Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104712 articles
Browse latest View live

Wastara Aondoka India kwa Matibabu Amwaga Chozi Airport Wakati Akiondoka

$
0
0
Wastara Aondoka India kwa Matibabu Amwaga Chozi Airport Wakati Akiondoka
Muigizaji wa filamu nchini Tanzania, Wastara ameondoka nchini kuelekea India kwa ajili ya matibabu ya mguu wake ulioanza kumsumbua mwishoni mwa mwaka jana huku akiwashukuru watanazania na Vyombo vya Habari kwa kuwa pamoja naye kipindi alivyokuwa akihitaji msaada wa fedha.

Wastara akiongea na waandishi wa Habari mapema leo Jumapili Februari 4, 2018 katika Uwanja wa Ndege wa Mwalimu Nyerere jijini Dar es salaam, amesema “nina washukuru sana vyombo vya habari wote kwa moyo wa upendo walionesha kwa sababu bila ya wao hata mimi nisingekuwa Wastara. Napenda kuwaambia watanzania kwamba tuamini sana maneno anayosema mtu kuliko neno analosema mtu mwingine kwa hiyo naamini kuna wengine watakuja na matatizo tujaribu kuwaangalia nawao pia”.

Na alipoulizwa kuhusu tuhuma za kutumia fedha za matibabu kwa starehe kama alivyowahi kuchangiwa kipindi cha nyuma na kwenda Dubai, Wastara amesema hajawahi kuchangiwa na Watanzania bali alisaidiwa Makamu wa Rais na hakutumia kwa matumizi mengine.

“Kwanza niseme sijawahi kuchangiwa na Watanzania mimi kama mimi, mara ya kwanza nilipoumwa aliyenichangia asilimia kubwa alikuwa ni Makamu wa Rais, na uzuri ni kwamba mpaka nafika hospitalini nilikuwa nampigia simu. Kilichosababisha watu waseme baada ya kufika hospitali kama hivi ninavyokwambia wiki tatu linapotokea tatizo kama umefanyiwa Oparesheni au upasuaji wowote niliambiwa unauwezo wa kukaa au kuishi kwenye hoteli karibu na hospitali..Ndipo watu wa karibu yangu wa Oman wakawa wamenipa Visa nikaenda kukaa huko kwa muda.“ameongea Wastara.

Lema Amtembelea Sugu Gerezani Awapa Neno Familia Yake

$
0
0
Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema (Chadema) amemtembelea gerezani mbunge mwenzake wa Mbeya Mjini, Joseph Mbilinyi ‘Sugu’ na kuifariji familia.

Lema ameieleza familia ya Sugu kuwa kukaa kwake mahabusu kumetokana na kuwatetea wananchi wa Mbeya na Tanzania kwa jumla na kwamba wabunge wengi wa upinzani wapo kwenye hesabu za kupelekwa gerezani, hivyo hawana sababu ya kunung’unika.

Mbunge huyo na mwingine wa Tandahimba (CUF), Katani Katani wakiongozwa na mwenyeji wao mbunge wa viti maalumu, Sophia Mwakagenda waliitembelea pia familia ya Sugu eneo la Sae, Mbeya.

Kabla ya kwenda nyumbani kwa mama mzazi wa Sugu, Desderia Mbilinyi, wabunge hao walikwenda Gereza Kuu la Ruanda jijini hapa kuwajulia hali Sugu na Katibu wa Chadema Kanda ya Nyanda za Juu Kusini, Emmanuel Masonga ambao wapo mahabusu baada ya kunyimwa dhamana na Mahakama ya Hakimu Mkazi Mbeya wakikabiliwa na kesi ya kutumia lugha ya fedheha dhidi ya Rais John Magufuli.

Lema alisema wamewakuta Sugu na Masonga wakiwa wazima, wenye afya njema na furaha, huku wakibainisha kwamba kukaa kwao mahabusu kumewapa ujasiri katika harakati za kisiasa.

“Mama sasa wewe unasikitika nini, wewe ni mama wa shujaa unalia nini? Kweli jela ni kubaya, lakini si kubaya kama umekwenda kwa sababu za kupigania haki za wananchi. Sugu hajaua, hajaiba televisheni wala hajabaka, hivyo mama wewe hapa inuka tembea kifua mbele kwamba mwanao yupo gerezani kwa sababu anatetea haki za wananchi, hii ni heshima kubwa sana mama yangu,” alisema Lema.

Lema alisema Sugu alishajitabiria kukaa gerezani kupitia nyimbo zake, na kweli sasa yupo gerezani.

“Lakini jua kwamba kuna siku, na kuna mwisho. Haya ni mapambano ya kiukombozi na ukiona hivi jua ukombozi umekaribia,” alisema.

Lema ambaye mara kadhaa amekaa mahabusu alisema kwa mpinzani kukaa gerezani au kufunguliwa kesi kunampa hekima, busara, kujenga mshikamono, moyo unaimarishwa na anakuwa na nguvu kubwa akitoka, hivyo anatamani na wabunge wengine wa upinzani wote wawekwe mahabusu ili wakapate ujasiri wa kuwapigania Watanzania.

Mbunge Katani alisema suala la Sugu na Masonga kukaa mahabusu kwake haoni kama ni kitu cha kushangaza bali kinampa faraja akiamini wakitoka huko watakuwa wamebadilika na kujazwa na ujasiri wa kuendeleza harakati za kuwapigania Watanzania.

Mbunge Sophia alisema, “Tunajua wananchi wana hasira kuona mbunge wetu yupo ndani kwa kunyimwa dhamana, lakini bado tunasisitiza waendelee kuwa watulivu.”

Akizungumza na wabunge hao, mama yake Sugu alisema ni jambo linalomnyima usingizi kuona mwanaye yupo mahabusu, lakini anajipa matumaini kwa kuwa mbunge huyo alianza harakati za kuwasemea wananchi akiwa bado mtoto mdogo.

