Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104432 articles
Browse latest View live

Prof. Jay Azuiliwa Kumuona Sugu

0
0

CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) Kanda ya Nyasa kimedai kuwa mbunge wa Mikumi, Joseph Haule ‘Prof. Jay na mkewe wamezuiliwa kuwanona Mbunge wa Mbeya Mjini, Joseph Mbilinyi ‘Sugu’ na Katibu wa CHADEMA Kanda ya Nyasa Emmanuel Masonga katika Gereza la Ruanda ambako wamewekwa mahabusu.

Mbunge wa Jimbo la Mikumi, Joseph Haule ‘Professor Jay’ akiwa ameambatana na Mkewe Grace Haule amefika Mbeya jana na leo tarehe 07 Februari 2018 ameenda katika Gereza la Ruanda mkoani humo kwa ajili ya kuwaona Mbunge wa Mbeya Mjini Mhe. Joseph Mbilinyi ‘Sugu’ na Katibu wa CHADEMA Kanda ya Nyasa Emmanuel Masonga ambapo amekataliwa kuwaona na uongozi wa Gereza hilo

Viongozi hao Sugu na Masonga wanaoshikiliwa kwa kunyimwa dhamana kesho Alhamisi tarehe 08 Februari 2018 watafikishwa mahakamani kwa ajili ya muendelezo wa kesi yao ambayo wanatuhumiwa kwa kutoa maneno ya fedheha.

Habari – CHADEMA
Kanda ya Nyasa
O7 Februari 2018.

Chadema Kanda ya Nyasa.

Sallam Sk Amuepushia Shari Ruge Baada ya Kusaga Kuingilia kati. Asema 'Tumekataa Kuwa Kaa'

0
0
Mtakumbuka siku ya leo, Meneja wa Diamond ametokwa na mapovu balaa akimshambulia mtu ambaye alikuwa hamtaji jina, badae akaahidi kusema ukweli kama alivyoandika hapa => Meneja wa wcb sallam sk atangaza kuachia ukweli wote muda mfupi ujao stay tune

Sasa basi, Sallam SK ameamua kubaki kimya baada ya Joseph Kusaga kumuombea msamaha mtesi wa wasanii ambaye ni Ruge Mutahaba. Pia ametahadharisha kuwa hawawezi kuwa kaa #TumekataaKuwaKaa

Sallam SK ameyaandika haya katika ukurasa wake wa Instagram,

Nanukuu

'Kwa Heshima ya Joe Kusaga kukuombea msamaha kwa leo Bw Ruge Mutahaba naamua kukusitiri, ila ukiendelea kuyafanya ambayo unayafanya basi nitayaanika maovu yako yote unayoyafanya kwenye Industry ya muziki. WCB haina tatizo na media yoyote na wala haina tatizo na Clouds Media Group ila huyu Ruge Mutahaba ndio mwenye tatizo #TumekataaKuwaKa''

Babu Tale na Salam SK Wamekuwa Mameneja wa Hovyo Sana Wanaombebesha Diamond Mzigo wa Migogoro na Media

0
0
Wasalaam wana JF...

Ni ukweli ulio wazi vyombo vyetu vyote vya habari vinatabia zinazo fanana na vinatofautiana sana kwa kiasi kidogo sana vyombo vyote vinapenda kubembelezwa ,kuabudiwa,kusifiwa na kupewa kipaumbele...lakini pamoja na haya yote wasanii wetu walio wengi wameweza kutoboa akiweno Diamond Platinumz...
Tutakuwa waongo na wanafiki tukihindwa kujua kuwa ukubwa na alipofikia Diamond kwa sasa kumechangiwa sana tena sana na vyombo vya habari hivi ambazo muda mwingine tunaviona vya wanyonyaji au havitoi haki au vina watangazaji wenye chuki na Roho mbaya kwa wasanii wetu tuwapendao.

Lakini pamoja na mabaya mengi ya media hizi Diamond ameweza kufikia hapa na nina fikiri kabisa alikuwa na watu wanao jua zaidi kutatua migogoro na kuimaliza inapotokea na kizuri zaidi hawa Mameja wake wamekuwa nae siku nyingi japo si sana lakini hivi karibuni Diamond na WCB wamekuwa wakiandamwa na migogoro na media tena migogoro isiyopatiwa ufumbuzi kwa makusudi na wachochea migogoro wakuu wamekuwa ni Mameneja wake wakina Babu Tale na Salam Sk...
Diamond si mkorofi ni mmoja wa watu hummble sana,pamoja na matatizo yake yote lakini si mtu anayependa migogoro na watu bali ni maneneja wake ndio si watatuzi wa migogoro bali ni wachochezi wa migogoro na media.....

