Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104785 articles
Browse latest View live

Mpasuko Mkubwa Ndani ya Kundi la Vichekesho Origina Comedy, Yadaiwa Kila Mtu Yupo Kivyake

$
0
0
Hakuna ubishi kua miaka michache iliyopita kund la Orijino Komedi ndio lenye mashabiki wengi hapa nchini. Ilikua ikifika mda wa kurushwa kipindi kila mtu alikua hangoki katika TV yake. Umaarufu wao uliongezeka zaid pale walipohama EATV na kuhamia TBC.

Umaarufu wao uliendelea kuwepo hadi siku za karibuni ambapo ulishuka kwa kasi sana, taarifa ambazo Bongoclan tumezipata ni kua kwa sasa kundi hilo limevunjika na kila mtu anafanya kazi kivyake. Chanzo chetu kutoka kituo cha TV walichokua wakifanya kazi kiasema kua kwa sasa kila mtu ana hamsini zake na hawafanyi kazi tena pamoja.


Kwa Habari na Picha zaidi Ingia Hapa INSTAGRAM

Diamond Platnum Amla Denda Wema Sepetu Live Live Mwanza Rock City

$
0
0
Yeah Huyo Ni Diamond Platnumz a.k.a Dangote Akifanya Yake Na Madame Wema Sepetu... Love Is In The Air

Kwa Picha zaidi Ingia Hapa: INSTAGRAM

Wema Sepetu Uso Kwa Uso na Jokate Mwegelo Ndani ya Ndege, Hicho Ndicho Kilichotokea

$
0
0
Jokate aliwahi kukiri kwenye exclusive na millardayo.com kwamba aliwahi kuwa na uhusiano wa kimapenzi na Diamond kwa muda usiozidi miezi miwili ambapo wakati yuko na Diamond zilitoka stori nyingi pia kuhusu uhusiano wa Wema na Jokate kuingia matatizoni.
Ni stori ambazo ziliandikwa sana na inawezekana mpaka leo watu wengine walikua wanaamini Jokate na Wema hawawezi kukaa meza moja ila Aug 9 2014 Wema Sepetu baada ya kuwasili Mwanza kwa ajili ya show ya Serengeti Fiesta 2014 baadae CCM Kirumba amepost hii picha.

Wakiwa kwenye ndege ya Fastjet Wema na Jokate wakitokea Dar es salaam walipiga selfie ambayo Wema ameipost kwenye instagram page yake na kuandika hayo maneno hapo chini akimaanisha wako poa sasa hivi.

Mwanamke Mmoja Nchini Brazil Amegundua Mumewe Waliyeishi Pamoja Miaka 15 ni Kaka Yake wa Damu

$
0
0
A woman went in search of her long-lost mother - and discovered she has unknowingly married her own brother.

Adriana, 39, and her husband Leandro, 37, have been together for seven years and have a six-year-old daughter.

The Brazilian couple - who didn't want to reveal their surnames - spent their lives trying to find their respective mothers, who were both called Maria, and had both abandoned their children when they were still babies.

But neither ever imagined - until this week - that the women they had both been searching for could have been the same person.

Adriana, a cosmetics saleswoman, hadn't seen her mother since she was just one, when she left home leaving her to be raised by the girl's father.


Meanwhile, truck driver Leandro found out aged eight that his own mother had also abandoned him, and that the woman he knew as his mum was actually his step-mother.

While Leandro stayed in the same town where he was born in the state of Sao Paulo, southeast Brazil, Adriana moved away to work as a housemaid, was married for 15 years and had three children.

The pair met for the first time ten years ago after Adriana's marriage broke down and she moved back to her home town, and they soon fell in love and moved in together.
Discovery: They were both abandoned as infants and spent their lives searching for their mothers called Maria

Discovery: They were both abandoned as infants and spent their lives searching for their mothers called Maria 
Related: Father-daughter couple describe their relationship

Still unable to forget the give up the search for her mother, last month Adriana decided to contact a a radio station in their town to ask for help - and this week the two were reunited live on air.