“Inauma sana mwanangu kukaa kule, lakini anatetea haki za binadamu wenzake na nafikiri anachotenda ni halali kabisa hakuna tofauti. Mwanangu alitabiri mengi tangu yupo hapa nyumbani akiwa mtoto mdogo anaimba nyimbo, anatabiri matatizo ya nchi kwa hiyo hatushangai sana.”

Alisema, “Hata Lema na wenzake hapa wananihamasisha, hivyo sioni kama amefanya kitu cha ajabu yule (Sugu) ndivyo alivyo tangu utoto wake, ndiyo maana tukamuita Joseph maana yake ni mfanyakazi bora.”

Shinikizo Zaidi Lamkabili Rais Zuma Ajiuzulu

$
0
0
Shinikizo Zaidi Lamkabili Rais Zuma Ajiuzulu
Rais wa Afrika kusini anakabiliwa na shinikizo zaidi kujiuzulu kufuatia mazungumzo na maafisa wa ngazi ya juu katika chama chake cha ANC sikuya Jumapili.

Haijafichuliwa mazungumzo hayo yalihusu nini lakini viongozi katika chama hicho wanatarajiwa kufanya mkutano wa dharura hii leo Jumatatu.

Cyril Ramaphosa aliichukuwa nafasi ya kiongozi wa chama cha ANC kutoka kwa Zuma, anayekabiliwa na tuhuma za rushwa.

Wachambuzi wanasema wakuu wa chama hicho wanajaribu kuondoa mvutano wa kung'ang'ania madaraka ambao unaweza kukigawanya chama hicho kabla ya uchaguzi mkuu mwakani.

Wanatarajiwa kuanza mchakato wa kumuondoa rais Zuma kupitia mfumo rasmi wa kumuondoa au kwa kuidhinisha hoja bungeni.

Maafisa sita wakuu wa chama hicho tawala waliwasili mmoja baada ya mwingine Jumapili katika makaaziya Zuma mjini Pretoria.

Walinyamaza kimya wakati mazungumzo yalipomalizika lakini wameitisha mkutano wa kamati kuu ya chama hicho Jumatatu.

Julius Malema, kiongozi wa upinzani na aliyekuwa mafuasi wa chama hicho cha ANC alisema kwenye mtandao wake wa Twitter kwamba rais Zuma amekataa kujiuzulu.

Zuma anastahili kusalia madarakani hadi uchaguzi mwaka ujao 2019. Hatahivyo chama hicho kimepoteza umaarufu wake katika muhula wa pili wa kiongozi huyo huku kukishuhudiwa pia kudorora kwa uchumi na tuhuma za rushwa.

Rais Zuma anakabiliwa na tuhuma za rushwa na jitihada za wapinzani na baadhi ya wafuasi wa ANC wanaotaka kumtimua madarakani.

Kwa mujibu wa taarifa rasmi, maafisa wa ngazi ya juu wa ANC wana 'jadiliana tu' na rais Zuma kuhusu "ugavi wa uongozi" ndani ya chama.

Lakini nyuma ya kauli hiyo nyepesi - vita vikali vya uongozi vinajitokeza katika nchi hiyo.

Rais Zuma bado yupo madarakani, lakini tangu Desemba mwaka jana, yeye sio mkuu tena wa ANC.

Waendesha mashtaka wakakamavu sasa wanaonekana kushika kasi katika uchunguzi dhidi ya tuhuma za rushwa zinazomkabili bwana Zuma na baadhi ya marafaiki zake wa karibu.

Wengi ndani ya ANC wanamtaka rais huyo ajiuzulu haraka iwezekanavyo, ili waweze kulenga kujenga upya sifa ya chama hicho kufuatia kuwadia kwa uchaguzi mkuu nchini mwakani.

Lakini kuna taarifa kwamba Zuma anajikita kisawasawa.

Anatarajiwa kulihotubia bunge wiki ijayo, lakini wafuasi wa upinzani wanataka kumzuia pia, wakieleza kuwa hastahili kusalia kama rais.

Kiongozi mpya wa ANC, Cyril Ramaphosa, ameshutumu wazi rushwa katika kiwango cha juu ndani ya chama na serikali, lakini anasisitiza kuwa rais Zuma hastahili kuazirishwa.

Uongozi wa CCM Wasitisha Kampeni Kwaajili ya Kushiriki Mazishi ya Kingunge

$
0
0
Uongozi wa CCM Wasitisha Kampeni Kwaajili ya Kushiriki Mazishi ya Kingunge
Uongozi wa CCM mkoa wa Dar es Salaam umesitisha kampeni za nje kwa siku moja (leo) kwa ajili ya kushiriki mazishi ya mwanasiasa mkongwe, Kingunge Ngombale Mwiru.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Katibu wa Siasa na Uenezi wa chama hicho, Simon Mwakifwamba imeeleza kuwa wanachama, makada na viongozi watashiriki kikamilifu katika msiba huo, hivyo hakutakuwa na kampeni za nje.

Alisema watazingatia ratiba iliyotolewa na msimamizi wa msiba huo Omary Kimbau, hivyo wanaCCM wafike mapema kwa ajili ya kumpumzisha kwenye makazi ya milele komredi Kingunge

Miujiza ya Sharifu Seif Mohamed..JE Umeachwa na Mme/Mke au Mpenzi, Umesongwa na Mitihani ya Maisha..Piga Simu Upate Muujiza Wako

$
0
0
SHARIFU SEIF MOHAMED ANAWASHUKURU WALE WOTE WANAOENDELEA KUPIGA SIMU, WENYE MATATIZO NA WALE WANAOTOA  SHUKRANI NA SHUHUDA JINSI TIBA ZAKE ZINAVYO WASAIDIA,

(Rudisha mahusiano yako ndani ya masaa 72 tu)

SHARIFU MOHAMED Ni  mtaalam na mnajimu maarufu wa nyota na kubashiri mambo yanayo watesa binadamu duniani kote na kupata ufumbuzi, Anatumia kitabu cha QUR'AN, Dawa za Asili, Dawa za Kiarabu na majini kwa kumtuliza mke/mme, mchumba au mpenzi ndani ya masaa 72 tu, na kutatua matatizo yote ya kimaisha,

