Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104709 articles
Browse latest View live

TAHLISO Yatoa Tamko Kuhusu Wanafunzi Wanaotaka Mwigulu Ajiuzulu Kwa Kifo Cha Akwilina

$
0
0
TAARIFA KWA UMMA
Ndugu waandishi wahabari tunawashukuru sana kwa kukubali wito wetu wakuja kujumuika pamoja nasisi.

Leo tarehe 3/3/2018 tumekutana na viongozi wa vyuo vikuu nchi nzima kwa ajili yakujadili changamoto zinazotukabili.

Kikao hiki ni cha TAHLISO Baraza Kuu (SENATE) kina husisha Maraisi wa serikali za wanafunzi wa Vyuo Vikuu nchini.

Tunatambua kwamba kuna kifo cha mwanafunzi mwenzetu Akwilina Akwilini,mwanafunzi wa chuo cha NIT kilichotokea mwezi wa pili. Tunawashukuru wanafunzi wenzetu kwa utulivu mkubwa na mshikamano waliouonesha tangu msiba ulipotokea, wakati wa kipindi cha majonzi hadi kufikia sasa.

Tunamshukuru Mhe.Raisi wa Jamuhuri ya Muunganowa Tanzania kwa kuingilia kati suala hili na kuagiza uchunguzi ufanyike na hatua za kisheria zichukuliwe kwa wote watakaobainika kuhusika na kifo cha Akwilina Akwilini.

Vilevile tunaishukuru Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia kwa ukaribu waliouonesha katika kipindi chote cha msiba.

Tunaomba wanafunzi waendelee kuwa watulivu wakati maagizo ya Mh. Raisi yakitekelezwa.

Aidha tunapenda jamiii tambue kuwa TAHLISO ndio chombo kikuu cha kuwasemea wanafunzi wote nchi nzima Tanzania na sio kikundi kingine chochote kile.

Vipo vikundi vingi vimejitokeza na kutoa matamko mbalimbali baada ya kifo hiki kutokea, vikundi vingine vikaenda mbali Zaidi kwakuwataka baadhiya watendaji wa Serikali akiwemo Waziri wa Mambo ya Ndani kujiuzulu jambo ambalo linaashiria vikundi hivyo kuongozwa ama kutumika na makundi ya kisiasa, haiwezekani kutaka watendaji wa Serikali wajiuzulu wakati uchunguzi bado unafanyika na matokeo ya uchunguzi huo bado hayajatoka.

Jambo la kusikitisha Zaidi kuna baadhi ya vikundi vimejitangaza kwamba vinaungwa mkono na Maraisi wa Vyuo Vikuu jambo ambalo sio la kweli, Marais wote wa Vyuo Vikuu tuko hapa Dodoma tunaendelea na vikao vyetu vya kujadili changamoto zinazowakabili wanafunziwa Vyuo Vikuu.

Tunatoa wito kwa vikundi vyote vinavyojihusisha nakutumia mwamvuliwa Marais wa Vyuo Vikuu kama kinga yao ili kuu hadaa Umma kwamba wanaungwa Mkono, vikundi hivyo viache tabia hiyo vinginevyo tutawachukulia hatua za kinidhamu.

TAHLISO tunasubiri matokeo ya Uchunguzi unaofanyika juu ya kifo cha Akwilina na tunaimani wahusika wote watachukuliwa hatua kali zakisheria.

Tunawaomba wanafunzi wote tuendelee kuwa watulivu wakati tukisubiri matokeo hayo na kujiepusha na maandamano na vitendo vyovyote vitakavyo sababisha uvunjifu wa Amani nakuleta mgawanyo miongoni mwa wanafunzi.

Hata hivyo namna bora yakufikisha hoja nikutumia njia ya majadiliano kama wasomi badala ya kutumia nguvu ama maandamano kwakutofuata taratibu na madhara yake ni kusababisha vuruguzi sizotakiwa na hatimaye kuhatarisha usalama na hivyo kuathiri jamii kwaujumla wake.

