Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104756 articles
Browse latest View live

Kiongozi wa Chama cha Upinzani Zimbabwe MDC ndugu Morgan Tsavingarai Amefariki Dunia

$
0
0
Kiongozi wa Upinzani wa Zimbabwe kutoka chama cha MDC, Morgan Tsvangirai amefariki dunia leo.

Alikuwa akipatiwa matibabu huko nchini Afrika Kusini.

Kwa muda mrefu amekuwa akisumbuliwa na ugonjwa wa saratani.

JOHANNESBURG – Zimbabwe's opposition Movement for Democratic Change (MDC) leader, Morgan Tsvangirai, has died.
[​IMG]
Details surrounding his death were not known but Tsvangirai was suffering from colon cancer and had previously been treated at a Johannesburg hospital.

Tsvangirai had a tumultuous and era-defining career in Zimbabwean politics.

He went from being a supporter of President Robert Mugabe, o becoming his most high-profile opponent.

Breaking News: Rais Jacob Zuma Akubali Yaishe..Aachia Madaraka Kwa Kujiuzulu

$
0
0

AFRIKA KUSINI: Rais Jacob Zuma ametangaza uamuzi wake wa kuachia Urais usiku huu

Asema asingependa damu imwagike na chama(ANC) kimeguke kwa sababu yake

Wananchi Wampasha DC Mbele ya Rais..Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Alhamisi ya February 15

$
0
0

Wananchi Wampasha DC Mbele ya Rais..Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Alhamisi ya February 15

Makonda: Kuna Gazeti Moja kazi yake ni Kunichonganisha

$
0
0
MKUU wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda, amesema kuna gazeti moja nchini limekuwa likiandika habari za kumchonganisha yeye na viongozi wengine au taasisi nyingine za serikali, jambo ambalo amesema halikubaliki wala hawezi kulifumbia macho.


Makonda ameyasema hayo jana, Feb. 14, 2018 wakati wa uzinduzi wa Jengo la Huduma za Mama na Mtoto katika Hospitali ya Amana, iliyopo Ilala jijini Dar ambapo mgeni rasmi alikuwa Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa.

Kauli hiyo ya Makonda imekuja kutokana na maamuzi yake ya kuvunja mabaraza yote ya ardhi ya mkoa wa Dar, na kutaka kazi hizo zifanywe na makatibu tarafa hadi pale ambapo utaratibu mwingine utawekwa, jambo ambalo baadhi ya vyombo vya habari na wanaharakati walidai kuwa anaingilia kazi ya mahakama.

“Kuna gazeti moja linahangaika sana kuandika vitu vibaya kuhusu Mkoa wa Dar, wanajifanya wanajua sana sheria, wanachonganisha, na leo nimeona wameandika tena, wasitupotezee muda.

“Aliyeanza kugombanisha duniani ni shetani, lakini ilifika wakati akashindwa, hili gazeti raha yao wanataka wasikie mahakama imemkataa Mkuu wa Mkoa, hawaoni mateso ya wanachi wala kuyaripoti.

“Sasa aelewe tu kwamba hawatafanikiwa, nimeangalia nikabaini kuna ardhi moja bosi wao aliichukuaga, ipo tu limebaki poli katika eneo moja katika Wilaya ya Ubungo, tutaangalia taratibu angalau tuwapatie watu lijengwe soko la kisasa pale,” alisema Makonda bila kutaja ni gazeti gani.

Chanzo: Global Publishers

Skendo ya Unga Ilivyomtafuna Baby Madaha

$
0
0
MWANADADA kutoka kiwanda cha filamu na muziki Bongo, Baby Madaha ameeleza kuwa katika maisha yake hakuna kitu kilichowahi kumtafuna na kumletea shida kwenye familia yake kama skendo ya kutumia unga.

Baby amesema kuwa, skendo hiyo ilitokana na kushiriki kwenye filamu mbalimbali akiwa kama teja, jambo ambalo lilisababisha watu wazushe kwamba alikuwa akitumia unga.

“Kiukweli skendo ya unga ilinitesa sana kiasi kwamba familia yangu wakajua kweli ninatumia unga, unajua mama yangu na mdogo wangu ni madaktari, kwa hiyo suala hilo lilikuwa ni la aibu kiasi kwamba walinichukua na kunipeleka hospitalini kupima huko ndiko nikagundulika kwamba nilikuwa situmii unga, hiyo ndiyo ikawa nafuu yangu,” alisema Baby Madaha.

Mwigulu Nchemba Awakemea Wanasiasa Wanaoihusisha Serikali na Kushambuliwa kwa Tundu Lissu

$
0
0
Waziri wa Mambo ya Ndani ya nchi Dkt. Mwigulu Nchemba amewataka wanasiasa kuacha kutumia kuumia kwa mbunge Tundu Lissu kama chambo ya kisiasa katika majukwaa.

