Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104690 articles
Browse latest View live

Ukijaliwa Kuwa Msichana Mzuri na Mrembo Usidhani Kamwe Utatetemesha Kila Mwanaume

$
0
0

Ukijaliwa kuwa Msichana mzuri na mrembo,usidhani utatetemesha kila Mwanaume, kuna wanaume na akili zao kichwani,urembo wako hauwasumbui kama bichwa lako ni kanyaboya,uzuri wako hausaidii kitu,na utashangaa no one is paying attention,watu utakaowapata ni walewale kanyaboya wenzako, na hawana futuretabaki unaliwa bure kila siku unatoa macho.

Ukipata mwanaume anakupenda unaanza drama zako na kupiga watu danadana,madai yako hujali na unadhani hata akiondoka utapata mwingine kisa wewe ni mzuri, la hasha Mwanaume akijitoa mhanga kukupenda kwa uzuri wako mheshimu,maana viumbe wa kike wakiwa wazuri ni shida na matatizo hakuna mtu anataka,sasa ukimwongezea na drama pamoja na yeye kujigeuza mpalestina kwako utajikuta umeolewa na kioo cha chumbani kwako,maana hicho ndo kinakudanganya sana kwamba we ni mrembo.

Watch out drama zina mwisho, leo unacheza na mioyo ya watu unajiona we kifaa usidhani wanaume hawaumii, tunaumia
sema hatusemi tu,machozi yetu kama ya samaki.

Unamkataa Mtu Halafu Unamtangaza Chuo Kizima au Ofisi Yote Hadi Walinzi Wanajua

$
0
0

Kuna watu wa ajabu sana.
Anatokea mtu anaweza kuwa mwanamke au mwanaume kuomba mahusioni ya kimapenzi kwa mwingine.

Sana sana kwenye jumuia mfano chuo,maofisini na ata kwenye viwanda mahali ambapo watu wanakutana mara kwa mara.

Mtu amekutungoza umemkataa au amekukuta tayar una mtu unaishi nae kuna sababu gan kumtangaza kwa watu wote kua fulan nimemkataa.

Kinachokufanya kila mtu
kumwambie kua umekataa mtu fulani nini?
Ili uonekana unatafutwa sana na watu au mzuri sana.

Ukimkataa mtu na yeye akikuelewa basi hakuna sababu yakutangaza chuo kizima au ofisi yote adi walinzi wajue.

Wenye tabia hii acheni Mara moja.

Nimetembea Na ‘house Girl’ Wangu Na Sasa Ana Mimba

$
0
0
Naitwa baba Zai wa Buguruni Dar, nimeoa na tumebahatika kupata mtoto mmoja. Kutokana na mke wangu kuwa anafanya kazi, tulilazimika kutafuta mfanyakazi wa ndani.

Mke wangu amekuwa akirudi kutoka kazini usiku sana na mimi huwa narudi nyumbani saa nane mchana. Nimejikuta muda mwingi nakuwa na mwanangu na ‘hausi geli’ tu ambapo mke wangu tumekuwa tukiwa na muda mzuri wa kuvinjari siku moja tu kwa wiki.

Nisiwafishe ‘hausi geli’ huyu alitokea kunipagawisha kutokana na umbile lake, sijui ni tamaa au nini lakini nikajikuta nimezama katika dimbwi la mahaba kiasi cha kufikia hatua ya kumchukulia kama mke wangu kwasababu huduma nyingi alikuwa akinipatia.

Kinachonipa wakati mgumu sasa ni kwamba, mke wangu anahisi kuwa natembea na huyu mfanyakazi wangu na kwamba ikibaini hivyo kwa ndugu jamaa na marafiki itakuwa ni aibu. Mbaya zaidi ‘hausi geli’ huyo sasa anadai ana mimba yangu. Hebu naomba unishari nifanye?

Acha Kusingiziwa singiziwa Mimba..Fahamu Jinsi ya Kutambua Siku za Hatari za Mpenzi za Kubeba Ujauzito..!!!

$
0
0
Moja ya makala zilizopita niliwahi kuongelea namna ya kupata mtoto wa kiume na jinsi ya kujua siku za mwanamke za hatari za kubeba mimba ni zipi lakini watu wengi wamekua wakinipigia simu kwamba hawakuelewa.

Siku za hatari za mwanamke ni zipi?
Hizi ni siku ambazo mwanamke akishiriki ngono bila kutumia kinga anapata ujauzito bila wasiwasi wowote labda kama ana matatizo yanayomfanya asibebe mimba au mwanaume wake ana matatizo.

Utazijuaje siku hizo?
Kwanza kabisa ili ujue siku zako za hatari lazima ujue idadi ya siku za mzunguko wako. Kuna aina tatu za mzunguko.. mzunguko mrefu ambao unachukua siku 35, mzunguko mfupi unaochukua siku 25 na ule wa kawaida unaochukua siku 28 na ndio mzunguko ambao watu wengi wanao.

Unajuaje mzunguko wako?
Hesabu siku tangu siku ile ya kwanza uliyoona siku zako za hedhi mpaka siku moja kabla ya kuona siku zako za hedhi zinazofuata. Unashauriwa uchukue miezi mitatu mpaka  sita ukihesabu ili ue na uhakika kwamba mzunguko wa tarehe zako haubadiliki, kama umeshahesabu siku za nyuma kabla ya kusoma makala hii ni vizuri pia. Mfano umeanza kuona siku zako tarehe moja mwezi wa nne alafu ziko zako zingine ukaziona tarehe 29 mwezi wa nne, chukua 29 toa 1 utapata 28.. maana yake wewe unamzunguko wa siku 28.

Je siku za hatari ni zipi? 
siku ya hatari ni siku ya 14 kabla ya kuona hedhi inayofuata na sio siku ya 14 baada ya kuona hedhi iliyopita na hapa ndio watu wengi wanachanganya na kupata mimba.

Mfano kama mzunguko wako ni siku wa kawaida siku  28, chukua 28 toa 14 utapata 14. Hivyo siku yako ya hatari ni siku ya 14, lakini kwa kua mbegu ya kiume inaweza kuishi mpaka siku tano na yai la kike linaweza kuishi mpaka masaa 24 ndani ya mfuko wa uzazi basi siku nne kabla na siku moja baada ya siku ya 14 ni hatari hivyo siku za hatari ni ni siku ya 10,11,12,13,14 na 15.

Kama mzunguko wako ni mrefu labda  siku 36 basi chukua 36 toa 14 utapata 22. Hivyo siku ya 22 ni hatari na zingine ni 18,19,20,21,22 na 23.

Kama mzunguko wako ni mfupi, mfano mzunguko wa siku 21, sasa ukichukua 21 ukatoa 14 unapata 7 yaani siku ya saba ni siku yai linashuka hivyo ni hatari kwa huyu mtu.hivyo siku zingine za hatari ni 3,4,5,6,7[mtoto wa kiume] na 8.

kama mzunguko wako ni  wa kawaida yaani siku 28 sasa chukua 28 toa 14 unapata 14 yaani siku ya 14 ndio hatari zingine ni siku ya 10,11,12,13,14,15


Dalili kwamba uko kwenye siku za hatari ni zipi?

