Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104687 articles
Browse latest View live

Maboresho Katika Application ya Udaku Special, Fanya Ku Update Ama Download Hapa Kwenye Simu yako

$
0
0
Maboresho Katika Application ya Udaku Special, Fanya Ku Update Ama Ku Download HAPA Kwenye Simu yako, Tumebadili Logo pamoja na Kuifanya App iwe nyepesi zaidi bila kuchukua nafasi kubwa katika Simu yako

UPDATE HAPA

DOWNLOAD HAPA

Breaking News: Moto Mkubwa Waunguza Soko Mbagala

$
0
0
Moto mkubwa umelipuka na kuunguza soko la wafanyabiashara wadogo wadogo (machinga) katika eneo la Mbagala Rangi Tatu – Dar, asubuhi hii Machi 6, 2018.

Sehemu iliyoathirika zaidi ni ile ya wauza mitumba huku baadhi ya bidhaa zao zikiteketea kwa moto lakini hakuna aliyeripotiwa kupoteza maisha wala kujeruhiwa.

Chanzo cha moto huo kinadhaniwa kuwa ni hitilafu ya umeme ambapo tayari gari la jeshi la zima moto limefika  kuzima moto huo.

Hivi Ndivyo Wastara Alivyokutana na Islaeli Mtoa Roho za Watu

$
0
0
Hivi Ndivyo Wastara Alivyokutana na Islaeli Mtoa Roho za WatuMWANAMAMA wa Bongo Movies aliyepitia masahibu mengi ya kimaisha, Wastara Juma amesema kuwa kutokana na mateso na magonjwa yanayomkabili, ameshamuona Malaika Israel Mtoa Roho mara nyingi mno, lakini kwa sababu Mungu bado anampenda, anaendelea kudunda kwa neema zake.

Akizungumza na Ijumaa Wikienda mara baada ya kurejea kutoka nchini India alikokuwa kwa ajili ya matibabu, Wastara alisema kuwa, alikuwa akikiona kifo mara nyingi mno, lakini anaamini Mungu anampenda ndiyo maana amemwacha salama hadi leo.

“Nimeshamuona Israel Mtoa Roho mara nyingi sana, lakini kwa sababu Mungu ananipenda, bado ninapumua. Ninaamini Mungu atanipa uhai mrefu kutokana na majaribu niliyopitia,” alisema Wastara ambaye alikatika mguu kabla ya kufiwa na mumewe, Juma Kilowoko ‘Sajuki’ n asana anakabiliwa na magonjwa mbalimbali.

Gazeti Lililomuandika Mange Vibaya Lapewa Onyo Kali na Serikali

$
0
0
Gazeti Lililomuandika Mange Vibaya Lapewa Onyo Kali na Serikali

Serikali imelionya Gazeti la Tanzanite kwa kuchapisha picha za utupu kitu ambacho ni kinyume na maadili ya kazi hiyo.

Hatua hiyo imekuja baada msemaji wa serikali Dkt. Hassan Abbas kuahidi kulichukulia hatua gazeti hilo baada ya kupokea malalamiko mengi kutoka kwa wananchi kutokana na ukakasi wa habari zake pamoja na picha wanazochapisha.


Onyo hilo limetolewa hii leo mjini Dodoma na Msemaji wa Serikali, Dkt. Hassan Abbas alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari.

Amesema kuwa wametoa onyo kwa Gazeti hilo kwakua ni jipya pia ni mara yake ya kwanza kutenda kosa kama hilo hivyo ni bora kujirekebisha.

Amesema kuwa Gazeti hilo halikuwa na kosa katika maudhui ya kuandika ila kosa kubwa ni kutumia picha za utupu, hivyo kwenda kinyume na maadili.

Picha: Hivi Ndivyo Polepole Alivyonusurika Kufa Baada ya Msafara Wake Kupata Ajali

$
0
0
Picha: Hivi Ndivyo Polepole Alivyonusurika Kufa Baada ya Msafara Wake Kupata Ajali
Msafara wa Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM Taifa Hamphrey Polepole umepata ajali katika eneo la kijiji cha Nyamidaho, Kata ya Makere wilayani Kasulu mkoani Kigoma.