But at the end of the interview on Radio Globo's 'The Time Is Now' programme, which specialises in finding lost relatives, the mother revealed she also had a son who didn't know her, Leandro.
GENETIC SEXUAL ATTRACTION: HOW ESTRANGED RELATIVES CAN MISTAKE KINSHIP FOR ROMANCE

A phenomenon called genetic sexual attraction can occur when estranged relatives meet for the first time as adults.

Feelings of intense intimacy can be confused as the brain struggles to associate each other as family.

When families grow up together, an inherent taboo is created which desensitises them to sexual attraction.

It is known as the Westermarck effect but is missing from relatives who do not know each other.

As it becomes clear that it is the same Leandro that she was married to, Adriana is heard weeping uncontrollably: 'I don't believe that you're telling me this. Leandro is my husband,' she sobs.

At the end of the interview she says: 'Now I'm scared to go home and find out that Leandro doesn't want me any more. I love him so much.'

Adriana and Leandro - who never married legally - yesterday told Radio Globo that they would stay together, despite the bombshell that they are actually brother and sister.

Adriana said: 'Only death is going to separate us. All this happened because God wanted it to happen.

'Of course it would have been different if we had known all this before, but we didn't and we fell in love.

'We thought it was funny that both our mothers had the same name, but it is a common name so we just thought it was a coincidence.

'At first we were really knocked by it all. But we had a family meeting and told everyone that we are going to stay husband and wife, whatever anyone might think.

'We have so many plans together, nothing's going to break us up, nothing.'

The couple said they don't blame their mother for leaving them, have spoken with her a number of times since and plan to meet up soon.

Haya Ndiyo Mavazi Wanayovaa Wahudumu wa Ndege Kujikinga na Ebola

$
0
0


Ugonjwa wa Ebola umelipuka sana huko Africa magharibi na umeua watu wengi sana. Hivi sasa mambo mengi yanafanywa ili kukinga watu dhidi ya maambuzi mampya.
Njia moja wapo ni kutenga na kulifunga eneo lolote ambalo lina mgonjwa wa Ebola. Lakini hivi ndivyo wafanyakazi wa ndege za Africa magharibi wanavyovaa ili kujikinga.

Dr Slaa :Wabunge wa Chadema Walioenda Bunge La Katiba Tulisha Wapuuza

$
0
0
Akiongea kuhusu wabunge wachama chake kuingia bunge la katiba, kupitia redio one katibu mkuu wa CHADEMA amesema wote walioenda kwenye bunge la katiba walishapuuzwa na chama mda mrefu.
Amesema adhabu sio lazima iwe ya wazi hata kupuuzwa ni adhabu pia.

Wamponda na Kumkejeli First Lady Wetu Alivyo Vaa Us Africa Summit

$
0
0
Kuna kipindi nakiangalia kwenye television ya Kenya the citizen kipindi kinaitwa fashion watch hiki kipindi kilikuwa maalum kwa jinsi maraisi wa Africa na wake zao walivyovaa na jinsi walivyo pozi kwenye picha , moja ya ma judge alikuwa yule Ian ambaye huwa ana judge kwenye shindano la uimbaji la project fame nilijisikia vibaya pale waliposema kuwa first lady wetu amevaa kama anakwenda msibani huku wanacheka dah noumah kweli

Angalia Jinsi Diamond Platnumz Alivyoiteka Mwanza kwenye Fiesta

$
0
0



Fiesta ilianza kunguruma Jana kwenye viwanja vya CCM Kirumba ambapo mkali wa Bongofleva Diamond Platnumz alifanya vitu vyake . Hizo ni baadhi ya picha za hiyo show Jana

Bonyeza hapa Kwa picha zaidi : INSTAGRAM

Binti Huyu Mrembo Anatafuta Kazi ya Secretary wa Boss Yupo Radhi Kufanya Kazi Mpaka Weekend

$
0
0

Huyu ndio Secretary Mitego.......Anaitwa LINDA...anatafuta kazi, anauzoefu wakutosha katka kumuhudumia bosi kuanzia chai ya ofisi hadi kumbebea koti la suti....Mtunza siri, mwaminifu mwenye kujitoa hadi siku za weekend na siku kuu...Siku zote anaamini bosi wake ndio kazi yake hivyo yupo tayari kujitoa kwa namna yoyote ili BOSS wake aridhike!!!...Ameambatanisha na picha hizi katika kujazia CV yake....ANAOMBA KAZI JAMANI...wasiliana nasi kupitiaemail yetu au comment hapo chini.