Kuongezeka kwa joto kidogo, tumbo kuuma kidogo, na ute mweupe kutoka sehemu za siri..

mwisho: maelezo hayo hapo juu yanaweza kusaidia kupanga uzazi, kuchagua jinsia ya mtoto au kutafuta mtoto. Lakini pia tarehe zote nilizoweka mabano ambazo ndio tarehe yai linashuka  ndio za mtoto wa kiume zingine zote zilizobaki ni za watoto wa kike. kwa lugha ya kingereza soma hapa

Dawa Bora za Nguvu za Kiume na Kukosa Hamu ya Tendo la Ndoa

$
0
0

DAWA BORA ZA NGUVU ZA KIUME NA KUKOSA HAMU YA TENDO LA NDOA
Baada ya utafiti wa muda mrefu juu ya matatinzo ya upungufu wa nguvu za kiume na ukosaji wa hamu ya tendo la ndoa ama kushindwa kurundia tendo kwa haraka Sasa inakuletea suluhisho juu ya matatizo haya kwa kutumia dawa za FULL POWER

Full Power dawa asili yenye vidonge inayotibu tatizo la upungufu au ukosefu wa nguvu za kiume dawa hii inamchanganyiko wa kutosha kuzalisha vichocheo vingi vya hernone za gestro gen zikiwemo vitamin b6 na b1 vitamin e pamoja na madini aina ya zinc

Itakufanya kuwa na nguvu na mzunguko mzuri wa damu na kuongeza hamu na uwezo wakufanya tendo la ndoa zaidi hatua nne au zaidi na kuchelewa kufika kileleni zaidi ya dakika 20/30 ZAT 50

Inarundisha maumbile ya uume yaani kurefusha na kunenepesha nchi 3/7 na upana cm 3/4 standard.kiafya haijalishi umri wako hata kwa wazee ukitumia maumbile yatabaki kuwa hivyo siku zote pia anatibu matatizo mengine kama presha kisukari ngiri chango la tumbo kujaa gesi kutopata choo vizuri minguu kuwaka moto matatizo ya uzazi bawasili na magonjwa ya zinaa kama kisonono na kaswende

Tunapatikana Dar es Salaam  na mikoan wasiliana na DR Oshinda no 0755505099 au 0714126118  Karibuni kwa hunduma bora

Makala:Kingunge Mwitikadi wa Mwisho Ameondoka...

$
0
0
Mzee Kingunge Ngombale Mwiru na mkewe, Mama Peras Kingunge enzi za ujana wao. Mzee Kingunge aliyekuwa mtumishi wa umma kwa zaidi ya miaka 50 amefariki dunia alfajiri ya Februari 2, 2018 akitanguliwa na Mama Peras aliyefariki Januari 4, 2018. Picha kwa hisani ya Familia ya Kingunge Ngombale Mwiru



Miaka michache iliopita, wakati somo wangu katika uandishi wa habari, hayati C. Stanley Kamana, alipofariki dunia, mmoja wa maswahiba wake, James Shani Mpinga, aliandika taazia kwa lugha ya Kiingereza aloipa jina “The Last Sub is no More”.

Neno sub hapo ni kifupisho cha neno sub editor. Katika vyumba vya habari, sub editor ni mtu muhimu maana yeye ndiye anayepitia habari na kuifanyia kazi kikamilifu kabla ya kwenda mtamboni.

Mpinga aliamini kwamba Kamana hakuwa na mfanowe katika eneo hilo hapa nchini. Wakati nataka kuandika kuhusu mzee Kingunge, nimekumbuka kuhusu kichwa cha habari cha Mpinga.

Nataka kusema mzee Kingunge pengine ndiye mwitikadi (Ideologue) wa aina yake wa mwisho kuwepo hapa Tanzania. Hakutakuwa na mwingine kama yeye. Na hatujawahi kuwa naye kabla yake.

Lakini, mwitikadi ni nani?

Mwitikadi ni tafsiri ya lugha ya Kiswahili ya neno lenye asili ya Kifaransa-IDEOLOGUE. Neno hili wala halikuwepo kwenye kamusi ya Kifaransa hadi kwenye karne ya 19. Ni neno jipya.

Hata hivyo, unaweza kulichambua pia katika Kiyunani na ukapata maneno mawili tofauti; Ideo-Hoja, Mawazo na Logos-usomi, uchambuzi.

Kwenye Kiswahili cha kawaida, unaweza kusema ideology ni somo la uchambuzi wa hoja kisayansi na mwitikadi ndiye hasa mtu anayefanya kazi hiyo.

Huyu ni mtu ambaye anayaweka maisha yake ya kisiasa katika kusoma na kubungua bongo yake kwa maslahi ya chama chake na taifa.

Mwenyekiti Mao alijua umuhimu wa kundi la waitikadi ndani ya chama na ndiye aliyekuwa mwanasiasa wa kwanza kuweka mgawanyo huu wa dhahiri kati ya watendaji na waitikadi.

Kazi ya waitikadi ni kusambaza sera na kutoa mwelekeo wa chama. Hawa si watu wa kuwapa mashirika waongoze au kuwa marais. Hawa ni watu wa kutoa miongozo. Kufikiri.

Chama cha Kikomunisti cha China kilikuwa na Lin Biao huku kile cha Urusi kikiwa na Leon Trotsky na baadaye Susilov.

Chama cha Congress cha Milton Obote wa Uganda kilikuwa na Yoga Adholu ambaye yu hai hadi leo.

Kwenye siku zake za mwisho wa utumishi, watu walikuwa wanahoji hivi huyu Kingunge amefanya lipi hasa maana? Walidhani kipimo cha utendaji wa gwiji huyu ni idadi ya majipu alotumbua, wahujumu uchumi aliowakama au miradi aloileta.

Hasha. Mwitikadi anapimwa kwa kukiweka chama chake madarakani, kwa kutengeneza wanasiasa wapya na kwa kuleta mawazo mapya.

Akiwa Mjamaa kindakindaki, Kingunge aliweza kukaa kwenye kamati moja ya mabepari maarufu kama Reginald Mengi na Iddi Simba kutengeneza mwelekeo wa sera mpya za CCM.

Kingunge alikubaliana na mawazo ya watu wenye mtazamo tofauti kama yakiwa na msingi.

Hii ni kwa sababu, kwa mwitikadi, jambo la msingi ni namna mchakato wa hoja ulivyoenda hadi kufikia kwenye uamuzi wa mwisho.

Bahati mbaya ya kizazi chetu ni kwamba waitikadi hawaonekani kuwa wa maana tena. Vyama vimetelekeza utaratibu wa kutengeneza vijana wa kuwa kama akina Kingunge.

Mzee Ngombale hakuibuka tu kama uyoga, kama ilivyokuwa kwa akina Biao, Susilov na Adholu. Watu wa namna hii wanatengenezwa.

Tatizo ni kwamba siku hizi kila kitu ni fasta fasta. Hata ubunge umekuwa ni wa fasta fasta tu. Manake leo mbunge wa Chadema au CUF anahamia CCM na kuwania ubunge bila kupitia mchakato wa kuivishwa kwenye itikadi.

Mwaka juzi, yupo mgombea wa upinzani aliyepanda jukwaani na kusema CCM Hoyee.

Nasubiri kusikia mgombea wa CCM Kinondoni akiwasalimu wananchi kwa kuwaambia Hakii!!!

Hakuna tena itikadi. Ni shaghalabahala. Pengine ndiyo maana Mwenyezi Mungu kaamua kumchukua mzee wa watu.

