Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104417 articles
Browse latest View live

Rais Magufuli Afanya Amteua Mnadhimu Mkuu wa Jeshi la JWTZ

0
0
Rais Magufuli Afanya Uteuzi Huu
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, na Amiri Jeshi Mkuu, Dkt John Pombe Magufuli ameteua Meja Yakubu Hassan Mohamed kuwa Mnadhimu Mkuu wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania(JWTZ) na kuwapandisha vyeo kutoka Brigedia Jenerali na kuwa Meja Jenerali.



Jeshi la Polisi Latoa Ufafanuzi Juu ya Kuokotwa kwa Mwili wa Mtu Ufukwenu

0
0
Jeshi la Polisi Latoa Ufafanuzi Juu ya Kuokotwa kwa Mwili wa Mtu Ufukwenu
Kamanda Mkuu wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Kinondon ACP Murilo Jumanne Murilo amezungumza na waandishi wa habari na kueleza kuwa jeshi hilo limeokota mwili wa mwanaume anayekadiriwa kuwa na miaka 35, katika eneo la ufukwe wa Coco Beach akiwa amefariki.

Kamanda Murilo ameeleza walipata taarifa ya kuonekana kwa mtu huyo kutoka kwa msamaria mwema na walipokwenda eneo la tukio waliukuta mwili wa mtu huyo ukiwa na majeraha na akiwa tayari ameshakufa.

Ameeleza kuwa Jeshi  la Polisi tayari limeanza mara moja kufanya uchunguzi ili kubaini chanzo cha kifo cha mtu huyo.

Jarada la Kesi la Mhasibu Mkuu wa Takukuru Lapelekwa kwa DPP

0
0
Jarada la Kesi la Mhasibu Mkuu wa Takukuru Lapelekwa kwa DPP
Jalada la kesi inayomkabili Mhasibu Mkuu wa TAKUKURU, Godfrey Gugai anayedaiwa kumiliki mali zenye thamani ya Sh. Bilioni 3 ambazo haziendani na kipato chake limepelekwa kwa Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP) kwa ajili ya kulipitia na kulitolea maamuzi.

Hayo yameelezwa na Wakili wa Serikali, Wankyo Simon mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Thomas Simba wakati shauri hilo lilipokuja kwaajili ya kutajwa.

Wankyo alieleza awali  jalada hilo lilipelekwa kwa DPP ambapo alilipitia na kulirejesha TAKUKURU na kuelekeza baadhi ya maeneo yafanyiwe uchunguzi zaidi.

Alidai kuwa maeneo hayo yamekwisha fanyiwa kazi na jalada limerejeshwa tena kwa DPP kwa ajili ya kulipitia na kulitolea maamuzi.

Wankyo baada ya kuyaeleza hayo aliiomba Mahakama iipangie kesi hiyo tarehe nyingine ili waweze kueleza hali ya upelelezi ikoje.

Kwa upande wa mshtakiwa Gugai alidai kuwa sasa wamefikisha siku 90 hivyo anaomba kesi ipangiwe siku saba ili waweze kujua hali ya upelelezi ikoje.

Baada ya kueleza hayo, Hakimu Simba aliiahirisha kesi hiyo hadi February 21,2018 na kuutaka upande wa mashtaka uhakikishe wanalifanyia kazi jalada hilo kwa kuwa limeanza kuzeeka.

Mbali na Gugai, washtakiwa wengine katika kesi hiyo ni George Makaranga, Leonard Aloys na Yasini Katera. Washtakiwa hao wanaokabiliwa na mashtaka 43 yakiwemo 20 ya utakatishaji fedha haramu, kumiliki mali zisizoendana na kipato na kughushi mikataba ya mauziano ya viwanja katika maeneo mbalimbali.

Rachel Afunguka Alivyokamatwa na Dawa za Kulevya Uarabuni

0
0
Recho Afunguka Alivyokamatwa na Dawa za Kulevya Uarabuni
Msanii wa muziki bongo Rachel maarufu kama Rachel Kizunguzungu, amefunguka juu ya sakata lake la kwenda nchi za Uarabuni na kukutwa na mabalaa, ikiwemo kutumia madawa ya kulevya na kutelekezwa huko na mwanaume aliyekwenda naye.


Akizungumza kwenye Planet Bongo ya East Africa Radio, Rachel amesema ni kweli alikwenda Arabuni kwani ilikuwa ndoto yake tangu utotoni, na alipokwenda hukomilikuwa ni kutimiza ndoto zake na kuamua kubaki kwa muda kula raha.

