Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104775 articles
Browse latest View live

Wasiliana na Mtaalam Chief Sultan Makata...Kumaliza Shida zako zilizoshindikana

$
0
0
CHIEF SULTAN MAKATA
Wasiliana na Mtaalam Huyu Kwani yeye hufaulu Pale wote waliko Shindwa na Pia Humaliza kazi zilizo Shindikana ama Zilizo Achwa ndani ya Siku Moja 1.
CHIEF SULTAN MAKATA ANAWASHUKURU WALE WOTE WANAOPIGA SIMU ZA SHUKRANI NA KUTOA SHUHUDA JINSI TIBA ZAKE ZINAVYO SAIDIA(Rudisha Mahusiano yako Ndani ya Saa 12 tu)

CHIEF SULTAN MAKATA ni Mtabibu wa Nyota za Binadamu na Dawa za Asili Mwenye Uwezo wa Kubaini Tatizo lako tu Pindi Utakapo Fanya Mawasiliano Kupitia Wasaa Husika.
(NA ANATIBU KWA NJIA YA SIMU UKIWA NCHI YOYOTE MKOA WOWOTE ENDAPO UTAFATA MAELEKEZO YAKE..)

Je Unasumbuliwa na Mapenzi..?
Umeachwa na UMPENDAE Awe Mume/Mke na Bado Unampenda
Je Umejaribu Sehemu Nyingi Bila Mafanikio?
Mpigie Simu sasa Hivi Ujionee Muujiza wa Papo kwa Papo..
Anauwezo wa Kurudisha Mahusiano yako na Kuimarisha NDOA Ndani ya saa 12 tu.
Je Umekimbiwa na Mumeo/Mkeo au Mpenzi na Anaishi na Mtu Mwingine..?
Muone akutatulie Anauwezo wa Hali ya Juu wa Kusambalatisha Mahusiano yao (Mfarakano/Kimavi) Endapo Utafata Atakacho Kuelekeza.

Je Una Mpenzi wako ana Pesa na unataka Kumkamata? Muone Maalim Hussein Atamfanya Atimize Ahadi zote Ndani ya Muda Mfupi..

CHIEF SULTAN MAKATA Anatumia Jina La Muhusika au Picha Kumaliza Tatizo..
Anatibu Kutumia QUR_AN DAWA ZA ASILI YA AFRICA, Dawa za KIARABU NA MAJINI..
ANATAFSIRI NDOTO. ANAPANDIKIZA NYOTA YA KUSHINDA BAHATI NASIBU, KUSAFISHA NYOTA NA KUKUPA MVUTO WA AJABU, KUTOA NUSKI NA VIFUNGO MBALIMBALI.

ZINDIKO ZA NYUMBA NA BIASHARA.. PETE ZA BAHATI.. HUMALIZA KABISA TATIZO LA NGUVU ZA KIUME NA KUREFUSHA UUME KWA SAIZI UNAYOTAKA. HUZUIA CHUMA ULETE KWENYE BIASHARA. HURUDISHA MALI ZILIZOPOTEA..
MAGONJWA SUGU, MIGUU KUWAKA MOTO AU KUFA GANZI, HUTIBU BUSHA BILA KUPASUA..ANAO UWEZO WA KUMRUDISHA  ALIE MBALI AU ALIECHUKULIWA MSUKULE..

Humaliza Kesi ya Aina Yoyote Ndani ya Siku 7 tu..
Hutoa Jini la MALI kwa wale Wanao Hitaji Utajiri Bila Masharti..

+255 677 805 105 WhatsAPP.
+255 746 426 604 Kupiga.

Msigwa Ampa Makavu Ampa Makavu Kigwangala " Unaisumbua Sekta ya Utalii na Maliasili"

$
0
0
Msigwa Ampa Makavu Ampa Makavu Kigwangala " Unaisumbua Sekta ya Utalii na Maliasili"
Mbunge wa Iringa Mjini kwa tiketi ya CHADEMA, Mhe. Peter Msigwa amefunguka na kumchana Waziri wa Maliasili na Utalii Dkt. Hamisi Kigwangala na kudai kuwa anafanya kazi kwa mizuka na mihemko na kuisumbua sekta ya Utalii na Maliasili nchini.

Msigwa amesema hayo wakatii alipokuwa akichangia bungeni taarifa ya Kamati ya Ardhi, Maliasili na Utalii na Kamati ya Kilimo, Mifugo na Maji, mjini Dodoma na kudai kuwa Mawaziri vijana wamekuwa na mihemko.

"Niwashauri hawa Mawaziri vijana fursa 'opportunity is atrracted by talent, skills, perfomance and abillity. Show your talent and abillity people will love you' hawa Mawaziri wa zamani hawa kwa mfano Lukuvi, Tizeba tunawaona wakijibu hoja wanajibu hoja siyo za kimihemko kiasi kwamba unaridhika hata Waziri akikujibu unapenda lakini Mawaziri vijana wengi mnaonekana mnayofanya katika Serikali hii kiasi kwamba Serikali ijayo muonekane hamna tija" kwa sababu mna mihemko sana"

Mbali na hilo Msigwa alikwenda mbali zaidi na kumnyooshea mkono Waziri wa Maliasili na Utalii na kudai amekuwa na maamuzi ya ajabu jambo ambalo linapelekea kiongozi huyo kuivuruga Wizara hiyo.

"Utalii huu umejengwa kwa muda mrefu sana na akitokea mtu mmoja anaamua kufanya tu kwa kutafuta umaarufu atauvuruga kwa muda mfupi sana, Utalii kwenye pata la taifa unaingiza asilimia 20 na forex ni kubwa inatokana na utalii kwa hiyo hicho si kitu kimoja mtu anaweza kuamka leo anasema nimeharibu na hii diplomasia ya kiuchumi inategemea sana na kutabirika, wawezekaji huko nje wanataka kuona kunatabirika wao kufanya biashara zao. Haiwezekani huyu Waziri anatoa amri mpaka mapolisi wanamkataa anashindwa hata kuwasiliana na Waziri wake wa Mambo ya Ndani, huyu huyu Waziri anatoa amri anapingana na Waziri wa Ardhi, huyu huyu Waziri mmoja anapingana na Waziri wa Uvuvi hatuwezi kuwa na Mawaziri ambao wanakuwa na mizuka na kufanya kazi kwa mizuka wote kama tunalipenda taifa letu tufanye kazi kwa kupendana" alisisitiza Mchungaji Msigwa

Dizeli, Petroli na Mafuta ya Taa Bei Juu

$
0
0
Dizeli, Petroli na Mafuta ya Taa Bei Juu
kawaida kwa Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA) kukuletea bei mpya za Mafuta nchini kila Jumatano ya kwanza ya mwezi na leo February 7, 2018 imetangaza bei mpya za mafuta zinazoanza kutumika leo huku bei za petroli, dizeli na mafuta ya taa zikiongezeka.

 Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Ewura, Nzinyangwa Mchany ametoa taarifa hiyo kwa waandishi wa habari ambapo amesema bei za rejareja zimeongezeka kwa Petroli ikiwa ni Tsh59 sawa na asilimia 2.70, Dizeli Tsh46 (sawa na asilimia 2.30), na mafuta ya taa kwa Tsh24 (sawa na asilimia 1.17).

Amesema bei za jumla nazo zimeongezeka ambazo kwa Petroli ni Tsh58.57 sawa na asilimia 2.85, Dizeli kwa Tsh46.48 (sawa na asilimia 2.44) na mafuta ya taa kwa Tsh23.75 (sawa na asilimia 1.24).

“Bei za jumla na rejareja kwa mafuta ya petroli na dizeli yaliyoingizwa nchini kupitia Bandari ya Tanga nazo zimeongezeka ikilinganishwa na toleo lililopita la Januari 3. Bei za mafuta ya taa hazijabadilika kwa sababu hakuna yaliyoingizwa nchini kupitia bandari hiyo Januari,” -Mchany.

“Ongezeko la bei za mafuta ya petroli na dizeli katika Mkoa wa Tanga linatokana na mabadiliko ya bei za mafuta katika soko la dunia na kuongezeka kwa gharama za usafirishaji,” -Mchany.

Mashinji: Mgombea Wetu wa Udiwani Alitekwa Alilazishwa Kupokea Milioni 8 Ili Ajitoe

$
0
0
Mashinji: Mgombea Wetu wa Udiwani Alitekwa Alilazishwa Kupokea Milioni 8 Ili Ajitoe
Katibu Mkuu wa Chadema, Dk Vincent Mashinji amesema mgombea udiwani wa chama hicho Kata ya Buhangaza Wilaya ya Muleba mkoani Kagera, Athanas Makoti (28) alilazimishwa kupokea rushwa ya Sh8milioni na watu waliomteka na kumjeruhi ili ajitoe kwenye uchaguzi.

Akizungumza na waandishi wa habari leo Februari 7, 2018 makao makuu ya Chadema, Kinondoni jijini Dar es Salaam, Dk Mashinji ameliomba Jeshi la Polisi kufanya uchunguzi wa tukio hilo na kuchukua hatua.

Makoti alitekwa Februari 2, 2018 katika mazingira ya kutatanisha na kupatikana Februari 5, 2018 saa moja asubuhi akiwa ametelekezwa na watu wasiojulikana jirani na Hospitali ya Kagando iliyopo Wilaya ya Muleba. Mgombea huyo amelazwa katika hospitali hiyo mpaka sasa.

Dk Mashinji amesema Makoti alikuwa anatoka kwenye maandalizi ya uchaguzi, akaita bodaboda ili arejee nyumbani lakini likatokea gari nyuma yake na kumchukua kwa nguvu.

“Watekaji hao walimfunga kitambaa usoni akapoteza fahamu. Walimzungusha maeneo mbalimbali na alipozinduka hakujua aliko. Walimtaka akubali kupokea Sh8 milioni na ajitoe kwenye uchaguzi, hata hivyo alikataa ndipo wakaanza kumtesa,” amesema Dk Mashinji,

“Hizi ni njama za kisiasa kutaka kuvuruga uchaguzi katika kata ya Buhangaza,” amesema.

Amesema kwa mujibu wa maelezo ya mgombea huyo, alitekwa kwa madhumuni ya kisiasa.

“Tunalaani  kitendo cha mgombea wetu kutekwa, kuteswa na kulazimishwa kupokea fedha ili ajitoe kwenye uchaguzi,” amesema.



Jeshi la Magereza Lawasimamisha Kazi Askari Wake 11

$
0
0
Jeshi la Magereza Lawasimamisha Kazi Askari Wake  11
Jeshi la Magereza Tanzania limewasimamisha kazi askari wake kumi na moja waliofikishwa mahakamani kwa tuhuma za mauaji ya mwanakijiji, Aloyce Makalla (41) wiki iliyopita.

Taarifa kutoka ndani ya jeshi hilo zinasema askari hao walisimamishwa kazi na Kamishna Jenerali wa Magereza, Dk Juma Malewa juzi.

Mkuu wa Magereza Mkoa wa Tanga, John Masunga alithibitisha kusimamishwa kwa askari hao lakini hakutaka kuzungumzia suala hilo kwa undani zaidi akisisitiza kuwa msemaji wa jeshi hilo ni Kamishna Jenerali pekee.

Askari waliosimamishwa ambao walishafikishwa katika Mahakama ya Wilaya ya Korogwe mwishoni mwa wiki mbele ya Hakimu Mkazi Mfawidhi, Kassim Mkwawa ni Jonas Makere, Shadrack Lugendo, Lazaro Stephen, Mussa Zuberi, Ramadhan Yusuf, Robert Alfred, Fhidirish Osmas, Alfonce Revocatus, Mbesha Naftari, Hamis Msola na Michael Elias.

Taarifa hiyo inaeleza kuwa hatua ya kuwasimamisha kazi askari hao imechukuliwa ikiwa ni kupisha vyombo vya sheria kufanya kazi yake kwa uhuru zaidi na kwamba hatima yao itategemea uamuzi wa mahakama hiyo.

Askari hao wa Wilaya ya Korogwe walifikishwa katika mahakama hiyo wakikabiliwa na shtaka la kumuua, Makalla, ambaye ni mkazi wa Kijiji cha Kerenge wilayani humo.

