Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104775 articles
Browse latest View live

Vigogo Saba wa Madini ya Tanzanite Waachiwa kwa Dhamana

$
0
0
Vigogo Saba wa Madini ya Tanzanite Waachiwa kwa Dhamana
Vigogo saba wa madini ya Tanzanite katika mji mdogo wa Mirerani wilayani Simanjiro na jijini Arusha, waliokuwa wanashikiliwa na Polisi kwa amri ya Mkuu wa Mkoa wa Manyara, Alexander Mnyeti  wakidaiwa kudhamini uchimbaji haramu wa madini hayo, wameachiwa kwa dhamana.

Akizungumza jana, Februari 12, 2018 na MCL Digital, Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Manyara, Agustino Senga amesema vigogo hao waliokuwa wanashikiliwa kwenye kituo cha polisi Mirerani wamepatiwa dhamana, lakini bado polisi wanaendelea na uchunguzi wa tukio hilo.

Wiki iliyopita Mnyeti aliagiza vigogo hao saba wa madini kukamatwa na kushikiliwa kwenye kituo cha polisi Mirerani wakidaiwa kufadhili uchimbaji huo haramu.

Amesema waliwashikilia wachimbaji hao baada ya kamati iliyoundwa na Mnyeti kupata taarifa kuwa vigogo hao wanashiriki kuwadhamini vijana wanaoingia kwa wizi kwenye migodi ya kampuni ya TanzaniteOne yenye ubia na Serikali kwa asilimia 50 kwa 50 na Shirika la Madini la Taifa (Stamico).

Amesema wamewapatia dhamana vigogo hao (majina yao tunayahifadhi kwa sasa) ila bado wanaendelea na uchunguzi wa tukio hilo.

"Bado tunaendelea na uchunguzi wa tukio hilo kwani watuhumiwa hao wanadaiwa kuwadhamini wachimbaji hao haramu ambao wanaingia migodini bila uhalali," amesema Senga.

Amesema kuna kamati maalumu iliundwa na mkuu wa mkoa huo kwa ajili ya kuchunguza suala hilo hivyo baada ya uchunguzi wa awali ikabidi vigogo hao wakamatwe.

Mwenyekiti wa Chama cha Wachimbaji Madini Mkoa wa Manyara (Marema), Sadiki Mneney amesema wao kama chama bado hawajatambua sababu ya kukamatwa kwa wachimbaji hao.

Mneney amesema baada ya wachimbaji hao kuachiwa kwenye kituo cha polisi Mirerani walipanda magari yao na kuondoka, hivyo bado hawajazungumza nao.

"Tumepata taarifa kuwa wameachiwa ila viongozi tulipanga kufuatilia jambo hili mjini Babati kwani tulikuwa hatujui ni sababu gani iliyofanya wachimbaji hao wa madini kushikiliwa kwenye kituo cha polisi," amesema Mneney.


Jalada la Walioisababishia Serikali Hasara ya Bilioni 2 Lafikishwa kwa DPP

$
0
0
Jalada la Walioisababishia Serikali Hasara ya Bilioni 2 Lafikishwa kwa DPP
February 13, 2018 Upande wa Mashtaka umeieleza Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kuwa jalada la kesi ya uhujumu uchumi wa kuisababishia hasara serikali ya bilioni 2.4 inayomkabili Mkurugenzi wa Tathmini ya Madini, Archard Kalugendo lipo kwa Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP) kwa ajili ya uchunguzi.

Mbali ya Kalugendo, mshtakiwa mwingine katika kesi hiyo ni Mthamini wa Madini ya Almasi wa Serikali, Edward Rweyemamu.

Wakili wa serikali,  Estezia Willson amemueleza Hakimu Mkazi Mkuu, Godfrey Mwambapa kuwa shauri hilo limeitishwa kwa ajili ya kutajwa na upelelezi haujakamikika.

Pia ameeleza kuwa jalada halisi la Kesi hivyo lipo kwa Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP) kwa ajili ya uchunguzi. Baada ya kueleza hayo, Hakimu Mwambapa ameahirisha kesi hiyo hadi February 27,2018.

Kwa pamoja washtakiwa hao wanakabiliwa na kesi ya uhujumu uchumi kwa kuisababisha serikali hasara ya zaidi ya bilioni 2.4.

Inadaiwa kuwa kati ya August 25 na 31, 2017 katika maeneo mbalimbali kati ya Dar es Salaam na Shinyanga, kwa pamoja na kwa vitendo vyao wakiwa wathamini walioajiriwa na Wizara ya Nishati na Madini waliisababisha serikali hasara ya kiasi hicho cha fedha.

