Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104417 articles
Browse latest View live

Mr Nice Amchana Dudu Baya "Ameyumba Kiuchumi Anasingizia Kuacha Pombe"

0
0
Mr NiceAmchana  Dudu Baya "Ameyumba Kiuchumi Anasingizia Kuacha Pombe"
Msanii muziki wa staili ya Takeu amabe anafanya vizuri kwa sasa na kibao chake kipya cha 'Tuheshimiane', Mr Nice amefunguka na kumchana Dudu Baya kuwa ameyumba kiuchumi ndio maana anasingizia kuacha pombe bila ya kusema ukweli unaomkabili.

Mr. Nice amebainisha hayo kupitia kipindi cha eNewz inayorushwa na tinga namba moja kwa vijana EATV baada ya kupita muda kidogo tokea Dudu Baya kutoa kauli yake ya kudai kwa sasa ameacha matumizi ya pombe.

"Mimi nina mpongeza kutokana sina sababu ya kumsikitia kwasababu ni maamuzi yake yeye mwenyewe, labda ameona mwili wake hauwezi kuhumudu, uchumi vitu kama hivyo. Kwa hiyo usikae kumpongeza tu muda mwingine anapaswa apewe pole maana anaweza akawa yupo katika matatizo makubwa mpaka yakamfanya akashindwa kununua hiyo pombe",amesema Mr. Nice.

Pamoja na hayo, Mr. Nice ameendelea kwa kusema "huwenda Dudu Baya ameteteleka kiuchumi ndio maana anasingizia kuacha pombe lakini mimi naendelea na maisha yangu, kuburudika ni moja ya sehemu ya maisha yangu maana wote hatuwezi tukafanana".

Aunty Lulu Awavuruga Wachina Wagombea Kumshika Wowowo Lake

0
0
Aunty Lulu  Awavuruga  Wachina Wagombea Kumshika Wowowo Lake
KATIKA hali ya kustajabisha, Wachina ambao hawakuweza kufahamika majina yao, wamenaswa wakipagawa na kugombea kumshika kalio, mtangazaji maarufu Bongo, Lulu Semagongo ‘Aunty Lulu’ nchini China.

Mrembo huyo amekwenda nchini humo hivi karibuni ambapo tukio hilo lilitokea alipohudhuria shoo ya mwanamuziki wa Tanzania anayeishi nchini humo aitwaye Zitha, iliyofanyika kwenye Ukumbi wa Shenzhen.

Kwenye video ambayo Risasi Mchanganyiko liliipata, ilimuonesha Aunty Lulu akigombewa na Wachina hao huku wengine wakionekana kumrekodi video kupitia simu zao ambapo wengi walionekana kuvutiwa zaidi na kalio kubwa la Aunty Lulu.

Akiongea na Risasi Jumatano moja kwa moja akiwa nchini China, Aunty Lulu alisema alishangazwa na jinsi Wachina hao walivyomshobokea hadi akaogopa kwani kila mtu alikuwa akimvutia kwake.

“Unajua wameshangazwa na kalio langu huku wanawake wao hawana makalio hivi, niliona wanacheza nikainuka kucheza nao hilo lilikuwa ni kosa kwangu walipagawa ile mbaya,” alisema Aunty Lulu.

Aidha, Aunty Lulu alisema kuwa kilichomtisha ni jinsi Wachina hao walivyomgombea huku wengine wakiomba kupiga naye picha na wakati walipokuwa wakipiga naye picha, kila mmoja alikuwa akimgusa kalio.

“Nilikuwa nadhani naweza kujiachia kama kwetu Tanzania lakini kwa jinsi nilivyogombewa nitakuwa makini sana maana naogopa kubakwa,” alisema Aunty Lulu.

Akielezea safari yake ya China, Aunty Lulu alisema amekwenda nchini humo kibiashara ambapo amekwenda kwa ajili ya kuchukua vitu vya dukani.

Tanzia: Aliyekuwa Mbunge wa Kigoma Mjini Afariki Dunia Muhimbili

0
0
Tanzia: Aliyekuwa Mbunge wa Kigoma Mjini Afariki Dunia Muhimbili
ALIYEWAHI kuwa Mbunge wa Kigoma Mjini, Dkt. Amani Walid Kabourou amefariki dunia usiku wa kuamkia leo katika Hospitali ya Taifa Muhimbili alikokuwa akipatiwa matibabu.

Dkt. Kabourou ambaye alizaliwa Mei 23, 1949, amewahi kuwa Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) na Mbunge wa Jimbo la Kigoma Mjini (CHADEMA) kabla ya kuhamia Chama Cha Mapinduzi (CCM) na kuwa Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Kigoma.

Aidha, Dkt. Kabourou amewahi kuwa Mbunge wa Bunge la Afrika Mashariki akiiwakilisha Tanzania kuanzia Juni 05, 2007 hadi Juni 04, 2012.

