Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104667 articles
Browse latest View live

Yanga Yawatoa Hofu Mashabiki Wake "Tutashinda Hata Bila ya Kuwa na Chirwa"

$
0
0
Kocha wa Yanga Awatoa Hofu Mashabiki Wake "Tutashinda Hata Bila ya Kuwa na Chirwa"
KIKOSI cha Yanga, kimeondoka jana asub­uhi kwenda Shelisheli kwa ajili ya mechi yake ya marudiano ya Ligi ya Mab­ingwa Afrika dhidi ya St Louis.

Hata hivyo, Yanga im­eondoka nchini bila kuwa na mshambuliaji wake wa kutumainiwa, Mzam­bia, Obrey Chirwa, kwa kile kilichodaiwa kuwa ni majeruhi. Inadaiwa ana maumivu ya misuli.

Hata hivyo, Kocha Msaidizi wa Yanga, Shadrack Nsajigwa, ame­watoa hofu wapenzi na mashabiki wa timu hiyo kuwa, watashinda mechi hiyo hata bila ya kuwa na Chirwa.

Akizungumza na Championi Jumatatu, Nsa­jigwa alisema kuwa wameji­panga kuhakikisha wanafanya vizuri katika mechi hiyo kwa hiyo anaamini kwa wachezaji walioondoka nao, wataiongoza timu hiyo kupata ushindi.

“Watu wengi walishitushwa na taarifa za Chirwa kutoku­wepo katika mechi yetu ya marudiano na St Louis, la­kini wanapaswa kujua kuwa mchezaji huyo siyo pekee ambaye hucheza uwanjani.



“Kwa hiyo, kuna mchezaji ambaye tumemwandaa ili kuziba nafasi hiyo na tunaamini atafanya vizuri, niwaombe tu wapenzi na mashabiki wetu kutokuwa na hofu na hilo, tutafanya vizuri,” alisema Nsajigwa.

Katika msafara wake huo, Yanga pia imewaacha Amissi Tambwe, Yohana Nko­mola, Donald Ngoma, Abdallah Shaibu ‘Ninja’ na Thabani Kamusoko ambao ni majeruhi.

Mtumishi wa TRA Hassan Abuutwalib Ashikiliwa na Polisi kwa Tuhuma za Kulawiti Mtoto wa Miaka 13

$
0
0
Mtumishi wa TRA Hassan Abuutwalib Ashikiliwa na Polisi kwa Tuhuma za Kulawiti Mtoto wa Miaka 13
Mtumishi wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Hassan Abuutwalib maarufu Kiringo anashikiliwa na Jeshi la Polisi kwa tuhuma za kumlawiti mtoto wa kiume mwenye umri wa miaka 13.


Akithibitisha kutokea kwa tukio hilo, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mjini Magharib Unguja, Hassan Nassir Ali amesema wamemkamata jana (Jumatatu) katika maeneo ya uwanja wa ndege Zanzibar alipokuwa akijaribu kuondoka kuelekea Mwanza.

"Mlalamikaje ambaye mwenye miaka 54 jina lake nalihifadhi alikuja kutoa malalamiko kuwa mtoto wake alichukuliwa na Kiringi na kumpeleka katika nyumba iliyokuwa haijamalizwa kujengwa huko Fuoni uwandani ambapo inadaiwa alifanikiwa kumlawiti baada ya kumpa dawa za kupoteza fahamu na kumsababishia maumivu sehemu zake za siri za nyuma", amesema Kamanda Nassir.

Aidha, Kamanda Nassir amesema uchunguzi wa madaktari ulithibitisha kuathirika sehemu za siri za nyuma za mtoto huyo

Kwa upande mwingine, Kamanda Nassir amesema ameunda timu ya uchunguzi iliyojumuisha wakuu wa upelelezi wa wilaya tatu wilaya ya mjini, wilaya ya Magharibi A na B ili wakachunguze ukweli wa tukio zima lilotokea.

Acacia Yaanza Kusaka Wawekezaji Kwaajili ya Kuingia Kwenye Miradi Yake

$
0
0
Acacia Yaanza Kusaka Wawekezaji Kwaajili ya Kuingia Kwenye Miradi Yake
Kampuni ya uchimbaji madini ya Acacia imeanza mazungumzo na wawekezaji mbalimbali kwa ajili ya kuingia ubia kwenye miradi yake. Acacia ambayo inamiliki migodi ya Buzwagi, Bulyanhulu na North Mara ilisema kwenye taarifa yake jana kuwa, mazungumzo hayo ni ya awali na si rasmi.

Taarifa ya kampuni hiyo imetolewa baada ya vyombo vya habari vya kimataifa kuripoti kuwa inafanya mazungumzo na mwekezaji kutoka China kwa ajili ya kuingia ubia wa kibiashara.

Pia, kumekuwepo na tetesi kuwa wawekezaji hao wa China wameanza kutembelea migodi inayomilikiwa na kampuni hiyo kwa ajili ya kutathmini kabla la kuingia ubia.

Kwa mujibu wa ufafanuzi huo Acacia imekubali kuwepo kwa wawekezaji hao lakini wapo katika hatua za awali na hakuna uhakika kama makubaliano yatafikiwa.

Akizungumza kuhusu ubia huo, Katibu Mkuu wa Wizara ya Madini, Profesa Simon Msanjila alisema Acacia wapo huru kuuza kampuni yao au vitega uchumi vyao kwa kufuata sheria.



   

Mtoto wa Drogba Afuata Nyayo za Babaake Apata Shavu Ligi Kuu ya Ufaransa

$
0
0
Mtoto wa Drogba Afuata Nyayo za Babaake Apata Shavu Ligi Kuu ya Ufaransa
Klabu ya soka ya En Avant de Guingamp ambayo inashiriki ligi kuu ya Ufaransa, imetangaza kumsajili mchezaji Isaac Drogba (17) amabye ni mtoto wa mchezaji wa zamani wa Chelsea Didier Drogba.

