Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104789 articles
Browse latest View live

Habari Njema: Tunatibu Busha, Korodani Kuvimba, Ngiri, Miguu Kufa Ganzi Pamoja na Matatizo ya Nguvu za Kiume

$
0
0

Ni dawa ya nguvu za kiume inayorefusha na kunenepesha uume saizi uipendayo (Inch 1-7) kwa muda wa siku 6 tu.Dozi hii itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa muda wa dakika 30, utarudia tendo la ndoa zaidi ya mara 4 bila hamu kuisha bila kujali umri na garantee ni miaka 60 baada ya kutibu tatizo.

Pia tunatibu Busha bila kufanyiwa Oparesheni, korodani moja kuvimba, ngiri, tumbo kujaa gesi na kuunguruma, kutopata choo vizuri, miguu kuwaka moto na kufa ganzi, chango la wanawake, kisukari na kutokwa na kinyama sehemu ya haja kubwa.

MIHAYO:
Inarudisha mke, mchumba, hawara na atakutimizia kila kitu unachotaka kutoka kwake ndani ya  saa 2 tu hata kama yupo mbali. atarudi na kumfunga asiwe na mwingine zaidi yako.

Umefukuzwa kazini? unataka kupandishwa cheo? Umepoteza pesa zako kwenye biashara bila kujua umepandikizwa chuma ulete? Njoo urudishe pesa zako. Unauza mali yako haiendi?


Wasiliana na mtaalam Challo kwa; 0714006521

Nyimbo za Babu Seya na Wanae Kuanza Kutoka Soon

$
0
0
Nyimbo za Babu Seya na Wanae Kuanza Kutoka Soon
Wanamuziki Nguza Viking maarufu ‘Babu Seya’ na mwanae Johnson Nguza ‘Papii Kocha’ wamesema Februari, 2018 nyimbo zao zitaanza kusikika maeneo mbalimbali nchini.

Kauli hiyo imetolewa jana Februari 9, 2018 na Papii Kocha wakati akizungumza katika kipindi cha Shilawadu kinachorushwa na televisheni ya Clouds, huku akiwataka Watanzania kukaa mkao wa kula kuwapokea upya.

Babu Seya, ambaye ni mtunzi wa kibao maarufu cha “Seya”, na mwanaye Papii Kocha wameshirikiana katika wimbo huo, ni miongoni mwa wafungwa 8,157 waliosamehewa na Rais John Magufuli siku ya Uhuru wa Tanganyika.

Walikuwa kati ya wafungwa 61 waliokuwa na adhabu za vifungo vya maisha na kunyongwa ambayo si rahisi kupata msamaha wa kawaida wa mkuu wa nchi unaotolewa siku ya sherehe hizo.

Baada ya msamaha huo, familia ya wanamuziki hao ilikwenda Ikulu kumshukuru Rais John Magufuli na siku chache baadaye Naibu Waziri wa Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo, Juliana Shonza aliwakutanisha na uongozi wa studio ya Wanene iliyokubali kuchukua jukumu la kuwarejesha tena katika muziki.

Watangazaji wa Clouds walizungumza na wanamuziki hao nje ya studio za Wanene ambako walikuwa wakiendelea na taratibu za kuandaa nyimbo zao.

“Wakati wowote tutatoa nyimbo na mwezi huu (Februari) Watanzania wakae mkao wa kula. Tunajua Watanzania wanatupenda na sisi tunawapenda. Matatizo tuliyopata ni makubwa kwa sasa tunahitaji sapoti yao tuweze kula, hata ngozi irudi vizuri tupake mafuta mazuri,” amesema Papii Kocha.

Alipoulizwa tukio ambalo hatalisahau, amesema ni ndugu zake waliofariki dunia wakati akiwa amefungwa.

Kuhusu mahusiano ya kimapenzi baada ya kutoka jela amesema, “Miaka 14 nayo ni mingi maisha yanatakiwa yaendelee. Hata mheshimiwa aliniambia nioe.”

Watangazji wa kipindi hicho walipomuuliza kama tayari amepata mchumba, Papii Kocha amesema, “Sijampata ila natafuta bwana si unajua lazima uangalie kwanza. Hata Diamond ameimba wimbo kwamba wazuri ni wengi ila kumpata mwenye mapenzi ya kweli ndio balaa. Michepuko haina dili.”