Dkt. Mwigulu amesema hayo jana mkoani Singida wakati wa kampeni za udiwani kata ya Mitunduluni.

Mwigulu  amewataka wanasiasa  waache kutumia matatizo ya ndugu yao kama mitaji ya kisiasa badala  yake waje na hoja za maana za kusaidia katika maendeleo ya nchi.

Aliongeza kusema kuwa mwaka uliopita uhalifu wa ajabu ulitokea ambapo kuna watoto wadogo wa chekechea walitekwa na kuuwawa ambao hawakuwa  hata na  shida na mtu yoyote na wazazi wao ni watu wa kawaida kabisa je serikali ndio imehusika.

“Sisi tunaoshughulika na maswala ya uhalifu tunatafuta wahalifu wanaofanya maswala ya kihalifu, kuna watu wanaona ni ajenda ya kisiasa wakati sisi tunaombea mtu apone” alisema Dkt. Mwigulu

Dkt. Mwigulu ameongeza na kusema kuwa je angeamua kuendelea  kusema kuhusu kupigwa risasi kwa mwanajeshi masaki inauhusiano gani na shida za kata ya Mitundulini, hivyo wananchi wa Singida wawaadhibu kwa kuwanyima kura katika uchaguzi wa tarehe 17 mwezi huu.

Uchaguzi mdogo katika kata ya Mitunduluni unafanyika baada ya Diwani aleyekuwepo katika kata hiyo kufariki dunia kwa maradhi. VIDEO:

Gigy Money Mapenzi Moto moto na Mpenzi Wake Wamalizana Ugomvi Wao

$
0
0
Gigy Money Mapenzi Moto moto na Mpenzi Wake Wamalizana Ugomvi Wao
MWANADADA ambaye ni mwana-muziki na muuza sura kwenye video za Kibongo, Gift Stanford ‘Gigy Money’, hivi karibuni amefunguka kwamba, hana matatizo tena na baba wa mtoto wake mtarajiwa aitwaye Mo Jay, na kwamba kila kitu kwa sasa wamekwisha kiweka sawa ambacho kilikuwa kinawafanya wagombane mara kwa mara.

Akichonga na Showbiz Xtra, Gigy aliongeza kuwa, wawapo wawili ‘tafaruku’ ndogondogo huwa hazikosekani, jambo ambalo lilikuwa linajitokeza kwao, lakini kwa sasa kila kitu kipo sawa na hawana tatizo kabisa.

“Sina shida yoyote na mpenzi wangu kwa sasa, kila kitu kipo sawa na yakiwepo ya kuzun-gumza kama tuna matatizo nitazu-ngumza huko mbele, lakini kwa sasa hakuna tatizo lolote,” alisema Gigy.

Mbowe Kuchunguzwa na Polisi

$
0
0
Mbowe Kuchunguzwa na Polisi
Kamanda wa Polisi Kinondoni, Murilo Jumanne Murilo amefunguka na kusema kuwa jeshi hilo sasa linachunguza kauli alizotoa Mwenyekiti wa CHADEMA Taifa kuhusu kifo cha Kiongozi wa CHADEMA kata ya Hananasif, ambaye mwili wake uliokotwa ukiwa na majeraha.


Kamanda Murilo amesema haya leo Februari 14, 2018 wakati akiongea na waandishi wa habari kuhusu mambo mbalimbali ikiwepo suala la uchaguzi na kusema kuwa wao kama jeshi la polisi wanachunguza taarifa alizotoa Mbowe kuhusu sakata la kifo cha kiongozi huyo wa CHADEMA.

"Moja ya kazi kubwa ya jeshi la polisi ni kuchunguza jambo hiyo ni kauli yeye ametoa na kauli yake tunaichunguza pia anasema hivyo kwa kuzingatia misingi ipi ambayo inamsukuma yeye kusema hayo anayoyasema, hatuwezi kuacha mtu akajisemea vitu kwa kusukumwa na hisia zake ndiyo maana sisi jambo linapotokea jambo la kwanza kabisa kufanya ni kuchunguza hatusukumwi na hisia za mtu kwa sababu tunajua yeye hajasomea kazi ya polisi na hayo anayotamka tunayachukua kama taarifa zingine za kawaida ambazo mwananchi yoyote anaweza kutupa" alisema Murilo

Aidha Murilo aendelea kudai kuwa wamekuwa wakimsikia sana Mbowe akitoa kauli mbalimbali