Ilidaiwa mahakamani hapo na mwanasheria mwandamizi wa Serikali, Saraji Iboru kuwa Januari 22 saa 9.30 katika kitongoji cha Mapangoni Kijiji cha Kerenge, washtakiwa hao kwa pamoja walimuua mwanakijiji huyo.

Iboru ambaye alikuwa akisaidiana na mwendesha mashtaka kiongozi, Shosa Naiman alidai kwamba siku ya tukio, washtakiwa hao walikwenda nyumbani kwa Makalla wakimtuhumu kwamba Januari 15 alimjeruhi askari mwenzao aitwaye Sajenti Stephen.

Washtakiwa hao hawakutakiwa kujibu chochote kutokana na Mahakama hiyo kutokuwa na uwezo kisheria wa kusikiliza kesi za mauaji. Hakimu Mkwawa aliahirisha kesi hiyo hadi Februari 15 itakapotajwa tena.

Prof. Jay na Mkewe Wazuiwa Kumuona Mbunge Sugu

$
0
0
Prof. Jay na Mkewe Wazuiwa Kumuona Mbunge Sugu
Mbunge Joseph Haule (Prof. Jay) akiwa ameambatana na mke wake Grace Haule wamezuiliwa na uongozi wa gereza la Ruanda liliopo mkoani Mbeya kumuona Bunge wa Mbeya Joseph Mbilinyi "Sugu" pamoja na Katibu wa CHADEMA Kanda ya Nyasa Emmanuel Masonga


Prof. Jay amethibitisha hayo kupitia moja ya kurasa zake za mtandao wa kijamii muda mchache alipowasili katika viwanja vya gereza la Ruanda kwa lengo la kutaka kuwajulia hali Sugu na Masonga ambao wamewekwa katika gereza hilo baada ya kunyimwa kwa dhamana katika kesi yao inayowakabiri.

Mbunge wa Mbeya Mjini Mhe. Joseph Mbilinyi 'Sugu' pamoja na Katibu wa CHADEMA Kanda ya Nyasa, Emmanuel Masonga wanakabiliwa na kosa la matumizi ya lugha ya fedhea dhidi ya Rais Dkt. Magufuli kesi yao itasikilizwa tena Februari 8 (Kesho) mwaka huu.

Zuma Abanwa Kila Kona Akubali Kuondoka

$
0
0
Zuma Abanwa Kila Kona Akubali Kuondoka
Rais Jacob Zuma atajiuzulu mara tu baada ya kukamilisha orodha ya masharti yake katika mpango uliofikiwa Jumanne kati yake na kiongozi mkuu wa ANC Cyril Ramaphosa kisha kuthibitishwa na vyanzo Jumanne usiku.

Makubaliano hayo ndiyo yaliyosababisha kuahirishwa kwa mkutano wa Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) wa chama tawala cha African National Congress (ANC) uliopangwa kufanyika Jumatano ili kulazimisha Zuma kuondoka ofisini.

Mkutano huo ulikuwa umepangwa kufanyika kwenye ukumbi wa Hoteli ya Mount Nelson mjini Cape Town na ungepokea mapendekezo kutoka Kamati Kuu ya Taifa ya ANC kwamba Zuma aondolewe kama mkuu wa nchi.

Mkutano kati ya Zuma na Ramaphosa ulifanyika baada ya Spika wa Bunge, Baleka Mbete kutangaza kuahirishwa kwa hotuba ya kitaifa iliyokuwa itolewe na Zuma Alhamisi

Zuma alitumia Jumanne asubuhi akifanya vikao na kamati za Baraza la Mawaziri mjini Tuynhuys. Baadaye, alikwenda Genadendal yaliko makazi yake ya kifahari huko Cape Town ambako alikutana na Ramaphosa baada ya saa 10:00 jioni pamoja na Katibu Mkuu wa ANC, Ace Magashule.

Januari 6, 2018, Mbete alitangaza kuahirishwa kwa muda usiojulikana kwa hotuba ya hali ya nchi maarufu kama Sona iliyokuwa itolewe na Zuma.

Jumanne jioni, Magashule aliiambia TimesLIVE kuwa mkutano kati ya marais wawili ulikuwa "wa kujenga na wenye mafanikio".

 "Nilikuwa huko ... niliwaacha marais wawili hao kujadili mambo yao mimi nilirudi kuungana nao mwishoni," alisema.

Magashule alisema Zuma na Ramaphosa walikubaliana kuwa uamuzi wa kuahirishwa hotuba ya rais ulikuwa sahihi.

"Walikubaliana pia kuwa mkutano wa dharura wa NEC ulioitishwa unapaswa kuahirishwa baada ya majadiliano yao yenye kujenga," alisema.

Magashule hakutaka kuthibitisha ikiwa Zuma amekubali kujiuzulu, ingawa viongozi wengine wa ANC walidokeza kuwa mpango uliokubaliwa utamwezesha Zuma "kuondoka kwa njia ya heshima".

Hata hivyo alidokeza kwamba majadiliano kati ya Ramaphosa na Zuma yaliridhia haja kubwa ya NEC kujadili kuondoka kwake.

Katibu mkuu huyo hakuweza kusema nani atatoa hotuba mara tarehe mpya itakapotangazwa.



Serikali: Uchumi wa Tanzania Umeimarika

$
0
0
Serikali: Uchumi wa Tanzania Umeimarika
Msemaji Mkuu wa Serikali, Dkt. Hassan Abbas, amesema hali ya uchumi wa Tanzania imeimarika ikilinganishwa na awamu zilizopita ambapo imeshika nafasi ya 48 kwa nchi zenye uchumi jumuishi duniani, pia ni ya pili Afrika ikifuatiwa na Tunisia ambapo kusini mwa jangwa la Sahara ni ya kwanza.

Abbas alikuwa akizungumza leo jijini Dar es Salaam na  waandishi wa habari ambapo mambo mengine aliyozungumzia ni kuhusu kifo cha mkongwe wa siasa nchini marehemu Kingunge Ngombale-Mwiru aliyemuita kuwa ni msahafu wa siasa za Tanzania.

Pia Abbas alitumia fursa hiyo akisema kwamba atakuwa na utaratibu maalum wa  kuzungumza na waandishi wa habari kila mwisho wa mwezi ambao utatolewa karibuni.