Wanasiasa wa Tanzania Igeni Mfano Huu wa Zito Kabwe

$
0
0
Katika kuonesha ukaribu na vijana na utayari wa kutoa msaada wa hali na mali, Mbunge wa Kigoma Kasikazini Mh Zitto Zuber Kabwe amemtungia mashairi msanii wa muziki wa Bongo fleva hapa Tzee Linex Sunday Mjeda, ambaye kwa sasa kitaa anahit na single ya ‘Honga honga’.

Ngoma aliyotungiwa na Mh Zitto inategemea kutoka hivi karibuni pamoja na video yake inayo kwenda kwa jina la ‘Wema kwa Ubaya’ ngoma ambayo imetengenezwa na Maproducer 3 Mo fire Monagangstar &Tuddy Thomas. Video imetayarishwa na Adam Juma. linex amedhibitisha hilo leo wakati mwandishi wa BK alipo mcheki hewani “Nikweli wimbo wa ‘Wema Na Ubaya’ kuna mashairi kanitungia Mh Zitto Kabwe na itatoka na video yake hivi karibuni”

Kwenu Wanawake: Kinachowapa Raha Ni Ukubwa wa Dushelele Au Ufundi Wa Mwenye Dushe?

$
0
0

Nimekuwa nikifuatilia comments za wadada wengi humu, naona wengi wao wanakandia vibamia, lakini timu vibamia nao wanakuja juu wakidai ufundi ndio muhimu. Sasa je ni kweli ufundi ndio muhimu kuliko ukubwa wa mtwangio?

Nyani Aliyejipiga Picha Azua Mgogoro

$
0
0
Mtandao wa Wikipidia umekataa kufuta picha ambayo Nyani ilijipiga ikisema kuwa kwa sababu picha hiyo ilipigwa na Nyani ambaye ni mnyama wala sio binadamu, basi inakuwa mali ya umma.
Hii ni baada ya mpiga picha, mmiliki wa kamera iliyotumika na Nyani huyo kujipiga picha, kusihi Wikipedia kufuta picha hiyo na kudai kuwa Wikipedia ilikuwa inaingilia haki zake za umiliki wa picha hiyo.
Mpiga picha, David Slater, alikuwa akijaribu kunasa picha za Nyani kwa masaa kadhaa, wakati ambapo Nyani mmoja alichukua mojawapo ya kamera za David na kujipiga mamia ya picha.
Picha hiyo aliyojipiga Nyani bila shaka ni ya kusisimua na imempeleka David kuwa maarufu ulimwengu mzima.
La kusikitisha ni kuwa hatimaye Slater sasa amejipata katika mvutano wa kisheria na Wikimedia kuhusiana na ni nani hasa mmiliki wa picha hiyo.
David, ambaye hutegemea upiga picha kama jinsi moja ya kujikimu kimaisha, yuko makini kuhakikisha picha hiyo imeondolewa kwa tovuti ya Wikipedia mara moja, huku Wikipedia ikidai kuwa iwapo kuna mmliki wa picha hiyo basi ni Nyani aliyejipiga picha hiyo.
Mvutano wa kisheria ilirejelewa kuangaziwa kufuatia uamuzi wa Wikipedia kuchapisha maombi yote iliyopata kuhusu kufuta au kuhariri habari au picha au video zozote ilizoweka kwenye tovuti zao.
Mojawapo ya maombi hayo ni David Slater kutaka picha aliyojipiga Nyani kuondolewa kwenye tovuti ya Wikipedia mara moja kwani ikiwa kwenye tovuti hiyo iko wazi kwa umma.

Ndege Nyingine Yaanguka na Kuwaua Abiria Wote Walio Kuwa Ndani

$
0
0
Ndege moja iliokuwa na abiria 40 imeanguka mjini Tehran nchini Iran.
Runinga ya taifa la Iran imesema kuwa abiria wote wamefariki .