Papii Kocha alipoulizwa ni kitu gani kiliwakuta mpaka wakahukumiwa kifungo cha maisha amesema, “Unajua Mussa alipochapa fimbo bahari ya shamu aliagizwa na Mwenyezi Mungu akawatoe watu wake awapeleke kwenye nchi ya ahadi. Ya Misri tuachane nayo tuangalie ya Kaanani.”

Kwa upande wake Babu Seya alipoulizwa tukio ambalo hatolisahau katika maisha yake amesema, “Tukio baya ni kufungwa kwa miaka hiyo yote na tukio la pili ni ule waraka tuliomuandikia Rais ambao Shilawadu mliusoma. Tunawashukuru sana.”

Hiki Hapa Kikosi Cha Yanga Kitaachoshuka Dimbani Leo

$
0
0
Hiki Hapa Kikosi Cha Yanga Kitaachoshuka Dimbani Leo
Mabingwa wa kihistoria wa ligi kuu soka Tanzania Bara klabu ya Yanga imeweka hadharani kikosi chake kitakacho shuka dimbani hii leo kuivaa timu ya St Lous  ya Seychelles katika mchezo wa klabu bingwa barani Afrika.

Yanga SC ambayo inaongozwa na Kocha wake Mkuu raia wa Zambia, George Lwandamina itashuka uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam kuikabili timu hiyo ya St Lous ikiwa ni mchezo wa raundi ya kwanza wa Klabu bingwa barani Afrika huku mgeni rasmi katika mechi hiyo akiwa ni Mh. George Mkuchika.

Kitambulisho cha Taifa Kimekua Dili

$
0
0

Kitambulisho cha Taifa Kimekua Dili
Kati ya vitu muhimu ambavyo mwananchi yeyote anapaswa kuwa navyo kwa sasa ni Kitambulisho cha Taifa.

Umuhimu huo hautokani na kumtambulisha mwananchi kuwa ni raia wa Tanzania tu, bali sasa ndicho kitakachomuwezesha kusajili kampuni, kuomba hati ya kusafiria na kupata cheti cha kuzaliwa.

Kitambulisho hicho kinachotolewa na Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (Nida), ni mkakati wa Serikali kuhakikisha kuwa kila Mtanzania mwenye miaka 18 na kuendelea anakuwa nacho ili kumwezesha kupata huduma muhimu.

Januari 31, Kamishna Jenerali wa Idara ya Uhamiaji, Dk Anna Makakala alisema ili Mtanzania apate hati ya kusafiria ni lazima awe na Kitambulisho cha Taifa na si vinginevyo.

Wakati Uhamiaji ikisisitiza kitambulisho hicho, jana Wakala wa Usajili wa Kampuni (Brela) ulitangaza kuanza kusajili kampuni kwa njia ya mtandao huku kigezo kikuu ili kusajili kikiwa Kitambulisho cha Taifa.

Taarifa ya Brela iliyotolewa jana inasema ambao hawajasajiliwa kupata vitambulisho, wataendelea kusajiliwa kwenye ofisi za Nida.

Juzi, Wakala wa Usajili, Udhamini na Ufilisi (Rita) ulisema kuanzia sasa, wananchi wanaweza kutumia Kitambulisho cha Taifa na cha kupiga kura kupata cheti cha kuzaliwa.

Baadhi ya mambo muhimu kuhusu kitambulisho hicho ni kusaidia kuongeza wigo wa mapato ya Serikali, kumtambua mhusika kirahisi anapohitaji kupatiwa huduma katika taasisi mbalimbali kama vile benki, taasisi za mikopo na huduma za afya.

Pia, vitarahisisha kuwatambua wakwepaji wa kurejesha mikopo kutoka kwenye benki na asasi mbalimbali za fedha nchini, kuweka kumbukumbu za matukio ya uhalifu katika daftari la kumbukumbu la kielektroniki.

Kitambulisho hicho kitawezesha pia kumtambua mtu anapofanya biashara au shughuli nyingine kwa kutumia majina tofauti. Vitahakikisha kuwa mtu anapata stahili zake za jamii.

Kwa mfano, kupata malipo ya pensheni, haki za matibabu, haki za kujiunga na masomo ikiwa ni pamoja na stahili zozote ambazo raia wa Tanzania anastahili kupata kirahisi kwani kupitia Kitambulisho cha Taifa, mwananchi atatambulika kirahisi (nani ni nani, yuko wapi na anafanya nini.

