Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104762 articles
Browse latest View live

Tusinyooshe Vidole Kifo cha Akwilina- Paul Makonda

$
0
0

Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda amewataka wananchi kuacha kunyooshea vidole na kurushia lawama juu ya kifo cha mwanafunzi Akwelina Akwilin kwani Jeshi la Polisi linaendelea kufanya uchunguzi wake na watakapomaliza watatoa taarifa kamili


Makonda ameeleza hayo wakati aliposhiriki katika ghafla ya kuaga mwili wa marehemu Akwelina katika chuo cha Taifa cha Usafrishaji (NIT) ili aende kupumzishwa kwenye nyumba yake ya milele huko Mkoani Kilimanjaro.

"Jeshi hili la Polisi litatupatia majibu watakapomaliza kazi yake, ombi langu kwenu wananchi wa Dar es Salaam hasa wale ambao hatujawahi kusomea mambo ya uchunguzi na wala hatuyajui tusiwe wa kwanza kunyoosha vidole na kuhukumu kabla hatuja hukumiwa. Mimi najua mtoa hukumu wa kweli ni Mungu na anazo siri zote kwa nini Akwilina ameondoka tarehe 16", amesema Makonda.

Pamoja na hayo, Makonda ameendelea kwa kusema "naendelea kuwasihi tuwape nafasi wenye majukumu yao watimize kazi yao na hatimae na sisi tuunganike mkoa kama taifa kuhakikisha amani inatawala katika mkoa wetu kwa kila mtu".

Kwa upande mwingine, Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda ameitaka familia ya marehemu Akwelina iwe yenye uvumilivu katika kipindi kigumu walichonacho kwa sasa.

Polisi Wakana, Wadai Wao Hawahusiki Kwa Lolote

$
0
0

Jeshi la polisi mkoa wa Njombe limekana kumkamata mwandishi wa habari Emmanuel Kibiki ambaye anadaiwa kukamatwa majira ya saa tisa usiku wa kuamkia leo Februari 22, 2018  na watu waliojitambulisha kuwa ni jeshi la polisi.

 Akizungumza na www.eatv.tv Kaimu Kamanda wa polisi mkoa wa Njombe, John Temu amesema kuwa wao hawajamkamata mwandishi huyo na kudai huenda akawa amekamatwa na taasisi zingine ila si jeshi la polisi.

"Hakuna ukweli wowote ule kama kungekuwa na ukweli stori ingekuwa imeshafika kwetu ila inawezekana labda taasisi zingine za upelelezi zinafanya kazi zikawa zimemkamata maana taasisi za upepelezi huwa zinawakamata watu zenyewe, kwa hiyo watu wanapicha tu kuwa mtu akikamatwa basi jeshi la polisi ndilo linakuwa limemkamata.Kwa sababu kama sisi tungekuwa tumemkamata mpaka asubuhi hao polisi wangekuwa wamewasiliana na mkoa kutoa taarifa" alisema John Temu

Februari 22, 2018 zimeibuka taarifa zikidai kuwa mwandishi wa habari wa Makambako amekamatwa majira ya saa tisa usiku na watu ambao walijitambulisha kuwa ni jeshi la polisi lakini upande wa jeshi la polisi wamekataa kuhusika kumkamata mwandishi huyo wa habari.

Rais Magufuli atoa wito Jumuiya ya Afrika Mashariki

$
0
0
Rais Dkt. John Pombe Magufuli ametoa wito kwa nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki kusimamia vizuri rasilimali walizonazo na kukusanya kodi vizuri ili waweze kutekeleza miradi mikubwa ya ujenzi wa miundombinu na kuimarisha huduma za afya kwa wananchi.

Rais Magufuli ametoa wito huo mjini Kampala Uganda wakati akichangia katika mkutano wa wakuu wa nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki unaojadili maendeleo na upatikanaji wa fedha kwa ajili ya miradi ya sekta ya miundombinu na afya.

