Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104785 articles
Browse latest View live

Mahakama Yamuamuru Shilole Kumlipa Mary Musa TZS 14M Kama Fidia ya Kutokuhudhuria Kwenye Show

$
0
0

Shilole aangua kilio baada ya mahakama kutoa hukumu kumtaka alipe million 14 za kitanzania kwa Mary Musa.

Mwaka 2017 katika mkesha wa Pasaka Shilole alilipwa mil.3 akatumbuize huko Mbagala lakini alishindwa kutokea kwa wakati hivyo mashabiki kupandwa na hasira na kuharibu Mali ukumbini Hapo.

Mary alifungua kesi kuomba alipwe fidia lakini Shilole akawa anapuuza wito wa mahakama.

Shilole ametakiwa kutoa pesa hizo ndani ya wiki moja la sivyo Mali zake zitashikiliwa.

Crediti: GPL

Urusi yajaribisha kombora jipya, Halina Ukomo wa Masafa na Linaweza Kupenya Kizuizi Chochote cha Makombora

$
0
0

Rais wa Urusi Vladimir Putin amesema jeshi lake limejaribisha silaha kadhaa mpya za nyuklia ikiwemo aina ya kombora ambalo halina ukomo wa masafa na linaweza kupenya ngome ya mfumo wowote unaokabiliana na makombora.

Alikuwa akizungumza na wabunge katika hotuba yake ya taifa kabla ya uchaguzi mkuu kufanyika Machi 18 nchini Russia. Putin atakuwa anatumikia awamu ya tatu kama rais na anatarajiwa kushinda na kuendelea kushikilia wadhifa wake kwa miaka sita.

Pamoja na kombora hilo, Putin amesema kuwa Urusi tayari imejaribisha kombora lake jipya ambalo linauwezo wa kufika katika mabara tofauti – linaloitwa Sarmat- ambalo ni la masafa marefu na lenye kubeba silaha nyingi zaidi kuliko lile la awali.

“Sarmat ni silaha yenye nguvu kubwa sana. Kutokana na maumbile yake hakuna mfumo uliopo wa kuzuia makombora unaweza kuwa ni kizuizi dhidi yake.”

Kiongozi huyo wa Urusi ameweka malengo ya kupunguza umaskini nchini Urusi kufikia asilimia 50 wakati wa kipindi kinachotarajiwa cha muhula wake unaofuatia na kueleza umuhimu wa kuendeleza technolojia ili kupeleka mbele maendeleo.

Vipaumbele vingine ambavyo amevigusia ni pamoja na kuboresha huduma za afya na miundo mbinu.

Stamina Afunguka Kwa Uchungu 'Wizara na Basata Mna Tatizo Gani na Wasanii Wetu?'

$
0
0
Rapa Stamina ambaye kwa pamoja na Roma Mkatoliki anaunda kundi la ROSTAM amefunguka kuonyesha kushangazwa na maamuzi yaliyofanywa na Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Juliana Shonza kumfungia Roma Mkatoliki.

Stamina amefunguka hayo baada ya kusikia Roma Mkatoliki amefungiwa kujihusisha na sanaa kisa kutofanya marekebisho ya wimbo wao wa Kibamia na kusema kuwa awali walipoongea na Waziri huyo aliwapa miezi sita ya kufanya marekebisho ya wimbo huo sasa iweje amechukua maamuzi ili hali hata muda ambao walipewa haujakwisha.

"Kibamia ilitoka Novemba 22, 2017 na BASATA Roma Mkatoliki tuliitwa Disemba 6, 2017 na Mhe. Waziri akasema wametupa miezi sita na leo ndio kwanza Machi 1, 2018 mbona miezi sita bado au miezi sita ya Tanzania iko tofauti na kalenda ya dunia nzima? Mna tatizo gani na wasanii wetu BASATA na Wizara? Mnakuza au mnauwa sanaa? alihoji Stamina

Stamina na Roma Mkatoliki kwa pamoja wanaunda kundi la ROSTAM ambao ndio wamiliki wa wimbo huo wa Kibamia lakini matokeo yake Roma Mkatoliki amechukuliwa adhabu peke yake kwa wimbo wa kundi hilo.