Diamond alikuwa na mgogoro na EATV/EARADIO jitihada zilifanywa hasa Fella kutatua huu mgogoro japo mgogoro huu ulikuwa ni wa watangazaji wa Planet bongo na Diamond kwa kuokoteza maneno ya vichochoroni....lakini pamoja na jitihada za Fella kutatua mgogoro huu Babu Tale na Salam hawakuwa tayari na wakaenda mbali zaidi kutopeleka nyimbo pale hata za wasanii wote wa WCB sasa mgogoro huu umegeuzwa wa WCB na EATV/EARADIO.

Sasa wameingia kwenye mgogoro na Clouds baada ya Mose iyobo kuwapiga wambea lakini hili limegeuzwa kama ugomvi wa Clouds na WCB na hii imechangiwa sana na Mameneja hawa wawili Salam na Tale maana kwakweli wana midomo mirefu sana na kibri kilichopitiliza na wameligeuza jambo lile kuwa anayetafutwa ni Diamond kushushwa baada ya Clouds fm kusema wamesikitishwa na wambea wao kutandikwa na Iyobo,najua Clouds wanacho hitaji ni kuombwa radhi na walitegemea ni Diamond,Tale au Salam ndio wajitokeze kuomba msamaha kwa Clouds saa hilo jambo halijafanyika.

Lakini pamoja na hayo yote nilitegemea Mamneja wa Diamond hasa Salam Sk wakimya na si wapiga kelele au kushutumu watu ooooh wanataka kumshusha Diamond,ooh wana chuki kitu ambacho pengine si cha uhakika bali ni hisia....kwakweli Maneneja wa Diamond wamekuwa watu wa kuendekeza migogoro na kumbebesha migogoro Diamond isiyo na tija......
Sioni sababu ya Salam kuanza kutamba na kutoa povu instagram kwa jambo pengine halipo kabisa maana hata dunia inajua kuwa ni vigumu sana kumshusha Diamond kwa sasa maana walishamuacha akapanda...

Kama ni swala la Iyobo kuwapiga wambea wa Clouds hayo ni maswala yanayo muhusu Iyobo na wale wambea waliotandikwa hivyo ni vyema na ni busara kwa mameneja kujiweka pembeni na jambo hilo kwanza ni jambo la wanawake hivyo si vyema kujihusisha nalo.

Pamoja na WCB kupanga kufungua vituo vyao vya radio bado kabisa vyombo vilivyopo vinahitajika sana tena sana kwa ustawi wa wa wasanii wa WCB hivyo ni vyema sana mameneja mkafanya jitihada za kutatua migogoro kuliko kuikuza.

Wasalaam

By Ruttashobolwa

Dawa Bora za Nguvu za Kiume na Kukosa Hamu ya Tendo la Ndoa

0
0
DAWA BORA ZA NGUVU ZA KIUME NA KUKOSA HAMU YA TENDO LA NDOA
Baada ya utafiti wa muda mrefu juu ya matatinzo ya upungufu wa nguvu za kiume na ukosaji wa hamu ya tendo la ndoa ama kushindwa kurundia tendo kwa haraka Sasa inakuletea suluhisho juu ya matatizo haya kwa kutumia dawa za FULL POWER

Full Power dawa asili yenye vidonge inayotibu tatizo la upungufu au ukosefu wa nguvu za kiume dawa hii inamchanganyiko wa kutosha kuzalisha vichocheo vingi vya hernone za gestro gen zikiwemo vitamin b6 na b1 vitamin e pamoja na madini aina ya zinc

Itakufanya kuwa na nguvu na mzunguko mzuri wa damu na kuongeza hamu na uwezo wakufanya tendo la ndoa zaidi hatua nne au zaidi na kuchelewa kufika kileleni zaidi ya dakika 20/30 ZAT 50

Inarundisha maumbile ya uume yaani kurefusha na kunenepesha nchi 3/7 na upana cm 3/4 standard.kiafya haijalishi umri wako hata kwa wazee ukitumia maumbile yatabaki kuwa hivyo siku zote pia anatibu matatizo mengine kama presha kisukari ngiri chango la tumbo kujaa gesi kutopata choo vizuri minguu kuwaka moto matatizo ya uzazi bawasili na magonjwa ya zinaa kama kisonono na kaswende

Tunapatikana Dar es Salaam  na mikoan wasiliana na DR Oshinda no 0755505099 au 0714126118  Karibuni kwa hunduma bora

Lemutuz Adai ni Rafiki Mkubwa wa Tundu Lissu...Adai Alimsaidia Wakiwa Marekani..

