Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104709 articles
Browse latest View live

Uwezi Amani Ngoma za Vigodoro Bado Zinaendelea Uswahilini Japo Serekali Ilipiga Marufuku-SeePhotos

$
0
0
 Japo Serekali Ilikataza Ngoma za Vigodoro Hapa Jijini Dar Inaonekana Bado agizo hilo alijachukuliwa ipasavyo baada ya Ngoma hizo kuendelea kuchezwa huko uswahili vibanda inama kama unavyoona kwenye picha, 
Dada huyu ambaye jina lake halikufahamika mara moja akikata mauno huku akionesha nguo yake ya ndani mbele ya kadamnasi bila hata chembe ya haya

Msanii Maarufu wa Kike wa Bongo Movies Ajichora Tatoo ya Davido

$
0
0
Katika kile kinachoonyesha kuwa ni shobo kwa msanii Davido mdada huyu maarufu hapa bongo kwenye Tasnia ya Bongo Movies amechora tatoo kiunoni ambayo ina jina la msanii davido, huku watu wakimponda kwamba hizo ni ndoto na wala davido hajui hata kama kuna mtu kama yeye duniani, haha lakini mwenyewe amedai ni kushow love, ipo tu siku atachora ya diamond au alikiba

Ndoa ya Lucy Komba na Mzungu Wake Yaingia Mizengwe

$
0
0
Stori: Gladness Mallya
HUKU akiwa kwenye vikao vya maandalizi ya harusi na Mzungu, staa wa filamu Bongo, Lucy Francis Komba (pichani na mchumba wake), amejikuta katika wakati mgumu baada ya habari kudai kwamba, mchumba wake huyo amemwambia ili ndoa ifungwe lazima aoneshe cheti cha kipimo cha Ukimwi kwanza.

Chanzo chetu cha habari kikizungumza na Amani juzi, kilisema kwa sasa Lucy anahaha kutafuta cheti feki cha kipimo hicho kwa kwenda hospitali mbalimbali ili anunue kwa gharama yoyote lakini imeshindikana.
“Ukweli Lucy anahaha kutafuta cheti cha Ukimwi, mchumba anasubiri akione vinginevyo hawatafunga ndoa,” kilisema chanzo.

Ilidaiwa kuwa, mpaka sasa Lucy ameshafika kwenye hospitali tatu kubwa mbili, TMJ na Marie Stopes ili kufanya maarifa lakini imeshindikana.

Baada ya kupata habari hizo paparazi wetu alimtafuta Lucy ambapo alikuwa na haya ya kusema: 
“Si kweli! Hao wanaosema hivyo ni wanafiki, sijui wanataka nini maana kila siku wanazusha mambo ya ajabu. Kwanza mimi huwa sitibiwagi kwenye hospitali hizo ulizozisema, natibiwa Regency.

“Kuhusu  kupima Ukimwi, mimi na mchumba wangu tulishapima hukohuko kwao Ulaya (Denmark) ndiyo maana tukaanza taratibu za ndoa.

“Namshangaa sana huyo aliyesema hayo hata kama ni mtu wangu wa karibu, mimi huwa simwelezi mtu mambo yangu binafsi kwa sababu duniani hakuna rafiki wa kweli, rafiki anakuchekea machoni lakini wote ni wabaya,” alisema Lucy.

Amani lilifika kwenye hospitali hizo lakini kukakosekana ushirikiano kwa madai kwamba, hakuna utaratibu wa kumtaja jina mgonjwa kama alikwenda kutibiwa.
GPL

Wanaswa Wakifanya Mapenzi Ndani ya Chumba Kimoja..Polisi Wawafunga Pinga na Kuwachukua

$
0
0
Tukisema dunia imekwisha watu hawaamini, mimi ninadhani ni wakati wakumgeukia Mungu sasa. Vijana hawo juu wamekamatwa kwa kosa la kufanya mapenzi wote wakiwa chumba kimoja
na wasichana wao.Najua msomaji utashtuka sana kwamba kwani kosa ni nini hapo, ila kwa wale wanajua sheria vizuri nadhani watajua kwamba hil ni kosa la jinai.

Taarifa zinasema baada ya watu kujua upuuzi uliokuwa unafanywa na wanaume hao wakliwa na wapenzi wao wote wakira uroda kwenye chumba kimoja, msamalia mwema alikwenda polisi kutoa taarifa na mara maaskari walikuja na kuwakuta vijana ndani ya mambo kitu roho inapenda(UTAMU KUNOGA).

Kwa sasa vijana hawa wanashikiliwa na polisi tayari kwa kufikishwa mahakamani kujibu shitaka hilo.

Miongoni mwa vijana hawo ambao mmoja wapo ameweza kutambuliwa kwa jina ni Jesse Orowo Omokoh raia wanigeria

Hapa wanavishwa pingu kama ishara ya kufahidi uhondo wakufanya mapenzi chumba kimoja.

Miss Tanga Azua Timbwili, Ataka Kuzichapa Kavu Kavu Kisa Ali Kiba

$
0
0
MISS Tanga 2011, Zubeida Seif ametaka kuzichapa kavukavu na mwenzake aliyefahamika kwa jina moja la Kelly kisa kikiwa ni mkali wa wimbo wa Mwana, Ali Saleh Kiba.

Tukio hilo lililoacha watu midomo wazi lilitokea juzikati katika baa moja iliyopo maeneo ya Mwenge, Dar ambapo ubishi ulianza baada ya Zubeydah  kutetea kuwa Ali Kiba anajua kuimba kuliko Nasibu Abdul ‘Diamond’ huku mwenzake akimpinga ndipo mtiti ulipoibuka.