Ajali hiyo imehusisha gari aina ya Toyota V8 yenye namba T150 EWE iliyokuwa ikiendehswa dereva aliyefahamika kwa jina moja la Kibuta wakati wakielekea katika ziara ya kiongozi huyo wilayani Kakonko, mkoani humo.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kigoma ACP Martin Otieno amethibitisha kutokea kwa ajali hiyo na kueleza chanzo cha ajali hiyo kuwa ni kupasuka kwa gurudumu la nyuma upande wa kulia.

Kwa mujibu wa Kamanda Otieno, waliojeruhiwa ni pamoja na Katibu wa CCM mkoa Naomi Kapambala, Mwenyekiti wa UVCCM Sylivia Sigura pamoja na Katibu Mwenezi, Feruz ambao wamekimbizwa katika hosiptali ya wilaya ya Kibondo kwa matibabu.

Poplepole amewasili leo mkoani Kigoma na kupokelewa wilayani Uvinza akitokea mkoani Tabora ambapo atakuwa Kigoma kwa takribani siku tatu.

Kumbe Daxx Ndo Baba Kijacho wa Dayna Nyange..... Dayna Afunguka A-Z "Ujauzito Haujifichi"

$
0
0
Kumbe Daxx Ndo Baba Kijacho wa Dayna Nyange Afunguka A-Z "Ujauzito Haujifichi"
Msanii Dayna Nyange amezungumza na kuelezea skendo zilizopo za yeye kuhusishwa kutoka na Daxx ambaye ni Fashion Model na ameonekana kwenye video mpya ya Dayna Nyange ya ‘Sale Sale’ ikiwa ni pamoja na kuhusishwa kuwa mjamzito.

Dayna Nyange amesema kwamba yeye anamahusiano na Daxx lakini siyo ya kimapenzi kwani yeye anaye mpenzi wake na ishu ya yeye kuwa na mimba kasema hajawahi kusema kama ni mjamzito lakini Mimba haijifichi na kama ipo watu wataona na waandae Pampas na maziwa ya mtoto.

Simba Yadhamiria Kuwamaliza Al Masry

$
0
0
Simba Yadhamiria Kuwamaliza  Al Masry
ILI kuhakikisha wanakiimarisha kikosi chao kila upande kuelekea mchezo wao dhidi ya Al Masry kutoka Misri, wachezaji wa Simba jana walishiriki darasa la saikolojia chini ya daktari na mwanasaikolojia maarufu nchini, Chris Mauki.


Mara ya kwanza Simba kumuita mwanasaikolojia huyo ilikuwa ni katika maandalizi ya mechi ya Ligi Kuu Tanzania Bara dhidi ya Azam FC na vinara hao wa ligi waliibuka na ushindi wa bao 1-0 lililofungwa na Emmanuel Okwi.

Simba inayodhaminiwa na Kampuni ya Kubashiri Matokeo ya SportPesa inatarajia kuwakaribisha Al Masry katika mechi ya kwanza ya raundi ya Kombe la Shirikisho Afrika itakayofanyika kesho kwenye Uwanja wa Taifa Dar es Salaam.

Mauki ametoa darasa na kuwaeleza wachezaji wanavyotakiwa kujijenga ujasili pale wanapokuwa ndani ya uwanja wakipambana kusaka ushindi.

"Mwanasaikolojia huyo aliwaambia aliwaeleza namna mchezaji anavyopaswa kujitambua na kujiamini pindi anapokuwa uwanjani wakati wa mechi ili kuisaidia timu kupata matokeo chanya," alisema kiongozi mmoja.

Baada ya mechi ya kesho, timu hizo zitaendelea na mechi zao za ligi na baadaye kurejeana katika mchezo utakaofanyika Machi 17 mwaka huu katika mji wa Port Said huko Misri.

Hali ya Tundu Lissu Yazidi Kutengema Sasa Aanza Kufanya Mazoezi Mitaani

$
0
0
Hali ya Tundu Lissu Yazidi Kutengema Sasa Aanza Kufanya Mazoezi Mitaani
Hali ya afya ya Mbunge wa jimbo la Singida Mashariki na Rais wa Chama cha Mawakili Tanganyika (TLS), Mhe. Tundu Lissu imeendelea kuimarika na sasa ameanza kufanya mazoezi mitaani.

