Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104768 articles
Browse latest View live

Tangaza Biashara Yako Hapa Uweze Kupata Wateja wa Haraka

$
0
0
Mtu wangu wa nguvu unaweza Tangaza Biashara yako hapa nasi uweze kuwafikia watu wengi zaidi kwa mara moja kupitia blog ya Udaku Special..

Piga simu 0714604974

Tangaza Biashara Yako Hapa Uweze Kupata Wateja wa Haraka

$
0
0
Mtu wangu wa nguvu unaweza Tangaza Biashara yako hapa nasi uweze kuwafikia watu wengi zaidi kwa mara moja kupitia blog ya Udaku Special..

Piga simu 0714604974

Kinacho Waweka Njia Panda Wadada Katika Umri wa Kuolewa na Kujikuta Umri Umeenda

$
0
0
Zama hizi hitajio la ndoa limekuwa ni kubwa zaidi, lakini jambo la kusikitisha ni kuwa ndoa zimekuwa ngumu sana. Na mabinti wamebaki njia panda (Dillema). Miongoni mwa mambo yanayowafanya wawe njia panda ni hali.

#Wanataka wenye mali,
wenye mali wengi hawana dini wala ucha mungu. Na wenye ucha mungu wanatakiwa na wengi. Jambo ambalo limefanya wawe wanachagua zaidi. Njia panda.

#Wanataka Mahandsome,
Mahandsome wengi ni Mario wanatumia uhandsome wao, kuwatumia mabinti tu . Na mwisho kuangukia Kwa wanawake wenye pesa zao. Na wao kuwa mamario. Na wenye dini ni kinyang'anyiro kwa mabinti. Njia panda.

#Wanataka wanaume wa pekee yao, wapeke yao ni maskini.
Na mabinti hao hawako tayari kwenda kuishi maisha ya kimaskini kupambana pamoja na mume ili wafanikiwe pamoja. Njia panda.

#Wanataka wenye elimu za vyuo vikuu kama wao, wenye elimu hizo hawawataki kwasababu ya changamoto wanazoziona vyuoni, wanataka wenye elimu ndogo zaidi. Njia panda.

#Wanataka waliojiimarisha kiuchumi hata kama ni uchumi wa wastani na awe na dini.
Hao wana namna hiyo wapo lakini Kwa kumuogopa Allah wameoa mapema na wana wake zao. Kwa hivyo ndoa hapo hi matala, mabinti hawako tayari na ndoa za wake wengi. Njia panda.

#Wanataka vijana wenye Elimu, vijana hao wapo lakini ndio kwanza wanaanza maisha, wana chumba cha kupanga. Wao wanataka wenye uchumi mzuri. Wenye uchumi mkubwa umri umekwenda. Njia panda.

#Wanataka waume wenye misimamo yao ya kimadhehebu, wanaume wa namna hiyo imma ni wachache au sio chaguo lao. Njia panda.

#Kuhadaiwa na mapenzi yasio rasmi, miaka kadhaa, wanakuja waposaji hawakubali. Mara wanatelekezwa. Njia panda.

#Wanaifanya ndoa ni second selection, maisha kwanza ndoa baada, wanapofeli katika malengo ya kimaisha ndoa wanaitafuta ndoa. Muda umeenda mvuto umepotea, kaingia kasoro tayari kwanini achelewe. Njia panda.

#kuhadaiwa na uzuri wao, na kukataa ndoa. kwa madai wao ni warembo kwa hivyo wataolewa tu. Na wakasahau wa simu sio housing bali ni software. Matokea umri unakwenda na wanabaki kuwa ni sehemu ya starehe tu kwa wanaume na sio wake wakuwekwa ndani. Njia panda.

Mara paaa miaka 30 hiyo, mwisho wa siku anaekuja na aje. Na kuanza wana nuksi, hali ya kuwa nuksi wamejitia wenyewe. Na matokeo yake mbio kwa waganga matapeli haziishi. Dillema/njia panda hiyo imwaacha mabinti wengi wanaugulia maumivu ya kutendwa katika magenta. Na mwisho ni maamuzi ya kutafuta japo mtoto wa nje wasijekufa bila ya kuacha kizazi.