0
0

Lemutuz Jana aliweka picha Hii kwenye ukurasa wake wa Instagram na kudai Tundu Lissu ni Rafiki yake mkubwa:

Jisomee Hapa chini alichoandika:

From @lemutuz_superbrand - SUPER MEMORY....nimeikuta maktaba ...with my Great Friend Mh. Tundu Lissu Mwaka 2010 baada ya kumpokea JFK/New York City na kumuendesha na gari langu binafsi mpaka Connectcut State/USA ..ambako tulienda kuhudhuria Sherehe za Dada yake kumaliza Degree at Conn. State University.....najua enzi hizo vijana wengi wadogo humu instagram mlikua hamjui lolote na wengi mlikua hamjazaliwa...ila mnajua kelele tu za mlango.....Ndugu yangu Lissu siasa pembeni Mungu Akutangulie Ndugu yangu Upone haraka! ...AMEN! - le Mutuz

Tundu Lissu Amuumbua Lemutuz Baada ya Kudai ni Rafiki yake " Lemutuz Asilazimishe Urafiki"

0
0

Baada ya Lemutuz kuandika katika ukurasa wake kuwa Tundu Lissu alikuwa rafiki yake mkubwa...Tundu Lissu amefunguka na kudai Lemutuz asilazimishe urafiki ambao haukuwepo...

Jisomee Hapa chini:
_

From @tundulissutz - LEMUTUZ ASILAZIMISHE URAFIKI USIOKUWEPO!!! .

Leo nimeonyeshwa post iliyopo kwenye Instagram account ya William Malecela aka Lemutuz.

Kwenye post yake, Lemutuz amedai kwamba mimi ni rafiki yake mkubwa na wa miaka mingi, kabla vijana wengi wanaopiga makelele mitandaoni hawajazaliwa.

Lemutuz ameeleza kwamba mwaka 2010 alinipokea Uwanja wa Ndege wa John F. Kennedy, mjini New York, nilipoenda kwenye mahafali ya dada yangu. .

Amewaambia wasomaji wake kwamba alinichukua kwenye gari yake binafsi kutoka JFK hadi Connecticut kwenye graduation ya dada yangu aliyodai ilikuwa Connecticut State University. .

Ili kuthibitisha kauli zake, Lemutuz ameambatanisha picha niliyopiga naye, ambayo nitaielezea shortly. .

Naomba kuweka ukweli wa kauli za Lemutuz wazi ili kuweka rekodi sawa.

Kwanza, nimemfahamu Lemutuz tangu mwezi Mei, 2011. Nilikutana naye mara ya kwanza kwenye mahafali ya mdogo wangu kaka (sio dada) Vincent Mughwai, aliyekuwa anasoma Bridgeport University (sio Connecticut State University). Kama nakumbuka vizuri, Lemutuz alikuwa MC kwenye shughuli hiyo. Na siku hiyo kulikuwa na Watanzania wengine wengi waishio Marekani. .

Lemutuz hakunipokea mimi JFK wala kunipeleka Bridgeport, Connecticut, kwenye gari yake binafsi. Hatukuwa tunafahamiana kabla ya kukutana kwenye graduation ya kaka Vince, siku kadhaa baada ya mimi, mke wangu na ndugu zangu wengine kuwasili Marekani. .

Pili, ni kweli tulipiga picha ambayo ameitoa kama uthibitisho wa 'urafiki' wetu. Siku hiyo, kama ilivyo kwenye shughuli kama hizo, nilipiga picha na Watanzania karibu wote waliohudhuria graduation hiyo...

Kama Lemutuz, wengi wa niliyopiga nao picha nilikuwa siwafahamu kabisa kabla ya kukutana nao siku hiyo. .

Tatu, tangu siku hiyo sijawahi kufanya mawasiliano na Lemutuz ya aina yoyote. Nakumbuka tu kukutana na kusalimiana nae bungeni mwaka 2012, wakati alipokuja Dodoma akitaka kugombea ubunge wa Afrika Mashariki. .

Mimi sijajua sababu ya Lemutuz kutaka kulazimisha urafiki na mimi usiokuwepo. Yeye ni rafiki mkubwa wa Bashite na mpiga debe wa Rais Magufuli. .

Mimi ni mpinzani mkubwa wa Magufuli na nimelipa gharama kubwa kwa sababu ya msimamo wangu tangu Magufuli aingie madarakani. .

Huo 'urafiki mkubwa' unaodaiwa kuweka kati yangu na Lemutuz msingi wake ni nini???
.

Mwisho, ukitaka kuongopa hadharani basi angalau uwe na kumbu kumbu sahihi. Lemutuz anadai tulikutana 2010 wakati ilikuwa Mei 2011. .

Anadai nilikwenda kwenye graduation ya dada yangu (ambaye hata jina hakumtaja!) wakati ilikuwa graduation ya kaka yangu Vincent Mughwai. .

Anadanganya ilikuwa Connecticut State University wakati ilikuwa Bridgeport University. Anadai alinipokea JFK wakati nilipokelewa na kaka yangu Vincent. .

Na tangu nimepigwa risasi na kujeruhiwa vibaya na wanaoitwa 'watu wasiojulikana', rafiki yangu mkubwa huyu hajawahi kunitumia hata kadi ya pole!!! .

Huu ni urafiki feki wa kuwadanganyia Watanzania wasioelewa. .

Msidanganyike!!!