“Kweli nilienda na nilienda na kazi zangu sio kwa ajili ya mapenzi, nakuhusu kubaki kule kule sikutamani, lakini ndoto zangu tangu niko shule ilikuwa kufika kwenye nchi za Arabuni, nikasema kwa nini nisikae hata miezi miwili mitatu tuienjoy! Nilikuwa na mpenzi wangu ambaye ni mwarabu, na nilipokuwa kule nilikaa mwenyewe, sikupokonywa passport na wala sikuzidisha muda wa kukaa, nilikuwa nimekaa mwenyewe kwa raha zangu na mtu wangu, hizo stori ni watu tu kujiongeza”, amesema Rachel.

Rachel amesema hata taarifa za yeye kuwa kwenye hali mbaya akitumia madawa ya kulevya hazina ukweli, hivyo watu wasiamini maneno wanayoyasikia kwa watu.

Zitto Kabwe Amtetea Samatta "Msimuingize Kwenye Haya Mambo Tafadhali"

0
0
Zitto Kabwe Amtetea Samatta "Msimuingize Kwenye Haya Mambo Tafadhali"
Mbunge wa Kigoma Mjini, Zitto Kabwe amefunguka na kumtetea mshambuliaji wa Kimataifa wa Tanzania ambaye sasa anakipiga klabu ya Genk ya nchini Ubelgiji , Mbwana Samatta kuwa ameshinda kwenda kumtembelea Tundu Lissu kutokana na ratiba yake kuwa ngumu.

Zitto Kabwe aliona aweke wazi hilo kufuatia baadhi ya watu kuanza kuhoji inakuaje mchezaji huyo yupo ameshinda japo kwenda kumtembelea na kumuona Mbunge Tundu Lissu ambaye anapatiwa matibabu nchini humo kufuatia kushambuliwa kwa risasi mwaka jana. Zitto Kabwe ndipo aliamua kuweka sawa kuwa mchezaji huyo kwa sasa ratiba yake ni ngumu lakini anaamini atakwenda wakati ukipatiakana.

"Mbwana ni mgonjwa pia. Hivi sasa yupo kwenye mazoezi chini ya ratiba ngumu Sana ili arudi hali yake ya kawaida. Mjue kuwa Mbwana ni profeshno hawezi kwenda kinyume na ratiba ya daktari kama huko kwetu. Msimwingize kwenye haya mambo tafadhali. Atamwona Lissu kwa wakati wake" aliandika Zitto Kabwe

Zitto Kabwe kwa sasa yupo nchini Ubelgiji ambapo alipata nafasi ya kumtembelea Mbunge Tundu Lissu anapopatiwa matibabu pia aliweza kumtembelea mchezaji huyo wa Genk

Hiki Hapa Kikosi cha Yanga Dhidi ya Majimaji Leo

0
0
Hiki Hapa Kikosi cha Yanga Dhidi ya Majimaji Leo
Baada ya kuibuka na ushindi wa bao 1 – 0 dhidi ya St Louis mchezo wa klabu bingwa Afrika hatimaye mabingwa watetezi wa ligi kuu soka Tanzania Bara klabu ya Yanga hii inatarajia kushuka dimbani kuivaa timu ya Majimaji hii leo.

Kuelekea katika mchezo huo muhimu kwa pande zote mbili kuhitaji kuibuka na ushindi ili kuondoka na pointi tatu, Yanga SC imeanika kikosi chake kitakachoshuka uwanjani.


Haji Manara Amvaa Goli Kipa wa Yanga

0
0
Haji Manara Amvaa Goli Kipa wa Yanga
Afisa habari wa Simba Haji Manara ambaye amekuwa na utamaduni wa kupenda kuwatania watani wao wa jado Yanga kupitia account zake za mitandao ya kijamii na imekuwa kama kitu cha kawaida.

Leo kupitia ukurasa wa instagram wa Haji Manara ameandika ujumbe wa kumkosoa golikipa wa Yanga raia wa Cameroon Youthe Rostand baada ya kutumia kauli mbiu ya Simba na kuandika “Yanga Nguvu Moja”



Baada ya kuona hivyo Haji Manara akaandika hivi “Nilisema wazi ipo siku kila mtanzania atashabikia Simba…imekuwa desturi kwa sasa kipa huyu wa Yanga kutumia kauli mbiu yetu..NGUVU MOJA…ile daima kuna mwiko nyuma kuna upawa haitaki kabisa!!”

Inawezekana Rostand kutokana na ugeni wake akawa hafahamu kuwa kauli ya “Nguvu Moja” ya Simba SC na ameichukulia kama ni usemi wa kawaida tu lakini kauli mbiu ya Yanga wao ni “Yanga daima mbele nyuma mwiko”

Uongozi wa Hospitali ya Amana Wamuomba Waziri Majaliwa Jengo la Amana Center

0
0
Uongozi wa Hospitali ya Amana  Wamuomba Wazili Majaliwa Jengo la Amana Center
Uongozi wa Hospitali ya Rufaa ya Amana wilayani Ilala umemuomba Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa kusaidia mchakato wa kulipata jengo la Amana Center ili litumike kupunguza uhaba wa majengo unaoikabili hospitali hiyo.

