Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104427 articles
Browse latest View live

Mbunge Mary Nagu Anashikiliwa na Polisi kwa Amri ya Dc wa Manyara

0
0
Mbunge wa Jimbo la Hanang, mkoani Manyara Dkt Mary Nagu (CCM) na mwenyekiti wa CCM wilaya hiyo waanashikiliwa na Jeshi la Polisi wilayani humo kwa amri ya Mkuu wa wilaya hiyo kutokana na sababu ya  kushindwa kuelewana kiutendaji.

Kwa mujibu wa mkuu wa wilaya Sarah Msafiri ameeleza kuwa ameagiza kukamatwa kwa Mbunge huyo baada ya kuchoka kumvumilia kutokana na kauli anazozitoa kwenye mikutano yake na wananchi akihamasisha wasishiriki shughuli za maendeleo.

Pia amemtuhumu Mbunge huyo kuwataka wananchi wasishirikiane naye jambo ambalo alidai ni sawa na kuwataka wananchi wasishirikiane na serikali kwa sababu yeye anasimama kama serikali

“Ni kweli tumemkamata na sababu kubwa ni kuhamasisha wananchi wasishiriki shughuli za maendeleo na pia anawataka wananchi wasishirikiane na Mimi wakati anajua Mimi nasimama kama serikali” -DC Msafiri

Kutana na Mtabibu Mwenye KUBRI kutoka kwa ALLAH simba Mtabibu wa Nyota za Binadamu na Dawa za Asili

0
0

Kutana na Mtabibu Mwenye KUBRI kutoka kwa ALLAH issa simba said Mtabibu wa Nyota za Binadamu na Dawa za Asili ya Africa Mwenye UWEZO Kubaini tatizo lako Pindi tu Utakapo Fanya Mawasilino Kupitia Wasaa Husika..JE UNASUMBULIWA NA Mapenzi? (Umeachwa na Umpendae,Awe Mume,Mke na Bado unampenda?Na Umejaribu Sehemu nyingi Bila Mafanikio?Wasilina na Maalim Hussein Ujione muujiza wa Papo kwa Papo.. anauwezo WA KURUDISHA MAHUSIANO NA KUIMARISHA NDOA YAKO NDANI YA SAA 12 TU. Umekimbiwa na Mumeo,mkeo au Mpenzi na anaishi na mtu mwingine? Muone akutatulie Anauwezo wa Hali ya Juu wa Kusambalatisha Mahusiano yao Endapo utafata Atakacho kuelekeza.
Atamfanya Atimize 5 zote kwa Muda Mfupi.
Issa simba said Anatumia Jina la Muhusika au Picha Kumal6uiza Tatizo lako..
Anatibu kwa Kutumia Vitabu vya QUR-AN Dawa za Asili za Africa,Dawa za Kiarabu na Majini.Anatafsiri Ndoto. Kushinda BAHATI NASIBU, KUSAFISHA NYOTA. Mvuto wa Mwili na BIASHARA, Kinga ya Mwili,ZINDIKO za Nyumba.MIGUU Kufa GANZI.Kufungua KIZAZI kwa wale walio fungwa kwa njia za KISHIRIKINA. Anakupa Jini la Mali kwa yule anaehitaji Utajiri BILA MASHARTI. Nguvu za KIUME, Humaliza Kesi zilishindika ndani ya siku 14 tu..na mengi zaidi +255 622588038au 0679119679 au +255 764318107
NB: TIBA KWA DINI ZOTE NA IMANI ZOTE...

DAR: Mnara wa Simu Waangukia Kituo cha Polisi Goba, Huduma Zasimama

0
0
Huduma zimesimama katika kituo cha Polisi cha Goba jijini Dar, baada ya mnara wa simu kuangukia kituo hicho, kutokana na upepo wa mvua iliyonyesha jana usiku

Diva Afunguka "Aslay Nitafanya Nae Anipe Mbegu zake Nipate Mtoto"

0
0
Diva aanza tena Kutuchanganya Afunguka haya "Aslay Nitafanya Nae Anipe Mbegu zake Nipate Mtoto"

Tazama VIDEO Hapa Chini:

Naziona Dalili za Kumwacha Mke Wangu..Kwa Hili Siwezi Vumilia

0
0
Ndugu zangu mwenzenu yamenikuta makubwa. Mimi nimeoa nikiwa mtu mzima sana. Tofauti ya umri na mke wangu ni miaka kumi na kenda. Miezi sita ya kwanza ndoa yetu ilikuwa ya furaha sana na hakika nilionja raha majinuni ya ndoa. Baada ya hapo ni mateso makubwa sana.