Kupitia mtandao wa Instagram, Drogba ameonyesha kufurahishwa na hatua hiyo kubwa aliyopiga mwanae kwa kuandika, “Couldn’t be more proud of you @isaacdrogba11 @eaguingamp Fiers de toi @isaacdrogba11 @eaguingamp.”



Frank Lampard ambaye amewahi kucheza na Drogba katika timu ya Chelsea, kupitia mtandao huo ame-comment kwa kuandika, “Congratulations! I remember Isaac as the small polite boy! Now a man!.”

Naye John Terry hakutaka hilo limpite akaamua ku-comment kwa kuandika, “Can’t believe how big he is mate, congratulations.”

Billnass Afunguka Kuhusu Muziki Wake "Sijashuka Kisanaa Kama Watu Wanavyodai"

$
0
0
Billnass Afunguka Kuhusu Muziki Wake "Sijashuka Kisanaa Kama Watu Wanavyodai"
Rapa Billnass ambaye anatamba na ngoma ya 'Sina Jambo' amesema kupotea kwake katika 'game' ya muziki hakumaanishi kwamba ameshuka kisanaa kama watu wanavyodai kwa kuwa hajatoa ngoma yoyote kwa sasa ambayo ikashindwa kufanya vizuri.

Billnass amebainisha hayo kupitia eNewz ya EATV baada ya kuwepo kwa tetesi kuwa ukimya wake umesababishwa na kuondoka kwa Petty Man katika 'label' ya LFLG na kumfanya msanii huyo kushindwa kujisimamia mwenyewe kazi zake.

“Huwezi kuzungumzia kushuka au kupanda kwa sababu bado sijatoa wimbo na 'fan base' yangu ni ile ile angalau ningekuwa nimetoa nyimbo zinakataa. Watu wanatoa nyimbo hata saba, nane, tisa zinakataa mimi sijatoa hata wimbo mmoja ukakataa kwa hiyo bado naamini 'material' ambayo ninayo ni mengi”, amesema Billnas

Ndalichako Afanya Ziara Chuo cha Kampala Abaini Kuwepo kwa Walimu Wanaoishi Bila Vibali

$
0
0
Ndalichako Afanya Ziara Chuo cha Kampala Abaini Kuwepo kwa Walimu Wanaoishi Bila Vibali
Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Profesa Joyce Ndalichako amefanya ziara Chuo Kikuu cha Kimataifa cha Kampala (KIU), kubaini baadhi ya walimu kuishi nchini bila vibali.

Katika ziara hiyo iliyofanyika leo Februari 20, 2018 Profesa Ndalichako ameambatana na Kamishna Jenerali wa Uhamiaji, Anna Makakala, mkuu wa Ithibati na Udhibiti Ubora wa Vyuo, Dk Valerian Damian na maofisa mbalimbali kutoka idara ya uhamiaji na Tume ya Vyuo Vikuu Tanzania (TCU).

Profesa Ndalichako amekumbana na changamoto mbalimbali, ikiwamo walimu wa chuo hicho kuajiriwa sehemu zaidi ya moja na kuishi nchini bila vibali.

"Wapo walioingia nchini kama wanafunzi lakini baada ya muda wakaajiriwa kama wafanyakazi, hii kwa sheria za nchi haikubaliki,” amesema Profesa Ndalichako.

Wanafunzi wa Kiume Wapaza Sauti Nao Wahitaji Ulinzi

$
0
0
Wanafunzi wa Kiume Wapaza Sauti NaoWahitaji Kulindwa
Kama utasikia ulinzi wa mtoto unazungumzwa na kupigiwa kelele kwa nguvu zote, kipaumbele huwa kwa mtoto wa kike na sio wa kiume.

Jamii inawatazama watoto wa kiume kama watu wasioonewa, wenye nguvu na uwezo wa kukabiliana na mambo magumu na wakati mwingine na huonekana hawapo kwenye mazingira hatarishi.

Mtoto wa kike anaangaliwa zaidi kwa sababu ya maumbile yake, hivyo wakati yeye anapewa vipaumbele vingi, mtoto wa kiume anasahaulika.

Wadau wa elimu wakiwamo walimu wanasema hali ni mbaya hata kwa watoto wa kiume.

Walimu waliohudhuria katika kampeni ya ‘Tumkumbuke na Mtoto wa Kiume’ inayoongozwa na Dahuu Foundation, iliyofanyika katika viwanja vya shule ya Msingi, Muhimbili jijini Dar es Salaam walivunja ukimya wakisema; ‘ hata watoto wa kiume wanahitaji kulindwa’.

Wanasema yapo matukio mengi ya watoto wa kiume kufanyiwa ukatili wa kijinsia ikiwamo kulawitiwa, huku jamii ikiwapa kisogo kwa kutowasikiliza.

Mwalimu wa shule ya msingi Mivinjeni, Manispaa ya Ilala Kiemena Athumani anasema wazazi wengi wamejisahau kwa kumhofia zaidi mtoto wa kike wakiamini wa kiume yupo salama.

“Ninayo mifano dhahiri ya watoto kufanyiwa ukatili huu, matukio haya yapo kwa kweli na ukatili huu unafanywa na ndugu wa karibu huko majumbani kama wajomba, kaka hata majirani,” anasema na kuongeza;

“Niliwahi kutana na kesi ya baba mdogo kumfanyia ukatili mtoto wa kaka yake, wazazi kuwalaza watoto wa kiume na wakubwa wakiamini ni salama ni hatari sana, sio salama kabisa,”

Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Muhimbili, Jovitha Mushi anasema matukio mengi yanawakuta watoto wa kiume bila kujua kwa sababu jamii imejikita zaidi kumkumbatia mtoto wa kike.

“Tumeshindwa kukimbia na mtoto wa kiume kama tunavyokimbia na watoto wa kike, hii ni hatari na uwepo wa kampeni hii utawakumbusha wazazi wajibu wao,”alisema.

Kaimu Ofisa Elimu wa Wilaya ya Ilala, Rehema Msologonhe anakiri kuwapo kwa ukatili mkubwa kwa watoto wa kiume kama ilivyo kwa watoto wa kike, japo wamesahaulika.