Vurugu zozote zitokanazo kwakutozingatia taratibu zinaweza kudhorotesha shughuli za kiuchumi kwa mtu mmoja mmoja na Uchumiwa Taifa letu.

Vile vile zinapoteza mvuto kwawawekezaji wanje na wandani, ikiwemo shughuli za utalii nchini ambazo zinachangia pato la Taifa letu.

Athari za Vurugu na kukosekana kwa amani zipo wazi natunaziona kwa nchi nyingine zikiwemo baadhi ya nchi jirani zetu ambao wamekua wakimbizi nchini kwetu kila siku.

Tunaona kuwa kama wanataaluma tunajukumu kubwa la kuelimisha jamii na kuwamfano bora wakutumia njia za majadiliano katika kujenga hoja zetu ilizitatuliwe kuliko kutumia njia ya maandamano au vurugu zisizo na ulazimawowote.

Taasisi hii ndio yenye dhamana ya kutetea nakusimamia maslahi ya wanafunzi wote wa vyuo na vyuovikuu Tanzania na si vinginevyo.

GEORGE ALBERT MNALI
MWENYEKITI
TAHLISO

Kutana na Mtabibu Mongwa Mganga wa Waganga Sasa Anapatikana Mikoa Yote

$
0
0
KUTANA NA MTABIBU MONGWA MGANGA WA WAGANGA SASA WAKO MIKOANI KARIBU YOTE NCHINI...
.
HIVYO WATATOA TIBA MAENEO YOTE YA MBEYA ,DODOMA, IRINGA , MOROGORO, MWANZA,ZANZIBAR

==>KWA WALE WENYE KUHITAJI TIBA

Husafisha nyota na kutoa Pete za bahati na kwawale walio sumbuka kwaajili ya matibabu na hawakufanikiwa chochote sasa njoo ujionee miujiza hapo kwahapo bila malipo yoyote malipo baada yakazi napia humpa mtu jini la mali kwayule anaye taka kumiliki bila mashariti yoyote
Tunatibu magonjwa mbalimbali yaliyo shindikana mpenzi aliye kukimbia nakumrudisha kwa masaa 24 tu napia natoa dawa za nguvu za kiume kuurefusha uume paka pale unapotaka .
Natoa dawa za biashara na mvuto ==tunatoa dawa zauzazi kwa wale kina mama wenye matatizoya uzazi walio angaika kwa muda mrefu bila kupata mafanikio yoyote njoo umalize tatizo lako sasa
Natoa mazindiko yanyumba na mwili biashara na mvuto kazini
Kupandisha nyota ili kungaa kupandishwa cheo kazini kurudisha mali zilizo pote zilizo ibiwa kuzulumiwa
Kesi zilizo shindikana uzimaliza mara moja namengine mengi ya siri piga simu

+255 764291657
+255 764291657
+255 764291657

Rommy jones Akanusha Uvumi wa Diamond Kuachana na Zari Hassan

$
0
0
Rommy jones Akanusha Uvumi wa Diamond Kuachana na Zari Hassan

Tazama Video Hapa Chini:

ON AIR: "Siolewi Leo Wala Siwezi Kuwa na Mtoto" - VANESSA MDEE

$
0
0
ON AIR: "Siolewi leo wala siwezi kuwa na Mtoto" - VANESSA MDEE

Tazama Video:

Waziri Atolea Ufafanuzi Kichwa cha Treni Ambacho Kilipata Ajali

$
0
0

aziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Prof.Makame Mbarawa amefunguka na kutolea maelezo juu ya kichwa cha treni ambacho kilipata ajali Februari 28, 2018 na kuhusishwa na moja ya vichwa vya treni ambavyo vilikutwa havina mwenyewe na Rais Magufuli.

