Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104414 articles
Browse latest View live

Serikali ya Kenya Yamfukuza kwa Nguvu Kiongozi wa Upinzani

0
0
Serikali ya Kenya Yamfukuza kwa Nguvu Kiongozi wa Upinzani
Serikali ya Kenya imemfukuza kwa nguvu na kumsafirisha kwenda nchini Canada mmoja wa viongozi wa upinzani Kenya, Miguna Miguna usiku wa kuamkia leo Februari 8 baada ya mahakama kudai aachiwe huru.

Katika akaunti ya Twitter ya Serikali inayofahamika kwa jina la ‘Nexus’ iliandika katika ukurasa huo Februari, 6 saa 7:19 usiku kuwa Miguna anaelekea nyumbani Canada baada ya mahakama kuamuru aachiwe.

Serikali imeandika kuwa Wizara ya Ulinzi ilitii agizo hilo na kumpatia tiketi ya kwenda nyumbani kwake Canada ambapo ana uraia wa nchi hiyo alioupata Juni 16, 2017.

“Miguna ameelekea nyumbani. Mahamakma iliamuru aachiwe na Wizara ya Ulinzi imetii amri na imempatia tiketi ya kwenda nyumbani. Tafadhali tunasisitiza alipatiwa kibali cha kuishi Canada Juni, 16 2017” umeandika ukurasa huo.

Miguna amesafirishwa na Shirika la Ndege la KLM ambalo lilipoulizwa na wananchi katika ukurasa wao wa Twitter unaofahamika kwa jina la ‘Royal Dutch Airline’ walipendekeza maswali yote waulizwe mamlaka husika kwa sababu za kiusalama.

Miguna alishikiliwa na Polisi Februari, 2 kwa tuhuma za kushiriki kuapishwa kwa Raila Odinga kama Rais wa watu wa Kenya Januari, 30.

Mwanasheria wa Miguna, Dk John Khaminwa amesema mteja wake kwasasa hayupo nchini humo.

“Ni kweli. Ameondolewa kwa nguvuy na ndege ya KLM na tunasikia ameelekea Canada. Ni uvunjaji wa haki” amesema Khaminwa.

Kuhusu sakata la uraia wake, Dk Khaminwa amesema Miguna aliukana uraia wa Kenya ila miezi miwili kabla ya uchaguzi mkuu aliomba tena.

“Miguna alipokamatwa Serikali ya Canada iliiandikia barua Kenya kuelezea kuwa mwananchi wao ananyanyaswa,” amesema Khaminwa.

Katika kipande kifupi cha video kinachosambaa mtandaoni kimemuonyesha kiongozi huyo akiwa katika ndege na amevalia suti, barakashia akiwa peke yake siti za mbele.


Mkurugenzi wa Benki ya Wanawake Mikononi mwa Takukuru

0
0
Mkurugenzi wa Benki ya Wanawake  Mikononi mwa Takukuru
WAFANYAKAZI 20 akiwamo aliyekuwa Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Wanawake Tanzania (TWB), Magreth Chacha, wamefikishwa kwenye vyombo vya dola vikiwamo Jeshi la Polisi na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) kwa tuhuma za kukosa uadilifu na kuisababishia benki hiyo hasara.

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu, alitoa kauli hiyo bungeni jana alipokuwa akijibu swali la nyongeza la Mbunge wa Viti Maalum (CCM), Faida Mohammed Bakar, aliyetaka kujua ni hatua gani za kisheria wamechukuliwa viongozi wa TWB kwa kukosa uadilifu.

“Mheshimiwa Waziri umekiri uadilifu hakuna katika benki hiyo na kwamba mnataka kuteua maofisa mbalimbali waadilifu jambo ambalo limedhihirisha kukosekana kwa uadilifu kwa viongozi. Je, hakuna viongozi waliochukuliwa hatua? Alihoji mbunge huyo.

Aidha alisema katika uanzishaji wa benki hiyo, wabunge wengi walichangia mtaji hususan wanawake, lakini hawajapewa shukrani hata ya kutambulika na kuhoji lini watapatiwa barua ya utambulisho na hisa zao.

Akijibu maswali hayo, Waziri Mwalimu alisema watumishi hao waliokosa uadilifu wamechukuliwa  hatua kuanzia Agosti, mwaka jana.

Alisema watumishi hao wamekosa uaminifu na kusababisha benki kupata hasara.

“Kuna mambo yamefanyika ya ovyo utakuta kuna Saccos imekopeshwa Sh. bilioni moja wanaifuatilia hiyo Saccos, hazionekani hizo fedha zimeenda kwa nani. Nataka kumhakikishia Mheshimiwa Faida kwamba tunaamini PCCB (Takukuru) na polisi watakamilisha uchunguzi haraka lengo ni watumishi hao waende vyombo vya dola na kuchukuliwa hatua,”alisema waziri huyo.

Mwalimu pia alisema serikali imedhamiria kuhakikisha wanapata fedha ya kukuza mtaji wa benki hiyo.

 “Tumepewa miezi sita na BoT (Benki Kuu Tanzania). Nawahakikishia wabunge kuwa Mkurugenzi mpya tuliyemwajiri amefanya kazi kubwa na ingawa ni Benki ya Wanawake tumemwajiri mwanamume ambaye ndani ya miezi mitano amefanya kazi kubwa sana ya kuhakikisha angalau hesabu za benki zinakaa  vizuri,” aliongeza waziri huyo.

Hata hivyo, alikiri kuwa wanatambua mchango wa wabunge wa Bunge la tisa ambao walinunua hisa kwa ajili ya kukuza mtaji wa benki na kwamba watapewa vyeti vyao vya hisa siku chache zijazo baada ya kukamilisha matakwa ya BoT.

Katika swali la msingi, Mbunge huyo alitaka kujua ni lini benki hiyo itaanzisha tawi lake Zanzibar kwa madhumuni ya kuwapatia huduma za kibenki na mikopo yenye riba nafuu kuwainua kiuchumi wajasiriamali wanawake.