Chama cha Wafanyakazi wa Serikali za Mtaa Kimelaani Hatua ya RC Makonda Kuwavua Madaraka Hadharani Watumishi

$
0
0
Chama cha Wafanyakazi wa Serikali za Mtaa Kimelaani Hatua ya RC Makonda Kuwavua Madaraka Hadharani Watumishi
Chama cha Wafanyakazi wa Serikali za Mitaa (Talgwu) kimelaani kitendo kikichofanywa na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda cha kuwavua madaraka hadharani watumishi wa umma wakisema ni kitendo cha kinyama.

Akizungumza leo Februari 13, 2018 wakati akitoa tamko la chama hicho, Katibu Mkuu, Rashid Mtima amesema chama hicho hakitetei watumishi waovu, bali taratibu zinatakiwa kufuatwa katika kuwawajibisha

Februari 10, 2018  watumishi wa idara za ardhi wa manipaa za Ubungo na Ilala walivuliwa madaraka hadharani hali iliyosababisha mmoja wao, Paul Mbembela (Mkuu wa Idara ya Mipango Miji Ilala) kuzimia kwa muda.

"Tunalaani, tunalaani, tunalaani sana kitendo kilichofanywa na Makonda. Sheria zinataka mtumishi anayekiuka kanuni na sheria za utumishi kushughulikiwa kwa siri hadi uamuzi wa mwisho utakapotolewa,” amesema.

" Jambo baya zaidi tunalolaani hata mtumishi huyo alipozimia Makonda aliendelea kusema Dar es Salaam oyee, huu ni unyama.”

Amesema kibinadamu baada ya Mbembela kuzimia mkutano huo ulipaswa kusimama kwa muda ili kumshughulikia mgonjwa.

Amewaasa wanasiasa na viongozi kufuata sheria wakati wa kushughulikia matatizo ya wafanyakazi.

Habari Njema kwa Wanaopenda Muonekano Mzuri, Dawa za Asili Zisizo na Kemikali

$
0
0

WEKA MUONEKANO WAKO VIZUR SASA, NIWAUZA WA PRODUCT ZA ASILI NA MAFUTA YASIO NA MADHARA YEYOTE WALA KEMIKALI KWA MATUMIZI NA MATOKEO NI KWAARAKA KUANZIA WEEK (2) HADI (4)🍌🍍🥑

1) KUTOA MVI SUGU PIA ZA KUZALIWA NAZO _100,000/
2) KUREFUSH NYWELE KUZIJAZA NA KUZUIAKUKATIKA 100,000/
3) TENGENEZA SHEPU YAKO KUWA NA UMBO ZURI (HIPS & BATKS)KUNADAWA AINA TATU (@)KUPAK 100,000/(B) KUNYWA (C)VIDONGE_130,000/
4)ONDOA NYAMA UZEMBE MIKONONI, KIUNONI KUPAK _100,000/
5)TOA KITAMBI KABISA(@) KUPAK 10O,000/ (B)VIDONGE/SLIMING MAJAN 130,000/
6) PUNGUZA MWILI MZIMA KUANZIA KILO UNAZOITAJI WEWE
@) DAW YA MAJIN NA VIDONGE_130,000/
7)PUNGUZA MAZIWA NA YASIMAME KAMA MWANZO _90,000/
8) PIA UNA KUONGEZA MAZIWA SAIZI UNAYOHITAJI WEWE_90,000/
9)ONGEZA UNENE WA MWILI MZIMA_100,000/
10) ONDOA MICHIRIZI ILIYO SHINDIKANA_80,000/
11) TOA MAKOVU, CHUNUSI, WEUSI KWENY MAPAJA KIKWAPAN_80,000/
13) KUWA MWEUPE WAKUPENDEZA(@) VIDOGO(WHITE SOLUTION)_130,000/(B)MAFUTA YAKUPAK 100,000/
14)TOA NDEVU VINYWELEO MWILINI _100,000/
15/ ONGEZA NGUVU ZA KIUME (@)JELI AINAZOTE 100,000/(B)VIDONGE MAX MAN NA AINA NYINGI_ 100,000/
16) ENGEZA MAUMBIL YA KIUME
@) (HANDSOME UP) MASHINE _200,000/
@) JELI NA VIDONG VYA SHARK_130,000/
17) RUDISHA HAMU YA TENDO NA KUCHELEWA KUFIKA KILELE_100,000/
18) RUDISH(BIKRA) 100,000/
19)ONDOA MAFUTA USONI _90,000/
20) ONDOA MIKUNJO USON_80,000/(21) ENGEZA MGUU_100,000/ 21) TUDISH NYELE KWENYE KIPARA 150,000/ 22) DAW YA NGIRI YAKUVIMBA NA KULEGEA 100,000/🍍🍉🥑