Pumzika kwa im

Le Mutuz: Historia ya Kweli Juu ya Maisha Yangu, My American Experience

$
0
0
Copy and Paste from lemutuz PART 1

safari yangu ya USA ulikua ni uamuzi wangu mgumu wa kuacha Ubaharia nikiwa Melini "MV. Luxemburg"ICMB Belgian Shipping Line tukiwa South China Sea tunatokea Shanghai/China tunarudi Singapore kazi yangu Melini nilikuwa Assistant Engineer au 0fisa wa Meli ndani ya Meli.

maisha ni kwa grade and class Maofisa mnaishi sehemu maalum na mnakula sehemu maalum na mna hang out sehemu maalum sheria za Meli hamtakiwi kuchanganyikana na Crew yaani Mabaharia wa kawaida infact hata Chakula ni tofauti Maofisa mnakula vizuri sana kuliko Mabaharia ...


l was a lucky man cause nilikuwa i ninasama Chuo Kikuu Cha Ubaharia Zeeman Marine Engineering College/Antwerpen, Belgium ambako nilijiunga nacho Miaka 4 na huu ulikua Mwaka wa Tano ninamalizia Leseni ya Uinjinia wa Meli ambayo ni Equivalent to Degree cause Melini zamani hakukuwa na Degree ila Leseni Only na Masomo ya Meli ni kila Miezi 6 Darasani na Miezi 6 unasafiri kufanya kazi Melini so by Mwaka wa Tano nilikuwa Baharia wa Ukweli nimetumia like 3 Years Baharini ambayo Practically katika Ubaharia inaitwa "SEA TIME" ambayo inaheshimika sana unapoamua kuomba kazi mpya ya Ubaharia Kampuni nyingine ndani ya Meli.


nilikuwa na Bosi wangu Engineer Feyerick Mzee aliyekuwa anavuta Cuban Cigar all the times binafsi nilikua sinywi Pombe wala kuvuta sigara hii ilinifanya kuwa Baharia maarufu sana ndani ya ile Melicause kila ljumaa tulikuwa tunapewa mgao wa Meli Katoni 5 za Beer, Katoni 2 za Sigara na Chupa 2 za Pombe Kali bure mimi nilikuwa always nabadilishana na Maofisa wengine wao wananipa Juice na Soda ...


Mzee Feyerick alikuwa na tabia ya kukaa chini na kunipa darasakuhusu Maisha nilikua kijana mdogo sana infact nilikuwa nimeichezea Miaka yangu kwenye makaratasi nikisaidiwa sana na Mwili Mkubwa lakini hata hivyo sura yangu ilikua inani betray always kuwa ni mdogo so nilikuwa natembea na Kitambulisho all the times ...

kama kawaida Mzee Feyerick my Bosi wa Engine Roomalinikumbusha sana kwamba Kijana mdogo achana na hii kazi ya Ubaharia haikufai i Nchi Kavu kasome utafute maisha bora ya kisasa", maneno mazito yalinigusa sana ..........ITAENDELEA PART 2..! From le Mutuz


Copy and Paste from lemutuz PART 2

my Boss Mbelgiji Feyerick alikua ananiambia the bitter truth kua niachane na mambo ya Meli akaniambia "Hii ni kazi ya Wazee na watu wasiokuwa na Maisha sio kwa kijana kama wewe" in all my childhood


nilikuwa naulilia Ubaharia nilianza nikiwa Jamhuri Primary School nilipokutana na "MABAHARIA WA NCHI KAVU" yaani Wanafunzi wenzangu Darasani kina Juma Jagan Burr (now in Canada) na Marehemu Raja Kaka hawa ndio Wanafunzi 2 walionipa the idea ya Ubaharia cause walikuwa na ndugu Mabaharia ambao walikuwa wakiwasaliana nao sana kutoka Nje l was in yaani "BAHARIA NCHI KAVU" Baba yangu mzazi then alikuwa Waziri wa Kilimo he was stunned kusikia kua nina mawazo ya kua Baharia alianza kusikia kutoka kwa marafiki zake ambao nilikuwa nawasumbua sana


kwa pembeni wanisaidie na ndato yangu nikimaliza tu Darasa la Saba they were all shocked that nitakuwaje Baharia at darasa la Saba tu? Baba yangu siku moja akanikalisha chini na akaniambia kuwa nisahau mambo ya Ubaharia its not for me settle kisaikolojia kuwa siwezi kuwa Baharia Darasa la Saba so nilichaguliwa kusoma Sekondari nikaendelea na masomo isipokuwa nikaanza Biashara ya kuuza Siagi


nikishirikiana na Rafiki yangu aliyenifundisha biashara hii Marehemu Koi Margai Mungu Amuweke Pema Peponi kila Jumamosi tunaruka na ndege ya Air Tanzania mpaka Musoma tunanunua siagi Kiwanda Cha Maziwa Musoma na kuirudisha Dar kuwauzia Wahindi tu hii mitaa ninayoshi sasa ndio maana ninawafahamu sana


mpaka leo kwenye kila safari tulikua tunapata faida ya at least Tsh, 20,000 wakati huo USD 1 ilikuwa Tsh, 10 tu nauli ya ndege kwenda Musoma na kurudi Dar ilikua Tsh, 950 tu Cargo tunalipia like Tsh. 3,000 kuileta Siagi kwa ndege na pia nikaingia biashara ya kuuza Dola za Kimarekani mtaani kwa bei ya ujanja.


officially nikawa a "MIDLLEMAN" mtu wa kati yaani mtu ukitaka kuuza anything hapa mjini ninakuuzia unanipa Kamisheni na Ninayemuuzia naye ananipa cha Juu Double kamisheni by the time namaliza High School nilikuwa na karibu Tsh. 1M Cash na USD 10,000 Cash Money nikaanza mipango ya kwenda Majuu ..ITAENDELEA PART 3 from lemutuz


opy and Pest from lemutuz PART 3

by the time nimefika Form Two I was a Super Street Smart nikaamua kuanza kuishi mwenyewe nikapata Studio Chumba kikubwa pale YMCA! pembeni ya Holidays In Hotel Downtown so nikahama kutokea lkulu kwa my Uncle Balozi Lusinde ambaye then alikuwa Waziri wa Mawasiliano


tulikuwa tunaishi nyumba ambayo sasa ni ofisi ya TAMWA tulikuwa kati kati ya Waziri wa Habari Marehemu Mwakawago na Waziri Mkuu Marehemu Kawawa na mabele yetu ni nyumba za Waziri wa Sheria Bomani na Waziri wa Fedha Jamal sijasahau mpaka leo the Good Life and the Bad life niliyoishi utotoni.

but all and all it was a good life after YMCA nilihamia Sido Hostel kati kati ya CBE na Maktaba ya Taifa hapa Kisutu Downtown so ni FACT that I have lived in Downtown almost all my life mpaka leo bado nipo Downtown


baada tu ya kumaliza Shule nikaenda JKT 0ljoro Arusha Mwaka mmoja kwa mujibu wa Sheria l was a Soccer Star na nilikuwa na Vijisenti so kila siku nilikuwa Dar naendelea na biashara zangu huku nipo JKT hahahaha nikirudi Camp nawapiga Chai Maafande no problem na nikicheza Soka timu ya Kikosi ninafunga magoli hakuna kelele za kwa nini sionekani Kambini...


wazo langu lilikuwa kwenda kutafuta Ubaharia lakini wa kusomea Shule 30 nika settle na idea ya kwenda Belgium Bongo enzi hizo ilikua huwezi kununua tiketi ya ndege kwa pesa za Tanzania mpaka uwe na kibali maalum kutoka kwa Gavana wa BOT wakati alikuwa Marehemu Nyirabu so nikaenda kuomba kumuona ofisini kwake kwa kisiingizo cha mtoto wa Waziri

nikaruhusiwa nukamuona lakini nikawa naomba Mungu asimpigie Baba yangu kumuuliza kama ameniruhusu so nilipokaa naye uso kwa uso nikaanza kumpiga porojo ili kumfanya asikumbuke a Baba yangu akaanza kucheka sana kufumba na kufumbua alishanipa Kibali cha kununua tiketi ya ndege kwa hela za Tanzania wakati huo USD 1ilikua Tsh. 16 na risiti ninazo mpaka leo

akaniambia niende kwa Mama Kimbe mama mzazi wa my Friend Matare Joseph Nyerere aliyekua 0fisa wa BOT ndiye aliyenimalizia paper work zote za kibali nikaenda Sabena Airways pale Samora Avenue ambapo sasa ni NHC Bulding nililipa Tsh. 120,000 nauli ya return to Brussels/ Dar itaendelea....PART 4!