Umuhimu mwingine ni kuondoa watumishi hewa kwenye mfumo wa malipo ya mishahara ‘payroll’ ya Serikali, kuimarisha utendaji kazi serikalini kwa kuwa na kumbukumbu sahihi za watumishi na malipo ya stahili zao, hasa pale wanapostaafu.

Pia, vitarahisisha kazi ya kuhesabu watu (sensa), kurahisisha kazi ya kuhuisha daftari la wapigakura, kazi ambayo kwa sasa hufanyika mara mbili kabla ya uchaguzi mkuu.

Lulu Diva Afunguka Kuhusu Uhusiano Wake na Rich Mavoko

$
0
0
Lulu Diva Afunguka Kuhusu Uhusiano Wake na Rich Mavoko
Msanii wa muziki Bongo, Lulu Diva amefunguka ukaribu wake na Rich Mavoko na namna unavyokuwa ukiripotiwa.

Muimbaji huyo ambaye anafanya vizuri na ngoma ‘Amezoea’ ameiambia Back Stage ya EA Radio kuwa hakuna mahusiano yoyote kati yake na Rich Mavoko na ni stori tu ambazo na wao wanazisikia.

“Rich Mavoko ni mshikaji wangu wa karibu sana na tunaongea mambo mengi sana, wala tulikuwa hatuzijali kwa sababu kila mmoja wetu anajua sio kweli au ni kweli katika moja,” amesema.

“Kila mmoja anajua ukweli ambao upo ndani ya moyo wake, tujawahi kuzizungumzia kwanza,” ameongeza.

November mwaka jana alipoulizwa kuhusu ku-date na Lulu Diva alisema wao ni marafiki wa kawaida tu.

Kim Jong-un Amualika Rais wa Korea Kusini

$
0
0
Kim Jong-un Amualika Rais wa Korea Kusini
Kiongozi wa taifa la Korea Kaskazini Kim Jong un amemualika rais wa Korea Kusini Moon Jae-in kuzuru Pyongyang.

Utakuwa mkutano wa kwanzakatika kipindi cha zaii ya mungo mmoja katika ya viongozi hao wa Korea.

Bwana Moon amesema kuwa Korea ni muhimu kuhakikisha kuwa mkutano huo unafanyika huku akiitaka Korea Ksakzini kurudi katika meza ya mazungumzo na Marekani.

Mualiko huo ulioandikwa ulikabidhiwa kwa rais wa Korea Kusini na dadake rais Kim Jong un , Kim Yo Jong.

Katika mkutano wa kihistoria uliofanyika katika jumba la rais kabla ya kuanza kwa michezo hiyo ya msimu wa baridi.

Bi Kim na kiongozi wa kisherehe wa taifa la Korea Kaskazini Kim Yong-nam ndio viongozi wa ngazi za juu kutoka Kaskazini kuzuru kusini tangu vita vya Korea 1950.

Viongozi hao kutoka Korea hizi mbili walikula kabeji, wali na kuzungumza kwa takriban saa tatu.

Wakati huohuo Rais wa Korea ya Kusini Moon Jae amekuwa ni mwenye shughuli nyingi za kupokea ujumbe wa ngazi ya juu katika ikulu yake ya mjini Seoul, baada ya ufunguzi rasmi jana wa michezo ya Olympic ya msimu wa baridi nchini humo.

Ujumbe unaoangziwa zaidi ni ule wa Korea ya kazkazini ambapo jana ameamkuana na dada yake kiongozi wa Korea kaskazini Kim Jong un

Ulikuwa ni mara ya kwanza ujumbe kama huo wa maafisa wa ngazi za juu zaidi wa Korea Kaskazini kuwahi kuzuru Korea Kusini tangu kumalizika kwa vita vya Korea miaka 60 iliyopita.

Dadake rais wa Korea Kaskazini kushoto na makamu wa rais wa marekani Mike Pence kulia
Makamu rais wa Marekani, Mike Pence alisusia mwaliko wa chakula cha jioni ambacho alitakiwa kukaa meza moja na kiongozi wa serikali ya Korea Kaskazini Kim Yong-nam.

Taarifa kutoka chombo cha habari cha Yo hap kimesema kuwa Pence alionana kidogo na bwana Kim wakati wakijaribu kukwepana kuonana uso kwa uso.

