Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104775 articles
Browse latest View live

Miujiza ya Sharifu Seif Mohamed..JE Umeachwa na Mme/Mke au Mpenzi, Umesongwa na Mitihani ya Maisha

$
0
0
SHARIFU SEIF MOHAMED ANAWASHUKURU WALE WOTE WANAOENDELEA KUPIGA SIMU, WENYE MATATIZO NA WALE WANAOTOA  SHUKRANI NA SHUHUDA JINSI TIBA ZAKE ZINAVYO WASAIDIA,

(Rudisha mahusiano yako ndani ya masaa 72 tu)

SHARIFU MOHAMED Ni  mtaalam na mnajimu maarufu wa nyota na kubashiri mambo yanayo watesa binadamu duniani kote na kupata ufumbuzi, Anatumia kitabu cha QUR'AN na Nyota

Je Umeachwa na UMPENDAE awe Mme/Mke na bado unampenda? Je Umekimbiwa na Mmeo/ Mkeo n anaishi na mtu mwingine? Je Umejaribu sehemu nyingi bila mafanikio? Mpigie simu SHARIFU SEIF sasa hivi ujionee Muujiza wa Papo kwa Papo, Anauwezo wa hali ya juu wa kusambaratisha mahusiano yao na kumrejesha kwako haraka sana na Kumfanya Atimize Ahadi zote Ndani ya Muda Mfupi Endapo Utafwata Atakacho Kuelekeza

 ZINDIKO LA NYUMBA NA BIASHARA, PETE ZA BAHATI, HUMALIZA KABISA TATIZO   HUZUIA CHUMA ULETE KWENYE BIASHARA, HURUDISHA MALI ZILIZOPOTEA, NA KUPONYA MAGONJWA SUGU ANAO UWEZO WA KUMRUDISHA ALIE MBALI AU ALIECHUKULIWA MSUKULE, KUPANDISHA NYOTA NA KUSHINDA BAHATI NA SIBU, KASAFISHA NYOTA NA KUKUPA MVUTO WA AJABU, KUTOA NUKSI NA VIFUNGO MBALIMBALI,  MAFANIKIO YA MAISHA NA UTAJIRI BILA MASHARI, NA MENGINE MENGI YA SIRI,

JE UMAHANGAIKA KUPATA MTOTO BILA MAFANIKIO? WASILIANA NA MTAALAMU HUYU KWANI YEYE HUFAULU PALE WOTE WALIPOSHINDWA, PIA UMALIZA KAZI ZILIZO SHINDIKANA NA WATAALAM WENGINE NDANI YA MASAA 24 TU,

(NA ANATIBU KWA NJIA YA SIMU UKIWA NCHI YOYOTE AU MKOA WOWOTE ENDAPO UTAFWATA MAELEKEZO YAKE)

Kwa ushauri na mawasiliano  zaidi Piga SIMU No:

Mobile +255 654-836970
WhatsApp 0622766715 

Inasikitisha! Mama Awaua Watoto Watatu wa Mke Mwenzie Kikatili Awacharanga Mapanga Kisha Mwenyewe Kujinyonga

$
0
0
Inasikitisha! Mama Awaua Watoto Watatu wa Mke Mwenzie Kikatili Awacharanga Mapanga Kisha Mwenyewe Kujinyonga
Mwanamke mmoja katika kijiji cha Nyahera Kaunti ya Kisumu nchini Kenya, amewaua watoto watatu wa mke mwenzie, na kisha mwenyewe kujinyonga.


Tukio hilo limetokea mwishoni mwa wiki hii ya tarehe 11, Machi, ambapo limeelezwa kwamba mwanamke huyo anayejulikana kwa jina la Jacinta Otieno, aliwaita watoto hao ambao walikuwa wanne kwenda kunywa uji nyumbani kwake, na ndipo alipoanza kuwacharanga na mapanga mpaka kuwaua na kisha mwenyewe kujinyonga, huku mtoto mmoja akinusurika baada ya kukata kwenda kunywa uji.

Jacinta alifanya tukio hilo baada ya mke mwenzie kwenda kanisani na kuwaacha watoto peke yao nyumbani ambako wanaishi jirani, huku mume wao akiishi jijini Nairobi na watoto wawili ambao amewazaa yeye.

Kwa mujibu wa majirani wawili hao wameelezwa kuwa hawakuwa na maelewano mazuri kutokana na wivu kwa mume wao, na kwamba Jacinta alishajaribu kutaka kujiua wiki moja iliyopita.

Watoto hao waliouawa walikuwa na umri wa miaka 7, 4 na 2, walikuwa wa mke mwenzie Hellen Otieno.

Kenyatta, Odinga Kimeeleweka! Waandaa Kufanya Ziara ya Kuzunguka Nchi Nzima

$
0
0
Kenyatta, Odinga Kimeeleweka! Waandaa  Kufanya Ziara ya Kuzunguka Nchi Nzima
Rais wa Kenya, Uhuru Kenyatta na  hasimu wake ambaye ni kiongozi wa umoja wa vyama vya upinzani nchini humo, Raila Odinga wamepanga kufanya ziara ya nchi nzima kuhamasisha amani, mshikamano na umoja.

Kwa mujibu wa gazeti la The Star limeripoti kuwa ziara hiyo itaanzia maeneo ambayo vyama vya upinzani nchini humo vina nguvu zaidi na kuendelea maeneo mengine.

Gazeti hilo limeripoti kuwa ziara hiyo itaanzia jimbo la Nyanza ingawaje tarehe rasmi ya ziara hiyo bado haijatangazwa.

Wakati hayo yakijiri, viongozi wa Umoja wa Vyama vya Upinzani nchini Kenya leo Jumatatu wanatarajia kuongea na waandishi wa habari kuhusu mustakabari na muelekeo wa umoja huo.

Wiki iliyopita Kiongozi wa Upinzani, Raila Odinga alikutana na Rais Uhuru Kenyatta kwenye Ikulu ya nchi hiyo ambapo kwa pamoja walikubaliana kujenga nchi na kuweka mbali tofauti zao za kisiasa.

Aunt Ezekiel Afunguka Sababu ya Kumshirikisha Mwanae Cookie Katika Filamu

$
0
0
Aunt Ezekiel Afunguka Sababu ya Kumshirikisha Mwanae Cookie Katika Filamu
Msanii wa filamu Bongo, Aunt Ezekiel amefunguka sababu ya kumshirikisha mwanae, Cookie katika filamu yake mpya ‘Mama’ ambayo ipo mbioni kutoka.

Muigizaji huyo ameiambia Bongo5 kuwa sababu ya kufanya hivyo ni ili kupata uhalisia na hisia za moja kwa moja.

“Amecheza kama mtoto wangu na amakuja kujaribu, kuwa sure kama anaweza kufanya kwa sababu mwisho wa siku Cookie ni mdogo sana lakini nilitamani kucheza naye ili nipate ile feeling like iniume kama kama Mama,” amesema.