TUNAPATIKAN DAR E SALAAM:PIA NJE YA NCHI TUNATUMA MIZIGO,NA KWA MIKOAN KOTE UTAPATA *KESSY* NI WAAMINIFU WA KUTUM MIZIGO NA KUFIKA KWA WAKATI PIGA CM (+255) 0719955528
0756259180
0785371237
@ *Pendeza_kessy_product*
Delivery POPOTE ULIPO,

Diamond Azidi Kuonyesha Ilipofikia Wasafi TV, Radio

$
0
0
Diamond Azidi Kuonyesha Ilipofikia Wasafi TV, Radio
February 13 2018 kupitia instagram page ya Diamond Platnumz amezidi kutuonyesha maandalizi ya Wasafi tv na Wasafi radio hii ni baada ya kupost video ya mnara kwa mara ya pili ambao unaonekana upo kwenye maandalizi kwaajili ya Wasafi tv na Wasafi radio.

Baada ya post hiyo kupitia instagram page ya Diamond Platnumz hajaandika chochote kuhusiana na Wasafi tv na Wasafi radio.

Diamond Platnumz alishawahi kupost mnara kupitia instagram account yake na wengi kutafsiri kuwa ndio maandalizi ya Wasafi tv na Wasafi radio na pia wasafi tv pamoja na Wasafi radio zitapatikana ndani ya makao makuu ya WCB.

Mnyeti Alivunja Baraza la Ardhi

$
0
0
Mnyeti Alivunja Baraza la Ardhi
Mkuu wa Mkoa wa Manyara, Alexander Mnyeti amelivunja baraza la ardhi la Kata ya Murray wilayani Mbulu mkoani Manyara  baada ya wananchi kulalamika kunyanyaswa, kuombwa rushwa na kunyimwa haki zao.

Akizungumza jana Februari 12, 2018 baada ya kulivunja baraza hilo, Mnyeti amesema hawezi kuliacha liendelee kufanya kazi kwenye eneo hilo wakati wananchi wanalalamikia kukosa haki zao.

Amemuagiza Mkurugenzi wa Halmashauri ya mji wa Mbulu, Anna Mbogo kuanza mchakato wa kupatikana viongozi wapya, waadilifu wa baraza la kata hiyo ili waendelee kuwatumikia wananchi.

Amesema mikutano ya wananchi kuwachagua wajumbe wengine inatakiwa kuanza upya ili nafasi za wajumbe wapya zipatikane na kuhudumia jamii ya eneo hilo.

"Tafuteni watu waadilifu, wenye weledi na hofu ya Mungu ambao wanaweza kuwahudumia wananchi ili washike nafasi hizo na kutekeleza majukumu yao ipasavyo," amesema Mnyeti.

Amesema kuwa baada ya kuwaondoa viongozi wa baraza hilo linalodaiwa kupokea rushwa wananchi waendeshe zoezi la kupatikana majina mapya kisha yapelekwe kwenye vyombo vya uchunguzi.

Mkazi wa kata ya Murray,  Michael Amme amelalamikia baraza hilo akidai kuwa halitendi haki na kuwaonea wananchi wanyonge.

Amme amesema kwa muda mrefu walikuwa wanalalamikia uamuzi wenye harufu ya rushwa kwa maelezo kuwa familia yao iliporwa eneo kutokana na maamuzi mabovu ya baraza hilo.

Hata hivyo, mjumbe wa baraza hilo Verani Anthony amesema wananchi wa eneo hilo wanapaswa kupatiwa elimu juu ya utendaji kazi wao.

Amesema wananchi hao wangepatiwa semina juu ya baraza hilo wasingelalamika kwani wao hutekeleza wajibu wao ipasavyo.

Pia, Mnyeti amemuagiza mkuu wa polisi wilaya ya Mbulu, kumkamata Mwenyekiti wa kijiji cha Murray, John Amme kwa kuwanyanyasa wananchi yakiwamo madai ya kuwapiga.

"OCD mkamate huyo mwenyekiti wa kijiji hiki ili akaeleze huko polisi kwa nini amemvunja mkono mwananchi kwa sababu kupiga watu si wajibu wake," alisema Mnyeti.

Kesi za Madai ya Talaka Zazidi Kuongezeka

$
0
0
Kesi za Madai ya Talaka Zazidi Kuongezeka
Kesi 1,218 za madai ya talaka visiwani Zanzibar zimeripotiwa katika mahakama mbalimbali za kadhi kuanzia Januari hadi Desemba, 2017.