Kupitia ukurasa wake wa Facebook, Zitto Kabwe ambaye ni mbunge wa sasa wa Kigoma Mjini amesema kwao huo ni msiba mkubwa, na umewaacha na majonzi tele

“Tumeamka asubuhi na habari za kusikitisha kuwa Dkt. Amani Walid Kabourou, Mbunge Mstaafu wa Kigoma Mjini ametangulia mbele ya haki. Hakika ni msiba mkubwa kwetu. Mola ailaze roho ya marehemu mahali pema peponi,” ameandika Zitto.

Donald Trump Ameporomoka Orodha ya Matajiri Duniani, Bill Gates Ashushwa Nafasi ya Kwanza

0
0
Donald Trump Ameporomoka Orodha ya Matajiri Duniani, Bill Gates Ashushwa Nafasi ya Kwanza
Jarida la Forbes limetoa orodha ya watu matajiri duniani, Rais wa 45 wa Marekani, Donald Trump ameporomoka kwa nafasi takribani 200.

Trump ametajwa kuwa na utajiri wa dola bilioni 3.1 huku akishika nafasi ya 766 ambayo inashikiliwa na watu wengine takribani 25.

Utajiri wa Rais huyo wa Marekani umetajwa kushuka kwa dola milioni 400 ambapo kwa mwaka jana alitangazwa kuwa na utajiri wa dola bilioni 3.5.




Katika orodha hiyo mwanzilishi wa Amazon, Jeff Bezos anashika nafasi ya kwanza akiwa na utajiri wa dola bilioni 112 akimbwaga Bill Gates anayeshika nafasi ya pili akiwa na utajiri wa dola bilioni 90.

Wakati huo huo mwanzilishi wa mtandao wa Facebook, Mark Zuckerberg anashika nafasi ya tano akiwa na utajiri wa dola bilioni 71. Aliko Dangote kutoka Afrika anashika nafasi ya 100 akiwa na utajiri wa dola bilioni 14.1.

Naye Mohammed Dewj wa Tanzania anashika nafasi ya 1561 akiwa na utajiri wa doala bilioni 1.5.

Baada ya Kichapo Toka kwa Township Rollers Yafunguka Kuhusu Mchezo wa Marudio

0
0
Baada ya Kichapo  Toka kwa Township Rollers Yafunguka Kuhusu Mchezo wa Marudio
Timu ya mabingwa watetezi wa Ligi Kuu Tanzania Bara, Yanga imefunguka na kudai itahakikisha mchezo wake wa marudiano dhidi ya Township Rollers inatoka na ushindi kwa kuwa wameshawajua wapinzani wao jinsi wanavyocheza hivyo haitawapa tabu.


Hayo yamewekwa wazi na Kocha msaidizi wa timu hiyo, Shadrack Nsajigwa baada ya timu yake siku ya jana (Machi 06, 2018) kuchapwa bao 2-1 katika dimba la Taifa Jijini Dar es Salaam kwenye michuano ya ligi ya Mabingwa Afrika katika hatua ya kufuzu makundi.

"Tumepoteza lakini hiki ni kipindi kimoja, nina imani kuwa mechi yamarudiano 'away' tutajitahidi kufanya vizuri ili tupate ushindi kama walivyofanya wao kwa kuwa tumewaona jinsi wanavyocheza. Kwa hiyo kikubwa tukiwa mazoezini tutajaribu kurekebisha makosa yetu tuliyokuwa tumefanya", amesema Nsajigwa.

Pamoja na hayo, Nsajingwa ameendelea kwa kusema "tulikuwa tunawaacha sana wakimiliki mpira wao kwa muda mrefu na kupelekea kushindwa kuwashambulia na pia tulikuwa kidogo tunachelewa kurudi nyuma ili kuweza kuwadhibiti wasiweze kufanya mashambulizi katika lango letu hicho ndio kikubwa nilichokiona. Tunajua tukienda kwao Botswana wanaweza kucheza mchezo tofauti lakini sisi tunajianda kwa jinsi tulivyokwisha kuwaona hapa nyumbani".

Mechi ya marudiano kati ya Yanga SC dhidi Township Rollers FC ya Botswana inatarajiwa kupigwa Machi 17, 2018 Jijini Gaborone Botswana ambapo Yanga italazimika kushinda zaidi ya mabao 2-0 ili kuweza kujihakikishia inatinga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika.

Mwanamke Ajinyonga Hadi Kufa Kisa Bata

0
0
Mwanamke Ajinyonga Hadi Kufa Kisa Bata
Mwanamke mmoja aliyetambulika kwa jina Constansia James mkazi wa kijiji cha Kisorya, tarafa ya Nansimo wilaya ya Bunda, amejiua kwa kujinyonga baada ya tuhuma za wizi wa Bata.

Imeelezwa kuwa Marehemu aliiba bata huyo kwa jirani yake aitwaye Venaida Charles ambapo baada ya kufuatiliwa aligundulika yeye ndiye mwizi na aliamuriwa kulipa fidia kwa jirani yake, na ndipo alipoamua kujinyonga masaa machavhe baada ya hukumu hiyo.

