Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104756 articles
Browse latest View live

Mbowe Amuwashia Moto Msajili "Mtungi Ndio Mtu Pekee Anayeharibu na Kuvuruga Vyama Siasa"

$
0
0
Mbowe Amuwashia Moto Msajili "Mtungi Ndio Mtu Pekee Anayeharibu na Kuvuruga Vyama Siasa"
Mwenyekiti wa CHADEMA Taifa, Mhe. Freeman Mbowe amefunguka na kudai Msajili wa vyama vya siasa nchini Jaji Francis Mtungi ndio mtu pekee anayeharibu na kuvuruga vyama siasa kuliko kiongozi mwingine yeyote yule aliyewahi kutokea.


Mbowe amebainisha hayo leo (Februari 27, 2018) wakati alipokuwa anazungumza na waandishi wa habari katika makao makuu  ya CHADEMA eneo la Magomeni, jijini Dar es Salaam baada ya kupita siku kadhaa tokea Jaji Mtungi kuipa barua chama hicho cha siasa kukitishia kutaka kukifuta.

"Muda unavyozidi kwenda namtambua vizuri Jaj Mtungi ni mtu wa aina gani. huyu ndio mtu anayevuruga vyama vya siasa kuliko kiongozi mwingine yeyote yule katika majaji au wasajili waliokwisha kutangulia tangu tulipo anzisha vyama vingi", amesema Mbowe.

Pamoja na hayo, Mbowe ameendelea kwa kusema 'lakini niseme tu ndugu zangu hizi chaguzi zote zitaendelea kuzaa majeraha na maumivu, kama hatuwa 'serious' hazitachukuliwa na kama 'movement serious' haitochukuliwa katika nchi hii kwa sababu hawa wenzetu hawaoni aibu wanajipanga na kulindwa na dola".

Kwa upande mwingine, Mbowe amesema chama cha CHADEMA sio chama cha kigaidi kama wanavyodhania bali ni chama makini kilichokuwa na mkusanyiko wa makabila na dini zote.

Korea Kaskazini Wadhamilia Kumfunga Miaka 30 Jela Rais wao wa Zamani

$
0
0
Korea Kaskazini Wadhamilia Kumfunga Miaka 30 Jela Rais wao wa Zamani

Leo February 27, 2018 Waendesha mashtaka wa Korea Kusini wanadhamiria kumfunga miaka 30 jela Rais wa zamani wa nchini humo Park Geun-hye katika kesi ya rushwa ambayo ilimpelekea kuvuliwa madaraka.

Taarifa hizo ambazo zimetolewa na Shirika la Habari la Yonhap limeripoti kuwa Park, 66, alifukuzwa mwezi March, 2017 na ameshafunguliwa mashtaka juu ya tuhuma za rushwa, matumizi mabaya ya madaraka na hata hivyo ameyakataa madai hayo.

Waendesha mashtaka hao pia wanataka Dola Bilioni 118.5 sawa na Tshs za Kitanzania Trilioni 283 kama faini kutoka kwa Park kutokana na makosa aliyoyafanya.

Mwanasheria anayemuwakilisha Rais huyo wa zamani Park Seung-gil, kwa niaba ya Park aliomba msamaha kwa kilio mbele ya Mahakama ya Wilaya ya Seoul akisema Park alijaribu sana kuongoza nchi mchana na usiku.

Serikali ya Botswana Yamtupia Lawama Kabila kwa Ghasia DR

$
0
0
Serikali ya Botswana  Yamtupia Lawama  Kabila kwa Ghasia DR,
Serikali ya Botswana ilisema Jumatatu ilimlaumu Rais Joseph Kabila wa Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo kwa kuwa kiini cha ukiukwaji wa haki za binadamu na kuzorota kwa hali ya usalama.

Taarifa iliyotolewa na Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa imemkosoa Kabila kwa kuendelea kungÆangÆania madarakani huku ikitoa wito kwa Jumuiya ya Kimataifa kuongeza shinikizo dhidi ya kiongozi huyo ambaye alipaswa kuondoka madarakani Desemba 2016.

Mbali ya Botswana kumlaumu Kabila, pia imewakosoa viongozi wengine wa Afrika ambao wameamua kubadili Katiba za nchi zao ili waendelee kubaki madarakani.

Viongozi hawa sasa wameamua kutumia njia kama vile kuchelewesha kufanya chaguzi au mabadiliko ya Katiba za Taifa kwa lengo la kuendelea kubaki madarakani,ö ilisema taarifa hiyo.