"Mhe. Mbowe tunamfahamu sana amekuwa akitoa matamko mengi mbalimbali hivyo jukumu letu ni kuchunguza itakavyo lazimika sisi tutamuomba atueleze anamaanisha nini kutamka hivyo itakavyolazimika lakini hatuwezi kusukumwa na kauli yake, tukatoka kwenye msingi wa upelelezi na kuburuzwa na hisia zake halafu baadaye tukosee ili haki isitendeke. Nachoweza kusema wahalifu wote tukichunguza na kuthibitisha huwa wanakamatwa"

Mgombea wa Ubunge Kupitia CCM Maulid Mtuli Aahidi Kuibadilisha Tandale

$
0
0
Mgombea wa Ubunge Kupitia CCM Maulid Mtuli Aahidi Kuibadilisha Tandale
Mgombea ubunge Jimbo la Kinondoni kupitia CCM, Maulid Mtulia amesema kwa muda wa miaka miwili alioliongoza jimbo hilo kwa tiketi ya CUF alikuwa mbunge wa mashaka.

Mgombea huyo aliyasema hayo akiwa Kata ya Ndugumbi akiongozwa na Mbunge wa Nzega Mjini, Hussein Bashe na Naibu Spika wa Bunge, Dk Tulia Ackson.

Alidai kipindi hiki akichaguliwa atahakikisha barabara ya Argentina na Tandale inajengwa kwa kiwango cha lami huku pembeni zikiwaka taa.

‘’Sikuweza kufanya lolote kwa wakazi wa Ndugumbi wakati nikiwa CUF, lakini sasa mkinichagua najua nitafanya nini,’’ alisema.

“Kwa kuwa nipo kwenye chama dume kilichopewa ridhaa na Watanzania kuleta maendeleo, baada ya kupata ubunge nitakwenda kujenga Mto Mwangosi.’’

Aliongeza kuwa, “Nakwenda kuhakikisha tunatumia pesa za Manispaa ya Kinondoni fungu la vijana, tutawapa mikopo wanunue pikipiki waweze kujiajiri.”

Kwa upande wake, mgombea ubunge Jimbo la Siha kwa tiketi ya CCM, Dk Godwin Mollel aliwaomba wananchi wamrudishe bungeni ili aweze kushirikiana na Serikali kufufua zao la kahawa.

Mgombea huyo pia alisema ataboresha miundombinu ya madarasa ya shule na mazingira ya upatikanaji wa elimu ili kuhakikisha elimu inayotolewa inakuwa bora na si bora elimu.

Akiwa katika Kijiji cha Kengia, Kata ya Kashashi, Dk Mollel alisema uboreshaji wa kahawa utasaidia kuwakomboa wananchi kiuchumi na kuachana na umaskini.

“Sikutumwa bungeni kuandamana na kufunga mdomo, bali kuwasemea na kuwaletea maendeleo. Sasa nitumeni nikakomeshe umaskini Kashashi kwa kufufua zao la kahawa na kuboresha mazingira ya upatikanaji wa elimu,” alisema.

Aliongeza kuwa Kata ya Kashashi inahitaji kusambaziwa umeme, hivyo akichaguliwa atahakikisha wananchi wanafikishiwa nishati hiyo na kuitumia kuanzishia miradi ya maendeleo ili wajikwamue kiuchumi.

Mgombea ubunge kwa tiketi ya CUF Jimbo la Siha, Tumsifueli Mwanri alisema akichaguliwa atahakikisha viwanja vya michezo vinakuwapo kila kijiji na vilivyovamiwa vinarudishwa.

Akizungumza na wananchi wa Kata ya Nasai wakati wa kuomba kura, alisema atahakikisha kila kijiji na kitongoji kunakuwa na viwanja vya michezo.

“Nataka kufufua michezo kwani michezo ni ajira na pia michezo inaboresha afya na kuepusha magonjwa ikiwamo kisukari, nipeni nafasi nifanye kazi,” alisema.

Kwa upande wake, mgombea ubunge wa CUF Jimbo la Kinondoni, Rajabu Salum akiwa Msisiri, Kata ya Makumbusho alisema wanacheleweshewa hati ya viapo vya mawakala wa chama chao.

“Wanataka kutoa hati za viapo siku hiyo ya kupiga kura ili baadaye waonekane wamechelewa nisichaguliwe,” alisema.

Mkutano wa kampeni wa Chadema uliokuwa ufanyike jana stendi ya zamani ya daladala iliyopo Mwenge ulizuiwa kwa kile ambacho Mkurugenzi wa Manispaa ya Kinondoni, Aaron Kagurumjuli alisema hawakuwa na ratiba ya kukutana eneo hilo.

Awali, wananchi waliokuwa katika eneo la Mwenge walisema kabla ya mkutano huo kuvunjwa kulikuwa na makada wa CCM waliowahi na kuanzisha mkutano wao.