Akijibu swali hilo, Naibu Waziri wa wizara hiyo, Dk. Faustine Ndugulile, alisema benki hiyo ilianza mwaka 2009 na mpaka sasa imefungua matawi mawili yaliyoko jijini Dar es Salaam  na vituo vya kutolea mikopo na mafunzo 305 katika mikoa ya Dar es Salaam, Mbeya, Njombe, Iringa, Mwanza, Ruvuma na Dodoma.

Aidha alisema hatua mbalimbali zinaendelea kuchukuliwa, ili kuhakikisha benki inajiendesha kwa ufanisi na kukuza mtaji ikiwamo kufanya mabadiliko kwa kuweka uongozi na watumishi waadilifu.

Ripoti ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) ya mwaka 2015/16, inabainisha kuwa benki hiyo ilitoa mikopo yenye jumla ya Sh. milioni 655 bila kufuata taratibu, ikiwamo kuthibitisha uwapo wa kampuni zilizokopeshwa.

Pia ilibainika kuwa hakuna dhamana iliyowekwa kwa mkopo wa Sh. milioni 200 iliyotolewa.

Kadhalika, ripoti hiyo ya CAG ilisema hakuna ushahidi unaoonesha kuwa uthamini ulifanyika kwa dhamana zilizowekwa dhidi ya mikopo yenye jumla ya Sh. milioni 330 na mikopo ya Sh. milioni 355 ilitolewa kwa wateja ambao muda wa matumizi ya leseni zao za biashara ulikwishamalizika.

Msajigwa Ashindwa Kuwaelewa Simba, Azam

0
0
Msajigwa Ashindwa Kuwaelewa Simba, Azam
Kocha Msaidizi wa klabu ya Yanga, Shadrack Msajigwa ameogopa kuongelea mechi ya watani wao wa jadi Simba dhidi ya Azam FC, kwa kudai wao wanajiangalia wenyewe na wala sio timu nyingine japokuwa lazima uwepo ushindani kwenye ligi.


Msajigwa amebainisha hayo baada ya kuulizwa swali kuhusiana na mchezo wa leo, ambao ni muendelezo wa mashindano ya 'VPL' utakaochapwa katika dimba la Taifa kwamba angependa timu gani itoke na ushindi dhidi ya mwenzake jambo ambalo kwake ameshindwa kulitolea majibu ya uwazi.

"Sisi mara zote tunajiangalia wenyewe japokuwa lazima kuwepo na ushindani lakini zile ni timu zinashindana na zipo kwenye Ligi Kuu Tanzania Bara kama zilivyo nyingine, kwa hiyo tunawaachia wao. Mtu ambaye atakaepoteza mchezo wa leo anazidi kujididimiza na nasi ndio tunasonga mbele", amesema Msajigwa.

Pamoja na hayo, Msajigwa amesema "kama tutakuwa tunaendelea kupata matokeo haya kila mechi na wenzetu wakipata mabaya basi itakuwa neema kwetu ila sisi tunawatakia mchezo mwema".

Kutokana na ushindi waliyoyapata jana (Jumanne) Yanga wa mabao 4-0 dhidi ya Njombe Mji wameweza kuishusha Azam katika msimamo wa Ligi na kukamata nafasi ya pili kwa alama 34, huku tofauti kati yake na vinara Simba ikiwa pointi 4 pekee.

Simba, Azam Kuonyeshana Ubabe Taifa Leo

0
0
Simba, Azam Kuonyeshana Ubabe Taifa Leo
WAKATI leo Jumatano Simba ikitarajiwa kuwa wenyeji wa Azam FC katika mchezo wa Ligi Kuu Bara, straika wa timu ya Simba, John Bocco amefunguka kuwa kwenye mchezo huu wanashuka dimbani wakiwa na lengo moja la kupata matokeo mazuri.

Mshambuliaji huyo mwenye mabao tisa kwenye ligi, ataiongoza timu yake hiyo ya Simba kucheza na Azam ambao wanashika nafasi ya pili kwenye msimamo wa ligi kwenye mchezo ambao utapigwa Uwanja wa Taifa, Dar.

Akizungumza na Championi Jumatano, straika huyo alisema: “Hakuna cha kupoteza kwenye mchezo huu, tunataka tushinde kwa ajili ya kuendeleza rekodi yetu iliyopita kwenye mechi tano ambazo zote tuliibuka na ushindi.

“Tunajua wapinzani wetu ni wazuri na wenye timu yenye ushindani lakini kwetu hatutaangalia hilo, kikubwa tunajipanga kupata matokeo mazuri mbele yao na wote kwa pamoja tunaamini tutalikamilisha hilo kwa umoja wetu,” alisema.

Hadi sasa Simba ndiyo vinara wa ligi wakiwa na pointi 38 baada ya mechi 16 za ligi kuu wakifuatiwa na Azam ambao wanashika nafasi ya pili wakiwa na pointi 33.

Yanga Sasa Yachoka Majeraha ya Ngoma Yaandaa Kamati ya Kumtema

0
0
Yanga Sasa Yachoka Majeraha ya Ngoma Yaandaa Kamati ya Kumtema
NI wazi sasa klabu ya Yanga imechoshwa na hali ya majeraha ya muda mrefu kwa mchezaji wake, Donald Ngoma, na sasa klabu hiyo inafikiria kusitisha mkataba na Mzimbabwe huyo, imeelezwa.
Katibu Mkuu wa Yanga inayodhaminiwa na Kampuni ya Kubashiri Matokeo Michezoni ya SportPesa, Charles Mkwasa, akizungumza jijini Dar es Salaam jana, alikiri kuwa nyota huyo amekuwa majeruhi wa mguu kwa muda mrefu na kwa sasa klabu hiyo inafikiria kuhitimisha mkataba wake kama itaonekana hataweza kurejea uwanjani hivi karibuni.

"Ipo kamati itafuatilia kwa karibu mustakabali wa afya yake, huwezi kumlipa mshahara mchezaji ambaye haitumikii klabu, tutafuatilia kwa karibu afya yake kwa kupitia ripoti ya madaktari na baadaye tutajua nini cha kufanya," alisema Mkwasa.

Mkwasa, alisema wachezaji wengine ambao walikuwa majeruhi wamepata ripoti zao na wanaendelea vizuri akiwamo Thaban Kamusoko na Amissi Tambwe.