Kabla ya Rais Magufuli kutoa mchango wake, Marais walioshiriki mkutano huo wamepokea taarifa ya mkutano wa majadiliano ya kisekta kuhusu mahitaji ya fedha kwa ajili ya kutekeleza miradi ya sekta ya miundombinu na afya ambapo imeelezwa kuwa katika miaka 10 ijayo nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki zitahitaji Dola za Marekani Bilioni 78 kutekeleza miradi ya miundombinu inayopendekezwa.

Katika mchango wake Rais Magufuli amesema pamoja na kutumia mfumo wa PPP ni muhimu kwa Serikali za kila nchi kusimamia vizuri ukusanyaji wa mapato ya kodi na rasilimali nyingine ili kutekeleza miradi ya miundombinu, afya na sekta nyingine.

Marais waliohudhuria mkutano huo ni Rais wa Uganda, Yoweri Kaguta Museveni, Rais wa Kenya, Uhuru Muigai Kenyatta, Rais wa Sudan Kusini,Salva Kiir Mayardit na Marais wa Rwanda na Burundi wamewakilishwa.

Breaking News: Diwani wa Chadema Kata ya Namwawala Afariki Kwa Kukatakatwa na Mapanga na Watu Wasiojulikana

$
0
0
Diwani wa Kata ya Namawala wilayani Kilombero, Godfrey Lwema (CHADEMA) ameuawa usiku wa leo nyumbani kwake kwa kukatwakatwa kwa mapanga na watu wasiojulikana.

Polisi ndo wanaelekea huko.

Taarifa za awali zinasema kuwa usiku umeme ulikatika katika nyumba yake. Luena akatoka nje kutizama kama kuna shot maana nyumba za jirani zilikuwa na umeme. Alipozunguka nyuma ya nyumba yake kukagua umeme akakutana na kikosi cha watu wenye mapanga wakamkatakata hadi wakamtoa roho.

Ee Mungu tuokoe.

R.I.P. LUENA R.I.P

Namwawala Kilombero- Morogoro

By Mdau JF

Ajali Tabata, Dar: Mwandishi Mariam Mziwanda wa Gazeti la Uhuru anusurika kifo. Akimbizwa Muhimbili

$
0
0
Mwandishi wa habari wa Gazeti la Uhuru, Mariam Mziwanda, amejeruhiwa katika ajali iliyohusisha magari matatu, eneo la Tabata TOT jijini Dar es Salaam, usiku huu baada ya gari dogo alilokuwa akiliendesha lenye namba za usajili T222 DJX kugongana na lori la mizigo lenye namba za usajili T 495 na kisha kuingia katikati na kubanwa na lori la mafuta lenye namba za usajili T 748 BMT.

Kwa mujibu wa dereva wa lori la mafuta lililohusika katika ajali, William Colonel, chanzo cha ajali hiyo ni mwendokasi wa lori la mzigo ambalo liliacha njia na kupanda kingo za katikati ya barabara, kisha kupinduka na kuangukia lori la mafuta na gari lililokuwa likiendeshwa na Mziwanda.

Lori la mafuta na gari dogo yote yalikuwa upande wa kushoto wa barabara.

Imeelezwa lori hilo baada ya kuanguka lililibana gari dogo lililokuwa katikati.

Shuhuda wa ajali hiyo, Adeodatus Sylivester Charles amesema "Nilimtambua majeruhi kwani namfahamu tangu akiwa mtoto na sasa ni mwandishi wa habari wa Gazeti la Uhuru".

Anasema baada ya ajali kutokea alikuta wasamaria wema tayari wanamtoa majeruhi kwenye gari akiwa ameumia sana.

“Nilikuta ametolewa kwenye gari yake akiwa ameumia sana, nikamsaidia kuvitoa vitu vyake kama simu na pochi na kumpelekea maana alikuwa analalamika simu yangu - simu yangu, na watu walikuwa tayari wameshasogea eneo la ajali wanagombania vitu hivyo.