"Kichwa kilichopata ajali ni moja ya vichwa ambavyo vilikuja mwaka mmoja uliopita hakikuwa bandarini na hivi vilivyopo sasa hivi, vilivyopo sasa vina namba kuanzia 9014 mpaka 9024 tuwe angalau tunatumia weledi kwenye kazi zetu. Picha iliyounganisha si miongoni mwa vichwa vya sasa vilivyopo bandarini nina imani teknolojia inaweza saidia maana yenyewe inatunza hebu google tu hiyo picha uangalie ni ya mwaka gani ili Kupata jawabu sahihi" alisema Mbarawa


Miezi kadhaa iliyopita Waziri huyo aliweka wazi nia ya Serikali kutaka kuvinunua vichwa hivyo vya treni 11 ambavyo vilikuwa vikisemekana kuwa havina mwenyewe na kudai kuwa walianza mazungumzo na muhusika ili kuona wanawezaje kufanya biashara.

Davido Adondoka Jukwaani Wakati Akipanda kwa Mbwembwe

$
0
0

Msanii wa muziki kutoka nchini Nigeria, Davido amejikuta akipoteza mzuka baada ya kujikwaa wakati akipanda kwa mbwembwe jukwaani tayari kwa kutumbuiza nchini Rwanda.

Davido ambaye alikuwa anaonekana kama tayari ameshapata ulabu ilimchukua sekunde kama 30 kukaa kimya jukwaani akivalishwa tena phone masikioni ambazo zilikatika alipojikwaa wakati akipanda jukwaani.

Hata hivyo, baada ya ajali hiyo ndogo Davido aliendelea kutumbuiza ambapo maelfu ya watu walihudhuria kwenye show hiyo ambayo ipo kwenye ziara ya Davido ijulikanayo kwa jina la  “30 billion africa tour 2018”  iliyofanyika kwenye uwanja wa mpira wa taifa wa Amahoro.

Akiwa nchini Rwanda, Davido ametoa msaada wa dola $5,000 sawa na Tsh milioni 11.2 kwenye shule ya muziki nchini Rwanda.

Breaking News: Watano wafariki Hiace yagongana na Basi la New Force

$
0
0

WATU watano wamefariki dunia leo asubuhi baada ya basi la New Force lilikokuwa linatokea Msamvu kwenda Mikese kugongana na gari dogo la abiria (Hiace) lililokuwa linatokea Msamvu, mkoani Mogororo.  Pia watu kadhaa ambao idadi yao bado haijajulikana, wamejeruhiwa.

Mashuhuda wa ajali hiyo wanasema chanzo ni dereva wa gari hilo la Hiace kutaka kulipita gari la mchanga lililokuwa mbele ambapo lilijikuta likigongana uso kwa uso na basi hilo.

Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Reli Nae Akanusha Kuhusu Kichwa cha Treni Kilichopata Ajali

$
0
0

Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la reli nchini TRC, Masanja Kadogosa amekanusha taarifa zinazoenea kuwa moja ya vichwa vya treni 11 vilivyokuwa katika mpango wa kununuliwa na Serikali kimeanza kutumika na kimepata ajali
-
Amesema kuwa kampuni ambayo Waziri alikuwa anazungumzia kuhusu kununua vichwa ni kampuni hiyo hiyo ambayo imeleta vichwa 13 kipindi cha nyuma
-
Anasema treni zina madaraja, mfano; daraja 90, 80 na 64. Kwa hiyo katika zile namba kwenye kichwa cha treni, 90 ni namba ya daraja halafu zinafuata namba nyingine
-
Anaendelea na kusema katika vichwa 13 vya mwanzo kimoja ndio kimeanguka kule KIgoma na si vile vilivyopo Bandarini
-
Hivyo, kichwa kile hakina uhusiano na vile vilivyopo bandarini

Miujiza ya Sharifu Seif Mohamed..JE Umeachwa na Mme/Mke au Mpenzi, Umesongwa na Mitihani ya Maisha

$
0
0
SHARIFU SEIF MOHAMED ANAWASHUKURU WALE WOTE WANAOENDELEA KUPIGA SIMU, WENYE MATATIZO NA WALE WANAOTOA  SHUKRANI NA SHUHUDA JINSI TIBA ZAKE ZINAVYO WASAIDIA,