Ndege hiyo ya kampuni ya Taban Air imeripotiwa kuanguka katika makaazi baada ya kupaa kutoka uwanja wa ndege wa Mehrabad Maghribi mwa mji wa Tehran.
Ndege hiyo inayojulikana kama Iran 141 ilitengezwa nchini Iran kupitia teknologia ya Ukraine.
Uchunguzi umeanzishwa kuhusu ni nini kilichosababisha ajali hiyo.
Iran imekabiliwa na ajali kama hizo katika siku za hivi karibuni kutokana na ndege zake zilizozeeka mbali na marekebisho mabaya inazozifanyia.

Angalia Picha za Samaki Mtu Aliyekutwa Pembeni ya Bahari..Nilikuwa Siamini Kama kuna Viumbe Hawa

$
0
0

Habari zilizotufikia, Samaki Mtu ama Nguva ni Samaki adimu kabisa duniani kumtia machoni ameonekana amefariki ama amekufa pembeni mwa ufukwe wa bahari huko BENIN, Ujerumani. Kama ulidhani ni hadithi za kuhadithiwa tu ujue hivi vitu vipo na vinaishi!!

Wananchi Wawataka Wanasheria Kuweka Pingamizi Mahakamani ili Bunge Maalum la Katiba Lisitishwe

$
0
0
Wengi wa wananchi wamekuwa wakilalamika sana kuhusu mwenendo wa Bunge la Katiba kuendelea ili hali ukweli ni kuwa kundi la wanaotetea maslahi halisi ya Wananchi (UKAWA) hawapo na pia mwenendo wa kuwatisha wanaotoa elimu na maudhui ya Rasimu ya 2 ya Katiba, kupitia vyombo vya Habari na midahalo, ufahamu ambao ni haki ya kila raia. 

Mitaani, watu wengi wanakasirika pia kuwa Taasisi ya kutetea haki za Binadamu (TLHRC) na Jukwaa la Katiba (JUKATA) kuendelea kutokuchukua hatua za kusheria, ambavyo wanasema ni ishara mbaya na kuwa wanaachia watawala waendelee kufanya wapendavyo kuunda katiba yao kwa kupitia wingi wao na kwa kumtumia Spika ambaye ameshindwa kuwa na dira ya kitaifa. 

Wengi wanatoa maneno ya hasira wakisema kuwa ..."kama Legal and Human Rights Centre (LHRC) mnao uchungu halisia kama tujuavyo, na jinsi walivyoonyesha wajumbe wenyewe wa Tume ya Warioba, tunaomba pamoja na timu ya JUKATA mpeleke 'zuio' mahakamani kuhakikisha kama yafaa Mahakama ilazimishe yafuatayo ili kufanya Bunge la Katiba lizingatie maslahi mapana ya utaifa na sio vikundi: 

Kuamuru Bunge la Katiba Kusitishwa kwa muda ili kuruhusu Wajumbe wote wa Katiba kama walivyoaninishwa ktk sheria kuwepo ndani ya Bunge hilo ili kulinda usawa na haki ya kila mwakilishi.
Kuzuia utekelezaji wa sheria iliyoaifuta tume ya Kutunga Katiba ili iendelee kuelimisha Bunge maana na maudhui ya Rasimu ya pili ili taifa lipate ufahamu unaostahili.
Kuamuru Serikali kuufungua Mtandao wa Tume ya Katiba uliofungwa ili kuwapa wananachi wote uhuru na uwezo wa kupata ufahamu wa mengi yaliyozuiwa wasiyajiue baada ya tovuti hiyo kufungwa.
Kutoa kinga kwa Vyombo vya Habari vinavyolenga kuendesha mijadala ya Wazi katika kuelimisha wananchi kuhusu maudhui ya ufahamu wa Rasimu ya 2 ya Katiba ili waweze kujiandaa kwa ufahamu ufaao kuelekea upigaji wa Kura kama hatua hiyo itafikiwa.
Kutoa tafsiri Kamili ya misingi ya Rasimu kulingana na sheria ya Katiba, na kuhakikisha misingi yake mikuu ya Rasimu ya 2 (ambayo yanatokana na maoni ya Umma) haiguswi au kumomonyolewa au kuvurugwa kwa hila na makundi ya wachache wanaoongozwa na Spika.
Kutoa kinga kwa waliokuwa wajumbe wa iliyokuwa Tume ya Katiba waendelee kuelimisha wananchi ktk makongamano ya wazi na kuwaongezea ufahamu zaidi maana Rasimu hiyo ndio msingi wa Katiba yao waliyoiomba kwa miaka zaidi ya 30."