Wasichokijua mabinti wengi ni kuwa sifa za mume kuoa ni mbili tu hakuna ya tatu. Na asipoozeshwa mwenye sifa hizo basi lazima kuwe na maharibiko
HII NI FAIDA MABINTI WOTE

Nafasi za Ajira Zilizotangazwa Leo Jumapili

Haya ndiyo mambo sita aliyoyataja Mchungaji KKKT ambayo yanaitafuna nchi

$
0
0
Mkuu wa pili wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) Jimbo la Kilimanjaro Kati, Mchungaji, Fred Njama amesema kuna mambo sita nchini ambayo hayako sawa.

Alitaja mambo hayo kuwa ni pamoja na hali ya uchumi, ajira kwa vijana, ughali wa matibabu na tangazo la elimu bure.

Mchungaji Njama ambaye pia ni mchungaji kiongozi wa Usharika wa Karanga mjini Moshi, alitaja mambo mengine kuwa ni hali ya kisiasa nchini na kundi kubwa la wastaafu kutolipwa mafao yao. Alitoa kauli hiyo jana wakati akiwasilisha taarifa yake katika mkutano mkuu wa 21 wa usharika huo wa Karanga, uliohudhuriwa pia na Askofu mstaafu wa Dayosisi ya Kaskazini, Dk Martin Shao.

Mkutano huo mbali na kuhudhuriwa na mkuu wa Jimbo la Kilimanjaro Kati, Mchungaji Kennedy Kisanga na wachungaji wa sharika jirani, ulihudhuriwa pia na wawakilishi kutoka jumuiya 32.

Kauli ya Mchungaji Njama imekuja siku chache baada ya Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania, (TEC) kuitaka Serikali ifufue mchakato wa uundwaji wa Katiba Mpya uliokwama.

Naibu Katibu Mkuu wa TEC, Padri Daniel Dulle alisema majadiliano yanahitajika ili kudumisha amani, heshima na kujenga taifa linaloheshimiana.

Hali ya uchumi
Akizungumzia hali ya uchumi nchini, Mchungaji Njama alisema awamu ya tano ilipoanza, watu walikuwa na mategemeo makubwa kwamba uchumi utaimarika lakini mambo yamekuwa tofauti.

“Umaskini unaendelea kuongezeka kwa nguvu. Tumeshuhudia biashara nyingi zikifungwa, wakulima wamekata tamaa, gharama za uzalishaji zimekuwa kubwa sana,” alisema Mchungaji Njama na kuongeza:

“Serikali haitoi ruzuku ila wakati wa kuuza mazao yao, wakulima hawajui wauze wapi na kwa bei gani. Wafugaji wanazalisha kwa gharama kubwa. Vyakula vya mifugo na dawa ni ghali.”

Hali ya kisiasa
Katika hotuba yake hiyo, Mchungaji Njama alisema kuna dalili za kuminywa kwa uhuru wa vyombo vya habari na siasa.

“Inavyoelekea uhuru umeanza kuminywa. Ulianza kwenye siasa, ukaja kwenye vyombo vya habari... Kwa mfano takwimu za uchumi au chochote hata kama kina ukweli lakini utawala hautaki kusikia ukizungumzia hadharani au kwenye daladala ni kosa la jinai. Matukio ya miili kuokotwa yamezidi,matumizi ya risasi yameanza kuzoeleka kama kitu cha kawaida. Watu kupigwa risasi kwa walio wanasiasa na wasio wanasiasa yanafanya watu waishi kwa hofu.”

Baadhi ya matukio ya watu kupigwa risasi, ni pamoja na lile la Septemba mwaka jana, la Mbunge wa Singida Mashariki (Chadema), Tundu Lissu aliyeshambuliwa akiwa nje ya nyumba yake mjini Dodoma.

Kadhalika, tukio la hivi karibuni la mwanafunzi wa Chuo cha Taifa cha Usafirishaji (NIT), Akwilina Akwilini wakati wa maandamano.

“Hali hii ikiachwa, nchi itaingia kwenye umwagaji damu mkubwa,” alitahadharisha na kuungwa mkono na baadhi ya waumini.

Ukosefu ajira kwa vijana
Akizungumzia hali ya ajira nchini, Mchungaji Njama alisema miaka ya nyuma vijana walijua kwamba wakisoma watapata ajira, lakini leo imekuwa ni kinyume chake na karibu kila nyumba ina kilio.

“Karibu kila nyumba ina kijana aliyemaliza chuo kikuu au vyuo vya kati. Kundi la wasio na kazi limeongezeka maradufu na hii si dalili njema,” alisema.