Aibu! Wanafunzi wanaswa GESTI Wakijiandaa kula URODA

$
0
0
Wanafunzi wawili, wa kike ana miaka 14  (darasa la saba), wa kiume miaka 15 (kidato cha kwanza) mjini Morogoro wanadaiwa kukutwa ndani ya gesti moja ikisemekana walikuwa na lengo la kuivunjilia mbali amri ya sita ya Mungu.

Tukio hilo lililojaza umati lilijiri hivi karibuni katika gesti hiyo ambayo inadaiwa haina usajili halali iliyopo jirani na soko.

Habari zinasema kuwa, siku hiyo denti wa kike alitumwa sokoni na mama yake kununua mahitaji mbalimbali ya chakula lakini alichelewa kurudi.

Ikazidi kudaiwa kuwa mama yake alimfuatilia huku akiwauliza watu, ndipo mbeya mmoja akamtonya kuwa amemwona binti yake akiingia gesti hiyo na kivulana! Mama wa watu, akiwa na mshangao, naye alizama ndani na kuwakuta chumba namba 5.

Mwandishi alifanikiwa kutinga eneo la tukio wakati wa sekeseke hilo na kuzungumza na mashuhuda wawili, Asha Chande na Tausi Omary. Alipowahoji walisema waliwaona wawili hao wakizama ndani ya gesti hiyo na walishangaa kwa nini walikubaliwa kwa vile wote ni watoto.

”Baada ya muda mama mmoja mtu mzima alifika hapa akiwa amefura  kwa hasira, akadai binti yake aliyemtuma sokoni ameingia gesti, mara na yeye  akaingia ndani, alimkuta yupo na mvulana huyo huku mfuko aliotumwa nao sokoni binti wa kike ukiwa chini ya kitanda.

“Aliwafurumusha, kivulana kimekimbia zake na huyu binti ndiyo kama hivi. Mbaya zaidi hapa ni sokoni, watu wameacha biashara na kujaa,” alisema Tausi.

Wakati sakata hilo likiendelea, baadhi ya watu walitaka kumwangushia kipondo denti huyo wa kike kwa kitendo chake cha kuacha alichotumwa na kuzamia kwenye mapenzi akiwa bado mwanafunzi.

Baadaye polisi  wa pikipiki walifika na kumchukua denti huyo kwa lengo la kumuokoa na kipigo na kwenda naye Kituo Kikuu cha Polisi Morogoro ambapo ilidaiwa kuwa polisi walishauri wazazi wa watoto hao wakayamalize nyumbani.

Juhudi za mwanahabari wetu kutaka kuzungumza na mlinzi wa gesti hiyo ziligonga mwamba baada ya muda mwingi kufunga geti kubwa.

Tofauti Kati ya Wanamuziki Diamond Platnumz na Ali Kiba

$
0
0
Moja ya mdau mkubwa wa muziki nchini na mmiliki wa G Records, studio iliyomtoa Alikiba, Guru Ramadhan aka DJ G-Lover, amezungumzia tofauti iliyopo kati ya Diamond na Alikiba aliyewahi kuwa chini yake.

Akizungumza na Vijimambo, Lover ambaye akiwa meneja wa Alikiba walitoa album mbili, amewaka bayana uwezo wa kila msanii na jinsi walivyojikuta kwenye biashara.

“Kwa kweli tofauti ukija kwenye masuala uimbaji, wengi wanaongelea hata katika mitandao tofauti tofauti kwamba Ali ana sauti nzuri na anaimba vizuri. Hata Diamond kuna wakati alikuwa anakiri kwamba angekuwa ana sauti kama ya Alikiba basi angefanya mambo makubwa zaidi,” amesema G. “Lakini unapokuja kibiashara Diamond huwa anazungumza kUwa yeye muziki wake anaufanya kibiashara na ndo maana ana team work kubwa ambayo inamsaidia yeye kujua ni kitu gani anatakiwa kufanya, kuna kitu gani anatakiwa kukifanya kwa upande wa muziki. Sasa kwa upande wa Ali kwa sasa hivi, kwa kipindi niko naye nilikuwa na team ambayo hata yeye alikuwa hajui mimi nipo na akina nani nyuma yangu. Alikuwa anajua kuwa yupo G, lakini nyuma yangu nilikuwa na watu takriban thelathini ambao ni team work ambayo ilikuwa inafanya kazi kwa Ali Kiba kujua ni kitu gani na kitu gani tunatakiwa tufanye ili afike na mpaka akafika hapo,” aliongeza.

“Diamond naYe anafanya vitu kama hivyo, unaweza kuona Diamond ana team ya watu watatu tu au wanNe ambao wanamsaidia, kwaHiyo utaona Diamond kuna watu kibao ambao amewapa ajira. Kwahiyo Diamond hawezi kuwaangusha watu ambao wapo nyuma yake ambao wamepata ajira kutoka kwake. Kwa mfano kuna utofauti mkubwa ambao Diamond amekuja nao ambao ukiangalia ni utaratibu uleule ambao nilikuwa nikiufanya kwa Ali. Kwahiyo sijui kuna utofauti gani kati ya manamament ya Diamond na ya Ali Kiba ya sasa hivi

UKAWA Wajitoa Rasmi Kwenye Mchakato wa Katiba, Wanazuoni Wawapa Somo.

$
0
0
KAMA ndivyo, huenda Bunge Maalumu la Katiba, linalotarajiwa kuanza awamu ya pili ya vikao vyake keshokutwa mjini Dodoma, litafanyika bila ya kuwa na wajumbe kutoka kundi la Umoja wa Katiba ya Wananchi (UKAWA).

Hali hiyo inatokana na kauli ya Ukawa, inayoundwa na viongozi wa vyama vya siasa vya upinzani na wafuasi wao, kwamba hawatashiriki katika Bunge hilo na kwenda mbali zaidi, wakidai hawana mpango wa kuwa na vikao vya maridhiano dhidi ya wenzao wa chama tawala, CCM baada ya kikao kingine cha juzi, kilichokuwa cha nne, kukwama.

