valverde ameeleza kuwa majukumu ya wacheaji wake nyota Lionel Messi na mchezaji ghali zaidi wa klabu hiyo Philippe Coutinho yanabadilika kutokana na aina ya mchezo.


Akiongea baada ya ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Valencia jana usiku, Valverde alisema Coutinho analazimika kucheza kiungo cha katikakati kutokana na Messi kupenda kucheza winga ya kulia lakini muda mwingine anaingia katikati kusaidia timu.

"Ni kweli Coutinho namchezesha katikati kwa sababu wakati mwingine Messi anapenda kucheza upande wa kulia, lakini tayari nimeshajua namna ya kumtumia badala ya kucheza kulia atakuwa anacheza pande zote mbili ili kumpa nafasi Messi upande wa kulia pamoja na katikati'', amesema.

Valverde ametetea pia uamzi wake wa kumchezesha Coutinho upande wa kulia ni kwasababu mchezasji huyo hucheza vizuri kwenye eneo hilo akiwa na Brazil ambayo inacheza soka sawa na Barcelona lakini ameona ampe nafasi kucheza winga zote huku akimwacha Messi acheze kila mahali.

Aidha kocha huyo raia wa Hispania pia amesema wanahitaji kumpumzisha Messi na majukumu makubwa ndani ya klabu. Messi jana alisaidia kupatikana kwa bao hilo moja baada ya krosi yake kuunganishwa kwa kichwa na Luis Suarez.

Kingunge Kuzikwa Jumatano Makaburi ya Kinondoni

$
0
0
Kingunge Kuzikwa Jumatano Makaburi ya Kinondoni
Mwanasiasa mkongwe nchini, Kingunge Ngombale-Mwiru anatarajiwa kuzikwa Jumatatu Februari 5, 2018 katika makaburi ya Kinondoni jijini Dar es Salaam.

Mwenyekiti wa kamati ya maziko ya mwanasiasa huyo, Omary Kimbau amesema  Kingunge atazikwa saa tisa alasiri.

Hata hivyo, amesema leo Ijumaa Februari 2,2018 kuwa utaratibu na mipango mingine inaendelea kufanyika.

Kingunge amefariki dunia leo alfajiri akipatiwa matibabu katika Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH).

Alikuwa akiuguza majeraha baada ya kung'atwa na mbwa mwishoni mwa mwaka jana nyumbani kwake.

Mpwa wa Kingunge, Tony Mwiru amesema familia inapitia kipindi kigumu kwa kuwa hivi karibuni wamempoteza mama yao, Peras.

Enock Mwiru ambaye ni mdogo wa marehemu na mtangazaji wa zamani wa iliyokuwa Redio Tanzania (RTD),  amesema  Kingunge alikuwa kiunganishi cha familia.

Mabalozi Juma Mwapachu na Ali Mchumo waliowahi kufanya kazi na Kingunge wamefika nyumbani kwa marehemu Kijitonyama kuhani msiba huo.

Balozi wa Uturuki Awakabidhi Tuzo Simba

$
0
0
Balozi wa Uturuki Awakabidhi Tuzo Simba
Balozi wa Uturuki nchini Mh. Ali Davotuglu amewakabidhi tuzo na medali, wachezaji ambao wamepata mafanikio katika mechi mbalimbali za timu hiyo ikiwemo tuzo ya mchezaji bora wa mwezi Disemba.


Hafla hiyo ambayo imefanyika jana usiku nyumbani kwa balozi huyo golikipa namba moja nchini Aishi Manula alikabidhiwa tuzo ya mchezaji bora wa mwezi Disemba wa klabu ya Simba.

Mbali na tuzo hiyo ya Manula wachezaji wengine walikabidhiwa medali za kuwa wachezaji bora wa mechi nne zilizopita ambao ni nahodha John Boko ambaye aliibuka mchezaji bora wa mechi dhidi ya Ndanda FC.

Mwingine ni kiungo Said Ndemla ambaye aliibuka mchezaji bora wa mechi ya Simba SC dhidi ya Kagera Sugar iliyopigwa mkoani Kagera na Ndemla kufunga bao moja pamoja na kusaidia jingine moja kwenye ushindi wa mabao 2-0.

Hafla hiyo maalumu iliandaliwa na Ubalozi wa Uturuki kwa ajili ya kujenga na kuimarisha ushirikiano mzuri kati ya klabu ya Simba na nchi ya Uturuki.

AU Yachukizwa Kuapishwa kwa Raila Odinga Yaitaka NASA Kuheshimu Matokeo

$
0
0
Mwenyekiti wa Tume ya Umoja wa Afrika (AU), Moussa Faki Mahamat amesema anafuatilia kwa karibu mabadiliko ya hali ya kisiasa nchini Kenya na ameonyesha kutofurahishwa na sherehe zilizoandaliwa na Nasa “kumwapisha” Raila Odinga kuwa “rais wa watu wa Kenya".

Mwenyekiti huyo alisema kumbukumbu zinaonyesha wa Ujumbe wa AU wa Uangalizi wa Uchaguzi wa Kenya uliongozwa na rais wa zamani Afrika Kusini Thabo Mbeki ulirejesha taarifa kwamba uliona uchaguzi ambao matokeo yake yalikubaliwa na Mahakama ya Katiba ya Kenya.