Lissu ambaye yupo nchini Ubelgiji akiwa katika matibabu alipopelekwa tangu mapema mwezi January mwaka huu, ameonekana kwenye picha kadhaa akiwa na mkewe katika mazoezi hayo.


Wameandamana Afrika Kusini Kushinikiza Ukweli wa Kifo cha Mtanzania Alieuawa

$
0
0
Wameandamana Afrika Kusini Kushinikiza Ukweli wa Kifo cha Mtanzania Alieuawa
Wanachama wa Shirika la Africa Diaspora Forum wamefanya maandamano nchini Afrika Kusini kushinikiza serikali ya nchi hiyo na ya Tanzania kubaini ukweli kuhusu kuuawa kwa mwanafunzi raia wa Tanzania mwezi February.

Baraka Leonard Naferi, mwanafunzi wa shahada ya uzamifu, alifariki baada ya kugongwa na gari la nje ya bweni la chuo kikuu.

Maafisa wa shirika hilo wameandamana kwa pamoja na baadhi ya wanafunzi na wafanyakazi wa Chuo Kikuu cha Johannesburg nje ya bweni linaloitwa Sophiatown ambapo mwanafunzi huyo aligongwa na kufariki.



Maandamano hayo yalikuwa salama na watu walikusanyika kwenye uzio mahali gari lilipo mgonga marehemu Baraka Naferi wakiwa wamebeba mabango yanayosema tunataka haki kwa Baraka, haki itendeke kwa Baraka.

Mtuhumiwa alikamatwa na polisi wa Afrika Kusini lakini baadaye akaachiliwa huru kwa dhamana. Polisi walisema hakukuwa na ushahidi wa kutosha wa kumfungulia mashtaka ya mauaji.

Ridhiwani Kikwete ndio Mbunge Anayeongoza Kupost Maendeleo ya Jimbo Lake Mtandaoni

$
0
0
Tumpongeze Mbunge huyu wa jimbo la Chalinze kwa matumizi mazuri ya mtandao wa twitter kwani haipiti siku bila yeye kupost kuhusu ujenzi wa zahanati,shule au viwanda.
Haipiti siku bila Ridhiwani kupost twitter juu ya utekelezwaji wa miradi au shughuli za maendeleo jimboni mwake.

Anaonekana akishiriki bega kwa bega na wananchi wake katika kutatua kero za jimbo lake.

Nikimuangalia Ridhiwani naanza kumkumbuka Deo Filikunjombe alivyokuwa anasimama bega kwa bega na wananchi wake kwenye kuleta maendeleo.

Hulka hii ya Ridhiwani inaelezea exposure yake kwenye hii mitandao ya kijamii ya ughaibuni ...na inamtofautisha na wenginewanaokesha mtandaoni ku-retweet news za BBC,DW na kujipendekeza kwenye twitter za CNN ili watambulike huko duniani 

Hongera Mbunge Ridhiwani na nina uhakika Ushindi wako jimboni Chalinze ni saa mbili asubuhi oktoba 2020

Soma Nafasi za Ajira Zilizotangazwa Leo

$
0
0

Kutana na Mtabibu Mongwa Mganga wa Waganga Sasa Anapatikana Mikoa Yote

$
0
0
KUTANA NA MTABIBU MONGWA MGANGA WA WAGANGA SASA WAKO MIKOANI KARIBU YOTE NCHINI...
.
HIVYO WATATOA TIBA MAENEO YOTE YA MBEYA ,DODOMA, IRINGA , MOROGORO, MWANZA,ZANZIBAR