Maskini Wastara Kumbe Ana Tatizo Jingine Kubwa Linalomsumbua...Mpasuko wa Fuvu la Kichwa

$
0
0
Msanii wa filamu nchini Wastara Juma amefunguka na kudai baada ya kufanyiwa vipimo vyote nchini India amebainika kuwa na tatizo kwenye fuvu lake la kichwa ambapo hilo ndio lililokuwa likimfanya akose usingizi hapo awali bila ya yeye kujitambua.

Wastara ameeleza hayo mara alipowasili katika ardhi ya Tanzania akiwa anatokea nchini India ambako alienda kufanyiwa matibabu ya mguu pamoja na mgongo uliyokuwa unamsumbua kwa kipindi kirefu lakini baada ya kufika huko alikutwa na matatizo mengine tofauti na hayo.

"Ni tatizo ambalo lilikuwa linahitajika kuchukuliwa umakini kwa sababu muda mwingi nilikuwa nalalamika kukosa usingizi, kitu ambacho mimi mwanzo nilikuwa nadhani labda ni kutokana na mawazo niliyokuwa nayo lakini siyo hivyo. Kwenye fuvu la kichwa kuna mpasuko kwa nje na kusababisha kama uvimbe jambo ambalo lilikuwa linanisababishia kukosa usingizi", amesema Wastara.

Pamoja na hayo, Wastara ameendelea kwa kusema "nimefanikiwa kupata dawa pia na ninatakiwa nitumie kila baada ya miezi mitatu na kama kuna uwezekano wa kupata matibabu hapa hapa nchini itakuwa vizuri. Wenyewe wamenishauri kama itawezekana niweze kupata bima ya afya kubwa kwa sababu kama kuna ulazima wa kurudi kila baada ya miezi mitatu iwe rahisi ili niweze kuangalia tatizo la kichwa kwa sababu sio jambo la kulifanyia masihara".

Kwa upande mwingine, Wastara amesema anamshukuru Mwenyezi Mungu kwa kumuwezesha kurudi salama nchini pamoja na tatizo lake la mguu linaendelea vizuri japokuwa bado yupo kwenye uangalizi.

Mke wa Roma Afunguka Baada ya Mumewe Kufunguiwa Miezi 6

$
0
0
Siku ya jana March 1, 2018 zimeripotiwa taarifa za kufungiwa Miezi 6 kwa msanii Roma Mkatoliki kutojihusisha na muziki kwa kosa la kutotii agizo la Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo lililomtaka kubadili maudhui ya wimbo wake wa ‘kibamia’.

Baada ya Taarifa hizo AyoTv na millardayo.com zimemtafuta Roma Mkatoliki bila mafanikio na ndipo zikampata mke wa Roma ambaye amesema kwamba Roma alienda South Africa kwaajili ya kushoot video mpya lakini kuhusu taarifa za kufungiwa ndo kwanza anazisikia japo awali Barua ya wito aliipata.

“Kwa kweli sizifahamu halafu ayupo kasafiri, walikuwa wameenda ku-shoot South, hizo taarifa ndo nazisikia kwako, nilichosikia ni kwamba ameitwa BASATA” -Mke wa Roma

Mbunge Kingu Ageuka 'Mbogo' Kwa Wanaomjadili

$
0
0
Mbunge wa jimbo la Singida Magharibi. Elibariki Kingu amefunguka kwamba yeye anakula bata (kufanya starehe) lakini pia anakumbuka kufanya maendeleo kwa kutumia uwezo wake binafsi ikiwa ni pamoja na wanachi na serikali kwenye jimbo lake.

 Mh. Kingu amesema amesema maeneno hayo huku ikidhaniwa kwamba anarusha dongo kwa mtu anayemsema kwamba hafanyi kazi ambapo Mbunge huyo amesema kwamba "Najenga mashule mapya karibu kila eneo kwa nguvu zangu, serikali yangu na wananchi, nanunua vifaa Tiba na kuipa serikali zahanati zote kwa pesa ambayo walipaswa watumie wanangu".