Anasema kuna hatari ya kuwapoteza kina baba bora na kuwa na wanaume wasio na nguvu za kiume siku za usoni, kama hali iliyopo itakaliwa kimya.

“Tunahitaji baba asimame kwenye nafasi yake kama baba, sasa tusipowasaidia watoto wetu itakuwaje? Ni kweli watoto wa kiume wanafanyiwa ukatili na wamesahaulika, ” anasema Msologonhe.

Mwanaharakati wa Haki za Binadamu, Efero Kusala anasema wakati mwingine mtoto wa kiume anaweza kuchelewa nyumbani wazazi wasihoji wala kutaka kutafiti alikokuwa wakiamini ni salama.

“Kumbe wakati anarudi amekutana na mtu aliyemfanyia jambo baya lakini amemkanya asiseme, kwa hiyo mtoto anaishia kuwa mnyonge mwisho, anaharibika,”anasema.

Anasema vile anavyolindwa mtoto wa kiume, hata wa kike anapaswa kulindwa vivyo hivyo, ili kuleta usawa wa kijinsia na kuwasaidia watimize ndoto zao za kielimu.

Simulizi ya watoto

“Sijawahi kufanyiwa chochote ila rafiki yangu alikuwa anapigwa na mjomba wake. Kila siku akija shuleni anashindwa kutembea ila alishaacha shule,”anasimulia mmoja wa wanafunzi waliokuwa kwenye maadhimisho hayo.

Mwanafunzi mwingine anasema aliwahi kukutana na ukatili siku moja kutoka kwa mgeni waliyemkaribisha nyumbani kwao.

“Mgeni alikuja nyumbani nikalala naye, siku moja lakini usiku alianza kuniumiza, nilimwambia mama akamfukuza,” anasema mwanafunzi huyo.

Miaka miwili iliyopita, mtoto wa kiume mwenye umri wa miaka 11, mkazi wa Buguruni Madenge jijini Dar es salaam jijini Dar es salaam alidaiwa kufanyiwa vitendo vya ulawiti na dereva wa bodaboada katika kituo cha Buguruni Sheli ambae alidaiwa kutoweka na kwenda mahali kusikojulikana mara baada ya tukio hilo kufanyika.

Mtaalamu wa masuala ya kuzuia maambukizi ya Virusi vya Ukimwi kutoka kwa mama kwenda kwa mtoto kutoka Shirika la Afya Duniani (Unicef), Hafsa Khalfani, anakiri kuwa Tanzania ni kati ya nchi zenye matukio ya unyanyasaji kwa watoto wote.

Takwimu za Unicef zinaonyesha asilimia 72 ya watoto wa kiume na 74 ya watoto wa kike, wamefanyiwa ukatili ikiwamo kipigo.

Takwimu hizo pia zinaonyesha asilimia 25 ya watoto wa kiume na kike wameshafanyiwa ukatili wa kisaikolojia.

Hafsa anasema uchunguzi wao unaonyesha pia watoto wa kwanza na wa mwisho kupanda magari ya wanafunzi wapo hatarini kufanyiwa ukatili wa kingono na wahudumu wa magari hayo.

“Kwa hiyo wazazi wawe tu makini kuwalinda watoto wote,“anasema.

Nini kifanyike?

Mkurugenzi wa Dahuu Foundation, Husna Abdul anasema wameanzisha kampeni ya kumkumbuka mtoto wa kiume baada ya kufanya tafiti shuleni na kugundua hali ni mbaya.

Husna aliyeamua kuanzisha harakati za kuwatetea watoto wakiume, anasema utafiti wake umeonyesha wengi wanafanyiwa vitendo hivyo na ndugu zao wa karibu.

“Watoto wengi wanafanyiwa ukatili na wazazi wao hawajui chochote kwa sababu hofu yao kubwa wameiweka kwa watoto wa kike peke yao, hii ni hatari,”anasema na kuongeza:

“Tulichogundua watoto wa kiume hawasikilizwi kabisa na chanzo cha ukatili huu kwa watoto ni sisi wazazi. Sasa tuvunje ukimya huu, tuwape nafasi tuwalinde pia na kuwasikiliza kama kweli baadaye tunahitaji baba bora.’’

Ofisa Programu wa idara ya utafiti na uchambuzi wa sera-HakiElimu, Florige Lyelu anasema njia pekee ya kupambana na hali hiyo kwa wanafunzi wa kiume ni wazazi na walezi kuwalinda bila ubaguzi kwa kuona wao hawapo hatarini.

“Kwa kweli kesi zipo nyingi tu hata mimi hilo nalitambua, kikubwa ni uangalizi wa karibu kwa watoto wetu. Wazazi na walezi waongee na watoto wao bila ubaguzi na kuhakikisha wanajua kila hatua ya makuzi yao,” anaeleza.

Kauli ya Serikali

Mkuu wa Wilaya ya Ilala Sophia Mjema anatoa wito kwa wahusika ikiwamo madawati ya jinsia kutowafumbia macho watuhumiwa wa kesi za ulawiti na ubakaji watoto.

Anasema dawa yao ni kuwachukulia hatua za kisheria ikiwamo kuwafikisha mahakamani.

“Watoto wazuri msikubali kabisa, hata kama mtu akisema atawapa pipi kataeni na mkaseme kwa wazazi au walimu au mtu yeyote awasaidie. Msikubali hata kidogo sawa ee!”anasema Mjema wakati akizungumza na watoto wa kiume wa shule ya msingi Muhimbili na kuongeza;

“Inaumiza jamani, hawa watu wakikamatwa wafungwe kabisa wakaishie huko huko jela wasionekane kabisa kwenye jamii yetu, hii ni hatari mno.”

Vigogo Saba Chadema Kuitikia Wito Sasa Kuelekea Polisi

$
0
0
Vigogo Saba Chadema Kuitikia Wito Sasa Kuelekea Polisi
Baadhi ya viongozi saba wa Chadema  wanaelekea Kituo Kikuu cha Polisi kuitikia wito wa kamanda wa polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Lazaro Mambosasa.