ôNi wazi kwamba viongozi kama hawa wanaongozwa na maslahi yao binafsi badala ya kujali maslahi ya taifa. Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo ni mfano kuntu. Tunaendelea kushuhudia kuzorota kwa haki za binadamu katika nchi hiyo na sababu kubwa ni kiongozi wake mkuu kuendelea kuchelewesha uchaguzi huku akiwa amepoteza udhibiti wa vyombo vya usalama.ö

Botswana ina uthabiti wa kimaadili wa kuzinyoshea kidole nchi nyingine kwa sababu Rais wake Ian Khama aliyeingia madarakani mwaka 2008 alitangaza Novemba mwaka jana kuwa atangÆatuka Aprili mwaka huu na kumwachia ofisi makamu wake Mokgweetsi Masisi kuongoza hadi uchaguzi mkuu mwaka 2019



Khama alichukua nafasi ya Festus Mogae kama rais mwaka 2008 baada ya kutumikia kama makamu wa rais kuanzia 1998. Mwaka 2009 alichaguliwa kuwa rais na aliongoza kipindi cha kwanza cha miaka mitano na mwaka 2014 alishinda kipindi cha pili na cha mwisho.

Lakini baadhi ya nchi kama vile Rwanda na Uganda zimebadili katiba zao kuwaruhusu viongozi wa sasa kutawala zaidi ya mihula miwili ya kikatiba na Burundi inahaha kubadili katiba.

Kabila aliingia madarakani mwaka 2001 akichukua nafasi ya baba yake Laurent DΘsirΘ Kabila aliyeuawa na walinzi wake.

Kutokana na Kabila kutotaka kuondoka yamekuwa yakifanyika maandamano nchi nzima kumtaka ajiuzulu lakini amekuwa akituma vikosi vya usalama kuzima hali iliyosababisha vifo na majeruhi.

   

Hizi Hapa Sababu Kuu za Wanaume Kupenda Wake za Watu

$
0
0
Hizi Hapa Sababu Kuu za Wanaume Kupenda Wake za Watu

ASSALAM aleikum mpenzi msomaji wangu, umzima? Unaendeleaje na mishughuliko yako? Mimi mzima, namshukuru Mungu kwa kunijaalia kuwa miongoni mwa wale wanaopendwa. Yes, mimi napendwa na hiyo ni bahati sana.

Wapo watu wanatafuta watu wa kuwapenda lakini mpaka sasa hawajawapata. Ndiyo maana nilishawahi kusema kwamba, ukibahatika kumpata mtu anayekupenda na kwa bahati nzuri na wewe ukawa na chembechembe za mapenzi kwake, shukuru Mungu na mshikilie.

Kumbuka mapenzi ndiyo yanachukua nafasi kubwa kwenye maisha yetu. Hata kama umzuri, una pesa nyingi na mali za kumwaga kiasi gani, kama huna mtu wa ‘kuinjoi’ naye, maisha yako lazima yatakuwa ni yenye upungufu mkubwa.

Ndiyo maana wapo ambao ni matajiri lakini kwa kuwa mapenzi yanawachanganya, wanafikia hatua ya kujiua. Hapo ndipo unathibitisha kwamba, mapenzi yanachukua asilimia kubwa katika maisha yetu ya furaha ya kila siku.

Mpenzi msomaji wangu, wiki hii nataka kuzungumzia sababu tano za kwa nini baadhi ya wanaume wanapenda sana kuwa na uhusiano na wapenzi wa watu.

Nimefikia hatua ya kuandika makala haya kwa kuwa, kila siku tunasikia fulani kafumaniwa na mke wa mtu au fulani anatembea na mpenzi wa mtu. Pia wapo wanawake ambao wameingia kwenye ndoa lakini bado wanasumbuliwa sana na wanaume.

Mbaya zaidi wanaume hao wanaelezwa kabisa kuwa, wameingia sehemu ambayo tayari mwingine kashajiweka lakini hawakubali, wanang’ang’ania.

 Achilia wapenzi tu, wapo pia wake za watu ambao wanatokewa na wanaume. Yaani mwanaume anajua kabisa huyu ni mke wa mtu na anampenda sana mumewe lakini jamaa linang’ang’ania lipewe nafasi kwa kuwa lishapenda.

Katika hili naomba niseme kwamba, si kila anayemtongoza mke wa mtu au mpenzi wa mtu ni kiwembe. Wapo ambao wana mapenzi ya kweli na wameshindwa kujizuia. Mwanamke anaweza kuwa ndani ya ndoa lakini akawa ameolewa na mwanaume ambaye siye aliyepangiwa na Mungu.

Katika mazingira hayo ndiyo unamkuta mtu anakomaa na mke wa mtu, kila siku anaimbisha akiomba apewe nafasi. Akiambiwa, ‘si unajua mimi mke wa mtu’ anasema, ‘sasa mimi nifanyeje wakati nahisi wewe ndiye mke wangu niliyepangiwa na Mungu?’