(Rudisha mahusiano yako ndani ya masaa 72 tu)

SHARIFU MOHAMED Ni  mtaalam na mnajimu maarufu wa nyota na kubashiri mambo yanayo watesa binadamu duniani kote na kupata ufumbuzi, Anatumia kitabu cha QUR'AN na Nyota

Je Umeachwa na UMPENDAE awe Mme/Mke na bado unampenda? Je Umekimbiwa na Mmeo/ Mkeo n anaishi na mtu mwingine? Je Umejaribu sehemu nyingi bila mafanikio? Mpigie simu SHARIFU SEIF sasa hivi ujionee Muujiza wa Papo kwa Papo, Anauwezo wa hali ya juu wa kusambaratisha mahusiano yao na kumrejesha kwako haraka sana na Kumfanya Atimize Ahadi zote Ndani ya Muda Mfupi Endapo Utafwata Atakacho Kuelekeza

 ZINDIKO LA NYUMBA NA BIASHARA, PETE ZA BAHATI, HUMALIZA KABISA TATIZO   HUZUIA CHUMA ULETE KWENYE BIASHARA, HURUDISHA MALI ZILIZOPOTEA, NA KUPONYA MAGONJWA SUGU ANAO UWEZO WA KUMRUDISHA ALIE MBALI AU ALIECHUKULIWA MSUKULE, KUPANDISHA NYOTA NA KUSHINDA BAHATI NA SIBU, KASAFISHA NYOTA NA KUKUPA MVUTO WA AJABU, KUTOA NUKSI NA VIFUNGO MBALIMBALI,  MAFANIKIO YA MAISHA NA UTAJIRI BILA MASHARI, NA MENGINE MENGI YA SIRI,

JE UMAHANGAIKA KUPATA MTOTO BILA MAFANIKIO? WASILIANA NA MTAALAMU HUYU KWANI YEYE HUFAULU PALE WOTE WALIPOSHINDWA, PIA UMALIZA KAZI ZILIZO SHINDIKANA NA WATAALAM WENGINE NDANI YA MASAA 24 TU,

(NA ANATIBU KWA NJIA YA SIMU UKIWA NCHI YOYOTE AU MKOA WOWOTE ENDAPO UTAFWATA MAELEKEZO YAKE)

Kwa ushauri na mawasiliano  zaidi Piga SIMU No:

Mobile +255 654-836970
WhatsApp 0622766715

Hali ni Tete Naweza Kutoka Nje ya Ndoa Muda Wowote..Naombeni Ushauri

$
0
0

Wadau mwenzenu nipo katika wakati mgumu sana nataka tubadirishane uzoefu. Mke wangu kasafiri kikazi nje ya nchi atakuwa huko kwa miezi Sita na tokea ameondoka ni miezi miwili tu imepita, mwenzenu sijafanya mapenzi mda wote huo wa miezi miwili na kichupa nahisi kimejaa.

Napata taabu sana nimejaribu kufanya mazoezi na kushiriki michezo mbali mbali kusahau maswala ya ngono, achilia mbali nikiwa ofisini naji keep busy sana lakini ikifika usiku nikiwa Kitandani napata taabu sana maana 'mzee' anasimama wima kwa mda mrefu sana hata usingizi inakuwa ishu kupata,

Mimi sitaki lakini mwili unahitaji kufanya mapenzi kwakweli, Hebu nipeni uzoefu nifanye nini ili katika hiki kipindi cha miezi sita nisitoke nje ya ndoa kwani ni miezi miwili tu hali imeshakuwa hivi, je kuna mtu amewahi kukaa mda mrefu kiasi hiki bila kufanya mapenzi? kama yupo anipe uzoefu alikuwa anafanya nini kuikabiri hii hali maana kuna kila dalili kwamba nitashindwa.

Mzee Aliyegundua Tanzanite Ataka Kuonana na Rais Magufuli

$
0
0
Mzee aliyegundua madini yanayopatikana Tanzania pekee ya Tanzanite, Mzee Jumanne Mhero Ngoma amesema kuwa ana lengo la kutaka kuonana na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ili kuongea naye kuhusu mchango wake kwa taifa hili hususani katika sekta ya madini.