Naibu Waziri wa Nchi Afisi ya Rais, Katiba, Sheria na Utumishi wa Umma na Utawala bora, Khamis Juma Maalim amesema hayo leo Februari 13, 2018 katika kikao cha Baraza la Wawakilishi wakati akijibu swali la mwakilishi wa Konde, Omar Seif Abeid.

Katika swali lake, Abeid alihoji sababu za ndoa nyingi hasa za vijana kudumu muda fupi, huku akitaka kujua katika kipindi cha mwaka 2017 ni madai mangapi ya ndoa yamefikishwa katika mahakama ya kadhi ili kupatiwa ufumbuzi.

Katika majibu yake Maalim amesema kiwango cha kesi hizo ni nyingi ukilinganisha na mwaka 2016 ambapo kulikuwa na kesi 1,000.

Amesema katika kesi za mwaka 2017,  kesi 884 ziliripotiwa katika mahakama za kadhi za Unguja,  440 zimetolewa uamuzi na 444 bado zinaendelea kusikilizwa katika mahakama hizo kwa hatua zaidi za kisheria.

Amesema kwa upande wa Pemba, kulikuwa na  kesi 334, kati ya hizo 249 zimetolewa uamuzi huku 85 zikiendelea kusikilizwa.

Kuhusu sababu za ndoa kuvunjika katika kipindi cha muda mfupi sambamba na kuwekwa sheria ya kuzuia utoaji talaka, Maalim amesema swali hilo ni zuri lakini ni ngumu kwa sababu jambo hilo litakwenda kinyume na maadili ya Wazanzibar walio wengi ambao ni Waislam.

“Kama tunavyoelewa wananchi wengi wa Zanzibar ni Waislam ni wazi kuwa kuandaa kwa Sheria kama hiyo ni kwenda kinyume na Sheria zilizowekwa na dini ya kiislam,” amesema,

“Hatuna utafiti ambao unaonyesha kuwa kati ya mwanamke na mwanaume nani ni sababu ya kutoka kwa talaka hovyo ijapokuwa suala la talaka ni la siku nyingi.”

Amesema kazi kubwa inayofanywa na wizara yake kwa kushirikiana na wadau mbalimbali ni utoaji wa elimu juu ya kuishi vema katika maisha ya ndoa, lengo ni kuona suala la talaka linapungua kwa kiasi kikubwa.

TFF Yamuadhibu Nyoso...... Yamfungia Kucheza Mechi Tano

$
0
0
TFF Yamuadhibu Nyoso...... Yamfungia Kucheza Mechi Tano
Beki wa Kagera Sugar, Juma Nyoso amefungiwa kucheza michezo mitano ya Ligi Kuu Tanzania Bara sambamba na faini ya Sh1 miolioni kwa kosa la utovu wa nidhamu.

Akifafanua adhabu hiyo, msemaji wa TFF, Clifford Mario Ndimbo amesema beki huyo amekutwa na hatia ya kumpiga shabiki mara baada ya mchezo dhidi ya Simba kumalizika.

"Kamati ya nidhamu ilimuita Nyoso ili kujitetea kama ilivyo kawaida lakini  kwa upande wake alikana kuhusika na tukio hilo na badala yake akadai alimkunja shabiki huyo.

"Lakini ripoti ya mchezo huo kutoka kwa mechi kamishina imeeleza kuwa Nyoso alimpiga shabiki huyo kwa kiatu na kisha akatumia goti," alisema Ndimbo.

Hata hivyo adhabu hiyo imetajwa  kutolewa kwa kanuni ya 36 ya Ligi Kuu inayohusu uchezaji wa kiungwana, kipengele cha (1),(2) na (5).

Pia kamati ilirejea aina ya matukio ya utovu wa kinidhamu ambayo amewahi kuyafanya beki huyo ambaye amewahi pia kuichezea Taifa Stars na klabu ya Mbeya City.

Polisi Waanika Sababu za Chadema Kupigwa Mabomu

$
0
0
Polisi Waanika Sababu za Chadema Kupigwa Mabomu
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kinondoni ACP Jumanne Murilo amekanusha habari za polisi kuvamia ofisi za CHADEMA zilizopo maeneo ya magomeni na kusema kuwa wao walirusha mabomu ili kutawanya watu waliokuwa wakiandamana kwa mwamvuli wa vyama vya siasa.