Madereva wote wa malori walitoka salama bila majeraha ya aina yoyote.

Chanzo: Mwananchi

Download Application ya MCHAMBUZI HURU Kwenye Simu yako Kusoma Habari za Siasa Kila Baada ya Lisaa Limoja

$
0
0
Maswala ya Siasa na Matamko ya kila siku ya Wanasiasa Hakikisha Umedownload App ya Mchambuzi Huru Kwenye simu yako


Kama we ni Mpenzi wa Habari za Siasa Usipitwe na Hii Application ya Mchambuzi..... 

Bonyeza HAPA Kudownload kwenye Simu yako



Miujiza ya Sharifu Seif Mohamed..JE Umeachwa na Mme/Mke au Mpenzi, Umesongwa na Mitihani ya Maisha..Piga Simu Upate Muujiza Wako

$
0
0


SHARIFU SEIF MOHAMED ANAWASHUKURU WALE WOTE WANAOENDELEA KUPIGA SIMU, WENYE MATATIZO NA WALE WANAOTOA  SHUKRANI NA SHUHUDA JINSI TIBA ZAKE ZINAVYO WASAIDIA,

(Rudisha mahusiano yako ndani ya masaa 72 tu)

SHARIFU MOHAMED Ni  mtaalam na mnajimu maarufu wa nyota na kubashiri mambo yanayo watesa binadamu duniani kote na kupata ufumbuzi, Anatumia kitabu cha QUR'AN na Nyota

Je Umeachwa na UMPENDAE awe Mme/Mke na bado unampenda? Je Umekimbiwa na Mmeo/ Mkeo n anaishi na mtu mwingine? Je Umejaribu sehemu nyingi bila mafanikio? Mpigie simu SHARIFU SEIF sasa hivi ujionee Muujiza wa Papo kwa Papo, Anauwezo wa hali ya juu wa kusambaratisha mahusiano yao na kumrejesha kwako haraka sana na Kumfanya Atimize Ahadi zote Ndani ya Muda Mfupi Endapo Utafwata Atakacho Kuelekeza

 ZINDIKO LA NYUMBA NA BIASHARA, PETE ZA BAHATI, HUMALIZA KABISA TATIZO   HUZUIA CHUMA ULETE KWENYE BIASHARA, HURUDISHA MALI ZILIZOPOTEA, NA KUPONYA MAGONJWA SUGU ANAO UWEZO WA KUMRUDISHA ALIE MBALI AU ALIECHUKULIWA MSUKULE, KUPANDISHA NYOTA NA KUSHINDA BAHATI NA SIBU, KASAFISHA NYOTA NA KUKUPA MVUTO WA AJABU, KUTOA NUKSI NA VIFUNGO MBALIMBALI,  MAFANIKIO YA MAISHA NA UTAJIRI BILA MASHARI, NA MENGINE MENGI YA SIRI,

JE UMAHANGAIKA KUPATA MTOTO BILA MAFANIKIO? WASILIANA NA MTAALAMU HUYU KWANI YEYE HUFAULU PALE WOTE WALIPOSHINDWA, PIA UMALIZA KAZI ZILIZO SHINDIKANA NA WATAALAM WENGINE NDANI YA MASAA 24 TU,

(NA ANATIBU KWA NJIA YA SIMU UKIWA NCHI YOYOTE AU MKOA WOWOTE ENDAPO UTAFWATA MAELEKEZO YAKE)

Kwa ushauri na mawasiliano  zaidi Piga SIMU No:

Mobile +255 654-836970
WhatsApp 0622766715

Dayna Nyange Afunguka Kuhusu Ujauzito Wake

$
0
0
Dayna Nyange Afunguka Kuhusu Ujauzito Wake
Msanii wa muziki Bongo, Dayna Nyange amefungua tetesi za kuwa mjamzito.