Kauli hiyo ya Mkwasa, iliungwa mkono na Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili ya klabu hiyo, Hussein Nyika, ambaye alisema ndani ya siku mbili watatoa msimamo wao juu ya mshambuliaji huyo mara baada ya kupokea taarifa ya madaktari.

"Ndani ya siku mbili tutajua nini cha kufanya, hatuwezi kukatisha ghafla mkataba wa mchezaji, tunasubiri ripoti ya madaktari kufahamu nini cha kufanya kama tutaambiwa hawezi (Ngoma) kurejea uwanjani hivi karibuni, hapo tutaangalia mengine kwa sababu huwezi kumlipa mshahara mchezaji ambaye hawezi kuitumikia klabu, analipwa kutokana na kucheza," alisema Nyika.

Ngoma, amekuwa na kipindi kigumu msimu huu baada ya kukosa sehemu kubwa ya msimu huu mpaka sasa, licha ya awali kuelezwa kuwa amepona majeraha yake wakati alipokwenda kujitibia nyumbani kwao Zimbabwe, na badala yake alicheza mechi tatu tu kabla ya kujitonesha tena na kukaa nje mpaka sasa.

ANC Yaahirisha Mkutano wa Kujadiri Hatima ya Zuma

0
0
ANC Yaahirisha Mkutano wa Kujadiri Hatima ya Zuma
Chama tawala nchini Afrika Kusini, ANC kimeahirisha mkutano wa viongozi wa juu wa chama hicho uliotarajiwa kujadili hatima ya Rais Jacob Zuma.

Rais Zuma yupo katika shinikizo kubwa ambalo linatoka ndani ya chama chake ambalo linamtaka ajiuzulu kufuatai kashfa ya ufisadi.

Mkutano wa kamati kuu ya chama hicho NEC unatarajiwa kufanyika siku ya februari 17 na 18 kwa mjibu wa taarifa iliyotolewa na kiongozi wa chama hicho cha ANC, Cyril Ramaphosa.

Hata hivyo badala yake taarifa iliyotolewa na chama hicho imeeleza kuwa wamekuwa na mazungumzo yenye ufanisi mkubwa na rais Zuma.

Baadhi ya mitandao nchini humo imekuwa ikieleza Rais Zuma anajiandaa kuachia madaraka iwapo makubaliano yatafikiwa na pande zote mbili.

Nafasi za Ajira Zilizotangazwa Leo Jumatano

0
0

Miujiza ya Sharifu Seif Mohamed..JE Umeachwa na Mme/Mke au Mpenzi, Umesongwa na Mitihani ya Maisha..Piga Simu Upate Muujiza Wako

0
0
SHARIFU SEIF MOHAMED ANAWASHUKURU WALE WOTE WANAOENDELEA KUPIGA SIMU, WENYE MATATIZO NA WALE WANAOTOA  SHUKRANI NA SHUHUDA JINSI TIBA ZAKE ZINAVYO WASAIDIA,

(Rudisha mahusiano yako ndani ya masaa 72 tu)

SHARIFU MOHAMED Ni  mtaalam na mnajimu maarufu wa nyota na kubashiri mambo yanayo watesa binadamu duniani kote na kupata ufumbuzi, Anatumia kitabu cha QUR'AN, Dawa za Asili, Dawa za Kiarabu na majini kwa kumtuliza mke/mme, mchumba au mpenzi ndani ya masaa 72 tu, na kutatua matatizo yote ya kimaisha,

Je Umeachwa na UMPENDAE awe Mme/Mke na bado unampenda? Je Umekimbiwa na Mmeo/ Mkeo n anaishi na mtu mwingine? Je Umejaribu sehemu nyingi bila mafanikio? Mpigie simu SHARIFU SEIF sasa hivi ujionee Muujiza wa Papo kwa Papo, Anauwezo wa hali ya juu wa kusambaratisha mahusiano yao na kumrejesha kwako haraka sana na Kumfanya Atimize Ahadi zote Ndani ya Muda Mfupi Endapo Utafwata Atakacho Kuelekeza

ANAZO DAWA ZA MAPENZI, NGUVU ZA KIUME, CHANGO NGIRI MAJI NA N.K, ZINDIKO LA NYUMBA NA BIASHARA, PETE ZA BAHATI, HUMALIZA KABISA TATIZO LA NGUVU ZA KIUME NA KUREFUSHA UUME KWA SAIZI UNAYOTAKA, HUZUIA CHUMA ULETE KWENYE BIASHARA, HURUDISHA MALI ZILIZOPOTEA, MAGONJWA SUGU, MIGUU KUWAKA MOTO AU KUFA GANZI, HUTIBU BUSHA BILA KUPASUA, ANAO UWEZO WA KUMRUDISHA ALIE MBALI AU ALIECHUKULIWA MSUKULE, KUPANDISHA NYOTA NA KUSHINDA BAHATI NA SIBU, KASAFISHA NYOTA NA KUKUPA MVUTO WA AJABU, KUTOA NUKSI NA VIFUNGO MBALIMBALI,  MAFANIKIO YA MAISHA NA UTAJIRI BILA MASHARI, NA MENGINE MENGI YA SIRI,

JE UMAHANGAIKA KUPATA MTOTO BILA MAFANIKIO? WASILIANA NA MTAALAMU HUYU KWANI YEYE HUFAULU PALE WOTE WALIPOSHINDWA, PIA UMALIZA KAZI ZILIZO SHINDIKANA NA WATAALAM WENGINE NDANI YA MASAA 24 TU,

(NA ANATIBU KWA NJIA YA SIMU UKIWA NCHI YOYOTE AU MKOA WOWOTE ENDAPO UTAFWATA MAELEKEZO YAKE)

Kwa ushauri na mawasiliano  zaidi Piga SIMU No:

Mobile +255 654-836970
WhatsApp +255 756-033670

Meneja wa Diomond Afunguka Kuhusu Nyama Zilizowekwa Ili Kumshusha Diamond

0
0
Meneja wa Diomond Afunguka Kuhusu Nyama Zilizowekwa Ili Kumshusha Diamond
Meneja wa msanii wa muziki Diamond Platnumz, Sallam SK amefunguka kwa kudai kwamba kuna watu wanataka kumshusha msanii huyo ambaye anafanya vizuri kwa sasa na wimbo, ‘Waka’ aliomshirikisha Rick Ross.