Hata hivyo, msafara wa mgombea ubunge wa Chadema, Salum Mwalimu ulifika eneo hilo majira ya saa 10 na kukuta mkutano wa CCM ukiendelea, ndipo walipowaonyesha ratiba maofisa wa polisi ambao waliuvunja mkutano huo.

Licha ya kuuvunja mkutano huo wa CCM baadhi ya mashuhuda waliokuwa katika eneo hilo walisema polisi haohao waliwakataza makada wa Chadema akiwemo Mwalimu kuendelea na mkutano jambo lililozua malumbano.

Akizungumza kwa njia ya simu, Kagurumjuli alisema mkutano huo ulivunjwa kwa sababu Chadema hawakuwa na ratiba katika eneo hilo.

“Kwenye ratiba yetu hakukuwa na chama chochote kilichotakiwa kufanya kampeni eneo la Mwenge. Chadema walitakiwa kufanya mkutano eneo la Ali Maua, Kata ya Kijitonyama. Ni makosa kubadilisha eneo la kampeni na ili ubadilishe ni lazima uandike barua,” alisema Kagurumjuli.

“Siyo Chadema tu, hata CCM walikuwa pale baada ya kuona nafasi, lakini tuliwafukuza.”

Hata hivyo, mgombea ubunge wa Chadema, Mwalimu alisema hakukuwa na sababu ya msingi kwa wao kuondolewa eneo la Mwenge kwa kuwa ratiba ilionyesha watakuwa Kata ya Kijitonyama, hivyo wana haki ya kufanya mkutano popote.

“Hakukuwa na sababu yoyote ya kutuondoa pale, hata OCD aliyekuwa pale nilimuuliza akasema hakuna sababu, basi tu kwa sababu ana risasi na mabomu anafanya ubabe,” alilalamika Mwalimu.

“Tulishakubaliana tangu mwanzo kwamba kama chama kimepangiwa kata fulani kinatawala kata yote bila kuingiliwa na chama kingine. Mbona nimefanya kampeni za nyumba kwa nyumba kata yote sijakatazwa?”

“Jeshi la Polisi limedhihirisha wanachotaka kukifanya Februari 17 na sisi hatutakubali kuwa wanyonge maana wanaona kuna wanaume na wavulana. Juzi kiongozi wetu ametekwa na kuuawa, mara wamevamia ofisi yetu na kupiga mabomu, leo wamekataza mkutano wetu. Sisi hatutakubali, tutapambana nao hadi mwisho.”

Hata hivyo, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kipolisi wa Kinondoni, Jumanne Muliro alipoulizwa kwa njia ya simu alisema hana taarifa za kuzuiliwa kwa mkutano huo.

Flora Temba, Bahati Chume (Moshi), Elizaberth Edward, Pamela Chilongola, Fortune Francis, Asna Kaniki, Elias Msuya na Ephrahim Bahem (Dar)

Huu Hapa Ujumbe wa Valentine Day kwa Irene Uwoya na Dogo Janja Kutoka Kwa Mama Mzazi Dogo Janja " Mdumu Kwenye Ndoa Kama Mimi"

$
0
0
Huu Hapa Ujumbe wa Valentine Day kwa  Irene Uwoya na Dogo Janja Kutoka Kwa Mama Mzazi Dogo Janja  " Mdumu Kwenye Ndoa Kama Mimi"
Mama wa Msanii wa Bongo Fleva, Abubakar Chande al-maarufu Dogo Janja ametoa ujumbe wa Valentine Day kwa mkwe wake Irene Uwoya ambaye amefunguka ndoa na mtoto wake huyo.

Akizungumza na Global Tv Mama Dogo Janja amewapa uhusia wa maisha ya ndoa kwa watoto wake hao na kuwataka kuelewana kutokana na maisha ya ndoa kuwa na vikwazo vya hapa na pale.

Pia amewaomba kudumu kwenye ndoa yao kama alivyo yeye na ndoa yake na kuomba uongozi wa Tip Top kumuongoza Dogo Janja ili kufikia malengo yake.

Bella, Jack Pemba Warudiana Waonekana Wakila Bata

$
0
0
Bella, Jack Pemba Warudiana Waonekana Wakila Bata
LICHA ya msanii wa Bongo Fleva, Isabela Mpanda ‘Bella’ kuwahi kukiri kwamba amemwagana na aliyekuwa mpenzi wake, tajiri Jack Pemba ambaye ni Mbongo anayefanya biashara zake nchini Uganda, hivi karibuni wamezua gumzo baada ya kuonekana wakijiachia na kutupia picha mtandaoni wakiwa pamoja.

Bella ambaye kwa sasa ni mjamzito anayetarajiwa kujifungua muda wowote, yeye na Jack Pemba walizua gumzo kwa mashabiki na watu wao wa karibu waliokuwa wakijiuliza kwamba inawezekana mwanaume huyo ndiye baba kijacho wa Bella!