"Hasikii la mwadhini wala la mtia maji msikitini"

Mke wangu kaanzisha tabia chafu sana na isiyo mpendeza MUNGU na walimwengu pia. Ilikuwa ni mwezi wa saba wa ndoa yetu usiku wa maanani ndipo kiini cha dukuduku langu lilipoanza. Baada ya kufanya tendo la ndoa kwa raundi ya kwanza ndipo mke wangu mpendwa aliponiomba "twende chooni" akimaanisha nimwingilie kinyume na maumbile.

Kwakweli ilibidi nifanye ili kumridhisha na kumuonya kwamba iwe ni siku ile pekee. Kuanzia hapo mke wangu kaweka msimamo kuwa hanipi haki yangu mpaka nimpe "kiu yake"

Nafikiria kumpa taraka mke wangu ukizingatia bado hatujazaa.

Naombeni ushauri wana mmu wapendwa.

".Heri kufa macho kuliko moyo"

Soma Nafasi za Ajira Zilizotangazwa Leo Alhamisi

0
0

Rais Magufuli Atoa Ujumbe Huu kwa Wanawake

0
0

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli amewapongeza wanawake wote duniani na kuwatakia kheri katika siku ya Wanawake Duniani inayoadhimishwa kila ifikapo Machi,8 ya kila mwaka.

Rais Magufuli kuupitia mtandao wa kijamii wa Twitter,ametoa salamu hizo huku akisihi jamii kuwaheshimu wanawake na kuwapa ushirikiano na kutambua juhudi za wanawake katika jamii yetu.


Dr John Magufuli

@MagufuliJP
Nawapongeza wanawake wote kwa kusherehekea siku yenu ya leo na hasa kwa mchango wenu mkubwa mnaoutoa kwa jamii. Daima tutaendelea kuwaheshimu, kuwapa ushirikiano na kutambua juhudi zenu katika kujenga ustawi wa jamii yetu.

Nawapongeza wanawake wote kwa kusherehekea siku yenu ya leo na hasa kwa mchango wenu mkubwa mnaoutoa kwa jamii. Daima tutaendelea kuwaheshimu, kuwapa ushirikiano na kutambua juhudi zenu katika kujenga ustawi wa jamii yetu.

Rais wa TFF Atuma Salamu za Rambirambi Cyprus

0
0
Rais wa TFF Atuma Salamu za Rambirambi Cyprus
Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania TFF Ndugu Wallace Karia ametuma salamu za pole kwa Chama cha Mpira wa Miguu Cyprus kufuatia kufariki kwa aliyekuwa Rais wa FA Costakis Koutsokoumnis.

Rais wa TFF Ndugu Karia amesema amepokea taarifa hizo kwa masikitiko makubwa kwa kumpoteza mmoja wa viongozi wakongwe wa mpira wa Miguu.

Koutsokoumnis alikuwa muhimiri mkubwa kwa soka la Cyprus na amefariki katika wakati ambao Cyprus na mpira kiujumla ulikuwa unamuhitaji,nimesikitishwa na kifo chake na ninatoa pole kwa familia yake,FA ya  Cyprus,FIFA na familia ya soka kwa ujumla” Alisema Rais wa TFF Ndugu Karia.

Mpaka mauti yanamkuta Koutsokoumnis alikuwa ndio Rais wa FA ya Cyprus na amekuwa kwenye kamati mbalimbali za FIFA akiwa Makamu Mwenyekiti na alianza kutumikia soka la Cyprus tokea mwaka 1990.

Amewahi kuwa Makamu wa Rais wa FA ya Cyprus kabla ya kuchaguliwa kuwa Rais wa FA hiyo mwaka 2001 nafasi aliyoitumikia mpaka mauti yanamkuta.

Koutsokoumnis amefariki Machi 5, 2018 akiwa na miaka 61 baada ya miezi kadhaa ya kupigana kupona ugonjwa wa kansa uliokuwa unamsumbua.