“Watanzania wameshachoka na vitu ambavyo tulikuwa tunavifanya, wanataka vitu vipya, sasa nimewatengenezea kitu kipya kutokana na mimi hadhi yangu ipo kivingine, now am mama kwa hiyo nafanya kama Mama,” ameongeza.

Aslay Afunguka Mahusiano Yake na Nandy

$
0
0
Aslay Afunguka Mausiano Yake na Nandy
Msanii wa muziki Bongo, Aslay amefunguka kuhusu ukaribu wake na Nandy kwa sasa.

Muimbaji huyo wa ngoma ‘Natamba’ ameiambia FNL ya EATV kuwa kinachowaunganisha ni kazi tu hakuna mahusiano ya kimapenzi kama inavyokuwa ikiripotiwa.

“Nafikiri mashabiki zangu ambao wananifuatilia wanajua ni mtu ambaye nina mtoto, kuna mwanamke ambaye nimezaa naye. Nandy tupo kwenye kazi tu, tunafanya lakini hamna chochote kinachoendelea kati yangu na Nandy,” amesema.

Aslay na Nandy kwa sasa wanafanya vizuri na ngoma ‘Subalkheri’ ikiwa ni ngoma yao ya pili kutoa pamoja baada ya Mahabuba.

Sajent, Tiko Hapatoshi! Kisa Dulla Makabila Kula Mzigo kwa Mashosti Hao

$
0
0
Sajent, Tiko Hapatoshi! Kisa Dulla Makabila Kula Mzigo kwa Mashosti Hao
UBUYU una tabia moja ya ajabu, ukiula sana, lazima ukuchubue mdomo, lakini siku zote mlaji haachi kuumung’unya! Msanii maarufu wa miondoko ya Singeli Bongo, Abdallah Ahmed ‘Dullah Makabila’, anadaiwa kuzua kizaazaa mjini.



Jamaa huyo anadaiwa kuwachanganya vilivyo waigizaji wawili wa Bongo Movies ambao awali walikuwa mashosti, Husna Idd ‘Sajenti’ na Tiko Hassan ambapo sasa hapatoshi. Uchunguzi wa Ijumaa Wikienda ulibaini kuwa, ubuyu huo uliwahi kusambaa, lakini nyuma ya pazia bado kukawa na vita kali ya chinichini kati ya kundi la Sajenti na lile la Tiko.



Vita hiyo ilijenga ngome mbili, kila moja ikirusha maneno makali kwa nyingine. Hata hivyo, katika vita hiyo, Tiko ambaye alidaiwa kumkwapua Dullah kwa Sajenti alionekana ndiye mbaya hivyo kuuzika urafiki wao waliokuwa nao kabla ya sakata hilo.


Sajent.

MSIKIE MTOA UBUYU

Mtoa ubuyu wetu alinyetisha kuwa, ni kweli kulikuwa na ukaribu kati ya Sajenti na Tiko, kiasi cha kuvaa nguo saresare au hata kwenda kwenye sherehe mbalimbali za mjini wakiwa pamoja.

“Chanzo cha kuvurugika kwa ushosti wao ni Dullah ambaye ilisemekana alimtema Sajenti na kwenda kutuliza mtima wake kwa Tiko,” alinyetisha mtoa ubuyu wetu.



SAJENTI AFUNGUKA

Baada ya kuunyaka ubuyu huo, Ijumaa Wikienda lilianza kwa kumtafuta Sajenti. Alipoulizwa kuhusu madai ya kutemwa na mwanaume wake na kwenda kwa rafiki yake, alitema cheche;

Ijumaa Wikienda: Sajenti mambo vipi? Kuna habari ya wewe kutemwa na Dullah kisha akaenda kwa Tiko wakati ninyi mlikuwa ni marafiki, je, kuna ukweli wowote?



Sajenti: Ni kweli, aliniacha yuko kwa Tiko sasa hivi..!

Ijumaa Wikienda: Imekuwaje sasa na ninyi mlikuwa marafiki?

Sajenti: Siku zote mwenye tabia hiyo hawezi kuiacha, ndivyo ilivyokuwa.

Ijumaa Wikienda: Kwa hiyo na wewe umekubali kumuachia hivihivi mpenzi wako?

Sajenti: Mbona nimeshaanza kusahau? Nipo na ninaendelea na maisha yangu mengine kabisa.


Tiko

HUYU HAPA TIKO

Baada ya kuzungumza na Sajenti, Ijumaa Wikienda lilimtafuta Tiko na kumuuliza kuhusu tuhuma hizo ambapo naye alifunguka akionesha kuwa kuna mchezo uliofanyika kati yao.

Ijumaa Wikienda: Tiko vipi hili sekeseke linaloendelea kati yako na Sajenti kuhusu wewe kutembea na Dullah wakati ninyi mlikuwa marafiki?

Tiko: (anaguna) kwanza kwenye upande wa urafiki, sidhani kama tulikuwa marafiki kihivyo.

Ijumaa Wikienda: Vipi kuhusu kutembea na Dullah wakati ulijua wazi ni shemeji yako kwa Sajenti?

Tiko: Ukweli ni kwamba, jambo hilo anaweza kulizungumzia Dullah maana sijui hata nitaelezaje, lakini ukweli ni kwamba Dullah anajua kila kitu. Baada ya kumsikia Tiko, Ijumaa Wikienda lilimsaka Dullah ambaye naye alibanwa kugonganisha mtu na rafiki yake kwani ilidaiwa kuwa alijua wazi walikuwa ni marafiki.

Dulla Makabila.

Ijumaa Wikienda: Dullah kuna madai kuwa umemtema Sajenti na kwenda kwa Tiko ambaye walikuwa ni marafiki na ulikuwa ukifahamu hilo, je, hilo likoje?

Dullah: Ni kweli kabisa hujakosea, niko na Tiko, lakini kuna vitu vilinifanya nifanye hivyo.

Ijumaa Wikienda: Lakini si ulijua wazi walikuwa ni marafiki? Kwa nini uliamua kuchanganya au kuwagombanisha?

Dullah: Mimi nilianza kumjua Tiko kabla hata ya Sajenti, ni mwanamke ambaye alikuwa akilini kwangu na pia sioni kama kuna shida hata kama walikuwa wanajuana ilimradi mmoja nimeshaachana naye

Ijumaa Wikienda: Kwa hiyo una mpango gani na Tiko?

Dullah: Unajua mara nyingi mambo yangu nataka yawe siri ila itajulikana huko mbeleni, itoshe tu kusema kuwa ninampenda sana Tiko.

Tundu Lissu Kufanyiwa Upasuaji wa 19 Mkewe Afunguka Haya

$
0
0
Tundu Lissu Kufanyiwa Upasuaji wa 19 Mkewe Afunguka Haya
Wakati Tundu Lissu akitarajiwa kufanyiwa upasuaji wa 19 katika Hospitali ya Chuo Kikuu cha Leuven nchini Ubelgiji keshokutwa, mkewe amesema walilitambua hilo tangu wakiwa Nairobi nchini Kenya.