==>KWA WALE WENYE KUHITAJI TIBA

Husafisha nyota na kutoa Pete za bahati na kwawale walio sumbuka kwaajili ya matibabu na hawakufanikiwa chochote sasa njoo ujionee miujiza hapo kwahapo bila malipo yoyote malipo baada yakazi napia humpa mtu jini la mali kwayule anaye taka kumiliki bila mashariti yoyote
Tunatibu magonjwa mbalimbali yaliyo shindikana mpenzi aliye kukimbia nakumrudisha kwa masaa 24 tu napia natoa dawa za nguvu za kiume kuurefusha uume paka pale unapotaka .
Natoa dawa za biashara na mvuto ==tunatoa dawa zauzazi kwa wale kina mama wenye matatizoya uzazi walio angaika kwa muda mrefu bila kupata mafanikio yoyote njoo umalize tatizo lako sasa
Natoa mazindiko yanyumba na mwili biashara na mvuto kazini
Kupandisha nyota ili kungaa kupandishwa cheo kazini kurudisha mali zilizo pote zilizo ibiwa kuzulumiwa
Kesi zilizo shindikana uzimaliza mara moja namengine mengi ya siri piga simu

+255 764291657
+255 764291657

Wanaume Wanaokunywa Pombe 'Perfomance' yao Kitandani ni ndogo

$
0
0
Mimi ni mwanamme na sinywi pombe wala kuvuta sigara. Naendelea
naandika uzi huu baada ya kuona mdau anauliza kunywa pombe then sex au kutokunywa pombe then sex ni wapi kuna raha?

Sasa nitajibu hii swali kwa hoja mbili
1/ Kiafya
2/ Kijamii

Kiafya

Sasa nianze kwa kuuliza unafahamu pombe ikuingiapo ubongoni mwako nini hufanyika? Kwa ufupi sana, ubongo wa mwanadamu umejazwa aina ya kemikali za mawasiliano kitaalamu huitwa neurotransmitters.

Hizi kemikali zimegawanywa katika makundi mawili, zipo ambazo kazi yake ni kuchochea utendaji sahihi wa ubongo ambazo kitaalam tunaziita excitatory neurotransmitters. Mfano glutamate.

Lakini pia zipo ambazo kazi zake ni kuslow down ufanyakazi wa ubongo yaani tunaziita inhibitory neurotransmitters. Mfano kuna gaba.

Nini hutokea baada ya pombe kuingia mwilini?

Pombe iingiapo katika ubongo wako kwanza kabisa inaenda kupungusa zaidi kiwango cha glutamate (excitatory neurotransmitter yenye kazi ya kuchochea ubongo kufanya kazi vzuri) at the same time inaongeza kwa kiwango cha juu gaba (inhibitory neurotransmitter ambayo kazi kubwa ni ku slow down ufanyaji kazi wa ubongo)

Nyote mnajua biology ya o level iliwahi kuwaonyesha ubongo na sehemu zake, kuna mtu asojua medulla au hypothalamus au cerebellum na gland km pituitary, n. K. N.K? Kuna mtu asovijua hiyo?.

Sasa nazungumzia parts ya ubongo ambayo moja ya kazi kubwa nikucontrol sexual activities yaaan hypothalamus sambamba na pituitary

Kitendo cha kupunguza kiwango cha glutamate katika ubongo huku kukiwepo na ongezeko kubwa la gaba, hupelekea kushushwa kwa kiwango cha nguvu za utendaji wa neva ndani ya hypothalamus naivyo kufanya hypothalamus na pituitary kurespond kwa *kuongeza hamu ya ngono, wakati huohuo kupunguza uwezo wa utendaji kazi wa ngono ( performance) yako.

Sasa hiyo inamaana gani? Inamaana yaivi, ukinywa pombe ndio unanyegeka lakini kwenye kugegedana utagonga kabao kamoja au viwili vya fasta fasta chali
Lakini pia nizungumzie medulla, moja ya kazi kubwa ya hii part ya ubongo ni kuongoza shuguli zote ambazo ni automatic ikiwemo na consciousness, sasa nini hutokea hapa? Pindi tu pombe ikuingiapo katika ubongo medulla hulazimika kukufanya wewe ujihisi usingizi nahivo utalala.

Sasa ndugu yangu, kwanza umenyegeka alafu performance imepungua, mbaya zaidi ukigegeda ni kamoja tu unapitiwa na bonge la usingizi, kwanini usichapiwe?

Kijamii
Katika kukaa na wanawake tofauti marafiki wakike, wote wanalalamika kutogegedwa vzuri, shida wanaume wanakunywa pombe. Lakini pia katika kukaa na wanaume wenzangu wanaotafuta ushauri na tiba zao, wanasema hawakazi zaidi ya mbili, ukifatilia shida ni wanywaji wapombe.