Afisa Mtendaji wa kata ya Kisorya, Revocutus Luheneja amesema kifo hicho kimetokea juzi majira ya saa 10:00 jioni ambapo asubuhi ya siku ya tukio marehemu  Constansia (37) alituhumiwa kuiba bata na kutakiwa alipe fidia.

Luheneja amesema jirani huyo aliyeibiwa bata, alimkuta mnyama wake akiwa amechinjwa kwa muuza nyama na alipomuuliza aliyemuuzia, alimtaja marehemu Constansia na ndipo walipochukua maamuzi ya kumtaka alipe fidia.

“Venadia alichukua vifaranga vilivyoachwa na bata huyo aliyeibiwa na kwenda kwa wazazi wa marehemu Constansia kudai fidia, Lakini wakati wanaendelea kufanya taratibu za kulipana fidia, mwanamke huyo alipopata taarifa hizo alikwenda moja kwa moja ya musimu mkazi wa kijijini hicho aliyokuwa anataka kupanga na kuamua kujinyonga kwa kamba,“amesema Luheneja.

Kwa upande mwingine, Afisa tarafa ya Nansimo, Jonas Nyaoja amesema tukio hilo limesharipotiwa katika kituo kidogo cha polisi cha Kisorya na mama aliyeibiwa bata huyo anashikiliwa na polisi kwa uchunguzi.

TFDA Kuzuia Uingizaji wa Soseji Kutoka Afrika Kusini

0
0
TFDA Kuzuia Uingizaji wa Soseji Kutoka Afrika Kusini
Mamlaka ya Chakula na Dawa Tanzania (TFDA) imesema itazuia uingizaji wa soseji kutoka Afrika Kusini zilizobainika kuwa na bakteria aina ya listeria.

Uamuzi wa TFDA unatokana na soseji hizo aina ya Polony kubainika kuwa na aina hiyo ya bakteria wanaosababisha ugonjwa wa listeriosis uliosababisha vifo vya watu 180 nchini Afrika Kusini.

Msemaji wa TFDA, Gaudensia Simwanza akizungumza na Mwananchi jana alisema mamlaka hiyo inalifanyia kazi suala hilo ikiwa ni pamoja na kuzuia uingizwaji wa soseji hizo nchini.

“Tunalifanyia kazi kwa kufanya ukaguzi na kujiridhisha kama soseji husika zipo katika soko,” alisema.

Soseji hizo kwa mujibu wa habari zilizochapishwa na vyombo kadhaa vya kimataifa zinatengenezwa na kiwanda cha tiger brands unit enterprises na cha RCL foods vyote vya Afrika Kusini.

Waziri wa Afya wa Afrika Kusini, Aaron Motsoaledi alikaririwa na mitandao ya kijamii akisema ameagiza kuondolewa sokoni soseji hizo, huku akiwashauri wananchi kuacha kula.

Motsoaledi alisema ingawa kiwanda cha RCL hakijatajwa kama chanzo cha ugonjwa huo, kitengo chake kinafanyiwa uchunguzi.

Ugonjwa wa listeriosis uliibuka Desemba mwaka jana na umeshasababisha vifo vya watu 180.

Akiuchambua ugonjwa huo, daktari wa Hospitali ya Rufaa ya Bugando, George Kanani alisema listeria ni aina ya bakteria ambao hupatikana kwenye maji, udongo na kinyesi.

Alisema binadamu huambukizwa wanapotumia vyakula au maji yenye bakteria hao.

“Sababu kuu zinazosababisha listeriasis ni nyama na maziwa mabichi,” alisema.

Dk Kanani alisema bakteria hao ni hatari na husababisha kifo wanaposhambulia mfumo wa fahamu na damu.

Alisema wanaoathiriwa kwa urahisi na bakteria hao ni watu wenye kinga ya mwili hafifu, wenye umri wa miaka zaidi ya 65, wajawazito, wanaoishi na Virusi vya Ukimwi (VVU), wenye matatizo ya figo, kisukari na waliofanyiwa upasuaji.

Akielezea namna bakteria walivyoingia katika soseji, Dk Kanani alisema yawezekana kulikuwa na shida katika usafi kiwandani wakati wa kuziandaa.

“Njia ya kuepuka ni usafi, kusafisha chakula, kuacha kutumia mboga za majani mbichi, kula vyakula vilivyopikwa vizuri. Bidhaa za nyama zinatakiwa kuandaliwa katika mazingira salama,” alisema.

Tamra Capstick-Dale, mhudumu katika duka kubwa (supamaketi) nchini Afrika Kusini la Pick n Pay alikaririwa katika mitandao ya vyombo vya habari vya kimataifa akisema wameshaziondoa soseji hizo katika maduka yao.

Tovuti ya kampuni ya Tiger Brands imeweka orodha ya nchi ambazo bidhaa zake husambazwa, miongoni mwa hizo ni Tanzania.

Mbunge Aongoza Wananchi Kuua Tumbili

0
0
Mbunge Aongoza Wananchi Kuua Tumbili
Mbunge wa jimbo la Bukoba vijijini Jasson Rweikiza kwa kushirikiana na wananchi pamoja na wawindaji wameamua kuingia porini katika maeneo ya Kemondo wilaya ya Bukoba mkoani Kagera kwa ajili ya kuwaondoa Ngedere ambao wamekuwa kero kubwa kwa wananchi wa maeneo hayo.