Sallam amedai kwamba hakuna mtu wakumshusha muimbaji huyo kwa hasa hasa kwenye utawala huu wa Rais John Pombe Magufuli.

“Kumbe tatizo ni kumpoteza huyu kijana?(Diamond) Waambie familia yako na wazazi waliyokuleta katika haya maisha huyu mtoto kaletwa kwa makusudi maisha haya, ili kuleta ukombozi wa dhuluma uliyokuwa unaleta kwenye Taifa hili, unatakiwa kujua Kwanza hili Taifa sasa Rais anaitwa John Pombe Magufuli,” aliandika Sallam kupitia instagram yake.

Habari ambazo zipo mtaani zinadai kwamba wasanii wa label hiyo hawapati airtime kama kipindi cha nyuma hali ambayo inatishia biashara ya wasanii hao.

Serikali Yaahidi Kuboresha Mishahara ya Walimu

0
0
Serikali ya Tanzania imeahidi kuanza kuboresha maslahi ya watumishi ya walimu ikiwemo mishahara yao kipindi hiki kutokana na kumaliza zoezi la muda mfupi la uhakiki wa wafanyakazi hewa katika sehemu mbalimbali za ajira.


Hayo yamewekwa wazi na Naibu Waziri Ofisi ya Rais-TAMISEMI George Joseph kakunda leo (Jumatano) katika mkutano wa 10 kikao cha saba cha Bunge kinachoendelea mjini Dodoma wakati alipokuwa akijibu swali la nyongeza kutoka kwa Mbunge wa Karagwe Innocent Bashungwa alipotaka kujua ni lini serikali itawapandishia mishahara walimu.

"Utaratibu huu ambao ulikuwa umesimama kwa kipindi kifupi cha miaka kama miwili hivi kupisha uhakiki wa watumishi ambapo ni zoezi lililofanywa kwa umahiri na ueledi mkubwa, baada ya kuwa tumelikamilisha sasa tutaingia kwenye awamu ambayo ni ya kuboresha maslahi ya watumishi ikiwemo mishahara yao", amesema Kakunda.

Kwa upande mwingine, Mhe. kakunda amewatoa hofu walimu wote ambao hawakupandishwa madaraja yao kutokea mwaka 2016 hadi 2017 na kudai katika mwaka huu wa fedha wameshafanya matayarisho wa kupandisha madaraja hayo.

Serikali ya Kenya Yawafutia Pasipoti za Kusafiria Maofisa 15 wa Nasa

0
0
 Serikali ya Kenya Yawafutia Maofisa 15 wa Nasa Pasipoti za Kusafiria
 Serikali imeamua kusitisha hati za kusafiria za viongozi kadhaa wa ngazi ya juu na wanasiasa wafuasi wa muungano wa upinzani wa Nasa ikiwemo ya gavana wa Mombasa, Hassan Joho.

Mbali ya Joho, wanasiasa wengine waliositishiwa hati zao za kusafiria ni seneta wa Siaya, James Orengo na seneta wa zamani wa Machakos, Johnson Muthama.

Mpangaji mkuu wa mikakati wa muungano huo, David Ndii pamoja na mfanyabiashara Jimi Wanjigi pia hawakuachwa katika mkumbo huo wa serikali kuzidisha kibano kwa wanasiasa wa upinzani baada ya hatua yao ya "kumuapisha” mgombea wao wa urais katika uchaguzi wa mwaka jana Raila Odinga kuwa "rais wa watu" ikiwa ni ishara ya kutotii serikali.

Katika barua waliyopelekewa viongozi hao wanaodaiwa kufikia 15, Mkurugenzi wa Uhamiaji, Gordon Kihalang'wa alisema kusitishwa kwa hati hizo kumefanyika kwa kuzingatia Sheria ya Wananchi na Uhamiaji ya mwaka 2011 inayotoa sababu za kusimamishwa.

Akizungumza na Daily Nation Jumanne, Muthama alisema viongozi kutoka idara ya uhamiaji walitoa barua hiyo ya kumjulisha kuhusu hatua ya kusitishiwa hati ya kusafiria kuanzia saa 7:00.

"Tunaona udikteta ukijitengeneza. Hawaheshimu sheria kwa sababu hili ni shambulio dhidi ya Sheria ya Haki ambayo haiwezi kuachanishwa," alisema.

Seneta huyo wa zamani ambaye pia ni kiongozi wa ngazi ya juu wa upinzani alisikitishwa kwamba njia zisizofaa zinazotumika kwake tayari zimemvuruga.

"Ilikuwa nimsindikize binti yangu Uingereza leo (Jumanne) saa 10:00 alasiri lakini sasa siwezi. Hii ni njia hatari ambayo serikali imechagua na lazima isitishwe," alisema.

Soma: Serikali yamfukuza kiongozi wa upinzani Kenya

Kinara wa Nasa, Kalonzo Musyoka ameelezea kusimamishwa kwa hati za kusafiria kwa viongozi wa juu wa Nasa na kufungwa kwa vyombo vya habari kuwa ni sifa za serikali yenye hofu.

"Hofu ambayo imeingia kwenye utawala huu inaelezea yote. Wanaziba uhuru wa vyombo vya habari kwa sababu hawataki ukweli, na sasa wameamua kuzuia watu kusafiri. Lakini kwa nini wana hofu? Kama wako imara kama wanavyosema, hofu ya nini?"  Aliuliza Musyoka alipokuwa kwenye ofisi za makao makuu ya chama chake cha Wiper jana.

Azam FC: Tumejiandaa Kuhakikisha Tunashinda Mchezo wa Leo

0
0
Azam FC: Tumejiandaa Kuhakikisha Tunashinda Mchezo wa Leo
Klabu ya soka ya Azam FC imesema imejiandaa vyema kuhakikisha inashinda mchezo wake wa leo dhidi ya Simba ili kuendelea kuikimbiza timu hiyo katika mbio za ubingwa kwakuwa wao ndio vinara.