Endeleeni kuongeza mapato ya serikali.

By Vladimirovich Putin

Kwanini Ali Kiba Hapati Offer za Matangazo ya Makampuni Makubwa kama Diamond Platnumz?

$
0
0
Nnje ya mziki biashara ya matangazo kwa makampuni makubwa imekuwa inalipa wasanii wengi na hivi majuzi Diamond amevuta mkwanja wa Billioni 1 kukitangaza kinywaji cha ufaransa cha Bllaire

Lakini king kiba hapati offer za matangazo makubwa kwa nini?

Hana mvuto au hana management nzuri inayomuunganisha na makampuni?

Na kama hataki pesa ndogo kutoka kwa makampuni kwa nini bado anapiga show za bei raisi za fiesta na zile za vichochoroni za club za ulaya?

By Mtotomtamuu

Rick Ross Atolewa Hospitali Baada ya Afya Yake Kutengemaa

$
0
0
Rick Ross Atolewa Hospitali Baada ya Afya Yake Kutengemaa
Rapper Rick Ross ameruhusiwa kurudi nyumbani baada ya kukaa hospitali kwa siku nne akipatiwa matibabu.

Bosi huyo wa Maybach Music Group alifikishwa hospitali mjini Florida siku ya Ijumaa baada kupata tatizo la kushindwa kupumua na kupoteza fahamu.

Kwa mujibu wa mtandao wa TMZ, rapper huyo ameruhusiwa Jumatatu asubuhi kurudi nyumbani lakini bado anaendelea kupata matibabu katika makazi yake.

Mtandao huo umeongeza kuwa Ross alihamishwa katika hospitali mbili tofauti kwa ajili ya kupat matibabu kutokana na hali yake ilivyokuwa.

Mwakyembe Mgeni Rasmi Mechi ya Yanga vs Township Rollers

$
0
0
Mwakyembe Mgeni Rasmi Mechi ya Yanga vs Township Rollers
Klabu ya Mabingwa Watetezi wa Ligi Kuu Tanzania Bara kupitia msemaji wake Dismas Ten imemtangaza Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Dkt. Harrison Mwakyembe kuwa mgeni rasmi kwenye mchezo wao leo dhidi ya Township Rollers FC ya Botswa.


Taarifa ya Dismas imeeleza kuwa Waziri Mwakyembe ndiye ataongoza maelfu ya mashabiki wa soka nchini watakaojitokeza kwenye uwanja wa Taifa kushuhudia mtanange huo.

"Kwenye mchezo wa leo wa Klabu Bingwa Afrika dhidi ya Township Rollers FC toka Botswa mgeni rasmi atakuwa Mhe. Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Dkt. Harrison Mwakyembe", imeeleza taarifa hiyo.

Mchezo huu unatarajiwa kuchezwa majira ya saa 10:00 alasiri kwa saa za Afrika Mashariki  na kati katika dimba la Taifa na baada ya wiki moja timu ya Yanga itaradhimika kusafiri kwenda nchini Botswana kwa ajili ya mechi ya marudiano.

Young Lunya Afunguka Kuhusu Uhusiano wake wa Kimapenzi na Wolper

$
0
0
Young Lunya Afunguka Kuhusu  Uhusiano wake wa Kimapenzi na Wolper
Msanii wa muziki kutoka kundi la OMG, Young Lunya amefunguka kuhusu tetesi za kutoka kimapenzi na Jacqueline Wolper.

Rapper huyo amesema habari hizo hazina ukweli wowote ila zimesababishwa na ukaribu wao pamoja na umaarufu.

“Wolper ni dada ambaye ananisapoti katika muziki wangu na nilivyopata hizo taarifa sikujisikia vizuri kwa kweli, nilijisikia vibaya kwa maana tunaheshimiana sana, sijashangaa sana kwa sababu ni msanii kwa hiyo ni lazima iwe hivyo,” amesema.

Katika hatua nyingine kundi hilo limesema lipo katika mchakato wa kutoa albamu ila hilo litafanyika baada ya kutoa kazi zao kubwa ambazo wanazo kwa sasa.