Kauli ya Ukawa ilitolewa jana, mbele ya waandishi wa habari na viongozi wa vyama vya siasa vinavyounda umoja huo, Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe, Mwenyekiti wa CUF, Profesa Ibrahim Lipumba wa CUF na Mwenyekiti wa NCCR-Mageuzi, James Mbatia. Kwa pamoja, walisema wameridhia kujiweka kando katika Bunge na vikao vya maridhiano. Chama cha NLD kinachoongozwa na Dk Emmanuel Makaidi, nacho kimejiweka kando.

Mbowe alifafanua kuwa baada ya kikao cha nne cha maridhiano kati ya umoja huo na CCM, kilichofanyika juzi chini ya Msajili wa Vyama vya Siasa, Jaji Francis Mutungi kuvunjika, wametafakari kwa kina na kubaini kurejea bungeni kuendeleza mivutano, hakutakuwa na tija kwa Taifa.

“Hivyo tumeazimia kutorejea tena katika Bunge la Katiba wala kushiriki mazungumzo yoyote kuhusu suala hilo, kutokana na ukweli kuwa mazungumzo haya yaliyovunjika, yalikuwa ya kuwezesha kupata Katiba bora, lakini CCM waliyafanya kuwa yenye maslahi ya chama chao, siyo Taifa.

”Na baada ya awamu nne za vikao vya mazungumzo kati yetu na CCM, Ukawa tunatangaza kwamba hatuko tayari kuendelea na mazungumzo na CCM wala kurudi katika mkutano wa Bunge Maalumu la Katiba, kwa kuwa kufanya hivyo ni kusaliti maoni ya wananchi na kutumia vibaya fedha za umma,” alisema Mbowe.

Kauli ya CCM Hata hivyo, kwa mara nyingine jana, Katibu wa Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) ya CCM, Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye alisema chama chake hakijashangazwa na uamuzi huo, kwa kuwa walifahamu Ukawa hawana hoja za msingi, hivyo wamekimbia aibu.

“Hata kwenye vikao, hawakuwa na kitu kipya, ni malalamiko tu huku wakishindwa kujenga hoja, kwa hiyo tulijua hawa wenzetu lazima mwisho wa siku wakimbie aibu yao…ni aibu tu imewashika, ndiyo maana wamepatafuta pa kutokea,” alisema Nnauye.

Wakati huo huo, Mkuu wa Shule ya Sheria nchini Kenya, Profesa Patrick Lumumba amewasihi wajumbe wa Umoja wa Katiba ya Wananchi (UKAWA) kuwa itakuwa si busara kutorejea bungeni Agosti 5, mwaka huu, badala yake watumie nafasi hiyo kurudi bungeni na kushindanisha hoja zao.

Alisema hayo katika mdahalo wa kutoa maoni na msimamo wa wananchi, juu ya mivutano ya makundi katika mchakato wa Katiba. Mada mdahalo huo ilikuwa ni “Nini suluhisho na wajibu wa makundi katika mchakato wa Katiba”.

Mdahalo huo ulitayarishwa na Chama cha Wanasheria wa Tanganyika (TLS). Ulifanyika katika ukumbi wa Ubungo Plaza, Dar es Salaam, jana.

“Katiba ni ya Watanzania, siyo wanasiasa wa Tanzania, wale waliomo ndani ya Bunge la Katiba ni wajumbe tu ambao wametumwa, kwa maana hiyo hata kama ni wanasiasa wako kule ni lazima wasahau vyama vyao na kuupa kipaumbele Utanzania wao,” alisihi Profesa Lumumba.

Alisisitiza kuwa Tanzania ina nafasi ya kipekee na kihistoria barani Afrika ya kupata Katiba mpya, bila mapigano ya aina yoyote. Alisema litakuwa ni jambo la kushangaza na kusikitisha, ikiwa amani iliyopo hivi sasa, itatumiwa na wanasiasa wenye ufinyu kwa mitazamo yao ya siasa na kusababisha mapigano.

Profesa Lumumba alisema Rais Jakaya Kikwete aliona umuhimu wa Tanzania, kuwa na Katiba mpya na aliamua kuanzisha mchakato wa kuandika Katiba hiyo.

Profesa huyo alisema Rais Kikwete anastahili kupongezwa na kila mtu, kwa hatua yake hiyo kubwa na nzuri kwa Taifa la Tanzania.

Alisema Tanzania inatakiwa kujifunza kuhusu uandikaji wa Katiba mpya, kutokana na makosa yaliyofanywa na nchi nyingine, ambako yalitokea mapigano

Ewe Rais Kikwete! Tenda Wema Nenda Zako, Usingoje Shukurani itakuletea Matatizo

$
0
0

Wakati wewe ukipambana kuleta maridhiano kila panapokuwa na migogoro inayohatarisha ustawi wa taifa, wengine wanafanya njama za kukwamisha maridhiano na kukudhihaki. Ewe Rais Kikwete, tenda wema nenda zako...... Mungu yuko upande wako na wenye hekma wanakuelewa vyema na watakuwa wanashukuru kwa jitihada zako.

Wakati ukijishusha ili kutoa ushirikiano na kutoa mwanya watu watoe yao ya moyoni bila woga, wengine wanatumia mwanya huo kujikweza na kutaka kujionesha wao ni akina nani na ikibidi kuvuruga hali ya mambo ili ikibidi udhalilike. Ewe Rais, Kikwete, tenda wema nenda zako!