Hitmaker huyo wa ngoma ‘Komela’ ameiambia XXL ya Clouds Fm kwa sasa hana ujauzito ila anachokumbuka kwa sasa ni ujauzito wake wa kwanza ambao aliupata akiwa na umri wa chini ya miaka 18.

“Nilipopata ujauzito sikuwa najua, nilikuwanahisi ni Malaria nikaambiwa niende kupima pale hospital ile karatasi ya majibu nilipewa nikambiwa nipeleke nyumbani nilipofika nilimkabidhi dada yangu sikujua kama ni majibu kuwa ni ujauzito,” amesema Dayna.

Dayna ameongeza kuwa mtoto wake kwa sasa ana umri wa miaka 11 na anahitaji afike mbali kielimu asiwe kama yeye ambaye alishindwa kumaliza elimu ya sekondari.
Siku ya wapendanao (Valentine Day) February 14 mwaka huu aliposti picha katika ukurasa wake wa Instagram ambayo ilipelekea wengi kudhani Dayna ni mjamzito.

Mtanzania Ahukumiwa Jela Ghana Baada ya Kukamatwa na Dawa za Kulevya

$
0
0
Mtanzania Ahukumiwa Jela Ghana Baada ya Kukamatwa na Dawa za Kulevya
MWANAMKE raia wa Tanzania, Basaida Zena Jafary amehukumiwa miaka mitano jela baada ya kukamatwa akiwa na mzigo wa madawa ya kulevya yenye uzito wa Kg 2.3 (Cocaine na Heroine) yanayokadiriwa kuwa na thamani ya Dola za Marekani 70,000 (zaidi ya Tsh. Milioni 155).

Bi. Zena ambaye ni mfanyabiashara wa chakula akiwa nchini alifika katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kotoka Ghana (KIA) akitumia Ndege ya Shirika la Rwanda Air yenye namba ET 200 ambapo maofisa hao walibaini shehena hiyo ya dawa hizo haramu zilizowekwa katika bahasha mbili.

Akihojiwa na maofisa hao, alikiri kumiliki bahasha hizo na kukiri kuwa alipewa na Bwana Mandanje Omari raia wa Tanzania na kutakiwa kuzifikisha kwa mtu mmoja anayeishi katika Jiji la Accra.

Queen Darleen Afunguka Hali ya Mahusiano ya Diamond na Zari

$
0
0
Queen Darleen Afunguka Hali ya Mahusiano ya Diamond na Zari
Msanii kutoka label ya WCB, Queen Darleen ametia neno katika ile drama ya Diamond na Zari The Boss Lady.

Muimbaji huyo ambaye ni ndugu na Diamond ameiambia The Playlist ya Times Fm kuwa kwa mara ya kwanza alishtuka kusikia Zari na Diamond wameachana ila ni kitu ambacho hadi sasa hakiamini.

“Off corse nilishtuka kuona vile nikahisi kama utani na sikutaka kuuliza au kuhoji kwa sababu ingeniumiza ila sitaki kuuliza au kuhoji kitu chochote,” amesema Queen Darleen.

“Kwa imani yangu naona bado wapo wote, kama wameachana, hawajaachana sitaki kujua na ninachojua wapo wote na ninaacha iwe hivyo katika nafsi yangu,” amesisitiza.

Queen Darleen

Siku ya wapendanao (Valentine’s Day) February 14 mwaka huu Zari The Boss Lady alitangaza rasmi kuachana na Diamond kutokana na kuchoshwa na habari za kusalitiwa ambazo husikika kila siku katika vyombo vya habari.