Gharama za matibabu
Kwa upande wa matibabu, Mchungaji Njama alidai matibabu yamekuwa ghali akitolea mfano wa upasuaji wa kawaida kufikia Sh500,000 mbali na vipimo vya CT-Scan na MRI ambavyo ghamara yake pia kubwa.

“Watu wanashindwa kumudu gharama za matibabu. Bima za wasio na ajira za Serikali zinabagua matibabu na dawa. Wazee ambao wanapaswa kutibiwa bure imekuwa ni nadharia,” alidai.

Elimu bure
Mchungaji Njama alidai kuwa tangazo la elimu bure limeleta kushuka kwa elimu kuliko wakati wowote na kutolea mfano kuwa kati ya shule 100 zinazofanya vizuri, za Serikali ni chache.

“Ninashauri wajumbe wa mkutano mkuu tuwaelimishe wazazi wasicheze na maneno ya wanasiasa. Kuna msemo unaosema gharama ya ujinga ni kubwa kuliko gharama ya elimu,” alisema.

Katika hatua nyingine, Askofu mstaafu Dk Shao, alilitaka kanisa hilo lisikae kimya na lichukue hatua ya kuzuia mafundisho potofu ndani ya kanisa, yanayotolewa na baadhi ya wachungaji.

Dk Shao alisema upungufu wa mafundisho ya kidini ni mkubwa na kuwataka wachungaji wa sharika za kanisa hilo, kutoruhusu kualika wahubiri wanaotoa mafundisho potofu kwa waumini.

Dawa Bora za Nguvu za Kiume na Kukosa Hamu ya Tendo la Ndoa

$
0
0

DAWA BORA ZA NGUVU ZA KIUME NA KUKOSA HAMU YA TENDO LA NDOA
Baada ya utafiti wa muda mrefu juu ya matatinzo ya upungufu wa nguvu za kiume na ukosaji wa hamu ya tendo la ndoa ama kushindwa kurundia tendo kwa haraka Sasa inakuletea suluhisho juu ya matatizo haya kwa kutumia dawa za FULL POWER

Full Power dawa asili yenye vidonge inayotibu tatizo la upungufu au ukosefu wa nguvu za kiume dawa hii inamchanganyiko wa kutosha kuzalisha vichocheo vingi vya hernone za gestro gen zikiwemo vitamin b6 na b1 vitamin e pamoja na madini aina ya zinc

Itakufanya kuwa na nguvu na mzunguko mzuri wa damu na kuongeza hamu na uwezo wakufanya tendo la ndoa zaidi hatua nne au zaidi na kuchelewa kufika kileleni zaidi ya dakika 20/30 ZAT 50

Inarundisha maumbile ya uume yaani kurefusha na kunenepesha nchi 3/7 na upana cm 3/4 standard.kiafya haijalishi umri wako hata kwa wazee ukitumia maumbile yatabaki kuwa hivyo siku zote pia anatibu matatizo mengine kama presha kisukari ngiri chango la tumbo kujaa gesi kutopata choo vizuri minguu kuwaka moto matatizo ya uzazi bawasili na magonjwa ya zinaa kama kisonono na kaswende

Tunapatikana Dar es Salaam  na mikoan wasiliana na DR Oshinda no 0755505099 au 0714126118  Karibuni kwa hunduma bora

Mamlaka ya hali ya hewa yatoa tahadhari kwa Wananchi

$
0
0
Mamlaka ya hali ya hewa iliyopo chini ya Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano nchini Tanzania imewatahadharisha wananchi kuwepo kwa hali mbaya ya hewa katika maeneo ya mikoa ya Dar es Salaam, Pwani, Lindi na Mtwara ndani ya saa 24 kuanzia leo.

Hayo yamebainishwa na taarifa zilizotolewa na mamlaka hiyo na kudai kutakuwepo vipindi vifupi vya mvua kubwa ambazo zinatarajiwa kunyesha katika baadhi ya maeneo ya mikoa ya Singida, Dodoma, Morogoro, Ruvuma, Njombe, Iringa, Mbeya, Songwe, Kilimanjaro, Manyara na Arusha

Mbali na hilo, TMA imesema kutakuwepo upepo mkali unaofikia kilomita 30 kwa saa kutoka Kaskazini- Mashariki kwa Pwani ya Kaskazini na kutokaa Kaskazini-Magharibi kwa Pwani ya Kusini huku hali ya bahari inatarajiwa kuwa na mawimbi makubwa kiasi.