Mvua Yaleta Maafa kwa Jeshi la Polisi

0
0
Mvua Yaleta Maafa kwa Jeshi la Polisi
Mvua zilizoambatana na upepo mkali zilizonyesha usiku wa jana zimeacha athari kubwa kwa Jeshi la Polisi kwa kuharibikiwa na jengo lao la ofisi pamoja na kujeruhiwa askari mmoja.


Akizungumza Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Kipolisi wa Kinondoni,  ACP Muliro Jumanne Muliro amekiri kutokea kwa tukio hilo na kusema ofisi ndogo iliyopo ndani ya jengo la serikali ya Mtaa wa Goba limeharibika kufuatia kuangukiwa na nguzo ya mnara wa simu kuangukia.

"Askari mmoja amejeruhiwa katika ajali hiyo ila alifanikiwa kukimbizwa katika hospitali ya Taifa Muhimbili kwa matibabu", amesema Kamanda Muliro.

Mbali na tukio hilo, mvua zilizonyesha usiku wa jana (Machi 07, 2018) zimeweza kuwaathiri pia baadhi ya jamii kwa kuezua paa za nyumba zao na kusababisha kukosa makazi.

Johari Amweka Wazi Mwanaye wa Miaka 3 Afunguka Kuuzu Aliyezaa Naye

0
0
Johari Amweka Wazi Mwanaye wa Miaka 3 Afunguka Kuuzu Aliyezaa Naye
Msanii filamu nchini Tanzania, Blandina Chagula maarufu kama Johari kwa mara ya kwanza amekiri kuwa na mtoto wa kike mwenye umri wa miaka 3 japokuwa mpaka sasa hataki kuweza wazi kama amezaa na Ray Kigosi au laa.

Johari ameeleza hayo wakati alipokuwa anajibu swali la Mwajuma Kawina aliyetaka kujua maendeleo ya mtoto wake aliyempa jina la Maria kwenye kipindi cha KIKAANGONI kinachorushwa mubashara kila siku ya Jumatano kuanzia saa 8:00 hadi 10:00 alasiri.

"Maria hajambo kabisa, yupo nyumbani. Siwezi kumuingiza mwanangu katika kuigiza maana huwezi kufahamu kipaji cha mtu akiwa bado mdogo maana ndio kwanza ana miaka mitatu", amesema Johari.

Nyota Wanne wa Kimataifa Watajwa Katika Kikosi cha Taifa Stars Kitakachokabiliana na Algeria, DR Congo

0
0
Hiki Hapa Kikosi cha Taifa Stars Kitakachokabiliana na Algeria, DR Congo

KOCHA wa Timu ya Taifa ya Soka Tanzania (Taifa Stars), Salum Mayanga, leo Machi 8, ametaja majina ya wachezaji 23 watakaoingia kambini kwa ajili ya michezo miwili ya kirafiki mwezi huu.

Katika orodha hiyo aliyoitaja asubuhi hii kwenye makao makuu ya shirikisho la soka nchini TFF Karume Ilala, Mayanga amewajumuisha kikosini nyota wanne wa kimataifa akiwemo nahodha Mbwana Samatta, Thomas Ulimwengu anayechezea klabu ya AFC Eskilstuna ya Sweden, Mlinzi wa Baroka FC ya Afrika Kusini, Abdi Banda na Faridi Mussa anayechezea Club Deportivo Tenerife ya Hispania.

Katika majina hayo 23 Simba imeongoza kwa kuchangia wachezaji wengi zaidi ambao ni 6 huku Yanga ikitoa wachezaji 5 huku nahodha wa Singida United Mudathir Yahya naye akijumuishwa kikosini

Taifa Stars inatarajia kucheza michezo miwili ya kirafiki ikianzia ugenini nchini Algeria Machi 22 dhidi ya wenyeji, The Greens kabla ya kurejea nyumbani, Dar es Salaam kuwakaribisha DR Congo Machi 27 Uwanja wa Taifa.

Ujumbe wa Lady Jaydee, Salama, Batuli na Mimi Mars Katika Siku ya Wanawake Duniani

0
0
Ujumbe wa Lady Jaydee, Salama, Batuli na Mimi Mars Katika Siku ya Wanawake Duniani
Ikiwa leo ni siku ya Wanawake Dunia watu mbali mbali wamekuwa na la kuzungumza katika siku hiyo muhimu.