Akizungumza na MCL Digital leo Februari 20, 2018 mkurugenzi wa itifaki, mawasiliano na mambo ya nje wa Chadema, John Mrema amesema viongozi hao wanajiandaa muda huu kuelekea kituoni.

Viongozi walioitwa na Mambosasa ni mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe, katibu mkuu wa chama hicho, Dk Vincent Mashinji, manaibu katibu wakuu (bara), John Mnyika na Salum Mwalimu (Zanzibar).

Pia wamo, mwenyekiti wa Baraza la Wanawake Chadema (Bawacha), Halima Mdee; mwenyekiti wa Kanda ya Serengeti, John Heche na Ester Matiko ambaye ni mweka hazina wa Bawacha.

Jana, Mambosasa aliieleza MCL Digital kuwa viongozi hao ni watuhumiwa na kama wameitwa polisi ni fadhila tu, ila kwa yaliyotokea wanapaswa kukamatwa.

Wito wa viongozi hao polisi umekuja siku siku nne tangu kutokea kwa kifo cha Akwilina Akwiline, mwanafunzi wa mwaka wa kwanza wa Chuo cha Taifa cha Usfairishaji (NIT).

Akwilina aliuawa kwa kupigwa risasi akiwa ndani ya daladala eneo la Mkwajuni, Kinondoni jijini Dar es Salaam wakati polisi wakiwatawanya wafuasi wa Chadema waliokuwa wakienda ofisi za mkurugenzi wa Halmashauri ya Kinondoni kudai viapo vya mawakala wao.

Hatimaye Familia ya Akwilina Anayedaiwa Kuuwawa na Polisi Imekabidhi Serikali Bajeti ya Maziko..... Ni Zaidi ya Milioni 80

$
0
0
Hatimaye Familia ya Akwilina Imekabidhi Serikali Bajeti ya Maziko..... Ni Zaidi ya Milioni 80
Familia ya mwanafunzi wa kwanza katika Chuo cha Taifa cha Usafirishaji (NIT), anayedaiwa kuuawa na polisi wiki iliyopita, Aquilina Akwilini imekabidhi serikali bajeti ya maziko ya zaidi ya Sh milioni 80.
Msemaji wa Familia, Festo Kavishe amekabidhi bajeti hiyo leo Jumanne Februari 20, kwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Dk. Leonard Akwipalo na Mkuu wa Wilaya ya Ubungo, Kisali Makori leo. "Hayo ndiyo makubaliano ya familia, tumewakabidhi wataenda na kujadiliana kisha tutakutana nao saa 10 jioni leo, kisha watatueleza ya kwao pia, tunachohitaji ndugu yetu apumzike kwa amani," amesema Kavishe.

Marehemu Aquilina ambaye aliuawa kwa risasi Ijumaa iliyopita akiwa katika basi baada ya polisi kuwatawanya wafuasi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), waliokuwa wakiandamana kwenda kwa Mkurugenzi wa Uchaguzi Wilaya ya Kinondoni kudai viapo vya mawakala wao, anatarajiwa kuagwa Alhamisi wiki hii katika viwanja vya NIT na kusafirishwa Rombo mkoani Kilimanjaro, Ijumaa.

TRA: Kakobe Anaifadhi Mabilioni ya Fedha Katika Majaba, Ndoo

$
0
0
TRA: Kakobe Anaifadhi Mabilioni ya Fedha Katika Majaba, Ndoo
Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) imebaini mambo matano baada ya kumchunguza Askofu Mkuu wa Kanisa la Full Gospel Bible Followship (FGBF), Zachary Kakobe, ikiwemo kukwepa kodi na kuhifadhi mabilioni ya fedha katika majaba na ndoo.

Taarifa iliyotolewa leo Februari 20 na Kamishna Mkuu wa mamlaka hiyo, Charles Kichere pia imesema Kakobe alimuandikia barua  Rais John Magufuli kutokana na matamshi yake kwamba ana fedha nyingi kuliko Serikali, kumuomba radhi.

Mambo yaliyobainika baada ya kufanyika kwa uchunguzi huo

1. Imesema Askofu huyo hana akaunti wala fedha katika taasisi ya fedha hapa nchini. Aidha uchunguzi ulibaini kuwa Askofu Kakobe ni mmoja wa wasimamizi wakuu wa akaunti za kanisa zilizopo katika benki ya NBC zenye jumla ya kiasi cha Sh8.2bilioni, kiasi hiki cha fedha kimetokana na sadaka, zaka na changizo ambazo zinatolewa na waumini wa kanisa tajwa hapo juu, hivyo kwa mujibu wa sheria hakitozwi kodi.

2. Kanisa lilikwepa kulipa kodi kiasi cha Sh20.8milioni.

3. Kampuni inayomilikiwa na watoto wa Askofu Kakobe ilikwepa kulipa kodi ya Sh37.2 ambazo zimelipwa baada ya uchunguzi. Kwa ujumla kiasi kilicholipwa kutokana na uchunguzi ni Sh58.1milioni.

4. Kanisa linatunza kiasi kikubwa cha fedha kwenda ndoo na ‘majaba’ kinyume na taratibu za utunzaji fedha.

5. Kanisa halitengenezi hesabu za mapato na matumizi ya fedha kitu ambacho ni kinyume na katiba ya kanisa na sheria ya usimamizi wa fedha ambayo imepelekea matumizi mabaya ya fedha za waumini kama vile safari za nje ya nchi ambazo zimedhaminiwa na kanisa lakini wanaosafiri ni Askofu na familia yake.

Mbunge Zanzibar Kuwachongea TFF kwa FIFA

$
0
0
Mbunge Zanzibar Kuwachongea TFF kwa FIFA
Siku moja kabla ya ujio wa ujumbe wa Fifa nchini Mbunge Malindi Zanzibar wa Chama cha Wananchi (CUF), Ally Saleh amesema anataka kukutana na Rais wa Fifa, Gianni Infantino ili kumueleza namna soka la Zanzibar limekuwa likibanwa na Shirikisho la Soka Tanzania Bara (TFF).