PART 4: "MY AMERICAN EXPERIENCE"

Niliamua kuonana na Captain na kumfahamisha kua nimemua kuacha kazi ya Ubaharia for Good tukiwa njiani kutoka Shanghai/China to Singapore sheria za Meli ni Baharia akisema ameamua kushuka Meli hakuna mjadala so Captain akamfahamisha Agent wa Meli Nchi kavu aliyenipokea tulipofika tu na kunipeleka Five Star Furama Hotel ambapo nilipewa mapumziko ya siku 5 kabla ya kuruka na Singapore Airlines to Bombay niliko connect na Ethiopian Airlines to Bongo ambapo nilikaa miezi 2 na kuruka tena

...KWANINI NILIACHA UBAHARIA? baada ya kukaa Baharini niligundua kuwa maisha ya Baharini yalikuwa ni madogo sana honestly no life na sikujua kua Binadam ukikaa wiki nzima unaona maji tu bila nchi kavu akili zinacheza kidogo na all and all nikagundua Mabaharia wanaorudi Bongo walikuwa na mbwembwe nyingi ambazo ni uncalled and unfounded for as opposed na uhalisia na ugumu wa kazi na maisha ya Baharini waliyoyaishi ...sawa kulikuwa na pesa ambazo ukijinyima zinakuwa nyingi ila tatizo ni matumizi yake hasa baada ya kupewa hela nyingi kwa wakati mmoja so binafsi nina conclude my mission at Ubaharia as an adventure ya kupanuka Akili na Kusafiri almost Robo tatu ya Dunia ...

THE BERMUDA TRIANGLE ni safari za Meli kutoka Europe kwenda Brazili au Latin America ni sehemu ya baharini ya hatari sana that Kampuni ya Meli inakupa option ya kubadilisha Meli ili usiende na ukiamua kwenda unalipwa Mshahara mara 2 ya kawaida binafsi niliwahi kupita mara 3 huwezi kua a Real Seamen kama hujapita hapo na Meli ...

Ni kwamba Meli ikifika hapo tu inachukuliwa na Maji ambayo yanazunguka kwa kasi kubwa sana na kuifanya Meli kupoteza Control na kuishia kuwa Controlled na Maji sasa mnakuwa mnaelea tu na ni Maji yenye uamuzi mzunguke kwa siku ngapi kwa kawaida hua ni siku 3 mpaka 5 then one day Maji yanawaachia mnaondoka but kivumbi cha kuzungushwa bila kupenda ni balaa na hasa kwenye kulala mnapewa mito maalum na kuipanga pembeni na kulala kati kati kama kwenye jeneza siku 3 au 5 za kukosa usingizi ni hatari sana kwa binadam.... Brussels/Belgium one week nikaruka tena to Montreal/Canada to Ottawa nikachukua basi Greyhound to New York City/USA! ....ITAENDELEA!



PART 5: "MY AMERICAN EXPERIENCE"

Maisha yamenifundisha somo moja muhimu na chungu kwamba "MUNGU HAWEZI KUTUPA BINADAM AMBACHO HATUJAMUOMBA" yaani toka nikiwa mdogo nilikuwa namuomba Mungu just a "COMFORTABLE LIFE" kumbe sijawahi kumuomba niwe "SUPER BILIONEA" ndio maana sijawa cause kwa njia za safari ya maisha yangu nilimopitia nilitakiwa kuwa by now lakini simlaumu Mungu cause huenda kutokuwa kwangu na mapesa mengi ndio kumenisaidia kuendelea kuishi mpaka leo kwa raha na Amani ya ajabu so ninaendelea kumuomba Mungu aendelee kunipa a Comfortable life yaani maisha ya kula vizuri na kulala vizuri na pesa kidogo mfukoni na kufanya lolote ninalotaka ambalo lipo chini ya uwezo wangu kama kusafiri popote Duniani kwa ndege na kukaa Mahoteli mazuri ya kisasa I love that.

Niligundua siku nyingi sana toka nikiwa mdogo kwamba I was born different nilizaliwa Mwanaume tofauti sana Mama yangu mzazi na Mama yangu wa Kambo originally walikuwa ni marafiki wa damu walioishia kuzidiana Akili na kugeuka kuwa maadui wa Ajabu na mimi nikawa caught up in the middle ya Uadui wao na the worst is Mama yangu wa Kambo was very educated as opposed na Mama yangu Mzazi ingawa wote leo ni Marehemu lakini kivuli cha Vita yao ninapigana nacho mpaka leo na ndipo Mange anapoingia in my picture cause ni agent tu wa hicho kivuli cha Shetani anayenisumbua toka utotoni kutokana na Vita kali ya Urithi wa Mali za Baba yangu ni Vita ya ajabu na ya kitoto sana inayowahusisha watu wengi mpaka waliosoma lakini wamefunikwa na Chuki dhidi yangu ambayo ni purerly Foolish and unfounded just UNCALLED FOR ....

Mange alianza rasmi kunishambulia baada ya kurudi Bongo Miaka 6 iliyopita alianzia Facebook na mashambulizi ya yake ya kwanza aliongelea urithi wa Baba yangu kwamba nimerudi Bongo kutafuta urithi ninayo quote yake mpaka leo so I hope nimewasaidia wale mnaojiuliza sana Chuki ya Mange kwangu inatokea wapi? ni kwamba Mange anawawakilisha baadhi ya Maadui zangu wa Maisha ambao wangependa kusikia nimekufa kwa sababu wana wasi wasi kua nitawadhulumu urithi wa Baba yetu ambaye bado yupo hai na huenda hata tukaondoka sisi tukamuacha ....hahahahha....there I was ndani Basi Greyhound to New York City/USA...ITAENDELEA


PART 6:- "MY AMERICAN EXPERIENCE" ...

Ndani ya Basi la Greyhound kutoka Ottawa/Canada tunaelekea New York City/USA nilikuwa ninawaza nitakapofika New York City itakuwaje? Simjui mtu so sitakuwa na mahali pa kulala JE ITAKUWAJE? but nikajikumbusha jinsi nilivyokwenda Belgium mara ya kwanza Miaka 5 nyuma so ghafla tukafika Border kama kawaida ya Uhamiaji ya USA wakishaona Passport yako inaonyesha uliwahi kuingia USA na kutoka huwa hawana tatizo na wakati huu Rais wa USA alikuwa ni President Ronald Reagan baada ya kugongewa mhuri wa kuingia nikalala usingizi mpaka Saa Nne Usiku tulikuwa tayari tupo Port Authority, West Manhattan New York City/USA mtaa wa West 42ND Street ambapo ndio mwisho wa Mabasi yote ya Mikoani yanayoingia New York City....