Michezo hiyo inaendelea wakati ambapo kuna mvutano juu ya mpango wa nyuklia wa Korea Kaskazini ambao unapingwa vikali na majirani zake na vilevile Marekani.

Katika shughuli hiyo, Bwana Moon alisema anatarajia mashindano hayo ya michezo ya Olimpiki msimu wa baridi yataweza kukumbukwa kama siku nzuri ya kuanza kuwa na amani.

Mama Samia Ataja Sababu za Kuzuia Vibali vya Sukari

$
0
0
Samia Ataja Sababu za Kuzuia Vibali vya Sukari
Makamu wa Rais, Samia Suluhu Hassan amesema baadhi ya wafanyabiashara kutokuwa waaminifu ni moja ya sababu ya Serikali kuzuia vibali vya kuagiza sukari ya viwandani nje ya nchi.

Akizungumza katika ziara ya kikazi ya siku nne iliyoanza jana Februari 9, 2018 baada ya kutembelea kiwanda cha Food and Beverage kilichopo Ipogola ndani ya Manispaa ya Iringa, amesema Serikali ipo katika uhakiki wa viwanda.

Amesema baada ya uhakiki kukamilika wamiliki wa viwanda watapatiwa vibali vya kuagiza Sukari.

"Serikali imekusudia kukuza sekta ya viwanda tunahitaji mageuzi ya kiuchumi na katika utekelezaji wa jambo hilo, ni lazima tuchukue tahadhari kudhibiti mianya yoyote ya uchakachuaji kwa manufaa ya wachache,” amesema.

" Katika suala la sukari kumekuwa na udanganyifu, wapo watu waliagiza sukari kwa madai kuwa ni ya viwanda lakini ilipofika waliisambaza na kuiuza mitaani.”

Katika hatua nyingine, Suluhu amewataka wakazi wa Iringa kutunza amani ili kuwezesha mazingira salama ya uwekezaji na ukuzaji wa uchumi.

"Hivi sasa tunaelekea Tanzania ya viwanda tunajenga uchumi wa viwanda ninaomba mtambue kuwa mahali popote penye vurugu hapawezi kufanyika uwekezaji wala kutengeneza fursa za uchumi,” amesema.

Awali akitoa taarifa ya mkoa, mkuu wa mkoa huo, Amina Masenza amesema hadi kufikia Desemba 2017 mkoa huo ulikuwa na viwanda 695 na kati ya hivyo vikubwa vipo 21 na vya kati 35 na vingine ni viwanda vidogo na vidogo zaidi huku sekta hiyo ikiwa imeajiri watu 15,000 sawa na asimilia 1.6 ya wakazi wa Iringa kwa mjibu wa sensa ya watu na makazi ya 2012.

Makonda Apokea Malalamiko Lukuki Kutoka kwa Wakazi wa Dar

$
0
0
Makonda Apokea Malalamiko Lukuki Kutoka kwa Wakazi wa Dar
Marehemu kutoacha wosia, sheria ya dini ya Kiislamu kutomtambua mtoto wa nje ya ndoa na kutofungua mirathi mapema kumetajwa kuwanyima haki wanufaika wa mirathi.

Hayo yameelezwa leo Februari 10, 2018 katika ukumbi wa Diamond Jubilee katika mkutano unaoendelea muda huu wa Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda kupokea taarifa ya malalamiko ya wananchi yaliyowasilishwa kwa wanasheria wa mkoa huo.

Akiwasilisha taarifa ya siku sita za kusikiliza malalamiko ya wananchi wa mkoa wa Dar es Salaam, mwanasheria Siraji Shabani amesema wamepokea malalamiko  87, kati ya hayo 40 yalikuwa mahakamani na 47 hayajafikishwa mahakamani kutokana na wahusika kutokuwa na elimu ya namna sahihi ya kufungua kesi za mirathi.

Shabani amesema changamoto kubwa waliyokutana nayo ni marehemu kutoacha wosia wa kisheria na kusababisha familia kushindwa kupata suluhisho la mali zilizoachwa.

“Mke na watoto iwapo mume amefariki ndiyo huwa waathirika wakuu wa mali za marehemu ambapo hudhulumiwa na ndugu wa familia ya marehemu,” amesema Shabani.

Ameitaja changamoto nyingine ni wanafamilia kutofungua mirathi kwa wakati na kusababisha kupitwa na wakati.