Akizungumza jijini Dar es Salaam jana Saleh alisema TFF imekuwa ikiangalia soka la Bara na kutoangalia soka la visiwani lenye programu nzuri za vijana.

"Zanzibar tuna programu nzuri za vijana, hata kufanya vizuri kwa timu yetu ya Taifa ni vijana ambao wamekuwa wanafanya vizuri katika ligi za vijana zinazoendelea," alisema.

Saleh aliongeza, TFF wamekuwa hawatetei kurejeshwa kwa uanachama wa Zanzibar, baada ya kufutwa uanachama licha ya kwamba awali shikilisho hilo ndio walisaidia kupatikana kwa uanachama awali wa CAF.

"Tumefutiwa uanachama, lakini wenzetu wamefumbia macho, tunataka tuandike barua ya wazi kwa rais wa Fifa ili wajue kama Wazanzibar hatujakubaliana nalo," alisema kiongozi huyo.

Ujumbe wa Fifa umeanza kuingia nchini leo tayari kwa mkutano wao wa kupanga ajenda za mkutano mkuu utakaofanyika Russia wakati wa Kombe la Dunia.

Katibu Mkuu wa TFF, Wilfred Kidau amezitaja ajenda kuu tatu za mkutano wa Fifa utakaofanyika Dar es Salaam ni kuhusu soka la vijana, kufuata mpangilio ya Fifa, pamoja na changamoto za klabu hasa katika upande wa leseni.

Mapema jana Waziri wa Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo, Dk Harrison Mwakyembe alisema mkutano huo utakuwa na watu sabini na wajumbe wataanza kuwasili nchini kesho (leo), huku rais wa Fifa atawasili siku moja kabla ya mkutano.

"Tunategemea kupokea watu takribani sabini katika kikao hicho, kuanzia kesho ndio wajumbe wataanza kuingia nchini, nitamchukua rais wa fifa na kumpeleka ikulu kuzungumza na rais John Magufuli kisha ndio ataenda katika kikao hicho ambacho hata mimi siruhusiwi kuingia," alisema Mwakyembe.

Familia ya Akwilina Yatoa Onyo kwa Wanaochangisha Fedha za Msiba Mitandaoni

$
0
0
Familia ya Akwilina Yatoa Onyo kwa Wanaochangisha Fedha za Msiba Mitandaoni

Familia ya mwanafunzi wa Chuo cha Taifa cha Usafirishaji (NIT), Akwilina Akwiline aliyeuawa kwa kupigwa risasi Februari 16, 2018  imewaonya watu wanaochangisha fedha za msiba wa mwanafunzi huyo mitandaoni.

Imesema inawafuatilia wanaofanya hivyo kutokana na kuibuka kwa tetesi kuwa michango hiyo inachangishwa kinyume na utaratibu kupitia mitandao mbalimbali.

Msemaji wa familia, Festo Kavishe leo Februari 20, 2018 amewaalika ndugu jamaa na marafiki kufika Moshi Hoteli saa 11 jioni kwa ajili ya michango ya msiba.

"Hatutaki wananchi wapitishe michango yao kwa njia ya simu kwa sababu matapeli wapo wengi sasa hivi, ukipata meseji ya kuombwa mchango fikisha nyumbani,” amesema Kavishe.

"Hata taasisi mbali mbali zinakuja kwa ajili ya kutupa pole  inasaidia katika msiba huu. Njia rahisi ya kuchangia msiba huo ni kufika nyumbani kwa dada yake Akwilina kufikisha mchango wako na sio kwa njia ya simu."

Viongozi Chadema Wawasili Kituoo Kikuu cha Polisi, Waachiwa kwa Dhamana

$
0
0
Viongozi Chadema Wawasili Kituoo Kikuu cha Polisi

Viongozi watano wa Chadema kati ya saba waliokwenda Kituo Kikuu cha Polisi kuitikia wito wa kamanda  wa polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Lazaro Mambosasa, wameachiwa kwa dhamana. 

Walifika kituoni hapo leo Februari 20, 2018 saa 6: 10 mchana na kuachiwa saa 7:45 mchana.

Viongozi walioitwa na Mambosasa ni mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe, katibu mkuu wa chama hicho, Dk Vincent Mashinji, manaibu katibu wakuu (bara), John Mnyika na Salum Mwalimu (Zanzibar).

Pia wamo, mwenyekiti wa Baraza la Wanawake Chadema (Bawacha), Halima Mdee; mwenyekiti wa Kanda ya Serengeti, John Heche na Ester Matiko ambaye ni mweka hazina wa Bawacha.

Jana, Mambosasa aliieleza MCL Digital kuwa viongozi hao ni watuhumiwa na kama wameitwa polisi ni fadhila tu, ila kwa yaliyotokea wanapaswa kukamatwa.

Waliofika kituoni hapo ni Bulaya, Mdee, Matiko, Heche na  Mnyika

Wito wa viongozi hao polisi umekuja siku siku nne tangu kutokea kwa kifo cha Akwilina Akwiline, mwanafunzi wa mwaka wa kwanza wa Chuo cha Taifa cha Usfairishaji (NIT).

Akwilina aliuawa kwa kupigwa risasi akiwa ndani ya daladala eneo la Mkwajuni, Kinondoni jijini Dar es Salaam wakati polisi wakiwatawanya wafuasi wa Chadema waliokuwa wakienda ofisi za mkurugenzi wa Halmashauri ya Kinondoni kudai viapo vya mawakala wao.

Simba Yajipanga Kuwang'oa Gendarmarie Leo

$
0
0
Simba Yajipanga Kuwang'oa Gendarmarie Leo
Timu ya Simba imeweka hadharani mbinu itakayotumia kuwang’oa wapinzani wao Gendarmarie katika mchezo wa leo saa 10: 00 jioni nchini Djibouti.

Simba na Gendarmarie zinatarajiwa kupepetana katika mchezo wa Kombe la Shirikisho Afrika. Mchezo wa kwanza uliochezwa Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam wekundu wa msimbazi walishinda mabao 4-0.