Mzee Ngoma (79) amesema amekuja Dar es salaam kupata fursa hiyo ya kuonana naye ili amsaidie kwani licha ya kuwa na jina kubwa na kufanya mambo makubwa katika nchi hii lakini bado serikali haioni umuhimu wake kwani amekuwa akifuatilia kupata japo stahiki yake.

Akieleza sababu kubwa inayompelekea kumuona Rais Magufuli, Mzee Ngoma amesema wanakijiji huko anakotoka hawaamini na wanamcheka kwani hali yake ni ngumu kimaisha na afya yake imekuwa ikidhoofu kwa magonjwa bila hata kupata matibabu kutoka serikalini.

Mzee Ngoma amesema wazo la kufikia hatua ya kuongea kwenye vyombo vya habari kutaka aonane na Rais Magufuli, limekuja baada ya juhudi za kuhangaika kwa Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam, RC Makonda kugonga mwamba, ambapo alitaka amfikishie ombi hilo ili ampelekee Rais Magufuli. Tazama video ya mzee hiyo akiongea juu ya dhumuni lake la kuonana na Rais Magufuli.

Jumanne Mhero Ngoma amezaliwa mwaka 1939 na ndiye Mtanzania aliyegundua madini ya Tanzanite ambayo yanapatikana Tanzania pekee. Uguduzi huu ulifanyika tarehe kama ya leo, 23 Septemba 1967. Madini haya yanapatika eneo la Mererani mkoani Arusha.

Mzee Ngoma alipewa tuzo kwa ugunduzi wa madini ya Tanzanite mwaka 1984. wakati akipokea cheti hicho alieleza kuwa “Mara ya kwanza kuyagundua madini haya nilikuwa mdogo sana. Nilikuwa na umri wa chini ya miaka 20 na nilikuwa porini nikichunga mifugo. Nilikuwa kwenye msitu ambao Wamasai walikuwa wameupa jina la Lalouo. Eneo ambako niliyaona lilikuwa linafahamika kwa jina la Naisunyai ambako kwa kawaida Wamasai walikuwa wakilitumia kunywesha mifugo yao,“.


Anaendelea kueleza Mzee Ngoma “Siku hiyo niliona vitu vinavyowakawaka. Nikawa najiuliza vitakuwa ni vitu gani? Awali nilidhani pengine ni nyoka au wanyama wa hatari. Nikasogea nikiwa na upinde na mshale wangu tayari kwa lolote. Nilipogusa na mti niliokuwa nimeushika, nikashangaa mawe yanayong’aa yakitoka ardhini. Vipande vidogo vidogo vyenye rangi ya bluu. Kwa kweli nilivipenda sana.”

Mzee ngoma kwa sasa anasumbuliwa na matatizo ya kupooza ambapo watoto wake wameitaka serikali imchukulie kwa ukubwa kama watu wengine mashuhuri wanavyopewa matibabu.

Washiriki wa Tuzo za Oscar Mwaka Huu Kutembelea Tanzania

$
0
0
Washiriki wa tuzo za Oscar mwaka huu kwa nyakati tofauti watatembelea Tanzania ikiwa ni moja ya zawadi kwao kwa kupendekezwa kuwania tuzo hiyo.

Mtandao wa CNBC unaripoti kuwa washiriki 25 waliopendekezwa katika vipengele vinavyopewa zawadi hiyo, kila mmoja ametengewa dola 40,000 za Marekani (takriban Sh90 milioni) kwa ajili ya safari ya kutembelea vivutio vya utalii nchini Tanzania.

Nyota hao Meryl Streep, Margot Robbie, Denzel Washington na wengine waliotajwa kuwania vipengele vya mwigizaji bora wa kike na wa kiume, mwigizaji msaidizi wa kike na wa kiume na mwongozaji bora wamezawadiwa siku 12 za kuzuru Tanzania kwa wakati watakaotaka.