Kuna Mbongo mshikaji wangu nilikuwa na namba yake ya simu aliahidi kuja kunipokea lakini dakika ya mwisho HAKUJA nikashuka na begi langu dogo la nguo kama kawa nikakuta Ma Homeless kibao wanajitayarisha kulala so nikatafuta mahali saafi nikatoa Blanketi langu cause ilikuwa ni Winter time January so kulala ni kwenye masofa ya Abiria wanaposubiria mabasi ya Usiku na Asubuhi so na mimi nikawa kama Abiria ninayesubiri Basi ilinichukua miezi 3 ya Beach life kama tunavyoita kwenye Ubaharia ...

Mwishoni tu mwa wiki ya kwanza nikawa nimepata kazi Dukani as a "STOCK PERSON" kwa Mshahara wa USD $ 5 kwa saa so kwa masaa 40 kwa Wiki nilikuwa ninalipwa USD $ 200 per Week so nikaamua kukusanya pesa kwanza kwa kuendelea kukaa bure pale Stendi ya Basi ...nikiwa kazini Dukani I was charming Kiingereza cha Kimarekani ni tofauti na cha Dunia nzima so to Americans I mean wateja wa Duka nilikuwa bonge la kichekesho na English yangu ya Europe sikuwa muoga kuongea huku nikiendelea kua kichekesho kwa Wateja hasa Wakina Mama pole pole nikaanza urafiki na Wasichana Wakizungu na Weusi cause Duka nililokuwa nafanya kazi lilikua linauza Vifaa vya Nyumbani sana ambavyo Wanawake ndio wateja wakubwa nikaishia kuwa rafiki na Mama mmoja Mzungu aliyeishia kunipeleka kwa mtoto wake aliyekua bosi wa Kiwanda cha Vifaa vya Umeme akanipatia kazi iliyoanza kunilipa USD 10 kwa Saa Moja ...ITAENDELEA!

PART 7: "MY AMERICAN EXPERIENCE"

Baada ya kuanza kazi ya mshahara wa Dola 10 kwa saa sasa nikawa napata Dola 400 kwa Wiki pia nikatafuta kazi ya Usiku kuanzia Saa Sita Usiku mpaka asubuhi Kituo cha Petrol mtaa wa Stanford Boulevard Mt. Vernon baadaye nikaacha nikawa nakaanga kuku KFC Usiku so kwa kazi zote mbili nilikuwa ninapata Dola 550 kwa Wiki ndio nikatafuta Studio ya Dola 100 kwa Wiki nikahamia kwangu sasa kwa mara ya kwanza after 3 Months za kuhangaika na pa kuishi in US maisha yanaenda fasta sana Unafanya kazi mahali Wiki moja then unahamia pengine hivyooo...

Now kazi nilizokuwa ninafanya hazikuhitaji Viza wala Papers cause zilikuwa ni kazi za Wafanya Biashara wanaokwepa kulipa Kodi guys haya mambo ya kukwepa Kodi hata Majuu yapo kwa hiyo walikuwa wananiajiri "Chini ya Meza" kule wanaita "UNDER THE TABLE" yaani unaajiriwa tu kishikaji shikaji ...nikaamua kutafuta kazi ya kunilipa vizuri kusudi nisome Shule always akili na mawazo yangu ndoto zangu zilikiwa ni EDUCATION kwanza cause nilifikiria sana kua nisiposoma nikiwa mdogo sitasoma tena na nilikuwa ninajua kua ndugu zangu wa Mama wa Kambo walikuwa wanasoma wakisukumwa sana na Mama yao aliyekua akitumia all influences za Nafasi ya kazi ya Baba yangu kuhakikisha wanasoma nilikuwa ninajiuliza nisiposoma nitakuwa mgeni wa nani one day? ..

Mungu alinipatia bahati kubwa sana in my life mpaka leo Sijawahi kunywa Pombe wala Kuvuta Sigara so pesa zangu zote nilikua naingiza Benki tu baada ya kulipia kodi ya Chumba cause now nilikua na uhakika wa Dola 2,000 kwa Mwezi Chumba Dola 400 zingine 600 mambo yote mengine na 1000 Benki but likaja tatizo la ID Card huwezi kuishi USA bila kuwa nayo nikajaribu kutafuta New York City ikawa taabu kidogo kuna rafiki yangu Baharia Alex alikuwa anaishi Boston/Massachusets State akaniambia niende kule ni rahisi kupata so nikaomba likizo ya Wiki kazini nikaenda Boston na kupata ID Card I was happy cause now kwa mara ya kwanza I was in the American System maana ID Card inaenda kwenye Databese ya System ya Taifa ..so nikarudi New York City nikaibadili na kuwa ya New York then nikaomba Social Security Card nikapata sasa nikaanza mbio za kusaka Leseni ya kuendesha Gari! ...ITAENDELEA!

PART 8: - "MY AMERICAN EXPERIENCE" ..

Baada ya kupata leseni ya Gari ya kawaida nikaamua kuanza kutafuta leseni kubwa ya kunifanya niendeshe Semi Trailers kazi ambayo ndio ilikua inalipa mshahara mzuri so nikaenda kufanya mtihani wake darasani nikashinda na kupata Kibali cha kuniruhusu kujifunza ili baadaye nikafanye mtihani wa Practical nikishinda niwe Dereva kamili so nikaenda kampuni ya American Harzardous Waste nikaomba kazi ya "UTINGO" ya kuwa msaidizi wa Dreva ili kusudi nipate nafasi ya kujifunza kuendesha nikafanye mtihani wa Leseni niwafanyie kazi Mzungu Jack Supervisor wa Madereva akaniajiri hapo hapo nikaanza rasmi kazi ya Utingo na kazi yangu ilikuwa kusafiri na Dreva na kumsaidia kushusha Makontena ya Harzadous Waste kwa kutumia Hydraulic Lift ambayo imefungwa nyuma ya Truck nilipewa Mzee wa Kijamaica kwa Jina Errol aliyeishia kunisaidia sana kuelekea kupata leseni yangu ...

Now tulikua tunaanza kazi Saa Moja Asubuhi tunatokea Yard The Bronx Market Terminal nyuma ya The Yankee Stadium Bronx tunaingia Manahattan au Brooklyn inategemea kila siku route zilikuwa zinabadilika na kazi yetu ilikuwa ni service kwa Hospitali Kubwa na Ndogo zote it was a fun Job kwanza ilikuwa inanipa nafasi ya kuijua New York City na Vitongoji vyake na pili ilikuwa ni kazi yenye Overtime sana kwani ni almost impossible kuifanya kwa masaa 8 tu kama inavyotakiwa so sasa nikawa na uhakika wa Dola 600 kwa wiki na bado pia nilianza kazi mpya ya kusafisha Jumba la Cinema Co-op City/Bronx ni kazi ambayo nilikua naingia Saa Sita Usiku mpaka Asubuhi ..

Kazi yangu usiku ilikua kusubiri Cinema iishe kuonyeshwa like Saa Sita na Nusu au Saba ninapewa Ukumbi wangu mkubwa mmoja kuusafisha mpaka Asubuhi I was fast nilikua na uwezo wa kusafisha kwa Masaa 2 tu ni kazi ambayo ilikua na changamoto moja kubwa kuondoa Big Gee kwenye Kapeti lakini tulikua tunapewa Special Spray inaondoa mara moja the best of this job was chenji wanazoangusha Watazamaji wa Cinema wakiwa kwenye viti ambavyo vinakua vimepinda ni kazi ambayo nilikua naifanya kwa siku 7 na nilikua na uhakika wa kuokota angalau Dola 10 to 20 kila siku ambazo zilikua nyingi sana kwa maisha yangu madogo sana....ITAENDELEA!