“Nawaona Bella na Jack Pemba wanajiachia tu huku Mbezi-Beach (Dar), wala hata hawaoni shida, sasa tunajiuliza huo ujauzito wa Bella ni wa Jack Pemba? Lakini Bella aliwahi kukiri kuwa ana mpenzi mwingine ambaye anafanya kazi benki, sasa hatuelewi maana hata baa aliyofungua Bella inasemekana amefunguliwa na huyo bwana,” alisema Mwanahawa Shaban ambaye ni jirani wa Bella.

Alipoulizwa Bella kama Jack ndiye baba mtoto wake mtarajiwa, alishikwa na kigugumizi akisema kuwa Jack Pemba alimtembelea tu kwenye baa yake ya Belas Bar iliyopo Mbezi-Beach, lakini hayo mengine hana majibu.

“Kuhusu mimba yangu kwamba ni ya Jack Pemba…sijui labda ni yake. Hapa amekuja kunitembelea tu kwenye baa yangu na kunisapoti pia,” alisema Bella.

Trump Atoka Kimapenzi na Nyota wa Filamu za Ngono

$
0
0
Trump Atoka Kimapenzi na Nyota wa Filamu za Ngono
Wakili binafsi wa muda mrefu wa Rais wa Marekani Donald Trump amekiri kumlipa nyota wa filamu za ngono dola 130,000, mwaka 2016.

Hatua hiyo inajiri wakati vyombo vya habari vikisema kwamba, nyota huyo wa filamu za ngono kwa jina Stromy Daniels alilipwa katika makubaliano ya kutozungumzia uhusiano wao.

Mrembo huyo aliwahi kusema kuwa alikuwa na uhusiano wa kimapenzi na Rais Donald Trump mwaka 2011 katika mahojiano lakini Wakili huyo alidai Rais Trump alikana kuwepo kwa uhusiano wowote kati yao.

Katika mahojiano ya mwaka 2011 na jarida la InTouch , nyota huyo wa filamu za ngono, alisema, alianza uhusiano na Rais Trump 2006 baada ya Melania Trump kujifungua mwanawe Barron.

Ripoti hizo zilizuka mwezi Januari wakati jarida la Wall Street liliporipoti kwamba alilipwa ili kuficha makubaliano fulani kabla ya uchaguzi mkuu wa 2016 hatua iliyomzuia kuzungumzia madai hayo.

Wananchi Wamchongea DC Mbele ya Mkuu wa Mkoa

$
0
0
Wananchi Wamchongea DC Mbele ya  Mkuu wa Mkoa
Jana haikuwa siku nzuri kwa mkuu wa Wilaya ya Mwanga, Aaron Mbogho baada ya wananchi kumshtaki kwa mkuu wa mkoa wakisema ameshindwa kutatua kero ya maji.

Katika kuonyesha ukubwa wa kilio chao, baadhi yao walimuomba mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, Anna Mghwira kuvaa kofia ya mkuu huyo ili awatumikie.

Wananchi wa kata za Toloha na Kiria wilayani Mwanga walieleza hayo juzi wakisema tangu Mbogho ateuliwe na Rais kuongoza wilaya hiyo hawajawahi kumwona katika maeneo yao akifuatilia changamoto zinazowakabili.

Katika mikutano iliyofanyika kwenye kata hizo kwa nyakati tofauti, wananchi hao walilalamikia kero mbalimbali lakini kubwa ikiwa ni ya maji.

Mkazi wa Kata ya Kiria, Ayubu Msangi alimuomba Mghwira aifanye Wilaya ya Mwanga iwe Moshi ili aweze kutatua kero zinazowakabili.

“Hatumtaki mkuu wa wilaya, ana dharau, hatufai kabisa, utakapochukua kero zetu na kuziacha ofisi ya mkuu wa Wilaya ya Mwanga wataacha palepale bila kuzifanyia kazi na kukudharau. Tunataka wilaya yetu sasa iwe ya Moshi ili tukipata tabu tukueleze wewe mama na mkuu wa wilaya yetu utakua ni wewe kuanzia leo,” alisema Msangi.

Msangi alisema wanapopeleka malalamiko kwenye ofisi za ngazi ya wilaya hakuna kinachotekelezeka, badala yake inayakumbatia.

Alisema kwa muda wa wiki mbili sasa, maji hayapatikani katika Kata ya Kiria hali ambayo inawalazimu kutembea umbali wa zaidi ya kilomita 13 kutafuta ndoo moja ya maji.

“Tatizo hili ni kubwa maana linaharibu shughuli za uchumi, tunaomba hatua ya haraka ichukuliwe. Wananchi wanashindwa kufanya shughuli yoyote kama tunavyojua, maji ni uhai,” alisema.