Kikosi cha Maangamizi cha Simba Hiki Hapa

$
0
0
Kikosi cha Maangamizi cha Simba Hiki Hapa
Kikosi cha klabu ya Simba hii leo kinatarajia kushuka dimbani majira ya saa 10:00 alasiri kuivaa Azam FC ikiwa ni mchezo wa ligi kuu soka Tanzania Bara.

Kuelekea katika mechi hiyo wekundu hao wa msimbazi wameanika kikosi chao kitakacho shuka uwanjani kuwavaa wana lamba lamba.


Chadema Yapokea Ushauri wa Slaa

$
0
0
Chadema Yapokea Ushauri wa Slaa
Chadema imesema imeupokea ushauri uliotolewa na aliyekuwa Katibu Mkuu wa chama hicho, Dk Willbrod Slaa kuwa vyama vya upinzani vitafute ufumbuzi wa zuio la mikutano ya hadhara mahakamani badala ya kulalamika.

Dk Slaa ambaye ni balozi mteule alitoa ushauri huo jana Februari 6,2018 alipofanya mahojiano na kituo cha televisheni cha Clouds.

Alipoulizwa kuhusu msimamo wa chama chake juu ya ushauri wa Dk Slaa, Katibu Mkuu wa Chadema, Dk Vincent Mashinji amesema leo Februari 7,2018 kuwa chama hicho kimeupokea ushauri huo na kitaufanyia kazi.

“Tumepokea ushauri wake, tunashukuru. Tutaufanyia kazi,” amesema Dk Mashinji alipojibu swali wakati wa mkutano na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam.

Katika mahojiano kwenye kipindi cha 360 kinachorushwa na kituo hicho cha televisheni, Dk Slaa ambaye kwa sasa anaishi Canada alisema anaungana na wale wanaodai kuwapo kwa mikutano.

“Sikubaliana na taratibu zinavyosemwa, tumepigwa marufuku na mimi naungana nao kwa sababu mimi sikubaliani na jambo lililopitishwa na Bunge linaweza kuondolewa kwa kauli,” alisema.

Maskini!.... Shida Zamfanya Mama Akamue Maziwa Yake na Kuuza Mtaani

$
0
0
Nimeipata hii stori ambayo inaweza kukuacha mdomo wazi mtu wangu ni kumhusu Mwanamke mmoja anayenyonyesha, ameshangaza watu siku za hivi karibuni baada ya kutangaza kuuza maziwa yake anayonyonyesha ili apate pesa ya matibabu ya mwanaye ambaye yuko mahututi hospitali nchini China.

Mwanamke huyo na mumewe walitengeneza video ya kutoa tangazo hilo, video hiyo ilisambaa sana kwenye mitandao ya kijamii nchini humo na kuamsha hisia tofauti za jambo hilo kwa watu mbalimbali.

Mtoto huyo ambaye yuko katika chumba cha wagonjwa mahututi anahitaji Dola 1600 sawa na Tsh Mil 3.8 ili matibabu yake kufanikiwa. Mwananmke huyo na mumewe wanaripoti kukaa mtaani mume akishikilia bango la biashara hiyo huku mwanamke akikamua maziwa hayo.

Offer ya Valentine Day..Ongeza Hips, Makalio na Imarisha Uume na Ongeza Hamu na Markson Products

$
0
0
OFFER YA VALENTINE DAY🎁
ONGEZA HIPS, MAKALIO, UUME, NGUVU NA HAMU YA TENDO LA NDOA SASA.
KATIKA KUSHEREHEKEA MSIMU WA SIKUKUU (Valentine day) TUNA PUNGUZO LA 20% KWA BIDHAA ZETU ZOTE, IKIWA NI SHUKRANI KWA KUTUUNGA MKONO.
BIDHAA ZETU ZOTE ZIMETENGENEZWA KWA MIMEA NA MATUNDA HAZINA KEMIKALI WALA MADHARA.
KWA WANAUME TUNATIBU

☆Kukosa hamu ya tendo.
☆Kuwahi kufika kileleni na kushindwa kurudia tendo.
☆Maumbile madogo ya uume.
☆Kuchoka sana wakati wa tendo na uume kusinyaa nk.
@markson_beauty_pr tumeandaa tiba bora kabisa kama ifuatavyo:-
1.HANDSOME UP ORIGINAL_ Inaongeza uume kwa size uipendayo na kuimarisha misuli (wiki 2) @240,000/=
2.SHARK POWER GELY_ Inaongeza uume inch 6 (wiki 4) @150,000/=
3VigRX CREAM_ Inaongeza uume inch 6.5 hadi 8 (wiki 2-3) @180,000/=
4.Vidonge maalum vya kuongeza nguvu na hamu ya tendo hata kwa wenye kisukari na BP @150,000/=
5. MAXMAN 2-Hii ni vidonge vinavyoongeza nguvu za kiume pamoja na uume @250,000/=
6.VIGA SPRAY OG_ Inaongeza uwezo ktk tendo na kuchelewesha kufika kileleni @150,000/=
PIA KWA WANAWAKE WANAOPENDA KUWA NA MUONEKANO MZURI ZIPO ZA👇👇👇
1.Kuongeza hips, makalio na mapaja @200,000/=
2.Kushepu mguu (CHUPA YA BIA) @150,000/=
3.Kuwa mweupe bila sugu kwa:-
(a)mafuta @150,000/=
(b) Vidonge @170,000
4.Kurefusha nywele na kutokukatika ovyo @130,000/=
5.Kuongeza hips, makalio na mapaja kwa vidonge (YODI PILLS ORIGINAL) @230,000/=
6Kupunguza au kuongeza maziwa kuyasimamisha @150,000/=
7.Kubana uke na kuondoa uchafu ukeni @130,000/=
8.Kupunguza unene na manyama uzembe @150,000/=
NB:Hakikisha unapata risiti yenye muhuri na garantii ili kukuhakikishia ubora na usalama wa bidhaa za MARKSON BEAUTY CO

Wasiliana nasi Popote
ulipo duniani kwa (+255)
0767447444
na 0714335378

UTAPATA HUDUMA.
👉🏻OUR WEBSITE:- www.marksnbeuty.org
👉🏻INSTAGRAM PAGE:-
@markson_beauty_pr

Korea Kaskazini Yazindua Pombe Mpya ya Kipekee

$
0
0
Korea Kaskazini Yazindua Pombe Mpya ya Kipekee
Korea kaskazini imezindua pombe mpya iliyotengenezwa kwa kutumia mbinu mpya na ya 'kipekee', inaarifiwa.