PART 9:- "MY AMERICAN EXPERIENCE"

Now nilikua napiga kazi ya kusafisha usiku fasta in 2 hours ukumbi una AC na Kapeti saafi so namaliza kazi like Saa Tisa natafuta kona moja safi nalala mpaka Saa 10 na Nusu naamka naingia kazini kwenye Trucks kule nako nilijiwekea tabia ya kuwahi mapema kusudi nipate nafasi ya kujifunza kuendesha mwenyewe na nilianza na kujifunza kurudi nyuma kwa muda mrefu by the time saa ya kuanza kazi ikifika nilikua nimeshatumia like lisaa limoja na mazoezi.

Baada ya Mwezi mmoja nikawa na uwezo wa kuanza kuendesha ila masharti ya Permit ni lazima niendeshe nikiwa na Dreva mwenye leseni kamili kwa sasa kazi zangu zote mbili zilikua zinanilipa Dola 1000 kwa Wiki kama kawaida naziweka Benki tu cause lengo langu lilikua kusoma tu! ...

Nilikua ninafanya kazi kama Punda mpaka sifa zangu zikaanza kuwafikia Wazungu na hasa mwenye Kampuni Msichana Mdogo Dina Muamerika Mtaliano aliyeachiwa Urithi na Baba yake na Mumewe Russ so siku moja Supervisor wangu Jack akaniita na kunipa Great News kua mwenye Kampuni ameniruhusu kuanza kufanya kazi peke yangu yaani nitakua ninaendesha Truck lenye Mataili 18 peke yangu yaani nitakua ninavunja Sheria kwa kuendesha na Permit tu Mzungu Jack akaniambia kuwa makini sana isipokua ukikamatwa tu akanipa namba maalum ya simu ya kupiga Mungu mkubwa sana .

Niliendesha kwa miezi 6 bila kukamatwa na sasa ndio umaarufu wangu wa kupiga kazi Fasta na Perfectly na Consistency ukaanza kua ndio the talk of all my Co-workers mpaka Viongozi wangu wa kazi ...lakini kwa mara ya kwanza in my life nikaanza kugundua kua KUMBE NINA UWEZO MKUBWA WA KUFIKIRI cause Wazungu ndio walioanza kunijadili sana nikiwa sipo na nikawa ninapata feed back kutoka kwa wafanyakazi wenzangu ambao hawakuwa wanapendezwa na sifa zangu za kupiga kazi.

Baada ya Miezi 6 sasa nikawa tayari kwenda kufanya mtihani wa Leseni CDL CLASS A & HAZARDOUS MATERIALS ni Leseni kubwa sana USA ni wachache sana wanazo maana ukishaipata unakuwa a Professional Driver unaweza kusafirisha mpaka Uranium au Silaha kitu ambacho the American Authority wanakiogopa sana sikulala usingizi siku ya kwenda kufanya mtihani sikua naamini kwamba hatimaye nitaipata hiyo Leseni...ITAENDELEA!

“Kauli Zetu Zinaweza Zisiifurahishe Serikali, Hili ni Tatizo Kubwa” –Hussein Bashe (+Video)

$
0
0
Mbunge wa Nzega mjini Hussein Bashe alisimama Bungeni Dodoma na kuchangia mapendekezo yake katika hoja tatu zilizowasilishwa na Serikali ambazo ni Hoja za kamati ya kudumu ya Bunge ya Bajeti, hoja ya kudumu ya uwekezaji ya bunge na mitaji ya umma, Hoja ya viwanda, biashara na mazingira ambapo Bashe alieleza namna ambavyo mzunguko wa fedha

 VIDEO:

Tazama Maisha ya Mbosso...Kutoka Mtaani, YaMoto mpaka WCB Wa

$
0
0
Hii ni historia ya maisha ya Mbosso kimuziki.

Unaweza tazama video fupi hapo juu....Mengi yamejaribu kuwasilishwa kwa video ili uweze kumfahamu Mbosso aka Mbosso khan aka Marombosso aka Mshedede aka African voice.
VIDEO:

Wastara Atoa Sababu ya Ndoa yake na Kigogo wa CCM kuvunjika

$
0
0
Msanii wa filamu bongo ambaye hivi karibuni amekuwa akipokea michango kutoka kwa watu mbali mbali kwa ajili ya matibabu, ameweka wazi moja ya sababu iliyofanya ndoa yake na kigogo wa CCM Sadifa Khamis kuvunjika baada ya muda mfupi.

Akizungumza na mwandishi wa eatv Wastara amesema mume wake huyo alionesha kutojali matatizo yake na badala yake kuweka pesa mbele, baada ya kudai risiti za matibabu aliyoenda kutibiwa India, kwa hela za michango ya watu mbali mbali, ili arudishiwe na bunge na ziingie mfukoni mwake.

Wastara amesema kitendo cha Sadifa kudai risiti hakikukifurahia, kwani pesa aliyokwenda nayo haikutoka mfukoni mwake, bali zilitoka kwa watu mbali mali wakiwemo Makamu wa Rais Mama Samia Suluhu, Msanii Alikiba, rafiki yake Sadifa na wengineo.

Diamond Azushiwa Skendo Nyingine Nzito

$
0
0
Mwanamuziki aliyeuteka ulimwengu wa Bongo fleva Naseeb Abdul ‘Diamond Platnumz’ amejikuta ndani ya skendo nyingine baada ya mwanadada mrembo anayeitwa Mia kukiri kuwa alilala na nae nyumbani kwake Madale.

Wiki chache zilizopita Diamond alikamata headlines zote kwenye mitandao ya kijamii baada ya msichana huyo aliyetambulika kwa jina la Mia kuonekana akijirekodi ndani ya nyumba ya Diamond iliyoko Madale.

Baada ya kusambaa kwa video hiyo, mara moja taarifa zilienea kuwa msichana huyo alikuwa ni mchepuko wa Diamond na alikwenda Madale, jambo ambalo lilizua tafrani hata kwa Zari ambaye aliamua kumrushia dongo na kusema Madale pamekuwa Guest house.

Lakini tetesi hizo zilizimwa siku inayofuata baada ya timu ya Diamond kusambaza picha na video zilizokuwa zinamuonyesha msichana yule akiwa nyumbani kwa Diamoand, Madale lakini safari hii alionekana akiwa amekumbatiana na Bajuni ambaye ni mmoja Kati ya madansa wa WCB. Hivyo kuonekana kuwa Mia alikuwa ana uhusiano na Bajuni na sio Diamond kama ilivyodaiwa awali.

Ikiwa ni wiki chache tu zimepita baada ya sakata hilo kutokea, mrembo Mia amefunguka na kueleza ukweli wote ambapo amedai kuwa habari zilizoenezwa kwenye mitandao ya kijamii sio za kweli kwani yeye alienda Madale kumfuata Diamond.

Katika mahojiano aliyofanya na kipindi cha Shilawadu kinachorushwa na runinga ya Clouds, Mia alifunguka na kusema kuwa, alipigiwa Simu na Diamond aende Madale mida ya saa nne usiku na alipofika akalala naye mpaka asubuhi ya kesho yake asubuhi ndipo alichukua simu yake akajirekodi video akiwa anatembea tembea nyumbani hapo.