By Tundu Lissu

Idriss Sultani: Umaarufu Wangu Wasababisha Wanawake Waniogope

0
0
Idriss Sultani: Umaarufu Wangu Wasababisha Wanawake Waniogope
Mfanyabiashara na mchekeshaji maarufu bongo Idriss Sultani amekiri wazi kwa sasa wanawake wengi na warembo wanamuogopa kuwa naye kwenye mahusiano kutokana na kazi yake pamoja na umaarufu alionao.


Idris amefunguka hayo leo akiwa kwenye kipindi cha Kikaangoni Live kinachorushwa kupitia ukurasa wa Facebook wa EATV nakusema kwamba wanawake wanaoonekana sahihi kwake yaani wenye msimamo, akili na wasio tegemezi wanaogopa kuwa naye kwa  kudhani kwamba  maisha yao yatakuwa yakufatwa fatwa na mapaparazi pamoja na magazeti ya udaku.

Idris ameongeza kuwa wakati mwingine anadhani kazi yake ya uchekeshaji nayo pia ndiyo sababu pia akose wanawake wenye vigezo vyake kwani watu wanahisi kuwa anakuwa hayupo 'serious' katika suala zima la mahusiano.

"Kabla mtu hajakutana na wewe anakuwa ameshakujaji kila kitu kiasi kwamba mpaka anakufikia anaweza kusema huyu dogo kichaa. Wanahisi sisi 'comedian' hatupo serious hawadhani kama tunaweza kupenda lakini cha ajabu wenzetu huko nje ya nchi wanapata wanawake wazuri yaani pisiii kweli kweli.." Idris

Idriss ameongeza kwamba "kuwa mchekeshaji n moja ya kigezo kinachonifanya nisipate 'a proper women' ninayemtaka.

Miujiza ya Sharifu Seif Mohamed..JE Umeachwa na Mme/Mke au Mpenzi, Umesongwa na Mitihani ya Maisha..Piga Simu Upate Muujiza Wako

0
0

SHARIFU SEIF MOHAMED ANAWASHUKURU WALE WOTE WANAOENDELEA KUPIGA SIMU, WENYE MATATIZO NA WALE WANAOTOA  SHUKRANI NA SHUHUDA JINSI TIBA ZAKE ZINAVYO WASAIDIA,

(Rudisha mahusiano yako ndani ya masaa 72 tu)

SHARIFU MOHAMED Ni  mtaalam na mnajimu maarufu wa nyota na kubashiri mambo yanayo watesa binadamu duniani kote na kupata ufumbuzi, Anatumia kitabu cha QUR'AN, Dawa za Asili, Dawa za Kiarabu na majini kwa kumtuliza mke/mme, mchumba au mpenzi ndani ya masaa 72 tu, na kutatua matatizo yote ya kimaisha,

Je Umeachwa na UMPENDAE awe Mme/Mke na bado unampenda? Je Umekimbiwa na Mmeo/ Mkeo n anaishi na mtu mwingine? Je Umejaribu sehemu nyingi bila mafanikio? Mpigie simu SHARIFU SEIF sasa hivi ujionee Muujiza wa Papo kwa Papo, Anauwezo wa hali ya juu wa kusambaratisha mahusiano yao na kumrejesha kwako haraka sana na Kumfanya Atimize Ahadi zote Ndani ya Muda Mfupi Endapo Utafwata Atakacho Kuelekeza

ANAZO DAWA ZA MAPENZI, NGUVU ZA KIUME, CHANGO NGIRI MAJI NA N.K, ZINDIKO LA NYUMBA NA BIASHARA, PETE ZA BAHATI, HUMALIZA KABISA TATIZO LA NGUVU ZA KIUME NA KUREFUSHA UUME KWA SAIZI UNAYOTAKA, HUZUIA CHUMA ULETE KWENYE BIASHARA, HURUDISHA MALI ZILIZOPOTEA, MAGONJWA SUGU, MIGUU KUWAKA MOTO AU KUFA GANZI, HUTIBU BUSHA BILA KUPASUA, ANAO UWEZO WA KUMRUDISHA ALIE MBALI AU ALIECHUKULIWA MSUKULE, KUPANDISHA NYOTA NA KUSHINDA BAHATI NA SIBU, KASAFISHA NYOTA NA KUKUPA MVUTO WA AJABU, KUTOA NUKSI NA VIFUNGO MBALIMBALI,  MAFANIKIO YA MAISHA NA UTAJIRI BILA MASHARI, NA MENGINE MENGI YA SIRI,

JE UMAHANGAIKA KUPATA MTOTO BILA MAFANIKIO? WASILIANA NA MTAALAMU HUYU KWANI YEYE HUFAULU PALE WOTE WALIPOSHINDWA, PIA UMALIZA KAZI ZILIZO SHINDIKANA NA WATAALAM WENGINE NDANI YA MASAA 24 TU,

(NA ANATIBU KWA NJIA YA SIMU UKIWA NCHI YOYOTE AU MKOA WOWOTE ENDAPO UTAFWATA MAELEKEZO YAKE)

Kwa ushauri na mawasiliano  zaidi Piga SIMU No:

Mobile +255 654-836970
WhatsApp +255 756-033670

Chabo Zamkimbiza Davina

0
0
Chabo Zamkimbiza Davina
MUIGIZAJI wa sinema za Kibongo, Halima Yahaya ‘Davina’ amejikuta akitoka nduki baada ya kushtukia anapigwa chabo na makonda wa daladala.