Je Umeachwa na UMPENDAE awe Mme/Mke na bado unampenda? Je Umekimbiwa na Mmeo/ Mkeo n anaishi na mtu mwingine? Je Umejaribu sehemu nyingi bila mafanikio? Mpigie simu SHARIFU SEIF sasa hivi ujionee Muujiza wa Papo kwa Papo, Anauwezo wa hali ya juu wa kusambaratisha mahusiano yao na kumrejesha kwako haraka sana na Kumfanya Atimize Ahadi zote Ndani ya Muda Mfupi Endapo Utafwata Atakacho Kuelekeza

ANAZO DAWA ZA MAPENZI, NGUVU ZA KIUME, CHANGO NGIRI MAJI NA N.K, ZINDIKO LA NYUMBA NA BIASHARA, PETE ZA BAHATI, HUMALIZA KABISA TATIZO LA NGUVU ZA KIUME NA KUREFUSHA UUME KWA SAIZI UNAYOTAKA, HUZUIA CHUMA ULETE KWENYE BIASHARA, HURUDISHA MALI ZILIZOPOTEA, MAGONJWA SUGU, MIGUU KUWAKA MOTO AU KUFA GANZI, HUTIBU BUSHA BILA KUPASUA, ANAO UWEZO WA KUMRUDISHA ALIE MBALI AU ALIECHUKULIWA MSUKULE, KUPANDISHA NYOTA NA KUSHINDA BAHATI NA SIBU, KASAFISHA NYOTA NA KUKUPA MVUTO WA AJABU, KUTOA NUKSI NA VIFUNGO MBALIMBALI,  MAFANIKIO YA MAISHA NA UTAJIRI BILA MASHARI, NA MENGINE MENGI YA SIRI,

JE UMAHANGAIKA KUPATA MTOTO BILA MAFANIKIO? WASILIANA NA MTAALAMU HUYU KWANI YEYE HUFAULU PALE WOTE WALIPOSHINDWA, PIA UMALIZA KAZI ZILIZO SHINDIKANA NA WATAALAM WENGINE NDANI YA MASAA 24 TU,

(NA ANATIBU KWA NJIA YA SIMU UKIWA NCHI YOYOTE AU MKOA WOWOTE ENDAPO UTAFWATA MAELEKEZO YAKE)

Kwa ushauri na mawasiliano  zaidi Piga SIMU No:

Mobile +255 654-836970
WhatsApp +255 756-033670

Anayetuhumiwa Kusababisha Kifo cha Radio Akamatwa

$
0
0
Anayetuhumiwa Kusababisha Kifo cha Radio Akamatwa
Mtuhumiwa namba moja ambaye anahusishwa na kifo cha msanii muziki nchini Uganda, Mowzey Radio amekamtwa na Jeshi la Polisi nchini humo.

Kijana Wamala Godfrey mwenye umri wa miaka 28 ndiye alikuwa akisakwa na polisi kama mtuhumiwa mkuu mara baada ya mmiliki wa bar, Egesa George na Meneja wake kilipotokea kifo cha Radio kushikiliwa na Polisi.

Mwimbaji Mowzey Radio alifariki dunia Februari Mosi mwaka huu kutokana na majeraha ambayo aliyapata kichwani kufuatia ugomvi katika bar hiyo.

Kamanda wa Polisi Kampala, CP. Frank Mwesigwa amethibitisha kushikiliwa kwa Wamala Godfrey na kueleza kuwa kwa sasa wanaandaa majalada ili kuweza kumfikisha mahakamani.

Gigy Money Alia na Mapenzi "Unabeba Mimba Anakuonyesha Dharau na Mwanamke Wake wa Nje Anakuonyesha"

$
0
0
Gigy Money Alia na Mapenzi "Unabeba Mimba Anakuonyesha Dharau na Mwanamke Wake wa Nje Anakuonyesha"
Msanii wa muziki Bongo, Gigy Money amefunguka yale anayopitia katika mahusiano yake kwa sasa.

Muimbaji huyo ambaye kwa sasa ni mjamzito ametupa lawama zake nyingi kwa wanaume kwa madai ni watu wasioridhika katika mapenzi. Gigy Money ametumia Instagram kuandika ujumbe mrefu kueleza yaliyo moyoni;

Kiukweli Leo nina stress sana na ndio maana nimeona bora niseme kwani nachokiamini mm sio peke angu ninayo yapitia haya kuna muda unaweza ukakufuru Mungu kwa maneno ambayo kesho na kesho kutwa uwezi kuyarudisha kinywani katika makosa ambayo najua nimeyafanya nikupenda lakini kupenda sio dhambi nimepitia mengi sana kwenye Mapenzi kiasi chakufikia kupungua kimwili akuna kitu kibaya na kigumu kama kumuaminisha mtu unampenda unaweka nguvu na jitihada zako katika mapenzi kuna muda unawaza sijui niachie ngazi.

Walio karibu na mm wanaweza wakawa wanajua was baadhi ya mateso na utumwa wa mapenzi nilio wahi kupitia na still bado najiuliza kwann wanaume niwagumu kuonesha hisia zao za ukweli inashangaza mwanaume anaeza kuishi na ww pika pakua lakini anaempenda yuko mbali na upeo wa macho yake hicho kitu naamini wanawake wengi hawakiwezi ikiwa mm ni mmoja wao kama sikutaki nitakwambia in good way bila hata kugombana lakini mwanaume awezi kua muwaz na hii labda anapata kitu kidogo kwako yawezekana pesa,mavaz au umaarufu yote yanawezekana kiukweli natamani ningekua gigy yule ambae naweza kua na maamuzi yangu binafsi lakini nashindwa naumia mapenzi ni kitu ovyooooo .