Wakati mataifa mengine na ulimwengu ukitambua mchango wako katika jamii, nyumbani wengi wanakubeza na kukukatisha tamaa, Ewe rais Kikwete, endelea na moyo wako wa kuwa mvumilivu na mtulivu wakati wote kwani wengi miongoni mwetu, katika yale yanayotokea, tungeweza kupata jazba na kufanya maamuzi ya hasira!.

Ewe rais Kikwete, Tenda wema nenda zako , wala usingoje shukurani kwani itakuletea matatizo. Mungu akujalie moyo mwepesi na utulivu kila unapokabiliana na changamoto kwa mambo yenye maslahi ya kitaifa na endelea kujishusha kwani kila anayejishusha basi huyo atakwezwa na kila anayejifaharisha ili watu wamjue yeye nani, hatimae atashushwa!.

Mungu akujaalie busara zaidi na hekma uweze kuendelea kuwa na moyo wa Ihsani.


Wachache wa kuelewa na waelewe, wale wa kuchanganyikiwa na wachanganyikiwe na wakutukana kwa sababu ya chuki nawatukane.

TBC Imevaa Koti la CCM, Nani Anabisha? Hongera ITV Kwa Kuelimisha Jamii

$
0
0
Hili liko wazi kabisa kuwa TBC1 na TBC FM badala ya kuwa chombo chenye maslahi kwa Taifa zima yaani wenye vyama na wasio na vyama lakini imegeuka kuwa chombo cha matangazo na uenezi wa CCM.

Taarifa zinazohusiana na mafanikio katika mikutano ya vyama vya upinzani ama asasi zenye mtazamo tofauti na CCM hazirushwi na Tv wala redio ya Taifa isipokuwa ya CCM ama vikundi vinavyoisifia CCM.
Makongamano mengi yanayofanyika nchini kuelimisha wananchi kuhusiana na mustakabali wa Taifa letu hayarushwi hata kwa kuchukuliwa vipannde hasa vinavyoikosoa serikali ya CCM.

Nadhani ninyi nyote ni mashahidi.
Je, nani anabisha na kwanini?

Hongera ITV Angalau Mpo Katikati na Mnaonesha vipindi Bila Kuwa Mlango wowote wa Kisiasa..

TAHADHARI: Tanzania Kuna Biashara ya Wauaji wa Kukodi

$
0
0
Mitandao ya kihalifu inazidi kujiimarisha nchini na sasa kumeibuka makundi ya wauaji wa kukodi katika mikoa ya kaskazini mwa nchi pamoja na Kanda ya Ziwa.

Mbali na mauaji ya albino na vikongwe ambayo yalipata kutikisa katika maeneo kadhaa ya nchi, wauaji wa kukodi wanatumika kutekeleza uhalifu huo kwa lengo la kulipiza kisasi, uporaji wa fedha, kujitanua kibiashara au kudhulumu mali na fedha.

Uchunguzi wa muda mrefu uliofanywa na gazeti hili umebaini kuwa silaha nyingi zinazotumika katika mauaji ya kukodi yanayofanyika mikoa ya Kanda ya Kaskazini, hununuliwa ama kukodishwa kutoka Namanga upande wa Kenya.

Wauzaji wa silaha hizo ni ama raia wa Kenya wenye asili ya Kisomali ama wahamiaji haramu wenye asili ya Kisomali wanaoingia nchini, wakitokea Somalia kupitia Kenya.

Uchunguzi umebaini kuwa bunduki aina ya Submachine Gun (SMG) huuzwa kati ya Sh3 milioni hadi Sh5 milioni na bastola zikiuzwa kati ya Sh500,000 na Sh1.2 milioni.

Pamoja na kutoka nje ya nchi, wauaji wengine wa kukodi hupatikana nchini kulingana na aina ya mtu wa kuuawa, mazingira na ugumu wa kazi.

Kwa Tanzania, mikoa inayoongoza kwa kuwa na wauaji wa kukodi ni Arusha na Manyara na Mkoa wa Kilimanjaro umekuwa ukiguswa kuwa jirani na mikoa hiyo.

Akizungumza kwa sharti la kutotajwa jina, mtoa taarifa wetu alisema alisema: “Hata sasa ukihitaji vijana wa kazi nitakuunganisha. Jambo muhimu hakikisha huwarushi (unawapa fedha zao), ukiwarusha lazima na wewe watakuua.”

“Yupo rafiki yangu anayewafahamu vyema kwa sababu amewahi kuwaunganisha na waliokuwa wakihitaji huduma yao,” alisema mtoa habari huyo.

Malipo ya kuua

“Malipo kwa kazi hii yanaanzia kati ya Sh1 milioni na Sh5 milioni kutegemea na uzito wa kazi husika,” alisema mtoa taarifa wetu anayeishi Arusha na akithibitisha kwamba anafahamiana na madalali wa wauaji hao.

Alisema mara nyingi wauaji hao hawataki kukutana na wateja moja kwa moja ili kuepuka kutambulika, badala yake hukutana au kuwasiliana na mtu wa kati (wakala) ambaye pia hupokea malipo na kuwakabidhi.


Hata hivyo, uchunguzi wa gazeti hili ulibaini kuwa kiasi cha malipo kwa mikoa ya Kanda ya Kaskazini ni kikubwa ikilinganishwa na Kanda ya Ziwa ambako hulipwa fedha kidogo.

Vyanzo hivyo vimedokeza malipo wanayopata katika mikoa hiyo ni Kati ya Sh200,000 hadi Sh1 milioni kwa kuzingatia eneo husika na walikotolewa na kwamba fedha hizo huwa ni ujira wa watu wawili au zaidi.

Katibu wa Jumuiya ya Kuhifadhi Mila na Desturi za Mtanzania Kanda ya Ziwa, Gambang’adi Kaliba anasema wanaokodiwa ni wale wasiokuwa na vipato, walevi na wavuta bangi ambao wamekata tamaa ya maisha, hivyo hupewa fedha kidogo kwa ajili ya mauaji hayo ya kikatili.