Mbunge huyo amefafanua kupitia Mtandao wake wa Instagram kwa kuweka majengo ya kituo cha afya cha Ihanja ambapo amesema kuwa licha ya kituo hicho kuwa cha kisasa lakini pia kitakuwa na uwezo wakufanya mpaka upasuaji mkubwa.

Kituo cha Afya cha Ihanja kinachojengwa chini ya uongozi wa Mbunge Kingu

"Mjinga mmoja anakaa kwenye 'keyboard' anasema eti mbunge ana kula bata bata nakula lakini ninajenga zahanati kila kijiji jimboni kwa pesa zangu, serikali na wananchi," ameandika Mh. Kingu.

Mh. Kingu ameongeza "Nimesaidia akina Mama mitaji pikipiki zaidi ya 50 mpaka sasa za milioni 90 nimegawa kwa vijana kwa hela yangu. huyu mpuuzi akitaka ajue mapenzi ya hawa wananchi aje aongee huu upumbavu wake kwa wapiga kura wangu kama hawajamchoma moto".

Ushuru wa Bidhaa za Chuma Yaleta Utata Baina ya Trump na Wafanyabiashara

$
0
0
Ushuru wa Bidhaa za Chuma Yaleta Utata Baina ya Trump na Wafanyabiashara
Washirika wakubwa wa biashara wa Marekani wamekasirishwa na tangazo la Rais wa nchi hiyo Donald Trump juu ya mpango wa kutoza ushuru kwa bidhaa za chuma na aluminiam zinazoingizwa.

Umoja wa Ulaya na Canada kwa pamoja zimesema zitafanyia kazi uamuzi huo, kupingana na tamko hilo.

Rais wa Tume ya Ulaya Jean Claude Juncker amesema uamuzi huo wa Marekani wa kutoza ushuru utahatarisha maelfu ya kazi barani Ulaya.

Nchi za Mexico, China na Brazil wanasema wataziangaliz hatua za kulipiza kisasi.

Bw Trump aliweka ujumbe katika akaunti yake ya Twitter na kusema Marekani ilikuwa imekumbwa na "sera mbovu na zisizo sawa za biashara".

Alisema bidhaa za chuma zinazo ingizwa zingetozwa ushuru ya asilimia 25 na aliminiam asilimia 10.

Lakini wakosoaji wake wamesema ushuru hizi hazitafanikiwa kulinda ajira za Marekani na hatinaye zingepandisha bei za bidhaa kwa wanunuzi.

Habari ziliathiri hisa za Asia ambazo zilishuka siku ya Ijumaa, huku hisa ya Japan, Nikkei ikipoteza zaidi ya asilimia 2.

Hisa za kampuni kubwa ya magari ya Japan, Toyota zilishuka na zaidi ya asilimia 2 na hisa za Nippon Steel pia zilishuka kwa zaidi ya asilimia 4.

Toyota imesema maamuzi ya Marekani " yangeathiri sana watengeneza magari na wanunuzi"


Bw Trump ameahidi kuijenga tena sekta ya chuma na aluminiam nchini humo ambayo amesema imetendewa vibaya na nchi nyingine hasa China kwa miongo mingi.

"Kama nchi yako haiwezi kutengeza aluminiam na chuma..ni kama hauna nchi tena," alisema

"Tunahitaji watengenezaji wazuri wa aluminiam ili kujilinda"

Tangu aingie madarakani amekuwa akisema kuwa uingizaji wa bidhaa kutoka China imedhoofisha viwanda.

Maneno ya Mtoto wa Sugu Amtoa Machozi Faiza "Mama Nimemuona Baba Anapelekwa Jela"

$
0
0
Maneno ya Mtoto wa Sugu Amtoa Machozi Faiza  "Mama Nimemuona Baba Anapelekwa Jela"
Muigizaji wa Bongo movie ambaye pia ni mzazi mwenzake na Mbunge wa Mbeya mjini Sugu, Faiza Ally ameeleza machungu yake baada ya mtoto wake kulia baada ya Baba yake kufungwa jela miezi mitano.