Mahamat amesema, “Kwa kuzingatia hali hiyo, na kwa mujibu wa vyombo vyote muhimu, hasa Mkataba wa Afrika juu ya Demokrasia, Uchaguzi na Utawala, Umoja wa Afrika unakataa vitendo vyote vinavyodhoofisha utaratibu wa kikatiba na utawala wa sheria.”

Mwenyekiti anahimiza wote wanaohusika kuacha vitendo viovu vinavyoweka uthabiti wa kisiasa nchini Kenya kuwa katika hatari. Anawahimiza wadau wote wachukue hatua kwa kuzingatia Katiba ya Kenya na maandiko mengine muhimu.

Kadhalika Mwenyekiti wa Tume anawahimiza watu wa Kenya kuendeleza kikamilifu njia sahihi za utawala wa sheria na kuimarisha taasisi zao za kidemokrasia, na kuachana na vitendo vingine vinavyoweza kudhoofisha utulivu wa nchi yao na maendeleo yake ya kijamii na kiuchumi.

Pia amesema Umoja wa Afrika uko tayari kusaidia njia yoyote inayoonekana kuwa sahihi ili kuondokana na mvutano wa sasa kwa misingi wa kuheshimu kanuni na utaratibu wa kikatiba na utawala wa sheria.

Habari Njema: Tunatibu Busha, Korodani Kuvimba, Ngiri, Miguu Kufa Ganzi Pamoja na Matatizo ya Nguvu za Kiume

$
0
0

Ni dawa ya nguvu za kiume inayorefusha na kunenepesha uume saizi uipendayo (Inch 1-7) kwa muda wa siku 6 tu.Dozi hii itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa muda wa dakika 30, utarudia tendo la ndoa zaidi ya mara 4 bila hamu kuisha bila kujali umri na garantee ni miaka 60 baada ya kutibu tatizo.

Pia tunatibu Busha bila kufanyiwa Oparesheni, korodani moja kuvimba, ngiri, tumbo kujaa gesi na kuunguruma, kutopata choo vizuri, miguu kuwaka moto na kufa ganzi, chango la wanawake, kisukari na kutokwa na kinyama sehemu ya haja kubwa.

MIHAYO:
Inarudisha mke, mchumba, hawara na atakutimizia kila kitu unachotaka kutoka kwake ndani ya  saa 2 tu hata kama yupo mbali. atarudi na kumfunga asiwe na mwingine zaidi yako.

Umefukuzwa kazini? unataka kupandishwa cheo? Umepoteza pesa zako kwenye biashara bila kujua umepandikizwa chuma ulete? Njoo urudishe pesa zako. Unauza mali yako haiendi?


Wasiliana na mtaalam Challo kwa; 0714006521 

Rugemalila Alalamika Mbele ya Hakimu "Sijapelekwa Muhimbili Kutibiwa na Wala Sijatibiwa Naomba Kibali Nikatibiwe India"

$
0
0

Rugemalila Alalamika Mbele ya Hakimu "Sijapelekwa Muhimbili Kutibiwa na Wala Sijatibiwa Naomba Kibali Nikatibiwe India"
Mfanyabiashara James Rugemalila anayekabiliwa na kesi ya utakatishaji fedha na uhujumu uchumi leo Ijumaa Februari 2, 2018 ameieleza Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kuwa hajawahi kutibiwa Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH).

Rugemalira ametoa madai hayo baada ya upande wa mashtaka kuieleza mahakama hiyo kuwa washtakiwa katika kesi hiyo wanatibiwa Muhimbili.

Rugemalira na mwenzake Habinder Sethi ambaye ni Mmiliki wa Kampuni ya Kufua Umeme ya IPTL, wanakabiliwa na kesi ya uhujumu uchumi, utakatishaji fedha  na kuisababisha Serikali hasara.

" Mheshimiwa hakimu sijapelekwa Muhimbili kutibiwa na wala sijawahi kutibiwa, bado nina uvimbe ambao ninahisi ni saratani" amedai Rugemalira.

Amesema anaomba apatiwe kibali cha kwenda kutibiwa India ambako ndipo alipotibiwa kipindi cha nyuma baada ya kugundulika kuwa na saratani.

"Daktari wangu na hospitali ninayotibiwa ipo India, hivyo upelelelezi unavyochelewa na hili dude (uvimbe) lilivyovimba ndio nazidi kuchanganyikiwa," amesema Rugemalira,

"Nataka kuweka kumbukumbu sawa, daktari wangu  Fred kutoka hospitali ya Sanitas  nilitaka aje aonyeshe vipimo vyake kama kweli sina saratani, lakini kwa bahati mbaya amefiwa na leo hayupo mahakamani."

Mshtakiwa huyo amedai hata muda wa kwenda kufanyiwa uchunguzi umeshapita kwani alitakiwa kwenda India kati ya Julai na Septemba mwaka 2017, lakini alishindwa kwa kuwa yupo rumande.