Kama TLHRC na JUKATA wanaipata hii, watoe 'what's next' ili wananchi wajue hatma ya haki na maoni yao, ili isiwe too late, na kuwa endapo itaachiwa Katiba itakayoundwa na wachache ikamilike, itakuwa ndio msingi na chanzo cha matatizo makubwa zaidi kitaifa ambayo yangeweza kuwekwa sawa na mahakama mapema kwa sasa! 

Nawasilisha.

Baada ya Gwajima Kununua Helikopta, Askofu Kakobe Ameyasema Haya.

$
0
0
Kama sehemu ya vyanzo vyako vya habari ni mitandao kama vile website, blogs, facebook, twitter na Instagram inawezekana hii stori ya Gwajima ambae ni Muhubiri wa Injili kununua Helikopta uliiona hata zaidi ya mara moja.
Hata hivyo Muhubiri mwenzake Askofu Zacharia Kakobe Aug 10 2014 amenukuliwa na gazeti la Nyakati na kuizungumzia hiyo Helikopta akisema ‘kitendo cha Gwajima kununua helikopta kwa ajili ya kazi zake za Injili kinastahili kufurahiwa na Wakristo wote wa kweli, tujifunze kupongezana.. nampongeza sana’
Kumiliki kwake Helikopta kutachangia katika kufuta dhana potofu ambayo imedumu kwa muda mrefu ya kuyaita Makanisa ya kilokole…. makanisa ya vichochoroni, Helikopta sio starehe na hata muundo wake sio wa starehe bali ni kazi, itamwezesha pia kufika maeneo ambayo gari sio rahisi kumfikisha kutoa neno la Mungu’ – Kakobe

Kuhusu Askofu Kakobe kununua Helikopta yake, amesema >>> ‘mimi sio mtu wa mashindano na pia kila mtu anakwenda sawa kutokana na ono aliloitiwa, haya sio mambo ya kushindana… hicho ndicho kinacholeta shida mara kwa mara, Gwajima ana Helikopta ni kwa manufaa ya Ufalme wa Mungu, mimi nina chakwangu ni kwa utukufu wa Mungu, hakuna haja ya kuigana’

AIBU! Baba Mzazi Ampachika Mimba Binti Wake wa Miaka 17

$
0
0
MKAZI wa Kijiji cha Bwekela wilayani Igunga mkoani Tabora, Kashinje Shima, anatafutwa na Uongozi wa kijiji hicho, kwa kumpa ujauzito mwanawe wa kumzaa mwenye umri wa miaka 17.
Ofisa Mtendaji wa Kijiji cha Bwekela, ambaye pia ni Kaimu Ofisa Mtendaji wa Kata ya Igoweko, Robert Ruhende, alilaani kitendo kilichofanywa na mzazi wa mtoto huyo na kusisitiza kuwa sheria lazima ichukue mkondo wake.

Akisimulia kisa hicho, mke wa mkazi huyo ambaye pia ndiye mama mzazi wa mtoto huyo, Geni Njiro, alidai alibaini hali hiyo Julai 23 mwaka huu, baada ya mwanawe wa kiume kumfumania baba yake na dada yake.

Kwa sasa kwa mujibu wa Geni, mwanawe huyo ambaye inadaiwa amekiri kushiriki kitendo hicho, ana ujauzito wa miezi saba.

Geni alidai kabla ya kugundua kitendo hicho cha kinyama kilichokuwa kikifanywa na mumewe, alihisi kuwa baba wa mtoto huyo alikuwa akitumia mwanya wa yeye mama kutokuwepo nyumbani, kufanya vitu visivyo vya kawaida.

Alidai kuwa alipata hofu kuhusu mwenendo wa mumewe na mtoto wake siku moja walipokuwa shambani wakiendelea na shughuli za kuvuna mazao, ambapo mumewe aliaga kurudi nyumbani.

Kutokana na hofu hiyo, Geni alidai aliamua kumtuma mtoto wake mkubwa wa kiume, ambaye hakutaka kumtaja jina, akafuatilie nyumbani kupata uhakika wa kile alichokuwa akihofia.