Akiwa porini mbunge Rweikiza amesema kuwa amepokea kero nyingi za wananchi na kwakuwa ana silaha akaamua kushirikiana na wawindaji ili kuondoa wanyama hao na kuahidi kuwa zoezi hilo litakuwa endelevu mpaka wahakikishe wanyama hao waharibifu wanatoweka.

Kwa upande wao baadhi ya wananchi wamesema kuwa inawalazimu muda mwingine kushindwa kupanda mazao ya chakula kwa hofu ya wanyama huku wakiongeza kuwa ngedere wamefikia hatua ya kuingia kwenye nyumba zao na kula chakula ambacho tayari kimepikwa.

Chadema Yamjibu Msajili wa Vyama vya Siasa

0
0
Chadema Yamjibu Msajili wa Vyama vya Siasa
Wakati Chadema ikijibu barua ya Msajili wa Vyama vya Siasa, Jaji Francis Mutungi kuhusu tuhuma za uvunjivu wa sheria ya vyama vya siasa na maadili ya vyama hivyo, huenda chama hicho kikakabiliwa na mambo matatu kama adhabu.

Chadema iliwasilisha majibu ya maelezo kuhusu tuhuma hizo jana katika ofisi ya msajili yakiwa ni ya pili baada ya yaliyowasilishwa awali kutomridhisha msajili.

Awali, Chadema ilitakiwa kutoa maelezo kwa kuvunja sheria kutokana na kufanya maandamano Februari 16 baada ya mkutano wa kampeni za uchaguzi mdogo wa ubunge wa Kinondoni uliofanyika Mwananyamala kwa Kopa jijini Dar es Salaam.

Baada ya kuwasilisha majibu hayo wiki iliyopita, msajili alieleza kutoridhishwa na aliiandikia Chadema barua nyingine akitaka maelezo kuwa mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe katika mkutamo huo wa kampeni alitoa lugha za uchochezi.

Katika barua zote mbili kwa Chadema, Jaji Mutungi amekitaka chama hicho kutoa maelezo ni kwa nini kisichukuliwe hatua za kisheria kwa kukiuka sheria ya vyama vya siasa na kanuni za maadili ya vyama hiyo.

Kwa mujibu wa kanuni za Oktoba Mosi, 2007 zilizosainiwa na Waziri Mkuu wakati huo, Edward Lowassa kifungu cha 6(1)(c)(d) zinaeleza wajibu wa msajili kwa vyama vya siasa.

Kifungu 6(1)(c) kinasema, “Kuzuia kitendo cha uvunjifu wa kanuni za maadili kisiendelee na kukitaka chama au kumtaka kiongozi wa chama kujirekebisha.”

Kifungu (d) kinasema, “Kutoa onyo la maandishi kwa chama au kiongozi wa chama husika.”

Kifungu (6)(2) kinaeleza, “Iwapo baada ya kutolewa onyo la kwanza kwa mujibu wa kanuni (1)(d), chama cha siasa kitaendelea au kiongozi ataendelea kukiuka maadili hayo, msajili atakemea hadharani ukiukwaji huo wa maadili.”

Hata hivyo, katika utekelezaji wa majukumu yake, msajili ana uwezo wa kuzuia ruzuku na hata kukifuta chama cha siasa.

Katika barua ya Chadema iliyosainiwa na Kaimu Katibu Mkuu, John Mnyika iliyowasilishwa jana kwenye ofisi ya msajili imeeleza masuala kadhaa yaliyowapata ikiwamo ya viongozi wake kutekwa, kuteswa, kushambuliwa na wengine kuuawa.

Chadema katika hoja ya kwanza inamweleza Jaji Mutungi kwamba katika barua yake, “Hujaeleza chanzo au sehemu ulipoyatoa maneno hayo na wala hujaeleza kifaa au chombo cha habari kilichotumika kunukuu maneno hayo iwe rahisi kwetu kutoa maelezo. Tuhuma zako hazina ushahidi wa aina yoyote ulioambatanishwa katika barua yako.”

Pili, Chadema inasema, Februari 27, Mbowe alihojiwa na Jeshi la Polisi katika Kituo Kikuu cha Kanda Maalumu ya Dar es Salaam kuhusu kauli aliyoinukuu Jaji Mutungi ambayo ni sehemu ya ushahidi mahakamani.

“Kwa kuwa bado shauri hilo la jinai halijamalizika na wakati huohuo ofisi yako inaendelea na uchunguzi wa kimaadili wa jambo hilohilo. Tunashauri usubiri jambo hilo limalizike kwa upande wa jinai kwa sababu ni ukiukwaji wa taratibu za kimahakama kwa mamlaka mbili tofauti kushughulikia jambo moja na lenye maudhui yanayofanana na kwa mtu yuleyule,” inasema Chadema.