'Subalkheri' Yawatokea Puani Aslay, Nandy Wapigwa Faini ya Milioni 5

$
0
0
'Subalkheri' Yawatokea Puani Aslay, Nandy Wapigwa Faini ya Milioni 5
Wasanii Aslay na Nandy wamepigwa faini ya milioni 5 kwa pamoja kutokana na kukiri, kukubali kosa kuimba wimbo wa 'Subalkheri Mpenzi' bila kufanya mawasiliano na wamiliki wa wimbo huo ambao ni kikundi cha Utamaduni cha taarab asilia visiwani Zanzibar.

Kikundi hicho kilikusudia kuwafikisha mahakamani wasanii hao lakini kabla ya kuchukua hatu hiyo Aslay na Nandy wakiwakilishwa na kiongozi wao walifika visiwani humo na kufanya mazungumzo na kikundi hicho ambapo wamehitaji kulipwa milioni tano. 

Katibu Mkuu wa kikundi cha utamaduni cha tarabu asilia, Taimur Rukuni Twaha, amesema kikundi  hicho cha tarab kimewataka wasanii hao kulipa faini kutokana na kuimba wimbo huo bila ya ridhaa yao, pia amedai kuwa wamekubaliana leo Alhamisi na kufikia muafaka huo baada ya wasanii hao kupitia kwa kiongozi wao kukiri kufanya kosa hilo. 

Twaha amesema licha ya kukiri makosa hayo pia meneja huyo wa Aslay ameomba kuingia mkataba na kikundi hicho cha tarab kufanya biashara ya kuziimba tena nyimbo zao zengine za zamani.

Katibu huyo amesema kuhusu nyimbo zao kuimbwa tena hilo bado hawajaafikiana kwa sababu walishapewa agizo na Rais mstaafu wa awamu ya tatu Dk Salmin Amour Juma wakati akiwa rais, kuwa wasikubali nyimbo zao za tarabu asilia kuzibadili na kuzifanya katika mfumo wa muziki wa kisasa.

Zitto Kabwe Anyimwa Dhamana Morogoro Arudishwa Rumande

$
0
0
Zitto Kabwe Akamatwa Anyimwa Dhamana
Kiongozi wa Chama cha ACT Wazalendo na Mbunge wa Kigoma Mjini Mhe. Zitto Kabwe jana usiku alikamatwa na kuchukuliwa maelezo katika Kituo Kikuu cha Polisi cha Mkoa wa Morogoro, ambapo baada ya maelezo hayo yaliyodumu kwa saa moja alipelekwa mahabusu kwa kunyimwa dhamana.

Polisi wanaituhumu ziara ya chama cha ACT Wazalendo kutembelea madiwani wao katika kata mbalimbali kwenye mikoa 8 nchini kuwa ni kosa kisheria.

Kwa mujibu wa maelezo ya Wakili  wake, Mhe. Zitto ametuhumiwa kufanya Unlawful Assembly S. 74 cap 16 ya Sheria ya Kanuni ya Adhabu.

Baada ya kuandika maelezo Zitto akiwa na Wakili wake, ndugu Emmanuel Lazarus Mvula, Maelezo ysliyoanza saa Saa 4:42 usiku wa jana, mpaka saa 5:40 usiku, Jeshi la Polisi limekataa kumpa dhamana na kumpeleka mahabusu ya Kituo Kikuu cha Polisi cha Mkoa wa Morogoro.

Wakili Mvula amesema pia Jeshi la Polisi limekataa kusema kama dhamana ipo wazi au la, au kuweka wazi masharti ya dhamana.

Young Killer Msodoki Afunguka Kuhusu Kutengana na Mpenzi Wake

$
0
0
Young Killer Msodoki Afunguka Kuhusu Kutengana na Mpenzi Wake
Msanii wa  Hip hop bongo Young Killer Msodoki amekiru kugombana na mpenzi wake Halimaty Msodoki 'Miss Hip Hop' kwa madai kwamba hivyo ni vitu ambavyo haviwezi kuzuilika hasa watu wanapokuwepo kwenye mahusiano.