Akizungumza mjini hapa jana, kocha msaidizi wa Simba Masoud Djuma alisema mbinu wanayotarajia kutumia ni kusoma mchezo huku wakicheza kwa kujilinda kabla ya kufunguka na kuanza kushambulia kwa nguvu.

Djuma alisema dakika za mwanzo watacheza kwa kuangalia kasi ya wapinzani wao kabla ya kujipanga na kuanza kusukuma mashambulizi langoni mwao.

"Tutawaacha wacheze kwa kuangalia wana mbinu gani wanatumia, tukishawasoma baada ya hapo tutafungua na kuwashambulia.

"Tunaongoza mabao manne kikubwa ni kulinda na kuongeza mengine kwasababu kila kitu kinakwenda vizuri ninachokiamini, tutafanya vizuri katika mchezo huo,”alisema Djuma raia wa Burundi.

Simba inapewa nafasi ya kusonga mbele katika mchezo wa raundi ya kwanza kutokana na mtaji mzuri wa mabao na huenda ikavaana na Al Masry ya Misri.

Marubani wa Kenya Waliotekwa na Waasi wa Sudani Kusini Waachiwa

$
0
0
Marubani wa Kenya Waliotekwa na Waasi wa Sudani Kusini Waachiwa
Waasi wa Sudani kusini wamewaachia marubani wawili wa Kenya waliotekwa zaidi ya mwezi mmoja uliopita baada ya ndege yao kupata ajali.

Msemaji wa waasi alisema wakenya hao waliachiwa baada ya kampuni ya bima kulipa zaidi ya dola za marekani 100,000 kulipa fidia ya kifo cha mtu mmoja aliyepoteza maisha baada ya ndege kuanguka.

Baada ya kutekwa kwa zaidi ya mwezi mmoja, Kepteni Pius Frank Njoroge na msaidizi wa rubani Kennedy Shamalla wameripotiwa kuwasili salama mjini Juba.

Msemaji wa wizara ya mambo ya nje ameiambia BBC kuwa wawili hao watarejea Kenya baadae leo.

Waasi waliwashikilia watu hao ndege yao ilipoanguka katika mji wa Upper Nile na kuripotiwa kumuua mwanamke mmoja na mifugo.

Awali waasi walitaka zaidi ya dola 200,000 lakini walifikia makubaliano baada ya majadiliano na maafisa wa Kenya.

Msemaji wa waasi amesisitiza kuwa malipo hayo sio kikombozi bali ni fidia baada ya ajali hiyo kusababisha vifo.

Waandamanaji Waweka Kambi Nje ya Ikulu ya Marekani Wakishinikiza Kubadilishwa kwa Sheria ya Bunduki

$
0
0
Waandamanaji Waweka Kambi Nje ya Ikulu ya Marekani Wakishinikiza Kubadilishwa kwa Sheria ya Bunduki
Vijana wengi na familia zao Jumatatu waliwasilisha kwenye Ikulu ya White House hoja yao ya kutaka sheria kali ya kudhibiti silaha ikiwa ni chini ya wiki moja baada ya mtu mmoja mwenye bunduki kuwashambulia wanafunzi na kusababisha vifo vya watu 17 katika jimbo la Marekani la Florida.

Watu wapatao 50 waliandamana Washington DC wakiwa na mabango yaliyoandikwa “Imetosha” na “Badili sheria za bunduki au badili Congress”.

Mkusanyiko huo umekuja katikati ya harakati zinazoongezeka za kutoa wito kwa Rais Donald Trump na wabunge wengine kuimarisha sheria za umiliki wa bunduki za Marekani wiki moja baada ya kufanyika shambulio baya dhidi ya wanafunzi katika historia ya nchi.

Watu wapatao 17 waliuawa pale mtu mmoja aliyekuwa amejihami kwa bunduki alipofyatua risasi kuwashambulia wanafunzi na walimu katika Shule ya Sekondari ya Marjory Stoneman Douglas Jumatano iliyopita.

Katika maandamano hayo ya Washington, waandamanaji walikuwa wakisoma majina ya waliouawa katika shambulio hilo lililofanyika Marekani kwa mara ya kwanza tangu mwaka 1999.

"Wako hapa kwa sababu wanasema sasa inatosha wakati umefika kwamba watoto shuleni wanapaswa kulindwa na ikiwa hiyo itamaanisha kubadilisha sheria za umiliki wa bunduki, basi hicho ndicho kinapaswa kutokea," alisema Fisher.

Trump pamoja na maofisa wengine wako chini ya shinikizo la kuacha ushirikiano na Chama cha Taifa cha Bunduki (NRA), kikundi chenye nguvu cha kushawishi umiliki wa bunduki ambacho kimelalamikiwa kuwa sababu ya wabunge wa Marekani kusita kupitisha sheria ya udhibiti silaha.

"NRA: Acha kuua watoto wetu!" lilisomeka moja ya mabango ya waandamanaji Jumatatu.

Japokuwa rais alituma salamu za rambirambi kwa ndugu wa wafiwa kutokana na shambulio la Florida, kwa kiasi kikubwa amejizuia kuzungumzia mabadiliko ya sheria ya umiliki wa bunduki.



Askofu Kakobe Amuangukia Rais Magufuli Amuandikia Barua ya Kumuomba Msamaha

$
0
0
Askofu Kakobe Amuandikia Barua Rais ya Kumuomba Msamaha

Kamishna Mkuu wa  Mamlaka ya Mapato (TRA) Bw. Charles Kichere amesema Askofu Kakobe aliandika barua kwa Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk. John Pombe Magufuli  na kuomba radhi kutokana na kauli yake ya kebehi pamoja na matamshi yake ya dharau kwamba ana pesa nyingi kuliko Serikali.