Mama huyo alidai baada ya mtoto wake huyo kufika nyumbani, ndipo alikuta baba yake wakifanya ngono na mdogo wake na kurudi shambani na kumpa taarifa mama yake.

Baada ya taarifa hiyo, mama huyo alidai kuwa aliamua kuita ndugu wa pande zote mbili, kwa ajili ya kuzungumzia unyama huo, ambapo baba huyo alipohojiwa katika kikao hicho cha familia, alikana kuhusika na tuhuma hizo.

Hata hivyo, mama huyo alidai babu wa mtoto huyo, alishauri waende kupima hospitali kupata ukweli, ndipo baba huyo alipokubali kuwa anatembea na mtoto wake.

Baada ya kukubali, inadaiwa baba huyo alitakiwa kulipa adhabu ya faini ya ng’ombe wawili, ambao aliwalipa na suala hilo kuwa limekwisha. Mwenyekiti wa Kitongoji cha Mwina, Bundala Makelema, alikiri kuwepo kwa suala hilo.

Alidai kuwa wakati mtuhumiwa huyo akilipa adhabu ya kimila ya ng’ombe wawili, yeye alishiriki kwa nafasi yake ya Kiongozi wa Kitongoji.

Hata hivyo, inadaiwa familia anayotoka mama huyo, ilipinga uamuzi huo wa kifamilia na kumruhusu ndugu yao, kuchukua hatua zaidi, ikiwemo kutoa taarifa katika vyombo vya habari.

Taarifa hiyo ilipofika kwa Ofisa Mtendaji wa Kijiji cha Bwekela, ambaye pia ni Kaimu Ofisa Mtendaji wa Kata ya Igoweko, Ruhende ambaye aliahidi kwenda Polisi ili hatua zaidi zichukuliwe, mama huyo alidai ndipo mumewe alipoamua kutoroka nyumbani na kwenda kusikojulikana.

Jack Patrick Ayeyuka Gerezani Huko Macau China Alipokamatwa Kwa Madawa ya Kulevya

$
0
0
Stori:  Shakoor Jongo

Nini kinaendelea? Video Queen wa Bongo anayeshikiliwa na jeshi la polisi nchini China kwa msala wa madai ya kukamatwa na madawa ya kulevya ‘unga’, Jacqueline Fitizpatrick Cliff ‘Jack Patrick’ anadaiwa kuyeyuka gerezani.

Kwa mujibu wa ‘mtu wetu’ aliyeambatana na rafiki zake Jack kwenda kumuona gerezani, Macau, Hong Kong nchini humo, walijikuta wakipigwa na butwaa kuambiwa hakuna mtu kama huyo gerezani hapo hivyo kuibua hofu kuwa huenda amenyongwa.

Uchunguzi wetu gerezani hapo ulibaini kwamba tofauti na hofu ya rafiki zake, kuna uwezekano Jack amehamishiwa gereza lingine lililopo nje kidogo ya Mji wa Macau.Chanzo chetu hicho kilidai kwamba habari za ndani zilieleza kwamba Jack amehamishwa gereza hivyo kwa maelezo zaidi watu wanaokwenda kumtembelea waende kwenye ofisi za gereza hilo alilokuwa awali watapewa maelekezo wapi alipo mtu wao.

“Unajua watu wanaokwenda kumtembelea Jack gerezani ni Watanzania walioko huku China kwa shughuli maalum hasa za sanaa, kama vile sarakasi au maigizo, wengine wote wanaogopa, wanajua wanaweza kukamatwa.

“Tulipokwenda na mazagazaga yetu tuliambiwa Jack amehamishwa gereza na inaonekana aliomba mwenyewe ila hatujui ni kwa nini alifanya hivyo,” kilisema chanzo hicho.Hivi karibuni Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje, John Haule alitoa taarifa na kutaja jumla ya watuhumiwa waliokamatwa kwa kesi za madawa ya kulevya ambapo alisema kuwa kuna Watanzania wengi wapo kwenye magereza mbalimbali China.