Alicia Lissu alisema hayo alipozungumza na Mwananchi jana baada ya mbunge huyo wa Singida Mashariki kueleza kuwa Jumatano atafanyiwa upasuaji wa mguu wa kulia ili kumwezesha kupona haraka.

Upasuaji huo ni mwendelezo wa aliokuwa akifanyiwa katika Hospitali ya Nairobi nchini Kenya alikokuwa amelazwa baada ya kushambuliwa kwa risasi zaidi ya 30 akiwa katika makazi yake mjini Dodoma Septemba 7, 2017.

Lissu alipelekwa kwa matibabu jijini Nairobi usiku wa siku aliyoshambuliwa baada ya kupata matibabu ya awali katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Dodoma.

“Tulipokuwa Nairobi madaktari walitueleza kutafanyika upasuaji mwingine kwa sababu pale kazi yao ilikuwa kuokoa maisha yake na kuweka mwili wake sawa kutokana na majeraha aliyokuwa amepata,” alisema Alicia.

“Upasuaji kwa mguu wa kulia ni kitu walichotueleza, walituandaa na hata tulipofika hapa madaktari wakataka kujiridhisha kwa kufanya vipimo kuangalia mwili wake utakuwaje kipindi cha mazoezi maalumu.” Alisema walifanya vipimo kuona uwezo wa mguu na hasa juu ya goti na wamejiridhisha kuwa ana maendeleo mazuri ya mazoezi na ana imani baada ya upasuaji ataendelea vizuri zaidi.

Alicia, ambaye kitaaluma ni mwanasheria alisema katika majuma yaliyopita Lissu aliruhusiwa kutoka hospitalini na alikuwa akienda kwa ajili ya mazoezi tu. Akizungumzia maendeleo ya Lissu kiafya, Alice alisema: “mwanzo niliwaza hataamka lakini ameamka, nina furaha sana amekuwa na maendeleo mazuri kwa miezi miwili tukiwa hapa.”

“Kutoka kitandani na kufikia hatua ya kusimama, kuanza kujihudumia ni hatua kubwa, nina furaha, namshukuru Mungu amesikia maombi yetu na ya wengine na hii ni faraja kwetu,” alisema.

Alicia alisema Lissu ambaye pia ni rais wa Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS) amekumbuka harakati zinazoendelea nchini akisema akipona anataka kurudi nyumbani ashiriki kupigania utawala bora.

Alisema baadhi ya wanaomtembelea Lissu wamekuwa wakimshauri akirejea nyumbani asirudi katika mazingira yatakayohatarisha maisha yake.

Lissu juzi alitoa taarifa ya maendeleo ya afya yake akisema anaweza kusimama bila msaada na amejuzwa na timu ya madaktari kuwa kasi ya mfupa wa juu ya goti kuunga ni ndogo.

“Madaktari wangu wamesema wasipoingilia kati na kurekebisha mfupa huo itachukua muda mrefu sana kuunga,” alisema.

Alisema madaktari wamemweleza hata mfupa huo ukiunga baada ya muda mrefu, hautaunga kwa namna utakayoondoa hatari ya kuvunjika baadaye.

“Kwa sababu hizi, madaktari wangu wamependekeza kufanya operesheni nyingine kwenye mfupa wa juu ya goti la kulia, Machi 14 nitarudi Hospitali ya Chuo Kikuu cha Leuven, Gasthuisberg kwa ajili ya kufanyiwa operesheni hiyo,” alisema.

Alisema yuko katika mikono salama ya kitabibu chini ya madaktari Profesa Stefa Nijs na Profesa Willem-Jan Mertsemakers ambao ni madaktari bingwa wa mifupa wanaosifika barani Ulaya.

“Hivyo, msiwe na hofu. Mungu wetu aliyeniwezesha kuwa hai sasa, ataendelea kutenda miujiza kupitia kwa madaktari bingwa hawa,” alisema.

Spika Afanya Mabadiriko Bungeni Ateua Wajumbe wa Kamati ya Kudumu

$
0
0
Spika Afanya Mabadiriko Bungeni Ateua Wajumbe wa Kamati ya Kudumu za Bunge
Spika Job Ndugai amefanya uteuzi wa wajumbe wa kamati za kudumu za Bunge.

Taarifa kwa vyombo vya habari iliyotolewa leo Machi 12,2018 inasema Spika amefanya uteuzi huo kwa mujibu wa Ibara ya 96 ya Katibu ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Taarifa hiyo imesema ibara hiyo imeweka wazi kwamba, Kanuni za Kudumu za Bunge zinafafanua muundo wa shughuli za Kamati za Bunge.

“Kwa msingi huo Kanuni ya 118 ya Kanuni za kudumu za Bunge, Toleo la Januari, 2016 imeweka Kanuni za Kudumu za Bunge zenye muundo na majukumu mbalimbali kama yanavyofafanuliwa katika nyongeza ya nane. Uteuzi wa wabunge kwenye kamati mbalimbali unaonekana utaratibu katika Kanuni ya 116.”

“Kanuni ya 116(1) inaweka utaratibu kwamba, ujumbe kwenye Kamati za Kudumu za Bunge utadumu mpaka mwisho wa Mkutano wa Kumi wa Bunge ambao ni nusu ya kwanza ya maisha ya Bunge,” anasema Spika Ndugai.

Katika uteuzi huo, wajumbe mbalimbali wamerejea katika kamati zao, wengine wakibadilishwa huku baadhi ya wenyeviti waliokuwa wakiongoza baadhi ya kamati wameondolewa.

 “Kwa mamlaka niliyopewa na Kanuni ya 115(3) na kwa kuzingatia vigezo vilivyoanishwa katika Kanuni ya 116(5) nimefanya uteuzi mpya wa ujumbe katika Kamati za Kudumu za Bunge. Wajumbe wa kila kamati wanawajibika kuchagua mwenyekiti na makamu mwenyekiti kwa mujibu wa Kanuni ya 116(10) kuwa viongozi wao,” amesema.


Sisafiri Kwenda Nje kwa Sababu Sio Jimbo Langu- Rais Magufuli

$
0
0
Sisafiri Kwenda Nje kwa Sababu Sio Jimbo Langu- Rais Dkt. Magufuli
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli amesema kuwa anapokea mialiko mingi kutoka nje ya nchi lakini amesema hawezi kusafiri kwenda huko kwasababu sio jimbo lake.

Akiwa ametimiza siku 859 madarakani, Rais John Magufuli ametembelea nchi chache huenda kuliko watangulizi wake wanne.

Magufuli ametembelea Kenya, Uganda, Rwanda na Ethiopia katika kipindi chote cha utawala wake huku akitimiza miaka miwili, miezi minne na siku saba tangu aapishwe kuwa Rais wa Tanzania Novemba 5, 2015.

