Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104417 articles
Browse latest View live

Mtanzania Aliyeuawa Afrika Kusini Mwili Wake Watua Dar Kuzikwa Leo Kisutu

0
0
Mtanzania Aliyeuawa Afrika Kusini Mwili Wake Watua Dar Kuzikwa Leo Kisutu
Mwili wa mwanafunzi Mtanzania aliyeuawa Afrika Kusini wiki mbili zilizopita umewasili nchini juzi usiku.

Baraka Nafari aliyekuwa Mhadhiri katika Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustino, Mwanza aliuawa usiku wa kuamkia Februari 23, huko Johannesburg, Afrika Kusini na watu wasiofahamika.

Habari zinasema aligongwa na gari mara mbili kwa kubamizwa ukutani.

Nafari alikuwa nchini humo akichukua masomo ya Shahada ya Uzamivu (PhD) katika Chuo Kikuu cha Johannesburg na alitarajiwa kuhitimu Juni mwaka huu.

Habari zilizolifikia gazeti hili zilisema, mwili wa Mtanzania huyo uliwasili nchini juzi usiku na unatarajiwa kusafirishwa leo saa tatu asubuhi kwenda Kigoma na baadaye Kasulu kwa mazishi.

Mke wa marehemu, Naomi Baraka alithibitisha kuwasili kwa mwili huo.

“Tumearifiwa kwamba mwili wa marehemu utawasili Kigoma kesho (leo) saa tano asubuhi na baada ya hapo utasafirishwa hadi Kasulu ambako nadhani kama mambo yatakwenda sawa tutazika alasiri,” alisema Naomi.

Baada ya mwili wa marehemu Nafari kufikishwa jijini Dar es Salaam Jumatano saa mbili usiku ulihifadhiwa Uwanja wa Ndege wa Julius Nyerere hadi leo alfajiri ambako unatarajiwa kusafirishwa kwa ndege ya Air Tanzania kwenda Kigoma.

Binamu wa marehemu, Uwezo Edward, anayeishi Cape Town alinukuliwa na baadhi ya vyombo vya habari akisema utata wa mazingira ya mauaji yametokana na ushahidi wa video ya (CCTV) wa siku ya tukio katika eneo alipokuwa ndugu yake huyo.

Alisema video ya CCTV, inaonesha Nafari na mwenzake walikuwa wanafuatiliwa nyuma na teksi ambayo ilikuwa na watu wawili ndani yake.

Uwezo alisema kufuatiliwa kwa tukio hilo na polisi wa Afrika Kusini kulianza baada ya yeye kutoa taarifa katika ubalozi wa Tanzania nchini humo.

Taarifa ya wanafunzi ilikosoa kile ilichokiita kuachiwa katika mazingira ya utata kwa wahusika wa tukio hilo ambao tayari walikuwa wametiwa mbaroni na polisi.

Msemaji wa wizara ya Mambo ya Nje, Mindi Kasiga akizungumza na vyombo vya habari alithibitisha kifo cha mwanafunzi huyo na kwamba walikuwa wakifuatilia taarifa zaidi kupitia ubalozi.


Video: Lulu Diva Afunguka Kuhusu Kumtelekeza Mtoto Wake Kijijini

0
0
Video: Lulu Diva Afunguka Kuhusu Kumtelekeza Mwanaye Kijijini

Msanii wa Bongofleva Lulu Diva ameendelea kuingia kwenye Headlines na hii ni baada ya kusambaa kwa story kwenye mitandao ya kijamii ya kwamba ana mtoto ambaye amemuacha kijijini kwa muda mrefu na kutokana na kumuacha muda mrefu mtoto huyo amuiti mama ila anamuita Dada.
 

Kenyatta, Odinga Wakutana Uso kwa Uso Wafanya Mazungumzo ya Siri

0
0
Kenyatta, Odinga Wakutana  Uso kwa Uso  Wafanya Mazungumzo ya Siri
Rais wa Kenya, Uhuru Kenyatta amekutana na Kiongozi Mkuu wa Umoja wa Vyama vya Upinzani nchini humo, Raila Odinga na kufanya mazungumzo ya siri.