 Kwa bahati mbaya zaidi unaweza kukuta na mwanamke naye licha ya kwamba ameolewa lakini naye anajihisi kumpenda mwanaume huyo na wakati huohuo hapati kile ambacho alikitarajia kwenye ndoa yake. Hapo ndipo unamkuta mwanamke anakuwa njia panda.

Anyway, hiyo ni mitihani katika maisha, sasa nirudi kwenye zile sababu za baadhi ya wanaume kuwatokea wake/wapenzi wa watu.

 PENZI LA DHATI

Kama nilivyosema, baadhi ya wanaume si kwamba wanaonyesha kuwa wao hawajatulia kwa kuwatokea wake za watu. Baadhi yao penzi la dhati walilonalo dhidi ya wale ambao wameshaingia kwenye ndoa ndilo huwasukuma kufanya hivyo.

Wanachokifanya wao ni kueleza hisia zao bila kujali kuwa, mlengwa ana mtu au laa. Ndiyo maana mtu huyo anaweza kuwa anajua ukweli kwamba fulani ni mke wa mtu lakini kwa kuwa anaamini huyo ndiye wake, analazimika kujaribu zali.

Mimi niseme tu kwamba, kwenye hili siyo dhambi kueleza hisia zako lakini ndugu yangu kama unajua kabisa huyo uliyempenda yuko ndani ya ndoa yake au ana mpenzi wake, pambana na hisia zako. Jizuie kwani kumpa usumbufu mke wa mtu ni kujitafutia matatizo bure.

HAKUNA GHARAMA

Baadhi ya wanaume wanawatokea wake za watu kwa kuwa hawatapata usumbufu wa pesa za matumizi, vocha, mavazi na vitu vingine. Wao wanaamini watakuwa wanatoa penzi tu lakini mambo mengine mwenye mke atahudumia.

Lakini wengine wanataka kuanzisha uhusiano na wake za watu kimaslahi. Kwamba mwanaume anaweza kuona mwanamke flani ameolewa na mwanaume mwenye nazo lakini mke anaonekana kutopata penzi analolihitaji. Yeye anatupa ndoano, akiamini akimridhisha kimapenzi, atakuwa anahongwa yeye na maisha yake yatakuwa poa.

Hata kwenye hili nikupe tahadhari. Kama unatokea kumpenda mke wa mtu ili umchune au ili kukwepa kugharamia, tamaa yako hiyo itakuponza. Acha utegemezi, mwanaume aliyekamilika ni yule mwenye uwezo wa kumtunza mtu anayempenda, usikimbie majukumu na kutaka vya mteremko. Kumbuka wengi walioingia kwenye uhusiano na wake za watu kwa tamaa za pesa na mali, yamewakuta makubwa.

 USUMBUFU HAKUNA

Kuna wanaume ambao hawapendi kusumbuliwa kwa mambo ya wivuwivu na wapenzi wao, mara nyingi mwanaume anapoanzisha uhusiano na mtu ambaye ana mtu wake anahisi hatasumbuliwa.

Yale mambo ya; ‘uko wapi baby’, uko na nani, nataka tuonane leo’ yanakuwa si kwa kiwango kile ambacho kinakuwepo kwa mtu ambaye hana mtu.

 HAKUNA KUGANDANA

Wapo wanaume ambao wao wanataka kila mwanamke mzuri bila kujali ameolewa au yuko singo. Lakini pia wapo ambao hawataki kuingia kwenye uhusiano na mwanamke ambaye atagusia future. Kwa kifupi wanaume wa staili hii wanaamini wakiwa na wake za watu, hawawezi kugandwa wala kuulizwa juu ya ‘future’.

 SIFA TU

Kama ulikuwa hujui wapo wanaume ambao wakitembea na mke wa mtu wanaona sifa sana. Akimtongoza mke wa mtu, akakubaliwa, roho yake inakuwa fresh. Na wengine hawawezi kubaki na siri, kila atakayekutana naye atamwambia; ‘yule mbona nishampitia’.

Hiyo yote sifa. Mtu yuko tayari kutumia gharama yoyote ili mradi atembee na mke/ mpenzi wa mtu, aandike historia kwamba fulani licha ya kwamba ni mke wa mtu lakini ameshatembea naye.

Mpenzi msomaji wangu, leo niishie hapo lakini nilichotaka ni kueleza tu sababu za kwa nini baadhi ya wanaume wanakuwa wasumbufu kwa wake za watu bila kujali hatari iliyo mbele yao. Nasema hatari kwa sababu kumpenda mke wa mtu, ukawa unamsumbua kila wakati hatari yake ni pale taarifa zitakapomfikia mwenye mali. Yatakayokukuta hapo ni aidha kuuawa au kufanyiwa vitendo vya kudhalilishwa. Ndiyo maana hapo kati nimesema kwamba, pambana na hisia zako. Kumbuka ule usemi usemao, mke wa mtu ni sumu!