“Katika magereza ya China hadi Februari (mwaka huu) tulipewa taarifa kwamba wapo Watanzania 177 magerezani na kati ya hao 15 wamehukumiwa kunyongwa kutokana na baishara hiyo ya madawa ya kulevya,” ilisema taarifa hiyo ya katibu mkuu.

Jack alikamatwa Macau, Hong Kong, mwaka jana hivyo kesi yake inaendelea kuunguruma. Tofauti na Beijing ambao huwa wananyonga watu wanaojishughulisha na unga, Hong Kong ni kifungo cha miaka kadhaa tu.

Imevuja Eti Kumbe Ney wa Mitego Ndio Mdudu kwenye Ndoa ya Wema Sepetu na Diamond

$
0
0
IMEVUJA kwamba Staa wa Bongo Fleva, Emmanuel Elibariki ‘Nay wa Mitego’ ndiye aliyemshauri Nasibu Abdul ‘Diamond’ asioe kwa sasa ili asishuke kimuziki.

Ushauri huo umekuwa mwiba kwa mpenzi wa Diamond, Wema Sepetu ambaye amekuwa na ndoto ya kuolewa na staa huyo anayekimbiza kitaani na wimbo wake wa Mdogomdogo.

Akifafanua zaidi kuhusiana na ushauri huo, Nay alisema: “Kuna mifano mingi sana nimeiona kutoka kwa wasanii ambao wameoa, wengi wao wameshasanda sasa mdogo wangu (Diamond) na yeye alipoleta hoja ya kutaka kuoa nikaona sasa anatafuta shimo la kwenda kujifukia, nikamshauri aache.”

Kumbe Manyaunyau ni Tapeli: Shahidi Aelezea Jinsi Walivyotapeliwa Sh 29.6 Mil na Mganga Huyo

$
0
0
Dar es Salaam, Shahidi wa pili katika kesi ya kujipatia Sh29.6 milioni kwa njia ya udanganyifu inayomkabili mganga wa jadi, Dunia Salumu (37) ‘Manyaunyau’ amedai kuwa walilazimika kuuza kiwanja na nyumba ya urithi kutafuta fedha za kununua mabeberu saba na mafuta ya ngamia ili kumpa mganga huyo kama masharti ya kumfufua ndugu yao aliyefariki dunia.

Manyaunyau alifikishwa kwa mara ya kwanza katika Mahakama ya Wilaya ya Ilala, Desemba mwaka 2013 akikabiliwa na shtaka la kujipatia fedha hizo kutoka kwa Tecla Modest.

Akiongozwa na Mwendesha Mashtaka, Nassoro Katuda shahidi huyo, Diana Steven (26) alidai kuwa baada ya kumaliza matanga ya mjomba wake, Saimon Modest aliyefariki mwaka 2008, wakiwa nyumbani Mchikichini, Dar es Salaam walisikia sauti ya mtu ikisema kuwa ‘mimi sijafa’.

Wakati Diana akiendelea kutoa ushahidi huo mrefu, Hakimu Wilberforce Luhwago, alimkatisha akieleza kuwa ameisikiliza kesi hiyo kwa muda mrefu na kuna nyingine za kusikiliza, hivyo itaendelea Agosti 13, mwaka huu.

Ushahidi wenyewe

Alisema siku tatu baada ya mazishi ya mjomba wake, ndugu yao aitwaye Hamisi akiwa na Manyaunyau walifika nyumbani kutoa pole na walipofika Manyaunyau alidai kuwa marehemu hajafa, bali ameuawa na kaka yake na amechukuliwa na Mpemba kwa ajili ya kwenda kuuza duka.

“Mimi na mama zangu wawili tulishtushwa na kuhoji, mtu aliyekufa anaweza akawa hai?” alisema Diana katika ushahidi wake uliochukua saa nane.

“Baada ya hapo alituambia siku iliyofuata twende ofisini kwake (Manyaunyau), Mburahati, tukiwa na Sh100,000. Mama zangu walisema hawana, lakini ndugu yetu mmoja aitwaye Bright Steven alikwenda kwenye ATM na kuchukua Sh80,000 na safari ikafanikiwa,” alidai.