 Askofu Zachary Kakobe akiendesha ibada katika  Kanisa la Full Gospel Bible Fellowship katika mahubiri aliyotoa kwenye  Ibada hiyo  akisema  “Yeye ana pesa kuliko Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania”,

Kamishna Kichere ameongeza kwamba kufuatia Matamshi hayo  Mamlaka ya Mapato TRA iliamua kufanya uchunguzi kufuatia kauli yake  hiyo aliyoitoa  ,mnamo tarehe 24.01.2018 ili kujiridhisha kama mapato yake yanalipiwa kodi.

Baada ya Uchunguzi huo Mamlaka ya mapato TRA imebaini  mambo kadhaa kutokana na   kufanyika kwa uchunguzi huo kufuatia kauli   ya Askofu Zachary Kakobe;

Kamishna Kichere amesema uchunguzi umegundua Askofu Zachary Kakobe hana akaunti wala fedha katika taasisi yoyote ya fedha hapa nchini.

Aidha uchunguzi ulibaini kuwa Askofu Kakobe ni mmoja wa wasimamizi wakuu wa akaunti za kanisa (Signatories) zilizopo katika benki ya NBC zenye jumla ya kiasi cha shilingi 8,132,100,819.00, kiasi hiki cha fedha kimetokana na sadaka, zaka na changizo ambazo zinatolewa na waumini wa kanisa tajwa hapo juu, hivyo kwa mujibu wa Sheria hakitozwi kodi.

Aidha imegundulika kuwa Kanisa lilikwepa kulipa kodi kiasi cha shilingi 20,834,843.00 ambazo zilitokana na uwekezaji katika makampuni ya kukuza mitaji.

Kodi hiyo imelipwa baada ya uchunguzi na kugundulika kwamba Kampuni inayomilikiwa na watoto wa Askofu Zachary Kakobe ilikwepa kulipa kodi kiasi cha shilingi 37,280,030.00 ambazo zimelipwa baada ya uchunguzi. Kwa ujumla, kiasi cha kodi kilicholipwa kutokana na uchunguzi huu ni shilingi 58,114,873.00.

 Kamishna Charles Kichere amesema Kanisa  hilo linatunza kiasi kikubwa cha fedha kwenye ndoo na ‘majaba’ kinyume na taratibu za utunzaji wa fedha, lakini pia uwekaji na utoaji wa fedha nyingi kutoka benki haushirikishi vyombo vya ulinzi na usalama kwa ajili ya usalama wa fedha zenyewe na wahusika.

Pia ilibainika kwamba Kanisa halitengenezi hesabu za Mapato na Matumizi ya Fedha kitu ambacho ni kinyume na Katiba ya Kanisa pamoja na sheria za usimamizi wafedha ambayo imepelekea matumizi mabaya ya fedha za waumini kama vile safari za nje ya nchi ambazo zimedhaminiwa na Kanisa lakini wanaosafiri ni Askofu na familia yake.

Vile vile fedha za Kanisa zinatumika kujenga nyumba ya mke wa Askofu, kwa jina lake na wala si kwa jina la Kanisa, kitu ambacho ni kinyume na taratibu za Kanisa.

Kamishna Kichere ametoa wito kwa Taasisi zote za dini ambazo zinajihusisha na shughuli zozote za kiuchumi kulipa kodi stahiki na kwa wakati kwa mujibu wa sheria, kanuni na taratibu za kodi.

Pia amezitaka Taasisi zote za kidini kufuata katiba zao ikiwa ni pamoja na kutengeneza hesabu za mapato na matumizi.

Miujiza ya Sharifu Seif Mohamed..JE Umeachwa na Mme/Mke au Mpenzi, Umesongwa na Mitihani ya Maisha..Piga Simu Upate Muujiza Wako

$
0
0


SHARIFU SEIF MOHAMED ANAWASHUKURU WALE WOTE WANAOENDELEA KUPIGA SIMU, WENYE MATATIZO NA WALE WANAOTOA  SHUKRANI NA SHUHUDA JINSI TIBA ZAKE ZINAVYO WASAIDIA,

(Rudisha mahusiano yako ndani ya masaa 72 tu)

SHARIFU MOHAMED Ni  mtaalam na mnajimu maarufu wa nyota na kubashiri mambo yanayo watesa binadamu duniani kote na kupata ufumbuzi, Anatumia kitabu cha QUR'AN na Nyota

Je Umeachwa na UMPENDAE awe Mme/Mke na bado unampenda? Je Umekimbiwa na Mmeo/ Mkeo n anaishi na mtu mwingine? Je Umejaribu sehemu nyingi bila mafanikio? Mpigie simu SHARIFU SEIF sasa hivi ujionee Muujiza wa Papo kwa Papo, Anauwezo wa hali ya juu wa kusambaratisha mahusiano yao na kumrejesha kwako haraka sana na Kumfanya Atimize Ahadi zote Ndani ya Muda Mfupi Endapo Utafwata Atakacho Kuelekeza

 ZINDIKO LA NYUMBA NA BIASHARA, PETE ZA BAHATI, HUMALIZA KABISA TATIZO   HUZUIA CHUMA ULETE KWENYE BIASHARA, HURUDISHA MALI ZILIZOPOTEA, NA KUPONYA MAGONJWA SUGU ANAO UWEZO WA KUMRUDISHA ALIE MBALI AU ALIECHUKULIWA MSUKULE, KUPANDISHA NYOTA NA KUSHINDA BAHATI NA SIBU, KASAFISHA NYOTA NA KUKUPA MVUTO WA AJABU, KUTOA NUKSI NA VIFUNGO MBALIMBALI,  MAFANIKIO YA MAISHA NA UTAJIRI BILA MASHARI, NA MENGINE MENGI YA SIRI,

JE UMAHANGAIKA KUPATA MTOTO BILA MAFANIKIO? WASILIANA NA MTAALAMU HUYU KWANI YEYE HUFAULU PALE WOTE WALIPOSHINDWA, PIA UMALIZA KAZI ZILIZO SHINDIKANA NA WATAALAM WENGINE NDANI YA MASAA 24 TU,

(NA ANATIBU KWA NJIA YA SIMU UKIWA NCHI YOYOTE AU MKOA WOWOTE ENDAPO UTAFWATA MAELEKEZO YAKE)

Kwa ushauri na mawasiliano  zaidi Piga SIMU No:

Mobile +255 654-836970
WhatsApp +255 756-033670 

TRA Yamwanika Askofu Kakobe..Yadai Fedha za Kanisa Zinatumika Kujenga Nyumba ya Mke wa Kakobe

$
0
0
Kufuatia kauliiliyotolewa na Askofu Zachary Kakobe wa Kanisa la Full Gospel Bible Fellowship katika mahubiri ya Ibada ambayo alisema kuwa “Yeye ana pesa kuliko Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania”, Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) ilifanya uchunguzi ili kubaini usahihi wa kauli hiyo.