Wawili hao wamekutana leo Machi 09, 2018 na kufanya mazungumzo yao Ikulu jijini Nairobi ikiwa ni masaa machache tangu aingie nchini humo Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani, Rex Tillerson.

Bado haijajulikana ni jambo gani wameongea wawili hao ambao ndiyo walikuwa wagombea urais wenye nguvu kwenye uchaguzi mkuu uliofanyika mwaka 2017.

Vyombo vya habari nchini Kenya vimedai kuwa kwenye mazungumzo hayo huenda wakagusia masuala ya kisiasa ambayo bado ni gumzo na tishio la usalama nchini humo.

Hata hivyo, Leo Rais Kenyatta baada ya mazungumzo hayo amepanga kuongea na Waandishi wa Habari baada ya kumaliza mazungumzo yake na Raila Odinga.

Kutana na Mtabibu Mwenye KUBRI kutoka kwa ALLAH simba Mtabibu wa Nyota za Binadamu na Dawa za Asili

0
0
Kutana na Mtabibu Mwenye KUBRI kutoka kwa ALLAH issa simba said Mtabibu wa Nyota za Binadamu na Dawa za Asili ya Africa Mwenye UWEZO Kubaini tatizo lako Pindi tu Utakapo Fanya Mawasilino Kupitia Wasaa Husika..JE UNASUMBULIWA NA Mapenzi? (Umeachwa na Umpendae,Awe Mume,Mke na Bado unampenda?Na Umejaribu Sehemu nyingi Bila Mafanikio?Wasilina na Maalim Hussein Ujione muujiza wa Papo kwa Papo.. anauwezo WA KURUDISHA MAHUSIANO NA KUIMARISHA NDOA YAKO NDANI YA SAA 12 TU. Umekimbiwa na Mumeo,mkeo au Mpenzi na anaishi na mtu mwingine? Muone akutatulie Anauwezo wa Hali ya Juu wa Kusambalatisha Mahusiano yao Endapo utafata Atakacho kuelekeza.
Atamfanya Atimize 5 zote kwa Muda Mfupi.
Issa simba said Anatumia Jina la Muhusika au Picha Kumal6uiza Tatizo lako..
Anatibu kwa Kutumia Vitabu vya QUR-AN Dawa za Asili za Africa,Dawa za Kiarabu na Majini.Anatafsiri Ndoto. Kushinda BAHATI NASIBU, KUSAFISHA NYOTA. Mvuto wa Mwili na BIASHARA, Kinga ya Mwili,ZINDIKO za Nyumba.MIGUU Kufa GANZI.Kufungua KIZAZI kwa wale walio fungwa kwa njia za KISHIRIKINA. Anakupa Jini la Mali kwa yule anaehitaji Utajiri BILA MASHARTI. Nguvu za KIUME, Humaliza Kesi zilishindika ndani ya siku 14 tu..na mengi zaidi

Piga simu +255 622588038au 0679119679 au +255 764318107

NB: TIBA KWA DINI ZOTE NA IMANI ZOTE...

Babu Seya Yupo ‘Singo’ atafuta mama wa kumfulia. .

0
0

Babu Seya Yupo ‘Singo’ atafuta mama wa kumfulia. .

Papii amesema wakati anakwenda jela alimwacha mchumba’ake na mtoto, Baba yake, Nguza Viking ‘Babu Seya’ amesema kipindi hicho hakuwa na mke kwani aliyekuwa mkewe ambaye ni mama yao akina Papii alikwa amefariki dunia.

‘’Nipo singo, natafuta mama mmoja mzee wakunifulia tu’ Babu Seya Afunguka.