Wasanii wa muziki, waigizaji na watangazaji wa kike wametumia mitandao ya kijamii kuizungumzia siku hiyo. Hivi ndivyo walivyoandika Lady Jaydee, Salama, Batuli na Mimi Mars
mimi_mvrs11HAPPY WOMENS DAY TO ALL THE FEMALES IN THE WORLD! God Bless Us and cheers to our day 🥂although we know WE RUN THE WORLD GIRLS 💪🏾 and let’s try support and empower each other this year and forever 🙏🏾 Let’s refuse to hate on each other Buh encourage and uplift our spirits because together We Are Magic 😃❤ LOVE YOU SISTERS✌🏽
Heri ya Siku ya Wanawake Duniani. Najipa Tuzo 3 za mwanamke jasiri mimi mwenyewe kwasababu nafahamu fika kuwa nastahili 🥇🥈🥉 . Shauri yako kama unasubiri kulala na mtu ili kupewa
officialbatuliactressNguvu Yetu Haina Mfano Katika Dunia
Uwingi Wetu Huonyesha Wazi Sisi Ndio Wenye Dunia
Tunapatikana Kila Mahala Na Tukikosekana Mambo Hayaendi Sawa
Hakuna Nyumba Inakosa Mwanamke Ila Zipo Nyumba Hazina Wanaume 💪🏾
Happy Women’s Day World 😘
#LetsCelebrateOurDay💕
#TagWanawakeTu
#ShowLove❤

Dear Always, Kama Tu Mkiweza Tengeneza Pedi Zishochuna Na Kuwasha Mngekua Mashujaa Zaidi Kwa Wengi Wetu... Happy Thank You!

Kihistoria, siku hiyo ilianza kwanza kwa kuitwa siku ya wafanyakazi wanawake ya kimataifa.

Maadhimisho yalianza March 8, 1857 baada ya wafanyakazi katika kiwanda cha nguo jijini New York nchini Marekani kugoma kutokana na mazingira mabaya ya kazi hali hiyo ilipelekea takribani wanawake 129 walipoteza maisha kutokana na moto kiwandani hapo

Mwaka 1910, nchini Denmark kulifanyika kongamano kuwakumbuka wanawake hao waliofariki na walipitisha kuwa March 8 ya kila mwaka, ifanyike siku ya Wanawake Duniani.

December 1977, Baraza Kuu la UN lilipitisha na kutangaza kuadhimisha Siku ya Haki za Wanawake na Amani ya Kimataifa.

Rais John Magufuli Anatarajiwa Kuzindua Tawi la Benki Chato

0
0
Rais John Magufuli  Anatarajiwa Kuzindua Tawi la Benki Chato
Rais John Magufuli kesho Machi 9, 2018 anatarajiwa kuzindua tawi la benki ya CRDB katika jengo jipya lililopo eneo la mlimani mjini Chato mkoani Geita.

Taarifa iliyotolewa leo na mkuu wa Wilaya ya Chato Shaban Ntarambe, inaeleza kuwa hafla ya uzinduzi wa tawi hilo itaanza saa mbili asubuhi katika eneo lilipo jengo jipya la benki hiyo.

Ntarambe amewataka wananchi wa Chato na maeneo ya jirani kujitokeza kumsikiliza rais na kushuhudia uzinduzi huo ambao unaendelea kufungua fursa za kiuchumi kwa wananchi.

Baadhi ya wananchi wa mjini Chato wamepongeza juhudi zinazofanywa na wadau wa maendeleo kusogeza huduma karibu na wananchi na kusema Chato ya sasa sio kama ya zamani na kwamba, uwepo wa miundombinu hiyo inafungua maendeleo.

Dawa Bora za Nguvu za Kiume na Kukosa Hamu ya Tendo la Ndoa

0
0

DAWA BORA ZA NGUVU ZA KIUME NA KUKOSA HAMU YA TENDO LA NDOA
Baada ya utafiti wa muda mrefu juu ya matatinzo ya upungufu wa nguvu za kiume na ukosaji wa hamu ya tendo la ndoa ama kushindwa kurundia tendo kwa haraka Sasa inakuletea suluhisho juu ya matatizo haya kwa kutumia dawa za FULL POWER

Full Power dawa asili yenye vidonge inayotibu tatizo la upungufu au ukosefu wa nguvu za kiume dawa hii inamchanganyiko wa kutosha kuzalisha vichocheo vingi vya hernone za gestro gen zikiwemo vitamin b6 na b1 vitamin e pamoja na madini aina ya zinc