Mganga Mkuu wa hospitali hiyo, Dk. Meshack Shimwela ametoa ombi hilo leo Februari 14,2018 wakati wa uzinduzi wa jengo la huduma ya mama na mtoto hospitalini hapo.

Amesema wamekuwa na mzozo wa mara kwa mara na watumiaji wa jengo la Amana Center kutokana na upigwaji wa muziki na burudani nyingine za sanaa.

Dk Shimwela amesema jengo hilo lipo karibu na hospitali na kelele zinasumbua wagonjwa, hivyo ameiomba Serikali ione umuhimu wa kuwapa jengo hilo ambalo wameliomba kwa muda mrefu.

Amesema hospitali hiyo hupokea wagonjwa kati ya 180 na 250 kwa siku, miongoni mwao wakiwa ni wajawazito ambao wanaojifungua kwa siku ni kati ya 60 na 100.

Mbunge wa Ilala, Mussa Zungu amesema Hospitali ya Amana imeomba jengo hilo linalomilikiwa na Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) na taarifa za maombi zimefika hadi kwa Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Lukuvi, hivyo Serikali ione haja ya kujibu maombi hayo.

Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda akisisitiza umuhimu wa Serikali kukabidhi jengo hilo kwa hospitali, amesema anaamini waziri mkuu anaweza kusaidia jengo hilo kukabidhiwa kwa Amana hata kabla ya Ijumaa Februari 16,2018.

Waziri Mkuu, Majaliwa akijibu ombi hilo ameagiza ofisa ardhi wa Wilaya ya Ilala kufanya tathmini ya majengo yanayoizunguka hospitali hiyo, ikiwa ni pamoja na kufahamu gharama za fidia zitakazohitajika ili kuruhusu upanuzi.

“Nimepokea ombi lenu, mkuu wa mkoa amesema kwa spidi mliyonayo nitashangaa kama itafika siku ya Ijumaa kwa kuchomeka chomeka huyu, wewe sema hospitali inahitaji hilo jengo,” amesema waziri mkuu.

Amesema kabla ya kutoa uamuzi wowote anahitaji kujiridhisha kuhusu mmiliki wa jengo na matumizi yake, ingawa ni wazi kwamba matumizi ya hospitali ni muhimu.

Dk Shimwela akizungumzia jengo jipya, amesema litaongeza idadi ya akinamama wanaohudumiwa kutoka 253 wa sasa hadi 353.

Amesema kutokana na huduma za afya za kisasa zitakazotolewa kupitia jengo hilo, zitapunguza idadi ya vifo vya akinamama kutoka 18 hadi 14.

Amesema kwa utaalamu mama aliyejifungua hutakiwa kuwa chini ya uangalizi wa wataalamu wa afya kwa saa 24 lakini kutokana na uhaba wa vitanda wengine huruhusiwa mapema.

Dk Shimwela amesema changamoto nyingine inayowakabili ni upungufu wa watumishi ambao wapo 392 (sawa na asilimia 46) wakati mahitaji ni watumishi 671.


Ndugu Watatu wa Familia Tajiri ya Gupta Wakamatwa na Polisi

0
0
Ndugu Watatu wa Familia Tajiri ya Gupta Wakamatwa na Polisi

Polisi wa kitengo maalumu cha kupambana na ufisadi (Hawks) wamethibitisha kwamba watu watatu wamekamatwa baada ya kuvamia mapema asubuhi makazi ya familia tajiri ya Gupta yaliyopo eneo la Saxonwold jijini hapa.

Pamoja na kuthibitisha kukamatwa watu hao, msemaji wa Hawks, Hangwani Mulaudzi hakutaka kuweka wazi majina ya waliokamatwa.

"Hebu tuseme tu kwamba mashtaka yao yanahusu udanganyifu," amesema.

Inaaminika kwamba kabla ya kuvamia makazi ya Gupta, maofisa wa Hawks walikuwa wamevamia kwanza makazi ya Bedfordview yanayoaminika kuwa ya Mkurugenzi mtendaji wa zamani wa kampuni ya Sahara Systems. Mulaudzi alikataa kutoa maoni ikiwa matukio mawili hayo yana uhusiano.

Shirika la habari la Reuters limeripoti kwamba Hawks pia walivamia ofisi za kampuni ya Oakbay ya Gupta zilizopo mjini Sandton Jumatano asubuhi.

Kwa mujibu wa mlinzi ambaye hakutaka jina lake litajwe, maofisa wa Hawks waliwasili wakiwa kwenye magari matatu karibu 1:30 na wakaingia ndani ya jengo hilo. Waliondoka muda mfupi baadaye, walinzi alisema.