Kwa mujibu wa gazeti la serikali Rodong Sinmun, kiwanda cha kutengeneza pombe nchini Taedonggang kinadai kuwa mbinu yake mpya ya kutumia ngano badala ya mpunga ni bora zaidi kuliko pombe nyingine zilizoko kwa ladha na hata harufu nakwamba imepokewa vizuri na waraibu nchini.

Taedonggang kimekuwa kikitengeneza pombe tangu mwaka 2015, na hii huenda inatokana na shutuma kutoka kwa kiongozi mkuu nchini Kim Jong-un kwamba pombe inayoingizwa nchini kutoka Korea kusini haina ladha, jarida la kila siku huko Seoul Chosun Ilbo liliripoti wakati huo.

Kwa kawaida, vyombo vya habari Korea kaskazini vinaitangaza pombe hiyo kama ufanisi katika mpango wa Kim Jong-un kuinusha viwango vya maisha katika nchi hiyo ya kikomyunisti, vikisema ni kutokana na ' jitihada za muda wote"kuyafanya maisha "kuwa ya raha zaidi kwa raia".

Chosun Ilbo anadai kuwa Kim anapenda pombe , na anaeleza kuwa kwa wakatimmoja alijaribu kuidhinisha kampuni ya utengenezaji pombe PyongYang kama iliyopo katika nchi ya Ujerumani biergarten. Hatahivyo kwa mujibu wa taarifa kutoka Korea Times, kampuni hiyo ya Ujerumani ilikataa ombi hilo .

Lakini kutokana na mambo mengi yanayofanyika katika nchi hiyo, haijulikani iwapo taarifa hizo kuhusu biergarten ni za ukweli au ni uvumi tu.

Tanzania Kinara wa Utawala Bora Afrika Mashariki

$
0
0
Tanzania Kinara wa Utawala Bora Afrika Mashariki
Orodha ya Hali ya Demokrasia Duniani (2017 Democracy Index) iliyozinduliwa Februari 2, mwaka huu na kuchapishwa na jarida kongwe na mashuhuri duniani la The Economist imeitaja Tanzania kuwa nchi ya kwanza katika masuala ya Utawala Bora kwenye ukanda wa Afrika Mashariki.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es salaam leo, Mkurugenzi wa Idara ya Habari – MAELEZO na Msemaji Mkuu wa Serikali, Dkt. Hassan Abbasi alisema kuwa Tanzania kuwa nchi ya kwanza kwenye masuala ya Utawala bora imeweza kusaidia ukuaji wa Uchumi wake.

“Utawala Bora ni kigezo muhimu cha ukuaji wa uchumi na hata ustawi wa jamii, kama ambavyo Orodha ya Hali ya Demokrasia Duniani iliyotolewa na jarida kongwe na mashuhuri duniani la The Economist imeitaja Tanzania ni ya kwanza katika ukanda wa EAC, ikifuatiwa na nchi za Kenya, Uganda, Rwanda, Burundi na DRC.

Pia, ripoti ya Foresight Afrika na taarifa ya Uchumi ya Benki ya Dunia vyote vimeitaja Tanzania kuwa katika nchi tano Bora za Afrika ambazo uchumi wake unakua kwa kasi katika mwaka 2018, nchi hizo ni Ghana, Ethiopia, Kodivaa , Senegali na Tanzania”.

Aidha, Dkt. Abbasi alisema kuwa ukuaji huo wa uchumi ni dhamira isiyoyumba ya Serikali ya Awamu ya Tano chini ya Dkt. John Pombe Magufuli, ikiwa ni pamoja na kuhakikisha uchumi mkuu unaendelea kujiakisi katika maisha ya watanzania kupitia utoaji wa huduma kwa wananchi na kuboresha sekta mbalimbali.

Katika sekta ya Afya, Dkt. Abbasi alisema kuwa pamoja na ujenzi wa vituo vya afya unaoendelea nchi nzima na uboreshaji wa hospitali, Serikali imetenga bajeti ya dawa na vifaa tiba kutoka Bilioni 31 mwaka 2015 hadi Bilioni 269. Aidha, bajeti ya sasa imewezesha Serikali kuboresha usambazaji wa dawa hadi kufikia asilimia 86 ya uhakika wa kupatikana dawa muhimu.

Bajeti hiyo imewezesha ukarabati wa wodi 5 za ICU na kuongezwa vitanda kutoka 21 mpaka 75, kununua mashine mpya za CT-Scan yenye uwezo mkubwa imenunuliwa katika hospitali ya Muhimbili na Taasisi ya Mifupa na Mishipa ya fahamu (MOI) zenye uwezo mkubwa ambapo wastani wa wagonjwa wanaopimwa imepanda kutoka 20 hadi 50 kwa siku.

Vifaa vingine vilivyonunuliwa ni pamoja na mashine 14 za upasuaji (diathermy machines) na mashine za kuchuja damu kwa ajili ya wagonjwa wa figo zipatazo 25 na kuongeza uwezo wa kuhudumia wagonjwa kutoka 68 kwa siku hadi 126.

Uboreshaji huo wa sekta ya afya umeifanya Muhimbili kuwa hospitali ya kwanza ya umma katika ukanda wa Afrika Mashariki kutoa huduma za juu za kibingwa hasa oparesheni ya kuweka vifaa vya kusaidia kusikia ambapo watoto 5 waliokuwa awali hawasikii kabisa walifanyiwa oparesheni mwaka jana na kusikia kwa mara ya kwanza katika maisha yao. Wengine 6 wamefanyiwa wiki iliyopita.

Katika sekta ya Sekta, Msemaji huyo wa Serikali alisema kuwa lengo la Serikali ni kufikisha huduma ya maji kwa asilimia 85 vijijini ifikapo mwaka 2020 kutoka asilimia 67.7 mwaka 2015, makao makuu ya mikoa asilimia 95, Dar es Salaam asilimia 95 na miji mikuu ya wilaya asilimia 90 ifikapo 2020.