“Watu wanalipwa Sh200,000 mpaka 500,000 kwa kuwa hawafanyi kazi wanaziona nyingi na wamekuwa wakijulikana katika baadhi ya maeneo kwa kuwa wakilewa hutamba na kuwa wako tayari kumwaga damu ya mtu maadam wapewe fedha,” anasema Kaliba.

Mkoani Mara, uchunguzi ulibaini kuwa kumekuwapo na mauaji ya aina hiyo na kwamba malipo kwa kifo cha mtu huwa ni kati ya Sh300,000 na 500,000.

Mwanaharakati wa Haki za Binadamu wilayani Ukerewe ambaye aliomba jina lake lihifadhiwe anasema wanapowakamata wahusika wa mauaji, baadhi hukiri kukodiwa kwa malipo ya Sh200,000 na kwamba idadi yao huwa ni kati ya watu wawili au watatu.

Mifano hai

Chanzo kimoja kutoka ndani ya Jeshi la Polisi mkoani Manyara kililiambia gazeti hili kuwa mauaji ya mmoja wa wafanyabiashara yalifanywa kwa kutumia mtandao huo.

Aliuawa mwaka jana wilayani Hai, Mkoa wa Kilimanjaro.

“Mirerani ndiyo umafia huo unatumika sana unajua kule ni unyama unyama kwa hiyo mtu kukuua kwa sababu ya mawe ni jambo la kawaida,” alidokeza polisi huyo.

Habari za kipolisi zinaeleza kuwa wauaji wa mfanyabiashara huyo walilipwa kati ya Sh3 milioni milioni na Sh5 milioni baada ya kukodiwa mahususi kutekeleza mauaji hayo.

Bunduki aina ya SMG inayodaiwa kutumika katika mauaji hayo ilinunuliwa kwa Sh4 milioni katika mpaka wa Tanzania na Kenya, Namanga kutoka kwa watu wenye asili ya Somalia.


Mauaji mengine yanayofanana na hayo yalitokea Januari 26, 2006 saa 2:30 usiku nje ya klabu maarufu ya Peters Club iliyopo Majengo katika Manispaa ya Moshi mkoani Kilimanjaro.

Siku hiyo watu waliokuwa na SMG walimmiminia risasi mfanyabiashara wa magari ya ‘dili’, Aristarik Msacky (34) na kutochukua chochote isipokuwa simu yake ya mkononi.

Kabla ya kuuawa, mfanyabiashara huyo alikuwa akinywa pombe na marafiki zake ndipo alipopigiwa simu ili atoke nje kuna ‘biashara’ na alipotoka nje ya baa ili kukutana nao ndipo alipouawa.

Tukio jingine ni lile la mkazi wa Kijiji cha Nyichoka wilayani Serengeti, Mara ambaye alituhumiwa kumuua mwendesha pikipiki (bodaboda), Julai 5 mwaka huu ambaye kwa mujibu wa polisi, alikiri kufanya mauaji hayo kwa kukodiwa.

Polisi walisema mtuhumiwa huyo (jina tunalihifadhi) alikiri kwamba yeye na mwenzake ambaye aliuawa na wananchi wenye hasira kali, walikodiwa na mkazi wa Park Nyigoti kutekeleza mauaji hayo kwa Sh500,000 kwa madai kuwa bodaboda alikuwa na uhusiano na wake zake.

Hata hivyo, mpaka wanatekeleza mauaji hayo kwa kumkatakata na kumtumbukiza mtoni, walikuwa wamelipwa Sh40,000 tu na kati ya fedha hizo Sh20,000 zilikuwa za kukodi pikipiki na zilizobaki kwa ajili ya chakula. Hadi mmoja alipouawa na yeye kukamatwa walikuwa wakimdadisi ‘bosi’ wao Sh460,000.

Msemaji wa Polisi

Msemaji wa Jeshi la Polisi, Advera Senso alisema polisi wapo kwa ajili ya kulinda usalama wa raia na mali zao na hivyo ndivyo wamekuwa wakifanya kila wakati, kutimiza wajibu huo.

Senso alisema kwamba endapo wakibaini kuwa kuna watu wanafanya uhalifu wa namna hiyo huwakatama na kuwafikisha mahakamani, huku akitoa mwito kwa wananchi na jamii nzima kutimiza wajibu wao wa kutoa taarifa za makundi kama hayo katika maeneo wanayoishi.

Halima Mdee Ajisalimisha kwa Mchungaji Gwajima

$
0
0
Katika hali ya kutokutegemea, Halima Mdee kaamua kujisalimisha kanisani la Ufufuo na uzima lililopo Kawe.

Kitendo hicho kimemuamsha Gwajima na kusema Kanisa la Ufufuo litakuwa naye katika uchaguzi wa 2015 na watamchagua tena.

Kanisa la Ufufuo na Uzima limemuahidi kumsaidia Halima Mdee kuhakikisha shule zote za Msingi Kawe zinakuwa na Umeme vilevile watahakikisha wanafunzi wote wa shule za Msingi Kawe wanakaa kwenye Madawati.

Gwajima kaitaka Serikali imruhusu kufanya Mikutano katika Mikoa ya kusini mwa Tanzania. Kasema gesi ni ya watanzania, Hata hivyo kasema migogoro ya Gesi haihusiani na imani za watu hivyo kataka waislam na Wakristo waruhusiwe Kufanya mikutano kusini Mwa Tanzania. Kaitaka serikali itambue gesi ni kwaajili ya Watanzania hivyo watanzania ndio inabidi wanufaike kwanza na hiyo gesi.