Kamanda Murilo ametoa kauli hiyo leo wakati akifanya mahojiano kwa njia ya simu katika kipindi cha East Africa Breakfast na kusema kwamba walichokifanya jana jeshi la polisi ni  kuzuia vitendo ambavyo vinaweza kuvunja sheria kwa kutumia muamvuli wa vyama vya siasa.

Akizidi kufafanua Kamanda Murilo amesema kwamba suala la ofisi za CHADEMA kuvamiwa yeye analisikia tu mitaani kwani anachofahamu askari walikuwa wakitawanya vijana zaidi ya 100 waliokuwa barabarani kwa mtindo wa maandamano yasiyo na kibali.

"Sisi hatujavamia. Suala la kuvamia nalisiakia tu mitaani. Sisi tunafanya kazi kwa kujitambua na kufanya kazi kwa misingi ya sheria. Mikutano ilianza vizuri na kuisha cha ajabu kilijitokeza kikundi cha watu zaidi ya 100 barabarani na kuanza maandamano ambayo yanasababisha usumbufu kwa watumiaji wengine wa barabara" amesema ACP Murilo.

Ameongeza kuwa  "Vijana 100 wakiwa barabaran wanakuwa na mihemuko na wengine wanaweza kutumia mwanya wa kisiasa kufanya uhalifu, Hatuwezi kuacha hizo rapsha zikatokea. Hatutavumilia. Tulipiga mabomu 4 ya machozi kuwatawanya watu waliokuwa wakiandamana".

Pamoja na hayo Kamanda Murilo amesema Polisi wamewashikilia watu waliokuwa wameingia barabarani wapatao kama 15 na kati yao hakuna viongozi kwa kudai kuwa viongozi wamejitahidi kuwa makini.

Akizungumzia kuwepo na kamera za kurekodi matukio kwenye kampeni Murilo amesema ni jukumu lao la kazi la kufuatilia kila linalotokea katika mikutano hiyo huku akisema kutokana na kamera hizo kufanya kazi kwa uwazi kumepunguza hata maneno ambayo yanaweza kuleta shida.

Peter Msigwa Amvaa Kigwangala Amtaka Atoe Ushahidi "Nipo Tayari Kujiuzulu Nafasi Yangu ya Ubunge"

$
0
0
Peter Msigwa Amvaa Kigwangala  Amtaka Atoe Ushahidi "Nipo Tayari Kujiuzulu Nafasi Yangu ya Ubunge"
Mbunge wa Iringa Mjini Mchungaji Peter Msigwa amefunguka na kuweka wazi kuwa endapo Waziri wa Maliasili na Utalii atatoa ushahidi wowote ambao unaonyesha yeye ana masilahi na makampuni ya uwindaji atajiuzulu nafasi yake ya ubunge.

Mchungaji Msigwa amesema hayo Februari 12, 2018 kupitia moja ya mitandao yake ya kijamii na kudai kuwa Waziri huyo amekuwa ni muongo na ni mtu ambaye hajiamini

"Kigwangalah ni muongo anyependa masifa, ni mtu asiyejiamini. Kama akitoa ushahidi wowote utakaodhihirisha kuwa nina masilahi na makampuni ya uwindaji nitajiuzulu ubunge .Nina wasiwasi na upbringing yake" aliandika Msigwa

Mbunge Msigwa amesema hayo kufuatia kauli ambayo Waziri Kigwangalla aliitoa siku chache zilizopita kupitia mtandao wake wa Twitter kuwa Mbunge huyo wa Iringa Mjini anahusika na ana hisa katika vitalu, jambo ambalo Msigwa mwenyewe amelipinga vikali na kuamua kuweka ubunge wake rehani endapo Waziri huyo atathibitisha hilo.

Akamatwa na Cocaine Kwenye Makalio ya Bandia

$
0
0
Akamatwa na Cocaine Kwenye Makalio ya Bandia
Polisi nchini Ureno wamemkamata mwanamume mmoja kwenye uwanja wa ndege huko Lisbon, ambaye alikuwa amebeba kilo moja ya cocaine kwenye makalio bandia.

Vyombo vya habari nchini humo vilisema kuwa raia huyo wa Brazil aliwasili kwa ndege kutoka mji wa Belém do Pará, kaskazini mwa Brazil.

Mihadarati ya Cocaine ya pauni milioni 50, yapatikana Uingereza
Mwanamume mwingine ambaye anashukiwa kuwa angepokea dawa hizo alikamatwa kwenye kituo cha treni cha mji huo.

Wanaume hao watakabiliwa na kesi ya ulanguzi wa madawa ya kulevya.