Huenda hilo lilimfanya jana atoe siri na sababu zinazomfanya asipende kusafiri mara kwa mara nje ya nchi.

Akiwa mjini Singida jana alikozindua kiwanda cha mafuta ya kupikia cha Mount Meru Millers Group, Rais Magufuli alisema amekataa zaidi ya mialiko 70 ya kwenda nje ya nchi kwa sababu hakuchaguliwa na Watanzania kwenda huko bali kuwatumikia.

“Nataka Tanzania yote niizungukie ndiyo maana sitaki kwenda nje, maana huko si kwenye jimbo langu, jimbo langu mimi ni Tanzania. Nimekataa mialiko zaidi ya 70. Niende nje kufanya nini wakati sijamaliza kutatua kero za wananchi.”

“Nataka nizitatue kero za wananchi walionipigia kura kwanza, walipanga foleni wakati wa mvua na jua kunichagua mimi na waheshimiwa wabunge,” alisema Rais Magufuli.

“Bado sijaenda, Iringa, Mbeya, Rukwa na sehemu nyingine, lazima nizunguke nchi yote kutatua kero za wananchi..” alisema.

Julai 4, mwaka jana, alisema alipata mialiko zaidi ya 60 kwenda nje ya nchi baada ya kuwa Rais, lakini aliikataa kwa sababu anataka kuishughulikia Tanzania kwanza.

Alisema hayo akiwahutubia wakazi wa Sengerema katika uzinduzi wa mradi wa maji.

Alisisitiza kuwa hana haja ya kwenda nje ya nchi kwa sababu bado ana mzigo mkubwa wa kumaliza ufisadi. “Niende nje kufanya nini wakati nitaenda tu nikishastaafu, nataka nimalize kwanza haya ya hapa ndani,” alisema pia mwaka jana mjini Sengerema.

Alipozungumza na watendaji mbalimbali wa Serikali Ikulu jijini Dar es Salaam Novemba 7, 2015, Magufuli alifuta safari za nje kwa watendaji wote wa Serikali na kusisitiza kuwa kama kuna ulazima, mhusika atapaswa kupata kibali kutoka kwa Katiba Mkuu Kiongozi.

Baadaye akizindua bunge la 11, Novemba 20 mwaka 2015, Magufuli alisema kuanzia mwaka 2013 hadi 2015, safari za nje zilikuwa zimeigharimu Serikali Sh356.3 bilioni.

Jana, Rais Magufuli katika uzinduzi huo wa kiwanda cha mafuta, aliagiza Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) na Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji kupandisha kodi kwa waingizaji wa mafuta ghafi ya chakula kutoka nje ya nchi.

Alisema hatua hiyo itawezesha wawekezaji wa ndani wa viwanda vya mafuta ya chakula kupata soko.

Rais Magufuli alitoa agizo hilo wakati ambao Serikali inafanya maandalizi kwa ajili ya bajeti ya mwaka wa fedha wa 2018/19.

Alisema anafahamu mchezo mchafu unaofanywa na waagizaji wa mafuta kutoka nje ya nchi ikiwa ni pamoja na kuua soko la ndani la mafuta ya chakula.

“Ninafahamu mchezo mchafu unaofanywa na waagizaji wa mafuta, wanapofanya hivyo lengo lao si kutengeneza soko la ajira bali ni kuua soko la mafuta,” alisema.

Rais Magufuli alisema, “wanachofanya wanaagiza mafuta kwa kisingizio kuwa ni crude oil (mafuta ghafi) yanayohesabika kama ni malighafi,” alisema.

Aliongeza kuwa, kwa kisingizio hicho, TRA na watu wengine hawawatozi kodi na wanapoyafikisha nchini waagizaji hao huyaweka kwenye madebe na kuyauza hivyo kutengeneza faida kubwa.

“Nataka mwaka huu... wabunge mko hapa na waziri uko hapa... na waziri wangu najua mnanisikia nataka mafuta hayo yanayoagizwa kutoka nje yatandikwe charge (gharama) kubwa sana,” aliagiza.

Alisema anafahamu waagizaji hao huwa wanajikusanya na kwenda bungeni kuzitembelea kamati za Bunge.

“Naomba wabunge na mawaziri msikubali lobbing (ushawishi) za namna hiyo, mnawaumiza wananchi,” alisema.

Rais Magufuli alisema mahitaji halisi ya mafuta ya chakula kwa mwaka ni tani 450,000 na nchi inazalisha tani 135,000 sawa na asilimia 30, huku asilimia 70 ya mafuta ikiagizwa kutoka nje.

Alisema wanapoagiza mafuta hayo wanatumia dola za Marekani, fedha ambazo zingeweza kutumika katika shughuli zingine.

Rais alisema mafuta ya chakula yanachukua nafasi ya pili ya bidhaa zinazoingizwa nchini kutoka nje.

“Lakini mtu wa kawaida angeweza kutuuliza kweli Tanzania tuna wajibu wa kuagiza mafuta, tutumie fedha yetu ya kigeni kununulia mafuta ya chakula?” alihoji.

“Mtu yeyote mwenye akili timamu atakushangaa, mimi ndugu zangu ni mtaalamu wa kutengeneza mafuta nimewahi kukaa viwandani ninafahamu mchezo mchafu wanaoucheza hawa waagizaji.”

Pia, alimuagiza Waziri wa Viwanda, Charles Mwijage akamweleze mwenzake wa Wizara ya Fedha, Dk Philip Mpango kuangalia namna wanavyoweza kuwapunguzia gharama za kodi wawekezaji wa viwanda vya ndani.

“Haiingii akilini kutoza Vat (Kodi ya Ongezeko la Thamani) na kutoza kodi zingine kwa mtu ambaye ana kiwanda hapa; anatumia umeme wa hapa, anatumia maji ya hapa, anatumia malighafi za hapa, ametengeneza mnyororo wa ajira mkubwa wa watu wa hapa,” alisema.

Aliongeza kuwa kiwanda kama hicho kitanunua umeme, hivyo Tanesco watachukua fedha na Wizara ya Maji pia itapeleka maji kwenye kiwanda.

“Yale maji yatalipiwa kodi na wakulima wataweza kuuza mazao yao na wafanyabiashara nao watapunguza gharama za kusafirisha bidhaa zao sababu kiwanda kipo karibu.”

Msinifananishe na Alikiba Bado Sijamfikia Hatua Aliyokuwa Nayo- Aslay

$
0
0
Msanii wa BongoFleva anayefanya vizuri na kibao chake cha 'SabalKheri Mpenzi' alichoshirikiana na Nandy, Aslay amewataka mashabiki zake kuacha kumlinganisha yeye na mkongwe Alikiba kwa madai bado hajaweza kufika hatua aliyokuwa nayo Kiba.