Kwa mujibu wa maelezo ya Mia,  Diamond alimuona akijirekodi kupitia kamera zilizokuwa mule ndani, ndipo akaichukua simu yake kwa lazima na kuanza kuisachi, kisha akaifuta kila kitu kilichokuwepo yaani picha zote mpaka video.

Aliendelea kueleza kuwa, baada ya hapo Diamond akawaita Bajuni na Harmonize na wakamlazimisha aanze kupiga picha na Bajuni ili ionekane kama ni wapenzi ili baadaye Diamond aje aseme alienda Madale kwa Bajuni na siyo kwake.

Mia aliongea kwa uchungu akidai amedhalilishwa na Diamond na watu wote wamejua kuwa yeye anatembea na Bajuni wakati alikuwa hajawahi hata kumuona hapo kabla wakati aliyeenda kumfuata Madale ni mwenyewe Diamond.

Wasiliana na Mtaalam Chief Sultan Makata...Kumaliza Shida zako zilizoshindikana

$
0
0
CHIEF SULTAN MAKATA
Wasiliana na Mtaalam Huyu Kwani yeye hufaulu Pale wote waliko Shindwa na Pia Humaliza kazi zilizo Shindikana ama Zilizo Achwa ndani ya Siku Moja 1.
CHIEF SULTAN MAKATA ANAWASHUKURU WALE WOTE WANAOPIGA SIMU ZA SHUKRANI NA KUTOA SHUHUDA JINSI TIBA ZAKE ZINAVYO SAIDIA(Rudisha Mahusiano yako Ndani ya Saa 12 tu)

CHIEF SULTAN MAKATA ni Mtabibu wa Nyota za Binadamu na Dawa za Asili Mwenye Uwezo wa Kubaini Tatizo lako tu Pindi Utakapo Fanya Mawasiliano Kupitia Wasaa Husika.
(NA ANATIBU KWA NJIA YA SIMU UKIWA NCHI YOYOTE MKOA WOWOTE ENDAPO UTAFATA MAELEKEZO YAKE..)

Je Unasumbuliwa na Mapenzi..?
Umeachwa na UMPENDAE Awe Mume/Mke na Bado Unampenda
Je Umejaribu Sehemu Nyingi Bila Mafanikio?
Mpigie Simu sasa Hivi Ujionee Muujiza wa Papo kwa Papo..
Anauwezo wa Kurudisha Mahusiano yako na Kuimarisha NDOA Ndani ya saa 12 tu.
Je Umekimbiwa na Mumeo/Mkeo au Mpenzi na Anaishi na Mtu Mwingine..?
Muone akutatulie Anauwezo wa Hali ya Juu wa Kusambalatisha Mahusiano yao (Mfarakano/Kimavi) Endapo Utafata Atakacho Kuelekeza.

Je Una Mpenzi wako ana Pesa na unataka Kumkamata? Muone Maalim Hussein Atamfanya Atimize Ahadi zote Ndani ya Muda Mfupi..

CHIEF SULTAN MAKATA Anatumia Jina La Muhusika au Picha Kumaliza Tatizo..
Anatibu Kutumia QUR_AN DAWA ZA ASILI YA AFRICA, Dawa za KIARABU NA MAJINI..
ANATAFSIRI NDOTO. ANAPANDIKIZA NYOTA YA KUSHINDA BAHATI NASIBU, KUSAFISHA NYOTA NA KUKUPA MVUTO WA AJABU, KUTOA NUSKI NA VIFUNGO MBALIMBALI.

ZINDIKO ZA NYUMBA NA BIASHARA.. PETE ZA BAHATI.. HUMALIZA KABISA TATIZO LA NGUVU ZA KIUME NA KUREFUSHA UUME KWA SAIZI UNAYOTAKA. HUZUIA CHUMA ULETE KWENYE BIASHARA. HURUDISHA MALI ZILIZOPOTEA..
MAGONJWA SUGU, MIGUU KUWAKA MOTO AU KUFA GANZI, HUTIBU BUSHA BILA KUPASUA..ANAO UWEZO WA KUMRUDISHA  ALIE MBALI AU ALIECHUKULIWA MSUKULE..

Humaliza Kesi ya Aina Yoyote Ndani ya Siku 7 tu..
Hutoa Jini la MALI kwa wale Wanao Hitaji Utajiri Bila Masharti..

+255 677 805 105 WhatsAPP.
+255 746 426 604 Kupiga.

Baunsa wa Diamond Amwagiwa Maji Jukwaani na suti zake Kaeleza Alivyojisikia

$
0
0
Baunsa maarufu anaye mlinda msanii Diamond, Mwarabu leo ilikuwa ni siku yake ya kuzaliwa ambapo Harmonize alimuita kwenye stage na kisha kumwagia maji na kumuimbia wimbo wa Happy Birthday, Bonyeza play kutazama ilivyokuwa..

VIDEO:

Tazama Dakika 3 za Balaa Alilofanya Diamond Mwembe yangu

$
0
0
Siku ya leo February 4, 2018 kundi la WCB limefanya utambulisho mwingine wa pili wa msanii Mbosso katika uwanja wa Mwembe Yanga, Temeke DSM ambapo wasanii wote wa WCB wali-perform na moja ya wasanii hao ni DIAMOND PLATNUMZ ambaye alitoa burudani katika viwanja hivyo..

VIDEO:

Sababu za Diamond Platnumz Kukataa Show Nyingi za Ndani

$
0
0
Sababu za Diamond Platnumz Kukataa Show Nyingi za Ndani

Tazama VIDEO Hapa Chini:

Kiwanja Cha Kujenga Nyumba Kinauzwa Eneo la Mapinga Karibu na Bunju B

$
0
0
Kiwanja cha Kujenga Nyumba Kinauzwa , Kina Size ya 20 Kwa 20 Mita, Kipo Eneo la Mapinga Karibu na Bunju B, Kipo Karibu na Barabara ya Lami
Shilingi Mil 7.5 Maongezi yapo Kidogo

Piga simu 0714604974 Kwa Mawasiliano zaidi

Kwanini Wanaume Wengi Wanaupungufu Wa nguvu Za Kiume Na Maumbile Madogo?

$
0
0
Asilimia 45 ya wanaume wapo tofauti na wengine kwa kuwatimizia vyema wake au wapenzi Wao na kuwasababishia kutoka nje ya ndoa zao.


NINI CHANZO CHA HAYO?Kupiga punyeto,Ngiri,Vidonda vya tumbo,Magonjwa ya moyo,Presha,Kisukari,Korodani moja kuvimba,Msongo wa mwazo,Kufanyiwa tohara ukiwa mtu mzima n.k.DOKTA MANYANDA sasa kapata tiba sahihi ya tatizo la NGUVU ZA KIUME.


MUHAMA:Hii hutibu na kuponyesha kabisa tatizo la nguvu za kiume,utakuwa na uwezo wa kurudia tendo zaidi ya mara tatu bila kuchoka na itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa mda wa dakika 15-20.DAWA hii imechanganywa miti 12.Hata wazee wenye umri mkubwa wanapona kabisa.OKO NDOA YAKO SASA.


MANGUNGU MIX: Ndio tiba tosha kwa sasa ambayo hurefusha na kunenepesha uume saizi uipendayo inch 1-8 na unene sentimita 1-5,dawa hii ipo ya kupaka na kunywa na haina madhara yoyote kwa mtumiaji.