Mwezi uliopita polisi nchini Ureno na Uhispania walikamata cocaine ndani ya mananasi yaliyokuwa yamessfirishwa kutoka Amerika ya Kusini.

Tatoo ya Neymar Yaibua Maswali Mengi kwa Mashabiki

$
0
0
Tatoo ya Mess Yaibua Maswali Mengi kwa Mashabiki
Wakati Real Madrid kesho inaivaa PSG katika mechi ya Ligi ya Mabingwa Ulaya, mshambuliaji wake nyota, Neymar ameongeza tatuu nyingine.

Wakati Neymar anarejea Hispania kwa ajili ya mechi hiyo, ameamua kuongeza tatuu ya Kombe la Ligi ya Mabingwa Ulaya.


Neymar ameongeza mchoro huo mguuni akionyesha ameipania mechi hiyo na ana imani wataivuka Madrid na kusonga mbele.

Mshambulizi huyo alijiunga na PSG akitokea FC Barcelona kwa dau la pauni milioni 198 na kuweka rekodi mpya ya usajili.


Nyota Hawa Wwa Yanga Kuikosa Mechi ya Kesho

$
0
0
Nyota Hawa Wwa Yanga Kuikosa Mechi ya Kesho
Timu ya Mabingwa wa soka Tanzania Bara Yanga SC inatarajiwa kushuka dimba la Uhuru Jijini Dar es Salaam kesho kuvaana na Majimaji FC huku ikiwakosa nyota wake watatu ambao bado ni majeruhi mpaka sasa.

Hayo yamebainishwa na taarifa zilizotolewa na uongozi wa timu hiyo kupitia moja ya kurasa zao za mitandao ya kijamii ambapo wamedai maandalizi dhidi ya mchezo huo wa muendelezo wa VPL dhidi ya Majimaji FC yamekamilika mpaka sasa.

"Tuko tayari kwa mchezo wa kesho, lakini hatutakuwa na wachezaji watatu ambao ni Yohana Mkomola, Amisi Tambwe pamoja na Donald Ngoma kutokana bado ni majeruhi hivyo hawatakuwa sehemu ya mchezo", imesema taarifa hiyo.

Kwa upande mwingine, timu ya Yanga imethibitisha kuwa ipo tayari kwa ajili ya safari yake kuelekea Shelisheli kwenye mechi ya marudiano dhidi ya St. Louis ambapo timu hiyo inatarajiwa kuondoka nchini Jumapili.

Kiongozi Mwenza wa Odinga Akataa Kuapishwa

$
0
0
Kiongozi Mwenza wa Odinga Akataa Kuapishwa
Ikiwa ni wiki mbili zimepita tangu Kiongozi wa umoja wa vyama vya upinzani nchini Kenya (NASA), Raila Odinga ajiapishe kuwa ni Rais wa watu nchini humo, hatimaye leo Makamu wake, Kalonzo Musyoka ambaye siku ya kuapishwa kwa Odinga hakuhudhuria amekanusha taarifa kuwa ataapishwa mwishoni mwa mwezi huu.

Kalonzo amesema kuwa taarifa hizo zinazosambaa kwenye mitandao ya kijamii kuwa ataapishwa mwishoni mwa mwezi februari, 2018 sio za kweli na hawezi kufanya hivypo kwa sababu ni kinyume na Katiba ya nchi hiyo.

“Najua Ruto anasubiri niapishwe ili apate sababu za kunifungulia mashtaka ya uhaini ili kuniharibia mipango ya kugombea urais mwaka 2022 dhidi yake, Kwani kuapishwa ni tukio la kinyume na katiba ya nchi na nasisitiza sitaapishwa kama inavyoripotiwa na baadhi ya vyombo vya habari,“amesema Msyoka leo Februari 13, 2018 alipokuwa mjini Machakos akiongea na viongozi wapya wanawake walioteuliwa na NASA.

Soma zaidi – Hatimaye Raila Odinga ajiapisha kuwa Rais wa Kenya mbele ya maelfu ya watu

Hata hivyo, kauli hiyo imewatibua maelfu ya watu nchini Kenya wengi wakimuita kuwa ni MSALITI na mtu muoga katika kupigania maslahi ya Wakenya.

RC Makonda Awawashia Moto Makampuni ya Udalali

$
0
0
RC Makonda Awawashia Moto Makampuni ya Udalali
MKUU wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda, amewataka wamiliki wa makampuni ya udalali jijini Dar es Salaam, kufuata taratibu za kisheria wanapokuwa katika majukumu yao ya kikazi katika kukamata au kuondoa mali za watu wanapokuwa wakidaiwa.