Siku chache zilizopita Mbunge wa Mbeya mjini kupitia tiketi ya CHADEMA Joseph Mbilinyi ‘Sugu’ alihukumiwa kifungo cha miezi mitano jela baada ya kukutwa na hatia ya kutoa lugha ya fedheha dhidi Rais Magufuli.

Kupitia ukurasa wake wa Instagram Faiza amesema kuna baadhi ya vitu ambavyo vilimfanya akose huruma na Sugu lakini mtoto wake Sasha alimfanya ajisikie vibaya alipomhadithia kuwa kamuona Baba yake akienda jela.

“Hivyo ni baadhi ya vitu tu ambavyo vinavyo nifanya nikose huruma nae lkn jana sasha alienda dukani na dada akaja kuniambia MAMA NIME MUONA DADDY JOSEPH KWENYE GAZETI ANAPELEKWA JELA ndio nikajisikia vibaya sana,” -Faiza

“Nikahisi nimekua mtu mbaya sana na mkatili kumtakia baba Sasha matatizo nilijaribu kuongea na mwanangu na kuona kweli uchungu una badilisha watu , asili yangu sio ubaya lkn uchungu umenifanya nisijali na nifurahie lililo tokea nimeona kama ni wkt wake na yeye wa kukutwa na majanga,” -Faiza

“Nimekosa raha sana na nimeamua kuandika haya kujiridhisha lkn napigana na akili yangu na moyo akili inajua kuwa ni Natural feelings kwa binaadamu lkn moyo unakataa unasema huyu sio mimi lkn sasa naamini usemi unao sema uchungu una badilisha watu.” -Faiza


Hivyo ni baathi ya vitu tu ambavyo vinavyo nifanya nikose huruma nae lkn jana sasha alienda dukani na dada akaja kuniambia MAMA NIME MUONA DADDY JOSEPH KWENYE GAZETI ANAPELEKWA JELA ndio nikajisikia vibaya sana nikahisi nimekua mtu mmbaya sana na mkatili kumtakia baba sasha matatizo nijaribu kuongea na mwanangu na kuona kweli uchungu una badilisha watu , asili yangu sio ubaya lkn uchungu umenifanya nisijali na nifurahie lililo tokea nimeona kama ni wkt wake na yeye wa kukutwa na majanga , nimekosa raha sana na nimeamua kuandika haya kujirizisha lkn napigana na akili yangu na moyo akili inajua kuwa ni Natural feelings kwa binaadamu lkn moyo unakataa unasema huyu sio mimi lkn sasa naamini usemi unao sema uchungu una badilisha watu . KASOME STORI NZIMA KWENYE BLOG YANGU CLIK HAPO JUU ITAKUPELEKA HUKO .

Rufaa ya Kupinga Hukumu ya Kifungo ya Sugu, Masonga Yapelekwa Mahakama Kuu

$
0
0
Rufaa ya Kupinga Hukumu ya Kifungo ya Sugu, Masonga Yapelekwa Mahakama Kuu
Rufaa ya kupinga hukumu ya kifungo cha mbunge wa Mbeya Mjini, Joseph Mbilinyi ‘Sugu’ na Katibu wa Chadema Kanda ya Nyanda za Juu Kusini, Emmanuel Masonga wanaotumikia jela miezi mitano imewasilisha Mahakama Kuu Kanda ya Mbeya jana Machi 1, 2018 na mmoja wa mawakili wa Sugu, Faraji Mangula na kupewa kumbukumbu namba 29/2018.

“Tayari rufaa yetu imepokelewa katika Mahakama Kuu (Mbeya), sasa tunasubiri ni kupangiwa tarehe ya kuanza kusikiliza. Tunawashukuru watu wa Mahakama hii wameshughulikia vizuri jambo hili,” alisema Mangula.

Mawakili hao wamekusudia kuomba dhamana kwa Sugu na Masonga ili wawe kuwa nje katika kipindi ambacho watakuwa wanasikiliza rufaa yao.

Sugu na Masonga walihukumiwa baada ya kutiwa hatiani kwa kosa la kutumia lugha ya fedheha dhidi ya Rais John Magufuli ambapo walitoa kauli hiyo Desemba 30, 2018 katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika Viwanja vya Shule ya Msingi Mwenge jijini Mbeya.