Itakufanya kuwa na nguvu na mzunguko mzuri wa damu na kuongeza hamu na uwezo wakufanya tendo la ndoa zaidi hatua nne au zaidi na kuchelewa kufika kileleni zaidi ya dakika 20/30 ZAT 50

Inarundisha maumbile ya uume yaani kurefusha na kunenepesha nchi 3/7 na upana cm 3/4 standard.kiafya haijalishi umri wako hata kwa wazee ukitumia maumbile yatabaki kuwa hivyo siku zote pia anatibu matatizo mengine kama presha kisukari ngiri chango la tumbo kujaa gesi kutopata choo vizuri minguu kuwaka moto matatizo ya uzazi bawasili na magonjwa ya zinaa kama kisonono na kaswende

Tunapatikana Dar es Salaam  na mikoan wasiliana na DR Oshinda no 0755505099 au 0714126118  Karibuni kwa hunduma bora

Jeshi la Polisi Mkoani Iringa Lafungua Jalada la Uchunguzi Juu ya Kutekwa kwa Abdul Nondo

0
0
Jeshi la Polisi Mkoani Iringa Lafungua Jalada la Uchunguzi Juu ya Kutekwa kwa Abdul Nondo
Jeshi la Polisi mkoani Iringa limefungua kuwa jalada la uchunguzi kwa lengo la kufahamu ukweli juu ya Mwenyekiti wa mtandao wa wanafunzi Tanzania, Abdul Nondo anaedaiwa kutekwa na watu wasiojullikana na kutelekezwa wilayani Mufindi.

Kamanda wa polisi Mkoa wa Iringa, Juma Bwire amesema Nondo aliripoti kituo cha polisi cha Mafinga wilayani Mufindi.

“Baada ya kumhoji Nondo alisema kuwa alitekwa na watu wasiojulikana ambao walimtekeleza Wilaya ni Mufindi,” -Kamanda Bwire

“Tunaendelea kufanya uchunguzi kama ametoa taarifa za uongo kwa nia ovu kwa lengo la kutaka kuhamasisha wanafunzi wenzake ili kuleta uvunjifu wa amani nchini tutamshughulikia kama wahalifu wengine na kama kweli atakuwa ametekwa tutawasaka wahalifu,” -Kamanda Bwire.

Evans Aveva Hali Tete Alazwa ICU Muhimbili

0
0
Evans Aveva Hali Tete Alazwa ICU Muhimbili

Rais wa Klabu ya Simba, Evans Aveva amelazwa katika kitengo cha wagonjwa mahututi Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH).

Hayo yameelezwa leo Machi 8 mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Wilbard Mashauri na wakili anayewatetea, Evodius Mtawala wakati kesi hiyo ilipotajwa mahakamani hapo.

“Mshtakiwa wa kwanza Aveva, tangu jana amelazwa katika kitengo cha wagonjwa mahututi hali yake siyo nzuri," ameeleza wakili Mtawala.

Hata hivyo, mwendesha mashtaka wa Takukuru, Leonard Swai naye ameliambia mahakama kuwa Aveva ni mgonjwa na kwamba upelelezi wa kesi hiyo bado haujakamilika.

Baada ya kutolewa kwa maelezo hayo, Mtawala ameiambia mahakama kuwa walizungumza na upande wa mashtaka wataeleza jalada la kesi hiyo bado lipo kwa Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP) na wameomba wapewe siku 14 ili waweze kueleza kitu.

Hakimu Mashauri ameiahirisha kesi hiyo hadi Machi 22, 2018.

Wakati kesi hiyo ikitajwa mahakamani hapo alikuwapo Godfrey Nyange maarufu Kaburu ambaye ni makamu wa rais wa Klabu ya Simba.

Washtakiwa hao wanakabiliwa na mashtaka matano ya  uhujumu uchumi ikiwamo kughushi, kuwasilisha nyaraka ya uongo na kutakatisha wa kiasi hicho cha fedha.

Washtakiwa hao wapo mahabusu kutokana na kukabiliwa na mashtaka ya utakatishaji fedha ambayo hayana dhamana kwa mujibu wa sheria.