Band ya Jeshi la Magereza ndiyo imealikwa kumpigia Nyimbo Halima Mdee atakapokuwa anasimama kutoa salamu. Kasema anamheshimu Halima Mdee kwa kuwa ndiyo Mbunge Mwanamke wa kwanza Tanzania na Dar es Salaam kutoka Upinzani kushinda Uchaguzi bila kutoa Rushwa.

Kasema Halima Mdee anaiwakilisha na kuitangaza vizuri Kawe hivyo wanakawe inabidi watambue Umuhimu wake.

Gwajima anasema sisi ni Watanzania hatupaswi kuwekewa mipaka sehemu ya kufanya Injili ndo maana nimenunua Helkopta kuzunguka Tanzania nzima hata huko Mtwara nitaenda japo Serikali inakataza. Watu wa Mtwara nao inabidi wamjue Mungu ili kupunguza Uharifu. Vilevile Gwajima na washirika wake wamesema wanaunga Mkono Serikali Tatu. Kasema wale wanaodai mbili hata hizo mbili hazipo. Zingekuwa mbili kama Tanganyika ingekuwepo.

Gwajima kasema Zanzibar ipo lakini ipo na Serikali nyingine ambayo ni Tata. Hivyo watu wanapaswa watambue uwepo wa Tanganyika. 

Kasema Tanganyika na Zanzibar ni mbili tayari hivyo tunatakiwa tupate ya Tatu ambayo inaziunganisha hizi mbili. 

VIDEO:

Ladies:Ringeni Sana Mlio Kwenye Miaka 18 mpaka early 20's..Ukifikisha Miaka 30 Hujaolewa Utajuta

$
0
0
Wanawake waliofika miaka 30 na kuendelea na hawajaolewa huwa wanahonga asikwambie mtu, lengo ni kumvutia mwanaume ili amuoe.

Kutokana na kupoteza matumaini ya kutokuolewa kwa muda mrefu ikitokea kwa bahati mbaya au nzuri kuna mwanaume kajitokeza na kaonyesha dalili za kumuoa basi mwanamke huyo atamuhonga mwanaume pesa mpaka basi.

Mara akununulie suti, mara mashati, mara soksi.... ni hatariiii aisee..... yani hata awe hana hela yupo radhi alale njaa ilimradi akufurahishe

Mwanamke aliyezidi miaka 30 na hajaolewa akimpata mwanaume mwenye uelekeo basi anaweza akawa hata anambeba njiani, hata umwambie nibebe kutoka ubungo mpaka kariakoo basi mwanamke huyo atakubeba.

Ringeni sana mlio kwenye miaka 18 mpaka early 20's....... UKIFIKA MIAKA 28/29/30 UTAJUTA, NA HIYO NDIO MPAKA UZEENI...
____________
____________
UPDATE: Maisha yenyewe ya kiafrika haya, mtu ukiishi sana unafika miaka 40 halafu leo uolewe na miaka 35 au 37. YAANI UNAKAA SIKU MBILI AU TATU KWENYE NDOA HALAFU UNAKUFA?????? NA UKISHAFIKA 30+ HUWEZI PATA MWANAUME ORIGINALI AU BRAND NEW, UTAISHIA KUPATA USED/GUBE GUBE LILILOSHINDWANA NA MKEWE.

Agness Masogange Aamua Kubadilisha Uraia..Kwa Sasa si Mtanzania Tena

$
0
0
Kama mnavyojua  kwakipindi cha miezi isiopungua mi nne sasa..
Dada yetu Agnes Gerald aka Masogange aliamia nchini 

Afrika Kusini..Ambako kimsingi alipata bwana wa kuishinaye huko.

Leo hii asubuhi kupitia ukurasa wake wa INSTAGRAM 

masogange ametupia picha ya pasi ya kusafiria ya Afrika 

Kusini...na ku-caption alama ya kupiga makofi....hii 

nikuuonesha kuwa kwasasa sio raia tena wa Tanzania..kwa 

mujibu wa sheria zetu hapa Tanzania,haziruhusu uraia wa 

nchi mbili kwa hiyo kama ni kweli basi Masogange sio 

mtanzania mwenzetu tena...Baadhi ya watu waliocomment 

kumsifia ameonesha kuwajibu kwa furaha zaidi...

Karrueche Dumps Chris Brown Over Rihanna Photos....CHeck Out

$
0
0
Karrueche Tran did not like the fan-made photos Chris Brown liked on Instagram.
Word is, after seeing that C. Breezy hearted a couple of Photoshopped pics of him and Rihanna, Karrueche called it quits on their on-again-off-again saga.
Things got worse, when Breezy went to St. Tropez and was photographed with one of Karrueche's friends. "Chris acts immature, like a child," a source told the site.
Apparently, Karrueche's been unhappy for a long time (there has been a lot of "off again") and this series of social media suicides made her so upset that she's changed her phone number to block the "Loyal" singer from calling.
Good news is, the lyrics to "Loyal" apply all around here, not only with this love triangle, but at least 1 million other people. "1,000,000 units! #Loyal has now reached platinum sales. Thank you Team Breezy!" Chris tweeted Thursday.
And Karrueche hasn't given up on love entirely. She's helping an online friend find a girlfriend.

Picha: Kwa Gari Jipya na Zawadi ya Shilingi Milioni 250, Harusi ya Pastor Myamba ni Funika Bovu!

$
0
0
Kwa ukubwa wa zawadi aliyopewa, huenda harusi ya Pastor Myamba ikawa harusi ya staa wa Tanzania iliyofana na yenye stunts zaidi. 

Muigizaji huyo wa filamu aliukimbia mji wa Dar na kwenda kufungia harusi yake visiwani Zanzibar ambako hakuishia kualika mastaa wenzie tu, bali pia zawadi alizopewa, zinatosha kuanzisha kampuni yake nyingine. 