Amewaomba pia  kuwaelimisha, badala ya kuwapiga viboko waendesha  bodaboda wanapokuwa wakitaka kuingia  maeneo ya Posta jijini Dar es Salaam.  Pia amewataka wawasilishe leo nyaraka zao za utambulisho wa kufanya kazi hizo zinazowaonyesha kuwa wao ni halali ili kuondoa makundi ya watu wanaojipenyeza na kujifanya  ndiyo wamiliki wa makampuni ya udalali.


Mwanasheria Mkuu Nchini Kenya Ajiuzulu

$
0
0
Mwanasheria Mkuu Nchini Kenya Ajiuzulu
Mwanasheria Mkuu wa nchi ya Kenya Profesa Githu Muigai amejiuzulu cheo hicho mchana wa leo baada ya kutumikia nafsi hiyo kwa muda wa miaka sita na nusu.


Taarifa hiyo imethibitishwa na Rais wa nchi hiyo Uhuru Kenyatta na kudai amepokea barua ya kujiuzulu Prof. Githu kwa masikitiko makubwa, hata hivyo Uhuru ametangaza nafasi hiyo kwa sasa itachukuliwa na Jaji Paul Kihara Kariuki.

Kwa upande mwingine, Rais Uhuru Kenyatta amemteua Abdikadir Mohammed kuwa Balozi wa South Korea.

Mwakyepe Awapa Ujumbe Huu Bongo Movie

$
0
0
Mwakyepe Awapa Ujumbe Huu Bongo Movie
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Dkt. Harrison Mwakyembe ameyataka mashirikisho ya Sanaa na Filamu kusimamia ubora wa kazi za sanaa ili kukidhi mahitaji ya walaji.


Akiongea na viongozi wa Mashirikisho hayo leo ofisini kwake Mwakyembe amewataka kusimamia ubora kwani ndio kitu pekee kitawafanya mashabiki kuzipenda filamu za nyumbani.

"Ongezeni juhudi katika kusimamia uboreshaji wa kazi za sanaa na filamu ili ziweze kuthaminiwa na kukidhi matakwa ya walaji kwa kuwafanya kupenda vya kwetu", amesema.

Kwa upande wake Katibu Mtendaji wa Bodi ya Filamu Tanzania Bibi. Joyce Fisoo ameyataka Mashirikisho ya sanaa na filamu kufuata na kusimamia sheria, kanuni na taratibu za kutafsiri kazi za filamu za nje kwa kuwa na kibali cha mmiliki wa filamu.



Naye Kaimu Mkurugenzi Idara ya Maendeleo ya Sanaa Bibi. Leah Kihimbi, ameyaasa mashirikisho ya Sanaa na Filamu nchini kusimamia vyema vyama vilivyopo chini ya mashirikisho hayo ili kuhakikisha shughuli zote za sanaa zinapita kwenye mashirikisho husika.


Zuma Kufuata Nyayo za Mugabe Akubali Kujiuzulu Atoa Sharti Hili

$
0
0
Zuma Kufuata Nyayo za Mugabe Akubali Kujiuzulu Atoa Sharti Hili
RAIS wa Afrika Kusini, Jacob Zuma ameridhia kuondoka madarakani, baada ya wito uliotolewa na Chama chake tawala cha ANC kumtaka kujiuzulu ndani ya masaa 48. Zuma ameridhia kujiuzulu kwa sharti kwamba, atafanya hivyo baada ya miezi mitatu hadi sita kuanzia sasa, ambapo bado uongozi wa ANC haujatoa jibu iwapo umeridhia sharti

ANC kikiongozwa na Cyril Ramaphosa, jana kilituma ujumbe maalum kumtaka rais huyo kuachia madaraka, kutokana na harakati nyingi za kumtaka afanye hivyo tangu mwaka jana.


Jacob Zuma anakabiliwa na tuhuma za rushwa na matumizi mabaya ya madaraka ambapo Bunge la nchi hiyo kujaribu kupiga kura za maoni ili kumuondoa lakini ilishindikana, ndipo chama kikafanya mkutano na kuchukua uamuzi huo mgumu wa kumtaka afanye hivyo, la sivyo kitamtoa kwa nguvu.


Endapo Zuma atafanya hivyo atakuwa amefuata nyayo alizopita rafiki yake mkubwa Robert Mugabe ambaye alikuwa Rais wa Zimbabwe, aliyetakiwa kufanya hivyo mwishoni mwa mwaka 2017 na jeshi la nchi hiyo, la sivyo lingetumia nguvu kumng’oa, na hatimaye kuachia madaraka.