Aslay ametoa kauli hiyo baada ya kupita kipindi kirefu kwa baadhi ya mashabiki kudai uwezo aliokuwa nao kwa sasa  anaweza hata akamfunika Alikiba pindi wakiamua kufanya 'show' ya pamoja au hata wakiandaa tamasha siku moja basi watu wengi wataenda kwa Aslay.

"Kama kuna mashabiki wanafanya kitu kama hicho wanakosea kabisa tena sio vizuri, kwa maana hao wameshafika katika level zingine, na mimi ninajitahidi nifike huko siku moja. Kwa hiyo ukinishindanisha kwanza utaniua kisaikolojia kwasababu nitajiona na mimi nimeshafikia hatua zao kumbe bado sana", amesema Aslay.

Pamoja na hayo, Aslay ameendelea kwa kusema "ukisema umlinganishe Aslay na Alikiba utakuta kuna vitu vingi vinakukosoa kwsababu yeye ameshaingia katika Tuzo mbalimbali kubwa mpaka kufika sasa hivi na hata akifanya 'show' anajaza watu kwa hiyo mimi naona sio watu wa kushindana nao sasa hivi".

Kwa upande mwingine, Aslay amesema muda huu kwake sio wa kushindana na wasanii waliyomzidi ufanisi na uwezo wa kimuziki bali anajikita zaidi katika kujiboresha ili nae siku afike walipofika wanamuziki wakubwa waliopo nchini Tanzania.

Kutana na Mtabibu Mwenye KUBRI kutoka kwa ALLAH simba Mtabibu wa Nyota za Binadamu na Dawa za Asili

$
0
0
Kutana na Mtabibu Mwenye KUBRI kutoka kwa ALLAH issa simba said Mtabibu wa Nyota za Binadamu na Dawa za Asili ya Africa Mwenye UWEZO Kubaini tatizo lako Pindi tu Utakapo Fanya Mawasilino Kupitia Wasaa Husika..JE UNASUMBULIWA NA Mapenzi? (Umeachwa na Umpendae,Awe Mume,Mke na Bado unampenda?Na Umejaribu Sehemu nyingi Bila Mafanikio?Wasilina na Maalim Hussein Ujione muujiza wa Papo kwa Papo.. anauwezo WA KURUDISHA MAHUSIANO NA KUIMARISHA NDOA YAKO NDANI YA SAA 12 TU. Umekimbiwa na Mumeo,mkeo au Mpenzi na anaishi na mtu mwingine? Muone akutatulie Anauwezo wa Hali ya Juu wa Kusambalatisha Mahusiano yao Endapo utafata Atakacho kuelekeza.
Atamfanya Atimize 5 zote kwa Muda Mfupi.

Issa simba said Anatumia Jina la Muhusika au Picha Kumal6uiza Tatizo lako..
Anatibu kwa Kutumia Vitabu vya QUR-AN Dawa za Asili za Africa,Dawa za Kiarabu na Majini.Anatafsiri Ndoto. Kushinda BAHATI NASIBU, KUSAFISHA NYOTA. Mvuto wa Mwili na BIASHARA, Kinga ya Mwili,ZINDIKO za Nyumba.MIGUU Kufa GANZI.Kufungua KIZAZI kwa wale walio fungwa kwa njia za KISHIRIKINA. Anakupa Jini la Mali kwa yule anaehitaji Utajiri BILA MASHARTI. Nguvu za KIUME, Humaliza Kesi zilishindika ndani ya siku 14 tu..na mengi zaidi

Piga simu +255 622588038au 0679119679 au +255 764318107

NB: TIBA KWA DINI ZOTE NA IMANI ZOTE...

Hiki Hapa Kikosi cha Yanga Dhidi ya Stand United Leo

$
0
0
Hiki Hapa Kikosi cha Yanga Dhidi ya Stand United Leo
Yanga SC yatangaza kikosi chake kitakacho ingia wanjani hii leo kuivaa timu ya Stand United mchezo wa ligi kuu soka Tanzania Bara.

Youthe Rostand, Juma Abdul, Gadiel Michael , Said Makapu, Kelvin Yondani, Maka Edward
Yusuph Mhilu, Pius Buswita, Obrey Chirwa, Raphael Daudi, Ibrahim Ajib

Kikosi cha akiba

Ramadhani Kabwili, Hassan Kessy, Haji Mwinyi, Abdalah Shaibu ‘Ninja’, Thaban Kamusoko, Emmanuel Martin, Juma Mahadhi.

Wananchi Watelekezwa Mwili wa Marehemu Nyumbani kwa Mwenyekiti wa Mtaa

$
0
0
Wananchi Watelekezwa Mwili wa Marehemu Nyumbani kwa Mwenyekiti wa Mtaa
Baadhi ya wananchi wa Mtaa wa Nyakabale wilayani Geita wametelekeza mwili wa marehemu nyumbani kwa mwenyekiti wa mtaa huu, Elias Ndarawa.

Ndarawa anatuhumiwa kutoshughulikia tukio la Zacharia Shaban kupigwa na polisi jamii hadi kufa.

Wananchi hao waliubeba mwili wa Zacharia na kuulaza kwenye kitanda cha mwenyekiti huyo.

Majaliwa Shaban ambaye ni ndugu wa marehemu Zacharia amesema leo Machi 12,2018 kwamba nduguye alipigwa Machi 5,2018 akiwa eneo la Mgodi wa Dhahabu Geita (GGM) akiokota mabaki ya mawe ya dhahabu maarufu magwangala.

Amesema Zacharia alipelekwa polisi alikokaa kwa siku sita na aliporudi uraiani hali yake ilikuwa mbaya.

Majaliwa amesema nduguye alipelekwa hospitali alikofariki dunia Jumamosi Machi 10,2018 na hadi sasa hakuna kiongozi aliyefika kwenye msiba huo wala kutoa kauli yoyote.

Mkazi wa mtaa huo, Johnson John amesema hawapo tayari kuzika hadi Serikali itakapotoa kauli kuhusu hatima ya maisha yao kwa kuwa polisi jamii wamekuwa wakiwapiga na kuwajeruhi.

Jana, Machi 11,2018 wananchi walivamia eneo la kituo cha polisi jamii kilichopo mtaa wa Manga na kukichoma moto kwa madai kwamba wamempiga na kumuua Zacharia

Diwani Chadema Afunguka Polepole Alivyomtumia Watu Kumshawishi Kujiunga na CCM

$
0
0
Diwani Chadema Afunguka Polepole Alivyomtumia Watu Kumshawishi Kujiunga na CCM
Diwani wa Gwarama Kakonko Kigoma amefunguka na kusema kuwa Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Humphery Polepole anatumia vijana mbalimbali kumshawishi ili akubaliane naye na kujiunga na Chama Cha Mapinduzi (CCM).


Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na CHADEMA na kuthibitishwa na Afisa Habari wa CHADEMA, Tumaini Makene imesema kuwa vijana hao wamekuwa wakihangaika sana kumshawishi diwani huyo ili ahamie CCM na kumuahidi kuwa watafanya kila mbinu ili ashinde tena uchaguzi akiwa ndani ya CCM.