" Mheshimiwa huu uvimbe wangu ni saratani  tu, kwa sababu nimeshapitia katika hali kama hii kwa miaka 10, ndio maana naomba kwenda kutibiwa India kwa sababu kule kuna vifaa vya kisasa"amedai.

Kutokana na madai hayo, Hakimu Mkazi Mkuu wa Mahakama hiyo, Huruma Shahidi amesema madaktari wa MNH ndio wenye kuthibitisha  mshtakiwa akatibiwe wapi.

Awali, Mwendesha Mashtaka kutoka Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), Leonard Swai amedai mahakamani hapo kuwa Serikali inajitahidi kuchukua hatua stahiki katika kuwapatia matibabu washtakiwa hao ikiwemo kuwapelekea Muhimbili.

Hakimu Shahidi ameahirisha kesi hiyo hadi Februari 16, 2018  itakapotajwa na washtakiwa hao kurudishwa rumande.

Washtakiwa kwa pamoja wanakabiliwa na mashitaka  12 ya  uhujumu uchumi, utakatishaji fedha  na kuisababisha serikali hasara ya  dola 22,198,544.60 za Marekani  na Sh 309,461,300,158.27.

Pius Msekwa Ashtushwa na Kifo cha Kingunge

$
0
0
 Pius Msekwa Ashtushwa na Kifo cha Kingunge
Spika mstaafu wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Pius Msekwa amemlilia mwanasiasa mkongwe nchini, Kingunge Ngombale Mwiru aliyefariki dunia leo asubuhi Februari 2,2018 Hospitali ya Taifa ya Muhimbili alikokuwa amelazwa kwa matibabu.

Akizungumza nyumbani kwake Oysterbay katika mahojiano na Mwananchi, amesema Kingunge amekuwa naye katika shughuli nyingi ikiwamo ndani ya kamati maalumu iliyoundwa na Mwalimu Julius Nyerere kuandaa mwongozo uliotengeneza Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Katiba ya Zanzibar.

Amesema Kingunge ameshika nafasi mbalimbali za uongozi serikalini ikiwamo waziri wa ushirika na alifanya kazi kubwa kwa vyama vya ushirika.

Amesisitiza kuwa licha ya Kingunge kuondoka ndani ya CCM, lakini ana historia ya kusimamia utengenezaji wa ilani ya uchaguzi ya chama hicho tawala katika chaguzi nyingi zilizopita.

Msekwa amesema amepokea kifo hicho kwa mshtuko kwa kuwa siku chache zilizopita mwanasiasa huyo mkongwe alifiwa na mkewe Peras.

Aukumiwa Baada ya Kumtilia Mkewe Pilipili Kwenye Chupi

$
0
0
Aukumiwa Baada ya Kumtilia Mkewe Pilipili Kwenye Chupi
Mtu mmoja anyejulikana kwa jina la Moses Okello amehukumiwa kifungo cha nje na kufanya kazi za jamii kwa siku 40, baada ya kukutwa na hatia ya kumtilia pilipili mke wake kwenye nguo ya ndani.


Mke wa Okello aliiambia mahakama kuwa mume wake huwa anapenda akiwa amevaa nguo hiyo, na siku hiyo alimlazimisha sana kuivaa na kutekeleza, na baada ya muda mfupi alihisi kuwashwa na kuvimba sehemu za siri na kuamua kwenda kumuona daktari, ndipo walipogundua ilikuwa ni pilipili.

“Aliniambia anavutiwa sana na mimi nikiwa nimevaa hiyo nguo akawa ananilazimisha kuivaa, baada ya kuivaa nikaanza kuhisi muwasho sana, nikaenda kumuona daktari na kugundua ilikuwa pilipili”, amesema Mke wa bwana Okello ambaye jina lake limehifadhiwa.

Moses alikiri kufanya tukio hilo kwa mkewe, na kusema kwamba ulikuwa ni utani ambao amezoea kufanyiana na mke wake huyo kipenzi.

Kinje Afunguka Kuhusu Kifo cha Baba Yake

$
0
0
Kinje Afunguka Kuhusu Kifo cha Baba Yake
KINJEKITILE Ngombale Mwiru ambaye ni mtoto wa mwanasiasa mkongwe nchini, marehemu Ngombale Mwiru ambaye amefariki leo asubuhi katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili, amesema taratibu za mazishi ya baba yao zitafanyika baada ya familia kukaa pamoja leo.

Akizungumza na waandishi wa habari waliofika nyumbani kwao, eneo la Victoria, Mwananyamala, jijini Dar es Salaam, amewapongeza madaktari wa Hospitali ya Muhimbili kwa jitihada zao za kupigania uhai wa marehemu lakini Mwenyezi Mungu alimpenda zaidi.

“Baada ya baba kuumwa na mbwa alianza kupata complications (matatizo) ya moyo na mapafu, hivyo kwa muda wa siku tatu alihangaika sana wakati akipatiwa matibabu, hivyo cha msingi ni sisi kumwombea kwa Mungu apumzike kwa amani,” alisema Kinjekitile
Viewing all 104709 articles
Browse latest View live




Latest Images