Ambapo hadi sasa kwa ujumla kuna takribani miradi 1,423 imekamilika na kuna vituo vya maji 117,190 vyenye uwezo wa kuhudumia watu milioni 29 sawa na asilimia 79. Katika miaka hii miwili pekee zaidi ya miradi 388 ilikamilishwa.
Dkt. Abbasi, anafafanua kuwa katika usambazaji wa umeme mijini na vijijini kazi imeendelea kwa kasi kubwa. Katika kutekeleza Mradi wa REA III, kiasi cha shilingi bilioni 985.9 zitatumika kuwafikishia wananchi umeme katika programu maalum iliyoanza kutekelezwa.

Alisititiza kuwa, “Serikali ya Awamu ya Tano inayoongozwa na Rais Dkt. John Pombe Magufuli, imedhamiria kutatua changamoto mbalimbali zinazowakabili wananchi si tu kwa maneno bali kwa vitendo, mfano namna ambavyo Serikali imeongeza wigo wa barabara vijijini na mijini, pamoja na kuundwa kwa wakala maalum (TARURA) ambao utajikita zaidi katika kuharakisha ujenzi wa barabara za vijijini”

Aliongeza kuwa mwaka huu Serikali inakusudia kutekeleza upanuzi wa njia za mwendokasi jijini Dar es Salaam kwenda njia za barabara ya Kilwa kwenda Mbagala yenye urefu wa kilomita 19 na barabara ya Uhuru kwenda Gongolamboto yenye urefu wa kilomita 23.9.

Aidha, Dkt Abbasi amewakumbusha watanzania kuwa wazalendo, kuunga mkono jitihada za Serikali kufanya kazi kwa bidii, kama ambavyo Serikali ya Awamu ya Tano inasisitiza wananchi kufanyakazi ili kuijenga Tanzania uitakayo.

Midoli ya Ngono Yatumwa kwa Wanafunzi wa Chuo Kikuu

$
0
0
Midoli ya Ngono Yatumwa kwa Wanafunzi wa Chuo Kikuu Canada
Muungano wa wanafunzi wa chuo kikuu nchini Canada wamepatwa na mshangao pale walipopokea mzigo wa kushangaza wa vifurushi vya midoli ya ngono mpaka taa .

Mizigo isiyotarajiwa iliyotumwa kupitia kampuni ya Amazon kwa watu zaidi ya kumi katika jumuiya hiyo ya wanafunzi.

Kuna ambao wamepokea mizigo mingi kama vifurushi 15 tangu mwezi Novemba,inayogharimu kiasi cha dola 1,000 kwa jumla.

Wengi walidhani kuwa ni mapambo yenye gharama kubwa lakini polisi wameanza uchunguzi juu ya suala hilo.

Mizigo hiyo iliyojumuisha chaja za simu,taa,simu aina ya ipad pamoja na madoli kadhaa ya ngono.

Amazon wamesema kuwa hawawezi kuzichukua bidhaa hizo ,kwa kuwa zililetwa katika daraja la tatu .Aidha Kampuni hiyo imesema itafanya uchunguzi lakini imewaambia wanafunzi kuwa haiwezi kutaja taarifa za mtu aliyefanya manunuzi kwa sababu ni za siri.

Rais wa muungano wa wanafunzi ametaja kuwa kupokea mzigo huo ni jambo linalostaajabisha sana.

Na kudai kuwa kwanza alidhani labda mzigo huo ni kwa ajili ya mfanyakazi wa chuo ndio ameagiza na anaona aibu kuudai,lakini alipobaini kuwa mzigo umeandikwa kwa ajili ya jumuiya ya wanafunzi nchini Canada, wakasema sawa,baada ya kusikia kuwa kuna idadi kubwa ya wanafunzi wamepokea hivyo wakaona kuwa na kuna jambo linaloendelea.

Jeshi la Zimamoto Arusha Lamuunga Mkono Rais JPM

$
0
0
Jeshi la Zimamoto Lamuunga Mkono Rais JPM
February 7, 2018 Jeshi la Zimamoto mkoani Arusha limekabidhi vifaa vya kuzimia moto, sita kwa Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mrisho Gambo kwa niaba ya Rais John Magufuli kwaajili ya nyumba za polisi zilizojengwa Arusha.

Akikabidhi vifaa hivyo Kamanda wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji Mkoa wa Arusha Kamanda Kennedy Komba amesema Jeshi hilo lina wajibu wa kuhakikisha ujenzi wa nyumba za makazi unazingatia vigezo vyote vya usalama, wao kama Jeshi wanaunga mkono jitihada za Rais Magufuli katika kuhakakikisha makazi ya askari polisi yanakua bora.

“Sisi kama Jeshi la Zimamoto na uokoaji tunaunga mkono jitihada za Amiri Jeshi Rais Magufuli sambamba na wadau wengine waliochangia ujenzi katika kuhakikisha nyumba hizi mpya za askari ambazo ziliungua moto miezi michache iliyopita zinakuwa salama kwa kuweka vizima moto katika kila nyumba kama matakwa ya usalama yanavyohitaji.” Kamanda Komba.

Naye RC Gambo amelipongeza sana jeshi hilo kwa kuonyesha moyo wa kujali jitihada za Rais na wao kufanya kitu ambacho kinatuma ujumbe kwa jamii juu ya umuhimu wa kuzingatia usalama dhidi ya Majanga

Ujenzi wa nyumba hizo 31 kwaajili ya makazi ya askari polisi umetokana na janga la moto lililosababisha jumla ya kaya 13 za askari katika kituo kikuu cha Polisi mkoani Arusha kupoteza makazi na mali miezi michache iliyopita.

Mradi huu wa nyumba za polisi umegharimu zaidi ya shilingi milioni 540 ambapo shilijngi milioni 260 zimetolewa na Rais Magufuli.

Idriss Afunguka Kumpa Mimba Wema Sepetu

$
0
0
Idriss Afunguka Kumpa Mimba Wema Sepetu
Muigizaji wa filamu na mchekeshaji mahiri katika masuala ya komedi Idris Sultan amefunguka na kuweka wazi kuwa ni kweli alifanikiwa kumpatia ujauzito Wema Sepetu tena wa watoto wawili lakini kwa bahati mbaya uliharibika.