Yanga Kuingia Kambini Leo Kwa Maandalizi ya Kuivaa Township Rollers

$
0
0
Yanga Kuingia Kambini Leo Kwa Maandalizi ya Kuivaa Township Rollers

Baada ya Yanga kurejea jijini Dar es salaam jana jioni ikitokea mkoani Mtwara ilipocheza mchezo wa ligi kuu dhidi ya Ndanda FC, timu hiyo inatarajia kuingia kambini leo kuanza maandalizi ya kuivaa Township Rollers.


Yanga ambayo ilibuka na ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Ndanda kwa mara ya kwanza kwenye uwanja wa Nangwanda Sijaona, katikati ya wiki ijayo itakuwa na kibarua cha mchezo wa Ligi ya Mabingwa Afrika dhidi ya Township Rollers ya Botswana.

Taarifa ya klabu hiyo imebainisha kuwa wachezaji wake waliokuwa majeruhi wakiwemo viungo washambuliaji,  Juma Mahadhi na Mzimbabwe Thabani Kamusoko, mshambuliaji Mzambia Obrey Chirwa wote wamepona.     

''Tunaingia kambini leo na tutakuwa na siku nne za kujiandaa na mchezo wetu wa kimataifa dhidi ya Township Rollers utakaopigwa Machi 6 kwenye uwanja wa taifa jijini Dar es salaam'', imeeleza taarifa hiyo.

Benchi la ufundi la Yanga chini ya kocha George Lwandamina anayesaidiwa na Mzambia mwenzake Noel Mwandila pamoja na wazawa Nsajigwa Shadrack na Juma Pondamali ambaye ni kocha wa makipa limejipanga kuhakikisha wanapata ushindi mnono ili kujiweka sawa na mechi ya marudiano huko Gaborone.

JE Umehangaika na Matatizo ya Kimapenzi Kwa Muda Mrefu? Muone Shehe Chalo Atakutatulia Matatizo yako Kirahisi

$
0
0
JE umehangaika na matatizo haya kwa muda mrefu mtalamu Challo anayo dawa ya kuvuta mpenzi Je unasumbuliwa na mpenzi umeachwa na mpenzi au Mme mke na Bado unampenda na umejaribu sehemu nyingine Bila mafanikio njoo utatuliwe haraka na kundumisha ndoa yenu..

Umekimbiwa na mmeo mkeo au mpenzi na anaishi na mtu mwingine atarundi haraka kusafisha nyota mvuto wa mwili na biashara minguu kufa ngazi kuwaka moto ngiri tumbo kuunguruma na wakina Baba wasiojiweza katika tendo la uyumba kuchelewa kufika kileleni tunatibu Busha Bila oprasheni bali kwa kutumia vitabu vya dini

Tunatoa pete ya utajiri Bila mashariti mkufu wa bahati unauza Mali ya haindi unapoteza pesa kwenye biashara yako Bila kujua unataka kupandishwa cheo

Wasiliana na mtalamu Shehe Challo 0714006521

Meneja Atiwa Mbaroni .....Amwingiza Irene Uwoya Matatani

$
0
0
Meneja wa Atiwa Mbaroni .....Amwingiza Irene Uwoya Matatani

MSANII wa fi lamu Bongo, Irene Uwoya ameingia matatizoni baada ya meneja wake wa bar iliyopo Sinza, Mariam Ismail ‘Mamakubwa’ kuwekwa mahabusu polisi kwa sababu ya kukiuka sheria ya vileo kwa kuuza vinywaji nje ya muda ulioelekezwa na serikali.



Kwa mujibu wa chanzo chetu tukio hilo lilijiri siku ya Jumatatu majira ya saa nane kasoro usiku, ambapo bar hiyo ilikuwa wazi ikiendelea na shughuli zake kama kawaida wakati kisheria inapaswa ifungwe saa tano usiku, ndipo askari wa doria wakamnasa meneja wake huyo.



“Inasemekana hiyo bar huwa inachelewa kufungwa mara kwa mara, sasa vyanzo vilivyopo jirani na eneo hilo vikatoa taarifa kwamba inakuwaje bar hiyo ifanye shughuli zake kinyume na sheria, nadhani ndiyo maana askari hao wa doria wakaweza kufi ka hapo.