Aslay afunguka kumpiga marufuku mama mtoto wake kuuza Sura

$
0
0
Msanii wa muziki wa kizazi kipya ambaye kwa sasa ni gumzo kwenye mitaa ya bongo Aslay, amefunguka kuhusu kumpiga marufuku mama mtoto wake, kufanya kazi aliyokuwa akiifanya.

Akizungumza kwenye FNL ya East Africa Television, Aslay amesema mama mtoto wake ambaye anafahamika kwa jina la Tessy, hawezi akaendelea kufanya kazi ya aliyokuwa akifanya ya 'video vixen', kwani amempiga marufu na kila alichokuwa akitafuta anampatia.

“Hawezi kuendelea mimi ndio nimesema hawezi kuendelea, sidhani kama sasa hivi anapenda tena kufanya, kwa sababu mara nyingi yupo na mtoto, na yeye  mwenyewe kuna mambo yake anafanya kitu kinachomuingizia hela, kwa sababu kule alikuwa anatafuta hela sasa hivi hela anapata”, amesema Aslay.

Msanii huyo pia ameweka wazi kuhusu tetesi za kuachana na mama mtoto wake huyo, na kusema kwamba hajawahi kuachana wala kutengana naye.

Je, Papii Kocha na Babu Seya watajihusisha na siasa baada ya kutoka jela? soma majibu yao

$
0
0
Wasanii wa muziki wa Dansi nchini Tanzania, Papii Kocha na Babu Seya wameamua kuweka wazi kuhusu tuhuma za baadhi ya mashabiki wao kwamba tangu watoke jela kwa msamaha wa Rais wamekuwa watu wanaojihusisha na masuala ya kisiasa.

Papii Kocha na Baba yake wamesema kuwa kwa sasa hawapo kabisa na masuala ya kisiasa kwani hao ni wanamuziki na hawajui hata jinsi ya kusimama jukwaani na kuhubiri siasa. Tazama video yao hapa chini wakifunguka.

VIDEO:

Video: Wema afunguka kuolewa na Diamond, pia ajibu kuhamishia show yake Wasafi TV

$
0
0
Msanii wa Filamu Bongo, Wema amejibu tetesi kuwa yupo mbioni kufunga ndoa na msanii wa muziki Diamond, pia amezungumzia kuhusu kuhamishia kipindi chake ‘My Shoes’ Wasafi TV.

VIDEO:

Said Kubenea Alipuka Ataka Tume Huru ya Uchaguzi Bungeni

$
0
0
Mbunge wa Ubungo, Said Kubenea amesema amepeleka bungeni barua ya kusudio la kuwasilisha hoja binafsi ya kuwa na chombo huru cha kusimamia uchaguzi.

Akizungumza na waandishi wa habari leo Jumapili Machi 11,2018 Kubenea amesema Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) si chombo huru cha kusimamia uchaguzi.

Amesema barua hiyo aliiwasilisha Alhamisi Machi 8,2018 katika ofisi ya Katibu wa Bunge mjini Dodoma, Kubenea amesema uchaguzi kusimamiwa na Tume isiyo huru inaweza kusababisha machafuko.

"Hatuwezi kuacha hali hii iendelee, vurugu zimekuwa zikitokea kwa sababu ya kuwa na Tume ya aina hii, tunataka chombo huru," amesema.

Amesema tangu nchi iingie katika mfumo wa vyama vingi mwaka 1992 uchaguzi umekuwa ukifanyika kwa kusimamiwa na Tume isiyo huru.

Mke Wangu Ana Mimba, Katokea Kunichukia na Kampenda Mume wa Mtu Jirani na Chumba Tulichopanga

$
0
0
Husika na kichwa cha habari hapo juu

Mimi kijana mwenzenu nasikitika sana na hii tabia ya mke wangu, kwakweli ana nichanganya sana jamani

Ana mimba ya miezi sita lakini katokea kunichukia sana jamani hataki hata kunisogelea wala kula chakula mezan pamoja na mimi

Lakini katokea kumpenda mme wa mtu ambaye ni jirani wa chumba hapa tulipopanga

Mke wangu ni mama wa nyumban na hana kaz lakin mimi huondoka asubuh sana kwenda job lakin hurud usiku wa saa tatu