Mara nyingi huwaga tunawapenda watu wenye uwezo wakawaida tukiamini mapenzi sio pesa ila wanaume wabongo wajeuri unabeba mimba dharau anakufanyia mwanamke wake wa nje atakuonesha kiukweli inauma ndio lakini naamini nihatua za maisha na ukuaji naamini nimedondoka hatua moja lakini naweza kuinuka hatua 8 Tanzania ni nchi inayoongoza kua na single mother’s sio wote baba wa watoto wamefariki wengi wetu huwaga tuna wakimbiza watoto wetu mbali na maisha na mateso tuliyo wahi kuyapitia kwa baba zao hakuna mtu anaeweza kunielewa ila mkiona mtu Ana type ivi ujue yanazidi hakuna kitu kibaya kama mtu akupendee kitu inauma sana.

Gigy Money ambaye ni hitmaker wa ngoma ‘Papa’ na kwa sasa ‘Mimina’ yupo katika mahusiano kwa muda mrefu na Mo J ambaye ni mtangazaji za Choice Fm.

Trump Ampiga Stop Diego Maradona Kuingia Marekani

$
0
0
Trump Ampiga Stop Diego Maradona Kuingia Marekani
Rais wa Marekani Donald Trump ameripotiwa kumpiga marufuku mchezaji wa zamani wa Argentina na mshindi wa Kombe la Dunia, Diego Maradona kuingia nchini Marekani.


Mwanasheria wa mwanasoka huyo wa zamani amesema kuwa Maradona hatohudhuria kesi yake jijini Miami kutokana na nyota huyo kuzuiwa na Rais Trump kwa madai kuwa alitoa lugha ya kashfa kwa Trump kwenye mahojiano na Television nchini Venezuela.

''Maradona hatoweza kuwepo kwenye kesi yake dhidi ya mke wake wa zamani kwasababu amezuiwa na Rais Trump'', amesema Mwanasheria huyo.

Muargentina huyo alihitajika kusafiri wiki hii kwenda Miami, Florida, kwenye kesi yake dhidi ya mke wake wa zamani Claudia Villafane, ambaye anamshitaki kwa kumuibia fedha na kununua mali mbalimbali nchini Marekani.

Maradona anakumbukwa kwenye fainali za Kombe la Dunia mwaka 1994 nchini Marekani, akiwa nahodha wa Argentina alirudishwa nyumbani baada ya kupimwa na kugundulika ametumia madawa ya kulevya aina ya Cocaine.

Mahakama Yamuondolewa Mamlaka DPP ya Kuzuia Dhamana ya Mshtakiwa

$
0
0
Mahakama  Yamuondolewa Mamlaka DPP ya Kuzuia Dhamana ya Mshtakiwa
Mahakama ya Rufaa imemwondolea Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP) mamlaka ya kuzuia dhamana ya mshtakiwa bila hata kulazimika kutoa sababu, baada ya kubatilisha kifungu cha 148 (4) cha Sheria ya Mwenendo wa Mashauri ya Jinai, kinachompa mamlaka hayo.

Kifungu hicho kinampa DPP mamlaka ya kuizuia Mahakama au ofisa wa polisi kutoa dhamana kwa mshtakiwa au mtuhumiwa baada ya kuwasilisha hati ya maandishi, kwa maelezo kuwa usalama au masilahi ya Jamhuri yataathirika.

Mahakama hiyo katika hukumu ya rufaa ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali dhidi ya mwanaharakati wa haki za binadamu, Jeremia Mtobesya imesema kifungu hicho ni kinyume cha Katiba na ni batili.

Hukumu iliyotolewa na jopo la majaji watano wa Mahakama ya Rufaa imekubaliana na ya awali iliyotolewa na Mahakama Kuu.

Majaji waliosikiliza na kutoa hukumu ya rufaa hiyo ni Bernard Luanda (kiongozi wa jopo), Kipenka Mussa, Bethuel Mmila, Stellah Mugasha na Jacob Mwambegele.

Hukumu hiyo ilisomwa Ijumaa iliyopita na Msajili wa Mahakama ya Rufaa, John Kahyoza aliyesema kifungu hicho kwa jinsi kilivyo, Mahakama au ofisa wa Polisi anakuwa hana uchaguzi zaidi ya kumnyima dhamana mshtakiwa au mtuhumiwa.

Alisema kifungu hicho hakikidhi matakwa ya kisheria kwa kuwa haipaswi kuwa ya maelezo ya jumla na kinaweza kutoa mwanya wa matumizi mabaya ya mamlaka kwa DPP.

Baada ya kufanya rejea ya sheria na uamuzi wa kesi kadhaa za ndani na nje ya nchi, Kahyoza alisema Mahakama imejiridhisha kuwa masharti ya kifungu hicho ni kinyume cha Katiba na hivyo ni batili.

Akizungumzia na Mwananchi jana kuhusu hukumu hiyo, Mtobesya alisema Mahakama imeitoa kwa misingi ya kikatiba.

“Katiba ndivyo inavyoelekeza kuwa mtu yeyote ana haki ya kusikilizwa na kila mtu ana haki ya kuwa huru. Sasa iwapo hizo haki zinaweza zikaondolewa, kuna utaratibu ambao unawekwa kisheria,” alisema.

Mtobesya alisema, “Kwenye ngazi zote, Mahakama Kuu na Mahakama ya Rufaa zimeangalia na kujiridhisha kwamba sawa hizo haki zinaweza kuwa si absolute (kamilifu) lakini je misingi ya kunyimwa hizo haki imefuatwa?”

Mwanasheria Mkuu wa Serikali alikata rufaa akipinga hukumu ya Mahakama Kuu ya Desemba 22,2015 iliyotolewa na jopo la majaji watatu wakiongozwa na Jaji Kiongozi, wakati huo, Shaban Lila. Majaji wengine walikuwa Sekieti Kihiyo na Profesa Eudes Ruhangisa. Katika shauri la msingi la madai namba 29 la mwaka 2015, Mtobesya ambaye ni wakili wa kujitegemea alidai kifungu hicho kwa jinsi kilivyo kinamnyima mshtakiwa aliye mahakamani au mtuhumiwa aliye polisi haki ya kusikilizwa.

Katika hoja za maandishi, alidai kila kesi inaangaliwa kwa mazingira yake na kwamba, kitendo cha DPP kuzuia tu dhamana kwa madai kwamba itaathiri masilahi ya umma bila kutoa sababu kinamnyima haki mhusika.