Akina Gupta ambao ni familia tajiri ya wazaliwa wa India wamekuwa wakishutumiwa kwa kutumia urafiki wao na Rais Jacob Zuma kwa manufaa binafsi na kibiashara. Familia hiyo ndiyo inatuhumiwa kuiweka Serikali mfukoni katika kashfa kubwa ya ufisadi.

Familia hiyo inayomiliki baadhi ya biashara nchini Afrika Kusini imeshutumiwa kutumia vibaya ushawishi wao na urafiki na Zuma kupata mikataba ya Serikali inayogharimu mamilioni ya dola za Kimarekani.

Mapema, Shirika la TimesLIVE liliripoti kuwa familia ya Gupta inayopigwa vita ilikuwa inataka kuingia makubaliano maalumu na Hawks. Habari kuhusu mpango huo zilivuja baada ya ripoti kwamba mwana wa Rais Jacob Zuma na mshirika wa biashara wa familia ya Gupta, Duduzane Zuma alikuwa amejiandaa kujipeleka pamoja na wanasheria wake kwa Hawks Jumatano.

Duduzane, akijibu ujumbe aliotumiwa na simu alizopigiwa alisema alikuwa katika mkutano, hivyo hawezi kuzungumza.

Viongozi wa Dini Wapewa Onyo Kali na Jeshi la Polisi

0
0
Viongozi wa Dini Wapewa Onyo Kali na Jeshi la Polisi
Jeshi la polisi mkoani Dodoma limewaonya viongozi wa dini mkoani humo ambao wanatabia ya kufanya vitendo vilivyo kinyume na mafundisho ya dini huku likiwaomba wananchi wawafichue viongozi hao ambao wenye tabia hizo.

Hayo yamesemwa leo Februari 14, 2018 na kamanda wa polisi mkoani humo, Kamishna msaidizi Mwandamizi wa polisi, Gilles Muroto.

Kamanda Muroto amesema kuwa kutokana na kukua kwa utandawazi kumekuwa rahisi kwa sasa watu kutumia nafasi hiyo kupotosha umma huku wakijinadi kuwa ni viongozi wa dini.

Muroto amesema viongozi wa dini watakaobainika kufanya vitendo hivyo au vya aina yoyote ile ya udhalilishaji jeshi la polisi halitawavumilia.

Kwa upande mwingine Kamanda Muroto amewaagiza viongozi wa dini kuhakikisha maeneo yao wanayofanyia ibada kunakuwa na ulinzi wakutosha ili kuzuia matukio ya kiuhalifu kutokea.

Soma na hii – Nabii Titto mbaroni baada ya kufanya mahubiri ya uongo kwa miaka 10

Onyo hilo linakuja baada ya mwanzoni mwa mwezi Januari Kiongozi mmoja wa dini aliyejitambulisha kwa jina la Nabii Tito kuhubiri kinyume na maadili ya umambo yaliyo nje na dini.

Kura ya Kutokuwa na Imani na Zuma Kupigwa Bungeni Kesho

0
0
Kura ya Kutokuwa na Imani na Zuma Kupigwa Bungeni Kesho
Kura ya kutokuwa na imani na Rais Zuma kupigwa Bungeni kesho baada ya Rais huyo kutotekeleza wito wa kujiuzulu ndani ya saa 48

 Wabunge wa ANC wataitumia hoja ya kutokuwa na imani na Rais Zuma ambayo tayari imewasilishwa Bungeni na chama cha Upinzani cha Economic Freedom Fighters(EFF) kinachoongozwa na Mwanasiasa kijana mwenye makeke, Julius Malema

Tangu Rais Zuma aingie madarakani hoja 5 za kutokuwa na imani naye zimewasilishwa katika Bunge la Nchi hiyo huku 3 kati ya hizo zikikosa kura kutoka kwa Wabunge wengi na mbili zikikosa vigezo hivyo kutofanikiwa kupigiwa kura

Mwili wa Aliyekuwa Katibu wa Chadema Kusafirishwa Iringa kwa Maziko

0
0
Mwili wa Aliyekuwa Katibu wa Chadema Kusafirishwa Iringa kwa Maziko
Mwili wa aliyekuwa Katibu wa Chadema Kata ya Hananasif jijini Dar es Salaam, Daniel John unatarajiwa kusafirishwa kesho kwenda Iringa kwa maziko.

John ambaye ni mpigapicha maarufu Hananasif aliuawa na watu wasiojulikana na mwili wake uliokotwa jana kwenye fukwe za Coco.

Akizungumzia maandalizi ya mazishi ya kiongozi huyo, mbunge wa Tarime Mjini, Ester Matiko ambaye anasimamia kampeni za Chadema katika kata hiyo amesema marehemu atasafirishwa kesho na kuzikwa Ijumaa.