Kuongeza Muda Madarakani ni Ushetani- Nape Nnauye

$
0
0
 Kuongeza Muda Madarakani ni Ushetani- Nape Nnauye
Wakati hoja ya kuongeza muda wa Rais kukaa madarakani kutoka miaka mitano hadi saba ikionekana kufifia, mbunge wa Mtama, Nape Nnauye ameibuka na kusema hatua ya baadhi ya viongozi wa Afrika kuongeza muda madarakani ni ushetani.



Kupitia ukurasa wake wa Twitter, Nape ameandika kuwa ni lazima ushetani huo upingwe kwa nguvu zote hasa na vijana, kabla haujaota mizizi na kusambaa.

Alipoulizwa jana, Nape ambaye amewahi kuwa Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo kabla ya kuvuliwa wadhifa huo na Rais John Magufuli alikiri kuwa Twitter hiyo ni yake ingawa hakuwa tayari kufafanua zaidi.

Mwishoni mwa mwaka jana, Mbunge wa Chemba (CCM), Juma Nkamia ndiye aliibua hoja ya kuongeza muda wa Rais kukaa madarakani akiahidi kuwasilisha muswada binafsi bungeni wa kufanya marekebisho ya Katiba ili kufanya uchaguzi mkuu wa Tanzania kufanyika baada ya miaka saba badala ya mitano ya sasa.

Kwa mtazamo wake, Nkamia anaamini kuwa kufanya uchaguzi kila baada ya miaka mitano ni gharama kubwa kwa nchi maskini kama Tanzania na kwamba katika kipindi cha miaka mitano, nchi imekuwa na uchaguzi wa Serikali za mitaa mwaka mmoja kabla ya uchaguzi mkuu na hivyo kufanya gharama za uchaguzi kuwa kubwa.

Anasema kutokana na hilo, Serikali badala ya kushughulikia kero za wananchi imekuwa ikishughulikia kutafuta fedha za maandalizi na uchaguzi.

Nkamia alisema inawezekana kufanya uchaguzi wote (Serikali kuu na Serikali za mitaa) kwa pamoja kama wafanyavyo Wakenya kwa kuwa na maboksi mengi wakati wa uchaguzi, badala ya kutumia gharama mara mbili kwa kipindi kimoja.

Hata hivyo, baadaye Nkamia alituma taarifa kwa vyombo vya habari kuwa ameondoa kwa muda hoja hiyo lakini siku chache baadaye hoja hiyo iliibukia Zanzibar baada ya wajumbe wa Baraza la Wawakilishi kutaka muda huo uongezwe na kuungwa mkono na Makamu wa Pili wa Rais Zanzibar, Balozi Seif Ali Idd akisema si wazo baya.

Hata hivyo, hoja hiyo ilijibiwa na Rais John Magufuli baada ya mazungumzo yake na Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Humphrey Polepole alipowataka wanachama wa CCM na umma wa Watanzania kuupuuza mjadala huo kwa kuwa haujawahi kujadiliwa katika kikao chochote cha chama na kwamba ni kinyume na katiba ya CCM na Katiba ya nchi.

Polepole akirejea mazungumzo hayo alibainisha kuwa Rais Magufuli hana mpango wowote na hatarajii kuongeza kipindi cha urais wakati wote wa uongozi wake.

Kauli ya Nape iliungwa mkono na Profesa wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), Benson Bana akisema ni ya hekima na busara.

Alisema viongozi wa Afrika wanapaswa kujua kuwa wananchi wamechoshwa na vitendo vya unyanyasaji, kung’ang’ania madaraka na kujilimbikizia mali.

Bana ambaye ni profesa wa Sayansi ya Siasa alitoa mfano wa kilichotokea Zimbabwe kuwa ni mgogoro wa kiutawala na kusababisha mdororo wa kiuchumi uliotokana na Rais Robert Mugabe kusababisha nchi hiyo kutengwa kwa kuwafukuza Wazungu nchini humo na kusababisha wananchi kukosa mahitaji muhimu.