Alidai maelezo hayo tu ya kuathiri masilahi ya umma hayatoshi bali anapaswa kwenda mbali zaidi na kutoa sababu na kisha mshtakiwa au mtuhumiwa naye apewe nafasi ya kusikilizwa ndipo Mahakama ipime na kutoa uamuzi kwa sababu hizo.

Mahakama Kuu katika hukumu yake ilikubaliana na hoja za Mtobesya, ikisema kifungu hicho kinamnyima mtu haki ya kusikilizwa na ni kinyume cha Ibara ya 13 (6) ya Katiba ya nchi.

Mahakama ilisema kifungu hicho kinaenda kinyume cha misingi ya kidemokrasia.

Hukumu hiyo katika kesi ya jinai, DPP na mshtakiwa wote wanakuwa na haki sawa lakini kifungu hicho kinaupa upande mmoja mamlaka zaidi na kuufanya mwingine kuwa dhaifu, hivyo kutokuwa na usawa.

Mahakama Kuu ilisema kifungu hicho kinaondoa mamlaka ya Mahakama kuwasikiliza wadaiwa.

Mwanasheria Mkuu wa Serikali hakukubaliana na uamuzi huo, hivyo alikata rufaa Mahakama ya Rufaa akiwasilisha hoja tano za kuipinga. Wakati wa usikilizwaji aliondoa hoja tatu zikabaki mbili.

Pamoja na mambo mengine, AG aliipinga hukumu hiyo akidai kifungu hicho kiko sawa kwa kuwa kuna ibara za Katiba ambazo zinakifanya kiwe hivyo kilivyo, sawa na ibara ya 30 (2) (a) ya Katiba.

Mtobesya kupitia kwa wakili wake Mpale Mpoki alipinga hoja zilizotolewa na AG kupitia Wakili wa Serikali Mkuu, Vitalis Timon akidai kifungu hicho kwa namna kilivyo hakimpi fursa mshtakiwa kusikilizwa kabla ya kuzuiwa dhamana kwa hati ya DPP.

Wakili Mpoki alidai kifungu hicho kinakiuka ibara ya 13 (6) ya Katiba ya nchi, huku akiungwa mkono na Profesa Gamaliel Mgongo Fimbo aliyealikwa na Mahakama kutoa maoni ya kitaalamu.

Profesa Mgongo Fimbo pamoja na mambo mengine alisema kifungu kinachomzuia mshtakiwa kusikilizwa maombi yake ya dhamana au kupinga hati ya DPP, hakiweki usawa wa usikilizwaji, hivyo kinakiuka ibara ya 13 (6) (a) ya Katiba.

Ibada ya Kumuombea Kingunge Yafanyika Nyumbani Kwake

$
0
0
Ibada ya Kumuombea Kingunge Yafanyika Nyumbani Kwake
Ibada ya kumuombea  mwanasiasa mkongwe marehemu Kingunge Ngombale Mwiru imefanyika nyumbani kwake Victoria, Kijitonyama wilayani Kinondoni.

Ibada imefanyika leo Jumatatu Februari 5,2018 ikiongozwa na katekista George Wilbard wa Kanisa Katoliki.

Baada ya ibada, mwili wa Kingunge utapelekwa katika viwanja vya Karimjee  kwa ajili ya utoaji wa heshima za mwisho.

Kingunge aliyefariki dunia Februari 2,2018 katika Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) alikokuwa akipatiwa matibabu baada ya kung’atwa na mbwa nyumbani kwake atazikwa katika makaburi ya Kinondoni jijini Dar es Salaam.

Kenyata Amtolea Uvivu Odinga Amtaka Aache Kumchafua

$
0
0
Kenyata Amtolea Uvivu Odinga Amtaka Aache Kumchafua
Ikiwa ni wiki moja imepita tangu Kiongozi wa Umoja wa Vyama vya Upinzani nchini Kenya kujiapisha kuwa Rais wa watu wa nchini hiyo, Hatimaye Rais wa Kenya anayetambulika kikatiba Uhuru Kenyatta amezungumza kwa mara ya kwanza kuhusu tukio hilo.

Rais Kenyatta amesema kuwa kujenga taifa ni kazi kubwa lakini kubomoa ni muda mfupi hivyo amemshauri Raila Odinga kuacha maneno yenye mizozo na kuchafuana nje ya nchi kwani kushindwa kwenye uchaguzi ni jambo la kawaida hata yeye alishawahi kushindwa na akajipanga tena.

“Kujenga ni ngumu lakini kupasua ni dakika moja, lakini hawaoni tabu kupasua afadhali apasue apate uongozi, awe mkubwa, ukubwa sio kiti ukubwa ukubwa ni vitendo ambavyo unawatendea wananchi ambao unataka kuwaongoza, na hivyo hivyo hata sisi tumekuwa twahimiza ni nini unawatendea wananchi wako. ukiwa umetoka nchi yako unaenda kutembea nchi nyingine kusema wale wanaoongoza kule wanastahili kufungwa. Si uje hapa Kenya kwetu utuambie,“amesema Uhuru Kenyatta huku akimshauri jambo la kufanya Raila Odinga.

“Huwezi kufanikiwa kwa kumtakia mwenzio mabaya, omba mwenyezi Mungu na uombe wananchi kwa njia tulivu uoneshe sera zako tofauti na sera za wale wengine na wananchi sio wajinga wapo na ujuzi wakuamua ni nani wanataka na nani hawataki. Kama hawakutaki safari hii we pumzika wacha wale wengine waendelee, mimi nimegombea mara nyingi, mimi nimewahi kusimama hii kiti nikashindwa na nikakaa nikatulia, Nikasema eehh Mwenyezi Mungu basi hii sio nafasi yangu wakati hii na nikakubali kushindwa, sasa ninaongoza na nitaongoza mpaka wananchi waseme basi wewe tulia, sasa shida iko wapi na tunabaki tunachafuana hapa kila siku, Lets us work together, Lets us keep Kenya moving ahead, lets us provide services to our people mambo hayo ndiyo ya muhimu na ndivyo tutaendelea na waseme na waseme hawatutishi,“amesema Rais Kenyatta kwenye kongamano la kuimarisha hali ya usalama nchini Kenya liliofanyika wikiendi iliyopita katika chuo cha Kenya School of Government (KSG) jijini Nairobi.