Jane Mkwizu mkazi wa Kijiji cha Kizungo kilichopo Kata ya Toloha alisema wanakwenda kutafuta maji mbali kuanzia saa kumi na moja asubuhi hadi saa 10 jioni ndipo huyapata na hujikuta wakirejea nyumbani saa mbili usiku.

“Tunaomba mama utusaidie. Wewe ni mwanamke mwenzetu, tunaomba usikie kilio chetu utufuatilie kama hayo maji yatarudi maana tumerudi kwenye umaskini ambao tulitoka miaka ya nyuma wakati wenzetu wanapiga hatua,” alisema.

Baada ya kusikiliza malalamiko hayo ya wananchi, Mghwira hakumpa nafasi mkuu wa wilaya kuzungumza badala yake, alimuagiza mhandisi wa maji Wilaya ya Mwanga, Ernesta Kihwele kufunga mabomba yote yaliyoungwa holela kwenye chanzo cha maji kilichopo Msitu wa Kindoroko.

“Naomba kuanzia sasa mabomba yote yakafungwe kwenye vyanzo vya maji isipokuwa mabomba yanayopeleka maji kwenye huduma za afya ili wananchi wa Toloha wapate maji hadi matangi yenu yajae ndipo mgao uanze,” alisema Mghwira.

Mkuu wa mkoa alisema mgao huo ukisimamiwa vizuri, maji yatapatikana kwa wote bila adha yoyote.

Mbali ya kero ya maji, wananchi wa Kata ya Kiria waliilalamikia halmashauri ya wilaya hiyo kwa kushindwa kutengeneza miundombinu ya barabara licha ya wakulima kutozwa Sh2,000 kwa gunia moja wanapotoa mazao shambani.

Mkuu wa wilaya ajitetea

Akizungumza kwa simu jana kuhusu malalamiko ya wananchi, Mbogho alisema hayana msingi kwa kuwa kila kitu huwa kinafanyika kiutaratibu na kwa mipango iliyopangwa kwa wakati.

“Mtu aje ofisini tujue tatizo lake liko wapi, kwani kuna mtu aliwahi kuja ofisini akafukuzwa? Kila kitu kinafanyika kiutaratibu na tunafanya vitu ambavyo viko kwenye bajeti,” alisema.

Mbogho alisema hawezi kuzungumzia kitu ambacho ni cha jumla jumla na pia hawezi kufanya kitu kilicho nje ya mstari.

Soma Nafasi za Ajira Zilizotangazwa Siku ya Leo

$
0
0

Miujiza ya Sharifu Seif Mohamed..JE Umeachwa na Mme/Mke au Mpenzi, Umesongwa na Mitihani ya Maisha..Piga Simu Upate Muujiza Wako

$
0
0

SHARIFU SEIF MOHAMED ANAWASHUKURU WALE WOTE WANAOENDELEA KUPIGA SIMU, WENYE MATATIZO NA WALE WANAOTOA  SHUKRANI NA SHUHUDA JINSI TIBA ZAKE ZINAVYO WASAIDIA,

(Rudisha mahusiano yako ndani ya masaa 72 tu)

SHARIFU MOHAMED Ni  mtaalam na mnajimu maarufu wa nyota na kubashiri mambo yanayo watesa binadamu duniani kote na kupata ufumbuzi, Anatumia kitabu cha QUR'AN, Dawa za Asili, Dawa za Kiarabu na majini kwa kumtuliza mke/mme, mchumba au mpenzi ndani ya masaa 72 tu, na kutatua matatizo yote ya kimaisha,

Je Umeachwa na UMPENDAE awe Mme/Mke na bado unampenda? Je Umekimbiwa na Mmeo/ Mkeo n anaishi na mtu mwingine? Je Umejaribu sehemu nyingi bila mafanikio? Mpigie simu SHARIFU SEIF sasa hivi ujionee Muujiza wa Papo kwa Papo, Anauwezo wa hali ya juu wa kusambaratisha mahusiano yao na kumrejesha kwako haraka sana na Kumfanya Atimize Ahadi zote Ndani ya Muda Mfupi Endapo Utafwata Atakacho Kuelekeza

ANAZO DAWA ZA MAPENZI, NGUVU ZA KIUME, CHANGO NGIRI MAJI NA N.K, ZINDIKO LA NYUMBA NA BIASHARA, PETE ZA BAHATI, HUMALIZA KABISA TATIZO LA NGUVU ZA KIUME NA KUREFUSHA UUME KWA SAIZI UNAYOTAKA, HUZUIA CHUMA ULETE KWENYE BIASHARA, HURUDISHA MALI ZILIZOPOTEA, MAGONJWA SUGU, MIGUU KUWAKA MOTO AU KUFA GANZI, HUTIBU BUSHA BILA KUPASUA, ANAO UWEZO WA KUMRUDISHA ALIE MBALI AU ALIECHUKULIWA MSUKULE, KUPANDISHA NYOTA NA KUSHINDA BAHATI NA SIBU, KASAFISHA NYOTA NA KUKUPA MVUTO WA AJABU, KUTOA NUKSI NA VIFUNGO MBALIMBALI,  MAFANIKIO YA MAISHA NA UTAJIRI BILA MASHARI, NA MENGINE MENGI YA SIRI,