Tatu, chama hicho kinasema hata kama maneno aliyonukuu yalitamkwa na Mbowe azingatie kuwa moja ya wajibu wa wanachama wa Chadema ambao umeainishwa katika Katiba ibara ya 5.3.5 ambayo yamenukuliwa:

“Kuwa tayari kupambana na namna yoyote ya uonevu, ukandamizaji, udhalilishaji na ubaguzi.”

Chadema imesema Mbowe kama mwanachama hakukosea kitu chochote katika maneno hayo kwa kuwa lugha hiyo ni wajibu wa mwanachama.

Hoja ya nne, Chadema inaeleza matukio kadhaa yaliyowafika viongozi wake tangu utawala wa awamu ya tano ulipoingia madarakani Novemba 5,2015 ikibainisha ni; kushambuliwa kwa risasi kwa mbunge Tundu Lissu, kupigwa kwa silaha za jadi kwa aliyekuwa mwenyekiti Mkoa wa Mwanza, Alphonce Mawazo Novemba 14, 2015 na kutekwa na kuumizwa kwa aliyekuwa mgombea udiwani wa Buhangaza wilayani Muleba mkoani Kagera, Nelson Makoti.

Pia, kutekwa, kuteswa hadi kuuawa kwa katibu wake wa Kata ya Hananasif, Daniel John, Februari 11 na kushambuliwa kwa mapanga na shoka hadi kuuawa diwani wa Namwawala wilayani Kilombero mkoani Morogoro, Godfrey Lwena.

Breaking News: Mwenyekiti wa Mtandao wa Wanafunzi Tanzania Atoweka Katika Mazingira ya Kutatanisha

0
0
Breaking News: Mwenyekiti wa Mtandao wa Wanafunzi Tanzania Apotea Katika Mazingira ya Kutatanisha
TAARIFA zilizoenea mchana huu zinadai kuwa Mwenyekiti wa Mtandao wa Wanafunzi Tanzania (TSNP), Abdul Nondo, ambaye pia ni mwanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) anadaiwa kupotea katika mazingira ya kutatanisha na hajulikani alipo tangu jana saa sita usiku.



Marafiki za Nondo wamedai alituma ujumbe kwa viongozi wenzake wa TSNP kuwa yuko katika hatari na baada ya kutuma ujumbe huo simu yake ilikuwa ikipokelewa lakini hakuwa akiongea chochote, na baada ya muda alianza kujiondoa kwenye magroup ya WhatsApp.



Taarifa kutoka kwa mmoja wa viongozi wa TSNP kuhusu Nondo inasema hajulikani alipo wakiwemo wazazi wake.   Viongozi wa TSNP wamefika Kituo cha Polisi kilichopo Chuo Kikuu cha Dar es Salaam(UDSM) na  kutoa taarifa za kupotea kwake.



Feb 18, 2018, Nondo alijitokeza na kuikosoa mienendo ya Jeshi la Polisi na Waziri wa Mambo ya Ndani, na mara ya mwisho kuongea na wanahabari, alishinikiza Waziri  Mwigulu Nchemba ajiuzulu. Hivi karibuni pia akizungumza na wanahabari aliwataka TAHLISO waache kuwa wasemaji wa wizara na serikali na kuwataka wakumbuke majukumu yao mazito ya kusemea wanafunzi wa vyuo vikuu kwa sababu wanalipishwa ada vyuo vikuu.

Mke wa Roma Amtoa Machozi Pam D

0
0
Mke wa Roma Amtoa Machozi Pam D
SIKU chache baada ya staa wa Hip Hop Bongo, Ibrahim Mussa ‘Roma Mkatoliki’ kufungiwa na Naibu Waziri wa Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo, Juliana Shonza kutofanya sanaa miezi sita kutokana na wimbo wake wa Kibamia kukosa maadili, msanii mwenzake, Pamela Daffa ‘Pam D’ amehuzunishwa zaidi na mke wa staa huyo aitwaye Nancy kwani ni mjamzito.

Akipiga stori na Risasi Vibes, Pam D ambaye yupo chimbo akiandaa ngoma yake yenye mahadhi ya Singeli alisema, taarifa za kufungiwa kwa Roma zilimpa mshituko mkubwa na kujikuta akivaa uhalisia wa mshituko huo na alioupata Nancy ambaye yupo kwenye harakati za mwisho za kujifungua.

“Hii ishu imeniumiza, sababu Roma maisha yake yanate-gemea sanaa ya muziki na kipindi hiki alikuwa bize akisaka pesa kwenye shoo mbali-mbali ili aweze kumlea vyema mtoto wake atakaye-zaliwa. Dah! Namu-ombea sana Nancy ajifungue salama na hili litapita tu!”alisema.

Hiki Hapa Kikosi cha Al-Masry Kitakachoshuka Dimbani Leo

0
0
Hiki Hapa Kikosi cha Al-Masry Kitakachoshuka Dimbani Leo
Wapinzani wa Simba SC katika michuano ya kombe la Shirikisho klabu ya Al-Masry imetangaza kikosi chake kitakacho shuka dimbani hii leo uwanja wa taifa kutafuta ushindi dhidi ya wenyeji wao hao wa Msimbazi.