WAKILI Fatma Karume na Bob Wangwe Kuishitaki Serikali ya Tanzania

$
0
0
WAKILI Fatma Karume  na Bob Wangwe  watafungua kesi mahakamani kupinga wakurugenzi kusimamia uchaguzi nchini.

 Akizungumza na wanahabari leo, jijini Dar, Fatma Karume amesema kuwa baadhi ya viongozi waliwahi kusikika wakijinadi kushinda uchaguzi hata kwa kile walichoita magoli ya mkono na kudai kuwa haki ya kura sasa inaonekana  haina thamani, hivyo wao wanataka kuipigania haki hiyo.

 Aidha, Fatma Karume amesema watu ambao waliweka mfumo huo wa wakurugenzi kuwa wasimamizi wa uchaguzi walikuwa na lengo lao na walifanya hivyo kwa kuwa walikuwa wanajua nini wanataka kufanya.
“Mtu akipiga kura haina thamani yoyote na matakwa yake hayasikilizwi kwa sababu kuna kitu kinaitwa goli la mkono, linalotoka kwenye mfumo ambao refa anaona. Refa wa haki hawezi kukubali goli la mkono. Nini kinafanya refa afumbe macho, asione watu wanaosema watashinda kwa goli la mkono. Kila mtu ana haki ya kupiga kura na ikahesabika. Kama kuna watu wanapiga magoli ya mkono haki yako hii inachukuliwa, yaani imetekwa.
Pia alisema kwa mujibu wa katiba ya nchi, msimamizi wa uchaguzi harushusiwi kuwa chini ya chama chochote cha siasa huku akidai wasimamizi wa kura wanavaa magwanda ya chama siku moja siku ya pili wanavaa sare za Tume ya Uchaguzi.

Baada ya kubainisha mapungufu hayo ya sheria, Fatma Karume akasema watakwenda mahakamani kuhoji kama mfumo huo unakubalika chini ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambayo inataka kila kura ihesabike na demokrasia ifuatwe.

Wako Wapi Mapedeshee Walioimbwa na Kugawa Pesa Kwa Wasanii wa Bendi?

$
0
0
Baadhi ya Mapedeshee  wa enzi hizo Wakiwa na Warembo Katika kipindi cha Mboni Show


Kwa wale mashabiki wa mziki wa dance nchini,hasa bend za Fm Acadamia,Twanga pepeta,Malaika Bend,Acudo impact,Mashujaa band,Msondo Ngoma,Sikinde n.k mtakua mashahidi katika hili,

Miaka michache iliyopita nyuma kulikua na wimbi kubwa la vibopa,matajiri au kwa jina lingine mapedeshee wa jiji hili la Dsm waliokua wakiimbwa sana na kutajwa tajwa kwenye nyimbo za bendi hizi kila mara au kwenye matamasha ya bendi hizi,hii ilipelekea wao kutawanya au kugawa pesa nyingi kwa wanamuziki husika (hasa wenye asili ya Congo) na kwa mashabiki pia hasa dada zetu wa bongo movie na wasanii.

Wakati mwingine walikua hata wakigawa dola ya mmarekani na euros.

Jambo la kushangaza siku hizi siwasikii wala kuwaona wakifanya kufuru hizo,
Napatwa na mashaka pengine nini kimewakuta?au wameamua kwenda kutapanya nchi za jirani kama Malawi na Msubiji?

Wadau unaweza mtaja pedeshee uliyekua unamwamini sana kwa kutapanya au moja ya tukio uliloshuhudia akitapanta.

Binafsi nakumbuka kufuru ya Pedeshee Ndama mutoto ya ngombe na Pedeshee Bitus dhahabu...wadau wakubwa wa Fm Academia wazee wa Ngwasuma popote pale ndani ya jiji hili hasa Mango Gardern na maeneo mengine.

By Jembelamkono

Mbowe: Kuna Njama za Kutupa Kesi ya Akwilina....Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumatano ya February 28

$
0
0


Mbowe: Kuna Njama za Kutupa Kesi ya Akwilina....Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumatano ya February 28

Serikali Yatangaza Adhabu Ukikutwa na Mwanafunzi wa Kike Nyumbani

$
0
0

WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema Serikali imedhamiria kuwalinda watoto wa kike na ndiyo maana tunawataka watoe taarifa za watu wanaotaka kuwakwamisha kimasomo kwa watendaji wa vijiji kwenye maeneo yao.
Alitoa agizo hilo wakati akizungumza kwa nyakati tofauti na wakazi wa wilaya ya Masasi akiwa katika siku ya kwanza ya ziara yake ya kikazi mkoani Mtwara.