Tukio hilo la aina yake lilitokea mwishoni mwa wiki iliyopita maeneo ya Ubungo- Mawasiliano wakati Davina na wenzake wakiwa wanarekodi sinema inayokwenda kwa jina la Kashinde ya inayoandaliwa na Kampuni ya Lugwa.

Wakati akibadilisha nguo kuuvaa uhusika wa ‘ukonda’ nyuma ya gari, ghafla walitokea makonda halisi ambao walimfanya atimke haraka akihofia kuchunguliwa.

“Daah! Kazi yetu hii ina changamoto wakati mwingine inabidi ujitoe kidogo ufahamu lakini pale niliamini hakuna mtu angeweza kufika sijui wale makonda walitokea wapi,” alisema Davina.

Sanchi Ataja Vigezo vya Mwanaume Ambaye Anataka Kuwa Mume Wake

0
0
Sanchi Ataja Vigezo vya Mwanaume Ambaye Anataka Kuwa Mume Wake
MWANAMITINDO mwenye umbo matata Bongo, Jane Rimoy ‘Sanchi’ ametaja vigezo vya mwanaume ambaye angependa kuwa mume wake.

Akizungumza na gazeti hili, Sanchi alisema kuwa anapenda sana mwanaume mwenye muonekano wa kimazoezi na pia mwenye kujielewa na kuweza kutafuta kwa hali na mali ili maisha yaeleweke.



Akizidi kutiririka, Sanchi alisema kuwa hapendi mwanaume ambaye amevutiwa kwa kumuona kwa umbo na sura yake bali mwenye kumpenda kweli kutoka moyoni.

“Unajua mwanaume anaweza kukuona akakutamani tu lakini anaweza akawa hana vigezo kabisa, kwangu mimi mwanaume mwenye muonekano wa kiume na mtafutaji ndiyo mwenye nafasi kwangu lakini mimi siangalii sura,” alisema Sanchi huku akisema mwanaume huyo bado hajampata hadi sasa.

Mtolea: Kusamehewa Babu Seya na Mwanaye Halikua Jambo Jema

0
0
Mtolea:  Kusamehewa Babu Seya na Mwanaye Halikua Jambo Jema
Mbunge wa Temeke kwa tiketi ya (CUF) Mhe. Abdalah Mtolea ameibua sakata la kusamehewa Babu Seya na mwanae, Johnson Nguza 'Papii Kocha' na kusema halikuwa jambo jema kwa kuwa watu hao mahakama iliwabaini kuwa ni wabakaji.


Mtolea amesema hayo leo Februari 7, 2018 akiwa bungeni na kudai kitendo cha watu hao kuachiwa na kupewa heshima na Serikali ikiwa pamoja na kuwapandisha kwenye majukwaa mbalimbali na kuwapa ufadhili haileti picha nzuri kwa jamii.

"Kwenye maadhimisho ya Uhuru wa Tanganyika ukatoka msamaha kwa Babu Seya na wenzake watu ambao pasipo na shaka mahakama zilithibitisha kwamba hawa watu ni wabakaji sasa tunapokuwa tunasamehe wabakaji uko wapi ulinzi wa watoto wa taifa hili,tunawapandisha kwenye majukwaa wafanye show yaani tunawaona kwamba ni kioo cha jamii je wanafundisha nini? Alihoji

Mhe. Mtolea aliendelea kusema kuwa "Je, mnataka kwamba siku ya mwisho tukiwauliza watoto ukiwa mkubwa unataka kuwa kama nani aseme nataka kuwa mbakaji?

Babu Seya na mwanaye Papii wanategemea kuachia kazi yao mpya muda si mrefu baada ya kuiaanda mara tu baada ya kupewa msamaha na Rais John Pombe Magufuli

Korea Kaskazini Kuonyesha Uwezo Wake wa Kijeshi Kabla ya Olimpiki

0
0
Korea Kaskazini Kuonyesha Uwezo Wake wa Kijeshi Kabla ya Olimpiki
Taifa la Korea Kaskazini linatarajiwa kuandaa maadhimisho ya 70 ya gwaride la jeshi lake kabla ya kufanyika kwa michezo ya Olimpiki ya majira ya baridi nchini Korea Kusini.

Gwaride la kila mwaka la Pyongyang linaloadhimisha kuanzishwa kwa jeshi la Korea Kaskazini limekuwa likifanywa kila mwezi Aprili kwa kipindi cha miaka 40.