Amesema changamoto nyingine ni mwingiliano wa maisha ambapo watoto wa nje ya ndoa kukosa haki ya kurithi kutokana na dini ya Kiislamu kutomtambua mtoto wa nje ya ndoa.

“Nashauri kuwapo utaratibu wa kuandika wosia, urithi kabla ili kuondoa mkanganyiko huu iwapo mmoja wa wanafamilia anapofariki,” amesema,

“Wanafamilia wawe waaminifu katika kusimamia mirathi ya jamaa zao ili kuwapatia haki watoto wa marehemu badala ya kutumia mwanya huo kuwadhulumu.”

Malalamiko hayo pamoja na mengine yatawasilishwa kwenye ofisi ya mkuu wa mkoa kwa ajili ya kupatiwa ufumbuzi.


Mfanyakazi Mwingine wa Ikulu ya Trump Aacha Kazi

$
0
0
Mfanyakazi Mwingine wa Ikulu ya Trump Aacha Kazi
Habari kutoka nchini Marekani leo February 10, 2017 ni kuhusu mfanyakazi wa Ikulu ya White house nchini humo ameacha kazi akiwa ni mfanyakazi wa pili kuacha kazi katika kipindi cha wiki moja kwa madai ya unyanyasaji.

Mfanyakazi huyo ambaye alikuwa Mwandishi wa hotuba za Ikulu hiyo David Sorensen ametangaza kuacha kazi baada ya mke wake wa zamani Jessica Corbett kuliambia gazeti Washington Post kwamba Sorensen alikuwa akimnyanyasa kimwili na kihisia katika kipindi chote cha ndoa yao ya miaka miwili na nusu.

Kujiuzulu kwa Sorensen kunakuja siku mbili baada ya Katibu wa Wafanyakazi wa Rais Trump, Rob Porter pia kujiuzulu baada ya wake zake wa zamani wawili kuweka madai ya kuteswa kimwili na kijinsia na Porter.

Sorensen ameeleza kuwa ameamua kujiuzulu ili kwamba Ikulu hiyo isichafuliwe na tuhuma hizo dhidi yake.

Mchezaji Zamani wa Club za Man United Afariki Dunia

$
0
0
Mchezaji Zamani wa Club za Man United Afariki Dunia
Mchezaji zamani wa club za Man United, Celtic na timu ya taifa ya Jamhuri ya Ireland Liam Miller amefariki dunia leo baada ya kusumbuliwa na ugonjwa wa kansa kwa miezi kadhaa sasa.

Liam Miller amefariki kwa kusumbuliwa na kansa ya kongosho na aligundulika kuwa na tatizo hilo toka mwezi November mwaka jana na kuanza kupatiwa matibabu nchini kwao Ireland na United State, Liam hadi umauti unamfika alikuwa na umri wa miaka 36.

Kiungo Liam Miller akiwa na club ya Celtic 2003/2004 aliichezea michezo 44 na kuisaidia kutwaa Ubingwa wa Ligi msimu huo, mwaka 2004 Liam alijiunga na Man United na kudumu nayo kwa miaka miwili hadi 2006 alipoamua kujiunga na Leeds United kwa mkopo na baadae Sunderland.

Rais Magufuli Afanya Uteuzi wa Kamishna wa Polisi Zanzibar

$
0
0
Rais Magufuli Afanya Uteozi
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli leo tarehe 10 Februari, 2018 amempandisha cheo na kumteua Bw. Mohamed Hassan Haji kuwa Kamishna wa Polisi Zanzibar.

Taarifa iliyotolewa na Katibu Mkuu Kiongozi Balozi John Kijazi imefafanua kuwa  Rais Dkt. Magufuli amempandisha cheo Bw. Mohamed Hassan Haji kutoka Kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP) na kuwa Kamishna wa Polisi (CP), na kisha kumteua kuwa Kamishna wa Polisi Zanzibar.

Kwa taarifa kamili soma hapa chini.


Hii Hapa Taarifa Kutoka Mamlaka ya Hali ya Hewa

$
0
0
Hii Hapa Taarifa Kutoka Mamlaka ya Hali ya Hewa
Mamlaka ya Hali ye Hewa Tanzania(TMA), imetoa taarifa ya ya baadhi ya maeneo nchini kuwa na hali ya mawingu, sehemu nyingine kuwa ngurumo katika maeneo machache na vipindi vya jua. Tazama jedwani kutazama hali ya hewa kwa baadhi ya maeneo nchini Tanzania.