Mwanasheria Mkuu wa Serikali Dkt. Adelardus Kilangi Aapishwa Bungeni

$
0
0
Mwanasheria Mkuu wa Serikali Dkt. Adelardus Kilangi Aapishwa Bungeni
NAIBU Spika wa Bunge, Dkt.  Tulia Ackson amemwapisha Mmwanasheria Mkuu wa Serikali (AG), Dkt. Adelardus Kilangi bungeni na kumkabidhia vitendea kazi kabla ya kuanza kwa Kikao cha Tano cha Mkutano wa 11 wa Bunge, Mjini Dodoma, leo Feb 5, 2018.
Dkt. Kilangi ambaye amekula kiapo cha uaminifu, aliteuliwa na Rais Dkt. John Pombe Mgufuli,  Februari Mosi, 2018 na Paul Ngwembe aliteuliwa kuwa Naibu Mwanasheria Mkuu wa Serikali.
Katika hatua nyingine,Magufuli alimtea aliyekuwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali, George Masaju na naibu wake, Gerson Mdemu kuwa Majaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania ambao waliapishwa juzi Jumamosi, Ikulu jijini Dar es Salaam.

Tunda Awekwa Kitimoto na Familia Yake Kisa Video Yake na Kinje Wakiwa Kwenye Mahaba Mazito Kusambaa

$
0
0
Tunda Awekwa Kitimoto na Familia Yake Kisa Video Yake na Kinje Wakiwa Kwenye Mahaba Mazito Kusambaa
Kufuatia sakata la video akiwa anafanya vitendo vya kimahaba na mume wa mtu, Kinjekitile Kingunge ‘Kinje’ kusambaa mitandaoni hivi karibuni, muuza sura katika video mbalimbali za wasanii wa muziki Bongo, Tunda Sebastian amejikuta akiwekwa kitimoto na familia yake.

Uchunguzi wa gazeti hili kupitia kwa rafiki wa karibu na Tunda ulionesha kwamba baada ya video hiyo kusambaa ilikuwa ni patashika nguo kuchanika kwani wazazi wake walikasirishwa mno na kitendo hicho, ndipo wakamweka kitimoto japokuwa hadi sasa hajakaa nao sawa.

“Familia ya Tunda ilimweka kitimoto mwanadada huyo na kumsema sana ambapo aliahidi kwamba atabadilika na akawaangukia wazazi wake na kuwaomba msamaha licha ya kuwa haikuwa kazi rahisi kwa kweli,” alisema rafiki huyo.

Ijumaa Wikienda lilimtafuta Tunda ambaye alieleza kuwa, baada ya video hiyo kuvuja kulitokea mtafaruku mkubwa kwa wazazi wake huku mpenzi wake akikasirishwa na kitendo hicho na hadi sasa hazungumzi naye.

“Nimejifunza sana maana ile video imenivuruga sana kwa kweli kwani wazazi wangu walikasirika sana, mpenzi wangu mpaka sasa haongei na mimi ila bado ninaendelea kumwelewesha kwamba ile ilikuwa ni pombe tu.

“Naamini hasira zake zikiisha atanitafuta tu maana najua ananipenda, nimekoma kunywa pombe na nimeshaacha kabisa kwa kweli,” alisema Tunda.



Video hizo zilikuwa gumzo mitandaoni kabla ya Kinje kufiwa na baba yake, Mzee Kingunge hivyo watu kuacha suala hilo kwani ni kumuongezea maumivu juu ya maumivu.

Siri Yavuja..... Kumbe Dokii Alikua Aolewe na Marehemu Mowzey Radio

$
0
0
Siri Yavuja..... Kumbe Dokii Alikua Aolewe na Marehemu Mowzey Radio
UKIPEWA ubuyu wa Zenji sharti uumun’gunye wenyewe mdomoni bila kitu kingine. Kufuatia kifo cha mwanamuziki wa Uganda, Mowzey Radio kilichojiri mwishoni mwa wiki iliyopita, ubuyu wa motomoto mjini unabumburua kwamba, kumbe mkongwe wa maigizo Bongo, Ummy Wenslaus ‘Dokii’ alikuwa aolewe na jamaa huyo.

Ubuyu huo uliochambuliwa vyema na Ijumaa Wikienda ulidadavua kwamba, Dokii alikuwa na uhusiano wa siri wa kimapenzi na Radio ambaye pia alikuwa ni prodyuza maarufu wa muziki nchini Uganda.
RAFIKI WA KARIBU ATHIBITISHA

Rafiki wa karibu wa Dokii alilithibitishia gazeti hili kuwa, Dokii na Radio walikuwa na uhusiano wa kimapenzi na kwamba walikuwa wakipendana mno.

Uchunguzi wa gazeti hili ulibaini kwamba, kuna kipindi Radio alitimba Bongo kwa ajili ya ziara ya kimuziki ambapo alifikia nyumbani kwa Dokii, Kigamboni jijini Dar.

“Ninajua kabisa Dokii atakuwa ameumizwa sana na kifo cha Radio ingawa hawezi kuweka wazi kwa kila mtu, lakini kiukweli ameumia sana,” alisema rafiki huyo wa Dokii.




Msambaza ubuyu huyo aliendelea kutiririka kuwa, kuna kipindi Dokii alishika ujauzito wa Radio na marafiki zake wote wakajua.

“Wakati Dokii akiwa mjamzito kulitokea kutokuelewana kati yao na hapo ndipo mimba ikayeyuka, lakini kama si hivyo sasa hivi Dokii angekuwa na mtoto wa Radio,” alizidi kumwaga ubuyu rafiki huyo na kuongeza:

“Walikuwa kwenye hatua za mwanzo za kuoana maana Dokii alikuwa hakauki Kampala (Uganda).”