Kwa mujibu wa JB aliyehudhuria harusi hiyo, Pastor Myamba na mkewe wamezawadiwa pamoja vitu vingine, gari jipya na pesa taslimu shilingi milioni 250!! 

Mapaparazi Wanasa Picha za Justin Bieber Akiwa Mapenzini na Msichana Mpya-Wapi Lulu Michael

$
0
0


Pop star Justin Bieber aliungana na Kanye West,Kim Kardashian,P.Diddy na mastaa wengine kwenye mapumziko kwenye visiwa vya Ibiza. Baada ya party ya pamoja kuisha kila mtu aliendelea na party kivyake na Justin Bieber alionekana aki-enjoy muda wake na mshichana asiyejulikana.
Mikao yao na ukaribu wao kutokana na picha zilizopigwa wakiwa kwenye luxury yacht zinaonyesha kabisa wapo kwenye mapenzi. Wawili hao walitumia muda huo kukaa pamoja,kissing,kunywa na vitu vingine vizuri. Mapaparazi hawakuwaacha baada ya kuwapiga picha usiku huo kwasababu hadi asubui walipata picha zao bado wapo pamoja.
Tetesi zinasema kwamba anaweza kuwa ni girlfriend mpya wa Justin Bieber.

Kakobe: Ninaunga Mkono Ukawa Kususia Bunge

$
0
0
Askofu Mkuu wa Kanisa la Full Gospel Bible Fellowship (FGBF), Zachary Kakobe ameongeza chumvi katika Mchakato wa Katiba kwa kueleza kuwa anaunga mkono msimamo wa Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa) kutorejea kwenye awamu ya pili ya vikao vya Bunge Maalumu la Katiba.

Matokeo na Ripoti Nzima ya Mchezo wa Tanzania vs Msumbiji hii Hapa

$
0
0
HATIMAYE safari ya timu ya Taifa ya Tanzania, Taifa Stars kuwania tiketi ya kucheza fainali za mataifa ya Africa, AFCON 2015 nchini Morocco amefia mikononi mwa timu ya taifa ya Msumbiji ‘Black Mambas’.
Taifa Stars ikiwa ugenini katika dimba la Taifa la Zimpeto nje kidogo ya jiji la Maputo imetandikwa mabao 2-1 katika mchezo wa marudiano wa kuwania kupangwa hatua ya makundi ya kusaka tiketi ya AFCON mwakani.
Katika Mechi ya kwanza iliyopigwa wiki mbili zilizopita jijini Dar es salaam, vijana wa Mholanzi, Mart Nooij walitoka sare ya mabao 2-2 na leo hii walihitaji kupata ushindi wa aina yoyote ile au sare ya kuanzia mabao 3-3.
Matokeo ya jumla baada ya mechi mbili, Msumbiji wamefanikiwa kufunga mabao 4 na Taifa stars matatu, hivyo vijana wa Nooij kutupwa nje ya michuano kwa wastani wa mabao 4-3.
Msumbiji walikuwa wa kwanza kuandika bao la kuongoza dakika za mwisho za kipindi cha kwanza kupitia kwa Josimar Tiago Machaisse, lakini Mbwana Ally Samatta akaisawazishia Stars katika dakika ya 77.
Dakika ya 83, kiungo mshambuliaji wa Msumbiji, mzoefu, mwenye ujanja mwingi wa kupiga chenga na kumiliki mpira, Elias Gasper Pelembe aliifungia ‘Domingues’ Msumbiji bao la pili na la ushindi.
Kihistoria Msumbuji wamemekuwa wababe wa Taifa Stars inapofika michezo ya mtoano, hasa kufuzu mataifa ya Afrika.
Mwaka 2007 Stars chini ya kocha Mbrazil, Marcio Maximo ilifungwa bao 1-0 katika mchezo wa mwisho jijini Dar es salaam kuwania kucheza fainali za mataifa ya Afrika mwaka 2008 nchini Ghana na ingeshinda ingefuzu.
Bao pekee la Msumbiji lilifungwa dakika ya za mapema kipindi cha kwanza na aliyekuwa nahodha wake, Tiko Tiko akiunganisha kwa kichwa krosi nzuri iliyochongwa kutoka winga ya kulia na Elias Pelembe.
Mwaka 2012 Taifa stars ilitolewa tena na Msumbiji kwa changamoto ya mikwaju ya penati katika mchezo wa kuwania kucheza fainali za kucheza fainali za mataifa ya Afrika mwaka 2013 nchini Afrika kusini.
Hatua hii ilifikia baada ya timu hizo kutoka sare ya bao 1-1 jijini Dar es salaam na kupata matokeo kama hayo mjini Maputo.
Kwahiyo Msumbiji bado wameendelea kuwa wababe wa Tanzania katika michezo ya mtoano.
Poleni sana Taifa Stars, Poleni Watanzania wote. Mipango mipya inatakiwa kuwekwa.
Source:shaffihdauda.com

Ali Kiba Atoa ya Moyoni 'Lulu Michael Anafaa Kuwa Mke'

$
0
0
Stori: Erick Evarist na Sifael Paul
HII ni exclusive! Kwa mara ya kwanza, staa anayeitikisa nchi kwa sasa na wimbo wake wa Mwana, Ali Kiba amefunguka kuwa mwigizaji kiwango Bongo, Elizabeth Michael Kimemeta ‘Lulu’ anafaa kuwa mke (wife material) huku akiweka wazi sifa kibao alizonazo, Wikienda liko bize kukujuza.