Breaking News: Uhuru Kenyatta na Raila Odinga Wamaliza Bifu Lao

0
0

NAIROBI, KENYA: Rais Uhuru Kenyatta na kiongozi wa NASA, Raila Odinga wamezungumza na kukubaliana kumaliza mgawanyiko uliopo na kuliunganisha taifa hilo kuwa moja

Raila Odinga amesema yeye pamoja na ndugu yake Uhuru Kenyatta wamekubaliana kuwa mgawanyiko ulikuwepo toka enzi za uhuru unaisha tangu leo

Kwa upande wa Uhuru Kenyatta amesema taifa la Kenya ni kubwa kuliko mtu yeyote, hivyo lazima viongozi waungane ili wananchi na taifa kwa ujumla liungane

Makubaliano hayo ya viongozi hao wawili yamekuja baada ya kufanya mazungumzo leo asubuhi Machi 9, 2018 katika jengo la Harambee House

Begi Lenye Viganja 54 vya Mikono ya Binadamu Laokotwa

0
0

URUSI: Begi lenye viganja 54 vya binadamu waliouawa kikatili lakutwa katika barafu. Hakijafahamika vilikatwa kwa nani na kwasababu ipi

Aidha zimekuwepo dhana kadhaa kuhusu viganja hivyo zinazodai kuwa vimekatwa kwa wezi ikiwa kama adhabu huku wengine wakidai kuwa zimekatwa kutoka kwa miili iliyotolewa viungo kwaajili ya biashara ya figo

Aidha katika eneo la jirani na sehemu vilipobainika viganja hivyo pia vimekutwa vifaa kadhaa vya Hospitali

Rais Magufuli Ayaonya Maandamano ya Mange Kimambi "Ngoja Waandamane Wataniona"

0
0
Rais Magufuli Ayaonya Maandamano ya Mange Kimambi "Ngoja Waandamane Wataniona"
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dr. John Pombe Magufuli amefunguka na kuzungumzia suala la maandamano na kusema atashughulika na watu ambao wataandamana ili wakawasilimulie wale watu ambao wamewatuma.


Rais Magufuli amesema hayo leo Machi 9, 2018  wakati akizindua tawi la benki ya CRDB Chato na kusema kuwa wapo watu ambao wanataka kuona amani ya nchi hii inavurugika jambo ambalo yeye hawezi kukubali kwa kuwa alihapa kulinda Katiba ya nchi.

"Wapo watu wameshindwa kufanya siasa za kweli wangependa kila siku tuwe barabarani tunaandamana, watu wao wanahamia huku wao wanataka wabaki wanaandamana kule nimeshasema ngoja waandamane wataniona, kama kuna baba zao wanawatuma basi watakwenda kuwasilimulia vizuri, niliapa kwa Katiba kwamba nchi hii lazima iwe ya amani na tunataka tujenge uchumi wa kweli ili Watanzania watajirike na hali ya Watanzania imeanza kwenda vizuri mwanzo ni mgumu lakini nataka niwaambie watanzania tupo kwenye wakati mzuri tuvumiliane ili tufike sehemu Tanzania iwe nchi ya asali" alisema Magufuli.


Nilipoingia Jera Nilimwacha Mtoto wa Miaka Minne Nimetoka Mwanamke Wangu Kachukuliwa na Mwanaume Mwingine- Papii Kocha

0
0
Nilipoingia Jera Nilimwacha Mtoto wa Miaka Minne Nimetoka Mwanamke Wangu Kachukuliwa na Mwanaume Mwingine- Papii Kocha
Msanii Papii Kocha amehojiwa leo kupitia kipindi cha Leo tena ya Clouds FM akiwa pamoja na Baba yake Babu Seya ambapo amezungumza baadhi ya mambo kuhusu wao, wakati wakiwa Gerezani na mpaka walipotoka ikiwa ni miaka 14 tangu wawe uraiani.