NITOFAUTI NA ULIZO WAHI KUZITUMIA.Pia tuna dawa za kupatanisha mke,mme,mpenzi au bosi wako kwa mda mfupi sana,Uzazi,Kusafisha nyota,


Je unamali yako unauza hupati wateja?

Wasiliana nami 0716-263605


DOKTA MANYANDA ANAPATIKANA KASULU KIGOMA,Kwa wale wa mikoani huduma hii utaipata popote pale

Mzee Kingunge Kuzikwa Leo Hii Hapa Ratiba ya Mazishi

$
0
0
Mzee Kingunge Kuzikwa Leo Hii Hapa Ratiba ya Mazishi
RATIBA  ya mazishi ya aliyekuwa mwanasiasa mkongwe, Kingunge Ngombale Mwiru, iliyotolewa na familia yake jana inaonyesha atazikwa leo Jumatatu katika shughuli itakayoanza saa 9:30 hadi 11:30 katika makaburi ya Kinondoni, jijini Dar es Salaam.

Taarifa hiyo iliyotolewa na mwenyekiti wa kamati maalum ya shughuli hiyo, Omary Kimbau, inaonyesha kwamba mwili wa marehemu utatolewa leo saa 10 jioni Hospitali ya Muhimbili na kupelekwa nyumbani kwake Victoria/Makumbusho ambako ibada na mila zitafanywa usiku mzima.

Kwa mujibu wa taarifa hiyo, shughuli zitakazofanywa kesho ni kama ifuatavyo:



Jumatatu tarehe 5/2/2018
– Saa 1:00 asubuhi mpaka saa 2:00 asubuhi waombolezaji kuwasili nyumbani kwa ajili ya kuanza taratibu za mazishi.
– Saa 2:00 asubuhi mpaka saa 3:30 asubuhi kupata kifungua kinywa
– Saa 4:00 asubuhi mpaka saa 5:00 misa nyumbani kwa marehemu
– Saa 6:00 mwili kuwasili Karimjee Hall  kuagwa
– Saa 6:00 mchana 9;00 kuaga mwili wa marehemu
– Saa 9:00 alasiri mpaka 9:30 kuelekea makaburini Kinondoni
– Saa 9:30 mpaka 11:30 maziko
– Saa 11:30 jioni 12:30 kuelekea nyumbani kwa chakula cha jioni
1:30 usiku mpaka. 2:45 chakula cha usiku waombolezaji wote
3:00 usiku- waombolezaji wote hitimisho la shughuli nzima

Kingunge Ngombale-Mwiru alifariki Ijumaa wiki hii katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili alikokuwa amelazwa akitibiwa majeraha baada ya kuumwa na mbwa wake.

Mke wa Mzee Majuto: Namuombea Sana Mume Wangu Apone Maana Ndiye Furaha Yangu

$
0
0
Mke wa Mzee Majuto: Namuombea Sana Mume Wangu Apone Maana Ndiye Furaha Yangu
MKE wa mchekeshaji maarufu Bongo, Amri Athuman ‘Majuto’, Aisha Yusuf amesema kuwa siku za hivi karibuni alipoanza kuugua tena mumewe amekuwa akikesha na kumuombea arudi katika hali ya kawaida kwani anapoumwa vitu vyote vinalala.

Akichonga na gazeti hili mke huyo alisema mume wake ni mcheshi sana na ni mtu anayeifanya familia kuwa na furaha kila wakati sasa anapokuwa mgonjwa nyumba inakuwa haina amani kabisa na hata watoto ambao amezoea kucheza nao wanapoa.

“Kila siku dua zangu ni kwa mume wangu maana ndiyo nguzo katika familia yetu na ni mtu mcheshi sana kwa familia hivyo namuombea sana apone maana ndiye furaha yangu,“ alisema mke wa Majuto.

Chuchu Agoma Kumzalia Mtoto Mwingine Ray

$
0
0
Chuchu Agoma Kumzalia Mtoto Mwingine Ray
UKITAJA ‘kapo’ za mastaa ambao wamefanikiwa kuwa kwenye uhusiano na kubarikiwa kupata watoto wakiwa pamoja, huwezi kuacha kuwataja mastaa wakubwa wa sinema za Kibongo, Vincent Kigosi ‘Ray’ na Chuchu Hans.

Wawili hawa ni kapo ambayo imefanikiwa katika hilo na uzao wao kuwa gumzo kila kona.

Chuchu ambaye amebarikiwa kupata mtoto wa kiume na Ray waliyempa jina Jayden, uhusiano wao huko nyuma ulikuwa wa kificho kikubwa, lakini kadiri siku zilivyosonga waliamua kuweka wazi.

Katika mahojiano ya Over Ze Weekend yaliofanyika ana kwa ana na Chuchu Hans, amezungumza mengi kuhusiana na maisha yao;

Over Ze Weekend: Unajisikiaje mtoto wenu kuwa gumzo kwenye mitandao ya kijamii?

Chuchu: Najisikia faraja na pia hakuna kitu kizuri kama mtu kumpenda mtoto wako. Kama mwanamke, lazima ujisikie faraja sana.

Over Ze Weekend: Kutokana na mtoto wenu kuwa kivutio, je hujabadili mawazo ya kutotaka kuzaa tena na kuolewa na Ray?

Chuchu: Msimamo wangu hauwezi kubadilishwa na mtoto. Kama nilisema hivyo, basi itaendelea kuwa hivyohivyo?

Over Ze Weekend: Kwa hiyo unaweza kwenda kuzaa tena na mtu mwingine na siyo Ray?

Chuchu: (kicheko)… mimi ningependa hapa nisiendelee kuzaa, lakini sijui huko mbele kitaka-chot-okea.

Over Ze Weekend: Kuna magumu yoyote uliyopitia kipindi cha ujauzito hadi kuzaa na ndiyo maana hutaki tena kuolewa?

Chuchu: Sitaki kuchuma ubaya kwa Ray, kuhusiana na malezi ya mtoto wake ni mtu ambaye anajali hilo na anampenda sana, kutoolewa ni uamuzi tu. Hata hivyo, kila mtu akili yake iko kwa mtoto, mambo mengine baadaye.

Over Ze Weekend: Mbona kuna tetesi kuwa unaishi nyumba moja na Ray?

Chuchu: Hilo sitaki kulizungumzia kabisa.

Over Ze Weekend: Kama wewe hutaki tena kuzaa na Ray, utajisikiaje akizaa mtoto na mwanamke mwingine?

Chuchu: Siwezi kujisikia chochote maana yeye ni mwanaume, anaweza kufanya lolote.

Over Ze Weekend: Inaonesha mtoto amepunguza kasi yako ya kufanya kazi zako za sanaa, unalizungumziaje hilo?

Chuchu: Hapana, nilitaka kumpa malezi ya kwanza kama mtoto, lakini sasa ameshatimiza mwaka, ninaweza kufanya kazi zangu na hata za mtu mwingine.

Over Ze Weekend: Hivi karibuni mwigizaji mwenzako, Blandina Chagula ‘Johari’ alifiwa na mama yake mzazi, Asha Chagula, lakini hukuonekana msibani, je, bado mna bifu?

Chuchu: (mshangao)… hapana! Nitaenda tu kumuona wala hatuna bifu.

Over Ze Weekend: Ninakushukuru sana Chuchu.

Chuchu: Asante na karibu.
Viewing all 104690 articles
Browse latest View live




Latest Images