Diana alisema baada ya kupeleka fedha hizo, Manyaunyau aliwapangia kwenda siku nyingine, akiwataka kurudi wakiwa na kitambaa cheusi na walipokipeleka alisema alikichukua na kukifunika kikaanza kutoa sauti ya mtu mzima ikisema: “Karibuni sana wajukuu zangu na maelezo yote mtapewa na mwenyeji wenu.”

Alisema Manyaunyau pia aliwataka wapeleke chupa sita za mafuta ya ngamia wakiyakosa wampelekee Sh1.8 milioni. Alisema walimpelekea fedha hizo walizozipata kwa kuuza sehemu ya kiwanja walichorithi kwa mama yao.

“Siku tuliyopeleka hiyo hela pia tulipeleka mtama, jogoo mwekundu na tulipelekwa katika pori lililopo Kibamba na kila tulipokuwa tukienda kule Kibamba tulikuwa tunakodi teksi kwa Sh40,000,” alidai Diana.

Alidai kuwa kabla ya kufika katika pori hilo, Manyaunyau aliwaagizia soda wakanywa na baada ya kumaliza aliwaambia wapige makofi huku wakisema hodi hodi mkubwa!

“Tuliingia katika pori hilo saa 2: 00 usiku, tukaona mwanga kama radi imepiga na tukaona kitu cheupe kama mtu kafunikwa sanda... ile tuliyoipeleka kwa Manyaunyau siku chache kabla ya kwenda katika pori hilo.

“Alituambia mtu wenu ndiyo huyo ila msimfunue kwa sababu ni mchafu, akasema inatakiwa hela ya kununua mafungu mawili ya dawa ya kumsafishia.

Sisi hatukuelewa, ndipo alipotuambia siku iliyofuata twende ofisini kwake atufafanulie. Tulipofika alituambia anataka mbuzi saba madume na Sh2 milioni na kwenda naye tena Kibamba.

“Tukiwa porini hapo tulisikia sauti ya babu ikisema marehemu wenu ameshikiliwa na wachawi, wanataka damu ya mbuzi saba, hivyo tulirudi nyumbani na kwenda kuuza tena kiwanja kilekile kwa mtu mwingine na kupata Sh4.9 milioni na kuzipeleka kwa Manyaunyau kununulia mbuzi hao,” shahidi alidai na kuongeza kuwa ‘babu’ alizidi kuongeza madai, mara hii akisema anataka nguo, mkeka na chakula nyumbani kwa Manyaunyau.

“Baada ya kauli ya babu, tulipeleka chakula kwa Manyaunyau na hapo alituambia tujiandae kwa safari ya Majohe na huko tulikwenda mimi na mama zangu wawili na mke wa Manyaunyau na tulipofika tuliongea tena na ‘babu’ na kutuambia tutafute Sh2 milioni nyingine kwa ajili ya kumkomboa ndugu yetu.”

Waliporudi kutoka Majohe, alidai kuwa walikwenda kukopa kwa riba na Manyaunyau alisema fedha hizo wazifunge katika kitambaa cheusi na kuziweka katika ndoo na kuzipeleka katika Msitu wa Majohe.

“Tulipofika Majohe tulipiga makofi na kuziweka zile pesa na siku iliyofuata Manyaunyau alituambia tutoe Sh3.5 milioni kwa ajili ya kukanyagia na sisi tulizipelekea hukohuko Majohe.”

Alidai kuwa siku iliyofuata walikwenda ofisini kwa Manyaunyau na kuambiwa kuwa wapeleke chakula nyumbani kwake baada ya hapo waende kumwangalia mchawi aliyemchukua ndugu yao huko Kibamba eneo la makaburi.

“Tulipofika eneo hilo la makaburi alitokea mtu mrefu sana akiwa ameshikilia mkia na akapiga magoti na hapo hapo alitokea tena mtu mnene na kusema hamuwezi kumuona ndugu yenu kwa sasa.”

Diana alidai kuwa baada ya kuambiwa hivyo, ilisikika sauti ya ‘babu’ ikisema watafute Sh5 milioni nyingine.

“Tulivyosikia hiyo sauti ya ‘babu’ akisema tutafute ndugu zangu walisema hawana hiyo hela na sauti ya babu iliendelea kusema kuwa nyie leteni tu hiyo hela marehemu akija atailipa,” alieleza.
Viewing all 104785 articles
Browse latest View live


Latest Images