1,A Maoud,
2,Shatta,
3,M Hamdi,
4,Koffi,
5,I Salah,
6,A mouusa,
7,F shawky,
8,A shokry,
9_Gomaa
10,Bance,
11,Grendo

Kikosi cha akiba

1,Mohmoud  Ellseyd,
2,Ahmed Gouda,
3,Abou Sheashaa,
4,Said Mourad ,
5,Mostafa Marcelo
6,Isshofu Quattara,
7,Abdelnasser di maria

Rais Magufuli Apokea kwa Masikitiko Kifo cha Dkt. Kaburu

0
0
Rais Magufuli Apokea kwa Masikitiko Kifo cha Dkt. Kaburu

RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli amepokea kwa masikitizo kifo cha aliyewahi kuwa Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Kigoma, Dkt Walid Amani Kaburu kilichotokea usiku wa kuamkia leo Machi 7, 2018 katika Hospitali ya Taifa Muhimbili Jijini Dar es Salaam alikokuwa akipatiwa matibabu

“Kwa masikitiko nimepokea taarifa ya kifo cha Mwenyekiti Mstaafu waCCM, Mkoa wa Kigoma, Dkt Walid Amani Kaburu kilichotokea usiku wa kuamkia leo Machi 7, 2018 katika Hospitali ya Taifa Muhimbili Jijini Dar es Salaam alikokuwa akipatiwa matibabu..

“Dkt Walid Amani Kaburu atakumbukwa kwa mchango wake alipokuwa kiongozi katika nyadhifa mbalimbali ndani ya CCM, na alipokuwa Mbunge wa Kigoma Mjini na Mbunge wa Bunge la Afrika Mashariki,” amesema Rais Dkt Magufuli katika salam zake za rambirambi zilizotolewa kwa umma na Msemaji wa Ikulu, Gerson Msigwa.

Huyu Ndio Paka Anayeharibu Mimba kwa Wanawake

0
0
Huyu Ndio Paka Anayeharibu Mimba kwa Wanawake
Daktari wa wanyama nchini Tanzania, Dkt. Obed Kiariro amedai kuna uwezekano mkubwa wa Paka anayefugwa majumbani hupelekea kuharibu ujauzito kwa binadamu endapo mnyama huyo hatopewa matunzo mazuri yanayostahili kwa wakati.


Dkt. Kiariro ameeleza hayo kupitia kipindi cha Supamix kinachorushwa na East Afrika Radio baada ya kuwepo matatizo mengi wanayoyapata jamii ya kike (wanawake) hasa hasa pale wanapokuwa wamebahatika kushika ujauzito na kwa bahati mbaya hutokea kuharibika bila ya kujua sababu za msingi kilichopelekea kupoteza ujauzito wake.

"Kuna ugonjwa tunaita 'toxoplasmosis' kitaalamu ugonjwa huu unatoka kwa Paka ambao unapelekea kutoka kwa mimba 'abortion', kama Paka hawatibiwi vizuri wala kuwepo na matunzo ya aina yeyote basi wanakuwa na ugonjwa huo na matokeo yake wanaambukia wanadamu. Unaweza ukawa na paka nyumbani unamtunza vizuri lakini huwezi kumzuia kwa namna yeyote ile kutokutana na paka wengine wanaozurura mtaani maana wakikutana tu wanaambukizana ugonjwa huo", amesema Dkt. Kiariro.

Mtazame hapa chini Dkt. Kiariro akielezea vizuri namna ya paka anayesababisha kuharibika kwa ujauzito (mimba).

LHRC Yaitaka NEC Kufanyia Kazi Changamoto Zilizoibuliwa na Wadau

0
0
LHRC Yaitaka NEC Kufanyia Kazi Changamoto Zilizoibuliwa na Wadau
Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC)  kimeitaka Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) kufanyia kazi changamoto zilizoibuliwa na wadau wakati wa uchaguzi mdogo wa ubunge Kinondoni na Siha bila kujali udhaifu katika uwasilishaji wa changamoto hizo.

Kituo hicho kimedai kuwa kuibuliwa kwa changamoto hizo kunalenga kujenga jamii yenye haki na usawa.

Hayo yameelezwa leo Jumatano Machi 7, 2018 na Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa LHRC, Naemy Sillayo alipokuwa akijibu hoja zilizotolewa na NEC wiki iliyopita kutokana na tamko lililotolewa na asasi za kiraia.

Sillayo amesema tamko hilo halikutolewa na LHRC bali lilitolewa na umoja wa asasi za kiraia ambao kituo hicho ni mwanachama.

Sillayo amesema LHRC inakubaliana na hoja iliyotolewa na azaki ya kutaka NEC kuboresha kanuni za usimamizi wa uchaguzi na kutovibana vyombo vya habari.

“Hilo litasaidia kutoweka mipaka kwa vyombo vya habari wakati wa kutimiza jukumu la kutoa taarifa kwa umma,"amesema.