Papii amesema kwamba wakati alipokuwa Gerezani alikuwa kwenye kitengo cha washonaji kofia na alijifunza kule kwa sasa anajua vizuri, lakini pia amesema kwamba aliacha mwanamke na mtoto wa miaka 4 lakini saivi katoka kamkuta ana miaka 18 na mwanamke wake aliyemuacha kakuta yupo na mtu mwingine.

“Niliacha mtoto anaitwa Aisha tulikuwa tunaishi pamoja na mama yake wakati naenda jela nilimuacha ana miaka minne, nimemkuta ana miaka 18 wakati nilipokuwa kule alikuwa anakuja japo siyo sana kwani muda mwingi alikuwa shule, mama yake alikuwa anakuja kuniona nilivyotoka mama yake naonana nae ni mzazi mwenzangu nimerudi nimemkuta na mtu wake miaka 14 siyo mchezo.”

“Hiyo hali nimeipokea kawaida maana kifungo chenyewe kilikuwa kinatisha sasa mwingine anaona labda nilikuwa nisitoke so maisha mengine lazima yaendelee hajafanya makosa kwa maamuzi yake maana maisha mengine lazima yaendelee.”

“Nakumbuka show yangu ya mwisho kubwa niliyowahi kuifanya ilikuwa ni Fiesta nyingine watu watakutana nayo kesho pale kingsolomoni.”

“Mimi na mzee wangu tunabahati sana siyo mchezo toka tupo gerezani mpaka sasa, ndugu zangu wananisaidia kwenye kujifunza kutumia mitandao ya kijamii kama Instagram ila whatsapp natumia mwenyewe mitandao mizuri lakini kama ukitumia vibaya inakuwa shida kidogo.”

“Jambo linalonishangaza toka nimetoka ni mwendo kasi sijapanda ila natamani sana kupanda mwendo kasi sijazunguka kabisa lakini ntaenda daraja la kigamboni kupiga picha, kule gerezani umeme ukikatika  hazipiti dakika mbili lazima urudi kuna jenereta”

Tunda Awapa Ushauri Wanawake " Acheni Wivu na Majungu

0
0
Tunda Awapa Ushauri Wanawake " Acheni Wivu na  Majungu
February 8,2018 ilikuwa ni siku ya wanawake duniani ambapo kila mwanamke alikuwa akisherekea siku hiyo ambapo wengine walipata jumbe nzuri kutoka kwa watu wao wa karibu na kuwatakia siku ya wanawake duniani.

Kupitia instagram account ya video vixen Tunda alitumia siku hiyo kuwasihi wanawake wote duniani kuwa na umoja na ushirikiano na kuacha  wivu ambao unatokea baina ya wanawake ili kuleta maendeleo.



“Wanawake leo inabidi tushirikiane ili tuweke mfano kwa vizazi vijavyo,Sio mawivu tu na majungu bila mwisho😏 #happywomensday

Rais Magufuri Ahaidi Kumpa Kazi Serikalini Dk. Kimei

0
0
Rais Magufuri Ahaidi Kumpa Kazi Serikalini Dk. Kimei

Rais John Magufuli amesema licha ya kuwa Mkurugenzi Mtendaji wa CRDB, Dk Charles Kimei anakaribia kustaafu ameahidi kumpatia nafasi katika Serikali ya Awamu ya Tano.

Rais Magufuli ametoa kauli hiyo leo Ijumaa Machi 9, 2018 wakati akizindua tawi la benki hiyo wilayani Chato mkoani Geita.

“Kimei wewe ustaafu tu lakini nasema nafasi bado zipo. Muda wako unamalizika CRDB lakini Serikalini bado unaweza kufanya kazi ndani ya Serikali bado upo na ninakuahidi asilimia 100,” amesema Rais Magufuli.