Matiko amesema vikao vya kukusanya fedha kwa ajili ya kusafirisha mwili wa mwanachama wao huyo vinaendelea kufanyika na kesho wanatumaini kusafirisha  kwenda Mafinga mkoani Iringa.

"Tumewasiliana na familia ya marehemu wametaka ndugu yao akazikwe Iringa. Tunafanya jitihada za kukusanya fedha ili kufanikisha mazishi ya kiongozi wetu," amesema.

Mbunge huyo amelitaka Jeshi la Polisi kufanya uchunguzi na kuchukua hatua dhidi ya watu waliohusika kukatisha maisha ya kijana huyo

Matiko amebainisha kuwa ana uhakika asilimia 100 kwamba hayo ni mauaji ya kisiasa kwa sababu marehemu alitishiwa maisha na watu ambao wanafahamika.

Akizungumzia mazingira ya kifo cha mumewe, mjane wake, Paulina Vitalis amesema kuna watu walikwenda nyumbani kwake Jumapili, Februari 11 kumuulizia mumewe akawaambia hayupo.

Amesema baada ya kuwajibu hivyo waliuliza tena kuwa  muda anaorudi nyumbani, akawajibu saa nne usiku

Amesema siku hiyo mumewe hakurudi nyumbani mpaka jana Jumanne ambapo alipata taarifa kwamba mumewe alikuwa ameuawa na mwili kuokotwa kandokando ya fukwe za Coco.

"Hakuna siku mume wangu aliwahi kuniambia kwamba anatishiwa maisha, lakini Jumatatu watu ndio waliniambia kwamba kuna watu walikuwa wanamtafuta sana," amesema mwanamke huyo ambaye alizaa mtoto mmoja na mwanasiasa huyo.

Akizungumza kwenye msiba huo nyumbani kwa marehemu Mtaa wa  Kawawa , Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe amesema kuuawa kwa John ni njama za washindani wao kwenye uchaguzi mdogo wa Jimbo la Kinondoni ili kuwapunguza nguvu.

Amewataka viongozi na wanachama wa Chadema kutorudi nyuma, bali waendelee na kampeni kama kawaida wakati watu wachache wakiratibu shughuli za mazishi ya kiongozi wao.

"Wenzetu wameamua kuua ili tu washinde uchaguzi huu, tusikubali kuvurugwa na msiba tukasahau uchaguzi. Tukifanya hivyo, lengo lao litakuwa limetimia," amesema Mbowe.

Amewataka wanachama wawe watulivu wakati shughuli za kupumzisha mwili wa marehemu zikiendelea na washirikiane na viongozi wanaoratibu mazishi katika kufanikisha suala hilo.

Awali, akizungumza kwenye msiba huo, mbunge wa viti maalumu, Susan Lyimo amesema hali ya kisiasa nchini sasa si nzuri kwa sababu viongozi hawataki kukosolewa.

"Hawataki kuona  kiongozi anatoka Chadema ndio maana wanatumia nguvu nyingi kuwadhibiti. Mtakumbuka Alphonce Mawazo aliuawa, Tundu Lissu naye alipigwa risasi na kunusurika kuuawa," amesema Lyimo.

Mkapa Aishauri Serikali Kuandaa Utaratibu wa Kupatikana Fedha Kwaajili ya Ukimwi

0
0
Mkapa Aishauri Serikali Kuandaa Utaratibu wa Kupatikana Fedha Kwaajili ya Ukimwi
Rais mtaafu wa Awamu ya Tatu, Benjamin Mkapa ameishauri Serikali kuandaa utaratibu endelevu utakaosaidia upatikanaji wa fedha kwa ajili ya Ukimwi.

Mkapa  amesema hayo jana wakati akizindua harambee ya kuchangia Mfuko wa Ukimwi iliyoandaliwa na Tume ya Kudhibiti Ukimwi Tanzania (Tacaids).

Mkapa amesema wafadhili wamepunguza misaada ya Ukimwi, hivyo fedha za ndani ni muhimu ili kupunguza utegemezi.

“Naipongeza Serikali kwa kuendelea kuchangia fedha kupitia bajeti zake, hata hivyo nashauri uwekwe utaratibu endelevu utakaosaidia kupata fedha za Ukimwi,” amesema

Amesema  kwa kutumia fedha za ndani zitasaidia wagonjwa wa Ukimwi kuwa na uhakika wa kupata matibabu.

Akitoa mfano, amesema  mwaka 2017/18 mahitaji kwa ajili ya kukabiliana na ugonjwa huo yalikuwa Sh1.2 trilioni, lakini fedha zilizoahidiwa na wafadhili ni Sh740 bilioni na upungufu ulikuwa Sh520 bilioni.

“Wafadhili wamepunguza misaada ya Ukimwi, tunapaswa kutafuta vyanzo vya mapato vya ndani ili kuziba pengo hilo,” amesema  Mkapa ambaye kipindi cha utawala wake ndiye aliyeutangaza ugonjwa huo kuwa janga la kitaifa mwaka 1999.