Nikifika nyumban get had nije nifunguliwe na mtu mwingine mke wangu yeye kalala tu na hata kama nikifika mlangon huwa hafungui upes yaan nitagonga mlango had bas na atakuja kufungua mda atakao taka yeye

Mfano jana nimefika nyumban saa tatu lakin alikuja kunifungulia saa tano usiku

Na kama nikiingia ndani anaanza kutema tema mate eti kuna kitu ndani kinanuka shombo ya samaki hasa mimi nikiingia

Yaani nakuwa naambiwa mda mwingine yule jamaa huwa anaingia hadi ndani mwangu kupiga story na mke wangu

Ina niuma sana mimi jamani

Nateseka sana jaman

Naomben ushauri wenu

London baby

Bosi wa Bank ya Baroda Afariki Dunia Akiaga Wafanyakazi Wenzake (VIDEO)

$
0
0

 BOSI wa Benki ya Baroda, Shri Praveen Nayar, alianguka na kufa Januari 31, mwaka huu, wakati akitoa neno la pongezi kwa wafanyakazi wenzake, ndugu zake na marafiki zake.

 Tukio hilo la kuanguka na kufariki kwake lililotokea katika chumba cha bodi ya wakurugenzi katika tawi la benki hiyo la  New Delhi, India, kutokana na shambulio la moyo, lililotokea mbele ya watu wote waliokuwa hapo katika chumba cha bodi ya wakurugenzi wa benki hiyo.

 Mkuu huyo alikuwa na tatizo hilo kwa muda mrefu ambalo siku anafariki, ilimchukua muda mfupi sana tangu alivyoanza kuwahutubia watu hao na kuaga dunia.


Jeshi la Polisi lawapiga marufuku ACT Wazalendo kufanya mikutano ya ndani

$
0
0
Jeshi la Polisi wilayani Mvomero Mkoani Morogoro limekiamuru chama cha ACT Wazalendo wilayani humo kusitisha kufanya mikutano ya ndani

Katika barua iliyosainiwa na SSP Julius S. Lukindo ambaye ni Mkuu wa Polisi wa wilaya hiyo imeelezwa kuwa Jeshi la Polisi kwasasa linashughulikia kesi nyingi za kisiasa hivyo ACT Wazalendo wanashauriwa kufanya mikutano hiyo siku za baadae

Maandamano Yamwibua John Cheyo....Ataka Mabaraza ya Vyama Yatumika Badala ya Watu Kuandamana

$
0
0

Mwenyekiti wa UDP, John Cheyo amesema mabaraza ya vyama vya siasa yakitumika kikamilifu yanaweza kuondoa malalamiko ya wananchi na viongozi wa upinzani.

Amesema hayo leo Machi 11,2018 akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam kuhusu vuguvugu la maandamano yaliyopangwa kufanyika Aprili 26,2018 yanayoratibiwa kupitia mitandao ya kijamii.

Cheyo amesema maandamano hayo ni uchochezi na uvunjifu wa amani na kwamba, mambo yanayolalamikiwa yangeweza kutatuliwa kupitia mabaraza hayo.

"Tusitake kufika hatua ya kuandamana barabarani ili kudai haki, Katiba mpya, Tume huru ya uchaguzi. Tukifikia huko amani iliyopo Tanzania tutashindwa kuipata tena na wananchi watakosa nchi nyingine yenye amani ya kukimbilia," amesema.

Cheyo amesema kama tatizo ni fedha kwa ajili ya mabaraza hayo kukutana, Rais John Magufuli anapaswa kutoa fedha kuyawezesha kufanya vikao.

"Siungi mkono hoja za kudai kuwepo mikutano ya hadhara hata kama ni kwa ajili ya kuongeza wanachama kama wanavyodai wengine, naamini kwa sasa mitando ya kijamii ina nguvu kuliko kitu chochote nchini," amesema Cheyo.

Amesema kabla ya kudai haki ya kuandamana, zipo nyingine wananchi wapaswa kuzipa kipaumbele zikiwemo haki ya kuishi, kupata maji safi na salama, elimu na afya.

"Hatuwezi kufika mahali tuseme nchi hii imepotea na hakuna demokrasia kisa tumekosa haki ya kuandamana, haki ya kufanya mikutano ya hadhara. Kila mtu alishuhudia mikutano ya kampeni za uchaguzi wa ubunge wa marudio katika majimbo ya Kinondoni na Siha ilivyogeuka sehemu ya kutukanana," amesema Cheyo.