Waziri Mkuu alisema watoto wa kike wanatakiwa kuheshimiwa katika jamii kwa kuachwa waendelee na masomo yao bila ya usumbufu wa aina yoyote na atakayebainika kukatisha masomo atachukuliwa hatua kali za kisheria.

Alisema Serikali itatoa adhabu kali ya kifungo cha miaka 30 jela kwa mtu atakayekatisha elimu ya mtoto wa kike iwe kwa kumuoa, kumpa ujauzo na hata ukikutwa naye nyumbani kwako, katika nyumba ya wageni.

“Tukikukuta na binti wa shule katika kona isiyoeleweka tunakukamata na kukuchukulia hatua za kisheria. Ole wenu vijana, mkibainika mmewapa mimba mabinti wanaosoma, adhabu yake ni miaka 30 jela.”

Waziri Mkuu alisema kwa wazazi au walezi watakaowaozesha watoto kike ambao bado wanafunzi na kwa upande wa wazazi watakaomsindikiza mtoto kwenda kuoa mwanafunzi wote watachukuliwa hatua za kisheria.

Pia Waziri Mkuu alitumia fursa hiyo kuwataka wanafunzi wote kusoma kwa bidii ili watimize ndoto zao na wasikubali kushawishika kwa sababu watashindwa kufikia masomo yao

Baada ya Tetesi Chirwa Anakwenda Simba, Yanga Yajibu Mapigo

$
0
0
Tayari tetesi zimeanza kuzagaa kwenye mitandao ya kijamii na baadhi ya vyombo vya habari vimeripoti kwamba, mshambuliaji wa Yanga Obrey Chirwa huenda akajiunga na ‘Wekundu wa Msimbazi’ Simba mara baada ya kumaliza mkataba wake na yanga ambao kwa sasa unaelekea ukingoni.

Mwenyekiti wa usajili na mashindano Hussein Nyika amekanusha tetesi hizo kwamba si za kweli huku akisisitiza Chirwa haendi popote labda kama Yanga wataamua kuwachi lakini si vinginevyo.

“Hawezi kwenda sehemu yoyote isipokuwa hadi sisi tutakaposema nenda lakini kama bado tunamuhitaji, hawezi kwenda sehemu yeyote”-amesema Hussein Nyika ambaye ni mwenyekiti wa usajili ndani ya Yanga.
“Niwatoe wasiwasi wapenzi na wanachama wa Yanga kwamba, mchezaji ambaye yupo Yanga si dhani kama anaweza kuondoka kwenda sehemu yoyote labda hadi Yanga watakapoamua aondoke lakini kama bado wanamuhita

Watu 9 Wauawa Baada ya Binti Kufuata Dini ya Mpenzi wake

$
0
0

Taarifa kutoka Nigeria ni kwamba watu 7 wamefariki dunia na wengine 15 kujeruhiwa vibaya baada ya kutokea vita Kaskazini Magharibi mwa Nigeria baada ya binti mmoja wa Kikristo kubadili dini na kuwa Muislamu.

Tukio hilo lililotokea katika Jimbo la Gwari ambapo binti huyo aliamua kujiunga na dini hiyo ya Kiislamu kutokana na ushawishi wa mpenzi wake, jambo lililosabisha hasira kwa vijana wengine wa Kikristo na kuanza kufanya vurugu na kuanza kuchoma moto nyumba.

Kamanda wa Polisi kwenye eneo hilo Muktar Aliyu ameliambia Shirika la Utangazaji la BBC kuwa mpaka sasa tayari wanawashikilia watu 10 wanaosemekana kuhusika na kisa hicho na uchunguzi zaidi unaendelea.

TFF imemfungia Kocha Miaka 5 Kujihusisha na Soka

$
0
0
Kamati ya maadili ya shirikisho la soka Tanzania TFF jana kupitia kwa afisa habari wa shirikisho hilo Cliford Ndimbo imetangaza kuwafungia miaka mitano kujihusisha na soka mwalimu Joseph Kanakamfumu na katibu wa Mvuvumwa FC Ramadhani Kimilomilo kwa kuwakuta na hatia ya makosa kadhaa llikiwemo kosa la kugushi leseni za wachezaji.

“Kamati ya maadili iliyokutana February 3 2018 pamoja na February 10 2018 pamoja na mambo mengine ilipitia na kutoa hukumu kwa watuhumiwa wa kugushi leseni za wachezaji”  Cliford Ndimbo>

Mtoto wa Miezi Minne Aibiwa Kanisani…ilikuwaje?

$
0
0
Jeshi la Polisi nchini Kenya linamshikilia Binti wa miaka 22 kwa tuhuma za kuhusishwa na wizi wa mtoto wa umri wa miezi minne wakati wako ndani ya kanisa katika Jimbo la Kirinyaga nchini humo.