Kiba ambaye hivi karibuni ameibua mijadala mingi katika mitandao ya kijamii, usafiri wa umma na kwenye baa juu ya ujio wake mpya akisemekana kurudia kiti chake ambacho alikikalia Mbongo Fleva, Abdul Nasibu ‘Diamond’ kwa muda, mwaka 2010 aliwahi kuripotiwa katika magazeti pendwa kwamba ana uhusiano wa kimapenzi na Lulu ambaye wakati huo alikuwa na umri chini ya miaka 18!

LULU ANAFAA KUWA MKE
Akizungumza mbele ya kinasa sauti cha Globa TV Online, Bamaga-Mwenge jijini Dar mwishoni mwa wiki iliyopita, Kiba ambaye anatarajia kuangusha shoo ya kihistoria Agosti 8, mwaka huu katika Tamasha la Usiku wa Matumaini kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar, alisema Lulu anafaa kuwa mke kwa vile ni mchapakazi sifa ambayo mke mwema anapaswa kuwa nayo.

AMMWAGIA SIFA
Kiba alisema Lulu anajua kuhangaika, anajua kupambana kusaka pato lake kihalali kupitia mauzo ya sinema zake anazozizalisha kitu ambacho kinawashinda mabinti wengi na kuangukia katika biashara ya kuuza miili (ukahaba).

Licha ya kummwagia sifa hizo, kipindi hicho alichokuwa akitajwa kuwa naye, Lulu alikuwa na matukio ambayo hayakuwa na maadili lakini Kiba hayo hakuyatilia maanani. 
Mwandishi: Unafikiri Lulu ni ‘wife material’ (mke mwema) ambaye unaweza kumweka ndani akalea watoto na kuijenga familia bora?

Kiba: Yeah! Anafaa kuwa mke, ni binti anayejituma, mchapakazi, mtafutaji. Kwangu mimi mtu wa namna hiyo ndiyo anafaa kuwa mke.
Mwandishi: So, unataka kutuambia kwamba unaweza kumuoa?
Kiba: Sijasema hivyo mimi, nimesema anafaa kuwa mke.

ACHOMOA KUBANWA KISHERIA
Licha ya kuchomoa ishu hiyo ya uhusiano, mapaparazi wetu walimbana zaidi staa huyo afafanue kwa nini alitajwa yeye na si msanii mwingine huku ikidaiwa kuwa, Lulu hakuwa ametimiza miaka 18 hivyo kubanwa kisheria (ya watoto na kujamiiana).
“Sijatembea naye ndiyo maana unaona hata sheria haijanihukumu, endapo ningekuwa nimetembea naye, basi sheria ingeweza kunitia hatiani na ningefungwa jela,” alifafanua Kiba.

AWASHANGAA WANAOMSHANGAA 
Kiba aliongeza kuwa, anashangaa sana kuona watu wanamsema vibaya yeye kupendwa na Lulu.
“Lulu ni msanii mwenzangu, anapenda kazi zangu na mimi napenda za kwake. Ni rafiki wa kawaida, hakuna kitu kingine cha ziada. Nawashangaa wanaozusha ya kuzusha, hivi kwani kuna tatizo Lulu akinipenda? Sidhani kama ni kosa, ana haki ya kunipenda kutokana na muziki wangu.

“Unajua muziki mzuri huwa unapenya automatically, huwezi kuzuia hisia za muziki, mtu unaweza ukawa humpendi msanii f’lani lakini ukapenda muziki wake, unajikuta tu unampenda, unaanza kuimba nyimbo zake,” alisema Kiba.

KUMBUKUMBU MBICHI
Juzikati wakati Kiba anatambulisha nyimbo zake mbili kwa mpigo (Mwana na Kimasomaso), Lulu, kupitia mtandao wa Instagram alitupia maneno ya kummwagia sifa staa huyo, liliibuka kundi ambalo linatajwa kuwa ni wafuasi wa mwigizaji Wema Sepetu ‘Team Wema’ na kuanza kumshambulia kwa maneno machafu.

KIBA AFUNGUKA
Akizungumzia ishu hiyo, Kiba alisema waliofanya hivyo hawakumtendea haki Lulu kwani ana haki ya kueleza hisia zake pale anapoguswa na muziki mzuri.
“Hawajatenda haki kwa sababu Lulu ni binadamu kama walivyo wengine, ana haki ya kupenda kitu kizuri,” alisema Kiba.

KUHUSU KIFO CHA KANUMBA
Kiba akizungumzia juu ya kuhusishwa na kifo cha aliyekuwa nyota wa sinema Bongo, marehemu Steven Kanumba ambapo alidaiwa kunaswa kwa meseji za mapenzi alizozituma kwa Lulu ndiyo zilizosababisha mtifuano ambao ulisababisha kifo cha Kanumba, alikana madai hayo.

“Si kweli, sikuwa nimewasiliana na Lulu siku hiyo kabla ya tukio. Nakumbuka nilikuwa safarini, baada ya tukio nilimpigia Lulu kutaka kujua ukweli wa taarifa za kifo kwa sababu marehemu alikuwa mtu wangu  wa karibu kama alivyo Lulu,” alisema Kiba.

AMGUSIA WOLPER
Kwenye mahojiano hayo, mkali huyo alizungumzia ishu ya mwigizaji, Jacqueline Wolper kukiri kwamba Kiba ndiye mwanaume aliyemtoa usichana wake kwenye simulizi iliyochapishwa katika Gazeti la Championi hivi karibuni.

“Mh! Aliwahi kukiri? Daah! Sijui bwana… Wolper ni mtu wangu wa karibu kama alivyo Lulu,” alisema kwa mkato Kiba.Juzi, Lulu alitafutwa na mapaparazi wetu ili  azungumzie ukaribu wake na Kiba, lakini simu yake muda mwingi iliita bila kupokelewa (tunaamini atasoma hapa, tunaendelea kumtafuta ili afunguke).
Viewing all 104709 articles
Browse latest View live




Latest Images