Hatahivyo vyombo vya habari nchini humo vilitangaza mapema mwaka huu kwamba tarehe ya kufanyika kwa gwaride hilo la kijeshi imebadilishwa hadi Februari 8.

Korea Kaskazini imepuuzilia mbali ukosoaji wa mpango wake ikisema kuwa hakuna mtu aliye na uwezo wa kuishutumu.

''Ni utamaduni na swala muhimu sana kwamba kila taifa duniani linasherehekea uzinduzi wa jeshi lake' , kilisema chama tawala cha wafanyikazi Rodong Sinmun.


Marekani imesema kuwa ingependelea gwaride hilo kutofanyika kwa kuwa kwa sasa watu wanalenga michezo ya Olimpiki.

Siku ya Alhamisi, Korea Kaskazini ilisema kuwa haina mpango wa kukutana na maafisa wa Marekani , kulingana na chombo cha habari nchini Korea Kaskazini KCNA.

Serikali ya Korea Kusini imesema kuwa mwezi uliopita kwamba wanajeshi 13,000 na vifaa 200 vilipatikana karibu na uwanja wa ndege wa Pyongyang katika kile kinachoonekana kuwa gwaride la majaribio.

''Kile tunachotarajiwa kuona katika gwaride hilo la kijeshi ni magari ya kubeba silaha, idadi yake na iwapo yanabeba silaha mpya'' , alisema David Schmerler, mchanganuzi wa Korea Kaskazini katika kituo cha James Martin cha masomo ya kuzuia kusambaa kwa silaha

Tanzia : Mwanasiasa Mkongwe wa Chadema Afariki Dunia

0
0
 Tanzia : Mwanasiasa Mkongwe wa Chadema Afariki Dunia
Mwanasiasa mkongwe na kada wa Chama cha kidemokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Tambwe Hizza amefariki dunia asubuhi ya kuamkia leo (Alhamis ) akiwa nyumbani kwake.


Taarifa hiyo imethibitishwa na mgombea Ubunge wa Jimbo la Kinondoni ambaye pia ni Naibu Katibu Mkuu wa chama hicho Salum Mwalimu alipowasili katika kipindi cha 'East Africa Breakfast' kinachorushwa kutoka East Afrika Radio.

"Ni kweli Tambwe Hizza amefariki nami nimetumiwa ujumbe mfupi mara nilipofika hapa East Afrika Radio kama kiongozi wa chama, hivyo naomba tupewe muda kidogo ili tuweze kufahamu zaidi chanzo cha kifo chake maana imekuwa ghafla sana kutokana mpaka jana usiku saa 5 nilikuwa nae", amesema Mwalimu.

Kwa upande mwingine, Salum Mwalimu amesema mpaka jana marehemu Tambwe Hizza alikuwa nae katika kuomba ridhaa kwa wananchi wa jimbo la Kinondoni ili aweze kuwa Mbunge wa Jimbo hilo katika siku za usoni.

Haji Manara Awatumia Vijembe Waliokuwa Wanambeza Okwi “Hivi Kale Kamsemo Kuwa Okwi Mhenga Bado Kapo?”

0
0
Haji Manara Awatumia Vijembe Waliokuwa Wanambeza Okwi “Hivi Kale Kamsemo Kuwa Okwi Mhenga Bado Kapo?”
Wekundu wa Msimbazi Simba SC Jumatano ya February 7 2018 walikuwa uwanja wa Taifa DSM kucheza mchezo wa marudiano wa Ligi Kuu dhidi ya Azam FC, Simba katika game hiyo walifanikiwa kuibuka na ushindi wa goli 1-0 limefungwa na Emmanuel Okwi dakika ya 37.

Goli hilo la Okwi linakuwa ni goli lake la 13 katika Ligi msimu huu akiongoza katika list ya wafungaji hadi sasa, baada ya game hiyo afisa habari wa Simba Haji Manara ametumia ukurasa wake wa instagram kuhoji kuhusiana na wale waliokuwa wanambeza Okwi na kumtania kuwa mhenga.


Hivi kale kamsemo kuwa Okwi ni mhenga bado kapo huko kwenu? Au kale kamsemo kuwa naniliu kashushwa na Mungu sikisikii siku hz, Muweke akiba bandugu,,mpo kimyaaaa kama mwanga alioanguka na Ungo sokoni…Bumbaaaaav 😂😂 @emmanuelokwi @nyoni #gongowazi#gongowazi“

Wema Sepetu na Diamond Watinga Mahakamani Kisutu...