Idris Sultan amesema hayo kwenye kipindi cha KIKAANGONI kinachorushwa kwenye ukurasa wa facebook wa EATV kila siku ya Jumatano kuanzia saa nane mchana mpaka saa kumi jioni. Moja ya shabiki alitaka kufahamu kama kweli alimpa ujauzito Wema Sepetu ndipo hapo aliposema ni kweli.

"Wema Sepetu kweli nilimpa mimba na ni kweli kwamba ilikuwa ni mimba ya watoto mapacha, hivyo haikuwa kiki na kweli nilikuwa kwenye mahusiano naye kwa takribani miaka miwili hivyo haikuwa kiki ile bali uhalisia" alisema Idris Sultan

Mbali na hilo Idris Sultan amedai baadaye aliamua kumuacha mwanadada huyo kutokana na mambo mbalimbali ambayo alimtendea na kuamua kusonga mbele na maisha yake binafsi

"Tangu nimekuwa maarufu sijawahi kuachwa, kabla ya umaarufu nimeachwa mara tatu, kwenye mahusiano huwaga sisemi 'its over', hivyo nilimuacha Wema Sepetu ila kwanini niliachana naye siwezi kuweka wazi, kufanya hivyo nitakuwa namkosea maana naweza kuweka mambo hadharani kumbe kuna mwanaume mwingine anamtaka saizi nitakuwa simtendei haki ila nachoweza kusema nilimuacha kwa sababu ya vitu alivyofanya kwangu" alisisitiza Idris Sultan

Dawa Bora za Nguvu za Kiume na Kukosa Hamu ya Tendo la Ndoa

$
0
0

DAWA BORA ZA NGUVU ZA KIUME NA KUKOSA HAMU YA TENDO LA NDOA
Baada ya utafiti wa muda mrefu juu ya matatinzo ya upungufu wa nguvu za kiume na ukosaji wa hamu ya tendo la ndoa ama kushindwa kurundia tendo kwa haraka Sasa inakuletea suluhisho juu ya matatizo haya kwa kutumia dawa za FULL POWER

Full Power dawa asili yenye vidonge inayotibu tatizo la upungufu au ukosefu wa nguvu za kiume dawa hii inamchanganyiko wa kutosha kuzalisha vichocheo vingi vya hernone za gestro gen zikiwemo vitamin b6 na b1 vitamin e pamoja na madini aina ya zinc

Itakufanya kuwa na nguvu na mzunguko mzuri wa damu na kuongeza hamu na uwezo wakufanya tendo la ndoa zaidi hatua nne au zaidi na kuchelewa kufika kileleni zaidi ya dakika 20/30 ZAT 50

Inarundisha maumbile ya uume yaani kurefusha na kunenepesha nchi 3/7 na upana cm 3/4 standard.kiafya haijalishi umri wako hata kwa wazee ukitumia maumbile yatabaki kuwa hivyo siku zote pia anatibu matatizo mengine kama presha kisukari ngiri chango la tumbo kujaa gesi kutopata choo vizuri minguu kuwaka moto matatizo ya uzazi bawasili na magonjwa ya zinaa kama kisonono na kaswende

Tunapatikana Dar es Salaam  na mikoan wasiliana na DR Oshinda no 0755505099 au 0714126118  Karibuni kwa hunduma bora

Msigwa Amchana Kigwangala Bungeni

$
0
0
Mbunge wa Iringa Mjini kwa tiketi ya CHADEMA, Mhe. Peter Msigwa amefunguka na kumchana Waziri wa Maliasili na Utalii Dkt. Hamisi Kigwangala na kudai kuwa anafanya kazi kwa mizuka na mihemko na kuisumbua sekta ya Utalii na Maliasili nchini.

Msigwa amesema hayo wakatii alipokuwa akichangia bungeni taarifa ya Kamati ya Ardhi, Maliasili na Utalii na Kamati ya Kilimo, Mifugo na Maji, mjini Dodoma na kudai kuwa Mawaziri vijana wamekuwa na mihemko.

"Niwashauri hawa Mawaziri vijana fursa 'opportunity is atrracted by talent, skills, perfomance and abillity. Show your talent and abillity,m people will love you'

"Hawa Mawaziri wa zamani hawa kwa mfano Lukuvi, Tizeba tunawaona wakijibu hoja wanajibu hoja siyo za kimihemko kiasi kwamba unaridhika hata Waziri akikujibu unapenda lakini Mawaziri vijana wengi mnaonekana mnayofanya katika Serikali hii kiasi kwamba Serikali ijayo muonekane hamna tija" kwa sababu mna mihemko sana"

Mbali na hilo Msigwa alikwenda mbali zaidi na kumnyooshea mkono Waziri wa Maliasili na Utalii na kudai amekuwa na maamuzi ya ajabu jambo ambalo linapelekea kiongozi huyo kuivuruga Wizara hiyo.

"Utalii huu umejengwa kwa muda mrefu sana na akitokea mtu mmoja anaamua kufanya tu kwa kutafuta umaarufu atauvuruga kwa muda mfupi sana

" Utalii kwenye pato la taifa unaingiza asilimia 20 na forex ni kubwa inatokana na utalii kwa hiyo hicho si kitu kimoja mtu anaweza kuamka leo anasema nimeharibu na hii diplomasia ya kiuchumi inategemea sana na kutabirika, wawezekaji huko nje wanataka kuona kunatabirika wao kufanya biashara zao.

"Haiwezekani huyu Waziri anatoa amri mpaka mapolisi wanamkataa anashindwa hata kuwasiliana na Waziri wake wa Mambo ya Ndani, huyu huyu Waziri anatoa amri anapingana na Waziri wa Ardhi, huyu huyu Waziri mmoja anapingana na Waziri wa Uvuvi hatuwezi kuwa na Mawaziri ambao wanakuwa na mizuka na kufanya kazi kwa mizuka wote kama tunalipenda taifa letu tufanye kazi kwa kupendana" alisisitiza Mchungaji Msigwa

Tanzania Kinara Utawala Bora Afrika Mashariki....Pia imetajwa kuwa miongoni mwa nchi zenye uchumi unaokua kwa kasi barani Afrika.