Kuhusu mashirika kunyimwa vibali vya uangalizi wa uchaguzi Sillayo amesema jambo hilo lilipeleka butwaa kwa azaki.

"LHRC pekee ndiyo asasi iliyopewa kibali kuangalia uchaguzi, tofauti na ilivyokuwa uchaguzi wa 2015; karibu asasi 400 ziliangalia uchaguzi. Asasi ziliomba lakini majibu yalikuwa nafasi zimejaa, tunasisitiza hili liangaliwe kwenye chaguzi zijazo na kutoa muda wa kutosha wa kutuma maombi kwa asasi,"amesema.

Hoja nyingine ambayo LHRC imejibu ni utaratibu mpya uliowekwa na NEC unaowataka watazamaji kuwasilisha taarifa zao ili zikaguliwe na kuridhiwa na tume.

"Utaratibu ulioanzishwa mwaka 2015 unaondoa dhana ya asasi za kiraia kuwa vyombo huru. Utaratibu huu unalazimisha ripoti ya awali ya uangalizi iwasilishwe kwa tume na ikiri kupokea ripoti hiyo ndipo Azaki zinazoangalia uchaguzi ziweze kutoa taarifa kwa umma.

" Hata hivyo tume haijaweka muda maalumu ambao itatumia kabla ya kukiri kuipokea ripoti ya uchaguzi,” amesema.

Amesema upo umuhimu wa NEC kuzishirikisha asasi za kiraia na wadau wengine katika maboresho ya sheria, kanuni na taratibu zinazoratibu utendaji wa tume hiyo na usimamizi wa uchaguzi kwa lengo la kuimarisha demokrasia nchini.

Nassari Ataka Serikali Kuwapa Wananchi Mbadala wa Bangi

0
0
Nassari Ataka Serikali Kuwapa Wananchi Mbadala wa Zao la Bangi
Mbunge wa Arumeru Mashariki (Chadema), Joshua Nassari ameitaka Serikali kuwapatia  zao mbadala wananchi wa jimbo lake ambao baadhi wamekuwa wakitegemea kulima bangi kama zao za biashara.

Akizungumza katika kikao cha kamati ya ushauri mkoa wa Arusha(RCC) leo Jumatano Machi 7, 2018 Nassari amesema wananchi hasa maeneo ya Kisimiri hawajui kilimo kingine cha biashara  zaidi ya bangi.

"Magunia mengi ya bangi yamekamatwa katika jimbo langu, lakini tulikubaliana kikao kilichopita cha RCC wananchi watafute zao mbadala walime hasa Pareto lakini hadi sasa hawajafundishwa kulima,”amesema.

Hata hivyo, Kaimu Mkuu wa Mkoa Arusha, Iddi Kimanta amesema kulima bangi ni kosa la kamwe Serikali haitawavulia.

Amesema bodi ya Pareto imeahidi kuanzia Machi itaanza kutoa elimu hivyo Nassari awe na subira.

Katibu mwenezi wa CCM Mkoa wa Arusha, Shaban Mdoe akichangia hoja amemtaka Nassari kuishukuru Serikali ya Awamu ya Tano kwa kufikia uamuzi kuwatafutia zao mbadala wananchi wa Meru.

"Nassari ashukuru sana  Serikali kwani ingeweza kupiga marufuku kilimo cha bangi kama madawa ya kulevya mengine bila kutoa mbadala" amesema.

   

Ray C Yamemfika Hapa Aamua Kuwatumia Ujumbe Mzito Marafiki Zake

0
0
Ray C Yamemfika Hapa Aamua Kuwatumia Ujumbe Mzito kwa Marafiki Zake
Staa mkongwe katika game ya muziki nchini Rehema Chalamila maaraufu kama “Ray C” ameamua kutoa ushauri kwa jamii kuhusu marafiki ambao wamejaa usaliti na kuwataka wakae mbali na kuwalinganisha na nyoka ambao mbele ya macho yako hujifanya wazuri wakati nyuma ni wabaya wako

Kupitia ukurasa wa instagram wa Ray C ameandika ujumbe huo nakusema

“Ukiona rafiki kakugeuka usije thubutu kuwa nae karibu tena huyo ni zaidi ya nyoka tena bora nyoka ukikutana naye harembi kujifanyisha mzuri kwako anakugonga tu fasta kabla hujamdhuru kuliko anayejifanya kwako mzuri ukigeuka anakun’gon’ga Rafiki Mashwain kibao mjini!☠😈#Chefusikidogo🚶‍♀️“

Kutana na Mtabibu Mongwa Mganga wa Waganga Sasa Anapatikana Mikoa Yote

0
0

KUTANA NA MTABIBU MONGWA MGANGA WA WAGANGA SASA WAKO MIKOANI KARIBU YOTE NCHINI...
.
HIVYO WATATOA TIBA MAENEO YOTE YA MBEYA ,DODOMA, IRINGA , MOROGORO, MWANZA,ZANZIBAR