Msemaji wa timu hiyo Jaffary Idd amesema kocha wa timu hiyo Aristica Cioaba ameandaa kikosi chake vizuri kwasababu wanaamini ushindi wa aina yoyote leo utawaweka katika mazingira mazuri ya kusaka ubingwa.

''Ushindi wowote kwa Azam leo maana yake tutakuwa tunamkimbiza kimya kimya kinara wa ligi na yoyote aliyepo juu kwenye msimamo'', amesema.

Aidha kwa upande mwingine Jaffary amesema kuwa wachezaji waliokuwa majeruhi akiwemo nahodha Himid Mao tayari wamepona na kujiunga na timu isipokuwa wawili tu ambao ni Waziri Junior pamoja na Joseph Kimwaga.

Azam FC kwasasa inashika nafasi ya tatu ikiwa na alama 31 nyuma ya Yanga yenye alama 34 na vinara Simba wenye alama 38. Mchezo wa leo utachezwa kwenye uwanja wa taifa jijini Dar es salaam.

Tetemeko la Ardhi Laangusha Maghorofa na Kuua

0
0
Tetemeko la Ardhi Laangusha Maghorofa na Kuua
Taarifa katika vyombo vya habari vya kimataifa leo February 7, 2018 ni kuhusiana na tukio lililotokea katika mji wa Hualien nchi Taiwan ambapo majengo marefu yameporomoka na kusababisha vifo vya watu wawili na wengine zaidi ya 200 wakijeruhiwa huku 150 wakiwa wamepotea.

Majengo hayo yameporomoka baada ya kutokea kwa tetemeko la ardhi katika mji huo lenye kipimo cha 6.4 lililoupiga mji huo wa kitalii usiku wa kuamkia Jumatano ya leo.

Inaelezwa kuwa watu wengi waliokuwa ndani ya majengo hayo bado wamenasa humo na juhudi za kuwanasua zinaendelea. Mji huo unakadiriwa kuwa na wakazi takribani 100,000.

Mwigulu Aongoza Oparesheni ya Kuteketeza Ekari Sita za Bangi

0
0
Mwigulu Aongoza Oparesheni ya Kuteketeza Ekari Sita za Bangi
Waziri wa mambo ya ndani nchini,Mwigulu Nchemba leo ameongoza oparesheni ya kuteketeza jumla ya ekari sita za bangi zilizokuwa zimelimwa katikati ya msitu ndani ya kijiji cha Engalaoni wilayani Arumeru mkoani Arusha.



Mwigulu akishirikiana na kamanda wa jeshi la polisi mkoani Arusha,(RPC)Charles Mkumbo pamoja na vikosi vya askari wa jeshi la polisi mkoani hapa walilazimika kuacha magari yao njiani na kutembea umbali wa kilomita 5 milimani kufika katikati ya msitu huo ambapo wamiliki wa mashamba hayo walitokomea kusikojulikana.

Akizungumza na waandishi wa habari wakati wa zoezi hilo Mwigulu alisema kwamba serikali itaendelea na oparesheni pande zote za nchi na haitasita kuwakamata wahusika wote na kutaifisha magari yatakayotumika kusafirisha bangi.

Akizungumza na askari waliokuwa wakishiriki katika zoezi hilo Mwigulu mbali na kuwapongeza kwa kazi wanayofanya lakini aliwambia kwamba pamoja na kufanikiwa kuteketeza madawa ya kulevya yanayolimwa mashambani lakini waongeze juhudi pia katika kupambana na madawa ya kulevya yanayotengenezwa viwandani.

“Niwapongeze sana songeni mbele na kazi ya kukamata madawa yote ya kulevya mmefanya kazi kubwa sana ya kukabiliana na madawa ya kulevya yanayolimwa mashambani ongezeni bidii kukamata na yale yanayozalishwa viwandani”aliwaambia Mwigulu

Hatahivyo, kamanda wa jeshi la polisi mkoani Arusha(RPC),Charles Mkumbo alisema kwamba jumla ya ekari sita za mashamba ya bangi zimeteketezwa na kusisitiza kwamba oparesheni hiyo ni endelevu katika mkoa wa Arusha na wilaya zake.

Mkumbo,alifichua mbinu mpya wanayotumia wamiliki wa mashamba hayo kwamba kwa sasa wameamua kulima mashamba hayo katikati ya misitu kwa lengo la kujificha ili kukwepa mkono wa sheria.

“Walidhani kulima bangi katikati ya misitu hatutawakamat sisi tuna mbinu nyingi na hatutakubali kuona vijana wetu wanaharibikiwa kwasababu ya bangi”alisema Mkumbo

Trump Ataka Kuonyesha Nguvu Zake za Kijeshi

0
0
Trump Ataka Kuonyesha  Nguvu Zake za Kijeshi
Rais wa Marekani Donald Trump anaripotiwa kuwauliza maafisa wakuu wa jeshi kuandaa gwaride kubwa zaidi nchini humo kuonyesha nguvu zake za kijeshi.

Afisa anayehusika na masuala ya habari katika ikulu ya white house, Sarah Sanders amesema rais Trump amewaagiza wakuu wa jeshi kupanga hafla hiyo ambayo raia wa taifa hilo watatoa shukrani na heshima zao kwa wanajeshi wao.

Ripoti zinasema kuwa rais Trump alifurahishwa mno na sherehe za Bastille nchini Ufaransa, ambako mbali na wanajeshi kuonyesha wanajeshi wake, magari ya kivita na vifaru pia inajumuisha maonyesho ya ndege za wana anga.

Siku ya kuwakumbuka wakongwe wa kivita huadhimishwa tarehe kumi na moja Novemba kila mwaka na inasemekana huenda sherehe hizo zikaandaliwa siku hiyo.

Tayari maeneo matatu ambayo huenda yakafikiriwa kuandaa sherehe hizo yametolewa.

Rais Trump anasemekana kupendekeza sherehe hizo kuandaliwa katika barabara ya Pennsylvania inayoliunganisha bunge la congress na ikulu ya white house na hoteli ya Trump International.

Lakini kuna wasi wasi kuwa baada ya sherehe hizo bara bara hiyo huenda ikaharibiwa kabisa kutokana na uzito wa vifaa vya kijeshi.