JE UMAHANGAIKA KUPATA MTOTO BILA MAFANIKIO? WASILIANA NA MTAALAMU HUYU KWANI YEYE HUFAULU PALE WOTE WALIPOSHINDWA, PIA UMALIZA KAZI ZILIZO SHINDIKANA NA WATAALAM WENGINE NDANI YA MASAA 24 TU,

(NA ANATIBU KWA NJIA YA SIMU UKIWA NCHI YOYOTE AU MKOA WOWOTE ENDAPO UTAFWATA MAELEKEZO YAKE)

Kwa ushauri na mawasiliano  zaidi Piga SIMU No:

Mobile +255 654-836970
WhatsApp +255 756-033670


Habari Njema: Tunatibu Busha, Korodani Kuvimba, Ngiri, Miguu Kufa Ganzi Pamoja na Matatizo ya Nguvu za Kiume

$
0
0

Ni dawa ya nguvu za kiume inayorefusha na kunenepesha uume saizi uipendayo (Inch 1-7) kwa muda wa siku 6 tu.Dozi hii itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa muda wa dakika 30, utarudia tendo la ndoa zaidi ya mara 4 bila hamu kuisha bila kujali umri na garantee ni miaka 60 baada ya kutibu tatizo.

Pia tunatibu Busha bila kufanyiwa Oparesheni, korodani moja kuvimba, ngiri, tumbo kujaa gesi na kuunguruma, kutopata choo vizuri, miguu kuwaka moto na kufa ganzi, chango la wanawake, kisukari na kutokwa na kinyama sehemu ya haja kubwa.

MIHAYO:
Inarudisha mke, mchumba, hawara na atakutimizia kila kitu unachotaka kutoka kwake ndani ya  saa 2 tu hata kama yupo mbali. atarudi na kumfunga asiwe na mwingine zaidi yako.

Umefukuzwa kazini? unataka kupandishwa cheo? Umepoteza pesa zako kwenye biashara bila kujua umepandikizwa chuma ulete? Njoo urudishe pesa zako. Unauza mali yako haiendi?


Wasiliana na mtaalam Challo kwa; 0714006521 

Mmh! Wabongo Noma Sana..... Cheki Ujumbe Wanaompa Zari Baada ya Kutangaza Kumtema Diamond

$
0
0
Baada ya Zari kutangaza rasmi kuwa kwa sasa hayupo tena kwenye mahusiano na mzazi mwenzie, Diamond Platnumz imeonekana hatua hiyo kupokelewa kwa mtazamo chanya na baadhi ya mashabiki wa Diamond Platnumz hususani wanawake.

Watu wengi ambao walikuwa wanawafuatilia wawili hao wameonekana wakitoa maoni ya kumpongeza kwa maamuzi aliyoyachukua ya kumuacha Diamond Platnumz.

Baadhi ya maoni ambayo yametolewa kwenye posti ya Zari kwenye mtandao wa Instagram, yamempongeza Zari kwa kumwambia kuwa yeye ni mwanamke jasiri na anayejitambua.

iam_golden_heartIt’s awise decision darling though it’s not easy. I salute you mum Tee
queen_godlistenAsante @zarithebossladyu have to be Your self cause hakuna namna ma dear and I appreciate Ur Opinions always
hamisi_wa_instarHongera sana @zarithebosslady umefanya maamuzi sahihi kabisa
selestina.makwega84😪😪😪Maamuzi magumu sana, MUNGU akutie nguvu.
karen.kamauyu r strong woman ever known.Love love love salute…
chivixhbMungu atakuongoza zaidi.mwache awe anavyotaka yy.
evelynnyamigishaI love your confidence and the fact that you don’t compromise with any piece of nonsense.. Go on boss lady, this life is too short to waste time on people who don’t know what they want @zarithebosslady
minacollection_znzNice strong women my dear wowow 😍❤️ww nimwanamke unaye jiamini kila siku hivo ndo anavo takiwa mwanamke @zarithebosslady
Hata hivyo sio mashabiki wote wamempongeza Zari wapo baadhi yao wamemkosoa kwa maamuzi hayo kwa kumwambia kuwa amekurupuka na amefanya maamuzi kwa hasira.