Inaelezwa kuwa binti huyo alikutwa na mtoto huyo aliyepotea tangu Jumapili ya February 25, 2018 katika kanisa la Jesus Winner lililopo katika kata ya Mitheru. Binti huyo amekutwa na mtoto huyo katika Jimbo jingine la Nithi.

Kwa mujibu wa mama wa mtoto Fidelis Mugo, alimwacha mwanae amebebwa na rafiki yake alipoenda kushughulikia jambo nje ya kanisa na pindi aliporudi rafiki aliyeachiwa mtoto alisema kuwa kuna muumini mwingine wa kanisa hilo aliomba ambebe.

Muumini huyo alitafutwa kanisani hapo lakini hakupatikana na ndipo ikabidi taarifa itolewe polisi na jitihada za kumtafuta mwizi wa mtoto huyo zilipoanza kufanyika.

Hakika Mungu ni Muweza! Afya ya Wastara Juma Yaimarika, Aandaliwa Mapokezi Makubwa na Bongo Movies

$
0
0

Taarifa iliyotolewa Afisa Habari, Uenezi , Mahusiano na UMMA wa Chama Cha Waigizaji Kinondoni, Masoud Kaftany imewaomba wasanii na Watanzania kwa ujumla wao wajitokeze kumpokea Wastara kesho Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere, Dar.



TAARIFA KWA UMMA
Imetolewa
Tar : 26 /February/2018

YAH : MAPOKEZI

Chama Cha Waigizaji Kinondoni ( Tdfaa Kinondoni ) Kinapenda Kuwajulisha Wana-Filamu na Watanzania kuwa kutakuwa na mapokezi ya ndugu yetu na mwanatasnia mwenzetu, Bi Wastara Juma yatakayofanyika siku ya Alhamis ya tarehe 1 March, 2018 saa saba kamili mchana Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere Dar es Salaam.

Chama kinawajulisha na kuwaomba waigizaji na wadau wote wa tasnia ya filamu tujitokeze kwa wingi kumlaki muigizaji mwenzetu na mpendwa wetu Wastara Juma kwa furaha baada ya kufanikiwa katika matibabu yake nchini India katika Hospitali ya Saifee iliyoko Mjini Mumbai.

UMOJA NI NGUVU NA UTENGANO NI UDHAIFU – PAMOJA TUNAJENGA TASNIA YETU..

Mungu amtie nguvu na amzidishie afya njema, Amin.

Masoud Kaftany
Afisa Habari, Uenezi , Mahusiano na UMMA.
Chama Cha Waigizaji Kinondoni.


Jike Shupa adaiwa kufuga mateja wa Unga nyumbani kwake

$
0
0

BAADA ya hivi karibuni kufunguka kuwa, anamsaidia mdogo wa Mbunge wa Bunda Mjini (Chadema), Ester Amos Bulaya, Deus Bulaya aliyeathirika na matumizi ya madawa ya kulevya ‘unga’, muuza sura kwenye video za wasanii wa Bongo Fleva, Zena Abdallah ‘Jike Shupa’ amekumbwa na skendo nzito kwamba anafuga mateja (watumiaji wa unga) nyumbani kwake.

Habari zilizoifikia Za Motomoto News, ni kwamba Jike Shupa ambaye anaishi maeneo ya Mwananyamala Hospitali, Dar amekuwa akiwafuga vijana kibao walioathirika kwa unga ambao wanapatikana kwa wingi eneo hilo huku akiishi nao nyumbani kwake bila utaratibu.

“Jike Shupa anawafuga mateja wengi sana maana ana chumba maalum kabisa kwa ajili yao na wengi ni wale wanaotumia dawa kwa ajili ya kuacha unga (methadone). Watu wanadai kwamba kuna vitu anafaidika navyo kwani watu kama hao wakati mwingine wanapora na kumletea yeye kama mama yao,” alisema Hassan, jirani wa Jike Shupa.

Za Motomoto News ilizungumza na Jike Shupa kuhusu tuhuma hizo ambapo alisema ni kweli alikuwa akiwasaidia vijana wengi ambao walikuwa wanatumia methadone, lakini kwa sasa wamesharudi makwao.

“Si kweli kwamba wanapora, nilikuwa ninawasaidia, lakini wameshamaliza muda wao wa kunywa dawa wamerudi makwao,” alisema Jike Shupa.

Sababu Kwanini Wanawake Wengi Hawapendi Kutoka na Wanaume Wafupi

$
0
0
Kuna utafiti niliusoma siku moja kuhusu wanaume wafupi, na walisema wanaume wafupi wana mapenzi ya kweli na ya dhati kuliko wanaume warefu, kitu ambacho siwezi bisha sababu, wanawake wengi huwa hawapendi kutoka na wanaume wafupi kwahiyo inawachukua sana muda kupata mwenza na lazima wawapende na wawape mapenzi ya kweli wanawake zao ili wasiwaache  kwa sababu wanawake wengi wanapenda mwanaume  warefu na wengi wana mvuto kuliko wafupi.