“Hata hivyo, hawakumkuta Uwoya, ikabidi wamchukue huyo meneja wake ambaye naye ni msanii, walichukua viti kadhaa vya bar kama ushahidi, akapelekwa Kituo cha Polisi mabatini (Kijitonyama), ambapo ndani ya muda mfupi wenzake walifi ka wakafanya harakati za kumtoa, akiwemo msanii wa siku nyingi Nora,”aliongeza mtoa habari.



Kufuatia ishu hiyo paparazi wetu alimvutia waya muhusika wa bar hiyo, Irene Uwoya ambaye alikana kuifahamu ishu hiyo na kusema kuwa:



“Mimi sifahamu chochote kuhusu kukamatwa kwa meneja wangu, wewe ndio unanijulisha maana ndio ninaamka na sikuwepo eneo la tukio, sijasafi ri ila sipo tu huko kazini.”



Kufuatia tukio hilo gazeti hili lilifuatilia Kituo cha Polisi Kijitonyama na kukuta kuna jalada la kesi limefunguliwa na kupewa namba KJN/RB/1749/2018 KUUZA POMBE BAADA YA MUDA KUISHA ambapo polisi mmoja alisema wanafanyia kazi.

Polisi Yawashkilia Watuhumiwa 11 kwa Tuhuma za Mauaji Diwani wa Chadema

$
0
0
Polisi Yawashkilia Watuhumiwa 11 kwa Tuhuma za Mauaji Diwani wa Chadema
Watu 13 wanashikiliwa na Polisi mkoani Morogoro kwa makosa mawili tofauti wakiwemo 11 kwa tuhuma za kuhusika katika tukio la kifo cha Diwani wa CHADEMA huku wengine wawili raia wa Kenya wakishikiliwa kwa tuhuma za utapeli wakijifanya wao ni (TRA).


Kwa mujibu wa kamanda wa Polisi mkoa wa Morogoro, Ulrich Matei amesema baada ya tukio la kuuwawa kwa Diwani wa Kata ya Namwawala wilaya ya Kilombero Godfrey Luena, Jeshi la Polisi mkoani humo liliendesha msako wa kuwabaini wahusika wa tukio hilo ambapo mpaka sasa jumla ya watu 11 wanashikiliwa kwa tuhuma za kuhusika na mauaji hayo.

Katika hatua nyingine, watu nwawili ambao ni raia wa Kenya wanashikiriwa na polisi Mkoani humo kwa tuhuma za kujihusisha na utapeli kwa kujifanya ni mawakala wa mamalaka ya mapato nchini.

Ndoto za Majimaji Kuchukua Ubingwa Zapotea...... Uongozi Wasema Hesabu Zimegoma

$
0
0
Ndoto za Majimaji Kuchukua Ubingwa Zapotea...... Uongozi Wasema Hesabu  Zimegoma
UONGOZI wa Klabu ya Majimaji, umesema hesabu zao za msimu huu za kuchukua ubingwa wa Ligi Kuu Bara zimegoma, hivyo hivi sasa wanapambana katika kuhakikisha hawashuki daraja.



Katika msimamo wa ligi hiyo, Majimaji inayodhaminiwa na Kampuni ya Sokabet ipo nafasi ya 15 katika ligi kuu ikiwa imecheza michezo 19 ikijikusanyia alama 15, ikiachwa alama 30 na vinara wa ligi hiyo, Simba wenye 45.



Akizungumza na Championi Ijumaa, meneja wa timu hiyo, Godfrey Mvula, alisema kuwa kwa sasa wamekwishakata tamaa ya kuweza kubeba ubigwa wa ligi kuu pamoja na kumaliza nafasi za juu, badala yake wanakazana kuhakikisha hawashuki daraja.