Msodoki ambaye amedumu kwenye mahusiano na mpenzi wake huyo tangu alipoanza kujulikana kwenye game ya Bongo Fleva ambapo watu wengi walikuwa wakisubiri ndoa amesema kwamba kutengana kwao hakujasababishwa na mapenzi bali mambo mengine ya kawaida kabisa.

Aidha amekiri mbele ya Kamera za eNEWZ  kwamba kwa sasa mrembo 'Miss Hip Hop' amerudi Mwanza kwa mambo yake binafsi lakini pia jamii inapaswa kutambua kwamba maswala ya mahusiano huwa yana mambo mengi ikiwemo ugomvi.

Pamoja na kubanwa kuhusu mwanadada aliyeonekana nyumbani kwake, Msodoki amefunguka kwamba mashabiki zake wanapaswa  kuelewa na kuamini kile wanachokiona kwani hawezi kuelezea maswala mengi kwa kuwa hata yeye anajaribu katika maswala ya mahusiano yakifanikiwa sawa na endapo yakishindikana itakuwa ndio basi.

Mbali na hayo Rapa huyo kutoka Mwanza amesema watu ambao wanasema na kutabiri kwamba Young  Killer hataweza kutengeneza tena  nyimbo kubwa kama Dear Gambe na alipofikia ndiyo mwisho wake na kusema kwamba watu wanaobet kwenye mziki wake ni sawa na kutema mate kulia na kufukia kushoto.

Diamond Kiboko Awapa Ujumbe Mzito Watoto Wake "Uzuri Mlionao Mkaenda Kuniletea Wakwe Vijuso....Dah Mtanisikitisha Sana"

$
0
0
Diamond Kiboko Awapa Ujumbe Huu Watoto Wake "Uzuri Mlionao Mkaenda Kuniletea Wakwe Vijuso....Dah Mtanisikitisha Sana"
Msanii wa muziki Diamond Platnumz ametoa onyo kali kwa vijana wake wa kiume Nilan na Daylan kwa kuwata asiwaletee wakwe vijuso.

Diamond katoa rai hiyo kwa watoto wake hao  ambao amezaa na wanawake  wawili tofauti ambao ni Zarina Hassan maarufu kama Zari The Boss Lady, na Daylan (AbdulLatif) aliyezaa na mwanamitindo Hamisa Mobetto kupitia mtandao wa kijamii wa Instagram.


Ikiwa bado siku moja iwe siku ya Wapenda( Valentine Day) Diamond na Hamisa walifikia makubaliano ya kumlea na kumuhuduamia mtoto wao wa kiume Dalyna, huku siku ya  Valentine iligeuka mbawa kwa Diamond baada ya kumwaga rasmi na Zari The Boss Lady chanzo kikwa ni kutokuwa muwaminifu katika mapenzi yao.

Rais wa Fifa Akoshwa na Tanzania "Tanzania ni Nchi ya Soka"

$
0
0
Rais wa Fifa Akoshwa na Tanzania "Tanzania ni Nchi ya Soka"
Rais wa Shirikisho la Soka la duniani (FIFA) Gianni Infantino, akiwa nchini Tanzania kuhudhuria mkutano wa shirikisho hilo nchini.

Mkutano huo ulishirikisha jumla ya mashirikisho 21 ya kandanda ambao ni wanachama wa shirikisho hilo.

Rais wa shirikisho hilo la soka duniani alikutana na Waziri Mkuu wa nchi , Kassim Majaliwa pamoja na Waziri wa Utamaduni na Michezo Harryson Mwakyembe.

Katika mkutano na waandishi wa habari, Bw Infantino amesisitiza kuzungumzia hali ya rushwa katika mpira wa miguu.

"Tumefanikiwa sana katika kuweka uwazi wa matumizi ya fedha za FIFA. Leo FIFA ni shirikisho lenye uwazi. Tunachapisha matumizi ya fedha zote. Kila mtu anaweza kufuatilia fedha zinatoka wapi na fedha zinaenda wapi."