TUMFUATE DOKII KIGAMBONI

Baada ya kupata ubuyu huo, Ijumaa Wikienda lilisaga soli hadi Kigamboni kumsaka Dokii ili aeleze ukweli juu ya jambo hilo ambapo alipopatikana, mambo yalikuwa hivi;

Ijumaa Wikienda: Dokii mambo vipi? Nilidhani upo Uganda!

Dokii: Uganda? Kuna nini huko?

Ijumaa Wikienda: Si kwenye mazishi wa Mowzey Radio?
Dokii: Jamani we’ acha tu, aisee ameniuma sana yule kaka, sijaenda, lakini unajua yule jamaa tumesoma shule moja ya muziki Uganda, tunafahamiana vizuri sana.

Ijumaa Wikienda: Nilijua usingekosa kwenda kwani kuna taarifa kuwa pia alikuwa mchumba wako!

Dokii: (anaguna) nani amekuambia? Kweli ninyi ni mapaparazi. Ndiyo ilikuwa hivyo, lakini hapa juzikati tulikuwa mbali kidogo maana tuligombana.

Ijumaa Wikienda: Kuna madai kuwa uliwahi kushika mimba yake, je, hilo likoje?



Dokii: Uwii…vitu hivyo nani amekuambia? Ilikuwa hivyo, lakini tumuache apumzike sasa.

Radio alikutwa na umauti mwishoni mwa wiki iliyopita baada ya kupoteza fahamu kwa siku kadhaa kufuatia kupigwa na baunsa alipokuwa klabu jijini Kampala, Uganda. Alitarajiwa kuzikwa wikiendi iliyopita jijini humo.

Mgombea Udiwani wa Chadema Aliyepotea Toka Februari 2, Apatikana Katika Mazingira ya Kutatanisha

$
0
0
Mgombea Udiwani wa Chadema Aliyepotea Toka Februari 2, Apatikana Katika Mazingira ya Kutatanisha
Mgombea udiwani (Chadema) Kata ya Buhangaza, Mchungaji Athanasio Makoti (28) aliyepotea Februari 2,2018 katika mazingira ya kutatanisha amepatikana akiwa hajitambui.

Makoti amepatikana leo Februari 5,2018 saa moja asubuhi, Katibu wa Chadema wilayani Muleba, Elisha Kabombo akisema alitelekezwa na watu wasiojulikana jirani na Hospitali ya Kagondo.

Amesema wananchi waliokuwa wakipita eneo hilo usiku wa kuamkia leo walimuona akiwa kando mwa  barabara ya kuelekea Bukoba, hivyo kumpeleka hospitali.

“Hali yake si nzuri kwa sababu hawezi kuzungumza vyema wala kuketi. Kawekewa dripu za maji. Tuzidi kumuombea,” amesema.

Kaimu Kamanda wa Polisi mkoani Kagera, Isack Msangi amethibitisha kupokea taarifa za kupatikana mgombea huyo. Amesema vyombo vya dola vinamhoji ili kuendelea na uchunguzi.

Mganga Mkuu wa Hospitali ya Kagondo, Dk Humphrey Batungi alipoulizwa afya ya mgombea huyo amesema ni mapema kuzungumza.

“Ninaelekea kwenye kikao nitafute mchana baada ya dawa anazotumia mgonjwa kufanya kazi na huenda akawa na mabadiliko,” amesema Dk Batungi.

Kaimu Kamanda wa Polisi mkoani Kagera, Isack Msangi amethibitisha kupokea taarifa za kupatikana kwa mgombea huyo. Amesema vyombo vya dola vitafanya mahojiano naye ili kuendelea na uchunguzi.

Katibu wa uenezi wa Chadema jimbo la Muleba Kusini na mratibu wa chama hicho jimbo la Muleba Kaskazini, Hamisi Yusufu amesema baada ya kufikishwa hospitali alikutwa na majeraha, huku akizungumza kwa shida.

Amesema mgombea huyo wa udiwani aliwaeleza amenyang’anywa fedha, waliomteka walimfunga kitambaa cheusi usoni na kumtaka asigombee uchaguzi utakaofanyika Februari 17,2018 na amekiri  kuwafahamu baadhi ya waliomteka.

Katika uchaguzi huo anachuana na mgombea wa CCM, Jenitha Tibeyenda na wa NCCR-Mageuzi, Grason Anaseti.

Mama Mzazi wa Sugu Afunguka Mazito Kushikiliwa kwa Mwanaye

$
0
0
Mama Mzazi wa Sugu Afunguka Mazito Kushikiliwa kwa Mwanaye
Mama mzazi wa Mbunge wa Mbeya Mjini Joseph Mbilinyi 'Sugu' amefunguka mazito kuhusu kushikiliwa kwa mtoto wake kwa kile kinachodaiwa kutoa lugha ya fedhea kwa Rais  na kusema yeye haoni kama amefanya kitu cha ajabu kwani hivyo ndivyo alivyo Sugu.


Mama mzazi wa Sugu alisema hayo Februari 4, 2018 alipotembelewa nyumbani kwake na Mbunge wa Arusha Mjini (CHADEMA) Godbless Lema na  Mbunge wa Tandahimba (CUF), Katani Katani ambapo kwa pamoja walikwenda kumtembelea Mbunge Sugu gerezani.

"Miaka mingi sana toka yupo hapa anaimba miziki yake na kusemea matatizo ya nchi hii kwa hiyo hatushangai sana, mimi sioni kama amefanya kitu cha ajabu kwani hivyo ndivyo alivyo toka utoto wake ndiyo maana tulimwita Joseph mfanyakazi maanake ni mfanyakazi bora. Lakini anatetea haki kwa binadamu wenzie kuanzia yeye mwenyewe, watoto zake hata wajukuu zake watapata haki, anachotenda ni halali sana na hakuna tofauti" alisisitiza Mama yake na Sugu

Mbunge wa Mbeya Mjini Mhe. Joseph Mbilinyi na Katibu wa CHADEMA Kanda ya Nyasa Emmanuel Masonga Januari 25, 2018 walirudishwa rumande tena na kesi yao itaendelea Februari 8, 2018. Viongozi hao wanashtakiwa kwa kesi ya uchochezi.