"Tangu juzi natafutwa eti nikubaliane na Ndugu Humphrey Pole pole ili nijiunge na Chama Cha Mapinduzi. Ndugu huyu alikuja Kakonko, wiki iliyopita na baadae akaenda Dodoma ila aliacha vijana wanaofanya biashara ya kununua madiwani Kakonko na wanazunguka, usiku na mchana wakitafuta madiwani wa upinzani, wamenipigia simu nyingi,nina Audio zao,wanaahidi kukupa stahiki zote,na wanasema wao wanahakikisha unashinda udiwani kwa gharama yoyote ile"

Diwani huyo aliendelea kusimulia kisa hicho na kusema kuwa kiongozi huyo alirudi tena jana Machi 11, 2018 kufuatilia maendeleo ya kazi yake hiyo aliyoiacha na kudai kuwa yeye hawezi kununuliwa.

"Sijawahi kuona biashara ya watu katika umri wangu, nimeiona sasa, tena safari hii anayetaka kununuliwa ni mimi, Mungu lehemu taifa lako. Pesa zimetengwa ili kumununua diwani wa Gwarama. Wanunuaji wetu wanatumia gari ya wagonjwa kukata misere mtaani kutafuta diwani ambaye wao wanataka akihame chama kwa Kusema nimekubali utendaji kazi"

Mbali na hilo Diwani huyo ameweka wazi kuwa hali ya madiwani wa Kakonko ni mbaya kwani wanadai posho zao za mwaka mzima na kusema kuna wakati wanaendesha vikao bila hata kuwepo kwa maji ya kunywa kama njia ya kutaka kuwategesha.

"Kakonko ina hali mbaya ya Kiuchumi kiasi kwamba madiwani tunadai posho miezi 12 sasa. Tunakopesha vikao, hatunywi maji kwenye vikao, kuna roho zipo zimesubiri uombe maji ya kunywa halafu upewe na sumu ili udiwani ambao ni uwakilishi wa wananchi ukome kwa kukukatiza maisha ili chama kinachoitwa pendwa kishinde, ushindi wa chama hiki ni mpaka adui afe kama siyo kufanywa kilema kwanza"

"Nimewaambia viongozi wa dini biashara hii kama imefika Gwarama, nao wamesema nisikubali kuuza Uwakilishi huu kwasababu ya kutafuta urahisi wa maisha na chakula.Na mimi nilishakubali kuongozana na maskini wenzangu. Naheshimu kura za maskini wenzangu, siwezi uza kura za hawa maskini wenzangu ili Mimi niutwae utajiri kwa kuwadhuru maskini." alisema diwani wa Gwarama

www.eatv.tv ilipomtafuta Katibu Mwenezi wa CCM, Humphery PolePole ili kujibu tuhuma hizo simu yake ilikuwa ikiita tu bila kupokelewa.

Mwigulu Amfananisha Abdul Nondo na Kinyango Aamua Kumchongea kwa Rais Magufuli

$
0
0
Mwigulu Amfananisha Abdul Nondo na Kinyango Aamua Kumchongea kwa Rais Magufuli
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mwigulu Nchemba amefunguka na kumwelezea Mwenyekiti wa Mtandao wa Wanafunzi Tanzania (TSNP), Abdul Nondo kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli na kumfananisha kijana huyo na kinyago.


Mwigulu Nchemba alisema hayo Machi 11, 2018 akiwa mkoani Singida na kusema kuwa wapinzania wamekosa ajenda ndiyo maana wamekuwa wakihangaika kutafuta njama za kuchafua taswira ya nchi ya Tanzania.

"Mhe Rais ndiyo maana unaona vinyago vingi vingi hivi kama hivi juzi anatokea kijana mdogo eti anasema ametekwa, eti ametekwa akapata na muda wa kutafuta perfume na nguo za kubadilishia kule atakakokuwa ametekwa, unaotoa wapi muda wa kujiandaa ni vitu vya kiajabu ajabu kama hivyo watu wanatafuta namna za kuchafua taswira za nchi yetu na jambo hili si jambo ambalo tutacheza nalo" alisisitiza Mwigulu Nchemba

Mnamo Machi 6, 2018 mwanafunzi huyo aliripotiwa kutoweka katika mazingira tatanishi na siku iliyofuata yaani Machi 7, 2018 majira ya jioni ilisemekana kijana huyo alijikuta Mafinga ambapo alikwenda kuripoti kituo cha polisi, kisha baada ya hapo alisafirisha kutoka Iringa na kuletwa jijini Dar es Salaam kisha kukabidhiwa kwa Mkuu wa Upelelezi jijini Dar es Salaam (DCI) ambapo mpaka sasa upelelezi wa tukio lake unaendelea.

Vigogo Mbaroni kwa Wizi wa Maji

$
0
0
Vigogo Mbaroni kwa Wizi wa Maji
Naibu Waziri wa Maji na Umwagiliaji, Jumaa Aweso amefanya ziara ya kustukiza katika Kiwanda cha Nguo cha 21st Century kilichopo mjini Morogoro na kuamuru kukamatwa kwa viongozi wake baada ya kubaini kuwa kiwanda hicho kinahujumu mapato ya Serikali kwa kuondoa mita inayorekodi matumizi ya maji nyakati ya usiku.



Mita hiyo iliyoondolewa na hivyo kufanya maji yatumike bila kujulikana kiwango cha matumizi hali ambayo imekuwa ikiikoseshamapato halali Mamlaka ya Maji safi na Usafi wa Mazingira Manispaa ya Morogoro (Moruwasa). Waliotiwa mbaroni ni pamoja na Meneja Uzalishaji wa kiwanda hicho, Clement Munisi, Meneja wa Fedha Jayesh Vajdya pamoja na Msoma mita wa kiwanda aliyejulikana kwa jina moja la Samuel.

Naibu Waziri huyo, alisema amefanya ziara hiyo ya kustukiza katika kiwanda hicho baada ya kupata taarifa kutoka wasamaria wema kuwa nyakati za usiku vinafanyika vitendo vya hujuma kwa kuondoa mita hiyo ili maji yatumike bila kupimwa kiwango chake cha matumizi na kisha kuirudishia nyakati za asubuhi.

Alisema kuwa licha ya Serikali ya awamu ya tano kujali uwekezaji wa viwanda lakini viwanda hivyo vinaenda kinyume kwa kuunganisha maji kwa njia isiyo sahihi na kwamba vinapaswa kulipa gharama za matumizi yake ili fedha hizo ziweze kuendelea kutoa huduma katika maeneo mengine si kuhujumu jitihada za Serikali za kuwapa maji kwa ajili ya matumizi ya uzalishaji.