Amesema ipo haja ya wadau kushirikiana na Serikali katika kuuchangia mfuko huo ili uweze kuhudumia wagonjwa.

Pia, aliziomba taasisi na mashirika ya umma kuchangia mfuko huo kwa kuwa bila kuwa na watu wenye afya njema Taifa halitapiga hatua za maendeleo.

Kwa upande wake, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Kazi, Ajira na Walemavu, Jenista Mhagama amesema  fedha zinazochangwa kwa ajili ya mfuko huo ziko salama.

Amesema mfuko huo umeweka mwongozo wa namna ya kutumia fedha hizo ili kuondoa matumizi yasiyokuwa ya lazima.

Akifafanua, amesema mwongozo huo unaonyesha kuwa asilimia 60 ya fedha zinazokusanywa na mfuko hutumika kwa ajili ya ununuzi wa dawa za kufubaza makali ya virusi vya Ukimwi (ARV).

Mhagama amesema  asilimia 25 ya fedha za mfuko huo hutumika kwa ajili ya huduma za kinga na usambazaji wa kondomu pamoja na utoaji wa elimu, wakati asilimia 15 hutumika kwa ajili ya uwezeshaji, ufuatiliaji na tathmini ya Ukimwi.

“Hivyo nawahakikishia wadau kwamba fedha mnazochangia kwa ajili ya mfuko huu ziko salama na zinatumiwa kwa malengo yanayokusudiwa,” amesema.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Mfuko wa Ukimwi (ATF), Godfrey Simbeye amesema hauwezi kutosheleza mahitaji yake kwa kutegemea uchangiaji wa harambee.

Pia, amesema wakati umefika wa kutafuta vyanzo vingine vya mapato ili viweze kusaidia katika mapambano dhidi ya Ukimwi.

“Kuna wataalamu wanaandika andiko ambalo litapendekeza kwa Serikali ili tuwe na tozo la Ukimwi kwenye manunuzi, hilo likifanikiwa tutakuwa tumepiga hatua kubwa,” amesema.

Deni Lasababisha Mtoto Kuzuiliwa Hospitalini Kwa Miezi Mitano Bila Mama Yake

0
0
Deni Lasababisha Mtoto Kuzuiliwa Hospitalini Kwa Miezi Mitano Bila Mama Yake
February 14, 2018 nimeipata hii kumhusu Mama mmoja ambaye ameelezea furaha yake baada ya zahanati moja ya binfasi kumuachilia mtoto wake mchanga baada ya kuzuiliwa kwa miezi mitano kutokana na kushindwa kulipa bili ya hospitali nchini Gabon.

Mama yake mtoto Angel amesema kuwa maziwa yake yamekauka baada ya kutenganishwa na mtoto wake kwa muda wa miezi mitano. Tukio hilo limewashangaza watu mbalimbali nchini humo ila baadaye mama huyo akapata msaada kutoka kwa Wananchi.

Bili ya dola 3,630 ambazo ni Tsh. Milioni 7 laki 2 na elfu sitini ililipwa baada ya kampeni kuanzishwa kwa niaba ya familia. Rais wa nchini hiyo  Ali Bongo alikuwa miongoni mwa wale waliotoa mchango.

Mkurugenzi wa kliniki hiyo alikamatwa Jumatatu kwa mashtaka ya kumteka nyara mtoto, lakini mashtaka hayo yakaondolewa baadaye. Angel baadaye aliachiliwa na kuondoka zahanati hiyo iliyo kaskazini mwa mji muu wiki hii.

Baada ya kuachiwa Mama yake mtoto huyo Sonia Okome amesema kuwa amehuzunika kwa kuwa hawezi kumyonyesha mtoto wake kwa sababu maziwa yalikauka. Pia alilalamika kuwa mtoto huyo hajapewa chanjo yoyote.

Serena Williams Aanza Kazi Mumewe Abembeleza Mtoto

0
0
Serena Williams Aanza Kazi Mumewe Abembeleza Mtoto
Mchezaji tennis Serena Williams amerudi uwanjani kwa mara ya kwanza toka ajifungue mtoto wake wa kike Alexis Olympia miezi mitano iliyopita.

Serena amerudi uwanjani kucheza michuano ya Fed Cup  Asheville USA lakini amezichukua headlines kufuatia kujitokeza uwanjani hapo mume wake na mtoto wake Alexis Olympia.

Mchezo huo ulihudhuria na kufuatiliwa na watu mbalimbali lakini kitendo cha mume wa Serena anayejulikana kwa jina la Alexis Ohanian alikuwa uwanjani hapo akiwa kambeba mtoto na kumnywesha maziwa wakati Serena akiwa anacheza kimewavutia wengi.