"Kama kitu mnachokidai kiliweza kusababisha watu kugombana na askari hadi mauaji yakatokea hicho kitu hakitusaidii kama nchi," amesema.

Cheyo amesema yanayodaiwa kwa nguvu hayana faida na manufaa ya kila siku kwa sababu watu wanahitaji kupata wakati wa kulima na kuvuna.

"Hiyo mikutano iliyoshupaliwa sasa na kuhitajika kwa nguvu zote si kweli kwamba kila siku watakuwa barabarani kuhutubia wananchi, fedha tutatafuta saa ngapi, tutalima saa ngapi, hivyo ni vyema tutambue kila kitu kinachofanyika kupitia mambo ya siasa kisiwe kisingizio cha kusema nchi haina amani, haina uhuru," amesema Cheyo.

Amesema viongozi wa dini wanapaswa kuwa kiunganishi cha wananchi na viongozi wa vyama vya siasa na si kufanya kinyume cha hilo.

Mbunge wa CCM ajitosa jimbo la Lissu, aanza kutoa misaada

$
0
0
Mbunge wa Singida Magharibi, Elibariki Kingu (CCM) ametoa msaada wa vitanda vya kujifungulia katika jimbo linaloongozwa na Tundu Lissu (CHADEMA).

Amesema kuwa ametoa msaada huo mara baada ya kufuatwa na kuombwa msaada na siyo kisiasa kama inavyozungumzwa na watu wengine.

Kingu ameeleza kuwa katika jimbo linaloongozwa na Lissu wapo madiwani wanaotoka katika chama chake (CCM) na ndiyo waliomfuata kuomba msaada kwake na wala hakuwa na nia ya kufanya kazi ndani ya jimbo hilo bali ni moyo tu.

Amesema kuwa asingeweza kwenda kutoa misaada katika majimbo ya wana CCM kwa kuwa hawakumuomba na kama ikitokea siku wakahitaji msaada wake yupo tayari kuwasaidia kwa kadri ya uwezo wake.

“Mimi sioni ubaya. Watu wameomba msaada wa vitanda kwamba kina mama wanateseka. Marekani leo wanaisaidia Tanzania haina maana kwamba Marekani mambo yako supa. Lakini Marekani inatoa misaada ya mabilioni. Mimi kwenda kutoa msaada jimboni kwa Lissu haina maana kwangu nimemaliza changamoto za kwangu,” amesema Kingu

Hata hivyo, Katika hatua nyingine Kingu amesema anamuombe Lissu ambaye amemtaja kama Kaka yake apone ili aweze kurejea kwenye majukumu yake.

Mwigulu aonya atakayeandamana ‘hata kuzunguka kitanda’

$
0
0

Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Mwigulu Nchemba amesema amemuagiza na kumuelekeza Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini (IGP) Simon Sirro kuwakamata watu wote ambao wamepanga njama za kutaka kuwauwa watanzania katika maandamano ambayo wameyapanga kuyafanya

Mwigulu ametoa hiyo wakati alipokuwa akitoa salamu zake kwa Rais Dkt. Magufuli aliyopo Mkoani Singida katika ziara yake ya kikazi ambapo leo hii (Machi 11, 2018) amezindua kiwanda cha Alizeti Mkoani humo na kusema kinachotafutwa katika maandamano hayo ni namna ya watu wanatawanywa ili kusudi waje kulalamika kuwa serikali ndio imeuwa watu wake.

"Njama hiyo tumeiona na mimi nimemuelekeza IGP Sirro kwamba hata kupanga njama ya kuua ni kosa, wachukue hatua kwa wale watu wanaopanga mipango ya aina hiyo na kuchafua taswira ya nchi yetu ama kwa mipango yao au ya wale wanaowatuma. 

"Watu wanataka mikusanyiko ili wafyatue na kuuwa watu  ili kuchafua taswira ya nchi yetu na tunayo mifano wa maeneo waliwahi kufanya jambo la aina hiyo na hatua zitachukuliwa", amesema Mwigulu.

Pamoja na hayo, Mwigulu ameendelea kwa kusema "Mhe. Rais ndio maana unaona vinyago vinyago vingi hivi kama hivi juzi alitokea kijana mdogo amesema ametekwa, eti ametekwa na akapata muda wa kutafuta pafyumu na nguo za kubadilishia kule atakapokuwa ametekwa.