Soma taarifa kamili;

Salum Mwalimu Ampa Makavu Mtulia

$
0
0
Salum Mwalimu Ampa Makavu Mtulia
Mgombea Ubunge wa Jimbo la Kinondoni (CHADEMA), Salum Mwalimu amemshambulia mgombea mwenzake Maulid Mtulia kwa maneno kuwa kazi ya Mbunge sio kuomba omba wala kulilia bali anapaswa kutetea haki na maslahi ya wananchi katika jimbo lake.


Mgombea huyo ametoa kauli hiyo akiwa kwenye muendelezo wa kuomba ridhaa huku zikiwa zimebakia takribani siku saba ili wananchi wa Jimbo la Kinondoni pamoja na Siha kushiriki zoezi la kupiga kura katika uchaguzi huo mdogo wa marudio na waweze kupata wawakilishi wao ambao kwa mara ya kwanza wataingia bungeni mjini Dodoma Aprili 03 endapo zoezi hilo litakamilika kwa amani na usalama.

"Kazi ya Mbunge ni moja popote pale utakapoenda duniani ambayo ni kusimamia haki, maslahi na mahitaji ya wananchi wake na sio kulilia, kuomba omba, kujiabisha abisha. Ukiwa unauwezo wa kusimamia haki kwa wananchi wako maghorofa yatakuja kwa sababu sio hisani ni haki yao kama  walipa kodi", amesema Salum Mwalimu.

Pamoja na hayo, mgombea huyo ameendelea kwa kusema "kama una uwezo wa kusimamia haki na unaujua wajibu wako haiwezekani Mbunge, wananchi wako wanavuliwa nguo kwa kuvunjiwa nyumba, wanakufa, wanadhalilika, heshima ya utu wao inapotea halafu wewe unacheka eti unasema utawajengea maghorofa. Kuna maghorofa makaburini, watu waliokufa utawalipa nini".

Kwa upande mwingine, Salum Mwalimu amedai yeye anajitambua hivyo atahikisha anasimama mbele kupigania haki ya wananchi wa Kinondoni bila ya kujali ni wakati gani uliokuwepo muda huo.

Huyu Hapa Chura Anayetafutiwa 'Mchumba'

$
0
0
Huyu Hapa Chura Anayetafutiwa 'Mchumba'
Wataalam wa kuhifadhi wanyama nchini Bolivia wameanza kutembea taifa zima wakimsaka chura wa 'kike' atakayejamiana na chura mmoja asiye wa kawaida ambaye wanahofia kizazi chake huenda kikaangamia.

Chura huyo aliyepewa jina la 'Romeo' na aliye na mwenye umri wa miaka 10, anaishi katika maji na amekuwa akimtafuta mwenzake kwa kipindi cha miaka tisa.

Tayari amewekwa katika mtandao wa kuwakutanisha wapendanao akisema : Namtafuta mpenzi juliet.

Wanasayansi kwa sasa wanatufa katika vidimbwi vya maji mbali na mito kwa chura wa kike ambaye atajamiana na chura huyo ili kuhifadhi kizazi hicho.

''Hatutaki yeye apoteze matumaini. lakini wahifadhi hao watalazimika kuongeza kasi ya kumsaka chura huyo wa kike kwa kuwa hawezi kuishi zaidi ya miaka 15''.

Hiyo inaamaanisha kuwa Romeo anayeishi katika pipa katika kumbukumbu ya Cochabamba amesalia na miaka mitano kuishi ili kuhifafhi kizazi chake

Hizi ni miongoni mwa harakati za wanasayansi kumtafutia mchumbaHaki miliki ya pichaMATCH
Image caption
Hizi ni miongoni mwa harakati za wanasayansi kumtafutia mchumba
Ikiwa ni kati ya kampeni ya kuchangisha $15,000, kabla ya siku ya wapendanao ya Valentine, mtandao huo wa kuwakutanisha wapendanao uliweka jina la Romeo pamoja na picha yake mbali na ujumbe unaomuhusu.