Katika tuzo zinazotolewa leo Machi 4,2018 nchini Marekani, washiriki katika vipengele hivyo watapewa begi lenye zawadi ikiwamo ofa ya kuzuru Tanzania na kutembelea vivutio vya utalii watakavyochagua.

Zawadi hizo zitatolewa na kampuni ya matangazo ya Distinctive Assets ambayo ni miongoni mwa wadhamini wa tuzo hizo kwa miaka 16.

Jumla ya zawadi zitakazoambata na vito vya thamani zitagharimu dola laki moja za Marekani ambazo ni wastani wa Sh220 milioni.

Nyota wengine ni Timothée Chalamet, Daniel Day-Lewis, Daniel Kaluuya, Gary Oldman, Sally Hawkins, Frances McDormand na Saoirse Ronan.

Mrembo Sanchi Afunguka Haitaji Mwanaume wa Kumuoa..'Mimi Pesa tu'

$
0
0
MWANA-MITINDO maarufu Bongo, Jane Ramoy ‘Sanchi’ ametoa la moyoni kuwa hahitaji mwanaume wa kumuoa kwa hivi sasa na kama angetaka, wapo wengi wamepanga msururu.

Mrembo huyo amefunguka hayo baada ya mitandao ya kijamii hivi karibuni kumuandama kuwa, iweje yeye ana ‘mzigo wa haja’ haolewi wengine ambao hawana hata shepu wanaolewa kila kukicha.

Kufuatia maneno hayo mtandaoni huku wengine wakipingana nayo kwa kusema siyo kila mwenye shepu ana haki ya kuolewa, Sanchi alisema:

“Jamani naomba watu wajue kabisa mimi sihitaji kuolewa kwa sasa, ningekuwa nataka kuolewa ingekuwa zamani, wapo wanaume wengi wanataka kuleta posa kwetu lakini sasa hivi nimesema hapana kwanza.”

Video:Watanzania Tunako Elekea Pabaya, Zuio la Kujengwa Msikiti Rukwa..

$
0
0
Watanzani tukitaka nchi yetu iendelee, tuachane na dhana za udini, Serikali ya Tanzania ni serikali inayoamini kuwa kila mtanzania ana haki ya kuabudu anachotaka,kilichotokea Rukwa msikiti umezuiliwa kujengwa na Mkuu wa Mkoa bila ya sababu za msingi,hii imeleta hasira kwa wale wenye imani ya uislam..

Yaliyoendelea Rukwa ni sawa na kuwaambia wale wanaojenga Makanisa kule Zanzibar wasijenea kwasababu Zanzibar asilimia 99% ya wazanzibari ni waislam...

Binafsi mimi naona hii ni hatari kwa umoja walioujenga waasisi wa nchi hii inayoitwa Tanzania,Watanzania tujiepushe na ujinga kama huu kama tunataka maendeleo ya kweli kwenye hili Taifa

VIDEO:

Gazeti la Tanzanite Kitanzani kwa Habari zisizo na ueledi. Waitwa ofisi ya Habari Maelezo Kujieleza

$
0
0
Leo kwenye mitandao ya kijamii imesambaa nakala ya gazeti la Tanzanite inayotarajia kutoka siku ya Jumatatu(Kesho) yenye maudhui yanayokinzana na maadili ya kitaaluma yanayomzungumzia mwanadada Mange Kimambi, kutokana na hilo, Ofisi ya Msemaji Mkuu wa Serikali imepata malalamiko na kuamua kuita wahusika kuja kutolea maelezo.