Yafuatayo ni mambo ambayo yalibainika baada ya kufanyika uchunguzi kuhusu kauli ya Askofu Zachary Kakobe;

1.Askofu Zachary Kakobe hana akaunti wala fedha katika taasisi yoyote ya fedha hapa nchini. Aidha uchunguzi ulibaini kuwa Askofu Kakobe ni mmoja wa wasimamizi wakuu wa akaunti za kanisa (signatories) zilizopo katika benki ya NBC zenye jumla ya kiasi cha shilingi 8,132,100,819.00, kiasi hiki cha fedha kimetokana na sadaka, zaka na changizo ambazo zinatolewa na waumini wa kanisa tajwa hapo juu, hivyo kwa mujibu wa Sheria hakitozwi kodi.

2.Kanisa lilikwepa kulipa kodi kiasi cha shilingi 20,834,843.00 ambazo zilitokana na uwekezaji katika makampuni ya kukuza mitaji.Kodi hiyo imelipwa baada ya uchunguzi.

3.Kampuni inayomilikiwa na watoto wa Askofu Zachary Kakobe ilikwepa kulipa kodi kiasi cha shilingi 37,280,030.00 ambazo zimelipwa baada ya uchunguzi. Kwa ujumla, kiasi cha kodi kilicholipwa kutokana na uchunguzi huu ni shilingi 58,114,873.00.

4. Kanisa linatunza kiasi kikubwa cha fedha kwenye ndoo na ‘majaba’ kinyume na taratibu za utunzaji wa fedha, lakini pia uwekaji na utoaji wa fedha nyingi kutoka benki haushirikishi vyombo vya ulinzi na usalama kwa ajili ya usalama wa fedha zenyewe na wahusika.

5.Pia ilibainika kwamba Kanisa halitengenezi hesabu za Mapato na Matumizi ya Fedha kitu ambacho ni kinyume na Katiba ya Kanisa pamoja na sheria za usimamizi wafedha ambayo imepelekea matumizi mabaya ya fedha za waumini kama vile safari za nje ya nchi ambazo zimedhaminiwa na Kanisa lakini wanaosafiri ni Askofu na familia yake.  Vile vile fedha za Kanisa zinatumika kujenga nyumba ya mke wa Askofu, kwa jina lake na wala si kwa jina la Kanisa, kitu ambacho ni kinyume na taratibu za Kanisa.

Aidha, wakati uchunguzi huo ukiendelea,mnamo tarehe 24.01.2018 Askofu Kakobe aliandika barua kwa Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuomba radhi kutokana na kauli yake ya kebehi pamoja na matamshi yake ya dharau kwamba ana pesa nyingi kuliko Serikali.

WITO:

  • Mamlaka ya Mapato Tanzaniainatoa wito kwa Taasisi zote za dini ambazo zinajihusisha na shughuli zozote za kiuchumi kulipa kodi stahiki na kwa wakati kwa mujibu wa sheria, kanuni na taratibu za kodi.
  • Mamlaka ya Mapato Tanzania inazitaka Taasisi zote za kidini kufuata katiba zao ikiwa ni pamoja na kutengeneza hesabu za mapato na matumizi.


Charles E. Kichere
KAMISHNA MKUU
MAMLAKA YA MAPATO TANZANIA

“Pamoja Tunajenga Taifa Letu”

Messi Ataonea Wengine Lakini kwa Chelsea ni nyoka wa Kibisa tu

$
0
0
Lionel Messi ni kati ya wanasoka ambao ukitaja wanasoka watatu kuwahi kutokea duniani baasi jina lake lipo na kwa wengi hata ukitaka kutaja jina la mchezaji mmoja baasi utakuta jina la Lionel Messi ndio linatajwa.

Messi anatisha na Messi anaogopesha, lakini cha ajabu na kustaajabisha ni kwamba Messi anaogopwa na kuonea watu wengine lakini akifika mbele ya Chelsea anakuwa nyoka wa kibisa (hana sumu).

Toka aanze kucheza soka la kimataifa katika klabu ya Barcelona hadi hivi sasa Lionel Messi amefunga jumla ya mabao 595 na ni mabao 5 tu kufika 600 lakini hadi hivi sasa hajawahi kugusa wavu wa Chelsea hata mara moja.

Chelsea ndio wanashikilia rekodi mbovu ya Messi kwani tangu aanze kupiga soka hajawahi kukutana na timu mara nyingi halafu asifunge kama ilivyo Chelsea, wameshakutana mara nane.

Msimu wa mwaka 2005/2006 katika hatua kama hii Barca waliwatoa Chelsea kwa jumla ya mabao 3 kwa 2 na Messi hakufunga, 2006/2007 Chelsea wakalipiza kwa Barcelona na kuwaondoa kwa bao la Didier Drogba nayo pia Messi hakufunga.

2008/2009 Messi alikuwepo kikosi cha Barca kilichokwenda fainali na hakuifunga Chelsea japokuwa yeye ndio alikuwa mpishi wa bao la Andres Iniesta lilioiondoa Chelsea katika michuano hiyo.

2011/2012 tena ikiwa mara ya 4 kukutana katika Champions League(sawa na mechi 8) Messi alishuhudia Barcelona wakiondolewa katika Champions League na akikamilisha idadi ya mashuti 29 langoni mwa Chelsea bila bao.
Viewing all 104667 articles
Browse latest View live




Latest Images