"Unatowa wapi muda wa kujiandaa ?, watu wanatafuta njia za kuchafua taswira ya nchi yetu, na jambo hili Mhe. Rais kama ambavyo ulishatoa maelekezo, si jambo ambalo tutacheza nalo wala mjadala, hakuna sababu ya maandamano wala hakuna sehemu ya kuandamania na hakuna ruhusa ya kuandamana".

Aidha, Waziri Mwigulu amesema endapo ikatokea hata watu wakaandamana ndani ya nyumba zao bado sheria itachukua mkondo wake dhidi ya watu hao.

"Ikitokea hata watu wakaandamana ndani ya nyumba wakazunguka kitanda na akatokea mtu akaumia, yule aliyeitisha waandamane pale atawajibika kwasababu watu wanafanya mzaha na maisha na dira ya nchi yetu ambapo Rais umejitoa muhanga kwa ajili ya kutengeneza urithi wa watoto wa Tanzania", amesisitiza Mwigulu.

Kwa upande mwingine, Waziri Mwigulu amesema yeyote atakayethubutu kutaka kuharibu taifa la Tanzania kwa kufanya vitendo vya uovu hawatoweza kumuacha salama.

Naunga Mkono Maandamano, Yakiitishwa Nitashiriki – Saed Kubenea (+video)

$
0
0
Mbunge wa jimbo la Ubungo,  Mhe. Saed Kubenea amesema yeye kama Mtanzania yupo tayari kuandamana endapo yatatokea maandamano ya kudai jambo lolote muhimu ndani ya Tanzania kwa sababu ni haki yake ya msingi na kikatiba.

Akizungumza na Waandishi wa Habari leo Machi 11, 2018 Kubenea amesema amekuwa akisikia mitandaoni kuna watu wanapanga maandamano lakini viongozi serikalini wamekuwa wakiyapinga na kudai kuwa haoni sababu ya serikali kufanya hivyo. Tazama mkutano wake na waandishi wa habari hapa chini:

VIDEO:

Flora Mbasha amjibu Emmanuel Mbasha kuhusu mtoto

$
0
0
Msanii wa nyimbo za Injili Flora Mbasha ambaye alikuwa mke wa mwanamuziki wa Injili Emmanuel Mbasha, amefunguka juu ya kitendo cha aliyekuwa mume wake kumlalamikia kumnyima mtoto kwenye mitandao ya kijamii.

Akizungumza na mwandishi wa www.eatv.tv, Flora Mbasha amesema hawezi kulizungumzia suala la hilo kwenye vyombo vya habari au kwenye mitandao, kwani yeye ndio anaujua ukweli, na iwapo mahakama ilimpa haki ya kumuona mtoto, kuandika kwenye instagram sio sahihi kwani mahakama haipo instagram.

“Siwezi kulizungumzia suala hilo kwenye vyombo vya habari, hilo suala kama aliandika kwenye instagram nami jibu ningelitolea instagram, na ukweli hamuujui sisi ndio tunaujua, na kama mahakama iliamua hivyo, na yeye kuandika instagram, kama mahakama iko instagram basi sawa acha aandike, ila siwezi kuliweka wazi”, amesema Flora Mbasha.

Wawili hao walitalikiana baada ya kesi aliyokuwa akituhumiwa Emmanuel kuisha na kukutwa hana hatia, na kisha Flora kuolewa na mwanaume mwengine.

Zitto Kabwe "Rais Anasema, IGP Anasema, Naibu wa Rais (DSM) Anasema, Waziri Anasema. Yote hii ya nini Mbona Mnapanick?"

$
0
0
Ameandika Zitto Kabwe:

"Mkuu wa Polisi anasema. Mkuu wa Majeshi anasema. Mkuu wa Wakuu wa Mikoa ( Naibu Rais 🙄 ) anasema. Waziri anasema. Rais anasema. Taharuki ( panick) yote hii ya nini? Siku chache zijazo mtasikia hapatakuwa na sherehe za Muungano, pesa zitaongezea bajeti ya kuvunja jengo la TANESCO pale Ubungo.

Taharuki ni ishara ya UDHAIFU. Someni Romania https://en.m.wikipedia.org/wiki/Romanian_Revolution na MAPINDUZI yao ya mwaka 1989." Zitto
Viewing all 104768 articles
Browse latest View live




Latest Images