“Tumekata tamaa kwenye ubingwa, hii ni baada ya kupiga hesabu kwani tulikaa chini tukatathmini tukaona kwamba tutashindwa, hivyo nafasi yetu iliyobaki kwa sasa ni kuhakikisha hatushuki daraja kwa kuhakikisha kwamba tunashinda michezo iliyobaki,” alisema Mvula

Mimi Mars Afunguka Uhusiano Wake wa Kimapenzi na Diamond

$
0
0
Mimi Mars Afunguka Uhusiano Wake wa Kimapenzi na Diamond
Msanii wa muziki Bongo, Mimi Mars amefunguka ukweli wa taarifa zilizodai alikuwa akitoka kimapenzi na Diamond Platnumz.

Mimi Mars amelazimika kuzungumzia hilo mara baada ya video iliyowahi kusambaa katika mitandao ikionyesha akicheza wimbo wa Diamond unaokwenda kwa jina la Eneka.

Muimbaji huyo kutoka label ya Mdee Music ameiambia The Playlist ya Times Fm kuwa taarifa hizo hazina ukweli wowote ila alichofanya yeye ni kucheza wimbo wa msanii huyo pekee na alikuwa hajua kama ni wa Diamond kwa wakati huo.

“Haina ukweli kabisa, kwanza cha kushangaza ni kwamba wakati nilikuwa nacheza huo wimbo nilikuwa hata sijajua kama ni wa Diamond,” amesema Mimi Mars.

“Nilikuwa nimeenda kwa fundi kuchukua ile nguo ambayo nimeivaa, kwa hiyo akaweka muziki akasema ebu cheza kidogo, so I was just dance the song mpaka baadaye nipo kwenye gari ndio najua huo wimbo ni wa Diamond, it was too late na ile video ilienda, kwa hiyo kulikuwa hamna ishu yoyote,” amesisitiza.

Ameongeza kuwa anataka kusikika na kuonekana katika masikio na macho ya mashabiki lakini si kwa mtindo huo na ni kitu kilichomsumbua kidogo. Mimi Mars kwa sasa anatamba na ngoma mpya inayokwenda kwa jina la Papara.

Hawa wa Ntarejea Hali Tete Alazwa Muhimbili

$
0
0
MWANAMUZIKI ambaye alishirikishwa kwenye Wimbo wa Nitarejea ya mwanamuziki wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’, Hawa Said hali yake imezidi kuwa mbaya baada ya kulazwa katika Hospitali ya Taifa Muhimbili jijini Dar akisumbulia na tatizo la ini.



Akizungumza na Ijumaa, mmiliki wa kituo cha kudhibiti matumizi ya madawa ya kulevya cha Pilli Missana Foundation, kilichopo Kigamboni jijini Dar, Pilli Missana alisema kuwa, tatizo la Hawa limetokana na matumizi ya madawa ya kulevya alilokuwa akichanganya na unywaji wa pombe kali.


“Unajua Hawa hali yake ilishaanza kutengamaa kabisa lakini kumbe alikuwa amepata tatizo la ini muda mrefu kutokana na unywaji wa pombe kali, kwa sasa hali yake si nzuri sana na anapatiwa matibabu katika Hospitali ya Muhimbili,” alisema Pilli.



Julai mwaka jana, Hawa alijitokeza hadharani na kuomba msaada baada ya kuathiriwa na unywaji wa pombe kali za kienyeji pamoja na madawa ya kulevya ambapo alipatiwa msaada na Kituo cha Pilli Missana na hali yake kuanza kuimarika kabla ya kupata tatizo jingine la ini.

Soma Nafasi za Kazi Zilizotangazwa Siku ya Leo...

Kutana na Mtabibu Mongwa Mganga wa Waganga Sasa Anapatikana Mikoa Yote

$
0
0
KUTANA NA MTABIBU MONGWA MGANGA WA WAGANGA SASA WAKO MIKOANI KARIBU YOTE NCHINI...
.
HIVYO WATATOA TIBA MAENEO YOTE YA MBEYA ,DODOMA, IRINGA , MOROGORO, MWANZA,ZANZIBAR