Tamasha za kijeshi sio za kawaida nchini Marekani kwa sababu ni ghali.

Sherehe za mwisho za kijeshi kuandaliwa baada ya vita vya ghuba iligharimu serikali dola milioni kumi.

Wanasiasa wa chama cha Democratic wameshutumu mpango huo kwa gharama kubwa na kusema kuwa fikra hizo zinatoa ishara za kutia wasiwasi.

"Ni njia ovyo ya kupoteza fedha!" alituma ujumbe wa twitter mwakilishi Jim McGovern. "Trump anaonekana kuwa dikteta zaidi ya rais , Wamarekani wanastahili kiongozi bora zaidi."

Mwakilishi Jackie Speier, ambaye ni mwanachama wa kamati ya bunge kuhusu huduma za kijeshi ameliambia shirika la utangazaji CNN: "Nilishangazwa na pendekezo hilo kwa kweli .... tuna kiongozi anayetaka kuwa kama Napoleon."



Mimi Mars Aweka Wazi Uhusiano Wake na Jux

0
0

Mimi Mars Aweka Wazi Uhusiano Wake na Jux
MIMI Mars ni miongoni mwa wanadada wanaofanya vizuri kwa sasa kwenye gemu la muziki wa Bongo Fleva. Jina lake alilopewa na wazazi wake ni Marianne Mdee na ni mdogo wa damu wa mwanamuziki Vanessa Mdee ‘Vee Money’.

Mbali na kuwa mwanamuziki, Mimi Mars ambaye hana muda mrefu kwenye gemu lakini akiwa na nyimbo kali zikiwemo Nadata, Shuga na wimbo mpya wa Sitamani, pia ni mtangazaji wa televisheni.

Katika makala haya Mimi Mars amefunguka mambo mengi kuhusu muziki wake pamoja na maisha binafsi.

Risasi Vibes: Ujio wako mpya mapokezi yake yamekuwaje?

Mimi Mars: Ukweli ni kwamba mapokezi yamekuwa mazuri, wimbo umefanya vizuri ndani na nje ya Bongo na hata idadi ya watu wanaonisapoti wameongezeka kiukweli.

Risasi Vibes: Kwa uonavyo wewe, nani ni mshindani wako kwenye muziki Bongo?

Mimi Mars: Kiukweli sina mshindani, kila mwanamuziki anafanya muziki kwa namna yake mwenyewe, kwa hiyo mshindani wangu naweza kusema ni mimi mwenyewe. Nashindana kila siku ili kuleta mvuto zaidi kwenye kazi zangu.

Risasi Vibes: Mwanamuziki gani wa kike anakuvutia na ambaye unapenda kufanya naye kazi ndani na nje ya Bongo?

Mimi Mars: Kiukweli wanamuziki wanaonivutia ni wengi ndani na nje ya Bongo. Lakini sana ningependa kufanya kazi na wanamuziki wa nje ya nchi wakiwemo Yemi Alade, Seyi Shay, Tiwa Savage, Niniola, Fena, Victoria Kimani, kiukweli listi ipo ndefu sana.

Mimi Mars.

Risasi Vibes: Tumeona Vee Money ametoka na albamu, wewe pia ni miongoni mwa timu yake, mipango ya kutoa albumu kwako ipo vipi?

Mimi Mars: Mpango wa kutoa albumu labda mwakani, lakini kwa sasa ninataka mashabiki wangu waifahamu sauti yangu na nguvu yangu ya muziki ili nitakapotoa albumu waweze kuifurahia zaidi.

Risasi Vibes: Mpaka sasa tangu uanze muziki ni mafanikio gani makubwa umeweza kuvuna?

Mimi Mars: Mafanikio ni makubwa sana na yanazidi kumiminika. Nimevuna mashabiki wengi, nimefanya matamasha makubwa mpaka nje ya nchi, kule Kenya. Lakini pia nimekuwa kwenye nomination za tuzo za Ami Afrika na ninaomba mashabiki wa muziki wanipigie kura ili tulete tuzo nyumbani kwenye kipengele cha Mwanamuziki Bora wa Kike Afrika Mashariki.

Risasi Vibes: Kazi zako zinasimamiwa na nani?

Mimi Mars: Ninasimamiwa na menejimenti ya Mdee Music pamoja na watu mbalimbali ambao wanahakikisha kazi zangu zinakwenda vizuri na katika mpangilio mzuri.

Risasi Vibes: Una kolabo ya nje yoyote ambayo umekwisha kufanya au unatarajia kufanya hivi karibuni?

Mimi Mars: Kolabo zipo nyingi na mashabiki watakwenda kuzisikia hivi karibuni. Maana mwaka huu ndiyo mwaka wa kila kitu kwangu kimuziki, yaani kufika mbali zaidi.

Risasi Vibes: Katika masuala binafsi, kipi amb-acho huki-pendi kwenye maisha yako?

Mimi Mars: Kiukweli sipendi uongo na unafiki. Unajua watu wa namna hii wanaweza hata kukuua, kwa hiyo hivyo ni vitu ambavyo sivipendi kabisa.

Risasi Vibes: Una mpenzi au mume na anaitwa nani?

Mimi Mars: Sina mpenzi, sina mume na akitokea huko siku za usoni bila shaka kila mmoja atafahamu.

Risasi Vibes: Unamzungumziaje Jux kama shemeji yako, kwako binafsi anapendeza kuwa na Vee Money na unawaona wapi katika uhusiano wao siku za usoni?

Mimi Mars: Jux ni mtu poa kusema kweli. Naweza kusema ni zaidi ya shemeji kwangu. Anajali, ana upendo wa dhati. Ana upendo na heshima. Na ninashukuru anavyompenda Vanessa. Ninaona anamfanya pia kuwa mtu bora katika kazi na hata maisha yao ya kawaida na ninawaona mbali.

Kama mwanafamilia ninafahamu wana mipango yao mikubwa, wakiamua ‘kushare’ na mashabiki watawaeleza, wasipoamua pia kama wanafamilia bado tunawaona mbali.

Risasi Vibes: Mengine ambayo ungependa kuzungumzia kuhusu muziki wako?