Habari Njema: Tunatibu Busha, Korodani Kuvimba, Ngiri, Miguu Kufa Ganzi Pamoja na Matatizo ya Nguvu za Kiume

0
0

Ni dawa ya nguvu za kiume inayorefusha na kunenepesha uume saizi uipendayo (Inch 1-7) kwa muda wa siku 6 tu.Dozi hii itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa muda wa dakika 30, utarudia tendo la ndoa zaidi ya mara 4 bila hamu kuisha bila kujali umri na garantee ni miaka 60 baada ya kutibu tatizo.

Pia tunatibu Busha bila kufanyiwa Oparesheni, korodani moja kuvimba, ngiri, tumbo kujaa gesi na kuunguruma, kutopata choo vizuri, miguu kuwaka moto na kufa ganzi, chango la wanawake, kisukari na kutokwa na kinyama sehemu ya haja kubwa.

MIHAYO:
Inarudisha mke, mchumba, hawara na atakutimizia kila kitu unachotaka kutoka kwake ndani ya  saa 2 tu hata kama yupo mbali. atarudi na kumfunga asiwe na mwingine zaidi yako.

Umefukuzwa kazini? unataka kupandishwa cheo? Umepoteza pesa zako kwenye biashara bila kujua umepandikizwa chuma ulete? Njoo urudishe pesa zako. Unauza mali yako haiendi?


Wasiliana na mtaalam Challo kwa; 0714006521 

Fahamu Mambo Yanayosababisha Gari Kuwaka Moto na Namna ya Kuepuka

0
0

Gari ni kifaa au chombo kinachorahisisha usafiri, lakini kinapaswa kutumiwa kwa tahadhari kubwa. Ajali zinazotokana na magari kuwaka moto, mara kadhaa zimekuwa zikisababisha hasara kubwa au hata kugharimu maisha ya watu.

Kwa hakika jambo hili si zuri, hivyo kila dereva au mtumiaji wa gari ni muhimu akachukua hatua za tahadhari mapema ili kukabili tatizo hili.

Gari kuwaka moto kunaweza kusababishwa na mambo mbalimbali, fuatilia makala hii kwa karibu ili ufahamu mambo 9 yanayosababisha gari kuwaka moto na jinsi ya kuyaepuka.

Kuvuja kwa mafuta

Ikiwa gari litavuja mafuta  ni rahisi sana kuwaka moto. Kumbuka mafuta ya gari pamoja na mafuta lainishi (oil) ni rahisi sana kushika moto.

Tafiti mbalimbali za ajali zimebaini kuwa kuvuja kwa mafuta ni chanzo kikubwa cha magari kuwaka moto.

Ni muhimu kuhakikisha unazingatia matengenezo na ukaguzi wa mara kwa mara wa gari lako ili kubaini kama kuna mahali panapovuja mafuta parekebishwe.

Hitilafu ya umeme

Gari lina mfumo wake wa umeme ambao unatakiwa uwe salama na ufanye kazi jinsi ipasavyo. Mfumo wa umeme unapokuwa na hitilafu, unaweza kusababisha cheche za moto na kusababisha gari kuwaka moto.

Ni muhimu kuhakikisha unatafuta mtaalamu wa magari akague na kurekebisha mfumo wa umeme wa gari lako kila mara. Pia ni muhimu kutumia vifa bora vya mfumo wa umeme wa gari, kwani vifaa duni vinaweza kusababisha moto.

Gari kupata joto sana

Gari halitakiwi lipate joto kupita kiasi. Ikiwa sehemu za gari zitapata joto kupita kiasi zinaweza kuyeyuka au kuwaka moto.

Inashauriwa kuhakikisha mfumo wa kupooza gari uko katika hali nzuri. Pia ni muhimu kupumzisha ghari mara kwa mara wakati wa safari ndefu ili lipoe.

Ajali

Msuguano unaweza kusababisha moto. Gari linapogongana na gari jingine au kugonga kitu kingine, linaweza kuzalisha cheche ambazo zitasababisha gari lishike moto.

Hivyo ni vyema kuzingatia kanuni za usalama barabarani ili kuepuka ajali.

Hitilafu ya kimuundo

Kuna wakati matatizo ya kimuundo ya gari yanaweza kusababisha gari kuwaka moto. Hata hivyo, kutokana na matatizo ya kimuundo kuhusiana zaidi na watengenezaji, tatizo la kimuundo linapobainika hurekebishwa mara moja na watengenezaji.

Ni muhimu kununua gari kutoka kwa watengenezaji wanaoaminika na wenye uzoefu ili kuepuka hitilafu za kimuundo.

Matengenezo duni

Kama jinsi ambavyo umekwisha kuona kwenye hoja zilizotangulia hapo juu, ni muhimu sana kuzingatia swala la matengenezo. Mifumo ya gari kwa ujumla inahitaji matengenezo sahihi na kwa wakati.