Vyombo vya Hapari Vyapigwa Stop Kurusha Vipindi Vinavyohusu Valentine Day

$
0
0
Vyombo vya Hapari Vyapigwa Marufuku Kurusha Vipindi Vinavyohusu Valentine Day
Tunapoelekea Siku ya Wapendanao yaani Valentines Day February 14, Mamlaka ya Vyombo vya Habari vya Kielektroniki nchini Pakistani (PEMRA) kupitia amri ya Mahakama ya Kiislam, imekataza vituo vyote vya televisheni na radio nchini humo kutorusha vipindi vyovyote vinavyohusiana na Siku hiyo ya Wapendanao.

Raia wa Pakistan Abdul Waheed mwanzoni mwa mwaka 2017 alifungua kesi mahakamani kushinikiza kufutwa kwa kusherehekewa kwa siku hiyo nchini Pakistani kwa madai kuwa siku hiyo inaeneza uasherati, uchafu na uovu nchini humo.

Februari 13, 2017 siku moja kabla ya Siku ya Wapendanao, Jaji Shaukat Siddiqui alitoa amri ya kupiga marufuku kabisa programu yoyote ya matangazo kuhusiana na siku hiyo pamoja na kuweka vikwazo vingine.

Kutokana na watu na mamlaka mbalimbali kutoa maoni yao kupinga suala hili, inatarajiwa kusherehekewa kwa siku hii pengine kukafutwa kabisa nchini humo. Maamuzi ya mwisho ya mahakama juu ya hatma ya siku hii bado yanasubiriwa.

Makonda Awawashia Moto Wakurugenzi

$
0
0
Makonda Awawashia Moto Wakurugenzi
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda amewabadilikia Wakurugenzi mbalimbali wa halmashauri za wilaya mbalimbali jijini Dar es Salaam kwa vitendo vyao vya kuwakaiimisha nafasi mbalimbali viongozi ambao hawana uwezo.


Makonda amesema hayo leo Februari 10,2018 alipokutana na wananchi wa Mkoa wa Dar es salaam ili kujibu kero na matatizo mbalimbali yanayowakabili ikiwa ni siku ya mwisho kwa zoezi la kupokea na kuzitafutia ufumbuzi kero hizo. Katika kusikiliza kero hizo baadhi ya watendaji wa Serikali walikuwa wakishindwa kujibu maswali ambayo Mkuu wa Mkoa alikuwa akiwauliza.

"Mkurugenzi huyu mmempaje nafasi ya kukaimu, kwa hiyo Mkuu wa Idara anampa mtu ambaye hana uwezo kukaimu idara ili asipate idara si ndiyo maana yake? Maana huyu ndani tunatabia moja Mkuu wa Idara hana uwezo sasa hivyo anampa nafasi mtu ambaye hana uwezo ili yule mwenye uwezo asionekane, sasa huyu hana majibu anafanya nini hapa? Hajui lolote wala hana ripoti yoyote sasa Kukaimu kwake kumeishia kwenye huu Mkutano tafuteni mtu mwingine akakaimu"

"Halafu nyinyi Wakurugenzi nisaidieni mnawapaje watu idara wasiokuwa na uwezo, yaani anaitwaje Mkuu wa Idara hakuna jambo linalonifedhehesha kuona wananchi wanapata shida, Mkuu wa idara anaulizwa kwenye eneo lako kuna migororo mingapi ya ardhi anakwambia kwangu hakuna kabisa lakini anasimama Mwanasheria anasema migogoro ipo na tunahangaika kuitatua na Mkurugenzi sasa huyo ni Mkuu wa Idara kweli? Halafu mwisho wa siku kinatukanwa Chama Cha Mapinduzi (CCM) kumbe kwa uzembe wa mtu mmoja aliyekaa kwenye kiti anakula mshahara wa wananchi bila kufanya kazi yake" 

Habari Njema: Tunatibu Busha, Korodani Kuvimba, Ngiri, Miguu Kufa Ganzi Pamoja na Matatizo ya Nguvu za Kiume

$
0
0

Ni dawa ya nguvu za kiume inayorefusha na kunenepesha uume saizi uipendayo (Inch 1-7) kwa muda wa siku 6 tu.Dozi hii itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa muda wa dakika 30, utarudia tendo la ndoa zaidi ya mara 4 bila hamu kuisha bila kujali umri na garantee ni miaka 60 baada ya kutibu tatizo.

Pia tunatibu Busha bila kufanyiwa Oparesheni, korodani moja kuvimba, ngiri, tumbo kujaa gesi na kuunguruma, kutopata choo vizuri, miguu kuwaka moto na kufa ganzi, chango la wanawake, kisukari na kutokwa na kinyama sehemu ya haja kubwa.