Cristiano Ronaldo Azindua Nguo Mpya za Ndani

0
0
Cristiano Ronaldo Azindua Nguo Mpya za Ndani
Mchezaji wa Real Madrid na timu ya taifa ya Ureno, Cristiano Ronaldo, jana Machi 8 amezindua nguo zake mpya za ndani (boksa) ambazo zimepewa jina la Spring/Summer 18 CR7 (SS18 CR7).


kwa mujibu wa tofui ya mchezaji huyo, imeonyesha kuwa nguo hizo zinauzwa kuanzia kiasi cha Euro 17.95 ambazo ni takriban shilingi 49,778 za kitanzania hadi Euro 26.95 ambazo ni zaidi ya shilingi 74,766.

Babu Seya na Mwanaye Wasimulia Maisha ya Jela "Nilichaguliwa Kuwa Nyampala Mkuu wa Gereza"

0
0
Babu Seya na Mwanaye Wasimulia Maisha ya Jela "Nilichaguliwa Kuwa Nyampala Mkuu wa Gereza"
Wanamuziki maarufu wa muziki wa dansi, Nguza Viking, maarufu kwa jina la “Babu Seya” na mwanaye, Johnson Nguza au “Papii Kocha” leo Machi 9, 2018 wameeleza shughuli mbalimbali walizokuwa wakifanya gerezani.

Wakati Papii Kocha akisema alikuwa akijishughulisha na ushonaji wa mazulia, Nguza amesema alichaguliwa kuwa mnyampala, akiwa na jukumu la kusimamia wafungwa katika masuala mbalimbali.

Babu Seya, ambaye ni mtunzi wa kibao maarufu cha “Seya”, na mwanae Papii Kocha ambaye wameshirikiana katika wimbo huo, ni miongoni mwa wafungwa 8,157 waliosamehewa na Rais John Magufuli siku ya Uhuru wa Tanganyika.

Walikuwa kati ya wafungwa 61 waliokuwa na adhabu za vifungo vya maisha na kunyongwa ambazo si rahisi kupata msamaha wa kawaida wa mkuu wa nchi unaotolewa siku ya sherehe hizo.

Wakihojiwa leo Ijumaa Machi 9, 2018 katika kipindi cha Leo Tena kinachorushwa na Redio Clouds, Papii Kocha amesema wakati akiwa gerezani alikuwa akifanya shughuli za ushonaji wa mazulia pamoja na vikapu.

“Nilikuwa sijui kabla ya kwenda gerezani lakini tulijifunza na kwa sasa naweza vizuri,” amesema.

Amesema mbali na ushonaji, pamoja na baba yake walikuwa wakifanya mazoezi ya muziki mara tatu kwa wiki.

Wa upande wake Nguza amesema alivyokuwa gerezani alikuwa nyampala mkuu wa gereza baada ya kuteuliwa na uongozi wa Jeshi la Magereza.

“Ni busara tu zilinifanya nikateuliwa. Kazi ilikuwa ngumu na isitoshe unaowaongoza ni wahalifu lakini busara tu ilitumika,” amesema.

Witness Ashindwa Kuzizuia Aweka Hisia Zake Awataja Wanaume Watatu Anaovutiwa Nao

0
0
Witness Ashindwa Kuzizuia  Aweka Hisia Zake Awataja  Wanaume Watatu Anaovutiwa Nao
Msanii wa muziki wa Bongo Fleva, Witness ameamua kuweka wazi hisia zake kwa kuuelezea umma kuwa hata yeye anavutiwa na watu maarufu ila kwa utofauti na wanawake wengine.

Witness amesema kuwa mara nyingi anapenda kutembelea kwenye kurasa za mitandao ya kijamii ya watu maarufu anaowapenda zaidi duniani na kutazama maisha yao huku akiwaombea wafanikiwe kwenye kazi zao.

Akielezea upendo huo, Witness amesema yeye yupo tofauti na wanawake wengine ambao wakiwaona watu maarufu wanatamani kutoka nao kimapenzi, bali upendo wake ni kuona watu maarufu wanaomvutia wakiwa na furaha na kufanikiwa zaidi.