Kwa mfano ikiwa hutozingatia matengenezo ya magurudumu, yanaweza kupasuka au kuwaka moto. Ni muhimu pia kuhakikisha mafuta lainishi (oil) yapo kwa kiwango kinachotakiwa ili kuepusha msuguano wa vyuma unaoweza kusababisha moto.

Vifaa vya nyongeza

Watu wengi hupenda kuongeza vifaa mbalimbali kwenye magari yao tofauti na vile vilivyotoka kiwandani pamoja na gari. Vifa hivi huweza kuwa taa, redio, mifumo ya ulinzi, n.k. Vifaa hivi vya nyongeza vingi havina ubora na havifungwi na wataalamu.

Hivyo mara nyingi vifaa vya nyongeza kwenye magari vinaweza kusababisha gari kuwaka moto. Ni muhimu kuhakikisha ubora wa kifaa pamoja na kuhakikisha ufungwaji sahihi na salama.

VIDEO: Jeshi La Polisi Kumchunguza Mbowe

0
0
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kipolisi wa Kinondoni, Muliro Jumanne Muliro amesema wanachunguza kauli ya Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA, Freeman Mbowe aliyoitoa kuhusu 'kuuwawa' kwa kiongozi wa Chama hicho huku akitoa shutuma kwa jeshi hilo kuhusika.

TAZAMA FULL VIDEO HAPA CHINI

Rais Zuma Agoma Katu Katu Kujiuzulu " Sijiuzulu ng’o"

0
0
Rais wa Afrika Kusini, Jacob Zuma amesema kwamba hajafanya kosa lolote, hivyo hawezi kujiuzulu kama chama chake cha African National Congress (ANC) kilivyokuwa kikimtaka afanye leo.

Rais Zuma ameyasema hayo alipokuwa akifanya mahojiano na kituo cha runinga cha SABC cha Afrika Kusini, baada ya chama chake kumtaka kujiuzulu kabla ya siku kuisha ama vinginevyo bunge litapiga kura ya kutokuwa na imani naye kesho.

Kumekuwepo na mashinikizo mbalimbali ya kumtaka Rais Zuma ajiuzulu kutokana na tuhuma mbalimbali za rushwa zinazomkabili.

Rais Zuma amesema, chama hicho na wengine wote wanaomtaka ajiuzulu hawamtendei haki kwa sababu hakuna  hata mmoja anayetoa sababu au kumwambia ametenda kosa gani hadi kustahili kujiuzulu.

Zuma amesema kwamba hapingani na chama hicho, lakini hakubaliani na uamuzi wanaotaka kuuchukua wa kumshinikiza ajiuzulu. Amesema alikubali kujiuzulu baada ya mwezi Juni, lakini walimkatalia.


Amesema kwamba licha ya mahojiano aliyoyafanya atatoa taarifa zaidi kuhusu shinikizo hilo. Aidha, ANC wamesema kwamba wamesikia kauli ya Rais Zuma na kwamba watatoa taarifa kamili baada ya kupata taarifa rasmi ya kiongozi huyo.

Mapema, kiongozi wa ANC, Jackson Mthembu alisema kuwa, kura ya kutokuwa na imani na Rais itapigwa bungeni Alhamisi ili Rais aondolewe, na Mwenyekiti wa ANC, Cyril Ramaphosa aatapishwa mara moja kuliongoza taifa hilo.

Kamati Kuu ya ANC ilikubaliana siku ya Jumanne kwamba Rais Zuma ajiuzulu ambapo walimtaka kufanya hivyo kabla ya Jumatano kuisha.

Wakati wa mahojiano yake, Rais Zuma hakuzungumzia jambo lolote kuhusu familia ya Guptas, ambayo inadaiwa kutumia ukaribu wake na Rais Zuma, kufanya ushawishi katika masuala mbalimbali ya kisiasa na kiuchumi nchini Afrika Kusini.

Breaking News..Zari Ambwaga Diamond Platnumz Siku ya Valentine Day...Kisa Kizima Hichi Hapa

0
0

Zarinah Hassan(Zari) ametangaza kuvunja rasmi mahusiano yake ya kimapenzi na Staa wa Bongo Fleva nchini humo, Nasibu Abdul(Diamond Platnumz)

Kwa kupitia ukurasa wake wa Mtandao wa kijamii wa Instagaram, Zari amesema kilichompelekea kufanya hivyo ni kutokana na Diamond kutokuwa mwaminifu kwenye mahusiano

Zari na Diamond katika kipindi chao cha mahusiano kilichodaiwa kuanza Novemba 2014 wameweza kupata watoto wawili, wa kike anaitwa Tiffah na wa kiume anaitwa Nillan
Viewing all 104417 articles
Browse latest View live




Latest Images