$
0
0
Na. Immaculate Makilika- MAELEZO
Orodha ya Hali ya Demokrasia Duniani (2017 Democracy Index) iliyozinduliwa Februari 2,  mwaka huu  na kuchapishwa na  jarida kongwe na mashuhuri duniani la The Economist  imeitaja  Tanzania kuwa nchi ya kwanza katika maswala ya Utawala Bora kwenye  ukanda wa Afrika Mashariki.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es salaam leo, Mkurugenzi wa Idara ya Habari – MAELEZO na Msemaji Mkuu wa Serikali Dkt. Hassan Abbasi alisema kuwa Tanzania kuwa    nchi ya kwanza kwenye masuala ya Utawala bora imeweza kusaidia ukuaji wa Uchumi wake.

“Utawala Bora ni kigezo muhimu cha ukuaji wa uchumi na hata ustawi wa jamii, kama ambavyo Orodha ya Hali ya Demokrasia Duniani iliyotolewa na  jarida kongwe na mashuhuri duniani la The Economist imeitaja Tanzania ni ya kwanza katika ukanda wa EAC, ikifuatiwa na nchi za Kenya, Uganda, Rwanda, Burundi na DRC.

Pia, ripoti ya Foresight Afrika  na taarifa ya  Uchumi ya Benki ya Dunia vyote vimeitaja Tanzania kuwa katika nchi tano Bora za Afrika ambazo uchumi wake unakua kwa kasi katika mwaka 2018, nchi hizo ni Ghana, Ethiopia, Kodivaa , Senegali na Tanzania”.

Aidha, Dkt. Abbasi alisema kuwa ukuaji huo wa uchumi ni dhamira isiyoyumba ya Serikali ya Awamu ya Tano chini ya Dkt. John Pombe Magufuli, ikiwa ni   pamoja na kuhakikisha uchumi mkuu unaendelea kujiakisi katika maisha ya watanzania kupitia utoaji wa huduma kwa wananchi na kuboresha sekta mbalimbali.

Katika sekta ya Afya, Dkt. Abbasi alisema kuwa pamoja na ujenzi wa vituo vya afya unaoendelea nchi nzima na uboreshaji wa hospitali, Serikali imetenga  bajeti ya dawa na vifaa tiba kutoka Bilioni 31 mwaka 2015 hadi Bilioni 269. Aidha, bajeti ya sasa imewezesha Serikali kuboresha  usambazaji wa dawa hadi kufikia asilimia 86 ya uhakika wa kupatikana dawa muhimu.

Bajeti hiyo imewezesha  ukarabati wa  wodi 5 za ICU na kuongezwa vitanda kutoka 21 mpaka 75,  kununua  mashine mpya za CT-Scan yenye uwezo mkubwa imenunuliwa katika hospitali ya Muhimbili na Taasisi ya Mifupa na Mishipa ya fahamu (MOI)  zenye uwezo mkubwa ambapo wastani wa wagonjwa wanaopimwa imepanda kutoka 20 hadi 50 kwa siku.

Vifaa vingine vilivyonunuliwa ni pamoja na mashine 14 za upasuaji (diathermy machines) na mashine za kuchuja damu kwa ajili ya wagonjwa wa figo zipatazo 25 na kuongeza uwezo wa kuhudumia wagonjwa kutoka 68 kwa siku hadi 126.

Uboreshaji huo wa sekta ya afya umeifanya  Muhimbili kuwa hospitali ya kwanza ya umma katika ukanda wa Afrika Mashariki kutoa huduma za juu za kibingwa hasa oparesheni ya kuweka vifaa vya kusaidia kusikia  ambapo watoto 5 waliokuwa awali hawasikii kabisa walifanyiwa oparesheni mwaka jana na kusikia kwa mara ya kwanza katika maisha yao.  Wengine 6 wamefanyiwa wiki iliyopita.

Katika sekta ya Sekta, Msemaji  huyo wa Serikali alisema kuwa lengo la Serikali ni  kufikisha huduma ya maji kwa asilimia 85 vijijini ifikapo mwaka 2020 kutoka asilimia 67.7 mwaka 2015, makao makuu ya mikoa asilimia 95, Dar es Salaam asilimia 95 na  miji mikuu ya wilaya asilimia 90 ifikapo 2020.

Ambapo hadi sasa kwa ujumla kuna takribani miradi 1,423 imekamilika na kuna vituo vya maji 117,190 vyenye uwezo wa kuhudumia watu milioni 29 sawa na asilimia 79. Katika miaka hii miwili pekee zaidi ya miradi 388 ilikamilishwa.

Dkt. Abbasi, anafafanua kuwa katika usambazaji wa umeme mijini na vijijini kazi imeendelea kwa kasi kubwa. Katika kutekeleza Mradi wa REA III, kiasi cha shilingi bilioni 985.9 zitatumika kuwafikishia wananchi umeme katika programu maalum iliyoanza kutekelezwa.

Alisititiza kuwa, “Serikali ya Awamu ya Tano inayoongozwa na Rais Dkt. John Pombe Magufuli, imedhamiria kutatua changamoto mbalimbali zinazowakabili wananchi si tu  kwa maneno bali kwa vitendo, mfano namna ambavyo Serikali imeongeza wigo wa barabara vijijini na mijini, pamoja na kuundwa kwa  wakala maalum (TARURA) ambao utajikita zaidi katika kuharakisha ujenzi wa barabara za vijijini”

Aliongeza kuwa mwaka huu Serikali inakusudia kutekeleza upanuzi wa njia za mwendokasi jijini Dar es Salaam kwenda njia za barabara ya Kilwa kwenda Mbagala yenye urefu wa  kilomita 19 na barabara ya Uhuru kwenda Gongolamboto yenye urefu wa kilomita 23.9.

Aidha, Dkt Abbasi amewakumbusha watanzania  kuwa wazalendo, kuunga mkono jitihada za Serikali kufanya kazi kwa bidii,  kama ambavyo Serikali ya Awamu ya Tano inasisitiza wananchi kufanyakazi ili kuijenga Tanzania uitakayo.
Viewing all 104775 articles
Browse latest View live




Latest Images