Jana Februari 14, 2018 usiku Zari kupitia ukurasa wake wa Instagram alitangaza kuwa hayupo tena kwenye mahusiano na msanii wa Bongo Fleva, Diamond Platnumz ambaye amezaa naye watoto wawili.

Hussein Bashe Alaani Tukio la Ukatili Aliyefanyiwa Kiongozi wa Chadema

$
0
0
 Hussein Bashe Alaani Tukio la Ukatili Aliyefanyiwa Kiongozi wa Chadema
Mbunge wa Nzega (CCM), Hussein Bashe ameungana na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) katika kulaani tukio la kikatili lililomtokea Katibu wa CHADEMA Kata ya Hananasif, Daniel John siku za hivi karibuni.


Bashe ametoa kauli hiyo katika jukwaa la CCM wakati akimuombea ridhaa mgombea wao Maulid Mtulia ili aweze kuwa muwakilishi wa Jimbo la Kinondoni katika siku zijazo endapo atapata kura nyingi za ndio siku ya kupiga kura ambapo mpaka sasa zimebakia takribani siku mbili.

"Naviomba vyombo vya ulinzi na usalama, vifanye kila jitihada kufanya uchunguzi wa kina ili aliyefanya uhalifu huu aweze kupatikana. Kumekuwa na tabia kila uchaguzi mdogo unapofanyika matendo ya kihalifu hufanyika halafu wenzetu wa upande wa pili huamishia kesi katika Chama Cha Mapinduzi (CCM)", amesema Bashe.

Pamoja na hayo, Bashe ameendelea kwa kusema "jambo hili lililotokea Jimbo la Kinondoni ni kulaaniwa, sisi tunalilaani na nyie wananchi wa Kinondoni muendelee kulilaani lakini tuombe ufanyike uchunguzi na anayehusika apelekwe kwenye vyombo vya dola, ashtakiwe na watanzania tuambiwe ni nani anayehusika na tukio hili".

Kwa upande mwingine, Kamanda wa Polisi Kinondoni Murilo Jumanne Murilo (jana) amesema Jeshi lake litachunguza kifo cha Kiongozi wa CHADEMA kata ya Hananasif, ambaye mwili wake uliokotwa ukiwa na majeraha kwa kufuata misingi ya kazi yao na siyo kusukumwa na hisia za mtu binafsi.

Rais Magufuli Amuapisha Mnadhimu Mkuu wa Jeshi la JWTZ

$
0
0
Rais Magufuli Amuapisha Mnadhimu Mkuu wa Jeshi la JWTZ
Rais John Magufuli amemuapisha Mnadhimu Mkuu wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ), Luteni Jenerali Yakubu Hassan Mohamed.

Luteni Jenerali Mohamed ameteuliwa jana Februari 14, 2018 kuwa Mnadhimu Mkuu wa JWTZ na kupandishwa cheo kutoka Meja Jenerali na kuwa Luteni Jenerali.

Luteni Jenerali Mohamed anachukua nafasi ya Luteni Jenerali, James Mwakibolwa ambaye amestaafu.

Mbali na uteuzi huo, Rais Magufuli pia amewapandisha vyeo kutoka Brigedia Jenerali na kuwa Meja Jenerali J.G. Kingu, M.S. Busungu, R.R. Mrangira, B.K. Masanja, G.T. Msongole, A.F. Kapinga, K.P. Njelekela, A.S. Bahati, M.E. Mkingule na S.S. Makona.

Taarifa ilitotolewa Ikulu jana imesema mabrigedia jenerali wote waliopandishwa vyeo watapangiwa vituo vya kazi baadaye.

Kabla ya kuapishwa kwa Luteni Jenerali Mohamed, Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi (CDF), Jenerali Venance Mabeyo aliwavalisha vyeo mameja jenerali waliopandishwa vyeo na Rais Magufuli.



Video: Hamonize Kiboko Atuma Ujumbe Huu Baada ya Zari Kumbwaga Diamond

$
0
0
Video: Hamonize Kiboko Atuma Ujumbe Huu Baada ya Zari Kumbwaga Diamond
February 14, 2018 mitandao ya kijamii ilichangamka sana baada ya post ya mzazi mwenza na Diamond Platnumz, Zari the Boss Lady kupost ua na ujumbe mzito wa kuachana na Diamond kitu ambacho baadae Harmonize amekuja kupost video fupi ya utani kuhusu hilo.

Harmonize amepost video hiyo inayomuonesha akiwa kwenye chumba cha kulala na mwanamke huku akiimba wimbo wa kuachwa na kisha kwenda kwenye ua huku akiliambia lile ua lisije kubadilika likawa jeusi, hata hivyo zari alipost ua lililobadilika rangi kutoka jekundu na kuwa jeusi.


Viewing all 104756 articles
Browse latest View live




Latest Images