Wanawake wengi wanapenda kutoka na wanaume ambao wamewazidi urefu hata kidogo, kuliko kuwa na mwanaume ambaye ni mfupi kuliko wao,wengi wanasema hii inaleta picha mbaya au muonekano mbaya wakiwa wanaongozana wanaita (not Marching), lakini kuna sifa nyingine za wanaume wafupi wanawake wengi wanasema zinawakera kama,

WIVU
Inasemekana wanaume wafupi wana wivu wa kupindukia na sio kama wanaume wengine warefu hawana wivu ila wao wivu wao unapitiliza kiasi cha kukera kwani wivu ukizidi sana ni kero katika mapenzi.

SIFA
Wanaume wengi wafupi wana sifa sana, kiasi cha kukera wanajisifia sana, na wanataka sana kuonekana, kama wapo eneo Fulani wakiingia sehemu mtajua kama kuna mtu kaingia sababu ya sifa zao na maneno yao japokuwa pia wana sifa moja ya kuwa wachechi sana.

GUBU
Hapa sasa ukichanganya na wivu ni balaaa maana mwanaume mwenye gubu ni zaidi ya mwanamke muongeaji, Gubu ni ile hali ya kukosoa kila kitu,kila kitu  kibaya, yeye haridhiki na chochote na hata utaonekana huwezi chochote akiwa karibu, hilo gubu au hata kama kila kitu kipo sawa atatafuta sababu ya kuongea tu.

Wanajidai Wanajua  kila kitu. ( Much know)
Much knows, hapa bwana unakutana na mtu  kila kitu anajua yeye, ni kero sababu akiwa mbele za watu atataka kila mtu ajue anajua nini kama inaongelewa siasa, mpira au mapenzi yeye fundi wa kila kitu, kitu ambacho kiukweli kinakera sana wakati mwingine.

MUONEKANO NA MVUTO
Wanawake wengi wasema wanaume wafupi hawana mvuto sana, kama wanaume warefu, kwahiyo hiyo ni moja ya sababu ya wao kutotaka kutoka na wanaume wafupi, japokuwa sio wanaume wote wafupi hawana mvuto.  Japokuwa inasemekana siku hizi hakuna anaeangalia urefu wako uzuri wako watu wanangalia sana mfuko wako tu, hayo ni maneno ya mitaani watu wanaongea. Mimi binafsi sijui kama ni hali halisi.

Twiga Stars kuchuana na Zambia michuano ya Afcon

$
0
0
Kikosi cha timu ya taifa ya wanawake (Twiga Stars).

Timu ya Taifa ya Wanawake(Twiga Stars) itacheza na Zambia katika mchezo wa kufuzu fainali za Africa kwa Wanawake zitakazochezwa Ghana baadaye mwaka huu.

Twiga Stars inatakiwa kucheza mechi zote mbili kati ya April 2 na April 10,2018 katika mchezo huo wa raundi ya kwanza.

Ngorongoro heroes kucheza na Dr congo fainali za africa

$
0
0

Timu ya Taifa ya Vijana chini ya miaka 20(Ngorongoro Heroes) imepangwa kucheza na DR Congo kwenye mchezo wa kutafuta tiketi ya kucheza fainali za Vijana za Africa zitakazochezwa Niger mwezi Novemba.

Mchezo wa kwanza utachezwa Tanzania kati ya Machi 30,31 na April 1,2018 na ule wa marudiano utachezwa Congo kati ya Machi 20,21 na 22.

Mshindi katika mchezo huo atacheza na Mali katika raundi ya pili itakayochezwa kati ya Mei 11,12 na 13,2018.

Mbowe,Viongozi wa Chadema waachiwa baada ya kuhojiwa kwa saa tano

$
0
0

Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe na viongozi wengine wac hama hicho wameachiwa kwa dhamana baada ya kuhojiwa Kituo Kikuu cha Polisi tangu saa 6:50 mchana

Viongozi hao walifika kituoni hapo leo Jumanne Februari 27, 2018 na kuachiwa saa 1:02 usiku, kuitikia wito wa polisi.

Walikwenda kituoni hapo baada ya Mbowe kumaliza mkutano wake na waandishi wa habari makao makuu ya chama hicho yaliyopo mtaa wa Ufipa, Kinondoni.

Mmoja wa mawakili wa viongozi hao, Frederick Kihwelo ameileza MCL Digital leo kuwa wote wameachiwa kwa dhamana kwa kutakiwa kuwa na mdhamini mmoja na kutakiwa kuripoti tena kituoni hapo Machi 5, 2018 saa 1 asubuhi.