==>KWA WALE WENYE KUHITAJI TIBA

Husafisha nyota na kutoa Pete za bahati na kwawale walio sumbuka kwaajili ya matibabu na hawakufanikiwa chochote sasa njoo ujionee miujiza hapo kwahapo bila malipo yoyote malipo baada yakazi napia humpa mtu jini la mali kwayule anaye taka kumiliki bila mashariti yoyote
Tunatibu magonjwa mbalimbali yaliyo shindikana mpenzi aliye kukimbia nakumrudisha kwa masaa 24 tu napia natoa dawa za nguvu za kiume kuurefusha uume paka pale unapotaka .
Natoa dawa za biashara na mvuto ==tunatoa dawa zauzazi kwa wale kina mama wenye matatizoya uzazi walio angaika kwa muda mrefu bila kupata mafanikio yoyote njoo umalize tatizo lako sasa
Natoa mazindiko yanyumba na mwili biashara na mvuto kazini
Kupandisha nyota ili kungaa kupandishwa cheo kazini kurudisha mali zilizo pote zilizo ibiwa kuzulumiwa
Kesi zilizo shindikana uzimaliza mara moja namengine mengi ya siri piga simu

+255 764291657
+255 764291657

Watuhumiwa Saba wa Wizi wa Korosho Wapandishwa Kizimbani

0
0
Watuhumiwa Saba wa  Wizi wa Korosho Wapandishwa Kizimbani
WATUHUMIWA saba raia  wa Zambia, leo Machi 7,  wamepandishwa katika  Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu wakikabiliwa na tuhuma za kula njama, wizi na utakatishaji wa fedha.


Wakisomewa  mashtaka  mahakamani hapo na Wakili wa Serikali, Mwanaamina Kombakono, akisaidiana na wakili wa serikali mwandamizi, Mutalemwa Kishenyi  watuhumiwa hao wametajwa kuwa ni Kirby Ng’andu, ambaye ni meneja uendeshaji wa kampuni ya Zambia Cargo and Logistics; Robert Christopher, wakala wa usafirishaji na Isihaka Ngubi, dereva;   Cathbert Mlugu, mlinzi;  Mrisho Mindu, Karani;  Giften John na Maulid Said.


Wamesomewa mashtaka hayo mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Huruma Shaidi,  ambapo imedaiwa kuwa  kati ya Januari 26 na Februari 2 mwaka huu,  katika kampuni ya Zambia Cargo and Logistics iliyopo Dar es Salaam, washtakiwa wote kwa pamoja walikula njama ya kutenda kosa la wizi.

Imedaiwa kuwa siku na mahali hapo, washtakiwa hao  waliiba katoni 700 za korosho zilizobanguliwa  zenye thamani ya Dola za Marekani 54,180 ambazo ni sawa na Sh. bn. 120.5 mali ya Barabara Trading Tanzania Ltd.



Imeelezwa kwamba  watuhumiwa hao wote pia walijihusisha na muamala unaohusiana na katoni hizo 700 za korosho zenye thamani hiyo ya fedha huku wakijua kuwa, mali hiyo ni zao lililotokana na kosa la wizi.



Watuhumiwa   wamekana kutenda makosa hayo na wamerudishwa rumande kwa kuwa shtaka la utakatishaji wa fedha halina dhamana na  wakili Kishenyi ameiambia mahakama kuwa upelelezi katika kesi hiyo bado haujakamilika na kesi  imeahirishwa hadi , Machi 9 mwaka huu.

Waziri Jafo Afunguka Kuhusu Kauli ya ‘U-tube’

0
0
 Waziri Jafo Afunguka  Kuhusu Kauli ya ‘U-tube’
 leo March 7, 2018 kumesambaa video ambayo ilikuwa ni kipande cha mahojiano baina ya mtangazaji wa kituo kimoja na television na Waziri wa TAMISEMI Selemani Jafo katika kipindi TV hiyo na video hiyo kuleta gumzo mtandaoni.

Waziri Jafo kwenye mahojiano hayo alitaja kifaa kinachopatikana maabara kinachoitwa U-tube na kusambaa kwa video hiyo kulitokana na watu kuhisi Waziri Jafo amekosea na amemaanisha mtandao wa YouTube na ndipo suala hilo lilipozua mijadala.

Kutokana na hilo Ayo TV na millardayo.com imemtafuta Waziri Jafo ambaye ameeleza kuwa hakukosea kusema neno hilo la U-tube, bali alimaanisha kifaa kinachotumika maabara kipindi akifafanua jinsi shule kongwe nchini zilivyo kwenye hali mbaya ya mpaka serikali ya awamu ya 5 imeamua kuzifanyia ukarabati.

“Hapo awali shule hizo unaweza ukakuta vifaa vya maabara ni chakavu, mfano Bunsen Burner na U-tube iliyokuwa inatumika miaka ya 80 zimechakaa mpaka kupoteza ubora wake lakini bado zinatumika mpaka sasa. Ndio maana serikali imeamua kuboresha shule hizo kongwe ili ziweze kurudi katika ubora wake.” – Waziri Jafo
Viewing all 104417 articles
Browse latest View live




Latest Images