==>KWA WALE WENYE KUHITAJI TIBA

Husafisha nyota na kutoa Pete za bahati na kwawale walio sumbuka kwaajili ya matibabu na hawakufanikiwa chochote sasa njoo ujionee miujiza hapo kwahapo bila malipo yoyote malipo baada yakazi napia humpa mtu jini la mali kwayule anaye taka kumiliki bila mashariti yoyote
Tunatibu magonjwa mbalimbali yaliyo shindikana mpenzi aliye kukimbia nakumrudisha kwa masaa 24 tu napia natoa dawa za nguvu za kiume kuurefusha uume paka pale unapotaka .
Natoa dawa za biashara na mvuto ==tunatoa dawa zauzazi kwa wale kina mama wenye matatizoya uzazi walio angaika kwa muda mrefu bila kupata mafanikio yoyote njoo umalize tatizo lako sasa
Natoa mazindiko yanyumba na mwili biashara na mvuto kazini
Kupandisha nyota ili kungaa kupandishwa cheo kazini kurudisha mali zilizo pote zilizo ibiwa kuzulumiwa
Kesi zilizo shindikana uzimaliza mara moja namengine mengi ya siri piga simu

+255 764291657
+255 764291657
+255 764291657

Waziri Mkuu Afanya Ukaguzi wa Usambazaji Maji Vijijini

$
0
0
Waziri Mkuu Afanya Ukaguzi wa Usambazaji Maji Vijijini
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amekagua mradi wa usambazaji wa maji kwenye vijiji vinavyopitiwa na mradi wa maji Mbwinji na ameridhishwa na unavyoendelea.


Waziri Mkuu alifanya ukaguzi huo katika kioksi cha kuchotea maji kilichopo kwenye kijiji cha Mbecha wilayani Ruangwa na kusema mradi huo unaosimamiwa na Mamlaka ya Maji na Usafi wa Mazingira Masasi-Nachingwea (MANAWASA) unatarajiwa kukamilika Machi 31, 2018.

"Huduma ya upatikanaji wa maji safi na salama kwa wananchi ni miongoni mwa vipaumbele vya serikali ya awamu ya tano, hivyo vijiji vyote vitapata maji. Serikali ya awamu ya tano ina mikakati mizuri inayolenga kumaliza tatizo la upatikanaji wa maji safi na salama katika maeneo yote yenye tatizo hilo nchini", amesema Majaliwa.

Aidha, Waziri Mkuu amesema vijiji ambavyo vimenufaika na mradi huo wilayani Ruangwa ni sita ambavyo ni Chiyapi, Nandanga, Ipingo, Lucheregwa, Litama na Mbecha.

Kwa upande wake, Mkurugenzi Mtendaji wa MANAWASA Mhandisi David Mwamsojo amesema mradi huo utagharimu sh. milioni 870.738 hadi kukamilika na kuhusisha vijiji 12 vilivyo kwenye umbali wa kilomita tano kutoka kwenye bomba kuu pamoja na ujenzi wa vioksi 18 vya kuchotea maji.

Yanga, Azam, Singida Kibarua Kizito Leo

$
0
0
Yanga, Azam, Singida Kibarua Kizito Leo
Jumla ya timu nane zilizofuzu hatua ya robo fainali ya michuano ya kombe la shirikisho nchini leo zinatarajiwa kujua wapinzani wao katika hatua hiyo kufuatia droo itakayochezeshwa leo.


Shirikisho la soka nchini TFF kupitia kamati yake ya mashindano hayo limekuwa likitumia utaratibu wa kuchezesha droo kila inapoingia hatua mpya. Baada ya mechi za 16 bora kukamilika na timu 8 kupatikana leo mechi za kusaka timu nne za nusu fainali zitajulikana.

Mabingwa wa kwanza wa michuano hiyo klabu ya Yanga wamefuzu hatua hiyo huku mabingwa watetezi Simba wakiwa tayari wameshaondolewa katika hatua za awali na timu ya Green Worriors ambayo nayo iliondolewa na Singida United.

Timu zingine ambazo zimeingia kwenye nane bora ni Azam FC, Singida United, Mtibwa Sugar, Njombe Mji, Tanzania Prison, Stand United pamoja na timu moja kutoka ligi daraja la kwanza lakini imepanda kucheza ligi kuu msimu ujao JKT Tanzania.
Viewing all 104785 articles
Browse latest View live




Latest Images