Alisema viongozi wa Afrika wanapaswa kujifunza kuwa wawapo madarakani hawana budi kutekeleza demokrasia ya kweli na kutojihusisha na vitendo vya rushwa lakini pia kutoa haki sawa na kuwaonya waliotia pamba masikioni na kujifanya hawaoni kinachoendelea:

“Tunashuhudia matendo ya majirani zetu Uganda kwa Rais Yoweri Museveni na DRC kwa Joseph Kabila. Viongozi wanapaswa kujifunza kwa haya yanayotokea katika nchi nyingine, wasitangulize masilahi yao,” alisema.

Akizungumza kwa simu, Nkamia alisema hoja yake ipo palepale na kwamba kwa sasa anaendelea na mashauriano na viongozi wake wa chama kuona ni kwa jinsi gani ataiwasilisha.

“Wakati nimeleta hoja ile mwenyekiti wangu wa chama Taifa hakuipenda na kusema tuachane nayo lakini nikuambie tu tunaendelea na mashauriano na viongozi wangu wa chama kuona ni jinsi gani nitaiwasilisha; kama nilivyosema awali simlengi Rais aliyepo madarakani,” alisisitiza Nkamia.

Hata hivyo, Nkamia alisema anamshangaa Nape kudhani kuwa wanaong’ang’ania madaraka ni viongozi wa Afrika pekee.

“Hii ni kansa kubwa kudhani mambo ya Wazungu ni sahihi, badala ya hiyo anayosema yeye wakati hata wao wana mambo yao mengi ambayo hayaridhishi,” alisema Nkamia.

Alitoa mfano wa Waziri Mkuu wa zamani wa Uingereza, Tony Blair na Kansela wa Ujerumani, Angela Merkel ambao wameongoza kwa vipindi zaidi ya viwili na kumtaka Nape kuacha kufikiri Afrika pekee ndiyo inafanya hivyo.

Bashe Awasilisha Hoja Binafsi Kutaka Uchunguzi wa Matukio Yanayotishia Usalama, Umoja Nchini

$
0
0
Bashe Awasilisha Hoja Binafsi Kutaka Uchunguzi wa Matukio Yanayotishia Usalama, Umoja Nchini



Mbunge wa Nzega Mjini, Hussein Bashe leo amewasilisha barua ya  hoja binafsi kuunda Kamati ya Bunge ili ichunguze matukio mbalimbali yanayotishia umoja,usalama na mshikamano nchini.  Nia hiyo ameieleza katika mtandao wa Tweeter ambayo iko hapa chini.

Hata hivyo, nia hiyo imeshutumiwa na watu kadhaa akiwemo Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema, aliyesema hatua hiyo ya Bashe ni ya “unafiki”, akimtaka mbunge huyo (Bashe) akikemee chama chake kirudishe uhuru wa kufanya mikutano kwa vyama vya upinzani, kuhakikisha watu hawatekwi na kuuawa.


Vilevile Mbunge wa Kigoma Mjini, akimjibu Bashe, alisema hatua hiyo ya mbunge huyo ni mwanzo mzuri na inabidi kuungwa mkono kwani ina nia njema.

Ujumbe wa Lema na Zitto pia tunauweka hapa chini:

Sarah Umwambii Kitu kwa Harmonize Aonyesha Jeuri Pesa kwa Mpenzi Wake kwa Kumpatia Zawadi Hii

$
0
0
Sarah Umwambii Kitu kwa Harmonize Aonyesha Jeuri kwa Kumpatia Zawadi Hii

Penzi la Harmonize na mpenzi wake, Sarah bado ni moto, tena wa kuotea mbali.

Safari hii Sarah amemuonyesha Harmonize ni kwa namna gani anampenda kwa kumnunulia saa ya mkononi ambayo inatajwa kuwa ya gharama zaidi.

Katika ukurasa wake wa Instagram Harmonize aliweka kipande kifupi cha video kinachoonyesha saa hiyo na kumshukuru Sarah kwa zawadi kama hiyo na kuwataka wanaohitaji kujua gharama yake kuitafuta mtandaoni.

Saa aliyozawadiwa Harmonize inajukalikana kwa jina la Patek Philippe, saa hii katika mtandao inaoneka kuuzwa kati dola za Kimarekani 78,999 hadi 119,999. Sawa na kati ya Tsh. 177,948,749 hadi 270,308,693.
Viewing all 104687 articles
Browse latest View live




Latest Images