Shamsa Ford Atoa ya Moyoni Kuhusu Bongo Movie

0
0
Shamsa Ford Atoa ya Moyoni Kuhusu Bongo Movie
Leo March 8, 2018 Muigizaji wa Bongo Movie Shamsa Ford ameeleza ya moyoni baada ya maneno ya watu kudai kuwa Bongo Movie imekufa kutokana na zile kazi za zamani kutoonekana tena mtaani.

Kupitia ukurasa wake wa Instagram amewaomba directors kurudisha Bong movie kwenye soko kwani ndio msingi mkubwa  wa kuwapatia kipato na kutekeleza majukumu katika  familia hata kama wengine hawalioni hilo.



“Nilipoangalia hii tamthilia (bwana samlati )kiukweli nililia mpaka kwikwi utasema ni kweli kikubwa nilichogundua ni kwamba story, director na uchezaji ni vitu muhimu vya kuzingatia..ila sisi daaa sijui tutafika lini  huku    @jb_jerusalemfilms @richiemtambalike @raythegreatest@joharichagulatz @cloud112_mina_new@mrutu_lion @ johnlister fanyeni kitu jamani nyie ndo wenye bongo movie pls irudisheni.”

“kupitia nyie imetusaidia wengine kupata ajira na kuendesha familia zetu. sasa hivi bongomovie ilipo naumia kwasababu Mimi ni mmoja ambae ninaishi kutokana na kazi yangu si kama wale wanaosema hawaishi kwa kutegemea movie..Nawategemea wakubwa wangu pls”

Johari apigana na Chuchu kisa penzi la Ray?

0
0
Ilisemekana kuwa Johari na Ray walikuwa wapenzi hadi waliofanikiwa kuzaa mtoto lakini baadaye akamsaliti na Chuchu na kusababisha ugomvi.. Mwenyewe afunguka kila kitu

VIDEO:

Zahara Zaire Akanusha Kuolewa na Alikiba

0
0
 Zahara Zaire Akanusha Kuolewa na Alikiba
Video vixen kutoka nchini Kenya aliyeng’ara katika ngoma ya Alikiba na Christian Bela ‘Nagharamia’ Tanasha Donna Barbieri Oketch a.k.a Zahara Zaire , amekana taarifa za kufunga ndoa na hit maker wa ‘ Seduce’ Alikiba.

Tanasha amekana taarifa hizo ikiwa ni wiki moja kupita tokea ripoti idai kuwa wawili hao wanamatarajio ya kufunga ndoa.
Mrembo huyo amekana taarifa hizo kupitia mtandao wa kijamii wa Snapchat kwa kuandika.

“I would like to clarify that the rumour that has been going round on numerous Tanzanian IG pages and blogs claiming that Ali Kiba and I are engaged are COMPLETELY FALSE. Kiba and I once worked together but have never been an item. #Falserum


Kingu: Kutekwa na Kuuawa ni Jambo la Kawaida Bunge Lisiunde Tume ya Kuchunguza

0
0
Kingu: Kutekwa na Kuuawa ni Jambo la Kawaida Bunge Lisiunde Tume ya Kuchunguza
MBUNGE wa Singida Magharibi kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Elibariki Kingu amedai kuwa vitendo vya watu kutekwa na kuuawa ni jambo la kawaida huku akilishauri Bunge kutounda Tume kuchunguza kwani itazua taharuki na Serikali haijashindwa kusimamia usalama wa nchi na raia wake.

Kingu amesema kuwa, matukio ya kihalifu yapo kila utawala na hakuna Taifa linaloweza kwenda bila ya kuwa na uhalifu.

Kauli yake inakuja wakati Taifa bado liko kwenye sintofahamu kuhusu kutekwa nyara kwa msanii Roma Mkatoliki na wenzake watatu, kupigwa risasi kwa Mbunge Tundu Lissu, Azory Gwanda, Ben Saanane, Salma Said na mauaji Alphonce Mawazo, Daniel John na Godfrey Lwena na mauaji ya wananchi wilayani Kibiti, Rufiji, Mkuranga- Pwani.

Kauli ya Kingu imekuja kama majibu kwa Mbunge wa Nzega, Hussein Bashe aliyewasilisha kwa Katibu wa Bunge barua ya kusudio la kuwasilisha Hoja Binafsi ya kuunda Kamati Teule ya Bunge kuchunguza matukio mbalimbali yanayoonesha kutishia umoja, usalama na mshikamano wa Taifa letu.

Viewing all 104427 articles
Browse latest View live




Latest Images