Mimi Mars: Ninashukuru kwa kila mtu anayenisapoti. Pia kwa ambao hawajasikiliza muziki wangu ningependa wasikilize, bila shaka wataipata sababu ya kunisikiliza. Sitawaangusha kama ambavyo nimekuwa nikisema mara zote. Asa-nte-ni.


Benki Kuu Imeyafungia Maduka 86 ya Kubadirishia Fedha za Kigeni

0
0
Benki Kuu Imeyafungia Maduka 86 ya Kubadirishia Fedha za Kigeni
Benki kuu ya TANZANIA imeyafungia maduka 86 ya kubadilishia fedha za kigeni baada ya kushindwa kutimiza masharti ikiwemo kutoa vielelezo vinavyoonyesha fedha za kigeni zinazotumika kwenye biashara hiyo zimetokana na chanzo kipi.


Akizungumza na waandishi wa habari waliohudhuria mafunzo ya kuandika habari za kiuchmi mkoani Mtwara meneja wa kitengo kinachosimamia fedha za kigeni kutoka benki kuu ya Tanzania Eliyamringi Mandari amesema kufungwa kwa maduka hayo kunatokana na oparesheni inayoendelea nchi nzima kwa sasa yenye lengo la kuleta ufanisi wa kazi katika maduka hayo.

Amesema upareresheni hiyo inakwenda sambamba na usajili upya wa maduka hayo ya kubadilisha fedha za kigeni ambayo imetokana na kanuni mpya ya kusimamia maduka hayo lengo hasa ni kuongeza ufanisi na  mitaji katika kuendesha biashara hiyo.

Hata hivyo amesema katika oparasheni hiyo maduka 297 yametuma maombi yao huku maduka  sitini na tano yanaendelea kufanyiwa kazi, sabini na moja tayari yamepatiwa leseni mpya pamoja na matawi yake arobaini.

Amesema maduka 86 yamefutiwa leseni kutokana na kushindwa kutimiza masharti ikiwemo kueleza vyanzo vya mitaji inayotumika katika kuendesha.

Biashara hiyo na kusisitiza wiki mbili zijazo zoezi hilo litakamilika na taarifa kamili itatolewa.

Kufuatia opareheni hiyo mandari amesema ni kosa la jinai kwa mtu yeyote kuendesha biashara ya fedha za kigeni bila leseni ya benki kuu adhabu yake ni faini shilingi milioni nne, ama kifungo cha miaka kumi na nne gerezani, ama vyote viwili.

Source: ITV

Habari Njema: Tunatibu Busha, Korodani Kuvimba, Ngiri, Miguu Kufa Ganzi Pamoja na Matatizo ya Nguvu za Kiume

0
0
Ni dawa ya nguvu za kiume inayorefusha na kunenepesha uume saizi uipendayo (Inch 1-7) kwa muda wa siku 6 tu.Dozi hii itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa muda wa dakika 30, utarudia tendo la ndoa zaidi ya mara 4 bila hamu kuisha bila kujali umri na garantee ni miaka 60 baada ya kutibu tatizo.

Pia tunatibu Busha bila kufanyiwa Oparesheni, korodani moja kuvimba, ngiri, tumbo kujaa gesi na kuunguruma, kutopata choo vizuri, miguu kuwaka moto na kufa ganzi, chango la wanawake, kisukari na kutokwa na kinyama sehemu ya haja kubwa.

MIHAYO:
Inarudisha mke, mchumba, hawara na atakutimizia kila kitu unachotaka kutoka kwake ndani ya  saa 2 tu hata kama yupo mbali. atarudi na kumfunga asiwe na mwingine zaidi yako.

Umefukuzwa kazini? unataka kupandishwa cheo? Umepoteza pesa zako kwenye biashara bila kujua umepandikizwa chuma ulete? Njoo urudishe pesa zako. Unauza mali yako haiendi?


Wasiliana na mtaalam Challo kwa; 0714006521

Uchambuzi wa Shaffih Dauda kuelekea Simba vs Azam leo Februari 7, 2018

0
0
Simba na Azam zinakutana kwenye mchezo wa ligi kuu Tanzania bara, hii ni mara ya pili timu hizi kukutana msimu huu huku kila timu ikiwa na nafasi ya kushinda taji la ligi msimu huu (2017/18) endapo kila timu itaendelea kufanya vizuri kwenye michezo yake iliyosalia wakati huu wa mzunguko wa pili.

Watoto wa Msimbazi ndio vinara wa ligi wakiwa wanaongoza kwa pointi zao 38 baada ya mechi 16 wakifuatiwa na watani zao Yanga ambao wana pointi 34 katika nafasi ya pili lakini wakiwa wamecheza mechi 17, Azam inasimama nafasi ya tatu ikiwa na pointi 33 kabla ya mchezo wa leo wakati Singida United ikiwa nafasi ya nne kwa pointi zao 30 kati ya miamba inayowania ubingwa.



Katika mchezo huu (Simba vs Azam) ili kila timu iendelee na dhamira yake ya kuchukua ubingwa inatakiwa ipate matokeo ya ushindi dhidi ya timu ambayo ni adui yake kwenye mbio za ubingwa, kwa hiyo ni mechi nzuri sana ambayo itakuwa na mvuto wa kipekee.

Bocco vs Azam mara ya pili



John Bocco amekuwa kwenye kiwango bora siku za karibuni, anakutana na Azam timu ambayo ana historia nayo, hadi sasa Bocco ameshafunga magoli tisa kwenye ligi huku akiwa amefunga magoli manne mfululizo katika mechi mbili zilizopita (Simba vs Singida United na Simba vs Ruvu Shooting).

Nahodha huyo wa zamani Azam atakuwa akiungana na Aishi Manula, Erasto Nyoni na Shomari Kapombe ambaye huenda akacheza kwa mara ya kwanza dhidi ya Azam tangu alipondoka na kurejea Simba, nyota hao wanne waliondoka kwa pamoja Azam na kusajiliwa Simba, mchezo wa awali uliochezwa Azam Complex, Kapombe peke yake ndio hakucheza kati ya waliondoka Azam kujiunga na Simba.