Amesema viongozi hao walianza kuhojiwa saa 8:30 mchana, baada ya kufanya mazungumzo ya tuhuma zinazowakabili.

Februari 20, 2018 Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam iliagiza kukamatwa viongozi saba waandamizi wa Chadema akiwamo Mbowe.

Wito huo ulikuja siku chache baada ya tukio la kuuawa kwa mwanafunzi wa Chuo cha Taifa cha Usafirishaji (NIT), Akwilina Akwilini.

Akwilina aliuawa kwa kupigwa risasi akiwa ndani ya daladala eneo la Mkwajuni, Kinondoni jijini Dar es Salaam wakati polisi wakiwatawanya wafuasi wa Chadema waliokuwa wakienda ofisi za mkurugenzi wa Halmashauri ya Kinondoni kudai viapo kwa mawakala wao.

Viongozi wengine waliohojiwa sambamba na Mbowe ni  naibu makatibu wakuu, John Mnyika (Bara) na Salum Mwalimu (Zanzibar).

Pia, wamo mwenyekiti wa Baraza la Wanawake Chadema (Bawacha), Halima Mdee; mwenyekiti wa Kanda ya Serengeti, John Heche na Esther Matiko ambaye ni mweka hazina wa Bawacha.

Mdee, Matiko, Heche na Mnyika walisharipoti awali na walitakiwa kurejea kituoni leo. Viongozi wengine waliwakilishwa na wanasheria.

Katibu Mkuu wa chama hicho, Dk Vicent Mashinji  hakwenda polisi kwa kuwa yupo nje ya nchi.

Tahadhari Kwa Wadada Mnaopenda Kuvaa Shanga Kiunoni...

$
0
0
Bwana Yesu asifiwe!!!

Wanawake wengi wanapenda kuvaa shanga kiunoni wakiamini zinawavutia wanaume wengi katika mapenzi.

Napenda kutoa tahadhali kwa wanaopenda kuzivaa hasa kiunoni kuwa asilimia 80% ya shanga zinazouzwa zikiwa zimeshasokotwa zinatengenezwa na waganga WA kienyeji au watu ambao ni mawakala WA shetani na kuzinuizia mapepo kwa malengo yafuatayo:


Kuharibu au kuiba nyota za watu
Kuwafunga wanawake uzazi
Kuwaunganisha na mtandao WA kuzimu
Kuvuruga mfumo WA hedhi WA wanawake
Kuwafanya wanawake kuwa makahaba, kwa sbb unatamani kukutana na wanaume wengi ili wakujue km unavaa shanga na unazitumia
Kuwafunga kimafanikio
Kuwafanya wasidumu kwny ndoa wanapoolewa.
Kuwafanya wafikirie ngono zaidi.


Sasa unaweza usinunue kwa mganga lakn aliyetengeneza ni mganga au agent WA shetani.

Ww unaweza kununua kwa MTU na ukamwona WA kawaida, au yeye anaeuza yamkini hajui lakn alyetengeneza alikuwa na kusudi.

Unahitaji kuwa makini sana Dada zangu na vitu vinavyovaliwa sirini.

Ni unaponunua ukazikomboa kwa damu ya Yesu ili kufuta Yale maagano na manuizo yalyoambatanishwa nayo.

Nami ninazikomboa kwa mamlaka ya Jina la Yesu kwa yeyote mwenye nazo nafuta manuizo yote kwa Damu ya Yesu, km unazo TYPE AMEN.

By Illovo

Ukiona Mwanaume Ana Miaka 27 Bado Hajajitegemea Huyu ni Hasara

$
0
0
Sifa ya mwanaume kujituma, kutafuta pesa na kujipanga. Hivi unakuta kijana umri unaenda bado anategemea kwa wazazi msosi ni hotpot family huyu ni hasara.

Kuna mwanaume mpaka anaoa bado yupo kwa wazazi na mke anampeleka hapo hapo kwenye nyumba ya familia, ndiyo hapo ndoa inakua ngumu kwa mawifi na mashemeji na wazazi zinaanza chokochoko kibao. Wanaume wa hivi ni walaini sana, hadi kitandani ni walaini.

Wapo sana wanaume wa hivi ila kiukweli mwanamke anavutiwa na mwanaume mgumu yaani anayejua kuhangaika na kujitegemea. Hawa wanategemea hadi siku ya ndoa wapewe zawadi ya kiwanja, au nyumba na wazazi. Wanataka sofa, kitanda, vyombo vya ndani siku ya harusi.

Shosti ukiona mwanaume wa hivi shituka mapema ni mwanaume Hotpot Family....
Viewing all 104756 articles
Browse latest View live




Latest Images