“Huwa ninajishangaaje mimi ni binadamu wa aina gani? Wanawake wengi wakiwapenda mastaa, haijalishi ni wa movie, muziki mpira ama kitu chochote kile, hutaka kuduu nao, But mimi nikimpenda staa au mtu sana anayefahamika huwa ninapenda kumuona, akifanikiwa zaidi pia hupenda awe na maisha mazuri na mwanamke mzuri ampendae yeye hata nikipita kwenye kurasa zao ninaona wana happy faces as a family I get to love them all and respect there women for loving the stars I love! Coz huwachukulia kama my blood brothers,“ameandika Witness kwenye ukurasa wake wa Twitter na kutaja orodha ya wanaume anaowapenda zaidi.

“ Mtu wa Kwanza ninayempenda bure na kumfurahia ni 1.@cristiano (Cristiano Ronaldo-Ureno) 2.@bustaryhmes (Busta Rhymes-Marekani) 3. @simplyluca (Luca Neghest-Tanzania) “ameandika Witness.

Hata hivyo ni hisia tu ya kawaida ambayo kila binadamu anakuwa nayo kwani kwenye orodha hiyo ya watu aliowataja, wote wana wenza wao na wanaishi na familia zao.

Victor Wanyama Ashinda Tuzo ya Goli Bora la Mwezi Ligi Kuu ya Uingereza

0
0
Victor Wanyama Ashinda Tuzo ya Goli Bora la Mwezi Ligi Kuu ya Uingereza
Mchezaji wa timu ya taifa ya Kenya na klabu ya Tottenham Hotspurs, Victor Wanyama, amefanikiwa kushinda tuzo ya goli bora la mwezi February katika ligi kuu ya Uingereza.



Wanyama ameshinda tuzo hiyo kupitia goli lake alilowafunga Liverpool katika sare waliyotoka ya kufungana mabao 2-2.

Wachezaji wengine ambao walikuwa wanawania tuzo hiyo ni Danilo na Sergio Aguero (wote kutoka Manchester City) , Mario Lemina (Southampton), Jose Izquierdo (Brighton), Mohamed Salah (Liverpool) na Adam Smith (Bournemouth).



Wakati huo huo kocha Chris Hughton wa Brighton, amefanikiwa kushinda tuzo ya kocha bora ya mwezi huo.

Chris ameisaidia Brighton kushinda alama saba kati ya michezo mitatu ambayo timu yake imecheza katika mwezi wa pili na kuifanya timu hiyo kushika nafasi ya 10 katika ligi kuu mpaka sasa.

Download Application ya Udaku Special kwenye Simu yako Kama Bado Hujadownload

0
0
Download Application ya Udaku Special kwenye Simu yako Kama Bado Hujadownload


DOWNLOAD HAPA
 


UPDATE HAPA

 

VIDEO "Wote Waliowahi Kutekwa na Kupatikana Hawajawahi Sema Chochote na Serikali Imekaa Kimya' Ole Sosopi

0
0
Mwenyekiti wa baraza la Vijana Chadema (BAVICHA) Ole Sosopi amezungumza na waandishi habari amezungumza kuhusu masuala mbalimbali ikiwemo suala la utekwaji kwa watu mbalimbali pamoja na miili kukutwa katika fukwe ya Coco Beach.

“Nitaje matukio machahe ambayo mnayafahamu hata nyie, alitekwa Roma na wenzake mpaka leo Serikali haijatoa taarifa yoyote, kwa bahati mbaya kila anayetekwa hajawahi kusema nini kilimtokea alipokuwa, Serikali imekaa kimya,” -Ole Sosopi

VIDEO:

Lulu Diva Afunguka Tuhuma za Kumtelekeza Mtoto Wake Kijijini

0
0

Msanii wa Bongofleva Lulu Diva ameendelea kuingia kwenye Headlines na hii ni baada ya kusambaa kwa story kwenye mitandao ya kijamii ya kwamba ana mtoto ambaye amemuacha kijijini kwa muda mrefu na kutokana na kumuacha muda mrefu mtoto huyo hamuiti mama ila anamuita Dada.