0
0

KISUTU: Msanii Wema Sepetu leo amefika Mahakamani kufuatilia kesi yake ya kukutwa na msokoto wa Dawa za Kulevya aina ya Bangi

Wema amefika Mahakamani hapo akiwa na Wakili Albert Msando aliyetangaza kumtetea baada ya Wakili Peter Kibatala kujitoa kumtetea msanii huyo

Wakati huo huo, Msanii wa Muziki nchini, Naseeb Abdul(Diamond Platnumz) naye amefika Mahakamani hapo na Mzazi mwenzake Hamisa Mobetto kwa ajili ya kusikiliza shauri lao la matunzo ya mtoto

Shauri hilo la matunzo ya mtoto lilifunguliwa na Hamisa Mobetto akiomba Mahakama iamuru Diamond kutoa matunzo ya mtoto kila mwezi

Pigo lingine kwa Chadema Wanachama wa Chadema 11 atimkia CCM

0
0

Wanachama 11 wa Chadema, akiwamo Mwenyekiti wa Serikali ya Kijiji cha Kasange, Wilaya ya Ngara mkoani Kagera, Zedekia Yusuf wamejivua uanachama na kutimkia Chama  cha Mapinduzi (CCM).

Akiwaongoza wenzake kutangaza uamuzi huo wakati wa sherehe za maadhimisho ya miaka 41 ya kuzaliwa kwa CCM zilizofanyika kiwilaya katika Kijiji cha Kasange, Yusuf ametaja migogoro baina yake viongozi na wenzake wa Chadema kuwa miongoni mwa sababu za yeye kutimkia CCM.

Ametaja sababu nyingine kuwa ni viongozi wenzake kukwamisha utekelezaji wa miradi ya maendeleo ikiwamo ujenzi wa miundombinu ya barabara, miradi ya elimu, afya na maji.

“Kwa bahati mbaya, wajumbe 13 kati ya 25 wa Serikali ya kijiji ambao wanatokana na Chadema ndiyo walikuwa kikwazo kwa kupitisha uamuzi,  baadhi wanaonekana kuwa wachochezi ikiwamo kugomea michango ya miradi ya maendeleo,” amesema Yusuf.

Akipokea wanachama hao wapya, Mjumbe  wa Halmashauri Kuu ya CCM mkoani Kagera, Issa Samma amewataka kushirikiana na wenzao waliowakuta ili kukijenga chama tayari kwa ajili ya ushindi katika chaguzi mbalimbali zijazo.

Akizungumzia wanachama wa chama chake kuhamia CCM, Mwenyekiti wa Chadema Wilaya ya Ngara, Kennedy Stafford amesema licha ya kuonyesha kutojali hisia na imani ya wananchi waliowachagua, mwenyekiti huyo na wenzake wana haki ya kikatiba na kisheria kujiunga na chama chochote cha siasa wanachokipenda.

Jamal Malinzi Hali Tete Mahakamani

0
0

Kesi inayomkabili aliyewahi kuwa Rais wa Shirikisho la Mpira nchini Tanzania (TFF), Jamal Malinzi ya kuhujumu uchumi imeahirishwa mpaka Feburuary 22, 2018 ya mwaka huu.

Chanzo cha kuahirishwa kwa kesi hiyo ni kutokana na DPP kushindwa kukamilisha kusaini hati ya mashtaka hayo.

Hakimu Mkazi wa Mahakama ya Kisutu, Wilbard Mashauri ambaye anasimamia kesi hiyo ameutaka upande wa Jamhuri kuhakikisha hati hiyo inasainiwa mpaka kufikia tarehe hiyo ili kesi iweze kuendelea mahakakamani hapo.

Awali Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) iliieleza Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kuwa wamekwisha kamilisha upelelezi wa kesi hiyo inayowakabili viongozi hao wa zamani wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF).

Kutana na Mtabibu Mwenye KUBRI kutoka kwa ALLAH issa simba said Mtabibu wa Nyota za Binadamu na Dawa za Asili

0
0

Kutana na Mtabibu Mwenye KUBRI kutoka kwa ALLAH issa simba said Mtabibu wa Nyota za Binadamu na Dawa za Asili ya Africa Mwenye UWEZO Kubaini tatizo lako Pindi tu Utakapo Fanya Mawasilino Kupitia Wasaa Husika..

JE UNASUMBULIWA NA Mapenzi? (Umeachwa na Umpendae,Awe Mume,Mke na Bado unampenda?Na Umejaribu Sehemu nyingi Bila Mafanikio?Wasilina na Maalim Hussein Ujione muujiza wa Papo kwa Papo.. anauwezo WA KURUDISHA MAHUSIANO NA KUIMARISHA NDOA YAKO NDANI YA SAA 12 TU.

Umekimbiwa na Mumeo,mkeo au Mpenzi na anaishi na mtu mwingine? Muone akutatulie Anauwezo wa Hali ya Juu wa Kusambalatisha Mahusiano yao Endapo utafata Atakacho kuelekeza.
Atamfanya Atimize Ahadi zote kwa Muda Mfupi.