Chadema Nao Wasimamisha Kampeni za Uchaguzi wa Marudio

$
0
0
Chadema Nao Wasimamisha Kampeni za Uchaguzi wa Marudio
Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) leo Februari 5, 2018 kimesimamisha kampeni za uchaguzi wa marudio ili kushiriki shughuli ya maziko ya Mwanasiasa mkongwe Kingunge aliyefariki dunia Februari 2, 2018 katika Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH)


Mwenyekiti wa CHADEMA Taifa, Freeman Mbowe amesema hayo leo na kuwakaribisha wanachama mbalimbali wa CHADEMA kushiriki katika mazishi ya kiongozi huyo

"Kwa heshima ya Mzee wetu Kingunge, leo Jumatatu 05/02/2018 CHADEMA haitafanya mikutano ya kampeni ili kushiriki shughuli ya maziko ya baba yetu, mpiganaji aliyechagua kuyapigania bila woga mabadiliko ya kweli hapa nchini. Tutatoa heshima za mwisho na kuuaga mwili wa Kingunge Karimjee na baadae kwenye kumpumzisha Mzee wetu kwenye makaburi ya Kinondoni" alisema Mbowe

"Wananachama wa CHADEMA, wapenzi, mashabiki na wananchi wote kwa ujumla mnakaribishwa kumsindikiza baba yetu katika safari yake ya mwisho"

Bwana ametoa, Bwana ametwaa jina lake lihimidiwe, Amina.



Maneno ya Ridhiwani Kufuatiwa Kifo cha Kingunge “Nimeamka Katika Usingizi, Najiuliza Niandike?”

$
0
0
Maneno ya Ridhiwani Kufuatiwa Kifo cha Kingunge “Nimeamka Katika Usingizi, Najiuliza Niandike?”
Bado watanzania na wanasiasa mbalimbali wapo katika majonzi na maombolezo ya kifo cha mwanasiasa mkongwe ambaye pia amewahi kuwa kiongozi wa serikali Kingunge Ngombale Mwiru ambaye atazikwa leo February 5 2018.

Mbunge wa Chalinze Ridhiwani Kikwete ni moja kati ya wanasiasa waliyoguswa na msiba wa mzee Kingunge na ameamua kutumia ukurasa wake wa instagram kuandika ujumbe huu.

“Nimeamka katika Usingizi nimemkumbuka Mzee Kingunge. Kwangu mimi huyu Mwalimu wa Itikadi ya Siasa ya Ujamaa na Kujitegemea atabaki kuwa Mwalimu. Najiuliza niandike au niache yabaki kifuani kwangu”

“Iko upande wa nafsi yangu unaniambia niandike kwa yale ninayofahamu kuhusiana na mzee kingunge na huko nafasi unaniambia nisubiri tukuhifadhi kwa nyumba ya milele ili niandike”

“Nitaandika tu……Ulikuwa Mzazi, Mlezi, mtuliza maumivu,rafiki , mcheshi na Uliyeamini katika kile unachokiamini.haukukamilika kama walivyokuwa wengine. ……Nitaandika Ngoja Tukuhifadhi Coming Soon…..Nitaandika”

Habari Njema: Tunatibu Busha, Korodani Kuvimba, Ngiri, Miguu Kufa Ganzi Pamoja na Matatizo ya Nguvu za Kiume

$
0
0
Ni dawa ya nguvu za kiume inayorefusha na kunenepesha uume saizi uipendayo (Inch 1-7) kwa muda wa siku 6 tu.Dozi hii itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa muda wa dakika 30, utarudia tendo la ndoa zaidi ya mara 4 bila hamu kuisha bila kujali umri na garantee ni miaka 60 baada ya kutibu tatizo.

Pia tunatibu Busha bila kufanyiwa Oparesheni, korodani moja kuvimba, ngiri, tumbo kujaa gesi na kuunguruma, kutopata choo vizuri, miguu kuwaka moto na kufa ganzi, chango la wanawake, kisukari na kutokwa na kinyama sehemu ya haja kubwa.

MIHAYO:
Inarudisha mke, mchumba, hawara na atakutimizia kila kitu unachotaka kutoka kwake ndani ya  saa 2 tu hata kama yupo mbali. atarudi na kumfunga asiwe na mwingine zaidi yako.

Umefukuzwa kazini? unataka kupandishwa cheo? Umepoteza pesa zako kwenye biashara bila kujua umepandikizwa chuma ulete? Njoo urudishe pesa zako. Unauza mali yako haiendi?


Wasiliana na mtaalam Challo kwa; 0714006521

Meya wa Iringa Apandishwa Kizimbani kwa Kosa la Kutishia Kuua

$
0
0
Meya wa Iringa Apandishwa Kizimbani kwa Kosa la Kutishia Kuua
Kesi ya kutishia kuua kwa bastola inayomkabili Meya wa Manispaa ya Iringa, Alex Kimbe inatarajiwa kuanza kusikilizwa leo.

Shauri hilo lililopo katika Mahakama ya Wilaya ya Iringa linaanza kusikilizwa leo Jumatatu Februari 5,2018 baada ya wiki iliyopita kuelezwa kuwa upelelezi umekamilika.

Katika kesi hiyo namba 189 ya mwaka 2017, Kimbe anadaiwa kutishia kumuua Alphonce Muyinga, ambaye ni katibu wa Umoja wa Vijana wa CCM (UVCCM).

Anadaiwa Novemba 26,2017 katika Kata ya Kitwiru ndani ya Manispaa ya Iringa wakati wa uchaguzi mdogo wa udiwani alitishia kumuua Muyinga kwa bastola kinyume cha sheria.

Shauri hilo linasikilizwa mbele ya Hakimu Mkazi, John Mpitanjia.
Viewing all 104712 articles
Browse latest View live




Latest Images