Bonyeza PLAY hapa chini kumtazama LULU DIVA akielezea..


Wanaume Wapeni Dose ya Nguvu Wanawake Zenu Wafike Kileleni

0
0
Nasikitisha na kushangaza,unakutana na Msichana wa miaka 28-30 anakwambia tangu aanze Mapenzi akiwa na Miaka 19 hakuna Mwanaume yoyote amewahi kumfikisha kileleni...

Imagine,anafanya Mapenzi miaka karibu 10 lakini anatumika yeye tu...Amekuwa Sugu sasa na kilele pekee anachokijua ni cha Mlima Kilimanjaro, amekata tamaa kama kuna kitu kama hicho duniani..

Ukikutana na mwanamke wa namna hii ili umridhishe inapaswa kwanza uende Gym, ule Siagi na jibini, dozi ya karanga na supu ya pweza wiki mbili umkeshee kisawasawa..

Lakini unapaswa pia kumfanyia Counselling ili aamini tena kwamba kilele sio Kibo na Mawenzi tu...inataka Moyo...

WANAUME:Msiwafanyie hivyo Wasichana, wapeni dozi inayostahili, ukipewa chezo kamua haswa, sio unakurupuka tu hueleweki unachofanya ni nini Robo saa unakoroma..Huo sio uanaume..Uanaume kazi..Mnatupa shida tunakuja kuoa Wanawake wamekomaa, hata utumie Mwiko kilele hakionekani hata kwa darubini...

Ukipewa Kazi itendee haki kazi...Kama hujui kukuna nazi waachie wakwezi...Girls wanapata shida sana, halafu we mtaani unajitamba kumbe huna lolote.



Watanzania Nani Katuroga?

0
0
Na Priva Abiud

Kwenye mechi ya Yanga wengi waliamini tumeenda kuhani msiba ila mechi ya Simba wengine wakaamini ndio siku ya mazishi yenyewe. Sitaki kuongelea sana ubora wa mechi yenyewe ila namna tulivyojiandaa. Kimsingi kulikuwa na idadi ndogo sana ya mashabiki uwanjani hasa hasa mechi ya Yanga. Hata Robo ya uwanja haikufika.

Wakati wa mahojiano nilipata bahati ya kuongea na kocha wa Township Rollers pia nilipata bahati ya kipekee kumhoji kocha mkuu wa Al Masry. Wote nilijaribu kujua mapokezi ya watanzania wameyaonaje.

Lengo langu ni kuwachokonoa kuwa wamejisikiaje tokea wanafika uwanja wa ndege mpaka uwanjani. Kocha wa Rollers alisema (All Tanzanians are beautiful, am truly satisfied) (amewapongeza watanzania na ameridhika). Kocha wa Al Masry akanijibu akaniambia (your amazing, we shall respect you) (watanzania mmetisha, na tutawaheshimu). Kocha wa Al Masry tena alinigeukia kabisa, nina imani alitabiri kuhusu swali langu na alifahamu vyema nimeliuliza kwa makusudi. Alifahamu wazi kuwa alichokutana nacho ni cha ajabu, mwarabu kushangiliwa na mtu mweusi tena kwenye ardhi ya watu weusi.

Amegundua ‘uzwazwa’ wetu hapa nchini. Amefahamu hatuna mshikamano hata kidogo. Waarabu na sisi ni ngozi tofauti kabisa. Amegundua kuwa kisaikolojia hawa hakuna kitu. Siwalaumu Simba wala siwalaumu Yanga ila nawalauamu watanzania. Haiwezekani kila mwaka timu ya taifa haifanyi vizuri halafu makelele tunayatupia TFF na kwa wachezaji.