Akizungumzia jitihada za kukuza soka barani Afrika, Bw Infantino ameelezea kuwa siku za nyuma Afrika ilikuwa inapata dola za kimarekani milioni 26 kutoka FIFA, lakini sasa hivi, Afrika inapata dola za kimarekani milioni 100 ili kuiinua mchezo wa soka.

Pamoja na hayo amesema katika kipindi chake amejaribu kuhakikisha ongezeko la timu za Afrika katika kushiriki michuano ya kombe la dunia .

Tangu aingie madarakani ,Rais huyo wa Fifa ameongeza idadi ya timu zitazoshiriki michuano ya kombe la dunia la mwaka 2026 toka 5 mpaka 7.

"Sitaki kuahidi lolote, ninatenda" Infantino ameelezea.

Kenya na Tanzania zashuka pakubwa orodha ya Fifa
Mchezo wa kandanda ya wanaume unafuatiliwa sana na una uwekezaji mkubwa duniani, matokeo ni kwamba mchezo huo kwa upande wa wanawake unaachwa nyuma.

Ajenda kubwa katika mkutano huo ilikuwa kujadili namna ya kukuza soka la wanawake na vijana pamoja na suala la usajili kwa njia ya mtandao.

Gianni amesema wamezungumzia kuanzisha ligi ya kimataifa ya wanawake.

"Tunataka kuzindua michuano mpya ya FIFA, ligi ya kimataifa ya wanawake. Tutaomba nchi zote kushiriki na tutatoa msaada wa fedha "

Mkutano wa Fifa una kauli mbiu ya "kurejesha kandanda kwa Fifa na Fifa kwa kandanda.

Soma Nafasi za Kazi Zilizotangazwa Siku ya Leo

$
0
0

Breaking News: Zitto Kabwe Aachiwa Huru kwa Dhamana ya Milioni 50

$
0
0
Breaking News: Zitto Kabwe Aachiwa Huru kwa Dhamana ya Milioni 50
Mbunge wa Kigoma Mjini na Kiongozi wa Chama cha ACT Wazalendo, Zitto Kabwe ameachiwa huru kwa dhamana ya Polisi yenye thamani ya Milioni 50 muda huu baada ya kulala mahabusu tokea jana (Alhamisi) usiku.


Hayo yamebainishwa na Wakili wa Mbunge huyo ni Emmanuel Lazarus Mvula ambae ndie aliyemdhamini Zitto na kusema anatakiwa kuripoti katika kituo kikuu cha Polisi cha Mkoa wa Morogoro siku ya Jumatatu Machi 12, 2018.

Mbunge Zitto Kabwe alikamatwa na Jeshi la Polisi la Mkoa wa Morogoro wakati akiwa katika muendelezo wa ziara yake iliyoanza Februari 19 akiwa pamoja na viongozi wengine wa ACT- Wazalendo wa malengo ya kushiriki kazi za maendeleo na kuzungumza na kamati za maendeleo za kata hizo.

Mrembo Vera Adai Hajawahi Kupenda...Yeye Pesa Mbele Kwanza

$
0
0
MREMBO kutoka Kenya, Vera Sidika hivi karibuni alisema hajawahi kukutana na mwanaume mwenye vigezo vyote ambavyo anavitaka, mazingira yaliyomfanya mpaka leo awe hajawahi kupenda.
Akijibu swali kutoka kwenye mtandao mmoja wa burudani nchini humo juu ya ujumbe aliouandika kwenye Mtandao wa Kijamii wa Instagram kwamba, wanaume wengi wanaovutia hawana pesa na wengi wasiovutia ndiyo wana pesa, Vera alisema:

“Ni kweli wanaume wengi ninaokutana nao lazima utakuta wana kitu kimoja, mvuto lakini hawana pesa au pesa lakini hawana mvuto. Sasa kwa upande wangu ninahitaji kumpenda mwanaume mwenye vitu vyote jambo ambalo sijawahi kukutana nalo na ndiyo maana sijawahi kupenda!”