Aliamuru viongozi hao kukamatwa mara moja na kwenda kuhojiwa na vyombo vya ulinzi na usalama na kisha kufikishwa mahakamani mara moja kwa kitendo cha kuhujumu mali za serikali. Naibu waziri alisema kuwa baada ya kukamatwa kwa viongozi hao na kutoa maelezo wanapaswa kupigiwa hesabu kulingana na wizi huo na kuunganishiwa faini. Hata hivyo alisema kuwa, wizara hiyo imeanza kazi ya kupambana na watu wote wanaohujumu miundombinu ya maji na wizi iwe kwa mtu mmojammoja au taasisi na viwanda lengo ni kuongeza makusanyo ya mapato yatakayochangia kuendeleza miradi mipya ya maji.

Akielezea jinsi walivyobaini hujuma hizo, mkuu wa kuzuia upotevu wa maji wa Moruwasa, Bertam Minde alisema alisema walibaini hujuma hizo kwa muda mrefu na kubadilisha mita tatu tofauti huku wakifanya ukaguzi wa mita hiyo nyakati za usiku. Alisema kuwa juzi (Machi 10, mwaka huu) walifanya ukaguzi mchana na kuona kiasi cha maji kilichotumika ni uniti 977 na walipofika usiku waliosoma tena wakati kiwanda hicho kikiendelea na kazi na kukuta uniti 984 huku mita yake ikiwa imefunguliwa na kuwekwa pembeni.

Mkurugenzi wa Moruwasa, Nicholaus Angumbwike alisema kuwa walianza kufanya uchunguzi kwa kipindi cha miezi mitatu baada ya kuona malipo ya kiwanda hicho yamepungua gafla kutoka Sh milioni 80 kwa mwezi hadi kufikia Sh milioni 20 wakati matumizi ya maji katika mitambo yao yakionesha ni juu. Mhandisi Angumbwike alisema waliamua kuwafungia mashine maalumu kabla ya mita inayoonesha kiwango cha matumizi ya maji yanayoelekea ndani ya kiwanda hicho pamoja na mita mpya na kusoma mara kwa mara mita hiyo na kubaini mita hiyo imekuwa ikifunguliwa nyakati za usiku.

Alisema kuwa kabla ya kufunga mita hizo waliwataarifu uongozi wa kiwanda hicho kuwa wawe makini na mita hizo mpya zilizofungwa na zitakuwa zikifanyiwa ukaguzi wa mara kwa mara lakini kiwanda hicho kiliendelea na wizi wa maji. Mwanasheria wa Moruwasa, Tumaini Kimaro alisema kuwa kitendo kilichofanywa na kiwanda hicho ni kosa la uhujumu uchumi na wizi wa mali za serikali na wanapaswa kufikishwa mahakamani kwa kosa hilo. Meneja uzalishaji wa Kiwanda hicho, Clement Munisi alisema bomba hilo ni mali ya kiwanda hicho na kama kweli mita imetolewa ni hujuma kwa mali za serikali ila hajui aliyefanya kitendo hicho.

Mwana FA Aungana na Mourinyo

$
0
0
 Mwana FA Aungana na Mourinyo
Msanii wa HipHop Bongo, Mwana FA ambaye ni shabiki maarufu wa klabu ya Manchester United ya England ameunga mkono kauli ya kocha wa timu hiyo Jose Mourinho, kuwa nyota Alexis Sanchez hatakiwi kulaumiwa kwa kiwango chake ndani ya muda mfupi.


Hivi karibuni Mourinho alisema kuwa wanaomlaumu Sanchez kwa kutoonesha kiwango kikubwa tangu asajiliwe msimu huu hawatakiwi kufanya hivyo kwani bado ana muda zaidi na yeye kama kocha analijua hilo na atalifanyia kazi.

Kwa upande wa Mwana FA yeye amesema Sanchez hatakiwi kulaumiwa kwani uzuri wa mchezaji muda mwingine huonekana timu ikiwa inafanya vizuri hivyo uwezo wa Sanchez utajieleza tu timu ikianza kufanya vizuri, kwasababu anajulikana ni mchezaji wa kuamua matokeo.

Aidha Mwana FA ameongeza kuwa yeye anaamini katika kuwapa wachezaji muda na suala la Sanchez limekuwa kama ilivyokuwa kwa nyota mwingine Paul Pogba ambaye alionekana kutofanya vizuri katika msimu wake wa kwanza.



Mkutano wa Kenyatta na Odinga Umezua Mgawanyiko kwa Upinzani Kenya

$
0
0
Mkutano wa Kenyatta na Odinga Umezua Mgawanyiko kwa Upinzani Kenya
Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta na kiongozi wa upinzani Raila Odinga walipokutana ghafla Ijumaa na kuahidi kuweka kando tofauti zao kwa maslahi ya taifa, hilo lilitazamwa na wengi kama ishara ya mwisho wa wingu la siasa ambalo limegubika taifa hilo tangu kufanyika kwa uchaguzi mkuu mwaka jana.

Bw Kenyatta na Bw Odinga waliitana "ndugu" na wakakubaliana kuundwe mpango wa pamoja wa kuangazia utekelezaji wa malengo ya pamoja ya viongozi hao wawili, ambao utazinduliwa rasmi karibuni.

"Huu ni mwanzo mpya kwa taifa letu," alisema Bw Kenyatta baada ya mkutano huo, akisisitiza kauli ya Bw Odinga kwamba "Tumekuja pamoja na ndugu yangu Kenyatta, tumeongea kwa kirefu na kukubaliana kwamba tunataka kuunganisha Kenya iwe taifa moja."

Katika mkutano wao, kuna wahusika ambao hawakuwepo ambao wengi walisubiri kusikia kauli yao.

Katika Muungano wa National Super Alliance (Nasa) ambao ulibuniwa mwaka jana, Bw Odinga alikuwa na viongozi wengine wa vyama vya upinzani, hususan makamu wa rais wa zamani Kalonzo Musyoka ambaye ni kiongozi wa chama cha Wiper Democratic Movement of Kenya Musalia Mudavadi wa Amani National Congress (ANC) na Moses Wetangula wa chama cha Forum for the Restoration of Democracy-Kenya (Ford-Kenya).

Wote wamekuwa viongozi wenza wa muungano huo.

Punde baada ya mkutano huo kufanyika, walikutana na kutangaza kwamba hawakuwa na habari kuhusu mkutano huo wa bw Odinga na Bw Kenyatta.

Kwenye taarifa ya pamoja, walisema hawana ufahamu kuhusu iwapo mazungumzo hayo ni sehemu ya mazungumzo ambayo Nasa, kama muungano wa siasa, umekuwa ukishinikiza kwamba yanafaa kufanyika kati ya serikali na upinzani.

Kenyatta na kiongozi wa upinzani Odinga wakutana
"Asubuhi ya tarehe 9 Machi 2018, tuliona kwenye vyombo vya habari mkutano kati ya Bw Uhuru (Kenyatta) na Bw Raila Amolo Odinga...Ingawa tumekuwa tukisisitiza mazungumzo yafanyike, sisi kama viongozi wenza wa Muungano wa Nasa, hatukuwa na ufahamu kuhusu majadiliano hayo yaliyofanyika Jumba la Harambee (Afisi ya Rais)," taarifa yao ilisema.