Makonda Awapa Onyo Kali Kampuni za Kukamata Bodaboda

$
0
0
Makonda Awapa Onyo Kali Kampuni za Kukamata Bodaboda
Mkuu wa mkoa wa Dar es salaam Mhe Paul Makonda ametoa onyo kali kwa kampuni zinazofanya kazi ya kukamata Pikipiki (bodaboda) kwa mtindo wa kuvamia kitendo kinachohatarisha usalama wa Dereva na Abiria.


RC Makonda amesema zipo baadhi ya kampuni zimekuwa zikivizia madereva wa Bodaboda kisha kuwavamia na kuwakamata na wakati huohuo kuwapiga kitendo ambacho amesema hawezi kukiruhusu kiendelee kwenye Mkoa wake.

Mhe. Makonda ametoa onyo hilo wakati wa kikao na Madalali wanaotekeleza hukumu za Mahakama na Bank kilicholenga kuwatambua na kupitia nyaraka zinazowapa mamlaka ya kufanya kazi hiyo ili Wasionekane Matapeli na waweze kupata ushirikiano wa serikali.


Uamuzi wa RC Makonda kukutana na madalali hao ni manyanyaso na ukandamizaji unaofanywa na baadhi ya madalali wanaopiga minada Nyumba, Magari, Viwanja, Mashamba, Ofisi na Mali za watu bila kufuata taratibu na kusababisha maumivu makali kwa wananchi.

Amesema zipo kampuni za udalali zinazofoji nakala za hukumu, mihuri, sahihi za mahakama,ofisi ya Mkoa, Wilaya na Mitaa na wakati mwingine kufanya minada bila kufuata taratibu.

Baadhi ya wamiliki wa kampuni za udalali

Kutokana na hilo RC Makonda amezitaka kampuni zote za udalali Dar es salaam kuwasilisha nakala za nyaraka ya usajili kwa mwanasheria wa mkoa zipitiwe na kujiridhisha ili wapewe ushirikiano na Serikali.

Nao Madalali wamemshukuru RC Makonda kwa uamuzi wa kuwatambua ili wapate ushirikiano wa Serikali kwakuwa wapo baadhi ya madalali waliokuwa wakifanya kazi hiyo kinyume na sheria na kuwachafulia kazi wale wenaofata taratibu za kazi hiyo.

Kutana na Mtabibu Mwenye KUBRI kutoka kwa ALLAH issa simba said Mtabibu wa Nyota za Binadamu na Dawa za Asili

$
0
0
Kutana na Mtabibu Mwenye KUBRI kutoka kwa ALLAH issa simba said Mtabibu wa Nyota za Binadamu na Dawa za Asili ya Africa Mwenye UWEZO Kubaini tatizo lako Pindi tu Utakapo Fanya Mawasilino Kupitia Wasaa Husika..

JE UNASUMBULIWA NA Mapenzi? (Umeachwa na Umpendae,Awe Mume,Mke na Bado unampenda?Na Umejaribu Sehemu nyingi Bila Mafanikio?Wasilina na Maalim Hussein Ujione muujiza wa Papo kwa Papo.. anauwezo WA KURUDISHA MAHUSIANO NA KUIMARISHA NDOA YAKO NDANI YA SAA 12 TU.

Umekimbiwa na Mumeo,mkeo au Mpenzi na anaishi na mtu mwingine? Muone akutatulie Anauwezo wa Hali ya Juu wa Kusambalatisha Mahusiano yao Endapo utafata Atakacho kuelekeza.
Atamfanya Atimize Ahadi zote kwa Muda Mfupi.

Issa simba said Anatumia Jina la Muhusika au Picha Kumaliza Tatizo lako..
Anatibu kwa Kutumia Vitabu vya QUR-AN Dawa za Asili za Africa,Dawa za Kiarabu na Majini.Anatafsiri Ndoto. Kushinda BAHATI NASIBU, KUSAFISHA NYOTA. Mvuto wa Mwili na BIASHARA, Kinga ya Mwili,ZINDIKO za Nyumba.MIGUU Kufa GANZI.Kufungua KIZAZI kwa wale walio fungwa kwa njia za KISHIRIKINA. Anakupa Jini la Mali kwa yule anaehitaji Utajiri BILA MASHARTI. Nguvu za KIUME, Humaliza Kesi zilishindika ndani ya siku 14 tu..
na mengi zaidi

+255 622588038au 0679119679 au +255 764318107
NB: TIBA KWA DINI ZOTE NA IMANI ZOTE.
Viewing all 104775 articles
Browse latest View live




Latest Images