Ameandika Msemaji Mkuu wa Serikali, nanukuu
''Nimepokea malalamiko mengi kuhusu maadili ya kitaaluma katika toleo linaloonekana mtandaoni la gazeti la Tanzanite.Gazeti hili limesajiliwa kutoka kila jumatatu,hivyo tumewaita wahusika kesho baada ya kuona nakala halisi ili kupata maelezo yao.''
Source:Jamii Forums

Maboresho Katika Application ya Udaku Special, Fanya Ku Update Ama Download Hapa Kwenye Simu yako

$
0
0
Maboresho Katika Application ya Udaku Special, Fanya Ku Update Ama Ku Download HAPA Kwenye Simu yako, Tumebadili Logo pamoja na Kuifanya App iwe nyepesi zaidi bila kuchukua nafasi kubwa katika Simu yako

UPDATE HAPA

DOWNLOAD HAPA


Asanteni

RC Makonda Awezesha Matibabu ya Ahmed Albaity Nchini China (Video)

$
0
0
Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Paul Makonda kwa kushirikiana na wadau wengine wamefanikiwa kupata fedha za matibabu zaidi ya tsh milioni 106 kwaajili ya matibabu ya Ahmed Albaity. Albaity amesafiri Jumapili hii kuelekea nchini China kwa ndege ya Emirates ambapo anatarajia kukaa zaidi ya wiki mbili.

VIDEO:

Wema Sepetu Apata Shavu Wasafi TV

$
0
0
Muigizaji wa Filamu nchini Tanzania, Wema Sepetu ametangaza kuwa ni moja ya watu maarufu watakaoonekana kwenye kituo cha runinga cha Wasafi TV kinachomilikiwa na msanii wa Bongo Fleva, Diamond Platnumz.

Wema amesema kuwa watu kwa sasa wanamuona yupo karibu na Diamond Platnumz wengi wakidhani labda wamerudisha mahusiano yao ya kimapenzi lakini hakuna chochote yeye anamchukulia kama Boss wake kwani tayari ameshapata shavu la kurusha kipindi chake Wasafi TV. Mtazame Wema Sepetu akizungumzia ishu hiyo

VIDEO:

Bongo5

Arsenal yageuzwa kitoweo EPL, Yapokea kipigo kingine

$
0
0
Klabu ya Arsenal imekubali kipigo kingine cha pili mfululizo kwenye michezo ya Ligi Kuu soka England, baada ya jioni ya leo kukubali kibano cha goli 2-1 dhidi ya Brighton & Hove Albion.

Magoli ya Brighton & Hove Albion yamefungwa na Lewis Dunk na Glenn Murray huku goli pekee la Arsenal likifungwa na Pierre-Emerick Aubameyang.

Mchezo uliopita Arsenali walikubali kipicgo cha goli 3-0 dhidi ya wababe wa EPL, Klabu ya Manchester City huku wakipoteza mchezo wa fainali ya kombe la EFL dhidi ya wababe hao.

Kwenye mchezo huo kama kawaida mashabiki wa Arsenal walikuwa wanaonesha mabango yaliyosomeka ‘WENGER OUT’ wakimshinikiza kocha wa klabu hiyo Mzee Wenger kuachia nafasi hiyo klabuni hapo.

Jaji Mutungi Awapa Chadema Siku Tano

$
0
0
 Msajili wa Vyama vya Siasa nchini, Jaji Francis Mutungi kwa mara nyingine ametoa siku tano kwa Chadema kujieleza kwa nini asikichukulie hatua kwa kukiuka sheria na kanuni za maadili ya vyama vya siasa.

Katika barua hiyo ya Jaji Mutungi ya Machi mosi, 2018 iliyopokelewa Chadema Machi 2 inatakita chama hicho kikuu cha upinzani nchini, kujieleza kwa nini kilivunja sheria na kanuni hizo Februari 16, 2018.

Barua hiyo ya Jaji Mutungi inatokana na kutoridhishwa na majibu ya barua yake ya Februari 21 aliyokiandikia chama hicho, akikipa siku tano kujieleza kwa nini kilivunja sheria na kanuni hizo.

Akizungumza na Mwananchi Digital leo Machi 4, 2018, mkurugenzi wa itifaki, mawasiliano na mambo ya nje wa Chadema, John Mrema amesema barua hiyo wameipokea jana na kesho wanatarajia kuijibu.
Viewing all 104709 articles
Browse latest View live


Latest Images