MIHAYO:
Inarudisha mke, mchumba, hawara na atakutimizia kila kitu unachotaka kutoka kwake ndani ya  saa 2 tu hata kama yupo mbali. atarudi na kumfunga asiwe na mwingine zaidi yako.

Umefukuzwa kazini? unataka kupandishwa cheo? Umepoteza pesa zako kwenye biashara bila kujua umepandikizwa chuma ulete? Njoo urudishe pesa zako. Unauza mali yako haiendi?


Wasiliana na mtaalam Challo kwa; 0714006521

Mkwara wa RC Makonda Nusura Uue...Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumapili ya February 11

$
0
0


Mkwara wa RC Makonda Nusura Uue...Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumapili ya February 11

Rais Magufuli Ampandisha cheo na Kumteua Mohamed Hassan Haji kuwa Kamishna wa Polisi Zanzibar

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli leo tarehe 10 Februari, 2018 amempandisha cheo na kumteua Bw. Mohamed Hassan Haji kuwa Kamishna wa Polisi Zanzibar.

Taarifa iliyotolewa na Katibu Mkuu Kiongozi Balozi John Kijazi imefafanua kuwa Mhe. Rais Magufuli amempandisha cheo Bw. Mohamed Hassan Haji kutoka Kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP) na kuwa Kamishna wa Polisi (CP), na kisha kumteua kuwa Kamishna wa Polisi Zanzibar.

Kamishna wa Polisi Mohamed Hassan Haji amepandishwa cheo na kuteuliwa kuwa Kamishna wa Polisi Zanzibar kuanzia leo tarehe 10 Februari, 2018.

Kabla ya uteuzi huu Kamishna wa Polisi Mohamed Hassan Haji alikuwa Mhasibu Mkuu wa Polisi Zanzibar.

Kamishna wa Polisi Mohamed Hassan Haji anachukua nafasi iliyoachwa wazi na Kamishna wa Polisi Hamad Omar Makame ambaye amestaafu.

Gerson Msigwa
Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU
Dar es Salaam
10 Februari, 2018

Tanzania Yaridhia Kufuta Tozo ya Dola za Kimarekani 40 Kwa Wasafirishaji wa Mizigo

$
0
0
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Tanzania imeridhia kufuta tozo ya Dola za Kimarekani 40 (USD40) inayotozwa kwa kila stika kwenye magari yanayosafirisha mizigo kwenda nje ya nchi. Hatua hii imefikiwa kwenye Mkutano wa Dharura wa Baraza la Mawaziri la Kisekta la Biashara, Viwanda, Fedha na Uwekezaji la Jumuiya ya Afrika Mashariki uliofanyika Jijini Arusha

Akizungumza katika Mkutano huo Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji Mhe. Charles Mwijage amesema Tanzania imefikia hatua hii ikiwa ni moja ya jitihada za kuendelea kuboresha mazingira ya biashara nchini na Jumuiya kwa ujumla.

Tozo hii imekuwa ikitozwa kwa kipindi cha muda mrefu kwa malori yanoyosafirisha mizigo kwenda sehemu mbalimbali nje ya mipaka ya nchi. B

aada ya tathimini Serikali imebaini kuwa tozo hii inasababisha usumbufu na kuongeza gharama kwa wasafirishaji wa mizigo. Hata hivyo hatua hii inaendelea kuifanya Tanzania kuwa mtekelezaji mzuri wa makubaliano na itifaki mbalimbali za Jumuiya ya Afrika Mashariki.

Mkutano huu uliofanyika kwa kipindi cha siku tatu tarehe 7 hadi 9 Februari 2018, pamoja na mambo mengine ulilenga kujadili na kutatua vikwazo vya kibiashara visivyo vya kiushuru (NTBs) ambavyo vimekuwepo kwa muda mrefu katika Jumuiya. Mkutano huu umefikia tamati leo katika Makao Makuu ya Jumuiya ya Afrika Mashariki Jijini Arusha.

Taratibu za kuanza kufuta tozo hii zinaanza kutekelezwa mara moja.

Imetolewa na:
Kitengo cha Mawasiliano yaSerikali,
Wizara ya Mambo ya Nje naUshirikiano wa Afrika Mashariki,
9 Februari 2018
Viewing all 104789 articles
Browse latest View live




Latest Images