Taarifa kwenye vyombo vya habari kenya zinasema Bw Odinga hajazungumza na viongozi wenzake watatu kuhusu yaliyojadiliwa katika mkutano wake na Bw Kenyatta Ijumaa.

Gavana wa Mombasa Hassan Joho ambaye ni katibu mkuu wa chama cha ODM chake Bw Odinga aliingia kwenye mitandao ya kijamii kujaribu kuondoa utata ambapo aliahidi wafuasi wa chama hicho kwamba wana imani na uongozi wa chama hicho

"Hauwezi kuwa na mazungumzo na mtu ambaye hamko katika ngazi sawa," alisema.
Bw Musyoka, Bw Mudavadi na Bw Wetangula walikuwa wamedokeza kwamba wangetafuta ufafanuzi zaidi kuhusu mazungumzo ya Ijumaa wakati wa mkutano mkuu wa muungano huo ambao ulikuwa umepangiwa kufanyika leo Jumatatu.

Dalili za mgawanyiko zilianza kuonekana pale taarifa za vyombo vya habari zilipodokeza kwamba kulikuwa na uwezekano Bw Odinga angesusia mkutano huo

Wakenya sasa, na zaidi wafuasi wa upinzani, wanasubiri kusikia taarifa ya viongozi hao baada ya mkutano wao.
Bw Odinga alisusia kushiriki uchaguzi wa marudio uliofanyika 26 Oktoba mwaka jana akishinikiza mageuzi yafanywe kwanza katika Tume ya Taifa ya Uchaguzi.

Uchaguzi huo ulitokana na hatua ya Mahakama ya Juu kufuta matokeo ya uchaguzi wa tarehe 8 Agosti ikisema ulikuwa na kasoro nyingi.

Mahakama hiyo ilikuwa inatoa uamuzi katika kesi iliyokuwa imewasilishwa na Bw Odinga kupinga matokeo hayo.

Bw Kenyatta alishinda uchaguzi huo wa marudio kwa kura 7.5 milioni ambazo ni sawa na asilimia 98 ya kura zilizopigwa.

Idadi ya waliojitokeza ilikuwa ni asilimia 38.84 ya waliokuwa wamejiandikisha kushiriki uchaguzi huo.

Uchaguzi ulitatizika sana katika maeneo yenye wafuasi wengi wa upinzani. Katika majimbo manne magharibi mwa Kenya ambayo ni ngome ya Bw Odinga, uchaguzi uliahirishwa kwa siku kadha na baadaye haukufanyika.

Mahakamani: Shaidi Afunguka Alichokikuta Chumbani kwa Wema Baada ya Kumpekua

$
0
0
Mahakamani: Shaidi Afunguka Alichokikuta Chumbani kwa Wema Baada ya Kumpekua
MJUMBE wa Shina Namba 39, nyumbani anakoishi msanii wa filamu, Wema Sepetu, Steven Alphonce ambaye ni shahidi katika kesi inayomkabili staa huyo, amedai wakati wa upekuzi walikuta kipande cha sigara wala si bangi.

Alphonce amesema hayo leo Jumatatu, Machi 12, katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Thomas Simba akiongozwa na Wakili wa Serikali, Constantine Kakula, wakati akitoa ushahidi wake katika kesi ya matumizi ya dawa za kulevya inayomkabili Wema na wenzake wawili na kusema alishiriki katika upekuzi nyumbani kwa Wema na kukuta kipande hicho cha sigara jikoni na chumbani kwa Wema anakohifadhi viatu na nguo.

Amedai kuwa bangi anaijua ikiwa shambani kwani aliwahi kuiona Shinyanga lakini ikiwa nje ya hapo hawezi kuitambua. Wema na wenzake wawili wanashtakiwa kwa kutumia dawa za kulevya aina ya bangi na walikamatwa Februari 4, mwaka jana.

Mugabe Alalamikia Namna Alivyong'olewa Madarakani.. Akataa Kukutana na Mrithi Wake

$
0
0
Mugabe Alalamikia Namna Alivyong'olewa Madarakani.. Akataa Kukutana na Mrithi Wake
Rais wa zamani Robert Mugabe, mwenye umri wa miaka 94, ameelezea masikitiko yake "namna alivyong’olewa madarakani," akisema hayuko tayari kukutana na mrithi wake Rais Emmerson Mnangagwa kwa mazungumzo.

Mugabe alisema hayo wakati mpasuko kati yake na Mnangagwa ukidaiwa "kuongezeka".

Kwa mujibu wa gazeti binafsi la Standard, Mugabe ameapa kwamba hawezi kujadiliana na Mnangagwa kufikia "maridhiano".

Utawala wa miaka 37 wa Mugabe ulifikia kikomo Novemba 15 baada ya operesheni ya kijeshi, ambayo baadhi ya watu waliisifu kama "marekebisho yasiyo ya umwagaji damu".

Mzee huyo, hivi karibuni, aliripotiwa kwamba alikuwa akiunga mkono chama kipya kiitwacho National Patriotic Front (NPF) kinachoongozwa na waziri wa zamani Ambrose Mutinhiri.

Mutinhiri, mkongwe wa vita vilivyopiganwa miaka ya 1970 dhidi ya utawala wa wachache, alikutana na Mugabe wiki chache zilizopita kabla ya kutangaza kwamba alikuwa ameunda chama kipya.

Gazeti la The Standard lilimnukuu Mutinhiri mwishoni mwa wiki akisema haoni uwezekano wa Mugabe na Mnangagwa "kupikika katika chungu kimoja".

Mutinhiri ameripotiwa akimnukuu Mugabe akisema: "ED (Mnangagwa) anafikiri mimi ni zuzu.

"Anawezaje kufikiri kwamba naweza kuamini madai yao kwamba wanalinda heshima ya rais, urithi wangu, wakati niko chini kwa sababu yao huku wakiniburuta kwenye matope?

"Watu, hasa ndani ya Zanu-PF, wanataka viongozi waaminifu wa kulinda urithi wa rais na wanasema wanalaani unafiki, wanashutumu ukatili wa kijeshi dhidi ya watu.

"ED anasema ananitaka nimwidhinishe, nitakuwa naidhinisha nini? Unafiki? Ukatili dhidi ya watu?

Matamshi hayo yamekuja baada ya gazeti hilo la kila siku kusema mwishoni mwa wiki kuwa waziri wa zamani wa serikali ya Mugabe alimshawishi mkongwe huyo wa siasa kukutana na Mnangagwa katika juhudi za kusawazisha mambo.

Mpango huo, ripoti hiyo imesema, ulihusu kumweka Mugabe kama “mzee” wa chama tawala ili kumuunga mkono Mnangagwa.

Viewing all 104775 articles
Browse latest View live




Latest Images