Simba ya sasa si ya Omog

Wakati Azam ilipokuwa mwenyeji wa mchezo wake wa kwanza msimu huu dhidi ya Simba, Joseph Omog alikuwa bado kocha mkuu wa Simba akisaidiwa na Jackson Mayanja ambaye baadae alijiuzulu, mchezo huo ulimalizika kwa suluhu lakini Simba ya sasa ipo chini ya makocha wapya na imekuwa tishio siku za karibuni.



Simba imebadilika ukiangalia walivyocheza mechi za hivi karibuni, usajili wa Asante Kwasi umeimarisha safu ya ulinzi, wamefunga magoli mengi na kuzuia kuruhusu magoli mengi. Simba imefunga magoli 38 huku ikiruhusu magoli sita (6) ya kufungwa katika mechi 16 ilizocheza hadi sasa, ndiyo timu pekee iliyofunga magoli mengi na kufungwa machache, hiyo inaonesha makali ya washambuliaji na viungo lakini pia ubora wa safu ya ulinzi.

Uwepo wa Said Ndemla na Jonas Mkude kwenye kikosi cha kwanza cha Simba imekuwa tofauti na msimu ulivyoanza, unaona faida  ya mchezaji kukaa benchi kwa sababu imewaletea ukomavu kwa sababu zamani mchezaji akikaa benchi akirudi anakuwa amekwisha lakini baada ya Mkude na Ndemla kupata nafasi wameonesha wanataka kuendelea kucheza kwenye kikosi cha kwanza kutokana na namna wanavyojituma.



Chini ya Omog wawili hao hawakuwa na nafasi za kudumu kwenye kikosi cha kwanza lakini baada ya timu kuwa chini ya Masoud Djuma na baadae ujio wa kocha mpya Pierre Lichantre umewafanya wawe wapya huku viwango vyao vikimshawishi kila mtu kuamini uwezo na ubora wa vijana hao waliolelewa katika klabu hiyo.

Azam si ya kubeza

Ukiitazama Azam lazima uwataje Razaq Abarola, Himid Mao, Mohamed Yakubu na Agrey Morris ambao wamekuwa katika viwango vya juu katika kikosi chao tangu kuanza kwa msimu huu huku wakicheza michezo mingi ya ligi ukilinganisha na wachezaji wengine ambao wamekuwa wakipishana kwenye kikosi.



Kinachowabeba Azam hadi sasa ni safu yao ya ulinzi, Yakubu, Razaq, Agrey Morris, wamecheza kwa viwango vya juu hadi sasa  wakiwa wameruhusu magoli saba kwenye wavu zao lakini pia sehemu ya kiungo Salmin Hoza ameleta changamoto mpya katika idara hiyo.



Azam haifungi magoli ya kutosha

Eneo ambalo linaonekana lina mapungufu kwa Azam ni idara ya ushambuliaji. Mbaraka Yufuph mara nyingi amekuwa akisumbuliwa na majeraha lakini Yahaya Zayd, Shabani Chilunda, Peter Paul kijana ambaye kila akipata nafasi anataka kumfurahisha kocha na kuonesha anastahili kuwa sehemu ya kikosi cha kwanza, vijana hao wakikomaa wataisaidia Azam kufikia malengo.

Azam imefunga magoli 19 tu katika mechi 16 ilizocheza hadi sasa wakati John Bocco na Emanuel Okwi kwa pamoja wameifungia Simba magoli 19 (Okwi 12, Bocco 9).



Azam wana kumbukumbu nzuri dhidi ya Simba, waliifunga 1-0 kwenye mchezo wa Mapinduzi Cup hatua ya makundi Januari 6, 2018 kwenye uwanja wa amaan visiwani Zanzibar huo ndiyo mchezo wa mwisho kuzikutanisha timu hizo siku za hivi karibuni

Kombe la EPL sasa nuksi kwa makocha, ukibeba tu msimu ujao unatimuliwa

0
0
Mzimu wa kubeba ndoo ya EPL na kutimuliwa umeshaanza kumuandama Antonio Conte, baada ya kuwapa Chelsea taji la EPL msimu uliopita sasa Muitaliano huyo yupo katika hati hati ya kuondoka katika ligi hiyo.

Lakini kwa siku za usoni hii imekuwa desturi ya EPL kwa kocha kuchukua kombe msimu huu na kisha msimu unaofuata anatimuliwa na hii imekuwa kwa makocha karibia wote 6 waliobeba makombe 6 yaliyopita.

Kumbukumbu hii inaanza msimu wa 2011/2012 baada ya Roberto Mancini kuwapa ubingwa Manchester City lakini baada ya ubingwa huo hakudumu, mwaka uliofuata yani 2013 Manchester City wakamtimua na nafasi yake kwenda kwa Manuel Pellegrini.

Baada ya Manchester City kuchukua ubingwa wa 2011/2012 msimu uliofuata wakawapa kombe Manchester United waliokuwa chini ya Alex Ferguson lakini kwa SAF hakuondoka bali msimu ulipoisha tu alistaafu.

2013/2014 Manchester City tena chini ya Manuel Pellegrini walichukua kikombe cha EPL lakini kabla hata ya msimu haujaisha Pellegrini alitangaza kwamba ataachana na City itakapofika mwaka 2016.

Jose Mourinho naye msimu wa mwaka 2014/2015 akabeba kombe la EPL, mwaka huo huo 2015 ambao Mourinho alichukua ubingwa mwezi wa 12 Chelsea waliamua kumfungashia virago na moja ya sababu ikiwa ni kutokuelewana na wachezaji pamoja na ugomvi na daktari Eva Carneiro.

Ilipofika msimu wa 2015/2016 Claudio Ranieri akafanya kile ambacho wengi hawakukitaraji baada ya kuwapa Leicester ubingwa wa EPL na mwaka 2017 dunia ikaamini hakuna huruma tena katika soka baada ya Leicester kumuonesha Ranieri mlango wa kutokea.

2016/2017 ndio msimu uliopita na ni zamu ya Antonio Conte sasa, kwa hali ya mvutano na kiwango cha Chelsea haihitaji akili kubwa kujua ni nini Roman Abromovich atakachomfanya hivi karibuni.
Viewing all 104414 articles
Browse latest View live




Latest Images