Issa simba said Anatumia Jina la Muhusika au Picha Kumaliza Tatizo lako..
Anatibu kwa Kutumia Vitabu vya QUR-AN Dawa za Asili za Africa,Dawa za Kiarabu na Majini.Anatafsiri Ndoto. Kushinda BAHATI NASIBU, KUSAFISHA NYOTA. Mvuto wa Mwili na BIASHARA, Kinga ya Mwili,ZINDIKO za Nyumba.MIGUU Kufa GANZI.Kufungua KIZAZI kwa wale walio fungwa kwa njia za KISHIRIKINA. Anakupa Jini la Mali kwa yule anaehitaji Utajiri BILA MASHARTI. Nguvu za KIUME, Humaliza Kesi zilishindika ndani ya siku 14 tu..
na mengi zaidi

+255 622588038au 0679119679 au +255 764318107
NB: TIBA KWA DINI ZOTE NA IMANI ZOTE...

Salum Mwalimu na Mtulia, Wavaana Live Uso Kwa Uso

0
0
Zikiwa zimebakia takribani siku 9 kuelekea marudio ya uchaguzi mdogo wa marudio katika Jimbo la Kinondoni hali imekuwa tofauti kwa wagombea Salum Mwalimu pamoja na Maulid Mtulia kwa kutoleana maneno ya kejeli pindi walipokutana uso kwa uso.

Wakizungumza katika nyakati tofauti tofauti leo (Alhamisi) kwenye kipindi cha 'East Africa Breakfast' kinachorushwa kutoka East Africa Radio wagombea hao ambapo ndio mara ya kwanza kukutana pamoja kuongelea masuala ya maendeleo katika jimbo hilo ambalo kila mmoja analiwinda kwa namna yake ili aweze kuwatumikia wananchi hao katika siku za usoni kutoka sasa.

Salum Mwalimu amesema sio kweli kwamba ukiwa katika chama tawala kama anavyojitapa mgombea mwenzake kuwa ndio chanzo cha kupelekea maendeleo wananchi kwa madai maendeleo yanapangwa ndani ya Bunge nasio penginepo.

"Mimi niseme tu maendeleo yanapangwa bungeni na hakuna mtu mwingine anaweza kupanga nje ya Bunge. Unapojadili bungeni mule hayapangwi kwa vyama, kwamba wewe ni chama X unapewa kikubwa na mwingine Y amepewe kidogo hapana. Keki ya taifa hii tunayoiita ni ndogo ndio maana uwezo wa kuhimili bajeti yetu ya maendeleo kwa mwaka haitoshelezi tunalazimika kuomba misaada na kulazimika kukomba sehemu nyingine mbalimbali", amesema Salum Mwalimu.

Kutokana na hayo, Maulid Mtulia amemjibu mwenzake kwa kudai hajui alisemalo kwa kuwa hajawahi kuwa hata Mbunge hivyo hapaswi kusema lolote juu ya hilo.

"Kwanza kaka yangu hajawahi kuwa Mbunge kwa hiyo anachokisema hakijui kama ninavyokijua mimi, mwenzake nimekaa miaka miwili na yeye anasema anataka kwenda kukalia kiti changu kwa hiyo kwa maana nyingine achunge maneno yake asiseme asiyoyajua. Mimi ndio napaswa kusema", amesema Mtulia.

Kwa muendelezo wa habari hii tazama hii video chini uone jinsi Salum Mwalimu pamoja na Maulid Mtulia wanavyoongea zaidi.

Majibu ya Serikali Kuhusu Zile Milioni 50 Ilizoahidi Kwa Kila Kijiji

0
0

Mkurugenzi wa Idara ya Habari na Msemaji Mkuu wa Serikali, Dk. Hassan Abbasi amesema kuwa serikali itaweka utaratibu utakaowezesha kutekelezwa kwa ahadi ya kutolewa milioni 50 kila kijiji, hivyo wananchi wasiwe na hofu.


Dkt Abbasi aliyasema hayo jana jijini Dar es Salaam alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari kuhusu masuala mbalimbali na miradi inayotekelezwa na serikali, na kuweka bayana kwamba, tayari mambo makubwa zaidi yameshafanyika, na hivyo hilo la milioni 50 kila kijiji litatekelzwa pia.


Majibu hayo aliyatoa baada ya mmoja wa waandishi wa habari kuulizwa swali, baada ya kuona ni mwaka wa tatu sasa tangu Rais Dkt Magufuli alipoingia madarakani, lakini ahadi yake ya kutoa TZS milioni 50 kila kijiji kwa ajili ya kuwasaidia kina mama na vijana kujikwamua kiuchumi haijatekelezwa.


“… 50 nyenyewe tutaweka utaratibu itakuja tu ikifika. Lakini maji si yanakuja bana, dawa si zipo, barabara si zipo, sasa kama wewe ulitaka ile 50 ili upige dili, tulia kwanza.”


Aidha, Dkt Abbasi amesema kwamba, ilani ya Chama cha Mapinduzi (CCM) haikusema ni lini ahadi hiyo itatekelezwa, kama ni 2017 au 2018, hivyo akawataka wananchi kuwa na subira, pindi utaratibu ukikamilika watapatiwa fedha hizo.
Viewing all 104432 articles
Browse latest View live




Latest Images