Lupita Nyongo Awaboa Ndugu zake Wakenya Uzinduzi wa Black Panther Kenya

$
0
0
STAA kutoka Hollywood mwenye asili ya Kenya, Lupita Nyongo hivi karibuni amejikuta akiwaboa ndugu zake Wakenya baada ya kushindwa kuhudhuria uzinduzi wa Filamu ya Black Panther uliofanyika nchini hapo Jumanne iliyopita.

Mashabiki wa mwanadada huyo kutoka Kenya, walianza kuonesha kutofurahishwa na suala hilo baada ya Lupita

 Kuonekana kwenye uzinduzi wa filamu hiyo Afrika Kusini huku akiwa amekacha uzinduzi wa filamu hiyohiyo nchini Kenya.

Hata hivyo, pamoja na lawama na madongo ambayo mwanadada huyo ametupiwa na mashabiki wake juu ya kuwasusa ‘nduguze’, hakujibu lolote wala kueleza ni kwa nini alikosekana kwenye uzinduzi wa Black Panther Kenya.

Wadada: Mtunusuru na Hizi Picha zenu Huko Mitandaoni

$
0
0
Juzi kati nilikutana na mrembo huko facebook. Kupitia picha alizoweka "nikashawishika" na "kuhamasika" kutoa mwaliko pasipo shuruti. Alionekana ni demu aliyekidhi vigezo vyangu alikuwa kimodo fulani hivi maji ya kunde fulani iliyofifia. Mwenyewe nikasema yes.

Baada ya chats za siku kadhaa tukakubaliana kukutana kwenye moja ya maeneo nayoamini sana hasa nikizingatia "ukisu" wa yule demu sikutaka sehemu ya maskharamaskhara. Huku na huko siku na muda vikawadia, demu akanishtua ameshakuja maeneo tuliyokubaliana.

Nami uzuri sikuwa mbali na hapo. Nikajisogeza kidogo nikapishana na dada mmoja kibonge kavaa mlegezo wa jinzi, shati la mikono mirefu lenye rangi ya ugoro huku likiwa limejaa alama za misalaba. Nikampita huyo dada huku nikielekea mashariki huku nikiitafuta ile sura ya fesibuku kulia na kushoto kwa eneo ile bila mafanikio. Punde simu yangu ikaita kucheki dem anapiga.

Akanambia keshaingia amekaa ananingoja, akanielekeza. Nilishangaa kidogo kwa sababu kwa jografia ya pale asingeweza kupita bila kuniona na watu hawakuwa wengi kivile. Kwa Haraka sana machale yakanicheza nikajiuliza asijekuwa ni yule demu wa misalaba niliyepishana naye hapa hivi punde. Maana nilijua kama ni yeye ishakuwa baala hii.

Nikajishawishi kimoyomoyo haiwezekan akawa ni yeye. Njkajitokeza kwenda kumcheki nakuta kumbe ndio dem yuleyule niliepishana nae, tena sasa kashazungukwa na wahudmu wanamsikiza anaagiza mapochopocho. Nikajisemea kimoyomoyo laahaula lakwata.. leo imekula kwangu vibaya. Nilitaka kupiga u-turn kisha nizimishe simu mazima nikaona itakuwa soo zaidi na hata hivo ningemtia hasara.

Nikaamua kuwa muungwana, basi kwa taaabu nikajivuta huku nikilazimisha 'kuitafuta' tabasamu ili demu asijekunishtukia. Tulipiga stori 2-3 nikajifanya kupokea visimu vya uongouongo hapo ili mradi nitafute sababu nitokomee zangu fasta maana hili disko limeshaingiliwa na mmasai.
Viewing all 104762 articles
Browse latest View live




Latest Images