Moja ya mambo ambayo Gomaa, Koffi na Ahmed waliyofurahishwa nayo sio matokeo ya magoli mawili ya ugenini, ni kwa namna tulivyowapokea na kuwashangilia utadhani sisi ni koloni la Hussein Mubarak. Mbaya zaidi kuna kijana mmoja aliomba jezi ya Ahmed jamaa akamwambiaa noooo (halafu na maneno ya kiarabu, mimi nahisi yale yalikuwa matusi) unadhani Simba wakienda Misri watatuchukuliaje? Je na nyie Yanga mkienda Misri Zamalek watawashangilia? Simba je? Mnadhani mkienda Botswana BDF watawapa shavu? Huko timu zenu zinakoenda nani atazishangilia? Kwa nini usibaki nyumbani kama timu yako haichezi?

Leo hii Simba atafungwa na waarabu, kesho Yanga mkienda si watajua ni wale wale wenye chuki za wenyewe kwa wenyewe. Wakija hapa wanajua wazi tuna mashabiki. Sio kwamba hawazijui Simba na Yanga wanazifahamu vyema na wanafahamu uendawazimu wetu ni utani wa jadi. Labda nikwambie kitu. Wakati mchezo haujaanza nilifika uwanjani saa 9. Upande wa kulia mwa uwanja palikiwepo mashabiki kama 50 hivi wa Yanga. Mwandishi mmoja wa CN Sport ya Misri akaenda makusudi kabisa kwenye lile jukwaa kuwapiga picha mashabiki wa Yanga waliokuwa wanamshangilia. Mashabiki wa Yanga wakafurahi na kuongeza spidi kweli… hivi kule CN Sport wakiwaoan hao waarabu si wanatuona kama watumwa wao? Hivi ni picha gani tumejenga kwa wabotswana na wa Misri?

Shida ipo wapi? Ni mpira gani huu? Soka letu litakuwa endapo tu pale timu mbalimbali zikija hapa zikala kichapo cha haja. Kinachokuza ligi zetu za ndani ni ushirikiano tu. Leo kocha wa Township Rollers anasema nilikuwa naijua hii mechi kabla ya hapo. Wala sikujishughulisha sana. Ivan Ntege anasema walijua timu za Tanzania ni dhaifu mno.
Kwa mfano tu, tukienda nje ya nchi yetu viwanja vyao vinakaribia kujaa. Vilabu husika vifanye yafuatayo. Kwa mfano kama tiketi ni 5000 nunueni tiketi 20,000 uzeni kwa bei ya shilingi 3000 jazeni mashabiki uwanjani kwenye mechi muhimu kama hizi. Mpira ni mashabiki. Umeona namna Simba walivyoshangilia kwa ari kubwa uwanjan? Licha ya kwamba walikuwa nusu, hivyo hivyo Yanga nao wanapaswa kufanya. Jazeni uwanja. Shangilieni kila dakika. Morali ndio kila kitu. Simba ikitoka haimfaidishi chochote Yanga, wala Yanga wakitoka haisaidii chochote.

Lakini moja wao anapofanikiwa ndiko wachezaji wetu wanasonga mbali wanaonekana na wanaenda vilabu vikubwa. Hakuna mchezaji anayefanikiwa kwa kushiriki kombe la Mapinduzi chuki zetu zibaki ndani taifa kwanza. Njia pekee michuano ya kimataifa.

Tunaendaje kule kama tutapigana vikumbo? Kazi ya matawi ya hizi timu ni nini? Kujazana ujinga? Mzee ana miaka 50 unaenda washabikia wageni? Ushauri wangu tu, Simba na Yanga jazeni mashabiki uwanjani. Wekeni tiketi kwa bei nafuu kila mtu aende taifa. Nchi za wenzetu wakati fulani watu wanajaa uwanjani bureee ili tu wasapoti timu zao. Leo jitu zima linatoa 10,000 kwenda kushabikia timu za nje? Ni undondocha huo.
Viewing all 104417 articles
Browse latest View live




Latest Images